tag:blogger.com,1999:blog-27469391461606174352024-03-13T21:58:08.871-07:00GETSUGA THE GREAT´S STATISTIKAnonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.comBlogger43125tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-55777615359273188982012-08-02T01:10:00.001-07:002012-08-02T01:10:46.963-07:00NAOMI AND RUTH<a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/msichana-ndotoni-mwanguep1.html?spref=bl"></a><br />
<h3 class="post-title entry-title" itemprop="name">Naomi and Ruth </h3><div class="post-header"> </div><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6NMpwmJVI0sGy8EYg6EtuSVxqbaU-Kvf6Rp1VLYN0Cs5voGdaBapg2snfoQ0CF5cipJk7pBIt4oOWswFmztt-1EjAMCHi4Jz4mUcNB_4ekL66Ro2IO7Ek626xYs1UXApp2XC9atALQ0Y/s1600/RuthandNaomi_eating_1020-1.jpg"><img alt="" border="0" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5483171674482206898" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6NMpwmJVI0sGy8EYg6EtuSVxqbaU-Kvf6Rp1VLYN0Cs5voGdaBapg2snfoQ0CF5cipJk7pBIt4oOWswFmztt-1EjAMCHi4Jz4mUcNB_4ekL66Ro2IO7Ek626xYs1UXApp2XC9atALQ0Y/s320/RuthandNaomi_eating_1020-1.jpg" style="cursor: pointer; float: right; height: 320px; margin: 0pt 0pt 10px 10px; width: 214px;" /></a><span style="font-size: large;"><br />
The <span class="yshortcuts" id="lw_1276649276_0">story of Naomi and Ruth</span> is a tale of faith, love, loyalty and redemption. The story begins when there was a great famine in the land of Israel. A man from Bethlehem named Elimelech took his wife Naomi and his two sons Mahlon and Chilion to live in Moab. </span><br />
<br />
<span style="font-size: large;">This country was just across the river Jordan but the people there were considered pagans and did not worship the one true God. The distance was only about 30 to 40 miles but as far as most Israelites were concerned, it was as far away as heaven and hell. However, the family went anyway and the son’s each married women of Moab. The two women were name Orprah and Ruth. After a time, Elimelech and both of her sons died. This left the three woman widowed and without protection. According to the laws at that time, women were not allowed to own property. So the women had no way of making a living. Since Naomi hand no kin in the land of Moab, she decided that the only thing for her to do was to go back to Bethlehem. She then encouraged both of her daughters-in-laws to go back to their families too. Neither one of the women wanted to leave Naomi. Eventually Orprah relented and returned to her kin, Ruth however would not go. She told her mother-in-law “ Intreat me not to leave thee: for whither thou goest, I will go; and where thou lodgest, I will lodge; thy people shall be my people and thy God my God.”<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">Ruth Loved and cared so much for Naomi that she was willing to leave her homeland forever. She was also willing to travel with her to a strange land where people might not accept her. Naomi’s example of living the gospel must have been very strong, because Ruth was also willing to turn from her religion and join the faith of her mother-in-law.<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">When Naomi returned to Bethlehem people came out to meet her and said “is this not Naomi?”. She told them not to call her Naomi anymore but to call her Mara, which means bitter because she said “the Almighty hath dealt bitterly with me.”<br />
Naomi had lost everything and was severally depressed but soon she turned her hope and ambitions to the one person in her life that had not been taken away from her. Her loving, faithful and obedient daughter-in-law Ruth.<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">Naomi told Ruth to go out to her kinsman’s field and to collect the grain that was left behind by the workers. For this was a law at that time that provided for the poor. Those in need were allowed to glean the fields after the reapers. Ruth did this faithfully and was able to provide quite well for herself and Naomi. Soon people began to ask about her and take notice of the loving service she gave to Naomi. One day <span class="yshortcuts" id="lw_1276649276_1">Boaz</span>, the kinsman who owned the field noticed Ruth too. He rewarded Ruth with special privileges and sent home extra food to her mother-in-law.<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">Now there was a law of Moses that provided for the welfare of widows in their society (Deuteronomy 25: 5-10). If a husband died, then it was the obligation of the nearest kinsman or blood relative to marry the widow and redeem the departed mans heritage. The firstborn of that marriage would then be raised to carry on dead man’s name.<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">Naomi understood this law and after learning of Boaz’s attention to Ruth, began to make a plan. In fact, the matchmaker told Ruth “I will not rest for thee, for that it may be well with thee” (Ruth 3:1).<br />
Naomi then instructed Ruth to get dressed up and to go into Boaz’s tent after he had eaten and went to bed. She told her to uncover his feet and lie down next to him, and then wait for him to tell her what to do. In this day and age, this seems like a very scandalous and strange thing to do but in their culture, this was acceptable. Ruth was taking advantage of the law and was purposing marriage to Boaz.<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">About Midnight Boaz woke up and was startled to find a woman lying next to him. He asked who she was; she replied “I am Ruth, thy handmaiden”. She was laying next to his feet in submission to him, showing that she was willing to serve him and to be an obedient wife. Normally, a man in this society proposed marriage by spreading his skirt, or robe, around his intended. So she asked him to spread his skirt over her and said “for thou are a near kinsman.”<br />
In Ezekiel 16:8, the Lord says: “Now when I passed by thee, and looked upon thee, behold, thy time was the time of love; and I spread my skirt over thee, and covered thy nakedness; yea, I sware unto thee, and entered into a covenant with thee, saith the Lord God, and thou becamest mine.”<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">Boaz accepted her as his own. Boaz then told her that he had heard of her story and all that she had done. He knew of her kindness to Naomi and of her character, he called her a <span class="yshortcuts" id="lw_1276649276_2">virtuous woman</span> and promised to seek her hand in marriage.<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">The next day, he went out to see Ruth's closest male relative. This man said that he could not marry Ruth and granted Boaz the right to marry her instead. I wonder if this kinsman was concerned that Ruth was from Moab. She was not an Israelite and there were religious and societal complications with a marriage like this.<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">Fortunately, this did not concern Boaz. He saw into the heart of Ruth and was only concerned with who she was and what she had become. They soon married and were blessed with a baby. Naomi became the grandmother and nursemaid to this child and was restored with great happiness. They named the child Obed. Obed was the father of Jesse, who was the father of David, who was a descendant of Jesus Christ.<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">The true meaning of the gospel comes out in this story. Boaz represents the Savior and Ruth represents us. Once we accept the gospel and turn away from our old life, the Lord will bring us in to his own. Ruth’s story shows us that participation in the kingdom of God is not decided by bloodlines but by our obedience to God’s will. Her humility and submission to Boaz demonstrates how we must also come to the Lord and ask for his blessings and entrance into his kingdom. It is only through the Lords good grace and works that makes this possible.<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">Boaz was Ruth’s kinsman. The Hebrew word for “kinsman” is “goel.” The Hebrew word for “Redeemer” is also “goel.” In Biblical times, these words were interchangeable. If a man was a kinsman, it was his duty to be a redeemer for his families’ inheritance. Boaz played a role very similar to the one that Jesus played for all mankind. Thus Boaz is a type of Christ’s love and redemptive power.<br />
</span><br />
<span style="font-size: large;">“Where you go, I will go…” With these words, Ruth sealed her fate. By seeking out the Savior with faith like Ruth, we too can secure our place with our Lord in Heaven.</span>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-79131628453410183752012-07-27T01:12:00.001-07:002012-07-27T01:12:41.025-07:00MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.1<a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/msichana-ndotoni-mwanguep21.html?spref=bl"></a><br />
<img alt="" class="spotlight" src="https://fbcdn-sphotos-a.akamaihd.net/hphotos-ak-snc7/581301_370720976320817_981641705_n.jpg" style="height: 113px; width: 168px;" /><br />
<div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.1.<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> GENEVIEVE aliwaangalia watoto wake mapacha na kujikuta akitabasamu, ujio wao duniani ulifuta machozi yake na kumuondolea aibu ya kuitwa mwanamke tasa kila alikokwenda. Alipoikumbuka safari ndefu aliyosafiri kuwatafuta watoto hao ghafla huzuni ikamuingia na kujikuta akilengwalengwa na machozi.<br />
<br />
Kabla hajaendelea sana na mawazo hayo mlango wa chumba ulifunguliwa, mume wake Phillip akatokeza nje akiwa amevaa shati lake jeupe, tai ya rangi ya kahawia na suruali iliyonyoshwa vizuri pamoja na viatu vilivyong’arishwa vyema, begani mwake alikuwa na begi la kompyuta yake ndogo.<br />
<br />
“Nini tena?”<br />
“Basi tu.”<br />
“Basi tu nini?”<br />
“Yaani kila siku ninapowaangalia Dorice na Dorica siamini kama hatimaye na mimi nina watoto tena wazuri kiasi hiki, badala ya kufurahi huwa naishia kuingiwa na huzuni.”<br />
<br />
“Mwaaa!” Phillip alimbusu mkewe kwenye paji la uso huku akitabasamu.<br />
“Asante.”<br />
“Usijali darling, ni jambo la kumshukuru Mungu. Usiiangalie sana historia, wewe furahia kwamba hatimaye sasa tuna watoto na leo wanakwenda kuanza darasa la kwanza kwa mara ya kwanza.”<br />
<br />
Phillip aliongea kwa sauti ya upole huku wote wawili wakiwaangalia watoto wao wazuri wa kike mapacha wakiwa wamekaa kwenye meza wakinywa chai, tayari walikuwa na miaka mitano, walikuwa na hamu kubwa ya kufika shuleni kuanza darasa la kwanza baada ya kusoma chekechea kwa miaka miwili.<br />
<br />
“Daddy!” Dorice alimuita baba yake.<br />
“Yes, darling.”<br />
“Guess what?” (Hebu buni kuna nini?)<br />
“What is it my sweetie!” (Nini mpenzi wangu?)<br />
“Today we are going to school!” (Leo tunakwenda shule.)<br />
<br />
“I know darling, make sure you do good in writing, reading and counting, okay?” (Najua mpenzi wangu, hakikisheni mnafanya vizuri kwenye kuandika, kusoma na kuhesabu, sawa?)<br />
“Yes daddy, I am going to be the first and Dorica the second.” (Sawa baba, mimi nitakuwa wa kwanza na Dorica wa pili.)<br />
<br />
“No! I will be the first and you the second.” (Hapana! Nitakuwa wa kwanza halafu wewe wa pili.) Dorica alijibu.<br />
Genevieve na Phillip wakacheka kwa sauti kisha kunyanyuka kwa pamoja mahali walipoketi kwenda kuwakumbatia watoto wao, wakawabusu na hapohapo kuanza kusali wakiwaombea wafanye vizuri shuleni.<br />
<br />
Zoezi hilo lilipomalizika, Phillip aliwaaga wote na kuwatakia siku njema kisha kutoka hadi nje ambapo aliingia ndani ya gari lake na kuondoka akiamini saa mbili kamili ikifika mke wake angewachukua watoto hadi barabarani ambako basi la shule lingepita na kuwabeba.<br />
<br />
Waliishi Upanga karibu kabisa na eneo la katikati la jiji la Dar es Salaam, lakini ofisini kwa Phillip ilikuwa ni maeneo ya Victoria kilomita kama ishirini hivi kutoka katikati ya jiji. Wakati watu wengi waliteseka kwenye msongamano wa magari asubuhi kwenda kazini sababu ofisi nyingi zilikuwa katikati ya jiji, yeye hakuelewa hata kama kulikuwa na msongamano, alipishana nao asubuhi akielekea kazini nje ya jiji.<br />
<br />
Baada ya kuingia tu ndani ya gari lake aliendesha kwa kasi ya kawaida akiwahurumia watu wa upande wa pili wa barabara ambao magari yao yalikuwa yamesimama bila hata kusogea mbele, kichwani mwake aliwaza sana juu ya watoto wake wa pekee Dorice na Dorica, wao ndiyo waliomfanya afanye kazi kwa nguvu sana kwa sababu hakutaka wapate shida maishani mwao.<br />
<br />
Katika umri wa miaka mitano tu tayari kila mmoja kwenye akauti yake ya Jumbo kwenye Benki ya CRDB alikuwa na kiasi cha milioni nane ambazo Phillip na mke wake walipanga kuendelea kuziongeza wakiwa wamedhamiria zifike milioni mia moja kwenye kila akaunti ya kila mtoto watakapokuwa na umri wa miaka kumi na minane.<br />
<br />
Mawazo hayo aliendelea nayo mpaka alipokuwa anakata kona kuingia ofisini kwake ambako aliegesha na kushuka, kabla hajaondoka simu yake ya mkononi ikalia, akifunga mlango aliibana kwa bega sikioni na kuanza kusikiliza taratibu akiwa bado hajaelewa ni nani aliyempigia kwani namba haikuonyesha jina bali maandishi “Call” peke yake ndiyo yaliyoonekana, ishara kuwa simu hiyo ilitoka nje ya nchi.<br />
<br />
“Naongea na Phillip?”<br />
“Ndiyo, nani mwenzangu?”<br />
“Huhitaji sana kufahamu jina langu, ila nimekupigia kukutaarifu kuwa kama kuna uwezekano naomba usiwapandishe watoto wako kwenye basi la shule, kuna bomu limetegwa ndani yake litalipuka muda mfupi tu wakishapanda, watakufa hapo hapo! Nimekupigia kwa sababu najua ni kiasi gani unawapenda watoto wako.” simu ikakatwa.<br />
<br />
Mwanzoni Phillip alidhani labda siku hiyo ilikuwa ni tarehe moja mwezi wa Nne, Siku ya Wajinga Duniani lakini alipoangalia saa yake mkononi alikuta ilikuwa ni tarehe tofauti. Upande mmoja wa moyo wake ukamwambia apuuze maneno hayo lakini upande mwingine ukamtaka ampigie simu mkewe haraka iwezekanavyo na kumsimulia habari hiyo ya kuogofya.<br />
<br />
Simu iliita sana lakini haikupokelewa, akaendelea kupiga tena na tena lakini hali ilikuwa hiyo hiyo. Akathibitisha haikuwa tabia ya Genevieve kutopokea simu yake hasa alipopigiwa na mume wake maana hawakuwa na tabia ya kupigiana simu zisizo na maana, hii ilimfanya Phillip aingie ndani ya gari lake haraka na kugeuza akiwa amepuuza hata muda wa kuwahi kazini, kwake familia kilikuwa kitu cha kwanza.<br />
<br />
Haraka akaanza kuendesha kuelekea mjini, hakwenda umbali mrefu akakutana na msongamano wa magari ambao wala ulikuwa hausongi mbele. Kwa mkono wa kuume akiwa ameshika usukani na kwa mkono wa kushoto simu ikiwa sikioni akiendelea kuwasiliana na Genevieve bila mafanikio, bado simu ilikuwa haipokelewi.<br />
<br />
Alipofika maeneo ya Morocco aliamua kuiingiza gari yake kwenye kituo cha mafuta cha Bonjour, kando tu mwa kibanda ambacho hutumika kuuza baga, akashuka haraka na kukimbia upande wa pili ambako alimkodisha mtu wa Bajaj aliyekuwa akipita na kumtaka amwahishe haraka sana mjini.<br />
<br />
Akiwa ndani ya Bajaj aliendelea kupiga simu huku wasiwasi wake ukiendelea kuongezeka, isingewezekana mke wake muda wote huo awe mbali na simu. Hakumpata Genevieve na Bajaj ilikuwa ikienda kwa mwendo mdogo sana, alipofika eneo liitwalo Mbuyuni alilazimika kumlipa dereva wa Bajaj ujira wake, akashuka na kukodisha pikipiki hiyo ndiyo ilimpeleka moja kwa moja hadi nyumbani kwake.<br />
<br />
“Genevieve! Genevieve!” Aliita akigonga mlangoni lakini hakuitikiwa na mlango ulikuwa umefungwa.<br />
Akaendelea kupiga simu, alipousikia mlio kutoka ndani tena sebuleni, alielewa mke wake alikuwa ameisahau simu ndani na kupeleka watoto barabarani. Haraka akarukia juu ya pikipiki na kumwamuru dereva aondoke kwenda barabarani mahali ambapo basi la shule hupita kuchukua wanafunzi.<br />
<br />
Walipokaribia eneo hilo aliliona gari la mke wake likiwa limeegeshwa kando ya barabara, yeye mwenyewe akiwa amesimama nje akiliangalia gari la shule likiondoka mwendo wa taratibu, tayari Phillip akawa amefika na kuruka kwenye pikipiki. Genevieve alipomuona alishituka sana.<br />
<br />
“Nini tena?”<br />
“Watoto wako wapi?”<br />
“Wako kwenye gari la shule.”<br />
“Mungu wangu!”<br />
“Nini?”<br />
<br />
Phillip akadandia tena pikipiki na kumwamuru dereva aanze kulifuata basi la shule wakimwacha Genevieve mahali alipokuwa, hawakwenda mbali sana, gari likiwa umbali wa kama mita hamsini kabla hawajalifikia, walisikia kishindo cha ajabu “Puuuuuu”. Wakaanguka chini, gari la wanafunzi lilikuwa limelipuliwa na bomu.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Nani amefanya unyama huu? Dorice na Dorica wamekufa?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.2.<br />
<br />
<br />
Ilikuwa ni familia yenye furaha, Genevieve na mume wake Phillip wakiwa na watoto wao mapacha Dorice na Dorica, watoto wa kike wenye sura za kuvutia ambao walifanana kupita kiasi. Ilikuwa ni kazi ngumu hata kwa wazazi wao kuwatofautisha. <br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Watoto hawa ndiyo walikuwa mzizi wa furaha ndani ya nyumba ya Genevieve na Phillip. Waliwapata kwa taabu mno, ndiyo sababu waliwapenda kupita kiasi. Asubuhi hii ya leo, Dorice na Dorica wakiwa na umri wa miaka mitano ndiyo wanapelekwa kwa mara ya kwanza shuleni kuanza darasa la kwanza baada ya kusoma chekechea kwa muda wa miaka miwili. <br />
<br />
Phillip ameamka asubuhi na kujiandaa kwa ajili ya kwenda kazini huku mke wake ambaye tangu ajifungue watoto hawa alikuwa mama wa nyumbani, aliwaandaa Dorice na Dorica tayari kwa shule. Phillip akampiga mke wake busu, vivyo hivyo watoto na kuwaaga akifahamu mke wake angewapeleka barabarani ambako wangechukuliwa na gari la shule muda ukifika, akaondoka zake kuelekea kazini.<br />
<br />
Waliishi Upanga lakini kazini kwa Phillip ilikuwa ni maeneo ya Victoria, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam hivyo yeye hakuwa na msongamano wa magari kuelekea kazini kwani wengi walielekea mjini kila asubuhi.<br />
<br />
Akiwa nje ya jengo la ofisi yake, simu yake ililia, akaipokea na kuongea na mtu aliyekuwa akipiga kutoka nje ya nchi. Hakuwa tayari kutaja jina lake, akampa taarifa kuwa ikiwezekana wasiwapakie watoto wao ndani ya gari la shule kwani lingelipuliwa kwa bomu.<br />
<br />
Mwanzoni Phillip alidhani ni utani lakini alipoamua kumpigia simu mke wake, ikawa inaita bila kupokelewa, moyoni akaingiwa na wasiwasi hivyo kuamua kugeuza kuelekea nyumbani ili amuwahi kabla hajawapeleka watoto barabarani kupanda basi la shule.<br />
<br />
Haikuwa rahisi, kwani pamoja na kuliacha gari lake na kukodisha Bajaj ambayo pia aliiacha na kukodisha pikipiki, alifika nyumbani na kumkosa mke wake, aliamua kumfuata barabarani ambako alikuta basi ndiyo kwanza limeondoka. Akamwamuru mwenye pikipiki alifuatilie kwani halikuwa mbali, lengo likiwa ni kuwashusha watoto.<br />
<br />
Walipolikaribia basi hilo, ikiwa ni mita chache tu walisikia mlipuko mkubwa, basi lilikuwa limelipuliwa na bomu.<br />
Je, nini kitaendelea? Nani kafanya unyama huu? Kwa nini? SONGA NAYO…<br />
<br />
Mlipuko huo uliwafanya Phillip na mwendesha pikipiki waanguke kando ya barabara, fahamu za Phillip zikapotea. Alipozinduka alijikuta kitandani, mkononi akiwa na dripu iliyodondosha matone kwa haraka kuingiza kwenye mishipa yake. Awali hakuelewa ni kwa nini alikuwa pale lakini alipotulia ndipo akakumbuka picha nzima ya tukio la kulipuka kwa basi lililobeba wanafunzi, wakiwemo watoto wake Dorice na Dorica.<br />
<br />
“Mamaaaaa! Watoto wanguuu! Nani amefanya kitendo hiki? Nitamjua,” aliongea kwa sauti ya juu huku akilia, wauguzi wakafika haraka na kuanza kumtuliza.<br />
<br />
Faraja zao hazikusaidia, alitaka aoneshwe mahali mke wake Genevieve alipokuwa. Wauguzi hawakuwa tayari, moyoni akaingiwa na wasiwasi kuwa huenda hata yeye alikuwa marehemu. Phillip akiwa kama mtu aliyechanganyikiwa, alinyanyuka kitandani na kusimama wima, dripu ikachomoka.<br />
<br />
Hakutaka kuongea kitu kingine zaidi, akatoka kuanza kukimbia kuelekea barabara ya Umoja wa Mataifa, karibu kabisa na Shule ya Al-Muntazir, ambako basi lililobeba wanafunzi lililipukia. Mbele kidogo alisimamisha gari ambalo kwa juu liliandikwa “Taxi”, likaegesha pembeni naye akaingia na kuketi kiti cha mbele kando ya dereva aliyemwangalia kwa jicho la wasiwasi.<br />
<br />
“Wapi braza?”<br />
“Pale chini.”<br />
“Wapi?”<br />
“Wewe twende.”<br />
<br />
“Nipe kabisa changu,” dereva alisema baada ya kuhisi abiria wake asingemlipa kwani alionekana ni mtu aliyechanganyikiwa.<br />
“Shilingi ngapi?”<br />
“Niambie kwanza unakwenda wapi.”<br />
<br />
“Kwenye basi lililolipukiwa na bomu.”<br />
“Ahaa! Shilingi elfu moja.”<br />
Phillip akaingiza mkono mfukoni na kukuta bahati nzuri pochi yake ilikuwepo, akaitoa na kuchomoa noti ya shilingi elfu kumi na kumkabidhi dereva wa teksi. Safari ikaanza kuelekea Al-Muntazir, mbele kidogo walikuta msongamano wa magari, barabara ilikuwa imefungwa kwa sababu ya ajali hiyo.<br />
<br />
Phillip akashuka bila hata kudai chenji yake na kuanza kukimbia kwenda mbele. Mtu yeyote aliyemwona lazima alijua akili yake haikuwa sawa, hakujali, akazidi kukimbia akimfikiria mke wake na pia watoto wake. Kila kitu kilichotokea kwake kilikuwa ni ndoto, isingewezekana hata kidogo watoto wake wazuri, tena mapacha, waliofanana kila kitu kwa sura kuwa wamekufa ghafla kiasi hicho?<br />
<br />
Alijiuliza bila kupata majibu akiamini muda si mrefu angezinduka ili amsimulie mke wake Genevieve ndoto hiyo, lakini ukweli haukubadilika. Alifika eneo la tukio na kukuta magari ya zimamoto na mamia ya watu wakiwa wamekusanyika kushuhudia kilichotokea. Lilikuwa tukio baya na polisi walikuwa kila mahali wakizuia watu kupita. <br />
<br />
Hawakuweza kumzuia Phillip ambaye alipenya mpaka mbele na kuanguka chini akilia baada ya kuyaona mabaki ya watoto wazuri waliokufa kinyama, kiatu kimoja cha Dorica alikitambua, pia chupa ya chai ya Dorice aliyowekewa maziwa na mama yake ilikuwa juu ya lami.<br />
<br />
Miili ya watoto wote ilikuwa imelazwa juu ya ardhi ikiwa imefunikwa na mashuka meupe, haikuwa rahisi hata kidogo kuitambua kwani iliharibika kupita kiasi. Phillip akanyanyuka na kuanza kuzunguka kwenye miili hiyo akifunua ili angalau aweze kuwaona watoto wake. Hapakuonekana mwili wa Dorice au Dorica, miili iliyokuwepo ilikuwa imesambaratishwa na kubaki kiungo kimoja kimoja.<br />
<br />
“Nani amefanya unyama huu? Nitamjua, sitarudi kazini mpaka siku nitakapomtia mikononi mwangu,” alijisemea Phillip akilia, kisha akakaa chini na kuanza kuiangalia miili hiyo huku akimfikiria mke wake Genevieve ambaye mpaka wakati huo alikuwa hajamwona.<br />
<br />
Siku iliyoanza vizuri hatimaye ilikuwa imeharibika, watu walikuwa wakilia kwa uchungu mkubwa, lilikuwa ni tukio baya kuliko jingine lolote kutokea. Phillip hakuwa tayari kuongea na waandishi wa habari walipomfuata. Tayari wazazi wa watoto wote waliokufa walikuwa eneo hilo, vilio vilienea. <br />
<br />
Baadaye miili ilianza kubebwa na kuingizwa kwenye gari tayari kupelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Muhimbili. Phillip aliamua kutangulia huko ili akaone mahali ambapo watoto wake wangelazwa. Alifika wakati magari yameshawasili, watu wengi wakiwa wamekusanyika na wafanyakazi wenzake ambao tayari walishapata habari walikuwepo kumfariji lakini alikuwa hafarijiki.<br />
<br />
“Jamani nisaidieni kujua mahali mke wangu alipo,” aliwaomba.<br />
Badala ya kumjibu au kusema chochote, wafanyakazi wenzake walikaa kimya, jambo lililoonesha kabisa walikuwa na kitu moyoni. Wasiwasi wa Phillip ukaongezeka, hakuelewa maisha yake yangeendeleaje bila kuwa na familia. Alikitamani kifo kama ingethibitika kuwa, watu wote aliowapenda hawakuwepo duniani.<br />
<br />
“Jamani niwaulize kama mnaweza kuwa mnafahamu mahali aliko Genevieve.”<br />
“Tunajua lakini...”<br />
“Lakini nini jamani, hebu nielezeni tu mahali aliko mke wangu, amekufa? Kwa mshtuko huu ukizingatia ana shinikizo la damu, anaweza kuwa amenitoka.<br />
<br />
Nitafanyaje mimi? Nitaishije mimi? Eee Mungu, ni kwa nini umeruhusu nipite kwenye jambo hili wakati unaelewa moyo wangu ni mdogo?” Aliuliza maswali mengi akiwa ameshikiliwa na wafanyakazi wenzake walioonekana kuwa na siri nzito mioyoni mwao.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.3.<br />
<br />
Familia yenye furaha, ya Phillip na mke wake Genevieve pamoja na watoto wao mapacha, Dorice na Dorica inapatwa na balaa ambalo hawakuwahi kulitegemea maishani mwao. <br />
<br />
Watoto hawa wawili waliokuwa mzizi wa furaha yao, baada ya kuhangaika kwa muda mrefu kuwapata wanasindikizwa na mama yao kwenda stendi ya basi ambako wanapanda basi la kuwapeleka shule; ni siku ya k<span class="text_exposed_show">wanza shuleni wakiwa darasa la kwanza baada ya kusoma chekechea na kumaliza. <br />
<br />
Phillip aliamka asubuhi na kuwapiga busu watoto wake wote wawili pamoja na mkewe, kisha kuondoka kuelekea kazini. Alipoegesha tu gari lake nje ya jengo la ofisi yao, simu yake ililia, akaangalia kwenye kioo na kukuta pameandikwa neno “Call” bila kuonyesha namba, akajua namba hiyo ilitoka nje ya nchi. Haraka akaipokea.<br />
<br />
Sauti aliyokutana nayo ilikuwa ya kukwaruza, ikimtaarifu kuwa kama kuna uwezekano asiwapandishe watoto wao kwenye gari la shule kwani kulikuwa na bomu lililotegwa ndani yake ambako lingelipuka wakati wowote na kuua watu wote waliokuwa ndani yake.<br />
<br />
Awali alizichukulia taarifa hizo kama utani, lakini baadaye akaamua kumpigia simu mke wake ili ampe taarifa hiyo asiwapeleke watoto kwenye gari la shule. Simu iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa, akaendelea tena na tena, hali ikawa ileile. Mwisho akafikia uamuzi wa kuendesha gari kurejea nyumbani. <br />
<br />
Hakwenda mbali sana kabla hajakutana na msongamano mrefu wa magari, akaamua kuliegesha la kwake pembeni na kuchukua Bajaj ambayo nayo ilishindwa, akalipa kisha kushuka na kuchukua pikipiki iliyomfikisha hadi nyumbani ambako hakumkuta mke wake ingawa simu iliiita kutoka chumbani.<br />
<br />
Akalazimika kumwamuru mwendesha pikipiki ampeleke hadi stendi ambako walimkuta mke wake akiliangalia gari lilivyoondoka, akashituka kumwona Phillip pale wakati alishaondoka kwenda kazini. Akawaulizia watoto, jibu alilopewa ni kwamba wameondoka na gari lililokuwa mita kama hamsini hivi kutoka waliposimama, Phillip akamwamuru mwendesha pikipiki alifuate.<br />
<br />
Kabla hawajalifikia gari hilo lililipuka vibaya, Phillip akazimia, alipozinduka alikuwa hospitali na kuondoka kurejea eneo la tukio ambako alikuta polisi wamekwishafika na magari ya zimamoto. Miili ya watoto iliyosambaratishwa kiasi cha kutokutambulika ilikuwa ikiondolewa kwenye gari lililowaka moto na kupelekwa chumba cha kuhifadhia maiti.<br />
<br />
Phillip akalia kwa uchungu na kuamua kufuatilia hospitalini, huko aliendelea kulia akiuliza ni wapi mke wake alipokuwa. Lilikuwa tukio la kusikitisha, siku iliyoanza vizuri sasa ilibadilika na kuwa mkosi.<br />
Je, nini kitaendelea? Nani amefanya unyama huu? Yuko wapi mke wa Phillip? SONGA NAYO…<br />
<br />
Wafanyakazi wenzake waliomzunguka wakiwa wamemwekea mikono mabegani na kumbembeleza ili asimame imara kama mwanaume katika kipindi hicho kigumu, hawakuwa na la kufanya aliposisitiza aonyeshwe mke wake. Wote walimuonea huruma, mmoja wao akaondoka hadi ofisini kwa daktari aliyempokea Genevieve alipofikishwa hospitali kutoka eneo la ajali.<br />
<br />
“Hakuna shida mpelekeni tu.” Alijibu Dk. Anorld Mapunjo.<br />
“Asante daktari, sisi tulikuwa tunaogopa kwa kudhani pengine tunaweza kumsababishia matatizo yale yale pia.”<br />
<br />
“Haina tatizo, kama ameweza kustahimili mshituko uliompata baada ya kuona gari linalipuka, hakuna kinachoweza kumletea matatizo tena. Si alikuwa amelazwa wodi ya Mwaisela?”<br />
“Ni kweli lakini aliporejewa na fahamu, aliondoka hospitalini hadi eneo la tukio, huko ndiko tulikokutana naye.”<br />
<br />
“Mpelekeni tu.”<br />
Reginald, rafiki mkubwa wa Phillip waliyefanya naye kazi kitengo cha uhasibu alirejea mahali alipowaacha wenzake na kuwapa taarifa ya daktari, wakaondoka pamoja hadi kwenye jengo lililoandikwa mlangoni Muhimbili Intensive Care Unit, kando kukiwa na maneno ya Kiswahili; Kitengo cha Wagonjwa Mahututi. Wakagonga mlangoni, muuguzi akafungua mlango.<br />
<br />
“Sista samahani.”<br />
“Bila samahani.”<br />
“Tumemleta huyu kaka ni mume wa Genevieve.”<br />
“Karibuni.”<br />
<br />
Huku akibubujikwa machozi na mwili wake kutetemeka, Phillip aliongozwa na rafiki zake akiwa ameshikiliwa kila upande na kuingizwa ndani ya jengo hilo na kuongozwa hadi kwenye chumba kilichokuwa kando, mlango ukafunguliwa tena na wote wakaingia ndani. Macho yake yakaenda moja kwa moja kitandani; Genevieve alikuwa amelala hapo akiwa hajitambui.<br />
<br />
Uso wake ukiwa umefunikwa na tabasamu kama vile alikuwa amelala macho yake yakiwa yamefungwa akikoroma na kuhangaika kuhema ingawa alikuwa akitumia mashine.<br />
<br />
Uchungu mkali ukauchoma moyo wa Phillip na machozi mengi yakamtoka, nguvu zikamwishia miguuni na kujikuta anaketi chini moyoni mwake akiilaani siku hiyo, kwamba haikustahili kabisa kuwemo katika orodha ya siku za dunia, ilikuwa mbaya na asingeisahau maisha yake yote.<br />
<br />
Nusu saa baadaye alijikakamua na kusimama wima, akasogelea kitanda na kuinamisha kichwa chake mpaka karibu kabisa na shavu la Genevieve, matone ya machozi yakadondoka kutoka kwenye ncha ya pua yake na kutua shavuni kwa mkewe. Mdomo wake ukamgusa shavuni, bila kuchelewa akampiga busu na Genevieve akatoa tabasamu la siku zote. <br />
<br />
Phillip alikuwa bado haamini kilichotokea, isingewezekana hiyo iwe kweli, alihisi labda alikuwa akiota ndoto au kuangalia sinema fulani ya kutisha iliyochukua kabisa hisia zake. Huo uliendelea kubaki ukweli akimwangalia Genevieve kitandani na kuwafikiria watoto wake waliosambaratishwa na mabomu, hasira ikapanda, akamchukia mtu aliyefanya hivyo na kutamani kukutana naye ana kwa ana. <br />
<br />
“Mke wangu, naomba usife, baki hai ili tumtafute pamoja mtu aliyefanya unyama huu wa kuwateketeza watoto wetu tuliowapenda kuliko kitu kingine chochote. Kama utakufa, basi tangulia ili mimi niikamilishe hii kazi.<br />
Nakupenda Genevieve.” Phillip aliongea kwa sauti ya upole, watu wote waliokuwemo chumbani wakajikuta wanachukua vitambaa vyao na kujifuta machozi, ilikuwa ni taswira mbaya mno kuishuhudia.<br />
<br />
Genevieve alikuwa amelala kitandani akiwa hajitambui, mashine ndiyo zilimsaidia kuhema na hata moyo wake kupiga. Pamoja na hali hiyo bado urembo wake ulionekana wazi, hakika alikuwa msichana mzuri kupindukia. Hakuna mwanaume angemuona akaacha kutamani kuwa naye maishani, wengi walikuja kwake kabla, lakini aliyekuwa na bahati hiyo ni Phillip peke yake. <br />
<br />
Kichwani mwa Phillip kuliendelea mawazo mengi, aliikumbuka tangu siku waliyokutana mara ya kwanza maeneo ya Posta jijini Dar es Salaam na kushangaa kama kweli msichana ambaye siku zote alimuota katika ndoto kumbe alikuwepo katika ulimwengu halisi, kabla hajaendelea sana na mawazo hayo mlango ukafunguliwa, akaingia Dk. Mapunjo akiongozana na mwanaume mrefu aliyenyoa mtindo wa panki.<br />
<br />
“Karibu baba, pole sana, tumepata tatizo kubwa, watoto wetu wote wamekufa na mke wangu yuko taabani hapa kitandani.” Phillip aliongea akikumbatiana na mwanaume huyo.<br />
“Usijali mwanangu, ndiyo dunia!”<br />
<br />
Alikuwa ni mzee Mpangal Anthony, mzazi wa Genevieve. Taarifa za kulipuka kwa bomu, vifo vya watoto na kuanguka kwa mwanaye na kupoteza fahamu alizipata akiwa nyumbani kwake maeneo ya Mbezi Beach na kuamua kwenda hospitalini kushuhudia mwenyewe. Pamoja na utu uzima wake, akiwa ameshuhudia mambo mengi duniani, kitendo cha kumwona amelala kitandani akiwa taabani, kilimfanya ashindwe kujizuia; machozi yakamtoka.<br />
<br />
“Mzee Mpangal, jikaze, tunakutegemea wewe ututie nguvu.” Ilikuwa ni sauti ya Dk. Mapunjo.<br />
“Inauma daktari.”<br />
“Pole sana.”<br />
<br />
Phillip alihisi kuchanganyikiwa, alishindwa kuelewa aumizwe na kipi; kufa kwa watoto wake ama hali mbaya ya mke wake kitandani. Alijisikia kama vile amesimama katikati ya mawe mawili makubwa yote yakitaka kumgandamiza yeye. Ilikuwa ni lazima asimame imara; vinginevyo angeweza kukatisha uhai wake. Hili liliwafanya ndugu wakae naye karibu muda wote.<br />
<br />
Hakuondoka wodini tangu alipoingia, muda wote alikuwa pembeni ya kitanda cha mke wake, hakupata hata lepe la usingizi au kufumba jicho kwa siku tatu mfululizo akiangalia kama Genevieve angefumbua macho yake, hilo ndilo jambo alilolisubiri kwa hamu kubwa.<br />
<br />
Baadaye alipata taarifa za ndugu zake wakiongozwa na Mzee Mpangala kukabidhiwa mabaki ya watoto wake kwa ajili ya mazishi, lakini habari zikasambaa kwamba ndugu waligawiwa vipande vilivyopatikana ili wakazike majumbani kwao bila uhakika kama kweli waliomchukua ni ndugu yao. Haukuwepo uwezekano wa kupima vinasaba vya DNA.<br />
<br />
“Baba naomba msizike mpaka mke wangu azinduke, najua Genevieve atazinduka ili aweze kushuhudia mazishi ya watoto wake.” Phillip aliongea kwa simu na mzee Mpangal huku akibubujikwa na machozi.<br />
<br />
“Lakini hali ni mbaya. Nashauri tuzike, Genevieve akirejewa na fahamu tutamwambia kilichotokea, bila shaka ataelewa.”<br />
“Hapana baba, nataka mke wangu ashuhudie watoto wake wakizikwa.”</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124ba4b634c4643622514">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.4.<br />
<br />
Juhudi zote za Mzee Mpangal kuhakikisha mabaki ya watoto yanazikwa ziligonga mwamba, Phillip aliendelea kusisitiza mke wake ni lazima azinduke na kuwashuhudia wapendwa wake Dorice na Dorica wakizikwa. <br />
Mzee Mpangal alishindwa tu kumueleza ukweli kuwa hata mabaki waliyopewa hakuwa na uhakika kama kweli walikuwa ni wajukuu zake, maana alikabidhiwa viwiliwili vya wa<span class="text_exposed_show">toto bila kichwa wala miguu.<br />
Hakutaka kabisa mwanaye ashuhudie picha hiyo lakini Phillip alipong’ang’ania ilibidi mzee atulie na kusikiliza maamuzi ya mzazi, mabaki yakarejeshwa tena chumba cha kuhifadhia maiti kusubiri Genevieve azinduke ndipo mazishi yafanyike.<br />
<br />
Phillip aliendelea kubaki wodini, karibu kila siku akilia, ulikuwa ni msiba mkubwa mno kwake. Juhudi za marafiki kumfariji zilikuwa zimeshindikana, alikuwa kando ya kitanda cha mke wake akiangalia kila kilichoendelea, ndani ya masaa ishirini na sita tu tangu mlipuko utokee alikuwa amepoteza uzito mkubwa sana wa mwili wake.<br />
<br />
Kichwani mwake yaliendelea maswali mengi yasiyo na majibu, nani alilipua basi? Kwa nini aliua watoto wasio na hatia? Je, kama kilikuwa ni kisasi mkosaji alikuwa ni yeye au wazazi wa watoto wengine? Moyoni akatamani kukutana na mtu aliyefanya ukatili huo bila kujali alikuwa analipa kisasi kwa nani. Ilikuwa ni lazima afahamu ukweli siku moja hata kama gharama ingekuwa ni uhai wake mwenyewe.<br />
<br />
“Tatizo Genevieve, angekuwa mzima hivi sasa ningekuwa nimeshapanga namna ya kumtafuta mtu huyo mbaya… hata hivyo ipo siku ataingia mikononi mwangu.” Alisema akijifuta machozi.<br />
Usiku na mchana alikuwa macho, mara nyingi akimwangalia Genevieve aliyekuwa akipumua kwa msaada wa mashine huku akikoroma, madaktari walisema shinikizo lake la damu lilikuwa juu sana na lilikuwa limegoma kabisa kushuka, mshituko alioupata ndiyo uliosababisha hali hiyo.<br />
<br />
Alfajiri ya siku ya nne ndipo alipoliona tabasamu la mke wake lililokuwa limepotea, hakuamini kama kweli macho yake yalikuwa yakimpa usahihi wa alichokiona. Ikabidi asogee karibu na kuthibitisha, moyo wake ukajaa furaha, akapiga magoti chini na kusali akimshukuru Mungu. Ghafla Genevieve akafumbua macho na kuangalia kila upande kama mtu aliyekuwa akijaribu kutambua mahali alipokuwa. <br />
<br />
“Genevieve! Genevieve!” Akaita lakini hakuitikia.<br />
Haraka akatoka akikimbia mpaka kwenye chumba cha wauguzi ambao aliwapa taarifa ya kilichotokea, nao katika hali ya kutokuamini wakaungana naye kukimbia hadi chumbani. Wakamkuta Genevieve amekaa kitandani kama vile hakuwa taabani muda mfupi tu uliopita, Phillip akaingiwa na furaha ambayo maelezo yake hayakuwepo, hali iliyosababisha machozi zaidi kumbubujika kwani kilichotokea kilikuwa ni muujiza.<br />
<br />
“Genevieve! Genevieve mke wangu, mimi ni Phillip, unanisikia?” Aliuliza lakini mke wake aliendelea kuwa kimya.<br />
“Mpigie simu Dk. Mapunjo umpe taarifa hii, mmoja wa wauguzi alisema.<br />
“Sawa acha nikampigie,” alijibu na kuondoka akikimbia, ingawa alivaa raba zilisikika vizuri sakafuni wakati akitimua mbio kuelekea ofisini.<br />
<br />
Baada ya muuguzi kuondoka, Phillip aliendelea kumwita mke wake lakini hali ilikuwa ni ile ile, hakuitika na aliendelea kuangaza huku na kule kama vile wafanyavyo watu wenye ulemavu wa kuona. Dakika ishirini baadaye muuguzi alirejea akiongozana na Dk. Mapunjo, alipomtazama Genevieve alifurahi na kuanza kumfanyia vipimo mbalimbali, akathibitisha kabisa kwamba shinikizo lake la damu lilikuwa limeshuka kufikia kiwango cha kawaida.<br />
<br />
“Sasa kwa nini namwita haitiki na hata nikimsogezea kidole machoni ingawa amefumbua macho hapigi kope?”<br />
“Hilo ndilo tatizo ambalo nimeligundua, mkeo amepatwa na tatizo jingine ambalo limetokana na shinikizo la damu kupanda sana, hivyo kuharibu vituo kwenye ubongo vinavyohusika na kuona pia kusikia, ni habari ya kusikitisha lakini ni bora nikwambie ukweli kwamba mkeo hataweza kuona wala kusikia tena maishani mwake.”<br />
“Mungu wangu!” Phillip alisema kwa huzuni.<br />
<br />
Hakuweza hata kusimama, akasogea pembeni kwenye kiti na kuketi kisha kuinamisha kichwa chake katikati ya magoti. Machozi yakaanza kudondoka taratibu na kulowanisha sakafu huku akiupitia mchakato mzima wa maisha yake, tangu alipozaliwa mpaka siku hiyo akiwa amefiwa na watoto wake wote kwenye mlipuko wa bomu ambao miili yao ilikuwa bado imehifadhiwa chumba cha maiti na sasa alikuwa amepokea taarifa kuwa, mke wake angekuwa kipofu na kiziwi maisha yote.<br />
<br />
Zilikuwa habari mbaya za kutosha kabisa mtu mwingine kufikiria kukatisha uhai wake. Phillip hakuuona huo kama uamuzi wa busara, asingeweza kujiua na kumwacha mke wake akiteseka, isitoshe alikuwa na kazi nzito ya kumtafuta mtu aliyetega bomu ndani ya basi na kuwaua pamoja na watoto wa wazazi wengine.<br />
<br />
Huyo ndiye aliyekuwa adui yake mkubwa, hakutaka kumwacha duniani akila starehe wakati aliwasababishia watu wengine uchungu, akaapa kumsaka kwa udi na uvumba kila kona ya dunia mpaka amtie mkononi. Ni kweli hakuwa mpelelezi lakini sasa ilimlazimu kuifahamu kazi hiyo ili aweze kukamilisha kazi yake kwa heshima ya watoto na mke wake.<br />
<br />
“Dorice! Dorica! Leteni viatu vyenu niwavalishe ili niwapeleke shule, leo ni siku ya kwanza ya darasa la kwanza, hamjafurahi? ” Genevieve alitamka maneno yaliyoonesha kabisa hakuwa na taarifa hata ya mahali alipokuwa na hakujua kilichotokea maishani mwake, moyo wa Phillip ukaumia zaidi.<br />
<br />
***<br />
Militon Lukinda alipandisha kwa kasi, alikuwa hatarini kuchelewa kikao cha asubuhi hiyo ambako yeye na wenzake Jacob Mkonyi na Albert Shitugugu walikuwa na kazi ya kuwakilisha taarifa walizozipata kwenye eneo la tukio ambako bomu lililipuka.Vijana hawa watatu ndiyo walikuwa na mwezi mmoja tangu warejee kutoka Houston, Texas, Marekani walikokwenda kuchukua kozi ya uchunguzi wa eneo ilipofanyika jinai, kwa lugha ya Kiingereza iliitwa Crime Scene Investigation.<br />
<br />
Serikali ya Tanzania iliamua kuwapeleka vijana hao kusomea elimu hiyo ili waweze kusaidia kwenye matukio mbalimbali ya ulipuaji wa mabomu yaliyojitokeza kwa sababu ya ugaidi. Hii ilikuwa ni baada ya Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania kulipuliwa na mtandao wa kigaidi wa Al Qaeda. <br />
<br />
Kazi yao ya kwanza tangu waingie nchini wakiwa na elimu ya kutosha ilikuwa ni mlipuko wa basi la wanafunzi, lililoteketeza jumla ya watoto kumi na nane waliokuwa wakipelekwa shuleni. Muda mfupi tu baada ya mlipuko huo, Milton na wenzake walifika na kulizungushia eneo hilo kamba maalum ili watu wasivuruge ushahidi kisha wao wakaanza kupiga picha na kuchukua vitu mbalimbali ambavyo vingewasaidia katika uchunguzi wao.<br />
<br />
Walichukua vipande vya bomu, nywele za watoto, mabaki ya nguo na hata damu iliyotapakaa katika baadhi ya sehemu na kwenda nazo moja kwa moja maabara ambako walimkabidhi Mzee John Simba, bingwa wa uchunguzi wa matukio kama hayo aliyepata elimu yake pia nchini Marekani na kufuzu kwa kiwango cha kuitwa Forensic Scientist.<br />
<br />
Asubuhi hiyo ndiyo siku ambayo ripoti ilikuwa inatolewa ili kuweza kujua ni aina gani ya bomu lilitegwa, pengine mtegaji alikuwa nani kama aliacha alama yoyote kwenye gari na kufahamu idadi ya watoto waliokufa ili umma uweze kutangaziwa.<br />
<br />
Aliufikia mlango ulioandikwa Crime Scene Investigation Bureau na kuufungua, kisha kunyoosha moja kwa moja hadi kwenye chumba cha mikutano. Alikuta watu wote wamekwishaketi ingawa kikao kilikuwa hakijaanza, naye akachukua nafasi yake na kutulia.<br />
<br />
Haukupita muda mrefu sana mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai, Kamishna Pius Kalinga aliingia na kuketi kwenye kiti chake kisha kukifungua kikao na kuomba Mzee Simba aanze kutoa taarifa ya uchunguzi alioufanya maabara ili kazi ya kumtafuta muuaji ianze mara moja.<br />
<br />
“Asante sana kamishna, kwanza kabisa nianze kwa kusema watoto waliokufa katika mlipuko huo si kumi na nane kama inavyodaiwa, vipimo vya damu na alama za vidole nilivyovifanya kwa kutumia sampuli nilizoletewa na wapelelezi, zinaonesha watoto waliokuwa ndani ya gari hilo wakati linalipuliwa ni kumi na sita!”<br />
“Mh!” Watu wote wakaguna.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Kama watoto walikuwa kumi na nane kwa nini Mzee Simba anadai waliokufa ndani ya gari walikuwa kumi na sita? Wengine wawili wako wapi? Je, muuaji ni nani na kwa nini aliwaua? Nini kitaendelea katika maisha ya Phillip na mke wake Genevieve ambaye hivi sasa amepata upofu na uziwi?</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124ba4b4ef52726677750">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.5.<br />
<br />
<br />
“UNA hakika walikuwa watoto kumi na sita tu?” Kamishna wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai alisema.<br />
“Kabisa, hivyo ndivyo nilivyogundua, ipo sababu ya kuzungumza na wazazi kuona kama kuna watoto hawakupandishwa, huenda watoto wengine hawakwenda shuleni siku hiyo lakini viongozi wa shule wakaendelea kuelewa basi lilibeba watoto kumi na nane,” Mzee Simba aliongea k<span class="text_exposed_show">wa kujiamini.<br />
<br />
“Tutahitaji kwenda shuleni kuongea na wazazi ili tuone idadi ya wazazi waliofiwa na watoto wao, hapo ndio tutapata jibu la uhakika… endelea...”<br />
<br />
“Bomu lililotumika ni la kutengeneza nyumbani na limetumia mtungi wa gesi aina ya compressed gas, madini ya Uranium 235 na Plutonium 239, pia kemikali ya Nitroglycerine. Cha muhimu hapa kama tunataka kumpata mtu aliyetega hili bomu ni lazima tufahamu mahali aliponunua Uranium na Plutonium.”<br />
<br />
“Kuna alama zozote za vidole?”<br />
“Hakuna, watu waliofanya kazi ya kutega bomu hili ni wataalam haswa kwani hawakuacha alama yoyote inayoweza kufanya wakakamatwa.”<br />
<br />
“Duh! Tuachie sisi kazi ya upelelezi, ninachotaka kifanyike mara moja ni kwenda shuleni kuthibitisha kama watoto waliokufa ni kumi na sita au kumi na nane, haiwezekani watoto wawili wakawa hawajulikani walipo na pia tupate kufahamu bomu lilitegwaje ndani ya gari, muelewe mahali ambako huwa linalazwa ili kama kuna mlinzi katika eneo hilo basi ahojiwe, lazima atakuwa anahusika,”<br />
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai aliongea na watu wote wakaitikia.<br />
<br />
Huo ukawa ndiyo mwisho wa kikao, watu wote wakasambaa wakiwa na nakala za taarifa iliyotolewa na watu wa Uchunguzi wa Vielelezo. <br />
Hakuna aliyekuwa na picha kamili kichwani mwake juu ya nani hasa alikuwa mhusika wa kutega bomu hilo, sababu ilikuwa ni ipi iliyopelekea watoto kumi na nane au kumi na sita wasio na hatia kuuawa kikatili kiasi hicho.<br />
<br />
Shule ya Kimataifa ya Holy Ghost ambako watoto Dorice na Dorica walitakiwa kuanza darasa la kwanza ilikuwa imegubikwa na msiba mkubwa mno, watu wengi walimiminika shuleni hapo kuomboleza.Eneo maalum lilitengwa kwa ajili ya watu kuweka maua na kadi za rambirambi, maelfu ya kadi na maua yalitupwa hapo yakiwa na ujumbe wa kuhuzunisha. <br />
<br />
Vilio vilitawala kila kona, haikuwezekana tena kuendelea na masomo. Ikabidi kila kitu kiahirishwe, vyombo vyote vya habari vilikuwepo, ilibidi rais na viongozi mbalimbali wa serikali wafike kutoa pole kwa msiba huo mkubwa uliolipata taifa. Katika hotuba yake, rais aliahidi kuwasaka magaidi waliofanya kitendo hicho kwa udi na uvumba mpaka wapatikane. <br />
<br />
Baadaye maaskari walifika na kuanza kuzungumza na walimu juu ya idadi ya watoto, wakakutanishwa na wazazi wote kumi na sita, familia kumi na saba yenye watoto wawili ilikuwa ni ya Phillip na mke wake Genevieve, askari walitaka pia kuwaona wazazi hao ili kuthibitisha kama kweli watoto walioteketea walikuwa ni kumi na nane kama walivyoagizwa na mkuu wao wa kazi.<br />
<br />
“Wapo Hospitali ya Taifa Muhimbili wakiendelea na matibabu, labda mnaweza mkawafuata huko kuthibitisha kama kweli watoto wao walikuwemo.”<br />
<br />
“Tutakwenda huko hospitali tuone kama tunaweza kuzungumza nao.”<br />
Pilikapilika zilizofuata hapo zikawa ni mazishi, wazazi walikataa kabisa watoto wao kuzikwa kwenye kaburi la pamoja, ikabidi wapewe mabaki ya miili ya watoto wao ili wakazike wenyewe. Kila mtu alipewa alichopewa, ilikuwa ni kama kuwagawia watu kilichopatikana, hatimaye wote kumi na saba wakapata kitu cha kwenda nacho nyumbani bila kujali ulikuwa mwili halali wa mtoto wao au lah.<br />
<br />
Mzee Mpangal ndiye aliyepokea mabaki ya Dorice na Dorica, alipowasiliana na Phillip kuhusu mazishi alikataa kabisa akitaka yahifadhiwe chumba cha maiti mpaka mke wake atakapozinduka ili ashuhudie mazishi ya watoto wake hata kama ingekuwa ni baada ya mwaka mmoja. <br />
<br />
Angekuwa na mamlaka ya kuzika Mzee Mpangal angefanya hivyo, lakini kisheria mzazi ndiye alikuwa na uamuzi hivyo alilazimika kukubaliana na uamuzi wa Phillip. Mabaki yakahifadhiwa chumba cha maiti kusubiri fahamu za Genevieve zirejee. <br />
<br />
Kila siku kwa Phillip ilikuwa ni machozi, akiwalilia watoto wake na kumsikitikia Genevieve ambaye aliendelea kulala kitandani bila fahamu mpaka zilipomrejea siku nne baadaye akiwa haelewi kilichoendelea, cha kusikitisha zaidi daktari akaweka bayana kuwa Genevieve alikuwa amepoteza uwezo wa kuona na kusikia na hata kumbukumbu zake hazikuwa sawa.<br />
<br />
“Daktari ni kwanini anaendelea kuwaita watoto eti awapeleke shule?”<br />
“Hana kumbukumbu, kilichompata ni hali fulani ambayo kitaalam inaitwa Concusion, yaani ubongo ulitikisika sana alipoanguka na kupiga kichwa chini, kumbukumbu zikafutika ni kama vile ambavyo hutokea katika kompyuta, vivyo hivyo kwenye ubongo wakati mwingine. Fahamu zake zitarejea baadaye lakini taratibu.”<br />
“Kuona?”<br />
<br />
“Vituo vyake vya kuona na kusikia kwenye ubongo vimeharibiwa sababu ya shinikizo la damu kupanda sana, hapo kwa kweli naomba tu niseme kwa uwazi kuwa, Genevieve hataweza kuona wala kusikia maisha yake yote.”<br />
<br />
Haikuwa mara ya kwanza kwa Phillip kusikia taarifa hiyo, muda mfupi tu kabla daktari alikuwa amemweleza lakini hakutaka kulichukua hilo kama jibu akidhani labda baadaye daktari angebadilisha. Roho ikamuuama, akahisi kitu kama kisu cha moto kikimchoma. Alipomwangalia Geneviveve kitandani alikosa uwezo wa kuyazuia machozi.<br />
<br />
“Genevieve awe kipofu? Watoto wangu wote wamekufa? Ni nani hasa aliyetega bomu kwenye basi la shule? Huyu ndiye adui yangu, nitamtafuta popote duniani mpaka nimtie mkononi, hata kama ni Osama bin Laden ambaye Marekani imeshindwa kumkamata, basi mimi nitamkamata, siwezi kumwacha mtu aliyeniharibia maisha kiasi hiki aendelee kutanua,” Philip aliwaza kichwani mwake.<br />
<br />
Hiyo ndiyo ilikuwa dhamira yake, kikwazo pekee alichokiona ni Genevieve, alishindwa kabisa kuanza msako wa magaidi akimuacha mkewe hospitali, hilo ndilo lilikuwa jambo baya la mwisho angeweza kulifanya maishani mwake kabla ya kufa. <br />
<br />
Aliendelea kuomba Genevieve apate nafuu na baadaye kutoka hospitali ili ajipange kwa kazi, hakutaka tena kurejea ofisini kwake, uhasibu haukuwa na maana tena, alichokihitaji maishani mwake kwa wakati huo ambacho kingemtuliza na kumpa faraja hakikuwa kingine isipokuwa kuwapata wauaji wake.<br />
<br />
Wiki moja baadaye Genevieve aliruhusiwa kutoka wodini kwani asingeweza kukaa hospitalini siku zote wakati alikuwa na nafuu, madaktari walitaka akaugulie nyumbani. Mpaka anaondolewa hospitalini bado hakuwa na uwezo wa kuona wala kusikia, kumbukumbu zake pia zilikuwa hazijarejea, hakujua kama watoto wake walishakufa, mara tatu kwa siku aliwaita huku akilia na kudai kwanini walikuwa wakiwekwa mbali naye.<br />
<br />
Jambo pekee lililokuwa limebaki likawa ni mazishi, Phillip hakuwa na ubishi tena juu ya watoto wake kuhifadhiwa kwani Genevieve hakuwa na fahamu ya chochote kilichoendelea. Maandalizi yakafanyika ndipo Dorice na Dorica wakazikwa bila Genevieve kuelewa kilichokuwa kikiendelea, baada ya hapo akarejeshwa nyumbani ambako maisha ya huzuni kwa Phillip yaliendelea. <br />
<br />
Nyumba ilikuwa kubwa mno kwake kwani sasa waliishi watu watatu peke yao; yeye, mfanyakazi wa ndani na Genevieve. Hii ilizidisha huzuni yake, kila siku alikuwa na picha ya watoto wake mkononi, hizo ndizo zilimfanya alie zaidi. Marafiki walijitahidi kuja kumtembelea na kumfariji lakini hawakuweza kumrejesha tena katika hali ya zamani, tayari alikuwa mtumwa wa huzuni na mateso na hakujua furaha ingerejea vipi maishani mwake tena.<br />
<br />
“Hodi...” alisikia sauti hiyo mlangoni akiwa amejilaza sakafuni sebuleni.<br />
Tangu apate matatizo na kurejea nyumbani kwake alilala sebuleni kila siku, hakutaka kabisa kwenda chumbani ambako kungemkumbusha mke na watoto wake.<br />
<br />
“Karibu...” akaitikia na kunyanyuka akijua ni wafariji walikuwa wamekuja kumtembelea asubuhi hiyo.<br />
Alipofungua mlango, macho yake yaligongana na wanaume watatu, mmoja wao akaonesha kitambulisho cha polisi kisha kujitambulisha na kueleza nia ya safari yao kwamba walikuwa ni wapelelezi waliofika pale kuzungumza naye juu ya tukio lililotokea ili awaeleze alichokifahamu ambacho waliamini kingewasaidia kuwajua watu waliofanya kitendo hicho.<br />
<br />
“Nasikia ulipokea simu ya mtu akikupa taarifa ya bomu kuwepo ndani ya gari la shule?”<br />
“Ni kweli.”<br />
“Unayo namba yake aliyekupigia?”<br />
“Haikuandika namba, iliandika tu neno Call!”<br />
“Tutaijua baadaye ni ya nani. Unadhani ni kisasi?”<br />
<br />
“Sidhani kama ni kisasi, sina ugomvi na mtu, maisha yangu yalikuwa haya haya siku zote, sipendi kabisa kugombana na binadamu wenzangu. Huyo niliyemtenda ubaya mpaka akafikia hatua ya kuua watoto wangu ni nani?” Phillip alibubujikwa na machozi akijieleza.<br />
“Hebu tueleze kidogo historia ya maisha yako.”<br />
“Ni ndefu.”<br />
“Tueleze tu hivyo hivyo.”<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Wauaji watapatikana? Watoto waliokufa katika tukio hilo ni kumi na sita au kumi na nane? Kama ni kumi na sita wawili wako wapi? Fuatilia KESHOOO,<br />
KUANZIA LEO EPISODE ZA HADITHI ZITAKUWA 5 TU KILA SIKU......USIKU MWEMA!!!!</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124bff004893951338879">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.6<br />
<br />
<br />
Polisi wameanza upelelezi wakijaribu kuchunguza ni nani hasa anayehusika na kutega bomu ndani ya gari la wanafunzi lililolipuka na kuua idadi ya watoto kumi na sita wasio na hatia.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Hii ni kwa mujibu wa polisi waliofanya uchunguzi. Kwa mujibu wa shule, idadi ya watoto wa shule waliokufa ni kumi nane, jambo ambalo limewashangaza watu wengi kiasi cha kushindwa kuelewa ni watoto wangapi hasa waliokufa kwenye mlipuko huo.<br />
<br />
Uchunguzi umeanzia eneo la tukio ambako vitu mbalimbali vilichukuliwa ili kuangalia kama mtegaji wa bomu aliacha alama yoyote, matokeo yametoka na kuonesha hakuna alama iliyobakia, mtegaji alikuwa ni mtaalamu wa kazi hiyo.<br />
<br />
Baada ya hapo polisi waliamua kumfuata Philip nyumbani kwake ambako tayari mke wake amekwisharuhusiwa kutoka hospitali akiwa hana kumbukumbu juu ya yaliyotokea, lengo ni kwenda kumuuliza juu ya simu aliyopokea ikimpa onyo asipakie watoto wake kwenye gari la shule sababu ndani yake kulitegwa bomu. Wapelelezi waliamini huo ungekuwa mwanzo mzuri wa kumpata muuaji.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO...<br />
<br />
“Nasikia ulipokea simu ya mtu akikupa taarifa za bomu kuwemo ndani ya gari la shule?”<br />
“Ni kweli!”<br />
“Unayo namba ya aliyekupigia?”<br />
<br />
“Haikuandika namba, iliandika tu neno ‘Call’!”<br />
“Tutajua baadaye ni nani! Unadhani ni kisasi?”<br />
“Sidhani kama ni kisasi, sina ugomvi na mtu, maisha yangu yalikuwa haya haya siku zote, sipendi kabisa kugombana na binadamu wenzangu. Huyu niliyemtendea ubaya mpaka akafikia hatua ya kuua watoto wangu ni nani?” Philip alibubujikwa machozi akijieleza.<br />
<br />
“Hebu tueleze kidogo historia ya maisha yako.”<br />
“Ni ndefu!”<br />
“Tueleze tu hivyo hivyo.”<br />
“Subirini kwanza nije,” Philip aliongea kisha kunyanyuka kwenda chumbani. Aliporejea dakika chache baadaye alikuwa na kitabu cheusi mkononi.<br />
<br />
Taratibu akaanza kukifungua huku askari wakimuangalia kwa mshangao, mioyoni mwao waliamini ndani ya kitabu hicho ndimo historia yake ilimokuwa. Wote wakakaa kimya kusubiri wakati wa kusisimua uanze.<br />
<br />
“Historia yangu ni ya kusikitisha, sijui kama itawasaidia chochote kwenye upelelezi wenu.”<br />
“Itasaidia sana.”<br />
“Kivipi?”<br />
<br />
“Tunaweza tukajua ni nani hasa amefanya ukatili huu.”<br />
“Lakini niliyepoteza watoto kwenye ajali si mimi peke yangu. Je, kama aliyefanya hivyo alikuwa akilipa kisasi kwa mzazi mwingine? Ikatokea tu kwamba watoto wangu wamo?” Philip aliuliza maswali ya mfululizo.<br />
<br />
“Tutaongea na wazazi wengine wote, kilichotufanya tukufuate wewe kwanza ni ile taarifa kwamba ulipigiwa simu ya onyo.”<br />
<br />
“This is my sad diary!” (Hiki ni kitabu changu cha kusikitisha cha kumbukumbu za matukio). Alianza kukisoma juu huku askari wakimsikiliza kwa makini, walijua lazima wangepata jambo la kuwawezesha hatimaye kumpata waliyekuwa wakimtafuta.<br />
<br />
“Why sad?” (Kwa nini yakusikitisha?)<br />
“They are memories I don’t want to remember!” (Ni kumbukumbu ambazo sitaki kuzikumbuka).<br />
<br />
***<br />
Juni 6, 1990, Sengerema Sekondari, Mwanza <br />
Namshukuru Mungu niko hapa sekondari, hii ni ndoto na ni jambo ambalo hakuna mtu anayeweza kuliamini. Bila shaka baba na mama yangu wangekuwa hai, wangefurahi sana kumuona mtoto wao amefikia kiwango hiki cha elimu, tena peke yangu kutoka kijijini kwetu.<br />
Acha nilale nikiamka asubuhi kabla ya kwenda darasani nitaendelea kuandika tena. Kumbukumbu hizi zitakuja kusomwa na watu siku moja hata kama nitakuwa nimekwisha kufa.<br />
<br />
Juni 7, 1990<br />
Usingizi ulikuwa mnono, nimeota ndoto moja tu leo, ya yule yule msichana mrembo ambaye kwa miaka mingi nimekuwa nikimuota, sura ile ile, sauti ile ile, umbile lile lile. Hakika msichana huyu ni mrembo, sijawahi kuona kama yeye hapa duniani. Leo aliniomba tuoane lakini nikakataa na kumwambia mimi bado mwanafunzi, lakini kwa nini ndoto hii kwa miaka yote? Hapa kuna jambo, iko siku nitakuja kulifahamu.<br />
<br />
Juni 8, 1990<br />
Bado watu wananitenga shuleni, eti kwa sababu wazazi wangu walikuwa wagonjwa wa Ukoma. Lakini tumekwisha fundishwa kwamba Ukoma sio ugonjwa wa kurithi, kwa kipindi kirefu nimenyanyapaliwa na kufanywa nijisikie sina amani ingawa mimi mwenyewe ugonjwa huo sina. Baadhi ya wasichana hata huniambia sitapata msichana wa kuoa. Sijali, msichana wa kwenye ndoto zangu ananitosha.<br />
<br />
Kila ninapokumbuka maisha yangu ya utotoni, kijijini nilipozaliwa na mateso niliyoyapata moyo wangu unauma sana. Hata hivyo namshukuru Mungu nimefika hapa nilipo. Ipo siku nitakuja kuwa na maisha bora. Hebu nijifute machozi…<br />
<br />
Philip aliendelea kuwasomea askari kitabu chake huku wote wakiwa kimya na wakionekana kuvutiwa na kila kitu alichokuwa akikisoma ingawa bado hawakupata picha hasa ya maisha yake kwa undani kwani maandishi hayo yaliandikwa kwa ufupi mno.<br />
“Unaweza kusimulia sasa vizuri ili tukuelewe?”<br />
<br />
“Nilizaliwa kijiji cha Bukokwa, mwaka 1976, katika familia ya bwana na bibi Robert Mpina, yenye watoto wawili mapacha. Mimi na ndugu yangu ambaye hivi sasa ni marehemu. Baba yangu alikuwa ni mwalimu ingawa mama yetu alikuwa ni mama wa nyumbani. Tukiwa na umri wa miaka mitano, pacha wangu aligongwa na gari na kufa pale pale. Naikumbuka sana hiyo siku, sijawahi kulia kiasi hicho tangu nizaliwe…” Philip akakohoa kidogo kusafisha koo.<br />
<br />
***<br />
Genevieve alikuwa kimya akiendelea kumshuhudia mume wake akisimulia historia ya maisha yake kwa watu ambao hakuwafahamu. Bado kumbukumbu zake zilikuwa hazijakaa sawa, hakuelewa chochote juu ya kilichowapata watoto wake. Aliendelea kuwaita akidhani labda walikuwa wamekwenda shule, ghafla akiwa katika mawazo hayo kitu kama filamu fupi kikampita akilini mwake. <br />
<br />
Alikuwa amesimama kando ya barabara, akilishuhudia gari lililobeba watoto wake likiondoka mahali alipokuwa. Muda huo huo akiendelea kushangaa, gari dogo aina ya Starlet lilisimama kando yake, msichana mmoja akachungulia kutoka ndani na kumsalimia akimuulizia barabara ya kwenda mjini. Kwa alivyoonekana msichana huyo hakuwa mtu wa kushindwa kufahamu barabara ya kumpeleka katikati ya jiji.<br />
<br />
“Yaani wewe dada hujui barabara ya kwenda mjini?”<br />
“Kwani kuna ajabu gani? Kama hutaki kunisaidia basi.” Dada huyo alijibu na kuanza kuondoka taratibu.<br />
<br />
Macho ya Genevieve yakarejea tena kwenye basi la wanafunzi, akashangaa kuona likiwa limesimama na tayari lilikuwa linaondoka, pia kulikuwa na gari jingine dogo jeusi ambalo liliondoka kwa kasi ya ajabu. Muda huo huo pikipiki iliyombeba Philip ikafika akiulizia watoto na kumuonesha basi, bila kupoteza wakati akaanza kulifuata, mbele kidogo ndipo likalipuka.<br />
Alipofikia hapo, kumbukumbu zikapotea tena.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.7.<br />
<br />
<br />
Muda mfupi tu baada ya kifo cha pacha wangu, wazazi hawakuwa tena na sababu ya kuendelea kuishi kijijini Bukokwa, isitoshe unyanyapaa dhidi ya ugonjwa wao ulikuwa umeongezeka sana. Walitengwa mno na kijiji, hakuna mtu hata mmoja aliyetaka kushirikiana nao, hata mimi kila mahali nilikopita niliitwa mtoto mkoma. Mwanzoni sikuelewa kabisa hiyo ilikuwa na maana ga<span class="text_exposed_show">ni, lakini baadaye nilielewa kila kitu na kuanza kujiona sina maana.<br />
<br />
Nilikuwa na umri wa miaka sita tu, huo ukiwa mwaka 1982, kwa umri wangu nilitakiwa kuwa nimekwishaanza darasa la kwanza lakini wazazi walishindwa kunipeleka shule ambako waliamini watoto wa watu wengine wangeendelea kunitenga. Niliumia kila nilipowaona watoto wenye umri kama wa kwangu wakienda shule kila siku asubuhi, ndani ya suruali za kaki na mashati meupe yaliyoitwa Shikibo.<br />
<br />
Katika umri huo tayari nilishaanza kuota sana juu ya mtoto huyu wa kike mwenye ngozi laini ya maji ya kunde, nywele nyingi kichwani, macho makubwa ya kulegea, shingo ndefu, midomo minene ya duara, pua iliyochongoka na vishimo kwenye mashavu ambavyo watu wengi siku hizi wanaviita ‘dimpoz.’<br />
<br />
Ninachoweza kusema tu ni kwamba ingawa mtoto huyu wa kike alikuwa mdogo sawa na umri wangu, sura yake ilivutia mno na katika umri wangu huohuo nilitamani kuwa naye. Nakumbuka katika ndoto yangu ya kwanza, nilikuwa ufukweni nikichezea maji, siku hiyo mimi na wazazi wangu tulikuwa tumekwenda huko kwa mapumziko.<br />
<br />
Nilishituka tu akiibuka kutoka majini mbele yangu na sikujua alikotokea, akatabasamu nami nikafanya hivyo. Tabasamu lake lilikuwa zuri mno, hakuna mwanadamu angeweza kujizuia kulijibu kwa tabasamu. Akanisogelea na kunisalimia kisha kuniambia alivutiwa sana na mimi.<br />
<br />
“Mimi bado mdogo mbona?”<br />
“Tutakua tu, nitakusubiri.”<br />
“Wewe ni nani?” Nilimuuliza.<br />
Hakujibu swali langu, akanitega mgongo kama vile alikuwa akiona aibu, kisha kuzama tena majini, sikumuona alikopotelea lakini mbele kidogo kichwa chake kilionekana na kutabasamu, akapunga mkono hewani kisha kujibinua na kuzama kwa mara nyingine ndani ya maji, sikumuona tena na nikazinduka.<br />
<br />
Sikumwambia mtu yeyote juu ya ndoto hiyo, sikuwa na mtu wa kumsimulia, niliichukulia kama ndoto ya kawaida na nisingeiota tena, haikuwa hivyo, niliendelea kumuota binti huyo karibu kila siku, akitokea eneo hilo hilo la baharini.<br />
<br />
Safari zote zilizofuata aliongea na mimi bila kuniangalia usoni kama vile alikuwa akiona aibu ya kunitazama, katika maongezi yake aliendelea kusisitiza namna alivyonipenda na alitaka siku moja tuoane na kuwa mume na mke halafu tupate watoto wawili mapacha kufidia pacha wangu aliyepotea.<br />
<br />
“Unajuaje kama nina pacha aliyepotea?”<br />
“Ninaelewa Phillip, nakufahamu sana.”<br />
“Wewe ni nani kwani?”<br />
“Muda wa kulifahamu jina langu utakapofika utanifahamu, kwa hivi sasa bado.”<br />
“Niangalie basi usoni.”<br />
<br />
“Siwezi…” Alijibu binti huyo na kuzama majini kabla hajamaliza sentensi yake.<br />
Kwa sababu ya manyanyaso yaliyokuwepo kijijini kwetu Bukokwa, baba na mama waliamua tuhame twende mjini Mwanza kutafuta maisha sehemu ambako hakuna mtu angeweza kuwanyanyapaa. Chaguo lao likawa ni kukimbilia mjini ambako wangejichanganya na watu wenye matatizo kama yao walioishi kwa kuombaomba.<br />
<br />
Kihistoria wazazi wangu walikutana kwenye kambi ya wagonjwa wa ukoma iitwayo Kidugalo, iliyoko wilayani Sikonge mkoani Tabora ambako baada ya kugundulika wana ukoma, walipelekwa na ndugu zao na hawakutakiwa kurudi tena nyumbani kwa sababu ugonjwa wa ukoma ulitafsiriwa kama laana na jamii. Katika mazungumzo yao niligundua walikuwa ni watu wa Kakonko huko Kigoma na waliwasiliana kwa lugha ya Kiha si Kisukuma kama walivyofanya watu wengine.<br />
<br />
Naikumbuka vyema siku tuliyopanda basi la African Bus Service kutoka Bukokwa kuelekea Mwanza mjini, mara tulipoingia tu ndani ya basi watu walianza kutukimbia wakiogopa kugusana na sisi, kondakta akatuchukua na kutupeleka kiti cha nyuma kabisa kilichokaliwa na watu sita, chote tukakikalia watu watatu, mimi na wazazi wangu.<br />
<br />
Ilikuwa saa kumi ya alfajiri basi lilipoanza safari na kuendelea mpaka kuingia Mwanza mjini saa saba za mchana, ulikuwa umbali wa kilomita kama sitini hivi lakini kwa sababu ya ubovu wa barabara tulitumia muda mrefu sana kusafiri. <br />
<br />
Wakati tunapita mitaani Mwanza, nilianza kuwaona watu wengine waliofanana kabisa na wazazi wangu kwa maumbile, hawakuwa na vidole na sura zao zilikuwa zimevimba nundu nyingi, wao pia walikuwa wakoma na waliketi kando ya barabara wakiwa na vikopo vidogo, kazi yao ikiwa ni kuomba kwa wapita njia.<br />
<br />
Tulipofika mtaa maarufu wa Uhuru mjini Mwanza kwenye daraja kubwa la Mirongo, tuliona kundi kubwa la wagonjwa wa ukoma wakiwa wamelala kwenye vibanda vilivyotengenezwa kwa maturubai kando ya mto, baba akanishika mkono na kuanza kunivusha upande wa pili kwenye vibanda hivyo.<br />
<br />
“Ng’wadila banamhala!” (Habari za leo wazee?) Baba aliwasalimia wanaume waliokuwa wameketi kando ya daraja kwa Kisukuma,<br />
“Ng’wadila, ulimhola bhabha?” (Salama, habari zako mzee?)<br />
“Nali mhola, kinehe ubing’we?” (Mimi sijambo, nyinyi je?)<br />
“Tuli mhola duhu!” (Hatujambo tu)<br />
“Niza nane, tugeme shihamo ukuchola sabo...” (Nami nimekuja, tujaribu kutafuta pamoja mali)<br />
<br />
“Tuliho, bejaga kanumba lulu aha mhelo aho!” (Karibu, tengeneza kijumba basi pale kando.)<br />
Wote walikuwa wagonjwa wa ukoma, wakipitia mateso na unyanyapaa wa aina moja, hawakuwa na la kufanya zaidi ya kupendana. Baba alisaidiwa kutengeneza kibanda kando kabisa ya mto, kibanda chake kikiwa cha mwisho. <br />
<br />
Hiyo ndiyo ikawa nyumba yetu na hicho ndiyo kikawa kijiji chetu, tulitakiwa kuishi hapo maisha yetu yote. Hapakuwa na uwezekano wa kurudi tena kijijini Bukokwa, hivyo kazi ya wazazi wangu kila siku asubuhi ikawa ni kuondoka pamoja nami kwenda mitaani kuomba wakiwa na kopo, mimi nikiwa nimeketi kando yao nikiangalia wapita njia na roho kuniuma.<br />
<br />
Sikupendezwa na maisha hayo na sikutaka kabisa na mimi nije kuishia hivyo, niliamini katika elimu na nilitamani kwenda shule, kila siku nilipowaona watoto wakipita mbele yangu kwenda shule roho iliniuma lakini sikuweza kuwaeleza wazazi wangu juu ya shule.<br />
<br />
Jioni tuliporejea kambini, baba aliketi na rafiki yake mpendwa Masalu Nkwabi, mgonjwa wa ukoma kutoka Ukiriguru nje kidogo ya mji wa Mwanza, alikuwa ameishi hapo kando ya daraja kwa miaka kumi na mbili na alikuwa mwenyeji sana katika mji huo.<br />
<br />
Kila siku mzee Masalu alitoka na baba yangu kwenda kutembea baada ya kurudi kutoka kuombaomba, mimi nikabaki na mama na waliporejea usiku walikuwa wamelewa kupita kiasi, mama alilalamika lakini baba hakusikia.<br />
<br />
Hata katika mazingira kama hayo, ingawa nililala chini nikiumwa na papasi pamoja na mbu bado niliendelea kumuota msichana yule yule, alinijia mara nyingi mno katika ndoto zangu tukiwa hapo hapo kando ya bahari na kuniambia aliyafahamu matatizo yangu na siku moja angekuja kuyaondoa kabisa mara tukioana.<br />
<br />
“Tutaoanaje wakati sote bado wadogo na sikufahamu?” <br />
“Tutakua tu Phillip na utakuja kunifahamu!”<br />
“Kwani wewe unaishi wapi?”<br />
“Huwezi kujua ninapoishi, hata ukijua huwezi kwenda kwani wewe ni wa ulimwengu mwingine na mimi vivyo hivyo natoka ulimwengu mwingine.”<br />
<br />
“Unamaanisha nini kusema hivyo?” Hakunijibu akapotelea majini.<br />
Bado sikumsimulia mtu juu ya ndoto hiyo, nilishamzoea sana msichana huyu kiasi kwamba hata nilipotembea nilijaribu kuangaza watu ninaokutana nao ili kuona kama ningeweza kukutana naye mahali fulani. Hakika haikuwa ndoto ya kawaida, kila kitu kilionekana halisia mno aliponijia, alizidi kuwa mzuri na kupendeza kadri siku zilivyozidi kwenda.<br />
<br />
“Shikamoo wazee!” Ilikuwa ni sauti ya mtu mmoja akipita kando ya njia, nikageuka kumwangalia, alikuwa Muasia mrefu mwembamba, nywele zake zikiwa zimefungwa kwa nyuma.<br />
“Marahaba hujambo?” Baba na mama wakaitikia.<br />
<br />
“Sijambo tu, naitwa Mustafa Kudret, natokea shirika linaloitwa Tujaliane, kazi yetu ni kuwasaidia watoto waishio katika mazingira magumu, nimemuona huyu mtoto hapa ni wenu?”<br />
“Ndiyo ni wetu.”<br />
<br />
“Anasoma?”<br />
“Hapana.”<br />
“Kwanini?”<br />
“Gharama.”<br />
<br />
“Eti wewe mtoto unaitwa nani?”<br />
“Phillip.”<br />
“Unapenda shule?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
Je, nini kitaendelea?, ni lazima ujue ni nani aliyetega bomu kwenye gari na kuwaua Dorice na Dorica pamoja na watoto wengine wasio na hatia.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c138fe043863416223">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.8.<br />
<br />
Upelelezi wa polisi kuchunguza ukweli juu ya bomu lililolipuka umeanza. Pamoja na uchunguzi walioufanya eneo la tukio na kuongea na mashahidi walioshuhudia, polisi walihitaji kuongea na Phillip ambaye alidaiwa kupokea simu ya onyo kabla ya tukio hilo, hivyo wakamfuata nyumbani kwake.<br />
<br />
Phillip aliyekuwa na masikitiko mengi aliamua kuwaeleza askari historia yote y<span class="text_exposed_show">a maisha yake akitumia kitabu alichotunza kumbukumbu zake tangu utotoni (diary). Lengo lilikuwa ni kutaka kuonesha ni kwa kiasi gani hakuwa na adui wa kuweza kuwaua watoto wake kinyama kiasi kile. <br />
<br />
Ameeleza alivyozaliwa na wazazi wenye ugonjwa wa ukoma. Kwa sababu ya kunyanyapaliwa wakaamua kuhamia Mwanza mjini ambako waliishi mtaani pamoja na ombaomba wengine mpaka siku alipokuja mtu mmoja na kujitambulisha kama Mustafa Kudret, kutoka Shirika la Kusaidia Watoto liitwalo Tujaliane. Mustafa aliwauliza wazazi wa Phillip kama mtoto wao alikuwa akisoma shule mahali popote. <br />
<br />
Wazazi wakaeleza ukweli kuwa Phillip alikuwa hasomi shule mahali popote sababu ya umaskini ingawa wangependa mtoto wao apate elimu ili asiishie kuwa ombaomba kama wao.<br />
<br />
Mwisho wa mazungumzo hayo, Mustafa, Mtanzania mwenye asili ya Asia, alimgeukia Phillip na kuendelea kumuuliza maswali, akakiri kupenda shule na huo ndiyo ulikuwa ukweli kuhusu yeye.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO...<br />
<br />
“Kweli unapenda shule?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Unataka kuwa nani ukikua?”<br />
“Rubani.”<br />
“Kabisa.”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Basi kesho nitakuja kukuchukua ukapime nguo za shule, halafu Jumanne nitakupeleka shuleni ukaanze darasa la kwanza.”<br />
“Sawa, asante!”<br />
<br />
Mustafa aliaga na kuondoka akiniacha katika furaha ambayo sikuwahi kuwa nayo tangu kuzaliwa kwangu. Hakuna kitu nilichohitaji kama shule, nilijua ingawa katika umri mdogo kabisa hicho kingenisaidia maishani. Hatimaye ndoto sasa ilikuwa inatimia, nilishinda na furaha siku nzima nikiwashuhudia wazazi wangu wakiomba kwa wapita njia na kudondoshewa visenti kwenye kopo, tena wakati mwingine kwa dharau kubwa, jambo lililoniumiza sana moyoni na kutamani kuibadilisha hali hiyo.<br />
<br />
Hiyo ilikuwa ni Jumapili jioni, tulirejea kambini kando ya mto ambako baba wala hakukaa sana, akaondoka na rafiki yake, Mzee Masalu kama ilivyokuwa kawaida yao kwenda kwenye vilabu vya pombe maeneo ya Mlango Mmoja. Mama alibaki nami akishughulikia chakula cha jioni. <br />
<br />
Baada tu ya kupata chakula cha jioni, nilitandika mkeka wangu chini na kulala. Nilipozinduka baadaye katikati ya usiku, si baba wala mama aliyekuwepo ndani ya kibanda chetu, nilikuwa nimelala peke yangu jambo ambalo halikuwa kawaida kabisa. Nikarejea usingizini, safari hii msichana wa kwenye ndoto zangu alinijia, akiwa amependeza kupita kiasi na kuniambia ilikuwa ni lazima tufunge ndoa. <br />
<br />
Tofauti na siku nyingine zote, nilijikuta nakubali bila kuhoji kuhusu umri wetu, akaniambia anichukue kwenda kunitambulisha kwa wazazi wake. Sikukataa, nikanyanyuka na kwa pamoja tukaanza kutembea tukipita kwenye mitaa yenye giza lakini macho yake yalimulika kama tochi kiasi cha kuonesha njia. Tukafika ufukweni mwa bahari na akaniambia nipande mgongoni, sikusita wala kuhoji swali lolote, moyo wangu pia haukuwa na woga ingawa sikumfahamu sana msichana huyo mdogo.<br />
<br />
Nikamdandia na akaanza kuogelea nikiwa mgongoni mwake, sote tukazama majini bila mimi kuwa na matatizo ya kupumua, tofauti na siku nyingine zote nilizoogelea ambazo sikuwa na uwezo wa kubaki ndani ya maji bila pumzi hata kwa dakika moja. Kwa karibu saa nzima msichana huyo aliogelea, tukipita sehemu zenye mwanga mkali na majengo mazuri, huku tukipishana na samaki wengi, wakati mwingine nyangumi bila hata kudhuriwa.<br />
<br />
“Tunakwenda wapi?” Nilimuuliza baada ya kuona hatufiki.<br />
“Kwetu.”<br />
“Kwenu wapi?”<br />
“Utapaona tukifika.”<br />
<br />
Safari ikazidi kusonga mpaka chini kabisa ya maji ambako tulikuta jumba kubwa la kifahari, tukaingia ndani yake na kupokelewa na sauti za shangwe ambazo sikuona zilitokea wapi kwani hapakuwa na mtu zaidi ya mimi na msichana huyo. Akanitoa hofu kwamba nisiogope na tukazidi kuingia ndani ya jumba hilo lililopambwa kwa vito vya thamani vyenye kung’ara ambavyo niliamini vilitengenezwa kwa almasi na dhahabu.<br />
<br />
“Baba!” Aliita msichana huyo.<br />
“Naam!”<br />
“Nimemleta mwanao ninayempenda kuliko binadamu mwingine yeyote kwenye ulimwengu wao. Niko tayari kuolewa naye, nihame huku na kwenda kuishi kwenye ulimwengu wao kwani yeye hawezi kuja huku,” aliongea msichana huyo nikizidi kushangaa alimaanisha nini aliposema ulimwengu wao.<br />
<br />
“Unampenda?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Uko tayari kuolewa naye?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Yeye anasemaje?”<br />
<br />
“Labda umuulize wewe.”<br />
“Uko tayari kumuoa binti yangu?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
Vigelegele vikasikika kila mahali ndani ya jumba hilo, lango kubwa likafunguka, wakaingia farasi wawili weupe nyuma wakiwa na tela lililopambwa vizuri kwa vitambaa vyeupe, likiwa na matairi ya rangi nyeupe. Farasi hao hawakuwa wa kawaida kwani walikuwa na mabawa, na ndimi zao zilitoa moto, macho yao yakiwaka kama tochi.<br />
<br />
Kufumba na kufumbua tukawa tumebadilika nguo tulizovaa, msichana akawa amevaa gauni la kijani lililong’ara kupita kiasi, hakika alipendeza nami nikawa nimevaa suti nyeupe. Sote wawili tukapandishwa kwenye tela na mikono ya watu ambao sikuwaona huku vigelegele vikisikika.<br />
<br />
“Tayari mmekwishafunga ndoa, nyie sasa ni mke na mume. Wewe kijana sasa hivi hutaitwa Phillip, bali Samir,” ilikuwa ni sauti ile ile ya baba wa msichana.<br />
<br />
Huku akionesha tabasamu msichana huyo alinigeukia na kunikumbatia, kwa mara ya kwanza akanipiga busu shavuni, nikausikia mwili wangu kama umepigwa shoti ya umeme kwa msisimko nilioupata. Farasi wakaanza kuondoka huku wakipaa kwa kutumia mabawa yao.<br />
<br />
Tukapitishwa kwenye jiji kubwa, maelfu ya watu wakiwa wamesimama kando ya njia wakitushangilia kwa ndoa hiyo, mikononi wakiwa wameshikilia matawi ya miti wakiyapeperusha hewani. Nilipowatazama vizuri niligundua hawakuwa binadamu wa kawaida, kwani usoni walikuwa na jicho moja tu kubwa katikati ya paji la uso.<br />
<br />
“Sasa tumeoana, unaweza kuniambia unaitwa nani?”<br />
“Mimi?”<br />
“Naitwa Zamaradi.”<br />
“Jina zuri.”<br />
<br />
“Asante Samir, tangu sasa wewe ni mume wangu, nakupenda. Nasikitishwa tu na taabu zitakazokupata huko kwenye ulimwengu unaoishi, utateseka sana lakini usiwe na wasiwasi, nitakuwa pamoja nawe.”<br />
“Unamaanisha nini Zamaradi?”<br />
<br />
“Kuna taabu kubwa inakuja mbele yako, hata leo hii utalia sana machozi,” aliongea msichana huyo.<br />
Ghafla niligutuka usingizini baada ya kusikia mlango wa bati kwenye kibanda chetu ukigongwa kwa nguvu, nikaketi kitako huku nikitetemeka.<br />
<br />
Nilikuwa nimeota ndoto ya kutisha kuliko zote nilizowahi kuota juu ya msichana huyo. Nilipozungusha macho yangu chumbani nilimwona baba ameketi kando yangu akilia, sikuelewa ni kwa sababu gani alikuwa katika hali hiyo na pia sikufahamu ni muda gani alirejea, mama hakuwepo.<br />
<br />
“Fungua, fungua mlango haraka.”<br />
“Baba kuna nini?” Nilimuuliza baba yangu.<br />
“Ni hasira mwanangu, nimefanya jambo ambalo sikutegemea kulifanya.’<br />
“Jambo gani?”<br />
<br />
“Nimewaua Mzee Masalu na mama yako.”<br />
“Umewaua?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Kisa?”<br />
<br />
“Nimewakuta wanafanya tendo la ndoa kwenye choo cha kilabu cha pombe tulichokwenda kunywa.”<br />
Sikuwa na cha kusema zaidi ya kuanza kumlilia mama yangu. Haikuwa rahisi kukubaliana na maneno ya baba, ilifanana kama nimetoka kwenye ndoto moja ya kutisha na kuingia kwenye nyingine.<br />
<br />
Mlango ukafunguliwa kwa nguvu, watu wawili wakaingia na kumvisha baba yangu pingu mikononi kisha kuondoka naye wakimsukuma. Sikubaki nyuma, nikaamua kufuatana nao nikilia hadi kituo kikuu cha polisi ambacho kipo karibu kabisa na bandari ya Mwanza.<br />
<br />
Baba aliingizwa ndani na kutupwa mahabusu, watu wote wakimwita kwa jina la Mkoma Mkatili. Alikuwa amefanya kitendo cha kinyama ambacho sikuwa tayari kukiamini mpaka nilipozishuhudia maiti za mama na Mzee Masalu zikiwa zimechinjwa kwa kisu kama mbuzi. Sikuwahi hata siku moja kufikiri baba yangu mzazi angekuwa katili kiasi hicho.<br />
<br />
Mustafa Kudret alikuwepo wakati wa mazishi ya mama yangu na Mzee Masalu kwenye makaburi ya Bugando ambako wafanyakazi wa Halmashauri ya Jiji walishughulikia kazi hiyo. Niliumia sana kumwona mama yangu akiingizwa ndani ya shimo na kufukiwa akiwa hana hata sanda. Hasira dhidi ya baba iliniingia ingawa bado nilikuwa na umri mdogo.<br />
<br />
Sikuwa na mahali pa kwenda baada ya mazishi hayo, Mustafa akalazimika kunichukua hadi kwenye kituo chao cha kulelea watoto wa mitaani. Kulikuwa na watoto wengi kama mimi ambao hawakuwa na makazi, nikatambulishwa kwao na wakaelezwa kwamba tangu siku hiyo ningekuwa miongoni mwao.<br />
<br />
Ingawa nililala ndani, kula chakula kizuri na Mustafa alininunulia sare za shule na kunipeleka Shule ya Msingi Nyakabungo wiki moja baadaye kuanza darasa la kwanza, sikuwa na furaha moyoni kwa sababu wazazi wangu hawakuwa pamoja nami kama nilivyozoea kuishi.<br />
<br />
Muda mwingi nilikuwa mtoto mwenye huzuni na watoto wengi waliokuwepo kwenye kituo hicho walikuwa ni wakorofi na wapenda ugomvi, hivyo walinigeuza ngoma. Kila siku nilikuwa nikipigwa asubuhi, mchana na jioni kiasi kwamba mwili mwangu ulijaa nundu na makovu. <br />
<br />
Hali hii ilinifanya nianze kubadilika, nikalazimika kuchukua hatua ya kujilinda na kujitetea pale nilipoonewa na silaha yangu kubwa ikawa ni wembe. Kila nilikokwenda wembe ulikuwa mfukoni na yeyote aliyenipiga, aliishia kuchanjwa. Nilikuwa na hasira kali sana dhidi ya mtu yeyote aliyenionea. <br />
<br />
Sikuacha kumfikiria baba yangu pamoja na kuwa alitenda kosa, kila kesi yake ilipotajwa na yeye kufikishwa mahakamani, nilikuwepo kushuhudia kilichoendelea. Kila aliponiona alilia kwani hali yake ilikuwa imedhoofu na alijua angekufa na kuniacha duniani peke yangu nikiteseka.<br />
<br />
“Nisamehe mwanangu, shetani ni mbaya.” Ndiyo maneno pekee aliyoyasema.<br />
Miezi sita baadaye, baba yangu hakuletwa tena mahakamani, nilipojaribu kuuliza kwa askari hawakunificha, walinieleza wazi kuwa baba alikufa akiwa mahabusu kwa ugonjwa wa kuhara na kutapika uliolikumba Gereza la Butimba. Nililia kupita kiasi kwani sasa ilithibitika kabisa nilikuwa yatima kamili.<br />
<br />
***<br />
“Usilie Samir, niko pamoja nawe katika shida zote, wewe ni mume wangu katika ulimwengu ninaoishi mimi, vumilia tu yote yatakwisha!” Ilikuwa ni sauti ya Zamaradi nikiwa usingizini kwenye kituo cha kulelea watoto.<br />
“Wazazi wangu wananiuma.”<br />
<br />
“Najua mume wangu, lakini mimi nipo. Endelea tu na shule mpaka umalize chuo kikuu”<br />
Hayo yalikuwa ndiyo maisha yangu ya kila siku, mchana niliishi maisha ya kawaida katika ulimwengu huu unaoonekana kwa macho lakini usiku niliishi maisha kwenye ulimwengu mwingine usioonekana kwa macho ya kawaida ambako nilikuwa mume wa msichana mrembo Zamaradi, huko ndiko nilipata furaha yangu tofauti na kwenye dunia hii ambako niliishi maisha ya kupambana na kupigana na watoto wenzangu.<br />
<br />
Sikuwahi kumwambia mtu yeyote juu ya ndoto yangu na msichana niliyemuota, ilikuwa ni siri ambayo sikutakiwa kufumbua mdomo kuisema kwa yeyote. Majeraha ya kuondokewa na wazazi wangu yalishapona na nikaendelea na masomo kama kawaida mpaka kufika darasa la saba nikiongoza darasani, hakuna aliyeamini nilikuwa mtoto wa mtaani.<br />
<br />
“Samir!”<br />
“Naam.”<br />
“Nina mimba.”<br />
“Mimba?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
Zamaradi aliniambia maneno hayo mara tu nilipomaliza darasa la saba, kwanza sikuamini lakini baadaye nilipoona tumbo lake linaongezeka ukubwa nikakubaliana naye. Miezi tisa baadaye alijifungua mtoto wa kike aliyefanana sana na yeye, ilikuwa furaha kubwa mno kwa kila mtu aliyeishi chini ya bahari, hatimaye tukawa tumepata mtoto. <br />
<br />
Katika ulimwengu ulioonekana kwa macho hakuna mtu hata mmoja aliyeelewa kwamba kwenye ulimwengu usioonekana kwa macho nilikuwa na mke na mtoto wa kike tuliyemwita jina la Mina. Hiyo ilikuwa ni siri ya kufa nayo moyoni mwangu. Kwa wanafunzi wenzangu nilionekana mtoto mwenzao, lakini nilikuwa mtu mzima kuliko mwanafunzi mwingine yeyote shuleni kwetu.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c13935411c24076809"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c138e7863066191982">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.9.<br />
<br />
<br />
Tayari nilikuwa katika mapenzi mazito na Zamaradi, kwenye ulimwengu halisi ulioonekana kwa macho hakuna aliyeelewa jambo hili, ilikuwa ni siri kubwa, nisingethubutu kufungua mdomo wangu na kuongea mbele ya wanafunzi wenzangu au hata kwa Mustapha Kudret ambaye kwangu alikuwa ni mzazi.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Kwangu haikuwa ndoto tena, kila kitu kilikuwa ni halisi maana karibu kila siku Zamaradi alikuja nikiwa usingizini kuniletea mwanangu Mina, nikashuhudia akiendelea kukua na kufanana na mama yake kwa kila kitu. Kwa jinsi mambo yalivyotokea, hakuna binadamu awaye yote angeamini kwamba ilikuwa ni ndoto tu, ndoto ya kila siku? Swali hilo ndilo lilinifanya nikubali kwamba nilikuwa mume wa mtu lakini kwenye ulimwengu mwingine.<br />
<br />
Hayo yakitokea niliendelea na shule kama kawaida, kila siku niliamka asubuhi nikiwa nimechoka sababu ya kukosa usingizi na kuelekea shuleni. Nguvu zangu zote zilielekezwa kwenye masomo, maumivu ya kufiwa na wazazi wangu tayari yalishaondoka moyoni, sasa nilitazama mbele ili niweze kujikomboa, nami nisiishie kuwa ombaomba kama ilivyokuwa kwa wazazi wangu.<br />
<br />
Darasani nilikuwa mwanafunzi bora, sikumbuki kushika namba chini ya mbili katika masomo yote mpaka namaliza darasa la saba, hii ilimfurahisha sana mfadhili wangu Mustapha Kudret, kwani nilikuwa mwanafunzi bora kuliko mwingine yeyote kwenye kituo cha kulea watoto yatima na viongozi wote walijivuna kuwa na mtoto kama mimi kwenye kituo chao.<br />
<br />
“Phillip!” Mmoja wa walezi aliniita.<br />
“Naam.” Nikaitika.<br />
“Wewe ni mfano wa kuigwa, ukiendelea hivi maisha yako baadaye yatakuwa mazuri, unaumwa macho?”<br />
<br />
“Hapana.”<br />
“Kwanini ni mekundu kiasi hicho?” Aliuliza Bibi Nyang’oma, mlezi wa watoto kwenye kituo akinisogelea kisha kuanza kunichunguza, jambo ambalo hakulifahamu ni kwamba usiku na mchana nilikuwa macho, kama nililala ni kwa saa moja au mbili nikicheza na mtoto wangu Mina katika ndoto.<br />
<br />
“Hata sijui ni kwanini?”<br />
“Au hupati usingizi wa kutosha usiku?”<br />
“Hapana shangazi, nalala vizuri tu.” Nilidanganya.<br />
Matokeo ya darasa la saba yalipotoka nilikuwa nimefaulu na kuchaguliwa kujiunga na Shule ya Sekondari ya Mwanza kwa ajili ya kidato cha kwanza, ilikuwa ni furaha kubwa mno kwangu na hata nilipolala usingizi, Zamaradi alikuja na kunisifia. <br />
<br />
Wote tukashangilia na akanichukua kunipeleka chini ya bahari ambako nilikutana na baba yake pamoja na watu wenye jicho moja, sherehe kubwa ikafanyika kunipongeza kwa ushindi wangu.<br />
<br />
“Unakwenda sekondari sasa, utakutana na wasichana wazuri sana, kumbuka tu kwamba wewe ni mume wa mtu kwenye huu ulimwengu ninaoishi mimi, usijaribu kunisaliti, ukifanya hivyo nitakasirika na nikikasirika naweza kukuadhibu vibaya na unajua hasira ni hasara, sipendi kukuua Samir. Leo nataka nikueleze ukweli mimi ni jini mahaba, ninao uwezo wa kukunyonya damu!” Zamaradi aliongea akimwangalia kwa makini, alionekana ni mwenye wivu kupindukia.<br />
<br />
“Siwezi kufanya hivyo.” Nilijibu huku nikitetemeka, hapo ndipo nikaelewa nilikuwa kwenye ulimwengu wa viumbe visivyoonekana, kumbe haikuwa ndoto ya kawaida bali ni maisha halisi chini ya bahari ambako majini yaliishi.<br />
<br />
“Shauri yako.” Zamaradi aliongea akiukunja uso wake na kunisababishia hofu zaidi, hakika alinitisha kugundua kwamba alikuwa ni jini.<br />
<br />
Nilipoamka na kurejea kwenye ulimwengu wa kawaida asubuhi ilikuwa ni furaha tupu kwa kila mtu kituoni, Mustapha aliandaa sherehe ya kunipongeza ambayo ilifanyika mchana bwaloni, kwani mimi ni pekee niliyekuwa nimechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kutoka kwenye kituo hicho.<br />
<br />
Siku iliyofuata maandalizi yalianza, Mustapha akaninunulia vitu vyote muhimu vilivyohitajika na wiki tatu baadaye nilipelekwa shuleni na kuanza masomo nikiwa nimemwahidi mfadhili wangu kufanya kila nilichoweza ili nisimwangushe, nikiweka wazi kabisa kuwa katika Tanzania nzima lazima ningekuwemo kati ya kumi bora ambao wangefanya vizuri.<br />
<br />
Haukuwa uongo, Shule ya Sekondari ya Mwanza ilikuwa miongoni mwa shule zenye wasichana wazuri sana nchini Tanzania, uwepo wa wakazi wengi wenye asili ya nchi jirani ya Rwanda na Ethiopia ulifanya mabinti wengi waliosoma katika shule hiyo iliyopo katikati ya Jiji la Mwanza barabara ielekeayo Hospitali ya Bugando, wawe wenye sura za kuvutia.<br />
<br />
Jambo ambalo sikulitarajia ni kwamba ningeweza kuwavutia wasichana wengi shuleni hapo, hata siku moja maishani mwangu sikuwahi kudhani nami nilikuwa miongoni mwa watu wenye sura ya kuvutia. Hata siku moja sikuwahi kumsikia mtu akiniambia hivyo, lakini nilipoingia Mwanza Sekondari wasichana walianza kunifuata wakijaribu kunishawishi nijiingize kwenye uhusiano wa kimapenzi.<br />
<br />
Mara zote niliisikia sauti ya Zamaradi ikinipa onyo kupitia masikioni mwangu. Hofu ya kuuliwa na jini ikanitawala, nikaogopa kufa, haukuwa utani Zamaradi alikuwa na uwezo wa kuondoa maisha yangu kama ningekwenda kinyume na ahadi niliyoiweka. Nikaamua kujiheshimu kwa sababu nilikuwa mume wa mtu mwenye mtoto mmoja kwenye ulimwengu usioonekana kwa macho ya kawaida.<br />
<br />
Tabia yangu ya kutopenda ngono, jambo ambalo lilifanywa sana na wanafunzi shuleni ilinifanya nionekane tofauti na wengine wote, ikanijengea sifa kubwa mpaka uongozi wa shule ukanichagua kuwa kiranja mkuu ili niweze kuwasimamia wenzangu nilipokuwa kidato cha pili. Hakuna aliyeelewa siri ya mimi kuwa na msimamo huo, haukuwa bure, ulitokana na hofu ya kifo iliyonitawala.<br />
<br />
Nikaendelea hivyo mpaka kumaliza kidato cha nne, matokeo yalipotoka nilikuwa nimechaguliwa kujiunga na Shule ya Sekondari ya kutwa ya Azania iliyopo jijini Dar es Salaam kwa masomo ya kidato cha tano na cha sita, Mustapha alifurahi mno na kwa sababu shule hiyo ilikuwa ya kutwa alilazimika kuwasiliana na kituo cha kulea watoto yatima cha Dogodogo ili waweze kunipokea na kunipa hifadhi kwa miaka miwili nitakayoishi jijini Dar es Salaam.<br />
<br />
Hapakuwa na tatizo lolote kwani uongozi wa kituo hicho ulikubali kunipokea, ndipo kwa mara ya kwanza shule ilipofunguliwa, nilipanda ndege nikiwa na Mustapha na kusafiri hadi Dar es Salaam, jiji ambalo siku zote nililisikia midomoni mwa watu au kusoma kwenye magazeti.<br />
<br />
Sasa nilitakiwa kuishi ndani yake kwa miaka miwili na pengine minne zaidi kama ningefanya vizuri kidato cha sita na kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, hiyo ndiyo ilikuwa ndoto yangu. Tulipokelewa vizuri kituoni na nikatambulishwa kwa uongozi na wanafunzi wengine ambao pia walikuwa yatima na walitunzwa kwenye kituo hicho, taarifa zangu zilishatangulia kwamba nilikuwa mwanafunzi niliyeshika namba tatu Tanzania nzima kwa mtihani wa kidato cha nne, hii ilinipa heshima kubwa miongoni mwa watoto wenzangu.<br />
<br />
Kwa mara ya kwanza nililala kwenye kituo hicho, Zamaradi akaniijia usingizini akiwa na mtoto wangu Mina, nilishangaa aliwezaje kunifuata mpaka Dar es Salaam kwa umbali wote uliokuwepo, akaniambia yeye na mtoto walikuwa ni roho, popote wanaweza kupatikana. Zamaradi aliendelea kunionya juu ya mafanikio niliyokuwa nikiyapata na tamaa ambazo zingenifuata kama nisingekuwa makini.<br />
<br />
“Kumbuka umeoa.’<br />
“Najua mke wangu.”<br />
“Usinisaliti.”<br />
“Siwezi.”<br />
“Ukinisaliti nitakunyonya damu Samir.”<br />
“Sitakusaliti mke wangu.”<br />
<br />
Hayo ndiyo yalikuwa maneno yake kila siku alipokuja ndotoni, yalinitia hofu sana na kunifanya niendelee kuwa mwaminifu kwake nikiogopa kufa. Kwenye kituo cha Dogodogo, kila siku asubuhi niliamka na kutembea na wenzangu hadi shuleni ambako tulisoma mpaka saa nane mchana ndipo tukapanda basi kuturejesha maeneo ya Posta ambako kituo kilikuwa, hatukuweza kutembea kwa miguu mchana sababu ya njaa.<br />
<br />
“Simamisha gari! Konda simamisha gari!” Nilipiga kelele nikiwa nimekaa kiti cha nyuma.<br />
“Vipi tena dogo?”<br />
“Nimemuona mtu.”<br />
“Hapa siyo kwenye kituo.”<br />
<br />
“Simama tu.”<br />
Tulikuwa tumefika kwenye mnara wa askari na macho yangu hayakuwa yamenidanganya, nilimwona Zamaradi akiwa na mtoto mgongoni! Hiyo haikuwa ndoto ni kweli nilimwona Zamaradi. Nikaendelea kusisitiza dereva asimamishe gari lakini hakuna aliyenisikiliza hatimaye likafika kwenye kituo cha Posta ya Zamani na kusimama, hapo ndipo palikuwa mwisho wa safari.<br />
<br />
Sikutaka kusubiri kupita mlangoni kama abiria wengine, nikaruka dirishani na kuanza kukimbia kurudi basi lilikotokea ili nimuwahi Zamaradi na mwanangu Mina, sikumuona kwenye Mnara wa Askari, nikaanza kuuliza walinzi kwenye maduka kama walimuona binti mwenye mtoto akipita maeneo hayo.<br />
<br />
“Yule mwenye kitoto kizuri kabisa?”<br />
“Ndiyo.” Niliitikia, mlinzi hakuwa amekosea, Mina alikuwa mtoto mzuri mno.<br />
“Ameelekea upande huu wa baharini.”<br />
“Asante.”<br />
<br />
Nikaanza kukimbia kuelekea baharini, mita chache kabla sijayafikia maji nilimuona binti huyo akiwa amenitega mgongo, mtoto wake akiwa mikononi, akitembea kwa haraka kuelekea majini, nikaongeza kasi nikimfuata. Lengo langu lilikuwa ni kumshika ili nimbakize duniani, nikashuhudia akiyakanyaga maji na kuanza kuingia ndani, tayari nilishafika na kumshika mkono kwa nguvu nikimvuta atoke majini.<br />
<br />
Alipogeuka kuniangalia kweli alikuwa Zamaradi.<br />
“Niachie.”<br />
“Huwezi kwenda.”<br />
“Kwanini?”<br />
“Nataka ubaki.”<br />
“Siwezi.”<br />
<br />
Tukaanza kuvutana, watu wengi wakaja wakikimbia ili kujua kilichokuwa kikiendelea mahali pale.</span></div></div></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.10.<br />
<br />
<br />
Tulianza kuvutana nikitumia nguvu zangu zote nilizojaliwa na Mwenyezi Mungu kuhakikisha Zamaradi na mwanangu Mina hawarejei tena chini ya bahari, nilimpenda sana mke wangu na sikutaka kabisa arejee tena kwenye ulimwengu usioonekana. Vurugu ilikuwa kubwa, watu wakazidi kujaa na kutuzunguka wakishuhudia ugomvi wetu bila kufanya chochote.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Lakini huyu ni mwanafunzi wa Azania, si mnaona sare zake?” Mwanamke mmoja alisikika akisema, tayari nilishamtoa Zamaradi ndani ya maji na kumlaza kwenye mchanga akiwa na Mina aliyekuwa akilia kwa nguvu mikononi mwake, nikaketi juu yake nikimgandamiza ili asiondoke.<br />
“We kijana mwachie bibi wa watu.”<br />
<br />
“Bibi gani, niacheni huyu ni mke wa...,” nilisema kwa sauti ya juu lakini kabla sijamalizia sentensi yangu nilikumbuka kuwa jambo nililotaka kulisema halikuwa la ulimwengu huu bali la ulimwengu wa ndotoni, ilikuwa siri yangu, sikutakiwa kumwambia mtu yeyote hivyo nikakomea hapo hapo lakini watu wote wakacheka kwa sauti ya juu, nikahisi waliona nimechanganyikiwa.<br />
<br />
“Mkeo? Huyu bibi? We mtoto unaumwa?”<br />
“Bibi yuko wapi? Naomba mniache.”<br />
Tayari polisi walishafika na kuanza kuwapangua watu kwa kutumia virungu vyao mpaka wakanifikia nilipokuwa nimemlalia Zamaradi kwa juu, mtoto akiendelea kulia, wakanishika na kuanza kunivuta. Kwa kuwa walikuwa polisi sikuwa na sababu yoyote ya kuendelea kulumbana nao, nikamuachia Zamaradi na kusimama kando huku nikimwangalia kwa jicho la upendo.<br />
<br />
“Vipi kijana? Mbona unamkaba bibi wa watu?” Mmoja wa wale askari aliuliza, nilipotupa macho kumwangalia mtu aliyekuwa amesimama mbele yangu, nilishangaa, nikaelewa ni kwa nini watu walikuwa wakicheka.<br />
<br />
“Mh!” Nikaguna, hakuwa Zamaradi bali mwanamke mzee mwenye umri usiopungua miaka sitini mikononi akiwa amembeba mtoto aliyeonekana ni mjukuu wake.<br />
“Huyu ndiyo unasema mkeo?”<br />
<br />
Nikaanza kulia nikawa nimeinamisha kichwa changu chini kwa sababu ya aibu, nilishindwa kuelewa ni jambo gani lilitokea kwani kwa asilimia mia moja mtu niliyemuona alikuwa ni Zamaradi akiwa na mwanangu Mina, iweje tena awe bibi kizee mwenye sura mbaya kiasi hicho? Sikupata jibu, nilipokumbuka maneno ya mtu aliyenielekeza kule ambako Zamaradi alielekea nikawa na uhakika kabisa sikukosea.<br />
<br />
“Yule mwenye kitoto kizuri?” Maneno ya mwanaume huyo yaliendelea kujirudia kichwani mwangu na kunifanya nishindwe kuelewa ni jambo gani lilitokea, sikuwa nimechanganyikiwa kama ambavyo watu wote walionizunguka walidhani.<br />
“Unaishi wapi?” Mmoja wa wale askari aliuliza.<br />
“Dogodogo.” <br />
“Twende.”<br />
<br />
Wakidhani nimechanganyikiwa, askari walinipakia ndani ya gari lao na tukaondoka moja kwa moja tukipitia Barabara ya Sokoine na baadaye kupita mitaa ya katikati ambayo siikumbuki jina mpaka tukafika kituoni ambako nilikabidhiwa kwa mkuu wa kituo baada ya kupewa historia nzima ya tukio.<br />
<br />
“Eti Phillip kimetokea nini?” Aliuliza mkuu wa kituo akionesha mshangao.<br />
“Sijui mama.”<br />
“Unaumwa?”<br />
“Hapana.”<br />
<br />
Mkuu wa kituo akawashukuru askari kwa msaada wao kisha wakaagana, hapo ndipo akanichukua hadi ofisini kwake na kuanza kunidadisi. Sikudiriki kufungua mdomo wangu kumwambia kitu chochote juu ya Zamaradi, muda wote akizungumza nilikuwa nikilia. Akajitahidi kunifariji kwa uwezo wake wote, mwisho nilipotulia alinichukua hadi chumbani kwangu, nikapanda juu ya kitanda na kujilaza, haukupita muda mrefu sana usingizi ukanipitia na ndoto ikaanza.<br />
<br />
“Samahani sana Samir, ni kweli nilikuja kwenye ulimwengu uonekanao kwa macho, nilitamani kukuona baada ya kukukumbuka sana. Lakini kama ujuavyo mimi na Mina si viumbe wenye miili, ni roho. Baada ya kutoka majini tuliwaingia bibi kizee mmoja na mjukuu wake tuliowakuta kando ya bahari, tukaitumia miili yao kuzunguka huku na kule tukikutafuta, tukaja hadi shuleni kwenu na kukuta unaondoka ndipo tukaanza kulifuatilia basi ulilopanda hadi ulipotuona.”<br />
<br />
“Zamaradi.”<br />
“Bee!”<br />
“Ni kweli unayoyasema?”<br />
“Ni kweli kabisa, ndiyo maana nimekuja kukuomba msamaha.”<br />
“Ni kwa nini hukukubali kubaki kwenye ulimwengu unaoonekana nilipokuwa nakuvuta pale kando ya bahari?”<br />
<br />
“Tusingeweza kuishi huko pamoja na wewe, tungetumia miili ya nani maana baada ya muda si mrefu wenye miili yao wangeihitaji na sisi tungekufa. Ikabidi turudi hadi ufukweni ambako tuliiacha miili hiyo na kuingia majini, ndiyo maana ukakutana na sura halisi ya bibi na mjukuu wake, nakupenda sana Samir.”<br />
“Nakupenda sana Zamaradi, unanitesa, tutaishi maisha haya hadi lini?”<br />
<br />
“Nisamehe mume wangu, hakuna maisha mengine tutakayoishi zaidi ya haya.”<br />
“Lazima siku moja utoke huko Zamaradi.”<br />
“Haiwezekani Samir.”<br />
“Mrudishe mtoto, uje peke yako.”<br />
<br />
Zamaradi aliondoka kwa sekunde chache tu na kurejea akiwa peke yake, akanikumbatia na wote tukalala juu ya mchanga kando ya bahari na kuanza kupapasana. Muda mrefu haukupita tulikuwa katikati ya tendo la ndoa kuthibitisha upendo wa mke na mume. Maumivu yote niliyokuwa nayo moyoni yakaisha, Zamaradi akanibusu usoni kisha akaniaga.<br />
<br />
“Oyaa! Vipi tena? Unanifanya mimi demu wako mshikaji?” Ilikuwa ni sauti ya Zakaria, mmoja wa watoto kwenye kituo hicho ambaye nililala naye kitanda kimoja.<br />
<br />
“Kwani vipi?” Nilimuuliza baada ya kuketi na kuwa na uhakika kabisa nilikuwa nimeota ndoto nikiwa na Zamaradi tena tukifanya mapenzi.<br />
“Umenikumbatia halafu unanifanyia vitu vya ajabu, au wewe ni ba…?”<br />
“Acha utani basi Zakaria, hiyo ni ndoto tu kwani wewe hujawahi kuota unafanya mapenzi?”<br />
<br />
“Siyo leo tu, tangu uje huwa hupitishi siku mbili na unaita jina hilo hilo la Zamaradi, huyu Zamaradi unampenda sana bila shaka.”<br />
“Ni ndoto tu.”<br />
<br />
Je, nini kitaendelea maishani mwa Phillip? Nani alitega bomu kwenye basi na kuua watoto wote? TUKUTANE KESHO JIONI....USIKU MWEMA!!</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c138bb241d90600593">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.10.<br />
<br />
<br />
Tulianza kuvutana nikitumia nguvu zangu zote nilizojaliwa na Mwenyezi Mungu kuhakikisha Zamaradi na mwanangu Mina hawarejei tena chini ya bahari, nilimpenda sana mke wangu na sikutaka kabisa arejee tena kwenye ulimwengu usioonekana. Vurugu ilikuwa kubwa, watu wakazidi kujaa na kutuzunguka wakishuhudia ugomvi wetu bila kufanya chochote.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Lakini huyu ni mwanafunzi wa Azania, si mnaona sare zake?” Mwanamke mmoja alisikika akisema, tayari nilishamtoa Zamaradi ndani ya maji na kumlaza kwenye mchanga akiwa na Mina aliyekuwa akilia kwa nguvu mikononi mwake, nikaketi juu yake nikimgandamiza ili asiondoke.<br />
“We kijana mwachie bibi wa watu.”<br />
<br />
“Bibi gani, niacheni huyu ni mke wa...,” nilisema kwa sauti ya juu lakini kabla sijamalizia sentensi yangu nilikumbuka kuwa jambo nililotaka kulisema halikuwa la ulimwengu huu bali la ulimwengu wa ndotoni, ilikuwa siri yangu, sikutakiwa kumwambia mtu yeyote hivyo nikakomea hapo hapo lakini watu wote wakacheka kwa sauti ya juu, nikahisi waliona nimechanganyikiwa.<br />
<br />
“Mkeo? Huyu bibi? We mtoto unaumwa?”<br />
“Bibi yuko wapi? Naomba mniache.”<br />
Tayari polisi walishafika na kuanza kuwapangua watu kwa kutumia virungu vyao mpaka wakanifikia nilipokuwa nimemlalia Zamaradi kwa juu, mtoto akiendelea kulia, wakanishika na kuanza kunivuta. Kwa kuwa walikuwa polisi sikuwa na sababu yoyote ya kuendelea kulumbana nao, nikamuachia Zamaradi na kusimama kando huku nikimwangalia kwa jicho la upendo.<br />
<br />
“Vipi kijana? Mbona unamkaba bibi wa watu?” Mmoja wa wale askari aliuliza, nilipotupa macho kumwangalia mtu aliyekuwa amesimama mbele yangu, nilishangaa, nikaelewa ni kwa nini watu walikuwa wakicheka.<br />
<br />
“Mh!” Nikaguna, hakuwa Zamaradi bali mwanamke mzee mwenye umri usiopungua miaka sitini mikononi akiwa amembeba mtoto aliyeonekana ni mjukuu wake.<br />
“Huyu ndiyo unasema mkeo?”<br />
<br />
Nikaanza kulia nikawa nimeinamisha kichwa changu chini kwa sababu ya aibu, nilishindwa kuelewa ni jambo gani lilitokea kwani kwa asilimia mia moja mtu niliyemuona alikuwa ni Zamaradi akiwa na mwanangu Mina, iweje tena awe bibi kizee mwenye sura mbaya kiasi hicho? Sikupata jibu, nilipokumbuka maneno ya mtu aliyenielekeza kule ambako Zamaradi alielekea nikawa na uhakika kabisa sikukosea.<br />
<br />
“Yule mwenye kitoto kizuri?” Maneno ya mwanaume huyo yaliendelea kujirudia kichwani mwangu na kunifanya nishindwe kuelewa ni jambo gani lilitokea, sikuwa nimechanganyikiwa kama ambavyo watu wote walionizunguka walidhani.<br />
“Unaishi wapi?” Mmoja wa wale askari aliuliza.<br />
“Dogodogo.” <br />
“Twende.”<br />
<br />
Wakidhani nimechanganyikiwa, askari walinipakia ndani ya gari lao na tukaondoka moja kwa moja tukipitia Barabara ya Sokoine na baadaye kupita mitaa ya katikati ambayo siikumbuki jina mpaka tukafika kituoni ambako nilikabidhiwa kwa mkuu wa kituo baada ya kupewa historia nzima ya tukio.<br />
<br />
“Eti Phillip kimetokea nini?” Aliuliza mkuu wa kituo akionesha mshangao.<br />
“Sijui mama.”<br />
“Unaumwa?”<br />
“Hapana.”<br />
<br />
Mkuu wa kituo akawashukuru askari kwa msaada wao kisha wakaagana, hapo ndipo akanichukua hadi ofisini kwake na kuanza kunidadisi. Sikudiriki kufungua mdomo wangu kumwambia kitu chochote juu ya Zamaradi, muda wote akizungumza nilikuwa nikilia. Akajitahidi kunifariji kwa uwezo wake wote, mwisho nilipotulia alinichukua hadi chumbani kwangu, nikapanda juu ya kitanda na kujilaza, haukupita muda mrefu sana usingizi ukanipitia na ndoto ikaanza.<br />
<br />
“Samahani sana Samir, ni kweli nilikuja kwenye ulimwengu uonekanao kwa macho, nilitamani kukuona baada ya kukukumbuka sana. Lakini kama ujuavyo mimi na Mina si viumbe wenye miili, ni roho. Baada ya kutoka majini tuliwaingia bibi kizee mmoja na mjukuu wake tuliowakuta kando ya bahari, tukaitumia miili yao kuzunguka huku na kule tukikutafuta, tukaja hadi shuleni kwenu na kukuta unaondoka ndipo tukaanza kulifuatilia basi ulilopanda hadi ulipotuona.”<br />
<br />
“Zamaradi.”<br />
“Bee!”<br />
“Ni kweli unayoyasema?”<br />
“Ni kweli kabisa, ndiyo maana nimekuja kukuomba msamaha.”<br />
“Ni kwa nini hukukubali kubaki kwenye ulimwengu unaoonekana nilipokuwa nakuvuta pale kando ya bahari?”<br />
<br />
“Tusingeweza kuishi huko pamoja na wewe, tungetumia miili ya nani maana baada ya muda si mrefu wenye miili yao wangeihitaji na sisi tungekufa. Ikabidi turudi hadi ufukweni ambako tuliiacha miili hiyo na kuingia majini, ndiyo maana ukakutana na sura halisi ya bibi na mjukuu wake, nakupenda sana Samir.”<br />
“Nakupenda sana Zamaradi, unanitesa, tutaishi maisha haya hadi lini?”<br />
<br />
“Nisamehe mume wangu, hakuna maisha mengine tutakayoishi zaidi ya haya.”<br />
“Lazima siku moja utoke huko Zamaradi.”<br />
“Haiwezekani Samir.”<br />
“Mrudishe mtoto, uje peke yako.”<br />
<br />
Zamaradi aliondoka kwa sekunde chache tu na kurejea akiwa peke yake, akanikumbatia na wote tukalala juu ya mchanga kando ya bahari na kuanza kupapasana. Muda mrefu haukupita tulikuwa katikati ya tendo la ndoa kuthibitisha upendo wa mke na mume. Maumivu yote niliyokuwa nayo moyoni yakaisha, Zamaradi akanibusu usoni kisha akaniaga.<br />
<br />
“Oyaa! Vipi tena? Unanifanya mimi demu wako mshikaji?” Ilikuwa ni sauti ya Zakaria, mmoja wa watoto kwenye kituo hicho ambaye nililala naye kitanda kimoja.<br />
<br />
“Kwani vipi?” Nilimuuliza baada ya kuketi na kuwa na uhakika kabisa nilikuwa nimeota ndoto nikiwa na Zamaradi tena tukifanya mapenzi.<br />
“Umenikumbatia halafu unanifanyia vitu vya ajabu, au wewe ni ba…?”<br />
“Acha utani basi Zakaria, hiyo ni ndoto tu kwani wewe hujawahi kuota unafanya mapenzi?”<br />
<br />
“Siyo leo tu, tangu uje huwa hupitishi siku mbili na unaita jina hilo hilo la Zamaradi, huyu Zamaradi unampenda sana bila shaka.”<br />
“Ni ndoto tu.”<br />
<br />
Je, nini kitaendelea maishani mwa Phillip? Nani alitega bomu kwenye basi na kuua watoto wote? TUKUTANE KESHO JIONI....USIKU MWEMA!!</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124c9e460227754940061">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.11.<br />
<br />
Bomu limelipua gari la shule,watoto wote waliokuwemo ndani ya gari hilo wamekufa. Inadaiwa walikuwa ni kati ya kumi na sita na kumi na nane, miongoni mwao wakiwemo watoto (Dorice na Dorica) wa Phillip na mkewe Genevieve ambao walihangaika kwa muda mrefu kuwapata.<br />
<br />
Kabla bomu hilo kulipuka Phillip alipokea simu kutoka kwa mtu asiyejulikana ikimtaarifu asiwapaki<span class="text_exposed_show">e watoto wake kwenye gari hilo kwani lingelipuka, juhudi zake hazikuzaa matunda kwani mke wake aliwapeleka stendi na kuwapakia. Phillip akiwa amebakiza mita chache tu kulifikia basi hilo akilifuatilia kwa pikipiki, lililipuka.<br />
<br />
Polisi sasa wameamua kuanza kumtafuta aliyetega bomu kwenye gari kwa kufanya mahojiano na Phillip, anasimulia historia ya maisha yake ili waweze kuona kama kuna mtu yeyote anayelipa kisasi. Anatumia kitabu chake cha kumbukumbu kuelezea juu ya msichana aliyemwota kila siku katika ndoto (Zamaradi) ambaye baadaye walifunga ndoa ndotoni na kuzaa mtoto mmoja (Mina).<br />
<br />
Katika maelezo yake amefika sehemu ambayo anaishi jijini Dar es Salaam kwenye kituo cha kulelea watoto cha Dogodogo baada ya kutoka Mwanza, akisoma kidato cha tano katika Shule ya Azania. Umetokea ugomvi mkubwa kati yake na kijana (Zakaria) aliyelala naye kitanda kimoja akidai kila siku Phillip huota ndoto akifanya mapenzi na mwanamke huku akimpapasa kijana huyo.<br />
Je, nini kitaendelea katika maisha ya Phillip? SONGA NAYO…<br />
<br />
Nilitumia muda mrefu sana kumwelewesha Zakaria juu ya ndoto yangu ingawa sikumfungulia ukweli kamili kwamba Zamaradi alikuwa ni mke wangu kwenye ulimwengu mwingine na tulikuwa na mtoto, mwisho akaelewa na kuahidi kunivumilia katika tatizo hilo huku akitoa angalizo kwamba kama ningeendelea kwa muda mrefu na tabia hiyo, angelazimika kuhama kitanda ili anipe nafasi ya kutanua na Zamaradi wangu. Wote wawili tuliishia kucheka, kwani aliongea kwa utani.<br />
<br />
Alikuwa rafiki yangu mkubwa tangu niingie kwenye kituo hicho cha Dogodogo na wote tulisoma Shule ya Sekondari ya Azania ingawa vidato tofauti, yeye alikuwa kidato cha sita mimi cha tano. Ni kweli tulipendana na kuheshimiana, alipoahidi kunivumilia nilijua alikuwa hadanganyi.<br />
<br />
“Sitaki kukuahidi kwamba sitaota.”<br />
“Hapana bwana ni lazima ujitahidi, unajua binadamu hupata anachokitegemea, unavyoonekana wewe haufanyi jitihada zozote kupambana na ndoto hizo, au unazipenda?” Zakaria aliuliza akatabasamu.<br />
<br />
“Siwezi kusema nazipenda au sizipendi.”<br />
“Unamaanisha nini?”<br />
“Tuyaache hayo.” Nilijibu kwa mkato na wote wawili tukanyanyuka kitandani na kuketi, saa yangu ya mkononi nilipoiangalia mishale ilisomeka saa kumi na mbili na nusu jioni, tayari ulikuwa ni wakati wa chakula cha usiku.<br />
<br />
Kwa hali niliyokuwa nayo sikuhitaji kula, moyo wangu ulikuwa umejawa na huzuni sana. Hivyo niliendelea kujilaza kitandani mpaka saa sita za usiku ndipo nilipopitiwa na usingizi tena, nikalala hadi saa kumi na mbili asubuhi ndipo kunyanyuka kwa ajili ya maandalizi ya kwenda shule. Zakaria hakulalamika tena kama nilimfanyia chochote, kwa hakika sikumuota Zamaradi.<br />
<br />
Saa moja kamili wanafunzi wote wa Azania tuliondoka kwenda shuleni, siku hiyo hata waalimu sikuwasikiliza vizuri, akili yangu yote ilikuwa imeishia kwa Zamaradi. Nilimfikiria mfululizo huku taswira yake na ya mtoto wangu mzuri Mina zikipita kama sinema kichwani. Nilitamani sana wangekuwepo kwenye ulimwengu uonekanao kwa macho, hakika nilishawazoea na siku zote nilijichukulia kama baba mwenye familia yake ingawa kwenye ulimwengu uonekanao kwa macho hakuna mtu hata mmoja aliyelifahamu jambo hilo.<br />
<br />
Maisha yakaendelea, ndoto hazikukoma, kila siku usiku Zamaradi alinitembelea na kuongea nami mambo mengi, alinieleza kuhusu ajali ambazo zingetokea na kunionya juu ya kusaliti penzi letu, akitishia kuniua kama ningefanya mapenzi na mwanamke mwingine yeyote. <br />
<br />
Kulipokucha aidha nilizishuhudia ajali zote alizoniambia au kuziona zikitangazwa kwenye taarifa za habari, kila kitu alichonieleza kilitokea, hata watu alioniambia kwamba wangekufa, walikufa kweli, hii ilinifanya nimuogope kupita kiasi nikiamini kama ningemsaliti, hakika angeniua.<br />
<br />
Mara tatu au nne kwa wiki tulifanya tendo la ndoa, hii ilikuwa ni kero kubwa sana kwa Zakaria, uvumilivu wake ukafika mwisho na kujikuta akiamua kuhama kitanda na kuniacha peke yangu. Nilimwomba samahani kwa yote yaliyotokea, tayari alishahisi nilikuwa na tatizo na mara kadhaa aliniambia niende kanisani kuombewa akidai nilikuwa na jini mahaba lililofanya mapenzi na mimi usiku.<br />
<br />
“Una jini Phillip.”<br />
“Jini? Siyo kweli.”<br />
“Kabisa, unahitaji kuombewa ili litoke.”<br />
Sikuelewa alichosema, nilimuona kama mtu ambaye hakujua alichokiongea. Niombewe litoke? Yaani Zamaradi na mwanangu waondoke katika maisha yangu? Hayo yalikuwa ni mambo yasiyowezekana, niliwapenda mno, kama ni jini mahaba basi nilikuwa tayari kubaki nalo siku zote za maisha yangu. Kauli hiyo ndiyo niliyojieleza mwenyewe kutoka ndani ya moyo wangu.<br />
<br />
Hata siku moja sikuwahi kwenda kuombewa wala kukiri kwa mtu yeyote kwamba nilikuwa na mke na mtoto katika ulimwengu usioonekana kwa macho, siku zikazidi kusonga nikisoma na kufanya vizuri shuleni, Mustapha alifurahi sana kila nilipompelekea ripoti na kuzidi kunisaidia.<br />
Maumivu yote ya kufiwa na wazazi yalishaondoka, hakuna mtu hata mmoja niliyeishi naye aliyeelewa kwamba nilikuwa ni mtoto wa wakoma. Watu wote waliniheshimu kituoni na hata shuleni sababu ya uwezo wangu wa darasani, kila mtihani nilishika namba moja, hivyo ndivyo ilivyokuwa mpaka nilipomaliza kidato cha sita na kurejea Mwanza ambako Zamaradi na mwanangu Mina waliendelea kunifuata.<br />
<br />
Majibu yalipotoka nilikuwa nimefaulu kuliko mtoto mwingine yeyote kwenye kituo cha Dogodogo, kwa Tanzania nzima nilikuwa nimeshika namba mbili kati ya wanafunzi wote waliofanya mtihani. Mustapha alifurahi mno, kwake ulikuwa ushindi mkubwa, kumwokota mtoto mtaani na kumfikisha hatua niliyokuwa nayo hakika halikuwa jambo dogo.<br />
<br />
Alikuwepo Ikulu ya Dar es Salaam tulipoitwa kwa ajili ya kupewa zawadi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, machozi yalinitoka, nilitamani sana baba na mama yangu wawepo kushuhudia hatua ambayo mtoto wao nilikuwa nimefikia maishani na kila mtu alikuwa na uhakika nisingekuwa mtu mdogo siku za usoni.<br />
<br />
Tulisaidiana na Mustapha kujaza fomu za vyuo vikuu na kozi mbalimbali ambazo nilitaka kusoma, kwa jinsi nilivyofaulu nilikuwa na uwezo wa kusoma kozi yoyote kuanzia uhandisi mpaka uanasheria, Mustapha aliponiuliza nilitaka kusoma nini nikachagua uchumi, hivyo tukajaza fomu za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa ajili ya kusoma shahada ya kwanza ya Uchumi.<br />
<br />
Baada ya zoezi hilo sote tulirejea Mwanza tena kwa ndege ambako niliendelea kufundisha katika Shule ya Sekondari ya Mwanza kwa kujitolea huku nikisubiri muda wa kujiunga na chuo kikuu, miezi michache baadaye ukawadia, nikawaaga wanafunzi pamoja na walimu tayari kwa kurejea Dar es Salaam kuanza masomo yangu ya miaka mitatu, ilikuwa ni huzuni kubwa shuleni lakini moyoni mwangu nilifurahi kwani taratibu nilikuwa najongea kuelekea kwenye ndoto yangu.<br />
<br />
Tukapanda ndege tena, mtoto wa maskini niliyezaliwa kifukara, nikaishi mitaani mpaka nilipookotwa na Mustapha, sasa maisha yangu yalishabadilika na kuwa mtu wa kuruka angani kila nilipotaka kusafiri, hakika nilimuona Mungu ni wa ajabu na kuamini kwamba kweli ilikuwa inawezekana kwa kila mtu aliyedhamiria.<br />
<br />
Hatukufikia tena Dogodogo Centre, Mustapha alichukua chumba hoteli moja maeneo ya Ubungo iitwayo Landmark, ambayo iko karibu kabisa na chuo kikuu. Tukalala mpaka siku iliyofuata ndipo tukaingia chuoni na kukuta kuna pilikapilika za wanafunzi kujisajili, wanafunzi walikuwa wengi mno, ilinichukua siku nzima kukamilisha mchakato mpaka kupewa bweni, nikapangiwa kwenye jengo liitwalo Hall 5. Mustapha akaondoka na kuniacha peke yangu.<br />
<br />
Siku iliyofuata ilikuwa ni ya kila kitivo kufanya utambulisho na kuzungushwa maeneo mbalimbali ya chuo ili kukifahamu vizuri chuo kikuu. Wanafunzi wote wa kitivo changu tuliongozana na mkuu wa kitivo kwenda kila mahali, kuanzia Nkrumah, vyumba vyote vye semina na hata sehemu ya kulia chakula.<br />
<br />
Katika pitapita hizo nilijifunza kitu kimoja, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kilikuwa na wasichana warembo kuliko wote niliowahi kuwaona, niliwaona hata waliomzidi Zamaradi kwa kila kitu, haikuwa rahisi kuamini lakini huo ndiyo ulikuwa ukweli. Kibaya zaidi mavazi yao, walivaa nguo za kuwabana au fupi zilizoonyesha maungo yao, ilihitaji moyo mgumu sana kufundisha katika chuo hicho kwani kulikuwa na kila ushawishi wa kumfanya mwalimu atamani kufanya mapenzi na wanafunzi wake.<br />
<br />
“Sijui maprofesa hapa wanafanyaje, maana wake zao ni wazee lakini wanafundisha mabinti wadogo ambao wako tayari kufanya lolote ili wafaulu mtihani, wanapona kweli hapa?” Nilijiuliza nikigeuka kuangalia nyuma, macho yangu yakatua kwa msichana ambaye kitu cha kwanza nilichokigundua mwilini mwake ni macho, yalikuwa yamelegea kama vile alitaka kusinzia, akatabasamu nami nikashindwa kujizuia na kujibu kwa tabasamu.<br />
“Hi!” Alinisalimia.<br />
<br />
“Hi!” Nami nikamjibu.<br />
“I am Tyra.”<br />
“Phillip.”<br />
“Nice meeting you Phillip. Are you from Dar?” (Nafurahi kukutana na wewe Phillip. Unatokea hapa Dar?)<br />
“No!” (Hapana.)<br />
<br />
“Where are you from?” (Unatokea wapi?)<br />
“I hail from Mwanza, but I did my A-level here.” (Natokea Mwanza lakini nilisoma kidato cha tano na cha sita hapa.”<br />
“Which school?” (Shule gani?)<br />
“Azania. What about you? Are you from here?” (Azania. Vipi wewe? Unatokea hapa Dar es Salaam?)<br />
<br />
“Yes. My parents live here but I did my A-level in South Africa.” (Ndiyo. Wazazi wangu wanaishi hapa lakini mimi nilisoma kidato cha tano na cha sita Afrika Kusini.)<br />
“So you are also taking Economics?” (Kwa hiyo pia unachukua Uchumi?)<br />
“Yes.” (Ndiyo.)<br />
“Why?” (Kwanini?)<br />
<br />
“My father wants me to run his businesses once I graduate, he is old now and I am the only kid in my family” (Baba yangu anataka niendeshe biashara zake nikihitimu, anazeeka sasa na mimi ndiye mtoto pekee kwenye familia yetu.) Aliongea Tyra huku nikimwangalia kutokea kichwani hadi miguuni, nikakiri kwa mdomo wangu sikuwahi kukutana na msichana mrembo kiasi hicho, hisia zikanituma kufikiri labda naye alikuwa ametokea kwenye ulimwengu usioonekana.<br />
<br />
Hatukusikiliza tena kilichokuwa kikisemwa na mkuu wa kitivo, maongezi yaliendelea kati yetu, Tyra alionekana kuvutiwa sana na mambo niliyoyaongea, hakutaka kukaaa mbali nami na kuna wakati akawa hata ananiwekea mkono begani kitendo kilichonifanya niione taswira ya Zamaradi kichwani akiwa amekunja uso wake kwa hasira.<br />
<br />
“Can you take your hand off my shoulder?” (Unaweza kuuondoa mkono wako begani kwangu?)<br />
“Yes I can. Why? You don’t like it?” (Ndiyo naweza. Kwanini? Hupendi?)<br />
“I always fear public opinion, we have just met. It might bring a bad impression.” (Siku zote huwa ninahofia maoni ya watu, ndiyo kwanza tumekutana, hii inaweza kuleta picha mbaya.) Nilisingizia hivyo lakini ukweli ilikuwa ni hofu ya Zamaradi, maneno yake kwamba angeniua kama ningejihusisha na msichana mwingine yalinitisha. <br />
“Okay!” Tyra alijibu kinyonge.<br />
“Take it easy.” (Usijali.)</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb1929af4368571964">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.12.<br />
<br />
<br />
“Okay!” Tyra alijibu kinyonge.<br />
“Take it easy.” (Usijali.)<br />
<span class="text_exposed_show"> Nilimpa jibu la kumfariji huku nikielewa kabisa alikuwa ameumia, pengine hakuwa na mazoea ya kukataliwa na wanaume kwa jinsi ambavyo Mungu alimpendelea na kumpa uzuri wa kila kitu. Kwa hakika lazima wavulana walikuwa wakimfuatilia sana, kila mmoja akitaka kuwa na uhusiano naye. <br />
<br />
Haukuwa uongo Tyra alikuwa mrembo, mimi mwenyewe nilikiri, kikwazo peke yake kilikuwa ni msichana wangu wa kwenye ndoto, tofauti na hapo nisingemwachia na sidhani kama kulikuwa na mwanaume yeyote duniani asiye na matatizo angeweza kuwekewa mkono begani na msichana mrembo kiasi hicho halafu akamwambia auondoe.<br />
<br />
Hatukuzungumza tena mpaka mwisho wa safari ya kukitembelea chuo kwa ajili ya utambuzi ingawa bado alikaa karibu na mimi, akionesha kama hajakerwa na kilichotokea. Mwisho tulirejea kwenye Ukumbi wa Nkrumah ambako mkuu wa kitivo alitushukuru wote kwa ushirikiano wetu na kuturuhusu kurejea mabwenini. Kwa sababu sikutaka kabisa uhusiano au mazoea na Tyra, niliondoka bila kumuaga.<br />
<br />
Nikiwa bwenini taswira yake iliendelea kunijia kichwani, moyo wangu ukaendelea kunithibitishia kabisa kuwa Tyra alikuwa ni msichana mrembo kiasi cha kudhani pengine yeye pia hakuwa binadamu.<br />
<br />
“Au Zamaradi kanitumia mpelelezi ili anipime? Yule msichana ni binadamu kweli?” Nilijiuliza maswali mengi mpaka nilipopitiwa na usingizi nikiwa bado sijapata majibu.<br />
<br />
Zamaradi akawadia akiwa na mwanangu Mina mikononi mwake, akaniwekea mtoto miguuni na kusimama pembeni huku sura yake ikiwa imekunjwa na macho yake kuwa mekundu. Siku hiyo ilikuwa ni ndoto tofauti na nyingine zote nilizowahi kuota siku za nyuma.<br />
<br />
“Yule msichana ni nani?” Akaniuliza akimsonta msichana aliyekuwa amesimama kando yake uso ukiwa umeelekezwa ukutani.<br />
“Nitamjuaje bila kumwona sura?”<br />
“Wewe hebu geukia huku.” Alimwamuru msichana huyo, akageuka kutuangalia, hakuwa mwingine bali Tyra.<br />
<br />
“Mwanafunzi mwenzangu.”<br />
“Nawaonya, kama mnasikia mnisikilize, nitawaua! Wewe binti huyu ni mume wangu, tuna mtoto mmoja, sitaki kabisa awe na uhusiano na mwanamke mwingine kwenye ulimwengu wenu, kaa naye mbali,” alifoka Zamaradi, Tyra akiwa kimya bila kusema chochote.<br />
<br />
Baada ya mzozo huo Zamaradi hakutaka kukaa, akamnyanyua mtoto na wote wakaondoka hadi ufukweni ambako walizama ndani ya maji na kupotea. Hapo hapo nikazinduka, Lameck kijana niliyepangwa kulala naye chumba kimoja alikuwa akiniamsha kunitaarifu kuwa muda wa chakula ulikuwa tayari.<br />
“Sijisikii kula Lameck.”<br />
“Sasa?”<br />
<br />
“Tumbo limejaa, acha nivae nifanye mazoezi kidogo ya kukimbia, ninaona kuna miinuko mizuri hapa mlimani inayotosha kabisa kuondoa kitambi.”<br />
“Wewe una kitambi Phillip?”<br />
“Ndiyo kinaanza.”<br />
<br />
“Acha utani, haya baadaye! Acha mimi nikapate msosi.” Aliongea Lameck na kuondoka akiniacha kwenye dimbwi la mawazo nikifikiria ndoto niliyoota na onyo lililotolewa na Zamaradi, nilielewa alikuwa hatanii, kama ningepuuza na kujiingiza kwenye uhusiano wa kimapenzi na mwanamke yeyote angeniua, alikuwa na wivu kupindukia. <br />
<br />
“Kwa hiyo ina maana nimeoa jini?” Nilijiuliza kichwani mwangu wakati nikivaa kaptura yangu ya khaki na raba za chapa ya DH, nilizonunuliwa na Mustapha kwa ajili ya mazoezi.<br />
Nilipomaliza kuvaa nilitoka nje na kuanza kukimbia taratibu nikipandisha na kushusha vilima mpaka nikafika kwenye daraja linalounganisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na eneo la Savei, hapa nikageuza na kuanza kurudi taratibu kurejea tena bwenini.<br />
<br />
Mita kama sabini hivi baada ya kuvuka lango kuu la kuingilia chuoni upande wa Chuo cha Ardhi, gari dogo aina ya Volkswagen New Model ya rangi nyeusi lilipunguza mwendo kando yangu kama vile mtu aliyekuwa akiliendesha alitaka kuniuliza njia, nikiwa na hofu nilishuhudia kioo kikishushwa, nikamwona msichana aliyevaa miwani mikubwa machoni akijaribu kunisemesha.<br />
<br />
“Phillip.” Nikashangaa aliponiita jina na kulazimika kuanza kutembea kisha kusogea dirishani. Alikuwa ni Tyra.<br />
“Vipi?”<br />
“Poa mambo?”<br />
“Safi tu.”<br />
<br />
“Naona unafanya mazoezi.”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Twende nikusogeze.”<br />
“Asante sana Tyra lakini nataka kukamilisha zoezi langu.”<br />
<br />
“Leo tu, twende nikupeleke mpaka bwenini kwako.”<br />
“Sitajisikia vizuri, acha tu nikimbie.”<br />
“Usiwe hivyo bwana.”<br />
“Tyra!”<br />
“Bee.”<br />
<br />
“Naomba unielewe, asante sana kwa msaada wako.” Nilijibu na kuanza kukimbia.<br />
Naye akaondosha gari lake taratibu na kuniacha, moyo ulikuwa ukinidunda kwa nguvu nikielewa kabisa macho ya Zamaradi yalikuwa yakiniangalia muda wote nikiongea na Tyra na nilijua usiku kwenye ndoto lazima angekuja na tungekuwa na ugomvi mwingine tena juu ya msichana huyo. Hakika nilishindwa nifanye nini.<br />
<br />
Nilirejea moja kwa moja bwenini ambako nilioga na baadaye kujitupa kitandani, sikuwa muumini wa dini hivyo hata kusali kabla ya kulala kuomba halikuwa jambo la muhimu, Ukristo kwangu ulikuwa ni jina la Phillip peke yake. <br />
<br />
Nilipitiwa na usingizi muda mfupi tu baadaye, cha kushangaza sikuota ndoto yoyote mpaka asubuhi nilipoamka na kuanza kujiandaa kwa kwenda darasani. Ni mimi niliyemwamsha Lameck ambaye alikuwa bado amelala. Nikaingia bafuni kuoga kichwani mwangu nikimfikiria Tyra, nilikosa njia ya kumweleza ukweli kuhusu mimi ili asizidi kunifuatilia kwani kufanya hivyo kungesababisha vifo vyetu sote.<br />
<br />
Nilikuwa mtu wa kwanza kuingia darasani, haukupita muda mrefu nikasikia muungurumo wa gari nje, sikusita kuchungulia na kuliona gari aina ya Land Rover Discovery New Model likiegesha, alikuwa ni Tyra kwenye gari jingine. <br />
<br />
Akashuka taratibu na kufunga mlango kisha kuanza kuingia darasani, macho yake yalipogongana na ya kwangu alishituka kama mtu aliyesahau kitu, akatabasamu na kurejea moja kwa moja hadi nje ambako alifungua gari lake na kutoa mfuko wa nailoni kisha kuanza kutembea nao kurejea darasani tena.<br />
<br />
Akaja mpaka mahali nilipokuwa nimeketi na kunyoosha mkono wake akinikabidhi mfuko huo, kwanza nilisita taswira ya Zamaradi ikiniijia kichwani. Nilijua kwa jinsi Tyra alivyoonekana kutekwa na mimi mfuko huo lazima ulikuwa ni zawadi.<br />
<br />
“Pokea tu Phillip kama utaona haifai unaweza kutupa jalalani au ukampa mtu mwingine au hata ukapeleka kanisani.” Aliongea Tyra kwa sauti ya chini iliyoonyesha masikitiko, akanilainisha na kunifanya nijikute nanyoosha mkono wangu na kuupokea mfuko huo bila kujua ndani yake kulikuwa na kitu gani.<br />
<br />
Baadaye darasa lilijaa, mhadhiri akaingia na kufundisha lakini sikumbuki kama nilielewa kitu chochote siku ile. Alipotoka tukapumzika kwa muda bila mimi kuufungua mfuko, ndipo mhadhiri mwingine tena akaingia na kuendelea mpaka mchana ndipo tukaingia bwalo la chakula, baada ya hapo nikaondoka kwenda bwenini ambako niliufungua mfuko wa Tyra na kukuta ndani yake kuna vifaa vya mazoezi.<br />
<br />
Badala ya kufurahi nilisikitika, mwili wangu ukawa umelegea kupita kiasi, sikuwa na desturi ya kusinzia mchana lakini nikajisikia usingizi na kulala ndani ya dakika kumi na tano. Zamaradi akawasili tena bila mtoto, mkononi mwake akiwa na mfuko wenye kung’ara na kuuweka mezani, kisha kuuchukua mfuko uliokuwa juu ya meza na kuondoka nao; nikazinduka usingizini na kukuta mfuko wa Tyra haupo.<br />
<br />
Haraka nikanyanyuka na kuufungua mfuko huo, kulikuwa na vifaa vya michezo, mkufu na pete ya kung’ara vilivyotengenezwa kwa madini ambayo sikuyaelewa. Zamaradi alikuwa ameniletea vifaa hivyo na kuondoka na vifaa vya Tyra, moyo wangu ukajawa na furaha, nilipomaliza kuvivaa, Lameck aliingia.<br />
<br />
“Duh! Mshikaji naona bling-bling! Umekuwa Jay Z, mawe ya uhakika mwanangu, inaonekana wazazi wako wako vizuri. Maana huu ni mtaji wa mtu wa biashara ya duka la jumla.”<br />
“Acha utani wako wewe.”<br />
<br />
“Haki ya nani tena! Hizi ni almasi, Tanzanite na Ruby, mimi mtoto wa Mererani nafahamu kila kitu.” Lameck aliongea akionesha mshangao, katika maisha yangu sikuwahi kukutana na madini ya aina yoyote hivyo hata sikuelewa thamani ya vito nilivyoletewa na Zamaradi.<br />
<br />
“Ulivitoa wapi mshikaji wangu?”<br />
“Nilipewa Zawadi.”<br />
“Na nani?”<br />
Kigugumizi kikanishika.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb191b1e7181842206">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.13.<br />
<br />
NILIOGOPA sana kumwambia Lameck ukweli, isingekuwa rahisi kuniamini hasa kama vile vitu vingekuwa kweli na thamani kubwa kama anavyosema. Nilibaki kimya nikimwangalia nikijaribu kufikiria jibu la kumwambia, lakini nilikosa.<br />
<br />
Hapo sasa Lameck naye akapata wasiwasi kidogo juu yangu, niliweza kugundua hilo kutokana na jins alivyokuwa akiniangalia. Kwa hakika macho <span class="text_exposed_show">ya Lameck yalikuwa yananipa ujumbe fulani.<br />
“Mbona umenyamaza ghafla rafiki yangu?”<br />
“Hapana.”<br />
<br />
“Sasa hivyo vitu vyenye thamani kubwa umevipata wapi?”<br />
“Lakini Lameck si nimeshakuambia kwamba nimepewa zawadi?” Nikamjibu kwa kumkazia uso.<br />
“Ni dhambi kujua mtu aliyempa rafiki yangu zawadi nzuri na za thamani kama hizi?”<br />
“Sijasema hivyo, lakini unatakiwa tu kufahamu kwamba ni zawadi.”<br />
“Nahisi kuna kitu unanificha.”<br />
<br />
“Wewe mbona unanichunguza sana? Kitu gani ninachokuficha?” Nikamwambia Lameck kwa hasira.<br />
Sikutaka kupoteza muda, nilimalizia kuvaa viatu kisha nikaondoka zangu pale bwenini na kumuacha akiwa anajiuliza maswali mengi kichwani mwake. Lengo langu la kuondoka kwa hasira ilikuwa ni kumfanya asiniulize tena maswali kuhusu vile vitu.<br />
Siku zote sikupenda kabisa kuulizwa maswali ambayo yanahusiana na mwanamke wangu wa ndotoni. Nilipotoka bwenini nilianza kufanya mazoezi ya kukimbia kama kawaida. Siku hiyo nilibadilisha ratiba.<br />
<br />
Nilitaka kuona kama uwezo wangu wa kubana pumzi ulikuwa umeongezeka. Sikuishia Savei kama siku nyingine, nilishuka na barabara mbele kidogo ya daraja linalotenganisha Savei na Chuo Kikuu, nikanyoosha hadi Mlimani City, nikakata kulia mbele ya sheli iliyokuwa barabarani kisha nikaendelea kukimbia nikiifuata Barabara ya Sam Nujoma.<br />
<br />
Siku hiyo nilijisikia vizuri sana kuliko siku nyingine, hata uwezo wangu wa kubana pumzi uliridhisha kabisa. Niliongeza mwendo hadi kwenye mataa ya kuongozea magari yaliyopo kwenye makutano ya Barabara ya Sam Nujoma na ile ya Chuo Kikuu.<br />
<br />
Hapo nikakata kulia kuifuata Barabara ya Chuo Kikuu, huku mawazo yangu yakiwa juu ya mlima mrefu na mkali uliokuwa mbele yangu, baada ya kupita geti la kuingilia chuo. Nilijikaza na kujipa moyo, kisha nikaendelea kukimbia taratibu huku nikihakikisha nabana pumzi zangu vizuri. Nilimaliza kupanda mlima ule vizuri bila kuchoka, nikiwa nakaribia kufika Utawala, gari aina ya Volkswagen ilinipita na kuegesha pembeni, kisha msichana mmoja mrembo sana.<br />
<br />
Alipogeuka nyuma, nikakutana na sura nzuri ya kuvutia ya Tyra. Nikashtuka sana!<br />
“Samahani naomba usimame Phillip,” Tyra akaniambia, nami nikasimama nikiwa nahema kwa kasi.<br />
“Samahani kwa kukusumbua.”<br />
“Usijali, lakini naweza kumaliza mazoezi yangu tafadhali?”<br />
“Unaweza lakini kuna kitu nataka kutoka kwako.”<br />
“Nini?”<br />
<br />
“Kwanza hongera sana kwa mazoezi, unajitahidi sana. Sijategemea kama una nguvu nyingi kiasi hiki. Nimekufuatilia kuanzia ulipokuwa unatoka. Hongera wewe ni mwanaume wa shoka.”<br />
“Ahsante, naweza kwenda?”<br />
“Hapana.”<br />
<br />
“Lakini ningependa kumaliza kwanza mzunguko wangu.”<br />
“Najua Phillip, naomba uwe mtulivu basi jamani, unisikilize kwanza.”<br />
“Sawa, unasemaje?”<br />
“Zawadi zangu vipi, ulizipenda?” Tyra akaniuliza.<br />
<br />
Swali lake hilo likanifanya nimkumbuke Zamaradi wangu, nikahisi lazima usiku angenifuata na kuniletea fujo. Katika maisha yangu sikupenda kabisa kugombana na Zamaradi, ingawa ni kweli kama siyo masharti yake makali, ningeamua kutoka na Tyra.<br />
<br />
Alikuwa mwanamke mzuri mwenye sifa zote, kwa mwanaume yeyote ambaye amekamilika, isingekuwa rahisi kukubali kupitwa na mwanamke mrembo kama Trya. Jibu la kumpa sikuwa nalo.<br />
“Mbona hunijibu au ndiyo umegawa kwa watu kama nilivyokuambia ikiwa mbaya ugawe?”<br />
“Sijafanya hivyo.”<br />
<br />
“Sasa umezipenda?”<br />
“Ndiyo!” Nikamjibu haraka ili kukwepa maswali yake mengine.<br />
“Kweli?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Mbona hujazivaa?”<br />
<br />
“Usijali nitavaa, kwa kuwa ninazo nyingi ndiyo maana nimevaa hizi leo.”<br />
“Sawa, nina jambo jingine muhimu zaidi ninalotaka kutoka kwako.”<br />
“Nini?”<br />
“Naomba nitoke na wewe leo jioni.”<br />
“Twende wapi?”<br />
“Nataka kukupa ofa ya chakula cha usiku.”<br />
“Wapi sasa?”<br />
<br />
“Siyo mbali hapo Samaki Samaki!”<br />
“Ni wapi?”<br />
“Mlimani City.”<br />
“Poa,” nikajibu haraka bila kufikiria.<br />
“Haya endelea na mazoezi yako!” Akaniambia.<br />
<br />
Sikuwa na muda wa kupoteza zaidi ya kurudi zangu barabarani na kuendelea na mazoezi kama kawaida. Kitu kilichokuwa kinanisumbua kwa kiasi kikubwa ni juu ya mtoko wangu na Tyra, niliamini kwa vyovyote vile Zamaradi wangu asingekubali, lazima ningegombana naye.<br />
Nilikimbia hadi bwenini, nilipomkuta Lameck akiwa ametulia kitandani kwake. Aliponiona naingia chumbani, alionekana kushtuka sana, kisha alipokutanisha macho yake na yangu, akanywea.<br />
<br />
“Nisamehe rafiki yangu Phillip, sikuwa na nia ya kukosana na wewe, sikujua kama hukupendezwa na maswali yangu,” akasema Lameck akionekana kumaanisha kutoka moyoni mwake.<br />
“Usijali yameisha,” nikamjibu kwa kifupi kisha nikaingia bafuni.<br />
<br />
Nilipotoka niliishia kupanda kitandani na kujipumzisha kidogo. Muda mfupi baadaye nilipitiwa na usingizi, saa 2:17 nilishtuka usingizini. Nikakumbuka ahadi yangu na Tyra. Pamoja na kwamba sikutaka kuwa naye kimapenzi, lakini sikutaka kukataa mwaliko wake. Nikaanza kujiandaa kwa ajili ya kwenda Mlimani City.<br />
<br />
***<br />
Tulikuwa tumekaa kwenye meza iliyokuwa na viti viwili tu; sehemu ambayo haikuwa na watu wengi, kwa hiyo tuliweza kusikilizana vizuri. Mezani kulikuwa na sahani mbili za chips samaki. Tukawa tunakula huku tukizungumza.<br />
<br />
Muda wote Tyra alikuwa akitabasamu na alionekana wazi kufurahishwa na kukubali kwangu ofa yake. Alikuwa amevaa nguo nzuri za kuvutia zilizoongeza uzuri wake. Ni kweli Tyra alikuwa mwanamke mrembo sana, nilimtamani na kumpenda hakika, lakini niliyapenda zaidi maisha yangu, maana Zamaradi alinihakikishia kwamba siku nikitembea na mwanamke mwingine angeniua, sikutaka jambo hilo litokee.<br />
<br />
“Ahsante sana kwa kuja!” Alisema Tyra akishusha uma wenye chips kinywani mwake.<br />
“Usijali ilikuwa lazima nije.”<br />
“Kwa nini?”<br />
“Nakuheshimu, najua una marafiki wengi sana, lakini umechagua kutoka na mimi, hiyo ni heshima kubwa sana ambayo ilikuwa lazima niikubali!”<br />
“Nimefurahi kusikia hivyo!”<br />
<br />
“Lakini Phillip naomba usinifikirie vibaya kwa swali nitakalokuuliza.”<br />
“Mbona unanitisha? Swali gani hilo?”<br />
“La kawaida tu, hivi una mpenzi?” Tyra akaniuliza.<br />
“Umesema?”<br />
<br />
“Una mwanamke unayetoka naye?” Akauliza tena.<br />
Mwanzoni nililisikia vizuri sana swali lake, lakini nilijifanya sijasikia ili nipate nafasi ya kufikiria jibu la kumpa.<br />
“Mwanamke?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Mpenzi?”<br />
“Ndiyo maana yangu!”<br />
“Lakini kwa nini umeniuliza swali hilo?” Nikamwuliza nikiwa nimetuliza macho yangu usoni mwake.<br />
“Jibu kwanza!”<br />
<br />
Taswira ya Zamaradi wangu ikanijia, nilitamani sana kumwambia sina mpenzi, lakini niliogopa ugomvi na Zamaradi. Sasa nikawa sina jibu, sikujua nikubali kuwa ninaye au sina. Nikabaki namtolea macho.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb190d633551529734">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.14.<br />
<br />
NDANI ya moyo wangu niliona kabisa cheche za mapenzi zikiwaka lakini Zamaradi ndiye alikuwa akinitesa. Ni kweli kabisa na hili napenda nikiri hata mbele yenu ni kwamba nampenda sana Zamaradi na mwanangu wa ndotoni Mina lakini ananinyima sana uhuru. <br />
<br />
Hataki niwe na mwanamke mwingine tofauti na yeye, wakati anajua wazi kabisa kwamba yeye hawezi kuja kuishi na mi<span class="text_exposed_show">mi katika ulimwengu huu unaoonekana. Tyra alikuwa na kila kitu kizuri. Mwanamke mzuri. Macho mazuri. Anajua kuzungumza kwa pozi na kumfanya mwanamume yeyote aliyekamilika achanganyikiwe kwa maneno yake matamu na kwa namna anavyotingisha midomo yake wakati anapozungumza.<br />
<br />
Kwa hakika nilimtamani, nilimpenda na ningejisikia faraja sana kama ningepata walau usiku mmoja akiwa amelala kando yangu, lakini kama ningethubutu kufanya hivyo usiku huo ungekuwa wa mateso na taabu kwangu maana lazima Zamaradi angekuja na kuniadhibu.<br />
<br />
Nilibaki nimetulia macho yangu yakiwa yametua juu ya uso wa Tyra ambaye alikuwa amependeza kuliko mwanamke yeyote eneo la Mlimani City usiku huo.<br />
“Phillip,” aliita Tyra akimuangalia kwa macho yaliyojaa mahaba mazito.<br />
“Nakusikia.”<br />
<br />
“Lakini mbona hujajibu swali langu?”<br />
“Huwa sipendi kuzungumza mambo ya siri kiasi hicho.”<br />
“Mambo ya siri? Unamaanisha nini?”<br />
“Si umeulizia juu ya mapenzi? Kwa kawaida huwa naona haya kuongelea mambo ya mapenzi hadharani,” nilijiumauma huku mwenyewe nikijua kwamba jibu nililolitoa halikuwa sahihi.<br />
<br />
“Kwani unaposema hadharani unamaanisha nini?”<br />
“Mbele za watu.”<br />
“Lakini hapa uko na mimi tu!”<br />
“Lakini lengo lako hasa ni nini?”<br />
“Nataka kujua!”<br />
<br />
“Halafu ukishajua?”<br />
“Samahani kama nitakuwa nimekuudhi.”<br />
“Usijali lakini uelewe kwamba huwa sipendi kuulizwa sana juu ya mambo ya mapenzi.”<br />
“Kwa hakika wifi yangu anafaidi sana. Amepata mwanaume mwenye msimamo mkali, naamini wewe ni baba bora.”<br />
“Asante.”<br />
<br />
Kitu ambacho Tyra hakukielewa ni kuwa maneno yake yalikuwa sawa na msumari wa moto uliotua katikati ya moyo wangu maana nilikuwa nampenda sana lakini nisingeweza kufanya kitu chochote kwa woga wa Zamaradi ambaye alikuwa na wivu kupindukia.<br />
<br />
Nikamtulizia macho yangu nikimkagua kuanzia chini hadi juu kwa hakika sikuona kasoro yake. Kwa mara nyingine napenda nikiri kwamba Tyra alikuwa mwanamke mzuri sana, tena kuliko hata Zamaradi wangu, mwanamke ambaye ndiye aliyenifundisha mapenzi na kunitia upofu wa kutoona wanawake wengine.<br />
<br />
“Mbona huna furaha?” Tyra aliniuliza baada ya kugundua tofauti niliyokuwa nayo ghafla.<br />
“Hapana, nipo sawa.”<br />
“Kwa muda mfupi niliokuwa na wewe nimeweza kugundua mambo mengi sana, naweza kusema kwa namna fulani nimeweza kuzijua tabia zako. Kwa hiyo ninapokuambia umebadilika namaanisha hivyo.”<br />
<br />
“Ni kweli kuna kitu nimekikumbuka kimenichanganya sana.”<br />
“Ni nini hicho?”<br />
“Kuna msiba ambao nimepata taarifa zake leo. Umenishitua sana.”<br />
“Wa nani tena?”<br />
<br />
“Ni Frank. Nilikuwa nasoma naye tangu shule ya msingi hadi kidato cha nne, amekufa, tena akiwa anakwenda chuoni Morogoro.”<br />
“Alipangiwa wapi?”<br />
“Chuo Kikuu cha Mzumbe.”<br />
“Ilikuwaje?”<br />
<br />
“Basi alilokuwa anasafiria tokea nyumbani kwao Njombe lilipinduka kwenye eneo la Mlima wa Kitonga, naambiwa maiti yake imeharibika sana. Inaniuma maana amekufa akiwa bado hajatimiza ndoto zake.”<br />
“Pole sana.”<br />
“Asante.”<br />
<br />
“Kwa kweli, kwa hilo unapaswa kuumia lakini usijali kila kitu kinapangwa na Mungu.”<br />
“Nashukuru kwa kunipa moyo.”<br />
Tyra alikuwa mwema sana kwangu, alitumia muda mwingi kuhakikisha nakuwa mwenye furaha. Msiba ule ulimgusa sana lakini hakujua kilichokuwa nyuma ya maelezo yangu yote.Ukweli ni kwamba hapakuwa na mtu yeyote aliyefariki kama nilivyomwambia, badala yake ilikuwa ujanja wangu wa kumfanya asiniulize maswali zaidi. <br />
<br />
Tukaendelea kula na kunywa kwa furaha hadi ilipotimu saa 5:30 za usiku ndipo Tyra akasema turudi chuoni. Wazo lake nilikubaliana nalo. Tukainuka kwa pamoja tukiwa tumeshikana mikono tukitembea moja kwa moja hadi kwenye maegesho ya magari tukaingia kwenye gari lake aina ya Volkswagen New Model.<br />
<br />
Nilikaa upande wa abiria Tyra akiwa amekalia usukani na kuanza kuendesha taratibu tukitokea upande wa Savei. Moja kwa moja Tyra akaendesha gari hadi Hall 5 ambako ndipo nilipokuwa naishi. <br />
<br />
Kabla ya kushuka Tyra akainama kidogo upande wangu akasogeza midomo yake karibu na wangu, nilishagundua alichotaka kukifanya. Ni wazi kwamba Tyra alitaka kunibusu, kitu ambacho sikuwa tayari kufanya. <br />
“Hapana.”<br />
<br />
“Tafadhali kidogo tu,”alisema Tyra akionekana kuzidiwa na mahaba mazito.<br />
“Hatuwezi kufanya hivyo, hatujafikia hatua hiyo. Tafadhali naomba uache. Acha nishuke niende zangu kulala!” nilimwambia kwa kujitetea lakini ndani ya nafsi yangu nilikuwa natamani sana.<br />
<br />
Hata hivyo, tamaa yangu ilikuwa zaidi ya hapo, nilitamani sana nibadilishane naye mate ikiwezekana nihamie naye katika ulimwengu mwingine wa huba. Ulimwengu ambao huwa nacheza na Zamaradi wangu kila siku lakini kwa kiumbe hiki kilichopo mbele yangu nilihisi ningepata ladha tofauti zaidi ya ile ambayo ninaipata kwa Zamaradi.<br />
<br />
Maneno yangu hayakumfanya Tyra aelewe ninachomwambia bado aliendelea kuinama huku akinivuta akiwa amedhamiria kunipiga busu. Ni kweli nilitamani sana, cheche za mapenzi ziliwaka ndani ya mwili wangu lakini nisingeweza kuruhusu jambo lile litokee maana ni sawa na kuruhusu kifo! <br />
<br />
Kwa haraka sana nilifungua mlango kisha nikaubamiza kwa nguvu, nikakimbia ndani nikimwacha Tyra akiwa haamini kilichotokea. Kitu ambacho nilishukuru ni kwamba hakuna mwanaume yeyote aliyeshuhudia kitendo kile maana kwa vyovyote vile ningefikiriwa tofauti.<br />
<br />
Isingekuwa rahisi mtu kuamini kwamba mwanamke mrembo kama Tyra anaweza akakataliwa. Hata hivyo, utetezi wangu ambao ni wa siri hakuna ambaye angeujua wala kuuamini ndiyo maana nikaamua kufanya suala lile siri yangu peke yangu. Ni mchana huohuo nilitoka kugombana na Lameck ambaye alikuwa ananihoji sana juu ya zawadi nilizokuwa nimeletewa na Zamaradi wangu.<br />
<br />
Nisingeweza kutamka chochote kuhusu uhusiano wangu na Zamaradi. Bila woga nilitembea mpaka kilipo chumba changu na kujaribu kusukuma mlango uliokuwa wazi. Nikaingia na kwenda kuketi moja kwa moja kitandani kwangu. Lameck akashituka usingizini.<br />
“Vipi kaka?” Lameck akanisalimia.<br />
<br />
“Poa, mambo?”<br />
“Safi bwana, naona ulikuwa kwenye mitoko, ukila kuku!”<br />
“Ah! Wapi bwana. Nilialikwa tu chakula cha usiku hapo Samaki-Samaki.”<br />
“Okay. Poa bwana, acha nilale maana kesho nataka kudamkia mazoezini asubuhi-asubuhi.”<br />
<br />
“Vizuri sana, naona umekuwa mshirika wangu sasa, usisahau kuniamsha. Lakini labda nikuulize: Na wewe unataka kutoa kitambi?” Niliuliza huku nikicheka.<br />
<br />
“Ha! Ha! Ha!” Lameck aliishia kucheka badala ya kujibu.<br />
Nikanyoosha mkono wangu kwenye swichi iliyokuwa inaning’inia kitandani kwangu, nikazima taa. Nikaanza kubembeleza usingizi, cha ajabu ulinichukua haraka kuliko siku nyingine yoyote.<br />
<br />
***<br />
Dalili zilikuwa ni zile zile, manukato yale yale lakini leo Zamaradi alinitembelea akiwa tofauti kabisa. Uso wake wa kimahaba haukuonekana, tabasamu tamu lilipotea. Hata unadhifu wake hakuwa nao, kilichoonekana ni wazi kabisa Zamaradi alikuwa amekuja kunitembelea kwa ugomvi.<br />
<br />
Hakuwa amechana nywele na macho yake yalikuwa mekundu kama alikuwa ametoka kulia muda mfupi uliopita au alikuwa anapuliza moto wa kuni wenye moshi mkali. Akanisogelea akichezesha midomo yake huku akiwa amekunja ndita usoni.<br />
<br />
“Phillip nakuambia nitakuua, nitakuua Phillip!” Zamaradi alisema kwa hasira huku akitetemeka, machozi yakichuruzika mashavuni mwake.<br />
Nikatetemeka kwa woga, nikakiona kifo mbele yangu.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb1901aa9070388164">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.15.<br />
<br />
NILIYATOA macho yangu nikiwa nimepoteza kabisa matumaini ya kuendelea kuishi. Zamaradii alionekana kukasirika sana, hakutaka mwanaume wake nichezewe na mwanamke mwingine yeyote. Nilitetemeka huku nikijaribu kumuomba msamaha Zamaradi ambaye alionekana kuwa na hasira sana.<br />
“Naomba usiniue mpenzi wangu nakupenda.”<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Kama unanipenda ungenidhalilisha?”<br />
“Lakini sijafanya chochote mama, alinialika tu chakula cha usiku.”<br />
“Na pale kwenye gari mlikuwa mnataka kufanya nini?”<br />
“Kwani wewe hujaona kama nilimkimbia? Siwezi kukusaliti mke wangu, nakupenda sana. Nimekuja hapa kwa ajili ya masomo tu na siyo vinginevyo.”<br />
“Ina maana wewe huwezi kujua kwamba yule msichana anakutaka?”<br />
<br />
“Sijajua mpenzi.”<br />
“Una uhakika?”<br />
“Ni kweli mpenzi sifahamu chochote.”<br />
“Acha utani, atakupotezea maisha yako yule.”<br />
“Mama hata kama nikijua au akisema, siwezi kumkubalia, maana nakupenda wewe tu.”<br />
<br />
“Unatakiwa kujua kwamba nitakuua, sina mzaha na hilo kabisa, nitakuua Phillip, tena nakuhakikishia mwanamke yeyote ambaye atajaribu kutembea na wewe, naye nitamuua.”<br />
“Nisamehe Zamaradi wangu, siwezi kufanya hivyo mpenzi.”<br />
Baada ya kusema maneno haya Zamaradi alitoweka, ghafla nikashtuka usingizini. Nikamuona Lameck akiwa ameniangalia kwa wasiwasi.<br />
<br />
“Vipi kaka?” Akaniuliza.<br />
“Poa.”<br />
“Mbona kama ulikuwa unaweweseka?”<br />
“Ndoto tu.”<br />
“Pole sana rafiki yangu.”<br />
<br />
“Ahsante, vipi saa ngapi?”<br />
“Saa kumi na moja kamili.”<br />
“Kuhusu mazoezi upo tayari?”<br />
“Ndiyo maana nimeamka muda huu.”<br />
“Sawa twende.”<br />
<br />
“Poa.”<br />
Nikaamka kitandani kisha nikavaa nguo zangu za mazoezi, Lameck naye akavaa kisha tukatoka nje ya chumba chetu tukaenda barabarani.<br />
“Vipi, twende mpaka wapi?”<br />
“Naona tuzunguke chuo tu.”<br />
<br />
“Hapana bwana itakuwa poa kama tutakwenda mpaka Morocco na kurudi, hapo tutakuwa tumepasha vizuri zaidi.”<br />
“Sawa.”<br />
“Haya, moja, mbili, tatu...” alihesabu Lameck na alipofika tatu tulianza kukimbia kwa pamoja.<br />
<br />
Mwili wangu ulipokea vizuri sana mazoezi yale lakini kiakili sikuwa sawa kabisa, muda mwingi nilihisi kama Zamaradi alikuwa mbele yangu. Siku hiyo usiku aliponijia katika ndoto alinitishia sana.<br />
<br />
Moyo wangu ulikuwa hauna amani, ni kama kimwili nilikuwa barabarani lakini kiroho nilikuwa nikimuwaza Zamaradi. Tulikimbia taratibu tukikata kushoto katika mzunguko wa Mlimani City na kunyoosha moja kwa moja hadi kwenye mataa ya Mwenge tulipokata kulia tukiifuata Barabara ya Ali Hassan Mwinyi.<br />
<br />
Kwenye mataa ya Bamaga tulinyoosha moja kwa moja tukikimbia njiani tukikutana na watu wengine wakifanya mazoezi kama sisi. Kwa hakika nilikuwa nimechoka sana niliishiwa na pumzi lakini sikutaka kukatisha mazoezi maana Lameck rafiki yangu asingejisikia vizuri.<br />
<br />
Nusu saa baadaye tulifika kwenye mataa ya Morocco tulipogeuza na kuanza tena safari ya kurudi chuoni. Lameck sasa akaonekana ameanza kuchoka lakini nilimpa moyo tukajitahidi kukimbia taratibu kwa safari ya kurudi chuo.<br />
<br />
Tulifika chuoni baada ya dakika arobaini na tano ikiwa ni robo saa zaidi ya muda tuliokwenda Morocco. Nilijua sababu kwamba uchovu wakati wa kurudi ulikuwa mkali zaidi. Tulifikia kwenye viwanja vya mchezo wa mpira wa kikapu.<br />
“Hongera sana Lameck sikutegemea kama una uwezo mkubwa kiasi hiki,” nilimwambia Lameck nikiwa nimemkumbatia.<br />
<br />
“Hata wewe pia hongera, umenisaidia sana kumaliza mazoezi.”<br />
“Nadhani sasa vitambi havina nafasi tena.”<br />
Wote tukacheka kwa furaha. Dakika chache baadaye watu wakaanza kuja uwanjani kwa ajili ya kufanya mazoezi ya mpira wa kikapu. Ni mchezo niliokuwa nikiupenda sana, kwa mara ya kwanza niligundua kwamba chuoni pale kulikuwa na timu ya mpira wa kikapu.<br />
<br />
“Kaka, kaka wamenitamanisha sana hawa jamaa, lazima na mimi nijiunge nao. Napenda sana basketball.”<br />
“Kweli?”<br />
“Ndiyo mchezo niupendao.”<br />
“Sawa tutaona.”<br />
<br />
“Nakushauri usiondoke, ikiwa nitapewa namba nitakuonyesha maajabu.”<br />
Kutokana na mapenzi yangu makubwa ya mchezo huo, taratibu nilianza kusahau mambo ya Zamaradi akili yangu ikahamia katika mpira wa kikapu. Nilichokifanya ni kwenda moja kwa moja kwa wale jamaa kisha nikaomba kuonana na kiongozi wao.<br />
“Mambo vipi?”<br />
<br />
“Poa shwari?”<br />
“Nipo poa bwana, samahani nataka kujiunga na timu yenu.”<br />
“Unaweza?”<br />
“Nadhani mnipe namba, mtanihukumu uwanjani.”<br />
“Karibu sana.”<br />
<br />
Baada ya pale nilitambulishwa kwa wachezaji wengine kisha tukaanza mazoezi madogo madogo ya viungo, baadaye tukaingia uwanjani. Uwezo wangu ukawachanganya, ingawa ilikuwa siku ya kwanza kucheza nao walikubali kwamba nilikuwa na kipaji kikubwa cha kucheza mchezo huo.<br />
<br />
Baada ya kumaliza mechi, Lameck alinikumbatia kwa furaha na kunipongeza. Hakuamini kama ningeweza kuonyesha uwezo mkubwa kiasi kile. Kwake ilikuwa maajabu makubwa. Tukaondoka kuelekea kwenye chumba chetu.<br />
Kila mmoja kwa wakati wake aliingia bafuni tukaoga kisha tukaenda mgahawani kupata kinywa, hapo ndipo siku yetu mpya ilipoanza.<br />
<br />
***<br />
Jioni baada ya kutoka kwenye kipindi nilivaa nguo za mazoezi kisha nikaenda uwanjani, sasa mchezo wangu mkubwa ukawa ni mpira wa kikapu. Wachezaji wengine wote hawakuchoka kunisifia kwa uwezo wangu mzuri wa kucheza mchezo huo.<br />
<br />
Kila siku nikawa nakwenda uwanjani na kujumuika na wenzangu. Mashabiki wa mchezo huo wakaongezeka, lakini kuna kitu cha kushangaza kidogo kilijitokeza, watazamaji wengi walikuwa ni wasichana kuliko wanaume ambao walikuwa wachache!<br />
Haikujulikana siri ya wanawake kuwa mashabiki wakubwa wa mchezo huo, hadi siku moja Lameck aliponiambia habari zilizonishangaza sana; wengi walikuwa wanakuja pale uwanjani kuniangalia mimi!<br />
<br />
“Unamaanisha nini Lameck?”<br />
“Wanakufuata wewe kaka!”<br />
“Ili wanifanye nini?”<br />
“Kaka utanashati wako umekuwa tatizo, wananong’ona huku tunawasikia, lakini kuna mmoja huyo kaka, usimlazie damu.”<br />
<br />
“Ni nani?”<br />
“Yule pale...” akasema akisonza kidole kumuelekea msichana mmoja aliyekuwa amesimama pembeni.<br />
“Ni mwanafunzi wa hapa?”<br />
“Ndiyo, yeye anasoma Sheria.”<br />
“Umeongea naye?”<br />
<br />
“Ndiyo, tena anasema anataka kuonana na wewe,” akaniambia.<br />
Moyoni nilishtuka sana, maana namjua vizuri sana Zamaradi alivyo mkorofi ninapozoeana na wanawake. Kwa kumtazama kwa mbali tu, nilikiri kuwa alikuwa mwanamke mzuri sana, tena kuliko Tyra. Pamoja na kwamba nilimhofia Zamaradi, lakini nilitamani sana japo nimuone kwa karibu.<br />
<br />
“Hebu mwite nimuone kwa karibu,” nikamwambia Lameck nikijichekesha, hakujua ndani ya moyo wangu nilikuwa na maumivu makubwa kiasi gani.<br />
Alichokifanya Lameck ni kumuonesha yule msichana ishara ya kumuita, muda ule ule akaanza kupiga hatua za taratibu kuja sehemu tuliyokuwa tumesimama. Moyo wangu ukafa ganzi, kadiri alivyozidi kusogea karibu zaidi, ndivyo uzuri wake ulivyozidi kuwa hadharani!<br />
“Mh! Sasa kama Zamaradi kweli ataniua, nipo tayari aniue tu!”<br />
<br />
“Hello Phillip, I am very grateful to meet you. Also thanks for accepting to talk to me. This is an opportunity that I will not play with. Surely my heart is so refreshed!” (Halo Phillip, nimefurahi sana kukutana na wewe. Pia nashukuru kwa kukubali kuzungumza na mimi. Hii ni bahati ambayo sitaichezea. Hakika moyo wangu umesuuzika vilivyo!) Sauti tamu kutoka kwa msichana huyo mzuri ilipenya ndani ya ngoma za masikio yangu kama shoti ya umeme.<br />
<br />
Hapo mtazamo wangu ulibadilika, yule msichana alikuwa zaidi ya Tyra ambaye nilihisi uzuri wake ulimzidi Zamaradi. Nikiwa nimesimama midomo yangu ikigoma kuongea chochote, yule msichana aliinua mkono wake akitaka kukutanisha na wangu. Nami nikainua wangu na kuupokea wake, hapo hapo nikaona taswira ya Zamaradi mbele yangu.<br />
“Nasema nitakuua...nitakuua Phillip...” alisema kwa sauti.<br />
Nikatoa macho kwa woga.<br />
<br />
Je, nini kitatokea? FUATILIA BAADAE USIKU EPISODE ZINGINE 5!!</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b8dbd8b39732672093"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.......EP.16<br />
<br />
<br />
Msimamo aliokuwa nao Phillip kwa muda mrefu sana umebadilika baada ya kuingia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kukutana na wanawake warembo kuliko kawaida. Katika maisha yake hakutegemea kama kungeweza kutokea mwanamke mrembo kumzidi Zamaradi. <br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Alimpenda sana Zamaradi wake na mwanaye Mina ambaye alifunga naye ndoa chini ya bahari kwa wazazi wake. Kwake alimaliza kila kitu akikutana naye kwenye ndoto. Hali ilibadilika alipoingia chuoni, maana siku ya kwanza alikutana na msichana aitwaye Tyra ambaye aliuteka moyo wake. <br />
<br />
Pamoja na kwamba Tyra mwanachuo aliyefika chuoni hapo kwa lengo la kusoma Uchumi ili afanye biashara za baba yake kuwa na uwezo wa kifedha na kubadili magari, Phillip ambaye alikiri moyoni kwamba alimpenda alishindwa kuwa naye kwa hofu ya Zamaradi.<br />
<br />
Mara kadhaa Zamaradi amekuwa akimtokea na kumuahidi kumuua iwapo angemsaliti kwa kutembea na mwanamke mwingine tofauti na yeye. Akiwa ameshamiri zaidi katika mazoezi huku akijitahidi kumkwepa Tyra, sasa amejiunga na timu ya mpira wa kikapu chuoni hapo. <br />
<br />
Kitu cha kushangaza siku chache baada ya yeye kujiunga katika timu hiyo mashabiki wameongezeka kuishangilia lakini wasichana ndio ambao wameongezeka kwa kiasi kikubwa zaidi. Phillip hakujua sababu ya ongezeko hilo la wanawake uwanjani lakini Lameck anamtoa mchanga machoni na kumweleza kwamba wanawake hao hufika viwanjani hapo kwa lengo la kumtazama.<br />
<br />
Siku moja akiwa ndio anamaliza mazoezi Lameck anamkutanisha na mmoja wa wasichana hao, wakiwa katika kusalimiana Phillip anakiri kuwa msichana huyo ni mzuri kuliko Tyra ambaye aliamini ni mrembo zaidi ya Zamaradi.<br />
Je, nini kitatokea? SONGA NAYO...<br />
<br />
SIKUTEGEMEA kama hali hii ingenipata lakini kwa mara ya kwanza nilianza kumchukia Zamaradi. Mwanamke huyo wa ndotoni alionekana kuwa kikwazo katika maisha yangu. Ananifanya nikose wanawake wengine wazuri zaidi yake.<br />
<br />
Ni ukweli kwamba mimi si mwanamme mhuni, lakini nina moyo unaopenda. Pengine ningeweza kuwa mwaminifu sana kwake na kutokumsaliti kabisa kama angekuwa anatokea katika maisha ya kawaida na kuwa nami lakini mapenzi yetu yanaishia kwenye ndoto tu.<br />
<br />
Kwa nini ananitesa? Kwa nini ananinyanyasa? Zamaradi kwa nini unanifanyia hivi? Nilimuangalia msichana aliyekuwa mbele yangu huku woga ukiendelea kunitawala ndani ya moyo wangu maana nilimfahamu vizuri sana Zamaradi.<br />
<br />
Nilipata burudani ya kipekee kutazama sura ya mwanamke mzuri mwenye umbo namba nane, nywele ndefu, macho mazuri na kila kilicho kizuri katika mwili wake lakini nilijua mwisho wake ungekuwa mbaya usiku maana Zamaradi asingekubali kuniacha hivi hivi. Ni jambo lililonitesa na kuniumiza sana. <br />
<br />
Nilitumia sekunde thelathini nzima nikiwa kimya namtazama msichana huyo ambaye tabasamu lake lilikuwa ndiyo kama kitambulisho chake cha kwanza kwangu. Kwa aibu nikaachana na mawazo ya Zamaradi kisha nikafungua kinywa changu, nikachezesha midomo yangu na kuanza kuzungumza.<br />
<br />
Moyo wangu ulikuwa unatetemeka, mwanamke aliyekuwa amesimama mbele yangu alikuwa mzuri sana, tatizo ni Zamaradi ambaye haishi vitisho kila kukicha.<br />
“Do not worry beautiful, I cannot turn down your call.” (Usijali mrembo, siwezi kukataa wito wako.)<br />
<br />
“Thank you very much, most of the girls here fight for a chance to meet you.” (Ahsante sana, wasichana wengi hapa wanatafuta nafasi ya kuonana na wewe.)<br />
“Wow! That’s wonderful. I think they have been moved by how I play. I think they want to congratulate me, isn’t it?” (Ha! Ni vizuri sana. Nafikiri wamevutiwa na jinsi ninavyocheza. Labda wanataka kunipongeza, au siyo?)<br />
“Big no! They simply want to be close to you.” (Hapana kabisa! Wanataka kuwa karibu na wewe tu.)<br />
<br />
“Why do you think why they fee so?” (Kwa nini unafikiri wanahisi hivyo?)<br />
“Phillip you are so cute, so every girl wants to be with you. For your information, the whole group of girls over there is vying to get you.” (Phillip wewe ni mtanashati sana, hivyo kila msichana anakutaka. Kwa taarifa yako, kundi lote la wale wasichana pale wanapigania kukunasa.)<br />
<br />
“Do you also mean you are one of them?” (Unamaanisha na wewe ni mmoja wao?)<br />
Lilikuwa swali mwafaka lililolenga kumkatisha maana tayari nilishaona mwendelezo wake kuishia mahali pabaya. Bado nilikuwa na hofu juu ya Zamaradi. Si kwamba nilihofia kifo changu pekee lakini pia ahadi ya Zamaradi aliyokuwa akiitoa kwangu mara kwa mara kwamba atamuua kila mwanamke atakayejaribu kuwa na mimi ilinitisha sana. <br />
<br />
Nilimuona akitazama chini kwa haya kisha akageuka nyuma kumuangalia Lameck lakini alikuwa ameshaondoka, nilichoelewa ni kwamba Lameck alimpisha ili aweze kuzungumza vizuri na mimi.<br />
“I have asked you a question?” (Nimekuuliza swali lakini?)<br />
“Of course, but I ask that I am not in a position to answer you today.” (Ni kweli, lakini naomba nisikujibu leo.)<br />
<br />
“Okay. May I know your name?” (Sawa. Naweza kujua jina lako?)<br />
“I’m Monalisa Malisa.” (Naitwa Monalisa Malisa.)<br />
“Oh! Malisa? Where do you hail from?” (Oh! Malisa? Unatoka mkoa gani?)<br />
“My family hails from Old Moshi, Kilimanjaro. Both my father and mom are big business persons. How about you?” (Sisi ni watu wa Old Moshi, Kilimanjaro. Wazazi wangu ni wafanyabiashara wakubwa. Vipi kuhusu wewe?)<br />
<br />
“It is a long story but I would like if we talk about you first. Which course are you pursuing?” (Ni habari ndefu lakini napenda leo tuongelee kuhusu wewe kwanza. Unachukua masomo gani?)<br />
“I am taking law, though it was not my particular choice. I was so interested in broadcasting but my parents wanted me to pursue this course so that I could be a lawyer in their companies.” (Ninachukua sheria, lakini halikuwa chaguo langu hasa. Nilipenda sana utangazaji lakini wazazi wangu wamenitaka niwe mwanasheria ili nije kuwa wakili wa kampuni zao.)<br />
<br />
(Nimefurahi kukutana na wewe.)<br />
“The same with me. Can you give a last offer?” (Hata mimi pia. Unaweza kunipa upendeleo wa mwisho?)<br />
“What kind of offer?” (Ni nini hicho?)<br />
“In which hall do you stay here?” (Unaishi bweni gani hapa?)<br />
“Hall Five, room Tarangire.” (Bweni namba tano, chumba cha Tarangire.)<br />
<br />
“Will you tolerate with my disturbances, because I will always need your closeness as I believe that I will benefit a lot from you.” (Utakubaliana na usumbufu wangu, kwa sababu ninahitaji sana ukaribu wako kwani naamini kupitia kwako nitafaidika na vitu vingi.)<br />
“You are welcome, please!” (Unakaribishwa sana!)<br />
<br />
Niliachana na Monalisa nikiwa na msisimko wa ajabu, kwa mara ya pili sasa nakutana na mwanamke mrembo mwenye uwezo mkubwa wa kifedha kwao. Tyra aliniambia kwamba anasoma Uchumi kwa ajili ya kusimamia biashara za baba yake, sasa nakutana tena na Monalisa ambaye naye anasema kwamba anasomea Sheria kwa ajili ya kuwa mwanasheria wa kampuni za wazazi wake.<br />
<br />
Kwangu mimi yalikuwa ni maajabu makubwa mtoto wa kimaskini kukutana na wanawake wanaoogelea katika utajiri. Hata hivyo, ilikuwa vigumu sana kwangu kuwapata maana vifo vingekuwa halali yao jambo ambalo sikutaka kabisa litokee. <br />
<br />
***<br />
Nilikuwa nimejilaza kitandani mkononi mwangu nikiwa na kitabu cha hadithi kilichoandikwa na mtunzi mahiri nchini Tanzania, Joseph Shaluwa. Nilikuwa nimezama kwenye hadithi hiyo, iliyokuwa nzuri sana. Nilipenda sana hadithi zake ambazo nyingi zilianzia magazetini.<br />
Nikiwa nimekaza macho yangu kwenye kitabu hicho, mara simu ya chumbani kwetu ikaita. Lameck aliyekuwa amekaa kwenye kiti akasimama na kwenda kuipokea. <br />
<br />
Sikujua ilitokea wapi na walizungumza nini lakini aliniita akisema ni simu yangu hivyo nizungumze nayo. Haraka nikateremka kitandani kisha nikachukua mkonga wa simu na kupeleka sikioni.<br />
<br />
“Phillip hapa, kutoka Tarangire Hall Five, naongea. Naomba nikusaidie tafadhali,” nilizungumza kwa sauti ya taratibu nikisubiri majibu kutoka upande wa pili.<br />
“Subiri nikuunganishe na simu yako kaka Phillip, kuna mtu anayeitwa Tyra yupo hewani,” nilisikia sauti hiyo simuni.<br />
<br />
Sikupata tabu kugundua kwamba ni Zena dada wa mapokezi ndiye alikuwa akiongea kwenye simu. Niliposikia kwamba aliyekuwa akihitaji kuongea na mimi alikuwa ni Tyra, mwili mzima ulisisimka.<br />
“Nitashukuru sana niunganishe tafadhali,” nilisema kisha muziki wa muda mfupi ukapita hewani kabla ya sauti tamu ya Tyra kutekenya ngoma za masikio yangu.<br />
<br />
“Hello, Phillip.”<br />
“Ndiyo Tyra. Mambo vipi?”<br />
“Poa naona umenisusa!”<br />
“Hapana bwana, mambo mengi!”<br />
“Mambo mengi? Acha hizo bwana.”<br />
<br />
“Kwa nini?”<br />
“Si useme tu Monalisa anakubana?”<br />
“Monalisa?”<br />
“Ndiyo...mbona unashituka? Ni nani asiyejua uhusiano wenu hapa chuoni?”<br />
Nikashtuka sana.</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb18ba2c7a85504600">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.17.<br />
<br />
SIKUTEGEMEA kama Tyra angeniambia maneno yale, ingawa hakuwa mpenzi wangu na wala Monalisa naye sikuwa na uhusiano naye wa kimapenzi, nilishtuka sana kugundua kwamba anajua, maana nilifanya siri.<br />
<br />
Ni kweli sikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Tyra, lakini nilipenda sana ukaribu wetu. Nilitamani aendelee kuwa karibu yangu. Kitendo cha yeye kuniambia kwamba Monalisa<span class="text_exposed_show"> ndiye ananifanya nimsahau yeye kiliniumiza sana, nikihofia kumpoteza.<br />
<br />
Kwa hakika nilipata wakati mgumu sana, nikatulia kwa muda nikitafakari kitu cha kumweleza ili anielewe. Kwa mbali nikasikia pumzi za Tyra zikitekenya ngoma za masikio yangu.<br />
“Halooo!”<br />
“Nakusikia Tyra!”<br />
<br />
“Mbona umenyamaza ghafla, ukweli unauma siyo?”<br />
“Ukweli upi jamani?”<br />
“Juu ya ubize wako!”<br />
“Unazungumzia kuhusu Monalisa siyo?”<br />
“Haswaa!”<br />
<br />
“Sikia nikuambie Tyra, unajua sina sababu ya kukuficha kama ni kweli niko naye, lakini napenda kukuhakikishia kuwa sina uhusiano wowote na Monalisa.”<br />
“Lakini mmekuwa gumzo chuo kizima.”<br />
“Sikuamini Tyra.”<br />
“Kwa nini wakati watu wanazungumza?”<br />
<br />
“Juu ya nini?”<br />
“Eti ni wapenzi.”<br />
“Siyo kweli, lakini lazima nikiri kwamba niliwahi kusalimiana naye uwanjani. Kikubwa alinipongeza kwa kucheza vizuri, labda watu waamue kuongezea yao kutokea hapo.”<br />
“Mh!”<br />
<br />
“Mbona unaguna?”<br />
“Haya bwana!”<br />
“Lakini ni vigumu sana watu kusema chochote, maana sijawahi kukutana naye tena baada ya hapo!”<br />
“Usijali nilikuwa nakuchemsha tu ingawa lisemwalo lipo, niambie una ratiba gani leo?”<br />
“Nipo nipo tu.”<br />
<br />
“Upo upo tu!”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Yaani hujui ratiba zako zilivyo au huna mpango wowote?”<br />
“Ndiyo maana nikakuambia kuwa nipo nipo tu, yaani sina kitu cha maana cha kufanya. Kama hivi hapa, najaribu kuupumzisha ubongo wangu kwa kusoma kitabu cha hadithi.”<br />
“Ok! Naweza kutoka na wewe tafadhali?”<br />
<br />
“Saa ngapi?”<br />
“Muda wowote, lakini si zaidi ya saa moja kutoka sasa.”<br />
“Kwenda?”<br />
“Nataka twende Bagamoyo.”<br />
“Poa nipo tayari hata sasa hivi.”<br />
“Basi poa, baada ya nusu saa nakuja kukuchukua. Uwe tayari.”<br />
“Sawa, lakini kuna nini huko Bagamoyo?”<br />
<br />
“Kupunga upepo tu, hakuna cha zaidi, kwani vipi wewe hupendi?”<br />
“Ufukweni?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Napenda sana.”<br />
“Haya mwaya jiandae nitakuja kukuchukua.”<br />
“Ok!”<br />
<br />
Tukakata simu. Bila kupoteza muda nikaenda bafuni kuoga kisha nikavaa nguo nilizozipenda kuliko zote, nikakisogelea kioo ili kinipe majibu ya nguo nilizokuwa nimevaa. Kikanipa jibu zuri sana.<br />
Kilinihakikishia kwamba nilikuwa nimependeza sana. Sikusema chochote, lakini Lameck alionekana kunishangaa kutokana na ubize niliokuwa nao baada ya kumaliza kuongea na ile simu.<br />
<br />
“Vipi, naona unajiweka safi, una mtoko nini?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Nani? Monalisa?”<br />
“Hapana...”<br />
“Tyra?!”<br />
“Ndiyo, ananipeleka Bagamoyo.”<br />
<br />
“Haya kaka, ndiyo raha ya utanashati, watoto wanajileta wenyewe,” akasema Lameck akicheka.<br />
“Hamna kitu.”<br />
“Sasa mimi natoka, acha nimsubiri hapo nje, maana ameniambia atafika baada ya nusu saa.”<br />
“Poa, starehe njema.”<br />
<br />
Sikujibu kitu zaidi ya kucheka. Lameck naye akakaukiwa kwa kicheko. Nikaanza kupiga hatua za taratibu kuelekea nje. Nilikuwa nimependeza sana, pia nilikuwa nanukia manukato mazuri. Nikatembea kwa kujiamini kuelekea nje.<br />
<br />
Nilisimama nje kwa dakika mbili tu nikaona gari aina ya Volkswagen New Model ya Tyra ikiegesha taratibu mbele ya bweni letu. Nikateremka ngazi taratibu kumwendea. Nililifahamu gari la Tyra, lakini mwenyewe alikuwa amefunga vioo vya gari lake ambavyo vilikuwa vyeusi. Nikazunguka upande wa abiria nikikaribia kabisa kushika kitasa ili nifungue na kuingia ndani.<br />
<br />
Ghafla kioo cha dirishani kikafunguka, nikakutana na tabasamu changa la Tyra, nikasita.<br />
“Mambo?” Tyra akanisalimia kwa sauti yake ile ile ya kumtoa nyoka pangoni.<br />
“Poa,” nikamjibu.<br />
“Karibu!”<br />
“Ahsante,” nikaitikia. <br />
<br />
Nikaupeleka mkono wangu kwenye kitasa cha kufungua mlango, kabla sijafanikiwa kukamilisha zoezi hilo nikasikia sauti ya kike ikilitaja jina langu. Sikujua ni nani lakini sauti ile haikuwa ngeni, nikageuza shingo kumwangalia. Sikuamini macho yangu nilikutana na uso mtamu wa Monalisa!<br />
“Phillip, please come here at once.” (Phillip, tafadhali njoo mara moja.) Alikuwa ni Monalisa akiniambia.<br />
<br />
“Phillip ingia kwenye gari bwana tuondoke. Ni nani huyo anayekusumbua?” Kwa mara ya kwanza nilisikia sauti ya Tyra ikitoka kwa ukali.<br />
Haukuwa ukali wa kawaida, bali ndani ya sauti yake kulidhihirika wivu wa wazi kabisa. Wivu ambao sikuwahi kuuona tena. <br />
<br />
Naomba nikiri kuwa nilichanganyikiwa maana viumbe hawa wawili ni kama walichagua waumbwe kama jinsi walivyoonekana. Nikamwangalia Monalisa, nikachanganywa na umbo lake namba nane, akiwa ameenea vyema ndani ya suruali ya jinzi nzuri na blauzi iliyoacha mabega yake wazi.<br />
<br />
Nikachanganyikiwa sana. Niliporudisha macho yangu kwa Tyra moyo wangu ulilipuka nilipoona miguu yake minene mizuri, iliyoonekana kutokana na kuvaa sketi fupi akiwa amekaa chini ya usukani. Hapo nikarudisha macho yangu kwa Monalisa, naye macho yake yalikuwa yanasema.<br />
<br />
“Njoo kwangu jamani, huoni nilivyo mzuri?” Maneno haya ni kama yalizunguka kichwani mwa Monalisa aliyekuwa amesimama akisubiri uamuzi wangu.<br />
Kwa hakika nilitakiwa nichague kwenda kwa nani, lakini nikiwa katika changamoto hiyo taswira ya Zamaradi ikaanza kunisumbua. Zamaradi mwanamke wa ndotoni mwangu. Niende wapi? Nikakosa uamuzi.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb18a7fc3d15052068">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.18.<br />
<br />
KWA hakika nilichanganyikiwa macho yangu yaliganda kwa muda ndani ya gari nikimwangalia Tyra kwa macho ya matamanio kisha nikayarudisha tena kwa Monalisa ambaye taratibu alikuwa akitembea kuja upande wetu.<br />
<br />
Mwili ulinitetemeka lakini nilijitahidi sana kuficha hali hiyo. Sikutaka kuonekana dhaifu lakini lazima nikiri kwamba wanawake hao wawili waliuchanganya san<span class="text_exposed_show">a moyo wangu. <br />
“Phillip get in the car, please!” (Phillip ingia kwenye gari tafadhali!)Tyra aliniambia kwa sauti yenye ukali kidogo.<br />
<br />
Kwa mara ya kwanza nilimshuhudia Tyra akizungumza kwa sauti ya ukali. Nilitulia kwa muda nikitafakari cha kufanya, kabla sijapata majibu tayari Monalisa naye alikuwa anaongea.<br />
“Come with me, please, baby!” (Tafadhali njoo huku, mpenzi.)<br />
<br />
Kwa kweli nilichanganyikiwa nikapoteza mwelekeo, nikashindwa kuelewa kitu cha kufanya. Sekunde chache baadaye Monalisa alikuwa ameshafika nilipokuwa nimesimama, akanipigapiga begani kisha akaanza kuzungumza tena:<br />
“Phillip why can’t you here my voice, please. Let’s go!” (Philip mbona husikii sauti yangu tafadhali. Twen’zetu!)<br />
<br />
“Excuse me, Monalisa. I am going somewhere with Tyra, I had an appointment with her.” (Samahani Monalisa. Ninakwenda sehemu fulani na Tyra, nilikuwa na ahadi naye.)<br />
Hata hivyo, moyoni nilijua kabisa kwamba nilimjibu kwa kumridhisha maana sikuwa na ahadi naye. Isitoshe hakuna yeyote kati yao niliyekuwa na uhusiano naye wa kimapenzi, hivyo nilikuwa na uhuru wa kufanya chochote bila ruhusa ya yeyote. <br />
<br />
“Where to?” (Wapi huko?)<br />
“Bagamoyo.”<br />
“Who is this girl?” (Huyu msichana ni nani?)<br />
“She is just my friend.” (Ni rafiki yangu tu.)<br />
<br />
<br />
“If it is so, can’t you postpone it as I have very important talks with you?” (Kama ndiyo hivyo, huwezi kuahirisha maana nina mazungumzo muhimu nawe?”<br />
Nilishangazwa na jinsi Monalisa anavyojiamini, isingekuwa rahisi kwa mwanamke mwingine kujiamini na kuongea na mwanaume maneno yale mbele ya mwenzake ambaye hajajua uhusiano wao.<br />
<br />
Sikuwa mwepesi kujibu swali lake, nilichokifanya ni kusoma kupitia macho ya Tyra. Nilichokifanya ni kuinama kidogo kisha kuchungulia kwenye kioo cha gari nikakutana na macho ya Tyra yakizungumza; alikuwa analia.<br />
Moyo wangu ukaenda mbio, Tyra hakujua kitu kimoja machozi yake yalimfanya azidi kuonekana mrembo zaidi. Nikahisi huruma moyoni mwangu. Ni kweli kwamba Tyra alitaka kutoka na mimi, tena ni yeye aliyenipigia simu kuniomba, nami kwa moyo mkunjufu nikamkubalia. <br />
<br />
Kwa vile hakuna yeyote kati yao niliyekuwa na uhusiano naye wa kimapenzi ilikuwa rahisi sana kufanya uamuzi. Kitu pekee nilichotakiwa kukifanya ni kuondoka na Tyra kama nilivyokuwa nimekubaliana naye mwanzoni. <br />
<br />
Nikainua kichwa changu kisha nikayatuliza macho yangu juu ya uso wa Monalisa. Midomo yangu ikaanza kucheza, nilikuwa natafakari maneno ya kumwambia ili aridhike. <br />
“Excuse me, Monalisa. I cannot go out with you today as I already have an appointment with Tyra. I am sorry for inconveniencing you, but I believe you will understand me.” (Samahani Monalisa. Siwezi kutoka na wewe leo kwa sababu tayari nilikuwa na ahadi na Tyra. Samahani kama nitakuwa nimekuudhi, lakini naamini umenielewa.)<br />
<br />
Baada ya hapo sikuongea neno jingine lolote zaidi ya kufungua mlango na kuketi upande wa abiria, nikageuza shingo yangu kumwangalia Tyra, alikuwa akijifuta machozi kwa kitambaa cheupe. <br />
“Excuse me, Tyra. I did not like this to happen. Let’s go,” (Samahani sana Tyra, sikupenda haya yatokee, washa gari twende), nilimwambia Tyra nikiwa nimeyatuliza macho yangu usoni mwake.<br />
<br />
Kitu cha ajabu, hakusema neno lolote zaidi ya kuwasha gari kisha akageuza na kuliondoa kwa kasi. Monalisa akabaki anatusindikiza kwa macho hadi tulipotokomea. Nilikuwa kimya kwenye gari, nikitafakari mambo yaliyotokea.<br />
Kwa kweli sikuwa na la kuzungumza na Trya ambaye alionekana kuvimba kwa hasira. Kimsingi hakuwa na sababu ya kukasirika maana ni kweli kwamba hakuwa na uhusiano na mimi. Ukimya wangu ulimfanya naye awe kimya!<br />
<br />
Mpaka tunafika Mwenge, hakuna aliyezungumza na mwenzake, gari likakata kushoto kuifuata barabara ya Bagamoyo na kwenda kwa kasi ile ile. Kwa bahati nzuri hapakuwa na foleni kabisa siku hiyo, hivyo alikuwa na uwezo wa kuendesha kwa kasi aliyoipenda.<br />
Nilijitahidi kukaa kimya, lakini tulipofika Mapinga, nilishindwa kuvumilia. Nikaamua kufungua kinywa changu na kuanzisha mazungumzo.<br />
<br />
“Mbona umenyamaza muda wote? Bado una hasira Tyra?” Niliongea kwa sauti ya taratibu kabisa. <br />
“Tutaongea Bagamoyo!”<br />
“Ok!”<br />
<br />
Ni kama Tyra alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mimi maana tukio la Monalisa lilimchanganya sana kichwa chake. Ni kweli hakufungua tena kinywa chake kuongea na mimi hadi tulipoingia Bagamoyo katika Hoteli ya Paradise, tukashuka na kwenda kukaa kwenye moja ya meza zilizokuwa ufukweni mwa Bahari ya Hindi.<br />
<br />
Punde mhudumu alifika kutusikiliza, tukaagiza vinywaji na vyakula. Muda mfupi baadaye alituletea vinywaji kisha akatuambia kwamba vyakula vilikuwa vikitayarishwa jikoni na vingeletwa mezani baada ya dakika thelathini na tano.<br />
Tukaanza kunywa pamoja lakini usoni Tyra alionekana kama anatunga sheria. Uso wake ulionesha kuwa ana mambo mengi sana yanayomchanganya. <br />
<br />
“Ndiyo umefanya nini Phillip?”<br />
“Kwa nini? Kivipi?”<br />
“Hujui ulichokifanya?”<br />
“Niambie basi!”<br />
<br />
“Sikutegemea kama uliniita ili uniumize. Kwa nini unanitesa kiasi hicho?”<br />
“Unajua mpaka sasa hivi sijakuelewa Tyra, bila shaka unazungumza kuhusu Monalisa.”<br />
“Ndiyo huyo huyo Monalisa wako ambaye nilikwambia mchana kwamba chuo kizima kinajua uhusiano wenu ukakataa, sasa nimeshuhudia kwa macho yangu.”<br />
<br />
“Tyra kwani sitakiwi kuwa na marafiki?”<br />
“Simaanishi hivyo lakini kwa nini unautesa moyo wangu kwa kiwango hicho?”<br />
“Inabidi uwe muwazi zaidi ya hapo!”<br />
<br />
“BABY I LOVE YOU SO MUCH I HAVE ALWAYS SHOWED YOU VARIOUS SIGNS AND DONE MANY THINGS TO SHOW YOU MY LOVE. DO YOU WANT TO TELL ME THAT YOU DO NOT SEE THEM? WHY DO YOU WANT TO TORTURE ME IN THIS WAY? PLEASE, I ASK YOU TO OPEN YOUR HEART FOR ME. I LOVE YOU PHILLIP!” (Mpenzi nakupenda sana, kila mara nimekuwa nikikuonesha ishara kadhaa za mapenzi yangu kwako. Unataka kuniambia huzioni? Kwa nini unataka kunitesa kiasi hiki? Tafadhali naomba uufungue moyo wako unikaribishe. Nakupenda Phillip!) Tyra alitamka maneno haya akionesha hisia kali za mapenzi.<br />
<br />
Nilisisimka mwili, aliongea maneno mazito ambayo yalinichoma. Kwa hakika nilimwonea huruma, nikatamani kuwa naye lakini tatizo lilikuwa ni Zamaradi. Kwa mbali nilianza kuhisi harufu ya manukato ya Zamaradi wangu. Woga uliongezeka baada ya kugundua kwamba tulikuwa tumekaa ufukweni mwa bahari, eneo ambalo ndani yake ndiyo makazi ya Zamaradi.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb18a7fc3d15052068"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb18a7fc3d15052068"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb18a7fc3d15052068"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb18a7fc3d15052068"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb18a7fc3d15052068"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb1896649246461852">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.19.<br />
<br />
HAKIKA Tyra alikuwa akinieleza maneno mazito sana, siwezi kumlaumu maana zilikuwa ni hisia kutoka ndani ya moyo wake. Alikuwa na haki ya msingi ya kueleza kila alichojisikia moyoni mwake.<br />
<br />
Nilitegemea kusikia maneno hayo, maana siku zote niligundua kwamba Tyra alikuwa akinipenda sana. Si yeye peke yake bali wanawake wengi kila wanaponitazama walivutiwa na mimi<span class="text_exposed_show">. Haikuwa kosa lake bali moyo wake. <br />
<br />
Ni kweli hata mimi nilimpenda sana, hilo napenda nikiri mbele yenu, lakini nisingeweza kuwa na mwanamke mwingine tofauti na Zamaradi. Natamani sana jambo hilo litokee lakini niliogopa kutokana na maneno ya Zamaradi aliyokuwa akijiapiza mara kwa mara anaponitokea usiku. <br />
<br />
Ukimya wangu ukamfanya Tyra apate wasiwasi, alitamani kusikia sauti yangu nikisema chochote kuhusu ombi lake. Akayatuliza macho yake usoni mwangu, nami pia. Hata hivyo, sikuwa na jibu la kumpa. <br />
“Phillip!” Tyra aliita kwa sauti ya taratibu sana.<br />
“Nakusikia.”<br />
<br />
“Nasubiri jibu lako.”<br />
“Samahani, hatuwezi kubaki kuwa marafiki?”<br />
“Hapana, acha utani wako bwana. Kumbuka hizi ni hisia za ndani ya moyo wangu. Naomba usizidhihaki, nipokee tafadhali. Nakupenda!”<br />
“Najua lakini kwa nionavyo mimi, tunapendeza tukibaki hivi tulivyo kuliko kuanza uhusiano mwingine mpya!”<br />
<br />
“Hapana sikia kilio changu, mimi nakupenda.”<br />
“Najua hata mimi nakupenda tena nakupenda zaidi ya unavyonipenda, lakini kwa sababu ya mapenzi hayo ndiyo maana sitaki tuanzishe kitu kingine tofauti.”<br />
“Mbona sikuelewi?”<br />
<br />
“Hautanielewa kirahisi lakini unachotakiwa kufahamu ni kwamba ni hatari sana mimi kuwa na uhusiano na wewe. Tafadhali naomba uelewe.”<br />
“Mbona sikuelewi? Unanichanganya kabisa!”<br />
<br />
Kufikia hapo nikazidi kuchanganyikiwa maana Tyra alikuwa king’ang’anizi kweli kweli. Akanisogelea nilipokuwa nimekaa kisha akanikalia, hapo woga ukanizidi, nikamwona kabisa Zamaradi akija mbele yangu, kitu ambacho sikutaka kabisa kitokee.<br />
<br />
Kwa mara nyingine nikaanza kumchukia tena Zamaradi, ni kweli alikuwa mwanamke mzuri lakini alininyima uhuru wa kufanya mambo yangu. Mbaya zaidi hatokei katika hali ya kawaida, ananinyanyasa na kuninyima uhuru.<br />
<br />
Lakini sikutaka matatizo na Zamaradi, hivyo nikamsukuma Tyra aliyeanguka pembeni. Akaanza kulia kwa uchungu huku akilaumu kitendo nilichomfanyia.<br />
“Kwa nini unanifanyia hivi, kwa sababu nimekupenda?”<br />
<br />
“Hapana napenda sana maisha yako, utapata matatizo, usitake kuwa na mimi. Tafadhali niondoe kichwani mwako, nifanye kama rafiki tu,” nikamwambia kwa uchungu moyoni.<br />
Maneno hayo ni kama hayakumwingia kabisa Tyra ambaye aliinuka pale chini na kunifuata kisha kunikumbatia kwa nguvu akiuleta mdomo wake kinywani mwangu, nilijua kilichotaka kutokea, sikuwa tayari. <br />
<br />
Nikamsukuma kwa nguvu, akaanguka pembeni. Nikatumia nafasi hiyo kukimbia. Nilipofanya hivyo alinikimbiza kwa nyuma huku akiita jina langu lakini sikugeuka. Hakuweza kunikimbiza umbali mrefu nikafanikiwa kutoka nje ya geti la Hoteli ya Paradise kisha nikasimamisha pikipiki iliyonipeleka hadi kituo cha mabasi.<br />
<br />
Hapo nikapanda basi linaloelekea Mwenge, Dar es Salaam. Moyoni nilikuwa na maumivu makali. Sikutaka kumuumiza kiasi kile Tyra lakini sikuwa na jinsi ya kufanya. Ilikuwa ni lazima niondoke maana maisha yake na yangu yalikuwa muhimu sana.<br />
<br />
Nilimfahamu vyema Zamaradi, siku zote huwa na hasira sana juu yangu, nilijua kama ningeendelea kuwa na Tyra katika hali ile, lazima angemdhuru. Lakini pia nilisubiri adhabu yangu usiku ambapo nilitegemea lazima angenijia. <br />
<br />
Nikiwa kituoni nilifanikiwa kupanda basi lililonifikisha mpaka Mwenge ambapo nilipanda daladala inayoelekea chuo. Niliposhuka katika kituo cha Utawala, macho yangu yaligongana na Monalisa aliyekuwa akiendesha gari aina ya Toyota Cresta. Akapiga honi kisha akafinya mkono kuashiria kuniita. <br />
<br />
“Nakuja!” nilisema nikivuka upande wa pili.<br />
“Ingia kwenye gari tafadhali,” alisema Monalisa kwa mtindo wa kuamrisha.<br />
Nami nikaingia. Hakusema neno lolote zaidi ya kuwasha gari kisha akakata kulia akiifuata barabara ya chuo kuelekea kwenye geti la kwenda Ubungo. <br />
“Vipi usharudi Bagamoyo?” aliuliza Monalisa akinitizama usoni.<br />
“Ndiyo!” Nikamjibu kwa kifupi.<br />
<br />
“Ok! Naona uliamua kuniacha sababu ya Tyra, lakini ni vile tu hujajua ni kiasi gani nakupenda. Ungenipa nafasi hiyo ningekuonyesha mapenzi motomoto.”<br />
Hakujua ni kiasi gani maneno yake yalinichoma maana nilimkimbia Tyra huko Bagamoyo kutokana na mambo kama aliyoniambia. Nilimshangaa lakini pia nilimwonea huruma. <br />
“Hatuwezi kubadilisha stori?”<br />
<br />
“Tunaweza, naona unachukia sana tukizungumza kuhusu huyo mwanamke wako.”<br />
“Halafu tunaelekea wapi?”<br />
“Hapa Mlimani City, hutaki kukaa na mimi japo tupate maji ya matunda?”<br />
“Ok!”<br />
<br />
Monalisa akaendelea kuendesha gari hadi Mlimani City ambapo tulitafuta sehemu tukakaa na kuanza kula na kunywa. Tuliongea mambo mengi sana, kitu kilichonifurahisha zaidi ni kwamba Monalisa alinielewa maana hakuzungumza tena mambo ya mapenzi. <br />
<br />
Tukaendelea kunywa kwa furaha hadi usiku sana. Monalisa akaniambia tuondoke, mimi nilikuwa nimeshika boksi lenye juisi na Monalisa alikuwa na boksi lenye mvinyo mweupe. Tulipoingia kwenye gari nikaanza kuhisi kuchangamka ghafla, ni hali ambayo sikuielewa, maana ilifikia mahali Monalisa alikuwa akinibusu nami nikamrudishia. Baada ya hapo sikukumbuka kitu chochote.<br />
<br />
***<br />
Utulivu ule ulinishitusha kidogo, lakini joto la mwanamke akiwa pembani yangu lilinizidishia woga, nilipofungua macho yangu na kujiangalia vizuri nikagundua kwamba nilikuwa mtupu na Monalisa. <br />
<br />
Haikunichukua muda mrefu kugundua kwamba nilikuwa nimefanya mapenzi na Monalisa tena pembeni mwa barabara, ndani ya gari. Nikashituka sana.<br />
“Umenifanya nini Monalisa?”<br />
<br />
“Usiogope kwani hujui tulichokifanya? Naomba unisamehe lakini sikuwa na njia nyingine yoyote ya kukufanya uelewe kwamba nakupenda.”<br />
“Utapata matatizo, nakuonea huruma sana, hatupaswi kufanya hivi.”<br />
<br />
“I DON’T CARE PROVIDED I LOVE YOU, I’M READY FOR ANY EVENTUALITY!” (Sijali, maadam nakupenda nipo tayari kwa lolote.) Monalisa aliniambia akionesha kujiamini sana.<br />
Nilimuonea huruma, maana hakujua kama kuna Zamaradi, mwanamke wa ndotoni mwangu ambaye ni hatari sana.</span></div></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb18a7fc3d15052068"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124cb188a239e40800146">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..20<br />
<br />
<br />
KIAPO alichoapa Monalisa baada ya mimi na Tyra kuondoka na kumwacha akiwa amesimama nje ya bweni letu kilikuwa ni kulipiza kisasi. Alijihakikishia kwamba adhabu pekee ambayo iliyomfaa Tyra ni kutoka na mimi kimapenzi. <br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Katika hilo hakujali njia ambayo angetumia, iwe kwa ridhaa yangu mwenyewe au kwa kutumia nguvu za ziada lakini kikubwa alichotaka kilikuwa ni kulala na mimi kimapenzi.<br />
<br />
Siku yake iliharibika lakini kwa sababu alishajua bweni nililokuwa ninaishi aliahidi kuniwinda hadi anipate tena siku ile ile. Wakati nilipokuwa nashuka kwenye daladala nikitokea Mwenge, yeye alikuwa kwenye mawindo. Alikuwa akiniwinda.<br />
<br />
Nilimkubalia ombi lake la kutoka naye usiku huo nikiwa sielewi kilichokuwa ndani ya moyo wake. Kwa bahati mbaya sana Monalisa alikuwa ameshakula kiapo kwamba lazima anipate. <br />
<br />
Mbaya zaidi hakujua matatizo ambayo angeweza kuyapata. Hakujua kwamba mimi ni mwanaume hatari ambaye sikutakiwa kutoka kimapenzi na mwanamke yeyote tofauti na Zamaradi.<br />
Nikiwa sina hili wala lile, nilimwomba niende uani kujisaidia. <br />
<br />
Cha kushangaza alitabasamu na kwa hakika niligundua kwamba alifurahishwa na safari yangu ya kwenda msalani, ingawa sikujua sababu.<br />
“Mbona unatabasamu?” nilimuuliza.<br />
“Basi tu!”<br />
<br />
“Haya bwana ngoja narudi muda si mrefu!”<br />
“Hata kama ukilala huko huko,” akasema kimizaha huku akicheka.<br />
Nikaondoka nikiwa na mawazo tele kichwani bila kujua sababu ya Monalisa kucheka. Muda mfupi baadaye nikarudi na kujumuika naye mezani. Kitu ambacho kilinishangaza ni uchangamfu wangu wa ghafla.<br />
<br />
“Mbona umechangamka sana?” Monalisa aliniuliza kwa sauti tamu huku akinitazama usoni.<br />
“Nimefurahi tu, kwani wewe hujafurahi?” Nilimjibu huku nikiwa sijielewi.<br />
“Nimefurahia pia, napenda siku zote uwe hivi.”<br />
“Nakuahidi.”<br />
<br />
Kwa hakika sikuelewa kilichoendelea lakini nilijishangaa sana uchangamfu ule wa ghafla. Kitu cha ajabu, kadiri muda ulivyozidi kwenda ndivyo nilivyozidi kuchangamka, baadaye nikahisi kizunguzungu kabisa. <br />
Hadi tunapanda kwenye gari lake nilikuwa sijielewi, kitu cha mwisho kukumbuka ni kwamba nilihisi usingizi mzito. Nikapotelea usingizini. <br />
<br />
***<br />
“Lakini nakuonea sana huruma, hukupaswa kufanya hivi Monalisa. Ni hatari!” nilimwambia Monalisa. <br />
“Nimeshasema kilichonifanya nifanye yote haya ni mapenzi yangu ya dhati si kitu kingine.”<br />
“Monalisa naomba uelewe, pamoja na kwamba umesema ni mapenzi yako ya dhati lakini yanaweza kukusababishia matatizo.”<br />
“Nipo tayari kwa lolote.”<br />
<br />
“Lakini umenifanyia nini?”<br />
“Naomba unisamehe, ukweli ni kwamba nilichanganya juisi yako na pombe kali. Naomba unisamehe.”<br />
“Sawa yameisha lakini ninakusikitikia sana.”<br />
“Kwani una nini wewe, mbona umesisitiza sana hilo?”<br />
<br />
“Huo ndiyo ukweli Monalisa, umefanya jambo baya na hatari sana.”<br />
“Sasa?”<br />
“Naomba unirudishe bwenini!”<br />
“Hatuwezi kuendelea kidogo?”<br />
“Jambo hili kamwe halitatokea tena, hujanifurahisha Monalisa.”<br />
“Nilishakuomba msamaha nadhani tuondoke.”<br />
<br />
Hatukuwa na kitu kingine cha kufanya zaidi ya kuvaa nguo zetu kisha Monalisa akawasha gari na kunirudisha bwenini. Akasimama nje ya jengo la bweni letu tukiwa tunaagana. <br />
“Samahani sana kwa yaliyotokea, usiku mwema,” Monalisa aliniambia.<br />
“Usijali, usiku mwema na wewe pia.”<br />
<br />
Nikashuka garini na kupanda ngazi fupi za kuelekea kwenye mlango mkubwa, Monalisa akawasha gari na kuondoka. Nilikuta mlango uko wazi, nikaingia bila kumwamsha Lameck, nikaenda bafuni kuoga kisha nikarudi kitandani kulala. Hofu yangu kubwa ilikuwa ni Zamaradi.<br />
<br />
***<br />
Nilishituka sana kumwona Zamaradi akija katika hali aliyokuja nayo. Hakuchana nywele, hakujiremba kama ilivyo kawaida yake, bali uso wake ulikunjamana na ulisoma hasira na kisasi. Ni dhahiri Zamaradi alikuja kwa ajili ya kutoa taarifa mbaya. Nikashituka sana. <br />
“Umefanya nini?” aliuliza Zamaradi kwa sauti ya ukali.<br />
“Nisamehe sikujua.”<br />
<br />
“Hukujua nini?”<br />
“Zamaradi hata wewe uliona kwamba alifanya kitendo hicho bila hiari yangu.”<br />
“Najua na ninakuhakikishia lazima nimuadhibu, lazima.”<br />
“Hapana naomba umsamehe Zamaradi, naomba umsamehe mpenzi wangu.”<br />
“Siwezi kufanya hivyo lazima nimshikishe adabu, ili liwe fundisho kwake na kwa wengine wenye tabia inayofanana na ya kwake.”<br />
<br />
Niliendelea kumshawishi Zamaradi asimdhuru Monalisa lakini alinihakikishia kwamba ni lazima angemfundisha adabu. Niliogopa sana lakini nilikuwa sina uwezo wa kumshawishi zaidi ya pale maana kuna wakati alinitishia kwamba angeweza kunidhuru hata mimi.<br />
“Samahani kwa yote, vipi mbona hujaja na mtoto? Nina hamu sana ya kumwona Mina wangu!” nilisema nikitegemea ningepunguza hasira zake.<br />
Kumbe nilikuwa najidanganya, muda huo huo Zamaradi alitoweka. <br />
<br />
***<br />
Siku nzima iliyofuata nilishinda nikiwa mnyonge, kwa kujikongoja jioni nilikwenda mazoezini. Sikumwona Monalisa kama kawaida yake. Nilicheza chini ya kiwango, baada ya mazoezi ambayo kwa hakika sikuyapenda kutokana na taswira ya Zamaradi kuniandama siku hiyo, nilitoka na kwenda bwenini. <br />
<br />
Nikiwa naelekea bwenini, nikashangaa kukuta watu wamesimama vikundi vikundi wakiongea. Moyoni nikashituka ingawa sikujua kilichowafanya wajikusanye katika vikundi. Nikasogelea kikundi kimojawapo kisha nikatega sikio kujua kilichokuwa kinazungumzwa. <br />
“Nasikia ameumia sana,” nilimsikia mmoja wa wanafunzi akizungumza.<br />
“Ndiyo ilikuwa ajali mbaya sana.”<br />
<br />
“Kwa hiyo amelazwa wapi?”<br />
“Yuko Muhimbili hajitambui kabisa, kwa kweli sijui kama atapona,” mwingine alidakia na kunifanya nishikwe na shauku ya kutaka kujua waliyekuwa wanamzungumzia.<br />
“Mnamzungumzia nani?” nikauliza nikionesha wasiwasi mwingi.<br />
“Usiniambie hujui, Monalisa amepata ajali mbaya sana jioni hii katika Barabara ya Sam Nujoma!”<br />
<br />
“Monalisa? Monalisa Malisa?” niliuliza nikitaka kupata uhakika zaidi.<br />
“Ndiye huyo huyo!”<br />
Moyo wangu ukaingiwa ubaridi mkali, nikaogopa. Mimi ndiye chanzo cha yote, nikajihukumu ndani ya nafsi yangu. Sikupata tabu kugundua kwamba ilikuwa ni kazi ya Zamaradi.<br />
<br />
Je, nini kitatokea?FUATILIA KESHO...</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124b46715c12682882297"><span class="text_exposed_show"> </span></div></span></div><span class="fcg"> </span>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com1tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-44891111500413566492012-07-27T01:02:00.001-07:002012-07-27T01:02:10.850-07:00MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..21.<a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/msichana-ndotoni-mwanguep46.html?spref=bl"></a><img alt="" class="spotlight" src="https://fbcdn-sphotos-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash3/600112_372768216116093_1626145363_n.jpg" style="height: 113px; width: 168px;" /><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..21.<br />
<br />
<br />
Phillip aliamini asingetokea mwanamke mrembo ambaye angempenda kama ilivyokuwa kwa Zamaradi, mwanamke wake wa ndotoni. Zamaradi ambaye ni jini asiyeonekana katika ulimwengu wa kawaida amemfanya Phillip mpofu, hivyo kushindwa kutambua uzuri wa mwanamke mwingine yeyote zaidi yake.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Katika uhusiano huo ambao baadaye ulizaa ndoa iliyofungwa chini ya bahari kwa wazazi wa Zamaradi, walibahatika kupata mtoto waliyempa jina la Mina. Siku zote hukutana usiku ambapo Phillip huwa katika ndoto. <br />
<br />
Imani hiyo ya Phillip ilibadilika baada ya kujiunga katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo alikutana na wanawake warembo kuliko Zamaradi. Kwanza alikutana na Tyra ambaye alitoka katika familia ya kitajiri na baadaye kukutana na Monalisa, kama ilivyo kwa Tyra naye alitoka katika familia yenye neema. <br />
<br />
Phillip ambaye alikuwa na umbo la mazoezi alijiunga na timu ya mpira wa kikapu chuoni hapo na kujizolea umaarufu mkubwa. Siku moja wakati Tyra amefika bwenini kwake kumchukua, anakutana na Monalisa naye akitaka kutoka naye.<br />
<br />
Akaamua kuondoka na Tyra na kumwacha Monalisa lakini walipofika Bagamoyo, Tyra akamweleza ukweli Phillip kwamba anampenda sana jambo ambalo Phillip hakukubaliana nalo. Hata hivyo, Tyra alikuwa mgumu kuelewa, Phillip akaamua kumkimbia na kwenda kupanda basi lililomfikisha Mwenge, hapo akapanda daladala na kurejea chuoni.<br />
<br />
Akiwa anashuka katika kituo cha Utawala, Monalisa alimwita na kutaka watoke naye, akakubali. Walikula na kunywa, bila kufahamu kwamba wakati alipokwenda msalahani alichanganyiwa pombe kali kwenye boksi la juisi yake, hivyo baadaye alilewa na kulala.<br />
<br />
Monalisa akatumia nafasi hiyo kukutana Phillip kimwili bila idhini yake. Baadaye alipozinduka na kujikuta mtupu, ndani ya gari lililoegeshwa pembeni ya barabara, akagundua kwamba Monalisa alikuwa amefanya naye mapenzi jambo lililomuuma mno maana alijua kwamba Zamaradi asingeweza kuvumilia.<br />
<br />
Siku iliyofuata ilikuwa nzito sana kwake, akajilazimisha kwenda mazoezini. Wakati anarudi akakuta watu wakiwa wamesimama vikundi vikundi na alipouliza akaambiwa kwamba Monalisa alikuwa amepata ajali mbaya ya gari. Moyo ukampasuka, akahisi ni Zamaradi.<br />
Je, nini kitatokea? SONGA NAYO...<br />
<br />
NILIPATA mshtuko mkubwa sana, nilimfahamu vyema Zamaradi wangu, asingeweza kuvumilia tukio lile. Moyo wangu uliniuma maana sikuwa tayari kwa kitendo alichonifanyia Monalisa bila idhini yangu.<br />
<br />
Uso wangu ulibadilika, nikaonesha wasiwasi mwingi, hivyo ili kukwepa maswali ya watu waliokuwa eneo lile, nikaamua kuondoka haraka. Kwa bahati nzuri kwenye chumba chetu Lameck hakuwepo, hivyo nilijifungia na kuanza kulia mwenyewe. <br />
<br />
Niliumia sana, sikulipenda kabisa tukio lile lakini nilijua kabisa Zamaradi aliamua kulipiza kisasi. Nilimaliza siku vibaya, ingawa tangu kulipokucha nilikuwa sina amani kabisa baada ya Zamaradi kunitokea ndotoni na kunihakikishia kwamba angelipa kisasi.<br />
<br />
Hata Lameck alipokuja aligundua tofauti niliyokuwa nayo, nilikuwa sina furaha kabisa, haikuwa rahisi kwake kunyamaza wakati aliniona nikiwa katika hali tofauti, hivyo alitaka kujua kilichokuwa kinanitatiza.<br />
<br />
“Kaka vipi mbona haupo sawa?” Aliniuliza Lameck.<br />
“Acha tu ndugu yangu, yaani nimechanganyikiwa kabisa.”<br />
“Nini kimetokea?”<br />
“Hujapata taarifa?”<br />
<br />
“Ya nini?”<br />
“Monalisa amepata ajali!”<br />
“Monalisa?”<br />
“Ndiyo. Nimepata taarifa nikiwa natoka uwanjani, yaani nimechanganyikiwa kabisa.”<br />
“Ana hali mbaya sana?”<br />
<br />
“Yupo Muhimbili, nasikia haongei mpaka jioni hii!”<br />
“Aisee, pole sana rafiki yangu, Mungu atamsaidia, atapona!”<br />
Tulizungumza mengi, usiku nikajilazimisha kulala ingawa ilikuwa shida sana kupata usingizi. <br />
<br />
***<br />
Tofauti na matarajio yangu, niliamka asubuhi bila Zamaradi kunitokea usiku wake. Jambo hilo lilinishangaza sana maana nilikuwa nina mashaka kwamba yeye ndiye aliyehusika na ajali ya Monalisa. <br />
<br />
Hata hivyo, mwenye ukweli alikuwa ni Monalisa, hivyo mara moja nikajiandaa na kuelekea katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikolazwa ili niweze kumuona na kuzungumza naye. Niliamini kupitia mazungumzo, ningegundua kama Zamaradi alihusika. <br />
Kwa bahati nzuri nilifika wodini kwake, nikamkuta ameshazinduka. Mwili ulisisimka sana, nikamuonea huruma.<br />
<br />
“Pole sana Monalisa!”<br />
“Ahsante Phillip mpenzi wangu!”<br />
“Nini hasa kilitokea?”<br />
<br />
“Yaani nashindwa kuelewa kabisa, nilikuwa kwenye mwendo wa kasi, nikashangaa namuona mwanamke mchafu akiwa amebeba mtoto anakatiza mbele yangu akiwa ametoa macho, ghafla nikapata ajali. Sikujua kilichoendelea, nilipozinduka nilijikuta hapa.”<br />
<br />
Hapo moyo wangu ukapiga kwa nguvu, nikajua wazi kwamba alikuwa ni Zamaradi akiwa na mtoto wetu Mina. Niliumia sana lakini kwa upande mwingine nilimlaumu Monalisa, maana nilimuonya mapema. <br />
<br />
“Ukikutana tena na huyo mwanamke utamkumbuka?”<br />
“Hapana, mpaka sasa nashindwa kuelewa, maana aliponitokea macho yalikuwa mazito na kuona giza. Sitamkumbuka hata kidogo. Eee Mungu wangu nisaidie!” Alitamka maneno hayo Monalisa huku akilia.<br />
<br />
Nilijitahidi kumtuliza lakini moyoni nikiujua ukweli. Sikuweza kuvumilia kukaa pale kwa muda mrefu, nilikuwa na uchungu mwingi moyoni, hivyo baada ya muda mfupi nilirudi chuoni huku nikiwa na uhakika kabisa aliyesababisha ajali hiyo ni Zamaradi.<br />
<br />
***<br />
<br />
Uso wake ulikuwa umekunjamana, ni wazi alikuwa na hasira kali sana na mimi. Kama ilivyokuwa safari iliyopita, alikuja akiwa na nguo chafu huku nywele zikiwa timutimu lakini alikuja na mwanetu Mina.<br />
<br />
Zamaradi alikuwa amekasirika sana, alionekana kuwa na maneno mazito aliyotaka kuniambia. Woga ukanizidi na wasiwasi tele moyoni. Nikiwa katika mshangao mkubwa, Zamaradi akanipa mtoto, nami nikampokea kisha nikaanza kucheza naye.<br />
“Naomba unisamehe Zamaradi, najua nimekukosea lakini si kwa kupenda mpenzi wangu.”<br />
“Sitaki kusikia upumbavu wako hapa.”<br />
<br />
“Tafadhali nipo chini ya miguu yako, naomba umsaidie Monalisa apone, najua unaweza kufanya kitu chochote ukitaka, lakini naomba umsamehe.”<br />
“Siwezi, tena nataka kukuhakikishia kwamba inawezekana nikamuua kabisa. Siwezi kuvumilia upumbavu kama huu. Kwani wewe huelewi kama mimi nakupenda? Nataka kukuhakikishia kwamba nitamuua Monalisa wako, mpumbavu kabisa!”<br />
<br />
“Usifanye hivyo tafadhali mpenzi, hata wewe unafahamu kwamba nakupenda na sina uhusiano wowote mbaya na Monalisa, tafadhali msamehe.”<br />
“Siwezi, siwezi nimesema siwezi, sasa atakula jeuri yake kitandani.”<br />
“Anateseka sana!”<br />
<br />
“Ndiyo lengo langu, acha ateseke, tena akicheza nitamuua.”<br />
Nilizungumza mengi sana kumshawishi Zamaradi abadilishe uamuzi wake, lakini hakuonekana kunisikiliza kabisa. Jazba ilikuwa imempanda sana, kwa ilivyoonekana alikerwa sana na kitendo cha Monalisa kutembea na mimi kwani siku zote hakupenda kuchangia mwanaume.<br />
<br />
Kila nilipojitahidi kumuomba amsamehe Monalisa, hakuonekana kunielewa kabisa, bado alikuwa na kisasi kikubwa moyoni mwake.<br />
“Nipe mwanangu niondoke,” baadaye alisema kwa ukali akinitazama usoni kwa macho yaleyale mekundu yanayotisha.<br />
<br />
“Bado nina hamu naye, huwezi kusubiri kidogo nicheze na mtoto?”<br />
“Phillip nipe mwanangu niondoke, mbona hunielewi?” Alisema Zamaradi kwa ukali zaidi. <br />
Ni sauti hiyo ndiyo iliyonifanya niamini kwamba hakuwa anatania. Nikampa mtoto, kisha muda huo huo akaondoka na kuniacha peke yangu. Hakika nilikuwa na mawazo sana, nilimuonea huruma Monalisa, sikutaka afe lakini hilo halikuwa ndani ya uwezo wangu, mwamuzi alikuwa ni Zamaradi. <br />
<br />
***<br />
Asubuhi nilipoamka nilikwenda Muhimbili kumuona Monalisa, vitisho vya Zamaradi viliniogopesha sana. Sikuwa na uhakika wa kumkuta akiwa mzima. Njia nzima nilikuwa mwenye mawazo mengi, nikiwa na mawazo mengi juu ya Monalisa. <br />
Nilipofika Muhimbili, moja kwa moja nilikwenda katika wodi aliyolazwa na kupiga hatua za taratibu hadi kitandani mwake. Nikamkuta Monalisa akiwa amelala, uso wake ukionesha uchungu mwingi. <br />
<br />
“Pole sana Monalisa, utapona tu. Mungu atakusaidia!” Nilimwambia Monalisa kwa sauti ya taratibu. <br />
Hakujibu kitu, badala yake mvua ya machozi ikaanza kutiririka machoni mwake. Nikazidi kupatwa na uchungu moyoni.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..22.<br />
<br />
NILISISIMKA mwili mzima nikiwa na hofu sana na Monalisa, sikujua ni kwa nini alikuwa akilia, lakini ndani ya moyo wangu nilianza kuhisi kwamba alikuwa na ujumbe mzito aliotaka kunipa.<br />
<br />
Nilianza kuhisi kwamba, Zamaradi aliamua kumtokea mwenyewe na kumuonya. Sikutaka jambo hilo litokee hakika, mapigo ya moyo wangu yakaenda kwa kasi ajabu, taratibu nikatoa kitamba<span class="text_exposed_show">a mfukoni mwangu kisha nikaanza kumfuta machozi yake.<br />
“Pole sana Monalisa, najua maumivu unayoyapata, lakini hakuna jinsi, vumilia Mungu atakusaidia.”<br />
<br />
“Hapana Phillip, mimi siwezi kupona.”<br />
“Kwa nini Monalisa?”<br />
“Naumwa sana, hali yangu inazidi kubadilika siku hadi siku, yaani sijisikii vizuri. Nitakufa nikikuacha mwanaume ambaye nakupenda kwa moyo wangu wote!”<br />
“Usiseme hivyo tafadhali, ukisema hivyo unaniumiza na mimi. Tafadhali nakuomba sana unyamaze!”<br />
<br />
Niliumizwa sana na maneno yake ambayo yalikuwa makali kuliko kawaida, aliposema ananipenda, ndiyo nikazidi kuchanganyikiwa, maana sababu ya yeye kuwa kitandani ni kunipenda!<br />
Sikutaka kukaa muda mrefu pale wodini, maana nilihisi kama nautesa moyo wangu. Nikatafakari kwa muda, nikitamani Zamaradi atokee ili niendelee kumsisitiza amsamehe Monalisa, lakini hilo halikutokea.<br />
<br />
“Monalisa hayo ni majaribu tu, tafadhali jikaze, utapona.”<br />
“Lakini ni vigumu kuzoea hii hali, sijui ni kwa nini balaa hili limenipata mimi.”<br />
“Hapo sasa utakuwa unakufuru, ni lazima ukubaliane na kilichotokea. Mwachie Mungu kila kitu, yeye ndiye mwenye uweza na atajua cha kufanya kwa ajili yako.”<br />
“Ahsante kwa kunipa moyo Phillip.”<br />
<br />
“Sawa, ugua pole, mimi nakwenda zangu.”<br />
“Ok! Phillip.”<br />
Nikaondoka pale wodini, nikiwa na msongo wa mawazo kichwani, moyo wangu ulikuwa kama umepigwa shoti ya umeme. Niliumia zaidi, maana nilikuwa nafahamu wazi kuwa sababu ya matatizo yale yote ni mimi.<br />
<br />
Niliporudi chuoni, sikufanya chochote kwa siku nzima zaidi ya kulala. Hata jioni sikuweza kwenda mazoezini, mwili wangu ulikuwa mzito sana. Nisingeweza kufanya chochote wakati Monalisa alikuwa akiteseka kwa ajili yangu.<br />
Rafiki yangu Lameck alishangazwa sana na mabadiliko yangu ya siku hiyo, sikuwa nimechangamka kama kawaida yangu.<br />
“Phillip una tatizo gani?”<br />
“Nipo sawa, rafiki yangu!”<br />
<br />
“Hapana, haupo sawa, lazima kuna tatizo. Kwanza hujaingia kwenye kipindi tangu asubuhi, halafu mazoezini hujaenda. Umebaki chumbani tu siku nzima. Lazima kuna kitu. Hebu niambie una nini rafiki yangu?”<br />
“Niamini mimi Lameck, hakuna tatizo, zaidi ya mambo ya kawaida tu kichwani mwangu!”<br />
<br />
“Mficha maradhi, kifo humuumbua, mimi ni kama ndugu yako sasa hivi. Tunaishi pamoja kwa muda mrefu sana, lazima unieleze kama una tatizo!”<br />
“Sina,” nikamjibu kwa kifupi na kugeukia upande mwingine kisha nikajifunika shuka gubigubi.<br />
Sikutaka kuzungumza zaidi, isingekuwa rahisi kumwambia kilichotokea, hiyo ilikuwa siri ya moyo wangu. Nikaamua kulala.<br />
<br />
***<br />
Kutokana na kuguswa sana na ajali ya Monalisa, kila siku asubuhi baada ya kuamka ilikuwa lazima niende kwanza Muhimbili kumjulia hali kisha niendelee na ratiba nyigine. Ndivyo nilivyofanya pia asubuhi hiyo.<br />
Nilijiandaa vyema kisha nikatoka na kwenda Muhimbili. Nilimkuta Monalisa akiwa katika hali mbaya sana, sikuweza kuendelea kumwangalia akipumua kwa shida huku machozi yakimtoka.<br />
<br />
Nilichokifanya ilikuwa ni kusimama mara moja na kwenda ofisini kwa Dk. Mang’ola ambaye ndiye aliyekuwa akimuhudumia tangu alipofikishwa hospitalini hapo.<br />
“Pole sana kijana,” Dk. Mang’ola aliniambia, nami nikiketi kitini.<br />
<br />
“Ahsante sana dokta, hali ya mgonjwa naona si nzuri kabisa, vipi kuna matumaini?”<br />
“Kwa kweli hali yake kwa sasa si nzuri. Unajua mgonjwa amevunjika uti wa mgongo, kwa hiyo amepooza mwili mzima isipokuwa kichwa tu! Jana jioni nilikuwa na mkutano na wazazi wake na ndugu zake wengine tukijadiliana kuhusu hali yake. Wameamua kumpeleka Uingereza kwa matibabu, kama mambo yataenda sawa, huenda kesho wakasafiri.”<br />
<br />
“Mungu wangu, Uingereza? Inamaana hapa mmejaribu kila njia mmeshindwa?”<br />
“Kwa kweli haiwezekani kabisa, lazima waende nje kujaribu, ingawa uwezekano wa kupona ni mdogo sana na hata akipona, maisha yake yote yaliyobakia atakuwa kitandani!” Dk. Mang’ola aliniambia.<br />
<br />
Moyo wangu uliingiwa na ubaridi mkali, sikuwa na uwezo wa kuendelea kumsikiliza daktari, nilisimama mara moja na kumuaga kisha nikaondoka zangu. Iliniuma sana kuona Monalisa anateseka, huku mimi nikiwa naijua sababu ya mateso yake.<br />
<br />
***<br />
Sauti kubwa ya mwanamke akicheka ndiyo iliyonishtua, baadaye nikaona mwanga mkali mbele yangu, ghafla nikaona cheche za moto zikiwaka kwa kasi sehemu niliyokuwa nimekaa.<br />
Kitambo kidogo, kicheko kikapungua na kuisha kabisa. cheche ziliendelea kutoka, kisha nikasikia sauti ya mtoto akilia. Hapo nikajua kila kitu; ni Zamaradi alikuwa amekuja kunitembelea.<br />
<br />
“Phillip mpenzi wangu, sikubahatisha kukupenda, nakupenda kwa dhati ya moyo wangu, hivyo siwezi kumruhusu mtu yeyote aniingilie. Sikia...kifupi najua kila kinachoendelea. Huyo mpumbavu wako watahangaika naye sana, lakini hatapona.<br />
<br />
“Najua kwamba wanataka kumpeleka Uingereza kwa kuwa wana fedha. Fedha zao si kitu katika mapenzi yangu kwako, Phillip nakuahidi lazima nitamuua Monalisa. Ngoja kwanza ateseke kidogo mpaka siku hasira zangu zitakapotulia kidogo nitamuua akapumzike!”<br />
<br />
“Usifanye hivyo Zamaradi tafadhali, nakuomba sana...najua amekosea, lakini ukumbuke kwamba si kwa makusudi, maana hajui yote haya. Msamehe tafadhali,” nikamwambia Zamaradi nikiamini angesikia maneno yangu, lakini ilikuwa kinyume chake.<br />
<br />
“Sina cha kuongeza, nakuhakikishia lazima nimfundishe adabu. Tena nakuambia, uwe makini na hao wanawake zako, akitokea mwingine akafanya ujinga kama wa Monalisa, dawa itaendelea kuwa ile ile, kuwaua tu!” Akasema Zamaradi kwa sauti iliyojaa hasira.<br />
“Tafadhali naomba usikilize sauti yangu, nipo chini yako Zamaradi, msamehe...nakuomba sana!”<br />
<br />
“Sina msamaha na msaliti, kifo ndiyo adhabu inayomstahili. Jiandae kuona maiti yake, tamaa ndiyo imemponza!” Akasema Zamaradi kwa hasira kisha akatoweka.<br />
Nikabaki natetemeka, huku machozi yakimwagika machoni mwangu.<br />
“Kwa nini Zamaradi hataki kunisikiliza?” Nikajisemea, lakini haikusaidia kitu.<br />
Tayari Zamaradi alishatoweka.</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..23.<br />
<br />
ZAMARADI tafadhali naomba ubadilishe mawazo!” Nilitamka kwa sauti kubwa.<br />
Ghafla nilishtuka. Nilikuwa peke yangu nikiwa natokwa na jasho mwili mzima. Zamaradi alikuwa ameshaondoka, akiniacha na mateso makali. Nilikuwa natetemeka kwa woga, nikihofia kifo cha Monalisa ambaye kama angekufa ni wazi kuwa mimi ndiye chanzo.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Phillip!” Ilikuwa ni sauti ya Lameck ikiniita.<br />
Sauti yake ilinishtua sana, sikutegemea kama angekuwa macho mpaka muda ule. Nilihofia kwamba inawezekana alinisikia wakati nikibishana na Zamaradi kuhusu Monalisa. Sikutaka kabisa agundue jambo hilo.<br />
<br />
“Phillip vipi, una tatizo gani?” Lameck akauliza, baada ya kuona simuitikii.<br />
“Niache tu kaka!”<br />
“Kwani vipi?”<br />
“Nilikuwa kwenye ndoto mbaya.”<br />
“Pole sana.”<br />
“Ahsante.”<br />
<br />
Nilipoangalia saa ya ukutani tayari ilikuwa imeshatimia saa 9:30 usiku. Bado kulikuwa na saa mbili na nusu mbele kabla ya kupambazuka. Kwa hakika sikutaka kabisa kifo cha Monalisa.<br />
<br />
Sikuwa na kitu kingine zaidi ya kuanza kulia. Nilianza kulia kwa sauti ndogo lakini muda ulivyozidi kwenda ndivyo sauti ya kilio changu ilivyozidi. Lameck akanisikia...<br />
“Phillip nahisi kuna kitu kingine zaidi unanificha.”<br />
“Nini hicho?” Nikamuuliza.<br />
<br />
“Kwa nini unalia?”<br />
“Mimeota ndoto mbaya sana, inanitisha na kunifanya niweweseke.”<br />
“Ndoto ni ndoto Phillip, haina uhusiano wowote na matukio ya kweli.”<br />
“Unaweza kusema hivyo kwa sababu haijakutokea wewe, lakini mimi inanitesa sana.”<br />
“Pole, jitahidi ulale. Puuza ndoto mbaya!”<br />
“Ahsante Lameck, sasa nitalala!”<br />
<br />
“Ok! Usiku mwema.”<br />
“Ahsante, nawe pia!”<br />
Hapo kidogo nikajitahidi kujikaza na kuishilia usingizini. Hofu yangu kubwa ilikuwa ni Zamaradi kunitokea tena baada ya kupitiwa na usingizi.<br />
<br />
***<br />
Nilikuwa wa kwanza kuamka asubuhi hiyo, nikaingia bafuni kuoga kisha nikajiandaa na kwenda kituoni kupanda daladala iliyonifikisha Mwenge ambapo nilipanda daladala ya kwenda Muhimbili.<br />
<br />
Niliposhuka katika kituo cha daladala cha Muhimbili nikatembea kwa kasi sana hadi katika wodi aliyokuwa amelazwa Monalisa. Kitu cha kushangaza sikumuona kitandani mwake.<br />
<br />
Nikapatwa na wasiwasi, kitu kilichovamia akilini mwangu kwa kasi, ni kwamba huenda alikuwa amekufa. Nikatoka mbio hadi ofisini kwa daktari. Hofu kubwa ilikuwa imetanda mbele yangu. Sikutaka kukutana na taarifa za kifo cha Monalisa.<br />
<br />
“Pole sana kijana, Monalisa amesafirishwa alfajiri ya leo kwenda Uingereza, hali yake ilibadilika na kuwa mbaya zaidi, hivyo wazazi wake wakaamua kufanya mpango wa kumuwahisha zaidi!” Dk. Mang’ola aliniambia baada ya kumuuliza alipo Monalisa.<br />
“Ameshapelekwa?”<br />
<br />
“Ndiyo!”<br />
“Mungu atamsaidia,” nikajikuta nikitamka maneno hayo.<br />
“Uingereza wana vifaa vizuri zaidi, inawezekana wakajitahidi kuokoa maisha yake. Tuombe Mungu!” Akasema Dk. Mang’ola.<br />
<br />
“Sawa dokta, acha mimi nikuache, nakutakia kazi njema.”<br />
“Nawe pia siku njema.”<br />
Nikatoka ofisini kwa dokta na moja kwa moja nikaenda kituoni nilipopanda daladala, safari ya kwenda chuoni ikaanza.<br />
<br />
***<br />
Kwa wiki nzima, sikuingia kwenye vipindi, nililala kila siku bwenini nikisingizia ugonjwa, ingawa ukweli niliokuwa nao moyoni ulikuwa mwingine kabisa. Nilikuwa na maumivu juu ya Monalisa.<br />
<br />
Baada ya muda huo nikaanza kujizoesha ratiba zangu kama kawaida. Nikawa naingia darasani na kwenda mazoezini jioni kama kawaida. Taratibu kumbukumbu za Monalisa zikaanza kupungua.<br />
<br />
Siku moja nikiwa naendelea na mazoezi uwanjani, nilikuwa nikishangazwa sana na jinsi wasichana walivyokuwa wakinishangilia kila ninapochoma mpira kwenye kikapu. Nikawa nawaangalia kwa kuibia, mara macho yangu yakagongana na msichana mmoja mrembo sana.<br />
<br />
Moyo wangu ukapasuka, alikuwa mwanamke mrembo kuliko kawaida. Muda wote uliobakia sikuweza kucheza vizuri, akili yangu ilikuwa kwa yule msichana. Baada ya kumaliza mazoezi, nilipotoka nje ya uwanja yule msichana alinifuata mbio.<br />
<br />
“Hongera sana Phillip!” Akasema akiachia tabasamu pana.<br />
Moyo wangu ukawa kama umepigwa ganzi. Tabasamu lake likanitetemesha na kuamsha hisia kali za mapenzi ndani ya mwili wangu. Alikuwa mwanamke mzuri kuliko kawaida, sikamsahau kabisa Zamaradi.<br />
<br />
“Phillip hongera...” akasema tena, baada ya kuniona nimekaa kimya badala ya kumjibu.<br />
“Nashukuru sana...vipi nimecheza vizuri?”<br />
“Sana.”<br />
“Ahsante kwa pongezi zako, sura yako ni ngeni sana machoni mwangu, bado mgeni au?”<br />
“Nipo muda mrefu na tangu nimesikia sifa zako, kila siku nimekuwa nikihudhuria hapa mazoezini kukuangalia ukicheza.”<br />
<br />
“Sifa gani hizo?”<br />
“Wewe hujui? Zaidi ya kucheza pia unavutia sana. Hukupata taarifa kwamba siku ambazo ulikuwa huji uwanjani mashabiki walipungua?”<br />
“Hivyo eeeeh! Sikujua hilo!”<br />
“Ndiyo hivyo sasa.”<br />
<br />
“Samahani napenda kujua jina lako!”<br />
“Naitwa Linna.”<br />
“Jina zuri sana, unachukua nini?”<br />
“Computer Science.”<br />
“Mh!”<br />
<br />
“Mbona unaguna?”<br />
“Wewe mkali sana, unasoma kozi ngumu namna hiyo, inaonekana ulipasua sana A Level!”<br />
“Kawaida tu!”<br />
“Sasa nataka kwenda, kama vipi tuongozane!”<br />
“Haina shida mimi nimekuja na gari. Unakaa bweni gani?”<br />
“Hall 5.”<br />
<br />
“Twende.”<br />
Nikachukua mfuko wangu wenye nguo, kisha nikaingia garini, tukaondoka uwanjani. Nilijitahidi sana kuficha hisia zangu, lakini ukweli ni kwamba hata Linna naye alionesha kunipenda. Alinipeleka mpaka bwenini kwangu.<br />
Tayari giza totoro lilishaanza kuingia. Akaegesha gari pembeni karibu na ngazi za kupandia kwenye lango kuu la kuingia bwenini. Linna akaniomba anibusu wakati wa kuniaga, nikakataa maana nilijua madhara yake.<br />
<br />
“Kwani una wasiwasi gani? Si tumeshakubaliana kuwa sisi ni marafiki?”<br />
“Ndiyo, sasa ndiyo unibusu?”<br />
“Mambo ya kizungu hayo!”<br />
“Hapana!”<br />
Nilikataa kwa nguvu zote, lakini ghafla Linna akanivuta na kunibusu kwa nguvu. Nikafungua mlango kwa hasira na kuondoka.<br />
<br />
***<br />
“Najua kilichotokea, siwezi kuvumilia, lazima nimfundishe adabu,” alikuwa ni Zamaradi akiniambia kwa ukali.<br />
“Lakini hatujafanya kitu Zamaradi.”<br />
“Kukubusu ni kosa kubwa sana kwangu, halafu mbaya zaidi alifanya ukaidi maana niliona wakati ukimzuia, sasa nitamfanya kinyago!”<br />
<br />
Nikashtuka sana, nikaanza kumuonea huruma Linna. Siku zote Zamaradi huwa hana utani katika kauli zake, ni wazi kuwa ilikuwa lazima amfanyie jambo baya. Nikaendelea kumsihi Zamaradi apunguze hasira na abadili mawazo lakini hakunielewa.<br />
Nikajiandaa kupokea taarifa mbaya juu ya Linna.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..24.<br />
<br />
KILA nilipokumbuka tukio la Monalisa la kupata ajali mbaya na kupooza mwili, tena akiwa amesafirishwa na wazazi wake kupelekwa nchini Uingereza kwa matibabu niliumia sana.<br />
<br />
Niliumia kwa sababu nilikuwa najua kila kitu kuhusu ajali yake. Mimi ndiye chanzo, jambo ambalo lilinitesa sana moyoni wangu. Mbaya zaidi ni Zamaradi ambaye kila wakati alinitokea usiku kwen<span class="text_exposed_show">ye ndoto na kunieleza ukweli kwamba kamwe hawezi kumsamehe!<br />
<br />
Zamaradi alinitisha sana kunieleza kwamba hata kama alikuwa amesafirishwa kwenda nje ya nchi, ni kazi bure maana hawatafanikiwa kumtibu na kupona. Alinihakikishia kuwa lazima atamtoa uhai.<br />
<br />
Nikiwa bado sijapona maumivu hayo ambayo yalinisumbua sana, Linna naye akafanya tukio ambalo halikumfurahisha Zamaradi, akanieleza wazi wazi kuwa atamkomesha.<br />
Ilikuwa lazima nichanganyikiwe sana. Usiku huo ukawa mgumu sana kwangu, sikufanikiwa kupata usingizi hata kidogo. Niliona maluweluwe huku matukio ya ajabu yakizunguka kichwani mwangu juu ya Linna.<br />
<br />
Namfahamu vizuri sana Zamaradi, huwa haahidi uongo hata mara moja na katika siku zote za maisha yangu na yeye ya kimapenzi, hajawahi kuniahidi ahadi ya uongo. Hilo liliniumiza sana, nilijua lazima kuna jambo baya lilikuwa njiani kumkuta Linna.<br />
<br />
Nilichanganyikiwa sana, nikatamani Zamaradi anitokee tena ili niendelee kumuomba msamaha, lakini hilo halikutokea. Niliamka asubuhi nikiwa sijaonana tena na Zamaradi, taa za hatari zikawa zinawaka ubongoni mwangu.<br />
<br />
***<br />
Ilikuwa Jumapili, nilipoamka sikutaka kwenda kanisani, kumbukumbu za Zamaradi zikaendelea kunitesa. Nilijihisi kama muuaji wa watu wasio na hatia. Nafsi yangu ilinisuta na hakika sikutaka Linna afe kwa kosa ambalo alilifanya bila kujua.<br />
“Lazima nifanye kitu fulani hapa, Linna anaweza kupata matatizo,” nikawaza kichwani mwangu.<br />
<br />
Hata hivyo kwa hakika sikujua ni jambo gani hasa ambalo nilipaswa kulifanya kwa ajili ya kumuokoa Linna. Kichwa changu kikawa kama kimejaa mambo mengi ambayo yalikuwa nje ya uwezo wangu.<br />
<br />
“Sijajua...lakini lazima nikutane naye,” nikaendelea kuwaza kichwani mwangu.<br />
Nilichokifanya ni kutoa simu yangu ya mkononi na kubonyeza namba zake. Simu iliita kwa muda mfupi sana, Linna akawa amepokea, akizungumza kwa furaha sana.<br />
“Hello Phillip!”<br />
“Vipi Linna?”<br />
<br />
“Poa.”<br />
“Kwa nini jana ulifanya vile?”<br />
“Nilifanyaje?”<br />
“Umesahau mara hii?”<br />
“Ni kuhusu kukubusu?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Mh! Yaani mpaka leo bado unakumbuka kitu hicho hicho jamani? Basi samahani kama nitakuwa nimekuudhi, lakini halikuwa lengo langu kukuchukiza.”<br />
“Unachukulia rahisi sana tatizo hili.”<br />
“Kwa nini?”<br />
“Unavyoongea tu!”<br />
<br />
“Kwani ni jambo kubwa kiasi hicho?”<br />
“Sikiliza Linna, hili ni jambo kubwa, nahitaji kuongea na wewe leo jioni. Utakuwa na nafasi tukutane?”<br />
“Hata sasa hivi nipo tayari.”<br />
<br />
“Hapana, iwe jioni tafadhali, maana sina muda kwa sasa.”<br />
“Saa ngapi?”<br />
“Tukutane saa 10.00.”<br />
“Unapenda wapi?”<br />
“Udasa Bar.”<br />
“Poa.”<br />
<br />
“Usipuuze ni lazima tuongee.”<br />
“Hamna shida Phillip, mtanashati wa chuo, nitakuja.”<br />
“We’ endelea kuchukulia utani, lakini ni kwa faida yako Linna!”<br />
“Faida yangu?”<br />
<br />
“Ndiyo!”<br />
“Kivipi?”<br />
“Utajua jioni.”<br />
“Haya tutaonana.”<br />
<br />
Tukakata simu zetu nikiwa na mawazo mengi sana, lakini ukweli ni kwamba sikupenda jinsi Linna alivyochukulia utani katika mambo muhimu kwa maisha yake kama yale. Hata hivyo isingekuwa rahisi kumlaumu kwa sababu hakujua alichokuwa akikifanya.<br />
<br />
***<br />
Nilifika katika Baa ya Udasa iliyokuwa ndani ya chuo chetu mapema sana. Cha ajabu wakati naingia tu, niliona gari lake limeegeshwa nje. Nikajua wazi kuwa alikuwa amenitangulia kufika.<br />
<br />
Nikampigia simu, akanielekeza mahali alipokuwa amekaa. Nikajongea taratibu na kumfuata. Alikuwa amekaa kimya akiendelea kunywa maji ya matunda.<br />
“Karibu Phillip,” akanikaribisha.<br />
“Ahsante, umefika muda mrefu?”<br />
“Tangu nusu saa iliyopita nilikuwa hapa. Ilikuwa lazima niwahi kabla yako.”<br />
<br />
“Vizuri.”<br />
Nilitulia kwa muda nikimwangalia na kujiridhisha kweli alikuwa mwanamke mrembo sana. Kwa hakika hakustahili kabisa kufa. Moyo wangu ukaenda mbio, nikashindwa kujua mahali pa kuanzia.<br />
<br />
Kwa jinsi ilivyoonekana, Linna alikuwa na shauku sana ya kutaka kujua nilikuwa nataka kumwambia nini. Alikuwa kimya kuliko kawaida, akionesha utayari wa kusikia chochote kutoka kwangu.<br />
Kinywa changu kilikuwa kizito kuongea, nilimwangalia kwa nukta kadhaa bila kutamka chochote. Naye alionekana kuanza kuingiwa na wasiwasi kidogo.<br />
<br />
“Linna, kwa nini jana ulifanya vile?” Nilimwuliza nikimwangalia usoni.<br />
“Samahani kwa kukuudhi, najua hukupenda lakini lazima niwe mkweli kwamba, nilifanya vile kwa hisia zangu za ndani kabisa kutoka moyoni.”<br />
“Hisia zipi?”<br />
<br />
“Phillip tambua kwamba wewe ni mwanaume mtanashati sana, hakuna mwanamke ambaye atakubali kupata nafasi ya kukaa na wewe sehemu ya peke yenu, akaacha kutamani angalau kupata busu lako. Ndivyo ilivyokuwa kwangu, nilitamani unibusu. Kama nilikukosea naomba unisamehe.”<br />
“Kwa hiyo unataka kusema kwamba unanipenda?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Acha kabisa Linna, mimi sitakiwi kuwa katika uhusiano wa aina hiyo kabisa.”<br />
“Hutakiwi kivipi, kwani wewe hunipendi?” akaniuliza.<br />
Lilikuwa swali gumu sana, nilichukua muda kidogo kumjibu. Ni kweli ndani ya nafsi yangu nilijihisi kumpenda sana Linna, lakini isingewezekana kutokana na masharti magumu ya Zamaradi.<br />
<br />
“Elewa tu hivyo.”<br />
“Mh!”<br />
“Usigune, ndiyo ukweli wenyewe ulivyo...halafu, vipi tangu hiyo jana hakuna tukio lolote lililotokea?” Nikamwuliza, lakini nikiogopa sana.<br />
“Tukio, unamaanisha nini?”<br />
<br />
“Basi, kama hakuna.”<br />
“Sijakuelewa Phillip, unamaanisha nini?”<br />
“Usijali,” nikamwambia na kubadilisha kabisa maongezi.<br />
<br />
Nisingeweza kuongea zaidi ya pale, maana kama baadaye angepatwa na tukio lolote, ingekuwa rahisi kulihusisha na maelezo yangu. Tukaanza kuzungumza mambo tofauti kabisa na yale.<br />
Saa tatu na dakika zake, usiku nikarudi zangu bwenini, lakini bado moyoni mwangu nilikuwa na wasiwasi mwingi. Zamaradi aliendelea kunitesa mawazoni.<br />
<br />
***<br />
Ndani ya gari alikuwa msichana mrembo sana, akiendesha gari kwa mwendo wa kasi. Alikuwa akitumia Barabara ya Sam Nujoma akitokea Ubungo. Muziki laini uliendelea kumsindikiza katika safari yake huku kiyoyozi kikimpuliza!<br />
<br />
Alipita eneo la Mlimani City kwa kasi sana, mbele kidogo ya kituo hicho akiwa anakaribia kufika katika mzunguko zinapokutana Barabara za Ardhi na Sam Nujoma, akashangaa kumuona mwanamke akiwa amesimama barabarani, mikononi mwake amebeba mtoto.<br />
<br />
Akashtuka sana na kupunguza mwendo, akiwa anajaribu kumkwepa akashangaa yule mwanamke anabadilika, wakaonekana wanawake wengi wanaofanana na yule aliyemuona awali, wote walikuwa wanalia, machozi yao yakitoka damu.<br />
<br />
Akakata kushoto ili aingie kwenye sheli ya Bonjour, lakini cha kushangaza akiwa anajaribu kukanyaga breki, gari ndiyo likaongeza kasi, kama amekanyaga mafuta! Akaenda kuvaa pampu moja ya mafuta aina ya petroli.<br />
<br />
“Puuuuuu....” mlio ukasikika na hapo hapo, moto mkali ukaanza kulipuka.<br />
Gari likaanza kushika moto, msichana huyo akiwa ndani yake. Alipiga kelele bila msaada wowote, magari mengine yaliyokuwa karibu yakatolewa, yeye akiendelea kuteketekea ndani ya gari.<br />
<br />
Akajitahidi kufungua mlango na kutoka ili kuinusuru roho yake, akiwa ndiyo anamalizia mguu wa mwisho, akahisi kama kuna mtu anamvuta. Akarudishwa ndani kwa kasi! Akaendelea kuungua!<br />
Sasa hakupiga tena kelele, alikuwa kimya! Msichana huyo mrembo alikuwa ni Linna.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012480977f621f42613929">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..25.<br />
<br />
Sauti ya msichana iliendelea kusikika kutoka katikati ya moto kuomba msaada lakini hakuwepo mtu mwenye uwezo wa kumsaidia, kila aliyekuwa karibu alijaribu kuokoa maisha yake. Lilikuwa ni tukio la kusikitisha, wote walimhurumia lakini hawakuwa na cha kufanya zaidi ya kushuhudia akifa.<br />
<br />
“Nakufa! Nisaidieni. Nateketea, niokoeni!” alizidi kupiga kelele msichan<span class="text_exposed_show">a huyo akiomba msaada. <br />
“Tufanyeje?” mmoja wa wafanyakazi wa kituo alimuuliza mwenzake.<br />
“Tuwapigie simu Zimamoto.”<br />
<br />
“Hawa ambao wakifika eneo la tukio wanakuwa hawana maji?”<br />
“Sasa tufanyeje?”<br />
“Mimi nashauri tuwapigie Knight Support au Ultimate Security, hao kidogo ni wepesi na huwa wanaegesha magari yao karibu kabisa na maeneo ya viwanda huku Mwenge.”<br />
“Uamuzi wa busara.”<br />
<br />
Wakati wanafikia uamuzi huo bado kituo kilikuwa kikiendelea kuteketea, Linna akiwa tayari amekwishanyamaza kuashiria kabisa kuwa roho yake ilishatoka. Kitendo cha mguu wake kubanwa na moja ya vyuma vya bodi ya gari ndicho kilichosababisha akumbwe na mkasa huo, laiti mguu wake ungeachwa huru angefanikiwa kutoka ndani ya gari lake kabla moto haujawa mkubwa na kuokoa maisha.<br />
<br />
“Ultimate Security hapa.”<br />
“Ndiyo, kuna kituo cha mafuta kinateketea.”<br />
“Wapi?”<br />
“Hapa Mwenge karibu kabisa na Mlimani City.”<br />
“Hicho cha kwenye kona ya Chuo Kikuu?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Wewe ni nani?”<br />
“Mfanyakazi wa kituo.”<br />
“Nani atalipia gharama ya kuzima?”<br />
“Nyinyi njooni tu mzime, bosi wetu atalipa.”<br />
“Una uhakika?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Basi tunawasiliana na wenzetu walioko Mwenge, Coca Cola.”<br />
<br />
***<br />
Bahati nzuri dereva wa gari la Zimamoto lililomilikiwa na Kampuni ya Ultimate Security alikuwa njiani kuelekea maeneo ya Ubungo, simu yake ilipoita aliipokea na kupewa maelekezo ya kwenda haraka eneo la tukio ili kujaribu kuokoa mali na maisha ya watu. Akabadilisha gia na kuwasha king’ora kilichokuwa kimezimwa na kuongeza kasi.<br />
<br />
“Nilishauona huo moto, moshi wake ni mkubwa mno, niko umbali wa kama mita mia mbili tu kufika eneo la tukio.”<br />
“Uzimeni haraka, watatulipa baada ya kazi.”<br />
“Sawa.”<br />
<br />
Dakika moja na nusu baadaye kwa sababu hapakuwa na msongamano wa magari barabarani, gari la Zimamoto lilifika na watu waliokuwa wamesimama mbali kuanza kushuhudia maji yakiruka na moto kuzimwa ndani ya dakika kumi. Gari la Linna lilikuwa limeteketea kabisa, yeye mwenye akiwa amelala nje ya gari hilo mguu mmoja ukiwa umebanwa.<br />
<br />
Alilala kifudifudi juu ya ardhi, hakuna sehemu ya mwili wake mgongoni kuanzia kichwani hadi miguuni iliyobaki bila kuungua, walichokifanya askari wa Zimamoto ni kumbeba haraka na kumpakia ndani ya gari lao kisha kuondoka kwa kasi kuelekea hospitali wakiwa hawajui ni ipi iliyokuwa karibu na kama mtu waliyekuwa wakijaribu kuokoa maisha yake alikuwa hai au la.<br />
<br />
“Wapi?” Dereva aliuliza.<br />
“Tutawahi Muhimbili kweli?”<br />
“Siyo rahisi.”<br />
“Sasa tutaelekea wapi?”<br />
<br />
“Tujaribu hospitali ya jeshi Lugalo.”<br />
“Ni mzima huyu kweli?”<br />
“Hakuna mwenye uhakika, wewe twende tu madaktari watajua baada ya kumpima.”<br />
Gari lilizidi kuendeshwa kwa kasi huku king’ora kikilia na kufanya magari mengine yaliyokuwa barabarani yapishe, dakika tano baadaye gari hilo liliegeshwa Idara ya Mapokezi Hospitali ya Lugalo na wauguzi wakafika na machela yao.<br />
<br />
“Mungu wangu.” Mmoja wa wauguzi alisahau maadili ya kazi yake na kujikuta akitamka neno hilo baada ya kuushuhudia mwili wa Linna.<br />
Haraka wauguzi wakavaa mipira mikononi mwao na kuushusha mwili huo ambao kila sehemu waliyogusa ilibanduka ngozi, hakika Linna alikuwa ameungua vya kutosha, hakuna sijui ni maneno gani yangetamkwa kuelezea vizuri hali hiyo zaidi ya mtu kushuhudia mwenyewe. Akashushwa na kulazwa juu ya machela kisha kukimbizwa chumba cha daktari.<br />
<br />
“She is still breathing, but this is a severe case of third degree burn!” (Bado anapumua, lakini ni mgonjwa aliyeungua vibaya kabisa, kiwango cha daraja la tatu..) Aliongea daktari wa kike akiwa amezungukwa na vijana walioonekana kuwa wanafunzi wa udaktari.<br />
<br />
“What is the prognosis in cases like this one?” (Nafasi ya kupona ikoje kwa wagonjwa kama huyu?) Mmoja wa wanafunzi madaktari aliuliza.<br />
“To be honest the prognosis is very poor, may be until a miracle happens!” (Kusema ukweli nafasi ya kupona ni ndogo, labda utokee muujiza.) Daktari aliongea na kuwaamuru wauguzi wamkimbize haraka sana mgonjwa chumba cha wagonjwa mahututi.<br />
<br />
Linna akabebwa na kupandishwa juu ya machela akiwa bado hajitambui.<br />
Kilichofanyika chumba cha wagonjwa mahututi ni kasi ya kumuongezea maji mfululizo ili kuziba pengo la maji yaliyopotea kwa kuungua, mashine ya hewa ya oksijeni ilifungwa puani na mdomoni kwake. <br />
<br />
Yote haya yalifanyika kujaribu kuokoa maisha ya msichana huyu ambaye mpaka wakati huo alikuwa hajatambulika, kwani sura yake ilikuwa imeharibika vibaya na hata gari lake pia liliteketea kiasi cha namba zake kutoonekana. Madaktari hawakujali hilo, cha muhimu kwao ilikuwa ni kumponyesha mgonjwa, mengine yangefuata baadaye.<br />
<br />
“Will she survive?” (Atanusurika?) Dk. Mafuru, bingwa wa upasuaji kwenye Hospitali ya Lugalo aliwauliza wenzake kwenye kikao cha kumjadili mgonjwa huyo.<br />
<br />
“Not possible, even if she does, she will never be the same again, the deformities caused by the scars will be too bad.” (Siyo rahisi, hata akinusurika, hatakuwa yule yule tena, vilema vitakavyosababishwa na makovu vitakuwa vibaya mno.)<br />
“Kama wazazi wake ni matajiri, wanaweza kumpeleka kwenye hospitali kubwa nje ya nchi ambako atafanyiwa upasuaji wa marekebisho, si chini ya operesheni hamsini au sitini hivi ndiyo zinaweza zikamsaidia, tofauti na hapo atakuwa na maisha magumu sana. <br />
<br />
Sijui kama anaweza kuona tena.” Dk. Matilda aliyempokea Linna kwa mara ya kwanza aliongea.<br />
“Nawashauri kwanza tushughulikie kuokoa maisha yake mengine yatafuata, ila kwa kweli ameungua, sijawahi kuona mtu aliyeungua kiwango hiki tangu nianze kazi hii miaka thelathini iliyopita.”<br />
<br />
“Tunaendelea na matibabu gani sasa?”<br />
“Drip za Normal saline kwa kasi na prophylactic anti-biotics, kuzuia maambukizi.”<br />
“Kama ipi hiyo anti-biotic?”<br />
“Urgumentin.”<br />
“Haya jamani tuwasiliane baadaye.”<br />
Kikao kikamalizika na madaktari wakasambaa kwenda kuendelea na kazi nyingine za kuhudumia wagonjwa.<br />
<br />
***<br />
“Mh!”<br />
“Mbona unaguna?”<br />
“Sijamsikia Linna akirudi.”<br />
“Hata mimi au tulipitiwa na usingizi?”<br />
“Hebu ngoja nikaangalie chumbani kwake, haiwezekani awe hajarudi mpaka saa hizi na hata kutupigia simu kutoa taarifa kwamba yuko na rafiki zake mahali fulani.” Mama yake Linna alisema na kukurupuka kitandani kisha kutembea moja kwa moja na kushusha ngazi hadi chini kilikokuwa chumba cha Linna, mlango ulikuwa wazi akaufungua na kuingia ndani.<br />
<br />
“Mh!” Akaguna tena baada ya kukuta binti yake hayupo, saa ya mezani ilisomeka saa 6:20. Haikuwa kawaida ya Linna kukaa nje mpaka muda huo bila kutoa taarifa kwa mama yake ambaye pia alikuwa rafiki yake mkubwa, mama akapandisha ngazi moyo wake ukiwa umejawa na hofu, hisia zilimtuma kuanza kuamini kulikuwa na tatizo lililompata mwanaye baada ya kuusikia kabisa mwili wake hauko sawa.<br />
<br />
“Hayupo.” Alimwambia mume wake.<br />
“Mh! Hebu piga simu yake.” Mzee alisema pia akianza kuingiwa na wasiwasi moyoni mwake.<br />
Simu ya Linna ilipopigwa ilionekana imezimwa, wakajaribu kupigwa kwa rafiki zake ambao mara nyingi alikuwa nao usiku jibu likawa wote walikuwa nyumbani kwao wamelala na hawakujua mahali Linna alikokuwa. Wasiwasi ukazidi kuongezeka. <br />
“Sasa atakuwa wapi?”<br />
“Hata sijui.”<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? FUATILIA KESHO KWA UTAMU ZAIDI.....WEEKEND NJEMA!!</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012480977f621f42613929"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012480977f621f42613929"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012480977f621f42613929"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012480977f621f42613929"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012480977f621f42613929"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012480977f621f42613929"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248bd526465c96389722">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..26.<br />
<br />
<br />
angu utotoni kijana Phillip alikuwa akimuota msichana mrembo na baadaye yeye na msichana huyo walifunga ndoa ndotoni na kuzaa mtoto mmoja. Kwenye ulimwengu halisi, hivi sasa Phillip ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambako wasichana wanahangaika kumpata bila mafanikio. <br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Msichana wa ndotoni (Zamaradi) alishamuonya kwamba kila mwanamke atakayekuwa na uhusiano naye atamdhuru. Jambo hili ni siri yake, kamwe asidiriki kuwaeleza wasichana waliomtaka kimapenzi kuwa yeye ni mume wa jini mkali na mwenye wivu.<br />
<br />
Wasichana wakidhani Phillip alikuwa mvulana mwoga, wakamfanyia njama na kumfanya ashiriki mambo ya mapenzi bila ridhaa yake. Kilichowapata wasichana hao ni ajali za gari; wa kwanza alikuwa ni Monalisa ambaye akiendesha gari kwa kasi, alishitukia mwanamke mwenye mtoto akisimama mbele yake.<br />
<br />
Wakati akijaribu kumkwepa gari lake lilipinduka, akaumia ubongo na uti wa mgongo hivi sasa amepooza na wazazi wake wanahangaika kutafuta matibabu sehemu mbalimbali duniani.<br />
Linna msichana wa pili naye akamshawishi Phillip na kumbusu kwa nguvu, muda mfupi tu baadaye akiendesha gari lake kuelekea nyumbani, mwanamke akaonekana katikati ya barabara, wakati akimkwepa gari liliacha njia na kuingia kwenye kituo cha mafuta na kugonga pampu ya mafuta ya petroli, moto mkubwa ukalipuka na kumuunguza vibaya.<br />
<br />
Zimamoto walifanikiwa kuuzima moto na kumtoa Linna akiwa katika hali mbaya, wakampeleka hospitali ambako madaktari wamempokea wakiwa na uhakika kabisa asingepona. Wazazi wake walipogundua usiku kwamba Linna hayuko ndani ya nyumba, walipiga simu yake bila mafanikio, wasiwasi mwingi ukawaingia zaidi hasa baada ya kuwapigia hata rafiki zake ambao pia walithibitisha kutomuona. Hivi sasa wamechanganyikiwa, hawajui cha kufanya.<br />
Je, nini kinaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
Wazazi walikuwa wamechanganyikiwa kabisa, Linna ndiye mtoto pekee aliyebaki, tegemeo lao na mrithi wa utajiri wao baada ya kaka yake kufariki miaka michache iliyopita. Hawakuwa tayari kumpoteza, kulifikiria jambo hilo tu peke yake kulimfanya mama yake Linna aanze kulia na mume wake kumpigapiga mgongoni akimfariji na kumwambia asiwe na wasiwasi Linna angerejea.<br />
<br />
“Kweli?”<br />
“Usiwe na shaka.”<br />
“Moyo wangu unaniambia mwanangu yupo katika matatizo.”<br />
“Hizo ni hisia tu mke wangu.”<br />
Waliendelea kumsubiri bila mafanikio, kila walipoisikia muungurumo wa gari nje ya nyumba yao, walisimama na kuchungulia wakiamini Linna alikuwa amerejea, haikuwa hivyo, magari mengi yaliyopita yalikuwa ni ya majirani. Walishangaa siku hiyo jinsi masikio yao yalivyokuwa na uwezo mkubwa wa kusikia kuliko siku nyingine.<br />
<br />
Mpaka saa kumi na mbili asubuhi Linna alikuwa hajarejea, walishapiga simu yake bila kufanikiwa kumpata na walikuwa hawajasinzia kabisa. Baba akainuka kitandani na kuchukua rimoti ya televisheni iliyokuwa juu ya meza ndogo kando mwa kitanda, akaibonyeza akiwa ameilenga runinga na kuiwasha.<br />
<br />
“Hii ni taarifa ya habari kutoka Shirika la Utangazaji la Taifa, msomaji wako ni mimi Leodgar Masome, …<br />
Dar es Salaam; Ajali mbaya ya moto imetokea jijini Dar es Salaam baada ya gari dogo kuacha njia na kugonga kituo cha mafuta cha Bonjour, dereva wa gari hilo ambaye amejeruhiwa vibaya kwa moto na hali yake ni mbaya amelazwa katika Hospitali ya Muhimbili… tuungane na mwandishi wetu Brighton Masalu aliyefika eneo la tukio…<br />
<br />
Mama yake Linna aliyekuwa amejilaza kitandani, aliposikia maneno hayo alikurupuka na kuisogelea runinga, yeye na mume wake wakaanza kuangalia namna moto ulivyokuwa ukiwaka huku gari la zimamoto likiendelea kuzima na baadaye majeruhi alivyotolewa ndani ya gari ambalo lilikuwa limebadilika kabisa na kuwa na rangi nyeusi.<br />
<br />
“Anaweza kuwa Linna huyu?” Mama yake aliuliza.<br />
“Hapana!”<br />
“Hata kama ni yeye, naomba hii isiwe ukweli, iwe ndoto!”<br />
“Hawezi kuwa yeye, gari lile si lake.”<br />
“Ile inaonekana kama Peugeot, siyo BMW!”<br />
“Kabisa.”<br />
<br />
“Afadhali, angekuwa yeye sijui ingekuwaje.”<br />
“Lakini atakuwa wapi, hata kama yuko kwa mpenzi wake ni bora arudi nyumbani, anatutesa sisi wazazi wake.”<br />
“Ni kweli kabisa.” Mama alijibu akihema kwa nguvu, mapigo yake ya moyo yalikuwa yamebadilika kabisa.<br />
<br />
Waliendelea kusubiri huku wakiwasiliana na ndugu, jamaa na marafiki ili kuona kama Linna alikuwa amefika kwao lakini kote hawakufanikiwa. Hii iliendelea kuwajaza wasiwasi, hatimaye ilipofika saa sita mchana wakafikia uamuzi wa kuondoka nyumbani kwenda kituo cha kati cha polisi ambako waliulizia kama kuna ajali yoyote ilikuwa imetokea, wakaelezwa ni ya moto peke yake iliyohusisha gari kwenye kituo cha mafuta.<br />
“Huyo majeruhi yuko hospitali gani?”<br />
<br />
“Muhimbili wodi ya wagonjwa mahututi.”<br />
“Ni vyema twende tukamuone, huwezi kujua anaweza kuwa ni mtoto wetu.”<br />
“Ushindwe katika jina la Yesu!” Mama yake Linna aliongea akimuangalia mume wake.<br />
“Nisamehe mpenzi wangu, ni mawazo tu.”<br />
<br />
Wakaingia ndani ya gari na kwenda moja kwa moja hadi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako gari liliegeshwa na wakashuka kisha kutembea kwa haraka hadi chumba cha wagonjwa mahututi, ingawa muda wa kuona wagonjwa ulikuwa umeisha, baba yake Linna alitumia kufahamika kwake kumshawishi muuguzi angalau awaruhusu waingie kumuona majeruhi wa moto.<br />
<br />
“Baba nawapa dakika mbili tu!”<br />
“Zinatosha sana mwanangu.”<br />
“Asante binti.” Mama alisema na wote wakaingia haraka na kupelekwa mpaka kwenye kitanda alicholazwa Linna, wakaanza kumwangalia kuanzia kichwani hadi miguuni, nywele zote zilikuwa zimeungua na ngozi ya mwili ilikuwa imebabuka na kuufanya uwe nyama iliyo wazi.<br />
<br />
“Ni yeye?” Baba yake aliuliza.<br />
“Hapana, huyu siye, afadhali!” Mama aliongea akitabasamu, kitendo cha kukuta mtu aliyeteketea ndani ya gari si Linna kilimfurahisha na kumfanya atamani Linna arejee nyumbani.<br />
“Lakini urefu ni sawa.”<br />
“Hata kama ni sawa, huyu si Linna.”<br />
<br />
Walipotoka hapo walirejea nyumbani, mioyoni wakidhani wangeweza kumkuta Linna amekwisharejea lakini haikuwa hivyo, mpaka saa moja jioni. Wakazidi kuchanganyikiwa, usiku wa siku hiyo pia hawakulala mpaka asubuhi ambapo walifikia uamuzi wa kwenda kituo cha polisi wakitaka kujua kama kweli gari lililoungua halikuwa la Linna.<br />
<br />
Walipofika kituoni walijitambulisha, bahati nzuri baba yake Linna alifahamika na watu wengi, hivyo haikuwa kazi ngumu kumuona mkuu wa kituo na kumweleza tatizo lake. Yeye ndiye aliyewachukua na kuwapeleka nyuma ya kituo ambako gari lilikuwa limeegeshwa, kwa jinsi lilivyokuwa limeteketea haikuwa rahisi hata kidogo kulitambua.<br />
“Ni lenyewe?” Mkuu wa kituo aliwauliza.<br />
<br />
“Siyo.” Mama yake Linna aliitikia.<br />
“Lakini mimi nina wasiwasi kidogo, muundo ndiyo wenyewe, nashauri nikimbie nyumbani mara moja nikachukue faili la gari la Linna ili tupate namba za chesisi yake, hiyo ndiyo itatupa uhakika kama kweli gari hii siyo ya mtoto wetu.”<br />
“Baba Linna, ya nini yote hayo? Au unataka mwanangu ndiyo awe ameteketea kwenye gari hii?”<br />
<br />
“Siyo hivyo mke wangu, moyo wangu umeingiwa wasiwasi, twende!” Aliongea mzee huyo na kwa pamoja wakamuaga mkuu wa kituo na kuingia ndani ya gari lao, safari kuelekea nyumbani iliwachukua dakika kumi na tano wakawa wameshafika, kuegesha na kupandisha juu kwenye chumba cha Linna ambako walifungua kabati na kulipata faili, haraka wakashuka hadi kwenye gari na kuondoka tena kuelekea kituoni.<br />
<br />
Mkuu wa kituo aliomba msaada wa maaskari ambao walifungua sehemu ya mbele ya gari na kukuta injini ikiwa imeungua lakini si kiasi cha maandishi ya kuchimbwa kwenye injini kushindwa kusomeka, haikuchukua muda mrefu namba za chesisi zikapatikana, wote wakasogeza vichwa vyao karibu na kuanza kusoma namba moja baada ya nyingine.<br />
<br />
“Uuuuwi! Maskini mwanangu Linna! Uuuuuwi!” Ilikuwa ni sauti ya mama yake akilia baada ya kugundua namba ya chesisi iliyoonekana ni ya gari la Linna, ilimaanisha mtoto wao ndiye alikuwa ameteketea ndani ya moto, yalikuwa ni maumivu makali yasiyopimika, kama mkuki wa moto kuuchoma moyo wa mtu akiwa hai. <br />
<br />
Mama akaanguka chini na kuanza kugalagala akilia, kazi ya mume wake ikawa ni kumbembeleza mpaka alipotulia ndipo kwa msaada wa polisi akasaidiwa kutembea mpaka kwenye gari, wakaondoka pamoja mpaka hospitali na kupelekwa tena kwenye kitanda cha mgonjwa.<br />
<br />
“Linna! Linna! Linna!” Mama aliita lakini Linna hakuitika, bado hakuwa na fahamu, alipumua kwa kutumia mashine ya oksijeni iliyokuwa kando ya kitanda huku dripu nyingi zikiingia mwilini mwake kupitia mirija.<br />
“Mama hawezi kukusikia, tangu amekuja hapa hana fahamu, ni ajali mbaya sana ya moto kuliko zote ambazo nimewahi kushuhudia.”<br />
<br />
“Mwanangu atapona daktari?” Baba yake Linna aliuliza, naye akijifuta machozi, haikuwa rahisi kujizuia kwa jinsi hali ilivyokuwa.<br />
“Ni kazi ya Mungu, tunajitahidi sana kufanya kazi yetu ambayo ni kutibu, lakini mponyaji ni Mungu.” Daktari huyo aliongea.<br />
“Bila shaka wewe ni Dk. Mafuru?”<br />
“Ni kweli.”<br />
<br />
“Nakufahamu sana.”<br />
“Hata mimi nawafahamu sana wazee wangu, sikujua tu kwamba huyu ni Linna, si rahisi kumtambua.”<br />
“Tusaidie daktari, angalau mtoto wetu apone.”<br />
“Mungu atasaidia, ila hata kama akipona, ukweli ni kwamba hawezi kuwa Linna yule yule tena, roho inaniuma sana, lakini sina jinsi. Sijui ni kwa nini Mungu huwa anaruhusu matukio kama haya?”<br />
<br />
“Sisi tunamshukuru Mungu, najua ni kwa nini ameruhusu jambo hili litokee.” Baba yake Linna aliongea kwa huzuni.<br />
Mama yake Linna alipiga magoti kando ya kitanda na kuendelea kulia huku akimuomba Mungu amsaidie mwanaye apone, muda huo baba yake Linna alikuwa akiwasiliana na uongozi wa Chuo Kikuu kuwapa taarifa za kupatikana kwa mtoto wao akiwa katika hali mbaya. Taarifa hizo zikabandikwa kwenye ubao wa matangazo na kuwataka wanafunzi wenye nafasi wafike haraka Hospitali ya Muhimbili kumuona mgonjwa, tayari ilikuwa saa tisa na nusu alasiri.<br />
<br />
***<br />
Baada ya chakula cha mchana, Phillip alikuwa katikati ya mawazo mengi chumbani kwake, akiyapitia mambo yaliyokuwa yakitokea maishani mwake, kuanzia kwa Monalisa aliyekuwa amepooza na sasa alikuwa hajui ni wapi alipokuwa Linna baada ya kumlazimisha busu mara ya mwisho walipoonana. Hisia zilimtuma kufikiri lazima kuna jambo lililokuwa limetokea, Zamaradi alikuwa amemtenda jambo, pengine kumuua na maiti yake kupotea.<br />
<br />
“Acha niende chuoni labda nitakuta amerejea, namuomba Mungu asaidie ili asije akawa ameingia kwenye matatizo.” Aliwaza Phillip na kunyanyuka kitandani kisha kuchukua begi lenye kompyuta yake na kuanza kutembea taratibu kuelekea darasani.<br />
Alishangazwa na umati mkubwa wa watu waliokuwa wamekusanyika mbele ya jengo la utawala, wakiwa katika vikundi vidogo vidogo wakijadili jambo huku wengine wakiwa kwenye ubao wa matangazo, wote wakisoma jambo. <br />
<br />
Akawahi hapo na kupenya katikati ya watu mpaka akaufikia ubao na kuanza kusoma, muda wote alipokuwa akisoma machozi yalikuwa yakimbubujika kwani alielewa kilichotendeka, hasira dhidi ya Zamaradi zikampanda akiamini kabisa alikuwa akiwadhuru watu wasio na hatia.<br />
<br />
“No! Something has to be done! I can’t let her continue tormenting innocent being.” (Hapana! Jambo fulani linahijika kufanyika, siwezi kumwacha aendelee kutesa viumbe wasio na hatia.) Alijisemea moyoni mwake Phillip na kwenda kando ambako alianza kulia kama jinsi wanafunzi wengine wengi walivyokuwa wakibubujikwa na machozi.<br />
<br />
Haukupita muda mrefu sana mabasi matatu yakafika na wanafunzi wakapanda, wote walikuwa wakielekea Hospitali ya Muhimbili kumuona mwanafunzi mwenzao, Phillip akawa miongoni mwao ili akamuone Linna. Moyoni alikuwa na maumivu makali mno, sababu alielewa kila kitu kilichokuwa kikiendelea na alihisi kuwajibika.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012480977f621f42613929"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012480977f621f42613929"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012480977f621f42613929"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248d8a619b5d41937917">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..27.<br />
<br />
Aliketi kiti cha nyuma kabisa dirishani, akiendelea kububujikwa na machozi, kando yake akiwepo Tyra, msichana mrembo ambaye pia alikuwa katika ligi ya kumpata. Mkono wa Tyra ulikuwa begani kwa Phillip akijaribu kumbembeleza asilie, kwake nafasi hiyo ilikuwa muhimu na alitaka kuitumia vyema kumuonyesha Phillip kwamba ni kiasi gani alimjali.<br />
<br />
“Tyra.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Bee!”<br />
“Toa mkono begani, usinipapase, utapata matatizo!”<br />
<br />
“Matatizo gani? Kama ni mapaparazi wa chuo mimi siwaogopi, siwezi kukuacha uendelee kulia, najua matukio ya Monalisa na Linna yamekuumiza sana. Usisikitike, Mungu hakuwapangia wao, pengine hii ilikuwa ni riziki yangu…”<br />
“Tyra!” Phillip aliita akimuangalia kwa jicho la huruma, alielewa ambacho kingefuata kama msichana huyo angeendelea na mpango wake, yeye pia angekutwa na matatizo kama yaliyowapata wenzake.<br />
<br />
“Bee!”<br />
“Nisikilize mimi, ninajua ninachokisema, tafadhali usinilazimishe nizungumze mambo mengine ambayo mimi sipendi kuyaongea.”<br />
“Mambo gani Phillip?”<br />
“Basi tu, wewe toa tu mkono.” Phillip aliongea akiutoa mkono wa Tyra begani kwake, wanafunzi wengine waliokuwa jirani waliangaliana, Tyra msichana mzuri na mwenye maringo kuliko mwingine yeyote katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alijisikia vibaya mno.<br />
<br />
“Haya bwana, sitakufuatilia tena, hii ni mara ya mwisho.”<br />
“Nashukuru.”<br />
Tayari basi walilopanda likawa linakata kona kutoka Barabara ya Umoja wa Mataifa na kuingia Barabara ya Malik kuelekea Muhimbili, hawakuongea tena kitu chochote mpaka wanashuka Idara ya Mapokezi. Walishangazwa na umati wa wanafunzi waliowakuta, kumbe wengi walitangulia hospitalini kutoka mabwenini, zaidi ya wanafunzi elfu nne walikuwa wamejaa mbele ya jengo la mapokezi, walikuwa wamezuiliwa kwenda chumba cha wagonjwa mahututi kumuona Linna, baadhi walikuwa wakilia.<br />
<br />
Aliposhuka ndani ya basi, Phillip hakutaka kuongea na mtu tena, alichagua eneo la pembeni karibu kabisa na Idara ya Maabara na kuketi kwenye msingi wa nyumba , akainamisha kichwa chake chini na kuendelea kulia, huku mkononi akiwa ameshikilia kijiti na kuandika juu ya ardhi; I love you, don’t die! maneno ya Kiingereza yaliyomaanisha; Nakupenda, usife.<br />
<br />
Akayasoma maneno hayo mara nyingi na kuzama ndani yake, kwa mara ya kwanza akaamini moyoni mwake alikuwa akimpenda sana Linna, bila Zamaradi kuwepo maishani mwake na akapewa nafasi ya kuchagua mwanamke wa kuoa, asingemchagua mwingine yeyote isipokuwa yeye, sasa alikuwa ameungua na moto, Zamaradi alikuwa amemteketeza, kwa hali aliyokuwa nayo lazima angekufa, moyo ukamuuma.<br />
<br />
“Haya tukusanyikeni! Wanafunzi wote tukusanyikeni, daktari anataka kuongea na sisi” Ilikuwa ni sauti ya Jason Mbwambo, rais wa serikali ya wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.<br />
<br />
Sauti hiyo ndiyo iliyomgutua Phillip na kumuondoa katika dimbwi la mawazo alilokuwa amezama ndani yake, akanyanyuka taratibu na kujikongoja mpaka mahali ambako wanafunzi wote walikuwa wakijikusanya, minong’ono ikaanza kusambaa kwamba Linna alikuwa amefariki dunia, taarifa hizo zilimuumiza sana, akabaki kimya katikati ya wanafunzi wenzake akimsubiri daktari aje atangaze. Dakika ishirini baadaye daktari alifika na kusimama mbele ya wanafunzi.<br />
<br />
“Habari zenu!”<br />
“Nzuri shikamoo daktari.”<br />
“Marahaba, naitwa Dk. Mafuru, mimi ndiye ninashughulika na tatizo la mwanafunzi mwenzenu, rafiki yenu Linna, nimejitokeza hapa kuwapeni habari kwamba, hali yake si nzuri, ameungua sehemu kubwa sana ya mwili wake. Tunajitahidi kadiri ya uwezo wetu kuokoa maisha yake, hatuwezi kusema atapona kwa sasa, ila tuendeleeni kumuombea! Hizo ndiyo habari nilizotaka kuwapatia. Kama kuna swali mnaweza kuniuliza.” Alimaliza daktari na kuanza kuwaangalia wanafunzi, mkono mmoja ulikuwa hewani.<br />
<br />
“Naitwa Phillip, sina swali ila nilikuwa naomba nikamuone mgonjwa.”<br />
“Suala la kumuona nyinyi nyote ni gumu, mgonjwa anahitaji utulivu, hivi sasa hana uwezo wa kuzungumza, hivyo kuwaruhusu kwa wingi wenu muingie itakuwa ni sawa na kumsumbua mgonjwa, lakini tunaweza kuruhusu viongozi wenu wawawakilishe.”<br />
“Sawa daktari!” Wanafunzi wengi waliitikia.<br />
<br />
Phillip hakuwa miongoni mwa viongozi wa serikali ya wanafunzi, lakini alishinikiza mpaka kujikuta yuko kati ya wanafunzi saba walioruhusiwa kuongozana na daktari hadi ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi, hakuamini alichokiona Linna alipoondolewa kifaa kilichomfunika juu yake kukiwa na mashuka na kubaki wazi, Phillip alilia, hakuwa Linna bali kiumbe kingine tu kilichochunwa ngozi na moto.<br />
<br />
“No! Huyu siyo Linna, nionyesheni mwingine.” Aliongea akijiunga na wanafunzi wenzake wote kulia, ilikuwa picha mbaya mno kuishuhudia.<br />
Haikuwezekana kabisa kubaki ndani ya chumba hicho, wote baada ya kupiga magoti pembeni mwa kitanda na kusali walinyanyuka, wakawapa pole wazazi kisha kutoka hadi nje ambako walishindwa hata kuwasilimulia wenzao walichokishuhudia. Dakika ishirini baadaye walipanda kwenye mabasi na safari kurejea chuo kikuu ikaanza, huko Phillip hakuwa na la kufanya zaidi ya kushuka na kwenda moja kwa moja bwenini kwake, akajifungia na kuanza kulia.<br />
<br />
Baadaye fahamu zilimpotea, ulikuwa ni usingizi mzito uliomchukua, akamshuhudia Zamaradi pamoja na mwanaye akimwijia, uso wake ukiwa na tabasamu, mkononi akiwa ameshikilia boksi na kuliweka juu ya meza. Phillip alikurupuka kitandani na kuanza kumfokea akilalamika ni kwanini alikuwa akitesa watu bila huruma kiasi hicho, Zamaradi hakuwa na la kusema zaidi ya sentensi “Samahani, nakupenda mno, niko tayari kufanya lolote kukulinda mume wangu.” <br />
<br />
Aliposema maneno hayo Zamaradi alipotea, Phillip akafumbua macho yake na kushuhudia juu ya meza kukiwa na boksi kama alivyoona ndotoni. Taratibu akajinyanyua kitandani kulisogelea boksi hilo, alipofungua ndani yake alikuta kuna mkufu, saa ya dhahabu na bulungutu la dola za Kimarekani. <br />
<br />
Pia kulikuwa na karatasi ndogo ambayo juu yake iliandikwa maneno “I am sorry!” kwa kutumia damu ambayo Phillip hakuelewa ilikuwa ni ya binadamu au mnyama gani. Taratibu akaanza kuhesabu noti za dola mia alizozikuta, zikatimia elfu kumi! Moyo wake ukaanza kushuka, hasira aliyokuwa nayo ikaanza kupungua hasa baada ya kuivaa saa mkononi pamoja na mkufu shingoni, tabasamu likarejea.<br />
<br />
***<br />
Hali ya Monalisa ilikuwa mbaya kupita kiasi, juhudi zote za madaktari zilionekana kugonga mwamba lakini wazazi wake hawakuwa tayari kukata tamaa. Ni kweli alikuwa amepooza na asingenyanyuka kitandani siku zote za maisha yake kwa maelezo ambayo madaktari waliyatoa lakini bado wazazi hao walitaka kujaribu njia nyingine, fahamu zilishamrejea binti huyo na alikuwa akilia akiwaomba wazazi wake wasihangaike sana.<br />
<br />
“Baba!”<br />
“Naam!”<br />
“Msihangaike, mliyoyafanya yanatosha, bila shaka huu ndiyo ulitakiwa kuwa mwisho wangu. Jambo moja tu naomba mnifanyie, nitafurahi sana.”<br />
“Jambo gani mwanangu?”<br />
“Nahitaji kuongea na mwanafunzi mmoja chuo kikuu anaitwa Phillip.”</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248f259e2c1456340512">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..28.<br />
<br />
“I think this is beyond our control, we cant save the life of this victim, she has severe bruises and burns which penetrated into her body. She must be referred,”<br />
(Nafikiri hii ni nje ya uwezo wetu, hatuwezi kuokoa maisha ya mwathirika huyu, ana malengelenge na majeraha ya moto yaliyopenya hadi ndani ya mwili wake. Lazima tumtafutie rufaa) aliongea Daktari Mafu<span class="text_exposed_show">ru wakati akijadiliana na Bodi ya Madaktari wa Muhimbili juu ya hali ya mgonjwa yule.<br />
<br />
Hospitali ya Muhimbili ndiyo iliyokuwa kubwa zaidi nchini Tanzania, hivyo kumtafutia rufaa kulimaanisha kumpeleka nje ya nchi kwenye hospitali bora zaidi. Wakati madaktari wakijadiliana, baba na mama yake Linna nao walikuwa wakifikiria suala hilo hilo.<br />
“Tangu tumlete mwanangu hapa hospitali sioni mabadiliko yoyote, mume wangu tusipochukua uamuzi wa haraka tutampoteza mtoto huku tunashuhudia.”<br />
<br />
“Ni kweli mke wangu, lazima tufanye jambo haraka. Hata kama tutalazimika kuuza kila tulichonacho ilimradi mtoto wetu akatibiwe mimi niko tayari,” aliongea baba yake Linna huku akijifuta machozi. Japokuwa alikuwa ni mwanaume na baba wa familia, hali ya mwanaye ilimfanya ashindwe kuyazuia machozi. Ikawa kila mmoja anajifuta machozi kutokana na hali aliyokuwa nayo Linna.<br />
<br />
Muda mfupi baadaye waliitwa kwenye chumba cha Daktari Mafuru na kuelezwa kile madaktari walichoona kinafaa.<br />
“Tumependekeza mkajaribu kwenye Hospitali ya Johannesburg Trauma Centre, pale huduma zao ni za hali ya juu hasa kwa wagonjwa waliopatwa na majanga kama hili lililomkumba binti yenu. Mungu atawasaidia na naamini atapona ingawa hataweza kuwa kama alivyokuwa kabla ya kupatwa na matatizo.<br />
<br />
Bila kupoteza muda, madaktari wa Muhimbili wakiongozwa na Dokta Mafuru walianza kufanya mawasiliano na wenzao wa Johannesburg Trauma Centre. Baba yake Linna alishughulikia taratibu za uhamiaji, akafuatilia vibali ubalozini na hatimaye kila kitu kikawa tayari.<br />
<br />
Kwa kutumia ndege maalum iliyokodiwa, Linna akasafirishwa hadi jijini Johannesburg sambamba na wazazi wake. Ndege iliyowabeba ilipotua nchini humo, tayari gari la wagonjwa (ambulance) kutoka kwenye hospitali ile lilikuwa likiwasubiri uwanja wa ndege. Linna akashushwa kwenye ndege na kuingizwa moja kwa moja kwenye ambulance, safari ya hospitalini ikaanza.<br />
<br />
Alipofikishwa Johannesburg Trauma Center, alipitishwa mpaka chumba cha wagonjwa mahututi ambapo alianza kutibiwa haraka. Kitu cha kwanza ilikuwa ni kumuunganisha na mashine ya kusukuma hewa ya Oksijeni iliyomsaidia kupumua.<br />
<br />
“She has been dehydrated! Her body is running a severe shortage of water and mineral salt. We need to hydrate her first before we proceed.”<br />
(Amepungukiwa na maji mwilini. Mwili wake una upungufu mkubwa wa maji na madini ya chumvi. Tunapaswa kumuongezea kwanza kabla ya kuendelea) Daktari Amstrong Reymann, mkuu wa kitengo cha majanga ya moto hospitalini pale alikuwa akitoa maelekezo kwa madaktari wenzake. Muda mfupi baadaye Linna akatundikiwa dripu ya maji na chumvi, huku akipakwa dawa za kuua wadudu (Antibiotics) mwili mzima.<br />
<br />
Kwa kipindi hicho chote, Linna alikuwa amelala usingizi wa kifo, akiwa haelewi chochote kilichokuwa kinaendelea kwenye ulimwengu wa kawaida.<br />
Baada ya dripu karibu sita kutiririka kwa kasi mishipani mwa Linna, mapigo yake ya moyo yalianza kuongezeka taratibu. Madaktari wakawa wanapishana kwenye kitanda chake kuhakikisha mgonjwa huyo anapona.<br />
<br />
Huduma bora za kiwango cha juu ilikuwa ni miongoni mwa sifa zilizoitangaza hospitali ile dunia nzima. Kila aliyewahi kutibiwa pale, hakuacha kusifia huduma bora kabisa za afya. Hali ile iliwapa matumaini wazazi wa Linna, wakapata moyo kuwa mtoto wao anaweza kupona ingawa hawakujua kama atarudia hali yake kama ya zamani.<br />
<br />
Baada ya mapigo ya moyo, kiwango cha maji na chumvi mwilini kuanza kuridhisha, Dokta Amstrong Reymann alishauriana na madaktari wenzake namna ya kuifanyia marekebisho ngozi ya Linna iliyokuwa imeharibika vibaya mwili mzima.<br />
“We need to implant her body with the modern skin grafting method, at least we can minimize the damage.”<br />
<br />
(Tunatakiwa kupandikiza ngozi mpya juu ya mwili wake kwa kutumia mbinu ya kisasa ya upandikizwaji wa ngozi, angalau tutapunguza madhara mwilini mwake)<br />
Kilichofuatia ilikuwa ni utekelezaji lakini kilichowakwamisha ikawa ni mahali pa kuipata ngozi ambayo ingetumika kwa zoezi lile.<br />
<br />
Mwili wote wa Linna ulikuwa hautamaniki na hakukuwa na sehemu ambayo ngozi yake haikuungua. Baada ya madaktari kukwama, waliwaita wazazi wake na kuwaeleza hali halisi. Suluhisho pekee lililoonekana kufaa ilikuwa ni wazazi wake kukubali kupimwa ngozi zao na kama zingeendana na mtoto wao, wangekatwa ili kumsaidia Linna.<br />
<br />
Waliingizwa maabara ambapo vipimo kadhaa vya ngozi vilichukuliwa. Majibu yalipotoka, wote walionekana kuendana na mtoto wao, hivyo zoezi ambalo lilifuatia lilikuwa ni kukata sehemu ya ngozi miilini mwao na kumpandikiza Linna. Wakaambiwa wakasubiri maelekezo nje.<br />
“Mmh! Unajua mke wangu mi naogopa sana. Niliwahi kusikia kuwa wakitaka kukutoa ngozi wanakata makalio.”<br />
<br />
“Baba Linna nawe, huachi woga wako wa kitoto. Hata kama ingekuwa usoni, si unamtolea mwanao? Au unataka afe?”<br />
“Basi mke wangu, nilitaka kukuchangamsha kidogo kwani ulikuwa umepooza sana,” aliongea Baba Linna wakati wakisubiri maelekezo ya daktari.<br />
<br />
Alichokizungumza baba yake Linna kilikuwa kweli kwani daktari Amstrong alipowaita ofisini kwake aliwaeleza kuwa kama watakubali, ngozi ya kwenye makalio yao ndiyo itakayokatwa kwa ajili ya kuipandikiza kwenye mwili wa Linna. Waliangaliana machoni kwa muda kisha wakatabasamu, kwa pamoja wakatingisha vichwa vyao kuonesha kuwa wako tayari.<br />
<br />
Kilichofuatia ikawa ni kuingizwa chumba cha upasuaji, mmoja baada ya mwingine. Wakakatwa ngozi kisha Linna akaanza kufanyiwa ‘skin grafting’. Baada ya baba yake kumaliza kufanyiwa zoezi lile, mama yake naye aliingizwa maabara. Matibabu kwa Linna yaliendelea na angalau akaanza kuonesha matumaini ya kupona ingawa bado alikuwa hajarejewa na fahamu zake.<br />
<br />
Licha ya wote kujitolea ngozi kwa ajili ya mtoto wao, bado haikutosha kuufunika mwili wote wa Linna. Ikabidi taratibu zifanyike za kuwaita ndugu zao wengine waliokuwa Tanzania kwa ajili ya kwenda kujitolea kuokoa maisha ya Linna.<br />
<br />
Ndugu saba wa ukoo wa akina Linna wakasafirishwa mpaka Afrika Kusini. Walipoenda kupimwa damu na ngozi zao, watano kati yao walionekana kuendana na Linna. Wakaingizwa maabara na kufanyiwa kama wenzao. Angalau ngozi ikatosha kufunika maeneo yote muhimu.<br />
Madaktari walihakikisha kuwa ngozi waliyoibandika mwilini mwa Linna inajishikiza vizuri na kuungana na mwili wake. Wakawa wanampa dawa nyingi za kuua wadudu na kulainisha ngozi.<br />
<br />
Hilo lilifanikiwa kwani mwezi mmoja tangu zoezi lile lifanyike, hatimaye Linna alirejewa na fahamu zake na kufumbua macho kwa mara ya kwanza. Tofauti na alivyokuwa awali kabla hajapatwa na ajali ile mbaya, upasuaji wa kupandikiza ngozi ulimfanya abadilike kwa kila kitu. Hakuwa Linna yule wa zamani, binti mrembo mwenye tabasamu pana muda wote. Alikuwa mtu mwingine tofauti kabisa, hali iliyomliza mno mama yake.<br />
<br />
Uso ulikuwa na alama nyingi za mishono, kichwa hakikuwa na nywele hata moja. Mwili mzima ulikuwa na viraka kama nguo iliyopelekwa kwa fundi mara nyingi. Hata hivyo wote walimshukuru Mungu kwa miujiza aliyoifanya kwani hakuna ambaye alikuwa na matumaini ya Linna kufumbua macho yake tena.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124809796329945987360"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248f2591290829639839">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP..29.<br />
<br />
Siku ya kwanza tangu Linna arejewe na fahamu ilipita, wazazi wake wakawa bado hawajamwambia nini hasa kilichomsibu. Kumbukumbu zake zilikuwa zikirejea taratibu sana, kiasi kwamba hakukumbuka nini kilichomtokea mpaka akawa pale.<br />
<br />
“Lakini kwani hapa ni wapi? Mbona hamtaki kuniambia ukweli?”<br />
<span class="text_exposed_show"> Baba na mama yake walitazamana kwa muda kama wanaoulizana wamwambie au la. Wakapeana ishara ambayo waliielewa wenyewe kisha mama yake akaanza kumweleza.<br />
“Hapa ni hospitali mwanangu, pole kwa yote yaliyokupata. Tunamshukuru Mungu kwa kukulinda mpaka leo.”<br />
<br />
“Kwani nini kilinipata mpaka nikaletwa hapa?” Alizidi kuhoji Linna lakini hakuna aliyemjibu.<br />
“Nataka kwenda ‘toilet’!”<br />
“Utaweza kusimama kweli, ngoja tumwambie nesi aje atusaidie kukuinua.”<br />
“Mbona naweza kuinuka mwenyewe,” Linna aliongea huku akijivuta pale kitandani na kusimama.<br />
<br />
Kwa kuwa alishatolewa dripu na ile mashine ya kusukuma Oksijeni aliyokuwa amefungiwa, haikumuwia vigumu kusimama. Mama yake akamsaidia kushuka kitandani na wakamshikilia huku na huku, wakampeleka chooni. <br />
<br />
Wakati wanaelekea chooni, walipofika sehemu iliyokuwa na vioo vikubwa ukutani, Linna alisimama kwa muda. Akawa ni kama anajishangaa kupitia vile vioo kwani tangu alipopatwa na masaibu yale, hakuwahi kujiangalia jinsi alivyo.<br />
<br />
“Yule ni nani?” Alinyoosha kidole kujionesha mwenyewe kwenye kioo. Baba na mama yake walitazamana tena, machozi yakawa yanawalengalenga. Mama yake alimkumbatia na kumwambia kuwa yule aliyekuwa anamuulizia ni yeye mwenyewe.<br />
<br />
“Mbona nimebadilika hivi? Noo! Siyo mimi, labda ni mtu mwingine,” aliongea Linna huku akianza kulia. Alikuwa amebadilika mno. Ilibidi wazazi wake wafanye kazi ya ziada mpaka akatulia na kukubaliana na matokeo.<br />
<br />
Walimfikisha msalani, akamaliza haja zake kisha wakamrudisha wodini. Alipofika tena eneo lile lenye vioo vikubwa, alizidi kujishangaa huku safari hii akishindwa kujizuia kulia.<br />
“Mi nafikiri tukamuite daktari kwa ajili ya kumjenga upya kisaikolojia ili akubaliane na hali halisi, vinginevyo atapata shida sana kuyakubali mabadiliko makubwa aliyonayo.”<br />
<br />
“Ni sawa, lakini kabla ya kumuita daktari hata sisi wenyewe tunaweza kumsaidia. Nafikiri huu ni muda muafaka wa kumueleza nini kilichompata mpaka akawa hivi.”<br />
“Unafikiri itasaidia?”<br />
“Yaah! Itasaidia sana.”<br />
<br />
Baada ya kuteta pembeni kwa muda mfupi, baba na mama Linna walirejea kwenye kitanda alichokuwa amelala mtoto wao aliyekuwa anaendelea kulia kwa uchungu, wakaanza kumbembeleza na kumweleza kila kitu kilichomtokea. Ni hapo ndipo kumbukumbu zake zilipomrudia vizuri. Alikumbuka siku aliyopata ajali mbaya kisha gari lake kulipuka baada ya kugonga pampu ya mafuta.<br />
<br />
“Mamaa nakufa! Niokoeee!” Alipiga kelele Linna kumbukumbu za jinsi ajali ilivyotokea zilipomrudia.<br />
“Tulia Linna, mshukuru Mungu kwamba mpaka muda huu uko hai,” aliongea mama yake huku akimshika mwanaye na kumtuliza pale kitandani.<br />
<br />
“Mamaa, nilimuona mwanamke akivuka barabara akiwa amembeba mtoto, nilipojaribu kumkwepa ndiyo gari likanishinda,” aliongea Linna huku akitetemeka mwili mzima. Zilikuwa ni kumbukumbu mbaya ambazo ama kwa hakika zilimfanya atie huruma.<br />
Maneno yale aliyoyasema kuwa alimuona mwanamke akivuka barabara akiwa amembeba mtoto, yaliwafanya wazazi wa Linna kuanza kuhusinisha ajali ya mtoto wao na ya mwanafunzi mwenzake, Monalisa.<br />
<br />
“Mbona Monalisa na yeye alipopata ajali alisema aliona mwanamke akivuka barabara akiwa amembeba mtoto?”<br />
“Lazima kuna jambo hapa! Siyo bure.”<br />
“Inawezekana kuna siri nzito iliyojificha nyuma ya pazia. Mimi si mwepesi wa kuamini nguvu za kishirikina, lakini katika hili nahisi zinahusika.”<br />
<br />
“Tumwachie Mungu, cha msingi mtoto wetu ameanza kupona.”<br />
Daktari Amstrong aliingia wodini na kukuta mama na baba Linna wanambembeleza mtoto wao. Alitambua matatizo ya kisaikolojia yanayoambatana na tatizo kama lile lililokuwa limemsibu Linna. Aliwaomba wazazi wake wamfuate ofisini kwa ajili ya maelekezo zaidi juu ya tiba ya Linna.<br />
<br />
“Japokuwa mgonjwa amerejewa na fahamu, bado tuna kazi kubwa ya kuurekebisha mwili wake. Hii ni hatua ya awali tu kwani kuna zaidi ya oparesheni nyingine 50 ambazo inabidi tumfanyie ili angalau kurejesha mwonekano wake wa awali.”<br />
“Oparesheni hamsini? Zote hizo za nini?”<br />
“Bado tunahitaji kurekebisha viungo kama macho, pua, midomo, masikio na vingine vingi, ajali ya moto ilimharibu kabisa.<br />
<br />
*** <br />
Hali ya Monalisa ilizidi kuwa mbaya licha ya kusafirishwa hadi nchini Uingereza. Kauli ya mwisho aliyoitoa ilikuwa ni kuwaomba wazazi wake wamkutanishe na Phillip kabla hajafa.<br />
Wazazi wake walimhakikishia kuwa watatimiza ombi lake. Kilichofuatia baada ya hapo ikawa ni baba yake Monalisa kusafiri hadi jijini Dar es Salaam kwa lengo la kumfuata Phillip.<br />
<br />
Alipowasili, alienda mpaka kwenye uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuomba kuonana na Phillip.<br />
“Mimi ni baba yake Monalisa! Amenituma nije kuonana na wewe na kukufikishia ujumbe kuwa anahitaji kuonana na wewe.”<br />
“Sasa atanionaje wakati yuko hospitali, tena Uingereza?”<br />
“Usiwe na wasiwasi, familia yangu itakugharamia usafiri na malazi, cha msingi ni utayari wako.”<br />
<br />
“Mimi niko tayari mzee wangu, hata sasa hivi!””Ok, safi kijana! Sasa jiandae, ngoja mimi nifuatilie taratibu zote za vibali vya usafiri. Naomba ukapige ‘passport’ na unipe kitambulisho chako, kesho mambo yote yatakuwa tayari,” aliongea baba Monalisa kisha akaagana na Phillip.<br />
<br />
Baada ya kuachana naye, alitamani Zamaradi amtokee na kumuombea tena msamaha Monalisa kwani kwa hali ilivyokuwa, uwezekano wa kupona ulikuwa mdogo. Phillip alibaki na msongo mkubwa wa mawazo juu ya hali ya Monalisa. Aliumia kuona mtu asiye na hatia akiangamia kwa sababu ya wivu wa Zamaradi.<br />
<br />
Alimuomba Mungu wake ampe ujasiri kwenye safari ile ngumu ya kwenda kuonana na Monalisa. Alijikuta machozi yakimlengalenga. <br />
Ndege ya Shirika la British Airways ilikuwa ikiiacha ardhi ya Tanzania na kupaa kuelekea jijini London, Uingereza. Phillip na baba yake Monalisa walikuwa ni miongoni mwa abiria waliokuwa ndani ya ndege ile. Hakuna aliyemsemesha mwenzake japo walikaa siti zilizokaribiana.<br />
<br />
Masaa machache baadaye, ndege ile ilikuwa ikitua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Heathrow jijini London. Abiria wote waliteremka, Phillip akiwa miongoni mwao sambamba na baba yake Monalisa.<br />
Hawakuwa na muda wa kupoteza. Waliunganisha moja kwa moja mpaka hospitali. Walipofika, baba yake Monalisa alimuomba Phillip amsubiri sehemu ya mapokezi kwa ajili ya kwenda kumuandaa mgonjwa.<br />
<br />
Katika hali ambayo hakuitegemea, Phillip alishtuka kumuona baba yake Monalisa akitoka wodini huku amejiziba uso wake kwa kitambaa. Alipomchunguza vizuri aligundua kuwa alikuwa akilia.<br />
“Mungu wangu! Nini tena?” aliongea Phillip na kuinuka kwa kasi kumfuata baba Monalisa.<br />
“Mzee kwani vipi?”<br />
<br />
“Hatunaye tena! Monalisa ametangulia mbele za haki?”<br />
“Niniii?” Phillip akiwa katika hali ya kutoamini kile alichokisikia, alishangaa mwanamke wa makamo akitoka wodi ile ile huku akilia na kuja kumkumbatia baba yake Monalisa. Alimtambua kuwa ni mama yake Monalisa.<br />
<br />
“Pigo kubwa kiasi gani? Yaani safari yote kutoka Dar es Salaam kumbe nakuja kuiona maiti yako? Kwa nini usingesubiri japo nikuone mara ya mwisho Monalisa! Eeeh Mungu, mpumzishe kwa amani!” aliongea Phillip huku akilia kilio cha kwikwi. Hakuna aliyekuwa na uwezo wa kumtuliza mwenzake, ikawa ni maombolezo wakati mwili wa Monalisa ukitolewa wodini na kupelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012494e71bd97860622054">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.30<br />
<br />
Lilikuwa ni tukio la kusikitisha mno, Phillip alilia kuzidi hata wazazi wa Monalisa. Moyoni mwake aligundua wazi kuwa hata yeye alimpenda msichana huyo kupita kiasi. Lakini sasa alikuwa amekufa kabla hawajaongea chochote, safari yake kuja Uingereza haikuwa na matunda. Alimlilia Monalisa kwa nguvu zake zote, hasa alipokumbuka namna walivyoishi vizuri chuoni. <br />
<br />
H<span class="text_exposed_show">asira zake zote zilielekezwa kwa Zamaradi, alimchukia, tena sana. Hakutaka tena kuwa naye kwa sababu alikuwa muuaji, aliyemuua Monalisa bila hatia na kumjeruhi Linna kwa moto ambaye pia Phillip aliamini, kwa hali aliyokuwa nayo, asingeweza kupona. Hakuwa na la kufanya zaidi ya kufikiria namna ambayo angeweza kujinasua kwa mwanamke huyo hatari.<br />
<br />
“Nataka kuishi maisha ya ukweli, nataka kuishi maisha halisi, sitaki tena maisha ya chini ya maji, lakini nitajitenganisha nayo vipi? Zamaradi ataniua,” Phillip alijiuliza bila kupata jibu.<br />
<br />
Taratibu za kuusafirisha mwili wa Monalisa kutoka Uingereza zilishughulikiwa na Watanzania waishio nchini humo kwa kushirikiana na ubalozi wao, wakati huo Phillip akiwa amechukuliwa chumba kwenye Hoteli ya Conrad ambako pia wazazi wa Monalisa waliishi.<br />
<br />
Hakuwa na jingine la kufanya akiwa chumbani isipokuwa kulia, hakulala wala kula chochote mpaka siku iliyofuata ambapo walipanda ndege na kusafiri watatu na mwili wa Monalisa hadi uwanja wa ndege, Dar es Salaam.<br />
<br />
Maelfu ya watu walikuwepo uwanjani, wengi wakiwa ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, marafiki na majirani wa familia ya kina Monalisa maeneo ya Upanga. Vilio vilisikika kwa mbali, wanafunzi wakimlilia Monalisa. Alipotoka nje ya uwanja, Phillip alikumbatiwa na Tyra ambaye alimchukua hadi kwenye maegesho ya magari, akafungua mlango na kumpakia.<br />
<br />
Baadaye msafara mrefu wa magari uliondoka uwanjani kuelekea Upanga, Phillip na Tyra wakiwa peke yao ndani ya gari, muda wote Tyra akimfariji na kumwambia asijali kwa yaliyotokea. Kwake kifo cha Monalisa kilimuumiza lakini pia ilikuwa nafasi ya yeye kumpata Phillip kwa urahisi hasa baada ya Linna kuungua vibaya kwa moto, alihisi Phillip alikuwa amemaanishwa kwa ajili yake.<br />
<br />
“Usilie Phillip.”<br />
“Sawa lakini inaniuma.”<br />
“Najua, ulikuwa unampenda sana Monalisa na pia Linna.”<br />
“Siyo hivyo, ananiuma kwa sababu amekufa akiwa bado kijana sana. Isitoshe ninajua kilichosababisha kifo chake.”<br />
<br />
“Si ni ajali au kuna kitu kingine?”<br />
“Siwezi kukuambia, niache tu nilie.”<br />
“Usiumie sana, mimi nipo, nitakufariji.”<br />
“Sawa. Una habari gani za Linna?”<br />
<br />
“Hali yake bado ni mbaya, amefanyiwa tena oparesheni nyingine jana. Ameharibika sana sura, havutii tena, sidhani kama kuna mtu atakuja kumpenda Linna kabisa.”<br />
“Hayo anayajua Mungu, hujafa hujaumbika. Pia yeye halikuwa kosa lake, najua kilichosababisha akaungua kwa moto.”<br />
<br />
“Ni nini? Maana nasikia maneno yanasambaa kwamba kuna mkono wa mtu, eti walimuona mwanamke mwenye mtoto katikati ya barabara kabla ya ajali kutokea.”<br />
Phillip hakujibu kitu tena, hakuwa tayari kujadiliana juu ya Zamaradi. <br />
<br />
Gari likazidi kusonga mbele mpaka wakafika nyumbani kwa kina Monalisa maeneo ya Upanga, ambako pia kulikuwa na mamia ya watu wakisubiri. Ulikuwa ni msiba mkubwa tena wa kifahari uliojaza watu wote maarufu na matajiri sababu baba yake Monalisa alikuwa miongoni mwao.<br />
<br />
“Naweza kubaki humu humu ndani ya gari?” Phillip alimuuliza Tyra.<br />
“Hakuna tatizo, tunaweza kubaki tu humu humu ndani mpaka baadaye.”<br />
“Hauna safari yoyote?”<br />
“Sina.”<br />
<br />
Phillip alilaza kiti naye kujilaza akiwa amefumba macho. Mawazoni aliendelea kumfikiria Monalisa, akahamia kwa Linna na baadaye kuendelea na Zamaradi. Roho ilimuuma sana hasa alipogundua kwamba hata Tyra pia kama angediriki kumshawishi au kumlazimisha kufanya tendo la mapenzi, pia angepatwa na ajali mbaya na hata kufa. Hapo Phillip akafumbua macho na kumuangalia Tyra.<br />
<br />
“Mbona unaniangalia kwa jicho hilo?”<br />
“Nakusikitikia.”<br />
“Kwa nini?”<br />
“Tyra!”<br />
“Bee!”<br />
<br />
“Naomba tu uniache, usije ukajaribu kunilazimisha kuwa mpenzi wako, utapata matatizo.”<br />
“Matatizo gani?”<br />
“Huoni yaliyowakuta wenzako?”<br />
“Toka hapa… Unataka kunitia woga? Hakuna chochote, hizi ni ajali za kawaida, usitake kujichukulia umaarufu kwamba wewe ndiye umezisababisha.”<br />
<br />
“Sijazisababisha mimi lakini yupo aliyezisababisha.”<br />
“Nani?”<br />
“Siwezi kukutajia ila fuata maneno yangu.”<br />
“Sitaki.”<br />
“Shauri yako.”<br />
<br />
Hivyo ndivyo ilivyokuwa, wote wawili walilala ndani ya gari, saa kumi na moja alfajiri, Phillip akiwa katikati ya usingizi alishitukia mwili wake unapapaswa, mwanzoni alidhani ni ndoto kwani hakutambua mahali alipokuwa lakini akili yake ilipokaa sawa, tayari Tyra alishamfungua zipu ya suruali yake na kuzitoa sehemu zake za siri nje.<br />
<br />
“Tyra! Utakufa,” alisema Phillip kwa sauti huku akinyanyuka.<br />
“Nakupenda Phillip, wewe ni haki yangu ndiyo maana akina Monalisa na Linna wamenipisha. Tafadhali nipe haki yangu,” aliongea Tyra kwa sauti ya upole uso wake ukiwa umejawa na aibu.<br />
<br />
“Haiwezekani, nakupenda mno ndiyo maana nakataa.”<br />
Tyra hakukubali, akaanza kulia huku Phillip akimuangalia kwa jicho la huruma, kwani alielewa ambacho kingefuata kama angeruhusu jambo hilo litendeke. Walishinda msibani Phillip akihuzunika kwa kifo cha Monalisa, huku Tyra akihuzunikia kitendo cha Phillip kumnyima penzi.<br />
<br />
“Unaweza kunipeleka bwenini nikabadili nguo?” Phillip alimwambia Tyra ilipotimia saa kumi jioni.<br />
“Hakuna shida.”<br />
“Twende basi.”<br />
<br />
Wakaondoka mpaka chuo kikuu ambako Phillip alishuka na wote wawili wakapandisha hadi ghorofa ya tatu kilipokuwa chumba chake, katika hali ambayo hakuitarajia, Phillip alibadilisha mawazo na kuamua Tyra aondoke ili yeye apumzike sababu alisikia usingizi, tena alikuwa mkali wakati akiongea maneno hayo.<br />
“Nikufuate baadaye?”<br />
“Nitakuja mwenyewe.”<br />
<br />
Tyra hakuwa na la kufanya isipokuwa kushusha ngazi hadi kwenye gari lake ambako alipanda, kuwasha na kuondoka kwa kasi kuelekea Upanga, akiwa amepanga kupitia njia ya Ubungo, Manzese, Magomeni, Faya na baadaye kuingia Upanga msibani kuungana na wanafunzi wenzake.<br />
<br />
***<br />
Zamaradi aliyashuhudia yote yaliyotokea ndani ya gari na hasira kali kumpanda, ilikuwa ni zamu ya Tyra kufa, tena alidhamiria kumuua pale pale ambapo ajali ingetokea. Baada ya hapo wabaya wake wote wangekuwa wamekwisha. Phillip akiwa usingizini alimtokea na kumpa taarifa ya jambo alilokuwa anakwenda kulifanya, akamsihi asifanye hivyo badala yake amsamehe Tyra.<br />
<br />
“Tena ukizidi kunizuia hata wewe nitakuua.”<br />
“Usifanye hivyo, hawana hatia, ni hisia za kimapenzi zinawasumbua, cha muhimu ni kwamba mimi nina msimamo.”<br />
“Haiwezekani. Lazima Tyra afe.”<br />
<br />
Tyra aliendesha gari lake kwa kasi akiwa hajui Zamaradi alikuwa akimsubiri kwa hamu kubwa kwenye taa za kuongozea magari za Faya. Kabla hajakata kona kuelekea Upanga, alipanga kuzipasua tairi zake zote za mbele na kisha kulipindua gari mara tano na hatimaye ligongane na gari jingine, huo ndio uwe mwisho wa Tyra.<br />
Alishuhudia gari likishuka maeneo ya Magomeni kuelekea Jangwani, akajiandaa kwa ajili ya kazi.<br />
<br />
Je, nini kitamtokea Tyra? TUKUTANE KESHO HAPA HAPA UNLIMITED SWAGGAZZ......USIKU MWEMA NAWAPENDA NYOOOTE!!!!</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501248097a5e78e41843464"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012494e666242672482726">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.31<br />
<br />
Jini Zamaradi, mke wa Phillip katika ulimwengu usioonekana amedhamiria kuwaua wasichana watatu (Tyra, Monalisa na Linna) ambao ni wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambako pia Phillip anasoma. Hakuna anayejua siri ya Phillip kuwa ni mume wa mtu kwenye ulimwengu usiooonekana, wasichana hao wanamuona ni mvulana mzuri na wanapanga kila mbinu ili waweze k<span class="text_exposed_show">umpata kimapenzi, hapo ndipo wakakutana na hasira ya Zamaradi.<br />
<br />
Kwanza alikuwa ni Monalisa, akamsababishia ajali mbaya ya gari iliyosababisha msichana huyo kupooza baada ya kuumia ubongo. Hivi sasa ameaga dunia na kurejeshwa nchini kutoka Uingereza kwa mazishi.<br />
<br />
Wa pili alikuwa Linna ambaye pia Zamaradi alimsababishia ajali mbaya ya gari iliyomfanya msichana huyo kuungua vibaya ndani ya gari lake alipogonga pampu ya mafuta ya petroli kwenye kituo cha Bonjour kilichoko njia panda ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam karibu na eneo liitwalo Mlimani City.<br />
<br />
Hivi sasa msichana huyu aliyeungua vibaya mwili wake yupo nchini Afrika Kusini akifanyiwa upasuaji kurekebisha mwili wake, sura imebadilika kabisa kwa sababu ya moto na Zamaradi anafurahia jambo hilo lakini Phillip anaumizwa sana kwani anajua kinachoendelea.<br />
<br />
Hawa wakiwa na hali hizo, Tyra pamoja na maonyo yote aliyopewa na Phillip anamfungua kijana huyo zipu ya suruali yake kwa lengo la kufanya naye mapenzi ndani ya gari lake, jambo hili lilimuudhi Zamaradi ambaye yupo kwenye taa za kuendeshea magari za Faya akimsubiri Tyra afike, apasue tairi za mbele za gari lake kisha kulipindua, huo ndiyo uwe mwisho wa msichana huyo mrembo. <br />
<br />
Tyra yupo maeneo ya Jangwani kwenye Barabara ya Morogoro, amebakiza mita chache tu afike Faya ambako jini Zamaradi anamsubiri kwa hamu kubwa akiwa amedhamiria kuing’oa roho yake bila huruma.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
“He is so handsome, I can’t resist him.” (Ni mzuri mno siwezi kujizuia nisimpende.) Tyra aliwaza akiwa ndani ya gari lake dogo aina ya Volkswagen New Model, muziki laini ukiporomoshwa na Celine Dion kupitia kwenye spika zilizoko kwenye mlango.<br />
<br />
Hakika msichana huyu alikuwa na kila kitu maishani mwake, kuanzia sura, umbile na utajiri wa wazazi wake. Simu yake haikutulia, wanaume wakimpigia simu kumtaka mapenzi na wote aliwakatalia, hakuwa na mpenzi kabisa ndani na nje ya Tanzania baada ya kuachana na mpenzi wake wa kwanza miaka mitano kabla, sasa alimtaka Phillip kwa gharama yoyote.<br />
<br />
Kwa kuwatazama watu hawa wawili na historia za maisha yao, utajiri wa familia zao, Basi msichana kama Tyra hakutakiwa kabisa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Phillip hata kama alikuwa na sura nzuri kiasi gani, lakini sasa alikuwa amenasa, akili yake haikufanya kazi sawasawa, taswira ya Phillip ilionekana kichwani mwake kila alikokwenda, hakuwa na nafuu yoyote hata alipolala usingizi, Phillip alionekana katika ndoto. <br />
<br />
Alishangazwa na umati mkubwa wa watu waliokusanyika kwenye viwanja vya Jangwani huku wengine wengi wakizidi kumiminika kuelekea kwenye viwanja hivyo, bila kutarajia akajikuta akishusha kioo cha gari lake na kuanza kusikiliza spika zikitangaza kwa sauti ya juu kutoka kwenye viwanja hivyo, mguu wake wa kulia ukahama kulia na kuja katikati, gari likapunguza mwendo.<br />
<br />
Najua mnayo masumbuko mengi maishani mwenu, wengine mna kila kitu lakini bado mnateseka, Yesu anawaita ili aje awatue mizigo yenu. Imetosha kusumbuka, iwe kwa magonjwa au maumivu ya moyo sababu kuna watu wamekutenda vibaya, Mungu wetu analijua hilo na sasa anataka kukuweka huru… Njoo kwake leo, hutajuta…<br />
<br />
Tyra aliyasikia maneno hayo kupitia masikio yake yote mawili, bila kupanga akakata kona kuelekea kwenye viwanja hivyo, hata siku moja hakuwahi kufika hapo kusikiliza neno. Hakuwa mtu wa kanisa sana, ni kweli alimwamini Mungu na alikuwa Mkristo lakini si mhudhuriaji wa ibada, siku zote alikuwa mtu wa starehe na kuhudhuria kumbi za starehe huku akiwacheka wanafunzi wenzake walioonekana wacha Mungu, akiwaita wanafiki.<br />
<br />
Aliegesha gari lake kando, akashuka na kujichanganya katikati ya maelfu ya watu waliokuwa wamekusanyika kwenye viwanja hivyo kumsikiliza Mhubiri wa Neno la Mungu, Mchungaji Moses Lubala kutoka Kanisa la Word Alive la jijini Dar es Salaam aliyekuwa akiendesha mkutano katika viwanja hivyo. <br />
<br />
Tyra alisimama na kuendelea kusikiliza mafundisho ya Mchungaji huyo, akiwataka watu wote kugeuka na kuacha njia zao mbaya, kwamba Yesu alikuwa amekaribia kurudi kuja kutoa hukumu ya kutupwa katika ziwa la moto, maneno hayo yakaingia moyoni mwa Tyra moja kwa moja, akiwa amefumba macho akaanza kuyapitia upya maisha yake, akajiona mwenye dhambi aliyestahili msamaha wa Mungu. Machozi yakambubujika, kwa mara ya kwanza maishani mwake akajikuta akitamani kumfahamu Mungu zaidi ya alivyokuwa akisikia kutoka kwa wazazi wake.<br />
<br />
“Wangapi wako tayari kukabidhi maisha yao kwa Yesu jioni ya leo ili aweze kuwabadilisha na kuwafanya wapya, ili hatimaye waweze kuurithi ufalme wa Mungu na pia kulindwa na mwovu Shetani ambaye kazi yake ni kuharibu… Kama wapo naomba wapite mbele.”<br />
<br />
Mtu wa kwanza kufika mbele ya jukwaa alikuwa ni Tyra, machozi yakimbubujika na mwili wake kutetemeka. Alikuwa amejisikia mwilini mwake hali ambayo hata siku moja haikuwahi kumtokea, akapiga magoti na kusujudu mbele ya jukwaa huku watu wengine wakizidi kumiminika.<br />
<br />
Mchungaji akawaongoza watu hao sala ya toba ili Mungu apate kuwasamehe dhambi zao, alipomaliza aliwaruhusu kuondoka lakini Tyra hakufanya hivyo, akaomba kuongea na Mchungaji baada ya mkutano kumalizika. Hicho ndicho kilichotokea, akamweleza mtumishi huyo wa Mungu kila kitu kuhusu maisha yake na hasa alivyoteswa na mapenzi ya Phillip, Mchungaji hakuwa na cha kufanya zaidi ya kumwombea ili roho hiyo imtoke.<br />
<br />
“Mchungaji naomba twende nyumbani ukawaone wazazi wangu!”<br />
“Unaishi wapi binti?”<br />
“Upanga.”<br />
“Nisubiri basi tumalize shughuli zote tutaongozana.”<br />
“Asante mtumishi.”<br />
<br />
Saa moja na nusu ndipo Tyra alimuongoza Mchungaji hadi kwenye gari lake, wote wawili wakapanda na kuondoka. Walipoingia tu barabarani, Zamaradi ambaye bado alikuwa hajaondoka eneo hilo alijiweka tayari kwa mashambulizi, hasira yake ilikuwa palepale na alitamani kumuondoa Tyra duniani ndipo kazi yake ikamilike. Gari lilipofika, alinyosha mkono wake ambao ulitoa kitu kama moto uliokwenda moja kwa moka kwenye gari kwa lengo la kupasua tairi, cha kushangaza tofauti na siku nyingine zote moto huo uligeuka na kuanza kumrudia yeye, ukampiga pamoja na mwanaye wote wakaanguka chini.<br />
<br />
“Mh!” Tyra aliguna.<br />
“Vipi binti?”<br />
“Gari imetingishika.”<br />
“Twende, nimekwishaelewa kilichokuwa kinaendelea, roho wa kifo alikuwa hapa akikusubiri wewe lakini Mungu amekunusuru.”<br />
“Kweli?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Kwani imekuwaje?”<br />
“Nimemwona mwanamke mmoja ana mtoto, akanyosha mkono wake ambao ulitoa nguvu za giza lakini nikaziamuru zimrudie yeye.”<br />
“Mh! Mwanamke na mtoto tena, inawezekana akawa ni yuleyule aliyewatokea rafiki zangu wawili, Monalisa na Linna, magari yao yakapinduka. Hivi sasa ninavyoongea na wewe Mchungaji Monalisa ni marehemu, Linna ni majeruhi wa moto aliyeungulia ndani ya gari lake…”<br />
<br />
Waliongea mengi Mchungaji akimsimulia Tyra juu ya mapepo na namna yanavyofanya kazi na kwamba kinga pekee ilikuwa ndani ya Mungu, ambako watu wote wamchao hawakuwa na hofu ya mapepo hata kidogo. Tyra akamuahidi Mchungaji kumcha Mungu kwa uwezo wake wote tangu siku hiyo.<br />
<br />
Kilichofanyika nyumbani kilikuwa ni utambulisho wa Mchungaji kwa wazazi wa Tyra ambao kwanza walishangaa sana kusikia mtoto wao aliyewahangaisha kwa muda mrefu amempokea Yesu, wakamtaka awe anakwenda kuabudu kanisani kwa Mchungaji Moses Lubala ili azidi kukomaa kiroho.<br />
<br />
Hivyo ndivyo ilivyotokea, kwani baada tu ya mazishi ya Monalisa, Tyra alianza kuhudhuria mafundisho na ibada kwenye kanisa hilo. Chuoni wanafunzi walimshangaa sana kwani tabia yake ilibadilika kabisa, hakuwa na makundi tena na hata hakudiriki usiku kutoka kwenda disko kama ilivyokuwa siku za nyuma.<br />
<br />
Kitu pekee kilichomsumbua akili ni Phillip, pamoja na kuokoka lakini bado alijisikia kumpenda kijana huyo, hiyo ndiyo vita aliyokuwa amebakiza na ilikuwa ngumu sana kupata ushindi. Hata hivyo, aliuahidi moyo wake kupambana mpaka hatua ya mwisho asirejee dhambini, baadhi ya wanafunzi Chuo Kikuu walimcheka na kudai alikuwa akiigiza ulokole, kwamba muda si mrefu angeanguka na kurejea tena kwenye dhambi zake.<br />
<br />
“Umebadilika sana siku hizi, nini siri ya mafanikio yako? Kifo cha Monalisa kimekuumiza sana labda?” Ilikuwa ni sauti ya Phillip alipomfuata kuzungumza naye.<br />
“Hapana. Ni Mungu, ameamua kubadili maisha yangu, nakukaribisha sana kanisani kwetu pale Sinza Mori.”<br />
“Ningependa kufika hapo kanisani ili nione kitu gani kimefanyika, wewe? Wewe Tyra? Ndiyo umekuwa hivi, siyo rahisi kuamini.”<br />
“Karibu.”<br />
<br />
Mazungumzo hayo ndiyo yaliwaunganisha zaidi, tangu siku hiyo wakawa karibu kuliko ilivyotokea baada ya tukio lililotokea ndani ya gari nyumbani kwao na Monalisa wakati wa msiba. Phillip akahudhuria kanisani ambako mafundisho yalimgusa, akakabidhi maisha yake kwa Yesu pia na kusimulia mkasa mzima uliomtokea wa kuoa jini ambaye alizaa naye mtoto na alikuwa na wivu mkubwa uliosababisha kuwashambulia wanawake wote waliompenda, Tyra hakuamini alichokisikia ndani ya ofisi ya Mchungaji, akalia machozi mbele ya Mchungaji.<br />
<br />
“Ndiyo maana nilikuwa nakwambia uniache.Wenzako niliwakataza hawakunielewa, roho inaniuma sana kwa yaliyowapata,” akamwambia Tyra akimpapasa mgongoni.<br />
“Usiwe na wasiwasi Phillip, Zamaradi hutamuona tena akikusumbua, wala mwanao ambaye pia ni jini, tulikutana nao njiani wakimsubiri Tyra, nguvu ya Mungu ikawashughulikia.”<br />
Phillip alilia kwa uchungu, akajisikia huru moyoni mwake. Taratibu akamnyanyua Tyra na kumkumbatia kisha kunong’ona sikioni mwake “I LOVE YOU TYRA, CAN YOU MARRY ME?” (Nakupenda Tyra, unaweza kukubali nikuoe?)<br />
<br />
“Oh, my God! I can’t believe this, are you sure?” (Oh, Mungu wangu! Siwezi kuamini hivi, una uhakika?) Tyra aliuliza maswali mfululizo akilia kwa furaha.<br />
“Absolutely! Our Pastor is my witness.” (Kabisa. Mchungaji ni shahidi wangu.)<br />
“Yes, I can marry you Phillip, I love you too.” (Ndiyo, niko tayari unioe, nakupenda pia.)<br />
<br />
Wiki moja baadaye walivalishana pete ya uchumba kanisani mbele ya waumini, ndugu na jamaa na kubatizwa, Tyra akabadilisha jina na kuitwa Genevieve, huku Phillip akiendelea na jina lile lile. Ndoa ilipangwa kufungwa baada ya kumaliza masomo yao, muda wote wakiwa chuoni wangeendelea kuwa wachumba. Mioyo yao ilijaa furaha.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012494e6553c2543556348">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.32<br />
<br />
<br />
Phillip na Tyra ambaye sasa alikuwa akiitwa Genevieve waliendelea na masomo huku kila mtu chuoni pale akiwashangaa. Wengi walikuwa wakimshangaa Genevieve kwani ndani ya muda mfupi tangu alipotangaza kumpokea Mungu, maisha yake yalibadilika sana. Hakuwa tena Genevieve wa kwenda kwenye kumbi za starehe na kuvaa mavazi ya kidunia.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Kila jambo alilifanya kwa upole huku jina la muumba wake likitawala mdomoni mwake. Hali kadhalika, Phillip naye alibadilika sana na sasa akawa mtakatifu kwa kila alichokuwa anakifanya. Japokuwa haikuwa rahisi kwake kuwasahau Zamaradi na mwanaye, alimshukuru Mungu kwa kumfungua kwenye kifungo kilichomtesa siku nyingi maishani mwake. Mawazo, akili na moyo wake alivielekeza kwa Genevieve na aliamini hakuna kitakachowatenganisha zaidi ya kifo.<br />
<br />
Siku zilizidi kusonga huku mapenzi yao yakiwa gumzo kila walikopita. Wapo waliowabeza na kuwaona kama watu waliokuwa wakiigiza ingawa pia wapo waliokuwa wanawaombea mema kwenye maisha yao.<br />
“Hivi mapenzi ya kilokole yanakuwaje?”<br />
“Yanakuwa kama mapenzi mengine, kwa nini unauliza hivyo?”<br />
<br />
“Nauliza kwa sababu nawashangaa sana Phillip na Genevieve, eti wanaigiza mapenzi ya kilokole, ina maana hawajawahi kuduu?”<br />
“Wewe nawe, maswali gani hayo unauliza, kwani hujui amri kumi za Mungu zinavyosema?”<br />
“Sawa najua kuwa Mungu amekataza watu kuvunja amri ya sita, lakini ukiwaangalia Phillip na Genevieve watakuwa hawajahi kukutana kimwili kweli?”<br />
<br />
“Bwana eeeh, hayo maswali kawaulize wenyewe, mi ninachojua ni kuwa haitakiwi wachumba kufanya tendo la ndoa mpaka watakapohalalishwa madhabahuni,” wanafunzi waliokuwa wakifanya ‘discussion ‘chini ya mti mkubwa kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliacha kujadili masomo na sasa wakawa wanawajadili Genevieve na Phillip.<br />
<br />
Kila mmoja alikuwa akiongea lake lakini ukweli walikuwa nao wenyewe. Kwa kutambua kuwa wanafuatiliwa sana na wenzao, Phillip na Genevieve hawakutaka kuingia kwenye skendo yoyote, wakawa wanajitahidi kuishi kwa kufuata maagizo yote ya Mungu. Hawakuacha kusali kila asubuhi, mchana na jioni bila kujali kama ilikuwa Jumapili au la.<br />
Siku zilizidi kuyoyoma na hatimaye wakamaliza chuo na kutimiza ahadi waliyokuwa wamewekeana, wakafunga ndoa na kuwa mume na mke halali.<br />
***<br />
MWAKA MMOJA BAADAYE<br />
“Haya ndiyo maisha niliyokuwa nayaota siku zote za uhai wangu,” aliongea Phillip wakiwa wamepumzika kwenye bustani nzuri za maua na mkewe, Genevieve.<br />
“Unamaanisha nini mume wangu?”<br />
<br />
“Siku zote nilikuwa nikiota kumpata mke mwema ambaye nitaishi naye maisha ya raha mustarehe, unajua mi nimekulia kwenye shida na dhiki sana,” aliongea Phillip huku akijaribu kuvuta kumbukumbu za maisha yake ya utotoni.<br />
<br />
“Jamani mume wangu, Mungu ndiyo anapaswa kushukuriwa kwa yote, najua umepitia mambo mengi magumu tofauti na mimi mkeo, lakini hatimaye ndoa imetuunganisha na sasa tumekuwa mwili mmoja,” aliongea Genevieve na kumbusu mumewe shavuni. Alishatambua kuwa kumbukumbu za maisha ya zamani ya mumewe zilikuwa zikimuumiza, jambo ambalo hakuwa akipenda litokee. Akawa mfariji mkubwa kwake.<br />
<br />
“Nakupenda sana mume wangu, mimi pia nilikuwa naota kumpata mwanaume kama wewe, una kila kitu nilichokuwa nakihitaji,” aliongea Genevieve huku akijilaza kifuani kwa mumewe. Hawakuitana tena majina yao waliyokuwa wanayatumia tangu wakiwa chuoni.<br />
Licha ya maisha ya kifahari waliyokuwa wakiishi, nyumba nzuri ya kifahari waliyoijenga baada ya kuunganisha mishahara yao na magari ya kisasa ya kutembelea, bado walikosa kitu cha muhimu, watoto.<br />
<br />
Mwaka mzima waliokaa ndani ya ndoa haukuwa na mafanikio yoyote, wakaanza kuandamwa tena na walimwengu ambao walikuwa wanawatania kuwa wanamaliza magodoro na kujaza choo.<br />
“Unajua mume wangu mi’ najisikia vibaya sana majirani na ndugu wanavyotudharau na kutunanga eti kwa sababu hatuna mtoto,” aliongea Genevieve huku akilengwa lengwa na machozi.<br />
<br />
“Usiwajali mke wangu, kuzaa ni majaliwa ya Mungu, mara ngapi tumefunga na kusali tukimuomba Mungu atupe mtoto? Naamini ameshasikia maombi yetu, hatupaswi kutilia mashaka ahadi za Mungu wetu,” aliongea Phillip kwa hisia.<br />
“Sawa mume wangu, lakini wakati tunasubiri majibu ya Mungu, kwa nini na sisi tusijaribu kwenda hospitalini?”<br />
<br />
“Wazo zuri mke wangu, lakini kama ikibainika mmoja wetu ana matatizo huoni ndiyo itakuwa sababu ya mapenzi yetu kupungua?”<br />
“Hapana mume wangu, nakuahidi kuwa hata kama ni wewe ndiyo mwenye tatizo, kamwe upendo wangu kwako hautapungua, nitazidi kukupenda daima.”<br />
<br />
“Hata mimi mke wangu nakuahidi kuwa kama mimi nikiwa mzima na tatizo likionekana lipo kwako, sitakutenga bali nitazidi kukupenda kwa siku zote za maisha yangu,” aliongea Phillip, wakakumbatiana kwa furaha. Walikubaliana kuwa siku inayofuata waende pamoja mpaka hospitalini kwenda kuonana na daktari anayeshughulikia masuala ya uzazi.<br />
Kesho yake waliongozana mpaka hospitalini, wakaonana na daktari ambaye aliwafanyia vipimo kwa kina.<br />
<br />
Majibu yalipotoka, Genevieve hakuwa na tatizo bali Phillip ilibainika kuwa mbegu zake za kiume hazina uwezo wa kurutubisha yai la mwanamke na kusababisha ujauzito.<br />
“Uliwahi kupata mtoto enzi za ujana wako kabla hujaoana na huyu mkeo wa sasa?” aliuliza daktari, swali ambalo lilimfanya Phillip azame kwenye dimbwi la mawazo.<br />
“Mume wangu daktari si anakuuliza?”<br />
<br />
Phillip alishindwa kujibu kwani ni kweli aliwahi kuwa na mtoto lakini siyo katika ulimwengu huu unaoonekana. Alishindwa kujua daktari atamuelewaje atakapompa ukweli huo wa maisha yake.<br />
<br />
“Sijawahi daktari, huyu ndiyo mke wangu wa kwanza na sina mtoto yeyote nje ya ndoa,” alijibu Phillip huku mkewe akimuangalia kwa huruma. Alipomueleza vile, daktari aliandika kitu kwenye cheti na kuwaomba wakasubiri nje kwa muda wakati anatafuta ufumbuzi wa tatizo lao.<br />
<br />
Aliwaita madaktari wenzake wawili na kujadiliana nao nini cha kufanya ili kumsaidia Phillip apate mtoto.<br />
“Her wife is physically fit, her uterus can conceive and the fallopian tubes are in good condition,” ( Mke wake yuko fiti, mji wake wa uzazi una uwezo wa kutunga mimba na hata mirija yake ya uzazi ipo kwenye hali nzuri)<br />
“How about him?” ( Vipi kuhusu yeye)<br />
<br />
“His sperms are not viable. They lack motility ability and they can’t swim to the uterus,” (Mbegu zake za kiume hazina rutuba. Zinakosa uwezo wa kujongea na haziwezi kuogelea kwenda kwenye mji wa mimba)<br />
Madaktari waliendelea kujadiliana juu ya tatizo la Phillip. Mwisho walifikia hitimisho la kumpa dawa ambazo zingeenda kuongeza nguvu na rutuba kwenye mbegu zake. Daktari aliyewapima akawaita Phillip na Genevieve ofisini na kuanza kuwapa ushauri nasaha kabla ya kumpa Phillip dawa za kutumia.<br />
<br />
“Mama jitahidi kumpikia mumeo vyakula vyenye wanga na mafuta ya asili kwa wingi. Pia inashauriwa mjizuie kukutana kimwili mara kwa mara ili kuzipa muda mbegu zake zikomae, mkizingatia haya naamini mwezi huu hautaisha bila majibu kuonekana,” aliongea daktari na kuwapa maelekezo mengine ya ziada.<br />
<br />
Alipomaliza waliaga na kuondoka, njiani wakawa wanamshukuru Mungu wao kwa kuwasaidia. Waliamini kwake hakuna linaloshindikana. Hakuna kitu walichokuwa wanakisubiri kwa hamu kama mtoto kwenye ndoa yao.<br />
<br />
Hata baada ya mwezi mmoja kupita, bado hawakuona dalili yoyote, Genevieve hakuwa amenasa ujauzito. Hali ile ikaanza kusababisha huzuni miongoni mwao. Ni kweli walikuwa wakipendana kwa dhati lakini walihitaji kitu kuurutubisha upendo wao.<br />
Genevieve alikuwa na kazi ya ziada ya kumfariji mumewe kwani majibu yale yalionekana kumsononesha zaidi, hasa baada ya kuambiwa tatizo lilikuwa kwake.<br />
<br />
“Au bado Zamaradi analipa kisasi kwenye maisha yangu? Lakini mbona tangu niokoke na kuoana na Genevieve hajawahi kunitokea tena? Na kama kweli sina uwezo wa kumzalisha mwanamke, mbona yeye alibeba ujauzito wangu na kunizalia mtoto?” Maswali mengi yaliyokosa majibu yalikuwa yakipishana kichwani mwa Phillip na kumfanya awe kama mwendawazimu.<br />
<br />
Licha ya hali ile, Genevieve aliendelea kumpenda huku akijitahidi kuwa karibu naye kwa kila jambo.<br />
“Mke wangu!”<br />
“Abee mume wangu?”<br />
“Kwa nini tusiende kujaribu kwa waganga wa kienyeji? Nasikia wengi wamefanikiwa.”<br />
“Haaa! Yaani mume wangu unaweza kukosa imani kiasi hicho hadi kuamua kutumia njia hiyo badala ya kumwamini Mungu?”<br />
<br />
“Kwani waganga wanaotibu si wanatumia miti iliyoumbwa na Mungu kututibu? Kibaya ni kupiga ramli mke wangu, sioni kama kuna tatizo kwenda kujaribu, hatuwezi kundelea kuishi maisha kama haya.”<br />
<br />
“Hapana mume wangu, niko radhi nisizae kabisa maishani mwangu, lakini kamwe siwezi kuabudu miungu wengine zaidi ya Mungu aliye juu.” <br />
Phillip na Genevieve walikuwa kwenye mjadala mzito juu ya hali ile yakutopata mtoto iliyowatokea. Phillip alionekana kuanza kukata tamaa kiasi cha kujaribu mbinu mbadala lakini mkewe hakuwa tayari.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea?fuatilia usiku....</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.33<br />
<br />
<br />
Phillip anakombolewa kutoka kwenye mateso ya jini Zamaradi baada ya kuokoka na kukabidhi maisha yake kwa Mungu, aliyemfanya aokoke ni Tyra ambaye muda mfupi baadaye alimchumbia na hatimaye kufunga ndoa mara tu walipomaliza masomo yao ya chuo kikuu.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Zamaradi hayuko tena katika maisha yake, wala hamtokei katika ndoto kama ilivyokuwa huko nyuma. Hivi sasa wanaishi vizuri kama mke na mume, wakiwa wamefanikiwa kimaisha kwa msaada mkubwa kutoka kwa wazazi wa Tyra ambao ni matajiri wa kutupwa. Wote wawili hawana taarifa tena juu ya Linna na kilichomtokea baada ya kufanyiwa upasuaji kurekebisha mwili wake. <br />
<br />
Kinachowatesa pamoja na mafanikio makubwa waliyo nayo ni mtoto, Phillip na Tyra wameshindwa kabisa kupata mtoto baada ya kuishi kwenye ndoa kwa miaka zaidi ya miwili. Jambo hili ndilo linawakosesha furaha pamoja na kwamba wana kila kitu.<br />
<br />
Baada ya kutafakari sana hatimaye walifikia uamuzi wa kutafuta msaada wa daktari, huko ndiko baada ya uchunguzi ilibainika kuwa, chanzo cha tatizo alikuwa ni Phillip ambaye mbegu zake hazikuwa na uwezo wa kumfanya mwanamke ashike mimba! <br />
<br />
Jambo hili linamuumiza sana Phillip na kumfanya akose kabisa raha ya maisha kwani anachohitaji ni mtoto, walipotafakari kwa muda, hatimaye Phillip alifikia uamuzi wa kutafuta tiba za jadi jambo ambalo Tyra hakukubaliana nalo.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
“Sasa tutafanya kitu gani mke wangu, mimi ndiyo mwenye tatizo na ninahitaji tiba ili niwe na uwezo wa kukupa ujauzito.”<br />
“Si kwa kwenda kwa waganga Phillip, tuendelee kumwamini Mungu, sisi tumeokoka hatuwezi kufanya jambo hilo. Tatizo ni kwamba umepoteza imani kabisa, hata maombi yako hayamfikii Mungu.”<br />
<br />
“Siyo rahisi kuendelea kuwa na imani, swala hili limeniumiza sana, nataka mtoto, nataka mtoto Tyra.”<br />
“Kuwa na imani, Mungu atajibu kwa wakati wake, Sara alisubiri miaka mingi kabla Isaka hajazaliwa, wewe umeshindwa nini?”<br />
<br />
Phillip akamuelewa mkewe, imani yake ikarejea tena. Tangu siku hiyo akawa ni mtu wa kuhudhuria maombi, aliposikia mhubiri mpya ameingia jijini Dar es Salaam alihudhuria na kueleza shida yake, maombi yakafanyika lakini bado hakuwa na uwezo wa kumfanya Tyra mjamzito, imani yake ikazidi kuporomoka tena.<br />
<br />
Kwa siri kubwa akaanza kuwa anamdanganya mke wake kwa safari za kikazi, kumbe alikwenda kwa waganga na waganguzi ambako alipewa dawa za mitishamba na kuzitumia kwa siri lakini nazo pia hazikumsaidia mpaka mwaka mmoja mwingine baadaye ukaisha wakiwa hawana mtoto, jamii nzima kuwateta kwa sababu tu hawakuwa na mtoto, jambo hili lilimuumiza sana Phillip na kumfanya wakati mwingine ajifungie chumbani na kulia.<br />
<br />
Hata kazi ilimshinda, ikabidi achukue likizo bila malipo.<br />
“Hakuna sababu ya kulia, kitu cha muhimu tutafute jibu la tatizo letu na usiwe na wasiwasi Phillip, nakupenda mno, tuwe na mtoto, tusiwe na mtoto, mimi nitaendelea kukupenda tu.”<br />
<br />
“Najua Tyra, lakini roho inaniuma sana, naamini anayenifanya hivi ni huyo huyo Zamaradi, kwa kweli simpendi.”<br />
“Usijali, yote yatapita.”<br />
<br />
Alikuwa ni Tyra, mwezi mmoja baadaye akipitia mtandaoni kujaribu kufuata suluhisho la tatizo lao aliposoma juu ya Dk. Zim Kohrer, Mjerumani bingwa wa masuala ya urutubishaji wa mayai ya uzazi na masuala ya viumbe vidogo ambaye kwa Kiingereza walimwita Consultant Embryologist. <br />
<br />
Daktari huyu maarufu nchini Ujerumani alikuwa amewasaidia watu wengi ambao hawakuwa na tegemeo la kupata mtoto, hatimaye kufanikiwa, nguli wengi kutoka Hollywood huko Marekani walimiminika katika Jiji la Berlin kupata huduma yake iliyowafanya baadhi kuzaa mpaka watoto pacha.<br />
<br />
“Nina habari njema!” Tyra alimwambia Phillip aliporejea kutoka kazini na kumkuta ameketi sebuleni akiwa mwenye mawazo mengi, Phillip akanyanyua kichwa na kumwangalia.<br />
“Habari gani?”<br />
“NImepata daktari wa kutusaidia tatizo letu.”<br />
“Wapi?”<br />
<br />
“Ujerumani.”<br />
“Ujerumani? Umempataje?”<br />
“Mtandaoni.”<br />
“Kweli?”<br />
“Ndiyo, ningependa tumjaribu naye.”<br />
<br />
“Siyo gharama kubwa?”<br />
“Ni kubwa lakini tutamwambia baba atusaidie…” Tyra hakumalizia sentensi yake simu ya mkononi ikaita, mara moja akabonyeza kitufe cha kupokea na kuiweka sikioni, akaanza kuongea.<br />
“Halo! Halo! Nini? Mama mbona unalia?...Nakuja.” Aliuliza maswali kwa mshituko.<br />
“Kimetokea nini tena?” Phillip aliuliza.<br />
“Baba ameanguka bafuni…. Twende haraka”<br />
<br />
Ilikuwa imetimu saa kumi na nusu jioni wakati wanaingia ndani ya gari, Phillip akiwa kwenye usukani na kuendesha moja kwa moja kuelekea nyumbani kwa wazazi wake Upanga wakitokea Mikocheni. Walipofika walipewa taarifa kuwa mzee alikimbizwa Hospitali ya Muhimbili, hawakutaka kupoteza muda wao hapo, gari ikageuzwa na kunyoosha hadi Muhimbili Idara ya Wagonjwa Mahututi ambako walikuta mama yake Tyra akilia, huku wauguzi na majirani wakiwa wamemzunguka.<br />
<br />
“Mama nini?”<br />
“Baba yako katutoka.”<br />
Tyra alianguka chini na kuanza kugalagala huku akilia kwa uchungu, Phillip akawepo kumnyanyua hadi kwenye gari ambako alianza kumbembeleza na kumpa maneno ya kumtia moyo. Ukweli haukubadilika, taarifa ilipotolewa baadaye na daktari ilithibitisha kuwa mzee huyo alikuwa amefariki kwa shambulio la moyo, Tyra alilia kupindukia kwa siku zote mpaka walipomzika huko Machame mkoani Kilimanjaro mamia ya watu wakiwa wamehudhuria kumzika mtu tajiri.<br />
<br />
Mpaka mwezi mmoja baadaye, Tyra na Phillip walikuwa bado wako kijijini Machame wakiomboleza msiba, tatizo lao la kukosa mtoto lilishapotea kabisa ubongoni, kilichokuwa kikifikiriwa wakati huo ni msiba mzito ulioipata familia. <br />
Kikao cha ndugu kilipokaa, mwanzoni mwa mwezi wa pili Tyra alisimikwa kuwa mrithi wa utajiri wote wa baba yake uliokadiriwa kuwa mamilioni ya dola yakiwa katika viwanda na biashara mbalimbali, kufumba na kufumbua jina la Tyra likabadilika, akaanza kuitwa Mkurugenzi.<br />
<br />
Kutajirika kwa Tyra, kulikuwa pia kutajirika kwa Phillip, watu hawa wawili walikuwa mtu na mke wake, hivyo kila alichokuwa nacho Tyra kilimstahili Phillip na alichokuwa nacho Phillip pia kilimstahili Tyra. Wote wakaacha kazi ili wasimamie mali za familia, pamoja na utajiri wote huo suala la mtoto liliwasumbua, walihitaji mtoto, hiyo ilikuwa furaha yao.<br />
<br />
“Kwanini tusisafiri kwenda Ujerumani kumuona Dk. Kohrer? Tuna fedha ya kutosha sasa kulifanya jambo hili.” Ilikuwa ni sauti ya Tyra siku moja wakiwa wamelala ndani ya chumba chao kikubwa chenye kila kitu.<br />
<br />
“Sina tatizo. Nahitaji sana mtoto mke wangu, inaniumiza sana mimi kuwa chanzo cha tatizo hili”<br />
“Usijali, hatuhitaji mtoto tu, tunahitaji watoto pacha kwa mara ya kwanza ili tufidie muda uliopotea, niko tayari kulipa chochote kwa daktari huyo ili awezeshe mimi kupata watoto wawili kwa wakati mmoja.”<br />
<br />
“Nitafurahi mno.”<br />
Kama utani, mwezi mmoja baadaye walikuwa ndani ya ndege ya shirika la ndege la Ujerumani Lufthansa, shirika la gharama kubwa pengine kuliko mengine yote duniani, wakiwa wameketi kwenye daraja la watu maarufu. Hii ilikuwa safari ya kwenda kwenye Jiji la Berlin kuonana na daktari aliyewasaidia watu wengi kupata watoto.<br />
<br />
Ilikuwa ni safari ya saa kumi na mbili, kwanza waliruka mpaka Amsterdam, Uholanzi, ambako waliunganisha na ndege nyingine ya shirika hilo hilo hadi Berlin, wakapokelewa na wafanyakazi wa Hospitali ya Freiburg ambao waliwapeleka kwanza hotelini ili wapumzike na siku iliyofuata waweze kumwona Dk. Kohrer. <br />
<br />
Mioyoni mwao walijawa na furaha kubwa kama vile tayari walishapata watoto waliowatarajia, hakuna walichokihitaji zaidi ya watoto wawili kwa wakati mmoja tena wote wawe ni wa kike.</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.34.<br />
<br />
PHILLIP alikuwa akikoroma huku mkewe akiwa amemkumbatia, walionekana kuufaidi usingizi lakini ghafla Genevieve aligutuka na kujikuta akitoka jasho jingi ingawa chumba chao cha kulala kilikuwa na kiyoyozi.<br />
“Vipi?” Phillip aliuliza baada ya kuzinduka usingizini na kumkuta mke wake ameketi kando ya kitanda akitetemeka.<br />
“Sidhani kama ni ndoto.”<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
“Kwani vipi?”<br />
“Nimeota ndoto ya kutisha.”<br />
“Ndoto gani?”<br />
“Eti Mzee Mpangala amefariki kwa shambulio la moyo, halafu mimi na wewe tumesafiri kwenda Ujerumani kumuona daktari uliyekuwa unamzungumzia.”<br />
“Ni ndoto tu, Mzee Mpangala hajafa ingawa ni kweli Dk. Zim Kohrer tumempata.”<br />
“Inawezekana ni kwa sababu ya mazungumzo yetu ya jana.”<br />
<br />
“Kweli kabisa.”<br />
“Acha nimpigie baba angalau niongee naye.”<br />
“Ni usiku sana atakuwa amepumzika.”<br />
“Phillip! Ni ndoto tu hii, yaani nimeona kila kitu mpaka tukiwa Machame kwenye mazishi.”<br />
“Ni ndoto tu mke wangu.”<br />
<br />
“Acha niongee na baba.”<br />
“Haya mpigie.”<br />
Huku Genevieve akitetemeka, moyo wake ukiwa bado hauamini kama kilichotokea ni ndoto alimpigia baba yake na kuzungumza naye, ingawa hakumweleza chochote juu ya ndoto aliyoota. Baada ya maongezi hayo ndipo alirejea kitandani na kujilaza kando ya mume wake, hawakupata usingizi tena muda wote walizungumzia habari ya watoto na safari ya Ujerumani.<br />
<br />
Wiki moja baadaye walisafiri mpaka Berlin na kutua kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Schonefeld ambako walipokelewa na wafanyakazi wa hospitali ya Freiburg ambao waliwapeleka moja kwa moja hospitalini kuonana na Dk. Zim Kohrer, mzee mfupi na mwenye mvi nyingi na aliyevaa miwani muda wote, uso wake ukiwa umejawa na tabasamu.<br />
“Mnahitaji kupumzika ili tuanze matibabu kesho?” Aliwauliza baada ya salamu ofisini kwake.<br />
<br />
“Hakuna sababu, hatujachoka kiasi hicho, karibu safari yote tulikuwa tumelala vitandani.”<br />
“Aha! Mmesafiri kwenye daraja la watu wazito bila shaka.”<br />
“Ni kweli.”<br />
“Basi tuanze.”<br />
<br />
Dk. Kohrer akafungua kompyuta yake na kuanza kuandika maelezo yao yote tangu walipooana, madaktari waliowaona na namna walivyofanya tendo la ndoa, mwisho akamuuliza Genevieve maswali mengi kuhusiana na mzunguko wake wa hedhi. Alipomaliza maswali hayo aliwaeleza juu ya vipimo ambavyo vingefanyika katika kulitafuta tatizo. <br />
“ Kwanza tutaupiga picha mfuko wa uzazi, mirija ya viwanda vya mayai ya Genevieve.<br />
<br />
Pia tutapata manii yako kwa ajili ya kuzichunguza ili tuone kama mbegu zako zina tatizo lolote, lazima tujue idadi yake na kama zina uwezo wa kurutubisha yai au la, yote haya ni muhimu tuyafahamu kabla ya kuchukua hatua yoyote.”<br />
“Hakuna tatizo lolote daktari, tumeacha shughuli zote kuja kukuona na tunaamini utakuwa na jibu la tatizo letu.”<br />
<br />
“Hakuna kisichowezekana, wengi wamepata furaha yao hapa hapa kwenye chumba hiki.” Dk. Kohrer aliongea akitabasamu.<br />
Kilichofuata siku hiyo ni kuchukuliwa vipimo, zoezi lilipokamilika waliondoka kwenda Hoteli ya Berlin Hilton ambako walifikia. Ilikuwa ni ya nyota tano, chumba kimoja kililipiwa dola elfu moja mia tano kwa usiku mmoja. Hapo ndipo Genevieve na Phillip waliamua kuishi mpaka wapate suluhisho la tatizo lao, gharama zote zikilipwa na Mzee Mpangala.<br />
<br />
Siku tatu baadaye wakiwa hotelini walipigiwa simu na Dk. Kohrer akiwataka wafike ofisini kwake mara moja kujadiliana juu ya majibu yaliyopatikana, mioyo yao ikiwa imejawa hofu na furaha waliondoka hadi ofisini kwake na kumkuta akiwasubiri kwa hamu kubwa. Tofauti na nyuso zao kuwa na wasiwasi, Dk. Kohrer alikuwa na uso wenye furaha na matumaini.<br />
“Tumekuja daktari.”<br />
<br />
“Imebidi niwaite maana majibu yote yamekamilika.”<br />
“Sawasawa.”<br />
“Itabidi niwe mkweli maana lengo ni kusaidia.”<br />
“Hakuna tatizo.”<br />
“Uchunguzi unaonyesha kwamba Genevieve huna tatizo lolote kabisa, tatizo liko kwa mumeo, Phillip…” Dk. Kohrer alimalizia kwa kuita.<br />
“Naam.”<br />
<br />
“Mbegu zako hazitoshi, ni chache na zaidi ya kuwa chache pia hazina mbio, zinashindwa kulifikia yai la mwanamke ili mimba itungwe. Nilipozichunguza zaidi nikagundua hata kama zikilifikia yai hazina uwezo wa kutungisha mimba, nimekuja kwenu na jibu lifuatalo, kama kweli mnahitaji mtoto hamna jinsi zaidi ya kutafuta mbegu za kiume za mtu mwingine ili tufanye kitu kiitwacho IVF.”<br />
“IVF ni nini daktari?”<br />
<br />
“Kirefu chake ni In Vitro Fertilization, kitakachofanyika hapo ni kuchukua mbegu za Genevieve na kuziunganisha na mbegu za mwanaume mwingine ili mimba itungwe kisha nitaipandikiza ndani ya tumbo la mkeo na itakua vizuri mpaka mpate mtoto au watoto mapacha kama mnataka.”<br />
“Inawezekana daktari?” Phillip aliuliza.<br />
<br />
“Kwanini isiwezekane, hizo ndizo kazi zangu, huwa nazifanya kila wiki.”<br />
“Mtu wa kutoa mbegu za kiume tutampata wapi?”<br />
“Tutatanganza mtandaoni, atajitokeza mtu na kulipwa si chini ya dola elfu kumi ili atoe mbegu zake. Kama mko tayari mnaweza mkaniambia niendelee na utaratibu wa kumtafuta mtoa mbegu, gharama zangu mimi zitakuwa dola elfu ishirini na mbili kwa mtoto mmoja na mara mbili yake kwa watoto pacha.”<br />
<br />
“Tuko tayari daktari, tunachohitaji sisi ni watoto.” Phillip aliongea uso wake ukiwa umeinamishwa chini ni kweli alikuwa hajisikii vizuri kuwa na watoto ambao si damu yake lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali.<br />
<br />
“Basi kesho fanyeni malipo ili mambo yafanyike haraka.”<br />
“Tutalipa daktari, wewe tafuta tu mtu wa kutoa mbegu.”<br />
“Hii hapa ndiyo namba ya akaunti yangu, mnaweza kuniingizia fedha hizo moja kwa moja pale NedBank.”<br />
“Hakuna shida.”<br />
<br />
***<br />
Novotroitsk, Urusi.<br />
Kilikuwa ni kipindi cha majira ya baridi nchini Urusi, watu wengi walijifungia ndani ya nyumba zao ambao waliwasha mitambo ya kuongeza joto. Watu kidogo sana kwenye mitaa ya mji wa Novotroitsk, maarufu kwa viwanda vya vyuma duniani, walikuwa nje sababu ya baridi. Barafu zilikuwa zimeganda juu ya ardhi, kiasi cha kuyafanya hata magari yashindwe kutembea kwa mwendo wa kasi. <br />
<br />
Katika hali hii mtu mmoja aitwaye Victor Fedorov, alikuwa nje akipigwa na baridi, hakuwa na mahali pa kuishi, alikuwa maskini kama walivyo maskini wengine wengi barani Afrika ingawa aliishi katika taifa lenye utajiri mkubwa. Moyoni alijawa uchungu, akitamani siku moja kuwa na mafanikio ndiyo maana alikimbia jijini Moscow alikozaliwa kuja kutafuta maisha kwenye mji huu mdogo wenye idadi ya watu wasiozidi laki moja kwenye mpaka wa Urusi na Kazakhstan.<br />
<br />
“Siku moja nitafanikiwa tu, sina sababu ya kuendelea kuishi Moscow wakati sina hata familia, mke na watoto wangu walishanikimbia sababu ya umaskini..” Aliwaza Victor.<br />
Kila alipotaka kupata joto aliingia kwenye vyumba ambavyo vilitoa huduma kwenye mtandao wa Intaneti kwa malipo, akalipa fedha kidogo na kupata joto huku akitafuta taarifa mbalimbali mtandaoni. Mchana wa siku hiyo baridi ilipomzidi alielekea kwenye chumba kimoja cha huduma hiyo na kuingia ndani ambako alilipia na kuonyeshwa kompyuta, akakaa na kufungua kisha kuanza kupita kwenye mitandao mbalimbali.<br />
<br />
“Sperm donor needed urgently! Ten thousand dollars will be paid.” (Mtu wa kutoa mbegu za kiume anahitajika haraka, dola elfu kumi zitalipwa.) Aliyasoma maneno hayo kwenye mtandao na moyo wake kushituka, alihitaji fedha kuliko kitu kingine chochote wakati huo na aliamini dola elfu kumi zingetosha kabisa kuanzisha biashara ya kununua vyuma na kuuza, kwa muda mrefu sana alikuwa ametamani kufanya hivyo lakini kikwacho kilikuwa ni mtaji.<br />
<br />
Haraka akajaza fomu iliyokuwepo akielezea utambulisho wake na mahali alipokuwa nchini Urusi ikiwa ni pamoja na kuweka anwani ya barua pepe na namba yake ya simu, baada ya kumaliza akaendelea na kupitia mitandao mingine. Masaa mawili kabla hajatoka ndani ya chumba hicho, simu yake iliita, namba iliyoonekana kwenye kioo haikuwa ya Urusi.<br />
“Halo!”<br />
“Halo! Victor?”<br />
<br />
“Ndiyo.”<br />
“Naitwa Dk. Kohrer, napiga simu kutoka Ujerumani nimeiona fomu yako sasa hivi mtandaoni kwamba uko tayari kutoa mbegu kwa gharama ya dola elfu kumi.”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Unaweza kunielezea jinsi ulivyo?”<br />
“Ni Mrusi, mweupe, mrefu na nina nywele nyeusi.”<br />
<br />
“Unaweza kupiga picha na kunitumia sasa hivi?”<br />
“Niko kwenye chumba cha Intaneti, hivyo ndani ya dakika kumi nitakuwa nimeishatuma.”<br />
“Nasubiri, nikishaipokea mara moja nitakupigia.”<br />
<br />
Dakika kumi na tano baadaye walikuwa kwenye simu tena, Dk. Kohrer akiongea na Victor kumthibitishia kuwa alikuwa amekubalika na angesafirishwa hadi Ujerumani kwa ajili ya kutoa mbegu ingawa kwa sharti moja tu kwamba hakutakiwa kukutana na watu ambao walihitaji mbegu yake, kazi yake ingekuwa ni kutoa mbegu, kulipwa na kuondoka.<br />
<br />
“Hilo si tatizo kwangu, cha muhimu ni malipo.”<br />
“Hakuna shida, nitakutumia sasa hivi namba ya tiketi na fedha ya matumizi njiani ili kesho usafiri kuja hapa Berlin.”<br />
“Hakuna shida.”</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.35<br />
<br />
<br />
BAADA ya Phillip na Genevieve kukubaliana na Dk. Kohrer juu ya gharama zinazohitajika kwa ajii ya kufanya IVF, njia ya kupandikiza mbegu za mwanaume mwingine ndani ya mji wa uzazi wa Genevieve kwa lengo la kupata mtoto, wawili hao walikamilisha malipo kupitia Benki ya NedBank kama walivyokubaliana na kilichofuatia ikawa ni kumtafuta mwanaume ambaye atakubali kut<span class="text_exposed_show">oa mbegu zake kwa malipo ya dola elfu kumi.<br />
<br />
Baada ya kutangaza mtandaoni, Victor Fedorov, mwanaume fukara anayeishi kwenye Mji wa Novotroisk, Urusi alijaza taarifa zake mtandaoni kuonesha kuwa yupo tayari kuchangia mbegu zake za kiume kwa malipo ya dola elfu kumi. Baada ya kujaza taarifa zake, Dk. Kohrer alimpigia simu na wakakubaliana kufanya kazi hiyo haraka kwa sharti moja la kutokutana na watu waliokuwa wakihitaji mbegu zake.<br />
<br />
Baada ya makubaliano,Victor alitumiwa tiketi ya ndege mpaka Ujerumani na siku iliyofuatia akawa tayari amewasili kwenye Hospitali ya Freiburg aliyokuwa akifanyia kazi Dk Kohrer.<br />
<br />
“Karibu bwana Victor, naitwa Zim Kohrer, mtaalamu wa embryology, kama tulivyozungumza kupitia mtandao, kuna biashara hapa ya kuuza mbegu zako za kiume kwa ajili ya kuwasaidia wanandoa wenye matatizo ya kupata mtoto.<br />
<br />
Hundi yako ya dola elfu kumi hii hapa, cha msingi twende maabara ukafanyiwe vipimo kuona kama huna matatizo yoyote kisha mambo mengine yatafuatia,” Dk. Kohler alikuwa akizungumza na mwanaume mrefu, mweupe mwenye nywele nyeusi, Victor kutoka Urusi.<br />
<br />
Hakuwa na kipingamizi chochote, kwake fedha ndiyo kitu alichokuwa anakihitaji kuliko vitu vyote. Baada ya kuingizwa maabara na kufanyiwa vipimo vya kina kuchunguza kama hakuwa na tatizo lolote, majibu yalipotoka alionekana kuwa na afya njema.<br />
<br />
Kilichofuatia ikawa ni kuingizwa tena kwa mara nyingine maabara ambapo alitolewa mbegu zake za kiume kwa kutumia utaalamu wa hali ya juu. Alipomaliza alikabidhiwa hundi yake kisha akaaga na kuondoka. Kwake ile ilikuwa ni zaidi ya bahati ya mtende kuota jangwani. Ufukara uliomtesa kwa kipindi kirefu hadi kusababisha mkewe na wanaye wamtoroke, sasa ulikuwa umefikia mwisho.<br />
<br />
Kwa kutumia dola elfu kumi alizozipata, alipanga kuanzisha biashara ya kununua vyuma na kwenda kuviuza, kazi ambayo aliitamani kwa siku nyingi lakini akawa anakwama kutokana na kukosa mtaji.<br />
Hakutaka kupoteza muda, jioni ya siku ile ile kwa kutumia tiketi aliyokuwa amekatiwa na Dk. Kohrer, alisafiri hadi Novotroisk, mji aliokuwa akiishi na kuanzisha biashara ya kununua vyuma kama alivyopanga.<br />
<br />
*******<br />
Phillip na Genevieve walikuwa chumbani kwao ndani ya hoteli wakiendelea kufarijiana, mara simu ya mezani ikaita. Kwa haraka, Phillip aliinua mkonga na kuongea na upande wa pili. Alikuwa ni Dk. Kohrer akiwataarifu kuwa kazi ya kupata mwanaume wa kutoa mbegu za uzazi tayari imekamilika na aliwataka wafike haraka hospitalini kwa ajili ya Genevieve kuchukuliwa mbegu zake tayari kwa kuunganishwa na mbegu ya mwanaume aliyepatikana, ambaye wote hawakutakiwa kukutana naye.<br />
<br />
“Mke wangu, kila kitu kipo tayari, daktari amesema tujiandae kwenda hospitali sasa hivi,” aliongea Phillip kwa furaha huku akimkumbatia mkewe. Kwa pamoja walimshukuru Mungu kwani hawakudhani kuwa kazi ya kumpata mtoa mbegu ingekuwa rahisi kiasi kile. <br />
Baada ya kujiandaa, Phillip na mkewe walishuka ngazi hadi kwenye maegesho ambako dereva wa hoteli alikuwa akiwasubiri, wakaondoka wakimhimiza aendeshe kasi hadi Hospitalini, gari likaegeshwa na wakashuka na kwenda moja kwa moja hadi ofisini kwa Dk. Kohrer aliyekuwa akiwasubiri.<br />
<br />
Bila kupoteza muda aliwaeleza mafanikio ya mpango wao huku akiwaonesha picha ya mwanaume aliyetoa mbegu zake na kila mmoja akaridhika na mwonekano wake.<br />
“Hamtakiwi kukutana naye kabisa, wala yeye hapaswi kukutana nanyi ili mradi amekwishatoa mbegu, kazi yake imekwisha!” Aliongea kwa msisitizo Dk. Kohrer.<br />
<br />
Kilichofuata kikawa ni Genevieve kuchukuliwa hadi chumba cha upasuaji mdogo ambapo zoezi la kuzinyonya mbegu kwenye viwanda vyake vya mayai lilifanyika, bahati nzuri alikuwa katika kipindi ambacho mayai yake yalikuwa tayari kwa kurutubishwa.<br />
<br />
Ilikuwa ni operesheni ndogo lakini ilichukua muda wa masaa matatu, ndipo mayai yakapatikana na Dk. Kohrer kuyachukua kwenye chombo maalum kiitwacho Incubator hadi maabara ambako alishirikiana na wataalamu wengine kuliunganisha moja ya mayai hayo na mbegu ya Bwana Victor Fedorov iliyogandishwa, ambaye tayari alikuwa ndani ya ndege akirejea Urusi.<br />
<br />
Zoezi la kurutubisha na kupandikiza kiumbe hicho ndani ya mfuko wa uzazi wa Genevieve na uchunguzi kama hakikuwa na matatizo yoyote lilipokamilika masaa arobaini na nane baadaye, alipewa muda wa mwezi mmoja kupumzika wodini ili kuhakikisha kiumbe hicho kinapata muda wa kuzamisha mizizi yake kwenye mfuko. <br />
<br />
Mambo yote yalipokamilika ikiwa ni pamoja na kulipa gharama zote zilizokuwa zinahitajika, Phillip na Genevieve waliruhusiwa kurejea Tanzania kwa makubaliano ya kuendelea kuwasiliana na Dk. Kohrer katika hatua zote za ukuaji wa ujauzito ule.<br />
Saa kadhaa baadaye wakawa ndani ya ndege ya shirika la usafiri wa anga la Ujerumani, Lufthansa. Mioyo yao ikiwa imejawa na furaha, hakika safari yao ilikuwa ya mafanikio makubwa.<br />
<br />
Walipowasili Dar es Salaam, waliendelea na maisha yao kama kawaida na baada ya wiki kadhaa kupita, Genevieve akaanza kuonesha dalili zilizoamsha matumaini mapya kwao. Alianza kusikia kichefuchefu na kuanza kuchagua aina ya vyakula.<br />
<br />
“Kaniletee ndimu mume wangu, halafu samaki wabichi siwatamani hata kuwaona, wananifanya nijisike kichefuchefu,” aliongea Genevieve kwa kudeka akiwa amejilaza kwenye kifua cha mumewe. Dalili zile zilimfurahisha zaidi Phillip kwani aliamini sasa na yeye atapata heshima kama wanaume wengine wenye familia.<br />
<br />
Mwezi wa nne wa ujauzito huo ulipoingia, afya ya Genevieve ikiwa nzuri, walikwenda hospitali kupima ili wapate uhakika wa jinsi mtoto alivyokuwa akiendelea kukua. Wakati wa kuwapa majibu, sura ya daktari ilikuwa imejawa na tabasamu.<br />
“Mimba inaendelea vizuri sana, tena nina habari nzuri za kuwapa... Genevieve una mimba ya watoto pacha!”<br />
<br />
“Asante Mungu, furaha yangu itakuwa mara mbili!”<br />
Hakuna aliyekuwa anaelewa namna walivyofanikisha suala lile la Genevieve kupata ujauzito, wakaendelea kuifanya siri kama walivyokuwa wamekubaliana. Kwa kadiri siku zilivyokuwa zinazidi kwenda mbele, ujauzito wa Genevieve ulizidi kuongezeka, tumbo lake likawa kubwa, hali iliyowafanya wote wawili kujisikia fahari kubwa mioyoni mwao.<br />
<br />
Ujauzito wake ulipofikisha miezi sita, Genevieve alilazimika kupumzika nyumbani na kuacha shughuli zote alizokuwa akizifanya, kama walivyokuwa wameshauriwa na Dk. Kohrer, lengo la kufanya hivyo likiwa ni kuzuia ujauzito ule kuharibika katika hatua za mwisho. Phillip akawa na kazi ya kumtunza mkewe kwa uangalifu, huku wakizidi kumuomba Mungu wao kila uchao.<br />
<br />
Hatimaye miezi tisa ilitimia, Genevieve akashikwa na uchungu wa kujifungua. Kwa kuwa Phillip alikuwa amemuandalia mkewe kila kitu, alipoanza kuonesha dalili za uchungu tu, alimkimbiza haraka hospitali.<br />
<br />
Alipofika mapokezi akiwa anaendesha gari mwenyewe, Phillip aliwasiliana na manesi wakunga ambao kwa haraka walisogeza kitanda cha magurudumu karibu na gari lake, Genevieve akateremshwa na kuwekwa juu yake, akawa anakimbizwa kuelekea kwenye wodi za wazazi huku akijinyonganyonga kutokana na maumivu makali aliyokuwa akiyahisi.<br />
<br />
Aliwekwa kitandani, Phillip akawa kando yake akishuhudia hatua kwa hatua namna mke wake alivyokuwa akifanya kazi ya kuwaleta watoto hao duniani! Jukumu lake lilikuwa ni kumfariji na kumtia moyo.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4ca429a84240737">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.36.<br />
<br />
<br />
Hospitali ya Aga Khan ilikuwa umbali wa kama mita mia mbili na hamsini tu kutoka walipoishi Phillip na Genevieve, ilikuwa hospitali kubwa ya gharama pale ambapo mtu alihitaji huduma kutoka kwa madaktari wake. Kwenye chumba ambacho mlangoni kilikuwa na kibao kilichoandikwa “Labour Room” ndimo alimokuwa amelala Genevieve akihangaika na maumivu, Phillip akiwa ka<span class="text_exposed_show">ndo yake, akimpapasa tumbo na kiuno kama njia ya kumpunguzia maumivu.<br />
<br />
“So painful!” (Inauma sana.) aliongea machozi yakimtoka.<br />
“I know, just be strong because soon you are going to be happy. Our dream is going to be realized and you are the dream bearer” (Najua, kuwa imara tu, sababu muda si mrefu utafurahi, ndoto yetu itatimia na wewe ndiye uliyeibeba ndoto.) Phillip alimwambia mke wake.<br />
<br />
Wauguzi walikuwepo muda wote kutoa kila aina ya msaada uliohitajika lakini kwa saa zote kumi na mbili lakini bado Genevieve hakuweza kujifungua, daktari akafikia uamuzi wa kumchoma sindano ya kuongeza uchungu, Oxytocin, ambayo ilipochomwa tu, muda wa kama masaa matatu baadaye, mtoto wa kwanza wa kike alitoka na akafuatiwa na mwingine wa pili ambaye pia alikuwa wa kike.<br />
<br />
Genevieve akainua kichwa chake na kuwaangalia watoto wake, machozi ya furaha yakamtoka, Phillip akasogea karibu na kumkumbatia. Hakika ndoto ilikuwa imetimia, haikujalisha kabisa mbegu za watoto hao zilitoka wapi, walikuwa ni watoto wao, Mungu alikuwa amewapa ili wawalee na kuwatunza.<br />
“Mwaaa!” Phillip alimbusu mke wake usoni.<br />
<br />
“Thank you, finally we are going to be the happiest couple on earth.” (Asante, hatimaye tutakuwa wanandoa wenye furaha kuliko mwingine yeyote duniani.)<br />
“Yeah!” (Ndiyo.)<br />
Watoto waliondolewa na kupelekwa kwenye chumba maalum ambako walivalishwa nguo na kufanyiwa huduma zote, Genevieve akatundikiwa dripu ya maji ya Glucose ili kumuongezea nguvu mwilini maana alikuwa amedhoofika sababu ya kusukuma watoto kwa muda mrefu. Masaa mawili baadaye, Phillip akiwa bado na mke wake wazazi wa Genevieve waliingia, wakiongozwa na mzee Mpangala, wote nyuso zao zilikuwa zimejawa na furaha.<br />
<br />
“Hongera mwanangu.”<br />
“Asante baba, nimekuletea wake wazuri wawili, kama ndoto yangu ya kwamba umekufa niliyoota ingekuwa kweli, basi ungewakosa.” Genevieve aliongea akiikumbuka ndoto mbaya aliyoota kabla hawajasafiri kwenda Ujerumani kuonana na Dk. Kohrer.<br />
<br />
“Ilikuwa ni ndoto tu mwanangu, hongera sana, ukoo unazidi kuongezeka.”<br />
“Kweli baba.”<br />
Ilikuwa ni siku ya furaha mno kwa kila mmoja wao, kitu kilichomsumbua Phillip moyoni ni historia ya watoto hao, bado alielewa kabisa uwazi kwamba hakuwa baba yao halisi. Kwa mbali hili lilimuumiza, kwani hakujua nini kingetokea iwapo yeye na Genevieve siku moja wangeshindwa kuelewana na hatimaye kutengana, hiyo ilimaamnisha angeweza kuambiwa watoto wale hawakuwa wake. Akajipa moyo kwamba Genevieve asingeweza kumfanyia kitendo hicho.<br />
<br />
Muda mfupi baadaye watoto walitolewa chumbani walikopelekwa na kuletwa kitandani kwa Genevieve, wakalazwa kando yake, kwa furaha akawafunua na kuanza kuwabusu. <br />
Mzee Mpangala na watu wote waliokuwa chumbani walionyesha mshituko kwa rangi za watoto hao hazikuwa za Waafrika halisi lakini hakuna aliyediriki kufungua mdomo wake kuulizia jambo hilo.<br />
“Wanafanana sana na marehemu bibi yetu mzaa mama, yeye alikuwa na asili ya Kibeligji,” Phillip aliongea baada ya kuzisoma kwa makini nyuso za watu waliokuwemo chumbani na kuugundua wasiwasi wao, hakutaka mtu yeyote aelewe siri ya kupatikana kwa watoto hao.<br />
<br />
“Duh! Tulitaka kushangaa, imekuwaje nyinyi Waafrika mzae watoto wa aina hiyo.” Mzee Mpangala aliongea.<br />
Hawakukaa sana baada ya hapo, ndugu na marafiki wakaondoka na kuwaacha Phillip na Genevieve peke yao wakiendelea kuweka msimamo wa kuificha siri ya watoto hao. Siku mbili baadaye waliruhusiwa kuondoka hospitali na kurejea nyumbani Upanga ambako furaha iliendelea mtindo mmoja, ndugu na jamaa wakiendelea kumiminika kuwaona watoto pacha wa Genevieve na Phillip.<br />
“Naomba nipewe nafasi ya kuwapa watoto wangu majina.” Genevieve aliongea mbele ya ndugu na jamaa.<br />
“Endelea.” Watu wote wakaitikia.<br />
<br />
“Hawa watoto wataitwa Dorice na Dorica!”<br />
“Yupi Dorice, yupi Dorica?” Phillip akauliza.<br />
“Wa kwanza kutoka ni Dorica na wa pili ni Dorice!”<br />
<br />
Makofi yakapigwa watu wakishangilia, majina yalikuwa yamewafanana kabisa watoto kwa jinsi sura zao zilivyokuwa nzuri. Miezi mitatu baadaye watoto wakiendelea kukua vizuri, Phillip alirejea kazini kwake kwenye kampuni ya simu za mikononi iliyoitwa T-Mobile ambako alifanya kazi kama mwanasheria na Genevieve akaendelea kufanya kazi kwenye kampuni ya baba yake ambako alitumia elimu yake ya uchumi akiwa Mkurugenzi Msaidizi, lengo la Mzee Mpangala lilikuwa ni kumrithisha kila kitu ili aendeleze mambo aliyoyafanya, muda wa kustaafu ukifika.<br />
<br />
Miezi tisa baadaye watoto walitimiza mwaka mmoja, sherehe kubwa ya kuzaliwa kwao ikafanyika, mpaka wakati huo hakuna mtu hata mmoja aliyejua siri ya namna walivyopatikana. Dk. Kohrer alialikwa siku hiyo kusherehehea mafanikio lakini aliombwa kutoongea chochote juu ya namna mimba ilivyotungwa, hiyo ilitakiwa kubaki siri mpaka mwisho wa dunia.<br />
<br />
***<br />
Victor Fedorov alipoingia nchini Urusi, taarifa ya kwanza aliyoipokea ni juu ya kifo cha mke na watoto wake kwenye milima ya barafu walikokwenda kushiriki mchezo wa kuteleza kwenye barafu. Ingawa siku zote alimchukia mke wake, Fedorov aliwapenda mno watoto wake Misha na Kunin, alilia na kuomboleza, kilichomsikitisha zaidi ni kwamba hakuweza kuziona maiti zao. <br />
<br />
Kilichofanyika baada ya hapo maishani mwake, hakikuwa kufanya biashara ya vyuma kama alivyokuwa amepanga baada ya kupokea dola elfu kumi kutoka kwa Dk. Kohrer, akaamua kuingia kwenye ulevi. Kazi yake kubwa ikawa kunywa na kulewa, lengo likiwa ni kupoteza mawazo ya kupoteza mke na watoto, maisha yakaharibika, akawa mtu wa kulala baa na mtaani. <br />
“Sina sababu ya kufanya kazi au biashara tena, acha ninywe tu.” Aliwaza na kila siku hilo ndilo jambo alilofanya; kunywa.<br />
<br />
Miezi mitatu baadaye, fedha zote ilikuwa imekwisha, akaanza kuteseka tena. Mwisho akiwa amebakiza dola tano mfukoni aliamua kuitumia kununua tiketi ya bahati nasibu kubwa iliyokuwa ikifanyika nchini Urusi, zawadi yake ikiwa dola milioni moja kwa ambaye angeshinda. Alifanya hivyo kama jaribio la bahati yake, ingawa hakuwa na uhakika wa kushinda.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Fuatilia ili upate kujua kitakachojiri kwenye maisha ya Phillip na mke wake Genevieve na watoto wao wazuri Dorice na Dorica</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4c2bc8c03627227">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.37<br />
<br />
<br />
Be the next Millionaire, ulikuwa ni mchezo mkubwa sana nchini Urusi, maelfu ya watu walishiriki wakijaribu bahati yao. Kila mwaka alipatikana mshindi mmoja tu katika nchi hiyo kubwa yenye idadi ya watu wasiopungua milioni 141, ushindani ulikuwa mgumu, hata Victor aliponunua tiketi yake alijua angeshindwa, hata hivyo alitaka kujaribu kwa sababu hakuwa na jambo <span class="text_exposed_show">jingine la kufanya.<br />
<br />
“Huwezi jua pengine naweza kushinda, hakyanani nikipata fedha tena safari hii sitafanya mchezo, namuahidi Mungu kwamba nitabadilika kabisa, sitakunywa pombe tena na nitatoa sehemu ya kumi kwake kama Zaka…Ee Mungu nisaidie”<br />
Aliitunza tiketi yake kwenye karatasi la nailoni ili isiweze kuharibika kwa unyevunyevu uliosababishwa na umande, kila siku jioni akiwa mtaani kwenye veranda alilolala ilikuwa ni lazima aifungue na kuanza kuzisoma namba zake.<br />
<br />
“18243004!” alitamani siku ya kutangazwa mshindi namba hiyo ndiyo isomwe, akiteseka kwa ubaridi aliendelea kusubiri mtaani kwa hamu kubwa, akipata msaada wa fedha ya chakula kwa kuombaomba kwa wapita njia, moyoni akijilaumu kwa kuchezea fedha aliyopata baada ya kuuza mbegu.<br />
“Siku itafika tu! Matangazo yatoke kwamba mimi ndiye mshindi wa Bahati Nasibu…ni Machi 16, siyo mbali, itafika tu!” aliwaza Victor akiwa mtaani.<br />
<br />
***<br />
Dorice na Dorica walikuwa wazuri mno, kila mtu aliwapenda, tena walikuwa ni wapole waliobebwa na kila mtu. Watu hawakusita kusema wangesumbua sana vijana wa kiume kama wangefikisha umri wa miaka kumi na sita, sura zao zilikuwa ni mchanganyiko wa baba na mama yao ambao kwa hakika walikuwa na mvuto wa kutosha.<br />
<br />
Wakaendelea kukua vizuri, siri ya walivyopatikana ikaendelea kufichwa, watu wote mpaka familia waliamini mbegu za Phillip ndizo zilizotumika jambo ambalo halikuwa kweli. Jambo hilo halikutakiwa kabisa kuvuja, hata wao wenyewe waliliongelea mara chache na hawakupenda kabisa lijitokeze, Genevieve alimheshimu Phillip kama baba wa watoto wake.<br />
<br />
“Hivi itakuwaje kama itakatokea siku moja siri ikavuja na aliyetoa mbegu zake akajitokeza na kudai Dorice na Dorica ni watoto wake?” Phillip alimuuliza mke wake siku moja akicheza na watoto wake sebuleni.<br />
“Haiwezekani, atajuaje?”<br />
“Huwezi kuelewa, lakini ikitokea hivyo, nakuhakikishia mke wangu kwamba nitakufa au nitaua mtu, hawa ni watoto wangu kabisa, ndivyo ninavyojisikia ingawa sikutoa mbegu, nawapenda kuliko kitu kingine chochote maishani mwangu, najua ndiyo watarithi kila kitu nitakachokipata!”<br />
<br />
“Ina maana unawapenda kuliko hata mimi mama yao?”<br />
“Siyo hivyo mke wangu, nyote nawapenda kwa upendo mmoja, teh! teh! teh!” Phillip alimaliza kwa kucheka.<br />
Miaka miwili na nusu baadaye Genevieve akiendelea kuendesha kampuni za baba yake kama Mkurugenzi Mkuu na Phillip akipandishwa cheo kuwa Mwanasheria Mkuu wa T-Mobile, Dorice na Dorica waliandikishwa chekechea katika shule ya Awali iitwayo Upanga Maranatha Kindergaten school.<br />
<br />
Ilikuwa ni siku ya furaha mno kwa watoto na hata wazazi wao, huko walijifunza kuandika, kuimba, kusoma na hata kuhesabu na uwezo wao ulikuwa mkubwa sana kuliko watoto wengine kituoni hapo, jambo hili liliwapa Phillip na Genevieve tumaini kubwa.<br />
“Wanaendelea vizuri sana, tumaini letu ni kwamba hata wakianza darasa la kwanza watakuwa na akili hivi hivi!” Ilikuwa ni sauti ya mwalimu akiwaeleza Phillip na mke wake siku ya mkutano wa wazazi na walimu shuleni.<br />
<br />
“Tutafurahi mno, ahsanteni sana kwa jinsi mnavyowafundisha watoto wetu”<br />
“Pia ninyi, kwa ushirikiano mnaotupa na malezi bora kwa watoto, hiyo inafanya kazi ya kuwafundisha iwe rahisi, ni wasikivu sana na wana adabu”<br />
Miaka miwili baadaye na nusu baadaye, Dorica na Dorice wakiwa na umri wa miaka mitano taratibu za kuwatafutia shule ya kuanza darasa la kwanza zilianza kufanyika, walikuwa wamekuwa kiasi cha kutosha, kiasi kwamba haikuonekana sababu yoyote ya kusubiri mpaka watimize umri wa miaka saba ambao watoto wengi walianza nao darasa la kwanza.<br />
<br />
“Mom I am so happy, tomorrow am going to be a big girl!” (Mama nina furaha mno, kuanzia kesho nitakuwa msichana mkubwa) ilikuwa ni sauti ya Dorica akimwambia mama yake huku uso wake ukiwa umejawa na tabasamu lililomfanya azidi kuvutia na kufanana kabisa na mama yake.<br />
“Me too mom!” (Mimi pia mama) Ilikuwa ni sauti ya Dorice.<br />
“Why?” (Kwanini?)<br />
“We are going to start Primary School!” (Tutaanza darasa la kwanza) wote wawili wakaitikia wakimkumbatia mama yao.<br />
<br />
Siku hiyo walilala usingizi wa mang’amung’amu, wakiifikiria siku iliyofuata, ya kwanza kuanza darasa la kwanza. Ilibaki kidogo tu walale wamevalia sare za shule kwa furaha waliyokuwa nayo. Phillip na mke wake walicheka sana, wao pia walilazimika kuingia kitandani saa nane usiku sababu wasingeweza kuwaacha watoto wakiwa macho peke yao.<br />
<br />
Kulipokucha Phillip na mke wake walishirikiana kuwaandaa, baadaye Phillip aliondoka akimwacha Genevieve ili muda ukifika awapeleke kwenye kituo ambako basi la Shule ya Holy Ghost lingepita na kuwachukua, baada ya hapo ndiyo yeye angerejea nyumbani kuendelea na shughuli nyingine.<br />
<br />
***<br />
Mamilioni ya watu nchini Urusi walikuwa nyuma ya runinga zao, ilikuwa ni siku ya Machi 16, kila mtu mkononi akiwa ameshika kipande cha karatasi, kilikuwa ni tiketi ya Bahati Nasibu ya Be the next Millionaire, kila mmoja aliamini yeye ndiye angekuwa mshindi na maisha yake yangebadilika kuanzia siku hiyo.<br />
<br />
Victor Fedorov, alikuwa nje ya baa iitwayo Zona, ambako watu wengi maarufu walikwenda kuburudika siku za mwisho wa wiki. Alikuwa hapo akiomba kwa watu waliokuwa wakiomba kuingia na kutoka ndani ya baa hiyo maarufu, yeye pia alikuwa na kipande chake cha tiketi mkononi, akichungulia ndani kwenye runinga kubwa iliyokuwa ukutani, ambayo ililengwa na macho ya watu wote wakitaka kushuhudia nani angeibuka Milionea.<br />
<br />
“Na mshindi ni mwenye tiketi namba…!” Mtangazaji, msichana mwembamba mrefu mwenye sura ya kuvutia aliyejaa sawasawa kwenye kikoo cha runinga alisema, watu wote wakawa kimya, mapigo ya moyo yakisikika namna yalivyogonga kifua, huku macho yao yakiwa yameelekea kwenye kipande cha karatasi na masikio yakiwa yameongezewa uwezo wa kusikia. Victor alikuwa kimya, yeye pia akiisoma tiketi yake.<br />
“Narudia tena mshindi ni mwenye namba 1824300…!”<br />
<br />
“Mungu wangu! Mungu wangu! Mungu wangu!” Victor alisema kwa sauti ya chini chini, mwili wote ukitetemeka na machozi yakimtoka, alikuwa amebakiza hatua moja tu maishani mwake awe milionea!<br />
Kilichofuata baada ya hapo, sekunde chache tu baadaye ni kelele nyingi nje ya ukumbi, mtu akipiga kelele na kushangilia, watu wote wakatoka mbio kwenda kuona nini kilichotokea lakini hawakumwona, alishapotelea gizani. Wakarudi ndani kuendelea na vinywaji, kila mmoja wao akisonya na kujisikia ni mwenye bahati mbaya.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4d5238493625723"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.38.<br />
<br />
<br />
…4!” ndivyo alivyomalizia mtangazaji.<br />
Victor hakuamini alichokisikia, hisia zake zilimtuma kuwa huenda masikio yake yalikuwa yamemdanganya au alikuwa akiota ndoto. Mshindi wa bahati nasibu wa dola milioni moja awe yeye? Lilikuwa ni jambo lisilowezekana kwa maskini ambaye hakuwa hata na mahali pa kulaza ubavu wake kuibuka na kitita hicho.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Kwa hofu kubwa aliyokuwa nayo ya kuuawa na pengine kunyang’anywa tiketi yake, Victor alikimbia umbali wa kama mita mia tano hivi na kuingia chini ya daraja ambako alizama huku akihema kwa nguvu katikati ya mapipa mawili ya takataka.<br />
<br />
“Siamini! Ahsante Mungu,” alijisemea moyoni mwake huku akiendelea kububujikwa na machozi ya furaha.<br />
Hakutoka hapo, wadudu waliendelea kumuuma lakini alijikaza mpaka kulipokucha. Saa kumi na mbili kasorobo ndipo alipoondoka katikati ya mapipa na kuanza kutembea kuelekea mjini ambako alianza kuzitafuta ofisi za Be a Billionaire mpaka akazipata na kuketi mbele ya mlango wake.<br />
<br />
Tayari mwanga wa siku ulishajitokeza na kulikuwa na baridi kali iliyomfanya atetemeke kiasi cha meno kugongana kama vile alikuwa na homa kali. Hakujali, mawazo yake yote yalikuwa kwenye dola milioni moja, tayari alikuwa tajiri. Kwa fedha hizo asingelala nje tena, angenunua nyumba nzuri yenye mitambo ya kuongeza joto.<br />
<br />
“Pombe basi tena! Sitafanya makosa ya mwanzo. Mungu amenipa nafasi nyingine,” aliwaza Victor.<br />
Saa mbili kamili mfanyakazi wa kwanza wa ofisi hiyo alifika na kumkuta Victor ameketi mbele ya mlango, haraka akamuamuru aondoke akidhani ni watu wasiokuwa na makazi, Victor aligoma kuondoka na kumwambia alikuwa na shida kwenye ofisi hiyo.<br />
<br />
“Hakuna msaada hapa.”<br />
“Sijaja kutafuta msaada, kwa fedha niliyonayo naweza kukuajiri wewe uwe unafua nguo zangu za ndani tu! Wala si suruali na mashati”<br />
“Kaka usinitukane, nahisi wewe ni punguani.”<br />
“Baada ya muda si mrefu utaanza kuniamkia.”<br />
“Akuamkie nani?” aliuliza mwanaume huyo huku akifungua mlango kisha kuingia ndani, Victor alimfuata kwa nyuma.<br />
<br />
“Kaka nimekwambia subiri nje.”<br />
“Soma hii…” Victor aliongea akimwonyesha tiketi.<br />
“Mungu wangu! Ni wewe? Shikamoo kaka, karibu kiti, utatumia kinywaji gani?”<br />
“Sihitaji chochote, hivi sasa ndiyo unaanza kuniamkia?”<br />
“Samahani sana, sikufahamu.”<br />
<br />
“Naomba fedha yangu niondoke.”<br />
“Kaka subiri, meneja anakuja muda si mrefu, atawaita waandishi wa habari na kukutangaza, hongera sana.”<br />
Victor hakujibu, alibaki kimya akionekana mwenye chuki sababu ya dharau alizofanyiwa. Nusu saa baadaye mwanaume mfupi mnene mwenye kitambi chenye uzito usiopungua kilo hamsini aliingia, mfanyakazi aliyetangulia akasimama kwa heshima na kumwamkia kisha kumtambulisha kwa Victor, yeye pia alionesha hali ya kutoamini.<br />
<br />
“Ni wewe?”<br />
“Ndiyo”<br />
“Unaishi wapi?”<br />
“Sina makazi, naishi mtaani.”<br />
<br />
Mchana wa siku hiyo, Victor alinunuliwa suti nzuri ya vipande vitatu, akanyolewa nywele zake vizuri, akavaa pamoja na viatu vyeusi vya ngozi vipya tayari kwa mkutano na waandishi wa habari akitangazwa kama mshindi wa dola milioni moja. Uso wake ulikuwa umejawa na tabasamu, hakuwahi katika maisha yake kupigwa picha nyingi kiasi hicho. Gazeti la jioni lilipotoka lilikuwa na kichwa cha habari kisemacho A homeless become a millionaire (Asiye na makazi aibuka milionea). Ilikuwa ni furaha isiyo na kifani.<br />
<br />
Urusi na dunia nzima ilisoma habari za Victor Fedorov, siku hiyo hakulala nje, alipangishiwa chumba kwenye hoteli ya nyota tano ya Hilton akifanyiwa kila kitu kama mfalme. Siku iliyofuata asubuhi taratibu za kufungua akaunti na kuhamisha fedha zake zilifanyika, dola milioni moja zikaingizwa kwenye akaunti yake.<br />
<br />
Kitu cha kwanza alichokifanya ilikuwa ni kuchukua moja ya kumi ya fedha hizo zote na kuzipeleka kanisani kama alivyomuahidi Mungu, kisha kuwakusanya watu wote wasio na makazi walioishi katika Mji wa Novotroitsk na kuwafanyia sherehe kisha kuwapatia mitaji wa biashara. Baada ya hayo hakutaka kuchezea fedha kama alivyofanya awali, alikimbia haraka kwenye soko la hisa ambako alionana na madalali na kuambiwa kampuni ya vyuma iitwayo Novic Metals, ilikuwa ikiuza hisa zake kwenye mnada.<br />
<br />
“Kwa dola laki tisa naweza kununua asilimia ngapi ya hisa?”<br />
“Asilimia themanini.”<br />
“Niko tayari.”<br />
“Unazo fedha?”<br />
“Ninazo.”<br />
<br />
“Wapi?”<br />
“Kwenye akaunti yangu.”<br />
“Benki gani?”<br />
“Russian Commercial Bank.”<br />
“Unaweza kuniruhusu nimpigie meneja wa Benki?”<br />
“Hakuna shida.”<br />
<br />
Hilo lilifanyika, dalali mkuu wa soko la hisa la Urusi akapata uhakika na biashara ikafanyika. Bila kutarajia wala kupanga, kampuni hiyo kubwa ya uchimbaji wa chuma ikawa mali ya Victor Fedorov. Wanahisa wote wakatangaziwa na kukutana naye kwenye mkutano wa wanahisa siku tatu baadaye. Hakuna aliyekuwa tayari kuamini kwamba mtu ambaye hakuwa na makazi, waliyempita mtaani akipigwa na baridi ndiye sasa alikuwa mmiliki wa kampuni hiyo.<br />
<br />
Victor akaanza kuchapa kazi akiwa na uchungu mkubwa wa maisha, alitaka kufanikiwa na alitamani kuwa tajiri. Hivyo alifanya kazi usiku na mchana, akiwa na chumba cha kuishi ndani ya kiwanda chake. Hii iliwafanya wafanyakazi wote wafanye kazi kwa kujituma, huku akitoa motisha kwa wale waliofanya kazi kwa bidii kuliko wengine.<br />
<br />
Miezi michache baadaye aligundua kuwa kilichoifanya kampuni hiyo isipate faida kilikuwa ni uvivu na kutojituma kwa wafanyakazi. Aliporekebisha tatizo, faida kubwa ilipatikana ndani ya miezi sita tu, kampuni ikaanza kukua na ndoto ya Victor kuwa tajiri ikaanza kuonesha njia. Akanunua nyumba kubwa na gari la kifahari kisha kumuoa binti mrembo aitwaye Maria Nosh kwenye harusi iliyokusanya matajiri na wanasiasa wengi kwenye mji huo. Tayari alishakuwa miongoni mwao.<br />
<br />
Wakati kampuni ikiendelea kukua, Victor ambaye aliwauzia Phillip na Genevieve mbegu zake za kiume, hakuweza kupata mtoto katika mwaka wa kwanza wa ndoa yake. Moyo wake uliumia kwani alihitaji mtoto kuliko kitu kingine chochote, alitaka mrithi wa utajiri wake baada ya watoto wake kufa mwaka mmoja kabla.<br />
<br />
Haraka yake ya kupata mtoto ilimfanya aachane na Maria Nosh mwaka mmoja na nusu tu baada ya ndoa yao, akamuoa mrembo mwingine aitwaye Milka Vashnic ambaye pia mpaka mwaka mmoja baadaye alikuwa hajapata mtoto, Victor akamuacha bila kujiuliza mara mbili.<br />
<br />
“Nahitaji mtoto, haraka iwezekanavyo,” alijisemea moyoni mwake, ghafla akazikumbuka mbegu zake alizouza kwa Dk. Kohrer. Akachukua simu na kuipiga namba yake akitaka kufahamu nini kilitokea baada ya yeye kuondoka Ujerumani.<br />
<br />
“Aaa! Yalikuwa mafanikio makubwa, walizaliwa watoto wawili.”<br />
“Wako wapi?”<br />
“Siwezi kusema, ni kinyume na taratibu za kazi yangu.”<br />
“Daktari, nawahitaji hao watoto, ni wa kwangu.”<br />
“Victor umechanganyikiwa?”<br />
<br />
“Sijachanganyikiwa, nahitaji watoto wangu kwa gharama yoyote.”<br />
“Utajuaje mahali walipo?”<br />
“Nitajua. Fedha haishindwi, mimi si maskini mlala nje tena.”<br />
“Siyo rahisi.”<br />
<br />
“Naapa kwa Mungu kuwa lazima watoto wangu nitawapata. Kama ni dola elfu kumi niliyopewa niko tayari kuirejesha hata kama ni mara kumi au mia moja zaidi lakini nipewe wanangu.”<br />
Tayari simu ilishakatwa upande wa Dk. Kohrer.</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4aa481a25724756">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.39<br />
<br />
ILIKUWA ni ofisi kubwa iliyopambwa kwa vioo kila upande na kulikuwa na meza kubwa pamoja na kabati iliyotengenezwa kwa fomaika, kando kulikuwa na mashine ya kuongeza joto chumbani kwa sababu baridi ilikuwa chini ya nyuzi sifuri kwa wakati huo kwenye mji wa Novotroitsk, nyuma ya meza hiyo aliketi mwanaume aliyevalia suti nyeusi ya vipande vitatu, tai nyekundu n<span class="text_exposed_show">a shati jeupe, uso wake haukuonekana wenye furaha hata kidogo.<br />
<br />
Alikuwa Victor Fedorov, ambaye miezi michache tu kabla alikuwa akiishi nje sababu ya kukosa makazi huku akipigwa na baridi. Sasa alikuwa mkurugenzi wa kampuni ya Novic Metals yenye wafanyakazi zaidi ya elfu mbili na mia tano, yeye akiwa mwajiri wao.<br />
<br />
Kichwani mwake alikuwa na wazo moja tu; watoto. Aliwataka watoto waliotokana na mbegu zake wapatikane na kusafirishwa kuja Urusi mara moja, uwezo wa kufanya hivyo alikuwa nao sababu ya utajiri mkubwa alioumiliki akiendesha kampuni ya kuchimba na kufua vyuma iliyoshika namba mbili kwa ukubwa nchini Urusi.<br />
<br />
“Nahitaji watoto wangu!” alisema Victor kwa Kirusi huku akipiga meza kwa nguvu.<br />
Moyoni mwake aliamini kuna jambo lingemwezesha kuwapata watoto hao zaidi ya kutafuta mpelelezi au kampuni ya upelelezi ambayo angeilipa ili ifanye kazi hiyo dunia nzima mpaka watoto watakapopatikana. Alizungusha akili yake huku na kule akitafakari na kufikiria kampuni yoyote ambayo ingeweza kumsaidia kulifanya jambo hilo hata kama malipo yangekuwa makubwa kiasi gani.<br />
<br />
“Niitie Ditrov,” alimwambia katibu muhtasi wake kupitia katika simu.<br />
“Sawa bosi!”<br />
Dakika tano baadaye mlango wa ofisi yake ulifunguliwa, akaingia mwanaume mfupi mwenye misuli aliyevalia suti ya rangi nyeusi pia, kwa kumtazama tu mtu yeyote angeamini lazima sehemu kubwa ya maisha yake ilitumika kubeba vyuma. Huyu ndiye alikuwa Ditrov mlinzi wa Victor Fedorov, ambaye historia yake ilihusisha mapambano katika vita vya Chechnya, kufanya kazi katika Shirika la Kijasusi la Urusi na kazi nyingi za hatari.<br />
<br />
“Ndiyo bosi.”<br />
“Nataka unisaidie.”<br />
“Niko tayari.”<br />
Victor alikwenda mbele na kumsimulia sehemu ya mkasa uliokuwa ukimkabili na kumwomba amsaidie kama alifahamu mtu yeyote nchini Urusi ambaye angeweza kufanya kazi ya kupeleleza mahali watoto wake walikokuwa, akamhakikishia kwamba angekuwa tayari kulipa kiasi chochote cha fedha ili mradi amweleze ni wapi watoto walipokuwa na ikiwezekana watekwe na kusafirishwa moja kwa moja hadi Urusi.<br />
<br />
“Inawezekana!”<br />
“Nani anaweza?”<br />
“Mimi.”<br />
“Kweli?”<br />
“Kabisa.”<br />
<br />
Baada ya mazungumzo ya muda wa karibu saa nzima, walikubaliana malipo ya dola laki moja na elfu hamsini ili kuhakikisha kwamba watoto hao wanapatikana, Victor alikubali na akaahidi kulipa kiasi cha dola elfu hamsini kama malipo ya utangulizi na baada ya hapo angeendelea kulipa dola elfu hamsini-hamsini mpaka fedha zote zikamilike lakini watoto wapatikane.<br />
<br />
Siku tatu baadaye kila kitu kilikamilika, malipo yakafanyika na Ditrov akapanda ndege na kuruka moja kwa moja hadi Ujerumani kwenye Jiji la Berlin kwenye kadi yake ya benki kukiwa na dola elfu hamsini, kwa fedha hiyo alikuwa na uhakika wa kupata kila taarifa muhimu juu ya watoto waliozaliwa kutoka kwenye kliniki ya Dk. Kohrer hata kama daktari huyo alikuwa hataki.<br />
<br />
Alitua kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Schonefeld saa kumi na mbili jioni kwa majira ya Ujerumani, hakuwa na mtu wa kumpokea, akachukua teksi na kumwamuru dereva ampeleke kwenye hoteli ya nyota tano na dereva huyo akampeleka katikati ya jiji ambako alipanga chumba ghorofa ya tano kwenye hoteli iitwayo Metropolitan, iliyoaminika kuwa ni ya gharama kubwa kuliko nyingine yoyote nchini humo.<br />
<br />
Baada ya chakula cha usiku na vinywaji kidogo kwenye baa ya hoteli hiyo, alipandisha hadi chumbani kwake ambako alitumia muda wa kama nusu saa kwenye mtandao akichunguza kliniki ya Dk. Kohrer, akagundua msichana wa mapokezi ambaye picha yake ilikuwa miongoni mwa picha za wafanyakazi wa kliniki hiyo aliitwa Nasha, kwa muonekana alionekana kama Msomali.<br />
<br />
“Huyu ndiye atanisaidia kujua ukweli ninaoutafuta,” alisema moyoni mwake na hakutaka kuendelea kuwaza tena, akavuta shuka yake na kujifunika gubigubi, dakika arobaini na tano baadaye alikuwa akikoroma na hakuamka mpaka kulipokucha asubuhi siku iliyofuata.<br />
<br />
Saa nne kamili alikuwa mapokezi ambako aliomba aelezwe utaratibu wa kukodisha gari ambalo angeendesha mwenyewe, akawashangaza wahudumu alipoulizia kama angeweza kupata Q7, gari la kifahari kupita kiasi, wakamwangalia kwa mshangao wakiwa hawaamini walichokisikia.<br />
<br />
“Q7?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Kwa nini Q7?”<br />
“Najua ni kwa nini.”<br />
“Twende,” mmoja wa wahudumu alimwita na kumchukua moja kwa moja hadi kwenye chumba ambacho mlangoni kiliandikwa maandishi: Metropolitan Car Hire.<br />
<br />
“Anataka gari la kukodi.”<br />
“Aina gani?”<br />
“Q7.”<br />
“Q7?” msichana aliyekuwa nyuma ya kaunta aliuliza.<br />
“Ndiyo.”<br />
“Hatuna Q7.”<br />
<br />
“Mna gari gani nzuri inayonifaa mimi na ya kifahari?”<br />
“Ferrari!”<br />
“Safi kabisa, inakodishwa kiasi gani kwa saa?”<br />
“Dola mia tano.”<br />
“Naitaka kwa saa ishirini na nne kazi yangu itakuwa imemalizika.”<br />
“Hakuna shida, unaweza kulipia.”<br />
<br />
Hawakuamini alipojaza fomu na baadaye kutoa kadi yake ambapo fedha zote za kulipia gari hiyo kwa saa ishirini na nne zilikatwa, akakabidhi hati yake ya kusafiria na kuonyesha leseni ya kimataifa ya udereva na hapo ndipo akapewa ufunguo wa gari na kuondoka moja kwa moja kuelekea ilikokuwa kliniki ya Dk. Kohrer, akiongozwa na kifaa maalum cha kuonyesha njia kilichokuwa ndani ya gari lake ambacho mtu aliandika jina la mahali alikokwenda kisha kilimwelekeza mitaa mpaka kumfikisha.<br />
<br />
Akaegesha gari mbele ya jengo kubwa la hospitali ya Freiburg na kushuka, kisha kutembea akiingia ndani ya jengo hilo mpaka mapokezi, haikumsumbua hata kidogo kumtambua Nasha, moyoni mwake akakiri msichana huyo alikuwa mrembo kupindukia.<br />
“How are you Nasha?”<br />
“I am fine and you?” (Mimi mzima wewe?)<br />
“I am fine too, do you remember me?” (Mimi mzima pia, unanikumbuka?)<br />
“Nop!” (Hapana)<br />
<br />
“I came here with my wife last year, you attended us very well, I am here to say thank you.” (Nilikuja hapa na mke wangu mwaka jana, ulituhudumia vizuri sana, nimekuja kukuambia ahsante.)<br />
“You are welcome!” (Karibu!)<br />
“Is doctor Kohrer in?” (Dk. Kohrer yupo?)<br />
“Yes, very busy though!” (Ndiyo, lakini ana kazi nyingi sana.)<br />
<br />
“Ok! Say hi to him! Can you come with me to my car? There is something I would like to hand you.” (Sawa, utamsalimia! Unaweza kunifuata kwenye gari? Kuna kitu ninataka kukupa.)<br />
<br />
“No problem!” (Hakuna shida) Nasha aliitikia na kuanza kumfuata Ditrov kwenda nje ambapo alifika na kufungua mlango wa gari, sauti ya Nasha kwa nyuma ikasikika akisema: “Oh! My God! You are riding a Ferrari? You must be very rich, you didn’t tell me your name sir?” (Oh! Mungu wangu! Unaendesha Ferrari? Lazima utakuwa tajiri sana, hukuniambia jina lako) Nasha aliongea akipokea bahasha kutoka kwa Ditrov, ndani yake kukiwa na dola elfu moja.<br />
<br />
“I am staying at the Metropolitan Hotel, please pass by for a cup of tea in the evening if you have time!” (Nimefikia Metropolitan Hotel, tafadhali ukipata nafasi jioni unaweza ukapita angalau tupate kikombe cha kahawa.)<br />
“No problem I will at 7:00!” (Hakuna tatizo nitapita saa moja.)<br />
“JOB DONE!” (Kazi imekamilika) Ditrov alijisemea moyoni mwake, akimkumbatia Nasha, wakaagana na akaondoka akimwacha amesimama mwenye mshangao.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf4e4674784645287"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501249cf49f728810387588">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.40.<br />
<br />
<br />
DITROV aliondoka akiendesha kwa mikogo Ferrari yake ya kukodi huku Nasha akimwangalia kwa mshangao, kwa tamaa zake msichana huyo alihisi hiyo ilikuwa ni bahati ya mtende iliyomwijia bila kutarajia. Hakuhisi kabisa kilichokuwa kikiendelea, kwake saa moja ya jioni ikaonekana ni kama mwaka kesho, alitaka muda huo ufike upesi ili achukue teksi na kwenda moja kw<span class="text_exposed_show">a moja hotelini kwa Ditrov, hakika alimtaka kwa udi na uvumba.<br />
<br />
“Warum hast du glucklich warden so plotzlisch”(Kwa nini umepata furaha hivyo ghafla?) msichana mwingine wa mapokezi alimuuliza Nasha.<br />
“Eine reiche person hat mich fur kafee eingeladen am Abend” (Mtu tajiri amenikaribisha kahawa jioni)<br />
“Vorsichtig sein.”(Uwe mwangalifu)<br />
“Ich beginne, ihn zu lieben” (Nahisi nimeanza kumpenda).<br />
<br />
Saa zilitembea taratibu mno siku hiyo, hatimaye saa 12:30, muda wa kutoka kazini ukawadia, Nasha akasaini kitabu na kubeba mkoba wake kwapani na kutembea hadi nje, kichwani mwake akimfikiria Ditrov tu, alihisi ndiye mwanaume wa ndoto yake ambaye kwa kipindi kirefu alikuwa akimsubiri na alitamani awe hajaoa ili baadaye amtamkie kwamba alitaka kuwa mume wake.<br />
<br />
Nje alipanda ndani ya teksi na kumwelekeza dereva ampeleke Metropolitan Hoteli ambayo ilikuwepo umbali wa nusu kilometa kutoka ilipokuwa kliniki ya Dk. Kohrer, dakika kumi baadaye waliegesha mbele ya jengo la hoteli hiyo, Nasha akalipa kisha kushuka na kunyoosha moja kwa moja hadi mapokezi.<br />
<br />
“Ich hier, um zu treffen Herr Ditrov” (Niko hapa kumuona bwana Ditrov)<br />
“Fur einem Moment zu warten”( Subiri muda kidogo) aliongea msichana huyo wa mapokezi na kupiga namba ya simu, akasikika akiongea na mtu upande wa pili, alipoweka simu chini alimwita kijana aliyekuwa kando yake ambaye alivalia suti nyeusi ya vipande vitatu na kumwomba ampeleke Nasha chumbani kwa Ditrov.<br />
<br />
kwa msaada wa lifti walipandisha hadi ghorofani ambako kengele iligongwa mlangoni, Ditrov akiwa kwenye taulo tu akafungua, moyo ukamwenda mbio Nasha alipomtazama jinsi mwili wake ulivyojazia sababu ya mazoezi, hakuonekana kama mzee, kifupi alimvutia kimapenzi. Mlango ulipofungwa nyuma yao, Ditrov alimshika mkono na kuanza kumvuta kumpeleka kitandani, akamsukuma na kumlaza chali.<br />
<br />
“You know what?”(Unajua nini?)<br />
“No!”(Hapana)<br />
“I love you and I want us to have sex”(Nakupenda na nitaka tufanye ngono)<br />
“Just like that?”(Hivyo tu?)<br />
“Yeah!” (Ndiyo)<br />
“No! Lets talk first!”(Hapana! Tuongee kwanza)<br />
<br />
Ditrov ambaye tayari alishavua taulo na kulitupa pembeni alisitisha zoezi na kuketi kando ya Nasha kisha kuanza kumwambia maneno ya mapenzi akieleza jinsi alivyompenda baada ya kumwona tu pale kliniki na hakuwa tayari kumpoteza msichana mrembo kama yeye.<br />
“I am ready to do anything but have you!”(Niko tayari kufanya lolote niwe na wewe!)<br />
“Are still married?”(Bado umeoa?)<br />
<br />
“No! I divorce my wife last year, right now I am looking for a woman with lucky, I think you’re the one”(Hapana! Nilimtaliki mke wangu mwaka jana, sasa hivi natafuta mwanamke mwenye bahati, nafikiri ni wewe) aliongea Ditrov akitabasamu.<br />
“Sure?”(Hakika?)<br />
“Yeah!”(Ndiyo)<br />
<br />
Maneno hayo yalimlainisha kabisa Nasha, akahisi kuishiwa nguvu mwilini mwake, ghafla akajiona mwenye bahati kuliko wanawake wengine wote chini ya jua ambayo hakutaka ipotee. Akamruhusu Ditrov azungushe mkono wake begani na kuanza kumpapasa taratibu nyuma ya shingo. Kitu kama umeme wenye nguvu kali, ukapita mwilini mwake na kumpiga shoti, akazidi kulegea, mhemo wake ukabadilika na taratibu akalazwa kitandani na kuanza kuvulishwa nguo alizokuwa nazo mpaka akabaki mtupu.<br />
<br />
Kilichofuata baada ya tukio hilo, hakielezeki, hakuwahi tangu azaliwe kukutana na mwanaume kama Ditrov, alihisi ni kwa sababu ya mazoezi aliyoyafanya. Ni kweli alikuwa na mchumba aliyetarajia kuolewa naye lakini kama Ditrov angetaka kumuoa na kuondoka naye kwenda Urusi, alihisi alikuwa tayari kwa hilo bila kuogopa lawama.<br />
“Ditrov!”<br />
“Yes” (Ndiyo)<br />
<br />
“Can I tell you something?”(Naweza kukueleza kitu?)<br />
“Go ahead”(Endelea)<br />
“You are good!” (Wewe ni mtaalam)<br />
“In?”(Katika?)<br />
“Love making!”(Kufanya mapenzi)<br />
<br />
“Thank you, that is just a beginning, lets take a fifteen minutes break and then I will show you who I am!”(Ahsante, huo ni mwanzo, tupumzike kwa dakika kumi na tano halafu nitakuonyesha mimi ni nani?)<br />
“Oh! My God! That’s just a beginning? You gonna kill me”(Oh! Mungu wangu! Huo ni mwanzo tu? Utaniua.)<br />
“No! You will enjoy it!”(Hapana! Utafaidi)<br />
Nusu saa iliyofuata ndani ya chumba hicho ilikuwa ni vilio na kelele zilizowasumbua mpaka watu wa vyumba vingine, Nasha alikuwa katika hali ambayo hakuwahi kukutana nayo, Ditrov akiwajibika ipasavyo, ghafla akasitisha huduma na kumwangalia Nasha machoni ambaye tayari alikuwa taaban akielekea mwisho wa safari yake.<br />
<br />
“Usiache!” Nasha alipiga kelele.<br />
“Listen, I want you to do me one favour!”(Sikiliza, nataka unifanyie upendeleo mmoja)<br />
“What is that favour baby? I can do anything for you, I love you so much Ditrov, you name it, I do it!”(Kitu gani hicho mpenzi? Naweza kufanya chochote kwa ajili yako, nakupenda mno Ditrov, ukikitaja tu nakifanya)<br />
<br />
“ I need one file from Dr. Kohrer’s Clinic!”(Nahitaji faili moja kutoka kwenye kliniki ya Dk. Kohrer)<br />
“Whose file is that?”(Faili la nani?)<br />
“A guy named Victor Federov, who donated sperms to a certain couple few years ago!”(La mtu aitwaye Victor Federov ambaye alitoa mbegu zake za kiume kwa wanandoa fulani miaka michache iliyopita)<br />
“When do you need it?”(Unalihitaji lini?)<br />
“Tomorrow!”(Kesho)<br />
<br />
“I will do that in the morning!”(Nitafanya hivyo asubuhi)<br />
“Thank you!” (Ahsante)<br />
Ditrov hakumwachia Nasha, usiku mzima alimfanyia mambo ambayo msichana huyo hakuwahi kukutana nayo, kifupi hawakulala na wala Nasha hakukumbuka kwenda nyumbani kwake. Saa mbili asubuhi ndiyo aliamka na kuanza kujiandaa, sababu hakutaka kwenda kazini na nguo zile zile, Ditrov alishuka hadi ghorofa ya chini ambako alimnunulia nguo nyingine mpya na kumletea, akavaa na kumbeba kwa gari hadi kliniki ambako alimwacha na kurejea hotelini.<br />
<br />
Saa nne kamili, simu chumbani kwa Ditrov iliita, akaikimbilia haraka na kuipokea. Ilikuwa ni sauti ya Nasha akipiga simu kutoka kliniki na kumtaarifu kwamba alishalipata faili hilo, Ditrov akamwomba alitoe kopi ili akienda hotelini ampelekee nakala.<br />
“It is an electronic file!”(Ni faili la kielekroniki) alijibu Nasha akimaanisha faili hilo lilikuwa kwenye kompyuta.<br />
<br />
“That is even better, send to my email now”(Hiyo ni nzuri zaidi, nitumie kwa barua pepe sasa hivi)<br />
“Five minutes!”(Dakika tano)<br />
Hivyo ndivyo ilivyotokea, dakika tano baadaye Ditrov alipofungua sanduku lake la barua pepe alikuta faili limetumwa, akafungua na kuanza kulisoma, hakuamini alichokishuhudia, kazi ilikuwa imekuwa rahisi kuliko alivyofikiria. Akafunga kompyuta yake na kulisogelea begi lake, haraka akalifungua na kuanza kukusanya kitu kimoja baada ya kingine akikiweka ndani ya begi.<br />
<br />
***<br />
Saa tano kamili Nasha alitoroka kazini kwake na kwenda moja kwa moja hotelini Metropolitan, lengo likiwa ni kwenda kumwona Ditrov, akili yake ilishachanganyikiwa kabisa, kazi zilikuwa hazifanyiki. Taswira ya mwanaume huyo ilikuwepo kila mahali, alitaka amwone tena kabla hajaendelea na kazi.<br />
Mapokezi hakuongea na mtu, akapitiliza moja kwa moja kwenye lifti na kwenda hadi chumbani ambako alikuta mlango umefungwa, akagonga kwa muda bila kufunguliwa. Alipohakikisha Ditrov hakuwemo chumbani ndipo akaamua kwenda mapokezi kuulizia.<br />
<br />
“Ameondoka!”<br />
“Ameondoka?”<br />
“Ndiyo”<br />
“Siyo kweli”<br />
“Amesaini hapa”<br />
Je, nini kitaendelea? Fuatilia kesho hapa hapa UNLIMITED SWAGGAZZ PAGE BILA KUSAHAU KUGONGA LIKE ILI NIKIPOST ZIKUFIKIE</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.41.<br />
<br />
Baada ya kuhangaika kwa muda mrefu katika ndoa bila kupata mtoto, Phillip na Genevieve wanaamua kusafiri hadi Ujerumani ambako kwa msaada wa Dk. Kohrer, inagundulika kuwa mbegu za Phillip hazina uwezo wa kurutibisha yai la mwanamke, hivyo Dk. Kohrer anaamua kununua mbegu kutoka kwa mwanaume masikini wa Kirusi, Victor Fedorov.<br />
<br />
Watoto pacha (Dorice na Dorica) <span class="text_exposed_show">wanazaliwa miezi tisa baada ya mbegu za Victor kuunganishwa na yai la Genevieve katika utaalamu uitwayo IVF (In Vitro Fertilization). Furaha inarejea kwa Phillip na mkewe Genevieve ingawa kilichotokea kinabaki kuwa siri ili kumlindia Phillip heshima yake. Wanawatunza watoto wao vizuri mpaka wanafikia umri wa kuanza darasa la kwanza, siku ya kwanza tu kupelekwa shule, basi ambalo ndani yake Dorice na Dorica walipanda wakiwa na watoto wengine kumi na nane lilipuka kwa bomu na watoto wote kuaminika kufa lakini mabaki yaliyopatikana ni ya watoto kumi na sita tu. Hesabu hizo zikazua kitendawili.<br />
<br />
Miaka michache baadaye, masikini Victor Fedorov maisha yalimbadilikia na kujikuta akiwa tajiri lakini asiye na mtoto, wanawake wote aliowaoa na kuwaacha walishidwa kumzalia hata mtoto mmoja. Hii ilimfanya akumbuke mbegu zake na kuamua kutumia fedha nyingi kutafuta mahali mbegu zake zilikotumika.<br />
<br />
Akampa kazi hiyo mlinzi wake, Ditrov, ili apeleleze na akafanikiwa kulipata faili kutoka kwenye kliniki ya Dk. Kohrer nchini Ujerumani baada ya kumdanganya msichana wa mapokezi aitwaye Nasha, ambaye amerejea hotelini kwa Ditrov na kukuta amekwishaondoka.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
KITU cha kwanza alichokifanya Ditrov bila kupoteza muda baada ya kulipata faili ni kumpigia simu Victor Fedorov kumtaarifu juu ya ushindi alioupata ndani ya muda mfupi, Victor alifurahi mno akiwa haamini alichokuwa akiambiwa. Mara moja akamtaka Ditrov apande ndege na kuruka hadi Moscow ambako angeunganisha ndege nyingine na kusafiri hadi Novotroisk, safari ambayo ingemchukua saa kumi na mbili.<br />
<br />
“Hakikisha unafika hapa ndani ya muda huo, kweli umepata faili?”<br />
“Ndiyo bosi, utakuja kuona.”<br />
“Tafadhali njoo, umenifurahisha mno, lazima nikupe motisha.”<br />
“Hakuna shida, nakuja.”<br />
<br />
Saa mbili baadaye Ditrov alikuwa ndani ya ndege ya Shirika la Ndege la Urusi akikatisha mawingu, fikra zake zilitawaliwa na kazi iliyokuwa mbele yake, ni kweli alikuwa amefanikiwa kujua mahali watoto wa Victor Federov walikokuwa lakini hakufahamu njia ambayo angeitumia kuwachukua na kuwasafirisha mpaka Urusi bila matatizo yoyote.<br />
<br />
Kompyuta yake ndogo ikiwa imefunguliwa, akiendelea kulisoma taratibu faili alilotumiwa ili apate kulielewa vizuri; Dar es Salaam, Tanzania, Upanga, Ally Khan Street, House Number 122, Phillip and Genevieve Mpangala. Alisoma maelezo hayo mara kwa mara akijiridhisha kisha kuitafuta ramani ya Jiji la Dar es Salaam iliyopigwa kwa setelaiti, akauona mtaa wa Ally Khan na kuanza kuitafuta nyumba namba 122 mpaka akaipata.<br />
<br />
“Lazima watakuwa matajiri pia, nyumba kubwa sana hii,” aliwaza Ditrov ndege ikizidi kusonga mbele.<br />
Saa tano baadaye, ndege ilianza kushuka na hatimaye kutua kwenye uwanja wa ndege wa Domodedovo ambako alishuka na kufanya taratibu za kuunganisha na ndege nyingine ya shirika hilo hilo iliyompeleka mpaka Novotroisk,<br />
Nje ya uwanja alipokelewa na Victor ambaye uso wake ulijawa na furaha. Wakaingia ndani ya gari aina ya Benz nyeusi na kuondoka hadi ofisini kwa Victor ambako kitu cha kwanza ambacho Victor alichotaka kukiona ni faili, Ditrov akafungua kompyuta yake na kuanza kumwonyesha kila kitu alichokipata.<br />
<br />
“Una uhakika ni wenyewe?”<br />
“Asilimia mia bosi.”<br />
“Hebu twende kwenye mtandao wa Google, tuangalie kama wana maelezo yoyote yanayowahusu.”<br />
“Hakuna shida,” alijibu Ditrov na kuutafuta mtandao huo mpaka akaupata na kuandika majina ya Phillip, Genevieve, Upanga Tanzania na kubonyeza kitufe kilichoandikwa Enter.<br />
<br />
Taarifa za Phillip na Genevieve tangu wakisoma chuo kikuu na baadaye kufunga ndoa zikaonekana, upande wa picha ilionekana ile waliyopiga kama familia na watoto wao wawili pacha, chini yake ikiwa imeandikwa “A wonderful and happy family of Mr Phillip and Mrs Genevieve”. Moyo wa Victor uliruka mapigo kadhaa baada ya kuiona picha hiyo.<br />
<br />
“Ndiyo, hawa ni watoto wangu.”<br />
“Wanafanana nawe kupita kiasi!”<br />
“Kabisa, ndiyo wenyewe kwa gharama yoyote ile nawataka hapa Urusi, unanisikia Ditrov?”<br />
“Nakusikia bosi. Unawataka lini?”<br />
<br />
“Nawataka jana!” alisema tajiri Victor akionesha ni kiasi gani aliwataka watoto wake, kiasi cha kufikiri wangekuwa hapo kuanzia jana yake.<br />
“Hakuna shida.”<br />
“Utafanyaje?”<br />
“Kwa hivi sasa sina jibu, nipe muda mpaka kesho niwasiliane na watu wangu.”<br />
<br />
“Hakuna shida, lakini naomba uelewe kwamba furaha yangu haiwezi kutimia kama watoto hawa sitawapata.”<br />
“Nitakuja na jibu zuri bosi wangu,” Ditrov akajibu kisha kuaga na kuondoka zake.<br />
<br />
Kufanya kazi ndani ya shirika la kijasusi la Urusi kwa miaka mingi kabla ya kuacha na kuajiriwa na Victor, kulimpa Ditrov nafasi ya kufahamiana na watu wengi waliojihusisha na ujasusi, miongoni mwao akiwemo Dimitri Coscov kiongozi wa kundi la uasi la Chechnya. Huyu ingawa alikuwa adui mkubwa wa Urusi, kwa upande wa Ditrov alikuwa rafiki yake mkubwa. Kitu cha kwanza alichokifanya baada ya kuondoka ofisini kwa Victor ni kumpigia simu.<br />
<br />
“Nina tatizo, nahitaji utaalamu wako kulitatua.”<br />
“Tatizo gani?”<br />
“Sitaki kuongea kwenye simu, napanda ndege sasa hivi kuja Grozny.”<br />
“Karibu.”<br />
<br />
Kesho yake majira ya jioni tayari alisharejea Novotroisk na kumpigia simu Victor ili kujua mahali alipokuwa, alikuwa bado yuko ofisini kwake kitini akiwafikiria watoto wake. Taarifa kwamba Ditrov alisharejea zilimfurahisha akamtaka afike ofisini mara moja ili aeleze mpango aliokuwa nao.<br />
“Tayari ninalo jibu.”<br />
“Naomba unieleze.”<br />
<br />
“Gharama yake ni kubwa lakini.”<br />
“Gharama siyo muhimu, cha muhimu ni watoto wangu.”<br />
“Tumegundua kwamba watoto hao wanaitwa Dorice na Dorica, wanategemewa kuanza darasa la kwanza wiki mbili zijazo. Ambacho tumepanga mimi na wenzangu tutakaofanya kazi hii ni kwenda huko Tanzania na kuthibitisha yote tuliyoyagundua, hatutaki kuamini mtandao moja kwa moja, tukishathibitisha kwamba ni kweli, watoto hao watatekwa siku watakayokuwa wanakwenda kuanza darasa la kwanza na wataletwa mpaka hapa Urusi.”<br />
<br />
“Mtafanyaje ili isijulikane?”<br />
“Watu ninaofanya nao kazi sitaki kukuficha ni waasi wa Chechnya ambao tumekubaliana kusafiri nao hadi Tanzania, ili kuudanganya ulimwengu, basi ambalo watoto hao watapanda litalipuliwa kwa bomu la kutengenezwa na waasi humo humo nchini Tanzania!”<br />
<br />
“Kwa hiyo na watoto wangu watafia kwenye basi hilo?”<br />
“Hapana wao watatolewa sekunde chache kabla basi halijalipuliwa kwa bomu, kitakuwa ni kitendo cha haraka, watu hawatakumbuka sababu ya hofu itakayowapata bomu likilipuka.”<br />
“Watasafirishwaje hadi hapa?”<br />
<br />
“Tulifanya utafiti na kugundua kuna ndege huwa zinasafirisha madini kutoka kwenye mgodi uitwao Deep Search Mining Company ambao uko katika mji mdogo uitwao Geita mkoani Mwanza. Ndege huwa zinaruka moja kwa moja kutoka mgodini hadi Canada, na tayari tumekwishafanya mazungumzo na mmoja wa marubani kwa malipo ya dola laki mbili ili baada ya kuwateka watoto hao wachukuliwe kwa ndege ya kukodi hadi mgodini na kupakiwa kwenye ndege itakayokuwa inaruka kwenda Canada. Huko tutakodisha ndege nyingine itakayoruka mpaka hapa, unauonaje mpango wetu?”<br />
<br />
“Uko sawa, lakini swali moja najiuliza, kuna namna yoyote ile ya kuwafanya watoto hao wasiwe na kumbukumbu kabisa ya mahali walipotoka?”<br />
“Tumelifikiria hilo bosi na uamuzi tulioufikia ni kwamba, baada tu ya kutekwa, watachomwa sindano ya dawa ya usingizi iitwayo Memory Eraser ambayo kazi yake ni kufuta kumbukumbu kwenye ubongo wa mwanadamu ili asikumbuke alikotoka fahamu zikimrejea.”<br />
“Dawa hiyo ipo?”<br />
<br />
“Ipo. Waasi wa Chechnya wanaitumia sana kupata wapiganaji, hiyo ndiyo tutatumia.”<br />
“Oh! Ahsanteni sana, kwa utaratibu huo nimewapata watoto wangu.”<br />
“Lakini gharama ya kazi yote hiyo ni dola milioni moja.”<br />
“Nitawaongezea laki mbili juu yake kama mtafanikiwa kuwafikisha watoto hapa.”</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124aac2aca62049489878">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.42.<br />
<br />
SIKU tatu baada ya kukamilika kwa mazungumzo kati ya Ditrov na Victor, tayari kundi la vijana tisa lilikuwa likishuka ndani ya ndege ya shirika la ndege la Urusi kwenye uwanja wa ndege wa Dar es Salaam, walionekana kama watu waungwana au wawekezaji waliokuja nchini Tanzania kuleta neema, jambo ambalo halikuwa kweli.<br />
<br />
Walikuwa ni waasi wa kundi la Chechnya waliok<span class="text_exposed_show">odiwa na Ditrov kwa kazi moja tu; kuwateka Dorice na Dorica na kuwasafirisha hadi kwenye mji wa Novotroitsk na kuwakabidhi kwa Victor, kazi yao ingekuwa imekwisha na kukabidhiwa kitita kisha kurejea Grozny.<br />
<br />
Mzungu mmoja ndiye aliyewapokea kwenye uwanja wa ndege, shati lake la khaki likiwa na nembo iliyoandikwa Deep Search Mining Limited. Alikuwa ni Meneja Mkuu wa mgodi huo uliokuweko katika mji wa Geita. Baada ya mazungumzo ya muda mrefu kwenye simu na kuingiziwa na Victor kiasi cha dola laki mbili kwenye akauti yake nchini Afrika Kusini, mzungu huyu alikuwa amekubali kuwasaidia Ditrov na vijana wake kukamilisha kazi iliyowaleta. <br />
<br />
“My name is Mike Eaglewood. You are all welcome to Tanzania.” (Naitwa Mike Eaglewood. Wote mnakaribishwa Tanzania.)<br />
“Thank you, a nice country.” (Asante, nchi nzuri.)<br />
Wakatembea mpaka kwenye maegesho ya magari na kupanda ndani ya gari aina ya Combi, Mike akaketi kwenye usukani na kuendesha taratibu mpaka maeneo ya Masaki nyumbani kwake. Ilikuwa ni nyumba kubwa na aliishi peke yake, hiyo ilimfaa Ditrov na vijana wake sababu walihitaji usiri wa hali ya juu hasa katika kazi ya kutengeneza bomu ambalo lingelipua basi lililobeba watoto wa shule.<br />
<br />
Kilichofanyika nusu saa baada ya kuingia ndani ya nyumba hiyo, hakikuwa kingine isipokuwa kikao cha kupanga mikakati ya utekelezaji, Mike akiwahakikishia kila kitu kingekwenda kama kilivyopangwa. Makubaliano yakafanyika kwamba yakodishwe magari mawili aina ya Benz ambayo yangetumiwa na kikosi hicho siku ya utekaji lakini pia kupeleleza mienendo ya familia ya Phillip.<br />
<br />
Pia uamuzi ukafikiwa kwamba baada ya watoto kutekwa, wangesafirishwa kwa njia ya barabara ndani ya kontena lililofungwa viyoyozi wakiwa tayari wamechomwa sindano ya kupoteza kumbukumbu hadi Geita ambako ndege ingekuwa imeandaliwa kwa ajili ya kuwabeba na kuruka nao moja kwa moja hadi Canada.Victor akaamua kuongeza dola nyingine laki tano kwenye milioni moja aliyokwishatoa ili kufanya zoezi hilo lifanyike kwa urahisi.<br />
“Zoezi la utekaji litafanyika siku gani?” Mike aliuliza.<br />
<br />
“Siku watoto watakapokuwa wanapelekwa shuleni.” Ditrov akajibu.<br />
“Mnaijua hiyo siku?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Mnaijuaje wakati nyie ndiyo mmewasili Tanzania?”<br />
“Phillip na Genevieve wana blog yao, kila kitu wanachokifanya huwa wanaweka huko. Tumesoma mtandaoni.”<br />
<br />
“Itakuwa siku gani?”<br />
“Tarehe kumi na nne, kama siku kumi na mbili kuanzia sasa.”<br />
“Tarehe tisa kuna kontena mbili zinaondoka hapa kwenda mgodini, tunaweza tukapakua mizigo kwenye moja ya kontena hizo na kupakia kwenye lori, halafu kontena hilo tukalifunga viyoyozi kisha tarehe kumi na nne kama mambo yatakwenda vizuri, tukaondoka na watoto hadi mgodini ambako tarehe kumi na tisa kuna ndege inaondoka kwenda Canada.”<br />
<br />
Wote wakakubaliana juu ya mpango huo na Ditrov akajitolea kusafiri na watoto ndani ya kontena akiwalisha mpaka wafike Geita, kilichofuata baada ya hapo ni kazi ya kulitengeneza bomu, vijana wawili kati ya tisa kwenye kundi hilo walikuwa ni wataalam wa kutengeneza mabomu ya petroli yanayoweza kutegwa na kulipuka baada ya muda uliopangwa.<br />
<br />
Kazi ya kutengeneza bomu kwa vifaa vilivyonunuliwa kwenye maduka na vituo vya mafuta jijini Dar es Salaam, ilikamilika siku ya tarehe kumi na tatu huku upelelezi juu ya shule ambayo watoto walitakiwa kupelekwa na gari asubuhi ya tarehe kumi na nne pia ukiwa mezani. <br />
<br />
Kwa kutumia ushawishi wa fedha, Ditrov na kundi lake wakijifanya wafadhili walimzoea dereva wa gari hilo mpaka akawapa ratiba kamili ya kazi yake kwa siku na mahali alipoliegesha gari hilo baada ya kazi na kurejea nyumbani.<br />
<br />
Ilikuwa ni kwenye ofisi ya CCM karibu kabisa na nyumbani kwake Magomeni Mapipa ambako pia walihakikisha wanaonekana kwa walinzi ili iwe rahisi kwao kurejea usiku na kutega bomu ndani ya gari bila kutiliwa mashaka wakijifanya walikuwa wakilirekebisha kabla dereva hajafika.<br />
<br />
Kwa ushawishi huohuo wa fedha walimfanya mlinzi wa ofisi ya CCM asiwatilie mashaka, watano wakiwa wamemzubaisha kwa maongezi walipofika alfajiri kumwuulizia dereva, wanne walikuwa kwenye gari, wawili kati yao wakitega bomu chini ya gari hilo huku kifaa kiitwacho Ignitor ambacho waya wake uliounganishwa kwenye betri ya gari na kuanza kuzunguka kikihesabu saa tayari kwa bomu hili kulipuka mara tu Dorice na Dorica wakipakiwa ndani ya gari hilo.<br />
<br />
Baada ya kazi hiyo waliingia ndani ya magari yao mawili aina ya Benz, wakimsubiri dereva ambaye kwa ratiba aliyowaeleza, gari lake lingeifika Upanga saa mbili asubuhi kwenye kituo ambacho Dorice na Dorica wangetakiwa kupanda.Walianza kulifuata taratibu kwa nyuma na kushuhudia likipakia watoto kituo kimoja baada ya kingine mpaka idadi ya watoto kumi na sita wakapanda, tayari likafika kwenye kituo cha Upanga ambako walimuona Genevieve amesimama na watoto wake, taratibu akatembea na kuwapakia gari liliposimama kisha kuanza kuwapungua mkono, jumla ya watoto kumi na nane wakawemo ndani ya gari hilo.<br />
<br />
Benz moja likapita na kwenda mbele ambako lilisimama ghafla kulizuia gari la shule na Ditrov akiwa na mmoja kati ya vijana wake wa kazi alishuka akiwa na bastola mkononi na kwenda moja kwa moja kwenye dirisha la dereva na kumwekea shingoni huku kijana mwingine akifungua mlango na kuwatoa Dorice na Dorica kisha kuwakimbiza kwenye gari lao, kilikuwa ni kitendo cha haraka mno kilichochukua sekunde kadhaa kiasi kwamba watu wengi waliokuwa jirani hawakushuhudia.<br />
<br />
Hazikupita hata dakika tatu, bomu likalipuka huku magari mawili aina ya Benz yakiondoka kwa kasi, ndani ya moja ya magari hayo Dorice na Dorica walikuwa wakipiga kelele huku wakichomwa sindano. Dakika chache baadaye walikuwa wakikoroma na safari iliendelea hadi Masaki, huko waliingizwa ndani ya kontena lenye viyoyozi, likafungwa na safari ikaanza.<br />
<br />
Ulikuwa ni msafara wa makontena mawili mbele yakiwa yamebandikwa maandishi makubwa yaliyosomeka “POISON IN TRANSIT” kuonyesha kwamba ndani yake kulibebwa sumu, hii iliwafanya maaskari njiani washindwe kuyasimamisha. Dorice na Dorica walikuwa ndani wakisafirishwa huku watu wote wakiwemo wazazi wao wakidhani walikufa kwenye mlipuko wa bomu.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124aac2a09d7f53361626">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.43.<br />
<br />
<br />
LILIKUWA ni tukio la kusikitisha, watu wengi walioona habari hiyo ya kulipuka kwa basi la wanafunzi na kuua watoto kumi na nane walilia machozi.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Tanzania ilikuwa imepatwa na msiba mkubwa ambao haukuwahi kutokea kabla, mpaka vyombo vikubwa vya habari duniani kama CNN, Sky News na BBC vilitangaza tukio hilo likidaiwa ni la kigaidi na kuhusishwa na Osama bin Laden, hakuna mtu hata mmoja aliyejua kilichotokea, kwamba mwenye watoto wake alikuwa ameamua kuwafuata. <br />
<br />
Polisi walikuwa kazini usiku na mchana katika jiji la Dar es Salaam, mipaka yote ikiwa imefungwa, mamia ya vizuizi yakiwa yamewekwa barabarani, ukaguzi katika kiwanja cha ndege cha Mwalimu Nyerere ukiwa umeongezeka, upekuzi kwenye nyumba za wageni ukifanyika usiku na mchana kuwasaka watu waliohusika na tukio hilo ambalo kwa maelezo ya mashuhuda, walikuwa ni wazungu.<br />
<br />
Juhudi zote hizi zikiendelea bila mafanikio, gari lililobeba kontena ambalo ndani yake walikuwemo Dorice na Dorica lilizidi kukata mbuga, likipita mikoa ya Morogoro, Dodoma, Singida hatimaye likafika Isaka mkoani Shinyanga na kukata kona kuelekea Kahama ambako lingenyoosha moja kwa moja hadi mgodini Geita.<br />
<br />
Hakuna askari aliyediriki kunyosha mkono wake hewani kulisimamisha baada ya kuona maandishi ya POISON IN TRANSIT, wote waliamini ni sumu iliyokuwa ikisafirishwa kwenda pengine nchi za Rwanda, Burundi, Congo au migodini.<br />
“Sumu hiyo.”<br />
<br />
“Inawezekana inapelekwa migodini kwa ajili ya kulipulia miamba.”<br />
“Ndiyo, hawa wazungu wanaleta tu sumu ambayo mwisho wa siku inaingia kwenye maji yetu ya kunywa na kutusababishia kansa.”<br />
“Kwani unadhani wao wanajali sana afya zetu, cha muhimu kwao ni dhahabu, basi!”<br />
<br />
“Inabidi serikali yetu ndiyo itulinde sisi wananchi.”<br />
Hayo yalikuwa ni maongezi ya maaskari wa usalama barabarani na maafisa wa Mamlaka ya Mapato waliolishuhudia kontena likipita mbele yao,bila kuelewa kuwa kitambaa chenye maandishi kuonyesha ndani kulikuwa na sumu kilikuwa ni geresha, kwani kama wangelisimamisha na kuomba lifunguliwe wangemkuta Ditrov akipulizwa na kiyoyozi huku watoto wawili wakiwa wamelala bila fahamu kando yake.<br />
<br />
Siku tatu baada ya kuondoka Dar es Salaam, gari hilo liliingia ndani ya ngome ya mgodi wa Deep Search Mining Limited usiku wa manane, wafanyakazi wengi wakiwa wamelala na Bwana Mike Eaglewood,<br />
<br />
Mkurugenzi wa mgodi huo ambaye alielewa kila kitu kilichoendelea baada ya kupewa kitita cha fedha aliwaongoza mpaka kwenye uwanja wa ndege wa mgodi huo ambako ndege iliyokwishapakiwa shehena ya mchanga wa dhahabu kwa ajili ya kupelekwa Canada ilikuwa ikisubiri.<br />
<br />
“Quickly!” (Haraka!) Bwana Eaglewood aliongea kwa sauti ya kuonyesha kwamba hapakuwa na muda wa kupoteza, kila kitu kilikuwa ni muhimu kifanyike kwa kasi ili ndege iruke kutoka kwenye uwanja huo akidai ilikuwa iimechelewa.<br />
“Yes sir!” (Sawa mkuu.) alijibu Ditrov akimalizia kuwachoma Dorice na Dorica sindano ya kuharibu kumbukumbu.<br />
<br />
Watoto hao wakashushwa wakiwa hawajui kinachoendelea na kupakiwa ndani ya ndege, kisha Ditrov na vijana wake pia wakaingia, cha kwanza alichokifanya ni kuwasiliana na Victor Fedorov na kumtaarifu juu ya mafanikio waliyoyapata na kumtaka aandae ndege ya kukodi kutoka Ottawa Canada kwenda Moscow ambako pia walitakiwa wakute ndege nyingine ya kukodi ambayo ingewapaleka moja kwa moja hadi kwenye mji wa Novostroitsk ambako Victor angewapokea.<br />
<br />
Hayo ndiyo yakawa makubaliano na Victor akawahakikishia kwamba kila kitu kingekwenda kama walivyopanga, akiwaeleza kuwa alichohitaji si kingine isipokuwa watoto wake. Hivyo alikuwa tayari kutumia kiasi chochote cha fedha nje ya makubaliano ya awali ili mradi Dorice na Dorica waingie mikononi mwake, hicho ndicho kitu pekee alichoamini kingempa furaha.<br />
<br />
Dakika kumi na tano baadaye injini za ndege ziliwashwa, mapanga yakaanza kuzunguka na ndege ikaanza kusogea mbele kisha kupaa na kuiacha ardhi ya Tanzania, Ditrov akatabasamu akiwaangalia wenzake.<br />
<br />
“Give me five, mission accomplished.” (Nipe tano, mpango umekamilika.) akaongea Ditrov akiinua mkono wake wa kuume juu na kuanza kugonganisha na wenzake.<br />
<br />
Ilikuwa ni safari ndefu yenye kuchosha lakini wao waliiona kuwa fupi sababu muda wote walikuwa wakinywa pombe, kuimba na kushangilia, fedha ambayo walikuwa wanakwenda kulipwa na Victor Fedorov ilikuwa kubwa mno, maisha yao yasingekuwa kama yalivyokuwa, wote waliamini tangu siku hiyo wangemiliki biashara kubwa na kujiepusha na mambo ya ugaidi.<br />
<br />
Saa kumi na tatu baadaye walitua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ottawa ambako muda mfupi tu baada tu ya ndege kutua na injini kuzimwa, mwanaume mrefu mwembamba aliingia kwenye ndege akiwa amevaa suti nyeusi na kuwaangalia watu wote walioketi vitini, kisha akamgusa Ditrov begani, ilivyoonekana alikuwa na maelezo ya kutosha kabisa ya mtu aliyekuwa akimtafuta.<br />
<br />
“Carry the children and follow me!” (Bebeni watoto na mnifuate.) aliongea mwanamume huyo.<br />
<br />
“Ok!” (Sawa.) Ditrov akaitikia na kunyanyuka alipokuwa ameketi na kuzunguka kiti cha kwanza, akambeba Dorice na kumuomba mmoja wa vijana wake ambebe Dorica, wakashuka hadi chini kulikokuwa na gari maalumu na kupanda,likaondoka na kutoka nje ya uwanja kupitia mlango wa nyuma na kuendeshwa hadi kwenye uwanja mwingine mdogo wa ndege ambako walipanda katika ndege ambayo nusu saa baadaye iliruka wakiwa pamoja na mwanaume aliyewaongoza.<br />
“Where to?” (Tunaelekea wapi?) Ditrov aliuliza.<br />
“Moscow.”<br />
<br />
“Thank you.” (Asante.)<br />
Watoto walikuwa bado wako usingizini, mpaka wakati huo walikuwa hawajaweka chakula chochote mdomoni, hata maji ya kunywa. Safari yao ilitegemewa kuwachukua muda wa masaa matano ndiyo watue kwenye uwanja wa ndege wa Sheremetyevo, jijini Moscow.<br />
<br />
Kwa maelezo ya mtu aliyekuwa anawaongoza, ndege nyingine ya shirika hilo hilo la kukodisha ingewapeleka moja kwa moja hadi Novotroitsk na hapo ndio ungekuwa mwisho wa safari yao. Ditrov na watu wake walikuwa na furaha mno, walikuwa wakisubiri kitu kimoja tu mbele yao; kufika na kukabidhiwa kitita, kisha kusambaa.<br />
***<br />
Ilikuwa yapata majira ya saa tatu na nusu za usiku, mvua ilikuwa ikinyesha sana kwenye mji wa Novotroitsk, sababu ya baridi kali watu wachache sana walikuwa nje, wengi walijifungia ndani ya nyumba zao kuota moto.<br />
<br />
Hali ilikuwa tofauti kwa Victor Fedorov, pamoja na utajiri wake wote, alikuwa uwanja wa ndege akiwa amebana kwenye moja ya kona, simu yake ikiwa kiganjani, subira yote hiyo ilikuwa ni kwa watoto wake, alitarajia wakati wowote kupokea simu kutoka kwa Ditrov ikimweleza kuwa tayari walishatua.<br />
<br />
“Driiiii! Driiiii! Driiiii!” ulikuwa ni mlio wa simu yake, haraka akaipokea na kuiweka sikioni na kuanza kusikiliza.<br />
“Ditrov?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Mmefika?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Subirini hapo hapo nakuja,” aliongea Victor na kuanza kutembea kwenda mahali alipoliacha gari lake na kuingia, kisha kuliwasha na kuondoka kuelekea kwenye lango la kuingilia uwanjani, askari akafika akitaka kujua ni nani alitaka kuingia uwanjani muda huo wa usiku.<br />
<br />
“Ah! Mzee,” askari huyo alisema baada ya Victor kuvua kofia yake kichwani, aliheshimika mno kwenye mji huo na alikuwa na uwezo wa kufanya chochote serikalini hata kumuachisha au kumhamisha mtu kituo cha kazi kama tu angegombana naye, hii iliwafanya wafanyakazi wengi wa serikali wamwogope.<br />
“Naomba nikampokee mgeni wangu.”<br />
“Hakuna shida, pita tu”<br />
<br />
Victor akaendesha gari lake mpaka ndani kabisa mwa uwanja mahali ilipoegeshwa ndege ya shirika la ndege la Cross Atlantic ambayo aliikodisha kuwasafirisha watu wake mpaka kwenye uwanja huo, mlango wa ndege ukafunguliwa, Ditrov na kundi lake akashuka wakiwa wamewabeba Dorice na Dorica ambao walikuwa bado wako usingizini, miili yao ikiwa imesinyaa sababu ya kukosa chakula na maji.<br />
<br />
Wakapanda garini, kabla gari haijaondoka, Victor alishuka kwenye usukani na kuzunguka upande wa pili, akapanda na kuanza kuwabusu watoto mfululizo huku akilia kwa furaha na kukiri kwa mdomo wake kuwa hakuwahi kutarajia siku moja angewaona watoto waliotokana na mbegu zake ambazo aliziuza sababu ya umaskini.<br />
“Huu ni ukombozi,” alisema maneno hayo akiliendesha gari lake kwa kasi kuelekea nyumbani, furaha aliyokuwa nayo ilikuwa ni kubwa mno, alitaka afike nyumbani haraka ili awachunguze vizuri watoto wake.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea watoto wakizinduka? Nini kinaendelea nchini Tanzania kwa sasa ambako inaaminika watoto hao wamelipukia ndani ya gari lililolipuliwa kwa bomu? Kitendawili cha mafuvu kumi na sita wakati watoto waliokuwemo ni kumi na nane kitateguliwaje?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124a7ded34a1a55913133"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124aac296e64261691159">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.44.<br />
<br />
MVUA kubwa ilizidi kunyesha kwenye Mji wa Novotroitsk ikiambatana na baridi kali iliyofanya watu wengi wajifungie majumbani mwao. Gari aina ya Volga GAZ-24 (New Era) la kisasa lenye vioo vyeusi lilikuwa likikatiza kwenye ukungu mzito kutokea kwenye Uwanja wa Ndege wa Novotroitsk kuelekea mahali yalipokuwa makazi ya Bilionea Federov. Ndani ya gari kulikuwa na wan<span class="text_exposed_show">aume wawili, Federov mwenyewe na mlinzi wake, Ditrov ambaye ndiye aliyekuwa kiongozi wa msafara ulioenda kuwateka Dorice na Dorica na kuwafikisha Urusi.<br />
<br />
Kwenye siti ya nyuma walikuwa wamelala watoto wawili, Dorice na Dorica ambao hawakuwa wakijitambua kutokana na kuchomwa sindano ya dawa ya Memory Eraser iliyokuwa na kazi ya kufuta kumbukumbu kichwani. Miili yao ilikuwa imesinyaa kwani hawakula chochote tangu walipotekwa jijini Dar es Salaam wakati wakipelekwa shule hadi wakati ule.<br />
<br />
Vijana wa kazi’ wa Kundi la Chechniya waliofanikisha kazi ile sambamba na Ditrov lilikuwa likiwafuata taratibu. Walikuwa wakielekea nyumbani kwa Federov kukabidhiwa mamilioni yao waliyoahidiwa baada ya kuikamilisha kazi ile.<br />
<br />
Walipofika nyumbani kwa Federov, tafrija fupi ya kuwapongeza wote waliofanikisha zoezi lile ikafanyika na makabidhiano ya fedha walizoahidiwa yakakamilishwa. Kila kitu kilikuwa kikifanyika chini ya ulinzi mkali kuzuia siri ile isivuje na kutua mikononi mwa watu wasiohusika.<br />
<br />
Siku ile ile daktari maalum akatafutwa na kupewa kazi ya kuhakikisha Dorice na Dorica wanarejea kwenye hali zao za kawaida lakini wakiwa hawakumbuki kitu chochote kuhusu maisha yao yaliyopita. Fedha ilitumika kisawasawa kwani waliongezwa dozi nyingine ya Memory Eraser, wakaachwa walale mpaka siku iliyofuatia.<br />
<br />
Furaha aliyokuwa nayo Federov haikujificha. Hakuamini kuwa hatimaye kazi ile ya kuwarejesha mikononi mwake watoto wake imefanikiwa. Alikuwa na furaha kubwa ambayo ilimfanya amuongezee Ditrov mshahara mara tatu zaidi ya ule wa awali aliokuwa anaupata.<br />
<br />
Siku iliyofuatia, Dorice na Dorica walirejewa na fahamu, kazi ya kuwalisha chakula bora ikaanza ili kufidia muda mrefu waliokaa bila kula chochote. Licha ya kuwa walikuwa wamerejewa na fahamu zao, hawakuonekana kukumbuka kitu chochote maishani mwao. Hata kula ilibidi waanze kufundishwa upya. Kila kitu kwenye vichwa vyao kilikuwa kimefutika kama kompyuta ‘iliyofomatiwa’.<br />
<br />
“Hawa ni wanangu waliokuwa wanaishi barani Afrika, nimeamua kwenda kuwachukua baada ya kuona nimezidiwa na upweke,” alisema Federov wakati akiwatambulisha Dorice na Dorica mbele ya walimu watatu ambao aliwapa kazi ya kuhakikisha wanawafundisha kila kitu upya kwani hakuna walichokuwa wanakikumbuka.<br />
Wakabadilishwa majina na kupewa ya Kirusi, Dorice akiitwa ‘Марина’ au Mahreenah (Marina) na Dorica akiitwa ‘Мария’ au Mahreeyah (Mariya).<br />
<br />
Wakafundishwa lugha ya Kirusi na taratibu wakaanza kuzoea majina yao na mazingira mapya.<br />
Walimu wale waliwafundisha kwa bidii kwani walikuwa wakilipwa mshahara mnono na ndani ya wiki moja wakawa na uwezo wa kutamka maneno machache ya Kirusi.<br />
<br />
Wakaamini kuwa walizaliwa kwenye mazingira yale na Federov ndiyo baba yao kama walivyofundishwa na walimu wao. Walibadilika kwa kila kitu na hawakukumbuka chochote kuhusu Tanzania.<br />
<br />
Siku zilizidi kusonga na watoto wale wakawa wanazidi kuzoea mazingira mapya. Waliendelea kufundishwa mambo mbalimbali ikiwemo tabia njema na maadili ya Kirusi, na taratibu wakaanza kufanana na watoto waliozaliwa eneo lile. Suala lile lilimpa faraja kubwa Federov, ule upweke uliomtesa kwa miaka mingi sasa ukabakia kuwa historia.<br />
<br />
“Baba, kwani mama yetu yupo wapi?” Dorice ambaye sasa alikuwa akiitwa Марина (Marina) alimuuliza Federov jioni moja wakati wakitoka kwenye matembezi ya jioni.<br />
<br />
“Mama yenu alifariki wakati mkiwa bado wadogo kwa ajali ya gari, lakini msiwe na wasiwasi kwani baba yenu nipo,” aliongea Federov na kuwafanya watoto wale waamini kile walichoambiwa.<br />
<br />
Kwa jinsi alivyokuwa anawapenda, alihakikisha wanapata mahitaji yote muhimu yakiwemo chakula, mavazi mazito yasiyoruhusu baridi kupenya na kila kitu kilichokuwa muhimu kwao. Hakutaka wapate shida kabisa. Alipofikiria kuwaandikisha shule, walimu wao walishauri kuwa wanapaswa kuendelea kufundishwa nyumbani kwa angalau mwaka mzima mpaka watakapozoea kabisa mazingira.<br />
<br />
***<br />
Phillip alikuwa na kazi ya ziada baada ya tukio lile la ajali iliyohusisha gari la shule ambalo kila mtu alikuwa anaamini kuwa Dorice na Dorica nao walikuwa ndani yake mpaka wakati linalipuliwa na bomu. Hali ilikuwa mbaya zaidi kwa mkewe, Genevieve ambaye alishindwa kukubaliana na ukweli kuwa hatawaona tena watoto wake, akapatwa na mshtuko mkubwa siku ile ya tukio na kupelekwa hospitalini kulazwa. Licha ya madaktari kujitahidi kwa kila namna kumsaidia, bado hakuweza kuzinduka.<br />
<br />
“Amka mke wangu, kila kitu kinapangwa na Mungu. Tazama amewachukua watoto wetu na kuwatanguliza mbele za haki, na wewe unataka kuondoka? Nitabaki na nani kwenye hii dunia mimi?” Phillip alikuwa akilia pembeni ya kitanda alicholazwa Genevieve hospitalini na machozi yake yakawa yanamdondokea usoni.<br />
<br />
Phillip akawa na kazi ya kuomboleza, kwanza kwa ‘kufiwa’ na wanaye, pili kwa hali aliyokuwa nayo mke wake kipenzi. Jitihada za kumrejesha Genevieve kwenye hali yake ya kawaida zilishindikana, akawa ni mtu wa kitandani saa zote.<br />
<br />
Madaktari waliielezea hali ile iliyompata kuwa ni huzuni kali ambayo huumaliza nguvu na kuudhoofisha ubongo na kusababisha ushindwe kufanya kazi yake ipasavyo, hali ambayo husababisha mgonjwa kupoteza fahamu kwa kipindi kirefu.<br />
<br />
“Inaonekana aliwapenda sana watoto wake, ubongo wake umeshambuliwa kwa kiwango kikubwa na uwezekano wa kurejea kwenye hali yake ya kawaida ni mdogo. Hata akizinduka atakuwa na tatizo la kuzimia mara kwa mara kwani ubongo wake utakuwa unazalisha chaji za umeme kila atakapokuwa anawakumbuka wanaye, hali ambayo ni hatari sana,” alisema daktari aliyekuwa akimhudumia wakati akimuelewesha Phillip hali ya mkewe.<br />
<br />
Hilo lilikuwa ni pigo lingine kwenye maisha ya Phillip. Furaha yote aliyokuwa nayo wakati familia yake ikiwa imekamilika, ilipotea kama mshumaa uzimikavyo gizani, akawa ni mtu wa kuomboleza na kulia muda wote.<br />
<br />
Hakuweza hata kuendelea na kazi yake kama awali, muda mwingi akawa anautumia hospitali kumuuguza mkewe ambaye kila siku hali yake ilikuwa inazidi kuwa mbaya.<br />
<br />
“Eeeh Mungu, nimekukosea nini mimi mja wako mpaka kustahili mateso makali namna hii?” alisema Phillip akiwa pembeni ya kitanda cha mkewe wodini huku machozi yakimbubujika kama chemchemi ya maji.</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501247d73f9dc4717007000"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.45.<br />
<br />
<br />
PHILLIP alikuwa kwenye kipindi kigumu kuliko kingine chochote maishani mwake, kufiwa na watoto wawili pekee aliokuwa nao katika ajali pamoja na kuuguliwa na mkewe mpendwa ambaye alikuwa amepoteza fahamu baada ya kushuhudia mlipuko wa bomu ulioua watoto wake, hayakuwa matukio madogo, hakika yalivuruga kabisa akili yake na kutamani siku zirudi nyuma ile ya mli<span class="text_exposed_show">puko wa bomu iondolewe katika historia ya maisha yake.<br />
<br />
Kwa hali ilivyokuwa, akiwa amechanganyikiwa kabisa, baada ya kuzunguka huku na kule mikononi mwa matabibu wa kitaalam na kienyeji, akiongozana na baba mkwe wake, hatimaye aliamua kuandika barua ya kuacha kazi ili ajikite moja kwa moja kwenye tiba ya mkewe.<br />
<br />
Maisha yalikuwa yamebadilika, kila siku alipobaki peke yake alilia. Genevieve alimuumiza sana moyo kwa alivyokuwa akiteseka, kichwani mwake hakuwa na kumbukumbu hata kidogo za yeye alikuwa nani, watoto wake walikuwa wapi, alionekana kama zezeta tu jambo lililomuumiza sana Phillip na kumfanya awe tayari kutumia kila alichokuwa nacho akitafuta tiba za mke wake mpendwa.<br />
<br />
Pamoja na yote hayo, hakusahau jambo moja kubwa kuwaombea marehemu watoto wake na hata kutembelea kaburi lao kila siku ya Jumapili, huo ndio ulikuwa utaratibu wake wa maisha. Alimsikitikia sana mke wake kwa sababu hakuelewa chochote kilichokuwa kikiendelea na kila siku ya Jumatano ya kila wiki alilazimika kumpeleka hospitali.<br />
<br />
“Hivi iko siku mke wangu atapona na kurejewa na kumbukumbu zake za nyuma?” alimuuliza Dk. John Lupimo, bingwa wa magonjwa ya akili katika hospitali ya Muhimbili.<br />
“Ndio.”<br />
<br />
“Tatizo lake ni nini?”<br />
“Linaitwa kitaalam Amnesia.”<br />
“Amnesia? Ndio nini? Na inasababishwa na nini?”<br />
<br />
“Ni tatizo la ubongo pale hasa unaposhindwa kuyavuta mafaili ya kumbukumbu kutoka kwenye stoo zake au kushindwa kutunza kumbukumbu, husababishwa na magonjwa ya akili au wakati mwingine ajali kwenye kichwa.<br />
<br />
Hii ndio iliyotokea kwa Genevieve baada ya kushuhudia gari lililowabeba watoto wake likilipuka, akaanguka chini na kupiga kichwa ardhini.”<br />
“Sasa itakuwaje?”<br />
<br />
“Tunampa dawa iitwayo Amytal, hii inasaidia kurekebisha kumbukumbu, ipo siku Genevieve atarejea kwenye hali ya kawaida, hutaamini!” Daktari aliongea na kumfanya Phillip atabasamu, kauli hiyo ikawa imempa matumaini makubwa kwamba siku moja mke wake atarejewa na fahamu zake ili wote wawili wachangie maumivu ya kufiwa na watoto wao ambayo Genevieve hakuwa na habari nayo sababu ya tatizo lake la akili.<br />
<br />
Kadiri siku zilivyozidi kusonga wakiwa wodini, ndugu na jamaa wakifika kuwasalimu, hali ya Genevieve iliendelea kuwa mbaya siku hadi siku, akazidi kukonda sababu ya kutokula chakula, matumaini yake ya chakula yakawa ni kwenye mpira kupitia puani au dripu.<br />
<br />
Yote hayo hayakuweza kusaidia, hatimaye mwezi mmoja baada ya bomu kulipuka, Genevieve akaaga dunia na kuzikwa kando ya kaburi la watoto wake, katika mazishi yaliyohudhuriwa na maelfu ya watu wengi waliomlilia, Phillip alilia kama mtoto mdogo na kuzimia mara kadhaa.<br />
<br />
“Life has no meaning any more, I better die!” (Maisha hayana maana tena, bora nife!) Phillip aliongea akibubujikwa na machozi mbele za watu waliokusanyika kumfariji, wengi wakiwa ni wafanyakazi wenzake pamoja na familia ya Phillip.<br />
<br />
Baada ya mazishi Phillip hakuongea tena, muda wote akawa kimya kuliko ilivyokuwa kawaida yake, alitambulika kama mtu mcheshi mwenye mazungumzo kwa ajili ya kila mtu lakini sasa akachagua kubaki kimya sababu ya simanzi<br />
<br />
alilokuwa nalo. Kitu kingine kilichojitokeza ni wakati wa usiku, alipiga kelele na kudai mke na watoto wake walikuwa wakimtokea na kumwambia awafuate, jambo ambalo hakuna hata mmoja aliyelithibitisha ingawa yeye alidai kila siku dirisha la chumba chake liligongwa na akaitwa jina.<br />
<br />
Habari hii iliwashtua watu wengi na kuwafanya waamue kuwa wanakesha usiku ili waone kama kweli kilichodaiwa na Phillip kilikuwa ni cha kweli, wiki nzima baadaye hakuna aliyewaona Genevieve na watoto wake wakipita, hiyo kathibitisha kabisa kwamba Phillip alikuwa akinyemelewa na tatizo la akili, hii ilifanya siku chache baadaye abembelezwe na kukubali kupelekwa kwa daktari ambako awali alikuwa hataki kwenda akidai yeye alikuwa mzima wa afya.<br />
<br />
“Kila siku mke na watoto wangu wanakuja kunigongea wakitaka niongozane nao, mimi sitaki kwenda huko ambako wao wanaishi, kuna mateso sana, hivi njia ya kwenda Kigoma inapitia Kigamboni? Ng’ombe na mbuzi yupi ni paka?” aliongea sentensi nyingi zisizo na maana.<br />
<br />
Tayari daktari akawa ameshaligundua tatizo lake, hapohapo hakupoteza wakati, akatoa maamuzi kwamba mgonjwa alazwe kwenye wodi ya wagonjwa wa akili kwa matibabu ili pia awe anakutana na mtoa nasaha ambaye angebadilisha maisha yake baada ya kufiwa na mke pamoja na watoto wake.<br />
<br />
Akaanza kupewa dawa ambazo hazikumsaidia chochote, aliendelea kuwa kimya huku mara kwa mara akilia na kuwaita mke na watoto wake. Kibaya zaidi alianza tabia ya kutupa nguo na kutembea utupu bila kujali heshima yake, hii ilifanya madaktari wamwandikie dawa zilizomfanya alale kwa muda mrefu ili kusaidia akili ikae sawa.<br />
<br />
Dawa hizo ziliposimamishwa wiki mbili baadaye, angalau aliweza kujisikia vizuri, madaktari wakaridhika kabisa na kuamua kumruhusu arejee nyumbani kuendelea na dawa taratibu.<br />
<br />
Huzuni yake ilikuwa pale pale, kila alipoyaona makaburi ya mke na watoto wake alipokwenda kuyatembelea alilia mno. Hakika alitamani kufa, akazidi kukonda sababu ya mawazo na hakujijali tena, wengi walimchukulia kama mtu aliyechanganyikiwa na akili sababu ya matatizo yaliyomkuta, alitembea sehemu nyingi akiongea peke yake.<br />
<br />
“Hallow!” ilikuwa ni sauti ya mwanamke nje ya duka kubwa la Imalaseko ambako Phillip alikuwa akipita, akageuka na kuangalia upande sauti ilikotokea.<br />
“Ndio dada.”<br />
“Wewe ni Phillip?”<br />
<br />
“Ndio, wewe ni nani? Sauti yako sio ngeni.”<br />
“Nini kilitokea mpaka ukawa hivi?”<br />
“Maisha tu dada yangu. Dunia inazunguka kwenye mhimili wake, watu tunaingia na kutoka.”<br />
<br />
“Nimesikitika sana.”<br />
“Kila mtu anayeniona anasikitika. Wewe ni nani lakini?”<br />
“Unataka kunifahamu?”<br />
“Ndio.”<br />
“Njoo ndani ya gari yangu tuongee, nitakukumbusha kila kitu.”<br />
“Kweli?”<br />
“Ndio.”<br />
<br />
“Naogopa kuingia kwenye gari lako!”<br />
“Hakuna sababu ya kuogopa, wewe njoo tu nataka kukuonyesha jambo.”<br />
<br />
“Mh!” Phillip aliguna, taswira ya Zamaradi ikamwijia kichwani, akaanza kuhisi pengine mtu huyo aliyekutana naye alikuwa jini ambaye angeweza kumdhuruHata hivyo, baada ya kusisitiziwa sana alijikuta anakubali na kuingia ndani ya Land Cruiser mpya ya rangi ya fedha, akaketi kitini kando ya dereva ambaye alikuwa ni mwanamke aliyekutana naye.<br />
“Unataka kufahamu mimi ni nani?”<br />
“Ndio.”<br />
<br />
“Subiri!” mwanamke huyo aliongea akijifunua wigi usoni mwake, akaiondoa pia sura ya bandia na yake halisi kuonekana. Macho yakamtoka Phillip kwa mshangao akiwa amejifunika kwa mikono yake yote miwili mdomoni, bila kusema chochote alianza kulia.<br />
“Usilie ndio dunia.”<br />
<br />
Je, mwanamke huyo ni nani? Nini kinaendelea kwa watoto Dorice na Dorica ambao tayari wapo nchini Urusi wakiwa wamepoteza kumbukumbu zote za Tanzania na<br />
wazazi wao baada ya kuchomwa sindano ya dawa iitwayo Memory Eraser ambayo hutumika kufuta kumbukumbu kwenye ubongo wa mwanadamu ili aanze upya kujifunza? Majina yao hivi sasa si Dorice na Dorica tena bali ni Mariya na Merina.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea?FUATILIA KESHO HAPA UNLIMITED SWAGGAZZ PAGE</span></span></div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-28329878239434075052012-07-27T00:46:00.001-07:002012-07-27T00:46:25.211-07:00MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.46.<a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/msichana-ndotoni-mwanguep81.html?spref=bl"></a><br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<img alt="" class="spotlight" src="https://fbcdn-sphotos-a.akamaihd.net/hphotos-ak-snc7/576830_376036342455947_1243126751_n.jpg" style="height: 113px; width: 168px;" /><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.46.<br />
<br />
BASI la shule lililobeba watoto kumi na nane linalipuliwa kwa bomu, watoto wote wanakufa palepale lakini baadaye yanapatikana mabaki ya watoto kumi na sita tu! Hiki kinakuwa ni kitendawili kwani kila mtu alikuwa na uhakika watoto waliopanda ni kumi na nane.<br />
<br />
Ukweli wa tukio hili ni kwamba, watoto wawili (Dorice na Dorica) waliondolewa kwenye gari na watekaji k<span class="text_exposed_show">abla ya bomu kulipuliwa. Watekaji hao walitumwa na Victor Federov, Mrusi bilionea asiye na mtoto ambaye wakati wa umasikini wake aliwahi kuwauzia Phillip na Genevieve mbegu zake za kiume.<br />
<br />
Phillip na mke wake Genevieve hawaelewi juu ya jambo hili, wanalia kwa kupoteza watoto wao wawili katika ajali hiyo mbaya iliyomfanya Genevieve aanguke chini na kupoteza fahamu, mshipa wa damu ukapasuka kwenye ubongo kwa sababu ya kupanda kwa shinikizo.<br />
<br />
Maisha ya Phillip baada ya hapo yanabadilika, akawa na kazi moja tu ya kumuuguza mke wake mpaka alipofariki na kufanya jumla ya watu waliofariki kwenye familia yake kufikia watatu. Amechanganyikiwa na kuwa kama mwendawazimu, akitambea na kuongea peke yake njiani.<br />
<br />
Kwa msaada wa ushauri wa kisaikolojia aliopewa hatimaye alirejea katika hali ya kawaida, ndipo akakutana na mwanamke nje ya duka kubwa la Imalaseko katikati ya jiji, wakapanda kwenye gari kwa ajili ya maongezi, mwanamke huyo alipovua wigi na kujifunua uso wake, Phillip alishtuka na kuanza kulia.<br />
Je, nini kitaendelea? Mwanamke huyo ni nani? SONGA NAYO…<br />
<br />
“NINI kilikupata dada yangu?” <br />
“Hunikumbuki?”<br />
“Kabisa.”<br />
“Mbona umelia?”<br />
“Nakuonea huruma.”<br />
<br />
“Nikikusimulia historia ya maisha yangu utanikumbuka, umewahi kuwa na rafiki msichana aliyeungua vibaya ndani ya gari?”<br />
“Wewe ni Lina?!” Phillip aliuliza tena mshangao macho yakiwa yamemtoka, hakuwa tayari kuamini kama kweli msichana aliyekuwa mbele yake ndiye Lina aliyewahi kuwa msichana mrembo ambaye sasa uso wake ulikuwa umejaa makovu.<br />
<br />
“Ni mimi, habari za siku nyingi Phillip?”<br />
Phillip hakujibu, akaendelea kububujikwa na machozi, kichwani mwake taswira ya Lina wa zamani ilikuwa ikionekana, hakika alikuwa ameharibika, uso wake ukiwa umejaa makovu makubwa, ilivyoonekana upasuaji wote wa kumrekebisha sura haukuwa na mafanikio makubwa kwani sura yake ya awali haikurejea. Hasira nyingi sana akazielekeza kwa Zamaradi.<br />
<br />
“Nisamehe!” Phillip alisema neno hilo pekee kwikwi ya kulia ilipomwachia.<br />
“Kwa kipi Phillip?”<br />
“Nahusika sana na ajali yako.”<br />
“Unamaanisha nini? Ulijua itatokea? Ilikuwa ya kupangwa?”<br />
“Hapana, ni historia ndefu naomba tu unisamehe.”<br />
<br />
“Hakuna shida, naweza kukusamehe lakini ni vizuri ukanieleza pia ni kwa nini unaniomba msamaha?”<br />
Phillip akajifuta machozi kisha kuanza kumsimulia Lina kila kitu kuhusu maisha yake, namna alivyoishi katika dunia mbili tofauti, inayoonekana na isiyoonekana akiwa mume wa Zamaradi, jini mwenye hasira ambaye alimshambulia kila mwanamke aliyemtaka kimapenzi. Lina alikuwa kimya akisikiliza.<br />
<br />
“Ndiyo maana nilikuwa sikubali uhusiano wa kimapenzi na msichana yeyote, lakini mabinti walinilazimisha na Zamaradi akawadhuru, ajali yako ilisababishwa na Zamaradi, yeye ndiye aliyemuua Monalisa pia katika ajali! Nisamehe sana kwa yaliyotokea, haikuwa nia yangu.”<br />
<br />
“Mh! Hii ni habari mpya, sikuwahi kufahamu jambo hili.”<br />
“Huo ndiyo ukweli.”<br />
“Huyo Zamaradi yuko wapi sasa?”<br />
<br />
“Nilipokutana na marehemu mke wangu na kuamua kuwa na uhusiano naye kimapenzi, Zamaradi alijaribu kutushambulia lakini kwa sababu tulikuwa tumekabidhi maisha yetu kwa Mungu na tulilindwa saa ishirini na nne alishindwa kutudhuru, tangu siku hizo sikuwasiliana tena na ulimwengu usioonekana, nikamuoa mke wangu na kuzaa watoto wawili mapacha ambao sasa wote wameniacha!”<br />
<br />
“Pole sana, nimesikia kila kitu kilichotokea, tuyasahau ya zamani tuangalie ulimwengu unaofuata mbele yetu.”<br />
“Umeolewa?”<br />
“Hapana, bila shaka hakuna mwanaume ambaye anavutiwa na mimi kwa jinsi nilivyo.”<br />
<br />
“Usiseme hivyo, mshukuru Mungu.”<br />
“Ahsante kwa kunitia moyo lakini mimi pia nataka nikuambie hata kama umepoteza mke na watoto wako, simama imara, endelea na maisha, usivunjike moyo, unakumbuka sura yangu mimi?”<br />
“Ndiyo”<br />
<br />
“Ilikuwa ya kuvutia, nikaipoteza katika ajali ya moto lakini bado nilisonga mbele, baada ya upasuaji wa kurekebishwa kufanyika, angalau kuwa hivi nilivyo niliendelea na masomo kwa msaada wa Umoja wa Mataifa mpaka nikapata shahada mbili za Uchumi na kuajiriwa nchini Marekani, nimehamishiwa hapa mwezi uliopita kuwa Mwakilishi wa Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa, WFP!”<br />
<br />
“Kweli?”<br />
“Ndiyo”<br />
“Umenitia moyo.”<br />
“Hivyo ndivyo maisha yalivyo Phillip, Wazungu wanasema life is a series of events, yaani maisha ni mfululizo wa matukio, linaondoka hili linaingia lile, hivyo unatakiwa kusimama imara.”<br />
<br />
“Ahsante sana.”<br />
“Unaelekea wapi hivi sasa Phillip?”<br />
“Nazungukazunguka tu!”<br />
“Karibu nyumbani basi.”<br />
“Hakuna shida twende nikapafahamu.”<br />
<br />
Lina akashuka na kuzunguka upande wa pili ambako alikaa kwenye usukani, akawasha gari na kuondoka moja kwa moja kupitia Barabara za Ohio, Ali Hassan Mwinyi na baadaye Haile Selasie kuelekea Masaki ambako Lina alipiga honi kwenye jumba lenye lango kubwa na likafunguliwa.<br />
“Mh!” Mlinzi akaguna.<br />
<br />
“Vipi?”<br />
“Gari ni lenyewe, sauti ni ile ile akini bosi siye.”<br />
“Mungu wangu…” Lina aliongea akijigusa kichwani na usoni, alikuwa amesahau kuvaa wigi na sura yake ya bandia ndiyo maana mlinzi wake akashtuka, kwa muda wote walioishi pamoja hakuwahi kumwonesha jinsi alivyokuwa.<br />
<br />
“Wewe fungua lango, mambo mengine hayakuhusu.”<br />
“Bosi haruhusu wageni kuingia bila miadi.”<br />
“Nakuambia fungua, unataka kazi au?”<br />
“Eebwana ee, usinizingue, rudi kinyumenyume egesha pale nje umsubiri mpaka aje.”<br />
<br />
“Sawa, ngoja nikamlete.” alijibu Lina na kuanza kurudi kinyumenyume bila ubishi, akaligeuza gari kwa kasi na kuondoka hadi barabarani ambako alizunguka upande wa pili na kuvaa wigi pamoja na sura yake ya bandia, akarejea tena kwenye usukani na kuendesha kwenda nyumbani kwake ambako baada ya honi lango lilifunguliwa.<br />
<br />
“Karibu bosi!”<br />
“Ahsante sana.”<br />
“Walikuwa wamekuacha barabarani?”<br />
“Ndiyo, kazi nzuri sana, nilitaka kukujaribu ili nione kama watu wanaweza kuingia hapa kwangu kwa urahisi tu. Safi sana, chukua hii elfu kumi utakunywa soda”<br />
<br />
“Teh! Teh! Teh! Ahsante bosi nitaendelea kufanya kazi kwa uaminifu mkubwa.”<br />
Gari likaingizwa ndani ya kuegeshwa sehemu yake, Lina akashuka na kumfungulia Phillip mlango kisha kumwita mlinzi na kumtambulisha kwamba huyo alikuwa rafiki pekee aliyeruhusiwa kumtembelea wakati wowote usiku na mchana bila kizuizi, Phillip na mlinzi wakashikana mikono.<br />
<br />
“Naitwa Phillip.”<br />
“Mimi ni Marwa, kutoka Taa-rime!”<br />
“Nafurahi kukufahamu.”<br />
“Na mimi hibyo, hibyo!”<br />
<br />
Phillip na Lina wakaanza kupandisha ngazi kuingia ndani ambako tofauti na watu wenye uhusiano wa kawaida, Lina akaanza kumtembeza Phillip kwenye nyumba yake kuanzia jikoni kisha kupandisha ngazi hadi kwenye chumba chake cha kulala ambako aliketi kitandani na kumwomba Phillip afanye hivyo hivyo.<br />
“Kaa tu usiogope, hakuna tatizo, jisikie uko nyumbani.”<br />
<br />
“Ahsante.”<br />
Kwa mara ya kwanza tangu apoteze familia yake, Phillip alijisikia faraja ya kweli moyoni mwake, akaketi kitandani kando ya Lina na wakaanza kuongea mambo mbalimbali kuhusu maisha tangu walipoachana, Lina hakuficha ukweli wake kwamba tangu aungue kwa moto hakuwahi kukutana na mwanaume hata akamwambia neno “Nakupenda” ingawa alikuwa na mafanikio makubwa mno maishani mwake.<br />
<br />
“Pole!”<br />
“Ahsante Phillip.”<br />
“Nakupenda.”<br />
“Kha!”<br />
“Mbona unashangaa?”<br />
“Una uhakika?”<br />
<br />
“Ndiyo.”<br />
“Hausemi tu kwa sababu una mfadhaiko baada ya kupoteza mke na watoto?”<br />
“Hapana, nakupenda Lina, nilivutiwa na wewe wakati ule ukiwa na sura ile, sidhani kama nahitaji kubadilika leo ukiwa na sura hii, upendo wangu ni wa kweli, naomba uniamini.”<br />
<br />
“Ghafla mno…”<br />
“Mapenzi ya kweli hayana maandalizi, isitoshe mimi ndiyo chanzo cha yote yaliyokukuta, naomba uamini nakupenda. Wewe ndiyo utakuwa faraja ya mtima wangu, utanipunguzia maumivu niliyonayo ndani, nikiwa na wewe nitakuwa mtu tena”<br />
<br />
Lina akainamisha kichwa chake chini, machozi yakaanza kudondoka na kulowanisha sakafu. Phillip akamsogelea na kumnyanyua, kisha kumkumbatia, akamvua wigi na sura ya bandia, halafu akamlaza chali kitandani na kuanza kumpiga mabusu mfululizo. Hisia za Lina zikawa kama mtu aliyekuwa akipigwa na shoti ya umeme.<br />
“Usinishangae Phillip, ni miaka mingi sijakutana na jambo hili.”<br />
“Basi leo ndiyo leo.”</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.47.<br />
<br />
<br />
KILIKUWA chumba chenye ukubwa usiopungua mita za mraba hamsini, kilijazwa samani nyingi zenye thamani kubwa, ukutani kukiwa na picha kubwa ya mwanaume akiwa na watoto wawili mapacha. Mwanaume kwenye picha hiyo ndiye aliyekuwa ndani ya chumba hicho akiwa ameketi nyuma ya meza kubwa, akiiangalia picha kubwa iliyokuwa mbele yake kwa umakini, ghafla akatabasamu.<br />
<span class="text_exposed_show">“Siwezi kuamini kama hawa watoto wako mikononi mwangu!” aliwaza Victor Federov.<br />
<br />
Moyo wake ulikuwa umejaa furaha kubwa kupindukia, ujio wa Dorice na Dorica ambao hivi sasa waliitwa Mariya na Marina ulifanyika kwa wakati muafaka. Kitu pekee kilichomsumbua akilini mwake ni kwa namna gani angeweza kuificha siri hiyo isivuje, kwani aliwahusisha watu wengi katika zoezi la utekaji na alielewa duniani hapakuwa na siri ya watu wawili, lazima siku moja kama si Ditrov basi watu aliokuwa nao, mmoja lazima angefungua mdomo na kuueleza ulimwengu namna watoto wake walivyopatikana. Mawazo hayo yalimfanya auchukue mkono wa simu uliokuwa kando yake na kuanza kupiga namba ya Ditrov.<br />
<br />
“Ndio mkuu.”<br />
“Uko wapi?”<br />
“Ofisini kwangu.”<br />
“Naomba uje haraka.”<br />
“Sawa.”<br />
Simu ikakatika.<br />
<br />
Dakika tano baadaye mlango wa ofisi yake ukagongwa na Ditrov akaingia na kuketi mbele ya meza ya Victor. Mwili wake ulikuwa umeongezeka zaidi sababu ya mazoezi, fedha nyingi aliyolipwa katika zoezi la kuwateka Dorice na Dorica ilikuwa imebadilisha kabisa maisha yake, sasa hakuhangaikia mambo madogo madogo tena, mara nyingi baada ya kazi alitumia muda mwingi kwenye jengo la mazoezi.<br />
<br />
“Ndio bosi nimeitika wito.”<br />
“Ahsante, suala langu sio kubwa, nataka kukuuliza kama watu wote ulioshirikiana nao kwenye operesheni hii unawafahamu!”<br />
“Sana, ni rafiki zangu.”<br />
“Wakati wowote unaweza kuwapata?”<br />
“Bila shida.”<br />
<br />
“Sasa sikiliza.”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Duniani hakuna siri ya watu …?”<br />
“Wawili.”<br />
“Ningependa kuona watu hawa wote wanakufa.”<br />
“Mh!”<br />
<br />
“Mbona umeguna? Nitalipa dola laki tano.”<br />
“Kweli?”<br />
“Bila shaka.”<br />
“Kama dola laki tano zipo, mimi naweza kufanya hivyo kazi bila matatizo. Ni kiasi cha kutafuta Blood Pressure Uplifter, ambayo wakishainywea kwenye chai au kinywaji chochote, shinikizo la damu litapanda na watakufa mmoja baada ya mwingine.”<br />
<br />
“Unaweza kufanya hivyo?”<br />
“Bila matatizo, ndiyo kazi yangu.”<br />
“Hiyo dawa utaipata wapi?”<br />
“Ninayo.”<br />
“Kabisa?”<br />
<br />
“Tangu enzi za KGB,” Ditrov aliongea akimaanisha Shirika la Ujasusi la Urusi ambalo aliwahi kulifanyia kazi miaka mingi kabla.<br />
“Basi kama ni hivyo, tekeleza.”<br />
“Fedha yangu?”<br />
“Ukimaliza kazi njoo unione.”<br />
<br />
“Ahsante.”<br />
Ditrov akaondoka kichwani mwake akifikiria dola laki tano ambazo angelipwa akimaliza kazi ya kuwaua watu wote alioshirikiana nao kwenye zoezi la utekaji, alielewa ingekuwa kazi rahisi sababu wote walimwamini. Alichokifanya kuanzia siku hiyo ni kuwa anawaita mmoja baada ya mwingine na kumpakia ndani ya gari lake hadi ufukweni mwa bahari kwa ahadi kwamba walikuwa wanakwenda kupunga upepo, huko aliitoa dawa hiyo na kumchanganyia mlengwa kwenye kinywaji, dakika chache baada ya kunywa hali ilibadilika, Ditrov akambeba ndani ya gari, njiani alikufa.<br />
<br />
Alichokifanya ni kutumia boti maalum aliyopewa na Victor Federov kuubeba mwili huo mpaka katikati ya bahari ambako aliufunga jiwe na kuuzamisha hadi kwenye kina cha maji, akiamini huko usingeonekana milele. Alifanya hivyo mpaka akawamaliza wote, akimpa taarifa Victor Federov juu ya maendeleo.<br />
“Hongera sana, njoo ofisini leo usiku kama saa saba hivi uchukue hundi yako.”<br />
<br />
“Nakuja bosi.”<br />
Katika muda huo huo aliopangiwa, ofisi ikiwa haina mtu, Ditrov alipandisha ngazi mpaka ofisini kwa Victor Federov ambako alipokelewa kama shujaa, akaketi kusubiri hundi yake, Victor alipofungua droo, badala ya kutoka na kitabu cha hundi, mkono ulitoka ukiwa na bastola yenye kiwambo cha kuzuia sauti.<br />
<br />
“Nilikuambia duniani hakuna siri ya watu wangapi?”<br />
“Wawili.”<br />
“Inabidi Ditrov ufe ili nibaki peke yangu.”<br />
“Hapana mzee nisamehe.”<br />
“Paa! Paa! Paa!”<br />
<br />
***<br />
Kitanda kilikuwa kinacheza kama vile ni cha spiringi, ingawa kilitengenezwa kwa mbao imara za mninga, Phillip alikuwa kazini akijituma impasavyo mwanaume aliyekuwa akitafuta sifa. Alitaka kumwonyesha Lina kwamba uzuri wake haukuwa umbile la sura tu, bali hata kwenye ukanda wa sita kwa sita alikuwa ni mtaalam haswa.<br />
<br />
Lina alikuwa akilia, si kwa maumivu bali kwa raha aliyokuwa akiipata. Ilikuwa imepita miaka mingi tangu akutane mara ya mwisho na mwanaume kimwili, moto uliomteketeza uliondoka na uzuri wake wote, hivyo hakuna mwanaume aliyevutiwa naye labda kwa wale walioangalia maumbile, maana mtaji peke yake aliokuwa nao ulikuwa ni hips zilizochomoza kama vilele vya mlima Meru!<br />
<br />
Miili yao ilikuwa imelowa kwa jasho ingawa kulikuwa na kiyoyozi chumbani kilichoonyesha joto lilikuwa sentigredi kumi na nane. Mashuka yote yalikuwa yamelowa, kijana Phillip akiwajibika, kwake kitendo cha ngono kilikuwa ni njia ya kumsahaulisha yaliyokuwa yakimsumbua akilini mwake, aliichukulia ni kama faraja.<br />
<br />
“Ahsante!” Lina alitamka maneno hayo Phillip alipojitupa kando yake.<br />
“Karibu.”<br />
“Sijawahi.”<br />
“Hujawahi nini?”<br />
“Kukutana na mtu wa aina yako, umezidi kunitia uchizi.”<br />
“Nakupenda Lina.”<br />
<br />
“Nakupenda pia Phillip, miaka yote, kama uliyoyasema ni kweli, basi mapenzi yangu kwako ndiyo yalinisababishia hata huu ulemavu.”<br />
“Ndio maana niko na wewe, ndio njia pekee ya kukulipa kwa kile ulichopoteza kwa ajili yangu.”<br />
<br />
Wakakumbatiana, Lina akiwa tayari kuanza tena lakini Phillip alimshauri wapumzike. Nusu saa baadaye ndipo walipoendelea mpaka usiku wa manane, kiasi kwamba Phillip hakuweza kuondoka tena, huo ndio ukawa mwanzo wa kuishi ndani ya nyumba hiyo akifarijiana na Lina ambaye kwake Phillip alikuwa kila kitu. Miezi sita ikapita na taarifa za uhusiano wao zikaenea kila mahali, wazazi wa Genevieve wakafurahishwa na jambo hilo wakiamini Phillip angesahau maumivu aliyokuwa nayo.<br />
<br />
“Kuna jambo nataka kukueleza.”<br />
“Jambo gani?” Lina aliuliza.<br />
“Nimefikia uamuzi wa kukuoa, wewe peke yako ndiye unaweza kunisahaulisha vifo vya mke na watoto wangu,” alisema Phillip.<br />
<br />
Hakuwa na habari kabisa juu ya kilichotokea, kwamba watoto wake hawakuwa marehemu bali walitekwa na vijana wa Victor Federov.<br />
“Unasema kweli Phillip?”<br />
“Kweli kabisa.”<br />
“Nipo tayari.”</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.48.<br />
<br />
“Lakini kuna kitu kimoja tu nataka kukueleza, kama utakubaliana nacho basi tutafunga ndoa yetu ili tuishi kwa furaha, kikikushinda basi tena maana mimi sina la kufanya, ni maumbile na sitaki kurudia tena kufanya kitendo nilichokifanya huko nyuma.”<br />
<br />
“Kitu gani hicho unachotaka kunieleza, usizunguke, niambie tu.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Bila shaka nimewahi kukueleza kwamba nina uwezo wa kutoa mbegu za kiume lakini hazina uwezo wa kurutubisha yai la mwanamke, hii ina maana kama tukioana hatutakuwa na uwezo wa kuwa na motto. Je, hilo ni kikwazo kwako?”<br />
“Hapana hata kidogo, cha muhimu kwangu ni kuwa na mtu anayenipenda, watoto ni majaliwa ya Mungu.”<br />
<br />
“Ahsante Lina,” Phillip aliongea akimvuta na kumkumbatia, kilichofuata baada ya hapo ni sauti zao kuendelea kushuka huku wakinong’ona, neno I love you, likisikika mara nyingi, ghafla ukimya ukasikika na milio ya “Jwig!Jwig!Jwig!” ikasikika! Kilikuwa ni kitanda kikipiga kelele. Phillip alikuwa kazini akifanya kila alichoamini alikuwa na utaalam nacho ingawa hakuwa na uwezo wa kupata mtoto.<br />
<br />
Siku iliyofuata kazini Lina alikuwa na jambo moja tu, kuwataarifu rafiki na wafanyakazi wenzake juu ya kilichokuwa kikifuata maishani mwake. Kila mtu akawa na hamu ya kumwona Phillip, aliyejitolea kumuoa Lina. Siku ya siku ikafika, Phillip akatambulishwa kwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam kwenye tafrija ndogo iliyofanyika katika Hoteli ya<br />
<br />
Johannesburg, ambayo pia Phillip aliitumia kumvisha Lina pete ya uchumba.<br />
Kamati ikaundwa na utaratibu wa michango kama ilivyozoeleka nchini Tanzania ukafuata. Kiasi kikubwa cha fedha kikakusanywa na hatimaye harusi kubwa tena ya kifahari iliyosimamiwa na familia ya Lina pamoja na familia ya Genevieve na ndugu wa Phillip ikafanyika, ndoto ya Lina kuolewa na Phillip ikatimia.<br />
<br />
Wakaanza kuishi pamoja kama mke na mume, katika maisha yaliyojaa furaha, huzuni zote zilizokuwa zimewafunika zikaondoka ingawa Phillip hakuisahau familia yake. Kila Jumapili ilikuwa ni lazima asindikizwe na mke wake wakiwa njiani kuelekea kanisani hadi makaburini ambako alisali akimkumbuka mke wake Genevieve na watoto wao Dorice na Dorica.<br />
<br />
Hakuwa hata na hisia kidogo kwamba watoto wake walikuwa upande wa pili wa dunia, nchini Urusi wakiishi na baba yao wa kuwazaa, pia wakiwa hawana kumbukumbu ya mahali walikotokea baada ya kumbukumbu zote kufutwa kichwani kwa sindano za dawa iitwayo Memory Eraser.<br />
***<br />
Ditrov alikuwa amelala sakafuni, risasi mbili zikiwa zimepenya mwilini. Kulikuwa na dalili zote kwamba alikuwa amekufa na Victor akiamini siri yake ya kuwatorosha Dorice na Dorica kutoka Tanzania isingevuja, alisogeza mfuko mkubwa wa nailoni aliokuwa ameuandaa kwa ajili ya kazi hiyo na kuanza kumwingiza ndani yake huku mwili wake wote ukitetemeka.<br />
<br />
Alikuwa na uhakika asilimia mia moja hakuna mtu angegundua kilichokuwa kikiendelea, taratibu akausogeza mfuko kando na kuanza kuisafisha sakafu mpaka alipohakikisha imetakata bila doa lolote la damu, akaunyanyua tena mfuko na kuupeleka mpaka kwenye lifti. Alipoingia ndani akabonyeza alama iliyoandikwa G, ili kuiamuru lifti ishuke moja kwa moja mpaka chini kulikokuwa na maegesho ya magari.<br />
<br />
“Afande! Afande! Afande!” aliita alipotoka kwenye lifti bila kuuchukua mwili wa Ditrov, alitaka kuhakikisha hakuna mtu eneo hilo, ukimya ulimthibitishia kwamba aidha askari alikuwa amelala au alikuwa amepandisha juu kwa walinzi wenzake.<br />
<br />
Akarejea kwenye lifti na kufungua, akaubeba mwili mpaka kwenye gari na kufungua buti kisha kuuingiza ndani na kufunika. Kwa kasi akazunguka upande wa dereva na kufungua mlango, akawasha na kuondoka kwa kasi, sehemu ya kutokea askari walimsimamisha lakini walipogundua ni bosi wao hawakuwa na swali.<br />
<br />
“Nahitaji jiwe, kamba ninayo,” aliwaza akiendesha gari kuelekea nyumbani kwake.<br />
<br />
Nyumba yake ilijengwa ufukweni kabisa na alimiliki boti iendayo kasi, hiyo ndiyo alipanga kuitumia kwa ajili ya kazi iliyokuwa mbele yake. Bahati nzuri hakuwa na mlinzi, alitumia mbwa na nyaya za umeme, hivyo alichofanya baada ya kuingia ndani ya ngome yake kabla hajafungua buti na kuutoa mwili wa Ditrov ni kutafuta jiwe kubwa na kushuka nalo hadi ufukweni, akalifunga vizuri na kamba.<br />
<br />
Bila kupoteza wakati akaja kwenye gari, akafungua buti na kuutoa mwili wa Ditrov ukiwa kwenye mfuko wa nailoni usiovujisha damu na kuubeba begani huku akikimbia nao ufukweni.<br />
<br />
Akaangaza macho yake huku na kule bila kuona mtu yeyote zaidi ya mbwa wake waliokuwa wakibweka, kilichosikika dakika chache baadaye ni muungurumo wa boti ikikata maji kuelekea katikati ya bahari.<br />
<br />
Dakika ishirini hivi baadaye, alizima injini na boti kusimama. Giza lilikuwa nene kila upande, hivyo hakumhofia mtu yeyote, haraka akalikamata jiwe na kulitupa majini kisha kuusukuma mfuko, taratibu ukaingia majini na kuanza kuzama.<br />
<br />
Huo ukawa mwisho wa Ditrov. Badala ya kusikitika, Victor Federov alitabasamu na kuwasha boti yake kisha kuondoka kwa kasi kurejea nyumbani ambako aliegesha na kuingia ndani bila mtu yeyote kugundua.<br />
<br />
Hakupata usingizi hata kidogo mpaka kulipopambazuka asubuhi,akajiandaa kwa ajili ya kwenda kazini ambako alifanya kazi kama kawaida, saa nne na nusu alimpigia simu katibu muhtasi wake na kumwomba amwitie Ditrov.<br />
“Hajaonekana tangu asubuhi bosi.”<br />
<br />
“Haiwezekani, mtafuteni haraka sana nina kazi ya kufanya naye.”<br />
“Sawa bosi.”<br />
***<br />
“Jina lako unaitwa nani?”<br />
“Marina!”<br />
“Na mwenzako?”<br />
<br />
“Mariya.”<br />
“Ninyi ni mapacha?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Baba yenu ni nani?”<br />
“Victor Federov.”<br />
<br />
“Ahaaa! Kumbe ni ninyi?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Karibuni sana Moscow International School.”<br />
“Ahsante.”<br />
<br />
Victor Federov aliwapenda sana watoto wake, kuthibitisha jambo hilo alihakikisha wanapata elimu bora. Alikuwa na fedha nyingi, utajiri wake ulitisha hata kama angetumia fedha zake kwa fujo kiasi gani, haikuwa rahisi kuzimaliza hivyo aliona ni bora kusomesha watoto wake kwenye shule nzuri ili wapate elimu bora itakayowasaidia kuendesha miradi yake vizuri baada ya yeye kuondoka duniani.<br />
<br />
Shule aliyoona inawafaa ni Moscow International School, ambayo kwa mwaka kila mtoto alilipiwa milioni ishirini na tano. Watoto walimfurahia baba yao, hawakuwa na kumbukumbu yoyote tena juu ya Tanzania wala Phillip na Genevieve.</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.49.<br />
<br />
VICTOR Fedorov alipohakikisha kwamba sasa alikuwa amemaliza zoezi zima la mauaji, alirejea nyumbani kwake na kuingia moja kwa moja chumbani kwake ambako alijitupa kitandani, hakika alijiona mshindi kwa kazi aliyokuwa ameifanya na sasa siri juu ya watoto ilikuwa imebaki kuwa yake peke yake.<br />
Hakupata usingizi hata kidogo mpaka kulipopambazuka asubuhi, akajiandaa k<span class="text_exposed_show">wa ajili ya kwenda kazini ambako alifanya kazi kama kawaida, saa nne na nusu alimpigia katibu muhtasi wake na kumwomba amwitie Ditrov.<br />
<br />
“Hajaonekana tangu asubuhi bosi.”<br />
“Haiwezekani, mtafuteni haraka sana nina kazi ya kufanya naye.”<br />
“Sawa bosi,” katibu muhtasi alijibu.<br />
Kwa muda wa nusu saa katibu muhtasi aliendelea kumtafuta Ditrov kwa namba zote alizozifahamu lakini hakupatikana, yeye pia akaingiwa na hofu, kwani haikuwa kawaida ya Ditrov kutofika kazini bila sababu yoyote na hakuwahi hata mara moja kuzima simu zake za mkononi.<br />
<br />
“Lazima atakuwa na matatizo huyu,” aliwaza katibu muhtasi akinyanyua simu ili amtaarifu bosi wake.<br />
“Ngrii! Ngrii! Ngrii!” simu ilisikika upande wa pili ikiita.<br />
“Ndiyo.”<br />
“Bosi mpaka sasa sijafanikiwa kumpata Ditrov.”<br />
“Umepiga simu yake ya mkononi?”<br />
<br />
“Ndiyo, bosi, tena zote mbili.”<br />
“Sasa atakuwa wapi huyu?”<br />
“Kwa kweli hata mimi inanishangaza.”<br />
“Jaribu kwa mara ya mwisho kumtafuta nitahitaji majibu kama bado atakuwa hapatikani basi taarifa itolewe polisi, sawa?”<br />
“Nitafanya hivyo,” alijibu katibu muhtasi na kukata simu.<br />
<br />
***<br />
Wakaanza kuishi pamoja kama mke na mume, katika maisha yaliyojaa furaha, huzuni zote zilizokuwa zimewafunika zikaondoka ingawa Phillip hakuisahau familia yake, kila siku ya Jumapili ilikuwa ni lazima asindikizwe na mke wake wakiwa njiani kuelekea kanisani hadi makaburini ambako alisali akimkumbuka mke wake Genevieve na watoto wao Dorice na Dorica.<br />
<br />
Wiki moja baada ya kufunga ndoa maisha yakiwa ya furaha Lina alitakiwa kurejea kazini, hivyo alilazimika kumpa Phillip taarifa juu ya habari hiyo.<br />
“Mpenzi!”<br />
“Ndiyo,” Phillip aliitika<br />
“Kesho nitaanza kazi.”<br />
<br />
“Vyema mke wangu mimi nitakuwepo tu hapa nyumbani.”<br />
“Nyumbani?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Ok! Nahitaji kufahamu ulisomea nini?”<br />
“Nilisomea mambo ya sheria.”<br />
“Unao uzoefu wa kutosha?”<br />
<br />
“Kabisa.”<br />
“Basi nitakutafutia kazi nahitaji utoke nyumbani ili usiwe mpweke.”<br />
“Mwaa! Mwaa!” Phillip alimbusu Lina mfululizo.<br />
“Ahsante nakupenda Phillip, hakika nitakufanya kuwa mwanaume mwenye furaha siku zote.”<br />
<br />
“Nitafurahi sana Lina, nakuwa mpweke zaidi pale ninapokumbuka familia yangu, hakika niliipenda lakini naona yalikuwa mapenzi ya Mungu wote wakaniacha, naamini ujio wako kwangu utanirejeshea furaha iliyopotea miaka mingi kabla.”<br />
<br />
“Hakika nakupenda amini,” Lina aliongea huku akimkumbatia Phillip wote kwa pamoja wakajifunika shuka na kulala. Kwao usiku ulionekana kuwa mfupi, hakuna aliyekuwa akitamani kumwacha mwenzake kitandani lakini kwa Lina ilikuwa ni lazima afanye hivyo kutokana na kazi yake. Hivyo alijilazimisha na kuamka kitandani kisha kuingia bafuni kuoga na kujiandaa tayari kwa kwenda kazini.<br />
“Nitarejea muda si mrefu, nikuletee nini mpenzi?”<br />
“Mh! Mh!” Phillip aliguna.<br />
<br />
“Sema basi nikuletee kitu gani?”<br />
“Nakuhitaji wewe,” alisema Phillip akimvuta Lina na kumpiga busu huku akimtakia siku njema.<br />
Taratibu akatoka chumbani na kufunga mlango nyuma yake huku akimwacha Phillip kitandani.<br />
<br />
****<br />
Kwa muda wa saa tatu katibu muhtasi aliendelea kujaribu simu ya Ditrov bila majibu yoyote na hata alipojaribu kutuma mtu nyumba kwake na sehemu mbalimbali ambazo alifahamu angeweza kuwepo, bado hakupatikana.<br />
“Ni vyema nikamtaarifu bosi juu ya Ditrov kwamba hapatikani,” aliwaza akinyanyua simu na sekunde mbili tu baadaye sauti nzito ikasikika upande wa pili.<br />
<br />
“Ndiyo.”<br />
“Bosi sijafanikiwa kumpata.”<br />
“Unasema?”<br />
“Ditrov hapatikani tumejaribu kufuatilia sehemu mbalimbali ambazo mara nyingi hupenda kutembelea, majibu yanayotolewa ni yaleyale kwamba hajaonekana.”<br />
<br />
“Mh! Piga simu polisi kisha utoe taarifa, inawezekana ametekwa au kuuawa na watu fulani, unanisikia?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Nahitaji kufahamu majibu ya polisi mara moja na kama inawezekana msako mkali ufanyike, nataka Ditrov apatikane haraka iwezekanavyo,” alisema Victor Fedorov kwa hasira kali na kukata simu.<br />
<br />
“Haa! Haaa! Haaa!” Victor Fedorov alicheka huku akinyanyuka kitini taratibu akasogelea picha kubwa iliyokuwa ukutani kisha kuibusu.<br />
“Merina! Mariya! Nitawapenda mpaka kufa siko tayari kuwapoteza kwa gharama yoyote ile, ndiyo maana nimeamua kumuua Ditrov ili kuficha siri hii. Mwaa! Mwaa!” Victor Fedorov aliongea akiikodolea macho picha hiyo.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Ditrov ndiyo huyo amezamishwa baharini.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.51.<br />
<br />
ILI asigundulike kwa mauaji ya Ditrov anampigia simu katibu muhtasi wake akimtaka amtaarifu Ditrov kwamba alikuwa akimhitaji ofisini kwake kwa kazi maalum. Ditrov anatafutwa kwa muda bila mafanikio.<br />
<br />
Katibu muhtasi anamrejeshea majibu kwamba mpaka wakati huo bado Ditrov alikuwa hajapatikana sehemu yoyote ile.<br />
<span class="text_exposed_show"> Uamuzi pekee wa Victor Fedorov aliyekuwa akifahamu wazi mauaji aliyoyafanya, anaamuru taarifa hizo zitolewe kwa jeshi la polisi ili msako maalum ufanyike haraka na Ditrov apatikane.<br />
<br />
Ili kuficha siri ya mauaji ya Ditrov, Victor Fedorov anaudanganya umma wa Urusi kwamba naye pia yuko tayari kufanya kila kinachowezekana ili mradi tu Ditrov apatikane, hivyo ameamua kwenda makao makuu ya polisi na kuzungumza na mkuu wao ili kama jeshi hilo lingehitaji msaada wowote kutoka kwake basi wasisite kumweleza.<br />
<br />
Baada ya maongezi hayo wote wawili waliagana na Victor Fedorov akatoka nje ya ofisi moja kwa moja akaliendea gari lake na kupanda kisha kuwasha na kuondoka kwa kasi ya ajabu, kwa kumwangalia alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa kwa upotevu wa Ditrov lakini ukweli ni kwamba aliidanganya dunia, aliufahamu ukweli wote na mpaka wakati huo alishaamini kwamba Ditrov alikuwa marehemu hivyo isingekuwa rahisi kupatikana tena.<br />
Je, nini kinaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
Jeshi la polisi nchini Urusi lilidhamiria kufanya kila kilichowezekana ambapo Ditrov alitafutwa kila pembe, Urusi ikabinuliwa nje ndani, vyombo vya habari, zikiwemo televisheni, vikirusha matangazo na kuonyesha picha ya Ditrov kwamba alikuwa amepotea katika njia ya kutatanisha na alikuwa akitafutwa kwa udi na uvumba na yeyote ambaye angefanikisha kupatikana kwake awe mzima au marehemu basi angelipwa kiasi kikubwa cha fedha.<br />
<br />
Watu nchini humo wakanyanyuka, wakaingia katika msako, Ditrov alikuwa akisakwa, kiasi kikubwa cha fedha alichokitangaza Victor Fedorov kiliwachanganya watu wengi.Wakati msako huo ukiendelea, Victor Fedorov alikuwa akifuatilia kila kitu kwa karibu, aliwaona watu wote kuwa wajinga kwake, kwani ukweli ni kwamba mpaka wakati huo Ditrov hakuwa tena hai, hicho ndicho alichoamini, hivyo hata zawadi aliyokuwa ameitangaza kwa umma alifahamu wazi kwamba isingekwenda kwa mtu yeyote yule.<br />
<br />
“Hata kitokee nini hawawezi kumpata niko tayari kufanya kila kitu watakachohitaji ili mradi tu kuuficha ukweli huu, sipo tayari, duniani hakuna siri ya watu wawili, hivyo kifo cha Ditrov kimefanya siri kubaki kwangu peke yangu, Mungu atanisamehe,” aliwaza akiangalia tangazo lililomwonyesha Ditrov likipita kwenye televisheni kubwa iliyokuwa ofisini kwake.<br />
<br />
Mpaka wakati huo jeshi la polisi lilishafanikiwa kukagua hospitali zote nchini Urusi na kupata kibali cha kuingia katika vyumba vya kuhifadhia maiti kumsaka mtu huyo lakini bado hakupatikana sehemu yoyote, nao pia wakaanza kupoteza matumaini kwani upotevu wa mtu huyo ulisababisha kusimamisha kazi zao nyingi sana kutokana na Victor Fedorov kuwa na nguvu na ushawishi mkubwa sana ndani ya nchi hiyo.<br />
<br />
Wiki ya kwanza ikapita msako ukiendelea kwa nguvu zote, wiki ya pili nayo ikapita hatimaye mwezi bila Ditrov kupatikana sehemu yoyote. Jeshi likashindwa kuelewa ni wapi alikokuwa mtu huyo.<br />
“Ngrii!Ngrii!Ngrii!” mlio simu ukasikika ndani ya ofisi ya Mkuu wa Polisi.<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Sawa mkuu, hakuna shida hata sisi wenyewe tumeona ni vyema tukapumzika ili tujipange tena upya kutafuta njia nyingine, zoezi hili limekuwa gumu sana kwetu,” aliongea Mkuu wa Polisi ofisini kwake.<br />
<br />
Victor Fedorov aliyekuwa upande wa pili wa simu ndiye aliyekuwa akiongea na mkuu huyo wa polisi akimpa ushauri wa juu ya zoezi hilo kwamba sasa lilikuwa limeshindikana hivyo watafute mbinu nyingine zitakazowezesha kupatikana kwa Ditrov.<br />
<br />
Mkuu wa polisi alikubaliana na Victor na kusitisha zoezi hilo akiwa haelewi kabisa upande wa pili wa myu huyo, akaunga mkono hoja na kukata simu.<br />
<br />
“Sasa nina hakika Ditrov atakuwa amekufa, laiti kama angepona angeshajitokeza ninavyomfahamu mimi ni mtu hatari sana huyu, hawezi kuwa hai akaendelea kujificha ni lazima angetoka na kuuelezea umma kila kitu,” aliwaza Victor Fedorov akiwa ndani ya ofisi yake.<br />
<br />
***<br />
Kitendo cha Lina kuongea na bosi wake na kumweleza kwamba katika ofisi yao alihitajika mwanasheria anayefahamu vyema sheria, kilikuwa ni kama bahati ya mtende, akatembea taratibu na kurejea ndani ya ofisi yake, huku machozi ya furaha yakimtoka, alishindwa kuelewa ni bahati gani iliyokuwa ikimtokea, machozi ya furaha yakaendelea kumtoka.<br />
<br />
“Ahsante baba, Mungu kweli unatenda, hatimaye Phillip naye amepata kazi?” alijiuliza.<br />
Kwa siku nzima, muda kwa Lina ulikwenda taratibu, saa zilikuwa hazisogei hamu yake kubwa ikiwa ni kurejea nyumbani na kumweleza Phillip juu ya habari aliyokuwa ameipata.<br />
“Phillip atafurahi sana kusikia habari hii,” aliwaza.<br />
<br />
Akiwa ofisini kwake akakivuta kiti na kuketi, sauti nyingi zikimwijia kichwani mwake, tangu siku aliyokutana na Phillip jinsi alivyomweleza kwamba bado alikuwa akimpenda na hatimaye kufunga ndoa na sasa alikuwa mke wa mwanaume aliyempenda kwa moyo wake wote.<br />
<br />
“Ni kweli Phillip amefiwa na mke na watoto wake, lakini ilikuwepo sababu jambo hilo litokee ili mimi niweze kumpata, masikini Genevieve watoto wake Dorice na Dorica nauahidi moyo wangu kumpa Phillip furaha yote mpaka mwisho wa maisha yetu, hakika ninampenda kwa dhati,” alijisemea Lina kwa sauti ya chini chini.<br />
<br />
Muda wa kurejea nyumbani ulipofika, hakuwa na sababu ya kuendelea kukaa ofisini, haja ya moyo wake ilikuwa ni kufika nyumbani na kumkuta mume wake mpendwa Phillip ili amweleze habari njema aliyokuwa nayo.<br />
Huku akitembea kwa madaha, mkononi akiwa amening’iniza funguo akalisogelea gari lake akaingia ndani na kisha kuondoka kwa mwendo wa kasi, mawazo yake yote yakiwa kwa Phillip.<br />
<br />
“Ninampenda, nafahamu wazi hata yeye ananipenda hanidanganyi hata kidogo, nitafanya kila kitu kuhakikisha simpotezi, mwanaume niliyempenda akanifanya nikapata matatizo mengi maishani mwangu ndiye aliyeko ndani ya nyumba yangu sasa tena akiwa mume wangu!” aliongea Lina huku akizidi kukanyaga mafuta.<br />
<br />
Kwa mwendo wa saa moja na dakika kadhaa tayari alikuwa nje ya lango la nyumba yake, bila kuchelewa akapiga honi na lango likafunguliwa, akapita moja kwa moja ndani bila kusema kitu chochote na mlinzi wake.<br />
<br />
“Mh!” mlinzi aliguna akishuhudia gari likizidi kutokomea. Kilikuwa ni kitendo cha ajabu sana kwani mazoea aliyokwishajijengea ilikuwa ni lazima asimamishe gari na kumtania kidogo lakini siku hiyo haikuwa hivyo kwa Lina ilionekana kuwa tofauti.<br />
“Pengine anaumwa au kuna nini kimempata? Si kawaida ya bosi wangu kuwa hivyo lazima takuwa na walakini. Ngoja nisogee karibu nione,” aliongea mlinzi akisogea kwa mwendo wa pole.<br />
<br />
“Bosi!” aliita.<br />
“Bee!” Lina akaitika akitembea kwa kasi kuelekea lango la kuingilia ndani ya nyumba yake.<br />
“Nini tatizo si kawaida yako kuwa hivyo unaumwa?”<br />
“Mh!” alijibu akiingia ndani.<br />
Mlinzi huyo alibaki hapo akiwa haelewi ni kitu gani kilikuwa kimempata bosi wake huyo, haraka akapata wazo kichwani mwake akaamua kuzunguka upande wa pili wa nyumba ambako dirisha la chumba cha bosi lilikuwepo huko.<br />
<br />
“Ngoja nisimame hapa kama kuna tatizo nitajua kupitia hapa,” aliongea mlinzi akisogea kwa kunyata dirishani.<br />
“Darling! Darling! Uko wapi? Tafadhali njoo, nakuhitaji haraka sana!” sauti ya Lina ilisikika.<br />
“Yes baby!” (Ndio mpenzi) sauti ya Phillip ikasikika kwa chini kutoka chumbani.<br />
“Bado umelala?” Lina aliuliza.<br />
<br />
“Ndiyo!” Phillip akajibu.<br />
Kwa mwendo wa haraka h Lina akatembea kuelekea chumbani akafungua mlango na kuingia, Phillip bado alikuwa kitandani akiwa amelala na shuka likiwa limemfunika mpaka kichwani.<br />
“No! Unaumwa?” Lina aliuliza.<br />
“Mh!” Phillip alijibu akitingisha kichwa.<br />
<br />
Bila kuchelewa Lina akalivuta shuka na kulitupa pembeni, Phillip akaonekana na alipomwangalia vyema usoni aligundua alikuwa akilia kwani macho yake yalivimba kupita kiasi.<br />
“What happened?” (Nini tatizo?)<br />
“Familia yangu, mke na watoto wangu wapendwa!” alijibu Phillip kwikwi ya kulia ikizidi kumkaba.<br />
<br />
“Sikiliza mume wangu hebu niambie unachohitaji tufanye nini ili upate furaha iliyopotea, niambie niko tayari kutoka moyoni mimi siipendi hali hii!”<br />
“Watoto! Nahitaji kupata mtoto angalau mmoja,” aliongea Phillip akilia kwa uchungu.<br />
<br />
Maneno hayo pekee yalimfanya Lina aelewe ni kiasi gani Phillip alikuwa katika upweke bila kuchelewa akaanza kuvua nguo moja baada ya nyingine na kuzitupa pembeni kisha kukisogelea kitanda na kupanda juu yake akamvuta Phillip na kumkumbatia, mabusu mfululizo yakishuka juu ya mwili wa Phillip na neno I love you, likisikika.<br />
<br />
Mlinzi akiwa amesimama nje ya dirisha bila kuelewa ni kitu gani kilikuwa kikitokea alisikia sauti nyingine.<br />
“Jwig!Jwig!Jwig!” kitanda kikipiga kelele.<br />
“Mh!” mlinzi aliguna akiondoka eneo hilo.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Nini kitatokea baada ya Lina kumweleza Phillip juu ya kazi iliyopatikana ofisini kwao? Je, watafanya nini kupata watoto? Fuatilia kesho kama kawa USIKU MWEMA NAWAPENDA NYOOOTE.....</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.52.<br />
<br />
KITENDO cha Lina kuongea na bosi wake na kumweleza kwamba katika ofisi yao alihitajika mwanasheria anayefahamu vyema sheria, kilikuwa ni kama bahati ya mtende, baada ya kumaliza maongezi Lina anatembea na kurejea ndani ya ofisi yake, huku machozi ya furaha yakimtoka, anashindwa kuelewa ni bahati gani iliyokuwa ikimtokea.<br />
<br />
Muda wa kurejea nyumbani unapofika, ni<span class="text_exposed_show"> wakati huo ndiyo haswa aliokuwa akiusubiri kwa hamu kubwa, ili akamweleza Phillip habari njema aliyokuwa ameipata.Moja kwa moja anatembea kutoka nje ya ofisi yake kisha kulielekea gari lake aina ya Land Cruiser, anafungua mlango na kuingia ndani yake kisha kuliwasha na kuliondoka kwa mwendo wa kasi mawazo yake yote yakiwa kwa Phillip.<br />
<br />
Kwa mwendo wa saa moja na dakika kadhaa tayari alikuwa nje ya lango la nyumba yake bila kuchelewa akapiga honi na lango likafunguliwa, akapita moja kwa moja ndani bila kusema kitu chochote na mlinzi wake, hali ambayo ilimshtua sana mlinzi huyo, kwani haikuwa kawaida ya Lina kufanya hivyo ilikuwa ni lazima amtanie kidogo kisha kuelekea kwenye maegesho.<br />
<br />
Hofu inamwingia mlinzi, hivyo kumlazimu kumfuata kujua ni kitu gani kilikuwa kimempata bosi wake, ananyata mpaka karibu na dirisha la chumba na kusikiliza, anasikia maongezi kidogo na baada ya muda sauti ya kitanda inasikika, anaguna na kuondoka eneo hilo.<br />
<br />
Upande wa pili wa hadithi hii tunamwona tajiri Victor Fedorov akiwa kifua mbele katika msako wa Ditrov, anaitumia nafasi hiyo kuficha uovu kwani ukweli wote anaufahamu. Zoezi hilo linaendelea kwa muda mrefu bila mafanikio, hatimaye jeshi la polisi linasimamisha msako ili kutafuta njia mbadala ya kumpata Ditrov. Taarifa hizo ndizo zinamfanya Victor Fedorov ajione mshindi.<br />
<br />
Je,nini kitaendelea? Ditrov amekufa kweli? Nini hatima ya Phillip na Lina? SONGA NAYO…<br />
<br />
Kwa muda wa saa mbili mfululizo, Phillip na Lina walikuwa kitandani kila mmoja akimwonyesha mwenzake ufundi wake wote kuhakikisha anapata furaha aliyoitarajia. Si Phillip wala Lina wote wawili walikuwa katika ulimwengu mwingine wakisahau shida na matatizo yote yaliyokuwa yamepita katika maisha yao.<br />
<br />
“Phillip” Lina aliita.<br />
“Naam mke wangu”<br />
“Leo nahitaji uniambie ni kitu gani nitakufanyia ili uwe na furaha, sihitaji kuona machozi yako kila wakati, yananisikitisha mno!”<br />
“Unajua nini?”<br />
<br />
“Mh!” Lina aliguna.<br />
“Lina.” Phillip aliita huku macho yake yakimuangalia Lina.<br />
“Bee.”<br />
“Nahitaji mtoto hata mmoja tu”<br />
“Hicho tu?”<br />
“Hakika ndicho.”<br />
<br />
“Phillip ni jambo la kuzungumza tu na si kuliweka kichwani mwako.”<br />
“Nitazungumza nini Lina ili hali unafahamu wazi kwamba sina uwezo wa kuzaa!”<br />
“Najua lakini kwangu hilo si tatizo.”<br />
“Kwangu ni tatizo mpenzi, nahitaji mtoto hata mmoja tu ambaye ataniita baba nami nitamwita mwanangu.”<br />
<br />
“Mh!” Lina akaguna tena huku akionyesha kusikitishwa na maneno ya Phillip.<br />
Kwa muda wote wapenzi hao walikaa kimya kila mmoja akifikiri ni jinsi gani wangeweza kupata watoto, kwa Lina halikuwa swali gumu kwani yeye alikuwa ni mzima kwa kila kitu tatizo pekee lilikuwa kwa Phillip ambaye mbegu zake hazikuwa na uwezo wa kurutubisha yai la mwanamke hivyo hata kama wangefanya tendo la ndoa kwa muda wa zaidi ya miaka kumi bado uwezekano wa kupata mtoto usingekuwepo.<br />
<br />
“Phillip!” Lina aliita akimgusa mumewe begani.<br />
“Nakusikia.”<br />
“Twende tukaoge kisha tujadiliane kuhusu jambo hili.”<br />
“Sawa.” Alijibu Phillip wakinyanyuka kutoka kitandani wakajikongoja hadi bafuni na kuanza kuoga.<br />
<br />
Kwa muda wa dakika kumi nzima waliutumia kuoga bafuni huko Lina akiongea mambo mengi kuhusu mapenzi, nia yake kubwa ikiwa ni kumfanya Phillip aondokane na msongo wa mawazo uliokuwepo kichwani mwake. Hatimaye wakamaliza na kurejea tena chumbani ambako Lina alimkaribisha Phillip kwenye kiti maalum kisha yeye akaelekea sebuleni ambako alifungua jokofu akatoa boksi la juisi, akachukuwa glasi mbili na kurejea chumbani.<br />
<br />
Kwa mwendo wa madaha huku akiwa ndani ya taulo dogo la rangi nyeupe, Lina alitembea mpaka karibu kabisa na Phillip, akaweka vitu alivyokuwa navyo mezani kisha kumsogelea Phillip na kumbusu mfululizo.<br />
“Mwaa!Mwaaa!Mwaaa!”<br />
“Ahsante,” alijibu Phillip kwa sauti ya chini.<br />
<br />
Akiwa hapo, Lina alifungua boksi na kuanza kumimina juisi kwenye glasi moja baada ya nyingine na kumkaribisha Phillip huku akinyanyua glasi na kuipeleka mdomoni mwake kisha kuirejesha tena kwa Phillip kama ishara ya kuonyesha pendo zito alilokuwa nalo juu yake.<br />
“Nakupenda.”<br />
“Mimi pia nakupenda Lina.”<br />
<br />
“Ahsante, lakini pia nina habari njema sana kwako.”<br />
“Kuhusu mtoto?” Phillip aliuliza.<br />
“Mh! Hapana lakini ni njema.”<br />
“Tafadhali nieleze usikawie.”<br />
“Mh! Mh!” Lina aliguna mfululizo.<br />
<br />
“Hebu shika mapigo ya moyo wangu yanasubiri habari hiyo kwa hamu kubwa, tafadhali nieleze kabla sija…” Phillip aliongea lakini kabla hajafika mwisho wa sentensi yake Lina akanyoosha mkono wake na kuziba mdomo wa Phillip.<br />
“Kunywa juisi kwanza nitakueleza si habari mbaya ni njema sana wewe mwenyewe hakika utafurahi.”<br />
“Kweli?”<br />
<br />
“Kabisa.”<br />
Taratibu wakaendelea kunywa juisi huku mikono ya Lina ikipita huku na kule mwilini mwa Phillip huku maongezi matamu kati yao yakiendelea.<br />
Hakika wawili hao walipendana kwa dhati, hawakuwa tayari kukumbuka historia zao za nyuma na hata ilipotokea jambo hilo likajirudia vichwani mwao basi waliona ilikuwepo haja ya kupuuza mawazo hayo na kuendelea na starehe.<br />
<br />
Muda ukazidi kusonga bila Lina kufungua mdomo wake kumweleza Phillip kitu chochote, moyoni akitafakari ni jinsi gani habari hiyo ingepokelewa kwani alifahamu wazi kwa Phillip kupata kazi ingekuwa njia moja wapo ya kumwondoa katika msongo wa mawazo aliokuwa nao na hilo lingekuwa limekwisha na jambo ambalo lingebaki kuwa kitendawili katika maisha yao, watoto ambao kwa Lina japo alikuwa mwanamke kamili hakuona umuhimu wowote alichohitaji yeye kwa wakati huo ni kuwa na mwanaume aliyempenda kwa dhati na si kingine.<br />
<br />
“Tafadhali Lina hebu nitoe katika mateso haya, nahitaji kufahamu ni kitu gani unataka kunieleza.”<br />
“Hakuna jambo baya mpenzi wangu ni habari juu ya kazi”<br />
“Kazi?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Imefanya nini?”<br />
<br />
“Amini tayari umepata kazi”<br />
“Mungu wangu! Unasema kweli Lina?”<br />
“Ni kweli na si ndoto, Phillip tayari umeishika kazi mikononi mwako.”<br />
“Wapi na lini?”<br />
“Hivi sasa ninavyozungumza na wewe kesho asubuhi na mapema tutaongozana, kitu cha muhimu ni vyeti vyako vyote.”<br />
<br />
“Sehemu gani?”<br />
“Ofisini kwetu, Phillip ni bahati iliyoje, leo nilipoingia tu ofisini bosi wangu akaniita na kunieleza kwamba shirika letu lilihitaji mtu anayefahamu vyema sheria, akili yangu ikakumbuka kwamba hata wewe ulisoma sheria na uliimudu vyema kazi hiyo.”<br />
<br />
“Lina ahsante kwa mara nyingine, nimeamini unanipenda nami ninakupenda pia, moyoni mwangu naanza kuamini kabisa kwamba Mungu alikuwa nayo sababu ya mambo yaliyotokea nyuma ya kupoteza mke na watoto wangu wote akifahamu wazi kwamba nitakutana na mwanamke mwingine atakayenipenda kama Genevieve, Mungu azilaze roho za wapendwa wangu hawa mahali pema peponi amina,” alisema Phillip machozi yakimtiririka, wakati hayo yakiendelea Phillip alihisi ni ndoto lakini alipofungua macho vizuri na kumwona Lina mbele yake akiwa katika sura ya kutabasamu, akanyoosha mikono na kumwelekea ambapo bila kuchelewa Lina akajichomeka katikati ya mikono hiyo wakakumbatiana na kuanza kulia.<br />
<br />
***<br />
Wiki moja baadaye Victor Fedorov akiwa ofisini kwake akiamini kabisa kwamba kila kitu kilikuwa kimekwenda kama alivyotaka, anashtushwa na taarifa ya habari kwenye televisheni.<br />
“Mh ni kitu gani hiki?” anajiuliza akisogea karibu kabisa ili kusikiliza kwa ukaribu.<br />
<br />
Mamia ya watu nchini Urusi walikuwa wakiandamana kupiga hoja ya jeshi la polisi kuhusu msako wa Ditrov, kwa ilivyoonekana wengi walikuwa wameumizwa na jambo hilo na walichokihitaji kwa wakati huo ni kufahamu ukweli juu ya mauaji hayo, wakisisitiza na kulaani kwa nguvu zote uamuzi huo, wananchi wengi wakidai kwamba nyuma ya pazia kulikuwa na siri nzito kwani kabla Ditrov hajapotea tayari washirika wake wote alioshirikiana nao katika kazi waliaminika kufa tena vifo vya kutatanisha.<br />
<br />
“Mh! Ni lazima niwafunge midomo, wataniletea matatizo hawa, sihitaji dunia ifahamu kwamba ninahusika na vifo hivi, nataka iendelee kubaki siri tena siri kubwa, sasa ni wakati wa kuonyesha jeuri ya fedha zaidi ili kulifanya jeshi la polisi likae kimya milele,” aliongea Victor akinyanyua mkono wa simu.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.53.<br />
<br />
“Hello!” akaita Victor Fedorov kwa sauti nzito.<br />
<br />
“Ndiyo,” sauti upande wa pili ikajibu.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
“Ah! Naweza kuongea na mkuu wenu, tafadhali?” aliuliza na ukimya wa ajabu ukatokea kwake akiwa bado ameshikilia mkono wa simu.<br />
<br />
Akili yake yote ilisharuka, hakuelewa ni nini kingefuata baada ya hapo kwani kwa jinsi wananchi walivyokuwa wamekasirishwa na mauaji yaliyotokea, waliapa kufanya chochote ili mradi tu wapate ukweli juu ya vifo vya ndugu zao.<br />
<br />
Walikuwa tayari kufa lakini jeshi la polisi litoe tamko ambalo lingewaridhisha wote.<br />
<br />
Pamoja na kiyoyozi kikali kilichokuwa ndani ya ofisi yake asubuhi hiyo Victor Fedorov alikuwa akitiririkwa na jasho mwili mzima akifahamu wazi kwamba kama ingetokea siri yake ikagundulika basi angepoteza kila kitu alichokuwa nacho, si utajiri tu hata watoto wake na heshima aliyokuwa amejijengea kwa muda mrefu. <br />
<br />
Akiwa hapo taswira za watoto wake pacha, Mariya na Marina zikamwijia kichwani mwake, ni watoto hao ndiyo walisababisha afanye mauaji yaliyotokea ili kuficha siri.<br />
<br />
“Naitwa Victor Fedorov, nahitaji kuonana na wewe tena ikiwezekana leo hii, ni muhimu sana, kuna taarifa nimeiona ofisi kwangu sasa hivi juu ya wananchi wanavyoandamana imeniumiza sana napenda nami niungane nao kufanya msako huo kwani nimepoteza mtu muhimu sana katika kazi zangu,” alisema akipigapiga meza kuonyesha msisitizo.<br />
<br />
“Karibu!” mkuu wa jeshi alijibu upande wa pili wa simu.<br />
<br />
“Ok! Nitafika hapo ofisini kwako muda si mrefu, ni vyema tukapata muda wa faragha kwa mazungumzo yetu na ningeomba asiwepo mtu mwingine yeyote wakati wa maongezi hayo.”<br />
<br />
“Sawa hilo litafanyika,” sauti upande wa pili ikajibu na hapohapo simu ikakatwa.<br />
<br />
Mkuu wa jeshi la polisi hakuelewa siri iliyokuwa ikimsumbua Victor Fedorov, alimwamini kwa asilimia mia moja kwamba naye alikuwa ameumizwa na mauaji hayo ndiyo maana alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha msako unafanyika kwa namna yoyote ile.<br />
<br />
Victor Fedorov akasimama kutoka kitini mwake na kutembea mpaka mbele ya kioo kikubwa kilichokuwa ndani ya ofisi yake, hapo akaweka tai yake vyema na kuangalia uso wake na kwa kutumia kitambaa kidogo alichokuwa nacho akajifuta uso wake kisha kuchukua miwani ya rangi nyeusi akaivaa.<br />
<br />
Kwa alivyoonekana, alidhamiria kuficha siri ya mauaji lakini msaada mkubwa ungetoka kwa jeshi hilo la polisi na kitu pekee ambacho angefanya ni kutumia fedha tu ili mambo yaende kimya na hatimaye kupotea kabisa.<br />
<br />
Akatoka nje ya ofisi yake na kumuaga katibu muhtasi wake kisha kutembea mpaka sehemu alipoegesha gari lake na kupanda, mwendo alioondoka nao eneo hilo ulimshangaza kila mmoja aliyemwona kwani haikuwa kawaida yake.<br />
<br />
“Mh!” mmoja wa wafanyakazi wake akaguna.<br />
<br />
“Leo kuna tatizo hapa si kawaida ya bosi, hata miwani ulishawahi kumwona ameivaa?” mwingine alidakia.<br />
<br />
“Mimi naona kupotea kwa Ditrov kumesababisha matatizo makubwa sana, alikuwa ni mtu wake wa karibu sana.”<br />
<br />
“Nakuunga mkono, hali hiyo imemchanganya kabisa bosi wetu,” yalikuwa ni maongezi ya wafanyakazi wawili waliokuwa nje ya ofisi wakimshuhudia Victor Fedorov akitokomea.<br />
<br />
Dakika kumi baadaye alishafika makao makuu ya jeshi la polisi Urusi, akaegesha gari na kushuka na kuanza kutembea kuelekea ndani ya ofisi, huku akiwa mwenye wasiwasi mwingi.<br />
<br />
Aliangaza huku na kule na kuingia ndani ambako alipokelewa na kukaribishwa moja kwa moja kwenye ofisi ya mkuu wa jeshi.<br />
“Habari za muda?”<br />
<br />
“Njema tu, pole na kazi.”<br />
<br />
“Ah, tumeshazoea sisi, ndiyo kazi zetu.”<br />
<br />
“Kuna jambo moja tu kwa sasa,” alisema Victor kwa kujiamini.<br />
<br />
“Sawa kabisa.”<br />
Mkuu wa jeshi akakaa vyema ili kumsikiliza Victor Fedorov.<br />
“Kuna kitu gani kinaendelea mpaka sasa juu ya msako wa Ditrov?” Victor Fedorov aliuliza akivua miwani yake.<br />
<br />
“Mh! Kama tulivyokubaliana, kwamba tusitishe zoezi mpaka tujipange upya halafu tuendelee lakini cha kushangaza wananchi wameanza kuingia mitaani kupinga uamuzi huo huku wakisisitiza msako uendelee tena kwa nguvu zote, wengi wakidai kwamba kabla ya kupotea kwa Ditrov washirika wake wote waliuawa tena vifo vya kutatanisha.<br />
<br />
“Kwa hiyo ninyi kama jeshi mmeamua nini?”<br />
“Tuendelee na msako…” alisema mkuu wa jeshi lakini kabla hajamaliza sentensi yake kelele za ajabu zikasika kutoka nje ya jengo.<br />
<br />
“Ndiyo, tunataka uchunguzi uendelee, tunataka kufahamu ndugu zetu wako wapi, tunajua kuna mtu mkubwa anayefanya mauaji hayo, pengine kwa sababu zake binafsi au kuficha siri fulani…Tunamtaka huyo atafutwe na ahukumiwe!” sauti zilisikika zikizidi kusogelea karibu kabisa.<br />
<br />
“Choma hiyo! Choma jengo bila kuogopa, hakuna kurudi nyuma tunahitaji kufahamu ukweli tumechoshwa na jeshi kila wakati kutudanganya tu, chomaaaaa!” sauti zilisikika zikisogea kuelekea makao makuu ya Jeshi la Polisi la Urusi.<br />
<br />
“Mungu wangu!” mkuu wa jeshi alisema.<br />
<br />
“Nini tena?”<br />
“Wananchi hatimaye wameamua kuja mpaka huku, hili jambo siyo dogo hata kidogo ni lazima msako uendelee haraka sana,” alisema Mkuu wa Jeshi la Polisi la Urusi huku akinyanyua simu. Lakini kabla hajabonyeza namba mlango wa chumba chake ukafunguliwa kwa nguvu na askari mmoja akaonekana.<br />
“Mkuu kuna matatizo.”<br />
<br />
“Kimetokea nini?”<br />
<br />
“Wananchi!”<br />
<br />
“Wanafanya nini?”<br />
<br />
“Wameamua kujitokeza kupambana na polisi eti wanadai kwamba kuna siri kubwa tunayoifahamu kuhusu mauaji yanayotokea.”<br />
<br />
“Kwahiyo?”<br />
<br />
“Wanaonekana wana hasira sana, tena wameshachoma vituo vya polisi karibu mji mzima na sasa wameingia hapa makao makuu.”<br />
<br />
“Hebu nitoke kuongea nao.”<br />
<br />
“Mkuu hapana, hutaweza! Wanaonekana kuwa na hasira nyingi sana.”<br />
<br />
“Ni lazima kifanyike kitu hapa kunusuru usalama wetu na mali za nchi.”<br />
<br />
“Kipi?”<br />
<br />
<br />
“Mabomu ya machozi kuwatanya kwa nguvu sehemu zote ambazo wameandamana, umesikia?”<br />
<br />
“Ndiyo mkuu,” alijibu askari huyo akitoka mbio kuelekea nje ambako alishuhudia maelfu ya watu wakizidi kusonga mbele kulielekea lango kuu ili waingie ndani na kufanya walichokitarajia.<br />
<br />
Askari huyo alipotupa macho mbele ili kuangalia vizuri, alishuhudia maaskari wengi wakiwa chini.<br />
<br />
Lilionekana kuwa jambo la kutisha wananchi walikuwa wamedhamiria kwa nguvu zote kuingia mitaani si kufanya fujo bali kulitia hekaheka jeshi la polisi ili liweze kuendelea na msako wake badala ya kukaa kimya.<br />
<br />
“Hatimaye mwisho wangu umekuwa mbaya!” Victor Fedorov aliongea kwa sauti huku akinyanyuka kitini.<br />
<br />
“Unasema?” mkuu wa jeshi aliuliza.<br />
<br />
“Mh!” Victor Fedorov aliguna, na tayari alishaukamata mlango wa chumba akaufungua na kutoka nje huku akikimbia.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Siri yake imegundulika? Nini hatima yake?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.54.<br />
<br />
<br />
Walikuwa ni watoto wazuri, hakuna mtu aliyewaona watoto hao na kusita kutoa sifa midomoni mwao, japo walikuwa wadogo lakini uzuri wao ulionekana waziwazi na watu wengi kusema kwamba wakikuwa wangekuwa tishio kwa wanaume wengi nchini Urusi.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Ni watoto hao Pacha Mariya na Merina ndiyo walikuwa wakileta machafuko nchini Urusi bila wao wenyewe kufahamu siri nzito ilikuwa imefichwa, wakilelewa vyema na kusoma katika shule ya gharama huku wakihudumiwa kwa kila kitu walichohitaji wakiandaliwa kuja kuwa warithi wa mali za baba yao.<br />
<br />
Kila aliyewaona watoto hao hakusita kujiuliza maswali juu yao, kwani walimfahamu vyema Victor Fedorov na historia ya maisha yake alishawahi kuoa wanawake kadhaa na kuachana nao bila kuzaa nao watoto lakini ghafla watoto wawili wakaibuka na watu kuelezwa kwamba walikuwa ni watoto wake.<br />
“Mh! watoto wazuri sana!”<br />
“Ni kweli”<br />
“Ni wa nani?”<br />
“Victor Fedorov”<br />
“Huyu tajiri hapa Urusi?”<br />
“Haswa ndiye.”<br />
“Amezaa lini na wapi?”<br />
”Kwa kweli hilo swali hata mimi sifahamu ila wenyewe watoto ukiwauliza wanasema Victor Fedorov ndiye baba yao.”<br />
<br />
“Mh! Haya ukiwaangalia wamefanana naye lakini walikuwa wapi na mama yao ni nani?”<br />
<br />
“Mambo ya Ngoswe mwachie Ngoswe mwenyewe,” walikuwa ni walimu wawili wakiongea wakati watoto hao wakipita mbele yao.<br />
***<br />
Taarifa aliyokuwa ameipata Phillip kutoka kwa Lina ilimpa furaha ya ajabu mno, hakika hakuwaza wala kutegemea tena kwamba baada ya kifo cha mke na watoto wake wapendwa angerejea katika hali ya kawaida kwani alishapoteza matumaini na hakuwa na furaha tena lakini kukutana na Lina kulirejesha furaha iliyopotea miaka mingi huko nyuma.<br />
<br />
“Ahsante mke wangu ninakupenda.”<br />
“Nakupenda pia Phillip.” Lina alijibu macho yake yote yakimwangalia Phillip.<br />
<br />
“Hakika sina cha kukuzawadia laiti kama ningeweza…”aliongea Phillip lakini sentensi yake ikakatishwa na busu la Lina ambalo lilitua moja kwa moja mdomoni mwake.<br />
<br />
“Najua unachotaka kusema.”<br />
“Mh! Nini?”<br />
“Unataka kuzungumza juu ya mtoto.”<br />
“Ni kweli kabisa mke wangu sina uwezo wa kuzaa.”<br />
“Tutapata mtoto.”<br />
“Kwa njia gani?”<br />
“Hata kama tutalazimika kutumia fedha zote tulizonazo lakini tupate mtoto!”<br />
“Kivipi Lina?”<br />
“Nitakueleza siku nyingine leo tupumzike kwa ajili ya kesho nitahitaji utafute vyeti vyako vyote na kuviweka pamoja tayari kwa kazi kesho.”<br />
“Kesho?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Mh!” Phillip aliguna.<br />
“Kwa nini unaguna?”<br />
“Kesho sijajiandaa kabisa mke wangu.”<br />
<br />
“Nasema kesho ni lazima tuondoke wote hapa nyumbani kwenda ofisini.”<br />
<br />
“Sawa tuombe uzima,” alijibu Phillip na wote wakajitupa kitandani taratibu wakiwa hapo waliongea hiki na kile hatimaye wakapitiwa na usingizi.<br />
<br />
***<br />
Baaada tu ya kutoka ofisini kwa mkuu wa jeshi la polisi, Victor Fedorov huku akipishana na watu wengi njiani alifanikiwa kulifikia gari lake na kuingia ndani, akaliwasha na kuondoka hapo kwa kasi ya ajabu kichwani mwake akiwaza kitu kimoja tu watoto wake.<br />
<br />
Ni kweli alifahamu wazi kwamba wakati huo walikuwa shuleni lakini hakuelewa walikuwa katika hali gani kwani kwa jinsi hali ilivyoonekana mambo yalikuwa yameharibika kabisa.<br />
“Watoto wangu,”alitamka Victor Fedorov.<br />
<br />
Shule waliyosoma Mariya na Merina haikuwa umbali mrefu sana kutoka mahali Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Urusi yalipokuwa hivyo wasiwasi wake ukazidi kuongezeka maradufu.<br />
<br />
“Kwa jinsi hali ilivyo lazima niwafuate watoto wangu,” aliwaza Victor Fedorov akiendesha gari kwa kasi kuelekea huko, kichwani akamkumbuka Ditrov na unyama aliomfanyia, akaziona pia taswira za watoto wake Mariya na Merina wakimfurahia machozi ya uchungu yakamtoka lakini akajipa moyo na kusonga mbele kuelekea shuleni kwa watoto wake.<br />
<br />
Kwa mwendo wa dakika kumi nzima aliendesha gari hatimaye akafanikiwa kufika eneo la shule akiwa hapo akashangazwa na ukimya wa ajabu uliokuwepo, hapakuonekana dalili ya walimu wala wanafunzi.<br />
<br />
Haraka bila kuchelewa Victor Fedorov akaegesha gari lake na kushuka huku akiangaza macho huku na kule.<br />
<br />
“Kimetokea nini hapa?” akajiuliza mwenyewe akitembea kwa kasi kuelekea majengo ya ofisi za walimu huko nako hakukuta mtu.<br />
“Mungu wangu watoto wangu, haiwezekani,” aliongea Victor Fedorov akiingia mlango mmoja baada ya mwingine kukagua.<br />
<br />
Shule ilikuwa kimya kabisa, hapakuonekana mtu yeyote eneo hilo zaidi ya karatasi zilizokuwa zikipepea juu kutoka ndani ya majengo kwenda nje. Moyo wake ukamwenda mbio, jasho jingi likamtoka na alipojaribu kupaza sauti yake na kuita majina ya watoto wake halikupatikana jibu lolote.<br />
<br />
“Nimekwisha!”alisema Victor Fedorov akiporomoka chini kama mzigo.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000700d1600325240">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.55.<br />
<br />
Oleg Malenko alikuwa ni mwanaume wa Kirusi, alizaliwa na kukulia nchi Urusi miaka mingi iliyopita, alikuwa ni baba wa watoto wawili na mke mmoja, jina lake lilifahamika kwa wengi kutokana na kazi zake za uvuvi kwani aliendesha maisha yake kwa kazi hiyo.<br />
Alikuwa ameifanya kazi hiyo kwa muda wa miaka isiyopungua kumi na tano na bado, pamoja na umri wake mkubwa<span class="text_exposed_show">. aliendelea kuifanya kwani ndiyo kazi pekee iliyoendesha maisha yake na familia yake.<br />
Alfajiri ya siku hiyo kama ilivyokuwa kawaida yake, alitoka nyumbani kwake mapema kuliko kawaida akimuaga mke na watoto wake kwamba alikuwa akielekea kazini kwake jambo ambalo liliishangaza sana familia yake lakini hawakutilia mashaka hali hiyo kwani walimfahamu vyema.<br />
Hakuishi maeneo ya mbali sana kutoka ufukweni ambako ndiko aliegesha mtumbwi wake mdogo, hivyo kwa muda wa dakika kumi tu tayari alishafika eneo la ufukweni, huku akiwa na taa ndogo mkononi mwake aliangaza macho yake huku na kule akijaribu kuangalia kama kulikuwa na mtu mwingine eneo hilo lakini hakuona kitu.<br />
Kwa ujasiri alitembea na kuusogelea mtumbwi wake kwa kutumia taa ndogo aliyokuwa nayo mkononi ambapo aliangaza ndani ya mtumbwi huo kuangalia kama kulikuwa salama. Bila kuchelewa akaiweka taa ndogo aliyokuwa nayo mikononi mwake na kuanza kuusukuma mtumbwi huo kuelekea majini, tayari kwa kuanza kazi.<br />
Alfajiri ya siku hiyo bahari ilionekana kuwa kimya kabisa, hapakuwa na purukushani kama ilivyokuwa kila siku, hivyo kuwa na uhakika kabisa kwamba angevua samaki wengi kwa sababu hakukuwa na watu wengine.<br />
Kwa mwendo wa dakika kumi nzima aliendelea kupiga kasia akisonga mbele zaidi, lengo lake likiwa ni kufika mahali ambako aliamini samaki wengi zaidi walipatikana lakini ghafla mbele yake aliona kitu cha ajabu ambacho hakukitarajia, moyo wake ukamwenda mbio pamoja na kwamba kwa wakati huo nchini Urusi kulikuwa na hali nzuri ya hewa, lakini Oleg alitiririkwa na jasho jingi si kwa sababu ya kazi aliyokuwa ameifanya bali kwa kitu kilichokuwa mbele yake.<br />
“Mungu wangu ni papa!”alijiuliza akinyanyua taa yake ndogo na kumulika eneo hilo.<br />
Akayatoa macho yake yote kuangalia mbele lakini kwa sababu ya mwanga mdogo uliokuwepo hakuweza kuona vyema, woga ukazidi kumwingia na wazo pekee lililomwijia kichwani mwake ni kugeuza mtumbwi wake haraka na kurejea alikotoka, jambo ambalo hakuwa na uhakika nalo kama angefanikiwa.<br />
Akiwa hapo alishuhudia mtumbwi wake ukiyumbishwa huku na kule, tayari alijua alikuwa katika hatari.<br />
“Leo ninakufa, sidhani kama nitasalimika, ” alijisemea Oleg huku machozi yakimbubujika.<br />
<br />
***<br />
Usiku ulionekana kuwa mrefu mno kwa Phillip, mawazo na akili zake zote zikiwa kwenye kazi ambayo Lina alikuwa amemuahidi. Moyoni akamshukuru Mungu kwa mara nyingi kwa kumwona na kumchagua yeye, ni kweli alikuwa katika majonzi mazito lakini alikuwa amepewa njia nyingine tena.<br />
“Jambo moja tu sasa litakalonisumbua ni jinsi gani nitapata tena watoto? Nahitaji watoto ambao watakuwa warithi wa mali zangu hapo baadaye,”aliwaza kichwani mwake akivuta shuka na kujifunika.<br />
Asubuhi ya siku hiyo yeye ndiye alikuwa mtu wa kwanza kuamka kitandani, taratibu bila kumwamsha Lina alitoka ndani ya chumba na kuelekea jikoni ambako aliandaa kila kitu kwa ajili ya kifungua kinywa na kurejea chumbani ambako alifungua kabati akatoa nguo na kunyoosha tayari kwa maandalizi ya kwenda kazini.<br />
“Darling?” (Mpenzi)<br />
“Yes baby.” (Ndiyo mpenzi)<br />
“Amka! Amka ukaoge sasa,” akasema Phillip kwa sauti ya kunong’ona.<br />
“Mh!” Lina aliguna akijinyosha kitandani.<br />
“Muda umefika?”<br />
“Zamani sana mke wangu.”<br />
Taratibu akafunua shuka na kunyosha mkono kuchukua simu yake ambayo haikuwa mbali, akatupa macho yake hapo na kugundua kwamba muda ulikuwa umewadia na alitakiwa kufanya haraka ili wasichelewe.<br />
Taratibu akashusha miguu yake kitandani huku akiwa katika hali ya usingizi, Phillip akamshika mkono na kumuongoza moja kwa moja mpaka bafuni ambako walioga na kutoka.<br />
“Utavaa nini leo?”<br />
“Mimi?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Nguo tayari nimeshanyoosha.”<br />
“Unasema kweli?”<br />
“Hakika, nimeamka kitambo kidogo.”<br />
Lina akasogea na kumbusu Phillip usoni ikiwa ni ishara ya kumshukuru, hakika watu hawa walikuwa katika penzi motomoto, kila mmoja akifanya mambo mazuri kwa mwenzake kadiri alivyoweza.<br />
Kwa pamoja wakavaa na kutoka chumbani kuelekea sebuleni ambako nako mambo yalizidi kumshangaza Lina kwani tayari chai ilishatengwa mezani, kazi yake ilikuwa ni kusogea na kunywa.<br />
“Leo umenifanyia mchezo wa ajabu sana mume wangu.”<br />
“Kwa sababu nakupenda kupita kawaida.”<br />
“Najua, nami pia ninakupenda sana Phillip.”<br />
Kwa pamoja wakasogea mezani na kuketi hapo, wakanywa chai na walipomaliza Lina akachukua ufunguo wa gari lake aina ya Land Cruiser na kumkabidhi Phillip.<br />
“Wewe leo ndiye dereva.”<br />
“Mh! Una uhakika?”<br />
“Kabisa gari hilo ni lako sasa.”<br />
“Na wewe je?”<br />
“Nitapata lingine muda si mrefu.”<br />
“Ahsante kwa kunipenda mke wangu.”<br />
“Usijali.”<br />
Huku mkono wa Phillip ukiwa kiunoni mwa Lina, taratibu wakitembea kuelekea eneo gari lilipoegeshwa, Phillip akabonyeza kitufe fulani kwenye ufunguo na milango ikafunguka kisha kushika mlango mmoja wa mbele akaufungua na taratibu akamkaribisha Lina ambaye aliingia na kuketi huku akitabasamu.<br />
Phillip naye akaelekea upande wa pili kwa dereva na kuingia ndani yake, akawasha gari kisha kutoka nje ya lango huku akipunga mkono kwa mlinzi ambaye naye aliachia tabasamu.<br />
<br />
***<br />
Baada ya kutangaziwa hali ya machafuko nchini Urusi uamuzi pekee uliofikiwa na uongozi wa shule ni kufunga shule kwa muda, mkutano ukaitishiwa na wanafunzi kupewa taarifa kwamba uongozi wa shule ulikuwa umeamua kusitisha masomo kwa muda kutokana na hali ilivyokuwa na kuwataka wanafunzi warejee majumbani mwao mpaka hali itakapotulia.<br />
Uamuzi huo pekee uliwafanya Mariya na Merina kutoa machozi, hawakuwa na uhakika kama wangeweza kufika nyumbani kwao salama bila matatizo yoyote, isitoshe walizoea kuletwa shuleni na kufuatwa na sasa walikuwa wakirejea nyumbani wenyewe bila dereva.<br />
“Mariya!” Merina aliita.<br />
“Bee!”<br />
“Twende huku.”<br />
“Mimi sitaki nitakaa hapahapa kungojea gari la nyumbani.”<br />
“Haliji sasa hivi na hali inazidi kuwa mbaya twende!”alisema Merina akimvuta Mariya ambaye muda wote alikuwa akilia.<br />
Kwa pamoja huku kukiwa na purukushani nyingi, wakafanikiwa kutoka nje ya lango la shule wakiwa hawaelewi ni wapi waelekee.<br />
“Merina! Mariya!” wakasikia majina yao yakitajwa.<br />
Wakatupa macho yao kugeuka ili waangalie ni wapi sauti hiyo ilitoka na alikuwa ni nani aliyewatamka kwa majina.<br />
“Mh! Unamjua?” Merina aliuliza.<br />
“Hapana!”<br />
“Lakini anatufahamu mbona ametuita kwa majina?”<br />
“Hebu twende tukamsikilize pengine ametumwa na baba aje kutuchukua!”<br />
“Mimi naogopa!” Mariya alijibu huku akisita.<br />
Mbele yao alionekana mwanaume mrefu, mwili wake ulikuwa umejazia, na kwa kumwangalia harakaharaka alionekana kuwa ni mtu wa mazoezi. Kichwani alivaa kofia kubwa, machoni alikuwa na miwani ya rangi nyeusi. Huku wakitetemeka kwa hofu, wakasogea karibu kabisa na mwanaume huyo.<br />
“Mariya! Merina!” akaita tena.<br />
“Bee!” wakaitika huku wakitetemeka kwa hofu.<br />
“Safi dili limekamilika,”alijibu mwanaume huyo na kwa haraka akawakamata kwa nguvu na kuanza kuwavuta kuelekea sehemu ambayo hawakuifahamu.<br />
Je, nini kitaendelea? Watoto hawa wamepelekwa wapi? Je, watapatikana au ndiyo mwisho wao? Ni nani huyu aliyewachukua?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500066906a48018538">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.56.<br />
<br />
Wakionekana wenye furaha mara kadhaa wakipigana mabusu bila kujali kwamba walikuwa barabarani, Phillip aliendesha gari na hatimaye kwa muda wa nusu saa wakafika ofisini.<br />
Ni Phillip aliyekuwa wa kwanza kushuka garini na kuzunguka tena upande wa Lina kisha kufungua mlango na kumshika mkono akimkaribisha.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Ahsante”<br />
“Mwaaa!”Phillip aliachia busu.<br />
Kitendo hicho kilishuhudiwa na watu wengi waliokuwa wamefika ofisini muda huo. Hakika mapenzi yao yalipendeza.<br />
“Si Lina yule?”<br />
“Ndiye.”<br />
<br />
“Na yule?”<br />
“Mume wake.”<br />
“Mh! Makubwa haya.”<br />
“Kwa nini?”<br />
“Si umeona mwenyewe,” yalikuwa ni maongezi ya wasichana wawili waliofanya kazi ofisi moja na Lina.<br />
Kwa pamoja wakatembea njiani wakipishana na watu kadhaa na kuwasalimia na Lina alifanya utambulisho kidogo na kuendelea mbele.<br />
<br />
“Ngo!Ngo!Ngo!” Sauti ya mlango ukigongwa ilisikika.<br />
“Ndiyo.” Sauti kutoka ndani ikajibu.<br />
Taratibu Lina akashika kitasa na kusukuma mlango kuingia ndani. Macho yake yakagongana moja kwa moja na bosi wake aliyekuwa ameketi nyuma ya meza kubwa ofisini kwake asubuhi hiyo.<br />
“Karibu sana Lina.”<br />
<br />
“Ahsante,” alijibu Lina na alipofungua mlango vizuri alionekana kuongozana na mtu mwingine.<br />
“Karibuni sana,” aliongea bosi huyo akijiweka vyema kitini huku macho yake yakimwangalia Phillip.<br />
***<br />
“Watoto hawa watanipa kile ninachokitafuta,” aliwaza mwanaume huyo akizidi kuwavuta watoto Mariya na Merina kuelekea sehemu ambayo hawakuifahamu.<br />
<br />
Badru Divostroc alikuwa ni mwanaume katili aliyeogopwa na watu wengi nchini Urusi kwa vitendo vyake vya kimafia, kutokana na ukatili wake huo watu wengi nchini humo wakambandika jina la Kuntakinte.<br />
Kwake yeye kupata alichokihitaji halikuwa tatizo, hakuogopa kumwaga damu za watu ili mradi tu atimize alichokikusudia.<br />
<br />
Kwa muda mrefu alifuatilia kwa ukaribu habari za tajiri Fedorov alitaka kumfahamu lakini hakupata mwanya huo, hivyo taarifa za Mariya na Merina ambao walikuwa ni watoto wa Victor Fedorov kuingia nchini Urusi kulimpa furaha ya ajabu.<br />
Baada ya kufuatilia kwa kina na kugundua kwamba Victor Fedorov aliwapenda watoto wake kuliko kitu kingine, aliamua kuwafuatilia kwa ukaribu akichunguza shule waliyosoma na ni gari lililowapeleka na kuwafuata kuwarudisha nyumbani.<br />
Kwa muda wa mwezi mzima alifanya kazi hiyo hatimaye akafanikiwa kugundua njia zote na namna watoto hao walivyopelekwa shuleni na kufuatwa wakionekana kuwa katika ulinzi madhubuti.<br />
<br />
Ni machafuko yaliyokuwa yakitokea nchini Urusi kwa wakati huo kwake yeye aliona ni kama bahati kwani nia yake ya kufanya utekaji nyara wa watoto wa tajiri kama Victor Fedorov kungempa alichokikusudia. <br />
“Leo nitajaribu kufanya utekaji nitatumia akili zangu zote kuwapata watoto wa Fedorov halafu…,”aliwaza huku akinyanyuka kitandani.<br />
<br />
Akiwa chumbani kwake akaisogelea televisheni yake na kuiwasha macho yake yakakutana moja kwa moja na habari za maandamano makubwa ya wananchi nchini Urusi waliokuwa wakipinga matokeo ya jeshi la polisi baada ya kusitisha msako wa kumsaka Ditrov, wananchi walikuwa wakiandamana mitaani wengi wakishinikiza msako uendelee.<br />
“Hureee! Hureee utajiri huo mikononi mwangu,”alipiga kelele akirukaruka chumbani mwake.<br />
<br />
Taarifa hiyo iliamsha vyema hisia zake, kwani kwa muda mrefu alikuwa amefanya kila alichoweza kupata utajiri aliokuwa nao Victor Fedorov lakini hakufanikiwa, sasa ulikuwa umekaribia kuingia mikononi mwake.<br />
Haraka bila kuchelewa akavuta suruali yake aina ya jeans, fulana pamoja na koti kubwa akavaa, akageuka tena upande mwingine akavuta soksi za mikononi na kuzivaa kisha kofia kubwa pamoja na miwani ya rangi nyeusi akakisogelea kioo kilichokuwa chumbani kwake na kujiangalia na kutikisa kichwa kwa jinsi alivyobadilika.<br />
<br />
Taratibu akanyanyua gorodo na kuchukua bastola yake ndogo na kuipachika kiunoni.<br />
“Hakuna mtu atakayeweza kunitambua kwamba mimi ndiye Badru…,’aliongea akifungua mlango ili atoke nje.<br />
Akitembea kwa kujiamini moja kwa moja akaliendea gari lake aina ya Noah akaingia na kuliwasha, mawazo yake yote yakiwa juu ya watoto wa Victor Fedorov, aliamini kama angefanikiwa kuwapata watoto hao na kuwateka hakika angepata malipo makubwa kutoka kwa tajiri huyo.<br />
<br />
Kwa mwendo wa dakika kumi nzima aliendesha gari hatimaye akafanikiwa kufika shule waliyosoma watoto hao. Akaliegesha gari lake mbali kidogo na shule kisha kushuka na kutembea njiani akipishana na watu wengi wakikimbia huku na kule.<br />
<br />
“Wale pale,”aliongea akisogea karibu kisha kuanza kuwaita kwa majina.<br />
“Wewe ni nani?”<br />
<br />
“Hakuna haja ya kunifahamu, twendeni huku.” Sauti ya mwanaume huyo ikajibu akiwavuta watoto hao.<br />
“Mariya” Merina aliita huku akilia.<br />
“Bee.”<br />
“Huyu ni nani na tunakwenda wapi?” Merina aliuliza swali jingine tayari wote wawili walikuwa wakilia huku wakijaribu kujitoa mikononi mwa mwanaume huyo.<br />
<br />
Kwa nguvu zake zote aliwavuta watoto hao mpaka wakalifikia gari ambalo lilikuwa limeegeshwa nje kidogo ya eneo la shule akafungua mlango na kuwatupia ndani yake, akaangaza macho huku na kule kuangalia kama kulikuwa na mtu yeyote karibu eneo hilo, wengi walionekana wakikimbia kunusuru maisha yao.<br />
<br />
“Ninachohitaji hivi sasa ni fedha, Victor Fedorov ni lazima atoe fedha kuwaokoa watoto wake vinginevyo nitawaua,” Badru aliwaza kisha aliwasha gari na kuliondoa kwa kasi.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012450005e707049522974">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.57.<br />
<br />
Mshtuko aliokuwa ameupata hakika ulikuwa hauelezeki, kupotea kwa watoto wake wawili? Lilikuwa ni swali ambalo halikuwa na jibu kichwani mwake, kwa dakika tano nzima aliendelea kubaki chini akiwa haelewi ni kitu gani angefanya ili kuwapata watoto wake Mariya na Merina.<br />
<br />
Machozi yakamtiririka, alipojaribu tena kupaza sauti yake akiwaita kwa majina bado hakusikia<span class="text_exposed_show"> sauti yoyote zaidi ya mwangwi uliopenya moja kwa moja masikioni mwake. Victor Fedorov akajiona ni mwanaume mwenye mkosi maishani mwake.<br />
<br />
Akiwa haelewi ni kitu gani afanye, alijikongoja na kunyanyuka chini bado akiendelea kuangaza macho yake huku na kule pengine kuona kama walikuwa wamejificha mahali na baada ya kumwona wangejitokeza awachukue na kwenda nao nyumbani. Haikuwa kama alivyowaza, bado Merina na Mariya hawakuonekana sehemu yoyote ile ndani ya shule. Jasho jingi likimtiririka, alijikongoja na kulifikia gari lake akafungua mlango na kuingia ndani kisha akaliwasha na kutoka eneo hilo la shule.<br />
<br />
“Watakuwa wapi hawa? Nini kimewapata watoto wangu,” alijiuliza maswali mfululizo bila kupata majibu.<br />
Nje ya lango la shule bado vurugu iliendelea kuongezeka, watu wengi wakionekana kukimbia huku na kule kuokoa maisha yao, akakodoa macho yake yote kuangaza kila upande akiwatafuta watoto wake lakini bado hakuwaona, lakini akiwa hapo akajipa moyo na kuamini kwamba huenda walimu waliamua kuwarudisha nyumbani kwa sababu ya machafuko yaliyokuwa yametokea siku hiyo.<br />
<br />
“Nakwenda nyumbani watakuwa huko nina uhakika,” aliwaza akikanyaga mafuta kusonga mbele.<br />
Victor Fedorov aliishi nje kidogo ya jiji, hivyo ilimchukua muda wa dakika arobaini kufika kwenye makazi yake, kichwani mwake akiwa na mawazo mengi juu ya usalama wa watoto wake ambao mpaka wakati huo hakufahamu kabisa ni wapi walipokuwa na kama walikuwa hai au wamekufa.<br />
<br />
“Piii!Piiii!” ilikuwa ni honi nje ya lango la kuingilia nyumbani kwake.<br />
Mara moja bila kuchelewa mlinzi alilifungua lango, akaingia ndani ya ngome ambapo aliliegesha gari lake kisha akashuka haraka.<br />
<br />
Akazungusha macho yake huku na kule ndani ya ngome yake lakini hakuona kitu, hata alipojaribu kuangalia gari ambalo mara kadhaa liliwapeleka shule watoto wake na kuwafuata, nalo pia halikuonekana sehemu yake.<br />
“Watoto wamerudi?” aliuliza kwa sauti ya ukali.<br />
“Hapana bosi.”<br />
<br />
“Unasema kweli?”<br />
“Nina hakika.”<br />
“Zhukov naye yuko wapi?”<br />
“Sijamwona.”<br />
<br />
“Mungu wangu watoto wangu!” alisema Victor Fedorov akichomoa simu yake ya mkononi mfukoni, akaonekana akibonyeza namba kadhaa kisha kuiweka sikioni na kusikiliza. Akiwa hapo mlinzi akamshuhudia bosi wake akitoka mbio kuelekea ndani bila kusema chochote, alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa kabisa.<br />
<br />
Aliingia ndani na dakika mbili baadaye alitoka nje mkononi akiwa na bastola, na bila kusema chochote akaamuru lango kuu lifunguliwe, akaingia ndani ya gari kisha kuliwasha na kutoka mbio kama vile alikuwa katika mashindano.<br />
“Nitaua! Nasema nitaua sina mchezo mbele ya watoto wangu,” alisema peke yake ndani ya gari.<br />
<br />
Huku akiwa katika mwendo wa kasi, Victor Fedorov aliendelea kuangaza macho yake huku na kule pembezoni mwa barabara lakini bado hakuwaona watoto wake. Alikuwa ameamua kuingia mwenyewe barabarani akiwasaka kwa udi na uvumba watoto wake Mariya na Merina ambao mpaka wakati huo hakujua walikuwa wapi na kitu gani kilikuwa kimewapata. Kwa saa saba mfululizo aliendelea kuwasaka huku akijaribu kuwasiliana na watu mbalimbali kwa msaada, lakini bado hawakupatikana sehemu yoyote.<br />
<br />
Hatimaye akaamua kuingia katika hospitali moja baada ya nyingine akiuliza kama kulikuwa na majeruhi yeyote au watu waliofariki, lakini bado jibu liliendelea kubaki palepale; hakukuwa na kitu cha aina hiyo.<br />
<br />
“Fyuuu!”akashusha pumzi kwa nguvu. Victor Fedorov hakuwa tayari kuwapoteza watoto wake alikuwa tayari kutumia kila kitu alichokuwa nacho lakini si kuwakosa maishani mwake, hakika aliwapenda kupita kawaida katika maisha yake yote yaliyobaki duniani, aliamini hakuwa na ndugu mwingine zaidi ya watoto hao.<br />
<br />
Siku hiyo ikapita kukiwa hakuna dalili zozote za kuwapata watoto wake na hata alipojaribu kurejea nyumbani na kuangalia bado walikuwa hawajaonekana, akiwa hapo akamkumbuka Ditrov na kuamini kwamba pengine asingemuua angekuwa msaada mkubwa katika kupatikana kwa watoto wake.<br />
<br />
“Ditrov angekua hai hakika ninaamini watoto wangu wangepatikana,” aliwaza akijifuta machozi.<br />
Kwa siku tatu mfululizo bado watoto waliendelea kusakwa huku na kule nchini Urusi pamoja na machafuko yaliyokuwepo, nchi hiyo ilibinuliwa nje ndani, msaada mkubwa ukifanywa na polisi lakini bado hawakupatikana.<br />
<br />
Hatimaye siku ya nne asubuhi Victor Fedorov akiwa ameshakata tamaa juu ya kuwapata watoto wake, wazo likamjia kichwani mwake kwamba ajaribu kutangaza katika vyombo vya habari juu ya kupotea kwa watoto.<br />
<br />
Huku akiwa mwenye mawazo mengi akakubaliana na wazo hilo.<br />
“Nitakwenda kwenye televisheni ya taifa na kutangaza pengine kuna mtu amewaona sehemu fulani,” aliwaza akilini mwake.<br />
<br />
Ndani ya nyumba yake hakukulika wala kukakalika, mawazo na akili yote ilielekea kwa watoto wake. Hivyo asubuhi hiyo alitoka nyumbani kwake na jambo moja tu; tangazo.<br />
<br />
Akaingia ndani ya gari lake na kuliwasha bila kusema chochote akamwonyesha mlinzi ishara na lango likafunguliwa, taratibu akaanza kutoka nje, lakini kabla hajafika mbali mbele yake aliona kitu ambacho hakikuwa cha kawaida.<br />
<br />
“Mh ni kitu gani kile?” alijiuliza akizima gari lake na kushuka kukielekea kitu hicho moyoni mwake akiwa na wasiwasi mwingi.<br />
<br />
Je, ni kitu gani hicho? Nini hatima ya Mariya na Merina? Watakufa au wataokolewa?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245000786c5842692572"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500057186f31921329">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.58.<br />
<br />
JASHO jingi lilikuwa kitiririka mwilini mwake, akatembea taratibu kukielekea kitu kilichokuwa mbele yake hatua chache tu tayari akawa amekifikia, alipotupa macho yake vyema kuangalia aligundua ilikuwa ni bahasha kubwa nyeupe na juu yake iliandikwa kwa maandishi ya rangi nyekundu akasimama kwa muda akijaribu kusoma ni kitu gani kiliandikwa juu yake.<br />
<br />
“Victor Fed<span class="text_exposed_show">orov!” Moyo wake ukazidi kumwenda mbio, kitendo cha kukuta bahasha hiyo nje ya lango lake hakikuwa cha kawaida tena na jina lake kwa maandishi ya rangi nyekundu? Likawa ni swali jingine kichwani mwake akazidi kuchanganyikiwa.<br />
<br />
Bila kupoteza wakati akiwa haelewi ni kitu gani kingetokea akapiga moyo konde na kuinama kuikota bahasha hiyo na kwa ujasiri wa hali ya juu haraka akaifungua ndani na kutoa kipande kidogo cha karatasi nacho pia kiliandikwa kwa rangi nyekundu.<br />
“Anayeua kwa upanga naye hufa kwa upanga” Kilisomeka kipande hicho cha karatasi.<br />
<br />
Victor Fedorov akiwa haamini maneno aliyokutana nayo ndani ya karatasi hiyo akapikicha macho yake tena na kurudia bado yaliendelea kusomeka hivyo hivyo kama mwanzo.<br />
“Mungu wangu!” Akasema kimoyomoyo akiketi chini na kuendelea kusoma zaidi.<br />
<br />
“Ninachohitaji kwako ni fedha, ili uweze kuwapata watoto wako Merina na Mariya kama unawahitaji wakiwa hai. Ninatoa muda wa saa ishirini na nne tu kuanzia sasa vinginevyo watakuwa marehemu, nakuhakikishia watakufa kifo kibaya kwa kuwakata kiungo kimoja baada ya kingine hadi umauti uwafike.<br />
Kumbuka kama unawapenda watoto wako ni vyema ukafanya kila unachoweza ili uweze kuwapata na usijaribu kutumia jeshi la polisi kwa usalama zaidi.<br />
<br />
Mara tu utakapokuwa tayari nitapenda unitaarifu kwa namba hizo hapo chini ili tukubaliane, sawa?<br />
Tahadhari mimi ni mtu hatari sana, ukigeuka nyuma utaniona , kushoto, kulia na mbele pia nipo hivyo kabla hujafanya maamuzi yoyote tumia busara zako zote vinginevyo utajuta…<br />
Kwa heri.” Ilisema sehemu ya barua hiyo.<br />
<br />
“Ni Ditrov.”Alinong’ona.<br />
Victor Fedorov akahisi vitu kama maji maji vikitiririka ndani ya suruali yake, hakika hakuamini alichokisoma kichwani mwake taswira ya Ditrov ikamjia akahisi pengine mtu huyo hakufa kama alivyofahamu.<br />
“Noooo!” Akapaza sauti.<br />
<br />
Akatupa macho yake pande zote nne bila kuona kitu akayerejesha tena kwenye saa yake ya mkononi akasoma akagundua amebakiza saa kumi na tisa tu muda aliokuwa amepewa na mtu aliyedai kuwa na watoto wake uwadie vinginevyo wangekufa.<br />
“Mariya! Merina!” Akaita akikimbia kuelekea ndani ya nyumba yake, bila kukumbuka gari alilokuwa ameliegesha pembeni kidogo.<br />
<br />
Moja kwa moja akagonga lango na mlinzi kulifungua bila kusema chochote akazama ndani akikimbia huku akilia.<br />
“Kuna nini tena?” Mlinzi aliuliza lakini hakujibiwa kitu chochote.<br />
Tayari Victor Fedorov alishazama ndani, kitu cha kwanza bila kupoteza wakati akaisogelea simu akainyanyua ili apige namba aliyokuwa ameisoma kwenye kipande cha barua kilichokuwa mkononi mwake.<br />
<br />
Huku machozi yakimbubujika akakikunjua kipande hicho na kuanza kuzisoma namba na kubonyeza moja baada ya nyingine kisha kuweka mkono wa simu sikioni akisikiliza upande wa pili.<br />
<br />
Takribani dakika tatu nzima simu hiyo iliita bila kupokelewa akili yake ikazidi kuvurugika akiwa haelewi ni kitu gani angefanya upande mmoja wa akili yake ukimwambia atoe taarifa hiyo kwa Jeshi la Polisi na mwingine ukimwambia kufanya hivyo ni kuwapoteza watoto wake wapendwa Mariya na Merina kwani alishapewa onyo juu ya jambo hilo.<br />
<br />
“Hapana ngoja niwe mvumilivu nitawapata tu, isije kuwa ni Ditrov hana huruma mtu huyu anachokisema kinakuwa kweli, atawaua watoto wangu!” Alijiuliza maswali mengi mfululizo bila kupata majibu.<br />
Dakika tano nzima baadaye alikuwa tena katika simu akibonyeza namba zile zile na kusikiliza ghafla akasikia sauti nzito upande wa pili ikapokea.<br />
<br />
“Ah!Ah!” Kigugumizi kikamshika pamoja na ukatili wake wote Victor Fedorov hapo alikuwa hana ujanja tena, alikuwa tayari kupoteza kila kitu alichokuwa nacho lakini si watoto wake, aliwapenda kupita maelezo.<br />
<br />
<span> “Niko tayari...sawa…ndiyo…hapana</span><wbr></wbr><span class="word_break"></span>…usiwaue…nitakupa hata kama ni utajiri wangu wote….Mungu wangu…niambie unapatikana wapi…nimekuelewa sitafanya hivyo… niambie unataka kiasi gani?” Yalikuwa ni maongezi katika simu na mtu mwingine upande wa pili ambaye hakuonekana na baada ya maongezi hayo simu ikakatwa.<br />
<br />
Akiwa amepigwa na butwaa, taswira za watoto wake Mariya na Merina zikamjia, masikioni mwake akasikia sauti zao wakimwita na kumwomba asiwaache wafe, Victor Fedorov akalia kama mtoto mdogo.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500050ce2a27432960">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.59.<br />
<br />
SURA yake ilikuwa imebadilika kabisa, macho yakabadilika na kuwa ya rangi nyekundu, mwili wake ukaanza kutetemeka kama mtu aliyekuwa na homa kali, Victor Fedorov akauona utajiri wote aliokuwa nao haukuwa na maana kwake kama tu angewakosa watoto wake ambao kwa hakika alikuwa ametumia kiasi kikubwa cha fedha ili kuwapata na sasa walikuwa katika hatari nyingine ya<span class="text_exposed_show"> kifo kama tu asingetimiza jambo alilotakiwa kulifanya ndani ya saa chache alizopewa.<br />
<br />
Kwa muda wa dakika tano aliendelea kutafakari na hakuelewa ni kwa nini mtekaji huyo alifanya tendo hilo, akavuta kumbukumbu zake nyuma akijaribu kufikiria watu wote aliowahi kuwakosea na kuwadhulumu lakini hakuna alichokumbuka.<br />
Mara kadhaa taswira ya Ditrov ilimjia lakini akatupilia mbali mawazo juu ya mtu huyo na kuamini kwamba tayari alishakufa.<br />
<br />
“Nilimuua ili kuficha siri sikuwa na tatizo jingine kabla!” alisema akitembea kukielekea kiti kilichokuwa mbele yake. Huku jasho jingi likimtiririka, akakisogelea kiti na kuketi, moyoni mwake akiwa na hofu juu ya watoto wake.<br />
<br />
“Nitatoa kiasi chochote cha fedha atakachohitaji mtu huyo ili mradi tu niwapate watoto wangu!” aliwaza akijifuta machozi.<br />
Alipotupa macho yake kwenye saa yake ya mkononi hofu ikazidi kumwingia, mbele yake kulikuwa na saa kumi tu zilizobaki katika saa ishirini na nne alizopewa na muuaji.<br />
<br />
Haraka akanyanyuka kitini na kusogelea tena simu akapiga namba zilezile alizobonyeza mwanzo kisha kuiweka simu sikioni, alikuwa hapo kuzungumza na mtu huyo ataje kiasi hicho cha fedha na sehemu ambapo angezikuta na yeye kupata watoto wake wakiwa salama.<br />
***<br />
Ilikuwa ni familia yenye furaha kupita kawaida, kila mtu aliyewaona aliona wivu, hakika walivutia, walikuwa na kila sababu ya kuitwa mke na mume. Lakini pamoja na mambo yote hayo kutawala maishani mwao, jambo moja tu lilikuwa likiwasumbua ni wapi wangepata mtoto.<br />
<br />
Kwa mwanamke halikuwa tatizo sana, kazi kubwa ilikuwa kwa mwanaume ambaye alitumia muda mwingi kufikiria namna gani angeitwa baba kama ilivyowahi kutokea miaka mingi kabla.<br />
“Darling” (mpenzi), Phillip aliita siku moja asubuhi.<br />
“Yes baby!” (Ndiyo mpenzi)<br />
<br />
“Ni miaka minne sasa tupo kwenye ndoa lakini mimi sina uwezo wa kuzaa nataka tuliongelee jambo hili ili tufikie muafaka juu ya nini cha kufanya, napenda niitwe baba hata kama mtoto huyo atakuwa si wa kwangu,” alisema Phillip.<br />
“Unamaanisha nini Phillip?”<br />
“Sina nia mbaya, ila nataka nikupe nafasi ya wewe kuzaa kwa sababu huna tatizo lolote.”<br />
“Mh!” Lina akaguna.<br />
<br />
“Ni ukweli mke wangu nakupenda sana lakini nitakupenda zaidi utakapofanikiwa kuniletea mtoto.”<br />
“Phillip mbona sikuelewi, mtoto atoke wapi? Ni kweli mimi sina tatizo lakini nitampata wapi mtoto ili hali wewe ndiye mume wangu na tayari una tatizo?”<br />
<br />
“Tafuta mwanaume yeyote ambaye atakuwa tayari kuzaa na wewe Lina halafu mimi nitalea mtoto huyo!” alisema Phillip akilengwalengwa na machozi.<br />
Ilikuwa ni kauli ngumu sana kuitamka mdomoni hasa kwa mwanaume aliyempenda mke wake kupita maelezo, lakini haikukwepeka kwa sababu walihitaji mtoto ndani ya nyumba ambaye angekuwa mrithi wa mali zote walizokuwa nazo.<br />
<br />
Lina akamwangalia Phillip kwa muda, hakuwa tayari kuamini kauli aliyoisikia mdomoni mwa Phillip, kwani katika muda wote walioishi pamoja ndani ya nyumba Phillip alionyesha kumpenda na mara kadhaa akimwomba kuwa mwaminifu katika mapenzi yao.<br />
“Phillip!” Lina aliita.<br />
<br />
“Yes honey” (ndiyo mpenzi) aliitikia Phillip huku macho yake yakimwangalia Lina kwa huruma.<br />
“Unamaanisha unachosema?”<br />
“Hakika, wala sina utani juu ya hilo.”<br />
<br />
“Ni kwa nini umefikia hapo, hivi kweli unanipenda?”<br />
“Nakupenda kupita maelezo wewe mwenyewe unafahamu.”<br />
“Sasa?”<br />
“Nataka kuitwa baba.”<br />
<br />
“Phillip hutaumia kugundua kwamba mkeo unayempenda kwa dhati amekutana na mwanaume mwingine kisha kupata ujauzito?”<br />
“Nimekaa na kufikiria kwa muda mrefu si kwamba sitaumia, ninachohitaji ni wewe kufanya kila unachoweza upate ujauzito halafu mimi nitautunza mpaka utakapojifungua mke wangu.”<br />
“Phillip kumbe hunipendi,” alisema Lina akibubujikwa na machozi.<br />
<br />
Phillip akanyanyuka kitini na kusogea karibu kabisa na kiti alichoketi Lina kisha kumkumbatia wote kwa pamoja wakaanza kulia.<br />
“Uamuzi wangu si mbaya, ninachohitaji wewe uwe na furaha mke wangu matatizo yangu mimi yasikufanye ukakosa kuitwa mama maishani mwako,” aliongea huku akimpigapiga Lina mgongoni.<br />
<br />
“Phillip hivi utajisikiaje kuona mimi ni mjamzito halafu si wa kwako?”<br />
“Kwa sababu nimetoa idhini mimi mwenyewe sitaumia, ninachotaka ni wewe uitwe mama na mimi baba basi.”<br />
“Ni ngumu Phillip, mimi siwezi kulisaliti penzi letu acha tubaki hivihivi bila mtoto naamini Mungu alikuwa na makusudi juu ya hilo.”<br />
<br />
“Unasema?” aliuliza Phillip akinyanyuka kitini, alikuwa hatanii bali alimaanisha alichokuwa akikisema. Haja ya moyo wake ilikuwa ni kuitwa baba bila kujali ni wapi mtoto huyo angepatikana.<br />
“Phillip.” Lina akaita huku akijaribu kumfuata.<br />
“Lina nataka mtoto!”<br />
<br />
“Phillip haiwezekani mimi siko tayari kusaliti penzi letu.”<br />
“Unanipenda?” Phillip aliuliza kwa kujiamini.<br />
“Nakupenda sana mume wangu.”<br />
“Basi nataka mtoto!” aliongea Phillip huku akitembea kuondoka eneo hilo.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500087cc5039373479"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124500048c23796527567">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.60<br />
<br />
“Mungu wangu! Ni papa?”alijiuliza huku akinyanyua taa yake ndogo na kumulika eneo hilo huku akitetemeka kwa hofu.<br />
Akayatoa macho yake yote kuangalia mbele lakini kwa sababu ya mwanga mdogo uliokuwepo hakuweza kuona vyema. Woga ukazidi kumwingia na wazo pekee lililomjia kichwani kwa wakati ule lilikuwa ni kugeuza mtumbwi wake haraka na kurejea alikotoka, jambo amb<span class="text_exposed_show">alo hakuwa na uhakika nalo kama lingesaidia kuokoa maisha yake.<br />
<br />
Akiwa hapo alishuhudia mtumbwi wake ukiyumbishwa huku na kule, akajua tayari amejiingiza kwenye hatari.<br />
“Leo ninakufa huku nikijiona,” alisema Oleg Malenko huku machozi yakimbubujika kwa wingi mashavuni. Hofu kuu ilikuwa imemkumba na hakuna alichokuwa anakisubiri zaidi ya kifo, tena cha kuliwa na papa.<br />
<br />
Aliifanya kazi ya uvuvi kwa kipindi kirefu lakini hata siku moja hakuwahi kukutana na dhahama kama ile. Zaidi alifanya kusimuliwa na wavuvi wenzake kwamba watu wengi hufa baharini, hasa wavuvi baada ya mitubwi yao kuvamiwa na kupinduliwa na samaki wakubwa.<br />
<br />
Kwa Oleg Malenko siku hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kushuhudia tukio hilo, akaamini kabisa kwamba kifo kilikuwa kimemkaribia. Taswira za mke na watoto wake zikawa zinapita kwa kasi kichwani mwake kama filamu ya kusisimua, machozi ya uchungu yakawa yanamtoka.<br />
<br />
Akiwa katika mawazo hayo, haraka alipata wazo la kupiga kasia kwa nguvu na kugeuza mtubwi wake kwa kasi kurejea upande aliokuwa mara ya kwanza lakini tayari alishachelewa, akahisi mtumbwi ukivutwa kurudi nyuma kwa kasi ya ajabu.<br />
“Nakufaa! Nakufaa!” alisema kwa lugha ya Kirusi akiomba msaada.<br />
<br />
***<br />
Muda mfupi baada ya kuzamishwa baharini akiwa amefungwa jiwe kubwa mwilini mwake ili asipate nafasi ya kujiokoa kwa lengo la kupoteza ushahidi, Ditrov alirejewa na fahamu baada ya kupigwa na baridi kali. Alijaribu kufurukuta kwa kupiga mbizi ili kujiokoa lakini hakufanikiwa.<br />
<br />
Alipotumia nguvu za ziada alizokuwa nazo mwilini mwake, bado aliendelea kutapatapa na sasa akawa anavutwa kuelekea chini ya bahari na lile jiwe kubwa alilokuwa amefunganishwa mwilini. Akiwa katikati ya hali ya kupoteza fahamu na uzima, alikumbuka picha ya tukio zima lililotokea ofisini kwa bosi wake, Victor Fedorov hadi wakati ule. Alikumbuka jinsi alivyofyatuliwa risasi bila huruma ambazo zilipenya kwenye mwili wake na kumsababishia maumivu makali.<br />
<br />
Akiwa katika hali hiyo kwa takribani dakika kumi nzima, aliendelea kujivuta huku na kule ndani ya maji ili kujiokoa lakini zoezi hilo lilionekana kuwa gumu kwake. Akawa anazidi kuzama! Ditrov alizidiwa nguvu na maji, akaanza kukata tamaa lakini upande mwingine wa akili yake alikuwa na matumaini makubwa ya kusalimika na kifo.<br />
“Ma…ji!” alitamka kwa tabu akiwa bado anatapatapa, moyoni akasikia sauti ikimwambia kuwa hapaswi kukata tama kwani kufanya hivyo kungemaanisha kifo chake.<br />
<br />
“Sitaki ku…fa!” akatamka tena kwa tabu.<br />
Hali yake ilizidi kuwa mbaya, uwezekano wa kutoka baharini akiwa salama ukazidi kupungua kutokana na maumivu aliyokuwa anayahisi baada ya risasi kuupenya mwili wake na kusababisha atokwe na damu nyingi. Pamoja na kuwa jabali, Ditrov hakuwa na uhakika kama angesalimika lakini bado hakukata tamaa.<br />
<br />
Ghafla akiwa katika hali ya kukata tama, alikumbuka kitu. Wakati anaingia ofisini kwa Victor Fedorov, ndani ya mfuko mmoja katika suruali yake alikuwa na kisu kidogo cha kukunja, akaamini huenda kingemsaidia kuokoa uhai wake.<br />
Kwa nguvu zake zote alijitahidi kuingiza mkono mfukoni lakini hakufanikiwa, akajaribu tena upande mwingine wa suruali yake na kukumbana na maumivu makali.<br />
<br />
Licha ya maumivu hayo alijaribu tena kuusogeza mkono wake zaidi mpaka akaufikia mfuko wa suruali, kwa taabu kubwa akafanikiwa kugusa kitu kigumu na kuamini kwamba kilikuwa chenyewe.<br />
Akiwa katika hali ya kutapatapa akafanikiwa kuupenyeza mkono mfukoni na kuchomoa kisu, kwa taabu kubwa akakishika vyema na kujaribu kuikata kamba ili ajinusuru na umauti uliokuwa ukiinyemelea roho yake.<br />
<br />
Hakuwa tayari kukutana na kifo. Ni kweli alifahamu wazi kwamba kila binadamu angeonja mauti lakini hakuwa tayari kufa kikatili kiasi hicho.<br />
“Nitajaribu mpaka mwisho, ikishindikana basi,”aliwaza akilini mwake.<br />
Kwa nguvu kidogo alizokuwa nazo alikishika vyema kisu kidogo alichokuwa nacho mkononi, licha ya maumivu makali aliyokuwa nayo upande wake wa kulia, aliikamata vyema kamba aliyokuwa amefungwa shingoni na kuanza kuikata.<br />
<br />
“Krii!Krii!Krii!” aliendelea kusugua kisu katika kamba ili ikatike na kumwacha huru. Kwa takribani dakika tano nzima aliendelea kung’ang’ana na kisu lakini zoezi hilo lilionekana kumshinda. Akaanza kuhisi fahamu zikipotea na nguvu kidogo alizobakiwa nazo zikamwishia. Licha ya hayo yote, bado hakuchoka, alitaka kuendelea kujaribu.<br />
<br />
***<br />
“Ngrii!Ngrii!Ngri” Ulikuwa ni mlio wa simu ndani ya nyumba ya Victor Fedorov. Aliinuka taratibu huku akitetemeka na kuisogelea simu hiyo ili aipokee akiwa haelewi ni nani alikuwa akipiga.<br />
“Ndiyo,” akajibu huku akitetemeka.<br />
“Muda unazidi kuyoyoma! Ninachohitaji kutoka kwako ni kiasi cha dola milioni 290 ili niweze kuwaachia watoto wako. Ningependa fedha hizo nizipate ndani ya Msitu wa Beloomut, kusini mwa Jiji la Moscow kwa usalama zaidi.<br />
<br />
“Msitu wa Beloomut?” aliuliza lakini kabla hajapata jibu kutoka upande wa pili wa simu, alisikia sauti za watoto wake wakimwita.<br />
“Daaaady!” (Babaaaa!) kilio kikali kilifuatia nyuma yake, Fedorov akazidi kuchanganyikiwa akili.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Victor Fedorov atakuwa tayari kutoa kiasi hicho cha fedha ili kuwakomboa watoto wake? Ni kwa nini muuaji ametaka fedha hizo zipelekwe kwenye Msitu wa Beloomut?<br />
ITAENDELEA, HOPE SINA TENA KESI NA NYINYI........SIKU NJEMAA....LOVE U ALL.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244fff29a39725883693">MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.61.<br />
<br />
HALI yake ilikuwa mbaya hakuwa na uwezo wa kutoka baharini akiwa salama, risasi zilizoupenya mwili wake zilifanya amwage damu nyingi. Pamoja na kuwa jabali, Ditrov hakuwa na uhakika kama angesalimika.<br />
Ghafla akiwa katika hali ya kukata tamaa akakumbuka kitu wakati anaingia ofisini kwa Victor Fedorov, mfuko mmoja katika suruali yake alikuwa na kisu kidogo cha k<span class="text_exposed_show">ukunja akaamini huenda kisu hicho kingemsaidia kwa asilimia zote.<br />
<br />
Kwa nguvu zake zote akajitahidi kuingiza mkono mfukoni lakini hakufanikiwa akajaribu tena upande mwingine wa suruali yake na kukumbana na maumivu makali lakini pamoja na maumivu hayo akajaribu kuusogeza mkono wake zaidi mpaka kuufikia mfuko wa suruali. Kwa taabu kubwa akafanikiwa kukuta kitu kigumu na kuamini kwamba kilikuwa chenyewe.<br />
<br />
Akiwa katika hali ya kutapatapa akafanikiwa kuupenyeza mkono mfukoni na kukichomoa kisu kwa taabu kubwa, akakishika vyema na kujaribu kuikata kamba ili ajinusuru na umauti uliokuwa ukiinyemelea roho yake.<br />
Hakuwa tayari kukutana na kifo, ni kweli alifahamu wazi kwamba kila binadamu angeonja mauti lakini hakuwa tayari kufa kwa ukatili kiasi hicho, hivyo alitaka kujiokoa.<br />
<br />
Upande mwingine wa hadithi hii tunamwona Victor Fedorov na sharti alilopewa la kuzipeleka fedha hizo kwenye msitu wa Beloomut. Je, atafanikiwa kuzifikisha na kuwapata watoto wake? SONGA NAYO…<br />
<br />
“Tafuta mwanaume yeyote ambaye atakuwa tayari kuzaa na wewe Lina halafu mimi nitalea mtoto huyo,” maneno hayo yalijirudia kichwani mwa Lina.<br />
Hali ya hewa ikabadilika ghafla furaha yote iliyokuwepo ndani ya nyumba ikapotea, Phillip akiwaza jambo moja tu mtoto, hata Lina alipojaribu kumpa ushauri bado hakusikiliza.<br />
<br />
“Phillip mimi siko tayari,” alisema Lina.<br />
“Unamaanisha nini?”<br />
“Siko tayari kusaliti penzi letu sababu kubwa ikiwa ni mtoto.”<br />
“Mimi ndiyo mumeo nimeshasema tafadhali fanyia kazi maneno yangu.”<br />
<br />
“Hapana, kwa hilo nimekataa.”<br />
“Lina unanipenda kweli?”<br />
“Asilimia mia moja.”<br />
“Basi fanya ninachotaka.”<br />
<br />
Lina hakujibu kitu akainamisha kichwa chake chini huku kwikwi ya kulia ikimkaba, hakuwa tayari kukubaliana na maneno ya mumewe, kwake yeye mapenzi yangekuwepo tu hata bila kupata mtoto. Ni kweli yeye binafsi alikuwa mzima, tatizo lilikuwa kwa mume wake lakini tangu mwanzo alishakubaliana nalo.<br />
Akiwa katika mawazo hayo akamshuhudia Phillip akitoka sebuleni na kuelekea chumbani huko hakuchukua muda mrefu sana akamwona tena akitoka mkononi akiwa na funguo za gari.<br />
<br />
“Phillip!” Lina aliita lakini hakuitikiwa badala yake akashuhudia macho makali ya Phillip yakimwangalia, yalionyesha dalili zote kwamba alikuwa na hasira kali. Akamshuhudia akifungua mlango na kutoka nje bila kusema neno lolote.<br />
Uchungu wa ajabu ukaugubika moyo wa Lina, hakuwahi kushuhudia katika kipindi chote cha miaka minne alichoishi na Phillip kama mke na mume kwamba siku moja ingegeuka na kuwa shubiri.<br />
<br />
Machozi ya uchungu yakamtiririka mashavuni mwake.<br />
“Mtoto! Mtoto analeta matatizo katika penzi letu,” alisema Lina akinyanyuka kitini kuelekea nje huko nako akamshuhudia Phillip akiwasha gari na kutokomea kwenda sehemu ambayo haikujulikana.<br />
<br />
***<br />
Msitu wa Beloomut ulikuwa ni wa hatari sana, kila mtu nchini Urusi aliuogopa, wengi wakaupachika jina la msitu wa ajabu kwa matukio mbalimbali ya kutisha yaliyowahi kutokea ndani yake.<br />
Iliaminika kwamba mpaka wakati huo zaidi ya Warusi elfu moja walishakufa baada ya kuingia ndani ya msitu huo na wengi wao miili yao haikuonekana kabisa. Ni matukio hayo ya kutisha ndiyo yaliyosababisha serikali ya nchi hiyo kuingilia kati na kuutangaza msitu huo kwamba ulikuwa tishio na watu kupewa onyo kwamba asitokee mtu yeyote kwenda eneo hilo.<br />
<br />
“Msitu wa Beloomut?” lilikuwa ni swali likipita kichwani mwa Victor Fedorov, pamoja na kuwa mwanaume wa shoka, jina hilo lilimtia wasiwasi, akavuta kumbukumbu zake mara kadhaa juu ya matukio mabaya yaliyowahi kutokea katika msitu huo, akaangua kilio.<br />
<br />
Kwa Victor Fedorov kiasi cha fedha alichotakiwa kukipeleka kwenye msitu huo hakikuwa tatizo, utajiri wake ulitisha lakini kitu kimoja tu kilimsumbua akilini mwake, ni majanga mengi juu ya msitu huo, hakuwa tayari kwenda kufa lakini aliwahitaji sana watoto wake na ili awapate ni lazima apeleke fedha hizo sehemu aliyoelekezwa.<br />
<br />
“Niko tayari kutoa kiasi hicho cha fedha lakini je, nitanusurika? Watoto wangu watakuwa hai?” bado aliendelea kujiuliza kichwani mwake. Pamoja na maswali yote hayo bado taswira za Merina na Mariya ziliendelea kuzunguka ndani ya akili yake, hakuwa tayari kuwapoteza, hao ndiyo ndugu pekee aliokuwa nao.<br />
<br />
“Nitafanya kila ninachoweza kuwakomboa watoto wangu hata ikitokea mimi mwenyewe nikafa lakini wao wapone,” aliwaza.<br />
Akili yake ikaonekana kusimama, kwa mara ya kwanza akamkumbuka Ditrov, kwa wakati huo alionekana kuwa ni mtu muhimu sana kwake, aliamini kabisa kwamba mtu huyo angekuwepo maishani mwake kila kitu kingekwenda kama alivyotaka kwani fedha zilikuwa kila kitu katika maisha yake.<br />
<br />
“Sitaki kujutia kifo cha Ditrov, nitapambana kiume,” alisema kwa sauti ya kunong’ona.<br />
Akiwa na hofu, taratibu alianza kutembea kuelekea chumbani ambako alifungua mlango na kuingia ndani akanyoosha moja kwa moja mpaka kwenye moja ya makabati makubwa na kufungua. Pamoja na utajiri wote aliokuwa nao, Victor Fedorov aliweka kiasi kikubwa cha fedha ndani ya nyumba ili kukwepa usumbufu wa kwenda benki mara kwa mara.<br />
<br />
Huku machozi yakimbubujika, akanyoosha mkono na kuvuta moja ya mifuko iliyoonekana ndani ya kabati hilo na kuutoa nje, fedha nyingi zikaonekana na bila kupoteza muda akaanza kuchukua bunda moja moja na kuyahesabu.<br />
“Nitafanya kila kinachowezekana kuwapata watoto wangu hata akitaka nusu ya utajiri wangu nitampa lakini …” hakumalizia sentensi hiyo mara mlio wa simu ndani ya nyumba yake ukasikika.<br />
<br />
***<br />
Kwa muda wa saa nne mfululizo Lina aliendelea kumsubiri Phillip lakini hakuonekana, hata alipopiga simu yake ya mkononi haikupatikana. Lina akachanganyikiwa, hakuelewa ni wapi alikuwa na kitu gani kilimpata kwani hali aliyoondoka nayo nyumbani siku hiyo haikuwa ya kawaida.<br />
“Mungu nisaidie arejee nyumbani akiwa mzima, nitaendelea kusubiri kama saa moja mbele asipotokea nitakwenda kutoa taarifa polisi, pengine amejinyo…” alisema Lina na sentensi yake kukatizwa na honi ya gari nje ya lango la nyumba yao iliposikika.<br />
<br />
Haraka akasimama kitini ili achungulie nje, akamshuhudia mlinzi akilisogelea lango lakini badala ya kufungua akachungulia, hofu ikazidi kumwingia.<br />
“Ngoja niende mwenyewe,” alijisemea Lina akitembea kutoka nje kuelekea langoni na bila kusema chochote akauliza swali moja tu kwa mlinzi huyo.<br />
<br />
“Ni Phillip?”<br />
“Hapana ni mgeni tu.””Mgeni? Hebu nimwone,” alisema naye pia akachungulia.<br />
Ilikuwa ni sura ngeni kabisa kati yao, alipoliangalia gari pia hakulifahamu, taratibu akasogea na kumsabahi kijana aliyesimama nje ya gari.<br />
<br />
“Ndiyo kaka nikusaidie?”<br />
“Samahani sijui hapa ndiyo kwa Phillip?”<br />
“Ndiyo!”alijibu Lina akionekana mwenye wasiwasi mwingi.<br />
“Amenituma barua hii hapa,” alisema kijana huyo akinyoosha mkono kumwelekea Lina ili amkabidhi bahasha ndogo iliyokuwa mikononi mwake.</span></div></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244e83d4723737335923"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244fff1ead8018973234">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.62<br />
<br />
HUKU akitetemeka aliunyoosha mkono na kupokea barua hiyo macho yake yote yakimwangalia kijana aliyemkabidhi, alitaka kumsoma vyema na kumwelewa alitoka wapi na alitumwa na nani.<br />
“Ahsante kaka sijui naweza kukuuliza jambo?”<br />
“Uliza tu dada yangu.”<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
“Naweza kufahamu barua hii imetoka wapi na kwa nani?”<br />
“Mh, kwa kweli sifahamu mimi nimetumwa tu kuileta hapa.”<br />
“Uliambiwa umpe nani?”<br />
“Mke wake Phillip?”<br />
<br />
Tayari mashavu ya Lina yalishajaa machozi, kichwani mwake alielewa kabisa kwamba barua hiyo ilitoka kwa Phillip hivyo alitaka kuthibitisha jambo hilo.<br />
Baada ya maongezi hayo kijana huyo aliingia ndani ya gari lake na kuliwasha kisha kuondoka.<br />
Taratibu huku mapigo ya moyo yakimwenda mbio, Lina alijikaza na kutembea kuingia ndani lakini hakufika mbali sana akaketi chini. Haraka akaanza kuchana bahasha ili asome barua iliyokuwa ndani.<br />
<br />
Mke wangu mpendwa,Kwanza kabisa amini kwamba ninakupenda kwa dhati Mungu ni shahidi juu ya hili, nimeamua kuondoka hapo nyumbani kutokana na hasira iliyokuwa ndani yangu. Lengo langu kwako si baya ni zuri, sihitaji kitu kingine kutoka kwako zaidi ya mtoto, napenda unizalie mtoto mmoja tu nami niitwe baba. Jambo nililokueleza mwanzo sikukosea, nilitamka nikiwa na akili zangu timamu. Lina naamini unanipenda ndiyo maana ukaamua kunipokea mimi na matatizo yangu yote. Tafadhali fanya kila unachoweza ili lengo letu litimie.<br />
<br />
Najua itakuwia vigumu kuamini maneno yangu lakini kipande hiki cha barua ni ushahidi tosha kwamba siwezi kukuruka hata kitokee nini, nakupenda mke wangu.<br />
Ni kweli inauma sana lakini hakuna jinsi fanya unavyoweza tafuta mwanaume ambaye wewe mwenyewe utamridhia na uhakikishe unapata ujauzito wake, mimi binafsi sihitaji kumfahamu hata kidogo ninachohitaji ni wewe kupata ujauzito basi.<br />
<br />
Najua kichwani mwako utakuwa na maswali mengi ambayo hayatapata majibu lakini huo ndiyo uamuzi wangu, Lina uvumilivu umefikia mwisho. Tafadhali mke wangu niamini niko tayari tena kwa moyo mkunjufu, nahitaji mtoto.<br />
Kama utakuwa tayari kukubaliana na jambo hili na mimi mumeo, basi nipigie simu na kunijulisha nami nitakuwa tayari kurejea nyumbani tuendelee kuishi kama awali.<br />
<br />
Sisi wewe tu unayelia machozi hata mimi mwenyewe nakiri kutoka ndani ya moyo wangu huku nilipo sina raha hata kidogo akili yangu yote ikiwa kwako mke wangu mpenzi.<br />
Tafadhali chukua hatua fanya maamuzi sahihi kisha utanijulisha.<br />
Nakupenda.<br />
Ilimaliza barua hiyo.<br />
<br />
Kwikwi ya kulia ikamkaba Lina, hakuwa tayari kuamini maneno yaliyokuwa ndani ya barua hiyo, taswira ya Phillip ikamjia kichwani mwake mfululizo, siku zote aliamini kwamba Phillip alikuwa ni mwanaume wa maisha yake lakini sasa kulikuwa na dalili zote kwamba penzi lao lilikuwa likielekea mwisho.<br />
“Nampenda sana Phillip lakini kwa hili sipo tayari,” alisema Lina huku akijifuta machozi, haraka akanyanyuka na kukimbilia ndani.<br />
<br />
Ulikuwa ni mtihani mwingine tena katika maisha yake. Hakuwahi kusikia wala kuona mwanaume aliyeweza kumtoa mkewe kwa mwanaume mwingine ili wafanye tendo la ndoa lengo hasa likiwa ni kupata ujauzito.<br />
“Mh! Phillip hivi amepatwa na nini? Kwangu mimi mtoto si kitu, ninachojali ni mapenzi ya dhati, kwa nini asikubaliane na mimi? Mungu wangu tafadhali okoa jahazi hili lisizame, mimi siko tayari kufanya hivi anavyotaka.” Aliongea Lina machozi yakimbubujika.<br />
<br />
Hatimaye usiku ukaingia bila kumwona Phillip akirejea nyumbani hapo ndipo akaamini kwamba mwanaume huyo alikuwa akimaanisha alichokisema.<br />
“Nitamsubiri mpaka asubuhi niangalie kama kweli hatarudi basi nitajua cha kufanya.”<br />
Usiku mzima hakupata hata lepe la usingizi, muda wote akimfikiria Phillip na mtihani aliokuwa amempa. Upande mwingine wa akili yake ulimwambia kwamba huenda mtu huyo alikuwa akimpima imani lakini upande mwingine ulimweleza wazi kwamba Phillip hakutania. Hatimaye mapambazuko yakawadia, Phillip akiwa bado hajarejea nyumbani, akayaamini maneno yake.<br />
<br />
Siku nzima Lina alishinda ndani, aliamua kupiga simu kazini kwake na kuwaeleza kwamba siku hiyo asingeweza kudhuhuria kwani alikuwa mgonjwa hivyo alihitaji kupumzika ili kuangalia afya yake. Aliamua kuuficha ukweli kwa kudanganya hivyo ili tu asipate bughudha, huku akiwa na mawazo mengi kichwani mwake Lina bila kula kitu chohote alirejea kitandani kwake na kulala usingizi.<br />
<br />
Saa zikazidi kusonga, hatimaye mchana ukaingia, akiwa hapo akapata wazo la kuamua kumpigia mmoja wa marafiki zake ofisini ili aongee naye na kumuuliza kama alishamuona Phillip ofisini siku hiyo. Akaisogelea simu kisha kubonyeza namba kadhaa na kuiweka sikioni.<br />
<br />
“Habari?” alisikika akisalimia mtu upande wa pili wa simu ambaye hakuonekana akatulia kidogo na kisha kujibu.<br />
“Oh! Leo naumwa rafiki siko sawa, nauliza jambo moja tu vipi leo umemwona shemejio?” akatulia tena.<br />
“Yupo, basi nilitaka tu kujua kama amekuja maana anaweza kusema amekwenda kazini kumbe kapita kona,” alidanganya kisha wakaagana na simu kukatwa.<br />
<br />
“Yaani Phillip! Phillip ananitenda hivi? Ameshindwa kurejea nyumbani lakini ameweza kwenda kazini? Lazima atakuwa na mwanamke sehemu fulani.<br />
Amepata wapi nguo za kuvaa? Kwa inavyoonekana Phillip hatanii anamaanisha anachokisema…lakini mimi siwezi kufanya anavyotaka…mh! Naona penzi letu limefikia mwisho,” aliwaza Lina. Lakini ghafla akarejesha akili yake nyuma na kukumbuka mmoja wa marafiki zake katika ofisi yake alivyokuwa akimsifia Phillip, alionekana kumpenda kama si kumtamani.<br />
<br />
“Inawezekana Magreth amenigeuka? Mara kadhaa amekuwa akimsifia sana Phillip, pengine ndiko huko alikokwenda? Hapana nitafanya uchunguzi kwanza.”<br />
Wiki nzima ikakatika bila Phillip kurejea nyumbani, hali hiyo ikazidi kumtia Lina kizungumkuti, ni hapo ndipo alipoamua kumpigia simu Phillip na kumweleza kwamba anamwomba arejee nyumbani ili wafanye mazumgumzo.<br />
“Tafadhali mume wangu naomba urudi nyumbani tuzungumze,” alisema Lina huku akilia.<br />
“Je, umekubaliana na mimi?” aliuliza Phillip.<br />
<br />
Kwa muda alikaa kimya akijaribu kutafakari ni jibu gani angempa mume wake ili akubali na kurejea nyumbani, hakuwa na jinsi alimhitaji mno. Huyo ndiye alikuwa mwanaume wa maisha yake, hakika alimpenda Phillip kwa dhati.<br />
“Ni…ko…taya…ri,” alitamka Lina huku akilia.</span></div></span></div><span class="fcg"> – </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501244fff169d3647065932">MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.63.<br />
BAADA tu ya kufanikiwa kuikata kamba na kutumia nguvu kidogo alizokuwa nazo huku damu nyingi zikimwagika sehemu ya bega la kushoto, alijaribu kupiga mbizi, lengo lake likiwa ni kujiokoa, kichwani mwake hakuwa na matumaini yoyote pamoja na kwamba alishapitia mambo mengi ya Kimafia lakini hilo kwake lilionekana kuwa gumu.<br />
<br />
Kadiri alivyoendelea kupiga mbizi ndivyo<span class="text_exposed_show"> fahamu nazo zilivyozidi kupotea taratibu, nguvu zikaonekana kumwishia, akazama mara ya kwanza na kuibuka juu akijaribu kupunga mikono hewani kuona kama angepata msaada wowote lakini haikuwa hivyo, akazama mara ya pili na kuibuka huku akimeza maji mengi akaanza kukata tamaa ya kuiona dunia akiwa hai.<br />
<br />
Ni wimbi hilo ndilo lililotingisha mtumbwi wa Oleg Malenko na kumfanya kuamini kwamba sasa kifo chake kilikuwa kimekaribia kwa kuliwa na samaki mkubwa, kichwani mwake hakuelewa kabisa kwamba alikuwa ni mtu aliyekuwa akitapatapa baharini ili kujiokoa.<br />
<br />
“Hapana nitahakikisha najiokoa, sipo tayari kuliwa na samaki hapa baharini,” alisema akiweka vizuri mtumbwi wake lakini ghafla alipotupa macho yake vizuri eneo hilo huku mapigo yake ya moyo yakimwenda mbio, alishuhudia mikono ya mtu ikichomoza kutoka ndani ya maji.<br />
<br />
“Mh! Mbona naona mikono?” alijiuliza akimulika eneo hilo kwa taa yake ndogo aliyokuwa akiitumia katika shughuli zake za uvuvi. Macho yake hayakukosea ni kweli alikuwa ni mtu ambaye hakuelewa alikuwa mzima au mfu, kwa macho alionekana tayari alishakufa.<br />
“Inawezekana amekufa lakini nitajuaje? Ni lazima nimguse kwa kasia ili nione pengine anaweza kuwa amezimia tu,” aliwaza.<br />
<br />
Ghafla akiwa katika mawazo hayo alishuhudia mtu huyo akizama na kuibuka juu akitapatapa kama mtu aliyekuwa akikata roho kisha kutulia kimya, mwili wake ukaelea juu ya maji. Haraka bila kuchelewa, Oleg, kwa kutumia kasia alilokuwa nalo mkononi mwake, akalikamata vyema na kusogea karibu kabisa na mwili wa mtu huyo ambaye kwa kumwangalia mara moja alionekana kuwa amekufa. <br />
<br />
Akiwa na hofu, akamgusa mtu huyo kwa kutumia kasia.<br />
“Uko hai kweli wewe? Masikini wamekuua?” alijiuliza Oleg kwa Kirusi akizidi kumgeuza mtu huyo ambaye bado alionekana kutulia.<br />
<br />
***<br />
“Tafadhali mume wangu naomba urudi nyumbani njoo tuzungumze,” alisema Lina huku akilia.<br />
“Je, umekubaliana na mimi?” aliuliza Phillip.<br />
Kwa muda alikaa kimya akijaribu kutafakari ni jibu gani angempa mume wake ili akubali na kurejea nyumbani, hakuwa na jinsi alimhitaji mno, huyo ndiye alikuwa mwanaume wa maisha yake hakika alimpenda Phillip kwa dhati.<br />
“Ni…ko…taya…ri,” alitamka Lina huku akilia.<br />
<br />
Akiwa hapo ghafla akasikia simu upande wa pili ikikatwa bila kupewa jibu lolote.<br />
“Amekata simu?” alijiuliza huku akijifuta machozi.<br />
Ulikuwa ni mtihani mgumu kweli kwa Lina lakini alitakiwa kuufanya na kufaulu kama tu alimhitaji Phillip maishani mwake, huku akilia akarejea moja kwa moja na kuketi kwenye kiti, tayari ilishatimu saa kumi na mbili za jioni na mawazo yake yote yakiwa kwa Phillip ambaye mpaka wakati huo hakuelewa kama angerejea nyumbani au la kwani hakuwa ametoa jibu lolote.<br />
<br />
“Piii! Piii! Piii!” ilikuwa ni honi nje ya lango la nyumba yao.<br />
“Naomba Mungu awe yeye, niongee naye na kumbembeleza ili anielewe mimi siko tayari kufanya tendo la ndoa nje ya ndoa yetu,” alijisemea Lina.<br />
Mawazo yake hayakukosea ni kweli alikuwa ni Phillip, Lina akanyanyuka kitini na kuusogelea mlango kisha kuufungua akimkaribisha ndani.<br />
<br />
“Karibu mume wangu.”<br />
“Mwaa!” lilikuwa ni busu lililotua moja kwa moja usoni mwa Lina kutoka kwa Phillip. Akiwa haamini alichokishuhudia kwa macho yake machozi ya uchungu yakamtoka Lina.<br />
“Tafadhali usilie mke wangu yote haya yanatokea kwa sababu moja tu, mtoto!”<br />
“Phillip, maisha bila mtoto hayaendi?”<br />
<br />
“Yatakwenda lakini mtoto ni lazima Lina, sikia nimekuja kwa suala moja tu,” alisema Phillip safari hii akionekana mpole.<br />
“Ndiyo.”<br />
“Lina ninakupa mwezi mmoja tu nipate matokeo ya mjadala wetu vinginevyo utanikosa kabisa katika maisha yako,” alisema Phillip akionyesha umakini wa hali ya juu.<br />
“Phillip hapana, bado nakupenda, nakuhitaji mume wangu.”<br />
<br />
“Basi kama hivyo ndivyo fanya ninachotaka.”<br />
“Nitafanya unachokitaka mume wangu lakini na nani?”<br />
“Hilo suala nakuachia wewe mimi nimetoa ruhusa fanya unachoweza Lina wewe ni mwanamke tumia akili zako.”<br />
<br />
“Mh!” Lina aliguna tayari Phillip alishanyanyuka kwenye kiti na kumwacha hapo peke yake akatembea kuuelekea mlango wa chumba chao, akaufungua na kuingia ndani. Lina akamwaga machozi, ni kweli alikuwa amefanikiwa kumrejesha Phillip nyumbani lakini hakuwa tayari kukabiliana na mtihani uliokuwa mbele yake kwani alishatumia akili zake zote kumshawishi kuondokana na mawazo hayo lakini ilionekana kushindikana, haja ya Phillip ilikuwa ni mtoto basi.<br />
<br />
***<br />
“Nitamuokoa hata kama atakuwa amekufa nitamzika kwa heshima zote, hastahili kuachwa kama mzoga!” alisema Oleg.<br />
Moyo wake uliingia huruma na aliumia zaidi alipomwangalia mtu huyo akielea majini mwili wake ukiwa mtupu bila nguo.<br />
“Ni kwa nini watu wanafanya ukatili wa aina hii? Alikosa nini huyu mpaka kustahili adhabu hii? Mungu nisaidie!” alisema mfululizo, muda wote huo akiendelea kumtingisha mtu huyo kwa kutumia kasia.<br />
<br />
Dakika tano nzima aliendelea kumtingisha bila mtu huyo kujigeuza wala kujitingisha hapo ndipo akaamini kwamba tayari alishakufa hivyo kufikia uamuzi wa kumtoa ndani ya maji ili ampeleke ufukweni na huko angetafuta sehemu na kumzika kwa heshima zote.</span></div></span></div><span class="fcg"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f3419a1195310775"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245b0228395709258166">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.64<br />
<br />
Huku akitetemeka na jasho jingi kumtoka, Oleg Malenko alijitahidi kwa nguvu zake zote kumtoa mtu huyo ndani ya maji na kumpandisha juu ya mtumbwi wake tayari kwa kurejea nchi kavu. Aliamini akifika huko ndiyo angefahamu ukweli wote kama alikuwa hai au amekufa.<br />
<br />
“Kama atakuwa amekufa basi itakuwa ni bahati mbaya, nitamzika,” aliwaza huku akimgusa mtu huyo shingon<span class="text_exposed_show">i mwake. Baada tu ya kumpandisha ndani ya mtumbwi, bila kuchelewa akaugeuza haraka na kuanza kupiga kasia kurejea nchi kavu. Haikumchukua muda, akawa tayari amewasili ufukweni, akaegesha vizuri mtumbwi wake na kushuka, mikononi mwake akiwa amembeba mtu huyo.<br />
<br />
Alipohakikisha kwamba tayari ameshayaacha maji kwa umbali mrefu, kwa haraka alimshusha chini na kumlaza, akainama na kuanza kusikiliza mapigo ya moyo. Kwa takribani dakika tatu nzima alikuwa akisikiliza lakini hakusikia kitu, kichwani mwake akaamini kabisa kwamba mtu huyo hakuwa hai.<br />
<br />
“Nitachimba shimo pale haraka haraka na kumfukia hapo,” aliongea kwa kunong’ona. Akaangaza macho yake huku na kule kuangalia kama kulikuwa na mtu yeyote eneo lile lakini hakufanikiwa kuona kitu.<br />
“Huu ndiyo muda, nikichelewa tu watu wakaniona watajua mimi ndiye nimemuua kumbe nasaidia tu,” akiwa katika mawazo hayo ghafla alisikia mtu akikohoa mfululizo.<br />
“Khoo!Khoo!Khoooo!” Oleg Malenko alishtuka na kugeuka kuangalia, lakini hakuona mtu, alipogeuka tena upande mwingine sauti ya kikohozi ikasikika, safari hii kwa nguvu.<br />
<br />
Haraka akatupa macho yake kumwangalia mwanaume aliyekuwa amelala chini, huyo ndiye aliyekuwa akikohoa mfululizo. Bila kuchelewa akasogea karibu ili asikie vizuri, hakukosea alikuwa ni yeye.<br />
“Mh! Amekohoa? Hajafa huyu, ngoja nimpe huduma ya kwanza niangalie itakuwajea,” alisema huku akimgeuza mtu huyo na kumlaza kifudifudi. Akapiga magoti juu ya mgongo wake na kumkandamiza ili kumsaidia kutoa maji yaliyokuwa tumboni mwake.<br />
<br />
Hakukosea, alichokuwa akikifanya kilikuwa ni sawa kabisa. Kwa takribani dakika tatu nzima aliendelea kumkandamiza mgongoni, maji mengi yakawa yanamtoka hadi alipohakikisha maji aliyoyameza mtu huyo yamekwisha. Akamgeuza na kumlaza kiubavu huku akijaribu kuongea naye.<br />
“Wewe ni nani? Umetoka wapi? Imekuwaje ukawa hapa?” aliuliza mfululizo lakini hakupata jibu kutoka kwa mtu huyo ambaye alilala kimya ardhini akitetemeka.<br />
<br />
“Tafadhali niambie nini kimekupata?” aliendelea kuuliza huku akimchunguza vyema mtu huyo.<br />
“Di…t…ro…” aliongea kwa shida lakini kabla hajamaliza sentensi yake, Oleg Malenko akashuhudia mtu huyo akirusha mikono na miguu kisha kutulia kimya.<br />
“Mh! Hizi damu zinatoka wapi?” alijiuliza huku akimfunua upande huo. Macho yake yakakutana na jeraha kubwa.<br />
“Hili ni jeraha la risasi ambalo limesababisha kuvuja kwa damu nyingi kiasi hiki, lazima nifanye kitu kuokoa maisha ya mtu huyu,” alisema huku akijaribu kumnyanyua sehemu aliyokuwa amelala.<br />
Wazo pekee likamjia kichwani mwake kwamba ni lazima mtu huyo apate matibabu haraka hospitalini lakini hakujua atampeleka hospitali gani.<br />
<br />
Hiyo ilikuwa ni kwa sababu ya machafuko makubwa yaliyoikumba nchi ya Urusi. Aliendelea kujiuliza ni hospitali gani angempeleka mtu huyo na kupokelewa bila maelezo ya kutosha! Akahisi hiyo ingekuwa hatari nyingine kwake. Alihisi anaweza kuingia kwenye kesi ambayo asingeweza kujinasua kama mtu huyo angekuwa amekufa.<br />
<br />
“Hapana, sitampeleka hospitali. Nitampeleka nyumbani kwangu, naamini hajafa. Huko nitampa matibabu mpaka apone kabisa, hapo atakuwa tayari kunieleza ukweli wa nini kilichompata,” alisema Oleg Malenko. Tayari mapambazuko yalishaanza kuchomoza.<br />
***<br />
Mapenzi yote yaliyokuwa katikati yao yalionekana kupotea, furaha ndani ya nyumba ikageuka na kuwa shubiri. Phillip akisisitiza jambo moja tu, mtoto! Kwa muda wa wiki nzima, Lina aliendelea kumbembeleza na kumsihi Phillip aachane na jambo lililokuwepo kichwani mwake na badala yake wale na kufurahia maisha.<br />
“Lina, hakika hujaweza kunishauri juu ya hili. Fanya ninachotaka halafu tutaelewana,” alisema Phillip huku akigeuka upande mwingine wa kitanda, akavuta shuka na kujifunika gubigubi. Hata Lina alipojaribu kumuita, bado hakujibu wala kugeuka. Kwa mara nyingine tena moyo wa Lina ukauma kupita kawaida, akanyanyuka kitandani, akafungua mlango wa chumba na kutoka nje huku akilia.<br />
<br />
<br />
Wakati akitembea kuelekea sebuleni ghafla wazo likamjia kichwani mwake. Akalikumbuka jina Daniel, kijana mtanashati kweli kweli ambaye kwa muda mrefu alikuwa akimfuatilia Lina akimtaka kimapenzi. Mara zote aliambulia majibu ya karaha na pengine yaliyouchoma moyo wake kama mkuki wa moto.<br />
<br />
<br />
“Daniel! Sijui atakuwa wapi kwa sasa? Na sijui kama bado atakuwa hajaoa! Je, nitaanzia wapi kumweleza kwamba nampenda ilhali nilishamuumiza moyo? Lakini nitajaribu, sipendi kumpoteza Phillip. Naamini huyu ndiye mwanaume wa maisha yangu yote,” alisema Lina, akakisogelea kiti na kuketi juu yake kwa muda. Aliendelea kutafakari juu ya tatizo lililokuwa ndani ya nyumba yake, alitakiwa afanye kitu fulani ili kuinusuru ndoa yake. Tayari mashavu yake yalishalowa kwa machozi.<br />
<br />
<br />
“Kesho asubuhi nitamtafuta Daniel, najua atashangaa lakini sina jinsi, huyu pekee ndiye atakayewe…” alisema lakini kabla hajamaliza sentensi yake, kwikwi ya kulia ikamkaba tena.</span></div></span></div><span class="fcg"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501245b0221c19e47374028">MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.65<br />
<br />
“Daniel! Sijui atakuwa wapi kwa sasa? Na sijui kama bado atakuwa hajaoa? Je, nitaanzia wapi kumweleza kwamba nampenda ili hali nilishamuumiza moyo? Lakini nitajaribu, sipendi kumpoteza Phillip, naamini huyu ndiye mwanaume wa maisha yangu yote,” alisema Lina akakisogelea kiti na kuketi juu yake, kwa muda aliendelea kutafakari juu ya tatizo lililokuwa ndani ya n<span class="text_exposed_show">yumba yake, alitakiwa afanye kitu fulani ili kuinusuru ndoa yake. Tayari mashavu yake yalishalowa kwa machozi.<br />
<br />
<br />
“Kesho asubuhi nitamtafuta Daniel najua atashangaa lakini sina jinsi, huyu pekee ndiye atawe…” aliwaza lakini kabla hajamaliza sentensi yake kwikwi ya kulia ikamkaba tena.<br />
<br />
<br />
Hakika hakuelewa maisha yake yangekuwa vipi kama tu asingeweza kukubaliana na Phillip, mumewe, ambaye mpaka wakati huo hawakuwa na maelewano mazuri ndani ya nyumba. Aliendelea kubaki eneo hilo bila kurejea chumbani hapo, kazi ikawa moja tu kulia mpaka usingizi ulipomchukua ambapo alizinduliwa na sauti ya mlango ukifunguliwa na aliponyanyua uso kuangalia alimwona Phillip akitembea kumsogelea.<br />
<br />
Bila kusema kitu alimshuhudia akimwinamia na kumbusu kisha kumpigapiga mgongoni.<br />
“Lina!”<br />
“Yes darling!” alijibu huku machozi yakimbubujika, akili yake ikarejea kwenye mazungumzo yote yaliyofanyika jana yake.<br />
<br />
<br />
“Naamini umeshapata jibu la tatizo linalotusumbua.”<br />
Bila kujibu chochote akiwa hapo akanyanyua uso wake na kumwangalia Phillip machoni.<br />
“Unalia nini?” lilikuwa ni swali kutoka kwa Phillip baada ya kumwangalia vyema Lina usoni aligundua macho yake yalikuwa yamevimba kupita kawaida.<br />
<br />
<br />
“Hakika huo ndio msimamo wangu mke wangu, ni kweli inauma lakini sina jinsi.”<br />
“Yupo mtu ambaye nimemfikiria jana usiku, huyu nadhani anaweza kunisaidia.”<br />
“Ni vyema ukafanya hivyo mara moja lakini tu awe ni mtu unayemwamini sana na nisingependa afahamu siri iliyoko kati yetu, cha muhimu ni wewe kujiweka sawa ili kupata ujauzito basi mambo mengine tutajua mbele ya safari. Sawa mke wangu?”<br />
<br />
<br />
“Sa…wa,” alijibu lina huku akilia.<br />
Bila kusema kitu Phillip akanyanyuka kitini kisha kumnyanyua Lina wote wawili wakaingia chumbani ili kujiandaa kwa ajili ya kwenda kazini, lakini mambo hayakuwa hivyo. <br />
<br />
Baada tu ya kuingia ndani huku wote wawili wakiwa kimya Phillip alimnyanyua Lina na kumrushia kitandani naye akifuata kwa nyuma bila kuchelewa, akaanza kumvua nguo moja baada ya nyingine kisha akabaki mtupu kama alivyozaliwa.<br />
<br />
<br />
“Lina nakupenda,” ilikuwa ni sauti ya Phillip ikipita masikioni mwa Lina.<br />
“Una..se…ma..kwe..li?” aliuliza lina kwa sauti ya kutetemeka.<br />
<br />
“Asilimia mia moja mke wangu mambo yote haya yanatokea si kwa sababu mimi nakuchukia hapana…” alisema Phillip akilivuta shuka na wote wawili wakajifunika gubigubi.<br />
<br />
<br />
Kilichofuata baada ya hapo hakiandikiki kwani ilikuwa ni kama vile watu wakiimba mapambio na wengine kuitikia, mara chache sana sauti ya Lina ilisikika lakini ilimezwa na mabusu mfululizo yaliyotoka kinywani mwa Phillip. Saa mbili baadaye wote wawili walikuwa hoi bin taaban jasho jingi likiwatiririka.<br />
“Nimeamua kufanya hivi kwa sababu nataka uamini kwamba ninakupenda kwa dhati na si kitu kingine, sawa?” Phillip alisema.<br />
<br />
“Ahsante!” alijibu Lina akimwangalia Phillip kwa jicho la huruma.<br />
“Hebu nieleze ni nani huyo unayemfikiria?” Phillip aliuliza kwa upole.<br />
“Yupo kijana mmoja anaitwa Daniel huyu tulisoma naye huko nyuma na alinipenda sana.”<br />
“Je, unamwamini?”<br />
<br />
“Asilimia zote labda itokee tu kwamba ameoa kwa sasa?”<br />
“Hata kama ameoa tunachohitaji sisi ni yeye kukupa mamba, basi, mambo mengine yote atuachie sisi wenyewe.”<br />
<br />
“Nipe muda nimtafute kisha nitakujulisha.”<br />
“Ahsante mke wangu sasa naamini kweli unanipenda.”<br />
“Nakupenda pia Phillip, yote haya nafanya ili kulinda penzi letu, sipendi kukupoteza, wewe ni wangu mpaka mwisho.”<br />
“Najua jambo hilo ila kitu kimoja tu nikuombe.”<br />
“Ni nini hicho?”<br />
“Nihakikishie kwamba baada tu ya kufahamu kwamba umepata mimba hutarejea tena kwa Daniel.”<br />
“Siwezi kufanya hivyo Phillip unanifahamu vyema, jambo hili linatokea kwa sababu wewe ndiye umetaka.”<br />
“Basi nakuamini fanya kila unachoweza umpate kisha utanijulisha kila hatua, sawa?”<br />
“Nitafanya hivyo,” alisema Lina na wote wawili wakanyanyuka na kuingia bafuni kuoga ili wajiandae tayari kuelekea kazini.<br />
<br />
Dakika tano baadaye tayari wote wawili walishakuwa tayari wakatoka mpaka nje ambako walisalimiana na mlinzi kisha wakaingia ndani ya gari, Phillip akiketi kwenye usukani, safari kuelekea ofisini ikaanza, njiani wakiongea mambo mengi kuhusu maisha na mapenzi yao na furaha ilionekana kurejea tena katika mapenzi yao.<br />
<br />
Kutokana na msongamano wa magari siku hiyo walilazimika kutumia saa moja mpaka kufika ofisini kwao, wakafika na kuegesha gari lao kisha kushuka. Phillip akazunguka mpaka sehemu alipokuwa amesimama Lina na kumshika mkono, kwa pamoja wakatembea kuingia ndani ya ofisi. Yalikuwa ni mazoea ya Phillip kumsindikiza Lina mpaka anahakikisha ameingia ndani ya ofisi yake ndipo yeye atoke na kuelekea ofisini kwake.<br />
<br />
Taratibu huku wakionyesha nyuso za tabasamu walitembea mpaka kuufikia mlango wa ofisi ya Lina, akafungua ili aingie ndani lakini kabla hajafanya hivyo akavutwa kwa nyuma.<br />
“Darling!” ilikuwa ni sauti ya Phillip.<br />
“Yes.” (Ndiyo.)<br />
“Nimesahau kitu.”<br />
“Kitu gani?”<br />
Bila kusema kitu chochote akamsogelea Lina na kuanza kumbusu mfululizo bila kujali watu waliokuwa wakipita eneo hilo.<br />
“Ahsante…” alisema Lina akitabasamu.<br />
“Tafadhali kumbuka kumtafuta Daniel” alisema Phillip kwa sauti ya kunong’ona.<br />
***<br />
“Vrooom!Vrooom!” ilikuwa ni sauti ya kitu kikiburuzwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine.<br />
Kwa sababu hakutaka jambo hilo ligundulike na mtu mwingine, aliamua kuuficha ukweli huo kwa kumburuza mtu huyo na kwenda kumweka pembezoni mwa mitumbwi mibovu amwache hapo na yeye atembee kurejea mpaka sehemu ambako aliamini angepata usafiri na amchukue tayari kwa kumpelekea nyumbani kwake ambako angefanya kila kilichowezekana kuokoa uhai wa mtu huyo.<br />
<br />
“Nikipata tu usafiri na kuongea na dereva anisaidie kumfikisha mtu huyu nyumbani itakuwa safi, nitamlipa kiasi atakachotaka lakini afiche siri hii,” aliwaza Oleg Malenko.<br />
<br />
Haraka bila kupoteza muda alipohakikisha kwamba amemweka mtu huyo sehemu salama, alitoka haraka na kuangaza macho yake huku na kule na alipohakikisha kwamba hapakuwa na mtu, akaanza kutembea kuondoka eneo hilo.<br />
<br />
“Nitamsaidia mpaka mwisho bila kuchoka kwa kumwangalia, anaonekana ni mtu mwema, naomba Mungu asije kuwa mtu mbaya,” alijisemea akizidi kusonga mbele.<br />
<br />
Dakika tano tu tayari alishatokeza barabarani, akaongoza moja kwa moja mpaka mahali ambako teksi zilisimama hapo kungoja wateja, akaisogelea moja na kuanza kuongea na dereva, kwa dakika tatu nzima walifanya mazungumzo na kuonekana kukubaliana, haraka akazunguka upande wa pili na kupanda kisha gari hilo kuondoka eneo hilo.<br />
<br />
“Nitakuonyesha sehemu ya kusimama kisha kuomba msaada wako ili tumchukue haraka kumpandisha ndani ya gari.”<br />
“Hakuna shida,” alijibu dereva huyo kwa lugha ya Kirusi.<br />
Haikuchukua muda tayari wakawasili eneo la tukio, Oleg Malenko akawa mtu wa kwanza kushuka ndani ya gari na kuanza kumwongoza mwenzake lakini kabla hawajamfikia, macho yake yalishuhudia jambo ambalo halikuwa la kawaida.<br />
“Mh!” aliguna.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Lina anakabiliwa na mtihani mzito. Je, atafanikiwa kuufaulu? Oleg Malenko ameona kitu gani? Fuatilia kesho kama kawa!!!goodnite NAWAPENDA NYOOOTEEE!!!</span></div></span></div><span class="fcg"> –</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f34a620d29879634"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012463bc2f100b49471849">MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.66<br />
<br />
HARAKA bila kupoteza muda anaangalia huku na kule na kuhakikisha kwamba alimweka mtu huyo sehemu salama. Oleg Malenko anatoka mbio eneo hilo kuelekea barabarani kichwani mwake akiwa na wazo moja tu, kutafuta gari ambalo lingemsaidia kumfikisha mtu huyo nyumbani kwake na huko angepata matibabu na kupona.<br />
<br />
“Nitamsaidia mpaka mwisho bila kuchoka, kwa kumwangalia anao<span class="text_exposed_show">nekana ni mtu mwema naomba Mungu asije kuwa mtu mbaya.” Aliongea akizidi kusonga mbele.<br />
<br />
Dakika tano tu tayari alishatokeza barabarani, akaongoza moja kwa moja mpaka mahali ambako teksi zilisimama kwa ajili ya kungoja wateja, akaisogelea moja na kuanza kuongea na dereva, kwa dakika tatu nzima walifanya mazungumzo na kuonekana kukubaliana, haraka akazunguka upande wa pili na kupanda kisha gari kuondoka eneo hilo.<br />
<br />
Haikuchukua muda wakawasili eneo la tukio, Oleg Malenko akawa mtu wa kwanza kushuka ndani ya gari na kuanza kumwongoza mwenzake lakini kabla hawajamfikia macho yake yalishuhudia jambo ambalo halikuwa la kawaida.Je, nini kinaendelea?<br />
<br />
Upande wa pili wa hadithi hii tunamwona Lina akifikiria jinsi ya kumpata kijana Daniel ambaye angeongea naye na kumshawishi wafanye tendo la ndoa na kupata ujauzito, ni mtihani mgumu lakini alitakiwa kuufanya ili kumlinda mwanaume aliyempenda kwa dhati.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea hapa? Atafanikiwa kumpata Daniel? Na nini kitatokea? SONGA NAYO…<br />
<br />
“Tafadhali kumbuka kumtafuta Daniel,” aliongea Phillip kwa sauti ya kunong’ona.<br />
Ni maneno hayo yaliyofanya kumbukumbu za Lina kurejea upya kichwani mwake, moyo wake ukaenda mapigo ya haraka haraka kama vile mtu aliyekuwa akikimbia mbio ndefu.<br />
<br />
“Mungu nisaidie kufanya jambo hili.” Alinong’ona akizama ndani ya ofisi yake. Taratibu akakisogelea kiti kikubwa kilichokuwa nyuma ya meza kubwa na kuketi huku jasho likimtiririka.<br />
“Sina namna ni lazima nimtafute Daniel tu ili kulinda penzi langu kwa Phillip.” Aliwaza.<br />
Kwa muda wa dakika tano nzima alikaa kimya akijaribu kutafakari nini cha kufanya lakini bado hakupata jibu na upande mmoja wa akili yake ulimwambia kwamba kama asingethubutu kufanya jambo hilo hakika angemkosa Phillip maisha yake yote.<br />
<br />
Akiwa hapo huku machozi yakimbubujika, Lina akavuta moja ya droo iliyokuwa karibu na meza aliyoketi, akaanza kuchambua karatasi moja baada ya nyingine akitafuta mahali ambako aliamini angeweza kupata maelezo ya namna ya kumpata Daniel.<br />
Alipitia karatasi moja baada ya nyingine na kwa bahati nzuri akafanikiwa kupata moja ya barua ambazo Daniel aliwahi kumwandikia miaka mingi.<br />
<br />
“Nimeipata.” Aliongea akiichomoa karatasi hiyo na kuishika vyema mikononi mwake ili asome.<br />
Taswira ya Daniel ikamjia kichwani mwake, akamwona jinsi alivyokuwa ni kweli alistahili kuitwa mwanaume wa shoka kwani alikuwa na kila sababu ya kupewa tunu hiyo, alikuwa ni kijana mrefu, rangi yake ya ngozi pia ilivutia na midomo yake ilikuwa minene na zaidi ya yote, Daniel alikuwa na kifua kipana kilichofanya kila mwanamke aliyemwona amtamani kimapenzi. Hakika alisisimua.<br />
“Anazo sifa zote lakini mimi …” Lina aliongea, hata kabla hajamalizia sentensi yake mlango wa ofisi yake ukagongwa.<br />
<br />
***<br />
“Mh!” Oleg Malengo aliguna akijaribu kuangaza macho yake huku na kule kama vile alikuwa akiangalia kitu fulani.<br />
“Kuna nini?” Dereva wa teksi naye akauliza akionesha wasiwasi mwingi.<br />
Bila kujibu swali alilokuwa ameulizwa alitembea haraka kusonga mbele hakika alionekana kama mtu aliyekuwa akisaka kitu ambacho hakikuonekana.<br />
<br />
“Kimetokea nini? Mbona alikuwa hapa?” Alijiuliza.<br />
Kwa ujasiri mkubwa akasogea mpaka mahali alipokuwa amemwacha mwanaume aliyemwokoa ndani ya maji lakini hakumwona, alichokuwa amekishuhudia kwa macho yake yote mawili ni alama za mburuzo ulioonekana ardhini.<br />
“Ameondoka.” Aliongea.<br />
“Nani?”<br />
<br />
“Yule niliyekueleza kwamba nahitaji unisaidie?”<br />
“Lakini si ulisema ana hali mbaya?”<br />
“Ni kweli nashangaa pengine amepata nguvu.”<br />
“Sidhani hebu kumbuka vizuri ni hapa kweli ulipomwacha?”<br />
“Hakika ni hapa alama zake zi hizi hapa.”<br />
<br />
“Mh.” Dereva teksi naye akaguna hakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea.<br />
Kabla ya Oleg Malenko kwenda kutafuta usafiri alipokuwa akimweka mwanaume huyo vyema eneo aliloamini kuwa ni salama na kuondoka kuelekea barabarani kwa ajili ya kutafuta usafiri jambo la ajabu lilitokea, upepo mkali ukiambatana na ubaridi mkali ulipiga eneo la ufukweni na upepo huo ndiyo uliosababisha mwanaume aliyekuwa katika hali ya kutojitambua aanze kutapatapa kutafuta msaada, hatimaye kujikuta amejiburuza na kuelekea nyuma ya mitubwi mibovu iliyokuwa karibu yake.<br />
<br />
“Kama kweli una uhakika basi atakuwepo hapa hapa hebu tufuatilie alama za miburuzo kuangalia ilipoishia.” Aliongea dereva teksi huyo na moja kwa moja wakaanza kuufuatilia miburuzo hiyo.<br />
“Umepita hapa.” Aliongea Oleg Malenko.<br />
Akili ya dereva teksi ilikuwa imefanya kazi sawasawa, ni kweli kabisa alikuwa hawajakosea wazo lake la kufuata miburuzo iliyokuwa ikionekana ardhini lilisaidia na hatua chache tu kutoka mahali waliposimama waliona miguu ya mtu.<br />
“Hii ni miguu ya mtu.”<br />
<br />
“Ni kweli, hebu tuone,” Oleg Malenko aliongea.<br />
Haraka haraka bila kuchelewa wakazunguka na kuanza kumwangalia mtu huyo usoni, alikuwa ni yule yule aliyekuwa amemwacha muda mfupi uliopita, akamgeuza na kumlaza chali mdomoni alionekana kutokwa na mapovu mengi.<br />
“Mh! Yuko hai kweli huyo?” Dereva teksi aliuliza.<br />
“Sijui hata mimi nashangaa, nilipomwacha muda mfupi hakuwa hivi alikuwa amepoteza tu fahamu.”<br />
<br />
“Sasa amefikaje hapa na ni kitu gani kimempata mpaka kufikia hatua hii?”<br />
“Sina jibu ila nisaidie tu tumwondoe hapa.”<br />
“Kwenda wapi, anaonekana tayari ameshakufa huyu.”<br />
Oleg Malenko akainamna na kumshika mwanaume huyo sehemu ya shingo yake kuangalia kama moyo yake yalikuwa yakipiga au la!<br />
“Bado hajafa nasikia mapigo yake yakipiga lakini kwa mbali.”<br />
<br />
“Ushauri wangu ni bora umwache afe tu hapa kwani hakuna mtu atakayegundua.”<br />
“Tafadhali nisaidie hata kama atakufa, basi afie ndani ya nyumba yangu wakati nikijaribu kumsaidia.” Aliongea Oleg Malenko kwa sauti ya upole.<br />
“Sawa nitakusaidia wewe tenga tu fedha yangu.” Aliongea dereva huyo kwa lugha ya Kirusi.<br />
<br />
Wote kwa pamoja wakainamna na kumnyanyua mwanaume aliyekuwa amelala chini na kuanza kutembea kuelekea sehemu walipokuwa wameegesha gari hapo wakamlaza tena chini na dereva kufungua mlango kisha wakamwinua na kumweka kwenye kiti cha nyuma, wote wakaingia ndani ya gari na safari kuelekea nyumbani kwa Oleg Malenko ikaanza, njia nzima alikuwa akimfikiria mgonjwa aliyekuwa naye, alitaka apone ili amsimulie ni kitu gani kilichompata.<br />
<br />
“Naomba Mungu amsaidie asife, apone.” Aliwaza kichwani mwake gari likizidi kuchanja mbuga.<br />
Baada ya mwendo wa nusu saa walishawasili nyumbani kwa Oleg Malenko, yeye akawa mtu wa kwanza kufungua mlango na kushuka bila kusema kitu akamwomba tena dereva wa gari aliyekuja naye amsaidie kumshusha mgonjwa, haraka wakafanya hivyo na kumwingiza mgonjwa ndani ya nyumba.<br />
“Ahsante sana rafiki.” Aliongea Oleg Malenko akimkabidhi dereva huyo kiasi cha fedha kama malipo yake na kumshukuru.<br />
<br />
***<br />
“Ngo!Ngo!Ngo!” Sauti ya mlango ikasikika na kumshtua Lina kutoka katika mawazo aliyokuwa nayo. Haraka bila kuchelewa hata kabla hajaitika akaifungua droo na kuitumbukiza barua hiyo haraka alipohakikisha kwamba alikuwa sawa akamkaribisha mtu aliyekuwa mlangoni.<br />
“Ndiyo karibu.” Aliongea kwa sauti ya upole.<br />
<br />
Mlango ukafunguliwa na mwanaume mmoja akaonekana akiingia.<br />
“Oh! Karibu sana bosi.” Aliongea Lina akionyesha tabasamu usoni mwake.<br />
“Natumaini hujambo, nimekuja kwa jambo moja tu hapa.”<br />
“Ndiyo bosi.”<br />
“Ah! Mwezi ujao kutakuwa na safari ya kwenda Ujerumani na itatuhusisha mimi na wewe ni vyema ukawa na ufahamu na jambo hilo.”<br />
<br />
Badala ya kujibu Lina akainamisha kichwa chake chini, si kwamba hakuifurahia safari hiyo, la hasha! Kichwa chake kilijaa mawazo mengi juu ya ndoa yake na kitu pekee alichokuwa akikihitaji ni kulinda penzi lake kwa Phillip basi.<br />
“Lina!” Sauti ikasikika.<br />
“Bee”<br />
<br />
“Kuna nini kinaendelea kichwani mwako? Hauko sawa kabisa.”<br />
“Hapana bosi niko sawa niko tayari kwa safari hakuna shida.” Alijibu Lina kwa sauti ya chini.<br />
Wakaagana, kisha bosi akafungua mlango na kutoka nje akimwacha Lina ndani ya ofisi peke yake.<br />
<br />
Huku akitetemeka taratibu akanyoosha tena mkono wake na kufungua droo ambayo ndani yake ilikuwepo barua iliyokuwa na maelezo yote jinsi ya kumpata Danniel akaichukua na kuanza kubonyeza.<br />
“Ngrii! Ngrii! Ngriii,”Simu ilikuwa ikiita upande wa pili.</span></div></span></div><span class="fcg"></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465704b044570524420">MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.68<br />
<br />
Tafa…dhali okoa mai…sha yangu si..taki kufa…,” alisema mwanaume huyo akijaribu kunyanyuka kitandani ili aketi lakini zoezi hilo lilionekana kuwa gumu kwake kutokana na jinsi hali yake ilivyokuwa.<br />
Oleg Malenko, huku akitia huruma alimsogelea mwanaume huyo na kuanza kumsaidia ili anyanyuke na kuketi. Zoezi hilo lilipokamilika naye pia akaungana naye kitandani lakini<span class="text_exposed_show"> kabla hajaanza kusema kitu chochote, mwanaume huyo huku akitetemeka aliomba maji ya kunywa.<br />
<br />
“Nisai…die ma…ji ya ku…nywa…,” alisema kwa tabu.<br />
Haraka bila kuchelewa akanyanyuka na kuisogea meza ndogo iliyokuwepo ndani ya chumba kile, akachukua kikombe kikubwa kilichokuwa juu yake ambacho ndani yake kulionekana kuwa na maji.<br />
“Haya hapa.”<br />
<br />
Huku akitetemeka mwanaume huyo akajitahidi kukipeleka kikombe hicho mdomoni na kuanza kunywa maji yaliyokuwemo ndani, haikuchukua hata sekunde tatu, yakawa yamekwisha.<br />
‘Inawezekana ana njaa huyu,’ aliwaza moyoni mwake huku akipokea kikombe na kukiweka mahali pake.<br />
Bila kusema kitu chochote, Oleg Malenko akausogelea mlango na kufungua. Akachungulia na kuita jina la mkewe, bila kuchelewa mkewe alifika, ikasikika sauti ya Oleg Malenko ikimwomba asaidie kupiga uji haraka kisha aulete chumbani mle kwa ajili ya mgonjwa.<br />
<br />
“Kwani ameamka?”<br />
“Ameamka lakini sijaweza kuongea naye, kwa anavyoonekana anahitaji kupata kitu kidogo cha kula.”<br />
“Afadhali! Mungu ni mwema jamani, nilishakata tamaa.”<br />
“Tafadhali nisaidie sasa hivi.”<br />
<br />
“Sawa,” alisema mwanamke huyo na hatua za mtu aliyekuwa akitembea kuondoka eneo hilo zikasikika. Oleg Malenko akarejea ndani ya chumba na kufunga mlango nyuma yake.<br />
“Naweza kukuuliza maswali machache?” alisema huku akisogea karibu kabisa na kitanda alicholala mgonjwa.<br />
Kwa ishara ya kichwa mwanaume huyo akaonesha kukubaliana na jambo alilolisikia kutoka kwa mwenyeji wake.<br />
<br />
“Wewe ni nani vile?” aliuliza tena lengo likiwa ni kupata uhakika wa jina alilolisikia mwanzo.<br />
“Ditrov!” alijibu kwa sauti ya kunong’ona.<br />
”Ah! Kumbe ni sawa kabisa na jina ulilolitamka mwanzo kabla hujapoteza fahamu, pole.”<br />
“Ahsante.”<br />
<br />
“Nini kilitokea mpaka ukawa kwenye hali hii?”<br />
Ditrov bila kujibu kitu chochote aliinamisha kichwa chake chini na kuanza kulia, aliishuhudia picha nzima ya tukio lote alilotendwa na Federov.<br />
“Mbona unalia?”<br />
<br />
“Nisaidie nipone, nitakueleza kila kitu. Ni habari ndefu kidogo lakini yenye machungu mengi,” alisema Ditrov huku akibubujikwa na machozi.<br />
“Nitakusaidia na nina uhakika uta...” alisema Oleg Malenko lakini kabla hajamalizia sentensi yake, mlango wa chumba walichokuwemo ndani yake ukasikika ukigongwa.<br />
“Ngo!Ngo!Ngo.”<br />
<br />
***<br />
Muda mfupi baada ya kukata simu ya Daniel, Lina alinyoosha mkono wake tena na kunyanyua mkono wa simu akaonekana akibonyeza namba kadhaa na kuiweka simu sikioni.<br />
“Hallow,” aliita na bila kuchelewa sauti nzito ikijibu upande wa pili wa simu ikasikika.<br />
“Phillip?” aliuliza.<br />
<br />
“Yes darling.” (Ndio mpenzi) Ilikuwa ni sauti kutoka upande mwingine wa simu.<br />
“Nimempata! Nimefanikiwa kuongea naye na tumekubaliana kukutana leo jioni Lamada Hoteli kwa mazungumzo zaidi,” alisema Lina na muda wote huo tayari machozi yalishalowanisha mashavu yake.<br />
“Lina?” Phillip akiwa upande wa pili wa simu aliita.<br />
<br />
“Be…e” aliitikia kwa sauti ya kutetemeka. Ni sauti hiyo ndiyo iliyomfanya<br />
Phillip ashtuke na kugundua kwamba Lina alikuwa akilia.<br />
“Nakuja hapo sasa hivi,” alisema Phillip na kuikata simu. Bila kuchelewa haraka akanyanyuka kitini na kuufungua mlango wa ofisi yake. Akatoka bila kusema kitu chochote, safari ya kuelekea ofisini kwa Lina ikaanza. Haikumchukua muda, baada ya dakika tatu tu akawa amewasili eneo hilo na kugonga mlango. Aligonga kwa muda lakini hakupata jibu, hatimaye akaamua kuusukuma na kuzama ndani.<br />
<br />
“Lina!” aliita baada ya kutupa macho yake mbele na kumwona Lina akiwa amejiinamia tena akionekana kulia.<br />
“Nini kimetokea tena? Kwa nini unalia?” aliuliza mfululizo.<br />
Akiwa hapo akamshuhudia Lina akinyanyuka na kumsogelea kisha kumkumbatia.<br />
<br />
“Phillip ninakwenda kufanya jambo ulilohitaji ili kulinda ndoa yetu, siko tayari kukupoteza mume wangu, naamini wewe ni wangu mpaka kifo… lakini ukweli kutoka ndani ya moyo wangu nasikia moto ukiwaka na kunipa maumivu makali. Nashindwa kuelewa ni kwa nini…” alisema Lina na kabla hajafika mwisho wa sentensi yake wakasikia hatua za mtu akisogea karibu kabisa na mlango wa ofisi ya Lina.<br />
<br />
Haraka Lina akamwachia Phillip na kujifuta machozi kisha kuzunguka upande wa pili ambako alikivuta kiti chake na kuketi. Hawakukosea, hatua walizozisikia zilikielekea eneo hilo zilikuwa ni za bosi wake Lina ambaye aliondoka hapo muda mfupi uliopita.<br />
Akabisha mlango na kukaribishwa kuingia ndani. Naye alishangazwa na hali aliyomwona nayo Lina.<br />
“Lina nini kimetokea? Unaumwa?” aliuliza kwa sauti ya upole.<br />
<br />
“Hajisikii vizuri ndiyo maana na mimi niko hapa, nataka kumpeleka hospitali,” Phillip alidakia.<br />
“Basi ni vyema ukafanya hivyo, nitaongea naye kesho kwani nilikuwa na habari njema za kumpa,” alisema bosi huyo na kutoka huku akifunga mlango nyuma yake.<br />
<br />
Alipotoka, kwa haraka Phillip akanyanyuka kitini na kumsaidia Lina kuweka ofisi katika hali ya usafi. Mambo yalipokamilika akamwomba amsaidie kubeba mkoba wake, wakatoka ofisini na kuelekea sehemu ambako waliegesha gari lao, wakapanda na kuondoka eneo lile.<br />
Njia nzima Lina alikuwa akilia. Hakuweza kuvumilia, mara kadhaa alimuuliza Phillip maswali na kujibiwa lakini hakuwa tayari kukubaliana na majibu hayo.<br />
<br />
“Sikia mke wangu, nakupenda sana na ili kukuhakikishia nitakupeleka mwenyewe mpaka hotelini na mimi nitakusubiri mpaka mwisho, umenielewa?” aliuliza Phillip akimpigapiga Lina mgongoni.<br />
“Fyuuu!” badala ya kujibu Lina akashusha pumzi.<br />
<br />
Phillip akazidi kukanyaga mafuta na nusu saa baadaye tayari walishafika nyumbani hapo wakashuka na kuingia ndani. Kwa muda wote huo, Lina alikuwa kimya kabisa, hakusema kitu chochote. Phillip akamshika mkono na wote kwa pamoja wakaingia chumbani, hawakutoka tena mpaka saa tano baadaye, wote wawili wakiwa wamevalia vizuri.<br />
<br />
Walitoka nje ya nyumba yao na kuingia tena ndani ya gari, safari kuelekea hotelini Lamada ikaanza. Njia nzima Phillip alijaribu kuongea na Lina akimsihi na kumbembeleza kuondokana na wasiwasi aliokuwa nao.<br />
“Lina tunaingia hotelini sasa, tafadhali hebu jifute machozi, nisingependa jambo hili ligundulike na watu wengi.”<br />
“Siwezi mume wangu, moyo unaniuma sana. Phillip unanifanya nianze kujilaumu ni kwa nini nilikubali kuolewa na wewe, hivi kweli umedhamiria?” aliuliza Lina.<br />
<br />
“Fanya kwa ajili yangu Lina nakuahidi kukupenda mpaka mwisho. Nitakaa hapa hapa nilipokushusha, ukitoka utanikuta nakusubiri, sawa mke wangu?” alisema Phillip huku akimbusu mfululizo.<br />
Taratibu Lina akashuka kwenye gari na kujiweka sawa kisha kumwangalia Phillip kwa macho ya huruma. Bila kusema kitu chochote akaanza kutembea kuondoka eneo hilo.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Lina ndiye huyo ameingia hotelini Lamada kwenda kukutana na Daniel. Nini kitatokea huko? Ditrov naye fahamu zake zimemrejea lakini bado yu katika hali mbaya. Nini hatima yake?</span></div></span></div><span class="fcg"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501246570408e3d88982782">MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.70<br />
<br />
JAMANI EPISODE ZIMEJICHANGANYA SANA, POLENI<br />
<br />
NDANI ya chumba wanaongea mengi juu ya maisha na jinsi walivyokuwa wamepotezana kwa muda mrefu. Daniel anasisitiza kwamba bado anampenda Lina pamoja na mambo yote yaliyotokea maishani mwao. Muda wote huo Lina alikuwa akibubujikwa na machozi, mara kadhaa taswira ya mume wake Phillip ilimjia kichwani mwake na sauti ikamsis<span class="text_exposed_show">itiza juu ya kuhakikisha anafanya tendo la ndoa ili hatimaye apate ujauzito.<br />
<br />
Ni mambo hayo ndiyo yaliyomfanya Lina azidi kulia, kitu ambacho kilimshangaza sana Daniel. Alitumia muda mwingi kumbembeleza Lina ili anyamaze lakini ilionekana kuwa ngumu.<br />
<br />
Kwa muda wa saa zima walikuwa chumbani, kazi ikiwa moja tu ya kumbembeleza Lina ili anyamaze ndiyo waendelee na mambo mengine. Hata alipopewa chakula alikataa bila kusema sababu, hatimaye Daniel uvumilivu nao unamshinda. Uchu wa kufanya tendo la ndoa na Lina unamkamata, anaona huo ndiyo muda muafaka kwake.<br />
<br />
Taratibu bila kusema kitu chochote baada ya kuwa ameshambembeleza kwa muda mrefu, anasogea karibu na Lina kisha anamnyanyua na kumlaza kitandani huku akimpiga mabusu mfululizo.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
HALI ya Ditrov ilikuwa ikiendelea vyema, akipata kila aina ya msaada kutoka kwa Oleg Malenko. Jeraha lake lilishapata nafuu kubwa na mwili wake ulionekana kurejea katika hali yake ya kawaida. Pamoja na yote hayo bado hakuwa tayari kueleza ukweli kwamba alitokea wapi na ni kitu gani kilisababisha akatoswa baharini.<br />
<br />
“Nashukuru Mungu unaendelea vizuri, nadhani sasa tunaweza kuongea kidogo kuhusu wewe,” Oleg Malenko alisema.<br />
“Sipo tayari kueleza chochote, kikubwa ninachokuomba ndugu yangu unitunzie siri ya mimi kuwepo hapa katika nyumba yako. Muda si mrefu nitaondoka ili kukuepushia matatizo.”<br />
<br />
“Matatizo yapi?”<br />
“Ni historia ndefu sana kuhusu mkasa ulionipata. Ninachokushukuru sana ni kuokoa maisha yangu.”<br />
“Hakuna shida,” alisema Oleg lakini tayari kichwani mwake alishaweka viulizo ni kwa nini mtu aliyekuwa ndani ya nyumba yake hakutaka kueleza ukweli wa nini kilichompata na zaidi ya yote alitaka jambo hilo lifanywe siri.<br />
<br />
Hivyo ndivyo maisha yalivyokwenda, Ditrov akawa ni mtu wa ndani muda wote akihitaji kubaki peke yake, jambo ambalo lilizidi kuitia shaka familia ya Oleg Malenko. Wiki ya kwanza ikakatika, hali yake ikazidi kuwa imara na wiki ya pili ilipofika katikati akaamua kuvunja ukimya. Alimwita Oleg Malenko ili waongee.<br />
<br />
“Hivi sasa wewe ni kama ndugu yangu kwani umeokoa maisha yangu. Nakushukuru sana lakini naomba msaada mmoja tu kutoka kwako.”<br />
“Sema tu ndugu yangu nitakusaidia.”<br />
“Nahitaji fedha kidogo kwa ajili ya nauli.”<br />
<br />
“Kwenda wapi?”<br />
“Nataka kurejea nyumbani,” alidanganya.<br />
“Hakuna shida, nipo tayari kukusaidia. Sijui unahitaji lini?”<br />
“Ikiwezekana kesho asubuhi ili niondoke hapa,” alisema Ditrov akionesha shaka machoni mwake.<br />
<br />
***<br />
“Nakupenda mpenzi wangu, ni muda mrefu nimengoja jambo hili litokee hatimaye leo hii limewadia. Nieleze ni kitu gani kimesababisha unitafute Lina, huu kwangu ni muujiza,” alisema Daniel akizidi kumwagia Lina mabusu mfululizo.<br />
“Mh!” Aliguna huku kwikwi ya kulia ikizidi kumkaba.<br />
“Lina,” Daniel aliita.<br />
<br />
“Tafadhali toa ushirikiano, kwa nini unalia?”<br />
“Hakuna kitu, nipo sawa.”<br />
“Si kweli! Kama upo sawa hayo machozi ni ya nini sasa?”<br />
“Una…ju…a nini?”<br />
<br />
Daniel akatulia kidogo ili asikilize ni kitu gani Lina alitaka kumweleza.<br />
“Nimefurahi kukutana na wewe Daniel, ni muda mrefu umepita eeh?” Aliuliza Lina akimpigapiga Daniel mgongoni. Mawazo na akili zake zote hazikuwa ndani ya chumba hicho, mara kadhaa taswira ya mumewe Phillip ilimjia kichwani mwake na hiyo ndiyo iliyomfanya abubujikwe na machozi muda wote.<br />
<br />
***<br />
Nje ya hoteli, Phillip bado aliendelea kubaki hapo akimsubiri mkewe Lina, mapigo yake ya moyo yalikwenda mbio hakuelewa ni kitu gani kingekuwa kimetokea ndani ya chumba kwani tangu mwanzo Lina alishaonesha dalili kwamba hakupenda kufanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine isipokuwa yeye tu.<br />
<br />
“Atakuwa amefanikiwa, ni muda mrefu tangu aingie huko,” aliwaza Phillip.<br />
Akaendelea kujiambia mwenyewe kwamba kusingekuwa na tatizo lolote, akatupa macho yake kwenye saa yake ya mkononi na kugundua kuwa tayari ilishatimu saa tatu na nusu za usiku. Mpaka wakati huo hakuwa na taarifa yoyote ya Lina.<br />
<br />
“Akichelewa zaidi nitampigia simu,” aliwaza Phillip akitoka ndani ya gari na kutembeatembea kulizunguka gari lake. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda kasi kwani hakufikiria kwamba Lina angechukua muda mrefu kiasi kile.<br />
<br />
***<br />
Ndani ya chumba, Daniel aliendelea kuongea mambo mengi juu ya maisha yake baada ya kuachana na Lina. Aliweka wazi zaidi na kumweleza kwamba tayari alishaoa na alikuwa na mtoto mmoja lakini akajiapiza kutoka ndani ya moyo wake kwamba alilazimika kuoa kwani umri ulikuwa ukienda. Akamwambia hakuwahi kumpenda mwanamke mwingine kama ilivyotokea kwa Lina.<br />
“Daniel unasema kweli?”<br />
<br />
“Huo ndiyo ukweli wangu, hutaniamini lakini…”<br />
“Usiseme hivyo bwana.”<br />
“Lina ukweli nilikupenda na nitaendelea kukupenda maisha yangu yote, hapa nilipo nahisi nipo ndotoni pengine nitaaamka muda si mrefu.”<br />
<br />
“Daniel uko na mimi wala si ndoto.”<br />
“Umefikiria nini mpaka kuamua kunitafuta Lina?”<br />
“Maisha yamesababisha hivyo, wahenga walisema milima haikutani lakini binadamu tunakutana, ndiyo kama hivi.”<br />
“Ahsante kwa kunikumbuka na kuniingiza tena ndani ya moyo wako.”<br />
<br />
Ukimya wa ajabu ukatokea kati yao, ghafla Daniel akaanza kumpapasa Lina sehemu mbalimbali za mwili wake huku akimpa maneno matamu yaliyoambatana na mabusu.<br />
“Leo sitarudi nyumbani, nitalala hapa na wewe. Nataka nikuoneshe ni jinsi gani ninavyokupenda Lina. Nataka ujue kwamba mimi ndiye Daniel wa ukweli, niambie unataka nifanye nini?” alisema Daniel huku akizidi kumpapasa mwilini.<br />
<br />
Tayari hamu ya mapenzi ilishawaingia, kila mmoja alikuwa akihemka, si Daniel wala Lina wote walikuwa taabani.<br />
“I lov..e yo…u ba…by...”(Nakupenda mpenzi) ilikuwa ni sauti nzito ya Daniel ambayo ilipenya na kwenda moja kwa moja kwenye sikio la Lina aliyekuwa amelala kimya bila kusema kitu chochote. Bila kupata kibali chochote kutoka kwa Lina, Daniel akaanza kumvua viatu na kuvitupa chini, taratibu akapanda juu na kuanza kumfungua vishikizo vya blauzi aliyokuwa amevaa.<br />
<br />
“Leo ndiyo leo nataka kuweka historia ya mapenzi kwako,” alisema Daniel. Tayari macho yake yalishabadilika rangi na kuwa mekundu.<br />
“Daniel!” Lina aliita.<br />
“Yes baby.”<br />
“Twende taratibu, usiwe na haraka.”<br />
<br />
“Nashindwa kuvumilia, nilikusubiri kwa muda mrefu.”<br />
“Hapana,” alisema Lina akijaribu kuitoa mikono ya Daniel kifuani kwake.<br />
“Basi naomba nitoe tu hii halafu...” alisema Daniel tayari alishamaliza vishikizo vyote vya blauzi.<br />
<br />
“Oh! My God!”(Oh! Mungu wangu!) alisema kimoyomoyo, hakuwa tayari kuamini alichokishuhudia juu ya kifua cha Lina. Chuchu ndogo zilizosimama vizuri zilizidi kumpagawisha Daniel, akawa anapumua kwa kasi kubwa.<br />
Je, nini kitaendelea?</span></div></span></div><span class="fcg"></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124657036805148396469">MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.72<br />
<br />
DITROV amepata nafuu na sasa ameomba msaada kutoka kwa Oleg Malenko ili aondoke sehemu hiyo mara moja na bila kujiuliza kwa kina Oleg anaahidi kumpa msaada huo ingawa hajui anataka kuelekea wapi.<br />
<br />
Upande wa pili, Lina na Daniel tayari wapo juu ya kitanda. Daniel anaonekana kuwa na hali mbaya zaidi kwani ana hamu kubwa ya kufanya tendo la ndoa na Lina, mwanamke ali<span class="text_exposed_show">yempenda kwa moyo wake wote lakini akashindwa kulifaidi penzi lake baada ya kumkataa. Nafasi ile ya kuwa wawili tu na Lina chumbani aliiona kama bahati ya mtende kuota jangwani, akazidi kuchanganyikiwa kwani alikuwa akilihitaji mno penzi lake.<br />
<br />
Baada ya mazungumzo marefu, akitumia muda mwingi kumbembeleza Lina aliyekuwa akilia, hatimaye Daniel anafanikiwa kufungua vishikizo vya blauzi ya Lina na kuziona chuchu ndogo zikiwa zimesimama kifuani. Kitendo kile kilifanya hamu yake ya kufanya mapenzi izidi kupamba moto, bila kusema kitu akaruka kutoka kitandani na kuanza kuchojoa nguo moja baada ya nyingine huku mhemko ndani yake ukizidi kuongezeka kadiri saa zilivyokuwa zinazidi kusonga mbele.<br />
<br />
Bila kusema kitu chochote, anarejea tena kitandani na kulala huku mikono yake ikizunguka juu ya mwili wa Lina ambaye alitulia kimya kitandani, wakiwa hapo mabusu ya mahaba yanamiminika mfululizo juu ya mwili wa Lina.<br />
<br />
Nje ya hoteli, uvumilivu umeanza kumshinda Phillip kwani ameshasubiri kwa muda mrefu bila kumwona mkewe akitoka, akaanza kuhisi huenda kuna kitu kibaya kimempata. Anajiambia moyoni kuwa aendelee kusubiri kidogo na kama hatatokea basi ataingia ndani ya hoteli kumtafuta.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
“Mbona anazidi kuchelewa? Au kapatwa na tatizo kubwa? Nahisi hayupo sawa, kwa nini harejei?” Phillip alijiuliza maswali mengi ambayo hayakuwa na majibu. Alikuwa akizungukazunguka pale nje kama mtu aliyepoteza kitu. Mara kwa mara alikuwa akiingia ndani ya gari na kushuka, akiwa haelewi nini anachokitafuta. Akili yake ilikuwa haitulii kabisa. <br />
<br />
Wivu na hofu vilikuwa vikimshambulia kwa wakati mmoja. Kuna wakati alihisi huenda Lina amenogewa na penzi alilopewa na mwanaume aliyeenda kukutana naye kiasi cha kujisahau. Akili nyingine ilimtuma kuwa huenda ameamua kuondoka na huyo mwanaume ingawa alishindwa kuelewa wamepitia wapi kwani muda wote yeye alikuwa pale nje.<br />
Hofu nayo haikumuacha, alihisi huenda amekumbana na kitu kibaya ambacho kimemdhuru na ndiyo maana hatoki mapema kama walivyokubaliana. <br />
<br />
Mambo yote yalikuwa yakipita akilini mwake kama mkanda wa sinema. Japokuwa ni yeye ndiye aliyetoa wazo lile, kwa upande mwingine alijikuta akijutia uamuzi wake lakini kwa kuwa alikuwa na shida ya mtoto, ilibidi avumilie.<br />
<br />
Phillip aliendelea kujizungusha huku na kule huku akiangalia saa yake karibu kila baada ya dakika moja. Aliona muda unaenda taratibu sana, akatamani angekuwa na nguvu za ziada za kuweza kuona kilichokuwa kinaendelea kwa Lina.<br />
“Zikipita dakika kumi kama bado hajatoka, itabidi niende mapokezi kuuliza, ikishindikana nitaenda mpaka kwenye chumba alichoingia,” alisema Phillip huku kichwa chake kikichemka kwa mawazo.<br />
<br />
Muda ulizidi kuyoyoma bila Lina kutoka, hali iliyozidi kumuweka Phillip kwenye wakati mgumu. Aliendelea kuhesabu sekunde, dakika na saa hatimaye uvumilivu ukamshinda. Kijasho chembamba kilikuwa kikimtiririka, akafunga mlango wa gari na kuanza kupiga hatua za taratibu kuelekea mapokezi huku akiendelea kujiuliza maswali mengi ambayo yote yalikosa majibu.<br />
***<br />
Baada ya kupata nafuu kwa msaada mkubwa wa Oleg Malenko, Ditrov alijiandaa kuondoka huku mawazo mengi yakipita ndani ya kichwa chake. Mazingira yaliyomfanya akaokolewa na Oleg Malenko yalimfanya atambue kuwa Mungu yupo kwani alishakata tamaa ya kuendelea kuishi. Alikuwa akijiuliza mara kwa mara kwamba alimkosea nini bosi wake, Victor Federov mpaka kufikia hatua ya kumpiga risasi na kwenda kumtosa baharini, tena akiwa amefungwa na jiwe kubwa shingoni.<br />
<br />
Kila alipokuwa anakumbuka jinsi alivyonusurika kufa, mwili wote ulikuwa ukimsisimka. Baada ya kuagana na mwenyeji wake pamoja na familia yake, Ditrov alianza safari ya kuondoka ndani ya nyumba ya Oleg Malenko, akiwa haelewi anaelekea wapi. Alitembea taratibu mpaka alipotoka nje, akageuka nyuma na kuwapungia mkono Oleg Malenko na familia yake kwa ishara ya kuwaaga.<br />
<br />
Wakamsindikiza kwa macho mpaka alipopotea kwenye upeo wa macho yao. Alikuwa anatembea huku kichwa chake amekiinamisha chini akiwa hataki mtu yeyote amtambue. Alikuwa akikwepa macho ya watu kwani aliamini wengi wao walikuwa wanamfahamu.<br />
“Mimi ni mwanaume bwana! Kama Mungu amenisimamia nimenusurika na mauti, hawezi kushindwa kuniongoza mahali pa kwenda wakati najiandaa kulipa kisasi.<br />
<br />
Nitatafuta sehemu yoyote ambapo nitajihifadhi wakati nafikiria jinsi ya kurudi kulipa kisasi, lazima nimfunze adabu Victor Federov. Tena kazi itakuwa rahisi kwani anaamini nimeshakufa, hajui kuwa Mungu ambaye nilishaacha hata kumuabudu miaka mingi iliyopita amenipigania na naendelea kupumua,” alisema Ditrov wakati akizidi kuchanja mbuga kuelekea mahali asikokujua.<br />
<br />
Kumbukumbu za kuhuzunisha ziliendelea kuzunguka ndani ya kichwa chake, akajikuta akishindwa kuyazuia machozi kumtoka, hasa alipokumbuka maisha aliyokuwa anaishi kabla ya kutokewa na balaa lile na kuponea chupuchupu kufa.<br />
Taswira ya maisha aliyokuwa anaishi, japokuwa yalikuwa yanategemea kufanya shughuli haramu mara chache, ilikuwa ikipita akilini mwake na kumfanya ashindwe kukubaliana na hali halisi.<br />
<br />
Maisha mazuri aliyoishi, tena ya kifahari yalimfanya asiamini kuwa wakati ule alikuwa akitangatanga mahali asipopajua na kuishi kama mkimbizi. Maisha ya kujificha kama digidigi hakuyazoea lakini sasa ndiyo alitakiwa ayaishi wakati anajiandaa kulipa kisasi akikwepa kugundulika kabla hajatimiza alichokipanga.<br />
<br />
Alitembea kwa muda mrefu mpaka akaanza kuhisi uchovu. Ukizingatia kuwa afya yake ilikuwa bado haijatengamaa, nguvu zilimwisha kirahisi. Akaamua kutafuta mahali pa kupumzika huku akiendelea kujiuliza kichwani mwake ni wapi angekwenda na kupata fedha za kumsaidia kukimu shida zake mbele ya safari. Alipiga moyo konde na kuamini kuwa hakuna linaloshindikana chini ya jua.<br />
<br />
“Najua nitapata shida sana lakini haya yote yatapita. Nitaanzia chini kabisa lakini naamini ipo siku nitapata fedha ambazo zitanifanya nirudi tena kwenye daraja la maisha ya kifahari kama ilivyokuwa mwanzo, nikila na kunywa hadi kusaza,” alijisemea Ditrov wakati akiinuka na kuendelea na safari yake baada ya kupumzika kwa muda.<br />
Kichwani mwake hakuwa na ramani ya mahali anapokwenda lakini aliamini atafika tu mahali palipotulia ambapo ndipo yatakapokuwa makazi yake ya muda wakati akijiandaa kulipa kisasi.<br />
<br />
***<br />
“Lina,” Daniel aliita.<br />
“Abee,” aliitikia kwa sauti ya chini.<br />
“Kweli unanipenda?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Kama kweli unanipenda tafadhali niache niwe huru juu ya mwili wako. Naomba unipe nafasi ya mimi kufanya ninachotaka, usinishike mikono na kunizuia, niache nifurahie mapenzi yako,” alisema Daniel kwa sauti ya kubembeleza kuonesha kuwa hamu yake ilikuwa imefika juu kabisa.<br />
Lina hakuwa mwepesi wa kukubali Daniel afanye kila alichokitaka kwenye mwili wake. Mara kwa mara alikuwa akiushika mkono wake na kumzuia kumpapasa maungoni mwake, jambo ambalo lilizidi kumpa Daniel wakati mgumu.<br />
<br />
“Yaani shida ya mtoto ndiyo inifanye nifanye jambo nisilolitaka, roho inaniuma sana,” alijisemea kimoyomoyo Lina huku dhamira yake ikigoma kabisa kumruhusu Daniel afaidi penzi lake. Daniel hakukata tamaa, aliendelea kumbembeleza Lina kwa maneno matamu huku akitumia ujanja kuupapasa mwili wake.<br />
<br />
Cha ajabu, kwa muda wote huo Lina alikuwa akibubujikwa na machozi kama yupo msibani, jambo lililomfanaya Daniel abaki njia panda. Alijiuliza kwa nini Lina analia kiasi kile wakati ni yeye ndiye aliyempigia simu na wakakubaliana kukutana pale.<br />
“Lina mpenzi wangu, naomba nipe haki yangu tafadhali, nionee huruma mwenzio nateseka,” Daniel alisema kwa sauti iliyokuwa inatetemeka baada ya kuzidiwa na haja ya mwili wake kulifurahia penzi la Lina.<br />
<br />
Alipoona hamjibu kitu bali anaendelea kulia, aliinuka kidogo na kujaribu kuivua sketi fupi aliyokuwa ameivaa Lina. Lina alishtuka na kuanza kumzuia, wakawa wanavutana pale kitandani.<br />
“Usitumie nguvu Daniel, niache nitavua mwenyewe,” alijitetea Lina lakini Daniel hakutaka kumuelewa. Akaikamata vizuri na kuivua kwa nguvu, Lina akabakia na nguo ya ndani pekee.<br />
<br />
“Duu! Leo sijui itakuwaje, si mchezo,” Daniel alijisemea kimoyomoyo wakati akimuangalia Lina aliyekuwa amebakiwa na ‘kufuli’ nyeupe iliyozidi kupandisha mashetani ya Daniel.<br />
“Nipe nafasi mpenzi wangu, mwenyewe utafurahi,” alisema Daniel huku akipeleka mikono yake kujaribu kulitoa kufuli la Lina.<br />
“Subiri Daniel, nitakupa nafasi lakini usiwe na papara, subiri kidogo,” alijitetea Lina huku akibana miguu yake na kumzuia Daniel.<br />
<br />
“Hakuna shida, nitasubiri hata ukisema mpaka usiku wa manane. Nakuhakikishia kuwa shughuli nitakayokupa leo, mwenyewe utanitafuta tena.”<br />
<br />
Lina alifumba macho na kumruhusu Daniel apitishe mikono yake kiunoni, akawa anampapasa kimahaba huku akimpiga mabusu mwili mzima. Alipoona Lina amejisahau, alishika pindo za kufuli lake na kuanza kuliteremsha kwa kushtukiza. Lina aliwahi kumzuia, lakini likiwa tayari limeshashuka mpaka karibu na magoti. Daniel aliendelea kusumbuana naye, hatimaye akafanikiwa na wote wakabaki kama walivyoletwa duniani.<br />
Je, nini kitaendelea?</span></div></span></div><span class="fcg"></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465702b273783396672">MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.73<br />
<br />
Uwiii!” Daniel alisema kimoyomoyo, macho yake hayakuwa tayari kuamini kile alichokuwa akikishuhudia mbele ya macho yake, uzuri wa Lina haukuwa na maelezo, akili ya Daniel ikazidi kuchanganyika zaidi aliposhusha macho yake na kuangalia mapaja ya Lina.<br />
“Mungu wangu! Ninaota au?” alijiuliza.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Huoti Daniel unachokiona ndicho.”<br />
“Lina!”<br />
“Yes.”<br />
“Hakika wewe ni mwanamke mrembo,” aliongea Daniel na tayari mikono yake ilikuwa ikipita huku na kule juu ya mapaja ya Lina huku akihemuka, akimeza mate mfululizo.<br />
Akamnyanyua Lina na kumlaza kifudifudi mikono yake yote miwili ikiendelea kucheza juu ya mwili wake laini.<br />
<br />
“Hakika wewe ni mwanamke mtamu.”<br />
“Whaaat?” (Nini?)<br />
“Naaminisha wewe ni mzuri sana.”<br />
“Kama wewe Danny.”<br />
<br />
“Sidhani,” alisema akishusha mdomo wake na kuanza kumng’ata ng’ata Lina jambo hilo likazidi kuwasha moto zaidi kwa Lina.<br />
“Mh! Mh! Baby, taratibu usiwe na shaka leo ni siku yako.”<br />
“Nahisi kuchelewa Lina tafadhali nipe.”<br />
“Ah! tucheze kwanza kidogo muda ukifika nitakupa.”<br />
“Shiiii! Mh! Uwiii! Yalaaa!” alilalama Daniel.<br />
<br />
Kwa muda wa saa mbili mfululizo waliendelea kucheza juu ya kitanda huku kila mmoja akionekana kukolezwa na mwenzake, mara kadhaa Daniel alimgeuza Lina akijaribu kumlaza chali lakini Lina alikataa akimweleza wazi kwamba muda muafaka ulikuwa bado haujafika.<br />
Kwa kuwaangalia wote wawili walikuwa hoi kwa mapenzi kila mmoja akiguna na kuongea maneno yake huku wakiendelea kushikana hapa na pale.<br />
<br />
“Lina inatosha tafadhali ni…pe,” aliongea Daniel lakini hakumaliza sentensi yake tayari mdomo wake ukafunikwa na kiganja cha Lina.<br />
“Shiii! Hebu jikaze bwa....” aliongea Lina lakini naye alionekana kuwa hoi kupita kawaida.<br />
Kwa sauti ya upole huku akionyesha tabasamu akamwomba Daniel naye alale ili aweze kumfanyia alichotaka kufanya, bila hiyana taratibu mwanaume akashuka kitandani na kulala akimpa Lina nafasi ya kufanya alichokusudia<br />
“Mh!Mh!Mhhhhh” ilikuwa ni miguno kutoka kwa Daniel.<br />
<br />
“Vipi?” Lina aliuliza.<br />
“Imetosha, naomba unipe ki…do..go,” aliongea.<br />
“Niachie nafasi kidogo nikupe raha Daniel ambayo nina hakika hutaisahau maishani mwako.”<br />
Ulimi wa Lina ulikuwa ukipita ndani ya sikio la Daniel.<br />
<br />
Ni tukio hilo ndilo lililofamfanya Daniel akajikunja kitandani kama jogoo, raha aliyokuwa ameisikia ilikuwa haielezeki hata kidogo, ni kweli alishakutana na wanawake wengi maishani mwake lakini kwa Lina ilionekana kuwa kiboko.<br />
“Lina niko tayari kuachana na mke wangu nikuoe wewe, unasemaje?”<br />
“Danny! Hebu acha utani unamaanisha unachokisema?”<br />
<br />
“Niko tayari hakika sitanii.”<br />
“Unaweza kumwacha sasa hivi tena kwa kumpigia simu?”<br />
“Haijalishi.”<br />
Daniel alikuwa amechanganyikiwa kabisa, akili zake ziligeuka na alikuwa tayari kufanya kila kitu ambacho Lina angemwambia ili mradi tu aendelee kupata raha aliyokuwa anaipata siku hiyo, kichwani mwake akisahau kabisa kwamba alikuwa ni baba wa watoto wawili waliomtegemea kwa kila kitu duniani.<br />
<br />
***<br />
Akiwa ndani ya gari lake usingizini, ubaridi mkali wa kiyoyozi ndiyo uliomshitua na kumfanya afungue macho na kuangaza huku na kule ndani ya gari na kugundua kwamba alikuwa peke yake bado, haraka akanyoosha mkono wake na kuwasha redio ndani ya gari na sauti ikasikika ikitangaza kwamba muda huo ndiyo ilikuwa ikitimu saa sita kamili usiku.<br />
<br />
“Mungu wangu mpaka saa hizi? Amepatwa na kitu gani huyu mwanamke?”<br />
aliongea Phillip akishuka ndani ya gari.<br />
Akiwa hapo akaangaza huku na kule bila kuona kitu chochote, taratibu akazima gari na kuchomoa funguo kisha kufunga mlango.<br />
<br />
“Lina amenisaliti hawezi kukaa ndani ya hoteli kwa muda mrefu kiasi hicho mkataba wangu mimi na yeye ni kuhakikisha anakutana na mwanaume huyo na kufanya naye tendo la ndoa baada ya hapo basi atoke na tuondoke, kwa nini amechukua muda mrefu kiasi hiki? Inawezekana amepewa mambo mazuri mpaka amenisahau?” aliongea Phillip akionyesha hasira nyingi.<br />
<br />
Hofu ilishaugubika moyo wake, akiwa haelewi ni kitu gani angekwenda kushuhudia huko, Phillip alianza kutembea kichwani mwake akijiuliza maswali mengi na mara kadhaa akianza kujilaumu kwa kitendo chake cha kumshawishi mkewe kwenda kukutana na mwanaume mwingine ili tu wafanye tendo la ndoa na kupata ujauzito ambao angeulea na kuutunza mpaka mtoto atakapozaliwa. Moyo wake ukauma.<br />
“Hivi kweli anaweza kuwa ameondoka na kuniacha mimi nikiwa hapa? Lina, sidhani lakini akili za mwanamke anazijua mwenyewe pengine ameamua kufanya kweli ili kunikomoa kwani hakuwa tayari kufanya jambo hilo, mimi ndiye nimemlazimisha.”<br />
<br />
Lawama nyingi akazielekeza kwake na kujiona ni mwanaume mjinga kiasi gani kwa kitendo cha kuruhusu mkewe kwenda kufanya ngono na mwanaume mwingine, hakika alifahamu wazi kwamba kama dunia ingefahamu jambo hilo basi ingekuwa ni aibu mpaka siku anaingia kaburini.<br />
<br />
Huku akiwa na wasiwasi mwingi moyoni mwake taratibu akaanza kutembea, lengo lake likiwa kuelekea eneo la mapokezi ambako angeingia na kuuliza.<br />
“Najua nitakutana na maswali mengi sana hasa ukizingatia kwamba ni usiku<br />
mkubwa lakini nitajibu moja baada ya jingine nikijifanya mimi ni dereva wake niliyekuwa nikimsubiri hapo nje,” aliendelea kuwaza akitembea taratibu.</span></div></span><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"><br />
</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501246570238f0581464386">MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.74<br />
<br />
Kwa fedha kidogo alizokuwa nazo, akiwa haelewi kabisa nini ingekuwa hatima ya safari yake hiyo, Ditrov alijipa moyo na kujiapiza kwamba ni lazima angefanya kila kinachowezekana kusukuma maisha yake kwenda mbele lakini zaidi ya yote akili yake ilifikiria juu ya kulipa kisasi kwa Victor Fedorov. Alijiapiza kuwa hata kama ingechukua miaka mingapi ni lazima jambo hil<span class="text_exposed_show">o litokee, hakufahamu lingetokea vipi lakini aliamini hivyo.<br />
<br />
Hasira ya maisha mapya ilikuwa imemkaa Ditrov kupita maelezo, alitaka kurejea kwenye hali yake ya awali na kuwa Ditrov yuleyule wa zamani, bila mtu yeyote kufahamu kwamba hakufa. Alipanga kujichimbia mahali na kuishi kwa siri kubwa akitafuta mbinu za kulipa kisasi kwa mtu aliyeamini kwamba alikuwa ni adui yake.<br />
<br />
“Yupo mtu mmoja tu nchini Urusi anayeweza kufanya kazi ninayotaka afanye. Nikitulia kidogo nitamfuta,” aliwaza siku moja akiwa ndani ya chumba chake kidogo kilichokuwa nje kabisa ya mji.<br />
<br />
Kwa muda wa wiki mbili mfululizo aliendelea kutafakari juu ya nani angeweza kufanya zoezi ambalo alilihitaji, hatimaye kumbukumbu zake zikamrejesha moja kwa moja kwa kijana mmoja aliyeishi nchini Urusi ambaye aliamini kabisa kwamba angeweza kufanya kile alichokitaka.<br />
<br />
Baada ya kuchunguza kwa muda mrefu, alimkumbuka kijana mmoja katili ambaye aliamini kabisa angeweza kufanya kazi ngumu iliyokuwa mbele yake. Mara kadhaa alikumbuka matukio ya kutisha ambayo aliwahi kufanya kipindi cha nyuma.<br />
“Nitampa kazi hii lakini sitaki afanye mauaji yoyote, kama ni kisasi nitalipa mimi mwenyewe,” aliwaza Ditrov.<br />
<br />
Kazi yake ikabaki kuwa moja tu, kutafuta simu ambayo angeitumia kuwasiliana na kijana huyo ili ampe kazi hiyo mara moja.<br />
“Kesho nitahakikisha napata simu kwa ajili ya mawasiliano,” alisema Ditrov akijaribu kuzungusha akili yake huku na kule. Akiwa hapo akaingiza mkono katika moja ya mfuko wake wa suruali akijaribu kukagua kama angepata akiba yoyote ambayo ingeweza kumsaidia kupiga simu.<br />
<br />
“Yes, hii itatosha kwa kazi hiyo,” alisema huku akitoka ndani. Nyumba aliyokuwa anaishi ilikuwa ndogo na iliyochakaa kupita kawaida. Hapakuwa na jirani yeyote maeneo hayo na ilivyoonekana, nyumba ile ilikuwa imetelekezwa kwa muda mrefu. Hapo ndipo Ditrov alipoweka makazi yake, akiishi peke yake.<br />
<br />
Licha ya mvua kubwa iliyokuwa inanyesha, Ditrov aliamua kutoka ili kwenda kutafuta mahali ambapo angepata simu na kupiga nchini Urusi ili aweze kuongea na mtu ambaye aliamini angemsaidia shida yake. Taratibu akatoka na kuanza kutembea, kichwani mwake akiwaza mambo mengi huku akitupa lawama nyingi kwa Victor Fedorov kwamba bila yeye maisha yake yasingekuwa kama yalivyo. Alipofikiria hivyo, moyo wake ukazidi kumuuma.<br />
<br />
“Mimi ni mwanaume, naamini nitashinda hata kama gharama yake itakuwa kubwa kiasi gani, lazima nishinde tu,” alisema huku akitokomea kwenda mbele.<br />
Kwa muda wa saa nzima Ditrov alitembea bila kukutana na mtu yeyote zaidi ya magari machache yaliyoonekana kupita eneo hilo kwa kasi huku baadhi ya watu waliokuwa ndani yake wakimshangaa.<br />
<br />
“Mh! Kwa nini watu wananishangaa kiasi hiki, inawezekana eneo hili ni hatari?” alijiuliza huku akisonga mbele. Hatimaye nusu saa baadaye alifanikiwa kufika katika mji mdogo ambao hata hakuufahamu jina lake. Akaona maduka kadhaa, huku akiwa na wasiwasi mkubwa akatembea na kusogea katika moja ya maduka yaliyokuwepo eneo hilo. Bado watu walionekana kumshangaa kwani alionekana kuwa mgeni kwa kila kitu.<br />
<br />
“Habari yako?” alimsabahi muuza duka.<br />
“Salama nikusaidie nini?”<br />
“Naweza kupata wapi huduma ya simu hapa?”<br />
“Hata hapa unaweza kuipata,” alijibu mzee aliyekuwepo dukani hapo na bila kusema kitu chochote Ditrov akainamisha kichwa chini kama mtu aliyekuwa anakumbuka kitu fulani, alipoinuka aliomba kalamu na karatasi kisha akaanza kuandika namba kwenye kipande cha karatasi.<br />
<br />
”Hii hapa.”<br />
Mzee mwenye duka akanyoosha mkono na kuipokea karatasi hiyo kisha bila kuchelewa akabonyeza namba alizopewa. Haikupita hata sekunde mbili, simu ikasikika ikiita upande wa pili.<br />
“Ngrii!Ngrii!Ngrii!” Haraka akakabidhi mkono wa simu kwa mteja wake.<br />
“Mimi ni Ditrov, sikufa kama watu wengi nchini Urusi wanavyofahamu, nilinusurika na nina kazi moja nzito ambayo nitataka uifanye kwa uaminifu mkubwa. Nakupa muda wa siku tatu tu iwe imekamilika, umenielewa?” Aliongea Ditrov kwa ukali, kitendo kilichofanya watu wote waliokuwepo eneo hilo kupigwa na butwaa.<br />
<br />
“Mungu wangu kumbe hukufa? Nini kilitokea mpaka ukawa hai? Dunia nzima inafahamu kwamba wewe na washirika wako wote mlishakufa?” Sauti ya upande wa pili ilisikika ikiuliza.<br />
“Ni historia ndefu kidogo lakini kwa ufupi nipo hai.”<br />
“Nisikilize vizuri, tena kwa makini usije ukafanya kosa kabisa.”<br />
“Nipo tayari.”<br />
<br />
“Nahitaji kupata fedha ndani ya siku tatu, hakikisha unafanikiwa vinginevyo hata wewe maisha yako yatakuwa hatarini,” alisema Ditrov kwa msisitizo.<br />
“Bosi nitazipata wapi? Tafadhali nipe maelekezo ya kufanikisha zoezi hilo.”<br />
“Wewe ni Mafia nz umeshafanya michezo mingi hatari, hilo kwako halitakushinda. Kumbuka nimekuwa bosi wako kwa muda mrefu hivyo nafahamu wazi siri zote na naamini unajua nini cha kufanya.”<br />
<br />
“Mh!”<br />
“Kumbuka nahitaji fedha hizo ndani ya siku tatu, nitakupigia simu baada ya siku mbili kujua umefikia wapi, sawa?” alisema Ditrov na alipomaliza alimkabidhi mkono wa simu muuza duka, akatajiwa gharama ya huduma ile na kulipa.<br />
<br />
Je, ni nani huyo? Ataweza kufanya kazi aliyoagizwa na bosi wake na kupata fedha zinazohitajika?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012445f35c9b5d14973008"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064">MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.75<br />
<br />
“Nitahakikisha napata ninachokitaka,” aliongea Ditrov akitokomea kuingia mashambani.<br />
Ditrov alikuwa amedhamiria na alitaka kutimiza alichokitamka kutoka mdomoni mwake pamoja na kwamba alifahamu wazi kwamba pengine zoezi hilo lingeweza kutoa hata uhai wa mtu lakini kwake jambo hilo lilionekana kuwa dogo.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Taratibu huku akionekana mwenye wasiwasi mwingi alianza kutembea na kutokomea kuingia zaidi mashambani ambako ndiko hasa kulikuwa na makazi yake, kichwani mwake akimfikiria Victor Fedorov na unyama aliomfanyia, hakika aliapa kumchukia mtu huyo maisha yake yote na aliuahidi moyo wake kufanya kila kilichowezekana mpaka afanikiwe kulipa kisasi hata kama ingechukua miaka mingapi lakini aliamini jambo hilo lingetokea.<br />
<br />
Kichwani mwake alidhamiria kabisa kulipa kisasi, lakini bila fedha? Jambo hilo lisingewezakana, alitaka kuwa na fedha hata kama kidogo tu ambazo zingempatia gari, simu na hata wafuasi wachache ambao angewatumia kumwinda mbaya wake huyo kila sehemu mpaka mwisho na hatimaye kumpata.<br />
<br />
“Nikifanikiwa nitatoka huku mashambani na kutafuta makazi mazuri kisha kuanza mchakato wa nini cha kufanya,” aliwaza.<br />
Siku ya kwanza ikapita akiwa bado yuko mashambani na chakula chake kikubwa kikawa ni matunda tu na maji kidogo yaliyopatikana eneo hilo.<br />
<br />
Hali yake iliendelea kutengemaa kadiri siku zilivyokwenda mbele, mara kadhaa akiikumbuka familia ya Oleg Malenko na kuishukuru kwa msaada wote iliyompatia.<br />
Akauahidi moyo wake siku moja kurudi kulipa fadhila kwa mema aliyotendewa na familia hiyo.<br />
<br />
“Ipo siku nitarudi naomba niwakute hai, najua watanidadisi sana lakini nitarudi na kuwapa shukrani zangu, wameokoa maisha yangu wale, sijui isingekuwa Oleg ingekuwaje kwani nilishakata tamaa nikiamini kwamba sasa ninakufa maji na maiti yangu kuliwa na samaki wakubwa baharini, hivyo hakuna mtu ambaye angefahamu nini kilitokea katika maisha yangu,” aliwaza.<br />
<br />
Siku ya pili asubuhi Ditrov alitoka tena kuelekea mji mdogo kwa lengo moja tu la kupiga simu kwa mtu aliyekuwa amempa kazi, alitaka kufahamu aliendeleaje na kumkumbusha kwamba ilikuwa imebaki siku moja tu mbele ili kukamilisha mpango mzima na kumtaka asifanye mchezo na suala hilo vinginevyo angekiona cha moto.<br />
<br />
Muda wote akitembea hakudiriki hata mara moja kuinua uso wake na kama alifanya hivyo ni mara moja tu na kuendelea na safari yake, hatimaye akafika kwenye mji mdogo sehemu ileile aliyowahi kupiga simu kwa mara ya kwanza na kutoa namba kisha kuomba msaada wa kupigiwa simu.<br />
<br />
Sekunde tatu tu baadaye alikuwa katika simu akiongea na mtu upande wa pili huku akionyesha msisitizo na kwa sababu aliongea kwa lugha ya Kirusi hakuwepo mtu eneo hilo aliyeweza kuelewa ni kitu gani aliongea, wengi walimtazama kwa macho na kugundua kwamba alikuwa na tatizo fulani kwani macho yake yalionekana mekundu muda wote alipokuwa akiongea na simu.<br />
“Sikia kwa makini nitakuwepo tena hapa muda kama huu kukupigia ili nikupe maelezo jinsi ya kunipata mara utakapofanikiwa kuchukua huo mzigo, sawa?” aliongea na kuuliza.<br />
<br />
“Sitaki uue lakini kama itatokea nitakupa ruhusa ya kujeruhi tu na si vinginevyo, nadhani unanielewa vyema sina mchezo na kazi yangu hasa pale ninapotaka kitu ni lazima nikipate…”aliongea Ditrov huku akitetemeka, alionekana kama mtu aliyekuwa na homa kali.<br />
<br />
Haraka akarudisha mkono wa simu huku akiuliza kiasi cha fedha anachodaiwa, bila kuchelewa akaingiza mkono mfukoni na kutoa kiasi hicho akalipa na taratibu akaanza kuondoka eneo hilo.<br />
“Mh!” Mtu aliyempa huduma ya simu dukani aliguna, alionekana kumshangaa Ditrov kupita kawaida, kwanza kwa jinsi alivyokuwa na sura yake ilitisha.<br />
<br />
Mwili wake mkubwa uliojazia vyema ni jambo lililosababisha kuingiwa na wasiwasi na kuamini kabisa kwamba mtu huyo hakuwa wa kawaida alikuwa na kitu alichokuwa akikitafuta.<br />
<br />
“Inawezekana akawa ni jambazi huyu,” aliongea macho yake yakimwangalia Ditrov kwa makini.<br />
“Nimesikia akisema kesho atarejea tena hapa dukani kwa ajili ya kupiga simu nitamwangalia tena na kama nitakuwa sijamwelewa vyema nitatoa taarifa polisi haraka ili waje kumkamata na kwenda kumhoji zaidi.”<br />
<br />
***<br />
Ndani ya chumba kila mtu alikuwa hoi kupita maelezo, kila mmoja akionekana kumhitaji mwenzake kwa hali na mali.<br />
Mara kadhaa Daniel alipojaribu kupeleka mkono wake kwa lengo la kushika chuchu za Lina ili azitumbukize mdomoni mwake, jambo hilo lilionekana kuwa gumu kwani Lina alimsukuma pembeni akimtaka kusubiri kwanza.<br />
<br />
“Lakini kuna tatizo gani mpenzi wangu mimi nakuhitaji sana.”<br />
“Najua lakini mimi siko tayari bado kidogo.””Unataka nikufanyie nini ili unipe nafasi Lina?”<br />
“Mh! Haya inatosha njoo basi.”<br />
<br />
Daniel akasogea karibu zaidi na Lina alipotupa macho yake kumwangalia usoni aligundua jambo fulani, macho yake yalikuwa mekundu kupita maelezo na mwili wake ulionekana kutetemeka.”<br />
“Daniel,” aliita.<br />
“Yes, Lina.”<br />
<br />
“Nipe kidogo halafu tupumzike, hali yangu kwa jinsi ilivyo hainiruhusu kuendelea zaidi ya hapa naweza kufa kama si kuzimia.”<br />
“Na wewe una haraka kama nini sijui!”<br />
“Nakuambia ukweli usiponipa naweza kufa muda si mrefu, nipe kidogo,” alibembeleza Daniel akionyesha umakini wa hali ya juu.<br />
Maneno hayo yakapenya moja kwa moja masikioni mwa Lina na kumfanya amwonee huruma Daniel kupita kawaida, kwa sauti ya upole akamnong’oneza Daniel sikioni mwake na kumweleza kwamba sasa alikuwa amekubali kufanya kitu alichokitaka.<br />
<br />
“Ahsante Lina, nataka uamini kitu kimoja tu.”<br />
“Kipi hicho?” aliuliza Lina kwa sauti ya mahaba.<br />
“Nakupenda sana mpaka sasa siamini kama umenikubali lakini nitaamini zaidi pale tu utakaporuhusu tukafanya tendo la ndoa.”<br />
Lina alikuwa kimya kitandani bila kujibu chochote huku machozi yakimbubujika, taswira ya mumewe Phillip ilionekana mbele yake ikimhimiza juu ya kukubali kufanya tendo hilo na Daniel.<br />
<br />
Ni hali hiyo ndiyo ilimfanya Daniel aamini kwamba sasa Lina alikuwa tayari kwa kila kitu bila kujiuliza mara mbili akamsogeza Lina karibu yake kisha kumlaza vizuri kitandani tayari kwa kazi moja tu kutimiza shughuli moja ya kumpa Lina raha ambayo kamwe hataisahau maishani mwake.<br />
“Lala vizuri basi mpenzi wangu tuanze...” aliongea Daniel kwa sauti ya kukatikakatika.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea?kesho kama kawa ila mjitahidi kuingia blog kwani huko ndo kuna mwanews ya kufa mtu! usipimie as u know me well na blog iko bomba sana inavutia kuna cha ya live hapo hapo yaani kila kitu,USIKU MWEMA NAWAPENDA NYOOOOTEEEE!!!!mwaaaas</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501246570079c7154525681">MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.76<br />
<br />
<br />
SIKU ya pili asubuhi, Ditrov alitoka tena kuelekea kwenye ule mji mdogo kwa lengo moja tu la kupiga simu kwa mtu aliyekuwa amempa kazi. Alitaka kufahamu amefikia wapi na kumkumbusha kwamba ilikuwa imebaki siku moja tu mbele ili kukamilisha mpango mzima. Alipanga kurudia kumsisitiza na kumtaka asifanye mchezo na suala hilo vinginevyo angekiona cha moto.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Muda wote wakati akitembea, hakudiriki hata mara moja kuinua uso wake na kama alifanya hivyo, aliangalia sehemu ambayo haina watu na kuendelea na safari yake. Hatimaye akafika kwenye ule mji mdogo, sehemu ileile aliyopigia simu kwa mara ya kwanza, akatoa namba kisha kuomba msaada wa kupigiwa simu.<br />
<br />
Sekunde tatu tu baadaye, tayari alikuwa katika simu akiongea na mtu upande wa pili huku akionesha msisitizo. Kwa sababu aliongea kwa lugha ya Kirusi, hakuwepo mtu eneo hilo aliyeweza kuelewa ni kitu gani alichokuwa anaongea. Wengi walimtazama kwa macho yaliyojaa viulizo na kuhisi kwamba alikuwa na matatizo makubwa kwani macho yake yalikuwa mekundu muda wote wakati akiongea na simu.<br />
<br />
Upande wa pili, Lina na Daniel wapo ndani ya chumba, kila mmoja akiwa hoi kupita maelezo. Daniel ndiyo alikuwa na wakati mgumu zaidi kwani alionekana kumhitaji mwenzake kwa hali na mali. Mara kadhaa Daniel alipojaribu kupeleka mkono wake kwa lengo la kushika chuchu za Lina ili azitumbukize mdomoni mwake, Lina alikuwa akimsukumia pembeni na kumtaka asubiri kwanza.<br />
<br />
Ghafla, Daniel anashuhudia machozi yakitiririka mashavuni mwa Lina, jambo ambalo analiona kama nafasi pekeee ya kutimiza alichokitaka, akamlaza vyema Lina kitandani tayari kwa kazi huku akijifanya kumbembeleza.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
KWAKE fedha hazikuwa na maana kuliko maisha ya watoto wake, Mariya na Merina ambao walikuwa kwenye hatari kubwa. Akiwa na hofu nyingi baada ya kumaliza kuweka kiasi cha fedha alichotakiwa kwenye begi, Victor Federov alilikamata sawasawa na kuanza kutembea kutoka nje ya chumba kuelekea sebuleni. Alipofika alipitiliza mpaka nje na kuingia ndani ya gari kisha kuliwasha, akiwa tayari kwa safari ya kuelekea Msitu wa Beloomut ambako alitakiwa kupeleka fedha hizo kama masharti ya kukabidhiwa watoto wake wakiwa hai. <br />
<br />
“No way out, I have to do this for my daughters,” (Hakuna jinsi, ni lazima nifanye hivi kwa ajili ya wanangu) Aliongea Victor Fedorov akiwa ndani ya gari lake.<br />
<br />
Lakini kabla hajaingia ndani yake alikumbuka kitu kimoja muhimu sana kwa wakati huo, bastola ambayo aliamini kabisa ingeweza kumsaidia kama tu angekutana na hatari yoyote katika safari yake, akalitupa begi la fedha ndani ya gari na yeye kutoka mbio kuelekea ndani ambako haikumchukua hata dakika tatu tayari akawa amesharejea na kuingia ndani ya gari tayari kwa safari ndefu.<br />
<br />
Moyoni mwake alikuwa na machungu makubwa, muda mwingi machozi yalikuwa yakimbumbujika. Hakuona tena thamani ya tajiri wake.<br />
“This is the worst day in my entire life” (Hii ni siku mbaya zaidi katika maisha yangu yote) alizidi kuwaza Fedorov.<br />
<br />
“Piiii! Piiii! Piii!” Ilikuwa ni honi ya gari akipiga kuomba msaada wa kufunguliwa lango na mlinzi ili atoke. Kwa kasi ya ajabu akaliendesha gari mpaka langoni na kabla hajatoka alisimama na kuongea jambo fulani na mlinzi wake kisha akapandisha kioo na kuondoka.<br />
<br />
Njia nzima aliliendesha gari akiwa ni mwingi wa mawazo kwanza maisha ya watoto wake na pili uhai wake yeye mwenyewe hakufahamu kabisa mtu aliyekwenda kukutana naye alikuwa vipi na ni kwanini alisisitiza fedha hizo zipelekwe katika msitu wa Beloomut ambao kwa hakika historia yake haikuwa njema.<br />
<br />
“Acha niende cha muhimu ni kupata watoto wangu kama ni hizi fedha nitapata tu nyingine…”Aliwaza akizidi kukanyaga mafuta na gari kusonga mbele.<br />
<br />
Mbele yake yalikuwa zilikuwa zimebaki saa saba tu ambazo zingefanya kutimia kwa saa ishirini na nne ambazo alikuwa amepewa na mtekaji wa watoto wake hivyo kuchelewa kwake kungesababisha maradha makubwa na hata kusababisha kupoteza maisha ya Merina na Mariya.<br />
<br />
Akiwa katika mwendo wa kasi akatupa macho yake kwenye saa yake ya mkono na kugundua kwamba alitakiwa kufanya kila alichoweza kuhakikisha saa hizo zinamkuta akiwa tayari ndani ya msitu wa Beloomut ili kunusuru maisha ya watoto wake. Akaongeza mwendo wa kasi zaidi na kufanya kila aliyekutana naye barabarani kushangaa na pengine kudhani kwamba alikuwa ni mwizi wa gari aliyekuwa ameiba sehemu fulani.<br />
<br />
Kwa Victor Federov mwendo ulionekana kuwa mrefu kila alipotupa macho yake kwenye saa yake aligundua muda ulikuwa ukizidi kusonga kama vile kulikuwa na mtu akihimiza kikimbiza saa mawazo mengi yakazidi kuufunika moyo wake akajikuta ameanza kukata tamaa juu ya kuwapata watoto wake wakiwa hai.<br />
<br />
“Oh my God, do something for my daughters, they are the only kids I have” (Oh..Mungu wangu, tenda jambo flani kwa wanangu, ni watoto pekee nilionao) alijikuta akitamka maneno hayo kwa nguvu japo hajawahi kukanyaga kanisani wala msikitini katika historia ya maisha yake.<br />
<br />
“Kama sitawakuta wakiwa hai hata mimi sitaona sababu ya kuendelea kuishi nitajipiga risasi ili nife.” Aliwaza machozi yakzidui kuuchakaza uso wake.<br />
<br />
***<br />
Hasira kali zilikuwa zimempanda kupita maelezo akisahau kabisa kwamba chanzo cha mambo yote hayo ilikuwa ni yeye kumruhusu mkewe kwenda kufanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine ili tu ashike ujauzito ambao angeulea na kuutunza mpaka mtoto atakapozaliwa.<br />
<br />
Phillip alitoka ndani ya gari lake na kufunga mlango nyuma yake bila kujiuliza mara mbili kwamba kitendo alichotaka kwenda kufanya ndani ya hoteli hiyo kilikuwa cha aibu kuwa alitembea moja kwa moja na kuingia mapokezi.<br />
“Habari yako dada?” Aliuliza kwa sauti ya juu.<br />
“Salama tu nikusaidie?”<br />
<br />
“Ah! Mh! Ah!”<br />
“Kaka nakusikiliza nimekuuliza nikusaidie?”<br />
“Ndio.”<br />
“Sijui naweza kufahamu jambo fulani hapa?”<br />
<br />
“Unaweza na hiyo ndiyo kazi yangu sema tu.”<br />
<span> “Nauliza…nauliza…”Aliongea</span><wbr></wbr><span class="word_break"></span> akirudiarudia.<br />
“Mh!” Msichana wa mapokezi aliguna yeye pia hakumwelewa Phillip alihitaji nini na kibaya zaidi tayari usiku ulikuwa umeshaingia.<br />
<br />
“Taratibu bila kusema kitu chochote huku macho yake yote yakimwangalia kwa makini alinyanyua simu na kupiga namba kadhaa hapo kisha kusikiliza.<br />
“Hallow…ndio…tafadhali naomba ulinzi hapa mapokezi… kuna mtu ameingia hapa hata simuelewi…sijui anataka nini…nimeongea naye simuelewi kabisa…inavyoonena kama vile amechanganyikiwa kidogo…tafadhali njoo mara moja… nina hofu kubwa sana…” Aliongea kwa sauti ya chini lakini bado Phillip aliendelea kusimama eneo hilo bila kusema kitu chochote alionekana kama mtu aliyepigwa na butwaa.<br />
<br />
Hazikupita hata sekunde tatu tayari watu wawili walioonekana kuwa walinzi waliingia mikononi mwao wakiwa wameshika bunduki. Kwa haraka wakatembea mpaka sehemu ambako alisimama Phillip na kumsabahi.<br />
“Sijui unahitaji nini ndugu yetu hapa?”<br />
“Mh!”<br />
“Tafadhali ongea vinginevyo tutavunja miguu yako sasa hivi.”<br />
<br />
“Kwa kosa gani sasa?”<br />
“Hii si sehemu ya kusimama tu kibaya zaidi ni usiku sasa, unahitaji nini tukusaidie?” Mlinzi mmoja aliongea huku akifoka tayari alishaiweka vyema bunduki kulenga miguu ya Phillip.<br />
“Tafadhali msinidhuru niko hapa kuhitaji msaada mmoja tu.”<br />
“Ndio tunaotaka kukusaidia.”<br />
<br />
“Nauliza….nauliza dada mmoja anaitwa…Lina.”<br />
“Lina?”<br />
“Ndio.”<br />
“Hebu niangalie kwenye kitabu cha wageni wangu leo.” Haraka dada wa mapokezi akavuta daftari kubwa na kuanza kufunua ukurasa mmoja baada ya mwingine akiangalia jina hilo.”<br />
<br />
“Hatuna jina la mtu huyo leo labda kama ana jina jingine.”<br />
“Hapana anaitwa Lina ndilo jina lake.”<br />
Phillip akabaki mdomo wazi hakuwa na namna nyingine ya kueleza kwani jambo lililokuwa likifanyika ndani ya hoteli hiyo chumbani lilikuwa ni siri kubwa bila kutarajia machozi yakaanza kumbubujika.<br />
“Mungu baba, niondolee kikombe hiki kinazidi kuwa cha moto zaidi” aliwaza Phillip akiwa amejiinamia.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Phillip atakuwa tayari kueleza ukweli ili apate msaada wa kumpata Lina? Nini hatima ya Victor Fedorov na watoto wake kwenye msitu wa Beloomut?</span></div></span></div><span class="fcg"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124656f3e9a1765744659">MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.77<br />
<br />
Huku akionekana mwenye wasiwasi mwingi machoni mwake, aliendesha gari mara kadhaa akigeuza shingo yake huku na kule kuangalia usalama kwani alifahamu wazi kwamba sifa za msitu huo nchini Urusi zilitisha kupita maelezo, njia nzima aliendesha gari bila kukutana na mtu yeyote na kwa ilivyoonekana hapakuwepo kiumbe hai kilichoishi ndani ya msitu huo.<br />
<br />
Moyoni mwake hak<span class="text_exposed_show">uwa na uhakika kama angeweza kutoka ndani ya msitu huo akiwa salama lakini zaidi ya yote ni watoto wake Mariya na Merina hao ndiyo walikuwa kila kitu na alitaka afanye kila alichoweza kuhakikisha anawapata wakiwa hai.<br />
“Ikitokea nikifa halitakuwa tatizo sana lakini watoto wangu wapone, najua wataweza kuendesha maisha kwa utajiri nilionao, ninashukuru kwamba nimeandika kila kitu kwa wakili wangu…”aliongea.<br />
<br />
Victor Fedorov alifanikiwa kuingia ndani ya msitu na kuegesha gari lake sehemu moja iliyoonekana kuwa wazi, hapo akajiweka sawa akiangalia usalama wake, taratibu bila kujiuliza mara mbili akalikamata vyema begi lililokuwa na fedha ndani yake kisha akaichomeka bastola yake kiunoni na kushuka garini.<br />
Akatupa macho yake huku na kule bila kuona kitu chochote, akiwa katika hali hiyo milio ya risasi ikasikika.<br />
<br />
“Puuu! Puuu! Puuu!”<br />
“Mungu wangu… hiyo ni milio ya risasi…isijekuwa…” aliongea akijaribu kuzungusha macho yake huku na kule na katika kuangalia vyema macho yake yakakutana na kitu cha ajabu mbele yake, mtu aliyevalia nguo nyeusi na uso wake ukiwa umefunikwa na kuacha sehemu ya macho tu.<br />
<br />
Mtu huyo alisimama pembeni kidogo mahali Victor Fedorov alipokuwa ameegesha gari.<br />
“Haaa! Haaa! Haaa” mtu huyo alicheka kwa sauti ya kebehi.<br />
Akitetemeka, akatembea akisogea kuelekea mahali aliposimama mwanaume huyo lakini kabla hajamfikia karibu sauti nyingine ikasikika.<br />
“Victor Fedorov?” mwanaume huyo aliuliza.<br />
<br />
“Ndiyo.”<br />
“Vyema umefika muda muafaka kabisa.”<br />
“Watoto wangu wako wapi?”<br />
“Usiwe na haraka watoto wapo lakini nataka kufahamu jambo moja; je umefika hapa na nani?”<br />
“Peke yangu kabisa hakuna mtu…”<br />
<br />
“Una uhakika?”<br />
“Asilimia mia moja.”<br />
“Kumbuka kama unaye mtu mwingine kwenye gari lako jambo hilo litamaanisha hatari kubwa pengine kupoteza watoto wote.”<br />
“Ninachokizungumza ni ukweli mtupu, tafadhali chukua fedha hizi hapa kisha unipatie watoto wangu,” aliongea Victor Fedorov machozi yakimbubujika.<br />
<br />
Pamoja na ukatili wake wote hapo alikuwa amefunga breki, hakuwa na namna nyingine yoyote ya kufanya zaidi ya kukubali kila alichokuwa ameelezwa ili mradi tu awapate watoto wake Mariya na Merina.<br />
“Daddyyyyy.” (baba.) Sauti hiyo ilipenya moja kwa moja masikioni mwa Victor Fedorov.<br />
Haraka akageuza shingo yake huku na kule kuangalia ni wapi sauti hiyo ilitokea lakini hakufanikiwa kuona kitu chochote, alirudisha macho yake kumwangalia mwanaume aliyekuwa mbele yake.<br />
<br />
“Najua wazi huwezi kukosa silaha ni vyema ukaiweka chini haraka.”<br />
Bila kusema kitu chochote akaichomoa bastola yake na kuitupa chini huku akiendelea kumsihi mwanaume huyo kumweleza ni wapi walipokuwa watoto wake.<br />
“Weka pia begi hilo hapo chini na urudi nyuma mita tano!” aliamuru mwanaume huyo.<br />
<br />
Taratibu, Victor Fedorov alitii kila alichoelezwa, akaliweka begi chini na kuanza kurudi kinyumenyume, macho yake yote yakimwangalia mwanaume huyo ambaye hakuonekana sura kwani kichwa chake kilifunikwa na kitu kama soksi iliyoacha nafasi ndogo sehemu ya macho tu.<br />
<br />
Wasiwasi mwingi ukamfunika na kumfanya ashindwe kuelewa ni kitu gani kingetokea mbele yake baada ya muda mfupi kwani kama ni silaha tayari alishaikabidhi kwa adui aliyekuwa mbele yake.<br />
“Mh!”aliguna huku akiendelea kurudi nyuma akahisi vitu vyepesi vikipenya kutoka ndani ya suruali yake kuelekea chini.<br />
<br />
***<br />
Baada ya mhudumu wa mapokezi kusoma kitabu cha wageni kwa muda akitafuta jina la Lina bila mafanikio, aliinua macho yake na kumwangalia Phillip ambaye naye alionekana kulengwalengwa na machozi akimweleza wazi kwamba jina hilo halikuwepo ndani ya kitabu chake labda kama mgeni wake huyo alikuwa na jina jingine alilolitumia.<br />
“Hapana jina lake ni hilo hilo la Lina.”<br />
<br />
“Kaka halipo tafadhali niamini na uondoke,” aliongea dada wa mapokezi akitoa ishara kwa walinzi waliokuwepo eneo hilo.<br />
Akiwa katika hali ya kupigwa na butwaa upande mmoja wa akili yake ulimwambia aondoke na kurejea nyumbani huko angeendelea kumsubiri mkewe mpaka atakaporejea lakini upande mwingine wa akili yake ulimwambia atoke nje ya hoteli hiyo na kuingia ndani ya gari lake akae hapo kusubiri mpaka mwisho.<br />
<br />
“Mzee nadhani umepata maelezo yanayotosha kabisa kukufanya uelewe, tafadhali tunaomba nafasi hapa.”<br />
Bila kujibu chochote Phillip akainua macho yake na kuwaangalia watu hao, moyo wake ulijaa siri nzito kupindukia lakini hakuwa na uwezo wa kumshirikisha mtu mwingine kwani jambo lililokuwa likifanyika ndani ya hoteli hiyo usiku huo lilikuwa ni siri kubwa.<br />
<br />
Machozi yakambubujika, taratibu akaanza kutembea kuelekea nje, moyoni mwake akijilaumu kwa kumtoa mkewe sadaka kwa mwanaume mwingine, akilini mwake akiamini kabisa kwamba Lina alikuwa ameamua kumkimbia.<br />
“Najutia maamuzi yangu haya isingekuwa mimi yote haya yasingetokea, Lina atakuwa ameamua kunitenda kama kisasi,” aliongea Phillip akiukaribia mlango ili atoke nje</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124656f37c81e52565151">MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.79<br />
<br />
“Hapana! Hapana Mariya usife mwanangu bado nakuhitaji amka uungane na mwenzako Merina yule palee,” aliongea mfululizo akizidi kumtingisha Mariya aliyekuwa amelala chini kimya bila kufungua macho wala kujitingisha.<br />
Hali ilionekana kuwa mbaya, Victor Fedorov alizidi kumtingisha mwanaye ili aamke lakini haikuwa hivyo, Mariya alikuwa amelala ardhini kimya kabisa, akatu<span class="text_exposed_show">pa macho yake huku na kule kama vile mtu aliyekuwa akitafuta kitu fulani vile, giza nalo lilianza kutanda katika msitu huo.<br />
“Ni lazima niondoke hapa haraka sana kabla giza halijaingia zaidi,” aliwaza akimnyanyua mtoto wake Mariya na kuanza kukimbia kuelekea kwenye gari lake.<br />
Haraka akamketisha na alipohakikisha kila kitu kilikuwa sawa akaingia ndani ya gari na kukaa kwenye usukani huku akiwa na hofu, akawasha na kukanyaga mafuta, lengo likiwa kuondoka eneo hilo.<br />
Akiwa ndani ya gari baada ya kutoka nje ya msitu huo alisimamisha gari na kuanza kumwita tena Mariya ambaye bado alikuwa ametulia kimya.<br />
“Mariya! Mariya! Nini kimekupata mwanangu?” aliuliza.<br />
“Daddy!” Merina aliita huku akitetemeka, yeye pia afya yake haikuwa nzuri, walidhoofika sana, miili yao ilikuwa michafu kupindukia hata nywele zao zilionekana kujisokota.<br />
“Yes, tafadhali nieleze ni kitu gani kimempata nduguyo?” aliuliza hamu yake kubwa ikiwa ni kufahamu tatizo lililotokea huko nyuma kabla hawajafika eneo hilo.<br />
Merina hakujibu kitu chochote, zaidi aliishia kuangua kilio kilichozidi kumtia wasiwasi baba yao akashindwa kuendelea na safari na kuliegesha gari pembeni kwanza ili azungumze na Merina ambaye alionyesha nafuu kidogo kuliko mwenzake Mariya.<br />
“Baba tafadhali endesha gari ukichelewa kidogo tu hata mimi nitakuwa kama Mari…”aliongea Merina na kabla hajamalizia sentensi yake naye pia akatulia kimya kitini.<br />
Victor Fedorov akazidi kuchanganyikiwa zaidi akashindwa afanye kitu gani kwani kila kitu kilichokuwa kikimtokea katika maisha yake kwa wakati huo kilionekana kuwa kama ndoto, alishatoa fedha nyingi ili kuokoa maisha ya watoto wake lakini ni hao sasa waliokuwa katika hali ya kufa kwani wote walionekana kupoteza fahamu, moyo ukamuuma sana akajutia uamuzi wake wa kuwateka watoto hao kutoka nchini Tanzania na kuwaleta nchini Urusi na sasa walikuwa wakifa bila hatia yoyote.<br />
“Ubinafsi umeniponza pengine Mungu ananipa pigo hili ili nitubu kwa dhambi niliyoifanya ya kuwateka watoto hawa, lakini si ni uzao wangu huu? Hapana, nasema hapana siko tayari nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu wote kuhakikisha maisha yao yanarejea tena naamini watakuwa hawajafa bali wamezimia tu…” aliwaza huku akizidi kukanyaga mafuta.<br />
Akili yake yote ilishahama na kwenda moja kwa moja kuokoa maisha ya watoto wake, alitaka afike nyumbani haraka na kutafuta daktari ambaye angeweza kufanya kila atakachoweza kuokoa maisha ya watoto hao pacha, hata kama safari hii ingegharimu utajiri wake wote aliokuwa nao, Victor Fedorov alikuwa tayari.<br />
Kwa muda wa saa tatu bado alikuwa barabarani, mara kadhaa akisimama na kuwaangalia watoto wake ili kujua hali zao, bado zilikuwa zilezile hawakuzungumza chochote zaidi ya kutulia kimya vitini.<br />
Saa sita baadaye huku akimwagika jasho mwili mzima tayari alishawasili nje ya lango la nyumba yake, akapiga honi na mara moja lango likaonekana likifunguliwa na gari kuzama ndani, bila kusema kitu chochote na mlinzi wake akaliendesha gari mpaka sehemu ya maegesho, akasimama na kushuka haraka garini kisha akafungua milango ya nyuma.<br />
“Mlinzi!”aliita kwa sauti ya juu na mara moja akakimbia na kusimama mbele ya gari lake.<br />
“Tafadhali nisaidie kubeba mtoto mmoja haraka kwenda ndani,” aliamuru tayari mikononi mwake alishambeba Mariya.<br />
Mlinzi hakuchelewa, alimbeba Merina wakaanza kukimbia kuelekea ndani.<br />
***<br />
Huku machozi yakimbubujika, moyoni mwake akiumia, Phillip alianza kutembea kuuelekea mlango wa mapokezi ili atoke nje na kuondoka eneo hilo kama alivyoamriwa.<br />
Walinzi wawili wenye silaha walikuwepo nyuma yake kumsindikiza, wao pia walionyesha kuchukizwa sana na kitendo alichokuwa amekifanya Phillip eneo lao la kazi hivyo hawakuwa na utani walitaka kulinda vyema kibarua chao.<br />
“Tembea haraka bwana tena tunakusihi uondoke eneo hili haraka sana kabla hatujakuchakaza…umesikia bwana mdogo…tembea…” aliongea askari mmoja akimsukuma kwenda mbele. Machozi yakambubujika kwa mara nyingine tena hakuwa tayari kuondoka hotelini hapo na kumwacha mkewe Lina ambaye aliamini kabisa kwamba bado alikuwepo ndani.<br />
Wakati mlinzi wa mwisho anatoka na kufunga mlango nyuma yake sauti kali ikasikika ndani ya hoteli hiyo mwanamke akilia kuomba msaada na kishindo cha mtu akikimbia kuelekea eneo la mapokezi kikasikika.<br />
“Uwiii! Nisaidieni! Tafadhali niokoeni jamani! Anani…”<br />
“Mh!” wote wakaguna.<br />
“Sauti kama ya Lina! Ni sauti ya mk…” aliongea Phillip mfululizo na kushindwa kumalizia sentensi yake, wote wakaonekana wakikimbia mbio kurejea ndani ya hoteli.<br />
<br />
Je, nini kitatokea? Sauti iliyosikika ndani ya hoteli Phillip ameitambua kwamba ni ya mkewe Lina, ni kitu gani kimempata huko?</span></div></span><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012465701ceb6504667064"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50124731ee7759488705440">MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.80<br />
<br />
Hapana! Hapana Mariya usife mwanangu bado nakuhitaji amka uungane na mwenzako Merina yule palee,” aliongea mfululizo akizidi kumtingisha Mariya aliyekuwa amelala chini kimya bila kufungua macho wala kujitingisha.<br />
Hali ilionekana kuwa mbaya, Victor Fedorov alizidi kumtingisha mwanaye ili aamke lakini haikuwa hivyo, Mariya alikuwa amelala ardhini kimya kabisa, akatup<span class="text_exposed_show">a macho yake huku na kule kama vile mtu aliyekuwa akitafuta kitu fulani vile, giza nalo lilianza kutanda katika msitu huo.<br />
“Ni lazima niondoke hapa haraka sana kabla giza halijaingia zaidi,” aliwaza akimnyanyua mtoto wake Mariya na kuanza kukimbia kuelekea kwenye gari lake.<br />
Haraka akamketisha na alipohakikisha kila kitu kilikuwa sawa akaingia ndani ya gari na kukaa kwenye usukani huku akiwa na hofu, akawasha na kukanyaga mafuta, lengo likiwa kuondoka eneo hilo.<br />
Akiwa ndani ya gari baada ya kutoka nje ya msitu huo alisimamisha gari na kuanza kumwita tena Mariya ambaye bado alikuwa ametulia kimya.<br />
“Mariya! Mariya! Nini kimekupata mwanangu?” aliuliza.<br />
“Daddy!” Merina aliita huku akitetemeka, yeye pia afya yake haikuwa nzuri, walidhoofika sana, miili yao ilikuwa michafu kupindukia hata nywele zao zilionekana kujisokota.<br />
“Yes, tafadhali nieleze ni kitu gani kimempata nduguyo?” aliuliza hamu yake kubwa ikiwa ni kufahamu tatizo lililotokea huko nyuma kabla hawajafika eneo hilo.<br />
Merina hakujibu kitu chochote, zaidi aliishia kuangua kilio kilichozidi kumtia wasiwasi baba yao akashindwa kuendelea na safari na kuliegesha gari pembeni kwanza ili azungumze na Merina ambaye alionyesha nafuu kidogo kuliko mwenzake Mariya.<br />
“Baba tafadhali endesha gari ukichelewa kidogo tu hata mimi nitakuwa kama Mari…”aliongea Merina na kabla hajamalizia sentensi yake naye pia akatulia kimya kitini.<br />
Victor Fedorov akazidi kuchanganyikiwa zaidi akashindwa afanye kitu gani kwani kila kitu kilichokuwa kikimtokea katika maisha yake kwa wakati huo kilionekana kuwa kama ndoto, alishatoa fedha nyingi ili kuokoa maisha ya watoto wake lakini ni hao sasa waliokuwa katika hali ya kufa kwani wote walionekana kupoteza fahamu, moyo ukamuuma sana akajutia uamuzi wake wa kuwateka watoto hao kutoka nchini Tanzania na kuwaleta nchini Urusi na sasa walikuwa wakifa bila hatia yoyote.<br />
“Ubinafsi umeniponza pengine Mungu ananipa pigo hili ili nitubu kwa dhambi niliyoifanya ya kuwateka watoto hawa, lakini si ni uzao wangu huu? Hapana, nasema hapana siko tayari nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu wote kuhakikisha maisha yao yanarejea tena naamini watakuwa hawajafa bali wamezimia tu…” aliwaza huku akizidi kukanyaga mafuta.<br />
Akili yake yote ilishahama na kwenda moja kwa moja kuokoa maisha ya watoto wake, alitaka afike nyumbani haraka na kutafuta daktari ambaye angeweza kufanya kila atakachoweza kuokoa maisha ya watoto hao pacha, hata kama safari hii ingegharimu utajiri wake wote aliokuwa nao, Victor Fedorov alikuwa tayari.<br />
Kwa muda wa saa tatu bado alikuwa barabarani, mara kadhaa akisimama na kuwaangalia watoto wake ili kujua hali zao, bado zilikuwa zilezile hawakuzungumza chochote zaidi ya kutulia kimya vitini.<br />
Saa sita baadaye huku akimwagika jasho mwili mzima tayari alishawasili nje ya lango la nyumba yake, akapiga honi na mara moja lango likaonekana likifunguliwa na gari kuzama ndani, bila kusema kitu chochote na mlinzi wake akaliendesha gari mpaka sehemu ya maegesho, akasimama na kushuka haraka garini kisha akafungua milango ya nyuma.<br />
“Mlinzi!”aliita kwa sauti ya juu na mara moja akakimbia na kusimama mbele ya gari lake.<br />
“Tafadhali nisaidie kubeba mtoto mmoja haraka kwenda ndani,” aliamuru tayari mikononi mwake alishambeba Mariya.<br />
Mlinzi hakuchelewa, alimbeba Merina wakaanza kukimbia kuelekea ndani.<br />
***<br />
Huku machozi yakimbubujika, moyoni mwake akiumia, Phillip alianza kutembea kuuelekea mlango wa mapokezi ili atoke nje na kuondoka eneo hilo kama alivyoamriwa.<br />
Walinzi wawili wenye silaha walikuwepo nyuma yake kumsindikiza, wao pia walionyesha kuchukizwa sana na kitendo alichokuwa amekifanya Phillip eneo lao la kazi hivyo hawakuwa na utani walitaka kulinda vyema kibarua chao.<br />
“Tembea haraka bwana tena tunakusihi uondoke eneo hili haraka sana kabla hatujakuchakaza…umesikia bwana mdogo…tembea…” aliongea askari mmoja akimsukuma kwenda mbele. Machozi yakambubujika kwa mara nyingine tena hakuwa tayari kuondoka hotelini hapo na kumwacha mkewe Lina ambaye aliamini kabisa kwamba bado alikuwepo ndani.<br />
Wakati mlinzi wa mwisho anatoka na kufunga mlango nyuma yake sauti kali ikasikika ndani ya hoteli hiyo mwanamke akilia kuomba msaada na kishindo cha mtu akikimbia kuelekea eneo la mapokezi kikasikika.<br />
“Uwiii! Nisaidieni! Tafadhali niokoeni jamani! Anani…”<br />
“Mh!” wote wakaguna.<br />
“Sauti kama ya Lina! Ni sauti ya mk…” aliongea Phillip mfululizo na kushindwa kumalizia sentensi yake, wote wakaonekana wakikimbia mbio kurejea ndani ya hoteli.<br />
<br />
Je, nini kitatokea? Sauti iliyosikika ndani ya hoteli Phillip ameitambua kwamba ni ya mkewe Lina, ni kitu gani kimempata huko? TUTAENDELEA BAADAE WAPENDWA</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012440df10bc0704015415"><span class="text_exposed_show"> </span></div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-73673988955945263692012-07-27T00:29:00.001-07:002012-07-27T00:29:41.083-07:00msichana ndotoni mwangu.....ep.81<a href="https://fbcdn-sphotos-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash3/532371_388654601194121_1436708921_n.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img alt="" border="0" class="spotlight" src="https://fbcdn-sphotos-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash3/532371_388654601194121_1436708921_n.jpg" style="height: 113px; width: 168px;" /></a><br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123fc3a38404812767595">msichana ndotoni mwangu.....ep.81<br />
<br />
Mariya! Merina! ” Victor Fedorov aliita akizidi kuwatingisha watoto wake lakini bado hakuwepo hata mmoja aliyeweza kujibu neno lolote.<br />
<br />
“Mlinzi hebu niletee maji haraka,” aliamuru, na bila kujibu kitu chochote, mlinzi alitoka mbio na sekunde tatu tu baadaye alirejea na maji kwenye bakuli kubwa.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Haraka akalipokea na kuanza kuwamwagia akiamini kwamba kufanya hivyo kungeweza kuwarejesha katika hali zao za kawaida lakini hilo halikutokea, akiwa hapo machozi yakambubujika, akaiona kabisa picha ya kubaki peke yake duniani na utajiri aliokuwa nao.<br />
<br />
Victor Fedorov akaikataa picha hiyo na kuendelea kuwatingisha tena na tena akiwaita watoto wake kwa majina.<br />
<br />
Watoto wake walikuwa wamebadilika kwa kiasi kikubwa, afya zao zilikuwa mbaya kupita maelezo, walikuwa wamebadilika kwa kila kitu kuanzia mavazi mpaka nywele, hali hiyo ndiyo iliyozidi kumtia wasiwasi Fedorov. Akiwa hapo ghafla akili yake ikamweleza kwamba kama alihitaji watoto wake wapone na kurejea katika hali zao za kawaida ni lazima atamfute daktari ambaye angewasaidia.<br />
“Jambo moja linaweza kufanyika kwa sasa?”<br />
“Jambo gani mkuu.”<br />
<br />
”Daktari, ni lazima nipate daktari ambaye atakuja hapa kuwaangalia nitamlipa kiasi chochote kile cha fedha ilimradi tu aokoe maisha ya watoto wangu,” aliongea kwa majonzi, na taratibu akanyanyuka na kuisogelea simu lakini kabla hajaifikia alimsikia mlinzi akiguna.<br />
<br />
Bila kujiuliza mara mbili akatoka mbio kuelekea eneo hilo, alichokishuhudia hapo kilimtoa machozi; Mariya na Merina walilala chini huku mapovu mengi yakitoka midomoni mwao pia walionekana kutupa mikono na miguu kama vile walikuwa wakikata roho. Victor Federov akalia kama mtoto mdogo.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
“Bosi hebu njoo uone mbona wanatoka mapovu!”<br />
“Mapovu?” aliuliza akikimbia kurejea eneo hilo. Ni kweli Mariya na Merina walikuwa wakitiririkwa na mapovu kutoka midomoni mwao.<br />
<br />
“Mungu wangu ni kitu gani hiki? watoto wangu wamepewa…”<br />
“Wamepewa nini bosi wangu?”<br />
“Wamepewa sumu hawa haya mapovu ni ya nini? Watoto wangu wanakufa wakati nikiwa tayari nimeshapoteza fedha nyingi, tafadhali msiniache, naomba msiniache nitabaki na nani katika dunia hii? Fedha na mali si kitu kama sina ndugu wala mtoto yeyote? Mungu nisaidie,” aliongea mfululizo.<br />
<br />
Akiwa hapo, Victor Fedorov akionyesha kukata tamaa kabisa, mawazo yake yote yakampeleka kwa jambazi aliyemwona ndani ya msitu wa Beloomut akamshuhudia akikimbia na begi lililojaa fedha nyingi ndani yake na kutokomea.<br />
<br />
“Kama ni fedha nilimpatia, kwa nini ameua watoto wangu? Kwa nini amewatesa viumbe wasio na hatia? Utajiri wangu umekwenda, na watoto pia wananiacha, nimekosea nini kwa Mungu? Pengine jambo hili linatokea kwangu kama adhabu kwa makosa niliyoyafanya huko nyuma? Hapana! Nashindwa kuelewa…” aliongea mfululizo akiwa pembeni mwa watoto wake ambao mpaka wakati huo walishatulia kimya, mapovu hayakutoka tena midomoni mwao na miguu na mikono yao ilikuwa imetulia kimya.<br />
<br />
“Yametimia!” hivyo ndivyo alivyosema Victor Fedorov na kuangua kilio kikali ndani ya nyumba, mlinzi akasogea karibu yake na kumbembeleza.<br />
“Haiko haja ya kuishi! Bora nife niuungane na familia yangu? Watoto wangu wa kwanza walikufa kifo kibaya wakati wakicheza mchezo wa kuteleza katika barafu na hawa nao …”<br />
Kwikwi ya kulia ikamkaba ni kweli taswira za watoto wake wawili pamoja na mkewe waliokuwa wamekufa miaka mingi kabla, ilimjia kichwani mwake akajiona ni mtu mwenye mkosi duniani hata thamani ya utajiri aliokuwa nao hakuiona, akatamani kuungana na familia yake.<br />
<br />
“Nitakufa! Si muda mrefu kuanzia sasa nitaungana na familia yangu…Mungu wangu…kwa nini yote haya…kwa nini mimi? Nimekosa nini?” alizidi kujilaumu.<br />
Akionyesha kukata tamaa kabisa, akasogeza mkono wake wa kulia na kuupeleka moja kwa moja upande wa shingo ya Mariya ili kupima mapigo yake ya moyo ambapo yalionekana kutulia akageuka tena upande wa pili na kugusa mapigo ya Merina nayo yalionekana kuwa kimya kabisa.<br />
<br />
Bila kusema tena neno lolote akatembea na kwenda kuketi juu ya kiti huku jasho jingi likimtoka na mwili wake ukitetemeka.<br />
“Bosi mimi naona tuwapeleke hospitali huko tutapata mtaalamu ambaye atasema neno.”<br />
<br />
“Lipi zaidi?”<br />
“Mimi nashauri tufanye hivyo pengine wamezimia tu.”<br />
“Nina hakika wamekufa, watoto wangu, wameniacha lakini naamini kabisa nyuma ya mchezo huu yupo mtu fulani sijui ni nani ila yupo, mbona nimetimiza masharti yote? Nimetoa fedha nyingi sana kuwakomboa lakini amenilipa ubaya?” aliongea muda wote huo akiwa ameketi akionyesha kukata tamaa juu ya maisha yake na mbele yake alifikiria kitu kimoja tu; kifo basi.<br />
***<br />
Baada tu ya kutoka ndani ya lango kuu la hoteli ya Lamada, Lina akiwa amejifunika shuka alikimbia na kuvuka upande wa pili wa barabara, watu wachache waliokuwepo eneo hilo wakimshangaa, lakini hakujali alidhamiria kuondoka hapo na kutokomea, huku akilia akasogelea moja ya teksi.<br />
<br />
“Wewe ni mtu au mzimu?” aliuliza dereva teksi aliyekuwa ndani ya gari, haraka akaufungua mlango na kutoka nje tayari kukimbia kwani mara kadhaa historia katika eneo hilo ilionyesha kwamba mizimu ilikuja hapo kutoka makaburi ya jirani hivyo kutokea kwa mtu huyo tena akiwa katika shuka nyeupe kulimwogopesha.<br />
“Kaka usikimbie tafadhali naomba msaada wako mimi ni mwanadamu wa kawaida.”<br />
<br />
“Mh! Hapana usinidanganye tena ona unaongea sauti ya mwanamke, kwa jina la Yesu toka mbele ya macho yangu!”<br />
“Mimi si mzi…” aliongea Lina lakini kijana huyo hakuwa tayari kumsikiliza bado aliendelea kurudi kinyumenyume akijiandaa kukimbia ili kuondoka eneo hilo.<br />
<br />
“Ona! Mimi ni mwanadamu!” aliongea akijaribu kufunua shuka alilojifunika.<br />
“Mungu wangu! Nakufa jamani, jini hili tena yuko…” alipaza sauti na kufanya teksi nyingine zote zilizokuwa jirani madereva wake wawashe magari yao na kuondoka eneo hilo kwa kasi.<br />
<br />
Kwa uwezo wake wote alijaribu kujitetea kuwafanya watu waliokuwepo eneo hilo wamwone kwamba alikuwa ni mwanamke wa kawaida lakini ilionekana kushindikana, teksi zote zikaondoka eneo hilo na kubaki moja tu ambayo dereva wake aliondoka na kuacha gari peke yake eneo hilo.<br />
<br />
“Nitafanya nini sasa?” alijiuliza huku akilia, alitaka kufanya kila kilichowezekana kuondoka eneo hilo kurejea nyumbani kwake, ndani ya moyo wake kulijaa hasira kali juu ya Phillip, hakika hakumpenda tena na aliapa kumchukia maisha yake yote yaliyobaki.<br />
<br />
“Phillip amenidhalilisha kupita maelezo, sipo tayari tena kuendelea kuwa naye! Yaani hivi? Mimi kabisa? Mh! Siyo Lina nadhani ni mzimu wake?” alijiuliza akizidi kusonga mbele, kichwani mwake hakuwa na picha ni wapi alikuwa akielekea lakini alitaka tu kuondoka eneo hilo.<br />
<br />
“Naamini nitapata tu njia ya kuondoka hapa kabla hakujapambazuka,” aliwaza.<br />
***<br />
“Ngrii! Ngrii!Ngriii!” Ulikuwa ni mlio wa simu, mlinzi wa Victor Fedorov baada ya kuona kwamba bosi wake alikuwa amekata tamaa aliamua kutumia uwezo aliokuwa nao, akasogea karibu na simu na kubonyeza namba kadhaa kitengo cha hatari akiomba gari la wagonjwa.<br />
<br />
“Naweza kupata gari la wagonjwa haraka sana?” <br />
Upande wa pili ulijibu.<br />
“Ni nyumbani kwa Victor Fedorov nadhani ni mtu anayefahamika sana hapa kwetu, tafadhali fanyeni haraka kuna wagonjwa hapa…” aliongea kwa msisitizo.<br />
“Hakuna haja tayari wamesha…” aliongea Victor Fedorov huku akilia.<br />
<br />
“Hapana bosi sisi si madaktari ngoja tuwapeleke hospitali pengine huko tunaweza kupata ufumbuzi wa tatizo.”<br />
“Kweli?”<br />
“Ni kweli kabisa.”<br />
“Mariya! Merina kweli mmeondoka na kuniacha wanangu? Maisha bila ninyi si kitu, nilijaribu kwa nguvu na uwezo wangu wote kuwapata lakini sasa mmeondoka wana…”<br />
<br />
Wakiwa hapo haikuchukua hata muda wa dakika tano tayari king’ora kikasikika nje ya lango la kuingilia ndani ya nyumba ya Fedorov, mlinzi akakimbia haraka kwenda kufungua geti, moja kwa moja gari likazama ndani na watu wawili wakiwa wamevalia nguo za rangi ya bluu wakashuka.<br />
<br />
“Yuko wapi huyo mgonjwa?”<br />
“Siyo mgonjwa ni wagonjwa wako wawili?”<br />
“Wawili?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Wako wapi?”<br />
“Huku! Twendeni huku nikawaonyeshe,” mlinzi aliongea akitangulia mbele huku akikimbia.<br />
<br />
Wote watatu wakazama ndani ambako mlinzi aliwaonyesha wagonjwa na kumtambulisha Victor Fedorov kwamba ndiye baba wa watoto hao na bila kusema kitu watu hao wakainama na kuanza kuwachunguza watoto hao wakishika sehemu mbalimbali za miili yao kuwaangalia na mwisho kabisa wakachukua kipimo maalum cha kusikiliza mapigo yao ya moyo.<br />
<br />
Muda wote huo wakihangaika, Victor Fedorov alikuwa pembeni yao naye pia akionyesha wasiwasi mwingi.<br />
“Wako hai?” aliuliza.<br />
<br />
“Mh! Mh!” waliguna kwa pamoja huku wakinyanyua macho yao kumwangalia Fedorov, naye akayasoma vyema na kuelewa ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.<br />
<br />
“Tafadhali nielezeni ukweli msinifiche jambo kuna kitu hapa.”<br />
“Mzee! Matumaini haya…” hawakumalizia sentensi yao wakamshuhudia Victor Fedorov akishuka chini na moja kwa moja akawainamia watoto wake na kuanza kuwabusu mfululizo huku akilia.</span></div></span></div><span class="fcg"></span><br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5190417484351831">MSICHANA NDOTONI MWANGU .......EP.82<br />
<br />
Lina aliendelea kutembea barabarani huku akilia akili yake haikuonekana kufanya kazi kwani kila kitu alichokifikiria kuwa msaada kwake kilionekana kukwamwa kabisa.<br />
<br />
“Ni lazima niondoke hapa kabla hakujapambazuka.” Aliongea akizidi kusonga mbele.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Huku akijilaumu moyoni mwake kwa mambo yote yaliyomtokea, aliamini bila kukutana na Phillip na kumpenda kisha kufunga ndoa naye hayo yote yasingempata, akazitupa lawama zote kwa mwanaume huyo na kumchukia kabisa.<br />
<br />
Jambo moja liliendelea kupita kichwani mwake ni kwamba, mara tu akifanikiwa kufika nyumbani ni kuchukua kila kilichokuwa cha kwake kisha kumwachia Phillip nyumba na yeye kwenda kutafuta sehemu nyingine ambako angeishi maisha yake.<br />
“Nitaondoka, nitamwachia Phillip nyumba, kwa kitendo hiki siko tayari kumsamehe amenidhalilisha sana,” bado Lina aliendelea kujilaumu.<br />
***<br />
Phillip aliyekuwa ndani ya hoteli pamoja na walinzi wawili waliushuhudia mchezo mzima jinsi ulivyokuwa ukiendelea lakini hakuthubutu kufungua mdomo wake kueleza jambo lolote.<br />
Kufanya kwake hivyo ingekuwa ni kujipalia makaa ya moto kwani mwanamke aliyetoka mbio ndani ya chumba akiwa na shuka tu mwilini mwake ni mkewe na kibaya zaidi mwanaume alikuwa akimfuata kwa nyuma huku akimwita ili arejee wamalizie shughuli iliyokuwa mbele yao, ilikuwa ni fedheha ya kutosha kwake.<br />
“Sijui anakwenda wapi? Masikini mke wangu… nisamehe halikuwa kusudio langu kutenda haya,” aliwaza huku akikimbia kuelekea lango kuu la kutokea hotelini ili ashuhudie ni wapi Lina alikuwa akielekea.<br />
Kabla hajatoka nje ya lango akalikumbuka gari lake, akaamua kurejea ili alichukue na kuondoka nalo kumfuatilia Lina, jambo hilo lilifanyika kwa haraka, alipolifikia bila kusema kitu akaingia ndani ya gart hilo na kuliwasha haraka akakanyaga mafuta na likatii amri ba kutoka nje ya hoteli hiyo.<br />
Aliwashuhudia walinzi wawili aliokuwanao wakiwa na mtu mwingine wa tatu na alipotupa macho yake kumwangalia mtu yule alimtambua kuwa ni mwanaume aliyekuwa na Lina ndani ya hoteli, alikuwa akiangua kilio huku akiongea maneno ambayo Phillip hakuyasikia vyema.<br />
“Nitamtafuta Lina mpaka nimpate nimwombe msamaha mke wangu najua ananipenda na atanisamehe,” aliongea akikunja usukuni na kutokeza barabarani.<br />
Moyo wake ulijawa hofu na kujitupia lawama nyingine lakini alijipa moyo baada ya kuamini kwamba jambo lililokuwa limetokea siku hiyo lilikuwa ni kati ya makubaliano yake na mkewe Lina.<br />
Hakuwa na ufahamu kabisa wa kile kilichotokea ndani ya chumba cha hoteli ile mpaka mfarakano ukatokea, hakufahamu kabisa kwamba Lina hakuwa tayari kufanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine, kwake yeye aliamini kwamba kufanya hivyo kungeidhalilisha ndoa yake kama si kuisaliti.<br />
Phillip akaliendesha gari taratibu huku akitupa macho yake huku na kule kuangalia kama angeweza kumwona Lina eneo hilo lakini hakufanikiwa.<br />
Baada ya mwendo mrefu alitupa macho upande wa pili wa barabara na kufanikiwa kulishuhudia kundi kubwa la watu walioonekana kubishana kitu fulani, wazo la kuwafuata watu wale kujaribu kuwauliza likamwingia kichwani mwake.<br />
Philip akaliendesha gari na kuelekea upande wa pili wa barabara na kupaki pembeni kisha kulizima kabisa, akashukua ndani na kuwasogelea watu wale waliokuwa wamekusanyika kila mmoja akiongea lake.<br />
“Habari za saa hizi jamani?” Aliuliza kwa sauti ya kiume.<br />
“Salama!”<br />
“Naomba kuuliza.”<br />
“Uliza tu tunakusikiliza.”<br />
“Sijui mmefanikiwa kumwona mwanamke mmoja akipita hapa?”<br />
“Mwanamke?”<br />
“Ndiyo”<br />
“Mh! Yule si mwanamke ni mzimu.”<br />
“Mzimu?”<br />
“Ndiyo, tena umevaa shuka nyeupe, umekimbilia kuleeee,” alisema mtu mmoja huku akinyosha kidole kuelekeza upande alipoelekea Lina.<br />
“Wapi?”<br />
“Wee kaka huo mzimu unaoulizia umekwenda kule.”<br />
Maumivu makali yakauchomoa moyo wake, yalikuwa kama vile mshale wa moto, Phillip akaonekana kama mtu aliyenyeshewa na mvua, bila kujibu chochote taratibu akaingia tena ndani ya gari lake na kuanza kuondoka eneo lile bila kuuliza tena swali kwa mtu yeyote.<br />
Watu waliokuwepo katika kundi lili wakazidi kumshangaa.<br />
***<br />
“Mzee hakuna haja ya kulia nashauri tuwapeleke watoto hospitalini.”<br />
“Kufanya nini wakati wameshakufa?” Victor Fedorov aliuliza huku machozi yakimbubujika.<br />
“Hakuna aliyesema wamekufa hawa ila…”<br />
“Ila nini? Mbona mnazidi kunichanganya ninyi?”<br />
“Bosi tufuate ushauri wa watalaam,” mlinzi wa Victor aliongea akimpigapiga bosi wake sehemu za mabegani.<br />
“Sawa lakini matumaini hayapo, watoto wangu wameniacha mkiwa, Mariya na Merina wameondok…” Victor Fedorov aliangua kilio huku kwikwi ikimkaba.<br />
Kwa Victor Fedorov tajiri ambaye alivuma kupita maelezo ilionekana kama ndoto, hakuwa tayari kuamini kwamba alibaki peke yake duniani huku akiwa ametoa karibu nusu ya utajiri wake wote kuwakomboa watoto wake Mariya na Merina lakini sasa nao walikuwa wamemwacha mkiwa katika dunia ambayo hakika hakufahamu nini ingekuwa hatima yake.<br />
Utajiri wake wote aliokuwa nao sasa ulikuwa hauna maana tena.<br />
“Ngoja twende hospitali nitajua kila kitu huko,” aliwaza kichwani mwake huku akishuhudia watoto wake wakibebwa mmoja baada ya mwingine na kuingizwa ndani ya gari la wagonjwa.<br />
“Mzee kwa sababu nafasi yetu ni finyu tungeomba uendeshe gari lako ukitufuata kwa nyuma”<br />
“Hakuna shida”<br />
Victor Fedorov akafanya hivyo lakini akamwomba mlinzi wake waongozane wote kwani hakuwa katika hali nzuri. Baada ya kuhakikisha kwamba kila kitu kilikuwa sawa nyumbani hapo wakafunga milango na wote kutoka.<br />
Gari la wagonjwa lilikuwa mbele yao huku likipiga king’ora cha kuashiria hatari na wao wakiwa nyuma huku Fedorov akionekana kuzama katika lindi la mawazo.<br />
Victor Fedorov aliendesha gari sambamba kabisa na gari la wagonjwa hakutaka kuliacha hata hatua moja, hamu yake kubwa ilikuwa ni kufika hospitalini na kuona watoto wake wakifanyiwa uchunguzi maalum ambao aliamini ungerejesha majibu yakatayomfanya arejee tena katika dunia, kwani tayari alishajihesabu kwamba alikuwa ni marehemu mtarajiwa kama tu angeelezwa kwamba watoto wake Mariya na Merina hawakuwa na maisha tena.<br />
“Hapana! Sitaki wafe, nataka waishi, Mungu naomba unisaidie jambo hili, nawapenda mno watoto wangu kama kweli watakuwa wamefariki basi na mimi nitakufa, hakika watazikwa siku moja na mimi,” aliongea kwa sauti iliyomshtua mlinzi wake ambaye muda wote huo naye alikjuwa akiwafikiria watoto hao.<br />
“Hawatakufa,” mlinzi alijibu akimwangalia Fedorov.<br />
“Vruuu! Vruuu!” Sauti ilisikika</span></div><br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5188220966957500">MSICHANA NDOTONI MWANGU .......EP.83<br />
<br />
“Vruuu! Vruuu!” sauti ilisikika.<br />
Kelele za matairi ya gari yakisugua barabara zilisikika, dereva wa gari alikuwa akijitahidi kadiri ya uwezo wake kukanyaga breki ili kunusuru maisha ya mtu aliyekuwa akikatiza barabarani asubuhi hiyo.<br />
“Mungu wangu! ” Victor Fedorov aliongea macho yake yote yakimwangalia mtu huyo, hasira ya ajabu ilikuwa imemshika lakini alipok<span class="text_exposed_show">umbuka kwamba alitakiwa kuondoka eneo hilo haraka kuliwahi gari la wagonjwa lililobeba watoto wake hakuongea neno jingine zaidi, akaliwasha gari na kuondoka eneo hilo haraka.<br />
<br />
“Pole sana bosi,” mlinzi aliongea.<br />
“Ni balaa hilo limeshapita zake.”<br />
“Dah! Sijui alikuwa haoni?”<br />
“Siyo kuona tu hata king’ora hakukisikia?”<br />
“Msamehe, pengine mawazo ya maisha yamemchanganya.”<br />
<br />
“Ni kweli kabisa nimeshamsamehe, ndiyo maana sikufanya chochote zaidi ya kumwangalia tu,” aliongea Fedorov akikanyaga mafuta kulifuata gari lililobeba watoto wake ambalo halikuwa umbali mrefu sana na gari lake.<br />
<br />
Kwa mwendo wa dakika kumi nzima aliendelea kulifuata gari la wagonjwa kwa nyuma, hofu yake ikizidi kuongezeka juu ya hali ya watoto wake, na mawazo mengi yaliufunika mtima wake. Ni mlinzi ndiye aliyekuwa pembeni yake kumfariji na kumweleza kwamba kila kitu kingekwenda sawa na hakusita kumweleza wazi kwamba watoto hao hawakufa bali walikuwa katika hali ya kuzimia na muda si mrefu baada tu ya kuonana na madaktari wangepata nafuu na wote kurejea nyumbani.“Ahsante ndugu yangu, sipendi kushuhudia vifo vya watoto wangu kwani hao ndiyo ndugu pekee niliobakiza duniani, kama ikitokea wakaniacha basi na mimi sitaweza tena kuendelea kuishi dunia ya peke yangu, nitawafuata.”<br />
<br />
Maneno hayo yalipita moja kwa moja masikioni mwa mlinzi na akili yake ikauona utajiri wa Victor Fedorov mikononi mwake kwani kama ingetokea watoto wale wakawa wamefariki dunia na Victor Fedorov kujiua kama alivyokuwa akisema basi utajiri wote ungekuwa wake, aliliamini jambo hilo kwa asilimia mia moja.<br />
“Akijiua kweli basi nitakuwa mrithi wake, kwani hana ndugu huyu na kama mwenyewe alivyokiri kwa kinywa chake, utajiri huo utakuwa mikononi mwangu, ” aliongea.<br />
<br />
Ni sauti ya Fedorov iliyomshtua na kumtoa katika dimbwi hilo la mawazo.<br />
“Je,uko wapi mbona umenyamaza ghafla, umepatwa na nini?”<br />
“Ah! Bosi unajua ninakuonea huruma sana…lakini zaidi afya ya watoto…”<br />
“Watakufa?” alidakia tena Fedorov.<br />
<br />
“Mh! Kwa kweli sijui chochote mpaka sasa ngoja tufike hospitali kwanza,” aliongea mlinzi huyo akimwangalia bosi wake kwa jicho la tamaa ya utajiri.<br />
“Ongea neno wewe sasa si mlinzi tu bali ndugu yangu.”<br />
“Unasema?”<br />
“Wewe ni ndugu yangu bwana,” kauli hiyo ikazidi kumchanganya zaidi ubongo wake.<br />
<br />
“Mh! Au amenigudua? Kwa nini ameniambia kitu ninachokifikiria?” alijiuliza kimoyomoyo na haikuchukua muda mrefu sana, tayari wakawa wameshafika hospitalini ambapo haraka wote wawili baada ya kuegesha gari sehemu ya maegesho wakashuka na kuanza kukimbilia eneo la mapokezi ambako gari la wagonjwa lilionekana.<br />
“Wakikaribia eneo hilo wakashuhudia machela mbili zikisukumwa kutoka ndani na kusogezwa karibu kabisa na mlango wa gari kisha kufunguliwa na watoto wawili wakatolewa na kuweka juu yake.<br />
<br />
“Tafadhali fanyeni haraka sana tujitahidi kuokoa maisha ya wagonjwa hawa,” ilikuwa ni sauti ya daktari aliyekuwepo ndani ya gari la wagonjwa.<br />
Wakati zoezi hilo likiendelea Victor Fedorov alishafika eneo hilo na kushuhudia machela zikisukumwa kwa kasi ya ajabu kuingizwa ndani ambako naye alizifuata kwa nyuma akiwa na mlinzi wake.<br />
<br />
“Na ninyi mnakwenda wapi huku?” ilikuwa ni sauti ya mwanaume aliyesimama eneo hilo akionekana kuwa mlinzi.<br />
“Watoto wangu, hawa ni watoto wangu.”<br />
“Watoto wako?”<br />
“Ndiyo,” alijibu akikimbia kuelekea mbele.<br />
<br />
“Na wewe ni nani?”<br />
“Huyo hapo ni bosi wangu mimi ni mlinzi wake.”<br />
“Wewe unaweza kubaki hapa acha mhusika afuate nyuma, sawa?” aliuliza akimzuia mlinzi aliyekuwa ameongozana na Fedorov.<br />
Akashuhudia Fedorov na wauguzi waliokuwa wakisukuma machela wakitokomea na kumwacha hapo peke yake akiwa hajui nini cha kufanya.<br />
<br />
***<br />
“Lina! Lina! Linaaaa!” ilikuwa ni sauti ya Phillip akiita jina la mke wake.<br />
Ni sauti hiyo ndiyo iliyopenya moja kwa kwa moja masikioni mwa Lina na kumfanya ageuke kuangalia ilitokea wapi, taratibu huku akibubujikwa na machozi akageuza shingo yake na kuangalia nyuma pamoja na kwamba kulikuwa na giza lakini aliweza kuona taa za gari zikija nyuma yake kwa kasi kubwa, akasimama. ”Tafadhali simama, simama tuongee mke wangu.”<br />
<br />
“Mh! Sauti ya Phillip hiyo,” aliongea.<br />
Akiwa hapo akashuhudia gari likisimama mbele yake na mwanaume akachomoka ndani yake akikimbia kumfuata.<br />
“Nisamehe mke wangu ishara ya magoti kwako ni kuonyesha kwamba nimekukosea,” aliongea Phillip akipiga magoti mbele ya Lina.<br />
Machozi yakambubujika Lina, hasira ilikuwa imemkaba zaidi alipomshuhudia mwanaume aliyempenda kupita kiasi akiwa mbele yake kumwomba msamaha na ni huyu ndiye aliyekuwa amesababisha kutokea kwa sakata lote hilo ndani ya hoteli ya Lamada.<br />
“Umenidhalilisha Phillip.”<br />
<br />
“Nisamehe ndiyo maana niko chini ya miguu yako.”<br />
“Phillip! Phillip nyanyuka uondoke sita…” aliongea Lina akijitoa mikononi mwa Phillip ambaye muda wote huo bado alikuwa chini amepiga magoti.<br />
Kwa nguvu zake zote Lina alijaribu kujitoa kwa Phillip lakini haikuwezekana, wote wawili wakajikuta wakigalagala chini.<br />
Phillip bado aliendelea kumwomba Lina msamaha akimsihi akubaliane na ombi lake pia akubali kuingia ndani ya gari waondoke kwenda nyumbani, huko wangemaliza tofauti zao zote.<br />
<br />
“Sitaki! Sitaki nasema sitaki mbona hutaki kunielewa, kwa kitendo hiki kilichotokea leo siko tayari kukusamehe.”<br />
“Nisamehe mke wangu mimi mwenyewe ninaumia moyo.”<br />
“Phillip uumie wewe? Nakuambia umenidhalilisha na si mimi tu hata Daniel, sidhani kama atakuwa tayari kunisamehe kwa ninavyomfahamu, huko aliko anapanga jinsi ya kulipa kisasi kwangu, masikini wa Mungu haikuwa dhamira yangu kufanya yaliyotokea ni wewe ndiye umeni…” aliongea Lina na kushindwa kumalizia sentensi yake kwani kwikwi ya kulia ikamkaba zaidi.<br />
<br />
Phillip akautumia udhaifu huo wa Lina na kumbeba juujuu kama mtoto kisha kumwingiza ndani ya gari yeye pia kukimbilia upande wa pili na kuingia kisha kuliwasha na kuondoka eneo hilo kwa kasi ya ajabu, watu wote waliokuwepo eneo hilo wakishangaa kwa kitendo hicho.<br />
***<br />
“Kazi uliyonituma mzee nimemaliza na mzigo ni huu hapa,” ilisikika sauti ndani ya chumba kidogo ndani yake, mwanga hafifu wa taa ulionekana na mzee mfupi akiwa ameketi pembezoni kabisa mwa chumba hicho akaonekana.</span></div></span></div><span class="fcg"></span><br />
<br />
<br />
<br />
<div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff517dcb7b96649832">MSICHANA NDOTONI MWANGU .......EP.84<br />
<br />
“Haraka wapelekeni chumba cha wagonjwa mahututi,” ilikuwa ni sauti ya mwanaume aliyekuwa kwenye korido ambaye kwa kumwangalia tu ilitosha kugundua kwamba ni daktari.<br />
<br />
Bila kusema kitu chochote, machela zote mbili zikaanza kusukumwa kupelekwa chumba cha wagonjwa mahututi huku Victor Fedorov naye akifuata kwa nyuma. Akili yake haikuonekana kufanya kazi kwa mate<span class="text_exposed_show">so aliyokuwa akiyashuhudia mbele yake, aliiona dunia haina maana kwake.<br />
<br />
“Nisaidie jamani watoto wangu wasife, hawa ndiyo ndugu pekee niliobakiza duniani, bila hawa hata utajiri wote nilionao mimi si kitu, niko tayari kutoa kiasi chochote cha fedha lakini ilimradi watoto wangu waokolewe…” alisema mfululizo.<br />
Hakuwepo mtu hata mmoja aliyeweza kuongea kwa wakati huo, si wauguzi wala madaktari, wote walikuwa na hofu kubwa juu ya maisha ya watoto hao. Hatimaye dakika tatu tu baadaye machela mbili ziliwasili nje ya wodi kubwa, Victor Fedorov akashuhudia maneno ICU juu ya mlango wa wodi hiyo.<br />
<br />
”Oh! My God!”(Oh! Mungu wangu!) alisema.<br />
“Shaka ondoa mzee, wanaingia kwenye chumba cha usalama, kila kitu kitakuwa sawa,” alisema muuguzi mmoja huku akimwangalia Fedorov kwa macho ya huruma.<br />
“Watapona kweli?”<br />
“Mh! Watapona.”<br />
<br />
“Mbona umeonesha kusita dada?”<br />
“Tuombe Mungu kwani mpaka sasa hatufahamu vyema tatizo linalowasumbua.”<br />
Wakiwa hapo, mlango ukafunguliwa na machela zote mbili zikaingizwa ndani na kumwacha Fedorov peke yake nje akiwa haelewi nini cha kufanya, akawa analia huku akizungusha macho yake huku na kule. Pembeni kabisa ya wodi aliuona msingi, pamoja na kwamba juu yake paliandikwa kuwa si ruhusa kukaa yeye alinyoosha moja kwa moja na kwenda kuketi juu yake.<br />
<br />
“Nitakaa hapahapa nikisubiri matokeo, siwezi kwenda mbali, moyo wangu umegubikwa na hofu kupindukia… masikini Mariya na Merina! Nimejitahidi kuokoa maisha yenu wanangu lakini naona Mungu hakupanga jambo hili, hakupanga muendelee kubaki na mimi baba yenu! Bora ningewaacha tu Tanzania pengine yote haya yasingetokea… lakini hapana ninyi ni sehemu ya damu yangu, isingekuwa rahisi kufanya hivyo,” Fedorov alikuwa akijisemea huku picha ya jinsi alivyotoa mbegu zake za kiume na kuziuza kwa familia ya Phillip na Genevieve ikijirudia kichwani mwake. Alikumbuka pia fedha nyingi alizotoa kwa ajili ya malipo kwa Ditrov ya kuwateka watoto hao kutoka mikononi mwa Phillip na kuwaleta nchini Urusi, hakutaka kuamini kuwa sasa walikuwa katika hali mbaya kiasi kile.<br />
<br />
Akiwa katika dimbwi hilo la mawazo, ghafla akasikia mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi ukifunguliwa na wauguzi wawili wakatoka mbio wakikimbia. Alipojaribu kuwafuata ili aongee nao na kufahamu hali za watoto wake, walimzuia na kumweleza kwamba walikuwa na haraka sana hivyo aendelee kusubiri eneo hilo mpaka watakaporejea.<br />
“Hatuwezi kukusikiliza, kuna jambo muhimu sana linatakiwa kufanyika sasa hivi.”<br />
“Nataka kujua hali za wanangu… nisaidieni jamani… akili yangu haifanyi kazi vizuri,” alisema mfululizo lakini tayari wauguzi hao walishaondoka na kumwacha hapo.<br />
<br />
Haikuchukua hata dakika tano, kwa mbali akawashuhudia tena wauguzi wale wakirejea, lakini safari hii wakisukuma vitu viwili kama mitungi mikubwa. Akili yake ikafanya kazi haraka na kugundua kwamba ilikuwa ni mitungi yenye hewa safi ya Oksijeni.<br />
“Hii si mitungi ya gesi kweli?”alijiuliza huku akikodoa macho kuangalia.<br />
Hakukosea, ilikuwa ni mitungi ya hewa ya oksijeni ikisukumwa kuingizwa ndani ya wodi ya wagonjwa mahututi, Fedorov akalia kwa uchungu.<br />
<br />
“Hali imekuwa mbaya mpaka wanawekewa hii?” aliuliza huku machozi yakibubujika mashavuni mwake. Kwa hali aliyoiona alizidi kukata tamaa ya kuwaona tena watoto wake wakiwa hai kwani mara kadhaa wagonjwa wengi waliowekewa hewa hivyo hawakuishi muda mrefu.<br />
“Ni kweli lakini yakupasa uwe mvumilivu, utaelezwa kila kitu kinachoendelea baadaye…” walisema wauguzi wale na kusukuma mitungi hiyo kuingia ndani ya wodi.<br />
<br />
Fedorov akalisikia jasho jembamba likitiririka mwilini mwake taratibu huku akiwa hajui nini cha kufanya, akajikongoja na kusogea pembeni huku moyoni mwake akiwaza jambo moja tu, kubaki hapo mpaka mwisho.<br />
“Sitaondoka, nitakaa hapa kusubiri,” alisema.<br />
***<br />
“Puuuh!”<br />
Ulikuwa ni mlio wa kitu kikirushwa juu ya meza.<br />
Mzee mfupi mwenye mwili uliojazia kisawasawa, huku akitabasamu alinyanyuka kwenye kiti na kusogea karibu na meza ambayo juu yake ilikuwa na mzigo.<br />
“Umeifanya vyema kazi hii,” alisema huku akipadisha suruali yake vizuri.<br />
“Bila shaka mzee, hakuna tatizo juu ya hilo?”<br />
<br />
“Una uhakika na maelezo yako kijana?” Sauti nzito ya mzee huyo ikasikika tena, safari hii akimzunguka kijana huyo kila upande na kukagua mifuko yote ya suruali yake akimtaka kusalimisha silaha yoyote aliyokuwa nayo juu ya meza.<br />
Bila kusema kitu chochote, kijana yule, huku akionesha kujiamini aliweka silaha zote mezani na alipomaliza aliachia kicheko.<br />
“Kwa nini unacheka?” aliuliza.<br />
“Bosi, inavyoonekana huniamini hata kidogo.”<br />
<br />
“Uaminifu wangu umesafiri mbali sana na sidhani kama utarejea leo kwa mchezo mbaya niliofanyiwa huko nyuma, sipo tayari kumwamini mtu yeyote tena maishani mwangu, labda roho yangu tu. Teh!Teh! Teh!” alimaliza mzee huyo kwa kicheko cha kejeli.<br />
“Hata mimi kijana wako?”<br />
“Nilichosema ndiyo hicho,”alisema huku akiendelea kuzungukazunguka ndani ya chumba hicho.<br />
<br />
“Sawa nimekuelewa bosi wangu, ni vyema ukanipatia mgao wangu na mimi niondoke kuendelea na masuala mengine.”<br />
“Naweza kuuliza tena?”<br />
“Bila shaka?”<br />
“Hukuua wala kujeruhi?”<br />
“La hasha!”<br />
<br />
“Watoto wote wawili wapo salama?” aliuliza mzee huyo akikodoa macho kumwangalia kijana aliyesimama mbele yake.<br />
“Mh!”<br />
“Unaguna nini?”<br />
“Nauliza tena wako salama?”<br />
“Baada ya kupata mzigo huu niliwarusha kutoka ndani ya gari langu mpaka chini, mmoja baada ya mwingine na mimi kuondoka eneo hilo haraka bila kuangalia nyuma... lakini pia…” kigugumizi cha ghafla kikamshika kijana huyo na kushindwa kumalizia sentensi yake.<br />
<br />
“Lakini nini? Umewaua?”aliuliza mzee huyo, safari hii kwa ukali.<br />
“Hawajafa ila hali zao ni mba…ya sijui kama wataiona ke…sho?”<br />
“Kwa nini?”<br />
“Niliwa…” alisema kijana huyo huku akitetemeka.<br />
<br />
“Unasema?” lilikuwa ni swali kutoka kwa mzee aliyekuwepo ndani ya chumba, bila huruma akaikamata vyema bastola iliyokuwa juu ya meza, akainyoosha na kulielekea paji la uso wa kijana aliyesimama mbele yake.</span></div></span></div><span class="fcg"></span><br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100">MSICHANA NDOTONI MWANGU .......EP.85<br />
<br />
KWA muda wa saa tatu mfululizo bado aliendelea kusimama nje ya chumba cha wagonjwa mahututi, macho yake yote yakielekezwa kwenye mlango huo ili kuona mtu ambaye angetoka na yeye kuweza kumuuliza nini kiliendelea kwa watoto wake Mariya na Merina.<br />
Victor Fedorov alikuwa ni mwanaume wa shoka lakini sasa alianza kuonyesha udhaifu wake kwani mpaka wakati huo tayar<span class="text_exposed_show">i alishakata tamaa, moyo wake ulimuuma kupita kiasi, akasikiliza sauti ndani yake ikimlaumu kwa kitendo chake cha kuwateka watoto hao kutoka Tanzania na kuwaleta nchini Urusi na sasa walikuwa wakifa bila hatia.<br />
<br />
Saa nne ilipogonga akaushuhudia mlango wa chumba hicho ukifunguliwa na kushuhudia machela ikisukumwa kutoka ndani ya wodi kwenda nje, juu yake ikionekana kulazwa mtu aliyefunikwa na shuka la kijani kuanzia kichwani mpaka miguuni, hofu kwamba tayari kulikuwa na tatizo ikaugubika moyo wake.<br />
“Mh!” aliguna akikimbia kuisogelea.<br />
“Unakwenda wapi?” sauti ya muuguzi ilisikika ikimuuliza.<br />
<br />
“Nataka nione hapo,” aliongea akinyoosha kidole chake cha shahada kuelekea ilipokuwa machela.<br />
“Kaka samahani sana sheria yetu ya kazi hairuhusu kufanya hivyo,” muuguzi huyo alijibu na tayari walishaanza kusukuma tena machela kuondoka eneo hilo, Victor Fedorov naye akifuata nyuma huku akilia.<br />
“Dada tafadhali niruhusu nimwone huyo aliyelala hapo nataka nijue tu pengine ni mwanangu.”<br />
“Mwanao?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Lakini hatuna ruhusa ya kufanya hivyo, kaka yangu, utanifanya nifukuzwe kazi.”<br />
“Nionee huruma.”<br />
“Hapana,” alijibu muuguzi huyo na kwa kasi ya ajabu akaisukuma machela kuondoka eneo hilo kuelekea chumba cha kuhifadhia maiti, Victor Fedorov akaangua kilio na kushuhudia machela hiyo ikizama ndani.<br />
Akaamini kwamba hakika mmoja wa watoto wake tayari alikuwa ameaga dunia.<br />
<br />
***<br />
“Nataka kuondoka na nitakuachia kila kitu ndani ya nyumba hii.”<br />
“Uende wapi mke wangu wewe ndiye wangu wa maisha.”<br />
“Nimeshachoka huwezi kunidhalilisha kiasi hicho halafu ukadai kwamba unanipenda.”<br />
“Chukua maneno yangu na uyafanyie kazi, wewe mwenyewe unafahamu ni jinsi gani ninavyokupenda.”<br />
“Mh! Unaniona mimi mjinga? Hivi unafikiri mimi mtoto, unanichapa halafu unanibembeleza kwa pipi?” aliuliza Lina akizidi kukusanya nguo zake na kuzitupia ndani ya sanduku.<br />
<br />
“Haiko haja ya wewe kuondoka, hapa ni kwako acha mimi niondoke.”<br />
Tayari Lina alishanyanyua sanduku akatembea na kuusogelea mlango wa chumba chao na kuufungua ili atoke nje.<br />
“Hapana mpenzi, tafadhali nisemehe hamu ya kuitwa baba ndiyo ilinifikisha hapo.”<br />
“Basi mtafute mwanamke mwingine ambaye atakubali kufanya unayotaka.”<br />
<br />
Ukimya wa ajabu ukatokea kati yao Phillip aliyekuwa amepiga magoti chini akakimbia na kulikamata sanduku la Lina huku akimsihi asifanye maamuzi kama hayo, lakini zoezi hilo lilionekana kushindikana na kujikuta akiambulia teke kutoka kwa mwanamke huyo.<br />
Hasira ya Lina ilionekana wazi, si kwamba kweli hakumpenda Phillip bali alimpenda kwa dhati lakini hakuwa tayari kukutana kimwili na mwanaume mwingine ili kupata ujauzito hivyo kitendo cha Phillip kulazimisha jambo hilo ndicho kilisababisha machafuko hayo kutokea ndani ya nyumba yao.<br />
<br />
“Umenidhalilisha sana ni wapi nitaficha uso wangu pale nitakapokutana na Daniel? Hivi huoni umenijengea uadui mkubwa sana? Kwa hilo siko tayari kukusamehe Phillip, mimi naondoka tutaonana tena kama si hapa duniani basi akhera,” aliongea Lina kwa sauti ya upole huku akifungua mlango wa sebuleni na kutoka nje.<br />
“Nakupenda mke wangu, ni shetani aliingilia kati penzi letu na kunipa akili isiyofaa.”<br />
“Eti shetani, usimsingizie bure huyo shetani ni wewe mwenyewe.”<br />
“Basi nakubali mke wangu nisamehe, tafadhali rudisha penzi lako kwangu tuanze upya, tukipanga ni namna gani tufanye ili tupate angalau mtoto mmoja.”<br />
<br />
“Phillip sahau jambo hilo halipo tena,” aliongea Lina akiingia ndani ya gari tayari kuondoka eneo hilo.<br />
“Hatanii, nikimwacha akaondoka nitamkosa nami sipo tayari,” aliongea Phillip na haraka akili ikamjia kichwani mwake, ili kumzuia Lina ni lazima aende na kulala mbele ya lango la kutokea.<br />
Haraka akatoka mbio na kwenda kujitupa katikati ya lango kuu la nyumba hiyo na kutulia kimya.<br />
<br />
Wakati yote hayo yakitokea Lina akiwa ndani ya gari lake akaliwasha na kuanza kurudi nyuma kwa kasi ya ajabu bila kuangalia. Kilichofuatia ni sauti ya mayowe iliyopigwa na mlinzi wa nyumba yao.<br />
“Mungu wangu utauaaa! Utauaaa!” ni sauti hiyo ndiyo iliyomfanya Lina afunge breki za gari kwa nguvu na kushuka kuangalia ni kitu gani kilikuwa kimetokea.<br />
“Phillip unafanya nini? Unataka nikugonge halafu nipate kesi?”<br />
<br />
“ Bora iwe hivyo kuliko kuondoka.”<br />
“Sikia wewe ni mtu mzima sasa tafadhali ondoka ili mimi nipite.”<br />
“Sitaondoka hapa mpaka utakaponipa msamaha wako.”<br />
“Unasema?”<br />
<br />
“Lina umesikia nini, nasema sina haja ya kurudia.”<br />
“Unacheza na mimi, wewe hufahamu kwamba siku zote ulikuwa ukiishi na mwanamke Mafia? Leo utanifahamu mimi ni nani? Naapa nitaondoka kwa nguvu wala sitanii...sasa kaa hapo ushuhudie ninavyoondoka. Pumbavu mkubwa wewe.”<br />
***<br />
“Kwa nini?”<br />
“Niliwa…” alisema kijana huyo huku akitetemeka.<br />
“Unasema?” lilikuwa ni swali kutoka kwa mzee aliyekuwepo ndani ya chumba, bila huruma akaikamata vyema bastola iliyokuwa juu ya meza, akainyosha na kulielekea paji la uso wa kijana aliyesimama mbele yake. Kwa alivyomfahamu mzee huyo hakika alikuwa hatanii alimaanisha alichokifanya, hofu ikaugubika moyo wake, akiwa haelewi nini cha kufanya akasikia kitu kama mkojo kikipenya kutoka ndani ya suruali yake.<br />
<br />
“Nisemehe mzee wangu.”<br />
“Nataka kufahamu ni kitu gani kiliendelea kwa watoto.”<br />
“Hawajafa, nina hakika watakuwa hai japo hali zao sielewi zinaendeleaje?”<br />
“Uliwapa nini?”<br />
“Mh!” kijana aliguna.<br />
“Husemi? Sasa nitakuonyesha mimi ni nani.”<br />
<br />
“Hapana! Nipe muda nitakueleza.”<br />
Mzee aliyekuwa ameiweka bastola kwenye paji la kijana aliyesimama mbele yake, taratibu huku akitabasamu akaishusha bastola hiyo chini.<br />
“Fyuuuu!” kijana alishusha pumzi.<br />
“Ninakupa dakika mbili tu kuanzia sasa uwe tayari kueleza kilichowapata watoto vinginevyo leo utani…” aliongea mzee huyo akiiweka vyema bastola yake.<br />
<br />
Dakika mbili zikakatika bila kijana huyo kufungua mdomo kusema neno lolote, jambo hilo ndilo lililomtia hasira mzee aliyekuwa amesimama ndani ya chumba hicho kidogo, akasogea karibu kabisa na kuiweka tena bastola juu ya paji la kijana huyo na haikuchukua hata sekunde mbili mlio wa bastola ukasika.<br />
“Paa! Paaa!” kicheko kikafuatia nyuma yake.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? <br />
N:B JITAHIDINI KUINGIA BLOG INAINGILIKA HATA KWA SIMU ZA KAWAIDA JAMANI, KWANI KUNA MASTORY YA KUFA MTU NA MIMI MUDA WANGU MDOGO HAUTOSHI NINGEPOST HUKU NA HUKU, NAWAPENDA SAAANA!!</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.86.<br />
<br />
MAMBO yanazidi kwenda mrama kwa Phillip ambaye kwa nguvu zake zote amejitahidi kumwomba mkewe Lina msamaha ili amsamehe na kuendelea na maisha lakini inaonekana kushindikana. Lina ameingia ndani ya chumba na kukusanya nguo zake kisha kuziweka ndani ya sanduku, anamwambia Phillip kwamba anaondoka mahali hapo na kumwachia kila kitu.<br />
<br />
Jambo hilo linaonekana kuwa gu<span class="text_exposed_show">mu kwa mwanaume huyo, akiwa hapo anamshuhudia Lina akitoka kuelekea nje, naye anamfuata kwa nyuma huku akiendelea kumsihi na kumwomba radhi kwa yote yaliyotokea. Anaingia ndani ya gari na kuliwasha kisha kuliendesha kuelekea langoni bila kufahamu kwamba tayari Phillip amefika eneo hilo na kulala usawa wa lango hilo, lengo kubwa likiwa ni kumzuia asiondoke.<br />
<br />
Upande wa pili wa hadithi hii, tunamwona mwanaume mmoja ndani ya chumba akiwa na kijana, baada ya maongezi ya muda mrefu mtafaruku unatokea na mzee huyo anataka kufahamu ni kitu gani kiliwapata watoto wawili pacha ambao walitekwa na kijana huyo kwa lengo la kujipatia fedha kutoka kwa baba yao tajiri, Victor Fedorov.<br />
“Ninakupa dakika mbili tu kuanzia sasa uwe tayari kueleza kilichowapata watoto, vinginevyo leo utani…” alisema mzee huyo huku akiiweka vyema bastola yake.<br />
<br />
Dakika mbili zikakatika bila kijana huyo kufungua mdomo wake kusema neno lolote. Ni jambo hilo ndilo lililomtia hasira mzee aliyekuwa amesimama ndani ya chumba hicho kidogo, akasogea karibu kabisa na kuiweka tena bastola juu ya paji la uso la kijana huyo, haikupita hata sekunde mbili, mlio wa bastola ukasika ndani ya chumba.<br />
“Paa! Paaa!” kicheko kikafuatia nyuma yake.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
<br />
“Unacheza na mimi wewe, hivi hufahamu kwamba siku zote ulikuwa ukiishi na mwanamke Mafia? Leo utanifahamu mimi ni nani? Naapa nitaondoka kwa nguvu zangu, wala sitanii! Kaa hapohapo ushuhudie ninavyoondoka. Pumbavu mkubwa wewe,” alisema Lina huku akitembea kwa kasi kulielekea gari na kuingia ndani yake.<br />
“Bora unikanyage nife lakini sipo tayari kukuacha uondoke, nakupenda sana Lina, mambo yote haya yaliyotokea ni Shetani tu.<br />
<br />
“Eti Shetani? Shetani ni wewe mwenyewe, hebu ondoka mimi nipite.”<br />
Phillip aliendelea kulala chini huku akilia, hakuwa tayari kushuhudia mwanamke aliyempenda akiondoka mbele ya macho yake. Ghafla akiwa hapo, taswira ya Genevieve mkewe ikamjia, watoto wake wawili, Dorice na Dorica nao pia wakapita kichwani mwake kama sinema kali, machozi yakazidi kumbubujika.<br />
<br />
“Bora nife niwafuate …” alisema Phillip, safari hii kwa sauti.<br />
“Bosi kuna kitu gani kimetokea? Mbona mnanichanganya?” mlinzi aliuliza.<br />
“Haya mambo hayakuhusu, ni vyema ukaachana nayo na wewe kuendelea na shughuli zako.”<br />
“Lakini mimi ni mmoja wa watu wa familia hii?”<br />
<br />
“Ondoka kafanye kazi, husikii?” aliuliza Phillip safari hii kwa ukali.<br />
Taratibu bila kusema kitu, alianza kutembea kuondoka eneo hilo na kusogea pembeni ambako aliendelea kutupa macho yake na kumwona Phillip akiwa bado hajabadilisha uamuzi wake wa kuendelea kulala eneo lilelile.<br />
“Akifanya mchezo huyu mwanamke atamkanyaga kweli, kwa inavyoonekana wana ugomvi mkubwa sana hawa, lakini ni wa nini?<br />
<br />
Mbona walitoka wote? Lakini mwanamke amerudi akiwa amejifunika shuka mwilini mwake? Mh! Hakyanani vile, kuna kitu kikubwa hapa kimetokea…” mlinzi aliendelea kuwaza kichwani mwake, yeye pia alishaanza kuhofia kibarua chake, alifahamu wazi kuwa kama kweli Lina aongeondoka, basi ajira yake ingekuwa matatani.<br />
Akalishuhudia gari likija kwa kasi ya ajabu kuelekea eneo hilo, alipoangalia vizuri kuona kama bosi wake Phillip alikuwa ameondoka, alishangaa kumuona akiwa bado amelala eneo lilelile bila kusogea.<br />
***<br />
Machela iliyokuwa ikisukumwa na kuingizwa chumba cha maiti ilimtia hofu sana Victor Fedorov, kichwani mwake hakuwa na picha kamili ya nini kingefuata baada ya hapo, mawazo mengi yakaufunika ubongo wake.<br />
“Sijui itakuwa nini? Lakini ngoja nirudi kule wodini, najua nitapata jibu kamili,” alisema mzee huyo na kuanza kutoka mbio kuondoka eneo hilo.<br />
<br />
Kwa dakika tatu nzima, aliendelea kukimbia hatimaye akakifikia chumba cha wagonjwa mahututi, akaweka kambi hapo kusubiri mtu ambaye angetoka eneo hilo na kumweleza ukweli juu ya afya za watoto wake na nini kilitokea.<br />
Kwa takribani dakika tano nzima, aliendelea kuketi eneo hilo, ghafla macho yake yakaushuhudia mlango wa chumba hicho ukifunguliwa na mtu aliyevalia koti jeupe akatokeza nje.<br />
“Ni daktari,”alisema.<br />
Mwanaume huyo akatembea kuelekea eneo alilokuwa ameketi Victor Fedorov na kumsabahi kisha kuanza kumuuliza maswali machache.<br />
<br />
“Kama sijakosea nadhani wewe ndiye baba wa watoto wale wawili?’<br />
“Eh! Ndiyo kabisa.”<br />
“Naweza kufahamu umekuja na nani?”<br />
“Mimi?”<br />
“Ndiyo mzee.”<br />
“Mh! Mh! Kwani kuna kitu gani daktari?”<br />
<br />
“Ni vyema nikafahamu, umekuja hapa na nani?”<br />
Swali hilo likaingia moja kwa moja masikioni mwa Fedorov na kwenda kugonga sehemu fulani ya ubongo wake. Akiwa hapo akanyanyua macho na kumwangalia daktari ambaye bado aliendelea kusimama pembeni akimwangalia.<br />
“Daktari?” aliita.<br />
“Ndiyo mzee.”<br />
<br />
“Nieleze ukweli, nini kimetokea ndani ya chumba hicho kwani muda mfupi uliopita nikiwa hapa nimeshuhudia machela ikipitishwa hapa kuelekea chumba cha kuhifadhia maiti na juu yake kwa nilivyoona kuna mtu…”<br />
“Si kazi yako hiyo mzee, hebu nijibu swali langu.”<br />
Victor Fedorov hakujibu tena kitu, akainamisha kichwa chake chini, hakuwa tayari kusikia kwamba mmoja kati ya watoto wake alikuwa ameaga dunia.<br />
“Tafadhali naomba kufahamu kuna ujumbe muhimu nataka kuutoa kwenu.”<br />
<br />
“Ninaye mlinzi wangu kule mapokezi.”<br />
“Tunaweza kuongozana?”<br />
“Hakuna shida,” alijibu Fedorov akitetemeka.<br />
Bila kuongea tena kitu chochote na daktari huyo, taratibu akaanza kutembea akimfuata nyuma. Hofu yake ikazidi kuongezeka kwani kitendo cha kuulizwa kwamba alikuja na nani hospitalini hapo kilizidi kumtia hofu, mambo mengi yakazunguka kichwani mwake bila kujua cha kufanya.<br />
<br />
“Nitapokea majibu yoyote nitakayopewa lakini si ya vifo vya watoto wangu.”<br />
Akiwa katika mawazo hayo ni sauti ya daktari ndiyo iliyomshtua, alikuwa akimuuliza yu wapi mtu aliyeambatana naye.<br />
“He! Kumbe tumefika mapokezi?”aliuliza.<br />
“Mzee akili yako iko wapi?” Daktari alimuuliza huku akimpigapiga mgongoni.<br />
“Yule paleee!”alinyoosha kidole chake cha shahada kuelekeza eneo alilokuwa ameketi kijana mmoja, haraka wote wawili wakatembea na kufika eneo hilo.<br />
<br />
“Habari yako?”<br />
“Nzuri tu.”<br />
“Nadhani wewe ni mmoja kati ya watu waliokuja na mzee huyu hapa kwetu.”<br />
“Ndiyo, ni bosi wangu huyu.”<br />
<br />
“Ni vyema tukaongozana wote mpaka ofisini kwangu, ningependa kuongea na ninyi kuhusu watoto waliofikishwa hapa asubuhi hii.”<br />
“Nini kimetokea? Hali zao zikoje? Wame…” Victor Fedorov aliuliza maswali mfululizo na alipotupa macho yake kumwangalia daktari aliyesimama mbele yake, aligundua kitu fulani katika macho yake.<br />
***<br />
“Piiii!Piiiii!Piiiii!” ilikuwa ni honi ya gari ikipiga kuomba kupishwa eneo hilo lakini mtu aliyeonekana kulala chini bado hakushtuka wala kujitingisha.<br />
“Mungu wangu! Mama yangu weee! Ayaaaa! Tayari ameua...” ilikuwa ni sauti ya mlinzi wa Lina akiwa pembezoni kabisa mwa kibanda kidogo karibu kabisa na lango la kutokea.<br />
“Nakufaaaaa!” Ndiyo sauti pekee iliyosikika.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.87<br />
<br />
UNAUA! Unaua! Mama yangu weee! Dah!”<br />
Ni sauti hiyo ndiyo iliyopenya moja kwa moja masikioni mwa Lina akiwa ndani ya gari lake huku akionekana kuwa mwenye hasira nyingi, hakuwa na habari kabisa kwamba wakati anamweleza Phillip kuhusu kuondoka eneo hilo hakufanya hivyo, aliendelea kubaki palepale.<br />
“Whaat?”(Nini?) alijiuliza baada ya kugeuka na kumwona mlinzi wake a<span class="text_exposed_show">kishika mikono kichwani huku akikimbia kuelekea langoni.<br />
<br />
Akiwa ndani ya gari huku akiwa haelewi nini cha kufanya, alimshuhudia mlinzi akiruka kutoka kwenye kibanda chake na kuruka kuelekea mbele ya gari lake.<br />
Bila kujiuliza akashuka haraka na kuugana na mlinzi wake, akamshuhudia Phillip akiwa chini ya gari. Alipomwangalia vizuri aligundua alikuwa akilia.<br />
“Niue! Nasema niue siko tayari kukuruhusu uondoke hapa na kuniacha peke yangu.”<br />
<br />
Maneno yale yakapenya tena moja kwa moja masikioni mwa Lina, naye akaangua kilio kama mtoto mdogo, akainama na kupiga magoti huku akimbembeleza Phillip atoke chini ya uvungu wa gari ili waongee.<br />
“Unasema kweli?”<br />
“Hakika nakuambia.”<br />
“Huwezi kunidanganya?”<br />
“Mimi? Nakupenda sana Phillip,” aliongea Lina akimshika Phillip mkono kumsaidia kutoka chini ya uvungu wa gari.<br />
<br />
Kwa takribani dakika tano nzima Phillip aliendelea kulala chini ya gari hata Lina alipombembeleza bado hakuwa tayari kuamini maneno yake, alichukulia kama yalikuwa ni gia ya kumtoa yeye ili apate nafasi ya kuondoka na kumwacha salama bila majeraha.<br />
Baada ya Lina kuona ameshindwa kumtoa Phillip, aliamua kumtumia mlinzi ambaye alikuwepo eneo hilo akatumia ushawishi wake wote ili kumtoa Phillip lakini naye hakufanikiwa.<br />
“Lina!” Phillip aliita.<br />
“Ukitaka nitoke hapa nipatie funguo za gari.”<br />
<br />
“Hicho tu?”<br />
“Ukifanya hivyo naweza kutoka.”<br />
“Basi chukua huu hapa,” Lina alijibu akinyoosha mkono uliokuwa na funguo kumwelekea Phillip ambaye aliunyakua kwa nguvu kama vile mwewe anyakuavyo kifaranga cha kuku akiwa haamini kinachotokea, akachomoza na kuketi kitako pembeni kidogo tu mwa Lina.<br />
“Nisamehe mke wangu.”<br />
“Nimekusamehe toka zamani sana twende ndani,” aliongea Lina akimshika Phillip mkono na kumnyanyua kutoka chini na wote wakaongozana kwenda chumbani kwao.<br />
<br />
Walipoingia tu, Lina hakuwa na mazungumzo mengine zaidi akamkamata Phillip kwa nguvu zake zote na kuanza kumvua nguo moja baada ya nyingine huku akimmiminia mabusu motomoto na alipomaliza akazikamata pia nguo zake na kuzitupa pembeni wote wawili wakabaki kama walivyozaliwa na kazi ikawa ni moja tu.<br />
Ndani ya chumba ni sauti pekee ya miguno na mihemo ya mahaba iliyosikika kila mmoja akionyesha ufundi wake kwa mwenzake, mara kadhaa Phillip akiendelea kumwomba mkewe msamaha kwa mambo yote yaliyotokea na kumweleza wazi kwamba alimpenda kwa dhati.<br />
<br />
“Je, ulifanikiwa kufanya tendo la ndoa na yule mwanaume?”<br />
“Mh!” Lina aliguna.<br />
“Nieleze mpenzi wangu ili nitoe dukuduku lililoko ndani ya moyo wangu.”<br />
“Kwa nini unauliza hivyo? Na kama je ilitokea nikafanya hivyo utaniacha?”<br />
Lilikuwa ni swali gumu kutoka kwa Lina kwenda kwa Phillip ambaye alikuwa kimya juu ya kitanda mikono yake ikiendelea kuupapasa mwili wa Lina.<br />
<br />
Kwa muda wa saa nne mfululizo bado walikuwa juu ya kitanda wakibadilisha staili kutoka moja kwenda nyingine ili mradi kila mmoja wao alikuwa akisikia raha.<br />
“Mpenzi hebu tupumzike kidogo mwili hauna nguvu kabisa.”<br />
“Unasema?” Phillip aliuliza.<br />
<br />
“Nimecho…kaaa,” aliongea Lina akitetemeka.<br />
“Bado nataka leo nikuonyesha ufundi wangu wote, nadhani utaamini maneno yangu kwamba ninakupenda.”<br />
“Ashhhhh! Ashhhhh! Hapa…na,” Lina alizidi kulalama kitandani.<br />
Kwa jinsi zoezi lilivyokuwa kwa Lina ilionekana ni pata shika nguo kuchanika, Phillip hakuwa tayari kumwachia Lina kwani alipania kumuonesha ufundi wake wote.<br />
<br />
***<br />
Victor Fedorov alisimama ndani ya chumba cha daktari akitetemeka mwili mzima, hakuelewa mpaka wakati huo ni ujumbe gani ambao daktari alikuwa akienda kuutoa kwao, hofu ya kwamba mmoja kati ya watoto wake alikuwa ameaga dunia hakuwa tayari kuupokea.<br />
“Daktari hebu nenda moja kwa moja kwenye ujumbe wako.”<br />
“Tafadhali naomba mketi kwanza.”<br />
“Haipo haja, tueleze tu tukiwa wima.”<br />
<br />
“Mh! Unajua ninyi sasa ni watu wazima yawapasa kukubali na kuelewa nini kinaendelea mpaka sasa,” Daktari aliongea na kutulia kidogo kisha kuendelea.<br />
“Kikubwa kilichonifanya niwaite ndani ya chumba hiki ni juu ya hali za watoto wenu ambao mpaka saa wako chumba cha wagonjwa mahututi wakipatiwa matibabu lakini…”<br />
“Fyuuuuu!” Victor Fedorov alishusha pumzi.<br />
<br />
“Kutokana na hali zao kuwa mbaya na sisi kama madaktari tumejitahidi kadiri ya uwezo wetu wote kuokoa maisha yao lakini hali inaonekana kuwa tete hivyo basi, ni vyema nikawashauri kuwahamisha kwenda katika hospitali kubwa zaidi pengine huko mnaweza kufanikiwa.”<br />
“Daktari kwani wanawasumbuliwa na kitu gani?”<br />
“Kwa inavyoonekana kama siyo njaa basi watakuwa wamepewa sumu.”<br />
“Sumu?”<br />
<br />
“Inavyoonekana.”<br />
“Mungu wangu walitenda ubaya gani watoto hawa mpaka kustahili adhabu hiyo?” Mlinzi wa Victor Fedorov aliuliza.<br />
“Nadhani sasa si wakati wa kuuliza hayo ni vyema mkafanya utaratibu na kuwahamisha haraka iwezekanavyo,” alimaliza daktari huyo huku macho yake yakimwangalia Victor Fedorov ambaye muda wote alinyamaza kimya akionekana mwenye mawazo mengi kichwani.<br />
<br />
***<br />
Central Clinical Hospital ndiyo ilikuwa hospitali iliyokuwa na sifa kila kona ya nchi ya Urusi na ilisifika zaidi kwa watendaji wake wa kazi, kuanzia madaktari, wauguzi na watu wengine wote waliofanya kazi ndani ya hospitali hiyo. Huko ndiko daktari aliyekuwa akiwahudumia watoto wa Victor Fedorov alishauri wapelekwe kwani aliamini kwamba kufika katika hospitali hiyo kungeweza kunusuru maisha ya watoto hao.<br />
“Huko mtapata kila kilicho kizuri, madaktari, wauguzi na hata huduma ili mradi tu uwe na fedha.”<br />
<br />
“Ahsante,” alijibu Victor Fedorov akimfuata daktari kwa nyuma mawazo yake yote yakahama kutoka eneo hilo na kwenda moja kwa moja kwa watoto wake, hao ndiyo walikuwa ni kila kitu kwake.<br />
Maandalizi yakafanyika haraka, gari maalumu la wagonjwa likaandaliwa na watoto wakatolewa chumba cha wagonjwa mahututi huku mashine ya hewa ya oksijeni ikiwa imefungwa kwa kila mmoja wao, hakika kwa kuwaangalia iliumiza sana, walilala kimya kitandani bila kujitambua.<br />
Victor Fedorov akashindwa kuvumilia, akamwaga machozi mfululizo.<br />
<br />
Je, watoto hao watapona au watakufa? Nini kinaendelea kwa Phillip na Lina?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.88<br />
<br />
“Haraka wapelekeni chumba cha daktari,” muuguzi aliyekuwa ameongozana na watoto wa tajiri Victor Fedorov kutoka katika hospitali ya awali kwenda Central Clinical Hospital alisema baada tu ya machela mbili zilizowabeba watoto wake kuteremshwa kutoka garini.<br />
Kwa jinsi hali ilivyokuwa, watoto hao walihitajika kuingia moja kwa moja kwenye chumba cha daktari bila kusu<span class="text_exposed_show">biri utaratibu mwingine. Haikuchukua hata sekunde tano wakawa tayari wamewasili ndani ya chumba cha daktari.<br />
<br />
<br />
“Nini tatizo?”<br />
“Wagonjwa sana.”<br />
“Naweza kufahamu nini kinawasumbua?”<br />
Ukimya wa ajabu ukatokea, hakuna mtu aliyeweza kueleza kilichokuwa kikiwasumbua watoto hao wawili.<br />
“Mzazi wao yupo wapi?” daktari aliuliza.<br />
“Mimi hapa,” alijibu Fedorov kwa sauti kubwa.<br />
“Sogea karibu.”<br />
<br />
<br />
Huku akionesha uso uliojawa na mashaka, Fedorov alisogea karibu kabisa na daktari.<br />
“Ndiyo, hali hii imeanza lini?”<br />
“Ni muda wa wiki sasa daktari lakini leo hali imebadilika zaidi.”<br />
Daktari aliyekuwepo ndani ya chumba kile alianza kumpima mtoto mmoja baada ya mwingine, mara kadhaa alitingisha kichwa chake na zoezi hilo lilipokamilika akawa anaandika maelezo fulani ndani ya mafaili ya wagonjwa. Alipomaliza alimwita muuguzi akimtaka awapeleke watoto hao kwenye wodi ya wagonjwa mahututi, zoezi hilo likafanyika mara moja.<br />
<br />
<br />
“Daktari, watoto wangu watapona?” Fedorov aliuliza huku macho yake yote yakimwangalia daktari huyo.<br />
“Mh!”<br />
“Tafadhali nijibu.”<br />
“Ah! Unajua? Lakini watapona.”<br />
“Umeonesha hofu sana, nini kinaendelea?” Fedorov aliuliza safari hii kwa sauti ya upole. Akili yake haikufanya kazi vizuri, alihisi kama anakaribia kuwa mwendawazimu.<br />
“Usijali, wapo katika mikono salama, watapona tu hawa,” daktari alijaribu kumpa moyo Fedorov ambaye kwa kumwangalia tu ungeweza kugundua ni kwa kiasi gani yupo kwenye mateso na maumivu makali.<br />
<br />
Machela mbili zilisukumwa moja kwa moja mpaka chumba cha wagonjwa mahututi, daktari akawa anafuata kwa nyuma.<br />
“Watoeni juu ya mechela na kuwalaza kwenye vitanda,” ilikuwa ni sauti ya daktari akiwapa maelekezo manesi.<br />
Haraka zoezi hilo likafanyika, watoto wote wawili wakalazwa juu ya vitanda vyao na daktari akaanza kufanya uchunguzi kwa kila mmoja akitafuta tatizo.<br />
<br />
<br />
Kwa muda wa takribani saa tatu na nusu, bado alikuwa akiendelea kuchunguza afya za watoto hao, vipimo kadhaa vikachukuliwa na kupelekwa maabara.<br />
Nje ya wodi, Fedorov aliendelea kusimama, hamu yake kubwa ikiwa ni kupata taarifa kutoka ndani ya wodi, jasho jembamba lilikuwa likitiririka mwilini mwake.<br />
“Mh! Mungu wasaidie wanangu, naamini hapa ndipo mahali ambapo watarejewa na fahamu zao na maisha yao kuendelea tena hata kama itanigharimu kia…” alisema lakini kabla hajamalizia sentensi yake, macho yake yalishuhudia mlango wa wodi ya wagonjwa mahututi ukifunguliwa, yule daktari aliyewapokea wale watoto akatokeza.<br />
<br />
<br />
Kwa mbali akanyoosha mkono wake kwa ishara na kumwita Fedorov.<br />
“Niambie daktari, umegundua tatizo gani?”<br />
“Mh, baada ya kufanya uchunguzi wa kina tumegundua tatizo.<br />
“Ahsante, ahsante sana daktari na Mungu akubariki. Je, mmegundua nini tatizo?”<br />
“Uchunguzi tuliofanya umebaini kuwa watoto wako walipigwa na kitu kizito kichwani au walianguka kutoka umbali mrefu kwani kuna baadhi ya mishipa imepasuka na kufanya damu kuvilia kwa ndani. Hilo ndiyo hasa tatizo kubwa linalowasumbua.”<br />
<br />
<br />
Sentensi hiyo ilipenya moja kwa moja masikioni mwa Fedorov, kumbukumbu ya namna watoto wake walivyorushwa kutoka garini na kudondoka chini kama mizigo ikamjia kichwani mwake kama sinema.<br />
“Mzee! Mzee tafadhali ongea na mimi.”<br />
“Mh! Inawezekana kabisa daktari lakini hilo si la muhimu sana kwangu, ninachotaka ni kuokoa maisha ya wanangu, basi.”<br />
“Hivi ninavyoongea na wewe tayari wanaandaliwa ili kuingizwa chumba cha upasuaji tukajaribu kutoa hiyo damu iliyovilia.”<br />
<br />
<br />
“Daktari watapona?” lilikuwa ni swali jingine kutoka kwa Fedorov, tayari daktari alishaanza kuondoka eneo hilo kurejea ndani ya chumba cha upasuaji.<br />
“Tuombe Mungu lakini pia tutahitaji utie saini sehemu fulani ya fomu zetu ili kukubaliana na suala la wanao kufanyiwa upasuaji.”<br />
“Nipo tayari daktari,” alijibu Fedorov huku mapigo yake ya moyo yakibadilika kwa kasi.<br />
<br />
<br />
***<br />
Mapumziko ndani ya chumba yalifanyika kwa dakika tano tu baada ya Lina kulia na kumbembeleza sana Phillip akidai kuwa amechoka. Baada ya dakika tano kuisha kazi ilianza upya. Phillip alitaka kuonesha kwamba alikuwa ni mwanaume wa kuotea mbali, hakika hakutaka kumpa Lina nafasi hata kidogo, jambo lililozidi kummaliza nguvu.<br />
“Mpenzi kwa leo inatosha, tafadhali nisikilize mimi ni wako tutafanya…”<br />
“Mwaaa!Mwaaa!” Phillip alimmwagia Lina mabusu mfululizo.<br />
<br />
Shughuli ilikuwa pevu kwani wawili hao walicheza ‘rigwaride’ kwa saa tano, Lina akionekana kuwa taabani. Hata sauti nayo ilishakatika kwa kulalama. “Nakupenda Lina ndiyo maana nafanya yote haya.”<br />
“Mi…mi…pi..a” alijibu Lina.<br />
“Nataka kuona nini mwisho wake.”<br />
“Uta..niu.a…utani..ua.”<br />
<br />
“Nataka kukupa raha ambayo nina hakika hukuwahi kuipata, leo ndiyo leo…” Phillip alizidi kujitapa huku akimpa Lina mambo, aliendelea kufanya hivyo mpaka saa saba zilipokatika, akakubali kushuka na kumwacha Lina huru baada ya kuridhika kabisa. Lina alilala kimya kitandani, macho na miguno ndiyo vitu pekee vilivyomfanya Phillip aamini kuwa bado alikuwa hai.<br />
“Ahhhhh!” Phillip alishusha pumzi ndefu, akasogea pembeni mwa Lina na kuketi kitako huku akimwangalia kwa jicho la husuda.<br />
<br />
<br />
“Nakupenda sana Phillip.”<br />
“Nakupenda pia Lina.”<br />
“Ahsante kwa mapenzi matamu, kweli leo nimekuaminia.”<br />
“Ha!Ha!Haaa!” Phillip alicheka huku akijifuta jasho kwa taulo lililokuwa pembeni.<br />
“Kweli sikutanii, hapa nilipo nipo hoi bin taaban sijiwezi kabisa.”<br />
“Ahsante mke wangu.”<br />
<br />
<br />
“Phillip,” Lina aliita kwa sauti ya upole.<br />
“Yes baby,” Phillip akajibu.<br />
“Ninalo wazo kichwani mwangu.”<br />
“Unataka kuniacha tena?”</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5127772171142226">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.89<br />
<br />
<br />
NDANI ya chumba cha upasuaji kulikuwa na hekaheka, madaktari wasiopungua watano wakiambatana na wauguzi waliingia na walionekana kuwa na hamu kubwa ya kutaka kuokoa maisha ya watoto wawili pacha waliolala kitandani bila kujitambua pamoja na kwamba walikuwa wagonjwa, uzuri wao ulionekana wazi. Si madaktari wala wauguzi waliokuwa na tumaini juu ya watoto hao, laki<span class="text_exposed_show">ni walitaka kujaribu.<br />
“Watoto waandaliwe kwa ajili ya upasuaji.”<br />
<br />
“Tayari daktari.”<br />
“Basi hakikisheni kabla ya yote mashine za hewa ya oksijeni zifungwe ili kuwapatia hewa safi haraka sana,” ilikuwa ni sauti ya daktari mmoja aliyekuwa karibu na kitanda cha mtoto mmoja.<br />
“Sawa daktari tunafanya hivyo.”<br />
“Wengine wagawanyike waende kwenye mashine nyingine haraka.”<br />
“Hakuna shida.”<br />
<br />
Haikuchukua hata sekunde mbili tayari watoto hao midomoni mwao zilishafungwa mashine hizo ili kuwasaidia kupata hewa safi.<br />
Mambo yote hayo yalifanyika chini ya uangalizi maalum wa madaktari wao ambao ndiyo walioshika usukani wa kuendesha kila kitu ndani ya wodi na baada ya kuhakikisha kwamba maandalizi yalitosha nao pia walijiweka sawa kwa kazi.<br />
Vifaa vyote muhimu vilisogezwa karibu, hakika kwa kuviangalia vifaa hivyo, kwa mtu mwenye akili timamu lazima ungeingia woga.<br />
“Ni vyema tukaanza kazi sasa, ni lazima tufanye kila kinachowezekana kuokoa maisha ya watoto hawa, ni wazuri mno kufa…sawa jamani?”<br />
<br />
“Hakuna shida daktari lakini pia bila kumshirikisha Mungu hakuna kitakachokwenda sawa,” aliongea muuguzi mmoja aliyekuwa pembeni, naye pia alionekana kuwaonea huruma watoto hao.<br />
Zoezi likaanza, visu na mikasi ikipita huku na kule ni jambo hilo pekee ndilo lililoonyesha kwamba watu ndani ya chumba hicho walikuwa bize kupindukia. Saa ya kwanza ikapita hatimaye ya tatu bado madaktari wakihangaikia kutoa damu iliyokuwa imevujia ndani ya ubongo wa watoto hao.<br />
<br />
***<br />
Nje ya wodi mambo kwa Victor Fedorov yalikuwa magumu, muda wote alikuwa akizungukazunguka huku na kule bila kutulia sehemu moja, alitaka kufahamu ni kitu gani kiliendelea ndani ya chumba, hivyo muda wote macho yake hayakubanduka kwenye mlango wa chumba cha upasuaji.<br />
Kwa saa tano aliendelea kubaki hapo, mwisho akaanza kukata tamaa kwani hakuwepo muuguzi wala daktari aliyetoka wodini.<br />
“Kinaendelea nini humo?” aliuliza na sauti hiyo ikapenya moja kwa moja masikioni mwa mlinzi wake, huyo ndiye aliyekuwa hapo kumfariji.<br />
<br />
“Bosi tuwe wavumilivu nahisi kazi ni kubwa.”<br />
“Mh! Hapana moyo wangu unahisi hatari.”<br />
“Kama ipi?”<br />
“Sidhani kama watoto wangu watapona tena, hakika hawataamka.”<br />
“Hapana lakini wewe siyo Mungu, hebu tumwachie yeye kila kitu anaweza,” mlinzi wake alizidi kumtia moyo na kumfariji wakati wote.<br />
<br />
“Uwii! Mamaaa! Wananguuuu jamani…” Fedorov aliangua kilio, uvumilivu ulionekana kumshinda kabisa.<br />
Saa saba baadaye bado hawakuona mtu, hofu ikawafunika mioyoni mwao nao pia wakashindwa kuelewa ni kitu kilikuwa kimetokea ndani ya chumba kwani isingekuwa rahisi mpaka wakati huo asitokee mtu yeyote.<br />
“Pengine wamepitia mlango mwingine,” aliongea Fedorov.<br />
“Hapana mlango ni huu mmoja na kama kuna tatizo ni lazima watupe taarifa sisi wahusika.”<br />
“Pengine wanaogopa au hawajui wataanzia wapi.”<br />
<br />
“Bosi si rahisi, ni lazima watueleze tena bila kificho.”<br />
“Basi tusubiri tuone,” aliongea Fedorov, tayari alishanyamaza kulia kwani maneno aliyopewa na kushauriwa na mlinzi wake yalionekana kuingia kichwani mwake.<br />
Wakiwa katika hali ya kupigwa butwaa, wakashuhudia mlango wa chumba cha upasuaji ukifunguliwa na machela ikitolewa na nyingine ikifuata kwa nyuma, Victor Fedorov akaamini kwamba hao walikuwa ni watoto wake.<br />
<br />
“Hao hapo,” alisema kwa sauti huku akisogea karibu kuhakikisha kama alichokuwa akikiona kilikuwa sawa au ni ndoto za mchana.<br />
Akionekana mwenye mawazo mengi na wasiwasi, akatembea kwa unyonge na kusogea karibu lakini muuguzi aliyesukuma machela hiyo alionyesha wazi kupingana na kitendo cha Fedorov kusogea karibu huku akimweleza wazi kwamba awe mvumilivu na muda si mrefu atapewa ruhusa ya kuwaona watoto wake.<br />
“Wanaendeleaje?” aliuliza tena.<br />
<br />
“Majibu yote kaka utayapata kwa madaktari.”<br />
“Wako wapi sasa?”<br />
“Subiri kidogo utawaona,” aliongea muuguzi akizidi kusonga mbele.<br />
Ni kweli alichokuwa ameelezwa na muuguzi, alipogeuza shingo yake kuangalia nyuma alishuhudia jopo kubwa la madaktari na wauguzi wakitoka, alipowaangalia vyema aligundua simanzi lililokuwa mioyoni mwao, naye bila kusita alisimama na kuwasubiri wafike karibu na mahali alipokuwa ili awaulize.<br />
<br />
“Daktari, hebu nielezeni juu ya hali za watoto wangu.”<br />
“Mh! Tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuondoa damu iliyokuwa imeganda ndani ya kichwa na kazi imekuwa ngumu sana ndiyo maana tumechukua muda wa saa saba, tunatumaini zoezi letu litafanikiwa kwa asilimia kubwa.”<br />
“Watapona?” aliuliza Fedorov.<br />
“Kazi yetu sisi ilikuwa ni kuondoa tatizo ambalo tumefanikiwa, mengine tumwachie Mungu…ah! Sijui unaweza kuja ofisi mara moja?” daktari alisema.<br />
<br />
“Bila shaka,” alijibu Fedorov akiungana na madaktari kuelekea ofisini kwa ajili ya kupata maelezo zaidi.<br />
Taratibu wakatembea na kuufikia mlango ambao ndiyo ulikuwa chumba cha daktari, akakaribishwa na kuingia huko na akaonyeshwa kiti ili aketi kwa mazungumzo zaidi.<br />
“Kwanza pole sana mzee wetu.””Ahsanteni poleni na ninyi.”<br />
<br />
“Ah! Sisi ni kazi yetu kuhakikisha tunafanya kila kinachowezekana kuokoa maisha ya wagonjwa,” daktari mmoja alijibu akimwangalia Fedorov ambaye aliketi pembeni, macho yake yakionesha wasiwasi mkubwa.<br />
“Hawa mbele yako ni madaktari waliohusika na upasuaji wa watoto wako.”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Kazi tumemaliza tunachosubiri sasa ni kuona kama tutakuwa tumefanikiwa.”<br />
“Nahitaji kufahamu kama tu wataamka,” Fedorov aliuliza.<br />
“Kuamka wataamka lakini ni baada ya saa ishirini na nne kuanzia sasa, yakupasa uwe mvulivu,” aliongea daktari mwingine.<br />
“Saa ishirini na nne?” aliuliza kwa sauti.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Watoto wataamka au watakufa? Ni jambo gani Lina anataka kumweleza Phillip?</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.90<br />
<br />
“SAA ishirini na nne?” Aliuliza kwa sauti.<br />
Muda wa saa ishirini na nne ulionekana kama miaka mitatu au minne kwa Fedorov, asingeweza kuvumilia kukaa mbali na watoto wake ambao kwake ndiyo walikuwa ndugu pekee duniani.<br />
“Daktari tafadhali naomba kwa ruhusa yako niwaone japo kidogo.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Mh! Kwa sheria za kidaktari haturuhusu mtu kufanya hivyo, yakupasa uwe mvumilivu mpaka baada ya saa hizo.”<br />
<br />
“Lakini sitaweza, natamani kuwaona watoto wangu,”aliongea tena huku akibubujikwa machozi.<br />
“Dk. Nyoshi mpatie ruhusa awaone japo kidogo tu pengine ataridhika.”<br />
“Lakini daktari wewe mwenyewe unafahamu utaratibu wetu.”<br />
“Najua ila nimemwonea sana huruma mzee huyu.”<br />
“Sawa,”alijibu daktari huyo akinyanyuka kwenye kiti.<br />
<br />
Taratibu mlango ukafunguliwa na daktari akaanza kumwongoza Fedorov kuelekea chumba cha wagonjwa mahututi.<br />
“Daktari naweza kukuuliza tena?”<br />
“Uliza tu hakuna shaka.”<br />
“Nataka kujua kama watoto wangu watapona.”<br />
“Kama nilivyokueleza mwanzo, kazi yetu sisi kama madaktari tumeifanya vizuri hiyo sehemu nyingine tumemwachia Mungu atende.”<br />
“Fyuuu!” Fedorov akashusha pumzi kwa nguvu.<br />
<br />
Wakaufikia mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi, mapigo ya moyo wa Fedorov yakaenda mbio mithili ya mtu aliyekimbia mita ndefu, walipomaliza kufanya taratibu zote wakaingia ndani.<br />
Baada tu ya kuingia, macho ya Fedorov yakapiga moja kwa moja juu ya vitanda viwili vikiwa vimezungukwa na mashine ya hewa ya oksijeni, machozi yakambubujika.<br />
“Mungu wangu!”Ndiyo sauti pekee iliyosikika.<br />
<br />
“Kuna nini?” Daktari akauliza.<br />
“Mariya! Merina,” alitamka majina ya watoto wake akisogea taratibu kuelekea kwenye vitanda hivyo huku macho yake yakishuhudia vichwa vya watoto hao vikiwa vimefungwa bandeji na kuachwa sehemu ndogo sana upande wa macho.<br />
“Daktari mbona kama wamevimba vichwa?”<br />
“Ni kweli kabisa lakini vitarejea katika hali yake ya kawaida kadiri muda unavyozidi kusonga.”<br />
“Mh!” Fedorov akaguna kuonyesha kuumizwa na hali hiyo.<br />
<br />
Kwa takribani dakika tano waliendelea kubaki ndani ya chumba hicho, Fedorov akizunguka kitanda kimoja na kurudi kingine na mara kadhaa akitamka;<br />
“Mungu, wasaidie watoto wangu napenda kuona wanapona…sitaki wafe nataka waishi…naomba unisaidie…”aliongea kwa sauti ya chini.<br />
<br />
***<br />
“Phillip,” Lina aliita kwa sauti ya upole.<br />
“Yes baby,” Phillip akajibu.<br />
“Ninalo wazo kichwani mwangu.”<br />
Phillip akageuka na kuketi vizuri macho yake yote yakimwangalia mwanamke aliyekuwa amelala kitandani, hofu ikaonekana kuufunika moyo wake akitaka kufahamu ni kitu gani hasa Lina alitaka kumweleza.<br />
“Unataka kuniacha?” Akauliza.<br />
<br />
“Haa!Haaa!Haaa!” Lina akacheka.<br />
“Ninakuomba usije ukanieleza kitu cha kuumiza mtima wangu.”<br />
“Phillip hivi unadhani ni rahisi hivyo?”<br />
“Nini?”<br />
“Kukuacha, nikuhakikishe siwezi si kwa sababu ya penzi ulilonipa leo la hasha lakini toka ndani ya moyo wangu ninakupenda na siko tayari kukukosa katika maisha yangu.”<br />
<br />
“Mh! Nieleze basi,” aliongea Phillip, tayari macho yake yalishabadilika na kuwa mekundu.<br />
Lina akajivuta kutoka kitandani na kuketi karibu, akamuangalia na kuachia kuachia tabasamu.<br />
“Kwanza naomba nikutoe wasiwasi mume wangu, ukweli ninachokueleza hapa ndiyo ukichukue na kukifanya kuwa ukweli, sikuwahi na wala sikufanya mapenzi na Daniel si kwamba sikuweza ila nakuheshimu sana…”<br />
“Ukweli?”<br />
<br />
“Hakika.”<br />
“Tukiwa katika harakati hizo nilikurupuka kutoka juu ya kitanda na kukimbia ndiyo maana nilitoka na shuka tu.”<br />
“Mwaa! Nakupenda Lina.”<br />
“Natumai nitakuwa nimekutoa wasiwasi juu ya hilo.”<br />
“Ni kweli kabisa lakini umeniambia unalo wazo.”<br />
“Mh! Unajua…nitapenda uuangane na mimi katika hilo.”<br />
<br />
“Lina niondoe jakamoyo nililonalo.”<br />
“Nataka tukubaliane ili tushirikiane kulifanya pamoja.”<br />
“Nimeshakueleza niko tayari kwa lolote,”aliongea Phillip kwa kujiamini.<br />
“Phillip nimefikiria sana juu ya mtoto, wazo pekee nililonalo nimeona tutafute mtoto wa kuasili.”<br />
“Mh!”<br />
<br />
“Kwa sababu ya tatizo ulilonalo ili mimi na wewe tuendelee kuishi na kupendana mpaka mwisho wa uhai wetu ni bora tuasili mtoto mmoja tu.”<br />
“Unamaanisha unachokisema.”<br />
“Hakika nimefikia hapo ili kulinda penzi letu.”<br />
“Lina!” Phillip aliita.<br />
“Na iwe hivyo.”<br />
<br />
“Jinsia gani?” Phillip aliuliza.<br />
“Chagua wewe.”<br />
“Hapana.”<br />
“Mimi binafsi napenda mtoto wa kike sijui wewe?”<br />
“Hata mimi,” Lina alijibu na kumpiga Phillip mabusu mfululizo.<br />
<br />
Takribani sekunde tano, Phillip alibaki kimya akizungusha akili yake, hakuwa tayari kukubaliana na maneno aliyoyasikia kutoka kwa mkewe Lina.<br />
“Lina nimeamini kwamba kweli unanipenda, ahsante mke wangu ninaungana na wewe asilimia zote na ninakuahidi kulitunza penzi letu hadi mwisho Mungu akiwa mlinzi wetu, sipendi na wala sitaki kukuudhi tena...” alimaliza Phillip akiachia mabusu mfululizo.<br />
Ghafla kama mshale uliofyatuliwa, akamkamata Lina na kumlaza tena kitandani na wote kujifunika shuka gubigubi, kilichofuata baada ya hapo kilikuwa hakielezeki wala hakiandikiki gazetini.<br />
<br />
Zoezi hilo lilipokamilika Phillip akamshukuru Lina akimweleza wazi kwamba angeshirikiana naye bega kwa bega kukamilisha mkakati wao wa kupata mtoto wa kumuasili.<br />
“Kesho tutaanza taratibu zote, nataka ndani ya mwezi huu tupate mtoto wetu ambaye tutamlea vyema nasi tuingie katika ulimwengu wa kuitwa baba na mama.”<br />
“Ahsante mke wangu, ahsante kwa kunipenda.”<br />
“Nakupenda pia.”<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Watoto Mariya na Merina watapona? Phillip na Lina je, watafanikiwa kupata mtoto wa kuasili? tukutane keshooo!!<br />
USIKU MWEMA NAWAPENDA NYOOOOTEEEE MWAAAAA!!!</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.92<br />
<br />
“KWANZA naomba nikutoe wasiwasi mume wangu, ninachokueleza hapa ndicho ukichukue na kukifanya kuwa ukweli.<br />
Sikuwahi na wala sitafanya mapenzi na Daniel, si kwamba sikuweza ila ni kwa sababu nakuheshimu sana…”<br />
“Lina nimeamini kwamba kweli unanipenda, ahsante sana mke wangu. Naungana na wewe kwa asilimia zote, nakuahidi kulitunza penzi letu hadi mwisho wa maisha y<span class="text_exposed_show">etu, ninaomba Mungu awe mlinzi wetu, sipendi na wala sitaki kukuudhi tena,” alimaliza Phillip huku akimuachia mabusu mfululizo.<br />
<br />
Ghafla, kama mshale uliofyatuliwa, Phillip anamkamata Lina na kumnyanyua juu, anamlaza tena kitandani na wote wanajifunika shuka gubigubi, kinachofuata baada ya hapo hakielezeki.<br />
Wanakubaliana kuwa siku inayofuata wafanye taratibu zote na kuzikamilisha ili wampate mtoto wa kuasili. Walikuwa na hamu kubwa ya kuitwa baba na mama.<br />
<br />
Baada ya kufikia muafaka wa kuasili mtoto ambaye wangemlea vyema na kumtunza katika maadili ya Kitanzania.<br />
Wanaendelea kucheza kitandani mpaka usingizi unawapitia.<br />
Upande wa pili, watoto wa tajiri mkubwa nchini Urusi, Victor Fedorov wapo hospitali na bado hali zao ni tete.<br />
Wanakaa kwa zaidi ya saa sabini na mbili bila kuzinduka. Hali hiyo inamtia shaka baba yao, Fedorov na haamini kama wanaweza kutoka ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi wakiwa hai.<br />
Je,nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
“HA! ” Ilisikika sauti ya mtu akiguna ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi ambako watoto wawili mapacha, Mariya na Merina walikuwa wamelazwa.<br />
“Kuna nini tena?” mwingine aliuliza.<br />
“Ameamka huyu! Ameamka.”<br />
“Mungu wangu! Kweli jamani.”<br />
<br />
Jopo lote la madaktari pamoja na wauguzi waliokuwa ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi walisogea karibu na kitanda.<br />
“Chafya!”<br />
“Mh! Kweli, hakyanani vile pacha mmoja ameamka na kupiga chafya.”<br />
“Kweli Mungu mkubwa,” alisema mmoja wa madaktari.<br />
“Kwa jinsi hali inavyoendelea, hata huyu mwingine ataamka muda si mrefu.”<br />
“Ona! Amefumbua na macho.”<br />
<br />
“Kweli,” daktari mwingine alijibu na wote wakatabasamu.<br />
Dalili iliyokuwa imeoneshwa na pacha mmoja ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi, ilimfurahisha kila mtu. Hofu iliyokuwa imeanza kutanda katika mioyo yao ikaondoka na matumaini mapya yakafufuka.<br />
Hakuwepo hata mtu mmoja aliyetaka historia mbaya juu ya upasuaji huo wa watoto iandikwe.<br />
<br />
<br />
“Hebu tuendelee kusubiri, tukiangalia nini kitaendelea kwa huyu pacha mwingine, naye ataamka muda si mrefu.”<br />
Maongezi yaliendelea ndani ya chumba hicho kila mmoja akisema lake juu ya upasuaji huo. Saa ya kwanza ikapita, matumaini ya pacha mwingine kuzinduka yakawa yanazidi kuongezeka, waliamini kwamba muda si mrefu naye angeamka.<br />
<br />
“Daktari ni vyema tukatoa taarifa kwa mzazi wake juu ya nini kinaendelea humu ndani,” alisema muuguzi mmoja.<br />
“Hakuna shida anaweza kupata kibali cha kuingia na kujionea mwenyewe.”<br />
Muuguzi mwingine akatembea na kufungua mlango wa kutokea ndani ya chumba hicho, akatokeza nje na kwa ishara akamwita mzee aliyekuwa ameketi chini pembeni ya mlango wa kutokea ndani ya chumba hicho kwa ishara.<br />
“Samahani kidogo tunakuomba,” sauti ya muuguzi ilipenya katika masikio ya mzee yule ambaye alikua ametawaliwa na uso wa huruma.<br />
<br />
“Mh! Nini tena watoto wangu wameamka?” alihoji huku akinyanyuka.<br />
“Tafadhali tunakuomba mara moja.”<br />
Taratibu bila kusema kitu tena mzee yule akatembea na kuufikia mlango kisha kuuliza tena swali kama alilouliza mwanzo.<br />
“Muuguzi nini kimetokea?”<br />
“Hakuna matatizo kuna habari njema kwako.”<br />
<br />
“Oh! Habari njema? Watoto wameamka?” Aliuliza.<br />
“Mh! Ni mmoja lakini mwingine bado.”<br />
“Hapana, kwa nini iwe hivyo?”<br />
“Utapata maelezo yote ndani ya chumba hiki, tafadhali ingia ndani na ufuate taratibu zetu,” muuguzi alisema na kuanza kumwongoza Fedorov kwenye chumba maalum.<br />
<br />
Mbele kidogo Fedorov akapewa maelezo kisha kuvishwa nguo maalum ambazo ilizivaa na kuingia ndani ya chumba hicho.<br />
Baada ya zoezi hilo kukamilika alianza kumfuata muuguzi ambaye alimwongoza moja kwa moja mpaka kwenye wodi ambayo alishuhudia umati wa wauguzi na madaktari ukiwa pembeni ya vitanda kila mmoja akionesha furaha.<br />
“Pole sana mzee wetu,”<br />
“Mh!” badala ya kujibu Fedorov aliguna tu na taratibu akasogea katika moja ya vitanda ambavyo juu yake ndipo walipolala watoto wake Mariya na Merina.<br />
<br />
“Mmoja wa pacha amepata fahamu zake japo bado hajaweza kusema kitu.”<br />
“Yupi?”<br />
“Huyo hapo.”<br />
“Mariya!” Fedorov akamwita kwa sauti na kusogea karibu zaidi akiwa hapo akashuhudia mtoto huyo akifumbua macho kwa tabu kisha kuyafumba, machozi ya furaha yakamtoka akainama na kumbusu kwenye paji lake la uso huku akiongea.<br />
<br />
<br />
“Nakupenda sana mwanangu nataka wote mtoke turejee nyumbani kuendelea na maisha, sipendi mniache, wewe umeamka lakini Merina bado…ahsante Mungu kwa kujibu sala zangu, sijui ningekuwa mgeni wa nani katika dunia hii, ahsanteni pia madaktari kwa kazi nzuri.”<br />
<br />
“Usijali kikubwa tunachoomba ni huyu mwenzake naye aamke,”<br />
“Tii! Tiii!” mlio ndani ya chumba ukasikika na kuwafanya watu wote wageuke kuangalia upande ulipotokea mlio huo.<br />
Ilikuwa ni mashine ya hewa ya oksijeni iliyokuwa imefungwa kwa mtoto Merina ikionekana kusimama.<br />
“Mungu wangu mashine inataka kusimama...”<br />
<br />
***<br />
“Ahsante mke wangu, ahsante kwa kunipenda.”<br />
“Ahsante nawe pia.”<br />
Safari ya kuelekea ofisini ikaanza furaha ya Phillip ikionekana wazi na mara kadhaa alikuwa akimgeukia Lina na kumweleza wazi kwamba alimpenda kupita maelezo.<br />
Nusu saa tu baadaye waliingia ofisini na kila mmoja kuingia mzigoni lakini vichwa vyao vilionekana kufikiria juu ya kesho yake, kwani walitaka kumaliza mambo hayo haraka sana.<br />
<br />
“Rafiki leo unaonekana una furaha sana, hebu niambie unafurahia kitu gani?” Rafiki mmoja wa Lina aliuliza.<br />
“Maisha, hakuna kitu kingine, pia nimempata mume anayenipenda kwa dhati.”<br />
“Mh! Mshukuru Mungu wako, mimi natamani kupata mume kama wako.”<br />
“Wee huko unakoelekea siko, usije ukaja…” aliongea Lina lakini kabla ya kumalizia sentensi yake rafiki yake akaingilia kati.<br />
<br />
“Ahaa! Rafiki siwezi bwana, Phillip ni shemeji yangu na atabaki kuwa hivyo maisha.”<br />
“Unanitia mashaka, unamsifia mno…haa!Haaa,” Lina aliongea na kuachia tabasamu lililoambatana na kicheko.<br />
Aliyekuwa ndani ya ofisi ya Lina alikuwa ni rafiki yake wa siku nyingi waliyesoma naye chuo Kikuu na hatimaye walijikuta pamoja tena katika ofisi moja lakini kila mmoja akiwa kwenye kitengo chake.<br />
Walipendana na kuheshimiana kwa kila kitu na huyo ndiye aliyekuwa msiri wake mkubwa, halikuwepo jambo lililoendelea kati yake na Phillip na rafiki huyo asilifahamu.<br />
<br />
“Mimi natoka nilikuja kukusalimu tu kwani ni muda sijakutia machoni.”<br />
“Ahsante,” alijibu Lina kwa kutabasamu.<br />
Saa zikazidi kusogea na hatimaye muda wa kutoka ukawadia, Lina akakusanya kila kilichokuwa chake, kabla ya kutoka ndani ya ofisi akanyanyua simu yake na kubonyeza namba kadhaa, baada ya muda akaonekana akizungumza na mtu upande wa pili.<br />
<br />
“Darling muda wa kuondoka umefika, nakuja kukupitia hapo sasa hivi, twende nyumbani tukampumzike,” alisema na kukata simu kisha akaanza kutembea kutoka ndani ya ofisi yake.<br />
Baada ya sekunde tatu tu alishafika nje ya mlango wa ofisi ya mumewe, akaugonga mlango.<br />
“Karibu,” sauti iliskika wakati alipokamata kitasa cha mlango na kufungua mlango, macho yake yakatua kwa Phillip aliyekuwa ameketi ofisini kwake akionesha tabasamu.<br />
<br />
“Twende nyumbani tukampumzike kesho tunatakiwa kuwahi mapema sana kituo cha Msimbazi kukamilisha kazi.., sawa?” alisema Lina akionesha kumsisitiza Phillip ambaye hakuwa na hiyana, akakusanya vitu vyake kisha akanyanyuka na kutoka nje kuelekea nyumbani.<br />
Kwao usiku ulionekana kwenda taratibu mno, saa zikisonga pole pole lakini hatimaye asubuhi ikafika na wote wakajiandaa kwa safari, Phillip akiwa ndiye dereva.<br />
<br />
Saa moja na nusu walifika katika kituo cha Msimbazi na kuelekea kwenye ofisi ya sista mkuu aliyewapokea na kuwakaribisha ndani ya ofisi ambako walikuta taratibu zote zimeshaandaliwa na mwanasheria aliyekuwa akiwasubiri.<br />
Baada tu ya utambulisho mfupi sista mkuu akawaomba waanze utaratibu ili kwenda na wakati, wakapewa fomu maalum Phillip na mkewe wakaisoma vyema na kuielewa kisha wakatakiwa kuijaza kwa ufasaha.<br />
Kwa takribani dakika kumi nzima walifanya zoezi hilo na walipolikamilisha wakairejesha tena kwa sista mkuu ambaye akawauliza kama wameyakubali masharti yote yaliyoandikwa ndani ya fomu hiyo.<br />
<br />
“Tunakubaliana na yote yaliyoandikwa humo na tuko tayari kumtunza na kumlea mtoto tutakayemchukua hapa kwa nguvu na juhudi zetu zote, tunahakikisha atapata maisha anayostahili.”<br />
“Basi ni wakati wa ninyi kula kiapo mbele ya mwanasheria wetu.”<br />
“Sawa sista,” walijibu kwa pamoja na baada ya muda wakala kiapo na zoezi hilo lilipokamilika sista mkuu akauliza walihitaji mtoto wa jinsia gani na umri wake.<br />
<br />
“Kuanzia miezi mitatu na awe wa jinsia ya kike.”<br />
Sista hakuongeza tena neno lingine, akawataka wamfuate, akawaongoza mpaka kwenye chumba kimoja kilichokuwa karibu kabisa na ofisi yake.<br />
Akawakaribisha na kuwaingiza ndani ambako kulikuwa na watoto wadogo wakiwa wamelala kwenye vitanda na wafanyakazi wachache wakiwa hapo kuwaangalia.<br />
<br />
Hapo walitakiwa kuchagua mtoto mmoja tu ambaye ndiye wangemchukua na kwenda kumtunza mpaka mwisho wa uhai wake, wakafumbua macho yao yote kuwaangalia watoto hao ambao kwa kweli walikuwa wazuri mno.<br />
“Mnachagua mmoja tu,” sista mkuu aliongea akitabasamu.<br />
“Mh! Watoto wote wazuri sijui tuchukue yupi kati yao,” Lina alimuuliza Phillip.<br />
<br />
“Huyu hapa anafanana na sisi,” alisema Lina.<br />
“Sawa…sista huyu ndiye tuliyemchagua,”<br />
aliongeza Phillip akimnyanyua mtoto mzuri aliyekuwa amelala kitandani, alikuwa ni mdogo lakini uzuri wake ulionekana wazi</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.93<br />
<br />
MAMBO hayakuwa kama walivyotarajia kwamba baada ya saa kadhaa mtoto huyo angeamka na kuungana na mwenzake, saa ya kwanza ikapita na sasa ilikuwa ikielekea ya pili, Victor Fedorov uvumilivu ukaanza kumshinda akajikuta akimwaga machozi kama mtoto mdogo, kazi ya wauguzi ndani ya chumba ikawa ni kumtuliza wakimtaka awe mvumilivu.<br />
“Lakini ni muda mrefu sana mbona mwe<span class="text_exposed_show">nzake amesharejewa na fahamu?” aliuliza akisogea karibu kabisa na kitanda cha pacha ambaye hakuonyesha dalili yoyote ya kuamka.<br />
“Ataamka, kuwa mvumilivu.”<br />
<br />
“Mbona kama ni upasuaji umefanyika kwa saa sawa iweje yule aamke na huyu bado?” bado aliendelea kuuliza maswali mfululizo.<br />
“Tafadhali tunaomba sasa mzee utupishe tuendelee na matibabu yetu tutakuwa tukikujulisha kila kitu kadiri muda unavyokwenda tunaomba uende nje,” aliongea daktari mmoja, muuguzi aliyekuwa karibu na Fedorov akamshika mkono na kumwongoza kutoka nje naye pia akijaribu kuongea maneno ya kumpa faraja.<br />
<br />
Mzee huyo akatoka akilia, mawazo na akili zake zote zilikuwa juu ya mtoto wake huyo ambaye hakuonyesha matumaini, akatembea hatua ya kwanza na ya pili kisha akageuka nyuma kuangalia mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi.<br />
“Sitakwenda popote nitakaa hapahapa mpaka mwisho nataka kujua nini kinaendelea,” aliongea Fedorov akiketi chini, akiwa hapo haikupita hata sekunde tatu mlinzi wake naye akaungana naye, pia akijaribu kumfariji mzee huyo lakini zoezi hilo lilionekana kuwa gumu.<br />
<br />
“Naumia, moyo wangu una wasiwasi mkubwa sana juu ya mtoto wangu…sijui kama ataamka…lakini kama kuna kitu kibaya kwa nini wanifiche? Nataka wanieleze ukweli ili nijiandae kwa tatizo linalokuja,” aliongea akibubujikwa machozi.<br />
“Hapana bosi hawezi kufa, Mungu mkubwa anatenda.”<br />
“Najua hilo lakini kwa sasa nimekata…….”<br />
“Hutakiwi kukata tamaa unachotakiwa kufanya hivi sasa ni kuamini kwamba naye pia ataamka, mimi ninaamini kwamba yuko katika mikono ya madaktari bingwa atapona tu.”<br />
“Mh! Labda hebu tuone,”aliongea Fedorov akijifuta machozi.<br />
<br />
***<br />
“Mnachagua mmoja tu,” sista mkuu aliongea akitabasamu.<br />
“Mh! Watoto wote wazuri sijui tuchukue yupi kati yao,” Lina alimuuliza Phillip.<br />
“Huyu hapa anafanana na sisi.”<br />
“Sawa…sista huyu ndiye tuliyemchagua.”<br />
<br />
Mabusu mfululizo yakatua kwenye paji la mtoto waliyemchukua, alikuwa ni mtoto wa jinsi ya kike, pamoja na kuwa mtoto mdogo uzuri wake ulionekana wazi, rangi ya ngozi yake ilifanana kabisa na ya Phillip, furaha ya ajabu ikatawala, hakuwepo hata mtu mmoja kati yao aliyeamini kwamba sasa wangekuwa wakiitwa baba na mama wa mtoto waliyemuasili kutoka katika Kituo cha Msimbazi.<br />
“Tutamlea na kumtunza mpaka mwisho wa uhai wetu tukimpatia kila aina ya mahitaji,” Phillip aliongea akimwangalia sista mkuu.<br />
“Ombi letu kwenu ninyi ni hili hapa,” sista aliongea.<br />
“Ndiyo sista tunakusiliza.”<br />
<br />
“Tutakuwa tukihitaji kumtembelea mtoto huyu kila baada ya mwezi mmoja kujua na kufahamu anaendeleaje, hiyo ni moja ya sheria zetu mpaka atakapofikisha umri wa miaka kumi na nane ambapo tutakuwa huru kumwacha aendelee na maisha yake kwani atakuwa ni mtu mzima.”<br />
“Hilo halina shaka sista na kama inawezekana tunaweza tu kuongozana mpaka nyumbani.”<br />
“Nitawapa mtu ambaye mtaongozana naye mpaka huko kwa ajili ya kupafahamu na kama kutatokea mabadiliko yoyote yawe ya kuhama nyumba au kwenda nje ya nchi ni vyema mkatujulisha mapema, sawa?” sista mkuu aliuliza.<br />
<br />
“Tumesikia,” Phillip na Lina walijibu kwa pamoja na kuanza kutoka nje ya chumba kuelekea ofisini kwa sista mkuu ambako wangekamilisha taratibu zote kisha kuondoka na mtoto waliyekuwa naye.<br />
Taratibu maalum zikafanyika ikiwa ni pamoja na kupigwa picha na kutia saini kwenye makubaliano yote yaliyofanyika ofisini kisha wakakabidhiwa mtoto na sista mmoja ambaye wangeongozana naye mpaka mahali wanapoishi. Wakatoka na kumshukuru sista kisha kutembea kuelekea sehemu waliyokuwa wameegesha gari, Phillip ndiye alikuwa dereva na Lina aliketi kiti cha nyuma akiwa amempakata mtoto.<br />
<br />
Gari liliendeshwa na kwa muda wa saa moja tu walifika nyumbani kwa Phillip na Lina wakamkaribisha sista waliyeongozana naye wakimweleza wazi kwamba hapo ndipo palikuwa nyumbani kwao ambako mtoto waliyekuwa wamemwasili angeishi maisha yake yote akitunzwa na kulelewa vyema.<br />
“Karibu sana sista hapa ndipo nyumbani kwetu ambako mtoto huyu atalelewa na kuishi, akitunzwa kwa hali na mali.”<br />
“Mh! Ahsanteni sana nafurahi kupafahamu tutakuwa tukija kila mwezi kumtembelea ili kujua maendeleo yake.”<br />
“Karibuni sana.”<br />
<br />
Dakika kumi na tano baadaye sista aliyeongozana na Phillip na Lina aliaga na kuondoka akiahidi kurejea tena baada ya mwezi mmoja kujua hali ya mtoto huyo. Wakamsindikiza kisha akaondoka.<br />
Kwa siku nzima walishinda ndani ya nyumba wakipanga mipango yote na jinsi ya kumlea na kumtunza mtoto huyo. Lina akatoa wazo kwamba ni vyema wangemtafuta mfanyakazi wa ndani ambaye angekuwa tayari kumlea mtoto huyo na wao wangemlipa mshahara ambao angeutaka.<br />
<br />
“Ni lazima atafutwe mtu wa kumlea mtoto huyu kwa upendo wote,” Lina aliongea.<br />
“Kabisa, lakini nashauri awe mtu mzima kidogo.”<br />
“Jinsi ya kumpata sasa ndiyo tatizo, sijui tuanzie wapi?”<br />
“Hebu subiri kidogo,” Phillip aliongea akinyanyuka kitini kuelekea chumbani.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.94<br />
<br />
PHILLIP alitembea moja kwa moja na kuelekea mlango wa chumba chao akaingia na haikumchukua hata sekunde tatu tayari akawa amerejea akamsogelea Lina aliyekuwa ameketi bado sebuleni akimsubiri.<br />
“Soma hapa,” shika hiki kipande cha gazeti halafu nitakuonyesha kitu.<br />
Lina bila kusema kitu akionyesha kushangazwa na mumewe akanyoosha mkono wake na kupokea kipande hicho k<span class="text_exposed_show">isha kutulia akisikiliza maelekezo.<br />
<br />
“Ndani ya kipande hicho kuna tangazo la kampuni inayowatafutia watu wafanyakazi wa majumbani.”<br />
“Mh! Wewe ulikitoa wapi na ulijuaje kama tunaweza kutafuta mfanyakazi siku moja?” Lina aliuliza akiachia tabasamu.<br />
“Si unajua tena sisi watu wenye upako huwa tunaona vitu mapema sana kabla…,” aliongea Phillip akimwangalia Lina na kuachia tabasamu.<br />
Lina akakodoa macho yake na kuanza kusoma kipande hicho cha gazeti, ghafla akakutana na tangazo hilo akalisoma kwa umakini wa hali ya juu mpaka mwisho na kukutana na namba za simu kwa ajili ya mawasiliano kama tu mtu angehitaji mfanyakazi.<br />
<br />
“Mh! Hili liko safi tena wako wa aina mbili kike na kiume sijui yupi mume wangu?” Aliuliza Lina.<br />
“Wewe acha utani wako mwanaume wa nini hapa ndani ataweza kulea kweli?”<br />
“Anaweza kwani si sheria na masharti tu.”<br />
“Hapana tutafute wa kike,” aliongea Phillip akijilaza kwenye sofa.<br />
<br />
Lina akanyoosha mkono wake na kuchukua simu yake ya mkononi kisha kuanza kubonyeza namba kadhaa na kuweka simu sikioni, haikumchukua hata sekunde mbili tayari upande wa pili ukasikika.<br />
“Ndiyo naitwa Lina napiga simu kutoka hapa hapa Dar es Salaam, nimesoma tangazo lenu na nahitaji kupata mfanyakazi wa ndani ambaye umri wake ni mkubwa kidogo atakayeweza kulea vyema mtoto mdogo,” alimaliza Lina.<br />
“Hakuna shida dada yupo anapatikana sijui unamhitaji kwa lini?”<br />
<br />
“Hata leo ikiwezekana.”<br />
“Basi ni vyema ukatueleza wewe unapatikana wapi nasi tutakuja moja kwa moja nyumbani kwako na watu wawili kisha wewe utamchagua mmoja,”<br />
“Sawa.”<br />
Zoezi hili likawa limekamilika Lina akatoa maelekezo ya jinsi ya kufika nyumbani kwao na watu hao wakakubaliana naye na kumweleza wazi kwamba baada tu ya nusu saa wangefika nyumbani hapo.<br />
<br />
“Unajua nini mke wangu?”<br />
“Mh!”<br />
“Ubongo wangu unazunguka kuhusu majibu ambayo tutawapa watu wakitaka kufahamu juu ya huyu mtoto wetu tuliyemwasili?”<br />
“Mume wangu siku zote huwa watu hawakosi cha kusema wataongea na kujiuliza maswali mengi sana juu ya mtoto wetu lakini mwisho watanyamaza, hili litabaki kuwa jambo la familia na si vinginevyo.”<br />
<br />
“Mwaa! Mwaa! Mwanamke una akili sana wewe,” Phillip aliachia mabusu mfululizo kwenda kwa Lina ambaye naye aliyapokea kwa bashasha huku akinyanyuka na kutembea kwa madaha kuelekea sebuleni kumwangalia mtoto mchanga aliyekuwa amelala.<br />
“Bado amelala huyu,” sauti ya Lina ilisikika kutoka chumbani.<br />
“Basi njoo tuendelee kuongea hapa tukisubiri wageni.”<br />
“Sawa nakuja lakini mume wangu jambo moja hatujalifanya bado.”<br />
<br />
“Lipi hilo?” Phillip aliuliza kwa kutahamaki.<br />
“Hatujampa jina mtoto wetu.”<br />
“Hebu anza wewe kutoa la kwako,” Phillip alimwambia Lina.<br />
“Wewe kama baba wa familia unatakiwa useme na mimi nitafuata.”<br />
<br />
“Kutoka ndani ya moyo wangu mimi napenda sana mtoto huyu aitwe Genevieve.”<br />
“Saaaafi!” Lina aliongea kwa sauti.<br />
Hiyo pekee ilitosha kabisa kuonyesha kwamba jina hilo lilikuwa limepita moja kwa moja bila kipingamizi kwa pamoja wakanyanyuka na kukimbilia chumbani alikolazwa mtoto.<br />
<br />
***<br />
“Nashauri huyu mtoto afanyiwe CT-Scan kuangalia tena upya mfumo mzima wa kichwa chake huenda kuna tatizo ambalo halikuonekana wakati wa upasuaji wa mwanzo,” aliongea daktari mmoja ndani ya chumba baada ya kuona kwamba hali ilikuwa si nzuri kwani saa nyingi zilishapita na tumaini la kurejewa na fahamu kwa mtoto mwingine halikuwepo.<br />
“Huo ni uamuzi mzuri.”<br />
Haraka akapandishwa katika machela na kuanza kusukumwa kuelekea kwenye chumba ambacho kipimo hicho kingefanyika na kutoa picha kamili ya tatizo ambalo lingeonekana.<br />
<br />
Mchakato mzima ukafanyika haraka picha ikachukuliwa na majibu hayakuchukua muda mrefu sana yakarejeshwa tena kwa madaktari ambao waliisoma vyema ripoti hiyo.<br />
“Mungu wangu!”<br />
“Nini tena?”<br />
“Mh! Haya majibu nakosea au nasoma sawa?”<br />
“Ni sawa kabisa daktari hivyo ndivyo yalivyo.”<br />
<br />
“Kwa hiyo?”<br />
“Hatuna jinsi ni lazima tufanye tena upasuaji ili kumsaidia huyu mtoto vinginevyo atakufa.”<br />
“Kwani kilitokea nini mpaka kuacha bonge hili la damu?”<br />
“Huu si wakati wa kulaumiana ni wakati wa kuokoa maisha ya mtoto huyu jamani mimi nashauri maandalizi yafanyike haraka sana na kazi ianze mara moja.”<br />
“Mzazi wake je?”<br />
<br />
“Ni lazima apewe taarifa na akubali jambo hili vinginevyo atampoteza mtoto wake.”<br />
“Sawa aitwe na kuelezwa kila kitu.”<br />
Muuguzi mmoja akatoka mbio na kumwita Fedorov akimtaka aingie ndani ya chumba ili kuongea na madaktari dakika moja tu baadaye watu wawili wakaingia ndani alikuwa ni muuguzi na Fedorov bila kupoteza muda daktari mmoja akamweleza wazi kwamba ililazimu mtoto wake arejeshwe tena chumba cha upasuaji haraka ili kuokoa maisha yake kwani picha iliyochukuliwa ilionyesha wazi kwamba kulikuwepo tatizo na kama tu wangezidi kumchelewesha basi asingeamka milele.<br />
<br />
“Mungu wa…ngu…sa…fari hii..hatapo…” Fedorov aliongea kwa sauti ya kukatikatika huku machozi yakumbubujika, macho yake yakashuhudia machela ikisukumwa haraka kutoka nje ya wodi hiyo kuelekea chumba cha upasuaji.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.95<br />
<br />
<br />
<br />
MTOTO aliyeingia katika maisha ya Phillip na Lina na kupewa jina la Genevieve alikuwa ameleta furaha kubwa sana katika ndoa hiyo, kwani walimpenda kupita kawaida wakihakikisha wanampatia kila kilichohitajika katika maisha yake.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Genevieve, hatimaye jina hili limerudi tena katika maisha yangu,” alitamka Phillip kwa sauti ya juu.<br />
“Naam, hilo ndilo litakuwa jina lake.”<br />
<br />
“Ahsante Lina hii itakuwa kumbukumbu kwa mpenzi mke wangu ambaye aliondoka duniani nikiwa bado nampenda, mtoto huyu ameziba kabisa pengo lake.”<br />
“Ninafurahi pamoja na wewe mume wangu, siku zote haja ya moyo wangu ni kukuona unayo furaha kama hii,” Lina aliongea akitabasamu.<br />
“Nitampenda mtoto huyu mpaka kufa.”<br />
“Naungana na wewe lakini ninalo swali moja kwako Phillip.”<br />
<br />
“Endelea.”<br />
“Nataka kujua kama utanipenda kwa dhati kama ilivyokuwa mwanzo.”<br />
“Lina! Hakika nakuhakishia kutoka moyoni mwangu kwamba ninakupenda mno.”<br />
“Ahsante kwa penzi lako Phillip, hebu twende chumbani mara moja,” aliongea Lina huku akimwangalia mumewe na kuachia tabasamu. Ni Lina aliyekuwa wa kwanza kusimama na kumsogelea mumewe kisha kumshika mkono na kumnyanyua kutoka kitini wote wakaanza kutembea kuelekea chumbani.<br />
<br />
Kilichoendelea ndani ya chumba hakika kilikuwa hakielezeki wala kuandikika gazetini, kwani miguno na mihemo ya kila aina iliendelea kwa muda wa saa nne mfululizo, kilichowashtua hapo ilikuwa ni sauti ya honi ya gari nje ya lango lao, kwa sababu walifahamu kwamba mlinzi alikuwepo kwa kazi hiyo wao waliendelea na shughuli zao.<br />
“Lina sasa inatosha bwana.”<br />
<br />
“Hapana, mimi bado sijachoka.”<br />
“Wewe mtoto ataa…” aliongea Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake wakasikia sauti ya mlango ukigongwa.<br />
“Bosi! Bosi kuna wageni hapa,” sauti ya mlinzi ilisikika.<br />
“Nenda wewe mimi mpaka nikaoge.”<br />
<br />
“Sawa hakuna shida mke wangu,” Phillip aliongea huku akisogelea bukta yake iliyokuwa pembeni kisha akaiweka mwilini na taratibu akafungua mlango na kutembea kuelekea sebuleni ambako alifungua mlango na kukutana na sura ngeni za watu watatu na mtu wa nne akiwa mlinzi.<br />
“Karibuni,” aliongea.<br />
“Ahsante sana, nadhani hatujakosea, hapa ndiyo nyumbani kwa Phillip.”<br />
“Ni kweli kabisa karibuni sana.”<br />
<br />
“Oke, sisi ni wale watu mliotupigia simu muda mchache uliopita mkihitaji mfanyakazi tuko hapa.”<br />
Wakaingia ndani na mlinzi kurejea sehemu yake ya kazi, haikuchukua hata sekunde tatu Lina naye akaungana nao sebuleni, mazumgumzo maalum yakaanza na hatimaye wakatakiwa kuchagua mtu mmoja kati ya wawili waliokuwepo hapo.<br />
“Sisi tunamchagua huyu hapa,” waliongea karibu kwa pamoja.<br />
<br />
“Hakuna shida hata sisi tulipendekeza huyuhuyu.”<br />
“Karibu sana mama sijui unaitwa nani?”<br />
“Naitwa Magdalena Simon, mwenyeji wa Rukwa na nimezaliwa miaka arobaini na saba iliyopita.”<br />
“Mh !” Phillip na Lina wakaguna, mwanamke huyo alikuwa ni mtu mzima si kwa mtoto mdogo tu bali hata kwao.<br />
“Mama utaweza kazi ya kulea mtoto kweli? Na je wewe katika maisha yako ulibahatika kupata mtoto?” Lina aliuliza akikodoa macho kumwangalia mwanamke huyo.<br />
<br />
“Mh! Mh! Hapana !” mwanamke huyo alijibu na walipomwangalia vyema usoni mwake waligundua alikuwa akibubujikwa machozi.<br />
“Basi mama sisi tunakupokea kwa mikono miwili ukae nasi na ulee mtoto wetu umpe mapenzi yote.”<br />
“Ahsante.”<br />
<br />
Makubaliano yakafanyika wakatakiwa kulipa kiasi cha fedha ambacho ndicho mwanamke huyo alitolewa kwao na wakamshukuru mtu aliyemleta mfanyakazi huyo huku akiwaeleza wazi kwamba angekuwa karibu nao kwa kila kitu kuhakikisha hapatokei tatizo lolote. Wakaaga na kuondoka.<br />
<br />
Wakampokea bibi Magdalena na kumwonyesha mambo yote yaliyomstahili ndani ya nyumba hiyo ikiwa ni pamoja na chumba ambacho angekitumia muda wote ambao angeishi hapo. Baada ya zoezi hilo wakamtaka aingie jikoni kuandaa chakula cha jioni hiyo ikiwa ni kama jaribio la kwanza kisha wao wakarejea chumbani.<br />
***<br />
Upasuaji wa pili ulikuwa umefanyika kwa ufanisi wa hali ya juu na madaktari wakihakikisha halijirudii tena tatizo kama lililotokea mwanzo wakiomba Mungu mtoto huyo mzuri anyanyuke na kuendelea na maisha.<br />
“Tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa, sasa atolewe humu na kurudishwa chumba cha wagonjwa mahututi.”<br />
<br />
“Sawa daktari,” wauguzi waliitikia, na bila kuchelewa machela ikaanza kusukumwa kutoka nje ya chumba ambako walimkuta Fedorov akiwa amesimama.<br />
“Oh! My God !” aliongea mzee huyo kwa sauti ya juu baada ya kuona bandeji iliyotapakaa damu ikiwa imefungwa kuzunguka kichwa cha mtoto wake.<br />
Machela ikapitishwa na wauguzi ambao hawakuongea kitu chochote zaidi ya neno moja tu.<br />
<br />
“Pole sana mzee.”<br />
“Ataamka baada ya saa ngapi?”<br />
“Saa kumi na mbili kuanzia sasa.”<br />
“Mh!” Fedorov aliguna hakika kwa kumwangalia tu mzee huyo ungegundua tu kwamba tayari alishachoka moyoni na tumaini lote lilishapotea katika maisha yake, mpaka kufikia hapo kwa umri aliokuwa nao hakuwahi kukutana na changamoto kubwa kama hiyo.<br />
<br />
Machela ikasukumwa na kuingizwa chumba cha wagonjwa mahututi pembeni tu ya pacha mwenzake ambaye kwa wakati huo tayari alishaanza kufungua macho na kuuliza maswali kadhaa japo kwa taabu akitaka kufahamu ni kitu gani kilitokea.<br />
Victor Fedorov akatakiwa kusubiri nje ya chumba hicho kwa muda mwingine wa saa kumi na mbili.je nini kitaendelea? tukutane kesho kama kawa mwaaaaaaast gudnite all</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.96<br />
<br />
UPASUAJI wa pili ulikuwa umefanyika kwa ufanisi wa hali ya juu na madaktari wakihakikisha halijirudi tena tatizo kama lililotokea mwanzo, wakiomba Mungu mtoto huyo mzuri anyanyuke na kuendelea na maisha.<br />
“Tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa sasa atolewe humu na kurudishwa chumba cha wagonjwa mahututi.”<br />
“Sawa daktari,” wauguzi waliongea na bila kuchelewa machela ik<span class="text_exposed_show">aanza kusukumwa kutoka nje ya chumba ambako walimkuta Fedorov akiwa amesimama.<br />
<br />
“Oh! My God,” aliongea mzee huyo kwa sauti ya juu baada ya kuona bandeji iliyotapakaa damu ikiwa imefungwa kuzungukwa kichwa cha mtoto wake.<br />
Machela ikapitishwa na wauguzi ambao hawakuongea kitu chochote zaidi ya neno moja tu.<br />
“Pole sana mzee.”<br />
“Ataamka baada ya saa ngapi?”<br />
<br />
“Saa kumi na mbili kuanza sasa.”<br />
“Mh!” Fedorov aliguna hakika kwa kumwangalia tu mzee huyo ungegundua kwamba tayari alishachoka moyo na tumaini lote lilishapotea katika maisha yake mpaka kufikia hapo kwa umri aliokuwa nao hakuwahi kukutana na changamoto kubwa kama hiyo.<br />
<br />
Machela ikasukumwa na kuingizwa chumba cha wagonjwa mahututi pembeni tu ya pacha mwenzake ambaye yeye kwa wakati huo tayari alishaanza kufungua macho na kuuliza maswali kadhaa japo kwa taabu akitaka kufahamu ni kitu gani kilitokea.<br />
Victor Fedorov akatakiwa kusubiri nje ya chumba hicho kwa muda mwingine wa saa kumi na mbili.<br />
Je, nini kinaendelea hapa? Mtoto atapona na kurejea katika hali yake ya kawaida baada ya tatizo kuondolewa? SONGA NAYO…<br />
<br />
“Paa! Paa! Paaa!” Ulikuwa ni mlio wa bastola ndani ya chumba kidogo chenye mwanga hafifu na mzee mfupi aliyejazia misuli akiwa amesimama mbele ya kijana mmoja akionekana mwenye hasira kali.<br />
“Usiniu…naomba uni…”<br />
“Unasema?”<br />
“Tafadhali mzee wangu kama ni huo mgawo wangu basi mimi nakuachia zote lakini wewe pia ufikirie maisha yangu.”<br />
<br />
“Ha! Haaaa!” Sauti ya kicheko kikali ikasikika tena mzee aliyesimama mbele ya kijana huyo huku akiwa amenyoosha bastola akashuka mkono wake na kuanza kutembea kumfuata mahali alipokuwa.<br />
“Simama,” alitamka kwa sauti ya ukali.<br />
“Mh!”<br />
“Ina manaa hujaelewa, nasema simama upesi.”<br />
<br />
Kijana yule bila kusema tena kitu akaanza kujivuta kutoka sakafuni na aliposimama tu wima vitu kama maji maji vilionekana kuchuruzika kutoka ndani ya suruali yake kwenda chini.<br />
“Hee! Umejikojolea?”<br />
“Nisamehe mzee wangu si kusudio langu ni bahati mbaya.”<br />
“Unaumwa?”<br />
“Hapana ni woga tu.”<br />
<br />
“Lakini wewe ni mtoto wa kiume unatakiwa kuwa shupavu.”<br />
“Mh!” Kijana huyo alibaki akiguna tu huku akiwa amekodoa macho yote kumwangalia mzee huyo.<br />
Kwa ishara akaongozwa ili kusogelea meza ambayo juu yake ilikuwa na begi.<br />
“Fungua,” mzee huyo aliamuru.<br />
<br />
Taratibu kijana akalisogelea begi na kuanza kulifungua huku akionyesha hofu nyingi machoni mwake. Kwa sekunde tatu tu tayari alishamaliza kulifungua na idadi kubwa ya noti ikaonekana ndani yake.<br />
“Tayari mzee,” aliongea kwa sauti ya upole.<br />
“Sawa kabisa, sasa nisikilize vyema tena kwa umakini mkubwa,”<br />
“Ndiyo mzee.”<br />
<br />
“Kwa kuwa umeonyesha kufanya kazi vyema na mimi tena kwa ujasiri wa hali ya juu nikiamini kabisa kwamba hakukuwa na madhara yoyote yaliyotokea juu ya watoto, basi nakupa mgawo huu, uende ukaanze maisha na kumbuka mtu aliyesimama mbele yako si mtu mzuri hata kidogo, upande wake wa pili unatisha sitasita kutoa uhai wako pale utakapokuwa umenisaliti au kufanya jambo tofauti na kiapo chetu, mambo yote yaliyotokea ndani ya chumba hiki ilikuwa ni kukupima imani, nilitaka kujua jinsi unavyoweza kuhimili vishindo.”<br />
“Ndiyo mzee.”<br />
<br />
“Una hakika watoto wako salama? Nisingependa kusikia watoto wamekufa kwani hawana hatia hata kidogo, mwenye hatia ni baba yao ambaye nitashughulika naye mwenyewe.”<br />
“Mh! Mzee sina uhakika ila watakuwa wazima.”<br />
“Haya kamata hii halafu utokomee nisikuone mbele ya macho yangu,”aliongea mzee huyo akimkabidhi kijana maburungutu ya noti yasiyopungua kumi. Akazungusha macho yake huku na kule ndani ya chumba hicho na kufanikiwa kuona mfuko mmoja mchafumchafu, huo ndiyo aliutumia kuweka fedha zake zote alizokabidhiwa muda mfupi uliopita akamshukuru mzee huyo na kuanza kutembea kuelekea nje.<br />
<br />
“Kumbuka hutakiwi kusema kitu chochote juu ya maisha yangu, sawa?”<br />
“Sawa mzee hakuna shida.”<br />
“Tumia fedha hizo kuendeleza maisha yako, hivi sasa wewe ni mtu mzima.”<br />
“Ahsante mzee wangu nami pia nakutakia maisha mema, utakapokuwa na shida usisite kunitafuta...,” aliongea kijana huyo akitokomea.<br />
<br />
Hivyo ndivyo Ditrov alivyoagana na kijana huyo kisha kwa kujiamini kabisa akatembea kulisogelea begi lililokuwa juu ya meza akalinyanyua na kumwaga fedha zote juu ya meza.<br />
“Yap! Federov alikuwa hajui anacheza na mtu wa aina gani, hajui kwamba sisi tulishatangulia zamani, sasa asubiri kisasi changu ni lazima nitamtenda ubaya…,” aliongea Ditrov kwa kujiamini.<br />
<br />
***<br />
Upasuaji ndani ya chumba ulifanyika kwa umakini mkubwa na hatimaye wakafanikiwa kulitoa bonge la damu lililokuwa limengandamiza ubongo wa mtoto Merina, wakarudisha kila kitu katika sehemu yake na wakamtoa kumpeleka chumba cha wagonjwa mahututi huku akiwa amefungiwa mashine ya hewa ya oksijeni ili kumsaidia kuvuta hewa safi.<br />
Muda wote huo Fedorov bado alikuwa nje ya mlango wa chumba hicho akizunguka huku na kule.<br />
<br />
“Ametoka!” alitamka baada tu ya kuona machela ikisukumwa kutoka ndani ya chumba cha upasuaji kutolewa nje.<br />
“Mzee tumefanikiwa kuondoa damu iliyoonekana na tunaamini sasa mtoto ataendelea vizuri lakini yahitaji saa kumi na mbili tena kupata fahamu zake,” aliongea daktari na machela ikasukumwa moja kwa moja chumba cha wagonjwa mahututi Fedovor akitakiwa kusubiri mpaka muda huo ufike na angepewa taarifa zote.<br />
<br />
Nje ya chumba hakutulia kabisa, alitaka kufahamu kila kitu kilichoendelea ndani ya wodi mara kadhaa akitupa macho kwenye saa yake ya mkononi kuangalia wakati hatimaye mpaka wakati huo saa kumi na mbili zilishapita hivyo mbele yake alikuwa na saa mbili tu muda alioelezwa na madaktari ufike na mtoto wake Merina kurejewa na fahamu. Macho yake yaliendelea kushuhudia wauguzi na madaktari wakitoka na kuingia kama vile walipeana zamu ndani ya chumba huku naye hofu ikimgubika likiwa limebaki saa moja tu mbele yake.<br />
<br />
***<br />
“Baba! Baba!” Aliita kwa sauti iliyosikika ndani ya chumba.<br />
“Mh!” muuguzi ndani ya wodi aliguna kuonyesha mshangao wa ajabu kwani kitendo alichokishuhudia hakikuwa cha kawaida mtoto Mariya alikuwa amenyanyuka na kuketi kitako kitandani.<br />
“Amemwita baba yake,” waliongea wakisogea karibu na kitanda alichokuwa mtoto huyo.”<br />
“Unajisikiaje?” walimuuliza.<br />
<br />
“Merina! Merina”<br />
“Unaitwa nani?”<br />
“Namtaka baba yangu…Merina uko wapi?” aliongea mtoto huyo huku akinyanyua mikono yake na kushika kichwa chake akakutana na bendeji kubwa, hiyo ndiyo ilimfanya azidi kulia.<br />
“Baaaaba!” akapaza sauti.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.97<br />
<br />
“Namtaka baba yangu…Merina uko wapi?” aliongea mtoto huyo huku akinyanyua mikono yake na kushika kichwa chake akakutana na bendeji kubwa, hiyo ndiyo iliyomfanya azidi kulia zaidi.<br />
“Baaaaba!” akapaza sauti.<br />
“Hebu mwiteni baba yake aje hapa haraka, hatakiwi kuongea muda mrefu kutokana na hali yake,” daktari aliongea kwa msisitizo na muuguzi akaonekana akitoka nje <span class="text_exposed_show">huku akikimbia.<br />
<br />
“Mzee tafadhali tunakuomba ndani ya chumba.”<br />
“Mh! Tatizo jingine tena,” aliongea tajiri Federov akinyanyuka kutoka chini alipokuwa ameketi, taratibu akatembea na kuingia ndani ya chumba ambako aliongozwa moja kwa moja mpaka mahali watoto wake pacha walipokuwa wamelala juu ya vitanda.<br />
Kwa macho yake akamshuhudia Mariya akiwa ameketi juu ya kitanda na alipotokeza tu mtoto huyo akaita tena kwa sauti ya juu.<br />
“Babaaa!”<br />
<br />
“Mwanangu, umeamka?”<br />
“Sogea karibu yangu baba.”<br />
Fedorov akasogea kisha akainamisha kichwa chake karibu kabisa na mwanaye, hapo akaachia mabusu mfululizo huku naye akilia.<br />
“Nini kimetokea baba? Kwa nini niko hapa? Merina, je, yuko wapi?”<br />
“Mh!” Watu wote ndani ya chumba waliguna. Hakukuwa na jibu kamili la kumpa Mariya kwamba pacha mwenzake alikuwa mgonjwa taabani muda mfupi uliopita.<br />
<br />
“Nataka kumwona Merina,” Mariya alizidi kusisitiza huku akizungusha kichwa chake huku na kule ndani ya chumba kama vile alikuwa akitafuta kitu fulani.<br />
Kwa nusu saa nzima walikuwa wamejaribu kumnyamazisha Mariya lakini ilionekana kushindikana, ni hapo ndipo daktari aliposhauri mtoto huyo aelezwe ukweli kwani kutokana na afya yake hakutakiwa kupata msongo wa mawazo ili kunusuru matatizo mengine yasitokee kwenye upasuaji wake wa kichwa.<br />
“Merina,” Fedorov aliita.<br />
<br />
“Mh!”<br />
“Merina yule pale, yeye bado hajaamka.”<br />
“Hajaamka? Kwa nini kalala mpaka sasa?”<br />
“La hasha si usingizi wa kawaida bali anaumwa.”<br />
“Anaumwa nini?” Aliuliza huku akizungusha mikono yake kushika sehemu ya kichwa.<br />
“Mwanangu hata wewe ni mgonjwa na hapa tulipo tupo hospitalini kwa muda sasa.”<br />
<br />
“Ina maana tunaumwa wote?”<br />
“Huo ndiyo ukweli.”<br />
“Basi nataka niende kumwona, si mmesema ndiye yule pale,” aliongea Mariya akielekeza kidole upande aliokuwa ameonyeshwa.<br />
Daktari aliyekuwa ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi akatakiwa kutoa ushauri kwani ili mtoto huyo anyamaze, ilikuwa ni lazima asogezwe mpaka karibu na kitanda cha pacha wake.<br />
“Kwa sababu kitanda kina magudurumu kisogezwe taratibu kwa uangalifu mkubwa mpaka pale ili akamwone mwenzake, nadhani baada ya jambo hilo ataacha kulia.”<br />
<br />
Ushauri uliotolewa na daktari ukafuatwa, taratibu kitanda kikaanza kusukumwa kuelekea eneo ambako kulikuwa na kitanda kingine ambacho juu yake alilala Merina akiwa hajitambui kabisa.<br />
“Huyu hapa Merina.”<br />
“Maskini wa Mungu kilitokea nini baba?”<br />
“Mlipata ajali mbaya, hiyo ndiyo iliyosababisha ninyi nyote kuwa hapa mkiwa mmeumia vibaya.”<br />
<br />
“Ajali! Baba!” Aliongea Mariya lakini kabla hajaenda mbali zaidi tukio zima la jinsi walivyotekwa na mwanaume wasiyemfahamu kisha kuwafungia mahali ambako walipata mateso wakiwa hawana chakula wala maji liliingia kichwani mwa Mariya kama sinema.<br />
“Baba na yule aliyetufunga vitambaa na kutupakiza ndani ya gari kisha kuturusha kama…” kwikwi ya kulia ikamkaba, alikumbuka kila kitu kilichotokea siku nyingi nyuma.<br />
“Nyamaza kulia mwanangu hayo yote yalishapita cha muhimu ni afya zenu.”<br />
<br />
“Lakini baba mbona mimi nimeamka na Merina bado, kwa nini?”<br />
“Huyu alipatwa na tatizo ambalo ilibidi afanyiwe tena upasuaji kwa mara ya pili lakini ataamka muda si mrefu.”<br />
“Napenda iwe hivyo, sipendi kumkosa nampenda mno,” aliongea Mariya akionyesha msisitizo.<br />
Baada ya mazungumzo hayo walimsihi arejeshwe sehemu alikokuwa lakini alionekana kugoma akisisitiza kubaki eneo hilohilo mpaka mwenzake aamke ili aongee naye.<br />
<br />
“Nitakaa hapahapa mpaka aamke, nataka kuongea naye, najua anasikia ila kujibu tu ndiyo tatizo…Merina! Merina tafadhali amka mimi Mariya nakuita… nakupenda sana, pia baba yuko hapa naye anataka kuona umeamka ili uongee nasi tunakumi…,” aliongea mtoto huyo kwa uchungu jambo lililowafanya wauguzi na madaktari waliokuwepo ndani ya chumba nao walengwe na machozi.<br />
Wakiwa katika mawazo hayo ghafla jambo lisilokuwa la kawaida likatokea.<br />
“Mh! Mh!” Ilikuwa ni sauti ya mguno kutoka kwa Merina, tayari zilishatimia saa kumi na mbili tangu atoke chumba cha upasuaji, watu wote wakaonekana kupigwa butwaa.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.98<br />
<br />
MIAKA mitatu baadaye furaha ikiendelea kutawala ndani ya familia ya Phillip na mkewe Lina, mtoto Genevieve akiendelea kukua vyema mara kadhaa wawakilishi kutoka kituo cha Msimbazi cha kulelea watoto walikwenda nyumbani kwa Phillip kufuatilia maisha aliyoishi mtoto huyo, walionyesha furaha na kumshukuru Mungu kwani alipata mapenzi yote ya baba na mama. <br />
“Hakika<span class="text_exposed_show"> Genevieve amekuwa binti mkubwa sasa.”<br />
<br />
“Sisi pia tunamshukuru Mungu kwa afya na baraka anazompa mtoto huyu.”<br />
“Amina,” aliongea Sista Maryjoyce.<br />
“Lakini pia anasoma shule nzuri sana mtoto wetu.”<br />
“Ah! Inaitwaje?”<br />
<br />
“Inaitwa FEZA huko ndiko tumeona inafaa na tunashukuru hata walimu pia wanatupa ushirikiano mzuri sana.”<br />
“Hakika mtoto huyu alikuwa anasubiri ujio wenu katika kituo chetu, hebu mwone nadhani anajua jinsi mnavyompenda.”<br />
“Hata sisi tunaona hivyo, tunaomba tu tuendelee kumwona akikua vyema.”<br />
“Hizo ni baraka za kila mzazi mwenye watoto.”<br />
<br />
Waliongea mengi huku wakiburudika kwa vinywaji, masista hawakusita kutoa sifa zao kwa familia ya Phillip wakimwombea kwa Mungu azidi kuwa na moyo huo mpaka mwisho. Baada ya mazungumzo hayo kwa sababu saa zilikuwa zimesonga sana wakaomba ruhusa ya kuondoka kurejea kwenye makazi yao, wakakubaliwa na kuondoka.<br />
Genevieve hakuwa mbali na mahali walipokuwa wameketi hivyo alipoona tu watu wakinyanyuka vitini alifahamu wazi kwamba walikuwa wakiondoka kitendo ambacho hakukipenda hivyo kuangua kilio.<br />
“Usilie mtoto mzuri tunakupenda tutakuja tena kukutembelea siku nyingine, sawa?” Sista MaryJoyce aliongea akimbembeleza Genevieve.<br />
<br />
***<br />
Mapenzi yote ya Phillip yakatoka kwa Lina na kuhamia kwa Genevieve, alitumia muda mwingi kukaa na mtoto huyo kuliko ilivyokuwa kwa mkewe jambo ambalo lilianza kuleta matatizo kwani Lina pia akitaka apate nafasi kwa mumewe.<br />
“Mume nami pia nahitaji mapenzi yako unanishangaza sana kutwa kucha wewe na mtoto tu… huna tena muda wa kuwa nami,” Lina aliongea siku moja wakiwa wameketi bustanini nje ya nyumba yao.<br />
<br />
“Lina yaani unasikia wivu hata kwa mtoto wetu? Mke wangu jamani si hivyo kumbuka ni mtoto huyu huyu aliyekuwa akitugombanisha mimi na wewe, tafadhali mpatie naye nafasi mbona mimi silalamiki pale unapomchukua na kutoka naye?”<br />
“Ah! Unajua nini?”<br />
“Mh!”<br />
“Naona kama umenisahau sana, maana kila ukitoka na kurudi mkononi umebeba zawadi zake tu mimi ah!”<br />
<br />
“Haa!Haa!Haaa! Lina huo ni wivu tu mke wangu achana nao hebu tushirikiane kumlea mtoto wetu bwana, Mungu ametubariki ametupa mtoto mzuri kweli kweli huyu akikua atakuwa tishio, nitashikia watu bastola.”<br />
“Mh! Haya ngoja tuone itakuwaje, mwaa!mwaa!” Lina aliongea akisogea karibu na Phillip kisha kumwachia mabusu kwenye paji lake la uso.<br />
“Ahsante! Mwaaa, hebu twende ndani kwanza mara moja” Phillip naye akajibu kwa busu huku akimtaka Lina waingie ndani.<br />
“Kufanya nini?”<br />
<br />
“Nasema hivi twende ndani.”<br />
“Mtoto je?”<br />
“Atabaki na Magdalena hana shida.”<br />
“Na wewe,” Lina aliyemfahamu Phillip kupita maelezo aliongea kwani mara kadhaa alipomtaka kwenda ndani basi lazima kulikuwa na jambo.<br />
“Hivi wewe umenielewa nakuhitaji ndani haraka sana,” Phillip aliongea akionyesha msisitizo na tayari alishaanza kupiga hatua kuondoka eneo hilo.<br />
<br />
Lina bila ubishi naye akaanza kufuata nyuma akiwa na mtoto alipoingia tu sebuleni akamkabidhi mtoto kwa Magdalena kisha naye kufuata nyayo kuingia chumbani.<br />
“Funga mlango kwa funguo,” alitamka Phillip.<br />
“Unataka kunipiga?”<br />
“La hasha mwanamke huwa hapigwi kwa ngumi na mateka, anapigwa kwa kipande cha khanga lakini wewe sitakupiga hivyo nita…” Phillip aliongea huku akimvuta Lina na kumtupia juu ya kitanda.<br />
<br />
***<br />
Miezi mitatu baadaye tayari afya za watoto wawili pacha Mariya na Merina zilikuwa zikindelea vizuri hatimaye wakawa wameruhusiwa kurejea nyumbani wakitakiwa kuhudhuria kliniki zao kila baada ya mwezi mmoja ili kuwaangalia kwa ukaribu.<br />
“Ahsanteni madaktari na Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya watoto wangu, sijui ningekuwa mgeni wa nani hapa duniani bila ya kuwa na watoto, utajiri wangu wote usingekuwa na maana, hakika ninawapenda sana wanangu,” aliongea Fedorov akichomoa burungutu la fedha na kuwapa madaktari pamoja na wauguzi kama ahsante kwa jinsi walivyojitoa kwake.<br />
<br />
“Ah! Mzee hakuna haja sisi ndiyo kazi yetu bwana.”<br />
“Najua ndiyo kazi yenu lakini hii si rushwa nawapa soda tu jamani ndugu zangu, tafadhali pokeeni vinginevyo nitajisikia vibaya sana.”<br />
Mabishano yakawa yametokea kwa muda wa dakika tano nzima, wakipiga hatua hiyo ya Federov kutoa fedha mfukoni mwake na kuwapatia lakini aliposihi na kubembeleza sana hatimaye walizipokea na kumshukuru.<br />
<br />
Utaratibu maalum ukafanyika na watoto wakachukuliwa kupelekwa nyumbani ambako furaha iliendelea, akawapokea tena na kuwakaribisha wao pia walikuwa na furaha lakini zaidi ya yote walitaka kufahamu ni kitu gani kilisababisha mpaka wakawa katika hali ile.<br />
“Wanangu ni historia ndefu sana sioni kama kuna haja ya kuwasimulia…nadhani mtaumia na nisingependa jambo hilo litokee tena, kwa ushauri wa madaktari hamtakiwi kupata kitu kitakachowafanya mfikirie sana.”<br />
“Basi baba hakuna shida lakini tunalo ombi moja kwako.”<br />
<br />
“Ombi gani tena?”<br />
“Tunataka kuendelea na shule ikiwezekana hata kesho.”<br />
“Hakuna shida mpumzike kwa muda wa wiki moja hivi halafu wiki inayofuata mtaanza tena shule.”<br />
“Ahsante baba tunakupenda sana,” waliongea Mariya na Merina kisha kunyanyuka vitini na kumsogelea baba yao, wakamkumbatia na kuanza kububujikwa machozi.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.99<br />
<br />
<br />
MIAKA kumi na tano baadaye.<br />
Maisha nyumbani kwa tajiri Victor Fedorov yaliendelea, Mariya na Merina walisahau kabisa mambo yote yaliyotokea maishani mwao.<br />
<span class="text_exposed_show"> Kilichotawala katika familia hiyo kilikuwa ni upendo, furaha na amani. Fedorov alihakikisha anafanya kila kitu kuwapa furaha watoto wake.<br />
Akiwa ameketi na Mariya na Merina, aliwaeleza kwamba maisha hayakuwa rahisi kama walivyofikiria hivyo kuwataka wasome kwa bidii ili nao wapate kitu ambacho kitaongoza maisha yao.<br />
<br />
“Nataka msome tena kwa bidii nami nitawaunga mkono kwa kila jambo, sawa wanangu?”<br />
“Ndiyo baba nasi hatutakuangusha.”<br />
Watoto hao kwa sababu walimpenda sana baba yao walijitahidi kufanya kila kilichokuwa kizuri ili wasimtie aibu, kwani walipata kila kitu walichohitaji.<br />
Hakika walijivunia kuwa na baba kama Fedorov bila kufahamu kwamba nyuma yake hakuwa mtu mzuri, alikuwa mtu hatari aliyeogopwa na kila mtu.<br />
<br />
“Nitahakikisha watoto hawa hawagundui jambo lolote linalohusu maisha yao na yangu,” aliongea Fedorov akisogelea kabati kubwa lililokuwa ndani ya chumba na kulifungua, taratibu akionekana mwenye wasiwasi mwingi akachomoa kitu kama faili na kuketi kitako juu ya kitanda.<br />
Kwa umakini wa hali ya juu akaanza kusoma karatasi moja baada ya nyingine. Lilikuwa ni faili lenye siri kubwa ambayo aliamini kabisa kwamba hakuwepo mtu yeyote aliyefahamu siri hiyo.<br />
“Maskini wa Mungu,” aliongea akigeuza shingo yake huku na kule na alipohakikisha kwamba hapakuwa na mtu aliyemwona akasogea tena mpaka kabatini na kulirejesha faili na kufunga mlango.<br />
<br />
“Nitahakikisha hakuna mtu hata mmoja atakayefahamu umafia nilioucheza, itabaki kuwa siri yangu tu.”<br />
Maneno aliyokuwa ameapa Fedorov yalimaanisha alichokisema lakini yeye kama mwanadamu hakufahamu kabisa kwamba maisha yake yalikuwa mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Alikuwa amefanikiwa kuficha siri kwa kuua watu wote waliofahamu umafia alioutenda.<br />
Ndani ya faili alilolihifadhi kabatini, kuliandikwa kila kitu jinsi alivyofanikiwa kuteka watoto wawili yaani Mariya na Merina kutoka Tanzania na kuwafikisha nchini Urusi huku akihakikisha wanafutwa kumbukumbu zote na kuwafanya wamtambue yeye kama baba yao, jambo ambalo lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa lakini pia mauaji ya Ditrov na wenzake ili kuficha mpango mzima wa utekaji nyara.<br />
<br />
Pia kulikuwa na wosia mzito juu ya mali na fedha zote alizokuwa nazo akiagiza kama litatokea lolote basi huo ndiyo urithi kwa watoto wake hao. Alipohakikisha kila kitu kimekwenda sawa, akapanda kitandani na kujilaza.<br />
***<br />
Kilichokuwa kinasikika ndani ya chumba kwa wakati huo ni kelele za kitanda tu, kwa zaidi ya saa tatu mfululizo Phillip na mkewe Lina walikuwa wakiwajibika ipasavyo.<br />
“Leo ndiyo leo asemaye kesho ni mwongo, Lina ukweli nakupenda kutoka ndani ya moyo wangu na furaha hiyo imeongezeka zaidi baada ya mtoto wetu Genevieve kuingia ndani ya familia yetu…mwaaa”.<br />
<br />
“Ahsante Phillip nami pia ninakupenda kuliko maelezo ndiyo maana sikuwaza kukusaliti hata mara moja, ingawa nilikuwa na uwezo huo.”<br />
“Mh! Usiseme hivyo mke wangu ni shetani tu, nilitamani kuitwa baba.”<br />
“Nami nililifahamu jambo hilo mapema ndiyo maana nikapata wazo la kuasili mtoto na kweli umekubali na sasa tunaye Genevieve.”<br />
“Nitampenda mtoto huyu mpaka mwisho, sipo tayari kuona akiteseka wakati nikiwa hai, sasa ni wakati wa mimi na wewe kufanya kazi kwa bidii ili mtoto aishi maisha ya kifalme baadaye au?”<br />
<br />
“Umesema kweli mu…” Lina alishindwa kumalizi sentensi yake, kigugumizi kikaonekana kumkamata.<br />
Waliendelea kubaki ndani ya chumba kwa muda mwingine wa saa mbili na kutimiza saa tano kamili.<br />
“Mume wangu sasa inatosha ni vyema tukatoka kwenda kumwangalia mtoto wetu ametumisi sana jamani.”<br />
“Umesema kweli kabisa lakini ni lazima nasi tupate nafasi kama hii.”<br />
“Ahsante nimeamini kwamba kweli unanipenda.”<br />
<br />
“Saaana!” Phillip aliongea akinyanyuka kitandani kuelekea bafuni kuoga.<br />
Hayo ndiyo yakawa maisha yao wakifurahia mtoto aliyeingia ndani ya familia yao, wote wakiamini kwamba ameleta upya furaha katika nyumba yao, kila mmoja akiahidi kumpenda na kumtunza kwa hali na mali lakini mapenzi ya Phillip yalionekana wazi kwa sababu mtoto huyo alipewa jina la marehemu mke wake.<br />
“Hatimaye Genevieve amerudi tena katika maisha yangu…,” aliwaza kichwani mwake akitoka ndani ya chumba kuelekea sebuleni.<br />
“Phillip nimekumbuka jambo moja.”<br />
<br />
“Lipi tena hilo?”<br />
“Kesho ni siku ya kutembelea makaburi ya ndugu zetu kuangalia na kuyaweka safi, sijui unakumbuka?”<br />
“Mh! Ahsante sana kwa kunikumbusha, ndiyo maana Mungu amenipa mwanamke kama wewe, hakika unajali.”<br />
Ilikuwa ni kama desturi kwa Phillip kutembelea makaburi ya mke na watoto wake kufanya ibada kisha kufanya usafi ikiwa ni ishara mojawapo ya kuwaenzi.<br />
<br />
***<br />
Tayari Mariya na Merina walishatimiza umri wa miaka kumi na nane na walihitimu elimu yao ya chuo kikuu, walitamani sana kufanya kazi lakini msimamo wa baba yao ulihitaji waendelee kusoma zaidi ili waje kuongoza makampuni aliyokuwa nayo, hivyo walitakiwa kupumzika kidogo kisha kuendelea na masomo ya juu zaidi.<br />
“Nataka muendelee kusoma zaidi ninyi ndiyo warithi wangu, mtapumzika kidogo halafu mtaendelea na masomo sijui mnataka kwenda nchi gani kwa mapumziko?”<br />
<br />
“Mh! Baba tunataka tukae hapahapa na wewe, hatuwezi kwenda mbali na upeo wa macho yako.”<br />
“Basi sawa na ni zawadi gani mnapenda?”<br />
“Mh! Gari aina ya Ferrari.”<br />
<br />
“Wow! Wazo hilo ndilo lilikuwa akilini mwangu, nilitaka kuwafanya miongoni mwa mastaa mjulikane ulimwengu mzima kama mimi ninavyojulikana.”<br />
“Ahsante baba kwa mapenzi unayotuonyesha, hakika unatupenda.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.100<br />
<br />
<br />
TAYARI ilikuwa imeshatimia miaka kumi huku mtoto Geneveive akikua vyema na akiendelea na masomo yake katika shule ya Feza, mapenzi mema aliyopewa na wazazi wake wawili yalimfanya ajisikie mwenye furaha sana.<br />
Phillip na Lina walimtunza na kumfanyia kila lililo jema wakihakikisha hapungukiwi na kitu chochote maishani mwake.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Phillip ni vyema sasa tukamweleza mtoto huyu siri ambayo tumeiweka ndani ya mioyo yetu kwa muda mrefu.”<br />
“Lina!” Phillip alimwita mkewe kwa mshangao.<br />
<br />
“Ni lazima siku moja aje kuufahamu ukweli mume wangu.”<br />
“Najua hilo lakini si sasa, bado umri wake ni mdogo, anahitaji kukua zaidi.”<br />
“Mh! Haya kumbuka lakini sisi ni binadamu lolote linaweza kutokea.”<br />
“Lina tafadhali achana na fikra potofu,” aliongea Phillip huku akimwita Genevieve asogee karibu yake.<br />
Alihakikisha mtoto huyo anapata mapenzi ya dhati kutoka kwake na mkewe, hakuwa tayari kuona mtoto huyo akiumia wala kuumizwa na mtu mwingine.<br />
<br />
“Nakupenda sana mwanangu.”<br />
“Ahsante baba yangu nakupenda pia.”<br />
“Genevieve mimi pia ninakupenda,” aliongea Lina akiachia tabasamu mdomoni mwake.<br />
Hayo ndiyo yakawa maisha yao ndani ya nyumba, kuonesha mapenzi ya dhati kwa vitendo na maneno kwa Genevieve huku wakiitunza siri ya kwamba hawakuwa wazazi wake wa kumzaa bali walimuasili kutoka katika kituo cha watoto Yatima cha Msimbazi.<br />
<br />
Waliendelea kubaki sebuleni kwa mazungumzo wakiongea na kufurahi pamoja, mara kadhaa wakimsisitiza mtoto Genevieve umuhimu wa shule, wakimtaka asome kwa bidii kwani elimu ndiyo ulikuwa urithi wake mkubwa katika maisha yake ya baadaye.<br />
“Chakula tayari karibuni mezani,” ilikuwa ni sauti ya mfanyakazi wa ndani, Magdalena akiwakaribisha mezani kwa ajili ya chakula, wakamshukuru na kusogea mezani.<br />
<br />
Saa mbili baadaye walishapumzika vya kutosha na mmoja baada ya mwingine wakaaga na kuingia ndani ya vyumba vyao kupumzika kwa ajili ya siku iliyofuata, Lina na Phillip nao wakiingia ndani ya chumba chao.<br />
“Mke wangu kusema ukweli ninakupenda sana.”<br />
“Mimi pia nakupenda Phillip sikuwahi kumpenda mwanaume mwingine maishani mwangu kama ilivyokuwa kwako.”<br />
“Ahsante kwa kunipenda lakini ninataka kukueleza kitu kimoja.”<br />
<br />
“Kitu gani?”<br />
“Ninapokuwa na wewe hivi huwa sichoki kufanya tendo la ndoa na wewe, nakuhitaji kila wakati mke wangu…mh! Unajua nini?...hebu sogea hapa…” aliongea Phillip kwa sauti ya kutetemeka huku akimvuta Lina upande aliokuwa ameketi yeye.<br />
“Mh! Mh! Bwa…na” aliongea Lina kwa sauti ya chini chini huku akisogea kumfuata mumewe.<br />
<br />
***<br />
Mapenzi makubwa aliyokuwa nayo kwa watoto wake alihakikisha wanayafaidi maisha yote mazuri, akiwapa kila kitu muhimu maishani, hivyo, baada ya maongezi yao kukamilika na watoto kuhitaji zawadi ya gari kama ambavyo baba yao alivyowauliza aliahidi kuwatafuta gari hilo ndani ya saa ishirini na nne tu.<br />
<br />
Saa sita zikakatika watoto Mariya na Merina wakimsubiri baba yao kwa hamu kubwa, ghafla wakasikia sauti ya honi nje ya lango la kuingia ndani ya nyumba yao, haraka wakanyanyuka kwenye viti kuelekea langoni ambako mlinzi alishafungua kuruhusu gari kuingia.<br />
“Gosh!” walijikuta wakitamka maneno hayo.<br />
Mbele ya macho yao yalishuhudia gari aina ya Ferrari ambalo walilihitaji ndani yake kukiwa na mwanaume mmoja aliyejazia misuli, akaliendesha na kuliingia ndani kisha kuliegesha sehemu maalum na kushuka.<br />
<br />
“Naitwa Ford niko hapa kwa maelezo ya bosi Fedorov,” aliongea mwanaume huyo.<br />
Mariya na Merina hawakujibu kitu chochote macho yao yalikuwa bize yakishangaa huku na kule kuangalia gari hilo, wakiongea wenyewe katika mioyo yao na kujijibu.<br />
“Hallow” aliita mwanaume huyo.<br />
<br />
“Subiri kwanza kaka tutaongea baadaye.<br />
Kwa muda wa nusu saa nzima waliendelea kulishangaa gari lililokuwa ndani ya ngome yao, wakijiuliza maswali mbalimbali na waliporidhika walimsogelea mwanaume aliyekuwa pembeni na kuongea naye akajitambulisha tena kwa mara ya pili kwao.<br />
“Ahaa! Karibu sana.<br />
<br />
“Mimi naitwa Mariya na huyu anaitwa Merina ni watoto wa Victor Fedorov.”<br />
“Vizuri nimetumwa na bosi wangu kuja hapa nyumbani si kuleta tu gari hili bali pia mimi ndiye nitakuwa dereva wenu kwa muda.”<br />
“Oh! Ahsante baba yuko wapi?”<br />
“Atakuja muda si mrefu mimi nimetangulia.<br />
<br />
Wakiwa katika maongezi hayo haikuchukua hata dakika tano, honi nyingine ikasikika nje ya lango la kuingilia ndani ya nyumba, mlinzi akaongekana akifungua lango na gari ya Fedorov kuingia ndani huku akipiga honi nyingi kuashiria furaha, akaliendesha gari mpaka sehemu ya maegesho akaliegesha na kushuka na watoto wake wote wawili wakamkimbilia na kumkumbatia huku wakimbusu kwa wingi katika mashavu yake.<br />
<br />
“I love you daddy,”(tunakupenda baba) walitamka maneno hayo wakimwangalia baba yao kwa macho ya upole.<br />
“I love you too,”(Nawapenda pia) Fedorov alijibu huku machozi yakimtiririka mashavuni mwake.<br />
“Baba kwa nini unalia?”<br />
“Mh! Hapana”<br />
<br />
“Tafadhali tueleze nini kimekupata huko ulikotoka?”<br />
“Hakuna kitu wanangu ila…”<br />
“Bosi! Bosi! Nini kimetokea nini huko utokako?”<br />
Victor Fedorov hakuwa na jibu la kutoa kwa wakati huo akasogea taratibu na kuketi pembeni ya msingi uliokuwepo hapo kwikwi za kulia zikamkamata.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Ni kwa nini analia? Tukutane kesho km kawa nite nite!!!</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP. 101.<br />
<br />
“NAITWA Ford niko hapa kwa maelezo ya bosi Fedorov,” aliongea mwanaume huyo.<br />
Mariya na Merina wakati hawakujibu kitu chochote macho yao yalikuwa bize yakishangaa huku na kule kuangalia gari hilo wakiongea wenyewe na kujijibu.<br />
“Hallow!” aliita mwanaume huyo.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Subiri kwanza kaka tutaongea baadaye,” alijibu Merina.<br />
<br />
Kwa muda wa nusu saa nzima waliendelea kushangaa gari lililokuwa ndani ya ngome yao wakijiuliza maswali mbalimbali na waliporidhika walimsogelea mwanaume aliyekuwa pembeni na kuongea naye akajitambulisha tena kwa mara ya pili.<br />
“Ahaa! Karibu sana. Mimi naitwa Mariya na huyu anaitwa Merina ni watoto wa Victor Fedorov.”<br />
“Vizuri nimetumwa na bosi wangu kuja hapa nyumbani si kuleta tu gari hili bali pia mimi ndiye nitakuwa dereva wenu kwa muda..”<br />
“Oh! Ahsante, baba yuko wapi?”<br />
<br />
“Atakuja muda si mrefu mimi nimetangulia.”<br />
Wakiwa katika maongezi hayo haikuchukua hata dakika tano honi nyingine ikasikika nje ya lango la kuingikua ndani ya nyumba mlinzi akaonekana akifungua lango na gari la Fedorov kuingia ndani huku akipiga honi nyingi na kuashiria furaha, akaliendesha mpaka sehemu ya maegesho, akaegesha na kushuka na watoto wake wote wawili wakamkimbilia na kumkumbatia huku wakimpiga mabusu mengi.<br />
“We love you daddy!” (Tunakupenda baba) walitamka maneno hayo wakimwangalia baba yao kwa macho ya upole.<br />
“I love you too!” (Nawapenda pia) Fedorov alijibu huku machozi yakitiririka mashavuni mwake.<br />
<br />
“Baba kwa nini unalia?”<br />
“Mh! Hapana.”<br />
“Tafadhali tueleze nini kimekupata huko ulikotoka?”<br />
“Hakuna kitu wanangu ila…”<br />
<br />
“Bosi! Bosi! Nini kimetokea huko utokako?”<br />
Victor Fedorov hakuwa na jibu la kutoa kwa wakati huo, akasogea taratibu na kuketi pembeni mwa msingi uliokuwepo hapo, kwikwi ya kulia ikamkamata.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
“TAFADHALI tueleze nini tatizo?”<br />
“Mh!”<br />
“Baba kwa nini unatuweka roho juu?”<br />
“Naomba nitamke wazi leo…” kwikwi ya kulia ikamkamata tena Fedorov na kuangua kilio kama mtoto mdogo.<br />
Kwa takribani dakika tano nzima waliendelea kubaki eneo hilo wakiwa wameshikwa na butwaa wakiwa hawaelewi ni kitu gani kilikuwa kimetokea huko alikokuwa kabla ya kufika nyumbani.<br />
<br />
Walipohakikisha ametulia hawakuchoka kuendelea kumuuliza tena.<br />
“Mnajua nini?”<br />
“Eh!”<br />
“Ninawapenda sana wanangu historia yenu inanikumbusha maisha ya nyuma ambayo yanaumiza kupita maelezo.”<br />
“Baba lakini ya kale yamepita na tazama yamekuwa mapya. Unamkumbuka mama yetu?”<br />
“Mh!”<br />
<br />
“Unakumbuka nini?”<br />
“Jinsi nilivyowalea mpaka kufikia hapa nikiwa sina msaada wowote.”<br />
“Lakini baba hata sisi tunakupenda kupita maelezo.”<br />
“Najua wanangu nami nawapenda pia.”<br />
“Ahsante kwa zawadi nzuri ya gari.”<br />
<br />
“Ni wajibu wangu kufanya hivyo kwenu kama wanangu na huyu hapa mbele yetu ndiye atakuwa dereva wenu mpaka mtakapokuwa mmefuzu vyema udereva, atawapeleka kokote mtakapotaka na kuhakikisha anawapa ulinzi wa kutosha.”<br />
“Ahsante baba,” walijibu Mariya na Merina wakitabasamu.<br />
“Leo nitaomba tujumuike wote kwa chakula cha jioni ili kukamilisha furaha yetu wanangu na kesho ninafikiria kufanya matembezi kidogo kwenye mchezo wa kuteleza kwenye barafu.”<br />
“Babaaa!”<br />
<br />
“Ni kweli kabisa kwa sasa ni msimu mzuri wa kwenda huko nitaondoka na nitarejea baada ya wiki tatu.”<br />
“Twende wote.”<br />
“Hapana acha mimi niende kwanza nikirudi mara nyingine nitawachukua wote.”<br />
“Sawa baba tutashukuru.”<br />
Wakaingia ndani na kujiandaa kwa ajili ya kutoka kwenda kula chakula cha jioni kama familia wakifurahia maisha na mapenzi makubwa waliyoyapata kutoka kwa baba yao. Kwa muda wa saa nzima walikuwa chumbani wakijiandaa na waliporidhika walitoka.<br />
“Wow!” sauti ya Fedorov ilisikika baada tu ya kuwaona watoto wake wakitoka chumbani.<br />
<br />
“Heheee!” walicheka.<br />
“Mmempendeza sana wanangu hakika ninyi ni mabinti wazuri sana.”<br />
“Ahsante baba.”<br />
Wakatembea kwa mwendo wa madaha na kulielekea gari lao aina ya Ferarri na kuingia ndani ambapo Fedorov naye akaingia kwenye gari lake, yeye ndiye akawa mtu wa kwanza kutoka ndani, gari walilopanda watoto wake likifuata kwa nyuma.<br />
Kwa mwendo wa nusu saa hivi walikuwa barabarani hatimaye wakafika kwenye mgahawa maarufu wa Kalinin. Fedorov akawa wa kwanza kushuka ndani ya gari na kubaki kusubiri watoto pamoja na dereva washuke ili waingie wote kwa pamoja.<br />
<br />
Akionekana wenye furaha, akawakumbatia watoto wake na kuanza kutembea kuingia ndani ya mgahawa, wote wakionekana wenye furaha kupita maelezo. Kwa umaarufu na utajiri aliokuwa nao mzee huyo nchini Urusi alipewa heshima kubwa sana, alipokelewa kwa furaha na wafanyakazi karibu wote katika mgahawa huo na akaongozwa kupelekwa sehemu maalum kabisa akikaribishwa mara nyingi.<br />
“Leo nimekuja na watoto wangu, huyu hapa anaitwa Mariya na huyu ni Merina, huyu mwingine ni dereva wao anaitwa Ford,” aliongea Fedorov kwa kujiamini kabisa.<br />
<br />
“Karibuni sana ndugu zetu.”<br />
Menu yenye orodha ya chakula na vinywaji ikawekwa mezani na mhudumu akiwataka wachague kitu ambacho wangependa kula na kunywa siku hiyo na wakionekana wenye furaha, kila mmoja aliagiza alichotamani kula.<br />
Wakala na kunywa wakifurahi pamoja na baada ya hapo walilipa na kuondoka na kuingia maduka mbalimbali kununua vitu walivyohitaji na kurejea nyumbani.<br />
<br />
“Usiku mwema wanangu!”<br />
“Kwako pia baba!”<br />
Wakaingia ndani ya vyumba vyao na kulala na siku iliyofuata Fedorov ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kuamka ili ajiandae kwa safari ambayo ingemchukua muda wa wiki mbili mfululizo akiwaacha watoto wake peke yao nyumbani, akatoka chumbani akiwa tayari na mizigo yake kisha kugonga mlango wa chumba cha watoto wake huku akiwaita majina akiwaaga na akiwatakia kila lililo jema na kutoa maelekezo ya mahali ambako wangechukua fedha za matumizi kwa muda wote ambao hangekuwepo.<br />
<br />
Kwa pamoja wakamrukia baba yao na kumkumbatia wakimtakia safari njema na kumtaka awahi kurejea nyumbani kwani kwa muda ambao hatakuwepo watakuwa wapweke sana.<br />
“Nitarejea muda si mrefu, mwaa ninawapenda sana,” aliongea lakini watoto wake walipomwangalia vyema usoni mwake waligundua alikuwa akibubujikwa na machozi na walipomuuliza ni kwa nini alipatwa na hali hiyo Fedorov hakujibu kitu zaidi ya kuanza kutembea kuelekea nje ya nyumba yake akiwa na begi kubwa mgongoni mwake.<br />
<br />
***<br />
“Phillip! Phillip!” Lina aliita mfululizo<br />
“Naam!”<br />
“Ah! Najisikia vibaya.”<br />
“Kidogo tu mke wangu sita…”<br />
“Mh! Siyo hivyo mwenzio najisikia kizunguzungu.”<br />
<br />
“Kizunguzungu?” aliuliza kwa mshangao.<br />
“Ndiyo, nipe…”<br />
“Lina acha basi utani wako unanicha…”<br />
“Hapana Phillip naumwa mbona naona giza!”<br />
“Eh!”<br />
<br />
“Nipe maji ya kunywa fanya haraka kabla sija…” aliongea Lina lakini kabla hajamalizia sentensi yake ukimya wa ajabu ukatokea na Phillip alipojaribu kumwita na kumtingisha hakupata ushirikiano wowote zaidi ya yote alimshuhudia Lina akilegea kama mlenda.<br />
“Mungu wangu! Kimetokea nini?” alijiuliza akimlaza Lina vyema kitandani na yeye kushuka kitandani.<br />
Phillip akalisogelea taulo lililokuwa pembeni na kujifunga kiunoni, jasho jingi likimtiririka.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP. 102<br />
<br />
Nipe maji ya kunywa fanya haraka kabla sija…,” aliongea Lina lakini kabla hajamalizia sentensi yake ukimya wa ajabu ukatokea na Phillip alipojaribu kumwita na kumtingisha hakupata ushirikiano wowote, zaidi ya yote alimshuhudia Lina akilegea kama mlenda.<br />
“Mungu wangu! Kimetokea nini?” alijiuliza akimlaza Lina vyema kitandani na yeye kushuka haraka kitandani, har<span class="text_exposed_show">aka akachukua taulo lililokuwa pembeni na kufunga kiunoni jasho jingi likimtiririka. Kitu kilichokuwa kikitokea mbele yake kilionekana kuwa ni ndoto kama siyo muujiza, akakizunguka chumba huku na kule akifikiria cha kufanya.<br />
<br />
“Lina! Lina mke wangu kimetokea nini?” aliita Phillip lakini hakupata jibu lolote kutoka kwa mkewe aliyekuwa kitandani akiwa ametulia kimya.<br />
“Hapa ni hospitali tu, hakuna kingine cha kufanya,” aliongea Phillip.<br />
Akiwa amechanganyikiwa alivaa shati kisha kumvalisha Lina, akausogelea mlango na kuufungua huku akiita jina la Bibi Magdalena ili aje kumsaidia.<br />
<br />
“Njoo haraka! Tafadhali njoo upesi,” alisisitiza Phillip.<br />
Haraka bila kuchelewa, Bibi Magdalena aliingia chumbani kwa Phillip na kumkuta Lina akiwa amelala kimya kitandani huku mumewe akizunguka huku na kule.<br />
“Nini kimetokea bosi wangu?”<br />
“Lina amenyamaza ghafla,” Phillip alimjibu Bibi Magdalena.<br />
“Umempiga?”<br />
<br />
“Huu si muda muafaka wa kuuliza hivyo tusaidieni nimpeleke hospitali,” Phillip alimwambia Bibi Magdalena.<br />
“Sawa bosi.”<br />
Haraka Phillip akamnyanyua Lina, Bibi Magdalena akitangulia mbele kufungua mlango, walipofika kwenye gari lililofunguliwa mlango, walimuingiza Lina na kumlaza siti ya nyuma kisha Phillip akazunguka upande wa pili na kuingia.<br />
Kabla hajaondoka, alimuaga Bibi Magdalena na kumwambia akifika hospitali atamfahamisha kilichomsibu mkewe.<br />
<br />
“Haya kila la kheri,” alijibu Bibi Magdalena akitembea kurejea ndani, furaha yote iliyokuwepo muda mchache uliopita ilikuwa imetoweka.<br />
“Sijui kapatwa na nini?” alijiuliza bibi huyo akiingia ndani.<br />
Kwa muda wa saa tatu na nusu Phillip bado alikuwa hajarejea, wasiwasi ukaugubika moyo wa Bibi Magdalana akitaka kufahamu ni kitu gani kilitokea huko alikokuwa Phillip na mkewe Lina ambaye alikuwa mgonjwa taaban.<br />
<br />
Saa zilipozidi kusonga mtoto Geneveve alianza kumsumbua Bibi Magdalena akitaka kujua wazazi wake walikuwa wapi.<br />
Bila kujibu kitu chochote yeye mwenyewe akiwa na wasiwasi mwingi moyoni mwake alimtuliza mtoto Theresia na kumtaka atulie kwani wazazi wake wangerejea muda si mrefu, akatoka nje na kuelekea kwa mlinzi na kumweleza wazi wasiwasi aliokuwa nao.<br />
“Hebu tusubiri kidogo pengine wako njiani.”<br />
“Mh! Ni muda sana mtoto naye ananisumbua sijui wamepatwa na kitu gani, eh haya ni matatizo mengine tena!” aliongea bibi huyo akionyesha kulengwalengwa na machozi.<br />
<br />
Ghafla wakiwa katika maongezi hayo, honi ikasikika nje ya lango la kuingilia ndani ya nyumba yao.<br />
“Si hao!” aliongea mlinzi akilisogelea lango na kufungua, hakuwa amekosea gari la bosi wake lilikuwa limesimama nje ya lango hilo.<br />
Taratibu bila kusema kitu akionekana mwenye mawazo mengi kichwani mwake, Phillip akaendesha gari mpaka sehemu ya maegesho. Alipoangalia kwenye kibaraza cha nyumba yake, akamshuhudia mtoto wake Genevieve akikimbia kumfuata.<br />
<br />
“Dady why are you crying?”(Baba kwa nini unalia?)<br />
“It’s too painful,”(Inauma sana)<br />
“What?”(Nini?)<br />
Kwikwi ya kulia ikamkaba Phillip, akajikuta akilia mbele ya mtoto wake kitu kilichozidi kumchanganya zaidi Genevieve, naye bila kutegemea akaanza kuangulia kilio.<br />
<br />
***<br />
Fedorov alitembea hatua mbili na kugeuka nyuma kuwaangalia watoto wake, hakuonekana kuwa na furaha kama ilivyokuwa siku zote aliposafiri kwenda mbali.<br />
Alipolifikia gari lake, akafungua sehemu ya kuweka mizigo akaweka begi na vifaa alivyokuwa navyo ndani kisha akawaita tena watoto wake;<br />
“Mariya, Merina.”<br />
<br />
“Bee,” waliitika wakikimbia kumfuata na walipomfikia karibu waligundua baba yao alikuwa tofauti kabisa.<br />
“Lakini unaonekana hauko sawa?” Merina aliuliza.<br />
“Unajua nini?”<br />
“Mh!”<br />
“Ninasikia sauti ndani ya moyo wake ikiniambia kwamba nisiwaache.”<br />
“Basi twende wote baba!”<br />
<br />
“Hapana nataka mbaki nyumbani nami niende kwenye mchezo huo nitarejea tu niombeeni wanangu,” aliongea Fedorov huku akiwakumbatia watoto wake.<br />
“Lakini umesema moyo wako hautaki kwenda huko?”<br />
“Hivyo ndivyo ninavyosikia ila acheni niende.”<br />
“Mh!” Mariya aliguna yeye pia alihisi kitu fulani ndani ya moyo wake lakini akajaribu kupingana na hisia hizo ili kumfanya baba yake arejee katika hali yake ya kawaida.<br />
<br />
“Nawapenda sana wanangu mbaki salama, nitarejea baada ya wiki mbili, mnapenda niwaletee nini nikirudi?”<br />
“Mh! Mh!”<br />
“Semeni basi!” aliongea Fedorov akifungua mlango ili aingie garini.<br />
“Tuletee zawadi ya saa.”<br />
“Hilo tu?”<br />
“Mh!” Waliitikia kwa kuguna huku wakitingisha vichwa vyao kuonyesha ishara ya kukubali.<br />
<br />
Fedorov akaingia ndani ya gari na kuliwasha kisha taratibu huku akiwaangalia watoto wake akaliendesha gari hadi langoni ambako mlinzi alifungua kisha akatoka ndani.<br />
“See you then,”(Tutaonana) ndiyo maneno pekee aliyoongea akitokomea.<br />
Wiki ya kwanza ikakatika hatimaye ikaja ya pili Mariya na Merina wakiwa tayari kumsubiri baba yao bila matarajio, walipojaribu kufanya mawasiliano naye kwa njia ya simu ya upepo bado Fedorov hakupatikana wakaanza kuingiwa na wasiwasi kwani halikuwa jambo la kawaida na kibaya zaidi safari hiyo aliondoka peke yake bila ya mlinzi.<br />
“Hivi unafikiri baba atakuwa wapi mpaka sasa?”<br />
<br />
“Kwa kweli sijui ila tusubiri tuone pengine yuko njiani.”<br />
“Mh! Nahisi hatari fulani ndani ya moyo wangu…,” aliongea Merina kwa sauti ya upole.<br />
Hatimaye wakiwa katika kusubiri wiki ya tatu ikaanza kuyoyoma bila baba yao kutokea, wakaingiwa na hofu na kuamua kutoa taarifa za kupotea kwa baba yao katika vituo mbalimbali vya televisheni na redio lakini hata baada ya matangazo kutolewa mzee huyo hakuonekana.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Fedorov yuko wapi? Nini kimempata Lina?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP. 103.<br />
<br />
MWEZI mmoja ulikuwa umekatika tayari watoto Mariya na Merina wakiwa katika kusubiri, mioyo yao ikiwa na huzuni kubwa kupita maelezo, ni mlinzi wa nyumbani kwao na dereva aliyewaendesha ndiyo waliotoa faraja kwa watoto hao wakiwapa moyo kwamba ipo siku Fedorov angerejea na huko alikokuwa hakukuwa na tatizo lolote kwani kama lingekuwepo mpaka wakati huo wange<span class="text_exposed_show">shapewa taarifa.<br />
“Msiwe na hofu atarejea tu, huyu mtu ni mfanyabishara pengine ameshatoka huko na kuelekea nchi nyingine.”<br />
“Lakini bila kusema kitu chochote?” Merina alihoji.<br />
<br />
“Inawezekana anajua hakuna kitu kibaya.”<br />
“Hapana mimi ninawaeleza wazi kabisa ipo sauti ndani ya moyo wangu inanieleza jambo fulani la hatari, lazima kuna tatizo,” Mariya aliongea akibubujikwa na machozi.<br />
“Usilie nyamaza baba atarejea tu tena si muda mrefu.”<br />
“Mimi nashauri tutoe taarifa polisi.”<br />
<br />
”Juu ya nini?”<br />
“Upoteaji wa baba yetu, mimi ninawaambia lazima atakuwa kwenye matatizo makubwa sana kama siyo kifo.”<br />
“Mh!” Wote wakaguna kwa mshangao.<br />
Baada ya maongezi hayo kwisha kila mmoja akionekana kuwa na msongo wa mawazo kichwani mwake, Mariya na Merina walinyanyuka na kuingia ndani ya chumba ambamo kwa takribani nusu saa nzima waliendelea kubaki huku wakiwaacha mlinzi na dereva waliokuwa wameketi bustanini wakiendelea kujiuliza maswali na ghafla wakiwa hapo wakawashuhudia tena watoto hao wakirejea.<br />
<br />
“Dereva tafadhali tupeleke.”<br />
“Wapi?”<br />
“Kituo cha polisi.”<br />
“Lakini tumepatana tuvute subira kidogo pengine yuko njiani anarejea.”<br />
“Hapana tumeamua twende tu polisi.”<br />
“Mh! Haya twendeni niwapeleke.”<br />
<br />
“Naweza kuongozana nanyi?” mlinzi aliuliza.<br />
“Hapana wewe baki tu hapa nyumbani tutarejea muda si mrefu.”<br />
“Sawa.”<br />
Wakatoka wakiongozana na dereva mpaka kwenye maegesho ya gari kisha wote wakafungua milango na kuingia ndani, Mariya na Merina wakiwa wameketi kiti cha nyuma na mara kadhaa wakiongea jambo fulani kwa kunong’ona.<br />
<br />
Gari likaendeshwa mpaka sehemu kulikokuwa na kituo cha polisi, hapo wakashuka na kuingia moja kwa moja ndani wakimtaka dereva aendelee kusubiri eneo lilelile.<br />
Wote wawili wakatembea na kuingia ndani ya kituo na kupokelewa na askari waliokuwa eneo hilo, kwa sababu ya umaarufu wao moja kwa moja wakaongozwa kuingia kwenye chumba maalum ambako walimkuta polisi akiwa ameketi akawakaribisha na kuwataka waeleze shida yao.<br />
“Ahsante sana,” aliongea Merina ambaye kwa kumwangalia tu machoni mwake ungegundua alikuwa akilia.<br />
“Kuna tatizo gani?” Polisi aliuliza.<br />
<br />
“Ni mwezi sasa umepita hatujui baba yetu yuko wapi?”<br />
“Tajiri Fedorov?”<br />
“Hujakosea,” Mariya alijibu.<br />
“Mh!” Polisi naye akaguna kuonyesha mshtuko, kwani historia ya mzee huyo ilifahamika nchini kote na kwa umafia wake aliogopwa na kila mtu.<br />
“Tunahitaji kutoa taarifa hii kwenu ili msako ufanyike haraka sana na kufahamu ni wapi alipo baba yetu, juu ya malipo hakuna shida ilimradi tu apatikane.”<br />
<br />
“Hata akiwa amekufa?”<br />
“Tunahitaji maiti yake.”<br />
“Basi hakuna shida tutafungua faili ambalo tutaandika malalamiko yenu kisha tutaanza msako na mnachotakiwa kufanya ni ninyi kutangaza kwenye vyombo vya habari vyote.”<br />
“Hakuna shida tutaifanya kazi hiyo, tunachotaka sisi ni kumpata baba yetu basi!” walijibu watoto hao kwa kujiamini.<br />
<br />
Baada ya kuhakikisha kwamba taarifa hiyo ilikuwa imefika jeshi la polisi, waliaga na kutoka nje wakitembea kuelekea lilipokuwa gari lao, wakapanda na dereva bila kusema kitu chochote akaliendesha moja kwa moja kuelekea nyumbani.<br />
Jambo moja lilitawala vichwa vyao: ni wapi baba yao alikuwa na kama alikuwa amekufa maisha yao yangekuwaje baada ya hapo?<br />
“Merina tunatakiwa tuanze kutangaza mara moja kwenye vyombo vya habari bila kuchelewa.”<br />
“Kazi hii tutampatia huyu dereva azunguke kwenye vyombo vyote vya habari hata kama watahitaji fedha lakini watoe tangazo hili.”<br />
“Hakuna shida.”<br />
<br />
Nusu saa tu baadaye gari lilishafika nyumbani kwa tajiri Fedorov, lango likafunguliwa na dereva kuingiza gari ndani wakashuka na kumsabahi mlinzi wao na hawakusema tena kitu chochote wakatokomea na kuingia ndani.<br />
Watoto hao waliendelea kubaki ndani ya chumba kwa zaidi ya saa tatu wakiongea mambo mbalimbali, hata mlango wa chumba chao ulipogongwa wakitakiwa kwenda kula waliendelea kugoma wakitoa agizo kwamba watu wengine waendelee nao wangejumuika baadaye.<br />
Hata walipoitwa tena baada ya saa sita waliendelea kubaki chumbani na safari hii hawakusikika wakijibu kitu chochote zaidi ya ukimya tu.<br />
“Mh! Wanafanya nini hawa?”<br />
<br />
“Sijui hata wakiitwa hawaitiki.”<br />
“Wasije kuwa wamechukua maamuzi mabaya.”<br />
“Haiwezekani hebu tuchungulie dirishani.”<br />
Mlinzi na dereva wakazunguka nyuma ya nyumba na kuelekea sehemu dirisha la chumba cha watoto hao lilipokuwa na walipojaribu kutupa macho yao ndani yalikutana na pazia zito likiwa limefunikwa kwenye dirisha hilo.<br />
***<br />
“Genevieve?” Phillip aliita kwa sauti ya upole.<br />
“Bee baba!”<br />
“Si kwamba napenda kulia mwanangu lakini…” kwikwi ya kulia ikamkaba tena Phillip akaangua kilio mbele ya mtoto wake.<br />
“Tafadhali nyamaza na utueleze tatizo, nini kimetokea huko?” Magdalena aliyekuwa mfanyakazi wa ndani nyumbani kwa Phillip aliongea.<br />
<br />
<br />
“Hali ya Lina ni mbaya sijui kama…” aliongea Phillip na kabla hajamalizia sentensi yake mlio wa simu ikiita ukasikika, taratibu akaingiza mkono wake mfukoni na kuichomoa haraka kisha akatupa macho kwenye kioo cha simu ili asome jina.<br />
“Hospitali!” Alitamka Phillip kwa sauti ya juu.<br />
<br />
Je, nini kinaendelea hapo? Simu iliyoingia ina ujumbe gani kwa Phillip? Fedorov, je, yuko wapi?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP. 104<br />
<br />
<br />
MSAKO nchini Urusi ulikuwa mkali kweli kweli polisi wakifanya kazi usiku na mchana kumsaka tajiri mkubwa nchini humo, Victor `Fedorov ambaye alitoweka katika mazingira ya kutatanisha, makundi kwa makundi yalikuwa yakigawanyika ambapo watu wengine walielekea sehemu ambako tajiri huyo alikwenda kwenye mchezo wa kuteleza katika barafu.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Mkuu tumefika mpaka hapa lakini hakuna mtu wala hakuna taarifa yoyote ile inayoonyesha kwamba kuna uhai wa mtu na kwa mujibu wa mazingira hatukushudia kitu chochote kinachoonyesha uwepo wa mwanadamu,” ilikuwa ni sauti ya polisi mmoja katika kundi la polisi wasiopungua kumi waliotumwa kwenda kufanya uchunguzi eneo ambalo ndilo hasa Fedorov aliaga kwenda huko.<br />
“Kitu gani kingine kimefanyika?”<br />
<br />
“Tumejaribu kwa uwezo wetu wote kuangalia pengine hata nyayo na nguo ili kuridhika na upelelezi wetu lakini hatujafanikiwa kuona kitu.”<br />
“Basi ni vyema mkarejea na kufanya mkakati mwingine.”<br />
“Sawa mkuu.”<br />
Simu ya upepo ikakatika na polisi wakajiandaa na kupanda ndani ya helikopta kisha kurejea jijini kwa mkakati mwingine.<br />
<br />
***<br />
Ndani ya chumba Mariya na Merina walikuwa wakipanga mkakati wa jinsi ya kumpata baba yao ambaye mpaka wakati huo hawakufahamu ni wapi alipokuwa na kama alikuwa mzima au la! Machozi na vilio vilitawala kila mmoja akionekana kumfariji mwenzake.<br />
“Baba atakuwa amekufa.”<br />
“Hapana usiseme hivyo.”<br />
<br />
“Nahisi hivyo si kawaida yake hata simu tu?”<br />
“Mh! Unasema kweli kwa jinsi anavyotupenda haiwezekani hata kidogo.”<br />
“Ngoja tuone uchunguzi wa polisi utasema nini?”<br />
“Hapana Merina ni muda mrefu sana…yapata miezi mitatu sasa lazina kuna tatizo mimi ninakuambia...”<br />
<br />
Mariya aliyekuwa ameketi kimya kitandani bila kujibu kitu machozi yakaonekana yakimbubujika, kichwani mwake hakupata picha kama kweli baba yao mpendwa angekuwa amekufa maisha bila yeye yangekuwaje? Ilikuwa ni picha ya kuumiza sana hakumfahamu mtu mwingine zaidi ya mlinzi na dereva waliyekuwa naye wakati huo.<br />
“Kama ikitokea mzee asionekane nini kitatokea katika maisha yetu?”<br />
“Kwa kweli sijui na hatukuwahi kumfahamu ndugu mwingine yeyote na kama sijakosea baba alitueleza kwamba mama yetu alifariki miaka mingi sana hivyo yeye ndiye alikuwa kila kitu.”<br />
<br />
“Sawa kabisa, kitu alichokuwa amekiongea Mariya kilikuwa ni ukweli, hawakufahamu ni kitu gani kingeendelea kwao, maisha yangekuwaje na ndugu wengine wangewafahamu vipi kwani Fedorov hakutaka kuwaeleza ukweli.<br />
“Lakini lazima kuna sehemu baba atakuwa ameandika kitu fulani hivi kweli hana ndugu?”<br />
“Wewe hivi unamjua vizuri baba?”<br />
“Namjua hebu…,” aliongea Merina akinyanyuka kitandani na kuanza kutembea kuelekea mlangoni akitoa ishara ya kumwita Mariya.<br />
“Twende huku.”<br />
<br />
“Wapi?”<br />
“Wewe twende tu utaona ninachotaka kwenda kufanya.”<br />
Baada tu ya kutoka ndani ya chumba chao wote wawili wakapiga hatua tatu kusonga mbele ambako macho yao yalikutana na mlango wa kioo hicho ndicho kilikuwa chumba cha baba yao.<br />
“Tuingie huku chumbani.”<br />
“Kufanya nini wakati ni chumba cha baba?”<br />
<br />
‘Wewe nifuate mimi acha ubishi wako.”Haraka bila kujiuliza mara mbili wakaufungua mlango na kuzama ndani Mariya akionyesha hofu kubwa.<br />
Kwa saa tatu mfululizo waliendelea kubaki ndani ya chumba cha mzee wao wakifanya upekuzi kila kona kusoma na kutafuta mahali ambako wangegundua kuwepo kwa nyaraka zozote za siri ambazo zingewazesha kupata angalau ndugu mmoja upande wa baba au mama yao. Lakini bado hawakufanikiwa mwisho nao wakaanza kukata tamaa kabisa lakini ghafla wakiwa hapo wakakumbuka kwamba walifanya upekuzi kila mahali na walikuwa wamesahau sehemu moja tu ndani ya chumba hicho kabati kubwa lililokuwa pembeni kabisa mwa chumba.<br />
<br />
“Bado hili kabati hapa.”<br />
“Ehhe kweli tulisahau.”<br />
Wote wakakimbia kulielekea kabati hilo na kufungua mlango mmoja baada ya mwingine kupekua ndani wakitoa nyaraka moja baada ya nyingine na kuzisoma lakini bado hawakuona sehemu yoyote ambayo iliandikwa kuonyesha kama Federov alikuwa nani na alitokea wapi akiwa na ndugu wangapi.<br />
<br />
“Mh! Mimi mwenzako nimechoka.”<br />
“Basi pumzika mimi niendelee lazima tupate kitu humu ndani ya hili kabati vinginevyo sitatoka hapa,” aliongea Merina akiangusha vitu kutoka ndani ya kabati bila kujali.<br />
“Mh!” Merina aliguna.<br />
<br />
“Nini?”<br />
“Hili kabrasha ni la nini?”<br />
“Hebu? Tena la rangi nyekundu?”<br />
“Fungua ndani tuone,” Mariya aliongea na taratibu akasogea karibu kushuhudia ni kitu gani kingeonekana ndani yake.<br />
<br />
Je, watoto hao watakutana na kitu gani ndani ya kabrasha hilo?</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3da5c6e08017422">MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP. 105<br />
<br />
Walikuwa wawili tu ndani ya chumba lakini kila mmoja alionekana kuwa na hofu, walitaka kufahamu ni kitu gani kilikuwa ndani ya kabrasha hilo na kibaya zaidi lilikuwa la rangi nyekundu na juu yake maneno “Nyaraka muhimu” yalisomeka.<br />
“Mh! Kwa nini maneno hayo?”<br />
“Hata mimi sijui ila ngoja tufungue tuone.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Mimi naogopa sana.”<br />
“Acha woga tunachotaka kufahamu sisi ni ndugu wa baba au upande wa mama yetu ambaye hatukuwahi kumfahamu.”<br />
“Haya fungua,” Mariya alizidi kusisitiza.<br />
Wakatembea na kuketi juu ya kitanda hapo wakiwa tayari kufungua kabrasha hilo na kwa ujasiri wa hali ya juu walilifungua na kuliacha wazi, kitu cha kwanza walichokishuhudia kilikuwa ni vyeti vilivyofungwa vizuri na vilivyoonyesha majina yao.<br />
“Majina yetu haya.”<br />
“Mh!” pacha mmoja aliguna na kuonyesha mshangao.<br />
Wakaendelea mbele zaidi kufunua katarasi nyingine, hapo walikutana na wosia mzito wa Victor Federov ukieleza kwamba yeye alikuwa nani na alitokea wapi, alizaliwa miaka mingapi iliyopita, haukuishia hapo ukaendelea mbele zaidi akitaja mali zote alizokuwa nazo na kiasi chote cha fedha alizokuwa nazo katika benki mbalimbali nchini Urusi, majengo makubwamakubwa na miradi mbalimbali na alitaka vitu hivyo vyote chini ya mwanasheria aliyekuwepo ndani ya wosia huo kama siku ikitokea akafa basi utajiri wote huo uende kwa watoto wake.<br />
Maneno yale yalichoma mioyo ya watoto hao, machozi mfululizo yakawabubujika wakilia na kuomboleza kwani mpaka wakati huo pamoja na kwamba walishatoa taarifa katika vyombo vya habari na taarifa nyingine kuzipeleka kwenye vyombo vya habari wakimtafuta baba yao kwa udi na uvumba, alikuwa bado hajapatikana.<br />
“Nahisi hatari fulani.”<br />
“Mimi pia naungana na wewe.”<br />
“Ni kwa nini baba aliamua kuandika kitu kama hiki? Je, alifahamu kwamba atakufa muda si mrefu? Na huyu mwanasheria ni nani?” walijiuliza maswali mfululizo.<br />
Huzuni ilikuwa imewagubika lakini pamoja na yote hayo bado hawakutaka kuacha kusoma nyaraka zote zilizokuwa ndani ya kabrasha hilo wakitaka kufahamu zaidi siri zilizokuwa ndani.<br />
“Historia kamili ya watoto Mariya na Merina ilipoanzia mpaka hapa walipo leo, jinsi walivyopatikana na nani hasa alikuwa ni mama yao mzazi” maneno hayo yalisomeka kwenye moja ya karatasi ndani ya kabrasha.<br />
“Mh!” wakaguna.<br />
Wakaendelea mbele zaidi na kukutana na jina Genevieve huyo ndiye alikuwa mama yao wa kuwazaa lakini mwanamke huyo aliolewa na mwanaume aliyeitwa Phillip na waliishi nchini Tanzania.<br />
Maswali mengi yaliendelea kuzunguka ndani ya vichwa vyao wakitaka kufahamu ukweli wa historia yao lakini kwa wakati huo hakuwepo mtu ambaye angewaeleza ukweli, mtu pekee waliyemtengemea alikuwa ni Victor Fedorov.<br />
“Baba anajua ukweli wote na sasa hayupo, hebu tuendelee mbele zaidi tutajua tu,” aliongea Merina akionyesha msisitizo.<br />
Kadiri walivyozidi kusonga mbele ndivyo mambo mengi makubwa yalivyoibuka na kuzidi kuwaacha midomo wazi bila kupata ufafanuzi wowote.<br />
“Mama yetu aliitwa Genevieve?”<br />
“Historia inaonyesha tulipatikana kwa kupandikizwa katika chupa?”<br />
Bado watoto hao waliendelea kujiuliza maswali mengi kichwani mwao huku huzuni ikigubika ndani ya mioyo yao, hakika walikuwa wamesoma kitu ambacho mpaka wanafikisha umri wa miaka kumi na nane hawakufahamu ukweli wa jambo lolote zaidi sana Fedorov ndiye alikuwa kila kitu.<br />
“Ni lazima tuzungumze na huyu mwanasheria pengine anaweza kutusaidia zaidi.”<br />
“Umeongea jambo la maana sana.”<br />
“Lakini kabla ya yote tusubiri kwanza tuone taarifa za polisi zitasemaje kuhusu baba yetu.”<br />
Hivyo ndivyo walivyokubaliana na waliamua kusubiri kwa muda mpaka miezi sita baadaye lakini bado Fedorov alikuwa hajapatikana nao pia wakaamini kabisa kwamba huenda baba yao alikufa katika mchezo wa barafu na maiti yake kufukiwa na theluji.<br />
Wakiwa wenye majonzi mioyoni mwao, walipanga kukutana na mwanasheria ambaye alikuwa kwenye nyaraka za Fedorov ili kuongea na kufahamu ukweli wa mambo yote.<br />
Waliamini huyo angeweza kuwasaidia kwa mambo yote muhimu na kufahamu zaidi utajiri wa baba yao, ni kweli wakafanikiwa kuonana naye na kuongea naye akawaambia alikuwa ameshtushwa na habari za kupotea kwa Fedorov lakini akawaahidi kwamba angefuatilia kwa karibu majibu ya polisi na angekuwa nao bega kwa bega.<br />
“Tunakushukuru kwa kila kitu lakini jambo moja tunaomba kutoka kwako.”<br />
“Hakuna shida.”<br />
“Pamoja na kwamba hivi sasa sisi ni watu wazima lakini tunahitaji uendelee kuwa mshauri na msimamizi wa mali za baba yetu.”<br />
“Niko tayari,” mwanasheria huyo aliongea kwa kujiamini.<br />
Wote kwa pamoja wakasimama na kumshika mkono huku wakimtaka kuwa karibu yao na kushirikiana naye kwa kila jambo, wakamshukuru na kuondoka kurejea nyumbani.<br />
“Wiki ijayo lazima tufunge safari kuelekea Tanzania tukamwone huyo anayedaiwa kuwa mama yetu,” Mariya aliongea na Merina akamuunga mkono.<br />
Maandalizi maalum yakafanyika na utaratibu ulipokamilika Mariya na Merina wakasafiri kuja Afrika ya Mashariki nchini Tanzania, hamu yote ikiwa ni kuwafahamu watu wawili Phillip na mkewe Genevieve, pamoja na kugundua ukweli wote wa jinsi walivyopatikana, walitamani kuwaona watu hao wakiamini kabisa kwamba walikuwa ni watu muhimu mno katika maisha yao.<br />
***<br />
“Haraka mpelekeni chumba cha wagonjwa mahututi na afungiwe mashine ya hewa ya oksijeni imsadie kupumua,” ilikuwa ni sauti ya daktari mmoja ndani ya wodi aliyekuwa akimhudumia Lina.<br />
“Kimetokea nini?”<br />
“Hali yake imebadilika ghafla, kwa inavyoonekana ana tatizo kubwa ndani ya kichwa chake ambalo linamsumbua.”<br />
“Mungu wangu na mume wake ameondoka sasa hivi kwenda nyumbani,” muuguzi aliongea.<br />
“Kama ana simu apigiwe haraka sana arudi hapa mara moja,” daktari alizidi kusisitiza.<br />
Muuguzi akachukua faili lililokuwa na kumbukumbu za Lina, hapo akakutana na namba ya mumewe Phillip, haraka bila kuchelewa akakimbia mpaka mapokezi ambako aliomba msaada wa kupigiwa namba hiyo.<br />
Haikuchukua hata dakika mbili tayari namba hiyo ikawa imeita.<br />
“Hallow, ndiyo hapa ni hospitali tunahitaji urejee haraka sana, hali ya mke wako ni mbaya na hivi sasa ninavyoongea na wewe tunajiandaa kumpeleka chumba cha wagonjwa mahututi…,” aliongea muuguzi huyo na simu ikakatika.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea?mzigo unaendelea kesho km kawa! love u all mwaaa!!gudnite!!!</span></div></span><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"><br />
</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012421161b050888010789">MSICHANA NDOTONI MWANGU.......EP. 106<br />
<br />
“Haraka mpelekeni chumba cha wagonjwa mahututi na afungiwe mashine ya hewa ya oksijeni imsaidie kupumua,” ilikuwa ni sauti ya daktari mmoja ndani ya wodi aliyekuwa akimhudumia Lina. <br />
“Kimetokea nini?”<br />
“Hali yake imebadilika ghafla kwa inavyoonekana ana tatizo kubwa ndani ya kichwa chake ambalo linamsumbua.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Mungu wangu na mume wake ameondoka sasa hivi kwenda nyumbani,” muuguzi aliongea.<br />
“Kama ana simu apigiwe haraka sana arudi hapa mara moja,” daktari alizidi kusisitiza.<br />
Muuguzi akachukua faili lililokuwa na kumbukumbu za Lina hapo akakutana na namba ya mumewe Phillip, haraka bila kuchelewa akakimbia mpaka mapokezi ambako aliomba msaada wa kupigiwa namba hiyo.<br />
Haikuchukua hata dakika mbili tayari namba hiyo ikawa imeita.<br />
“Hallow, ndiyo hapa ni hospitali tunahitaji urejee haraka sana hali ya mke wako ni mbaya na hivi sasa ninavyoongea na wewe tunajiandaa kumpeleka chumba cha wagonjwa mahututi…,” aliongea muuguzi huyo na simu ikakatika.<br />
“Wiki ijayo safari kuelekea Tanzania ni lazima, tukamwone huyo anayedaiwa kuwa mama yetu,” Mariya aliongea na Merina akamuunga mkono.<br />
Maandalizi maalum yakafanyika na utaratibu ulipokamilika Mariya na Merina wakasafiri kuja Afrika ya Mashariki nchini Tanzania, hamu yote ikiwa ni kuwafahamu watu wawili, Phillip na mkewe Genevieve pamoja na kugungua ukweli wote wa jinsi walivyopatikana, walitamani kuwaona watu hao wakiamini kabisa kwamba walikuwa ni muhimu mno katika maisha yao.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO...<br />
<br />
Taarifa walizokuwa wamezisoma Mariya na Merina kwenye kabrasha la siri la baba yao, hakika lilikuwa limewatia simanzi kubwa ndani ya mioyo yao, pamoja na kwamba waliufahamu ukweli wote lakini watoto hao walihitaji kumwona mama yao na mtu mwingine aliyekuwa ametajwa ndani ya nyaraka hizo aliyejulikana kama Phillip, walitamani kufika nchini Tanzania kwa gharama yoyote ile ilimradi tu wakutane na watu hao.<br />
<br />
<br />
Maandalizi yakafanyika haraka chini ya Mwanasheria wao wa familia ambaye ndiye alisimamia kila kitu na safari nzima ya watoto hao akihakikisha kwa fedha zilizokuwepo wangeweza kusafiri salama na kurejea salama bila matatizo yoyote yale.<br />
“Mariya lakini huyu ndiye baba yetu mzazi,”<br />
“Ni kweli kabisa hilo sina shaka nalo tatizo moja tu linakuja ni kwa nini baba hakuwa mkweli kwetu?”<br />
<br />
<br />
“Pengine alifahamu tukipata habari hizo tutaumia kwani kwa maelezo yaliyotolewa ni kwamba baba aliuza mbegu zake za kiume kwa familia ya Phillip ambazo zilipandikizwa kwa mwanamke aliyeitwa Genevieve huyo ndiye mama yetu lakini pia Phillip ni mtu muhimu kwetu ni kama baba ni lazima twende haraka, nakumbuka kuna wakati baba aliwahi kutueleza kwamba mama yetu alikufa, hivi inawezekana kweli?”<br />
“Inawezekana hawezi kusema uongo kama huo,”<br />
<br />
<br />
“Twende mambo mengine yote tutayajua huko huko?”<br />
“Tutafanya nini ili kuwafahamu watu hao?” Mariya alimuuliza Merina.<br />
“Tutatumia vyombo vya habari kutangaza na ikiwezekana kuzungumza kabisa na vyombo hivyo,” Merina alijibu.<br />
“Kivipi?”Mariya alihoji.<br />
<br />
<br />
“Fedha ni kila kitu kwetu,” Merina aliongea kwa kujiamini.<br />
Hivyo ndivyo walivyomaliza mazungumzo yao na kuanza kujitayarisha kwenda Afrika wakiwa hawaelewi kabisa ni wapi baba yao alipokuwa na alipatwa na kitu gani lakini walilazimika kufanya hivyo kwa sababu ya nyaraka za siri walizozisoma. Mioyo yao iliuma mara kadhaa walipomkumbuka baba yao, ucheshi,utani na mapenzi makubwa aliyokuwa nayo kwao hakika kwa wakati huo vilikuwa vimekosekana.<br />
<br />
<br />
“Mimi naona ni bora tukaondoka na huyu mwanasheria wetu ili akasaidie mchakato huu.”<br />
“Mh! Wazo zuri sana hebu tumpigie simu naye afanye maandalizi ili kesho jioni tuweze kuondoka.”<br />
<br />
Wakafanya kama walivyokubaliana simu ikapigwa na mwanasheria kupewa taarifa kwamba safari iliyokuwepo mbele yao ililazimu kuongozana nao kwa gharama yoyote.<br />
Hivyo ndivyo walivyofanya siku iliyofuata safari ikaanza, hamu yao kubwa ikiwa ni kuwafahamu watu hao wawili, Phillip na Genevieve, walitamani kuongea nao ili kufahamu ukweli juu ya nini kilichotokea.<br />
<br />
<br />
Safari yao ilisadikiwa kuchukua saa nane mpaka kufika nchini Tanzania ambako wangefanya utaratibu maalum wa kuwapata walengwa ambao walikuwa ni Phillip na Genevieve.<br />
***<br />
Simu iliyokuwa imeingia kwa Phillip ikimtaarifu kwamba alitakiwa kufika hospitalini mara moja ilikuwa imemchanganya kupita maelezo, akiwa hapo alihisi hatari na kuiona taa nyekundu ikiwaka ndani ya kichwa chake.<br />
<br />
<br />
“Lina! Lina atakuwa amezidiwa,” hivyo ndivyo alivyoongea huku akitweta na bila kuchelewa aliwaaga bibi Magdalena na mtoto wake Genevieve waliokuwa pembeni yake akiwaambia wazi kwamba alitakiwa kurejea hospitalini haraka sana.<br />
“Twende wote baba,” Genevieve aliongea.<br />
“Hapa…,” alijibu Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake bibi Magdalena aliingilia.<br />
“Ni lazima tuongozane nasi tufahamu nini kimetokea huko, hatuko tayari kubaki hapa nyumbani, sawa?”<br />
“Mh! Unajua.”<br />
<br />
<br />
“Phillip hakuna haja ya mabishano hapo Genevieve hebu twende…,” bibi Magdalena aliongea akimvuta Genevieve kuelekea kwenye gari.<br />
Wote wakaingia ndani na Phillip akiwa ndiye dereva alionekana kuwa mtu mwenye msongo mwingi wa mawazo lakini hayo ndiyo yalikuwa maisha hakuwa na mtu mwingine wa kumsaidia tatizo lililokuwa mbele yake, kwa kasi ya ajabu akaliendesha gari hatimaye akafanikiwa kufika hospitali ndani ya dakika kumi na tano tu.<br />
<br />
<br />
Haraka akaegesha gari sehemu maalum na kushuka mbio bila kusema chochote kuelekea chumba ambacho ndicho hasa Lina alilazwa, Genevieve na Magdalena wakimfuata kwa nyuma nao pia wakionekana wenye wasiwasi mwingi.<br />
<br />
<br />
Dakika tano tu baadaye alifanikiwa kufika kwenye wodi hiyo lakini alishangazwa na ukimya uliokuwepo eneo hilo, bila kuuliza wala kusubiri akausukuma mlango na kuzama ndani, kitanda kilikuwa kitupu.<br />
“Nini kimetokea?” alijiuliza na ghafla akiwa katika kujiuliza muuguzi aliingia ndani ya wodi hiyo.<br />
“Dada! Dada!” aliita mfululizo.<br />
“Ndiyo kaka yangu nakusikiliza.”<br />
“Nauliza mgonjwa aliyekuwa amelazwa hapa muda mchache tu, anaitwa Lina.”<br />
<br />
<br />
“Lina?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Mh!” badala ya kujibu muuguzi aliguna.<br />
“Kwa nini unaguna dada?” aliuliza Phillip akimwangalia muuguzi machoni na kugundua kitu tofauti.<br />
“Ah! Hebu subiri kidogo.”<br />
“Dada mbona sikuelewi tafadhali nieleze nini kimetokea hapa?” Phillip aliuliza akionyesha msisitizo.<br />
<br />
<br />
“Kaka hali ya mgonjwa imebadilika ghafla kwa ujumla ni mbaya…,” aliongea muuguzi huyo lakini hakumaliza sentensi yake mlango ukafunguliwa kwa nguvu.<br />
“Monica!” ilikuwa ni sauti ya kiume ikiita ndani ya wodi.<br />
“Bee!” aliitika muuguzi huyo.<br />
“Unagonja nini tunasubiri hilo faili haraka?”<br />
<br />
<br />
“Sawa daktari lakini kuna huyu kaka hapa anauliza kuhusu mgonjwa Lina.”<br />
“Hebu nifuateni nyuma haraka,” daktari huyo aliongea na wote wakaanza kutoka mbio kumfuata kwa nyuma.<br />
Hawakupiga hata hatua kumi mbele ya mlango uliokuwa umeandikwa ICU walishuhudia machela ikitolewa kwa mwendo wa kasi kupelekwa sehemu ambayo hawakuielewa, Phillip alikuwa wa kwanza kutupa macho juu yake na kumwonga Lina akiwa amelala kimya mdomoni mwake akiwa amefungwa mashine ya oksijeni.<br />
“Mke wangu!” aliongea kwa sauti ya juu.<br />
<br />
<br />
“Hali yake ni mbaya tunajaribu kuokoa maisha yake imetulazimu kumpeleka chumba cha upasuaji haraka sana…” aliongea daktari huku machela ikisukumwa kuingizwa ndani ya chumba cha upasuaji, Phillip, Genevieve pamoja na Magdalena wakitakiwa kubaki hapo kusubiri.</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3eb736b58713812"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012422c4a1f46f64684390">SICHANA NDOTONI MWANGU.......EP. 107<br />
<br />
Baada ya Lina kuingizwa chumba cha wagonjwa mahututi, uchunguzi maalum uliendelea na Phillip ndiye aliyetakiwa kutoa historia ya mkewe kwani kwa wakati huo hakuwa akijitambua. Akawa tayari kueleza kila kitu kilichomtokea mkewe ikiwepo ajali ya moto aliyoipata baada ya gari lake kuwaka moto.<br />
Katika kufanya uchunguzi kuwa rahisi, jopo la madaktari likaanza kazi<span class="text_exposed_show">, na ni hapo ndipo walipogundua kwamba jeraha la moto alilolipata Lina lilileta madhara makubwa sana kwa ndani, madhara ambayo hayakufahamika mapema hivyo walitaka kujaribu kumsaidia kwa kumfanyia upasuaji ili kuondoa tatizo lililoonekana ndani ya kichwa.<br />
Wakiwa katika hali ya kusubiri kuona kama angerejewa na fahamu zake ili kukamilisha vyema uchunguzi wao, hali ya Lina ilibadilika ghafla, ni hapo ndipo walipolazimika kumkimbiza chumba cha upasuaji ili kuokoa maisha yake.<br />
“Hali yake ni mbaya tunajaribu kuokoa maisha yake imetulazimu kumpeleka chumba cha upasuaji haraka sana…,” aliongea daktari huku machela ikisukumwa kuingizwa ndani ya chumba cha upasuaji, Phillip, Genevieve pamoja na Magdalena wakitakiwa kubaki hapo kusubiri. Hayo yalikuwa maneno pekee aliyotamka daktari na kuingia ndani ya chumba.<br />
Walibaki nje ya chumba wakionyesha hofu kubwa, Phillip yeye alishindwa kujizuia akajikuta akitokwa na machozi.<br />
“Baba usilie mama atapona tu,” Genevieve aliongea akimpigapiga baba yake.<br />
“Najua atapona lakini…” kwikwi ya kulia ikamkamata Phillip binafsi ndani ya moyo wake kwani aliufahamu ukweli kwamba Lina alikuwa katika hali ya kufa kwani ripoti ya uchunguzi iliyokuwa imefanyika ilionyesha wazi kwamba alikuwa na tatizo kubwa ndani ya kichwa chake na tayari lilikuwa limechelewa kupata ufumbuzi.<br />
Kwa muda wa saa nne mfululizo waliendelea kusubiri, hamu yao kubwa ikiwa ni kufahamu ni kitu gani kiliendelea ndani ya chumba cha upasuaji, macho na masikio yao yote yalielekea kwenye mlango wa chumba kuangalia na kusikiliza.<br />
“Mbona wamechukua muda mrefu sana,” aliuliza Phillip.<br />
“Inawezekana bado wanafanya upasuaji.”<br />
“Mh!”<br />
“Hebu tuvute subira kidogo tuangalie,” Magdalena aliongea akijaribu kumpa Phillip moyo wa matumaini.Waliendelea kusubiri saa nyingine mbili na kufanya idadi ya saa kutimia sita lakini bado hawakuona muuguzi wala daktari akitoka ndani ya chumba hicho, wakaanza kukata tamaa na mioyo yao kuhisi kuna jambo la hatari lilikuwa limetokea na taa nyekundu iliyoashiria hatari ikawa kichwani mwa Phillip.<br />
“Lazima kuna tatizo siyo rahisi,” aliongea Phillip akitembea kusogelea mlango wa chumba cha upasuaji, akapiga hatua tatu mbele lakini kabla hajanyanyua hatua ya nne mlango wa chumba hicho ukaonekana ukifunguliwa na mwanaume aliyevalia koti jeupe akatokeza, Phillip alipomwangalia alimgundua kwamba alikuwa ni daktari hivyo wakajikuta wakigonganisha macho na daktari akainama chini.<br />
Taratibu akionekana mwenye huzuni akamsogelea Phillip kisha akamsabahi na kumtaka kuongozana naye mpaka ofisini kwa maongezi zaidi.<br />
Ndani ya ofisi tu baada ya kuingia daktari hakutaka kupoteza muda zaidi alimtaka Phillip aketi kwenye kiti naye akaketi, ni hapo ndipo alipomweleza ukweli ambao alitakiwa kuufahamu.<br />
“Pole sana ndugu yetu, sisi kama madaktari pamoja na wauguzi tumejitahidi kadiri ya uwezo wetu wote kuokoa maisha ya mke wako lakini imeshindi…”<br />
“Lina wangu amefariki?” Phillip alitamka kwa sauti akinyanyuka kitini.<br />
“Wewe ni mwanaume hebu jikaze kidogo kwani hayo ndiyo maisha yetu.”<br />
“Daktari! Daktari unamaanisha unachosema?”<br />
“Ni kweli tupu mkeo amefariki dunia akiwa juu ya kitanda cha upasuaji muda mfupi tu baada ya kupasua kichwa chake.”<br />
“Uwiii!Uwiiii!” Phillip alipiga mayowe akiwa hataki kuamini maneno aliyoyasikia kutoka kwa daktari kwamba mkewe mpendwa alikuwa ameaga dunia.<br />
“Huo ndiyo ukweli wote, tunasikitika sana lakini pia tunakupa pole.”<br />
Phillip hakujibu kitu tena akanyanyuka kwenye kiti akaufungua mlango na kutoka mbio kuelekea chumba cha upasuaji huku akilia kwa sauti ambayo ndiyo iliyowashtua Genevieve na Magdalana waliokuwa wameketi nje ya wodi wakimsubiri.<br />
“Lina hayupo nasi tena, ameondoka ametuacha” aliongea Phillip huku akilia.<br />
“Lina amefariki?”<br />
“Huo ndiyo ukweli hatutamwona tena,” wakiwa hapo wakashuhudia mlango ukifunguliwa na machela iliyoonekana kubeba mtu juu yake akiwa amefunikwa kwa shuka la rangi ya kijani kuanzia kichwani hadi miguu ikapitishwa mbele yao.<br />
“Mke wangu! Huyu ni mke wangu nataka nimwone, Lina wangu kweli umeniacha kama alivyoniacha Genevieve?” Phillip alilia kwa uchungu akitamka maneno ya kuumiza moyo. Wakiwa hapo huku wote wakilia wakashuhudia machela ikisukumwa na kupelekwa chumba cha maiti.<br />
Huku wakiwa na uchungu mioyoni mwao wakaondoka kurejea nyumbani ili kufanya taratibu nyingine, taarifa mbalimbali zikatolewa juu ya tukio hilo, simu nyingi zilipigwa na watu wengi walifika nyumbani kwa Phillip kumpa pole na kuomboleza, wengi wao wakiwa wafanyakazi waliofanya kazi na Lina ofisi moja.<br />
Siku tatu zikatolewa kwa maombolezo, watu wakilia wengi wakisikitikia kifo kilichomkuta Lina. Familia za Phillip na Lina zikajumuika pamoja hatimaye mazishi yakafanyika Phillip akitaka mkewe huyo azikwe pembeni tu mwa kaburi la mkewe wa kwanza na watoto wake. Jambo hilo likafanikiwa na Lina akazikwa akiwaacha watu wengi katika majonzi, kwa Phillip ikionekana kuwa kama ndoto lakini huo ndiyo ulikuwa ukweli.<br />
Ni wiki moja tu baada ya Phillip kumzika mkewe mambo yalianza kubadilika, mara kadhaa akionekana kama mtu aliyekuwa na tatizo la akili na alipoulizwa hakuwa na jibu la kutoa zaidi ya kububujikwa na machozi, kazini nako mambo hayakwenda sawa hivyo wakalazimika kumpa likizo ya muda akae nyumbani pengine akili yake ingetulia.<br />
Ni kama vile uamuzi huo walikuwa wameukosea, kwani Phillip badala ya kubadilika hali ndiyo ikazidi kuwa mbaya, akawa mlevi kupindukia na kuongea peke yake, jambo lililozidi kuishangaza familia yake.<br />
“Baba kwa nini umekuwa hivyo?” Genevieve aliuliza. Alikuwa ni mtoto mdogo lakini alikuwa na upeo wa kufahamu mazuri na mabaya.<br />
“Dunia hainitendei haki, ilichukua mke na watoto wangu wawili na sasa imegeuka na kumchukua Lina… ni bora na mimi niwafuate na kuungana nao, bora nife…nasem…” aliongea huku kwikwi ya kulia ikimkaba, haraka akanyanyuka kutoka kitini na kukimbia kuelekea chumbani.<br />
“Baba!Baba!” mtoto Genevieve alikimbia kumfuata baba yake lakini tayari alishachelewa aliposhika mlango ili ausukume kuingia ndani ulionekana kufungwa.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da3f50b8208501829"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012422c49b509c67363695">MSICHANA NDOTONI MWANGU.......EP. 108<br />
<br />
Genevieve aliendelea kugonga mlango kwa muda bila baba yake kuitikia, naye pia akaanza kulia akimwita bibi Magdalena aje ili waungane kusaidia kumfanya Phillip afungue mlango. Kwa muda wa nusu saa nzima bado walisimama nje ya mlango wakimsihi Phillip afungue lakini hakufanya hivyo zaidi sauti ilisikika kutoka ndani ya chumba ikiwaeleza wazi kwamba alitaka ku<span class="text_exposed_show">fanya uamuzi mgumu hivyo alihitaji nafasi.<br />
“Phillip lakini ni vyema ukatambua kwamba maisha baada ya kifo cha mkeo ni lazima yaendelee.”<br />
“Najua hilo tangu mwanzo lakini inauma, ni bora nikaungana nao.”<br />
“Usimkufuru Mungu na huyu mtoto?”<br />
“Mtoto? Ah! Atapata wasamaria wema wengine wa kumtunza.”<br />
“Baba! Baba!” Genevieve aliita na kwikwi ya kulia ikamkaba, hakuongea tena kitu akatoka mbio eneo hilo na kukimbilia ndani ya chumba kisha naye kujifungia.<br />
Ukawa ni mtihani kwa bibi Magdalena hakufahamu nini afanye kwani kila kitu kilionekana kwenda kombo, kwa muda aliendelea kusimama eneo hilo akitafakari nini cha kufanya hatimaye wazo likamjia ndani ya kichwa chake kwamba ni lazima Phillip akubali kushuka kwani hali ya Genevieve ilikuwa mbaya kutokana na sentensi aliyokuwa ameitamka muda mfupi uliopita.<br />
“Genevieve ameumizwa na kauli yako, hivyo amekimbia kuelekea chumbani, kwa ujumla ameumia.”<br />
“Unasema?”<br />
“Hivyo ndivyo, tafadhali nakusihi utoke na kumwendea ili kumbembeleza.”<br />
Ukimya wa ajabu ukatokea na sekunde tatu tu mlango wa chumba ukaonekana ukifunguliwa na Phillip kutokeza huku jasho jingi likitiririka mwilini mwake, hakusema kitu zaidi ya kukimbia kuelekea upande ambako ndiko chumba cha Genevieve kilikuwepo. Akausukuma mlango na kuingia ndani ya chumba na kilichosikika muda mfupi tu ndani ya chumba hicho ni kilio, wote wawili walikuwa wakilia.<br />
***<br />
Ndani ya hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam ndimo Mariya, Merina na Mwanasheria wao walipokuwa wamefikia hapo ndipo pangekuwa nyumbani kwao kwa muda wote ambao wangekuwa Afrika, nchini Tanzania kusaka ukweli wa maisha ya baba yao Victor Federov kwa gharama yoyote ile.<br />
“Tutapumzika leo na kesho tutaanza mchakato, lazima kwanza tuitishe mkutano na waandishi wa habari lakini kabla ya hayo tunahitaji kukutana na mtu mmoja ambaye tutamfanya rafiki huyo ndiye atatusaidia.”<br />
“Mh! Naona kama ni zoezi gumu kidogo,” Mariya.<br />
“La hasha! Ni kitu rahisi nitampata mtu hapa hapa hotelini,” mwanasheria aliwaambia.<br />
“Haya ngoja tuone lakini pia uwe makini kwani hapa tupo ugenini,” Mariya alishauri.<br />
“Usiwe na shaka Mariya kila kitu kitakwenda sawia.”<br />
Baada ya mazungumzo hayo kukamilika pamoja na kwamba alikuwa ni mgeni kabisa, Morgan alitoka ndani ya hoteli hiyo kuangalia mazingira akitafuta ni namna gani angepata msaada ambao ungemsaidia kufanya kazi yake kwa urahisi, kwa kutumia lifti akashuka mpaka mapokezi hapo akawasabahi watu aliowakuta na ghafla kabla hajapiga hatua kutoka nje ya hoteli hiyo macho yake yakagongana na mtu aliyekuwa ameketi pembeni kabisa mwa hoteli hiyo mkononi akiwa na gazeti lililosomeka Uwazi, akapata hamu ya kusogea karibu yake ili aongee naye mambo kadhaa kwake hiyo akaiona kama bahati.<br />
“Habari?” alisabahi kwa lugha ya Kiingereza.<br />
“Nzuri tu,”<br />
“Ah! Naitwa Morgan natokea Urusi.”<br />
“Oh! Karibu mimi naitwa Erick Evarist naishi hapa hapa Tanzania,” Erick alijitambulisha.<br />
“Naweza kuungana na wewe hapa?”<br />
“Bila shaka karibu.”<br />
“Napenda kukufahamu zaidi.”<br />
“Ni mwandishi wa habari nafanya kazi zangu kwenye Kampuni ya Global Publishers.”<br />
“Oh! My God!” Morgan alipaza sauti na kuwafanya watu wote waliokuwa eneo hilo kuacha shughuli zao wakabaki kumshangaa. Erick naye akashindwa kuelewa ni kitu gani kilikuwa kinatokea eneo hilo.<br />
Kabla hajaendelea kusema chochote, Morgan akamwomba Erick wasogee pembeni ili waweze kuongea zaidi.<br />
“Hakuna shida,” Erick aliongea akimfuata mwanaume huyo na wote wakaketi kwenye viti vilivyokuwa hapo na mazungumzo maalum yakaanza, Morgan akimweleza wazi kwamba alifurahi kukutana naye na kazi iliyokuwa imemleta nchini Tanzania ni kutaka amsaidie kwa kila kitu na kama angehitaji kiasi chochote cha fedha angekuwa tayari kumpatia lakini tu amsaidie.<br />
Hakuficha kitu akaweka kila kitu wazi kwamba walikuja nchini hapo kutafuta ukweli wa mwanaume aliyeitwa Phillip na mkewe Genevieve na hawakuwa na msaada wowote.<br />
“Niko tayari kukusaidia.”<br />
“Kivipi?”<br />
“Nitakusaidia ufanye kitu kinachoitwa Press Conference, utakutana na waandishi wa habari ambao nitaongea nao kuwaeleza shida yako halafu utatakiwa kufanya kikao cha pamoja kisha kupiga picha ili kuandika habari hizo kwenye magazeti yetu, watu wakisoma naamini utapata ufumbuzi wa tatizo lako.”<br />
“Inaweza ikachukua muda gani kuanzia sasa?”<br />
“Kazi hiyo nitaifanya leo na kesho nitakupa majibu,”<br />
“Tutakutana wapi?”<br />
“Nitakuja hapa hapa hotelini lakini ni vyema ukanipatia namba yako ya simu ili iwe rahisi kuwasiliana na wewe.”<br />
“Ahsante rafiki, wewe kwangu ni kama malaika, chukua hii,” aliongea Morgan akichomoa kadi yake yenye namba za simu na kumkabidhi Erick ambaye aliipokea, wakaagana wakiahidiana kukutana tena kesho yake.<br />
Baada tu ya Erick kuondoka eneo hilo, Morgan alipandisha lifti haraka kwenda chumbani kwa akina Marina kuwaeleza kila kitu. Mariya na Marina walifurahi sana kupewa habari hizo njema.<br />
“Mungu yupo pamoja nasi, naona mwanzo umekuwa mzuri,” Mariya aliwaambia.<br />
“Tena tutakapofanikisha jambo hili itabidi tukamtolee shukurani ya pekee,” Marina aliunga mkono.<br />
Wakiwa pale hotelini, waliona saa zinachelewa ili kuifikia siku iliyofuata ambayo mwanasheria wao angekutana na Erick na kumpa utaratibu wa mkutano wao na waandishi wa habari ambao ungemaliza kazi iliyowaleta Tanzania.<br />
Kama walivyokuwa wamepanga kesho ikawadia, Morgan akiwa tayari kumsubiri Erick afike ili waendelee na mazungumzo yao na kuona walikuwa wamefanikiwa kwa kiasi gani kuhusu shughuli iliyokuwa mbele yao.<br />
Ilipotimu saa tatu kamili asuhubi, Erick aliwasilia hotelini hapo na mazungumzo yakafanyika na mwisho ukaonekana kuwa mzuri akimweleza wazi kwamba alishafanikiwa kukutana na baadhi ya waandishi na kuwaeleza habari hiyo na walipanga kukutana siku iliyofuata pale hotelini.<br />
Morgan akashukuru na kupeana ahadi ya kukutana na Erick siku iliyofuata kisha wakaagana.<br />
Muda huo huo alifanya utaratibu wa kupata kibali cha kufanya mkutano ndani ya hoteli hiyo, ambapo alipewa chumba kikubwa kilichotumika kwa shughuli hiyo.<br />
***<br />
Hali ya Phillip ilikuwa imebadilika kabisa utanashati wote aliokuwa nao kipindi akiwa na mke wake ukawa umepotea, mahudhurio ya kazi nayo yalionekana kusuasua kitendo kilichofanya mpaka mabosi wake waaanze kuingiwa na wasiwasi.<br />
Nyumbani nako hali ilikuwa tofauti kwani muda mwingi aliutumia kulala na alipochoka alitoka bila kuaga na kuingia mtaani kunywa pombe ili kupoteza msongo wa mawazo.<br />
Phillip akawa ni mtu wa kukitamani kifo kuliko kitu kingine, haikuishia hapo akaanza tabia ya kutoka nyumbani na kwenda makaburini na alipofika huko alitafuta kaburi la mkewe Lina na kulala juu yake.<br />
Ni hali hiyo ndiyo iliyozidi kuichanganya zaidi familia yake nao pia wakaingiwa na wasiwasi na kuamini kwamba si muda mrefu Phillip angekuwa mwendawazimu, ndugu na jamaa wakakaa kikao kuangalia ni jinsi gani wanaweza kumsaidia na walipomuuliza, jibu lilikuwa moja tu.<br />
“Nataka kufa, basi.”</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012422c4929b0131911357">MSICHANA NDOTONI MWANGU.......EP. 109<br />
<br />
MAISHA yalikuwa yamebadilika kabisa kwa Phillip ni kama vile dunia yake ilikuwa imegeuka na kuwa nje ndani, akapoteza kabisa mwelekeo wa maisha yake na kusahau kwamba alikuwa ana jukumu la kumlea mtoto mdogo Genevieve ambaye bado alihitaji ushauri wa wazazi wake japo tayari mmoja alishaaga dunia.<br />
Ushauri na ushawishi mkubwa wa ndugu, jamaa na marafiki haukusa<span class="text_exposed_show">idia kitu na hata walipoamua kutumia ofisi yake kumshauri bado hakubadilika ndiyo kwanza alizidisha ulevi na kutembea barabarani kutwa nzima akiongea na kutukana watu bila sababu.<br />
<br />
Phillip akawa ameharibikiwa kabisa, ofisi ikaamua kumwachisha kazi kwa nguvu lakini wakiahidi kumsaidia kama tu msaada wowote ungehitajika, nyumbani nako hali kwa mtoto ikawa mbaya hata shule akawa haendi tena kwa sababu hapakuwa na ada ili aweze kuendelea na masomo, hakika maisha yakawa magumu kupindukia.<br />
Lakini bado watu mbalimbali waliomfahamu Phillip hawakumwacha peke yake waliendelea kumshauri na kumpa moyo kwamba maisha yaliendelea na kamwe yasingesimama. Phillip akapokea ushauri wao ambao uliingia sikio la kulia na kutokea sikio la kushoto kwani hakuweza kubadilika, zaidi sana vituko viliongezeka nao pia wakaanza kuchoka na kumwacha afanye alivyopenda.<br />
<br />
***<br />
Ndani ya hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam chumba maalum kilikuwa kimeandaliwa tayari kwa mkutano mfupi ambao ungefanyika siku hiyo. Mariya na Merina ambao ndiyo waongeaji wakubwa, pembeni yao akiwepo mwanasheria aliyesimamia mambo yote zikiwemo mali za baba yao Victor Fedorov ambaye mpaka wakati huo hakufahamika kama alikuwa amekufa au la!<br />
Waandishi walikuwa ni wengi mno mikononi mwao wakiwa na kalamu zao na kamera ili kuchukua habari ambayo ingepelekwa katika vyombo vyote vya habari yaani magazeti, redio na televisheni.<br />
<br />
Mkutano ukawa umeanza, Mariya na Merina wakijitambulisha kwamba walikuwa akina nani na walitokea wapi na nini lilikuwa lengo lililowaleta nchini Tanzania, waliongea katika lugha ya Kirusi na Morgan akaitohoa katika lugha ya Kiingereza na baadaye Erick Evarist akatafsiri katika lugha ya Kiswahili.<br />
Wakisisitiza kwamba walihitaji kufahamu mahali ambako Phillip na mkewe Genevieve wangepatikana na kwa gharama yoyote ile wangekuwa tayari kutimiza hilo lakini tu wapate ushirikiano.<br />
<br />
Hivyo ndivyo mambo yalivyoendelea ndani ya hoteli hiyo kwenye chumba maalum, kwa muda wa saa nzima watoto hao waliendelea kuongea na waandishi wa habari wakiwaomba na kuwasihi kusaidia kuandika habari hizo ili hatimaye mtu anayetafutwa aweze kupatikana kwa urahisi.<br />
“Wanamtafuta nani?”<br />
“Wanasema wanatafuta familia ya Phillip na mkewe Genevieve.”<br />
“Mh!”<br />
<br />
“Kwa nini?”<br />
“Hata sisi hatujui ila wanasema kwamba Genevieve ndiye mama yao mzazi.”<br />
“Hawa watoto mbona siyo Watanzania?”<br />
“Unalosema ni kweli lakini hatuwezi kujua, sisi tufanye tu kazi yetu,” yalikuwa ni maongezi kati ya waandishi wa habari waliokuwepo kwenye mkutano huo wakijiuliza maswali mengi juu ya mkutano huo na watu waliouitisha.<br />
<br />
Baada ya habari kukamilika Mariya na Merina wakawashukuru waandishi huku wakiwashika mkono na kuwapatia bahasha ambayo ndani yake haikufahamika ilikuwa na nini na kuwatakia kila la kheri katika utendaji wa kazi zao na kuwaeleza wazi kwamba ili waweze kuwapata watu waliowahitaji, waliwategemea sana wao.<br />
Waandishi nao wakashukuru wakiahidi kufanya kila kilichowezekana habari hiyo ichapishwe katika magazeti na ikiwezekana kutangazwa katika vyombo vyote vya habari zikiwemo redio na televisheni.<br />
<br />
Baada ya waandishi kuondoka, wakarejea ndani ya vyumba vyao hamu yao kubwa ikabaki kusubiri nini magazeti yangeandika, ambapo macho na masikio yao yote yakaelekezwa huko.<br />
“Nafikiria kila kitu kitakwenda sawa, tusubiri kesho tuone,” Morgan aliongea.<br />
“Hata mimi nahisi hivyo ngoja tuone,” waliendelea kuongea wakijipa matumaini kwamba kila kitu kingekwenda sawa.<br />
Saa zikazidi kusonga mbele hatimaye kiza kikaingia, hapo wakaamua kula chakula cha usiku na kuingia kwenye vitanda vyao wakiwa na hamu ya kujua kesho yake kitatokea nini.<br />
<br />
***<br />
Asubuhi ya siku iliyofuata Morgan alikuwa wa kwanza kutoka ndani ya chumba na bila kufanya kitu chochote akashuka kwa lifti mpaka mapokezi hapo akasabahi watu aliowakuta kisha kutoka nje ya hoteli kuelekea barabarani akitafuta mahali ambako angekutana na wauza magazeti na kununua ili kusoma kama habari yao ingekuwa imeandikwa siku hiyo.<br />
Ni kweli kabisa alichokuwa amekifikiria kichwani mwake hakikuwa uongo, mtu wa kwanza tu aliyekutana naye akiwa na magazeti mkononi akamwita na kuchukua moja ya magazeti aliyokuwa nayo, macho yake yakakutana na picha ya Mariya na Merina mbele yao kukiwa na vipaza sauti vingi, hakuelewa lugha ya Kiswahili lakini aliweza kuisoma picha.<br />
<br />
Akamwomba tena muuza magazeti ampatie magazeti mengine zaidi, nayo habari iliyosomeka ukurasa wa kwanza tu wa magazeti hayo ilikuwa ileile ya kwao, furaha ikamjaa moyoni mwake akajiona mshindi kati ya washindi na akalazimika kununua magazeti zaidi ya sita akalipa na kurejea ndani ya hoteli huku jasho likimtoka.<br />
Haraka akapandisha lifti na moja kwa moja akauendea mlango ambao ndani yake walilala Mariya na Merina akagonga kwa nguvu na kusubiri mlango ufunguliwe na akiwa hapo akashuhudia Mariya akichungulia baada ya kufungua mlango.<br />
<br />
“Magazeti haya hapa,” aliongea akinyoosha mkono kumpatia Mariya magazeti yote aliyokuwa nayo.<br />
Kwa macho yake yote mawili akashuhudia kurasa za mbele za magazeti hayo zikiwa na picha yao kubwa akacheka na kutabasamu na bila kusema neno akarejea ndani ya chumba chao huku akimwita Merina.<br />
“Merina! Merina, amka uone mwenyewe magazeti karibu yote yameandika habari yetu, kazi imekuwa rahisi sana kuliko tulivyotarajia…,” aliongea Mariya bila kuweka kituo.<br />
<br />
Furaha ilikuwa imetawala ndani ya chumba wakiamini kwamba muda si mrefu kila kitu kingekwenda sawa kama walivyofikiria, kwa pamoja wakakumbatiana na kupigana mabusu lakini ghafla wakiwa katika furaha yao hiyo taswira ya baba yao Victor Fedorov mwanaume aliyewapenda kupindukia ikawajia, ni kweli walikuwa na furaha ya kuufahamu ukweli mwingine uliokuwa umejificha lakini pia Fedorov alikuwa ndiye mzazi wao halisi pamoja na mambo yote mabaya aliyoyatenda bado walimpenda.<br />
“Sijui atakuwa wapi? Amepatwa na kitu gani? Inauma sana,” aliongea Merina huku akilia.<br />
<br />
***<br />
Asubuhi ya siku iliyofuata baada tu ya Merina na Mariya kufanya mkutano jana yake na waandishi wa habari, Phillip alikuwa katika mitaa ya Posta akikatisha huku na kule bila kuelewa anakwenda wapi.<br />
Ghafla mbele yake akaiona meza ya magazeti na kuamua kutupa macho juu yake ili angalau asome kilichokuwa kimeandikwa siku hiyo, akasogea karibu kabisa na muuza magazeti kisha kumsabahi.<br />
“Habari za leo?”<br />
“Nzuri tu kaka karibu.”<br />
<br />
“Ahsante, naweza kupitishapitisha macho kidogo?”<br />
“Bila shaka lakini usiguse kama hutalinunua.”<br />
Akaitika kwa ishara ya kutingisha kichwa kisha akasogea karibu na meza hiyo na kutupa macho juu ya magazeti, ni habari ya kwanza tu katika gazeti la Uwazi ikamshtua.<br />
“Mh!”<br />
<br />
“Mbona umeguna kaka?”<br />
“Hii habari, inanihusu mimi kabisa na hao ni watoto wangu lakini walikufa.”<br />
“Wewe mzee chizi nini utakuwa hamnazo watoto wako? Wewe? Hebu ondoka hapa haraka kabla sijakuitia mgambo wa jiji.”<br />
“Dorice na Dorica,” alitamka kwa sauti ya juu.<br />
Nimekuambia ondoka haraka,” aliongea muuza magazeti huyo akimvuta Phillip kumwondoa eneo hilo.<br />
<br />
“Usinifanyie hivyo ndugu yangu nakuambia ukweli tafadhali nipe gazeti nione vizuri.”<br />
“Wazee wengine bwana sijui wachawi au wanatumwa kuwangia biashara za watu! Asubuhi hii, kama unataka gazeti si ununue lakini siyo ujipendekeze kwa watoto wa watu.”<br />
“Usinivu…,” aliongea Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake tayari akashuhudia vibao mfululizo vikipita mashavuni mwake.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da401ba8991525243"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012422c4882b4a14322535">MSICHANA NDOTONI MWANGU.......EP. 110<br />
<br />
<br />
VIBAO mfululizo vilikuwa vimetua kwenye mashavu ya Phillip na kumpeleka chini akajikuta ameketi kitako bila kutarajia huku akilia na kujaribu kumweleza kijana yule ukweli kwamba habari iliyoandikwa ilimhusu yeye na watoto wake ambao hakika kwa wakati huo walikuwa ni marehemu.<br />
Ni kilio cha Phillip ndicho kilichokusanya watu eneo la tukio, wengi wakijaribu kud<span class="text_exposed_show">adisi ni kitu gani kilikuwa kimetokea asubuhi hiyo. Kijana wa magazeti akaanza kusimulia tukio zima, muda wote huo Phillip akiendelea kulia.<br />
<br />
Bahati nzuri asubuhi hiyo watu wengi walikuwa wakielekea makazini kwao, ni mfanyakazi mmoja aliyefanya kazi na Phillip alipita eneo hilo naye akitaka kuangalia nini lilikuwa tatizo. Akiwa hapo akatupa macho yake katikati ya umati wa watu akamwona mwanaume akiwa chini tena akilia.<br />
“Mh!” akaguna akisogea karibu ili kuhakikisha kitu alichokiona.<br />
“Phillip!” alitamka kwa sauti ya juu na kufanya watu wote kumwangalia yeye.<br />
<br />
“Namjua huyu ni shemeji yangu pia ni mfanyakazi mwenzangu, jamani amefanya nini tena? Halafu ana tatizo la akili kidogo toka amefiwa na mkewe amekuwa hivyo, hebu njoo,” msichana huyo aliongea.<br />
“Blandina sitaondoka hapa mpaka nipate gazeti.”<br />
“Gazeti?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Lina nini?”<br />
“Nimesoma kwa macho yangu habari kwamba Dorice na Dorica wako hapa Tanzania tena wananitafuta mimi na mama yao.”<br />
“Phillip!”<br />
“Hutaamini lakini huo ndiyo ukweli, wewe nunua usome kisha utanipatia na mimi.”<br />
<br />
Msichana huyo bila ubishi akafungua mkoba wake na kutoa noti ya shilingi mia tano kisha kununua gazeti la Nipashe haraka akatupa macho yake ukurasa wa mbele, yeye pia akashuhudia picha kubwa iliyoonyesha wasichana wawili na chini yake kulionekana habari iliyowahusu lakini pia ikimtaja Phillip kwa majina yote matatu na Genevieve ambaye kwa historia aliyokuwa ameipata alikuwa ni mke wa Phillip aliyefariki dunia miaka kadhaa iliyopita.<br />
“Naota au?”<br />
<br />
“Huoti unachokiona hapo ni kweli tupu, tafadhali nisaidie nahitaji kujua wako wapi niwafuate nikaongee nao niujue ukweli,” aliongea Phillip akinyanyuka kutoka chini.<br />
Watu wote waliokuwa eneo la tukio pamoja na kijana aliyekuwa akiuza magazeti wakaonekana kupigwa na butwaa kwani kwa wengi Phillip alionekana kichaa.<br />
“Twende,” aliongea msichana huyo akimshika Phillip mkono, wakatembea mpaka kwenye mgahawa mmoja hapo wakaketi na kwa umakini wa hali ya juu wakaanza kusoma habari hiyo mwanzo mpaka mwisho na kuelewa sehemu ambayo watoto hao walikuwa wamefikia.<br />
<br />
“Nisaidie ndugu yangu nahitaji kuonana nao leo hii.”<br />
“Hakuna shida ila watakubali? Unayo kumbukumbu gani itakayokufanya wakuamini kwamba wewe ni baba yao?”<br />
“Ninazo nyingi tu mojawapo ni picha zao za utotoni ziko nyumbani naweza kwenda kuzichukua.”<br />
“Basi twende tukajaribu,” msichana huyo akaamua kushirikiana na Phillip ili kumsaidia.<br />
<br />
Wakatembea mpaka kando kidogo na hapo akaita teksi ambayo iliwapeleka moja kwa moja nyumbani kwa Phillip ambako aliingia ndani na bila kusema kitu chochote akaingia chumbani kwake na kutoka na bahasha mkononi huku akikimbia akitoka tena nje na kuielekea teksi iliyokuwa ikimsubiri, akaingia ndani na dereva akaondoka kwa kasi ya ajabu moja kwa moja kuelekea katika hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam ambako wangejitambulisha na kuomba kuonana na Mariya na Merina.<br />
Njia nzima Phillip alikuwa akilia, hakuamini mambo yaliyokuwa yanamtokea maishani mwake na mara kadhaa akamwomba msichana aliyekuwa naye ajaribu kumfinya pengine angeamka kutoka usingizini.<br />
<br />
“Phillip shemeji yangu huoti hata kidogo yote yanayotokea ni kweli tupu, tatizo ni moja tu iweje watoto waliokuwa wamekufa na kuzikwa wawe hai? Hapo mimi nashindwa kabisa kuelewa na je, watakubali na kuamini kwamba wewe ndiye baba yao?”<br />
Swali hilo lilipenya moja kwa moja masikioni mwa Phillip na kwenda ndani kabisa ya kichwa chake, akaiona picha yote jinsi walivyohangaika mpaka kufikia kununua mbegu za mwanaume mwingine ambaye aliitwa Victor Fedorov, alipofika hapo machozi yakambubujika.<br />
<br />
Gari likaendeshwa na hatimaye nusu saa tu baadaye lilishawasili nje ya hoteli hiyo maarufu na wakalipa kisha kushuka kutembea kuelekea mapokezi ambako wangejitambulisha na kuomba kusaidiwa shida yao.<br />
Kwao zoezi halikuwa gumu walifanya kama walivyopanga na kufanikiwa kuonana na watoto hao wawili. Mapokezi simu ikapigwa moja kwa moja kwenye chumba alicholala Morgan na simu hiyo ikapokelewa.<br />
<br />
“Naongea kutoka mapokezi hapa kuna wageni wenu wawili.”<br />
“Wawili? Wa jinsia gani?”<br />
“Mwanamke na mwanaume.”<br />
“Mh! Sawa waeleze tutakuwa hapo baada ya dakika tano kuanzia sasa hivi.” Morgan alijibu na kukata simu na bila kuchelewa akatoka chumbani kwake kwenda kwa akina Marina hapo akawapa taarifa na kuwataka wajiandae kukutana na wageni waliokuwa wamefika pale kuwatafuta.<br />
<br />
“Pengine ndiyo hao tunaowatafuta.”<br />
“Umejuaje hebu tukawaone kwanza.”<br />
Haraka wakajiandaa na walipokuwa tayari wakatembea kuelekea sehemu kulikokuwa na mlango wenye lifti wote watatu wakashuka kuelekea chini wakitamani kuonana na watu hao.<br />
“Je, tutawaamini vipi kama kweli ndiyo wenyewe?” Morgan aliuliza.<br />
<br />
“Kabla ya yote tutahitaji kuwasikiliza kwanza wao na kama kuna kitu chochote kinachoonyesha kwamba wao ndiyo haswa walengwa wa safari yetu.”<br />
“Hilo nakubaliana na wewe,”Merina alidakia na tayari walishafika chini mlango wa lifti ukaonekana kufunguka na kutoka nje.<br />
<br />
Huku vichwani mwao wakijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu wakatokeza mapokezi na macho yao kukutana na watu wawili, mwanamke na mwanaume, ambao hawakuwafahamu kabisa lakini ghafla kabla hawajapiga hatua nyingine kwenda mbele zaidi wakashtushwa na sauti kubwa ndani ya chumba.<br />
“Dorice! Dorica! Si mliku…,” aliongea Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake akaanguka chini kama mzigo.<br />
<br />
Je, nini kitaendele</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012422c4882b4a14322535"><span class="text_exposed_show"> </span></div></span></div><span><span class="UIActionLinks UIActionLinks_bottom" data-ft="{"tn":"=","type":20}"><button class="like_link stat_elem as_link" data-ft="{"tn":">","type":22}" name="like" title="Tilkendegiv, at du synes godt om dette" type="submit"><span class="default_message"></span></button></span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501242a4a2eb06944671655">MSICHANA NDOTONI MWANGU.......EP. 111<br />
<br />
<br />
GARI likaendeshwa na hatimaye nusu saa tu baadaye lilishawasili nje ya hoteli hiyo maarufu na wakalipa kisha kushuka kutembea kuelekea mapokezi ambako wangejitambulisha na kuomba kusaidiwa shida yao. Kwao zoezi halikuwa gumu, walifanya kama walivyopanga na kufanikiwa kuonana na watoto hao wawili. Katika eneo la mapokezi simu ikapigwa moja kwa moja kwenye ch<span class="text_exposed_show">umba alicholala Morgan na simu hiyo ikapokelewa.<br />
“Naongea kutoka mapokezi, hapa kuna wageni wenu wawili.”<br />
<br />
“Wawili? Wa jinsi gani?”<br />
“Mwanamke na mwanaume.”<br />
“Mh! Sawa waeleze tutakuwa hapo baada ya dakika tano kuanzia sasa hivi.” Morgan alijibu na kukata simu na bila kuchelewa akatoka chumbani kwake kwenda kwa akina Marina hapo akawapa taarifa na kuwataka wajiandae kukutana na wageni waliokuwa wamekuja hapo kuwatafuta.<br />
<br />
“Pengine ndiyo hao tunaowatafuta.”<br />
“Umejuaje hebu tukawaone kwanza.”<br />
Haraka wakajiandaa na walipokuwa tayari wakatembea kuelekea sehemu kulikokuwa na mlango wenye lifti, wote watatu wakashuka kuelekea chini wakitamani kuonana na watu hao.<br />
<br />
“Je, tutawaamini vipi kama kweli ndiyo wenyewe?” Morgan aliuliza.<br />
“Kabla ya yote tutahitaji kuwasikiliza kwanza wao na kama kuna kitu chochote kinachoonyesha kwamba wao ndiyo haswa walengwa wa safari yetu tutafahamu huko.”<br />
“Hilo nakubaliana na wewe,” Merina alidakia na tayari walishafika chini mlango wa lifti ukaonekana kufunguka na kutoka nje.<br />
<br />
Huku vichwani mwao wakijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu wakatokeza mapokezi na macho yao kukutana na watu wawili, mwanamke na mwanaume, ambao hawakuwafahamu kabisa lakini ghafla kabla hawajapiga hatua nyingine kwenda mbele zaidi wakashtushwa na sauti kubwa ndani ya chumba.<br />
“Dorice! Dorica! Si mliku…” aliongea Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake akaanguka chini kama mzigo.<br />
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…<br />
<br />
ULIKUWA ni mshtuko mkubwa Phillip alipoanguka chini watu wote ndani ya chumba walianza kukimbizana huku na kule kutafuta msaada, Blandina aliyekuwa ameongozana na Phillip yeye pia alikuwa akilia huku akimwita Phillip.<br />
“Tafadhali usife, huu ndiyo wakati wa kuufahamu ukweli, amka nakuomba.”<br />
Lakini bado Phillip aliendelea kulala chini akiwa hajitambui.<br />
<br />
Haraka daktari aliyefanya kazi ndani ya hoteli kwa dharura akaitwa na mara moja akaanza kumpatia Phillip huduma ya kwanza ili kumnusuru na umauti ambao ulikuwa unamnyemelea.<br />
Kwa takribani nusu saa nzima daktari aliendelea kumpatia huduma ya kwanza Phillip mwisho naye akaanza kukata tamaa akieleza wazi kwamba ni vyema mtu huyo akapelekwa hospitali kwa uchunguzi zaidi.<br />
<br />
“Hospitali?”<br />
”Ndiyo kwa jinsi hali ninavyoiona ni bora iwe hivyo.”<br />
“Mh!” Blandina akaguna lakini ghafla wakiwa katika kujadili wakashuhudia Phillip akifungua macho yake na kuangaza huku na kule ndani ya hoteli.<br />
Haraka kama vile alikuwa akiota akakurupuka kutoka chini na kusimama akionekana kutafuta kitu ambacho hakikuonekana kwa wengi.<br />
“Bahasha yangu! Nataka bahasha yangu nilikuwa nayo muda si mrefu.”<br />
<br />
“Hii hapa,” Blandina aliongea akinyoosha mkono kukabidhi bahasha kwa Phillip.<br />
“Nasema ukweli watoto hao hapo ni wa kwangu lakini sikuwahi kuwapa majina hayo ya Mariya na Merina waliitwa Dorica na Dorice!”<br />
“Lakini hawa ni Mariya na Merina si majina hayo unayosema wewe!”<br />
“Hakika ninawaeleza ni watoto wangu ushahidi wangu upo, ni picha nakumbuka vizuri sura zao na mama yao pia,” Phillip aliongea mfululizo.<br />
Morgan ambaye ndiye alikuwa mwanasheria aliyeongozana na akina Merina na Mariya akasogea karibu na Phillip ili kupata ushahidi wa picha kama Phillip mwenyewe alivyosema.<br />
<br />
“Naweza kuona picha hizo?” aliuliza.<br />
“Hizi hapa,” Phillip aliongea akifungua mfuko wa khaki na kuchomoa picha zilizokuwa ndani yake akazikabidhi kwa Morgan ambaye alianza kupitisha macho juu yake.<br />
“Mh!” akaguna, picha zilizokuwa mikononi mwake zilikuwa za watoto wawili waliokuwa wamesimama mbele yake yaani Merina na Mariya akashuhudia picha nyingine za watoto hao wakiwa na mama yao mzazi ambaye ndiye aliitwa Genevieve, yeye pia akapigwa na butwaa.<br />
<br />
Mariya na Merina nao pia wakasogea karibu na Morgan ili kushuhudia kilichokuwa kikiendelea, macho yao yakatua moja kwa moja katika picha zao na mwanamke mmoja akiwa pembeni yao, huyo ndiye alikuwa mama yao.<br />
“Anafanana na sisi kabisa kwa kila kitu,” waliongea kwa sauti.<br />
“Ni kweli yawezekana huyo ndiye tunayemtafuta.”<br />
“Je, yuko wapi mwanamke huyu?”<br />
<br />
“Genevieve alikufa!”<br />
“Unasema?”<br />
“Amini ninachowaambia, huo ndiyo ukweli wangu kama mnaweza kusadiki maneno yangu basi sadikini,” Phillip aliongea huku kwikwi ya kulia ikimkaba.<br />
Maswali yakawa mengi bila majibu, ni kweli walimtafuta mwanaume aliyeitwa Phillip na mkewe Genevieve lakini kilichozidi kuwashangaza zaidi ni kwamba iweje mwanaume huyo aseme kwamba walikufa na kuzikwa miaka mingi iliyopita ili hali wao walikuwa hai?<br />
<br />
Baada ya mvutano mrefu wakaomba chumba maalum ili waweze kuongea vizuri kuupata ukweli waliokuwa wakiutafuta Morgan akiwa ndiye kiongozi wa kikao, huko waliongea mengi Phillip akijaribu kueleza ukweli na ni kwa nini aliamini watoto hao walikufa. Akasimulia ajali ya gari kulipuliwa kwa bomu na watoto wote kufahamika walikufa.<br />
Ilikuwa ni historia chungu lakini ilibidi Merina na Mariya waikubali, wakataka kuonyeshwa makaburi ili wakashuhudie kwa macho yao, jambo ambalo halikuwa na tatizo. Historia nyingine iliyokuwa imewaumiza watoto hao ni taarifa kwamba mama yao alikufa muda mrefu lakini pia alizikwa pembeni mwa makaburi yao.<br />
<br />
“Hatuna muda wa kupoteza tunachohitaji sisi ni kuona hayo makaburi tena kama inawezekana sasa hivi,” Morgan aliongea.<br />
“Hakuna shida tunaweza kwenda,” Phillip aliongea kwa majonzi.<br />
Safari kuelekea makaburini ikaanza na kwa sababu walitumia usafiri wa kukodi haikuchukua muda wakawasili katika makaburi ambako walisemekana kuzikwa, wakashuka wakiwa na hamu ya kufahamu historia ya kifo. Kwa sababu makaburi yao hayakuwa mbali sana haikuchukua muda kuyafikia ambapo wakashuhudia picha zikiwa katika fremu kwa pamoja wakaangua kilio.<br />
<br />
“Ni kwa nini haya yote? Mbona sisi tuko hai? Kuna nini kilitokea? Lazima ipo siri ambayo hatuwezi kuifahamu, na huyu ndiye mama yetu?” wakauliza.<br />
“Mnachokiona wanangu ndicho kilichotokea, sikuwahi kufahamu kwamba hamkufa, mimi pia nahisi ni mchezo ulichezwa naomba mnisamehe.”<br />
“Ukweli ni historia inayosikitisha sana lakini hatuna budi kuikubali pamoja na kuugundua ukweli huu wewe utabaki kuwa ba..ba..ye…tu!” waliongea watoto hao huku wakilia.<br />
<br />
Mioyo yao ilikuwa imeumia kupita kiasi kwa historia waliyokuwa wameipata lakini upande mwingine walionekana kufurahia kujua ukweli kwani walioufahamu kama ndiyo ukweli haukuwa sawa, Federov alikuwa ndiye baba yao halisi na mama yao alikuwa Genevieve lakini Phillip alihusishwa zaidi kwani ndiye aliyewalea wakiwa watoto wadogo baada ya kununua mbegu za kiume kutoka kwa Fedorov.<br />
“Tunakupenda sana,” waliongea wakitembea kuondoka eneo la makaburini kurejea hotelini ndani ya vichwa vyao wakiwaza na kuwazua mambo mengi bila kupata majibu, walihitaji kupata historia zaidi ili waamini kwa asilimia zote.<br />
<br />
“Lakini tunahitaji kupata historia ya ndani zaidi ili kukufahamu vizuri.”<br />
“Hakuna shida niko tayari kueleza kila kitu ambacho mtahitaji.”<br />
Wakati wakiongea hayo walishafika eneo la maegesho la hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam, wakashuka na kuingia ndani ili kuendelea na maongezi zaidi wakiwa tayari kumsikiliza Phillip.<br />
<br />
Walitaka kusikia kama Phillip angekuwa tayari kusema ukweli wake wote alioufahamu ili nao waoanishe na maelezo ambayo waliyasoma kutoka kwenye nyaraka za baba yao.<br />
“Historia nitakayosema inaumiza kupita maelezo lakini naomba muipokee kwa mikono miwili na kuichunguza hapo ndipo mtaugundua ukweli wote.”<br />
“Mh! Tuko tayari kukusikiliza.”<br />
<br />
“Mimi na mama yenu ambaye ni marehemu yaani Genevieve tulifunga ndoa miaka mingi iliyopita na maisha yetu yalikuwa ya raha mustarehe, jambo moja tu lilikosekana kwa bahati mbaya mimi sikuwa na mbegu za uzazi za kuweza kuzalisha mwanamke hivyo tukatafuta daktari ambaye tulimpata kama sikosei aliitwa Dk. Koher huyu alitusaidia sana na tukafanikiwa kupata mbegu za kununua kwa mwanaume mmoja aliyekuwa maskini akiishi mtaani, huyo aliitwa Victor Fedorov. <br />
<br />
Ukafanyika utaalam wa kitabibu na ninyi mkazaliwa, furaha ndani ya nyumba ikaongezeka huku tukiwalea vyema na kuwatunza mpaka mlipofikisha umri wa miaka mitano ndipo tukaamua kuwapeleka shule lakini siku moja asubuhi nikapata ujumbe kwamba gari iliyokuwa imewabeba ilitegeshwa bomu hivyo lingelipuka na watoto wote kufa.<br />
<br />
Nilijitahidi sana kunusuru maisha yenu lakini nilishachelewa, gari likalipuka na watoto wote ndani ya basi kuaminika kufa, tulilia na kuomboleza baadaye tukafanya mazishi ndiyo yale makaburi niliyowapeleka yakiwa na picha zenu juu. Akili yangu inavurugika zaidi iweje leo muwe hai tena katika nchi nyingine kabisa…,” aliongea Phillip muda wote huo akibubujikwa na machozi.<br />
“Usilie tafadhali nyamaza.”<br />
“Inanichanganya akili iweje muwe hai wakati mlishakufa tukawazika? Hapana hii ni ndoto pengine nitaamka na kukuta kila kitu kiko sawa, hebu nifinye.”<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Historia aliyoitoa Phillip mbele ya watoto wake baada ya kutoka makaburini wataiamini?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da425d61016624855"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501242c4e8bd34540039443">MSICHANA NDOTONI MWANGU.......EP. 112<br />
<br />
PHILLIP hakuwa katika ndoto kama alivyokuwa akifikiria kwani mambo yote yaliyokuwa yakimtokea yalikuwa ya kweli japo historia iliumiza mioyo ya wengi.<br />
Vilio na machozi kwa Merina na Mariya havikukauka, walilia na kuomboleza kwa mambo mengi lakini kubwa zaidi ni lile la kuelezwa kwamba walikufa miaka mingi iliyopita kwa ajali ya bomu ambalo lilitegwa kwenye ga<span class="text_exposed_show">ri lao la shule na kuzikwa sehemu ambayo waliishuhudia kwa macho yao.<br />
<br />
“Ni nini kilitokea? Kuna nini baba alifanya? Huu lazima utakuwa ni mchezo,” Merina na Mariya walisema kwa lugha ya Kirusi.”<br />
Muafaka ukawa umefikiwa kwamba Phillip apewe muda wa kutafuta nyaraka zote muhimu za kumtambulisha kwamba yeye ndiye haswa alikuwa baba aliyewalea watoto hao. Akapata cheti cha ndoa na nyaraka nyingine kadhaa, pia baadhi ya ndugu nao wakasimama kusema ukweli mbele ya mwanasheria Morgan aliyepewa jukumu la kuongoza mambo yote yaliyotakiwa.<br />
<br />
Siku ya kwanza ikapita, ikaja siku ya pili na hatimaye wiki ikakatika wakiwa bado katika uchunguzi mzito. Vielelezo vingi vilipatikana na baadhi ya watu wakatoa ushahidi wao kuhusu Phillip.<br />
Jinsi watu wengi walivyotegemea ndivyo ilivyokuwa kwani baada ya uchunguzi wa kina, ukweli ulibainika. Phillip akaonekana kuwa mwenye haki pamoja na kwamba hakuwa baba wa kuwazaa watoto Mariya na Merina.<br />
“Nini kinaendelea kwa sasa?” Morgan aliuliza siku moja.<br />
<br />
“Nadhani mtu pekee wa kumtafuta kwa sasa ni Eric Evarist ili atusaidie tena tupate nafasi ya kuzungumza na waandishi wa habari.<br />
Jambo hilo likafanyika mara moja, mwandishi huyo akatafutwa na kupewa taarifa kamili. Siku mbili baadaye, kilifanyika kikao kingine ndani ya hoteli ileile waliyofikia.<br />
Waandishi wa habari wakafurika ndani ya chumba maalum tayari kwa kuchukua taarifa muhimu, macho na masikio vikawa makini kabisa kuhakikisha hawakosei kitu chochote.<br />
<br />
Hata waandishi wenyewe baada ya kusikia historia iliyokuwa imetolewa na mashahidi wa pande zote mbili, walishtushwa sana. Kilichowatatiza ni kwamba, iweje watu waliozikwa siku nyingi wawe hai tena?<br />
“Ndugu zangu ninayo mambo matatu tu muhimu ya kuongea nanyi asubuhi ya leo lakini nianze kwa kuwaomba radhi kuchukua muda wenu mwingi kuja hapa kwetu,” aliongea Morgan na alipomaliza akapokelewa kwa shangwe, nderemo na makofi mengi ndani ya chumba.<br />
<br />
Mariya na Merina ndiyo walioanza kufungua mkutano huo, wakati wakiongea, Morgan ambaye ndiye alikuwa mwanasheria wao, alikuwa akitafsiri kwa lugha ya Kiingereza ambayo waliamini kabisa itaeleweka kwa watu wote. Walipomaliza, Phillip naye alikaribishwa kuongea na waandishi, akaeleza kila kitu bila kificho. Machoni mwa watu alionekana kama mwongo aliyetaka kujipatia fedha kutoka kwa watoto hao matajiri lakini Morgan alikanusha vikali uvumi huo, akasimama kumtetea Phillip kwa kipindi chote.<br />
“Hadanganyi, ni kweli ndiye baba halisi wa watoto hawa.”<br />
<br />
“Mh!”<br />
“Huo ndiyo ukweli?”<br />
“Lakini anasema wake walishakufa miaka mingi iliyopita kwa ajali, pengine wanafanana tu.”<br />
“Uchunguzi wa kina umefanyika na tumegundua kila kitu, kwa hilo naomba tukubaliane na tuungane na huyu ndugu yetu hapa,” Morgan alisema kwa kujiamini.<br />
<br />
Wakiwa hapo, waliongea mambo yote lakini jambo moja likabaki kuwa siri ya familia kwamba watoto hao walikuwa si mali ya Phillip kwani hakuwa na uwezo wa kumpa ujauzito mwanamke. Jambo hilo liliendelea kubaki siri ya familia ili kulinda heshima yake.<br />
Kwa muda wote huo, Phillip aliendelea kumwagika machoz. Si kwamba alikuwa akiliakwa majonzi bali furaha ya kukubaliwa na watoto wake wawili ambao kwa wakati huo walishabadili majina na kuitwa Merina na Mariya (Dorice na Dorica) ndiyo kitu kilichomliza.<br />
Wote kwa pamoja wakasimama na kukumbatiana, watoto pia walikuwa wakilia kwa furaha kwani walimpata mtu waliyekuwa wakimtafuta pamoja na kwamba Genevieve ambaye ndiye mama yao alishakufa.<br />
<br />
Kazi yote ikawa imeachwa mikononi mwa vyombo vya habari kutangaza ukweli kwa Watanzania kwamba mwanaume ambaye ndiye hasa alikuwa akitafutwa, alikuwa amepatikana na Mariya na Merina wakishirikiana na mwanasheria wao walikuwa wakiwashukuru watu wote waliofanikisha kupatikana kwa Phillip. Mariya na Merina walikuwa na hamu kubwa ya kuwafahamu ndugu wengine wa Phillip, ikabidi wasubiri vyombo vya habari vifanye kazi yao.<br />
<br />
Baada ya waandishi kuondoka, Phillip aliwaongoza Mariya, Merina na Morgan kuelekea nyumbani kwake ambako angekutana na familia yake, yaani mtoto wake Genevieve na bibi Magdalena ili kufahamiana zaidi, jambo ambalo lilichukua muda wa nusu saa hivi. Baada ya kufika nyumbani kwa Phillip, mapokezi yakafanyika kisha wakaungana na familia kufahamiana zaidi.<br />
Waliongea mengi huku furaha ikitawala, mara kadhaa Phillip alionesha mapenzi ya dhati kwa watoto wake kwa kuwapiga mabusu mfululizo kama ishara ya mapenzi ya dhati kwao. Baada ya kumaliza utambulisho huo, waliaga na kuondoka wakimtaka Phillip kufika hotelini asubuhi ya siku iliyofuata ili wazungumze zaidi.<br />
***<br />
Magazeti yote ya siku iliyofuatia yaliandika habari ya kupatikana kwa Phillip, mwanaume aliyekuwa akisakwa kwa udi na uvumba ambaye haswa ndiye alikuwa baba wa Merina na Mariya watoto wa Kirusi waliokuja nchini kuufahamu ukweli wa maisha yao.<br />
Vichwa vingi vya habari vilisomeka tofauti, wapo walioandika: “Baba wa watoto ajitokeza.” Mengine yakataka vipimo vya vinasaba (DNA) vifanyike ili kujua ukweli wa historia. “Watoto walioaminika kufa miaka mingi iliyopita wafufuka,” liliandika gazeti lingine. Kila gazeti liliandika lilivyotaka ilimradi kufanya biashara. Lakini wote hao hawakuufahamu upande wa pili wa shilingi kwamba nyuma yake kulikuwa na historia nyingine, tena ya kusikitisha ambayo ilikuwa ndani ya mioyo ya watoto wenyewe na Phillip.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501242c4e7fe97937592495">MSICHANA NDOTONI MWANGU.......EP. 113<br />
<br />
WATANZANIA wengi wakabaki midomo wazi baada ya kusoma habari hizo kwenye vyombo vya habari mbalimbali. Wengi wakijiuliza kuna kitu gani kilitokea mpaka dunia ikaamini kwamba watoto hao waliokuwa wakiuza magazeti kwa wakati huo walikuwa wamekufa kumbe walikuwa hai. Maswali hayo yote hayakuwa na majibu na yakaendelea kuwa kitendawili kwa wengi.<br />
Wakati dunia iki<span class="text_exposed_show">shangaa kwa upande wa Mariya, Merina na Phillip, kwao ilikuwa furaha kubwa, wakifurahia kuonana wakiwa hai, masikitiko makubwa yalitokea tu pale walipomkumbuka mama yao yaani Genevieve lakini wakajipa moyo na kuamini kwamba hiyo ndiyo dunia waliyoishi ndani yake, furaha kidogo na uchungu mwingi.<br />
<br />
Si watoto tu waliowaza siku iliyofuata hata Phillip naye hakupata hata lepe la usingizi, akifikiria kesho yake ingekuwaje, lakini alikabidhi kila kitu mikononi mwa Mungu ili yeye ndiye awe jaji wa kila jambo ambalo lingekwenda kutokea, lakini zaidi alitaka watoto hao wafahamu kwamba pamoja na kuwa hakuwa baba yao wa kuwazaa lakini aliwapenda kwa dhati kupita maelezo na shahidi pekee alikuwa ni Mungu na mama yao Genevieve ambaye kwa wakati huo alikuwa ni marehemu.<br />
<br />
Akaamka na kujiandaa na baada ya maandalizi hayo akatoka sebuleni na kuisabahi familia yake, hapo akaaga na kuondoka kuelekea hotelini akiahidi kurejea muda mfupi baadaye na kuwapa taarifa ni kitu gani kilizungumzwa. Njia nzima aliwaza na kuwazua bila kupata majibu, hatimaye nusu saa tu baadaye akawasili kwenye hoteli waliyokuwa wamefikia watoto wake, hapo akaingia moja kwa moja mapokezi na kuomba mawasiliano nao.<br />
<br />
“Niko hapa kuonana na watu watatu, Mariya, Merina na Morgan,” aliongea.<br />
“Sawa, karibu sana kaka taarifa zako ninazo kitambo sana.”<br />
“Ahsante,” alijibu Phillip akijivuta kuelekea kwenye kiti kilichokuwa maeneo hayo na kuketi kusubiri na haikuchukua muda akawaona watoto hao wakitokeza na kutembea kumwelekea huku wakionyesha uso wa tabasamu wakamsabahi na kumkaribisha kwenye chumba maalum ambacho kiliandaliwa.<br />
<br />
Wakaingia ndani na kuanza mazungumzo ambayo hakika Phillip mwenyewe hakuwa tayari kuyaamini mara zote alibubujikwa na machozi mfululizo. Morgan aliyekuwa pembeni akiwa ndiye mkalimani akitafsiri jambo moja baada ya jingine na mwisho muafaka ukawa umefikiwa.<br />
“Kwa muda wa wiki nzima tumesubiri kuona kama kungejitokeza mtu mwingine na kudai kwamba sisi ni watoto wake lakini historia yako uliyotueleza inaendana kabisa na vielelezo vyetu.<br />
<br />
“Awali tulikuwa navyo hivyo tumelazimika kukuamini kwa asilimia zote ingawa ukweli wote uko wazi, hakika pamoja na mambo yote yaliyotokea maishani mwetu, wewe bado utabaki kuwa baba yetu.” “Tutakupenda mpaka mwisho na hivi tunavyoongea na wewe tayari tumeishaanza kufanya utaratibu maalum wa kuondoka na wewe, si wewe tu bali pia familia yako yote ili tukaishi wote kama ndugu.”<br />
“Ahsante, ahsanteni kwa kunijali wanangu hakika mnanipenda lakini kuna jambo moja linalosumbua ubongo wangu…,” aliongea Phillip lakini hakuweza kumalizia sentensi yake kwikwi ya kulia ikamkaba.<br />
<br />
“Ni kwa nini unalia?”<br />
“Mh! Unajua…”<br />
“Hebu nyamaza ueleze linalokusibu.”<br />
“Nalia furaha lakini pia swali moja linazunguka kichwani mwangu ni kwamba itakuwaje tukifika huko wakati ukweli wote mmeufahamu kwamba mimi si baba yenu?”<br />
“Wewe ndiye baba yetu hakika tunayo kila sababu ya kusimamia hilo hata ikiwezekana kwa mtutu wa bunduki.”<br />
“Mnasema kweli?”<br />
<br />
“Kweli kabisa!”<br />
“Na je vipi kuhusu Victor Fedorov ambaye ndiye mhusika wa kila kitu?””Tutakwenda kujua hukohuko kwani yapata kipindi kirefu sasa tangu ametoweka katika mazingira ya kutatanisha na hivi tunavyoongea nawe tumeliachia kazi jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kujua ni wapi alipo na kama yuko hai au la!” Mariya aliongea akimpigapiga Phillip mgongoni.<br />
<br />
Hatimaye muafaka ukafikiwa kwamba kwa kuwa Mariya , Merina na Morgan walikuwa wametoa muda wa wiki nzima kusubiri kuona kama kungetokea jambo lolote lakini halikuwepo, uamuzi pekee walioufikia ni kuondoka na Phillip na familia yake yote. Hivyo utaratibu ukaanza mara moja wakitakiwa kuwakilisha vielelezo vyao vyote muhimu ili kupata vibali vya kuondoka nchini.<br />
Hilo ndilo likawa jambo kubwa mbele yao, kwa Phillip yote hayo yakionekana kuwa ndoto akiamini kwamba ipo siku angeamka kutoka katika usingizi mzito aliokuwa amelala na kuona kila kitu kikiwa tofauti. Siku zikazidi kusonga mbele Morgan akishughulikia vibali vyote muhimu, hatimaye baada ya muda mrefu akafanikiwa kuvipata na furaha ikaendelea kutawala kati yao.<br />
<br />
“Nashukuru Mungu kila kitu kimekwenda sawa, kilichobaki mbele yetu ni safari tu nadhani ni bora tukafanya maandalizi haya haraka ili turejee nyumbani kuendelea na shughuli nyingine kubwa, zaidi ni ile tuliyoiacha ikiendelea kuhusu Victor Fedorov, ni lazima tufahamu nini kiliendelea baada ya sisi kuondoka, alipatikana akiwa hai au alifikwa na umauti?” aliongea Morgan akionyesha msisitizo na kuwafanya watu wote waliokuwepo hapo wakimsikiliza kumwaga machozi, kwani bado watoto Mariya na Merina walimhitaji baba yao kupita maelezo ili naye ashuhudie kilichokuwa kimetokea na kumkubali Phillip na familia yake yote kama mmoja wa familia yao.<br />
<br />
Kila kitu kikaenda kama walivyotarajia, Phillip akapewa nafsi ya kuaga ndugu, jamaa na rafiki zake akitakiwa kuwataarifu juu ya safari ambayo ilikuwa mbele yake naye akafanya hivyo bila kusita huku furaha ikiendelea kutawala katika moyo wake, kwa walio wengi walionekana kumpongeza na kufurahia tukio hilo lakini baadhi pia wakionekana kuumizwa kwa kumkosa kwani pamoja na matatizo yote aliyokuwa nayo alikuwa ni mtu wa watu.<br />
<br />
Siku mbili baadaye safari ilishawadia wote kwa pamoja wakiwa ndani ya gari la kukodi liliwachukua na moja kwa moja kuwapeleka uwanja wa ndege ambako wangefanya utaratibu na kuondoka kuelekea nchini Urusi kwenda kufaidi maisha.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da42db49397890024"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">MSICHANA NDOTONI MWANGU.......EP. 114<br />
<br />
KWA Phillip, Genevieve na bibi Magdalena jambo lililokuwa likitokea mbele yao lilionekana kama ndoto na muda si mrefu wangezinduka kutoka katika uzingizi mzito. Lakini ukweli ulikuwa umebaki pale pale kwamba walikuwa safarini kuelekea nchini Urusi wakiambatana na wenyeji wao watatu yaani Merina, Mariya na Morgan ambaye alisimama kama mwanasheria wao.<br />
<br />
Ndege w<span class="text_exposed_show">aliyokuwa wamepanda iliondoka uwanja wa ndege wa Dar es Salaam saa tisa na ilitarajiwa kutua nchini Gairo kwa mapumziko kidogo, hatimaye Moscow ilitakiwa kutua muda wa saa mbili asubuhi na hapo ndipo ingekuwa mwisho wa safari yao.<br />
Kama walivyokuwa wametarajia waliwasili saa mbili kamili za asubuhi, ndege ilipokanyaga tu ardhi ya nchi hiyo Mariya na Merina wakawa wa kwanza kushuka huku wakiwakaribisha Phillip na familia yake, muda wote huo furaha ilikuwa ikitawala kati yao walishasahau machungu yote na kilichokuwa mbele yao ni kuyafaidi maisha.<br />
<br />
“Karibuni sana nyumbani,” Morgan aliongea kwa lugha ya Kiingereza.<br />
“Tunashukuru sana,” Phillip alijibu akiachia tabasamu laini usoni mwake.<br />
Wakati Phillip akifurahia kuingia nchini urusi, kichwani mwa Mariya na Merina pamoja na kuwa na furaha walifikiria jambo moja tu, baba yao alikuwa wapi hivyo walipanga baada ya kufika tu kwenda kufuatilia taarifa za uchunguzi wa polisi ili kujua nini kilitokea baada ya wao kuikabidhi kazi ya kumsaka baba yao mikononi mwao.<br />
<br />
Wakaondoka ndani ya uwanja wa ndege moja kwa moja kuelekea nyumbani, huko wakapokelewa na wenyeji wao kisha wakawakaribisha Phillip na familia aliyoambatana nayo.<br />
Wakahakikisha kila kitu kinakwenda sawa na wageni walikuwa wamepata mahitaji yote muhimu wao wakaaga na kutoka kuelekea makao makuu ya polisi kufuatilia majibu ya uchunguzi, wakiongozana na Morgan.<br />
<br />
Gari likaendeshwa kwa kasi na baada ya nusu saa tu baadaye walishawasili kituoni hapo.<br />
Kwa umaarufu wao walikaribishwa moja kwa moja ndani na kuonana na mkuu wa polisi wakafanya mkutano mfupi wakitaka kujua nini kiliendelea na ripoti ya polisi haikufichwa ilielezwa wazi kwamba tangu kupotea kwa Victor Fedorov yapata miezi sita, walikuwa wamefanya kila walichoweza na juhudi zote zilionekana kufikia ukingoni, wakapitiliza mbele zaidi na kusema kwamba huenda alikufa na kufunikwa na barafu nzito hivyo kumpoteza kabisa.<br />
<br />
Baada ya taarifa hiyo huzuni kubwa ikawafunika wao pia wakahisi kukata tamaa ya kumwona tena baba yao akiwa hai, lakini wakatamani kuona hata maiti yake tu waizike kwa heshima zote lakini hilo nalo lilikuwa limeshindikana, wakabaki njia panda wakisubiri muujiza. Huku wakionyesha masikitiko makubwa wakamshukuru mkuu wa polisi, wakamuaga na kurejea nyumbani.<br />
Mioyo yao iliuma kupita kiasi, mara kadhaa kumbukumbu za baba yao ziliwajia ndani ya vichwa vyao wakikumbuka wema, ucheshi na upendo mwingi aliowaonyesha na sasa alikuwa ametoweka kama upepo mbele ya macho yao.<br />
<br />
Ni mawazo hayo ndiyo yaliyosababisha watoto hao kububujikwa na machozi, hakika walikuwa wamepoteza mtu muhimu sana katika maisha yao na asingekuwepo wala kutokea mwingine ambaye angeweza kukidhi shida zao ni kweli alikuwa mkosaji lakini bado aliendelea kubaki kuwa ndiye baba halisi na kibaya zaidi na cha kuumiza, mama yao waliyefunga safari mpaka Afrika, nchini Tanzania kumfuata naye alishakufa miaka mingi iliyopita.<br />
<br />
Baada ya gari kufunga breki ndani ya jengo lao, haraka bila kuongea kitu watoto hao wakashuka mbio huku wakikimbia na kuingia ndani ambako nako walipita mbio sebuleni na kuingia chumbani kwao, jambo hilo liliwashangaza wengi na hata Phillip aliyewashuhudia alipojaribu kufuatilia hakupata jibu la kueleweka zaidi sana alisikia sauti ya vilio ikiambatana na kwikwi.<br />
<br />
“Morgan kimetokea nini huko mlikokwenda?”<br />
“Hali ni mbaya mpaka sasa hakuna taarifa yoyote muhimu juu ya Victor Fedorov na uchunguzi wa polisi umefikia kikomo jambo moja tu naweza kusema huenda alikufa na kufunikwa na barafu nzito, basi”<br />
“Mungu wangu!” Philllip aliongea kwa sauti ya juu.<br />
“Huo ndiyo ukweli japo unauma hatuna budi kuukubali,” Morgan aliongea naye machozi yalionekana kububujika kwenye mashavu yake.<br />
<br />
“Inauma,” Phillip alijibu.<br />
Morgan na Phillip waliendelea kubaki sebuleni kwa muda mrefu wakiongea mambo mengi kama kubadilishana mawazo hatimaye ushauri ukatoka kwamba Mariya na Merina waitwe ili waweze kuongea nao mambo fulani.<br />
<br />
“Hata mimi naunga mkono jambo hilo ni lazima tuwape maneno ya faraja, walikubali tukio hilo na kusubiri kama pengine atakuwa hakufa basi ipo siku atajitokeza na kuugana nao,” Phillip aliongea na sekunde tatu tu baadaye Mariya na Merina walishafika sebuleni na kuungana nao, hapo wakafanya mkutano mfupi wa majonzi wakijaribu kuwaeleza wazi kwamba hapakuwa na sababu ya kuhuzunika kwani kila jambo linalotokea katika maisha ya mwanadamu waamini kwamba lilikuwa na sababu.<br />
<br />
Wakionyesha majonzi makubwa, wakakubaliana na kilichotokea, zaidi sana Morgan aliwataka kufahamu haki zote za baba yao na yeye angekuwa nao bega kwa bega kuhakikisha hakuna kinachopotea.<br />
Maneno hayo yakawa yamerejesha furaha kwa watoto hao, wakageuka upande aliokuwa ameketi Phillip na kwa pamoja wakatamka maneno haya;<br />
<br />
“Umekuja kuchukua nafasi ya baba yetu, hakika wewe ndiye, kuanzia leo utachukua majukumu yote na kuifanya familia kuwa yenye furaha siku zote, tafadhali tunakuomba ukubali na kwa pamoja tunasema tunakupenda,” aliongea Merina kisha walisimama na kutembea kumwelekea Phillip.<br />
<br />
Walipomkaribia wakapiga magoti na kuanza kulia huku wakimweleza kwamba walimpenda sana.<br />
“Ninawepanda pia wanangu Mungu alikuwa nayo sababu niwashukuru pia nanyi kwa kunikubali kunipokea na kunilea, Mungu awabariki sana,” Phillip aliwaambia Merina na Mariya.<br />
Kwa pamoja wakakumbatiana na kuanza kulia, yalikuwa ni machozi ya furaha pamoja na kwamba walikuwa katika masikitiko makubwa ya kupotelewa na baba yao kipenzi.<br />
<br />
Baada ya muungano huo wote kwa pamoja walidhamiria kushikamana kama ndugu wakiapa kutimiza wajibu na kulinda heshima ya baba yao ambaye alikuwa ndiye muasisi wa utajiri wote waliokuwa nao.<br />
“Jambo la muhimu hivi sasa pamoja na yote tuliyoongea ni muhimu tukatangaza habari za kifo cha Victor Fedorov kwenye vyombo vya habari kwa muda usiopungua mwezi mmoja tuone nini matokeo yake,” Phillip alitoa wazo na wote wakalipokea kwa mikono miwili.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea baada ya kutangaza kifo kwa mtu ambaye hakujulikana alikufa au yu hai?</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da4367f8477790572"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501242c4e715b3782246814">MSICHANA NDOTONI MWANGU.......EP. 115<br />
<br />
Ilionekana kuwa safari nyingine ngumu lakini ilikuwa ni lazima waizoee na kuikubali ili maisha yaendelee kwani hivyo ndivyo dunia ilivyokuwa. Kwa pamoja wakakubaliana na kusimama, tegemeo lao kubwa kwa wakati huo akiwa ni Phillip, ndiye alikuwa baba wa familia kipindi chote wakisubiri kuona nini kingetokea baada ya kutangaza kwenye vyombo vya habari.<br />
“Tuta<span class="text_exposed_show">kupenda mpaka mwisho na jambo pekee kwa hivi sasa ni vyema Genevieve akaanza shule haraka iwezekanavyo ili naye apate elimu kama sisi,” Mariya aliongea siku moja wakiwa sebuleni.<br />
“Ni kweli kabisa ni lazima aanze shule mara moja, kesho nitakwenda kuongea na mwalimu wa shule tuliyosoma.”<br />
“Ada je?”<br />
“Tutalipa hakuna shida huyu ni mdogo wetu ni lazima tutimize wajibu kwake.”<br />
“Ahsanteni wanangu Mungu awabariki sana,” Phillip aliongea huku akibubujikwa na machozi.<br />
Furaha ilikuwa imeizunguka nyumba ya Victor Fedorov, kazi zote zikiwa chini ya usimamizi wa Phillip kama baba na Morgan ambaye alikuwa ndiye haswa mwanasheria wa miradi yote iliyomilikiwa na tajiri huyo.<br />
Siku nazo zikazidi kusonga mbele mambo yote yakiwa sawa kama walivyopanga, Genevieve akiwa tayari ameshaanza shule, Phillip, Mariya na Merina wakihakikisha miradi yote inakwenda sawa.<br />
Mwezi wa kwanza ukapita bado wakiwa katika kusubiri, taarifa mbalimbali zikiendelea kutolewa na vyombo vya habari wakati mwingine hata televisheni kubwa nchini humo, lakini bado hakukuwa na majibu yoyote hatimaye nao wakaanza kukubaliana na madai ya polisi ya uchunguzi wao walioufanya kwa kina na kuamini kwamba huenda mzee huyo alikufa na kufunikwa na barafu nzito.<br />
“Pengine inawezekana kweli baba alikufa kitambo kama uchunguzi unavyosema.”<br />
“Hapana hebu tusubiri pengine anataka kutupima kama tumekua.”<br />
“Mariya hakyanani amini tu kwamba baba amefariki.”<br />
“Sijakataa, inawezekana ikawa hivyo ninachokiona mimi hebu tusubiri zaidi.”<br />
“Sawa,” Mariya aliitikia.<br />
Kwa muda wa miezi minne mfululizo bado waliendelea kusubiri huku wakiendelea na shughuli zao kama kawaida na ilipotimia mwezi wa tano wakaanza kuchoka na kukata tamaa kwani walikuwa wamefuatilia kwa karibu sana kila kitu kuchunguza kwa umakini wa hali ya juu na jibu walilokuwa wamelipata halikutofautiana na polisi. Huzuni na majonzi vikatawala upya wakikumbuka mema yote aliyowatendea baba yao enzi za uhai wake.<br />
Hatimaye ikatimu miezi sita wakiwa katika kusubiri mwisho wakafikia uamuzi wa kuutangazia umma kwamba Victor Fedorov aliaminika kufa katika mchezo wa kuteleza kwenye barafu.<br />
“Ni lazima sasa tutangaze kwamba Victor Fedorov alikufa.”<br />
“Tunaungana na wewe.”<br />
“Je, kama ikitokea siku moja akarudi?”<br />
“Hiyo itakuwa habari nyingine lakini sidhani kama jambo hili litatokea.”<br />
“Mh!”<br />
“Huo ndiyo ukweli, hakuna haja ya kuguna wala kujiuliza mara mbilimbili.”<br />
“Morgan kesho asubuhi mchakato huo uanze, sisi kama watoto wa marehemu tupate wasaa japo wa dakika kumi tu katika televisheni ya taifa kuuelezea umma juu ya jambo hilo.”<br />
“Nakubaliana nanyi na kazi hiyo kesho asubuhi itafanyika.”<br />
Saa zikazidi kusonga mbele hatimaye kesho waliyoisubiri kwa hamu kubwa ikawadia na Morgan akafanya taratibu zote na kurejesha majibu kwa Mariya na Merina kwamba alishafanikiwa kuongea na televisheni hiyo kubwa. Maandalizi maalum yakafanyika hatimaye wakaiweka habari hiyo kweupe ikiliacha taifa la Urusi katika mshangao mkubwa na maumivu kutokana na ushirikiano wa mzee huyo kwa jamii iliyomzunguka, umaarufu wa Victor Fedorov ulikuwa mkubwa hivyo kitendo cha kutangazwa kwamba aliaminika kufa kiliwaumiza wengi.<br />
Majonzi, vilio na kuomboleza vikatawala nyumbani kwake, watu mbalimbali maarufu wakiongozwa na rais wa nchi hiyo walifika kutoa pole na rambirambi, wengi wao wakitaka kujua historia kamili ya tukio. Sehemu maalum ilitengwa na kuweka picha kubwa ya Fedorov huku chini yake kukiwa na maneno “Герой ушел” yakimaanisha “Shujaa ameondoka”.<br />
Kutokana na umaarufu wa tajiri huyo nchini Urusi, serikali ikatoa wiki nzima ya maombolezo ishara tosha kwamba alikuwa kipenzi cha watu wengi, hakuwepo mtu hata mmoja aliyefahamu upande wake wa pili kwamba alikuwa ni mtu hatari kupindukia.<br />
Ikiwa ni siku tatu tu tangu kufanyika kwa maombolezo ya Fedorov, kama familia waliamua kwenda kutembelea eneo ambalo ndilo haswa lililoaminika kuchukua maisha ya baba yao kipenzi ambapo mashada mengi yakawekwa eneo hilo pamoja na picha yake kama kumbukumbu pekee katika maisha yao na zoezi hilo lilipokamilika wakarejea nyumbani kuendelea na maombolezo.<br />
Siku ya nne asubuhi jambo la ajabu likatokea na kufanya watu wengi kupigwa na butwaa, ni taarifa kwamba mwili wa mtu asiyefahamika ulikuwa umeonekana ndani ya shimo kubwa lililokuwa Mashariki ya Urusi na mtu mmoja aliyekuwa akifanya mchezo wa kuteleza katika barafu ndiye aliyegundua hilo na kuamua kutoa taarifa polisi ambao walifika mara moja eneo hilo.Gari maalum likatolewa likiwa na polisi ndani yake na likaenda moja kwa moja mpaka eneo husika ili kushuhudia tukio hilo, na ni kweli kabisa wao pia macho yao yaliona kama walivyokuwa wameelezwa.<br />
Haraka taratibu za kuutoa mwili zikafanyika na kuufikisha katika hospitali kuu nchini humo kwa utambuzi, watu wengi walifika na kuangalia kama wangeweza kumfahamu.<br />
***<br />
Akiwa mafichoni aliweza kufuatilia mambo yote ya tajiri huyo mkubwa lengo lake likiwa ni kutaka kulipa kisasi kwa ubaya aliomtendea, hakuwepo mtu hata mmoja aliyefahamu kwamba Ditrov alikuwa hai sehemu fulani kama ilivyoaminika kwa wengi alishakufa muda mrefu.<br />
“Nitakaa hapa huku nikifuatilia nijue jinsi ya kumpata huyu mpumbavu na kulipa kisasi, safari hii atanijua mimi ni nani,” aliwaza Ditrov siku moja lakini ghafla akazipata habari kwamba Victor alitoweka katika mazingira ya kutatanisha na alikuwa akitafutwa bila mafanikio na kama familia walishaamua kuliweka jambo hilo wazi kwamba alikufa.<br />
“Mh! Atakufaje kabla sijakutana naye? Lakini acha afe ili mimi niendelee kula maisha na sasa nitarejea nyumbani,” alijisemea Ditrov. Akafanya maandalizi ya safari kurejea nyumbani nchini Urusi, huko ndiko alikofahamu ukweli kwamba hakika mwanaume huyo alikuwa amekufa na mwili wake ulikuwa umeokotwa kwenye shimo wakati wa mchezo wa kuteleza katika barafu na watoto wake walithibitisha jambo hilo.<br />
“Maisha sasa mswano pamoja na ubaya wake Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amina!” alimaliza Ditrov huku machozi yakimlengalenga.<br />
***<br />
“Mimi naona tukafanye ukaguzi wa mwili huo,” Morgan aliongea ikiwa ni siku ya nne tu.<br />
Bila ubishi wakaondoka nyumbani kuelekea hospitali kila mmoja akiwaza jambo kichwani mwake, bila kupoteza muda moja kwa moja mpaka chumba cha kuhifadhia maiti hapo wakajitambulisha na kuomba kuutambua mwili wa mwanaume aliyeonekana akiwa amekufa.<br />
“Mh!” Merina ndiye aliyekuwa wa kwanza kukagua.<br />
“Kwa nini umeguna?”<br />
“Hapana siye baba, mbona amevimba kiasi hiki? Halafu amekuwa mweusi kupindukia.”<br />
“Hebu?” Mariya akadakia naye bila kukawia akatupa macho yake kuangalia na ghafla wakashuhudia kilio kikali ndani ya chumba.<br />
“Huyu ndiye!” ndilo neno pekee aliloweza kutamka Mariya na kufuatiwa na kwikwi kali.<br />
“Unasema?” Phillip akauliza.<br />
“Hakika nawaambieni aliyelala hapo ni baba yetu!”<br />
Morgan akasogea karibu na kuangalia kwa umakini ni kweli alikuwa Victor Fedorov, mwili wake ukiwa katika hali mbaya kutokana na kukaa katika barafu kwa muda mrefu.<br />
“Hii ni maiti ya Fedorov!”<br />
“Mna uhakika?”<br />
“Ulio kamilifu, hatujakosea hata kidogo, tungependa kupewa kibali cha kuuzika kwa heshima zote,” ndivyo alivyotamka huku akiukagua vyema mwili huo.<br />
<br />
Taratibu maalum zikafanyika wakitafuta vibali husika ili kupata ruhusa ya kuuzika mwili huo kwa heshima zote na hatimaye uchunguzi ulipokamilika na kuridhika wakakabidhiwa mwili wa Fedorov ili wauzike.<br />
<br />
Jambo hilo liliamsha vilio upya watu wakalia na kuomboleza, wengi wakionekana kuzimia kwa tukio hilo lakini hatimaye mwili wa Fedorov ukashushwa kaburini kwa heshima zote, watu mbalimbali wakahudhuria msiba huo. Lilikuwa ni tukio la kuhuzunisha sana pengine kuliko yote yaliyowahi kutokea kwa wakati huo. Tajiri mkubwa, Victor Fedorov akawa amezikwa.<br />
Kama familia, baada ya maziko wakatoa muda wa mwezi mzima kuomboleza wakisimamisha shughuli zote kwa ajili ya maombolezo.<br />
Mwezi mmoja ulipomalizika wakiwa katika majonzi walianza tena kazi zao na Phillip akateuliwa kushika wadhifa wa Victor Fedorov, akipewa majukumu yote kama baba wa familia hiyo mpya.<br />
Furaha, upendo na amani vikitawala ndani na nje ya familia huku akipewa heshima zote kwa kila kitu. Maisha kwa Phillip yakanyanyuka tena baada ya kuwa ameshaumizwa moyo mara kadhaa lakini akaonekana kusahau na kufurahia maisha mapya akifuta maumivu yote aliyowahi kuyapata maishani mwake.<br />
“Мы любим не только вас, но и Женевьевы и его жены Магдалены. Для нас вы являетесь частью нашей крови ...”<br />
(Tunakupenda si wewe tu bali pia Genevieve na bibi Magdalena. Kwetu sisi ninyi ni sehemu ya damu yetu...) waliongea Mariya na Merina kwa lugha ya Kirusi na wote kwa pamoja wakanyanyuka na kumsogelea Phillip wakammwagia mabusu mfululizo huku wakimkumbatia, ishara tosha kwamba walikuwa wamemkubali na kumpokea kama baba yao katika maisha yote yaliyobaki baada ya Victor Fedorov kufariki.<br />
“Морган! Женевьева! Г-жа Магдалена пожалуйста, приезжают сюда, чтобы быть счастливыми вместе.” (Morgan! Genevieve! Bibi Magdalena tafadhali njooni huku tufurahi pamoja.) Mariya alipaza sauti yake kuwaita watu hao ambao walikuja mbio na wote kwa pamoja wakakamilisha furaha kwa kukumbatiana wakiachia vicheko.<br />
MWISHOOOOOOO!!!!!<br />
Nachukua nafasi hii kuwashukuru wapenzi wangu wote kwa kunivumilia tangu mwanzo mpaka mwisho wa hadithi hii.<br />
<br />
WHATS NEXT??????......nite nite!!!</span></div></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da43e0a9752206615"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da448dc2923844354"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501240da469934b61922624"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50ead81545160622"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff50f2222e71714696"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff511e160296242085"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff513b7e6180920720"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5147d76290100508"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff5159fb9664169863"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123ff51746a9502618100"><span class="text_exposed_show"> </span></div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com1tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-89035109135468973402012-07-27T00:10:00.001-07:002012-07-27T00:10:01.986-07:00JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.1<a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/story-bomba-ya-maloveeee.html?spref=bl"></a><br />
<div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"></span></div><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"></span></div><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"></span></div><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"></span></div><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"></span></div><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"></span></div><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"> <img alt="" class="spotlight hidden_elem" src="https://fbcdn-photos-a.akamaihd.net/hphotos-ak-snc7/481353_367145660011682_861590223_a.jpg" style="height: 528px; width: 528px;" /></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"> JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.1<br />
<br />
<br />
Majira ya saa nane za usiku msichana Suzana alikuwa akitoka kujirusha katika ukumbi wa Bilicanas. Kilichomshtua kilikuwa kutoweka kwa mpenzi wake Sammy ambaye aliondoka bila kumuaga. Wazo lake la kwanza lilikuwa Sammy kaondoka na msichana mwingine akijua kabisa yeye ndiye mchumba wake.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Akiwa amekasirika kwa kitendo cha Sammy kuondoka na kumuacha peke yake, kila alipopiga simu yake iliita bila kupokelewa kitu kilichoonesha dharau. Aliamua kurudi nyumbani kwake japo alipanga siku ile kwenda kulala kwa Sammy. Aliendesha gari akiwa amefura kwa hasira huku machozi yakimtoka kutokana kitendo alichotendewa na mpenzi wake ambaye ndiye aliyemtoa kitandani alipokuwa amekwisha kulala. Suzana awaliza mengi juu ya kitendo cha mpenzi wake kumwita klabu na kumkimbia.<br />
<br />
Wakati akitoka Bilicanas mvua ilianza kunyesha, hakutaka kuisubiri aliamua kwenda nayo ili awahi kunyumba angalau alale kwa muda mchache ili asubuhi awahi kanisani misa ya kwanza.<br />
<br />
Mvua ilikuwa kubwa iliyoambatana na upepo mkali kitu kilichomfanya ashindwe kuona mbele ilimbidi alisimamishe gari pembeni ya daraja ya Salenda ili kusubiri upepo upungue ndipo aendelee na safari yake. Upepo ule haukuchukua ulitulia na mvua ilikuwa imekatika.<br />
<br />
Alipowasha gari liligoma kuwaka, alirudia zaidi ya mara tano kuzungusha funguo lakini liligoma kuwaka. Kuteremka kwenye gari alishindwa kutokana na hali ya kiza cha kutisha nje. Wasi wasi ulimtawala na kujiuliza atatokaje pale au ndio atalala mpaka asubuhi.<br />
<br />
Hasira zilizidi kumpanda Suzana kutokana na kukimbiwa na mpenzi wake na kuharibikiwa na gari. Kutokana na hofu aliyokuwa nayo alihakikisha milango na vioo vyote vimefungwa vizuri. Alijikuta akipiga dua kumuomba Mungu amuokoe la janga lile kwa kupata msaada wa watu wenye gari kumsaidia kuwasha gari lake. Lakini kwa muda ule hakukuwa na dalili ya gari lolote kupita.<br />
<br />
Akiwa ameinama mikono ameikutanisha kifuani kwake alishtushwa na upepo makali uliovuka toka baharini na kulifanya gari lake kuyumba na kusogea kidogo. Kwa woga uliompata Suzana alijikuta akitokwa na haja ndogo bila kuelewa. Alitamani kulia lakini aliamini sauti yake haitasaidia lolote kwa vile hakukuwa na wakumsaidia.<br />
<br />
Aliinama kwa woga hakutaka kuangalia popote zaidi ya kusubiri chochote kitakachomtokea. Baada ya muda hali ile ilitulia, Suzana alinyanyua kichwa taratibu ili achukue simu ampigie baba yake amfuate eneo lile ambalo lilikuwa limemuweka katika hali ya hatari.<br />
<br />
Aliponyanyua uso achukue simu iliyokuwa kwenye kwenye dash board, alishtushwa na mwanga mkali kama jua la saa saba mchana. Aliangalia katikati ya bahari palipokuwa kunatoka mwanga ule. Alituliza macho baada ya kumuona mwanamke aliyekuwa amevaa gauni jeupe lilikuwa liking’aa kutokana na mapambo yake.<br />
<br />
Hali ile ilimfanya asahau yalitomtokea muda mfupi na kutuliza macho kumuangalia yule mwanamke aliyekuwa akitembea juu ya maji huku nyuma akisindikizwa na wasichana walikuwa wamebeba vikapu vidogo vilivyokuwa na maua ambayo walimwagia kila hatua ilivyopigwa huku wakiimba nyimbo nzuri.<br />
<br />
Suzana alijikuta akipata ujasiri wa ajabu kwa kufungua dirisha kidogo ili aweze kusikia watu wale walikuwa wakiimba kitu gani. Zilikuwa sauti nzuri kama za kaswida zilizoibwa kwa lugha ya kiarabu. Nyimbo zile zilimvutia na kujikuta akiwa na hamu ya kuwaona watu wale waliokuwa wakitembea juu ya maji huku kwa mstari mbele akitangulia yule mwanamke ambaye usoni kwake kulikuwa kunawaka kama taa na kushindwa kuiona sura yake vizuri.<br />
<br />
Suzana alijikuta akisahau kama wale watu walikuwa wakitembea juu ya maji zaidi ya kushangazwa na sherehe ile ambayo toka azaliwe hajawahi kuona sherehe ya aina ile ya mtu mmoja kutangulia mbele wengine kumfuata nyuma huku wakimuwagia maua na kumwimbia nyimbo nzuri.<br />
<br />
Baada ya muda watu wote walikaa mstari mmoja, kisha yule mwanamke aliyekuwa amepeneza kuliko wote alipita katikati yao na kupigiwa vilegele huku akitupiwa maua. Manukato ya maua yalisambaa mpaka ndani ya gari la Suzana alilokuwa amefungua kioo kidogo kusikia nyimbo alizokuwa anaimbiwa yule mwanamke ambaye alionekana kama bibi harusi lakini muda wote hakumuona bwana harusi wala mwanaume kwenye kundi lile.<br />
<br />
Yule mwanamke alipita kwenye mstari mpaka mwisho alitembea peke yake bila kufuatwa na mtu kisha aligeuka na kuwapungia mkono wenzake ambao nao walimpungia huku wakimrushia maua. Baada ya kutembea kidogo Suzana alimshuhudia yule mwanamke alikunja gauni lake usawa na kifua na kushangaa kumuona akitembea ndani ya maji yaliyokuwa yamemfika tumboni.<br />
<br />
Suzana alijikuta akishtuka na kujiuliza yupo ndotoni au anaona kweli, kilichomshangaza ni umbali aliotoka yule mwanamke akitembea juu ya maji. Lakini cha kushangaza alipokaribia ufukweni alionekana yupo ndani ya maji yaliyomfikia tumboni.<br />
<br />
Aliendelea kumtazama amuone anakwenda wapi, yule mwanamke baada ya kutoka ndani ya maji alitembea juu ya mchanga kulifuata lile gari. Kila hatua ilivyokuwa akipiga ilizidi kumtisha Suzana, alijikuta akimshangaa kutaka kuijua sura yake. Alituliza macho yake kwenye uso wa yule mwanamke aliyekuwa akiisogelea gari huku manukato makali yakizidi kujaa ndani ya gari.<br />
<br />
Kilichomshangaza zaidi ni sura ya yule mwanamke alikuwa akifanana naye kwa kila kitu umbile na sura. Suzana alishtuka na kufunga kioo haraka ili mtu yule ambaye yeye alimuona wa muujiza asiingie kwenye gari. Yule mwanamke alisogea kwenye gari na kuligusa, ajabu baada ya kuligusa lile gari alitoweka ghafla.<br />
<br />
Suzana akiwa anatetemeka alijaribu kuwasha gari kwa mara nyingine, ajabu ya Mungu gari liliwaka aliondoka eneo lile kwa mwendo wa kasi. Alipofika nyumbani kulikuwa kumekucha, alikwenda kuoga haraka ili awahi kanisani kwani muda ulikuwa umekwenda.<br />
<br />
Baada ya kuoga alirudi ndani, lakini alishtushwa na harufu ya manukato ambayo aliyasikia muda mfupi darajani gari lake lilipozima na kuenea hadi ndani ya gari lake. Hakutaka kulifikiria sana lile kwa muda ulikuwa umekwenda, alikwenda kwenye kabati kubadili nguo ili awahi kanisani.<br />
<br />
Baada ya kumaliza kubadili nguo alijikuta akiingiwa na uvivu na kwenda kukaa kwenye kitanda haikupita muda. Usingizi mzito ulimshika na kulala bila kujielewa, aliposhtuka usingizini alishtuka kuiona familia yake yote imesimama mbele yake. Alijiuliza kuna nini, alipojiangalia alijiona alikuwa amevaa nguo za kuendea kanisani.<br />
<br />
“Suzana upo sawa?” Mama yake alimuuliza.<br />
“Mbona unaniuliza hivyo? Halafu mbona kama wote mlikuwa mnalia kuna nini mbona mnanitisha?<br />
<br />
Nini kimemtokea Suzana mpaka familia yake ikusanyike mbele yake huku wakitokwa na machozi. Kuyajua yote fuatana nami katika simulizi hii mpya ya kusisimua..</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">JINI WA DARAJA LA SALENDA.........EP.2.<br />
<br />
LIPOISHIA;<br />
Yule mwanamke alipita kwenye mstari mpaka mwisho, alitembea peke yake bila kufuatwa na mtu kisha aligeuka na kuwapungia mkono wenzake ambao nao walimpungia huku wakiendelea na zoezi la kumrushia maua. Baada ya kutembea kidogo Suzana alimshuhudia yule mwanamke akikunja gauni lake usawa wa kifua na kushangaa kumuona akitembea ndani ya maji yaliyok<span class="text_exposed_show">uwa yamemfika tumboni.<br />
<br />
Suzana alijikuta akishtuka na kujiuliza yupo ndotoni au anaona kweli, kilichomshangaza ni umbali aliotoka yule mwanamke akitembea juu ya maji. Lakini cha kushangaza alipokaribia ufukweni alionekana yupo ndani ya maji yaliyomfikia tumboni.<br />
<br />
Aliendelea kumtazama amuone anakwenda wapi, yule mwanamke baada ya kutoka ndani ya maji alitembea juu ya mchanga kulifuata gari lake. Kila alivyopiga hatua Suzana alizidi kutishika, alijikuta akimshangaa na kutamani kuijua sura yake. SASA ENDELEA...<br />
<br />
Alituliza macho yake kwenye uso wa yule mwanamke aliyekuwa akiisogelea gari huku manukato makali yakizidi kujaa ndani ya gari.<br />
<br />
Kilichomshangaza zaidi umbile la yule mwanamke ambaye mwanzo alionekana kama mrefu tena mweupe lakini kila alivyomsogelea sura na umbile la yule mwanamke lilibadilika na kufanana naye kwa kila kitu. Suzana alishtuka na kufunga kioo haraka ili mtu yule ambaye yeye alimuona wa muujiza asiingie ndani ya gari.<br />
<br />
Yule mwanamke alisogea kwenye gari na kuligusa, ajabu baada ya kuligusa, alitoweka ghafla. Suzana akiwa anatetemeka alijaribu kuwasha gari kwa mara nyingine, ajabu ya Mungu gari liliwaka aliondoka eneo lile kwa mwendo wa kasi. Alipofika nyumbani kulikuwa kumekwisha pambazuka, alikwenda kuoga haraka ili awahi kanisani kwani muda ulikuwa umekwenda sana.<br />
<br />
Baada ya kuoga alirudi ndani, lakini alishtushwa na harufu ya manukato ambayo aliyasikia muda mfupi darajani gari lake lilipozima na kuenea hadi ndani ya gari lake. Hakutaka kulifikiria sana lile kwa sababu muda ulikuwa umekwenda, alikwenda kwenye kabati kubadili nguo ili awahi kanisani.<br />
<br />
Baada ya kumaliza kubadili, alijikuta akiingiwa na uvivu na kwenda kukaa kwenye kitanda haukupita muda usingizi mzito ulimshika na kulala bila kujielewa, aliposhtuka usingizini alishtuka kuiona familia yake yote imesimama mbele yake. Alijiuliza kuna nini, alipojiangalia alijiona alikuwa amevaa nguo za kuendea kanisani.<br />
“Suzana upo sawa?” Mama yake alimuuliza huku akifuta machozi.<br />
<br />
“Mbona unaniuliza hivyo? Halafu mbona kama wote mlikuwa mnalia kuna nini mbona mnanitisha?<br />
“Suzana,” mama yake alimwita tena akiwa bado anamshangaa..<br />
“Abee mama.”<br />
“Upo sawa?” Mama yake alimuuliza huku akimkagua mwanaye kwa kumshika kila kona ya mwili.<br />
<br />
“Nipo sawa mama, kwani vipi?”<br />
“Siamini kweli Mungu wa ajabu.”<br />
“Mama mbona sikuelewi nilitokewa na nini?” Suzana alizidi kushangaa.<br />
<br />
“Hebu nyanyuka kwanza.”<br />
Suzana alinyanyuka kitandani kuonesha yupo sawa, wote waliokuwa mule ndani walishukuru Mungu.<br />
“Kwani muda huu ni saa ngapi?”<br />
<br />
“Saa kumi na moja.”<br />
“Jamani ina maana sikwenda kanisani?” Suzana alizidi kujishangaa.<br />
“Kwani ilikuwaje?” Mdogo wake wa kike alimuuliza huku akionesha kumshangaa dada yake.<br />
<br />
“Hata najua, nashangaa kuwaona mpo mbele yangu mkitokwa na machozi kwani nilikuwa kwenye hali gani?”<br />
“Mmh, haielezeki.”<br />
“Mbona mnanitisha.”<br />
“Ulitaka kwenda kanisani misa ya ngapi?”<br />
<br />
“Ya kwanza, ooh, nimekumbuka nilihisi uchovu na kuja kujilaza kilichoendelea sikujua, kwani mama nini kimenitokea?”<br />
“Tumepigiwa simu na shoga yako kuwa upo katika hali isiyoeleweka, ndipo tulipozoana na wadogo zako kuja hapa. Tulipofika tumekukuta umepoteza fahamu hujitambui hata mapigo yako ya moyo yalionesha kusimama.”<br />
“Mungu wangu!” Suzana alishtuka sana.<br />
<br />
“Basi tulichanganyikiwa, lakini sikutaka kuamini kama kweli utakuwa umekufa, ndipo tulifanya maombi ambayo yamekufanya unyanyuke na kuonesha kama ulikuwa katika usingizi mzito. Hatuamini kama huna tatizo lolote.”<br />
“Ni ajabu kulala muda mrefu kiasi hicho sijawahi kutokewa na kitu kama hicho, lakini nipo sawa kama uchovu ni wa kawaida tu.”<br />
<br />
“Mmh, haya ni maajabu makubwa sana, kuna umuhimu wa kwenda kwanza hospitali kuichunguza afya yako.”<br />
Suzana hakutaka kubishana na familia yake, walimchukua na kumpeleka hospitali ya TMJ. Walipofika walimueleza daktari hali waliyomkutana nayo na baada ya maombi kuamka kama alikuwa usingizini.<br />
<br />
Alichukuliwa vipimo vyote ambayo havikuonesha ugonjwa wowote, waliruhusiwa kurudi nyumbani. Siku ile alichukuliwa kwenda kulala kwa wazazi wake, usiku kwake ulikuwa mrefu kuwaza yote aliyokutana nayo na hali iliyomtokea. Mpaka siku ya pili inaingia hali ya Suzana ilikuwa nzuri hakuonesha mabadiliko yoyote.<br />
<br />
Siku hiyo aliondokea kwa wazazi wake kwenda kazini, alipofika kazini alikuwa mtu mwenye mawazo mengi juu ya matukio yaliyomtokea toka alipokimbiwa na mpenzi wake kwenye ukumbi wa Club Bilicanas, matukio ya ajabu aliyoyaona baharini kwenye sherehe ya ajabu.<br />
Kingine hali waliyomkutanayo kama mtu aliyekuwa amefariki, na kushangazwa na jinsi alivyoamka na kukutwa hana ugonjwa wowote zaidi ya uchovu wa usingizi. Alijiuliza hali ile imemtokea kwa sababu gani, akiwa katika dimbwi la mawazo shoga yake kipenzi Sharifa aliingia.<br />
<br />
“Vipi shoga mbona leo sikusomi?”<br />
“Mmh, shoga wee acha tu kuna mambo yamenitokea yananichanganya.”<br />
“Yapi? Hebu kaa chini nikueleze yaliyonisibu najuta kwenda club usiku.”<br />
“Yepi tena hayo shoga?”<br />
<br />
Suzana alimueleza yote aliyokutatana nayo usiku na hali iliyomkuta baada ya kumaliza kuoga ili aende kanisani na alipoamka na kukukuta watu wamemzunguka na kumueleza walimkuta akiwa kama amekufa.<br />
“Haa! Shoga unayosema ni kweli?”<br />
“Kweli kabisa.”<br />
<br />
“Huyo mtu unasema umemuona wapi?”<br />
“Daraja la Salenda”<br />
“Mmh!” Sharifa aliguna.<br />
“Mbona unaguna?”<br />
“Mbona tukio linafanana kama langu.”<br />
Sharifa naye alikutana na tukio gani linalo fanana na Suzana?</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123797aed9f2b76403676"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012">JINI WA DARAJA LA SALENDA......EP.3<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
Kingine, hali waliyomkutanayo kama mtu aliyekuwa amefariki dunia na kushangazwa na jinsi alivyoamka na kukutwa hana ugonjwa wowote zaidi ya uchovu wa usingizi. Alijiuliza hali ile imemtokea kwa sababu gani. Akiwa katika dimbwi la mawazo shoga yake kipenzi, Sharifa aliingia.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Vipi shoga mbona leo sikusomi?”<br />
<br />
“Mmh, shoga wee acha tu kuna mambo yamenitokea yananichanganya.”<br />
“Yapi? Hebu kaa chini nikueleze yaliyonisibu najuta kwenda klabu usiku.”<br />
“Yapi tena hayo shoga?”<br />
<br />
Suzana alimueleza yote aliyokutana nayo usiku na hali iliyomkuta baada ya kumaliza kuoga ili aende kanisani na alipoamka na kukukuta watu wamemzunguka na kumueleza walimkuta akiwa kama amekufa.<br />
“Haa! Shoga unayosema ni kweli?”<br />
“Kweli kabisa.”<br />
<br />
“Huyo mtu unasema umemuona wapi?”<br />
“Daraja la Salenda”<br />
“Mmh!” Sharifa aliguna.<br />
“Mbona unaguna?”<br />
“Mbona tukio linafanana na kama langu.” SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Lako?”<br />
“Eeeh.”<br />
“Tukio gani?”<br />
“Unajua kuna mtu nilimueleza akasema eti ni uongo na uzushi, si unakumbuka kuna tukio moja lilitamba katika vyombo vya habari?”<br />
“Tukio gani?”<br />
<br />
“Lile la msichana kuota manyoya baada ya kumpa msaada ombaomba kwenye Daraja la Salenda?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Mimi nilikuwa mmoja ya watu walio kataa katakata kuwa ni uzushi, Suzana mimi ni mbishi sana kukubaliana na jambo linaloonekana ni la kusadikika.”<br />
“Mh.”<br />
<br />
“Basi wiki iliyopita katika majira ya saa kumi na mbili jioni nikiwa narudi nyumbani, si unajua foleni za Dar. Toka pale Palm Beach magari yalikuwa yakienda taratibu sana, tulipofika katika Daraja la Salenda magari yalisimama. Niliendelea kusubiri huku nikisikiliza nyimbo za Injili.<br />
<br />
“Nje ya magari kulikuwa na ombaomba wachache, sikushughulika nao, niliendelea kusikiliza muziki nikisubiri foleni isogee. Nilishtushwa na dirisha kugongwa kwa nje, niliponyanyua macho nilimuona ombaomba wa kike akitaka msaada kwangu.<br />
<br />
“Huruma iliniigia, nilifungua dirisha kidogo na kumpa noti ya elfu moja, halafu nilifunga dirisha na kuendelea kusikiliza muziki. Nilishtushwa tena dirisha kugongwa, nilipoangalia nilimuona yule yule ombaomba wa kike. Nilijiuliza ana shida gani ya kugonga tena, safari hii nilijikuta nimefungua kioo mpaka chini na kumuuliza:<br />
<br />
“Una shida gani tena?”<br />
Yule ombaomba aliyekuwa ameinama na uso wake kuzibwa na nywele nyingi alinyanyua uso wake na kunitazama, alionesha kama kunishangaa. Nilijiuliza mbona amenishangaa huenda kanifananisha na mimi nilikaza macho kumwangalia.<br />
<br />
Kilichonishangaza zaidi ilikuwa sura yake iliyofanana sana na yangu kama pacha. Moyo ulinilipuka ajabu, kuna kitu nilikiona kikitoka kwenye macho yake na kupiga kwenye macho yangu na ghafla alitoweka.”<br />
“Weee!” Suzana alishtuka.<br />
<br />
“Ndiyo maana nikasema tukio kama langu japo tofauti yake ni ndogo sana. Baada ya foleni kuanza kutembea, niliondoa gari na kwenda moja kwa moja nyumbani. Amini Suzana tukio lile wala sikulitilia maanani kwa vile sikulielewa na pia sikuwa muumini wa mambo ya kishirikina.”<br />
“Mh!”<br />
<br />
“Basi shoga, siku ile nyumbani nilikutana kimwili na mume wangu. Kama kawaida mzunguko wa kwanza ulikwenda vizuri, ajabu wa pili hakuwa na nguvu. Kila alivyojitahidi nguvu zake za kiume ziligoma.”<br />
“Mmh!” Suzana aliguna na kujitengeneza vizuri kwenye kiti chake.<br />
“Tokea siku ile mpaka leo mume wangu hana nguvu za kiume.”<br />
“Usiniambie!”<br />
<br />
“Kweli kabisa.”<br />
“Sharifa unataka kuniambia ombaomba yule ndiye aliyesababisha yote hayo?”<br />
“Sasa napata picha kuwa sehemu ile kweli kuna kitu kinafanyika.”<br />
“Kwa hiyo unataka kusema ni kweli pale kuna jini kama watu wanavyoamini?”<br />
<br />
“Sina uhakika kama ni jini lakini kuna kitu kibaya.”<br />
“Kwa hiyo hata ya mwanamke kuota manyonya ni kweli?”<br />
“Inawezekana.”<br />
“Mmh! Kama ni kweli basi tuna hatari, kwani yule mwanamke alipatikana?”<br />
“Nilisikia alionekana ufukweni akiwa uchi na akili zake kama chizi.”<br />
“Unataka kuniambia ndiye aliyetutokea?”<br />
<br />
“Huenda.”<br />
“Basi kuna umuhimu wa kulifanyia kazi jambo hili.”<br />
“Ngoja tutafute ushauri wa watu wazima.”<br />
“Kwani mumeo ulimueleza uliyokutana nayo?”<br />
“Sikumueleza kwa kuamini hali ile imetokana na yeye kutoka nje ya ndoa.”<br />
“Una uhakika gani?”<br />
<br />
“Suzana, sasa naingiwa na imani hiyo kutokana na tukio lililokutokea wewe.”<br />
“Sharifa kabla ya kutafuta ufumbuzi mbadala kwa nini usikae chini na mumeo kutafuta sababu ya yeye kuwa vile?”<br />
“Suzana mume wangu namfahamu vizuri, hata kama anatembea nje haijawahi kutokea, ninaye mwaka wa kumi sasa.”<br />
<br />
“Mmh! Bado haijawa sababu, kwani yeye anasemaje?”<br />
“Kwa kweli nyumba yetu imeingia matatizo ya kulaumiana huku nikimlaumu mume wangu na yeye kusema haelewi sababu ile inatokana na nini.”<br />
“Mmekwenda hospitali?”<br />
“Suzana wazo hilo sikuwa nalo, akili yangu yote niliielekeza kwenye lawama.”<br />
<br />
“Sharifa hasira siku zote haijengi ulitakiwa kumsikiliza mwenzako.”<br />
Wakiwa tukiwa katikati ya mazungumzo Brighton mpenzi wa Suzana aliingia. Baada ya kusalimiana Sharifa aliwaaga na kuwaacha wapendanao wazungumze. Baada ya kuondoka Sharifa alimuangalia Brighton kwa jicho la hasira.<br />
“Vipi sweet, mbona unaniangalia hivyo?”<br />
<br />
“Brighton wewe wa kunifanya hivyo, nimepungukiwa nini mwilini mwangu kufikia hatua ya kunidhalilisha kiasi hicho,” Suzana alimlalamikia mpenzi wake.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a79451510085989">JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.4.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
“Sikumueleza kwa kuamini hali ile imetokana na yeye kutoka nje ya ndoa.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Una uhakika gani sababu ya mumeo kuwa hivyo ni kutokana tukio lile?”<br />
“Suzana sasa naingiwa na imani hiyo kutokana na tukio lililokutokea.”<br />
<br />
“Sharifa kabla ya kutafuta ufumbuzi mbadala kwa nini usikae chini na mumeo kutafuta sababu ya yeye kuwa vile?”<br />
“Suzana mume wangu namfahamu vizuri, hata kama anatembea nje haijawahi kutokea ninaye mwaka wa kumi sasa.”<br />
<br />
“Mmh! Bado haijawa sababu, kwani yeye anasemaje?”<br />
“Kwa kweli nyumba yetu imeingia matatizo ya kulaumiana huku nikimlaumu mume wangu na yeye kusema haelewi sababu ile inatokana na nini.”<br />
<br />
“Mmekwenda hospitali?”<br />
“Suzana wazo hilo sikuwa nalo, akili yangu yote niliielekeza kwenye lawama.”<br />
“Sharifa hasira siku zote haijengi ulitakiwa kumsikiliza mwenzako.”<br />
<br />
Wakiwa katikati ya mazungumzo Brighton mpenzi wa Suzana aliingia, baada ya kusalimiana Sharifa aliwaaga na kuwaacha wapendanao hao wazungumze. Baada ya kuondoka Sharifa alimuangalia Brighton kwa jicho la hasira.<br />
<br />
“Vipi Sweet mbona unaniangalia hivyo?”<br />
“Brighton wewe wa kunifanya hivyo, nimepungukiwa nini mwilini mwangu kufikia hatua ya kunidhalilisha kiasi hicho?” Suzana alimlalamikia mpenzi wake. SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Suzana nimekufanya nini tena mpenzi wangu?”<br />
“Hujui...hujui eeh, juzi umenifanya nini Bilicanas?”<br />
“Sasa Suzana nani wa kulaumiwa kati yangu na wewe?”<br />
“Brighton unachukua mwanamke unaniacha club peke yangu, nilikulazimisha kuwa na wewe siku hiyo, si ni wewe ndiye uliyenipigia simu nije tujumuike wote kisha nikalale kwako.<br />
<br />
Kama ulijua una miadi na mwanamke mwingine kwa nini uliniita?” Suzana alijisahau kama yupo ofisini na kujikuta akitokwa na machozi ya uchungu.<br />
“Mimi?”<br />
“Kwani nazungumza na ukuta?”<br />
<br />
“Suzana juzi si nilikuacha unakunywa mimi nikapanda juu kuzungumza na Shakoor, nilipoteremka nilishangaa kukuta meza nyeupe na vinywaji vipo kama nilivyoviacha. Nilijua umekwenda msalani lakini muda ulipokwenda sana ilibidi nitoke nje kukutafuta. Kilichonishangaza sikukuta gari lako ilibidi nikodi teksi hadi nyumbani kwa kuamini umekwenda huko.<br />
<br />
“Kila nilipopiga simu yako iliita bila kupokelewa, nilipofika nyumbani kwangu sikukuta, nilisubiri kwa saa moja mpaka saa tisa na nusu. Baada ya kutokukuona niliamua kukufuata kwako, nilikuta mlango umefungwa. Nilipomuuliza mlinzi aliniambia hujarudi.<br />
<br />
“Hapo nilichanganyikiwa, nilijiuliza utakuwa wapi? Huwezi kuamini mpaka kunakucha nilikuwa sijapata jibu. Simu yako kila nilipopiga iliita bila kupokelewa, nilirudi nyumbani na kuamua kujilaza kidogo niende kanisani misa ya pili kutokana na uchovu wa kutopumzika.<br />
<br />
“Amini usiamini nimeamka saa tatu usiku toka saa moja asubuhi nilipoweka ubavu, toka nizaliwe na kuwa na akili zangu timamu sijawahi kutokewa na usingizi wa ajabu kama ule. Hata nilipoamka nilikuwa kamsa mlevi niliyekunywa pombe nyingi, sikunyanyuka kitandani niliendelea kulala, huwezi kuamini nililala bila kula kwa saa 24 na nilipoamka leo asubuhi nilikuwa na nguvu kama sijatokewa na kitu chochote.<br />
<br />
“Nilipitia kwako mlinzi alinieleza kama ulirudi, lakini kuna kitu kilitokea kilichoonesha kuna jambo limekupata na kuchukuliwa na familia yako. Mimi kiguu na njia mpaka kwenu, nilipofika niliambiwa umekuja kazini na afya yako ni salama. Kwani ulitokewa na nini?”<br />
“Yangenitokea bila wewe?”<br />
<br />
“Bila mimi kivipi Suzana?”<br />
“Eeh, kama ningekwenda kwako unafikiri ningekutana na mauzauza, Brighton uliondoka na mwanamke unajitetea tu,” Suzana alizidi kulakamika.<br />
“Suzana mpenzi wangu tuna muda gani juzi nifanye hivyo?”<br />
“Si umenichoka.”<br />
<br />
“Suzana naapa kwa jina la Yesu Kiristo uliniacha juu sikutoka na mwanamke muulize hata Shakoor kama nilitoka na mwanamke au muulize mlinzi wako nimefika kwako saa ngapi?”<br />
“Itanibidi nikubali kwa vile nakupenda.”<br />
<br />
“Suzana mpenzi wangu niamini siwezi kwenda kunyume na ahadi yetu, nakupenda na sitakusaliti hata siku moja.”<br />
“Basi yamekwisha lakini uliniumiza sana.”<br />
“Mh, eti ulipatwa na nini?”<br />
<br />
“Samahani Brighton toka niingie ofisini sijafanya kazi yoyote, naomba unipe muda baada ya kazi nikitoka hapa nikakuja kwako moja kwa moja tuzungumze, ni mazungungumzo marefu.”<br />
“Nigusie hata kidogo”<br />
“Ni kuhusu nilipotoka Bilicanas na mambo niliyokutata nayo njiani.”<br />
“Mambo gani?”<br />
<br />
“Nimekueleza nitakueleza au unataka nifukuzwe kazi?”<br />
“Basi mpenzi wangu nimekuelewa.”<br />
Waliagana Brighton na mpenzi wake Suzana na kumuacha akifanya kazi. Baada ya kuondoka Brighton, Suzana alijikuta akihamia kwenye maelezo ya Brighton juu ya hali iliyomtokea ya kulala zaidi ya saa kumi na nne. Alijiuliza kama yeye alikutana na maajabu yale, Brighton alikutana na kitu gani.<br />
<br />
Kazi kwake ilikuwa nzito siku ile, aliomba ruhusa na kurudi nyumbani kupumzika, kabla ya kutoka alimjulisha mpenzi wake kuwa anatangulia nyumbani kwake.<br />
<br />
Baada ya kutoka kazini alikwenda moja kwa moja nyumbani kwa mpenzi wake, kwa vile alikuwa na funguo za nyumba alifungua na kuingia ndani. Alipoingia alishangaa kukuta chumbani kumesafishwa tofauti na siku zote, mara nyingi usafi wa nyumba ile alikuwa akifanya yeye.<br />
<br />
Ile haikumsumbua akili yake aliamini kutokana na msongo wa mawazo hali ya usafi ya nyumba ingemfanya asisumbue mwili wake zaidi ya kwenda moja kwa moja chumbani kujilaza. Hali ya hewa ndani ilikuwa nzuri tofauti na siku zote huku harufu ya manukato aliyowahi kuyasikia alipokutana na maajabu ya dalaja la Salenda.<br />
<br />
Upepo mwanana uliompuliza ulimfanya apitiwe na usingizi bila kujijua, katikati ya usingizi alishtushwa na Brighton akimpapasa.<br />
“Aah, mpenzi umerudi zamani?”<br />
“Kama robo saa.”<br />
<br />
Kwa vile Brighton alikuwa amekwishaoga Suzana naye alikwenda kuoga na kujumuika wote kitandani. Kama kawaida walisafiri katika meli ya wapendanao, safari ya kwanza ilianza vizuri kila mmoja aliifurahia. Baada ya safari ya kwanza kwisha Suzana hamu ilikuwa bado haijamuisha alitaka asafiri safari moja zaidi ndipo wapumzike.<br />
<br />
Ajabu kila alipomgusa mwenzake jogoo alikataa kuwika kitu kilichomshtua Suzana.<br />
“Vipi mpenzi mbona hivi?”<br />
“Hata mimi nashangaa.”<br />
Nini kimempata Brighton? Au ndiyo yaliyompata mume wa Sharifa?</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a69fe2b31227830">JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.5.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
Kwa vile Brighton alikuwa amekwishaoga, Suzana naye alikwenda kuoga na kujumuika wote kitandani. Kama kawaida walisafiri katika meli ya wapendanao, safari ya kwanza ilianza vizuri kila mmoja alifurahia safari ile.<br />
<span class="text_exposed_show"> Baada ya safari ya kwanza kwisha, Suzana hamu ilikuwa bado haijamuisha, alitaka asafiri safari moja zaidi ndipo wapumzike.<br />
Ajabu kila alipomgusa mwenzake, jogoo alikataa kuwika kitu kilichomshtua Suzana.<br />
“Vipi mpenzi mbona hivi?”<br />
“Hata mimi nashangaa.”<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Au umeanzia kwa mwingine?”<br />
“Lakini kwa nini kila linapotokea tatizo unanifikiria vibaya kuwa nilikuwa na wanawake? Siku hizi sina kazi, kazi yangu kutembea na wanawake,” Brighton alilalamika.<br />
“Mbona leo imekuwa hivi?”<br />
<br />
“Hata mimi nashangaa.”<br />
Suzana alijitahidi kumkanda mpenzi wake kumrudisha kwenye hali ya kawaida lakini hakukuwa na mabadiliko, jogoo alikataa kuwika. Aliamua kumwacha ajipumzishe waendelee baadaye. Alijilaza pembeni ya Brighton aliyeonekana mwingi wa mawazo.<br />
<br />
Suzana akiwa amejilaza alikuwa na yake aliyokuwa akiwaza, ghafla mazungumzo yake na Sharifa yalijaa kichwani na kuyakumbuka maneno aliyoelezwa juu ya tatizo la mume wake.<br />
<br />
“Basi shoga, siku ile niliporudi nyumbani nilikutana kimwili na mume wangu kama kawaida mzunguko wa kwanza ulikwenda vizuri, ajabu wa pili hakuwa na nguvu kila alivyojitahidi, nguvu za kiume ziligoma.”<br />
<br />
Sauti ile ilijirudia kichwani mwake na kumfanya atishike na kuamini huenda tatizo la Sharifa limempata na yeye. Bila kujielewa, alijikuta akikaa kitako na kumshtua Brighton aliyekuwa katika dimbwi la mawazo.<br />
“Brighton,” alimwita kwa sauti ya juu japo alikuwa pembeni yake.<br />
“Unasemaje?”<br />
<br />
“Hali hii imekutokea mara ngapi?”<br />
“Suzana swali gani hilo, toka niwe na wewe hali hii imeshanitokea?”<br />
“Hapana, basi utakuwa na tatizo la muda mrefu.”<br />
<br />
“Lakini siamini huenda ni uchovu ngoja nipumzike kidogo tutaendelea,” Brighton alimtoa hofu Suzana.<br />
“Mmh! Sawa,” Suzana aliguna akiwa na wasiwasi na maneno aliyoelezwa na Sharifa ya mpenziwe kuwa amekufa nguvu za kiume.<br />
<br />
Kila mmoja alilala upande wake, mchana waliamka na kwenda kupata chakula cha mchana. Wakiwa wamekaa wanakula, Brighton akamsifia Suzana kwa usafi aliofanya na kuifanya nyumba ipendeze.<br />
“Mpenzi umetumia muda gani kufanya usafi ule?”<br />
“Usafi gani?”<br />
<br />
“Wa nyumba,” kauli ile ilimshtua Suzana na kuamini kabisa tayari nyumba yao imeingia kwenye tatizo lakini hakutaka kulikubali mara moja ili kuficha kila anachokiwaza, alijikuta akikubali pongezi zisizo zake.<br />
<br />
Baada ya kupata chakula walirudi nyumbani kupumzika, kwa vile kila mmoja alikuwa na hamu na mwenzake baada ya kuoga walipanda kitandani kujiachia kwa raha zao. Lakini hali ilikuwa mbaya zaidi Brighton hakuwa na nguvu za kiume.<br />
Hali ile ilizidi kumweka Suzana kwenye hali mbaya, hakukubaliana nayo, aliendelea kumsaidia mpenzi wake lakini hali ilikuwa ile ile.<br />
Suzana alijikuta akiangua kilio kitu kilichomshtua Brighton na kuhoji:<br />
<br />
“Suzana mbona unalia?”<br />
“Brighton unajiona upo sawa?”<br />
“Sijajua nikujibu nini?”<br />
“Hujioni haupo sawa?”<br />
“Hali ya leo inanishangaza hata mimi si kawaida yangu.”<br />
“Inawezekana kuwa ndiyo yenyewe,” Suzana aliropoka.<br />
“Yenyewe nini?”<br />
<br />
“We acha tu, kesho nitakwenda kumweleza Sharifa.”<br />
“Kumweleza nini?” Brighton alizidi kuyashangaa maneno ya mpenzi wake.<br />
<br />
“Naomba leo tuachane na hilo.”<br />
“Kwani umegundua nini kuhusu tatizo langu?”<br />
“Brighton sijagundua lolote.”<br />
“Mbona unasema utanijibu kesho?”<br />
“Sijajua nini tatizo, linafanana na la Sharifa.”<br />
“Sharifa ana tatizo gani?”<br />
“Brighton tutazungumza kesho, naomba niondoke.”<br />
“Si ulisema utalala?”<br />
<br />
“Kwa hali hii siwezi kulala niache tu niwahi nyumbani.”<br />
Brighton hakuwa na la kusema zaidi ya kumruhusu Suzana akalale kwao. Suzana akionekana amechanganyikiwa, aliwasha gari na kurejea kwake. Alijikuta akilia njia nzima juu ya hali ya mpenzi wake huku akijiuliza kama itakuwa hivyo mpenzi wake amekufa nguvu za kiume atafanya nini? Alipoingia ndani kwake alijitupa kitandani hata usingizi ulivyomchukua hakujua.<br />
<br />
Suzana alishtuka siku ya pili, alijiandaa kwenda kazini huku akiwa na shauku ya kuonana na Sharifa kumwelezea yaliyomsibu kama yake. Alipofika kazini kiti alikiona cha moto, hakukaa, alikwenda moja kwa moja ofisini kwa Sharifa. Sharifa alipomuona alishtuka na kumkaribisha:<br />
<br />
“Mmh! Dada mbona asubuhi asubuhi?”<br />
“Wee acha tu, ukiona hivyo ujue kuna jambo.”<br />
“Karibu, mi ndo naingia sasa hivi hata vumbi sijafuta kwenye kompyuta.”<br />
“Yaani wee acha tu,” Suzana alisema huku akiketi kwenye kiti.<br />
“Mh, kuna kipi kipya?”<br />
<br />
“Kuna mapya! Yale yaliyokutokea yamefika na kwangu.”<br />
“Yapi hayo tena?”<br />
“Si yaliyomtokea mume wako.”<br />
“Unamaanisha jogoo kushindwa kuwika?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Ehe!”<br />
<br />
Suzana alimwelezea Sharifa yaliyomkuta, baada ya kumsikiliza alishusha pumzi na kusema:<br />
“Unajua unaweza kuona nakutania .”<br />
“Kwa kipi?”<br />
“Jana usiku nilipokutana na mume wangu huwezi kuamini, nimefurahia tendo kama kawaida.”<br />
<br />
“Wewee! Mara zote?”<br />
“Tena ajabu lilikuwa penzi tamu ajabu hata asubuhi nimeamka nilihisi kama siku ya kwanza kuonana na mume wangu.”</span></div></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a5eea4823528906">JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.6.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
Suzana alimuelezea Sharifa yaliyomkuta, baada ya kumsikiliza alishusha pumzi na kusema:<br />
<span class="text_exposed_show"> “Unajua unaweza kuona nakutania!”<br />
“Kwa kipi?”<br />
<br />
“Jana usiku nilipokutana na mpenzi wangu huwezi kuamini nimefurahia tendo kama kawaida.”<br />
“Wewee! Mara zote?”<br />
“Tena ajabu lilikuwa penzi tamu ajabu hata asubuhi nimeamka nilihisi kama siku ya kwanza kuonana na mume wangu.”<br />
“Usiniambie,” Suzana alishika mkono kwa mshtuko. SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Hata nashindwa kuelewa hali ya jana inatokana na nini?”?”Au alikwenda hospitali?”<br />
“Walaa, hata yeye anashangaa.”<br />
“Sasa kwangu imetokana na nini?”<br />
“Hapo ndipo nashindwa kujua hali hii inatokana na nini.”<br />
<br />
“Yaani nashindwa kuelewa na kubakia njia panda, niliamini lililonitokea jana ndilo lililokutokea wewe wiki moja iliyopita. Leo imekuwa tofauti kabisa uliponieleza hali imebadilika.”<br />
“Suzana hebu nawe angalia kwa wiki tuone mabadiliko, huenda vyakula tunayokula vimesababisha upungufu wa nguvu za kiume.”<br />
<br />
“Lakini Sharifa upungufu gani hata kunyanyuka kidogo.”<br />
“Suzana hata kwangu ilikuwa hivyo hivyo, jana sikuamini, tena mume wangu ndiye aliyeniamsha usingizini.”<br />
“Basi inawezekana tatizo hili limeingia, kwani hujawahi kusikia mwingine zaidi yetu mwenye tatizo kama hili?”?”Mmh! Sijawahi.”<br />
<br />
“Kama lako limekwisha huenda langu bado nalo litakwisha.”<br />
“Ondoa wasiwasi nina imani litakwisha.”<br />
“Mmh! Sawa.”<br />
<br />
Suzana alimuaga Sharifa na kurudi ofisini kwake, alipofika alijikuta akicheka peke yake na kuamini huenda tatizo lile huondoka bila dawa.<br />
Siku hiyo Suzana alishinda akiwa bado yupo njia panda, baada ya kuamini alichokiona Daraja la Salenda ndicho kilichosababisha hali ile.<br />
<br />
Lakini ilikuwa tofauti baada ya kukutana na Sharifa na kumueleza kuwa hali ya mumewe kukosa nguvu za kiume imekwisha. Pamoja na kusikia nguvu za mume wa Sharifa zimerudi katika hali yake bado alikuwa na maswali juu ya hali ile kuwatokea wanaume wawili tofauti ilitokana na nini?<br />
<br />
Suzana naye alijipa moyo kuwepo na mabadiliko kwa mpenzi wake, lakini walipokutana zaidi ya mara tatu hakukuwa na mabadiliko yoyote. Bado alijipa moyo kwa vile wiki ilikuwa bado haijakatika. Akiwa ofisini kwake akiendelea na kazi alimuona Sharifa akiingia kwa mwendo wa kujivuta.<br />
<br />
Alipomuona alishtuka na kumuuliza:<br />
“Vipi shoga mbona hivyo?”<br />
“Wee acha tu, hata sijui hili ni balaa gani?”<br />
“Kwa nini? Hebu kaa kwanza.”<br />
<br />
Baada ya kuketi Sharifa alishusha pumzi huku akiuma meno kuonesha kuna kitu kilimuuma sana.<br />
“Vipi shoga kulikoni?”<br />
“Mmh! Hata nashindwa nianzie wapi.”<br />
“Kivipi tena Sharifa mbona unanitisha.”<br />
<br />
“Hebu ngoja,” alisema huku akijiweka vizuri kwenye kiti.<br />
Suzana alimuangalia Sharifa kwa huruma alivyokuwa akiugulia maumivu.<br />
“Jamani Sharifa si uende hospitali?”<br />
“Hata sielewi ugonjwa huu ni wa hospitali au vipi.”<br />
“Kwa nini?”<br />
<br />
“Hadithi bado inaendelea?”<br />
“Hadithi gani tena Sharifa?”<br />
“Si ile niliyokueleza.”<br />
“Ya?”<br />
<br />
“Kuhusu mume wangu na matatizo yake.”<br />
“He! Yamerudi tena?”<br />
“Tena sasa hivi hata kuielezea siwezi.”<br />
“Sharifa mbona unanitisha au bado ni yale yale ya Daraja la Salenda?”<br />
<br />
“Inaweza kuwa hivyo.”<br />
“Mmh! Ehe, kwa hiyo tatizo limejirudia?”<br />
“Hapana, ila limezuka lingine.”<br />
“Lipi hilo?” <br />
<br />
“Basi shoga siku ile baada ya kukueleza raha nilizipata kwa mume wangu usiku wake vilitokea vitu vya ajabu. Nilipokutana na mume wangu nilishangaa kuhisi maumivu makali kama vile maumbile yake yameongezeka hata kuingia ilikuwa shida.”<br />
“Weweee!”<br />
<br />
“Basi shoga wacha nipige kelele za maumivu ambazo zilimshtua mume wangu na kuniuliza hali ile imeanza lini la kuyaona maumbile yake yananiumiza. Nilivumilia lakini sikuona raha yoyote zaidi ya maumivu. Mpaka tunamaliza sikuwa na hamu tena sehemu za siri zilikuwa zikiniuma sana.<br />
<br />
“Siku ya pili sikuwa tayari kuendelea kuumizwa, lakini mume wangu alikuwa akinishangaa na kusema mbona yupo kawaida. Siku ile tulifanya gizani, lakini jana tuliwasha taa na kuyaona ya kawaida. Hata tulipokuwa kwenye zoezi sikuhisi maumivu yoyote.<br />
<br />
“Baada ya kufanya mapenzi na mume wangu kila mmoja aligeuka upande wake kulala, katikati ya usingizi niliota kuna mtu kaingiza mkono sehemu zangu za siri na kuanza kukoroga, kitu kile kilifanya nihisi maumivu makali sana chini ya tumboni.<br />
<br />
Niliposhtuka usingizini nilishtuka kumuona mume wangu akiwa juu yangu, kutokana na maumivu niliyokuwa nikisikia nilimsukuma kwa miguu. Baada ya kumsukuma tumbo lilinikata kwa muda kisha lilitulia.”<br />
<br />
“Jamani kama angekuwa na shida na wewe kwa nini usikuambie kuliko kukuingilia bila taarifa?” Suzana alichangia.<br />
“Hata mimi nashangaa mume wangu toka anioe hajawahi kufanya vile.”<br />
“Wewee!’” Suzana alishtuka kusikia vile.<br />
<br />
“Hebu ona ajabu nyingine baada ya kumsukuma mume wangu na miguu na kuanguka upande wa pili, aliendelea na usingizi mzito na asubuhi nilipomuuliza alishangaa huku akiapa kwa miungu yote hakuniingilia usiku.”<br />
<br />
“Weweee!”<br />
“Yaani nilimueleza yote lakini alibisha na kusema labda nilikuwa naota.<br />
Nilimueleza kuwa alikuwa juu yangu na hali niliyosikia, bado alikataa.<br />
<br />
Basi shoga yangu tokea hapo nilishangaa kuiona damu yangu ya hedhi, ilikuwa ajabu kuingia hedhi mara mbili kwa mwezi. Hata kutembea sitakiwi kuharakisha, nikiharakisha chini ya kitovu pananivuta sana.”<br />
<br />
“Sharifa unajua tunafanya uzembe, tukija shituka tumekwisha umia.”<br />
“Na kweli hili jambo siwezi kuliacha lipite hivi hivi, sasa hivi mapenzi nayaogopa kwani yamekuwa mateso.”<br />
<br />
“Si ulinieleza kuna mtu unayemfahamu tulifanyie kazi, nipo tayari kukusaidia <br />
Mpaka hatua ya mwisho.”<br />
“Nimekuelewa acha nikapumzike, kiuno chote kimenishika na mama amesema anikute nyumbani.”<br />
<br />
Suzana na Sharifa waliagana, baada ya kutoka shoga yake Suzana alizidi kuchanganyikiwa. Alijiuliza ni kitu gani tena kilichomtokea Sharifa, alipanga amtafute mtu amuelezee matatizo ya mpenzi wake.</span></div></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602">JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.7.<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
“Nimekuelewa, acha nikapumzike nyumbani kwani kiuno chote kimenishika na mama amesema anikute.”<br />
Suzana na Sharifa waliagana, baada ya kutoka, Suzana alizidi kuchanganyikiwa juu ya hali ya shoga yake. Alijiuliza ni kitu gani kilichomtokea Sharifa, alipanga amtafute mtu amwelezee matatizo ya mpenzi wake.<br />
<span class="text_exposed_show"> SASA ENDELEA...<br />
<br />
Sharifa akiwa na maumivu makali ya chini ya tumbo, alitembea taratibu kurudi nyumbani. Suzana alipata wazo la kumsindikiza shoga yake ambaye aliamini kabisa alihitaji msaada wake. Alitoka haraka nje na kumkuta akimtafuta dereva wa kampuni ampeleke nyumbani.<br />
<br />
“Sharifa acha nikupeleke mimi.”<br />
“Suzana endelea na kazi, acha tu nitafika.”<br />
“Haiwezekani, lazima nikusindikize.”<br />
“Mmh! Sawa.”<br />
<br />
Suzana alikimbilia kwenye gari lake na kuligeuza haraka kisha akasimamisha pembeni ya Sharifa na kumfungulia mlango. Sharifa aliingia na kufunga mlango. Alimpeleka kwake kupitia Barabara ya Ali Hassani Mwinyi. Ajabu walipokaribia Daraja la Salenda, Suzana alipunguza mwendo na kumfanya Sharifa aliyekuwa amejilaza kukaa kitako.<br />
<br />
Wote walijikuta wakitupia macho maeneo ya baharini labda wataona kitu chochote lakini hawakuona kitu walichokikusudia zaidi ya kuwaona watu wakitembea juu ya mchanga baada ya bahari kupwa. Baada ya kila mmoja kuwa na uhakika hakuna kitu, Suzana aligeuza uso wake na kubadili gia ili waendelee na safari yao.<br />
<br />
Sharifa alikuwa wa kwanza kushtuka na kupaza sauti yake...<br />
“Suzana umemuona yule mwanamke pale pembeni ya barabara?”<br />
Suzana aligeuza shingo tena kuangalia sehemu aliyooneshwa na rafiki yake, kweli alimuona mwanamke mmoja mrefu aliyekuwa amevalia gauni la rangi nyekundu na mtandio wake mwepesi ulioziacha nywele zake nje. Ajabu wakati huo gari lao lilizimika ghafla.<br />
<br />
“Suzana vipi, mbona hivyo?”<br />
“Hata mimi nashangaa gari limezimika ghafla.”<br />
“Makubwa, sasa yule dada ni nani?”<br />
“Hata najua, muone jinsi alivyo mzuri, tena anatuchekea labda anatujua.”<br />
<br />
“Mmh! Lakini mbona sielewi, nausikia mwili wote ukinisisimka.”<br />
“Siyo wewe tu, hata mimi nasikia nywele zikinisisimka.”<br />
“Mmh! Inawezekana mtu yule si mzuri?”<br />
“Na kweli Suzana, hebu yaone macho yake! Mbona siyaelewi... Mungu wangu! Ona miale inatoka machoni kwake, Suzana washa gari tuondoke.”<br />
<br />
Suzana alijaribu kuwasha gari lake lakini liligoma kuwaka, walijikuta wakizidi kupagawa na kutamani kupiga kelele. Sharifa alishtuka kuona mabadiliko kwa yule mwanamke aliyekuwa bado amesimama sehemu ile ile chini ya mti.<br />
“Suzana haya ni maajabu!”<br />
“Ya nini?”<br />
<br />
“Muone yule mwanamke, si alikuwa amevaa gauni jekundu na mtandio?”<br />
Suzana alinyanyua uso kumuangalia yule mwanamke na kumuona akiwa na gauni lingine la rangi pinki lililokuwa limempendeza zaidi ya mwanzo, nywele zake zikiwa zimetengenezwa vizuri na kuongeza urembo wake.<br />
<br />
“Mmh! Kweli! Kama sikosei alikuwa na gauni jekundu.”<br />
“Unajua yule si kiumbe wa kawaida, huenda ni jini.”<br />
“Jini?”<br />
<br />
Kauli ile ilifanya wasikie msonyo mkali ambao ulifanya tumbo la Sharifa livurugike ghafla, baada ya muda lilitulia na kurudi katika hali ya kawaida. Yule mwanamke waliyekuwa wanamshangaa aliwapungia mkono kama anawafahamu, wakajikuta wote wakimpungia mkono, aligeuka na kuondoka kuelekea baharini.<br />
<br />
Walijikuta wakimsindikiza kwa macho yule mwanamke aliyeanza kuelekea katikati ya bahari na kupotea machoni mwao.<br />
“Mmh! Suzana hii nini?”<br />
“Hata sijui.”<br />
<br />
“Sasa yule atakuwa nani?”<br />
“Yaani nazidi kuchanganyikiwa, ulisikia ule msonyo?”<br />
“Nisiusikie vipi wakati umelifanya tumbo langu lingurume na kutulia.”<br />
<br />
Ajabu nyingine, Suzana alipojaribu kuwasha gari liliwaka, wakaamua kuendelea na safari yao huku kila mmoja akijiuliza yule mwanamke mzuri aliyevalia gauni lenye mshono mzuri ambao hawakuwahi kuuona.<br />
“Jamani haya ni maajabu, sasa yule mwanamke ni jini?”<br />
<br />
“Lakini jini gani anavaa nguo nzuri kama zile tena za gharama?”<br />
“Mmh! Makubwa, hata sielewi eneo hili lina nini. Kuna umuhimu wa kuulizia zaidi kwa watu ili tupate ufumbuzi.”<br />
<br />
Suzana aliendesha gari mpaka nyumbani kwa Sharifa, bahati nzuri walimkuta mama yake ameshafika nyumbani kwake. Hali ya Sharifa ilikuwa tofauti na muda mfupi uliopita akiwa ofisini. Alishangaa kujiona akiwa mzima kabisa, wala hakutembea kwa kupinda mgongo kwa maumivu ya tumbo tena.<br />
<br />
Hali ile ilimshangaza hata Suzana kumuona shoga yake yupo katika hali nzuri.<br />
“Sharifa vipi maumivu yamekwisha?”<br />
“Huwezi kuamini sasa hivi sijambo kabisa, siumwi chochote mwilini.”<br />
<br />
“Mmh! Mbona mwaka huu wa maajabu, kila dakika kinazuka kitu kipya machoni mwangu.”<br />
<br />
“Shoga karibu ndani umsalimie mama uwahi kazini.”<br />
Suzana aliingia ndani kwa Sharifa kumsalimia mama yake. Alipoingia nusura akimbie kwa mshtuko, aliyeambiwa ni mama yake Sharifa alikuwa ni yule mwanamke mrembo waliyemuona maeneo ya Daraja la Salenda.<br />
<br />
“Karibu mwanangu.”<br />
“A..a..sante.”<br />
Alishangaa kumuona akitabasamu lakini ajabu Sharifa hakuonesha mabadiliko yoyote zaidi ya kuendelea kumtambulisha kwa mama yake.<br />
“Sharifa huyu ndiye mama yangu.”<br />
<br />
Suzana alijiuliza iweje amshangae baharini lakini nyumbani amtambulishe kuwa ni mama yake. Tofauti yake ilikuwa vazi alilovaa, muda ule alivaa hijabu nyeusi na mtandio mwepesi.<br />
<br />
Suzana aliaga na kutaka kuondoka baada ya kushindwa kumuelewa mama. Ghafla yule mama alibadilika na kuwa mtu wa makamo tofauti na mwanzo. Suzana aliaga ili aondoke baada ya kushindwa kuelewa alichokiona mbele yake.<br />
<br />
Kila dakika imekuwa ikimshangaza Suzana, ni kweli aliyemuona mbele yake ni yule waliyemuona baharini na aligeuka na kuwa mtu mwingine?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a48857412540802">JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.8.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
Alishangaa kumuona akitabasamu, lakini ajabu Sharifa hakuonesha mabadiliko yoyote zaidi ya kuendelea kumtambulisha kwa mama yake.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Sharifa huyu ndiye mama yangu.”<br />
<br />
Suzana alijiuliza iweje amshangae baharini lakini nyumbani amfahamishe ni mama yake. Tofauti yake ilikuwa vazi alilovaa muda ule lilikuwa hijabu nyeusi na mtandio mwepesi. Suzana aliaga ili aondoke baada ya kushindwa kumuelewa mama, lakini ghafla yule mama alibadilika na kuwa mtu wa makamo tofauti na mwanzo. Suzana alishindwa kuelewa alichokiona mbele yake. SASA ENDELEA...<br />
<br />
Akiwa njiani alijiuliza maswali yasiyo na majibu juu ya mambo aliyokutana nayo ya kumuona mwanamke mzuri aliyebadilika nguo, pia kutambulishwa tena kuwa ndiye mama yake Sharifa. Alijikuta akijiuliza Sharifa huenda naye ni jini lakini wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kwa Sharifa, mtu aliyemfahamu muda mrefu hakuonesha kitu chochote cha kumfanya amdhanie kuwa si mtu wa kawaida.<br />
<br />
Alijiuliza ilikuwaje amuone akifanana na mwanamke waliyemuona pembeni mwa Barabara ya Ali Hasani Mwinyi karibu na Daraja la Salenda na baadaye kumuona mtu tofauti. Aliamua kurudi ofisini kuendelea na kazi.<br />
<br />
******<br />
Jioni akiwa nyumbani alipigiwa simu na Sharifa, aliipokea na kuzungumza.<br />
“Vipi shoga za muda?’<br />
“Nzuri tu, vipi unaendeleaje?”<br />
“Huwezi kuamini sijambo kabisa kama siyo mimi niliyekuja ofisini nikitembea kwa shida, kingine kilichonishangaza ni kukatika ghafla kwa damu yangu ya hedhi.”<br />
<br />
“Wewee!”<br />
“Yaani Suzy siamini kila dakika kwangu ni miujiza.”<br />
“Mmh! Makubwa.”<br />
“Halafu Suzy eti kuna kitu gani kisicho cha kawaida ulikiona tulipofika nyumbani?”<br />
“Kitu gani?”<br />
“Kisicho cha kawaida ambacho kilikutisha,” swali lile lilimshtua Suzy na kujiuliza kwa nini ameulizwa.<br />
<br />
“Kwa nini umeniuliza swali hilo?”<br />
“We nijibu kuna kitu nataka kukuambia.”<br />
“Ni kweli, we umejuaje?”<br />
“Hivi nd’o nimeingia toka kwa mtaalamu mama alinipeleka.”<br />
“He ! Amesemaje?”<br />
“Mmh! Shoga mazito si ya kuyazungumza kwenye simu.”<br />
“Kwa hiyo?”<br />
<br />
“Kama unaweza kuja nyumbani njoo, maana hapa nilipo niliyoelekezwa yamenichosha.”<br />
“Mmh! Lazima nije?”<br />
“Basi shoga njoo usikie mambo ya dunia.”<br />
Taarifa zile zilimfanya Suzana ajiandae haraka haraka na kuingia ndani ya gari lake, tayari kwenda kwa Sharifa akiwa na shauku ya kutaka kujua kitu gani kilichomfanya aseme vile. Alimkuta Sharifa akimsubiri kwa hamu.<br />
<br />
“Karibu shoga yangu.”<br />
“Asante.”<br />
“Naona ndiyo unatoka kuoga?’<br />
“Wee acha mwili ulikuwa umechoka kila kona, karibu.”<br />
“Asante,” Suzana alijibu huku akikaa kwenye kochi.<br />
“Mh! Shoga lete habari,” Suzana alianzisha mazungumzo.<br />
<br />
“Basi shoga baada ya kuondoka nilibakia na mama na kumueleza yote yaliyonitokea hata tukio la kuonana na yule mwanamke leo.”<br />
“Ehe.”<br />
“Mama alinieleza lazima yule atakuwa jini.”<br />
“Ehe.”<br />
<br />
“Basi alinichukua na kunipeleka kwa mzee mmoja mtaalam wa majini, tulipofika tulikaribishwa kwenye chumba kilichokuwa na mkeka na nyuma yake kulikuwa shuka nyekundu, pia kulikuwa na picha za kuchora za simba na viumbe visivyoeleweka.”<br />
“Mmh.”<br />
<br />
“Basi mganga huyo kijana akachukua kioo kidogo na kunitaka niweke mkono juu yake na kuniuliza matatizo yangu. Baada ya muda akatanitaka nitoe mkono na kunitaka nikitazame kile kioo kwa muda kisha alishusha pumzi.<br />
<br />
“Huwezi kuamini wakati akikitazama kile kioo jasho lilianza kumvuja yule mganga kama kamwagiwa maji, kitu kilichonishtua sana. Baada ya kushusha pumzi alichukua kitambaa na kukifuta na kutuuliza.”<br />
<br />
“Mnataka mtatuliwe matatizo yenu au unataka kujua sababu ya yote yaliyotokea?”<br />
“Wewe utakavyoona inafaa,” Mama alijibu.<br />
“Mama si huwa nasikia eti waganga wanajua kila kitu kilichotokea kabla ya kutibu?” Niliuliza.<br />
<br />
“Ni kweli tunajua na yote nimeyaona hapa,” mganga alinijibu.<br />
“Sasa si ungeniambia ili nijue natibiwa kitu gani?”<br />
“Hakuna tatizo, kwa hiyo upo tayari kuyasikia yaliyokusibu?”<br />
“Nipo tayari,” nilimjibu.<br />
<br />
“Haya vizuri,” Baada ya kusema vile alichukua unga na kuumwaga mbele yake huku akisema maneno kwa sauti ya chini. Baada ya kusema vile alikichukua kioo na kuangalia tena kwa muda wa kama dakika kumi kisha alitugeukia na kusema:<br />
“Kama nitakuwa nasema uongo naomba ukatae, sitaki nionekane nazungumza tofautina ukweli.”<br />
“Sawa.”<br />
<br />
“Unaitwa Sharifa, sawa?”<br />
“Ndiyo”<br />
“Umeolewa?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Ndani ya wiki tatu kumetokea matatizo ndani ya ndoa yako?’<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Wasiwasi wako ni tukio lililokutokea katika Daraja la Salenda?”<br />
“Kweli.”<br />
“Basi ni kweli tatizo lako lilitokana na tukio la darajani ambalo lilipelekea kukuingizia mgogoro ndani ya ndoa yako. Yule uliyekutana naye ni Jini Balikis, kazi yake kubwa ni kuvuruga ndoa za watu. Si wewe tu kuna watu wengi wamekumbwa na mgogoro huu hata kufikia hatua ya kuachana.<br />
<br />
“Hata rafiki yako kipenzi ana tatizo hilo, tena yule ndiye chaguo la Jini Balkis kwa vile ni mwanadamu pekee aliyeshuhudia sherehe ya kuagwa kwake kuja duniani.<br />
<br />
“ Tuachane na hayo ya shoga yako najua naye ana yake, ila tatizo la mumeo kukosa nguvu za kiume linatokana na kufanya mapenzi na Jini Balkis.<br />
“Kila mnapofanya mapenzi, jini huyo hufika katika eneo la tukio hilo na kuziondoa nguvu za mumeo ili asiweze kukuridhisha vyema.<br />
<br />
“Anafanya hivyo makusudi ili aweze kufanya naye mapenzi yeye wakati wa usiku mkiwa mmelala.<br />
“Kama nasema uongo muulize mumeo kama huwa hafanyi mapenzi na mwanamke mzuri kiasi cha kufikia kukuona wewe hufai tena kwake.”<br />
<br />
Huu ni mwanzo wa siri ya Jini la Daraja la Salenda. Nini kiliendelea?</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a3e5a3880155125">JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.9.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
Kama nasema uongo muulize mumeo kama huwa hafanyi mapenzi na mwanamke mzuri usingizini hadi kufikia hatua ya kukuona hufai tena kwake.”<br />
<span class="text_exposed_show"> SASA ENDELEA...<br />
<br />
Kauli ile kwa kweli ilinishtua sana, basi mganga akaendelea kuchimbua mambo na kusema:<br />
<br />
“Baada ya kufanya vile kitu kile kilikutia wasiwasi kiasi cha kufikiria kutafuta ufumbuzi baada ya kupata tatizo kama hilo kumtokea shoga yako. Kumbuka mwanzo uliamini kabisa tatizo lile linatokana na mwenzako kutokuwa mwaminifu ndani ya ndoa yako kweli?”<br />
“Kweli.”<br />
<br />
“Baada ya kupanga mipango ya kutafuta ufumbuzi wa mumeo kupoteza nguvu za kiume na shoga’ako kukutwa kama mtu aliyekufa, pale shoga’ako kama wangechelewa alikuwa anabadilishwa kwa kuchukuliwa maiti yake ambayo ingepelekwa chini ya bahari na yeye Jini kukaa na mchumba wake.”<br />
<br />
Kauli ile ilimshutua sana Suzana na kujikuta akishika mdomo kwa mshtuko.<br />
“Mungu wangu, ina maana pale nilikuwa nakufa?” Suzana alimuuliza Sharifa.<br />
<br />
“Shoga hebu tulia kwanza unisikilize utaniuliza maswali mwisho japo nina imani maelezo nitakayokupa hutahitaji kuniuliza swali.”<br />
“Mmh! Inatisha sana, haya endelea.”<br />
Basi mganga akaendelea kunieleza:<br />
<br />
“Kilichomrudisha shoga yako duniani ni maombi yaliyofanywa na familia yake bila hivyo maisha yake yote yangekuwa chini ya bahari na jini yule kuishi na mpenzi wake kwa kuwa shida yake ilikuwa kusambaratisha ndoa za wanadamu au uhusiano wa watu waliopendana. Baada ya shoga yako kurudi katika hali yake ya kawaida na wewe mumeo akapoteza nguvu za kiume.<br />
<br />
“Mlipokutana na kuhadithiana juu ya kilichotokea Daraja la Salenda na matukio yaliyowatokea. Alihamia kwa shoga yako kumtoa nguvu za kiume mpenzi wake. Mwanzo shoga yako hakuwa na imani kuwa kuna vitu kama hivyo vinatokea, vilipomtokea kama ulivyomuhadithia mumeo kutokewa na hali ile, hapo ndipo akaamini kabisa ni kweli tatizo lipo katika Daraja la Salenda.<br />
<br />
“Jini Balkis aliwachezea akili kwa kumrudishia mumeo nguvu za kiume ili taarifa za shoga zako zipingane na ukweli ambao ungepata picha ya tukio la Daraja la Salenda.<br />
<br />
Kumbuka usiku wa siku ile ulipokutana kimwili na mumeo kulikuwa na tofauti kubwa na siku zote tangu muoane, kweli au uongo?” Mganga aliniuliza.<br />
“Kweli,” nilijibu huku nikiona aibu kutamka maneno yale mbele ya mama.<br />
“Unajua ni kwa nini?” Aliniuliza.<br />
“Hata sijui.”<br />
<br />
“Majini wanapotaka kufanya mapenzi na wanadamu huwapaka mafuta sehemu za siri ili asipungukiwe nguvu za kiume ili waweze kumpa raha kwa muda mrefu. Hawapendi kukatishwa raha, huchukia sana. Mwanzo walikuwa wakifanya mapenzi na wanadamu bila kutumia kitu chochote.<br />
<br />
“Lakini tatizo la nguvu za kiume ndilo lililowakasirisha na kutafuta njia ya kustarehe na mwanadamu kwa muda mrefu. Njia ilikuwa ni kutafuta dawa ya kumwezesha mwanaume awe na nguvu muda wote wa kufanya mapenzi chombo kisilale, nina imani umenielewa kusema chombo?” Mganga aliniuliza.<br />
<br />
“Ndiyo nakuelewa endelea mzee wangu,” nilimjibu huku nikihisi mwili ukinisisimka kwa yale niliyoyasikia. Basi mzee akaendelea huku akiangalia kioo kama anasoma kitu.<br />
<br />
“Basi baada ya kujua kesho yake shoga yako naye yamemtokea kama yako na kuamini kabisa mtaamini kilichotokea kinatokana na tukio la Darajani Salenda. Usiku mkiwa mmelala, Jini Balkis alikuja na kumpaka mafuta yale mumeo sehemu za siri ambayo yalizifanya sehemu zake zinyanyuke. Mumeo alikuamsha usingizini kutaka haki yake, kweli au si kweli?” Mganga aliniuliza.<br />
<br />
“Kweli,” nilimjibu kwa aibu mbele ya mama aliyekuwa ametulia akisikiliza kwa makini.<br />
“Najua hukuamini kuikuta hali yake tofauti na siku zilizopita za kukosa nguvu za kiume, ulishtuka, hukushtuka?”<br />
“Nilishtuka.”<br />
<br />
“Hata ulipokubali kufanya naye mapenzi bado hukumuamini, ulijua ni yale yale ya siku zote, lakini ilikuwa tofauti na siku zote. Pia kulikuwa na tofauti kubwa siku za nyuma ulipofanya mapenzi kwa muda mrefu ulikuwa unachoka sana lakini siku ile ilikuwa tofauti, kweli au si kweli?”<br />
<br />
“Kweli.”<br />
“Usijibu kwa kuniogopa, nijibu kwa uhakika siyo ukubali hata la uongo.”<br />
“La uongo nitakuambia lakini yote unayosema ni kweli.”<br />
“Najua asubuhi ulipoamka ulijishangaa kuwa na nguvu za ajabu huku ukikumbuka penzi tamu la mumeo ambalo hakuwahi kukupa tangu akuoe.”<br />
“Ni kweli.”<br />
<br />
“Ni kwa nini hukuchoka kama siku zote?”<br />
“Hata sijui, nilifikiri labda kutokana na kukaa muda mrefu bila kukutana na mume wangu.”<br />
“Unataka kuniambia kipindi hiki ndicho kirefu kuchelewa kukutana na mumeo?”<br />
“Hapana.”<br />
<br />
“Unajua sababu ya kufurahia penzi la siku hiyo na asubuhi kuamka na nguvu za ajabu hata kazi siku hiyo ulifanya ukiwa na furaha tele moyoni?”<br />
“Hata sijui.”<br />
“Nawe ulipakwa mafuta yale ambayo hutumia majini wa kike, kujipaka sehemu za siri ambayo huongeza raha ya mapenzi kiasi cha kumfanya mwanaume asikuchoke na yeye kusikia raha ya mapenzi.<br />
<br />
Hata wewe hukuchoka na kusikia raha muda wote wa kufanya mapenzi na ulipoamka hukusikia uchovu wa mwili. Kwa kutumia mafuta yale unaweza kufanya mapenzi ya nguvu kila siku.”<br />
“Mmh! Kumbe.”<br />
<br />
“Wakati wewe unakula raha ndiyo siku hiyo shoga yako yalimtokea kama yaliyokutokea wewe siku za nyuma za mumeo kupoteza nguvu za kiume. Shoga yako alikuja kazini akiamini ungeungana naye kwenye tatizo lake lakini ilikuwa kinyume kitu kilichomchanganya mwenzako na kuwa njia panda tatizo la nguvu za kiume za mpenzi wake lilitokana na nini.<br />
<br />
“Baada ya Jini Balkis kuwachanganya, wazo la kutafuta ufumbuzi wa tatizo lenu lilifutika. Hali ile mwenzako aliamini huenda itaisha kutokana wewe kumuhakikishia tatizo lake linaweza kwisha kama lako bila kwenda popote. Naye aliamini na kumpa nafasi Jini Balkis kufanya mapenzi na mpenzi wake usingizini hadi kufikia hatua ya kutokuwa na hamu naye.<br />
<br />
Siri ya Jini Balkis imewekwa hadharani, je, ufumbuzi utapatikana au ndiyo kumwagia mafuta kwenye moto?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a3e5a3880155125"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a3e5a3880155125"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a3e5a3880155125"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a3e5a3880155125"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a3e5a3880155125"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a35417151477384">JINI WA DARAJA LA SALENDA......EP.10.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
“Nawe ulipakwa mafuta yale ambayo hutumia majini wa kike, kujipaka sehemu za siri ambayo huongeza raha ya mapenzi kiasi cha kumfanya mwanaume asikuchoke na yeye kusikia raha ya mapenzi. Hata wewe hukuchoka na kusikia raha muda wote wa kufanya mapenzi na ulipoamka hukusikia uchovu wa mwili. Kwa kutumia mafuta yale unaweza kufanya mapenzi kila sik<span class="text_exposed_show">u bila kuchoka.”<br />
“Mmh! Kumbe.”<br />
<br />
“Wakati wewe unakula raha ndiyo siku hiyo shoga yako yalimtokea kama yaliyokutokea siku za nyuma za mumeo kupoteza nguvu za kiume. Shogayo alikuja kazini akiamini ungeungana naye kwenye tatizo lake, lakini ilikuwa kinyume kitu kilichomchanganya mwenzako na kuwa njia panda tatizo la nguvu za kiume za mpenzi wake lilitokana na nini.<br />
<br />
“Baada ya jini Balkis kuwachanganya wazo la kutafuta ufumbuzi wa tatizo lenu lilifutika. Hali ile mwenzako aliamini huenda itaisha kutokana wewe kumhakikishia huenda tatizo lake likaisha kama lako bila kwenda popote. Naye aliamini na kumpa nafasi jini Balkis kufanya mapenzi na mpenziwe usingizini kufikia hatua ya kutokuwa na hamu naye. SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Baada ya kuweza kukuchanganyeni akili, penzi mlilofanya na mumeo lilirudisha mapenzi yaliyoanza kutoweka. Kitu kile kilimuudhi sana jini Balkis na kuamua kukukomoa. Najua alichokufanya nikikueleza utaogopa lakini kwa vile umetaka mwenyewe sina budi kukueleza,” kauli ya mganga ilinitisha lakini kwa vile maji nilikwisha yavulia nguo nilikuwa sina budi kuyaoga. Basi mganga akaendelea.<br />
<br />
“Usiku mlipokuwa mkifanya mapenzi bila kuzima taa jini Balkis alishindwa kufanya kitu chochote, kosa kubwa mlilofanya japo msingeweza kujua madhara yake. Nina imani mapenzi uliyofanya wakati wa giza na mwanga kuna mabadiliko yalitokea ulipofanya mapenzi?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Mlipokuwa mkifanya mapenzi gizani ulihisi maumbile ya mumeo kuwa makubwa na kusababisha uumie sana badala ya raha ikawa maumivu.”<br />
“Ni kweli kabisa.”<br />
<br />
“Basi wakati mlipokuwa mkifanya mapenzi gizani, mumeo aliondolewa juu yako na jini Balkis aliingiza mguu wake uliokuwa na kwato kama mbuzi na kuanza kukusukumia ndani.”<br />
Kauli ile ilinifanya nisijikie vibaya mpaka tumbo likaanza kunikata chini ya kitovu, nikiwa navuja jasho la hofu. Mganga aliendelea kunieleza maneno niliyohisi yananikata maini.<br />
<br />
“Basi ulijikuta ukivumilia huku ukiumia, ilifikia hatua kutotamani tena kufanya mapenzi na mumeo kwa kuamini maumbile yake yameongezeka ukubwa. Lakini ulipowasha taa ulishangaa kuyaona ya kawaida uliyoyazoea, kweli si kweli?”<br />
<br />
“Kweli,” nilijibu huku nikizidi kumuogopa mganga kuwa na uwezo wa ajabu kuyajua mambo ambayo hakuyaona lakini utafikiri alikuwepo.<br />
“Ajabu hukumwambia mumeo, kwa nini?”<br />
“Hata sijui,” nilimjibu.<br />
<br />
“Baada ya kuamua kutofanya mapenzi na mumeo kuogopa kuumizwa badala ya kupewa raha, uliamua kutafuta visingizio ili usikutane naye kimwili, uongo kweli?”<br />
“Kweli.”<br />
“Jana kuna kitu cha ajabu kimekutokea ndiyo sababu ya kumpigia simu Bi mkubwa wako?”<br />
<br />
“Ni kweli.”<br />
“Basi, baada ya kuona hufanyi tena mapenzi na mumeo, jana ulipolala uliota ndoto kuna mtu anakuingiza mkono sehemu zako za siri na kuanza kukukoroga kama anavuta kitu toka sehemu zako cha siri na ulipoamka ulijikuta ukitoka damu ambazo uliamini ni za hedhi japo ulishangaa kutokwa na damu ya hedhi mara mbili kwa mwezi kitu ambacho hakikuwahi kukutokea maishani mwako.”<br />
“Ni kweli.”<br />
<br />
“Unajua madhara yake?”<br />
“Hapana!.”<br />
“Naomba uwe na moyo mgumu kwa vile alichokifanya kwa tiba ya kubabaisha hutapona milele.”<br />
“Mungu wangu,” kauli ilitushtua mimi na mama na kujiuliza ni ugonjwa gani tena huo Yaillah.<br />
<br />
“Baba ni ugonjwa gani tena huo?” Ilibidi mama aulize baada ya mimi kuwa katika wakati mgumu nilishika mikono kifuani, nilimuomba Mungu aniepushe na balaa linalotaka kunikumba.<br />
<br />
“Jina Balkis alijiulaumu kwa kuamini alifanya kosa ambalo aliliona limempotezea mapenzi ya mumeo kwake,” mganga alimjibu mama.<br />
“Mapenzi yapi hayo?” Mama aliendelea kuuliza.<br />
<br />
“Kosa kubwa alilofanya ni kumpaka mafuta ya kuongeza ladha ya mapenzi mwanao, kumbuka maumbile ya jini na mwanadamu yanatofautiana, kwa vile yako ya kibinadamu baada ya kukupaka ilizidi raha mara dufu na thamani yake kwa mumeo ilishuka. Alichokifanya kilikuwa kukutoa kizazi kitu ambacho ndicho kitakacho vunja ndoa yenu. Katika ndoto ulichokiota ndicho kilichotendeka usiku wa jana. Jini Balkis alikutoa kizazi na sasa hivi huwezi kuzaa tena maishani mwako.”<br />
<br />
“Mungu wangu,” kauli ya mganga ilinikata maini.<br />
“Sasa baba utatusaidia vipi?” Mama bado alikuwa na ujasiri kutaka kujua nini hatima ya ukatiri wa jini Balkis kwangu.<br />
“Mmh! Ndiyo maana nikasema ipo kazi tena kazi kubwa sana si ya kitoto na tukifanya mchezo tutapotea wote.”<br />
<br />
“Jamani, tupotee kivipi?”<br />
“Vita yake ni kubwa sana, kumdhibiti naweza lakini kama nitakufanyia kinga ya kukufunga huwezi kupona tena. Na kosa lolote linaweza kuhatarisha maisha yetu. Hawezi kukubali kuona anazuiwa kutimiza dhamira yake, kwa kutumia nguvu zake anaweza kututeketeza wote.”<br />
<br />
“Unataka kutuambia kuna uwezekano wa kupona?”<br />
“Upo, lakini ndiyo mzame sana.”<br />
“Baba wewe huwezi?” Mama aliuliza tena kwa vile mimi nilikuwa nimechanganyikiwa kwa niliyoyasikia.<br />
<br />
“Uongo mbaya, mimi siwezi kukirudisha kizazi chake, si yeye ni wanawake wengi wametolewa na yote kaenda kuiweka chini ya bahari kwenye mwamba wa maji yaliyotulia pia hayafikiwi na kitu chochote kitakachoweza kugusa kizazi kile. Kama utaenda hospitalini wanawake wengi wanasumbuliwa na maradhi ya tumbo na wengi maradhi yao kwa tiba ya kisasa hayaonekani lakini siri ni kwamba wengi wao wameondolewa kizazi na kingine sasa hivi matatizo ya nguvu za kiume yamekuwa mengi ambayo yameweka migogolo lakini mabwana hao wakifanya mapenzi ndotoni na mwanamke mzuri hujikuta hawana hamu na wake zao.”<br />
<br />
“Ni kwa sababu gani?” Mama aliuliza.<br />
“Hakuna sababu nyingine ni ya huyo huyo jini Balkis ambaye amekuja duniani kwa sababu ya kuharibu ndoa za watu pia kupata tiba ya tatizo lake la uzazi. Tatizo hili litakwisha akiisha maliza kazi yake ya kupata vizazi mia, ambao walipata bahati ya kutokutana naye. Lakini wengine wote ambao hawatapata tiba mapema ndiyo watakuwa tasa milele.”<br />
<br />
Siri nzito za jini Balkis zinazidi kufunguka, nini hatma ya yote je kuna tiba sahihi ya tatizo hilo? Kuyajua yote hayo tukutane EPISODE 11. KESHOOO........</span></div></span><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"><br />
</span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"><br />
</span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"><br />
</span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"><br />
</span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012391512eb94c46982529">JINI LA DARAJA LA SALENDA.......EP.11<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
Eneo hilo halifikiwi na kitu chochote kinachoweza kugusa kizazi kile. Kama utaenda mahospitalini wanawake wengi wanasumbuliwa na maradhi ya tumbo. Wengi maradhi yao hayaonekani kwa vipimo vya kisasa lakini siri ni kwamba wengi wao wameondolewa vizazi.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Kingine sasa hivi matatizo ya nguvu za kiume yamekuwa mengi ambayo yamesababisha migogoro mikubwa. Wanaume hao wakifanya mapenzi ndotoni na mwanamke mzuri hujikuta hawana hamu na wake zao.”<br />
“Ni kwa sababu gani?” Mama aliuliza.<br />
<br />
“Hakuna sababu nyingine zaidi ya huyo huyo jini Balkis ambaye amekuja duniani kwa sababu ya kuharibu ndoa za watu pia kutafuta tiba ya tatizo lake la uzazi. Tatizo hili litakwisha akishamaliza kazi yake ya kupata vizazi mia. Watakaokuwa na bahati ya kutokutana naye watasalimika. Lakini wengine wote ambao hawatapata tiba mapema ndiyo watakuwa matasa milele.” SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Unafikiri ni mganga gani anaweza kutusaidia?” Nilimuuliza nikiwa nimekata tamaa.<br />
<br />
“Mmh! Nendeni Bagamoyo kwa mzee mmoja maarufu sana maeneo ya Mlingotini, anaitwa Ustaadh Sudi Makata.”<br />
“Una uhakika?”<br />
<br />
“Japo sina uhakika kwa asilimia mia, lakini yule bwana namwamini sana.”<br />
“Tutamjuaje?”<br />
“Mkifika pale Bagamoyo maeneo ya Mlingotini muulizeni mzee Njiwa Manga.”<br />
<br />
“Ni tofauti na ustaadhi Makata?”<br />
“Hapana ndiye huyo huyo Makata, jina la Njiwa Manga kapewa na watoto aliokuwa akiwatuma wamkamatie njiwa manga kwa ajili ya kazi zake za majini. Kila mtoto aliyetumwa akimuona alimwita babu wa njiwa manga. Basi ikawa njiwa manga, njiwa manga mpaka leo.”<br />
“Mmh! Tutajitahidi twende haraka.”<br />
<br />
“Wala msiwe na haraka, jipangeni kwani tatizo limekwishatokea,” mganga alitutuliza.<br />
“Sawa tutafanya hivyo.”<br />
<br />
“Ila leo nitakupa dawa ya kuoga na kufukiza ndani mwako, lakini hapa naona itakuwa vigumu kwa vile mumeo haamini ushirikina. Kwa hiyo dawa ya kufukiza iache ila utaoga hii ambayo itakusaidia kumfukuza jini Balkis asikusogelee. Pia kuna kitu nilisahau kuwaeleza, leo wakati mnarudi nyumbani kutoka ofisini, mlipofika daraja la Salenda mlimuona mwanamke mmoja mrembo sana akiwa amesimama pembeni ya barabara chini ya mti?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Baada ya hapo gari lilizima ghafla?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Yule mwanamke mlimuona akibadilika mavazi?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Basi yule ndiye jini Balkis, ni mwanamke mzuri sana ambaye hakuna mwanaume yoyote anayemtaka akamkataa. Lakini ana roho mbaya, kwa sababu ana matatizo ya uzazi, dawa aliyoelezwa ni kutafuta vizazi vya wanawake mia moja ili atengenezewe dawa ya kupata mtoto.”<br />
<br />
“Mungu wangu, kama ni hivyo unafikiri nitaweza kupona kweli?” Niliuliza kwa sauti ya kukata tamaa.<br />
“Ukiwahi utapona! Mpaka sasa inaonesha ana vizazi ishirini na mbili, bado vingi na havipati kwa urahisi namna hiyo.”<br />
“Mbona mzuri sana, jini gani anavaa nguo kama binadamu, si huwa nasikia wana mabawa?”<br />
<br />
“Wenye mbawa si majini bali malaika, wao ni kama binadamu kabisa, wanaishi maisha kama watu ila wamepewa uwezo wa kujibadili kuwa katika umbile lolote watakalo, pia wana nguvu za ajabu walizobarikiwa na Mungu za kuonekana wanapopenda wao.”<br />
“Kumbe!”<br />
<br />
“Alifanya vile ili mmuone, baada ya hapo aliondoka na ninyi gari lenu liliweza kuondoka, kitu ambacho kiliwahi kumtokea shoga yako siku aliyohudhuria sherehe ya kuagwa jini Balkis kuja duniani rasmi. Mlipofika nyumbani kwako kuna kitu kimoja kilitokea ambacho shoga yako ilifikia hatua ya kukufikiria vibaya na kuamini huenda na wewe ni jini.”<br />
<br />
“Mungu wangu, kitu gani hicho?”<br />
“Alipoingia ndani taswira ya sura ya jini Balkis ilitanda kwenye uso wa mama yako, kitu kilichomshtua sana. Baadaye alijiondoa na bi mkubwa kuwa katika hali yake ya kawaida. Shoga yako aliondoka akiwa hakuamini kabisa. Kama unabisha ukirudi nyumbani muulize kaona nini.”<br />
<br />
Basi baada ya maelezo yale tulirudi, huwezi kuamini kidogo gari linishinde kuendesha kutokana na mshtuko nilioupata. Lakini mama alinipa moyo kwa kuniambia ili nipate ukweli wa kile nilichoambiwa na mganga lazima niende kwa waganga zaidi ya mmoja. Lakini nilimweleza mama mbona yote aliyoyasema yana ukweli kwa asilimia mia?<br />
<br />
Lakini mama alinieleza inawezekana ni kweli kwa asilimia kumi, mengine tusiyoyajua huwa ni uongo wa waganga ili kujipatia pesa. Nilimueleza mbona hakutaka pesa zaidi ya kutueleza twende kwa mganga mwenye uwezo zaidi yake.<br />
<br />
Mama alinikata maini kwa kunieleza kuwa waganga wana tabia ya kutafutiana wagonjwa na kugawana pesa kwa kuufanya ugonjwa uonekane mkubwa usioweza kutibiwa. Tukienda kwa mganga mwenzake tutaambiwa pesa nyingi ambazo hatutaweza kukataa.<br />
<br />
“Kwa hiyo mama hata kutolewa kizazi ni uongo?” Nilimuuliza.<br />
“Uongo, nilishindwa kumkatalia angeona namuingilia kwenye kazi yake.”<br />
<br />
“Kwa hiyo mama nisiwe na wasiwasi?”<br />
“Ondoa wasiwasi, kitu kama hicho hakipo.”<br />
Basi shoga niliporudi kidogo moyo ulitulia japo maelezo yote kila nilipoyafikiria mwili ulisisimka. Niliporudi hata bila kupumzika nikakupigia simu. Basi shoga habari ndiyo hiyo tumekamatwa na jini sijui Balkis,” Sharifa alimueleza Suzy aliyekuwa ametulia kama sanamu asiamini alichokisikia toka kwa shoga yake.<br />
<br />
“Sharifa acha kuligeuza jina lake si umesema anaitwa Balkis.”<br />
“Kweli, Balkis.”<br />
“Mmh! Mbona kama...”<br />
“Kama nini?”<br />
<br />
“Sijaelewa basi inaonekana hata mimi ana mengi juu yangu, kuna umuhimu kesho kunipeleka na mimi,” Suzy alimweleza shoga yake huku wasiwasi ukiongezeka moyoni mwake kwa kuamini mpenzi wake anaweza kumuacha kwa penzi la ndotoni na jini Balkis linalotumia dawa ya kuongeza ladha ya mapenzi na yeye kuonekana si mali kitu.<br />
<br />
“Sawa tutakwenda.”<br />
Waliagana kwa Suzana kurudi nyumbani kwake kutafakari aliyoelezwa na Sharifa, moyoni alikuwa na mambo mawili; kukubali na kukataa. Akili yake ilikuwa kwenye kukataa na kuamini hakuna vitu kama vile.</span></div></span><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"><br />
</span></div></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"><br />
</span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"><br />
</span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"><br />
</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a3e5a3880155125"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a3e5a3880155125"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012394fcdf149797876570">JINI LA DARAJA LA SALENDA.......EP.12.<br />
<br />
<br />
<br />
Basi shoga niliporudi kidogo moyo ulitulia japo maelezo yote kila nilipoyafikiria mwili ulisisimka. Niliporudi hata bila kupumzika nikakupigia simu. Basi shoga habari ndiyo hiyo tumekamatwa na jini sijui Bakils,” Sharifa alimueleza Suzy aliyekuwa ametulia kama sanamu asiamini alichokisikia toka kwa shoga yake.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
“Sharifa acha kuligeuza jina lake si umesema anaitwa Balkis.”<br />
“Kweli, Balkis.”<br />
“Mmh! Mbona kama...”<br />
“Kama nini?”<br />
<br />
“Sijaelewa basi inaonekana hata mimi ana yangu mengi juu yangu, kuna muhimu kesho kunipeleka na mimi.” Suzy alimueleza shoga yake huku wasiwasi ukiongezeka moyoni mwake kwa kuamini mpenzi wake anaweza kumuacha kwa penzi la ndotoni na jini Balkis alinalotumia dawa ya kuongeza ladha ya mapenzi na yeye kuonekana si mali kitu.<br />
<br />
“Sawa tutakwenda.”<br />
Waliagana kwa Suzana kurudi nyumbani kwake kutafakari aliyoelezwa na Sharifa, moyo alikuwa na mambo mawili kukubali na kukataa. Akili yake ilikuwa kwenye kukataa na kuamini hakuna vitu kama vile.<br />
sasa endelea...<br />
<br />
Tatizo la Brighton kukosa nguvu za kiume lilimnyima raha na kuamua kwenda hospitali kutafuta ufumbuzi wa tatizo ambalo hata yeye hakuelewa limetokana na nini. Alikwenda hadi katika hospitali ya TMJ kwa rafiki yake, baada ya kumuelezea tatizo lake daktari alitaka kumpima ili ajue tatizo ni nini.<br />
<br />
Brighton aliingizwa kwenye chumba maalumu na kuvua nguo zote na kubakia na nguo ya ndani, kisha alielelezwa apande kwenye kitanda nilichokuwa mule ndani na kujilaza kusubiri kufanyiwa uchunguzi. Baada ya daktari kuingia chumbani na boksi la gloves kwa ajili ya kumfanyia uchunguzi wa awali. Alichukua gloves ili aanze kufanya uchunguzi hata kabla hajamgusa sauti ilisikika toka nje.<br />
ilimwita:<br />
<br />
“Dokta kuna mgonjwa yupo serious sana.”<br />
“Sorry Mr Brington, nakuja mara moja,” daktari alisema huku akigeuka na akitoka chumbani kumuwahi mgonjwa.<br />
<br />
“Hakuna tatizo,” Brighton alijibu akiwa bado amejilaza kitandani.<br />
Baada ya muda mchache alishangaa kumuona muuguzi wa kike akiingia chumbani mule bila hodi. Brighton alishtuka kumuona muuguzi wa kike mwenye asili ya kiarabu akiingia bila hodi wakati yeye amelala kitandani na nguo ya ndani tu.<br />
<br />
“Wee vipi?” Brighton alishtuka na kutaka kuziwahi nguo zake.<br />
Lakini muuguzi alikuwa ameishawahi kuingia na kumshika kifuani kumrudisha kitandani.<br />
“Brighton hebu tulia.”<br />
Kauli ile ilimshtua Brighton na kujiuliza yule muuguzi amejuaje jina lake, lakini bado alitaka kuamka ili achukue nguo zake.<br />
<br />
“Brighton mbona unakuwa si muelewa, nimetumwa nije nikusaidie tatizo lako.”<br />
Kauli ilimshangaza sana Brighton na kuamua kutulia, lakini hakupenda mwanamke yule aliyeonekana ni muuguzi kumchunguza matatizo yake. Baada ya kutulia yule muuguzi ambaye alikuwa mrembo kupindukia huku akinukia manukato mazuri sana ambayo hakuwahi kuiyasikia alisema:<br />
<br />
“Sikiliza Brighton, tatizo lako si la dawa za kizungu, si lilitokea wakati ukifanya mapenzi na mpenzio?”<br />
“Ndiyo,” Brighton alikubali huku akijiuliza taarifa zile nani kamwambia.<br />
“Basi nitakupa dawa ya kupaka, wala usikubali dawa za kizungu italala moja kwa moja.”<br />
<br />
“Hiyo ni dawa gani?”<br />
“Dawa ya asili ya mafuta mazuri,” Alisema huku akitoa kichupa kidogo kwenye matiti na kujipaka mkononi, bila kuvaa gloves alitelemsha nguo ya ndani kidogo na kuanza kumchua sehemu za siri. Ilikuwa ajabu sehemu zake zilisimama na kumfanya Brighton azidi kushangaa.<br />
<br />
“Sasa hii dawa nitakuachia, kwa vile muda huu natoka, tutaonana siku nyingine. Ila hapa hospital sitakuwepo naacha kazi.”<br />
“Kwa nini mrembo?”<br />
<br />
“Nimeamua tu.”<br />
“Nikitaka kukuona?”<br />
“Si rahisi, la muhimu umepona kampe raha wifi?”<br />
“Umeolewa?”<br />
“Ukitaka mazungumzo mengi utanikuta nje, sasa hivi vaa nguo zako akija daktari mwambie umekwishapona na usikubali kumjibu zaidi ya kuondoka.”<br />
<br />
Baada ya kusema vile yule muuguzi mrembo alitoka na kumuacha Brington akivaa nguo. Akiwa anamaliza kuvaa viatu daktari aliingia na kumkuta anataka kuondoka.<br />
<br />
“Vipi best, mbona unataka kuondoka, samahani nimechelewa hata mgonjwa mwenyewe nimemuona?”<br />
“Una maana gani?”<br />
“Hata hao wauguzi nawaelewa wanasema alikuja dada mmoja wa Kiarabu, alipofika katikati ya korido alidondoka na kuanza kutoa povu, ndipo waliponifuta ili nikampe msaada wa haraka. Lakini ajabu mgonjwa mwenyewe sikumkuta.”<br />
<br />
“Sasa kaenda wapi?”<br />
“Hata wanajua.”<br />
“Labda kapata nafuu kaondoka.”<br />
“Si rahisi kwa hali aliyokuwa nayo si rahisi kuondoka.”<br />
<br />
“Mmh! Sasa atakuwa amekwenda wapi?”<br />
“Hata najua, hebu tuendelee na matibabu yetu.”<br />
“Nimepona,” Brighton alijibu kwa mkato.<br />
<br />
“Mr Brighton najua nimekuchelewesha, samahani sana hebu rudi nikufanyie uchunguzi.”<br />
“Mr Paul nipo sawa.”<br />
“Si kweli, najua umekasirika.”<br />
<br />
“Sijakasirika Mr nipo sawa, nimeshangaa kujiona nipo sawa nikiwa nimelala kitandani, kama itarudia nitakueleza.”<br />
“Heri tungejua tatizo ili lisije likarudia tena.”<br />
“Halitatokea tena.”<br />
<br />
“Si kweli najua umekasirika.” <br />
“Niamini Mr Paul wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu, kwani umetumia muda gani wa kunifanya nikasirike. Na kwa nini nikasirike wakati ulikimbilia kuokoa maisha ya mtu.”<br />
“Kama hujakasirika sawa.”<br />
<br />
Brighton aliagana na Dokta Paulo na kutoka nje ya hospitali, alipofika nje aliingia kwenye gari lake na kuamua kurudi nyumbani. Ili kuiamini dawa yake kabla ya kuondoka alimpigia simu mpenzi wake Suzana.<br />
<br />
“Mpenzi naomba leo uje nyumbani nina imani tiba ya tatizo langu imepatikana.”<br />
“Tiba ya nini?”<br />
“Kwani nasumbuliwa na nini?”<br />
“Lile tatizo la kitandani?”<br />
<br />
Ni kweli Brighton amepona? Yule aliyempa dawa ni muuguzi kweli?</span></div></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a51bd2c98007602"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_5012396b494370b09146276">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.13<br />
<br />
<br />
Hilo hilo.”<br />
“Brighton hebu acha utani.”<br />
<span class="text_exposed_show"> ”Kweli mpenzi wangu, huwezi kuamini ugonjwa ulivyopona.”<br />
“Au ulikwenda kwa Babu?”<br />
<br />
“Walaa, tukikutana nitakueleza maajabu yaliyonitokea, ilikuwa kama bahati ya mtende.”<br />
“Basi leo mtoto hatumwi dukani nina usongo na wewe ile mbaya.”<br />
<br />
Baada ya Suzana kukata simu alijikuta akizidi kuchanganyikiwa na maelezo ya mganga kuhusu mpenzi wake na taarifa za kupona kwake. Alijikuta akianza kuamini maneno ya mama Sharifa kuwa waganga wengi ni waongo, kazi yao kuwatisha wagonjwa ili wapewe pesa nyingi.<br />
<br />
Alijikuta akifuta wazo la kwenda kwa mganga ili na yeye akaangaliziwe mambo yake. Aliona kuna uongo mkubwa kati ya maneno ya mganga na mpenzi wake, alipoambiwa kuwa mpenzi wake hamhitaji tena kwa vile anafanya mapenzi na jini Balkis kwenye ndoto.<br />
<br />
Ujumbe wa mpenzi wake kumhitaji kimapenzi ulidhihirisha jinsi mganga alivyowadanganya. Aliona kwenda kwa mganga ni kupoteza muda na kumpa pesa za bure. Muda ule ule alimpigia simu Sharifa kuahirisha safari ya kwenda kwa mganga.<br />
<br />
“Shoga, kesho safari ya kwa mganga imekufa.”<br />
“Vipi shoga, mbona hivyo?”<br />
“Aah! Basi tu, tutakwenda siku nyingine.”<br />
“Mmh! Sawa.”<br />
<br />
Wakati Suzana akiahirisha kwenda kwa mganga kuangalia matatizo yake, Brighton baada ya kutoka ndani ya hospitali alipepesa macho labda atamuona muuguzi aliyemtibu. Lakini hakumuona, alitaka kwenda kumuuliza ndani ya hospitali, lakini alikumbuka kauli ya yule muuguzi ambaye hata jina lake hakulijua, alimkataza asimuulize mtu yeyote habari zake.<br />
<br />
Aliingia ndani ya gari yake na kuondoka huku akiwa na shauku ya kumuona yule dada mrembo mwenye roho ya huruma. Mpaka anaondoka eneo la hospitali hakumuona. Alijikuta akiwa na shauku ya kumuona yule mrembo ambaye alisema mengi wangezungumza nje ya hospitali.<br />
<br />
Alipokaribia maeneo ya Makumbusho alishtuka kumuona yule dada akiwa katika vazi refu zuri lenye mvuto, lililoongeza uzuri wake akilipungia mkono gari lake. Alilisimamisha mbele yake kidogo, yule mwanamke mrembo alisogea hadi kwenye gari na kufungua kisha aliingia ndani na kukaa kwenye siti.<br />
<br />
Baada ya kukaa na kufunga mlango wa gari, Brighton aliondoa gari bila kujua mrembo anaelekea wapi. Baada ya mwendo mfupi aliitwa jina lake.<br />
“Brighton.”<br />
“Naam.”<br />
<br />
“Za muda?”<br />
“Nzuri.”<br />
“Unaelekea wapi?”<br />
“Nilikuwa narudi nyumbani, lakini nitakusikiliza wewe unakwenda wapi.”<br />
“Umeoa?”<br />
<br />
“Bado.”<br />
“Na Suzana?”<br />
“Suzana! Umemjuaje?”<br />
“Jibu swali,” yule mwanamke alisema huku akimuangalia jicho lililolegea.<br />
“Ni mchumba wangu, si mke wangu.”<br />
“Ina maana ukipata mtu mwingine utakuwa tayari kumuoa na kumuacha Suzy?”<br />
“Itategemea.”<br />
<br />
“Itategemea nini, wakati tayari Suzana ni mchumba wako?”<br />
“Itategemea uwezo wake katika ufahamu wa maisha, Suzana mchumba wangu pamoja na kunipenda, tatizo lake anapenda sana starehe. Kwangu namuona kama si mwanamke anayefaa kuwa mke wangu.”<br />
<br />
“Kwa mfano mimi nikitaka unioe itakuwaje?”<br />
“Mmh! Nitakuweza?”<br />
“Kivipi?”<br />
<br />
“Unaonekana unatoka katika familia ya watu wenye uwezo.”<br />
“Familia yangu ingekuwa na uwezo ningefanya kazi pale hospitali?”<br />
“Hata mimi nashangaa.”<br />
<br />
“Niambie kweli kama utakuwa tayari kunioa niwe mkeo, kila kitu nitashughulikia mimi, nakuahidi kuyabadili maisha yako.”<br />
“Mmh! Nipe muda.”<br />
“Brighton sina muda mwingine zaidi ya huu.”<br />
<br />
“Nimekubali.”<br />
“Kama umekubali naomba leo nikalale kwako.”<br />
“Mmh! Kwa nini tusifanye siku nyingine?”<br />
“Au kwa vile umemwita Suzana?”<br />
“Umejuaje?” Brighton alishtuka tena.<br />
<br />
“Brighton, nimekueleza sitaki maswali ninapokuuliza swali nataka jibu.”<br />
“Ni kweli, leo nilimualika aje tulale pamoja.”<br />
“Tatizo nini?”<br />
“Sasa itakuwaje wewe uwepo na yeye aje?”<br />
<br />
“Wee mwache aje alale, mimi nitalala chumba kingine.”<br />
“Si atakuona?”<br />
“Hawezi kuniona, labda umwambie wewe.”<br />
“Kwa hiyo utaingia nyumbani saa ngapi?”<br />
<br />
“Muda wowote, usiwe na wasiwasi.”<br />
Brighton alielekea nyumbani kwake akiwa na wasiwasi wa kugonganisha wanawake.<br />
<br />
Brighton anakutana na mtihani mzito wa kuvunja uchumba wake na Suzy, Suzy atakubali kirahisi kumpoteza mpenzi wake?</span></div></span></div></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_501237c9a85221912561012"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.14.<br />
<br />
<br />
****<br />
Walipofika nyumbani yule mwanamke aligundua wasiwasi wa Brighton, alimgeukia na kumuuliza:<br />
<span class="text_exposed_show"> “Mbona una wasiwasi?”<br />
“Bado siamini kama Suzana akija hawezi kukuona, kwa nini nisimzuie asije?”<br />
“Hapana Brighton, kwa vile umemuita, mwache aje tu.”<br />
“Anaweza kuja chumba utachokuwemo itakuwaje?”<br />
“Naomba uwe mwelewa, wee mwache aje na mimi hawezi kuniona.”<br />
<br />
“Mmh! Sawa.”<br />
Brighton alikubali kwa shingo upande, lakini moyoni alikuwa na kiburi cha ajabu, kama Suzana atamuona mgeni wake, atakuwa tayari kwa atakachokiamua.<br />
“Brighton bafu lipo wapi?” Mgeni aliuliza.<br />
“Lipo ndani ya chumba cha kulala.”<br />
“Naomba nikaoge.”<br />
<br />
“Ruksa.”<br />
Mwanamke mrembo alielekea chumbani ili aende bafuni kuoga, kila hatua aliyopiga kuelekea chumbani ilimchanganya sana Brighton, alijiuliza imekuwaje mwanamke mzuri kama yule kumpenda yeye kwa haraka. Katika maisha yake aliwahi kuona wanawake wazuri lakini yule alikuwa ni zaidi.<br />
Baada ya mgeni kuingia chumbani, wazo la haraka kwa Brighton lilikuwa kumpigia simu Suzana kumzuia asije. Ili mgeni asisikie alitoka nje lakini ilikuwa ajabu simu ya Suzana haikupatikana, kitu kilichozidi kumweka kwenye wakati mgumu wa kuweza kumzuia asifike nyumbani kwake.<br />
<br />
Akiwa bado anatafakari jinsi ya kutatua tatizo lile, sauti ndani ilimwita.<br />
“Mpenzi upo wapi?”<br />
“Nipo nje.”<br />
“Njoo basi.”<br />
<br />
Brighton aliingia ndani huku akijitahidi kuficha hofu yake, picha aliyoiona mbele yake ilimfanya afikiche macho kujiuliza anachokiona ni kweli au yupo ndotoni. Mbele yake alikuwa amesimama mwanamke mrembo ajabu akiwa amejifunga mtandio mwepesi sehemu ya makalio na kifuani. Sehemu nyingine ya mwili wake ilikuwa wazi. Lilikuwa umbile lenye kumtia msisimko mwanaume yeyote rijali. Alijikuta akipigwa na butwaa kama ameona meli ikitembea barabarani.<br />
“Mbona unanishangaa?” Mgeni alimuuliza.<br />
“Lazima niseme ukweli, wewe ni mwanamke mzuri sana.”<br />
<br />
“Asante, hata wewe ni mwanaume mzuri sana.”<br />
“Nashukuru.”<br />
“Brighton mbona unajiweka roho juu, hebu mwache Suzana aje.”<br />
“Umejuaje?” Brighton alishtuka kusikia vile.<br />
“Unaniuliza nimejuaje, ina maana ninachosema ulifanya siri?”<br />
“Hapana, sipendi litokee tatizo lolote, unaweza kuniona sina maana.”<br />
“Aliyekueleza umruhusu Suzana aje nani?”<br />
<br />
“Wewe.”<br />
“Sasa tatizo nini, nimekueleza mwache aje kwani chumba nitakachokuwa hawezi kuingia.”<br />
“Wewe unajiamini nini?”<br />
“Utajua baadaye sasa hivi ni haraka, mimi si mkeo mtarajiwa?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Kipi kimekufanya ukubali niwe mkeo?”<br />
<br />
“Hata sielewi lakini kitendo chako cha kujitolea kunitibu bila gharama ugonjwa ambao ulinisumbua sana, imeonesha jinsi gani ulivyo muhimu sana kwangu.”<br />
“Kingine?”<br />
“Nimetokea kukupenda na kila dakika mapenzi yangu kwako yanazidi kuongezeka.”<br />
“Nashukuru kusikia hivyo, nina imani kuna vitu umehisi kuvikuta kwenye mwili wangu, basi nakuhakikishia kukufurahisha katika maisha yangu yote.”<br />
“Nitashukuru.”<br />
“Brighton nipo chumbani, Suzana amekaribia kufika.”<br />
<br />
“Umejuaje?”<br />
“Brighton mbona kila ninachokizungumza kwako kinakushangaza?”<br />
“Unanishangaza kuzungumza vitu ambavyo kwa mtu yeyote ni vigumu kuvijua.”<br />
“Brighton najua una hamu kunifahamu kwa undani, hata jina langu hulijui?”<br />
“Ni kweli, hebu niambie jina lako unaitwa nani?”<br />
“Sasa mbona mpaka nimekueleza mimi au hukupenda kulijua jina langu?”<br />
“Huwezi kuamini, jinsi nilivyopagawa kukupata, hata kuuliza jina niliona kazi, najiona kiumbe mwenye bahati ya mtende.”<br />
<br />
“ Naitwa Balkis Bakilas, naomba nikuache Suzana anaingia sasa hivi, nakusihi usioneshe wasiwasi wowote.”<br />
“Umejuaje?’<br />
“Kuwa mwelewa,” baada ya kusema vile aligeuka na kuelekea chumba cha wageni.<br />
Kila hatua aliyopiga kuelekea chumbani huku akimuachia Brighton sehemu za nyuma ambazo ziliumbwa kwa mpangilio. Alijikuta akimeza mate huku akimsindikiza kwa macho. Hata alivyoingia mpenzi wake Suzana hakumuona, alishtuka alipoulizwa swali.<br />
<br />
“Brighton mbona umeshangalia huko hadi naingia wewe huna habari, kuna nini?”<br />
Suzana aliuliza huku macho yake yakiangalia alipoelekea Balkis.<br />
“Aa..aah,” Brighton alibabaika kujibu.<br />
“Brighton kuna nini?”<br />
“Ha..ha..kuna kitu.”<br />
<br />
“Au ulifikiri siwezi kuja?” Suzana alisema huku akimbusu na kukaa pembeni yake.<br />
“Wala.”<br />
“Mbona kama haupo sawa?”<br />
“Nipo sawa.”<br />
“Nakuja.”<br />
<br />
Suzana alisema huku akinyanyuka na kuelekea chumba alichoingia Balkis, Brighton alijikuta akipatwa na mshtuko, wasiwasi wake ulikuwa huenda Suzana alimuona akiingia hivyo alikwenda kumfumania. Alitaka kumkataza lakini mdomo ulikuwa mzito.<br />
<br />
Ni kweli Suzana kamuona Balkis? Na kama kamuona nini kitatokea?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983de3564c25012551">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.15.<br />
<br />
<br />
Suzana alikwenda hadi mlango wa chumba cha wageni na kuingia ndani, Brighton mapigo ya moyo yalikuwa makubwa. Alijisogeza hadi kwenye kochi na kujilaza akiwa ameshikilia mkono mmoja kifuani kuizuia presha kutokana na vurugu itakayotokea chumbani.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Siku zote Suzana alimhakikishia Brighton kuwa siku atakayomkuta na mwanamke ndiyo siku atakielewa kichaa chake. Akili nyingine ilimtuma awahi chumbani kabla Suzana hajafanya lolote. Alinyanyuka alipokuwa amejilaza na kwenda chumba cha wageni.<br />
<br />
Alipofika alifungua mlango na kuingia ndani, Suzana aliyekuwa akianua nguo yake ya ndani, alishtuka na kumuuliza:<br />
“Vipi mbona umeingia kama unafukuzwa?”<br />
<br />
“Aa..aa..,” alijibu kwa kubabaika huku akipepesa macho chumbani kumtafuta Balkis.<br />
“Vipi mbona unatembeza macho chumba kizima kuna nini?” Suzana alimuuliza.<br />
“Walaa, niliweka CD yangu kwenye meza.”<br />
“Sasa ulivyokuja hivyo, umeniona mimi mwizi?”<br />
“Walaaa, nilikuwa najiuliza niliiweka huku au wapi?”<br />
“Brighton, umeanza lini kuweka vitu vyako humu chumbani?”<br />
<br />
“Suzana hii ni nyumba yangu, nina uhuru wa kuweka kitu popote.”<br />
“Mbona leo Brighton sikuelewi?”<br />
“Kivipi?”<br />
“Umekuwa mtu mwenye mawazo mengi pia mwenye hasira tofauti na siku zote.”<br />
“Nipo sawa.” <br />
Brighton bado hakuamini kama kweli chumbani hakuna mtu, wasiwasi wake huenda amekwenda choo cha wote kilichokuwa upande wa mwisho wa nyumba ile. Bila kuongeza neno alitoka na kwenda moja kwa moja msalani ili kumuwahi kama Balkis yuko huko asitoke.<br />
<br />
Alipofika msalani hakukuta kitu, alijikuta akibaki akilishangaa bafu huku akijiuliza Balkis amekwenda wapi, ikiwa hakuna mlango mwingine wa kutokea. Akiwa bado ameshangaa Suzana alisimama tena nyuma yake na kumuuliza:<br />
“Brighton upo sawa?”<br />
“Nipo sawa.”<br />
<br />
“Hapana, kuna kitu kinakusumbua hutaki kuniambia.”<br />
“Suzy, nipo sawa.”<br />
“Hapana Brighton una tatizo unanificha, mimi nani kwako?”<br />
“Mpenzi wangu.”<br />
“Nani wa kumueleza shida zako?”<br />
“Lakini Suzy mimi sina tatizo lolote,” Brighton aliendelea kujitetea japo maji yalikuwa shingoni.<br />
<br />
“Sikubali, kuna kitu unanificha, basi mimi nipo chumbani ukimaliza matatizo yako utanikuta.”<br />
Suzana alisema huku akielekea chumba cha kulala, baada ya kuondoka Brighton aliendelea kuelea kwenye bahari ya mawazo juu ya kitu kilichotokea muda mfupi pale alipomshuhudia Balkis akiingia chumba cha wageni na wakati huo Suzana alikuwa anaingia. Bila kupumzika, alikwenda moja kwa moja chumba cha wageni alichoingia Balkis.<br />
<br />
Lakini cha ajabu, Balkis hakuwepo chumbani wala msalani, alijiuliza atakuwa wapi? Alijikuta akirudi tena chumba cha wageni kupata uhakika kama kweli Balkis hayumo. Chumba cha wageni hakikuwa na vitu vingi vya kuweza mtu kujificha, kitanda na tivii ndogo. Alipofungua mlango na kuingia, alishtuka kidogo akimbie alipomkuta Balkis akiwa amejilaza kitandani akiwa amepitiwa na usingizi. Kwake aliona kama maruweruwe, alifikicha macho kutaka kupata uhakika wa kile alichokiona mbele yake.<br />
<br />
Akiwa bado kapigwa na butwaa, Balkis aligeuka na kufumbua macho, alipomuona Brighton aliachia tabasamu na kusema:<br />
“Mpenzi mbona umeingia bila hodi?”<br />
“Aah! Ulikuwepo?”<br />
“Kuwepo wapi?”<br />
“Chumbani.”<br />
“Chumba gani?”<br />
<br />
“Si humu ndani.”<br />
“Ndani wapi?”<br />
“Sijakuelewa, hebu nieleweshe vizuri, nilikuwa wapi kivipi?” <br />
“Muda mfupi ulikuwa wapi?”<br />
“Brighton, swali gani hilo? Nimekuaga nakuja chumbani na umekuja umenikuta, sasa unaniuliza swali gani hilo?”<br />
“Mbona nimekuja chumbani sikukukuta?”<br />
<br />
“Hukunikuta! Hapa unazungumza na nani?”<br />
“Suzana alikuja huku, kwa wasiwasi wa kukuona ilibidi nije ili isitokee vurugu lakini sikukuona.”<br />
“Sijui unamaanisha nini, hebu nenda kwa Suzana ukamuondoe wasiwasi, nimekueleza mapema acha kujitia jakamoyo.”<br />
<br />
“Umejuaje?”<br />
“Ukirudi nitakuambia, muwahi mchumba wako.”<br />
Brighton alitoka kwenda chumbani kwake na kumuacha Balkis akimsindikiza kwa macho.<br />
Ni kweli Suzana alimuona Balkis? Mbona hakuonekana mwanzo chumbani?</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.16.<br />
<br />
<br />
<br />
Brighton alijitahidi kurudi katika hali yake ya kawaida kabla ya kuingia chumbani. Alipoingia alimkuta Suzana amekaa upenuni mwa kitanda akiwa ameshika tama.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Suzana mpenzi wangu vipi?”<br />
“Vipi nikuulize wewe?”<br />
“Mbona mimi nipo sawa, hebu twende tukaoge mpenzi wangu tuje tulale.”<br />
<br />
Alimshika mkono na kumnyanyua kisha waliongozana naye bafuni, baada ya kuoga walirudi kitandani. Kwa vile Suzana alikuwa na hamu na mpenzi wake, baada ya kuikosa huduma ya kitandani kwa muda mrefu. Brighton hakujiamini kwa asilimia miamoja kukifanya alichomuitia mpenzi wake.<br />
<br />
Lakini ilikuwa kama alivyoelezwa na Balkis kuwa dawa aliyompa inafanya kazi, Suzana aliweza kufurahia mapenzi kwa muda wote, Brighton alijikuta akijisahau kuwa Balkis naye anamhitaji, baada ya kumstarehesha mpenzi wake alipitiwa na usingizi mzito.<br />
Ulipofika usiku wa manane Brighton alishtuka usingizini na kujikuta akifanya mapenzi na Balkis tena chumbani kwake. Baada ya penzi tamu la Balkis ambao aliamini hakuwahi kupewa chini ya jua zaidi ya ndotoni. Alipepesa macho mule chumbani labda atamuona Suzana lakini hakumuona.<br />
<br />
Ili kupata uhakika Suzana yupo wapi alimuaga Balkis kwenda msalani, pamoja na kuwa na choo cha chumbani lakini alitoka kwenda cha watu wote. Ajabu Balkis hakumuuliza chochote, alitoka mpaka chumba cha wageni na kukikuta kitupu. Alikwenda hadi msalani pia hakumuona.<br />
Alijiuliza Suzana atakuwa wapi au ameondoka, lakini haikuwahi kutokea Suzana aondoke usiku tena bila kuaga. Alijikuta akijiuliza bila kupata majibu kuwa yupo ndotoni au kweli, alitoka hadi nje ya nyumba lakini hakukuwa na dalili zozote za kuwepo Suzana.<br />
<br />
Alimfuata mlinzi wa Kimasai na kumuuliza kama Suzana ametoka.<br />
“Rafiki shemeji yako ametoka?”<br />
“Sijaona yeye ikitoka, niliiona inaingia tu.”<br />
“Rafiki lazima ulilala, mbona ndani hayupo?”<br />
“Sijasinzia rafiki, shemeji haijatoka imo ndani.”<br />
“Kweli?”<br />
<br />
“Kweli kabisa rafiki.”<br />
Brighton aliamini kabisa mlinzi alipitiwa usingizi wakati Suzana anatoka, akiwa bado anajiuliza ni kweli Suzana alikuja au ilikuwa ndoto. Lakini akili yake ilimweleza kuwa Suzana alikuja kweli wala haikuwa ndoto na kufanya naye mapenzi na kila mmoja alipitiwa na usingizi mzito.<br />
<br />
Lakini aliposhtuka na kujikuta akifanya mapenzi na Balkis tena penzi tamu adhimu, bado alikuwa njia panda kujiuliza kilichotokea ni nini yupo ndotoni au ni kweli. Kwa maelezo ya mlinzi kuwa kweli alimuona anaingia lakini hakumuona anatoka ilizidi kumchanganya.<br />
<br />
Hata kama kweli alitoka bado asingeondoka bila kuaga, na kitu kile hakikuwahi kutokea toka waanze uhusiano wao. Akiwa bado yupo njia panda kwa kile alichokuwa akikiwaza juu ya kuyeyuka kwa mpenzi wake . Sauti ya Balkis alimtoa kwenye dimbwi la mawazo.<br />
“Brighton huku ndiko msalani?”<br />
“Aa..aah... nilikuwa napunga upepo.”<br />
<br />
“Imeanza lini na leo iwe ya pili?”<br />
“Ni kawaida yangu wala si leo.”<br />
“Kweli?”<br />
“Kweli kabisa.”<br />
“Kwa hiyo nikuache uendelee kupunga upepo?”<br />
“Hapana, wacha turudi ndani.”<br />
<br />
Brighton alirudi ndani na Balkis, walipofika kitandani bado alikuwa na mawazo, lakini hakutaka kuumia kichwa alimuuliza Balkis.<br />
“Eti Suzana wakati anaondoka ulimuona?”<br />
“Swali gani hilo Brighton?”<br />
“Ooh! Basi.”<br />
<br />
“Kwanini unaniuliza habari za mpenzi wako mimi zinanihusu mimi?” Balkis alimuuliza kwa sauti kali kidogo.<br />
“Hapana mpenzi, inawezekana ulikuwa ninaota.”<br />
“Kuota nini?”<br />
<br />
“Kuwa Suzana alikuja leo.”<br />
“Kama alikuja yupo wapi?”<br />
“Inawezekana nilikuwa naota.”<br />
“Kama ulikuwa unaota basi tulale,” Balkis alimkumbatia Brighton, hakuchelewa usingizi mzito ulimpitia. <br />
<br />
****<br />
Suzana aliposhituka usingizini hakuamini macho yake alipojikuta yupo nyumbani kwake amelala kitandani. Alirudia kutazama tena ni kweli au alikuwa akiota, akili yake ilimjulisha kuwa jana alipigiwa simu na mpenzi wake Brighton kuwa amepata dawa ya matatizo ya nguvu za kiume na alipokwenda kweli alikuwa amepona.<br />
<br />
Alikumbuka Brighton alimpa penzi tamu na kujikuta wote wakipitiwa usingizi, lakini ilikuwa ajabu kuamka asubuhi na kujikuta amelala kitandani kwake. Alijiuliza simu aliyopigiwa alikuwa anaota au kweli, kila alipolazimisha labda ni ndoto akili ilikataa na kuamini kabisa alikwenda kwa Brighton.<br />
<br />
Alijiuliza labda baada ya kufanya mapenzi alirudishwa nyumbani, lakini kwa upande wake kitu kama kile hakikuwahi kutokea. Kingine kilichomshangaza hata kama alirudishwa akiwa amelala hakuwa na fahamu. Alikaa kitandani kwa muda na kukumbuka anatakiwa kujiandaa kwenda kazini.<br />
Aliamka na kwenda kujiandaa, alipofika kazini bado akili yake haikumpa alimtafuta Sharifa amueleze kilichomtokea.<br />
<br />
Suzana na Brighton kilichowatokea watakigundua? Wakikigundua watachukua hatua gani? Balkis atatimiza dhamira yake?</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dd5770970703290">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.17.<br />
<br />
<br />
<br />
Alipofika alimkuta ndiyo kwanza anafuta vumbi kwenye kompyuta yake, Sharifa alipomuona Suzana aligundua ana matatizo.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Karibu shoga.”<br />
<br />
“Asante,” alijibu huku akisogeza kiti na kuketi.<br />
“Mbona uko hivyo?”<br />
“Mmh! Kuna kitu kimenitokea jana sikielewi hata kidogo!”<br />
“Kitu gani hicho?”<br />
“Unakumbuka jana nilikupigia simu?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Nikakueleza kuwa nimeahirisha kwenda kwa mganga?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Basi, Brighton si aliniita na kunieleza kuwa amepata dawa ya tatizo lake na kukosa nguvu za kiume.”<br />
“Ehe?”<br />
<br />
“Baada ya kunieleza vile nikaona hakuna sababu yoyote ya kwenda kwa mganga kwa vile dawa imepatikana.”<br />
“Ehe!”<br />
“Basi jana saa moja usiku nikaenda kwa mpenzi wangu.”<br />
“Lete raha dada.”<br />
“Tumekutana kama kawaida, baada ya kuoga tulipanda kitandani, si unajua usongo niliokuwa nao.”<br />
<br />
“Najua sana.”<br />
“Basi shoga, kama alivyonieleza ndivyo ilivyokuwa, mtoto wa kike nikajilia raha nilizozipoteza muda mrefu.”<br />
“Alikuwa na nguvu kama kawaida?”<br />
“Tena ziliongezeka mara mbili.”<br />
<br />
“Mmh! Makubwa, kampata mganga gani huyo?”<br />
“Anasema alikwenda hospitali.”<br />
“Jamani ona sasa, kumbe tunakimbilia kwa waganga tiba ipo hospitali, nilikueleza toka awali waganga wengine wanatengeneza ugonjwa, ionekane kweli tuna matatizo makubwa ili tuwape fedha nyingi.”<br />
“Shoga bado nakuja sijafika kwenye pointi yangu.”<br />
“Ipi tena?”<br />
<br />
“Sababu iliyonifanya nisiingie ofisini kwangu na kuja moja kwa moja kwako.”<br />
“Una tatizo gani?”<br />
“Tulipomaliza kufurahishana na mpenzi wangu huku nikifurahia mafanikio makubwa baada ya kupona tatizo lake, tulipitiwa na usingizi mzito. Lakini kwa maajabu makubwa nimeamka asubuhi na kujikuta nipo kwangu!”<br />
“Kujikuta kwako kivipi?”<br />
<br />
“Kitandani kwangu nimelala!”<br />
“Sasa kipi cha ajabu?”<br />
“Ina maana hujanielewa?”<br />
“Nimekuelewa! Yaani jana baada ya kukutana na mpenzi wako asubuhi ulipoamka ulijikuta umelala, sasa kipi cha ajabu kama ulilala usiku na asubuhi ukajikuta kitandani?”<br />
<br />
“Hebu nielewe vizuri nisemayo, jana nilikwenda kwa Brighton kama ilivyo kawaida, ninapokwenda hulala huko huko, hata safari yangu ya kuja kazini huianzia kwake.”<br />
“Hilo nalijua, sasa hapo tatizo nini?”<br />
“Jamani huoni tatizo! Nilale kwa Brighton niamke kwenye kitanda nyumbani kwangu tena nikiwa peke yangu.”<br />
<br />
“Suzana! Unayosema ni kweli au ulikuwa unaota?”<br />
“Sharifa, yaani niote mchana na usiku? Sikukupigia simu?”<br />
“Ulinipigia?”<br />
“Saa ngapi?”<br />
<br />
“Mchana”<br />
“Sasa huko kuota gani?”<br />
“Mmh! Basi kama ni kweli usemayo kuna namna lazima tuliangalie kwa macho mawili.”<br />
“Yaani toka nimeamka sijielewi kabisa.”<br />
“Umempigia simu Brighton kumuuliza?”<br />
<br />
“Huwezi amini kila nikipiga simu yake inaonekana anazungumza.”<br />
“Basi kuna umuhimu wa wewe kwenda kwake ili ukapate ukweli, japo mimi bado naamini baada ya kunipigia simu inawezekana kabisa ulipitiwa na usingizi na kuota ulikuwa na Brighton na asubuhi ulipoamka ukajishangaa upo kitandani kwako. Lazima utaamini kabisa umetokewa na kitu kisicho cha kawaida.”<br />
<br />
“Sharifa hiki ninachokueleza ni kweli kabisa si cha kuota, haya ni maajabu.”<br />
“Au ndiyo Jini Balkis?”<br />
“Jini Balkis! Kama ni Balkis, Brighton asingeweza kufanya kazi.”<br />
“Nimekueleza yule jini ana mambo mengi ya kukuchanganya pale unapokaribia kuujua ukweli.”<br />
Suzana anaanza kuingia kwenye mtihani mzito wa Jini Balkis, nini hatima ya yote?</span></div></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dcdde2b63327819">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.18.<br />
<br />
<br />
“Kwa hiyo kuna umuhimu wa kwenda kwa mganga?”<br />
“Ikiwezekana, lakini kwanza nenda kwa mwenzako ili umuulize kama kweli jana mlilala pamoja.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Mmh! Itabidi nifanye hivyo.”<br />
“Asubuhi hii?”<br />
<br />
“Sharifa siwezi kufanya kazi vizuri, akili yangu bado ipo njia panda ukweli wa kitu hiki nitaupata kwa Brighton.”<br />
“Kazi?”<br />
“Lazima niombe ruhusa, nimechanganyikiwa, sijui itakuwaje kama huyo jini atakuwa kanivaa na mimi?”<br />
<br />
“Kama kukuvaa kakuvaa muda mrefu, sasa inawezekana ndiyo anajionesha kwamba na wewe upo kwenye mtandao wake.”<br />
“Mungu wangu! Kama ni hivyo nitakuwa nimekwisha,” Suzana aliingiwa na hofu.<br />
“Suzana acha kujikatia tamaa, hebu tafuta ukweli ili tujue tufanye nini, ikiwezekana twende leo leo, nitaomba ruhusa nikusindikize.”<br />
<br />
“Basi wacha nikaombe ruhusa niende kwa Brighton nikapate ukweli, bila hivyo nitachanganyikiwa.”<br />
“Haya shoga utanijulisha,” Suzana aliagana na Sharifa na kwenda kuomba ruhusa kisha alielekea nyumbani kwa Brighton.<br />
***<br />
Balkis akiwa amejilaza kitandani na Brighton, alimuona Suzana akielekea pale, kama kawaida yake alimueleza mpenzi wake:<br />
“Suzana anakuja.”<br />
“Umejuaje?”<br />
<br />
“Nijue vipi, la muhimu jiandae kumpokea mpenzi wako.”<br />
“Sasa nimpeleke chumba gani?”<br />
“Mlete humu humu.”<br />
“Wewe unatoka?”<br />
“Niende wapi?”<br />
<br />
“Si chumba wa wageni.”<br />
“Mi sitoki, Suzana anakuja kukuuliza kama jana alikuja kulala hapa.”<br />
“Umejuaje?”<br />
“Nisikilize kwanza ndipo uliniulize maswali.”<br />
“Mh!”<br />
<br />
“Naomba unisikilize, ukijichanganya shauri yako.”<br />
“Mbona unaniambia hivyo?”<br />
“Ndiyo maana nakueleza, nisikilize kwa makini.”<br />
“Sawa.”<br />
“Suzana anakuja kuulizia kama kweli jana alikuja hapa, mjibu kuwa hakuja. Tumeelewana?”<br />
“Lakini mbona mimi nafahamu jana alikuja?”<br />
<br />
“Kama alikuja mbona asubuhi hukumuona?”<br />
“Hata mimi nashangaa.”<br />
“Wewe na Suzana mliota ndoto ya aina moja kuwa jana mlikuwa pamoja lakini kila mmoja alipoamka hakumuona mwenzake.”<br />
<br />
“Balkis! Mbona unanitisha, wewe ni nani?”<br />
“Kwani wewe unanionaje?”<br />
“Nakuona mtu wa kawaida, lakini unayozungumza yananishangaza sana.”<br />
“Mbona ya kawaida, ni kipawa ambacho mwanadamu hupewa na Mungu kujua yajayo.”<br />
“Mmh! Nilikufikiria vibaya.”<br />
<br />
“Ulinifikiria vipi?”<br />
“Labda jini!”<br />
“Brighton tokea lini jini akazungumza na mwanadamu?”<br />
“Huwa nasikia majini huweza kujigeuza na kuwa wanadamu na kuishi nao.”<br />
“Kama ningekuwa jini ungefanyaje?”<br />
“Ningekufa kwa mshtuko.”<br />
<br />
Mara kilipita kimya cha ghafla, kitu kilichomshangaza Brighton. Haukupita muda mlango wa chumbani uligongwa.<br />
“Mkaribishe Suzana,” Balkis alimwambia Brighton aliyepatwa na mshtuko.<br />
“Wapi?” Ilikuwa ajabu Balkis alizungumza kwa sauti ya juu, lakini Brighton aliuliza kwa sauti ya kunong’ona.<br />
<br />
“Kuwa muelewa, nimekueleza mkaribishe humu ndani.”<br />
“Ili atufumanie?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Ili iweje?”<br />
“Utajua akiishaingia ndani.”<br />
<br />
Sauti ya kugonga mlango iliendelea nje huku ikionekana kabisa kitendo cha kuchelewa kufunguliwa mlango kilimuudhi sana Suzana.<br />
“Brighton kama hutaki nije kwako si uniambie kuliko kunifanyia visa?”<br />
“Mkaribishe,” Balkis alimueleza Brighton kwa kumkaripia.<br />
“Ingia,” alimkaribisha akiwa na wasiwasi mkubwa.<br />
<br />
Suzana aliingia na kwenda kukaa kitandani, pembeni kabisa ya Balkis. Brighton alikuwa kama mtu aliyeshikwa na ganzi na kushindwa kuelewa kama mpenzi wake ameingia ndani. Suzana baada ya kuingia alimshangaa kwa mara nyingine.<br />
“Brighton upo sawa?”<br />
<br />
“Eeh.... aah.. Unasema?” Brighton alijikuta akibabaika kujibu.<br />
“Makubwa ina maana hujaniona naingia?”<br />
“Nimekuona.”<br />
“Hata kunikaribisha? Kweli mapenzi yamekwisha,” Suzana alizungumza kwa sauti ya kilio.<br />
“Suzana...,” Brighton alipotaka kusema alimtupia jicho Balkis aliyekuwa amejilaza pembeni ya Suzana huku akitabasamu.<br />
<br />
“Brighton, una nini mpenzi wangu?”<br />
“Si..si..sina,” majibu ya Brighton yalizidi kumshangaza Suzana.<br />
“Kuna nini humu ndani, mbona sikuelewi? Jana nilikuja ukawa katika hali hii hii na leo tena, kuna kitu gani mpenzi wangu! Kwa nini hutaki kuniambia?”<br />
“Brighton mkatalie kwamba jana hakuja hapa,” Balkis alimwambia kwa sauti aliyosikia Brighton peke yake.<br />
<br />
“Brighton mbona kama haupo na mimi! Una nini mpenzi wangu?” Suzana aliporomokwa na machozi na kumfuata Brighton alipokuwa amesimama kama kapigwa na shoti ya umeme. Alianza kumpapasa huku akiendelea kumuuliza jinsi alivyoonekana mtu aliyehama kimawazo.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea? Brighton atamsikiliza nani kati ya Suzana na jini Balkis?</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.19.<br />
<br />
<br />
Brighton alikuwa kama yupo ndotoni akijiuliza yanayotokea mbele ya macho yake ni kweli au ni kiini macho. Chumbani kulikuwa na watu watatu, Balkis hakujificha zaidi ya kulala kitandani, tena peupe. Hata Suzana alipoingia, pamoja na kukaa pembeni yake hakuonesha kuona kitu cha tofauti mle ndani.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Alizidi kuingiwa na wasiwasi kuwa huenda Balkis si kiumbe cha kawaida, hata sauti yake aliyompa maelezo bado ilionesha kuisikia peke yake. Kuhama kimawazo kulizidi kumnyima raha mpenzi wake ambaye naye alikuwa na yake yaliyotakiwa kupata majibu kutoka kwa Brighton.<br />
<br />
“Brighton jana nimekuja hapa na kulala na wewe, lakini ajabu nilipoamka asubuhi nimejikuta nipo kitandani kwangu. Ni kweli jana nilikuja au nilikuwa naota?”<br />
“Brighton, kataa! Sema hakuja?” Balkis alipaza sauti ya juu.<br />
Lakini Brighton alijikuta mdomo ukiwa mzito kumjibu mpenzi wake huku jasho la hofu likimtoka.<br />
<br />
“Brighton una nini mpenzi wangu, nijibu basi, si ni wewe ndiyo ulinipigia simu jana na kuniambia nije?”<br />
“Brighton kataaa,” Balkis alizidisha sauti iliyoumiza ngoma za sikio.<br />
“Brighton kuna nini hapo kitandani mbona unapaangalia sana, au kuna mwanamke?”<br />
“Ha..ha..kuna..ki..”<br />
<br />
“Brighton unafanya nini?” Balkis alipiga kelele iliyokuwa na mlio mkubwa kama radi iliyofanya ngoma za sikio za Brighton zisikie maumivu makali.<br />
“Brighton mpenzi wangu una nini au umeshavamiwa na jini Balkis?”<br />
“Nani?” Jina la Balkis lilimshtua.<br />
<br />
Kauli ile ilimuudhi jini Balkis, akapuliza upepo uliompata usoni Suzana ambaye aliishiwa nguvu na kupitiwa na usingizi mzito. Brighton alimuwahi kabla hajaanguka chini na kumlaza kitandani pembeni ya Balkis.<br />
“Suzana... Suzana,” alimwita kwa kumtikisa.<br />
<br />
Suzana hakujibu kitu, alionekana mwenye usingizi mzito. Brighton alimuona Balkis jinsi alivyompuliza hadi kupitiwa na usingizi mzito.<br />
“Balkis umemfanya nini Suzana?”<br />
“Acha upumbavu,” Balkis alimjibu kwa hasira.<br />
<br />
“Balkis mbona sikuelewi?”<br />
“Hunielewi kivipi?”<br />
“Itakuwaje umpulize mtu apoteze fahamu?”<br />
“Nilikwambia nini?”<br />
“Nilikwambia utoke, kwa nini hukutoka?”<br />
<br />
“Mimi ni nani yako?”<br />
“Kwa tabia yako ya miujiza siwezi kukuoa, unaonekana si mtu wa kawaida.”<br />
“Unasemaje?” Kauli ile ilimchefua Balkis.<br />
“Siwezi kukuoa.”<br />
“Kweli?”<br />
<br />
“Kweli,” Brighton alijibu kwa kujiamini.<br />
“Asante.”<br />
Baada ya kusema vile Brighton alishangaa kuona sura ya Balkis ikijikunja na kuwa kama mzee, uzuri wote ulipotea. Wasiwasi ilizidi kumjaa kwa kuamini huenda kweli Balkis si mwanadamu wa kawaida bali ni jini.<br />
<br />
Baada ya kugundua kuwa Balkis si kiumbe wa kawaida, aligeuka ili awahi kuchukua Biblia ili amkemee, hakupiga hata hatua moja, mkono wa Balkis alinyooka na kuwa mrefu, ukamrudisha alipokuwa, kisha alimshika sehemu za siri na kuzivuta kwa nguvu kama anatoa kitu.<br />
<br />
Brighton alihisi kama amepigwa shoti ya umeme sehemu za siri kisha alizisikia zikiwa za baridi kama zimetoka kwenye jokofu. Kwa sauti kali ya hasira Balkis alisema:<br />
“Hutasimamisha milele, na mkeo hatazaa milele.”<br />
<br />
Baada ya kusema vile aliingiza mkono sehemu za siri za Suzana ili amtoe kizazi, kabla hajamtoa Brighton alipiga kelele:<br />
“Hapana, Balkis usifanye hivyo.”<br />
“Lazima niwatie adabu, binadamu gani asiye na shukrani.”<br />
“Nisamehe Balkis nipo tayari kukuoa.”<br />
<br />
“Mpaka kwa shinikizo?”<br />
“Siyo hivyo, mambo yako yananichanganya nashindwa kukuelewa wewe ni mtu wa aina gani?”<br />
“Mimi ni jini?”<br />
“Eeh!” Brighton alishtuka.<br />
“Unashtuka nini, mimi ni jini la chini ya bahari.”<br />
<br />
“Mungu wangu nimekwisha miye.”<br />
”Uishe kivipi, katika muda tuliokuwa wote uligundua tofauti gani kwangu?”<br />
“Sijagundua.”<br />
“Penzi langu na wanadamu wenzio lipi lilikuwa tamu?”<br />
“La kwako.”<br />
<br />
“Mimi na mchumba wako nani mzuri?”<br />
“Wewe.”<br />
“Nani aliyesema kwamba Suzana hafai kuolewa?”<br />
“Mimi.”<br />
<br />
“Nilijitoa kwako ili kurudisha furaha iliyopotea, pamoja na kukubali kunioa bado nilimheshimu mpenzi wako, kosa langu nini?”<br />
“Nisamehe.”<br />
“Nitakusamehe, lakini nakurudishia ugonjwa wako ambao hautapona milele.”<br />
“Nisamehe Balkis nilikuwa sijajua.”<br />
<br />
“Hujajua nini?”<br />
“Hata sijui nilimaanisha nini nimechanganyikiwa Balkis, nisamehe sana.”<br />
“Mimi nakusamehe, lakini nakuacha na matatizo yako na mpenzi wako.”<br />
“Hapana usinifanye hivyo.”<br />
Balkis atamsamehe Brighton?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.20.<br />
<br />
<br />
<br />
“Nimekubali kuendelea kuwa na wewe Balkis usinifanye hivyo,” Brighton alijitetea kwa kupiga magoti mbele ya Balkis.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Kwa nini hutaki kunisikiliza?”<br />
“Nilichanganyikiwa baada ya kukuona ndani, nilijua lazima Suzana atakuona.”<br />
“Nilikueleza mimi ni nani?”<br />
<br />
“Jini.”<br />
“Jini huonekana kwa kupenda, Suzana asingeniona hata mara moja.”<br />
“Ningejuaje bila kuniambia?”<br />
“Kweli kosa ni langu la kutokukueleza mapema, nitakurudishia nguvu zako na leo hii nitaondoka na wewe kwenda kwetu kuishi maisha mazuri.”<br />
“Wapi?”<br />
<br />
“Ujinini,” Balkis alizungumza kwa sauti ya upole huku akijirudisha katika hali yake ya uzuri wa shani.<br />
“Na Suzana?”<br />
“Mwache tu, sitamdhuru, nitamrudisha kwake akiamka atajikuta kitandani amelala.”<br />
Baada ya kusema vile alimkumbatia Brighton na wote walitoweka mle ndani na kutokea pembeni ya bahari maeneo ya Daraja la Salenda.<br />
<br />
“Unanipeleka wapi?”<br />
“Brighton mpenzi acha woga, tunakwenda kwetu chini ya bahari.”<br />
“Si nitakufa na maji?”<br />
“Huwezi, ni sehemu nzuri sana ukifika hutakumbuka kurudi duniani.”<br />
“Nitaishi vipi na majini na mimi ni mwanadamu?”<br />
<br />
“Kama nilivyokueleza majini tupo kama wanadamu wa kawaida na kufanya mambo kama ninyi.”<br />
“Mmh! Sawa.”<br />
Walitembea taratibu kuelekea ndani ya maji, Brighton alikuwa na wasiwasi wa kuzama, wasiwasi wake labda Balkis anataka kumzamisha na kumuua baada ya kuonesha kiburi.<br />
“Balkis usiniue,” alijitetea.<br />
<br />
Balkis badala ya kumjibu alicheka sana, jambo lililozidi kumtisha Brighton, hakusimama aliendelea kusogea mbele katikati ya bahari akiwa bado amemshika mkono. Maji yalimfika magotini, tumboni yakaanza kuelekea kifuani mwishowe yakavuka mabega.<br />
“Balkis naomba unisamehe usiniue kwenye maji.”<br />
“Brighton hakuna mtu anaweza kuitupa shuka yake wakati wa baridi.”<br />
“Una maana gani?”<br />
<br />
“Wewe ndiye shuka langu, siwezi kukupoteza, bora nipotee mimi.”<br />
Wakati huo maji yalikuwa yamewafika chini ya kidevu, Balkis alimshika Brighton kichwani na kumzamisha ndani ya maji kwa nguvu, alitaka kupiga mayowe lakini alikuwa amechelewa. Aliposhtuka alijikuta wametokea kwenye mji mzuri ajabu.<br />
<br />
“Brighton, karibu sana huu ni mji wetu, nawe utaishi kama mfalme, mimi ni mtoto wa Mfalme wa Majini. Baba yangu anaitwa Bashami Hudirud.” <br />
“Asante.”<br />
Walikuja vibaraka weusi kama wanadamu wa kawaida lakini miili yao ilikuwa na nguvu sana. Juu walikuwa vifua wazi na chini walikuwa wamejifunga shuka kama nepi wakiwa wameongozana na vijakazi waliojifunga shuka nyeupe na kuiacha migongo yao nje wakiwa wamebeba maua na farasi weupe wawili waliokuwa wametandikwa matandiko ya dhahabu.<br />
<br />
Vibaraka wenye nguvu walimbeba Brighton na kumketisha juu ya farasi, baada ya kukaa walimbeba Balkis na kumketisha kwenye farasi mwingine aliyekuwa mzuri kuliko aliyembeba Brighton. Baada ya wote kukaa kwenye farasi, safari ilianza kuelekea kwenye jumba la kifahari.<br />
Brighton alipatwa na wasiwasi kukuta mji unaosemwa ni wa majini ni mzuri ajabu na viumbe wake ni watu wa kawaida kama wa duniani. Ila njia nzima hakuna gari wala chombo chochote kinachotumia moto.<br />
<br />
Alikaribishwa ndani huku akipigiwa muziki wa vyombo vitupu lakini ulikuwa mtamu masikioni. Kabla ya kuingia ndani lilitandikwa zulia jekundu ambalo hakuwahi kuwaza kulikanyaga katika maisha yake. Baada ya kuingia ndani alikaribishwa na wasichana wazuri waliovalia magauni meupe yaliyowapendeza, walimwaga maua ya kunukia.<br />
“Brighton karibu kwetu,” Balkis alimkaribisha Brighton kwenye sofa lililotengenezwa kwa manyoya ya kondoo.<br />
<br />
“Asante,” alijibu huku akikaa kwenye sofa lililomfanya ahisi usingizi.<br />
“Jisikie upo nyumbani.”<br />
“Asante, mbona ni tofauti na nilivyofikiria?”<br />
“Kuhusu nini?”<br />
“Nilijua ninyi ni viumbe wa ajabu wenye mikia na meno ya kutisha, mbona ni binadamu kama sisi, kwa nini mnaitwa majini?”<br />
<br />
“Majini ni viumbe wenye uwezo mkubwa wa kufanya jambo lolote tofauti na wanadamu. Lakini nasi tunamuabudu Mungu kama ninyi.”<br />
“Mbona mnaua watu?”<br />
“Unatushangaa kwani hakuna wanadamu wanaoua wenzao?”<br />
“Wapo.”<br />
<br />
“ Mbona mnatushangaa sisi?”<br />
“Lakini nasikia majini hutumika kuwaua watu?”<br />
“Bado hakuna kitu tofauti na wanadamu, kuna wanadamu wachawi mbona hao hamuwazungumzii.”<br />
“Lakini mbona nasikia kuna majini kazi yao ni kuua tu sijui Jini Makata.”<br />
<br />
“Brighton hakuna wanadamu wanaotumwa kuua, hakuna majambazi wanaoua na kuchukua mali zao? Duniani sasa hivi kuna vita, wanadamu wanauana mamia kwa mamia bila sababu, hapo napo kuna majini?”<br />
Swali lile lilimfanya Brighton akose jibu, Balkis aliendelea kuzungumza.<br />
<br />
<span> Je, nini kitaendelea?........TUKUTA</span><wbr></wbr><span class="word_break"></span>NE KESHO KWA MUENDELEZO WA STORY HII.........TUPIA MAONI YAKO HAPA?UMEJIFUNZA NINI?STORY UNAIONAJE? JE HAYA HAYAWEZI KUTOKEA KTK MAISHA HALISI?.....</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a2fe36b94a45633808">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.22<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> sorry ep.21 imefutika....<br />
<br />
IIPOISHIA;<br />
“Ewe mwanadamu, acha kumkosea heshima mtukufu mfalme, kila utakalojibu tanguliza neno mtukufu mfalme.” Mkuu wa watwana alimkumbusha tena Brighton.<br />
“Ndiyo mtukufu mfalme.”<br />
“Vizuri, Balkis.”<br />
“Mtukufu Mfalme.”<br />
<br />
“Unajua sababu ya kukutuma duniani?”<br />
“Ndiyo mtukufu mfalme.”<br />
“Mbona imekuwa kinyume?”<br />
“Mtukufu mfalme nimekwisha kujibu kila kitu.”<br />
“Bado hujanibu.”<br />
<br />
“Unataka jibu gani mtukufu mfalme?”<br />
“Sababu kuu ya kukutuma huko, hujanijibu.”<br />
“Ni kweli mtukufu mfalme shida kubwa ni kuongeza familia yetu.”<br />
“Sasa kwa nini umekaidi amri yangu, nakuomba urudi duniani akaifanye kazi niliyokutuma.” SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Mtukufu mfalme, kupitia huyu mwanadamu nitapata mtoto unayemtaka. Nina imani tatizo lilikuwa damu zetu kukosa virutubisho. Lakini damu ya mwanadamu huwa ina virutubisho vingi.”<br />
“Hatutaki mtoto mchanganyiko.”<br />
“Lakini mtukufu mfalme si atakuwa mwanangu?”<br />
“Sipo tayari kuchanganya damu.”<br />
<br />
“Mtukufu mfalme, nami sipo tayari kumpoteza mpenzi wangu.”<br />
“Tunabishana?” mfalme Barami alikuja juu.<br />
“Baba hatubishani, ila ukweli ni huo.”<br />
“Mwana wa mfalme mwite mtukufu mfalme si baba,” mtwana mkuu, Kulani alimwambia Balkis aliyekuwa amemvunjia heshima baba yake na kusimama wima.<br />
<br />
“Wewe nani unayeingilia mazungumzo na baba yangu? Nani kakupa ruhusa ya kunikemea. Huna heshima, kibaraka mkubwa wee,” Balkis alimfokea mkuu wa watwana.<br />
“Balkis umekosa heshima?” mfalme Barami alimfokea mwanaye.<br />
“Sijakosa baba, natetea haki yangu.”<br />
<br />
“Kulaniiii, wachukueni mkawaweke kwenye chumba cha giza haraka.”<br />
Mfalme Barami alisema kwa sauti ya juu baada ya kumuona mwanaye amemvunjia heshima. Kulani na wenzake waliwabeba juu juu na kwenda kuwafungia katika chumba cha giza.<br />
<br />
****<br />
Suzana alishtuka siku ya pili na kujikuta akiwa amelala kwa mara nyingine kitandani kwake. Alijiuliza kuwa pale kitandani ni kweli au anaota, kumbukumbu zake zilimkumbusha kuwa jana yake alitoka nyumbani na kwenda ofisini na kisha alitoka.<br />
<br />
Breki yake ya kwanza ilikuwa ofisini kwa shoga yake Sharifa na kumuelezea yaliyomsibu baada ya kulala kwa mpenzi wake Brighton, lakini ajabu siku ya pili alijikuta kitandani kwake. Alikumbuka baada ya kumuelezea shoga yake alimpa ushauri kabla ya kufanya lolote aende kwa Brighton kupata ukweli kama ni ndoto au kweli.<br />
<br />
Suzana akiwa bado amekaa kitandani aliendelea kuvuta kumbukumbu ya mambo aliyoyafanya jana yake. Alikumbuka baada ya kushauriana na Sharifa aliaga kazini na kwenda moja kwa moja kwa mpenzi wake. Alipofika Brighton alionesha kubabaika hata majibu yake yalikuwa kama mtu aliyemfumaniwa.<br />
<br />
Baada ya hapo hakumbuki kilichoendelea mpaka alipoamka na kujikuta tena kitandani kwake. Tukio la kujikuta kwake tena wakati anaamini jana asubuhi alikwenda kwa Brighton lilizidi kumchanganya akili.<br />
Kabla hajafanya lolote simu yake iliita alipoangalia ilikuwa ya Sharifa, aliipokea na kuzungumza.<br />
<br />
“Haloo Sharifa.”<br />
“Eeh, Suzy vipi, ndiyo ukaondoka kimoja na simu ukazima. Lakini hiyo ni tabia gani ukiwa na tatizo tuko pamoja likikuishia ananisahau?” Sharifa alilalamika upande wa pili.<br />
“Najua utanilaumu bila kujua.”<br />
“Suzy hata kama ulichokifuata kimekwenda vizuri, kwa vile uliniacha na mimi na maswali ulitakiwa kunijulisha.”<br />
<br />
“Sharifa nashindwa sijui nikuambie nini?”<br />
“Uniambie nini Suzy? Kitendo cha kukosa uungwana kwa kweli siyo kizuri hasa tukiwa watu wa karibu.”<br />
“Kabla sijakuambia kitu naomba nikuulize swali?”<br />
“Uliza tu. ”<br />
<br />
“Ni kweli jana nilikuja ofisini kwako asubuhi?”<br />
“Mbona unaniuliza hivyo?”<br />
“Shoga yangu nina maana kubwa sana ya kukuliza hivyo naomba unijibu usinidanganye.”<br />
“Ni kweli ulikuja.”<br />
<br />
“Si nilikuja kukueleza maajabu yaliyonitokea nilipolala kwa mpenzi wangu na kujikuta kitandani kwangu?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Ni kweli asubuhi sikufanya kazi nilikuaga nakwenda kwa Brighton.”<br />
“Ndiyo.””Basi dada yangu yaliyonitokea juzi kuamkia jana ndiyo aliyonitokea jana kuamkia leo.”<br />
<br />
“Una maana gani kusema hivyo?”<br />
Suzana alimweleza yote aliyokutana nayo na siku ya pili alipoamka na kujikuta kitandani kwake.<br />
“Suzana usiwe unachanganya mambo, pengine ulipotoka hapa badala ya kwenda kwa Brighton ulikwenda kwako ukalala na kupitiwa na usingizi mzito?”<br />
<br />
“Sijafikia huko kiasi cha kupoteza kumbukumbuku hivyo, nilipotoka ofisini nilikwenda moja kwa moja kwa Brighton. Jamani hata kama nilirudi nyumbani asubuhi ile ndiyo nilale nishtuke asubuhi ya siku ya pili?”<br />
“Mmh! Suzana kuna tatizo.”<br />
<br />
“Yaani huwezi kuamini sasa ndiyo inajidhilisha kuwa kuna kitu kinanichezea akili.”<br />
“Kwani Brighton yeye anasemaje?”<br />
“Lazima na yeye atakuwa na tatizo, siku mbili hizi simwelewi kabisa, amekuwa kama mtu aliyechanganyikiwa.”<br />
<br />
“Suzana umezidi ubishi kila kitu nilikueleza, lakini hutaki kuamini wacha yakukute.”<br />
<br />
Suzana yupo njia panda anataka kujua yaliyomzunguka ni kweli au ni ndoto.</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.23<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
<br />
“Tuache masihara, hebu nipelekwe kwa huyo mtaalamu, kilea kidonda mwisho kukatwa mguu.”<br />
“Leo ndiyo unagundua, nilikueleza toka mwanzo kuwa majini wana hadaa inayokuchanganya na mwisho wa siku wanakuingiza sehemu mbaya.”<br />
“Sharifa huu si wakati wa kunilaumu, nahitaji msaada wako la sivyo nitachanganyikiwa.”<br />
“Kama upo tayari, twende pamoja Bagamoyo.”<br />
<br />
”Lini?”<br />
“Leo hii.”<br />
“Saa ngapi?”<br />
“Safari yetu itakuwa saa tatu?”<br />
“Basi shoga tutakuwa wote hali inatisha.”<br />
<br />
Walikubaliana kwenda wote Bagamoyo, baada ya kukata simu Suzana alinyanyuka kitandani ili kujiandaa na safari ya Bagamoyo. <br />
Baada ya maandalizi waliingia kwenye gari kwenda nyumbani kwa Sharifa kumpitia kwenda kwa mganga Bagamoyo. Njiani alijitahidi kumpigia simu Brighton simu yake haikuwa hewani, aliachana naye na kuendelea na safari yake mpaka kwa Sharifa.<br />
<br />
Aliwakuta wameisha jiandaa wakimsubiri, walipomuona tu hawakutaka kupoteza muda.<br />
“Jamani tutatumia magari yote?” Suzana aliuliza.<br />
“Hakuna haja ya kutumia magari yote, moja tu linatosha”<br />
“Hakuna tatizo.”<br />
<br />
Walikubaliana kwenda kwenye usafiri mmoja walipanda kwenye gari la Sharifa na kuelekea Bagamoyo. Walitumia dakika arobaini na tano kufika Bagamoyo, walipofika waliuliza wenyeji sehemu aliyopo mganga Njiwa Manga.<br />
“Samahani kaka,” Sharifa alimuuliza kijana mmoja aliyepita karibu na mlango wa gari lake.<br />
“Bila samahani dada yangu,” kijana yule alijibu huku akisogea karibu.<br />
“Habari za saizi?”<br />
<br />
“Nzuri tu dada.”<br />
“Eti, Njiwa Manga anaishi wapi?”<br />
“Njiwa Manga! Yupi, yule mganga?”<br />
“Eeh, huyo huyo.”<br />
“Unaona hii barabara kubwa?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Ifuateni, acha barabara ndogo mbili zinazokatisha kulia, ya tatu ufuate nenda moja kwa moja mpaka mbele utaona kuna nyumba ina bendera nyekundu hapo hapo kwa mzee Njiwa Manga.”<br />
“Asante,” Sharifa alishukuru huku akimpa elfu mbili.<br />
“Nashukuru dada yangu.”<br />
<br />
Waliachana na yule kijana na kufuata maelekezo yake, walipofika barabara ya tatu inayoingia kulia waliifuata na kwenda mwendo kidogo mpaka kufika kwa mganga Njiwa Manga. Walipaki gari sehemu iliyo salama na kutelemka, ilikuwa sehemu yenye eneo kubwa lililokuwa na nyuma kubwa moja na pembeni kulikuwa na mabanda madogo.<br />
“Karibuni,” binti mmoja aliyekuwa amevalia gauni refu na kitambaa kichwani aliwakaribisha.<br />
“Asante,” waliitikia kwa pamoja.<br />
<br />
“Karibuni kwenye benchi hapo chini ya mti.”<br />
“Asante,” walikwenda wote kukaa chini ya mti kusubiri maelekezo.<br />
Ilipita zaidi ya saa nzima bila kupata maelezo yoyote zaidi ya kukaribishwa kana wageni wengine na kuonesha sehemu ya kukaa.<br />
<br />
“Samahani dada,” Sharifa alimwita yule msichana aliyewakaribisha na kuendelea kuwakaribisha wageni wengine kama watatu, mmoja alikuja na gari na wengine wawili walikuja kwa miguu kuonesha walikuja na usafiri wa daladala.<br />
“Bila samahani,” alisema huku akisogea kuwasikiliza. <br />
“Eti mganga tumemkuta?”<br />
<br />
“Yupo, kama asingekuwepo nisingewaacha mkae mpaka muda wote huu.”<br />
“Kwa hiyo tutaonana naye saa ngapi?”<br />
“Mmh! Sijajua ila si muda mrefu, leo hakuna wagonjwa wengi.”<br />
“Wengine wapo wapi?”<br />
“Wapo ndani, wakipungua nanyi mtaingia.”<br />
<br />
“Haya,” waliachana na yule msichana aliyerudi sehemu yake kusubiri wateja wengine.<br />
Baada ya nusu saa waliitwa ndani, wakati huo ilikuwa imefika saa tatu na nusu asubuhi. Waliongozana wote watatu mpaka kwenye sebule kubwa iliyokuwa imetandikwa zuria bila kiti. Baada ya kuketi msichana aliyewafuata aliingia chumbani na kuwaacha wasubiri.<br />
<br />
Ilipita kama robo saa tena waliitwa ndani, waliingia wote watatu. Chumbani kulikuwa na mzee wa makamo aliyeonekana kula chumvi nyingi kutokana na kuenea mvi sehemu kubwa ya nywele zake. Alionekana ni mtu wadini kutokana na mavazi yake ya kanzu iliyokuwa nyeupe sana na juu alivalia kilemba cheupe. Pembeni yake kulikuwa na msahafu.<br />
“Asalamu aleykum,” mama Sharifa alimsalimia mganga.<br />
<br />
“Waleyku msalamu, karibuni.”<br />
“Asante,” waliitikia kwa pamoja.<br />
“Shikamoo,” Sharifa na Suzana walimwamkia mganga.<br />
“Marahaba mabinti zangu, karibuni.”<br />
“Asante.”<br />
“Haya, mna shida gani?”<br />
<br />
“Kuna vitu vimewatokea mabinti zangu, mpaka sasa vinawachanganya, japo kuna sehemu tulikwenda na kuelezwa tatizo lao, mmoja hakuwepo na mwisho wa yote ilionesha tatizo lile kwa upande wake ni zito hivyo alituelekezwa kuja kwako,” mama Sharifa alitoa maelezo mafupi.<br />
“Mmh, nimekupateni, nipe majina yao.”<br />
<br />
Nini kitaendelea, watapata msaada kwa mganga Njiwa Manga?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.25.<br />
<br />
LIPOISHIA:<br />
“Nina imani mmebahatika kumuona Balkis jinsi alivyo mwanamke mzuri sana, ambaye hakuna mwanaume atakayemtaka akamkataa. Mchumba’ako akaingia kichwa kichwa kumtaka kimapenzi, kana kwamba hana shida na mumeo, alipoonesha dalili za kumtaka alimuuliza maswali ya mitego, kama angekuwa na akili angetambua kuwa yule si mtu wa kawaida. SASA ENDELEA...<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Lakini kutokana na kuchanganyikiwa na mapenzi, hakupata muda wa kujiuliza, Balkis alimuuliza maswali kuhusiana na uhusiano wenu, hakushangaa mtu kuonana naye mara ya kwanza kumuulizia vitu ambavyo hata watu wenu wa karibu hawajui.<br />
<br />
Alipomuulizia kuhusu kumtaka yeye wakati wewe ni mchumba wake, mwenzio alikukana na kusema kuwa wewe ni mpenzi wake si mke wake. Alipoulizwa kama yupo tayari kuoa mwanamke mwingine na kuachana na wewe, kutokana na kiwewe cha mapenzi alikubali kuwa yupo tayari na kuusema udhaifu wako.<br />
<br />
“Alipoulizwa tena yupo tayari kumuoa yeye Balkis alikubali. Aliutumia udhaifu wa mchumba wako kujenga uhusiano wa haraka na kutaka kuwa naye siku ile, pia alikubali. Walikubaliana kwenda nyumbani kwa mchumba wako, ili kutowagonganisha, mchumba wako alitaka kukupigia simu ili usiende, lakini Balkis alimzuia asikupigie simu na kukueleza uende na ulipokwenda ulimuona jinsi alivyobabaika baada ya kuingia na kwenda moja kwa moja chumba cha wageni alichokuwa ameingia Balkis muda ule ule. Ulishtuka baada ya kumuona ameingia ghafla chumbani, ni kweli?”<br />
<br />
“Ni kweli,” Suzana alijibu kwa sauti ya chini huku akiwa anaona muujiza mkubwa kutokana na maneno ya mganga ambayo mwanzo aliyaona kama simulizi ya kusisimua isiyo na ukweli. Lakini swali lile lilikuwa kama kitu kilichomtoa kwenye bumbuwazi.<br />
<br />
“Basi kitendo cha kuingia na kwenda moja kwa moja kilimtia wasiwasi mkubwa mchumba wako kwa kujua lazima utamkuta Balkis na kumfumania. Hata lugha zenu ziligongana kitu kilichokushangaza. Kingine kilichokushangaza kilikuwa kwa mpenzi wako kuwa tofauti na siku zote kukujibu kwa ukali jambo la kawaida.<br />
<br />
Baada ya kumuona humuelewi, ulikwenda chumba cha kulala, yeye alirudi hadi chumba cha wageni na kushangaa kumkuta Balkis akiwa amejaa tele kitandani. Alipotaka kujua alikuwa wapi alimwambia akuwahi chumbani ili akurudishe kwenye hali ya kawaida.<br />
<br />
Baada ya kuingia chumbani, penzi alilokupa ndilo lilikuchanganya na kusahau yaliyotokea muda mfupi. Usiku jini Balkis alikuja kukuchukua ukiwa usingizini na kukurudisha kwako na yeye kulala na mchumba wako mpaka asubuhi. Wote mlipoamka mlishtuka lakini hakuna aliyejua ukweli wa tukio la usiku ni kama ndoto au kweli.<br />
<br />
Ulipokwenda kwake asubuhi ya jana kupata uhakika kwa kilichotokea, ndani walikuwa mchumba wako na Balkis, ndiye aliyemweleza ujio wako. Ulipofika alikuwa mule mule chumbani amelala kitandani. Wewe hukumwona ila mwenzako alimwona kama kawaida, kitu kile ndicho kilichompa kigugumizi.<br />
<br />
Hali ile ilikuchanganya na kumuona kama mtu mwenye matatizo, wakati huo Balkis alimwambia mchumba wako kwa sauti ya juu ya kumkemea kuwa akikuuliza useme hukuja jana ili ujue kilichotokea si kweli bali ni ndoto.<br />
<br />
Lakini kwa yeye kuwepo pembeni ya kitanda karibu na Balkis aliyekuwa amelala pembeni yako bila wewe kumuona, ilizidi kumchanganya.<br />
<br />
Mchumba wako alipatwa na kigugumizi kwa kujua utanamuona Balkis, kubabaika kwake kulikufanya umtilie wasiwasi na kumuuliza swali ambalo lilimchanganya pale ulipotaja jina la Balkis kama jini, jina ambalo lilikuwa la mpenzi wake, kumtaja kama jini ilimuudhi sana Balkis na kukupuliza upepo uliokufanya upoteze fahamu.<br />
<br />
Kitendo kile mchumba wako alikiona na kumpandishia na kutaka kujua amekufanyia nini, Kauli ile ilimfanya Balkis kukasirika na kuondoa nguvu za kiume za mchumba wako na kutaka nawe kukutoa kizazi.”<br />
<br />
“Mama yangu!” Suzana alishtuka na kushika mdomo kusikia vile.<br />
“Usiogope, hakukutoa kizazi baada ya mchumba wako kumuomba msamaha na kuwa tayari kumuoa baada ya kumkataa kutokana na vitendo vyake visivyo vya kawaida. Baada ya Balkis kumsamehe aliamua kuondoka naye kwenda kuishi chini ya bahari.”<br />
<br />
“Mamaaa!” Suzana alipiga mayowe ya mshtuko.<br />
“Mungu wangu unataka kutuambia Brighton yupo ujinini?” Mama Sharifa aliuliza.<br />
“Ndiyo, lakini kwa sasa yupo katika matatizo.”<br />
“Matatizo! Matatizo gani tena jamani?” Suzana aliuliza kwa huzuni.<br />
<br />
“Baada ya kufika katika mji wa majini, baba mzazi wa Balkis alishtuka kuona mwanaye amekwenda na mwanadamu akimsema ndiye mume wake badala kupeleka alichotumwa.<br />
Hapo palitokea kutoelewana kati ya Balkis na baba yake, baba akitaka mwanaye arudi duniani kuendelea kutafuta vizazi zaidi vya wanawake ili apate dawa ya kuweza kupata ujauzito ili aolewe na jini mwenzake.<br />
<br />
Lakini Balkis hakuwa tayari kuolewa na jini mwenzake baada ya kuonja penzi la mwanadamu. Yeye aliamini kuolewa na mwanadamu kusingekuwa na haja ya kuendelea kuwatoa uzazi wanawake. Kwani angekutana kimwili na mwanadamu angeweza kupata bila kutumia dawa hiyo.<br />
<br />
Hapo ndipo palipozuka mvutano wa mtoto na baba, Balkis aliamini kwa vile anapendwa sana na baba yake atakubaliwa, lakini baba yake hakuwa tayari kuchanganya damu ya jini na mwanadamu. Baada ya kuona mtoto wake amemkosea adabu, alimuamuru mkuu wa Watwana anaitwa Kulani, Jini mweusi lakini mwenye nguvu. Kumchukua Balkis na mchumba wako kuwapeleka katika chumba cha giza.”<br />
<br />
“Kwa hiyo ndiyo harudi tena?” Suzana aliuliza.<br />
“Anaweza kurudi lakini mpaka atoke sehemu aliyofungwa.”<br />
“Bila ya hivyo hawezi kutoka?” Sharifa aliuliza.<br />
<br />
“Inategemea na uamuzi wa mfalme wa bahari kumtoa.”<br />
Mambo yanazidi kuwa mazito. Je, Brighton atapona au atauawa katika mji wa majini? Mganga njiwa Manga atawasaidia?</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468dc0a9f23064361"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.28.<br />
<br />
<br />
Ilipoishia:<br />
“Bila ya hivyo hawezi kutoka?” Sharifa aliuliza.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Inategemea na uamuzi wa mfalme wa bahari kumtoa.”Sasa endelea:<br />
<br />
<br />
“Hawezi kumuua?” Suzana aliuliza kwa sauti ya kukata tamaa.<br />
“Hawezi, nina imani atatoka tu, kinachotakiwa ni kuvuta subira.”<br />
“Mmh! Na mimi tatizo langu?” Sharifa aliuliza.<br />
<br />
“Wewe tatizo lako limepata bahati moja kubwa ambayo sawa na bahati ya mtende.”<br />
“Bahati gani?” Sharifa aliuliza huku akijiweka sawa.<br />
“Kitendo cha kufungiwa Balkis katika chumba cha giza, kimewawezesha kuja huku bila ya matatizo.<br />
“Una maana gani?” Sharifa aliuliza.<br />
<br />
“ Majini ni viumbe wasiokubali kuona wanavurugiwa mipango yao, Balkis kama angekuwa hajafungiwa lazima angeizuia safari yenu.”<br />
“Angeizuia kivipi?”<br />
“Mngekutana na vitu vya ajabu njiani hata kupinduka na gari lenu.”<br />
“Si tungekufa?”<br />
<br />
“Msingekufa, mngeumia tu ili msiweze kumfuatilia.”<br />
“Na bahati nyingine?”<br />
“Bahati nyingine wakati wa kufanya dawa ya kurudisha kizazi chako hakutakuwa na upinzani wowote. Wala kazi yako haitahitaji vitu vingi vya kufanya na itaanza leo saa sita za usiku baharini.”<br />
“Kama angekuwepo?”<br />
<br />
“Mmh! Pangechimbika, waganga wengi wamepoteza maisha kwa ajili ya kutaka kuvuruga mipango ya majini. Pia tungehitaji vitu vya gharama ili kumdhibiti hapo kazi ingetakiwa kufanyika saa nane za usiku baharini katika maji ya shingo.”<br />
“Mmh! Sasa akitoka si ataweza kutuua?”<br />
<br />
“Balkis ni jini lenye huruma sana, katika maisha yake hapendi kufanya vitu vibaya, hata kuolewa ilikuwa ni shinikizo la wazazi wake tu ambao walimlazimisha kutafuta vizazi vya wanawake ili aweze kupata tiba ya matatizo yake ya kushindwa kupata ujauzito.<br />
<br />
“Mwanzoni alikataa katakata lakini aliahidiwa kupewa zawadi kubwa kama atapata mtoto hasa wa kiume. Alikubali kuifanya kazi ile kwa shingo upande, lakini moyoni mwake hakupenda hata siku moja kutenda kitendo chochote kibaya kwa wanadamu, siku zote aliwaza kuishi duniani na kuolewa na binadamu.<br />
<br />
“Hata kazi ya kutoa vizazi ilimchukua muda mrefu sana, kitu kilichowafanya wazazi wake kumleta duniani moja kwa moja ili aweze kupata vizazi hivyo kwa muda mfupi, bila kujua Balkis hakupenda kuifanya kazi ile.<br />
<br />
“Siku Suzana alipoona sherehe ya ajabu juu ya bahari, hiyo ndiyo ilikuwa siku rasmi ya kuja duniani kwa Balkis kusaka vizazi vya wanawake na kuvipeleka baharini. Aliandaliwa jini mwingine ambaye kazi yake ilikuwa ni kuvipokea vizazi hivyo juu ya bahari katika eneo lile la Daraja la Salenda na kuvipeleka kwenye stoo chini ya bahari.<br />
<br />
“Lakini ilikuwa tofauti na walivyotegemea wazazi wake, tangu Balkis alipofika rasmi duniani kwa kazi hiyo, kwa siku moja alipeleka vizazi vinne tu na chako kikiwa kimojawapo.<br />
Kazi aliyotumwa alisahau baada ya kuvutiwa na uzuri wa mchumba wa Suzana na kujikuta akianzisha uhusiano wa siri bila mwenzako kujua.<br />
<br />
“Katika harakati za kuhakikisha anamdhibiti mchumba wako, muda mwingi aliutumia kuhakikisha anamchukua jumla badala ya kuifanya kazi aliyotumwa.<br />
“Aliweza kuwagonganisha kwa kuziua nguvu za kiume za mchumba wako na usiku ulipoingia alizirudisha ili afaidi yeye.<br />
<br />
“Hali ile ndiyo iliyowasukuma kutafuta suruhu ya tatizo lenu, alipoona mmeanza kupata mwanga aliwachanganyeni kwa kuzirudisha kitu kilichokufanya uone kama hakuna tatizo.Balkis alipofanikiwa kumnasa mchumba wako kwenye mtego wake, hakupanga kuondoka naye mapema.<br />
“Mngeendelea kushea mapenzi bila wewe kujua mpaka angeshika ujauzito.<br />
“Kosa alilolifanya mchumba wako ni kwenda kinyume na yale aliyokuwa akielekezwa na Balkis.<br />
<br />
“Kubabaika kwake kulipelekea wewe kuingia wasiwasi na kutamka neno lililomchukiza Balkis na kukupulizia hewa iliyokupoteza fahamu.<br />
Hali ile ilimfanya Balkis aone mpango wake umeharibika mapema, ili asiweze kumpoteza mpenzi wako aliamua kuondoka naye kwenda chini ya bahari.<br />
<br />
“Kutokana na huruma yake aliamini kama ataolewa na binadamu atakuwa ameokoa tatizo la wanawake kutolewa vizazi. Lakini ilikuwa tofauti na walivyotegemea wazazi wake ambao wao walimtuma kuishi duniani ili kufanikisha kupatikana kwa vizazi vingi vya mwanamke vitakavyomuwezesha kupata dawa ya kushika ujauzito ili aolewe na jini mwenzake.<br />
<br />
“Walishangaa kumuona akiwa na mwanaume wa kibinadamu na kumtambulisha kwao kama ni mume wake. Kitendo kile kiliwaudhi sana, naye hakutaka kukubali.Baada ya mvutano Balkis na mchumba wako waliwekwa kwenye chumba cha giza.”<br />
“Sasa kama unasema wazazi wake hawakukubali wataweza kumtoa salama Brighton?” Suzana aliuliza.<br />
<br />
“Hapa inaonesha maisha yake yapo zaidi ya hapo, Kwa hiyo hawezi kuuawa.”<br />
“Kama umeona anaweza kuendelea kuishi, itakuwa wapi duniani au kuendelea kufungwa kwenye chumba cha kiza?” Suzana alikuwa na shauku kutaka kujua hatma ya mchumba wake.<br />
“Kwa kweli haioneshi ataishi wapi ila kuna maisha marefu ya mchumba wako.”<br />
“Vipi kuhusu kazi yangu ya kurudisha kizazi kuna vitu vinatakiwa kwenda kununua?” Sharifa aliuliza. <br />
<br />
“Anatakiwa njiwa mwekundu tu, kwenye mabanda yangu anapatikana.”<br />
“Na mimi kumpata mchumba wangu utanisaidiaje?”</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.27<br />
<br />
LIPOISHIA;<br />
“Sasa kama unasema wazazi wake hawakukubali wataweza kumtoa salama Brighton?” Suzana aliuliza.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Hapa inaonesha maisha yake yapo zaidi ya hapo, kwa hiyo inamaanisha hawezi kuuawa.”<br />
“Kama umeona anaweza kuendelea kuishi, itakuwa wapi duniani au kuendelea kufungwa kwenye chumba cha giza?” Suzana alikuwa na shauku kujua hatima ya mchumba wake.<br />
<br />
“Kwa kweli haioneshi ataishi wapi ila kuna maisha marefu ya mchumba wako.”<br />
“Na kuhusu kazi yangu ya kurudisha kizazi kuna vitu vinatakiwa kwenda kununua?” Sharifa aliuliza. <br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Anatakiwa njiwa mwekundu tu, kwenye mabanda yangu atapatikana.”<br />
“Na mimi kumpata mchumba wangu utanisaidiaje?”<br />
“Kama akitoka kwenye chumba cha giza tutampata, lakini kumtoa kule ni kazi ngumu, haonekani kila nikimtafuta.”<br />
<br />
“Kwa hiyo utanisaidia vipi?”<br />
“Kwa vile kazi ya mwenzako ni nyepesi ngoja tuifanye usiku wa leo, ya kwako itabidi nichimbe sana kuona kama kuna uwezekano wa kumtoa hata akiwa chumba cha giza.”<br />
Walikubaliana kuifanya kazi ile usiku wa siku ile, mganga aliwaruhusu wakapate chakula na kupumzika ili kuvuta muda. <br />
***<br />
Majira ya saa sita usiku Sharifa alisimamisha gari lake pembeni kabisa na bahari maeneo ya pwani ya Bagamoyo, sehemu aliyoelekezwa na Mganga Njiwa Manga. Hali ya hewa ilikuwa giza la wastani, kwa mbali ilionekana miale ya moto ya wavuvi wa usiku.<br />
Baada ya kusimamisha gari hakuteremka walisubiri maelekezo ya mganga. Mganga Njiwa Manga alianza kuteremka kisha aliwaita, wote walitoka nje ya gari.<br />
<br />
Baridi la ufukweni lilikuwa kali, kila aliyekuwepo pale lilimchonyota hadi kwenye mifupa. Mganga alitoa vifaa vya kufanyia kazi, njiwa wa kazi alikuwa ameshikiliwa na Sharifa.<br />
<br />
Wote walikuwa kimya wakimsikiliza mganga ambaye alikuwa akitembea kuelekea baharini, mawimbi muda ule hayakuwa makali sana yalipiga taratibu. Mganga aliingia majini usawa wa maji ya mafuti na kumwaga vitu huku akizungumza maneno kwa sauti ya juu.<br />
“Ewe jini la bahari nakuletea zawadi hii ili bahari iwe tulivu, pia nimekuletea zawadi ya njiwa ili kuniruhusu niifanye kazi yangu bila kikwazo.”<br />
<br />
Baada ya kusema vile aligeuka bila kutoka ndani ya maji na kumwita Sharifa.<br />
“Kavue nguo zote kisha ujifunge upande wa kanga halafu uingie ndani ya maji na njiwa wako.” <br />
<br />
Sharifa alifanya kama alivyoelekezwa na mganga, aliingia ndani ya maji na kuwaacha mama yake na Suzana wakiwa wamesimama huku wakiendelea kupigwa na baridi kali ya upepo utokao baharini. Aliingia ndani ya maji ya baridi huku akiwa na hofu ya kutojua mganga anataka kumfanya nini hasa akiwa amejifunga upande wa kanga bila kitu chochote mwilini.<br />
<br />
Alipomfikia mganga alisogea naye mbele hadi maji ya shingo njiwa wake akiwa amemnyanyua juu. Baada ya kufika kimo kile cha maji, mganga alimwambia Sharifa amuweke kichwani, naye alifanya vile. Mganga alimshika sikio la kushoto na kuanza kuomba kwa lugha ya kiganga.<br />
<br />
Aliomba kwa kuzungumza maneno haraka haraka bila kumeza mate kwa zaidi ya nusu saa. Baada ya robo saa Sharifa alianza kusikia vitu vikikoroga tumboni, Sharifa alishindwa kufanya kitu kutokana na mikono kuwa kichwani amemshikilia njiwa.<br />
<br />
Mganga aliendelea kuzungumza maneno ya kiganga akiwa bado amemshikilia sikio, tumbo nalo liliendelea kumkoroga huku mwili ukizidi kupungua nguvu. Mara alianza kuona kiza mbele na kuangukia ndani ya maji na njiwa wake mkononi.<br />
<br />
Mganga aliwahi kumdaka na kujitahidi kumsimamisha lakini miguu haikuwa na nguvu, alipiga kelele kuomba msaada kwa mama Sharifa na Suzana waliokuwa nje ya maji. Nao walijikuta wakiingia kwenye maji na nguo zao bila kujijua kuwahi kutoa msaada kwa mganga.<br />
<br />
Walipofika ndani ya maji ya shingo walimsaidia mganga kumsogeza ufukweni, walipofika ilionesha kama Sharifa amepoteza fahamu.<br />
“Mganga mbona hivi?” Mama Sharifa aliuliza.<br />
“Ni kawaida kuna kitu kilikuwa mwilini mwake kimetoka lakini baada ya muda atakuwa katika hali ya kawaida.”<br />
<br />
Pamoja na Sharifa kupoteza fahamu mganga aliwaomba wambebe hadi ndani ya maji ili aendelee na tiba yake.<br />
“Sasa baba si unamuona alivyo kwa nini tusisubiri arudiwe na fahamu kisha uendelee na tiba?” Mama Sharifa aliuliza akiwa amejawa na wasiwasi juu ya hali ya mwanaye.<br />
“Mama unanifundisha kazi?” Mganga alimuuliza kwa sauti ya ukali.<br />
“Samahani baba.”<br />
<br />
“Sipendi kufundishwa kazi kama ulikuwa unajua kwa nini mlimleta kwangu?”<br />
“Nisamehe baba yangu.”<br />
“Basi naomba kila utakachokiona hapa ukae kimya.”<br />
“Nimekuelewa baba yangu nisamehe sana.”<br />
“Haya mbebeni muda unakwenda.”<br />
<br />
Mama Sharifa na Suzana walimbeba Sharifa mpaka maji ya chini ya mafuti mganga alimuomba Suzana akae chini ili ampakate mgonjwa. Suzana alifanya kama alivyoelezwa na mganga kisha Sharifa alilazwa chali juu ya Suzana. Mama yake alimshika sehemu ya kichwani ili kisiingie kwenye maji. Baada ya kulazwa mganga aliendelea na tiba yake kwa kuendelea kusema maneno ya kiganga kwa zaidi ya nusu saa. Huku njiwa aliyekuwa amelowana akimshikilia kwenye tumbo la Sharifa.<br />
<br />
Baada ya muda mganga alinyamaza ghafla na kupita kimya kizito kikifuatiwa na upepo mkali. Baada ya muda upepo ulikoma. Suzana na mama Sharifa kila mmoja aliingiwa na wasiwasi kutokana na hali iliyojitokeza mle baharini. Kila moja alimuomba Mungu kimoyomoyo.<br />
<br />
Baada ya upepo kutulia ilisikika sauti ya Sharifa ikiita.<br />
“Mama...mama...mama.”<br />
Mama Sharifa hakuitikia alimuangalia mganga aliyekuwa bado akitazama upepo ulipotokea na kunyanyua mkono.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468b8652878498329">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.29.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
“Nipo mimi” Suzana alijibu.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Haya fanyeni haraka mkimaliza mniite.”<br />
Walimbeba Sharifa ambaye hakuwa na nguvu hadi ndani ya gari na kumbadili nguo zake kisha walimwita mganga ili waondoke kurudi nyumbani.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
Mganga aliingia kwenye gari, Suzana aliliendesha mpaka nyumbani kwa mganga, walipofika walimteremsha Sharifa ambaye alitembea kwa tabu. Walipomfikisha sebuleni walimlaza kwenye mkeka na kumsuburi mganga aliyekuwa amemshika njiwa aliyekuwa tayari ameshamchinja tangu baharini.<br />
<br />
Mganga alimwomba mkewe awape nguo za kujifunga wateja wale kutokana na nguo zao kulowana na maji ya bahari walipokuwa wakimtoa Sharifa kwenye maji. Baada ya kubadili nguo alimpa mkewe yule njiwa na kumweleza amnyonyoe na kumchemsha. Mkewe alimchukua na kuondoka naye na kuwaacha kina Suzana sebuleni.<br />
<br />
Majira ya saa kumi za usiku mganga alimwamsha Sharifa na kumpa dawa ya njiwa aliyechemshwa kwa ajili ya kumla akiwa katika sufuria ile ile aliyochemshiwa.<br />
“Mle njiwa wote na unywe na supu yake,” mganga alimwambia Sharifa ambaye bado mwili wake ulikuwa hauna nguvu.<br />
<br />
Sharifa alianza kumla njiwa na kunywa supu yake kwa shida kwa vile alichemshwa bila kuwekwa chumvi, alipomuona kama anamshindwa kutokana na kutokuwa na kiungo hicho aliuliza.<br />
<br />
“Mbona hana chumvi?”<br />
“Huyo hawekwi chumvi, jitahidi umle vivyo hivyo, tena una bahati njiwa ni mdogo, watu wanakula kuku mzima bila chumvi.”<br />
<br />
Sharifa hakuongeza neno alimuinamia njiwa wake na kuendelea kumla taratibu mpaka alipommaliza, wakati huo Suzana na mama yake walikuwa wakikoroma. Baada ya kumaliza kumla njiwa aliruhusiwa kuendelea kulala na wenzake ambao walikuwa hawajitambui kwa usingizi.<br />
<br />
Wote waliamshwa alfajiri kwa ajili ya tiba ya mwisho ya kuoga maji ya bomba yaliyochanganywa na yale ya baharini. Baada ya kuoga waliingia kwenye chumba cha mganga kwa ajili ya mazungumzo ya mwisho kabla ya kuruhusiwa kwenda nyumbani.<br />
<br />
Wote walikaa kwenye mkeka baada ya mganga kutulia kwa muda huku akipitia maelezo kwenye karatasi nyeupe iliyoandikwa kwa wino mwekundu kisha alisema kwa sauti ya chini:<br />
“Nina imani kazi yetu imekwenda vizuri sana tofauti na nilivyofikiria, shughuli kama hii niliifanya siku za nyuma kwa muda wa wiki nzima, tena nikiwa na majeraha mengi kutokana na kushindana na jini.”<br />
<br />
“Unataka kuniambia nimepona?” Sharifa aliuliza.<br />
“Umepona.”<br />
“Kwa hiyo nina uwezo wa kushika mimba?”<br />
“Bila shaka.”<br />
<br />
“Nashukuru sana mzee wangu,” Sharifa alinyanyuka kwa lengo la kumpigia magoti.<br />
“Hapana mama kaa tu, wakushukuriwa ni Mungu yeye ndiye mwenye kukubali au kukataa maombi yetu.”<br />
<br />
“Ina maana kama Balkis angekuwa hakufungwa kazi isingeisha leo?” Suzana aliuliza.<br />
“Kazi ya kushindana na majini ni ngumu msione imekwenda kirahisi kiasi kile, kama Balkis angekuwa hajafungwa vita ingekuwa kubwa asingekubali tuchukue kizazi katika stoo yake. Lazima ingetakiwa niwe na vijana wangu wa kazi na katika kumdhibiti wangetakiwa mbuzi wekundu wawili, shuka nyekundu mbili na vitu vingine vingi.”<br />
<br />
“Kutokana na kauli za mganga wa awali kuwa matatizo mengi ya tumbo yanatokana na jini Balkis kuchukua vizazi vya wanawake, lakini mbona ni wanawake wengi wana matatizo tofauti na idadi ya vizazi vilivyoko kwenye stoo ya Balkis?” Sharifa aliuliza.<br />
<br />
“Kama nilivyowaeleza majini wanaishi kama wanadam, jinsi matatizo yetu yanavyofanana basi na ya majini huwa ni vivyo hivyo. Majini wengi wenye matatizo ya kukosa uzazi hutumwa duniani kuifanya kazi kama ya Balkis, hivyo vita si vyake peke yake ni kwa majini wengi.”<br />
<br />
“Mungu wangu sasa tutapona vipi?” Suzana aliuliza.<br />
“Kupona inategemea na wewe kuonana na watu wenye uwezo kama sisi au kusimama katika imani yako.”<br />
“Kusimama kwenye imani una maana gani?” Sharifa aliuliza.<br />
<br />
“Kila anayesimama katika imani humtanguliza Mwenyezi Mungu mbele kwa kila jambo, kabla ya kulala huomba ulinzi wake na baada ya kuamka humshukuru kwa kumvusha usiku salama, kisha humuomba tena amlinde na mchana wote.”<br />
“Mbona tunafanya hivyo?” Alisema Suzana.<br />
<br />
“Unaweza kuwa unafanya kutimiza wajibu wa maombi lakini imani yako si kamili, siku zote imani husimama kwa matendo siyo kwa maneno.”<br />
“Unataka kuniambia aliyesimama kwa imani ya matendo mema hawezi kupatwa na tatizo hili?’<br />
<br />
“Litaingilia vipi wakati Mungu ndiye mlinzi wake, hata hao majini wanamuogopa na kumuabudu yeye.”<br />
“Kutokana na maelezo yako sasa hivi nimepona kabisa?” Sharifa aliuliza.<br />
“Umepona na wala haitakutokea tena.”<br />
“Kwa mfano Balkis akitoka gerezani, akijua nimerudishiwa kizazi changu si litakuwa tatizo?”<br />
<br />
“Tatizo litabakia kwake, wewe utakuwa salama kuanzia asubuhi hii.”<br />
“Ile hali ya tumbo kuvurugika nilipokuwa pale baharini ilitokana na nini?”<br />
“Kizazi chako kilikuwa kikirudi sehemu yake.”<br />
<br />
“Baba tunashukuru kwa msaada wako,” mama Sharifa alisema kwa niaba ya mwanaye.<br />
Nini kiliendelea?</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468b06e3d20048028">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.30.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
Uso wake ulionesha huzuni kitu kilichomtisha mumewe ambaye alitaka kujua kulikoni.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Vipi mahabuba wangu?”<br />
“Mambo yameharibika.”<br />
“Kivipi?”<br />
<br />
“Mpango wetu umeingia kwenye mtihani wa kwanza.”<br />
“Mtihani upi?”<br />
“Kizazi kimoja kimechukuliwa.”<br />
“Tufanye haraka kabla hakijarudishwa kwa mwenyewe tumtume Kulani akaifanye kazi hii kabla hakujapambazuka.”<br />
<br />
“Tumechelewa tayari kimeisharudishwa kwa mwenyewe.”<br />
“Umejuaje?”<br />
“Damu ya sehemu kilipotoka nilipoigusa imeganda kidoleni.”<br />
<br />
“Ooh! Nani anataka kuchezea himaya yangu lazima nimkomeshe,” Mfalme Barami Hudirud alisema kwa hasira.<br />
“Hebu kaniletee damu ya sehemu iliyotoka kizazi ili nimjue ni nani?”<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
Malkia Huleiya alikwenda hadi kwenye chumba cha siri na kurudi na damu ya sehemu iliyochukuliwa kizazi cha Sharifa na kumpelekea mumewe.<br />
“Naomba niilambe.”<br />
Malkia Huleiya alimlambisha mumewe, mfalme alitulia kwa muda kisha alisema:<br />
“Nimeishamjua, nitamtuma Kulani akishindwa nitakwenda mwenyewe.<br />
<br />
Lazima nitamuonesha mimi ni nani.”<br />
“Umemgundua ni nani?”<br />
“Kuna mshenzi mmoja anataka kushindana na nguvu zangu, nataka mpaka kutakapopambazuka awe amebakia jina.”<br />
<br />
“Kulaniiiiii,” aliitaka kwa sauti ya juu ambayo kama mwanadamu angeisikia basi angepasuka ngoma za masikio.<br />
Kulani aliyekuwa mbali alikuja mbio na kupiga magoti mbele ya mfalme.<br />
“Rabeka mtukufu mfalme.”<br />
“Nataka uende duniani, damu hii itakuongoza mpaka kwa mtu huyu, nataka umfutilie mbali, sawa?”<br />
<br />
“Sawa mtukufu mfalme.”<br />
“Haya ondoka mbele yangu, usirudi mpaka umemfutilia mbali kiumbe huyo dhaifu anayetaka kucheza na nguvu zangu.”<br />
Kulani alizama chini ya ardhi na kutoweka, baada ya muda alikuwa pembeni ya bahari eneo la Bagamoyo, aliilamba damu aliyopakwa kidoleni ambayo ilimuelekeza aende upande upi. Alitoka eneo baharini na kuelekea kwa Mganga Njiwa Manga.<br />
<br />
Alitembea taratibu toka eneo la bahari akiwa katika umbile la kibinadamu, hakuchelewa kufika kwenye makazi ya watu. Aliilamba tena ile damu iliyokuwepo kidoleni mwake, kwa vile kulikuwa na giza, sehemu ya Mganga Njiwa Manga ikawaka mwanga wa taa.<br />
<br />
Mwanga ule ulimuongoza hadi karibu kabisa na nyumba ya Mganga Njiwa Manga. Nia yake kubwa ilikuwa kwenda mpaka mlangoni na kugonga ili akifungua tu wakutane uso kwa uso na ammalize pale pale kisha aondoke kabla hakujapambazuka.<br />
<br />
Alitembea kuelekea eneo la nyumba ya mganga, ajabu alipokaribia nyumba yake alishangaa kuona moto ukiwaka kuizunguka nyumba ile. Hali ile ilimshtua sana, aligeuka na kutimua mbio hadi baharini ambako alikunywa maji mengi na kurudi hadi kwenye eneo la nyumba ya mganga.<br />
<br />
Alipoikaribia moto uliwaka tena, alilisogelea eneo la nyumba huku akimwaga maji aliyoyachukua baharini kwa lengo la kuuzima moto ule. Alifanikiwa lakini alipotaka kuingia kwenye himaya ile moto uliwaka tena. Alijikuta akifanya kazi ya kwenda baharini na kurudi, kila alipouzima moto na alipotaka kuingia uliwaka tena.<br />
<br />
Kulani alijikuta akitumia muda mwingi kwenda baharini kuchukua maji na kurudi huku moto ukizimika na kuwaka. Mpaka kulipokuwa kunakaribia kupambazuka hakuweza kuingia katika himaya ya Mganga Njiwa Manga. Kwa upande wake aliiona kazi imekuwa ngumu au maji yalikuwa marefu na kuamua kurudi chini ya bahari, aliogopa kutokana na kauli aliyopewa na Mfalme Barami Hudirud kuwa asirudi chini ya maji mpaka ahakikishe amemmaliza Mganga Njiwa Manga.<br />
<br />
Kulani alijikuta kwenye wakati mgumu katika kazi ile, tofauti na zilizotangulia ambazo alizifanya kwa muda mchache. Lakini ile ilikuwa ngumu kwake, baada ya kukutana na kikwazo cha moto.<br />
Aliamua kurudi hadi baharini akiwa katika umbile lile la kibinaadamu, alisubiri jua litochomoze ili aweze kwenda jirani kwa mganga na kumsuburi akitoka ammalize.<br />
<br />
Jua lilipotoka na watu kuwa wengi kujaa ufukweni kwa ajili ya kununua samaki na wengine wakipanda ngarawa kwenda kuvua.<br />
Kulani alijichanganya na watu bila ya kujulikana kama ni jini. Baada ya pwani kuchanganya na watu kuongezeka, alijitoa eneo la bahari na kwenda kwa mganga kwa kutembea kama mtu wa kawaida.<br />
<br />
Kila aliyemuona hakumdhania vibaya, aliacha eneo la bahari na kuingia makazi ya watu, alipokaribia maeneo ya nyumba ya mganga aliuona moto ukiwaka tena. Alikwenda kwenye nyumba ya jirani na kuomba kupumzika, kutokana na kuonekana kama mstaarabu, alikaribishwa na kupewa kiti. Mwenyeji wake hakujishughulisha naye aliendelea na shughuli zake na kumuacha Kulani akitupia jicho njia ya kutokea kwa Mganga Njiwa Manga.<br />
Jini Kulani ataweza kutimiza azma yake ya kumuua Mganga Njiwa Manga?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468a7d82f70631904">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.31<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
Kila aliyemuona hakumdhania vibaya, aliacha eneo la bahari na kuingia makazi ya watu, alipokaribia maeneo ya nyumba ya mganga aliuona moto ukiwaka tena. Alikwenda kwenye nyumba ya jirani na kuomba kupumzika, kutokana na kuonekana mstaarabu alikaribishwa na kupewa kiti. Mwenyeji wake hakujishughulisha naye aliendelea na shughuli zake na kumuacha K<span class="text_exposed_show">ulani akitupia jicho njia ya kutokea kwa Mganga Njiwa Manga.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
Muda ulikwenda bila mganga kuonekana, kila alipopata wazo la kwenda kwenye nyumba ile alishangaa kuuona moto ukiwaka, lakini ulipotulia nyumba ilikuwa katika hali ya kawaida. Alijikuta yupo kwenye wakati mgumu akiamini kabisa ngoma ile ni nzito kwake kuchezeka.<br />
<br />
Kilichomchanganya zaidi ilikuwa ni kauli ya mfalme Barami Hudirud ya kuhakikisha anammaliza mganga ndipo arudi, japo muda aliopewa ulipita.<br />
Kulani alipata pigo baada ya mwenyeji wake kutaka kuondoka, akiwa bado kichwa kinamuuma alimwambia:<br />
<br />
“Samahani kaka.”<br />
“Bila samahani.”<br />
“Nataka kuondoka kwenda pwani.”<br />
“Hakuna tatizo funga mlango wako mimi niache hapa nimekaa baada ya muda nitaondoka.”<br />
“Hapana kaka sikujui nimekukaribisha kibinadamu, lakini siwezi kukuamini kukuachia nyumba yangu, dunia haiaminiki siku hizi.”<br />
<br />
“Sawa.”<br />
Kulani alikubali kuondoka pale, lakini sehemu iliyokuwa nzuri kupaona kwa mganga ilikuwa kwenye nyumba ile iliyokuwa ikitazamana na ya mganga. Aliondoka kwa kuzunguka nyumba ile na kujigeuza haraka kuwa mjusi. Aliupanda ukuta haraka na kwenda kujificha chini ya bati bila kuonekana.<br />
<br />
Mwenye nyumba ile alishtuka na kuzunguka nyuma ili kupata uhakika kama kweli yule mgeni atakuwa ameondoka. Lakini ajabu alipozunguka nyuma ya nyumba iliyokuwa na uwazi mkubwa wa kumuona mtu kama anatembea kutoka pale, hakumuona mgeni wake. Alijiuliza kwa sauti:<br />
<br />
“Sasa atakuwa amekwenda wapi, mtu azunguke sasa hivi asionekane, mmh! Lisiwe jini lile, Mungu aniepushie mbali.”<br />
Kulani alimtazama na kutulia akiwa amejilaza kwenye ukuta chini ya bati. Baada ya kusema yale mwenye nyumba ile aliondoka na kumwacha Kulani palepale nyumbani bila kujua.<br />
<br />
Baada ya kuondoka, Kulani aliendelea kumsubiri mganga palepale ukutani chini ya bati katika umbile lile lile la mjusi kama atatokea Mganga Njiwa Manga amvae na kumuulia mbali. Alisubiri kwa saa kumi mpaka jioni ilipoingia ndipo alipomuona akiwa anamsindikiza mmoja wa wateja wake.<br />
<br />
Jini Kulani aliteremka na kurudi katika umbile la mwanadamu na kumfuatilia kwa nyuma bila ya mganga kujua. Nia yake ilikuwa kukutana naye wakati anarudi ili amvae. Taratibu alitembea kumfuata kwa nyuma mganga aliyekuwa mbele akitembea huku akizungumza na wateja wake.<br />
<br />
Njiani Mganga Njiwa Manga alianza kuhisi kama ardhi inatetemeka na mwili kuwa mzito, kitu kile kilichomfanya ageuke na kutazama nyuma. Alishtuka kukiona kiumbe cha ajabu kwa mbali kikija taratibu. Kwa haraka alichutama chini na kushika michanga huku akilikemea jitu lile ambalo liligundua limejulikana.<br />
<br />
Wakati Kulani akijitayarisha kumvaa Mganga Njiwa Manga baada ya kugundua amejulikana, kabla hajamfikia alirusha vumbi la mchanga lililomuingia machoni na kumpofua macho. Alipiga kelele za maumivu na kujipiga chini kwa hasira na kusababisha kishindo kizito kilichotikisa eneo kubwa la Bagamoyo.<br />
<br />
Kishindo kile kilisababisha watu waliokuwa karibu na sehemu kilipotokea waanguke na kupoteza fahamu. Nyumba nyingine zilipata nyufa kutokana na kushindo cha Kulani kupasua ardhi na kupotea. Baada ya robo saa hali ya eneo la Bagamoyo ilirudi kuwa ya kawaida.<br />
Baada ya kurudi hali ya utulivu Mganga Njiwa Manga alinyanyua alipokuwa ameangukia baada ya kurushwa na udongo uliotoka kwenye shimo alilozama jini Kulani baada ya kupofuka macho. Alimtuma mtu kwenda nyumbani kumletea dawa ambayo alikunywa na kujimwagia kichwani.<br />
<br />
Baada ya kuyafanya yale alikwenda hadi kwenye shimo lililokuwa limechimbika kama kumelipuka bomu. Sehemu ile aliweka dawa kisha aliondoka na kurudi nyumbani kwake. Alipofika nyumbani mwili ulikuwa umechoka sana, hakuweza kuendelea na kazi ya matibabu, aliwaomba wagonjwa wake apumzike baada ya kunusurika kifo toka kwa jini ambaye hakujua ametoka wapi.<br />
<br />
Siku ile hakufanya kazi yoyote, alilala mpaka siku ya pili huku akiviona viungo vyake vikipoteza nguvu. Hata alipolala hakuweza kujigeuza mpaka siku ya pili, kwake ulikuwa upinzani mkubwa katika kazi yake. Mara nyingi upinzani uliishia nje ya ngome yake, lakini hakikuwahi kiumbe chochote cha ardhini majini au angani kilichoweza kumdhuru.<br />
<br />
Pia katika kazi yake haikuwahi kutokea kiumbe kilichowahi kumvizia njiani kwa ajili ya kumdhuru. Wengi walivamia sehemu aliyokuwa akifanya kazi na kukutana na vikwazo. Lakini uwezo wa kinga yake ya mwili ndiyo uliomsaidia, bila hivyo angemalizwa na jini yule.<br />
***<br />
<br />
Jini Kulani baada ya kuzama chini ya ardhi kwa kujipigiza kwa hasira, aliibukia pembeni ya bahari. Alitembea taratibu huku akipapasa ili kuingia majini. Baada ya kutembea kwa muda alibahatika kuyakanyaga maji. Pale pale alizama chini.<br />
Mfalme wa bahari alishangaa kumuona Mkuu wa Watwana Kulani amesimama mbele yake akiwa haoni.<br />
<br />
“Kuna nini tena kimekusibu mtwana wangu mtiifu?”<br />
“Mtukufu mfalme, safari yangu imekuwa mbaya.”<br />
“Kulani umefanya makosa, kwa nini jana hukurudi?”<br />
“Niliogopa mtukufu mfalme kurudi bila kutimiza ulichonituma.”<br />
“Umekitimiza?”<br />
<br />
“Hali yangu kama unavyoniona.”<br />
“Tatizo nini?”<br />
“Nimepofuka mtukufu mfalme.”<br />
“Lakini hujanijibu, umemmaliza?”<br />
“Sikuweza, yule mtu hata wewe sikushauri uende.”<br />
“Kwa nini?”<br />
<br />
“Amejidhatiti, ana nguvu za ajabu sijawahi kuona, ameizindika ngome yake haiingiliki, na yeye mwenyewe alichonifanya sitasahau mpaka nakufa.”<br />
<br />
Jini Barami Hudirud, mfalme wa bahari atakubali ushauri wa Kulani kuachana na Mganga Njiwa Manga?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c04a2217767927"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468a0238357342359">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.32<br />
<br />
<br />
“Hapana lazima niende, hawezi kushindana na nguvu zangu.”<br />
“Mtukufu mfalme, bado himaya ya chini ya bahari inakuhitaji lazima atataka kutumia nguvu za ziada kukumaliza. Nashukuru sikugusana naye ningeweza kupoteza maisha.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Kwa hiyo tuwaache wanadamu watuchezee?”<br />
<br />
“Hapana, ila nguvu zinazidiana, yule mwanadamu ana nguvu za ajabu sana, nilijitahidi kuuzima moto alioutega kwenye himaya yake, nilishindwa kila nilipouzima na nilipotaka kuingia uliwaka tena nikajikuta kukipambazuka bila ya kuweza kuingia kwenye himaya yake. Ndiyo sababu ya kuchelewa kurudi na kuamua kubaki ili nihakikishe nammaliza akitoka kwake. Lakini haikuwa hivyo matokeo yake nimekuwa kipofu.”<br />
<br />
“Mmh! Nimekuelewa, basi mpelekeni akapate tiba.”<br />
Watwana wengine walimchukua Kulani na kwenda kumpatia tiba ya macho, baada ya kuondoka, mfalme alimgeukia mkewe aliyekuwa kimya akimuangalia Kulani kwa huruma.<br />
“Mke wangu umeona hali ilivyo, unanishauri nini kutokana na hali aliyorudi nayo Kulani?”<br />
<br />
“Mmh! Mume wangu hali inatisha, inaonesha wazi vita ni nzito, tukifanya mchezo tutakwisha, mpaka Kulani kusema hivyo ujue kuna kazi. Kwa nini tusiachane na mpango wa kumfuatilia huyo mwanadamu?”<br />
“Lakini mke wangu si unajua uwezo wangu? sijawahi kushindwa na kitu,” Mfalme alijitapa.<br />
<br />
“Naujua vizuri, hata Kulani anaujua lakini mpaka kakukueleza vile naomba umsikilize huenda kuna kitu amekiona kinaweza kukupotezea maisha kama utashindana na yule mwanadamu.”<br />
“Lakini kumbuka jini ana nguvu kuliko mwanadamu?’<br />
“Lakini mwanadamu ndiye kiumbe mwerevu kuliko viumbe wote wa Mungu?”<br />
“Hilo nalijua lakini bado hawawezi kushindana na sisi.”<br />
“Mume wangu majini sisi hatuna ushirikiano, kuna majini wengine huwakinga mwanadamu na kuwafanya kuchanganya nguvu za kijini na akili ya kibinadamu lazima tu atakushinda.”<br />
“Kwa hiyo tufanye nini?”<br />
“La muhimu tuachane na mpango huo.”<br />
<br />
“Na suala la Balkis kuolewa na jini mwenzake?”<br />
“Hilo nalo ni gumu, tuendelee kumshawishi aweze kubadili mawazo na kuendelea na kazi ya kukusanya vizazi vya wanadamu na kutengenezewa dawa.”<br />
“Mimi nina hasira, jaribu kuongea naye wewe.”<br />
<br />
“Nitafanya hivyo jioni nitazungumza naye.”<br />
Walikubaliana mke wa mfalme azungumze na Balkis ili aweze kubadili uamuzi wake wa kung’ang’ania kuolewa na mwanadamu.<br />
****<br />
Baada ya kuamka siku ya pili, Mganga Njiwa Manga bado mwili wake haukuwa na nguvu, wagonjwa wengi waliofika siku ile hawakupata huduma kutokana na hali yake. Ilibidi siku ile na yeye kutumia dawa za kujifusha na kunywa ili kujirudisha katika hali ya kawaida, baada ya kukumbwa na upepo wa jini Kulani.<br />
<br />
Kilichomshangaza kilikuwa rangi ya jini yule, alikuwa mweusi kama rami tofauti na majini wote aliowahi kukutana nao. Siku ya pili tangu akutane na dhahama nzito ya jini Kulani, aliendelea na kazi ya kutoa huduma kwa wagonjwa wanaotoka mbali.<br />
<br />
Baada ya kuingia katika chumba chake kutoa huduma, alitulia kwenye mkeka kisha aliweka ubani kwenye kitezo na kutulia kwa muda ili ajiandae kwa matibabu ya wagonjwa waliokuwa wameongezeka kutokana na kusimama kwa huduma yake.<br />
<br />
Ilikuwa ajabu baada ya moshi wa ubani kupanda juu, ulimfuata mbele ya uso wake na akaanza kuona picha asiyoielewa. Alikiona kiumbe cha ajabu kikitoka kwenye maji na ghafla kiligeuka na kuwa mwanadamu, kisha kilitembea taratibu toka kwenye ufukwe na kuingia maeneo ya watu.<br />
<br />
Baada ya kiumbe kile kilichojigeuza kuwa binaadamu kukaribia ngome yake, kilijigeuza umbile na kurudia lile alilotoka nalo chini ya maji. Ajabu kilipotaka kuingia kwenye himaya yake aliona moto ukiwaka kuzunguka eneo lake, ghafla kiumbe kile kilitoka mbio kurudi baharini na kuchota maji kisha kuja kuzima moto.<br />
<br />
Kiliendelea kuzima moto mpaka kulipopambazuka, kila kilichoendelea alikiona mpaka kupambana na jini lile. Hapo ndipo alipogundua jini lile lilitoka wapi, alicheka na kuona kinga aliyokuwa nayo ndiyo iliyomsaidia bila hivyo angekufa vibaya.<br />
Taratibu moshi ulipungua na hali ya ndani ikarudi kuwa ya kawaida, Mganga Njiwa Manga aliendelea kuweka tena ubani uliotoa moshi wa kawaida bila kuwepo na kitu kisichokuwa cha kawaida. Alimtuma msaidizi wake kuwaita wagonjwa.<br />
<br />
Nini kiendelea baada ya mganga kuonekana kudhibiti nguvu za kijini? Je, nini hatma ya Brighton katika chumba cha giza?</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a468c8288e75245177"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a46899547389327963">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.33<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> CHINI YA BAHARI<br />
Malkia Huleiya, mama mzazi wa Balkis alikwenda hadi chumba cha giza na kuomba Balkis atolewe, baada ya kutolewa alimpeleka kuoga na kukaa naye kwenye pwani ambayo huitumia kupumzika familia ya kifalme. Muda wote Balkis alikuwa akibubujikwa na machozi.<br />
Baada ya kukaa kimya kwa muda malkia Huleiya alimwita mwanaye.<br />
“Balkis”<br />
<br />
“Abee mama.”<br />
“Najua utatuona sisi wazazi wako makatili lakini unajua kabisa ubaya wa wanadamu na pia ni aibu jini kutoka katika ukoo wa kifalme kuzaa na mwanadamu.”<br />
“Mama kabla ya kuzungumza lolote naomba mumtoe mpenzi wangu na kama hamtaki awe huku naomba mumrudishe duniani.”<br />
<br />
“Hakuna tatizo.’ Alitumwa mtu kwenda kumtoa Brighton kwenye chumba cha giza na kumpa maji ya kuoga kisha kuwekwa kwenye chumba kizuri. Baada ya hatua zile mazungumzo yaliendelea.<br />
“Nina imani imefurahi?” Mama yake alimuuliza.<br />
“Siwezi kufurahi kwa vile sijatimiza dhamira yangu.”<br />
“Ipi?”<br />
<br />
“Ya kuolewa na mwanadamu.”<br />
“Hilo ndilo baba yako hataki kusikia.”<br />
“Lakini kumbuka tunachokifanya hakimpendezi Mwenyezi Mungu.”<br />
“Kipi hicho.”<br />
<br />
“Cha kuwafanya wanawake matasa.”<br />
“Ni kweli, lakini tunafanya hivyo kwa ajili yako.”<br />
“Kama unaona kufanya vile ni dhambi kwa nini msiniache na mpenzi wangu aliyekuwa tayari kukaa huku hata watoto wangezaliwa wangekuwa wetu.”<br />
“Mwanangu hujui vita ya wanadamu ni kubwa, huwezi kuamini kizazi kimoja kimechukuliwa. Kama kizazi kimechukuliwa je, mwanadamu watakubali aishi huku?”<br />
“Mwanadamu kanipenda mwenyewe wala sikumlazimisha.”<br />
<br />
“Lakini si ana mchumba wake?”<br />
“ Alimkana mbele yangu na kuwa tayari kunioa.”<br />
“Kwa sababu hakujua kuwa wewe ni jini.”<br />
“Hata alipojua alikubali ndiyo maana nimekuja kuishi nae huku.”<br />
“Lakini kumbuka baba yako alikuwa akikutegemea sana, ulichokifanya kimemchanganya sana.”<br />
<br />
“Lakini mama tatizo nini, kutafuta vizazi vya wanawake na kuzaa bila vita na wanadamu kipi bora, ona kama ulivyoniambia mkuu wa watwana Kulani kawa kipofu, kwa nini tusiachane na vita na wanadamu ili hamu ya mtoto apatikane bila kupata madhara zaidi.”<br />
“Uamuzi wako umemuweka baba yako katika wakati mgumu, kumbuka anakupenda kuliko kitu chochote, hakuota hata siku moja utamkosea heshima.”<br />
<br />
“Ni kweli najua baba ananipenda lakini alitakiwa kunisikiliza kuliko kuchukua maamuzi mazito, ona katumia nguvu nyingi matokeo yake Kulani kawa kipofu.”<br />
“Balkis mwanangu hakuna jini anayekubali kushindwa na mwanadamu.”<br />
“Ni kweli lakini kuna wanadamu nao huamini kabisa majini hawawawezi, kama wameweza kuchukua kizazi kimoja wanashindwa nini kuvichukua vyote?”<br />
<br />
“Balkis mwanangu kama ungekwenda kwa kitu tulichokutuma, nina imani kazi yako ingekuwa nyepesi sana kuliko ulichokifanya cha kuanzisha uhusiano na mwanadamu.<br />
“Kitendo kile kilituchanganya sana hasa baba yako, hata kuzungumza na wewe alishindwa na kunituma mimi. Anaamini hata matatizo ya Kulani chanzo ni wewe.”<br />
“Chanzo ni mimi kwa vipi? Wakati niliwakataza tuachane na vita na wanadamu lakini mkawa wabishi.”<br />
<br />
“Balkis mwanangu naomba uifanye kazi tuliyokutuma, tunaamini wewe ni mtoto mwenye heshima na usikivu. Nakuomba chonde chonde mwanangu msikilize baba yako.”<br />
“Mamaa kwa nini msinikubalie, kwani kuna ubaya gani?”<br />
“Kumbuka baba yako ni mfalme wa majini, ni aibu kwa mwanaye kuolewa na mwanadamu, ndiyo maana alikutuma kutafuta kizazi cha mwanamke ili kuhakikisha unapata tiba na kuolewa na jini mwenzako.”<br />
<br />
“Kwa hiyo nimrudishe Brighton duniani?”<br />
“Ikiwezekana.”<br />
“Mbona unasema ikiwezekana.”<br />
“Lazima tumuulize baba yako ataamua nini juu ya mwanadamu aliyejua siri yetu.”<br />
“Sasa naona unataka kuharibu mazungumzo, mmenikataza kuolewa na mwanadamu basi nimrudishe kwao.”<br />
<br />
“Lakini si atakuwa amejua siri yetu?”<br />
“Sasa mnataka kumfanya nini?”<br />
“Sijajua mpaka tupate maelekezo ya baba yako.”<br />
“Sikiliza kama nimekubaliana na uamuzi wenu wa kuachana na mwanadamu ili niendelee na kazi yangu ya kutafuta vizazi vya wanawake, naomba kwenye suala la kurudi kwao mpenzi wangu msiniingilie.”<br />
<br />
“Lakini kumbuka mwanangu chini ya bahari hii mwenye sauti ya mwisho ni baba yako.”<br />
“Hata awe na sauti gani uamuzi wowote tofauti na kumrudisha duniani hatutaelewana.”<br />
<br />
Nini hatima ya Brighton? Je, ataruhusiwa na mfalme kurudi duniani baada ya kuijua siri ya majini?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a46891338324871965">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.34<br />
<br />
<br />
<br />
“Mbona umefika mbali, ngoja nimpelekee taarifa hizi, atafurahi sana kusikia kuwa umekubali kurudi dunia kutafuta vizazi vya wanawake. Pia nitamueleza suala la mpenzi wako la kurudishwa duniani. Siamini kama atakuwa na maamuzi mazito ya kukuumiza.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Mmh! Haya basi naomba nafasi ya kuzungumza na Brighton.”<br />
“Mmh! Basi ataletwa huku ili baba yako asijue chochote.”<br />
<br />
Baada ya kusema vile, Huleiya aliondoka na kumuacha Balkis akiwa amejilaza kwenye kiti cha uvivu. Japo moyo ulimuuma kumuacha Brighton mwanaume aliyeamini ndiye mume wa maisha yake. Bado hakuamini kama anaweza kutoa siri za majini. Lakini aliamini hakuwa akijua lolote katika siri za chini ya bahari kutokana na kufikia kwenye chumba cha giza.<br />
<br />
Baada ya muda Brighton alifikishwa bustanini na kukutana na Balkis, baada ya kukutana Balkis alimueleza hali halisi na yeye kuwa tayari kumrudisha duniani. Kwa upande wake Brighton alijikuta akizama kwenye dimbwi la mahaba ya Balkis na kumuomba atafute njia yoyote ili asirudishwe duniani.<br />
<br />
“Mpenzi kwa nini usimbembeleze baba yako ili tuishi pamoja?”<br />
“Hilo ndilo lilikuwa lengo langu lakini limeleta mtafaruku mkubwa ndani ya familia. Kwa hiyo nakuomba ukubali kurudi duniani ila sitakuwa mbali nawe.”<br />
<br />
“Mmh! Sawa lakini nitalikosa penzi lako.”<br />
“Ni kweli, lakini lazima nikubaliane na matakwa ya wazazi wangu.”<br />
“Sawa, sina jinsi,” Brighton alikubali kwa shingo upande.<br />
<br />
Malkia Huleiya baada ya kuzungumza na mwanaye alipeleka taarifa ya kikao kwa mumewe mfalme Barami. Alipofika alimkuta akimsubiri kwa hamu.<br />
“Karibu malkia wangu.”<br />
<br />
“Asante mfalme wangu.”<br />
“Mh, nijuze yaliyojiri huko?”<br />
“Mmh! Namshukuru Mungu yamekwenda vizuri.”<br />
“Kakubali?”<br />
<br />
“Ndiyo.”<br />
“Ooh! Afadhali.”<br />
“Lakini..”<br />
“Lakini nini tena malkia wangu?” Mfalme alishtuka.<br />
<br />
“Kuhusu yule mpenzi wake.”<br />
“Ana nini?”<br />
“Anataka arudishwe duniani.”<br />
<br />
“Ina maana hajui sheria yetu mwanadamu anayejua siri zetu huwa harudi tena duniani?”<br />
“Hapo ndipo penye tatizo.”<br />
“Tatizo gani?”<br />
“Mwanao anataka amrudishe duniani.”<br />
“Haiwezekani.”<br />
“Amesema iwe isiwe lazima tumrudishe duniani.”<br />
<br />
“Yeye ni nani anayetaka kutulazimisha tufanye anavyotaka, siwezi kuwa na sauti mbili katika himaya yangu ya chini ya bahari.”<br />
“Lakini mume wangu..”<br />
“Hakuna cha lakini, aendelee na kazi ya kutafuta vizazi tena tutampangia kwa siku moja alete vingapi ili awahishe kutimiza lengo la kuolewa tuondokane na adha hizi.”<br />
“Mume wangu si vyema kila wakati kutumia nguvu, ifike wakati mwingine uwe unawasikiliza walio chini yako.”<br />
<br />
“Siwezi, nasema kauli yangu ni ya mwisho na maamuzi yangu yaheshimiwe,” mfalme alikuwa mkali.<br />
“Mume wangu hii itakuwa vita nyingine, kwa jinsi nilivyomsikiliza mwanao hawezi kukubali hili.”<br />
“Nitakachomsikiliza ni kumuacha hai, lakini si kumrudisha duniani.”<br />
“Mwanao amesema kwa hili hamtaelewana.”<br />
“Hebu kamlete hapa,” mfalme alisema kwa hasira.<br />
<br />
Alitumwa kijakazi kumfuata bustanini, Balkis alifika mbele ya baba yake kusikiliza kile alichoitiwa.<br />
“Abee mtukufu mfalme,” Balkis aliitikia akiwa amesimama mbele ya baba yake.<br />
“Kwanza nimefurahi kusikia umeweza kubadili uamuzi wako ila umeniudhi kwa kunilazimisha nifanye utakavyo.”<br />
“Baba kukulazimisha kitu gani?”<br />
“Kuhusu kumrudisha mwanadamu duniani.”<br />
<br />
“Sasa tatizo liko wapi? Mmemkataa asinioe sasa si nimrudishe nilipomtoa.”<br />
“Ina maana hujui sheria za majini, kama mwanadamu atajua siri zetu?”<br />
“Nazijua lakini huyu nimemleta miye hakujileta mwenyewe, wala hakuletwa kwa lipizo.”<br />
“Sheria za huku mwanadamu yeyote atakayeingia huwa hatoki salama, lakini kwa heshima yako hatutamuua bali ataishi huku milele.”<br />
<br />
“Kwa hilo baba sitakubali hata kwa kukatwa kichwa, ni mimi ndiye niliyemlazimisha kuja huku iweje mumshikilie?”<br />
“Hiyo ndiyo sheria ya huku kamwe haibadiliki.”<br />
“Nasema kwa hili itabadilika.”<br />
“Tunabisha?”<br />
<br />
“Hatubishani ukweli ndiyo huo, ikifanywa kinyume nikiondoka hapa sitarudi tena.”<br />
“Sooba,” alimwita mtwana msaidizi wa Kulani kwa sauti ya juu.<br />
“Rabeka mtukufu mfalme,” Sooba aliitika na kusimama imara mbele ya mfalme.<br />
<br />
“Mpeleke huyu kwenye chumba cha giza.”<br />
Balkis alichukuliwa tena na kurudishwa kwenye chumba cha giza. <br />
Nini kiliendelea?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983db7850c93207838"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983dc4032435025460"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a46886c86793834244">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.35<br />
<br />
<br />
<br />
Baada ya mwezi mmoja na nusu kupita, Suzana akiwa ofisini kwake, muda mfupi baada ya kuingia alijikuta akiwa na mawazo mengi. Hiyo ilikuwa ni kutokana na maneno ya Mganga Njiwa Manga alipokwenda kwake jana yake kufuatilia suala la kurudi mchumba wake Brighton, aliyekuwa chini ya bahari katika chumba cha giza.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Majibu ya mganga yalimkatisha tamaa tofauti na alivyofikiria kupatiwa matibabu kama ya Sharifa ya kuingizwa ndani ya maji ya bahari usiku wa manane. Alishangaa kuambiwa baada ya kukutana naye na kuchukua vitabu vyake vya uganga na kuvisoma kwa muda. Alipomgeukia alimueleza:<br />
<br />
“Kazi yako inanichanganya sana, mpenzi wako bado yupo chumba cha giza, inaonesha alitolewa na kurudishwa tena, kuna utata mkubwa juu ya hatima ya mumeo kutolewa chini ya bahari kurudishwa duniani.”<br />
“Mungu wangu! Si atauawa?” Suzana aliuliza.<br />
“Hawezi kuuawa, inaonesha uhai wake bado mrefu.”<br />
“Sasa itakuwaje ikiwa kila siku mambo yanazidi kuwa mabaya kwake, huoni kama maisha yake yapo hatarini?”<br />
<br />
“Ni kweli yapo hatarini lakini..”<br />
“Lakini nini mganga? Naomba msaada wako wa kumtoa huko.”<br />
“Nilikueleza toka siku ya kwanza kuwa ni vigumu kumtoa kwenye chumba cha giza kwani kila nikimtafuta haonekani. Kuna siku mchana nikiwa katika shughuli zangu nilikiona kivuli cha mchumba’ako, ilionesha ametolewa chumba cha giza lakini usiku nilipotaka kuifanya kazi ile sikumuona.<br />
<br />
“Kitendo kile kilinichanganya sana, hasa baada ya kuwa nimefika baharini na mbuzi wangu wawili, mweupe na mwekundu. Nilijikuta nikimtafuta tena lakini sikuweza kumuona. Niliamua kurudi nyumbani ili kuangalia upya, wasiwasi wangu nilidhani labda amekwisharudi duniani.<br />
<br />
“Nilimtafuta kila kona ya dunia mpaka chini ya udongo sikumuona, kila nilipomtafuta ilionesha bado yu hai, lakini alikuwa haonekani zaidi ya kiza kinene. Baada ya kuhangaika sana niliweza kukiona kivuli chake kwa taabu sana kikionesha yupo kwenye chumba cha giza.<br />
<br />
“Lakini kila nilivyojaribu kumvuta hakuonekana, huwezi kuamini kazi yako nimeifanya kwa muda mrefu bila mafanikio kuliko kazi nyingi nilizowahi kufanya. Wakati nikiendelea kuhangaika kutafuta nilishangaa kuona taarifa ikinionesha kuwa mumeo atatoka chini ya bahari bila kutumia dawa yoyote.”<br />
<br />
“Sasa atatokaje ikiwa bado ameshikiliwa na majini?”<br />
“Mara zote huongozwa na maandiko ya vitabu vya uganga ili niweze kumtibu mgonjwa, siwezi kukurupuka ndiyo maana dawa zangu huwa sibahatishi.”<br />
“Hakuna njia nyingine ya kunisaidia?”<br />
<br />
“Siwezi kukudanganya ila nakuhakikishia mpenzi wako atarudi bila dawa yoyote.”<br />
Suzana alikubali kwa shingo upande kwa kuamini sifa za mganga yule kuwa hashindwi na kitu ni za uongo. Aliona ni ajabu Brighton kurudi bila dawa yoyote. Baada ya kuondoka na kurudi nyumbani aliondoa tumaini la kurudi kwa mpenzi wake.<br />
<br />
Akiwa bado ofisini, katikati ya mawazo ya kukumbuka maelezo ya mganga yaliyomkatisha tamaa, baada ya kuonekana ameshindwa kumrudisha mpenzi wake na kuweka visingizio lukuki. Alishtushwa na sauti ya Sharifa aliyeingia ofisini kwake bila kumuona kutokana na kuzama kwenye dimbwi la mawazo.<br />
<br />
“Suzana vipi shoga mbona unaonekana upo mbali, una tatizo gani?”<br />
“Ooh! Shoga karibu.”<br />
“Mbona hivyo, una tatizo gani maana nimeingia bila wewe kuniona?”<br />
“Sharifa ina maana huyajui matatizo yangu?”<br />
“Nayajua lakini leo umekuwa tofauti na siku zote.”<br />
<br />
“Ni kweli.”<br />
“Tatizo nini?”<br />
Suzana alimtonya Sharifa aliyoelezwa jana yake na Mganga Njiwa Manga alipofuatilia kumrudisha duniani mpenzi wake. Kutokana na majibu yake juu ya mganga, ilionesha kabisa hakukuwa na uwezekano wa kurudishwa kwa mchumba wake.<br />
<br />
“Nina imani mzee yule si mganga, wala hana lolote! Anafanya kazi kwa kubahatisha, iweje aweze kumuona ashindwe kumrudisha? Kisa, oooh, nilimuona mchana usiku akapotea, mwongo mkubwa hana lolote yule,” Suzana alilalamika.<br />
“Lakini si alikueleza atarudi, tena kizuri hakukudanganya, au ulitaka akudanganye ili achukue fedha zako?”<br />
<br />
“Kuna mtu gani anaweza kutoka kwa majini bila dawa au maombi?”<br />
“Muamini yule babu, analokueleza ndilo linalokuwa.”<br />
“Kipi cha kunifanya nimuamini zaidi ya sifa za kusikia?”<br />
“Basi shoga mguu huu ni wako.”<br />
“Una maana gani?”<br />
<br />
“Mambo yamejibu.”<br />
“Mambo gani?”<br />
“Kazi ya mzee Njiwa Manga.”<br />
“Kazi gani?”<br />
“Kweli Suzana umechanganyikiwa.”<br />
<br />
“Unafikiri kidogo, mtu siku zinakatika hakuna dalili zozote za kurudi kwa mpenzi wangu.”<br />
“Suzana kwa mganga Njiwa Manga si nilikwenda kwa ajili ya kurudishiwa kizazi?”<br />
<br />
“Ndiyo.”<br />
“Basi majibu yametoka.”<br />
“Ina maana wewe ni mjamzito?”</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123a4687e678309846759">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.36<br />
<br />
<br />
<br />
“Ndiyo maana yake.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Utani huo.”<br />
“Kweli shoga nimeamini yule babu ni mganga kweli.”<br />
“Kama ni hivyo basi hataki kunisaidia.”<br />
“Amekataa vipi wakati kakueleza ukweli juu ya ramli yake ilivyomuongoza. Ingekuwa hawezi kitu angekwambia japokuwa hajawahi kushindwa matatizo ya majini.”<br />
<br />
“Mmh! Kwa hiyo una uhakika kuwa Brighton atarudi bila kufanya dawa yoyote?”<br />
“Kama amekueleza atarudi ujue atarudi, si alikwenda baharini na mbuzi wawili. Kama angekuwa hataki kukusaidia asingeona umuhimu wa kwenda kujisumbua baharini saa nane za usiku.”<br />
“Mmh! Mimi nilijua labda ni njia ya kujitetea tu.”<br />
<br />
“Suzana, kwa taarifa nilizozipata kutoka kwa mama, Njiwa Manga kazi ya uganga huu ni mwaka wa thelathini na siyo watu wa hapa tu nchini, kuna watu wanatoka mbali kwa ajili ya kufuata tiba zake. Si hivyo tu, ameshachukuliwa sana na watu wa mbali kwa ajili ya kwenda kufanya matibabu, kuna kipindi alikuwa akiondoka zaidi ya mwaka, kitu ambacho baadaye alikiona kuwa si kizuri kwa watu wengi hukosa huduma zake na kuamua kutosafiri.<br />
<br />
“Si wewe hata mimi siku tulipokwenda baharini na hali iliyonitokea kisha kusema eti tayari kizazi changu kimerudi niliona ni uongo. Lakini hali iliyonitokea hivi karibuni na kufanya vipimo vyote na kujiona nina ujauzito nimekubaliana na mama kuwa, kweli mzee Njiwa Manga ni mganga wa kweli.<br />
<br />
“Kwa hiyo shoga yangu nakuomba uvumilie kama amekuhakikishia uhai wa mpenzi wako ni mrefu ni kiasi cha kuvuta subira, nina uhakika alichosema kitakuwa kweli.”<br />
“Mmh! Itabidi nikubali lakini moyo haunipi kabisa.”<br />
“Sikuzuii kufikiria hivyo, lakini amini usiamini mzee Njiwa Manga ni mganga wa kweli.”<br />
“Mmh! Haya,” Suzana alikubali kwa shingo upande.<br />
<br />
“Basi shoga mguu ulikuwa wako kukujulisha mzee Njiwa Manga amefanya mambo, punguza mawazo kila alilosema mganga litatimia mimi naamini Brighton atarudi bila ya dawa kama alivyosema.”<br />
“Kama alichokisema ni kweli nitampa zawadi kubwa.”<br />
“Hata mimi najiandaa kumpelekea zawadi kubwa, sijui hata nimpelekee nini?”<br />
“Utakachojaaliwa.”<br />
<br />
“Shoga baadaye.”<br />
“Sawa, wacha na mimi nianze kazi kidogo umeichangamsha akili yangu bila hivyo siku ya leo ingekuwa ngumu kwangu.”<br />
“Najua hata mimi baada ya kuona mabadiliko ya mwili moyo wangu ndipo ulipofunguka.”<br />
“Wacha na mimi nisubiri.”<br />
Sharifa alirudi ofisini kwake na kumuacha Suzana akijiandaa kuanza kazi za siku ile.<br />
****<br />
<br />
Baada ya Balkis kupelekwa katika chumba cha giza, mfalme alionekana kuzidi kukasirika kwa kuona mtoto wake amemkosea adabu. Mkewe muda wote alikuwa ameinama bila kusema kitu, baada ya mwanaye kurudishwa chumba cha giza alimgeukia mumewe na kumuuliza kwa sauti ya ukali ambayo hakutakiwa kuitoa mbele ya mfalme.<br />
“Sasa ulinituma kufanya nini na umefanya nini?”<br />
<br />
“Kwanza punguza sauti yako ujue unaongea na nani?”<br />
“Nazungumza na mume wangu na aliyepelekwa katika chumba cha giza ni mwanangu,” bado malkia Huleiya hakushusha sauti yake.<br />
“Unabishana na mimi?” Mfalme aliuliza kwa sauti ya juu.<br />
“Sibishani na wewe kwa vile anayeteseka ni mwanangu.”<br />
“Lakini huoni kama amevunja sheria ya majini pia na wewe unanivunjia adabu kama mumeo na mfalme wako?”<br />
<br />
“Nimekuvunjia adabu kivipi wakati nakueleza kitu cha kweli?”<br />
“Kwa hiyo nivunje sheria kwa ajili ya mwanao?”<br />
“Kwani unataka aolewe na jini mwenzake au atoroke?”<br />
“Siwezi kuvunja sheria, majini wengine watanielewa vipi?”<br />
<br />
“Kwani si ni wewe ndiye uliyeiweka sheria hii kwa roho mbaya yako baada ya majini wengi kuwa na uhusiano na wanadamu. Umemkataza mwanao asiolewe na mwanadamu, anakuomba umrudishe duniani mpenzi wake hutaki. Kuna faida gani kuwa mfalme wakati huna mapenzi hata na familia yako.”<br />
<br />
“Kwa hiyo nawe unaungana na mwanao?”<br />
“Ndiyo na pia nasema hivi, Soobaaa,” malkia Huleiya alimwita mkuu wa watwana msaidizi kwa sauti kubwa.<br />
<br />
“Wa nini?” Mfalme Balami aliuliza.<br />
“Naam Malkia mtukufu,” Soba aliitikia akiwa amesimama mbele ya malkia.<br />
“Soba kamtoe haraka Balkis.”<br />
Soba alibakia amesimama na kusita kutekeleza amri hiyo kwa kuhofia kupingana na mfalme.<br />
<br />
Ni kweli kauli ya mganga Njiwa Manga itatimia? Mfalme wa majini atasalimu amri kwa mkewe?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af647dfa5570776150">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.37<br />
<br />
Soba alibakia amesimama kama sanamu, malkia Huleiya alipaza sauti yake tena:<br />
”Soooba hujanielewa, kamtoe haraka Balkis chumba cha giza.”<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Bado Soba alibaki amesimama huku akisubiri mfalme ataamua nini baada ya mkewe kutoa amri ya kupingana na mumewe kwa mara ya kwanza. Siku zote alijua mwenye sauti ya mwisho ni mfalme, malkia sauti yake siku zote aliitoa kwa taratibu tena ya chini. Toka awe ndani ya jumba lile la kifalme hakuwahi kusikia amri kali ya malkia.<br />
<br />
“Sooooba, unanidharau?” Alimuuliza huku akiteremka sehemu ya juu alipokuwa amesimama pembeni ya mumewe.<br />
<br />
Soba bado alisimama kikakamavu kusubiri kauli ya mfalme aende au la, aliamini siku zote mke wa mfalme hakuwa na maamuzi tofauti na mumewe. Kitendo cha Soba kukataa kwenda kumtoa Balkis kilimuudhi sana malkia na kuona umevunjiwa heshima.<br />
<br />
Pembeni yake kabla hajafika kwa Soba alichomoa upanga uliokuwa kiunoni kwa mmoja wa walinzi wa nyumba ya mfalme na kulipunga hewani usawa wa shingo ya Soba. Wengi walijua anamtisha ili akubali kumfuata Balkis chumba cha giza alipofungiwa na mumewe.<br />
<br />
Soba naye aliendelea kusimama kikakamavu akisubiri kauli ya mfalme aliyekuwa amepata kigugumizi kwa kitendo cha mkewe kumvunjia heshima mbele ya wasaidizi wake na watwana.<br />
Panga alilopunga hewani bila hiyana lilitua kwenye shingo ya Soba na kutenganisha kichwa ni mwili. Kitendo kile kilimtisha kila mmoja aliyekuwepo pale, hata mfalme hakuwahi kuona hasira nzito ya mkewe kama siku ile. Kila mtwana aliyekuwa pembeni yake aliingiwa na mchecheto wa kuhofia maisha yake.<br />
<br />
Malkia Huleiya baada ya kuona mwili wa Soba ukianguka chini kama gunia na kichwa kikigaagaa chini, alishtuka kwa kuona ameua, alilitupa upanga chini kisha aliangua kilio na kukimbilia chumbani. Kila tukio lililotokea muda ule lilimshangaza kila mmoja.<br />
<br />
Mfalme alijikuta amebaki amesimama kama sanamu asielewe kilichotokea ni kweli au alikuwa akiota. Ulikuwa mwaka wa sabini na tano toka amuoe mkewe aliyekuwa msikivu na mtulivu pia mnyenyekevu kwa mumewe muda wote. Malkia Huleiya siku zote alikuwa kiumbe mwenye huruma na kumkanya mumewe pale anapotumia nguvu bila kutumia muda wa kufikiri katika maamuzi yake ya kutoa adhabu kwa majini yanapofanya kosa.<br />
<br />
Lakini siku ile kwa mara ya kwanza alifanya kitendo kilichomshtua kila mmoja aliyemfahamu. Hata adhabu anapotoa mfalme, yeye ndiye aliyesimama kutetea.<br />
Lakini kitendo cha kutenganisha kichwa na kiwiliwili cha jini hakuwahi kukifanya zaidi ya mumewe ambaye kila alipokosewa adhabu yake kubwa ilikuwa kutenganisha kichwa na kiwiliwili.<br />
<br />
Kitendo cha mkewe kumuua mtwana mkuu msaidizi aliyekuwa akitegemewa na mfalme baada ya Kulani kuwa kipofu kilimfadhaisha sana.<br />
<br />
Alitoka sebuleni na kumfuata mkewe aliyekuwa amejitupa kitandani akilia kwa uchungu huku akijutia kitendo cha kumuua Soba.<br />
Japo Soba alionesha jeuri lakini moyoni alijuta kwa uamuzi mzito alioutoa kwa kumtenganisha kichwa na mwili.<br />
<br />
“Malkia wangu,” mfalme Balami alimwita mkewe kwa sauti ya upole.<br />
“Nisamehe mume wangu, nimeshindwa kuzuia hasira zangu, yote ni kwa ajili ya mapenzi mazito kwa mwanetu wa pekee Balkis.”<br />
<br />
“Najua mke wangu, lakini kitendo chako kimenifanya nijione nina mke mwenye maamuzi mazito.”<br />
<br />
“Hapana sikutarajia kutoa uamuzi mzito kama ule, lakini yote umeyasababisha wewe.”<br />
“Hapana mke wangu, ningejuaje uwezo wa maamuzi yako bila kufanya vile?”<br />
“Si kwa kutoa roho ya kiumbe kisicho na hatia.”<br />
<br />
“Ile imeonesha kumbe hata nikiondoka au nikifa hakuna mtu wa kukuchezea, kwa kitendo kile Balkis namtoa kwenye chumba cha giza pia kumrudisha duniani mchumba wake bila masharti.”<br />
“Unasema kweli?” Malkia Huleiya alishtuka kusikia kauli ya mumewe.<br />
<br />
“Kweli kabisa, hii itakuwa kama zawadi kwa ujasiri uliouonesha mbele yangu.”<br />
“Asante mume wangu kwa uamuzi wako uliorudisha furaha yangu.”<br />
“Si kurudisha furaha yangu tu bali kuendelea na msimamo huo huo ili kuongeza heshima ndani ya himaya yangu.”<br />
<br />
Baada ya makubaliano alitumwa kibaraka kwenda kumtoa Balkis kwenye chumba cha giza lakini aligoma kutoka kama hawatamuachia Brighton. Waliamuliwa kwenda kuwatoa wote, walifanya hivyo na Balkis alikubali kutoka ndani ya chumba cha giza.<br />
<br />
Pia alitoa masharti kuwa, kabla ya kuzungumza lolote wahakikishe Brighton anatolewa chini ya maji na kurudishwa duniani. Kwa vile uamuzi ulikuwa amepitishwa ombi lake halikupingwa na baba yake. Lakini kabla ya kurudishwa duniani Brighton alipewa masharti na mfalme kuwa siku atakayoitoa siri ya majini ndiyo siku ya mwisho ya uhai wake. <br />
<br />
Baada ya kukubaliana na masharti, Brighton alisindikizwa na watwana kumi baada ya kumfikisha pembeni mwa bahari walimlaza pembeni. Ubaridi wa alfajiri na maji vilimfanya Brighton ashtuke na kujikuta amelala ufukweni, miguu ikiwa majini na mwili nchi kavu. Baada ya kunyanyuka alipokuwa amesimama kwa mshtuko. Aliifahamu sehemu ile ilikuwa ni eneo la daraja ya Salenda.<br />
<br />
Baada ya kujinyanyua alipokuwa amekaa, alitembea kuelekea barabarani ili apate lifti ya kumrudisha kwake.<br />
<br />
Je, kurudi kwa Brighton ndiyo mwisho wa Balkis kuchukua wanaume wa kibinadamu?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123983df16f5770629750"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6470ef5f13847023">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.38<br />
<br />
<br />
<br />
Brighton alitembea kusogea barabarani kwa mwendo wa taratibu kutokana na mwili wake kukosa nguvu. Alikuwa akitembea kwa mwendo wa kuyumba yumba hadi alipofika chini ya mti uliokuwa pembezoni mwa barabara na kuuegemea kutokana na kuishiwa nguvu.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Suzana akiwa kwenye gari lake akielekea kazini, alishtuka kuona kitu ambacho hakukitegemea kwa muda ule. Roho ilimwambia aamini kitu anachokiona lakini akili ya kawaida ilikataa kwa kuamini kitu kile. Baada ya kuvuka eneo lile bado roho ilimwambia kuwa kitu alichokiona ndicho chenyewe.<br />
<br />
Alisimamisha gari na kuliegesha pembeni, kisha aliteremka kwenye gari na kurudi sehemu alipomuona mtu aliyemfananisha. Alitembea taratibu hadi sehemu ile alipokiona kitu alichokifananisha. Brighton alikuwa kama mtu aliyelewa pombe kutokana na kuzidi kuishiwa nguvu.<br />
<br />
Suzana alipomkaribia, alipunguza kasi ya mwendo wake zaidi huku akimkazia macho mtu yule, alipomsogelea karibu aligundua aliyekuwa mbele yake ni kipenzi chake Brighton.<br />
“Brighton,” alimwita kwa sauti ya juu japo hakuwa mbali naye.<br />
Brighton alinyanyua kichwa na kumtazama aliyekuwa akimwita, macho yake yaliona maluweluwe japo alimfahamu aliyekuwa mbele yake.<br />
<br />
“Brighton,” Suzana alimwita tena huku akiogopa kumgusa.<br />
“Suzana,” Brighton alimwita baada ya kuitambua sura ya mpenzi wake.<br />
“Ni wewe Brigton?”<br />
“Ni mimi Suzana umejuaje kama nipo hapa?”<br />
“Ha! Siamini,” Suzana alimvamia Brigton na kumkumbatia kwa furaha.<br />
<br />
“Ni mimi mpenzi wangu,” Brighton alisema huku akitokwa na machozi.<br />
“Hapana Brighton, twende nyumbani,” alimshika mkono na kwenda naye kwenye gari.<br />
Suzana aliligeuza gari na kurudi nyumbani kwake kwa kuwa alijua nyumbani kwa Brighton kusingekuwa katika hali ya usafi baada ya nyumba kukaa kipindi kirefu bila ya matunzo. Alipofika nyumbani alimtengea maji ya kuoga, kisha akamtayarishia chakula.<br />
<br />
Baada ya kula Brighton alionekana kuwa na uchovu, aliamua kujilaza na usingizi mzito ukamchukua. Suzana alijikuta akiahirisha kwenda kazini ili aweze kuwa karibu na mpenzi wake aliyemtafuta kama maji kwenye ardhi kame.<br />
<br />
Alijikuta akiyakumbuka maelezo ya mganga Njiwa kuwa, Brighton angerudi bila tiba yoyote, hamu yake kubwa alitaka kujua mpenzi wake alikuwa wapi na aliishi maisha gani. Alijikuta akisahau hata kutuma ujumbe kazini kuwaarifu mabosi wake kama amepata dharura, muda mwingi alimuangalia mpenzi wake aliyekuwa amelala.<br />
<br />
Alimpapasa akiwa haamini kama kweli mtu aliyekuwa amechukuliwa na majini angeweza kurudi salama. Akiwa katika dimbwi la mawazo simu yake iliita. Alipoangalia juu ya kioo aliliona jina la Sharifa.<br />
“Haloo Sharifa.”<br />
“Suzana, upo sawa?”<br />
“Nipo sawa.”<br />
<br />
“Mbona hujaonekana kazini?”<br />
“Huwezi kuamini yaliyosemwa yametimia?’<br />
“Yepi hayo?”<br />
“Brighton amerudi.”<br />
“Acha utani!”<br />
<br />
“Kweli kabisa na sasa hivi nipo pembeni yake.”<br />
“Suzana hebu acha kunirusha roho.”<br />
“Sharifa, naamini kabisa mzee Njiwa Manga ni mganga wa kweli.”<br />
“Si ulikuwa unamuona tapeli.”<br />
“Wee dada wee, kuchanganyikiwa kubaya.”<br />
<br />
“Kwa hiyo kazini itakuwaje?”<br />
“Naomba uniombee ruhusa kuwa naumwa nitakuja kuchukua ‘sick sheet’ baadaye.”<br />
“Mmh! Huwezi kuamini furaha niliyoipata leo haina kifani ili kujiridhisha na maneno yako nitaomba ruhusa kuja kumuona shemeji.”<br />
<br />
“Njoo dada umuone, huwezi kuamini amerudi amenenepa na kupendeza.” <br />
“Basi nakuja na sick sheet yako kabisa.”<br />
“Utakuwa umefanya jambo la mbolea.”<br />
“Basi nakuja,” Sharifa alionekana kuwa na mshawasha wa kumuona Brighton. <br />
<br />
****<br />
Baada ya kutolewa kwa mpenzi wake chini ya bahari, Balkis alifurahi sana na kukubaliana na wazazi wake kurudi duniani kutafuta tena vizazi. Kitendo cha kukubali kulimfanya mfalme afanye sherehe kubwa ya kumuaga kwa mara ya pili. Sherehe ilifanyika juu ya bahari.<br />
<br />
Majira ya saa saba za usiku Balkis aliagwa eneo la bahari na kuingia duniani kwa mara nyingine tena. Aliondoka eneo lile kwa kutembea taratibu pembeni mwa barabara eneo la Daraja la Salenda kuelekea maeneo wanayoishi binadamu. Alipokaribia njia panda ya Masaki aliona gari dogo likisimama ghafla na kuteremka mwanamke na baadaye akafuatia mwanaume.<br />
<br />
Balkis amerudi tena duniani, nini kitatokea?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6470ef5f13847023"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6470ef5f13847023"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6470ef5f13847023"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6470ef5f13847023"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6470ef5f13847023"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6470ef5f13847023"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6470ef5f13847023"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6466803987451427">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.39<br />
<br />
Hakutaka kujionesha kwao, alisimama pembeni yao aone kuna nini. Cha kwanza kilichomvutia kilikuwa tumbo lililoonesha ujauzito la mwanamke aliyetoka kwenye gari. Kingine kilikuwa sura na mvuto wa mwanaume aliyefuatia. Mwanamke alionekana mwenye hasira sana kutokana na maneno yake.<br />
<br />
“Umenifuata ili iweje? Nimekwambia niache na maisha yangu na ujauzito huu naut<span class="text_exposed_show">oa.”<br />
“Lakini mbona umefikia huko mke wangu?”<br />
“Wewe si unaniona mimi si mwaminifu, basi kwa taarifa yako kuanzia leo achana na mimi.”<br />
<br />
“Mke wangu mimi mumeo nina haki ya kukuuliza jambo lolote linalokwenda kinyume na maadili ya ndoa.”<br />
“Kama umeniona nimetoka nje ya maadili ya ndoa si uniache.”<br />
“Siwezi kukuacha kwa vile bado ni mke wangu.”<br />
<br />
“Kwani ndoa lazima, ukiona hivyo ujue sina shida na wewe.”<br />
Mwanamke alionesha jeuri kwa mumewe, Balkis alitulia ajue mwisho wake.<br />
“Mke wangu bado tuna nafasi ya kulizungumza hili,” mwanaume alimbembeleza mkewe.<br />
“Ngoja nikueleze kitu, ujauzito huu sio wako na mwenye ujauzito huo utamuona muda si mrefu.”<br />
<br />
“Mke wangu umefikia hivyo?”<br />
“Ulikuwa hujui?”<br />
“Usifanye hivyo mke wangu bado nakupenda sana.”<br />
“Mimi sikupendi,” mwanamke alisema huku akifunua simu na kupiga namba, alimsikia akizungumza.<br />
<br />
“Eeh... nipo njia panda ya Masaki... njoo utanikuta.”<br />
“Mke wangu unampigia simu nani?”<br />
“Mume mwenzio anayejua kulea asiye na gubu kama wewe.”<br />
“Mke wangu ni maneno gani hayo?”<br />
“Najua litakuuma na mwaka huu wako, kama ulimwacha mkeo kwa ajili yangu sasa imekula kwako.”<br />
<br />
Maneno yale yalimchoma sana Balkis aliyekuwa amesimama pembeni yao akifuatilia mazungumzo yale. Alimuonea huruma mwanaume aliyekuwa akimbembeza mwanamke mpaka kumpigia magoti na machozi yakimtoka. Alitamani kuingilia ugomvi ule lakini hakuna ambaye angemuelewa kwa muda ule kutokea mbele yao.<br />
<br />
Alitulia kufuatilia mazungumzo yale bila kuzungumza chochote, mwanaume akiwa bado anaendelea kumbembeleza mkewe, gari aina Toyota VX lilisimama pembeni ya gari la wanandoa wale.<br />
Baada ya kusimama aliteremka mwanaume mwenye mwili uliojengeka kimazoezi aliyekuwa amevaa bukta na fulana ya mikanda. Yule mwanamke alimsukuma mwanaume aliyekuwa amepiga magoti na kumfuata aliyekuja na VX.<br />
<br />
“Vipi Sweet?” aliuliza yule mwanaume.<br />
“Si huyu bwege ndiyo anayeniwekea usiku.”<br />
Walizungumza wakiwa wamekumbatiana pembeni ya mwenye mke aliyekuwa bado amekaa chini baada ya kusukumwa na mkewe. Kitendo kile kilimtoa machozi Balkis na kuapa kuwashikisha adabu.<br />
“Pole sweet, twende zetu.”<br />
<br />
Walishikana mikono na kwenda ndani ya gari na kumuacha mwanaume akilia kwa uchungu huku akizungumza maneno yaliyokwenda na upepo lakini Balkis aliyasikia.<br />
“Kweli mwanamke shetani yaani yote niliyokufanyia umeniona sifai, nimekosana na familia yangu kwa ajili yako. Mwisho unanivua nguo mbele za watu, sioni faida ya kuishi bora nife.”<br />
<br />
Kauli ile ilimtoa machozi Balkis na kuona jinsi gani wanawake wanavyoweza kuwaingiza wanaume kwenye matatizo. Alimuona yule mwanaume kama mtu aliyechanganyikiwa akienda ndani ya gari na kutoka na kipande cha kamba ili ajinyonge.<br />
<br />
Alisogea kwenye mti wa pembeni na kuifunga ile kamba, akatafuta tawi zuri ambalo alifunga kamba ili ajinyonge. Kabla hajajitundika Balkis alijitokeza mbele yake, jamaa alishtuka kumuona mwanamke mzuri kasimama mbele yake usiku ule wa manane. Alipomuona alisogea pembeni ya kamba ili Balkis asijue kama alikuwa anataka kujinyonga.<br />
“Mudy kwa nini unataka kujiua?” Balkis alimuuliza.<br />
<br />
Balkis atamuacha Mudy ajiue nini adhabu ya mke wa Mudy? Kuyajua yote tukutane Risasi Jumatano.<br />
Mudy kama alivyoitwa na Balkis alishangaa kuona mwanamke mzuri mbele yake usiku ule tena akimfahamu kiufasaha.<br />
“Umenijuaje?” alimuuliza.<br />
<br />
“Kukujua si muhimu kuliko kujibu swali langu kwa nini unataka kujinyonga?”<br />
“Nani kakwambia?”<br />
“Mudy niambiwe na nani wakati naiona kamba ikining’inia?”<br />
“Basi tu nimeamua.”<br />
<br />
”Uamue nini wakati umekataliwa na mkeo.”<br />
“Wewe umejuaje?”<br />
“Kwani uongo?”<br />
“Hata kama si uongo wewe umejuaje na usiku kama huu unatoka wapi huogopi?”<br />
“Mudy si muda wa kutaka kujua nimejuaje au natoka wapi? Unataka kuniambia wanawake wamekwisha mpaka umng’ang’anie mwanamke asiyekupenda?”<br />
<br />
“Sio kumng’ang’ania, bali kanitia umaskini wa kutumia fedha nyingi kwa ajili yake.”<br />
“Sikiliza Mudy, ulitakiwa kumshukuru Mungu kwa kukuonesha hili mapema, au ulitaka ufilisike kabisa ndiyo akuache.”<br />
“Kama hivi nimekosana na ndugu na jamaa zangu kwa ajili yake wakisikia ameniacha nitakuwa mgeni wa nani?”<br />
<br />
“Sikiliza Mudy, hakuna mtu anayechukiwa milele, kama utaomba msamaha watakusamehe.”<br />
“Mmh! Kwangu ni ngumu, kuwa na mwanamke yule niligeuka adui wa familia, wote waliniombea mabaya. Leo wasikie si utakuwa sherehe, kwa vile hunijui sikujui kwa nini usiniache nitimize dhamira yangu?” Mudy alimuomba Balkis amuache ajiue.<br />
<br />
Balkis atamuacha Mudy ajiue nini adhabu ya mke wa Mudy?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6466803987451427"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6466803987451427"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6466803987451427"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6466803987451427"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6466803987451427"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af6466803987451427"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af645e1e2d94052747">JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.40<br />
<br />
<br />
<br />
“Sina budi kufanya hivyo.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Sikiliza Muddy, ulitakiwa kumshukuru Mungu kwa kukuonesha jambo hili mapema, au ulitaka hadi ufilisike ndipo mkeo akuache?”<br />
<br />
“Nimekosana na ndugu na jamaa zangu kwa ajili yake, wakisikia ameniacha nitakuwa mgeni wa nani?”<br />
“Sikiliza Muddy, hakuna mtu anayechukiwa milele, kama utawaomba msamaha ndugu na jamaa zako watakusamehe.”<br />
<br />
“Mmh! Kwangu ni vigumu, kwa kuwa mwanamke yule alinifanya niwe adui wa familia, wote waliniombea mabaya. Leo wakisikia si itakuwa sherehe, kwa vile hunijui sikujui kwa nini usiniache nitimize dhamira yangu?” Muddy alimuomba Balkis.<br />
<br />
“Inawezekana wewe ndiye hunijui lakini mimi nakujua vizuri, toka ulipoanza maisha ya shida, hadi pale mpenzi wako wa kwanza alipoiba fedha kwao zilizokufanya upate utajiri na kukuvimbisha kichwa kwa dharau na kukufanya uwatelekeze mkeo na mtoto wako.<br />
<br />
“Mkeo kwa aibu kutokana na kuidharau ya familia yake, baada ya kumtelekeza aliamua kunywa sumu pamoja na mtoto wake. Kwa vile ulikosa shukrani wala fadhila, kifo cha mkeo na mtoto wala hakikuugusa moyoni mwako, ukaamua kuendelea na maisha yako na mpenzio mpya ambaye mlifunga ndoa ndani ya wiki tatu baada ya vifo hivyo.<br />
<br />
“Fedha zilikupa jeuri na kudharau wazazi na nduguzo waliokueleza tabia chafu za mkeo, kwako uliona kama wanaleta fitina ili muachane. Lakini ukweli uliuona baada mambo kuanza kukuendelea kombo, mke uliyemuoa tabia yake ni kuharibu ndoa za watu baada ya kukufilisi mwisho wake ndiyo kama ulivyokuwa ukitaka kufanya.<br />
<br />
“Lakini kwa tabia hiyo nitawakomesha, siwezi kuona familia zinahangaika kwa ajili ya upumbavu wa watu wachahe,” Balkis alisema kwa sauti ya hasira.<br />
“Kwani dada wewe ni nani na utawakomesha vipi?”<br />
“Utajua muda si mrefu.”<br />
<br />
“Samahani dada yangu wewe ni nani maana unanijua vizuri kuliko hata watu wangu wa karibu.”<br />
“Naitwa Balkis.”<br />
“Hii siri yangu nani kakwambia?”<br />
“Narudia tena usitake kumjua aliyeniambia,zaidi ya kujua ubaya wa mtu uliyekuwa naye. Kwa mchezo wake ndoa yako ni ya tano kuvunjwa na yeye na kila alipopita aliacha msiba, ningechelewa kidogo jina lako lingebaki historia midomoni mwa watu.”<br />
<br />
“Mmh! Wewe huku unatoka wapi usiku huu?”<br />
“Kwetu siyo mbali naomba ikiwezekana ukalale kwa vile najua huwezi kuendesha gari kutokana na kuchanganyikiwa. Ningekuwa nimeaga nyumbani ningekupeleka kwako.”<br />
“Unataka nikalale kwako na mumeo?” Muddy aliuliza.<br />
<br />
“Sijaolewa.”<br />
“Unakaa na nani?”<br />
“Nipo na wazazi wangu.”<br />
“Ulijuaje kuna tukio hili?”<br />
<br />
“Nilipokuwa nimelala nilisikia mkibishana, nikatoka ndani na kusogea hadi pembeni yenu kwa vile kila mmoja alikuwa na hasira hamkuweza kuniona. Nilipowaona niliwatambua kutokana na maelezo ya watu juu ya matatizo yenu ya ndoa kutokana na kuijua tabia ya mkeo toka zamani.<br />
<br />
“Mambo mengi nilikuwa nayajua, nilipotoka nje na kuwakuta sikushangaa kusikia tambo za mkeo. Baada ya kuondoka nilijua nini kinafuata, nilijua utataka kujinyonga tu kama walivyofanya wanaume wengi walioachwa kama wewe. Kwa vile ulikuwa hujui upande wa pili wa mkeo.<br />
<br />
“Hata mkeo alipoondoka anaamini kabisa uamuzi utakaochukua ni huo, hushangai alikueleza uchukue kamba bila kukupa maelekezo. Kesho anasubiri kusikia kifo chako na kuchukua vitu vyako vyote bila familia yako kuambulia chochote.<br />
<br />
“Na hata akisikia hujafa lazima atafungua kesi ya kudai mgawane mali kuhakikisha anakufilisi kabisa. Utavumilia lakini mwisho wake ni kujiua kwa sumu au kamba. <br />
<br />
“Niliona kuna umuhimu wa kukueleza kilichokuzunguka katika ndoa yako, yule si mwanamke ila ni mwizi tena muuaji. Hebu niangalie mimi nilivyo mrembo, yule mkeo tapeli ananifikia?” Balkis alimuuliza Muddy huku akijigeuza na kupigwa na mwanga wa taa za barabarani.<br />
<br />
“Hawezi kukufikia.”<br />
“Sasa mwanamke kama mimi nikikupa penzi la kweli bila kuhitaji fedha zako unasemaje?”<br />
“Unataka kuniambia mwanamke mzuri kama wewe hujaolewa?”<br />
“Sijaolewa bado nipo kwa wazazi wangu kama nilivyokueleza awali.”<br />
<br />
”Maeneo haya unakaa nyumba gani?”<br />
“Ingia kwenye gari nikakuoneshe.”<br />
Muddy aliingia kwenye gari na Balkis naye aliingia upande wa dereva na kuanza kuendesha gari. Baada ya mwendo mdogo gari lilikata kushoto na kuingia kwenye jumba la kifahari.<br />
<br />
Muddy pamoja na kuwa mwenyeji wa eneo lile lililopo karibu na Daraja la Salenda hakuwahi kuliona jumba zuri la kifahari. Baada ya gari kuingia katika jumba lile ambalo toka azaliwe hakuwahi kuingia, Balkis alimkaribisha hadi chumbani.<br />
<br />
“Karibu mpenzi nikupoze machungu yote.”<br />
“Asante.”<br />
Balkis alimshika mkono Muddy na kumuongoza, hakuamini mahaba aliyooneshwa na Balkis mwanamke mwenye uzuri wa ajabu.<br />
<br />
Nini hatima ya Muddy mikononi mwa Balkis? Kuyajua yote tukutane kesho hapa hapa UNLIMITED SWAGGAZZ!!!!!<br />
*story unaionaje?<br />
*mpk sasa umejifunza nini?<br />
*je tufanyeje ili kuepukana na balaa km hili???</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af645e1e2d94052747"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af645e1e2d94052747"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af645e1e2d94052747"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af645e1e2d94052747"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123af645e1e2d94052747"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf53f432e85974323">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.41.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
“Karibu mpenzi nikupoze machungu yote.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Asante.”<br />
Balkis alimshika mkono Mudy na kuingia naye ndani, Mudy hakuamini mahaba aliyooneshwa na Balkis, mwanamke mwenye uzuri wa ajabu.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
Muddy aliingizwa kwenye jumba la kifahari lililokuwa na mapambo ghali ambayo aliwahi kuyaona katika picha za majumba ya Falme za Kiarabu.<br />
“Karibu sana.”<br />
“Asante.”<br />
<br />
“Muddy naomba ukaoge kwanza ndipo tupumzike.”<br />
Muddy alinyanyuka na kupelekwa kwenye bwawa la kuogelea lililokuwa mbele ya nyumba. Baada ya kuoga alipewa taulo laini la sufu na kupewa makubazi ya kuvaa kisha alirudi ndani. Kwa vile usiku ulikuwa umeingia sana alipelekwa moja kwa moja kitandani.<br />
<br />
Kila mmoja alilala chumba chake, Muddy alilala usingizi mzuri ajabu ambao hakuwahi kulala katika maisha yake. Alijikuta akitamani siku moja aishi maisha kama yale. Balkis aliingia katika mawazo ya Muddy na kuamini kama atatumia udhaifu ule basi atampata kirahisi.<br />
<br />
Majira ya saa kumi na nusu za usiku Balkis alimuamsha Muddy kisha alimpa chai yenye viungo na kumueleza:<br />
“Muddy muda wa kurudi baba yangu umekaribia, naomba nikurudishe kwako.”<br />
<br />
“Mmh! Sawa lakini bila ya baba yako nisingeamka mapema sijawahi kulala usingizi mtamu kama leo.”<br />
“Muddy, jitahidi kumuondoa akilini mkeo tapeli ambaye hatarudi kwako tena baada ya kukamilisha kilichomleta. Ukimuona anarudi ujue anaifuata roho yako. Kama utaachana naye nakuhakikishia kuishi maisha mazuri. Kama utakuwa mkweli na mwaminifu, nitayabadilisha maisha yako,” Balkis alimueleza Muddy ambaye hakuamini nguo zake kufuliwa usiku ule na kupigwa pasi kisha kupuliziwa manukato.<br />
<br />
“Kama unayosema ni kweli mke wangu hatarudi basi, nitakuwa na wewe.”<br />
“Muddy usitake kuniudhi, wewe ni mwanaume gani mkeo anachukuliwa mbele yako unaishia kulia, kwa kinywa chake kakueleza hakutaki, unataka upate ukweli gani?”<br />
<br />
“Ni kweli usemayo, lakini kumbuka yule bado ni mke wangu, hivyo tunaweza kuzungumza na kuyamaliza.”<br />
“Muddy nikueleze mara ngapi? Siku utakayorudiana na mkeo ujue ndiyo siku ya mauti yako. Wewe si mtu wa kwanza kufanyiwa hivyo, kama huamini kesho utaletewa karatasi itakayokutaka ufike mahakamani kwa ajili ya madai ya kugawana kidogo ulichobakia nacho.<br />
<br />
“ Kibaya ni kwamba una deni la mkeo ambalo litasababisha usipate hata fedha nusu ya kuuza vitu vyenu. Kwa vile hukujua deni alilokukopesha riba yake inazidi thamani ya vitu ulivyobakia navyo.<br />
“Kwa vile ni mzoefu wa mchezo ule, lazima atashinda kesi na wewe utachanganyikiwa, kitakachofuatia itakuwa ni kuokota makopo. Inawezekana una masikio ya kenge mpaka utoke damu ndipo usikie, usinitafute wala ukiniona usinifuate.”<br />
“Sasa dada utanisaidiaje?”<br />
<br />
“Niite Balkis.”<br />
“Sasa Balkis utanisaidiaje?”<br />
“Nakuomba chochote atakachokifanya asikushtue, wewe kubaliana nacho, mimi nitakuwepo mahakamani siku ya mwisho.”<br />
<br />
“Nitashukuru.”<br />
“Basi acha nikuwahishe kabla baba hajarudi.”<br />
Walitoka na kuingia kwenye gari, kisha Muddy aliendesha kurudi nyumbani kwake baada ya akili yake kuwa imetulia kidogo. Alipofika waliingia wote ndani, Balkis hakukaa sana aliondoka na kumuacha Muddy amalizie usingizi.<br />
<br />
***<br />
Muddy alishtuka saa nne asubuhi na kujikuta akiwa na mawazo juu ya matukio yaliyomtokea jana ya kuachwa na mkewe pia kukutana na mwanamke mrembo mwenye mapenzi na huruma, Balkis. Pamoja na kuoneshwa ukarimu wa hali ya juu bado kitendo cha mkewe kumkataa kilimuumiza na kukumbuka vitu vingi alivyopoteza kwa ajili yake.<br />
<br />
Alikumbuka jinsi alivyotelekeza familia yake kwa ajili yule mwanamke na kusababisha kupoteza mke na watoto. Bado hiyo haikutosha, aliweza kutumia fedha nyingi alizowekeza mke wake wa kwanza vibaya kiasi cha kumtia katika umaskini.<br />
<br />
Pia alisababisha kutengwa na familia yake na kuwa adui yao mkubwa baada ya kugoma kutoa fedha za matibabu zilizosababisha dada yake mkubwa kupoteza maisha baada kukatazwa na mkewe asitoe kitu.<br />
Kila alipokuwa akifikiria yote yale moyo ulikosa amani, aliamini njia nyepesi ya kukimbia aibu ile ni kunywa sumu au kujinyonga. Akiwa katikati ya uamuzi mzito, hodi mlangoni iliyahamisha mawazo yake yaliyokuwa yamefanya atokwe na machozi na macho kuwa mekundu kutokana na maumivu ya moyo.<br />
Alifuta machozi na kwenda hadi mlangoni na kufungua, alikutana na kijana mtanashati.<br />
<br />
“Karibu,”<br />
“Asante, siingii ndani natoka mahakama ya mwanzo kuna barua ya madai toka kwa aliyekuwa mkeo.”</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf53f432e85974323"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf53f432e85974323"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf53f432e85974323"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf53f432e85974323"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf53f432e85974323"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf536ab5f10023524">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.42.<br />
<br />
<br />
<br />
LAKINI likatokea jambo la ajabu, Muddy kila alipokuwa akikitafuta kisu hakukiona. Alihangaika nyumba nzima, hakukiona. Wazo lingine lilikuwa ni kutafuta kamba ili ajinyonge, vile vile alishangaa kuikosa kamba hata ile aliyotaka kujinyongea usiku na kuiacha kwenye gari, alipoifuata pia hakuikuta.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Hakurudi ndani, alikwenda dukani na kuchukua sumu ya panya, aliichanganya katika chupa ya maji ya kunywa kisha akanywa yote na kwenda kulala akisubiri malaika wa kifo amchukue.<br />
***<br />
Ashura mke wa Muddy alikuwa mwenye furaha, yeye pamoja na mwanaume wake walikuwa wakipongezana kwa kazi kubwa waliyoifanya ya kumfilisi Muddy.<br />
“Nina imani kazi imekwenda vizuri,” mwanaume huyo alisema.<br />
<br />
“Ni kweli, lakini pamoja na kuyafanya yote bado namuonea huruma Muddy. Kwa nini tusimuachie gari na nyumba?” Ashura alisema katika hali ya kumuonea huruma Muddy.<br />
“Tukiwa na huruma hatuwezi kuifanya kazi hii, ona leo tulivyo na utajiri wa kutisha.”<br />
“Mmh! Kweli.”<br />
<br />
Wakati Ashura na mwanaume wake wakiwa katikati ya mazungumzo, mlango uligongwa. Wote walikaa kimya kusikiliza, mlango ulipogongwa tena mwanaume alinyanyuka na kwenda mlangoni. Alipoufungua alikutana uso kwa uso na Balkis, akamkaribisha.<br />
“Karibu mrembo.”<br />
<br />
“Ahsante sijui Ashura anakaa hapa?”<br />
“Wewe nani?”<br />
“Sasa kaka yangu badala ya kunijibu, unaniuliza mimi nani?”<br />
<br />
“Eeh, si vibaya kukujua wewe ni nani kwa vile unayemuuliza ni mke wangu na wewe ni mgeni kwangu.”<br />
“Mimi naitwa Balkis, ina maana Ashura ameshaachana na Muddy?” Balkis aliuliza swali la uongo.<br />
“Hiyo haikuhusu, sema kilichokuleta.”<br />
“Kilichonileta ni kuonana na Ashura.”<br />
“Karibu ndani.”<br />
<br />
Alimkaribisha sebuleni ambapo alimkuta Ashura amejilaza kwenye kochi. Ashura alimshangaa yule mgeni kutokana na uzuri wake wa ajabu, pia vito vya thamani alivyovaa mwilini mwake. Hata manukato yake yalikuwa mageni puani ambayo yaliifanya nyumba nzima kunukia.<br />
“Habari Ashura?”<br />
<br />
“Nzuri, umenijuaje?”<br />
“Ina maana jina lako ni siri? Wanapaswa kulijua watu wachache?”<br />
“Siyo kwamba ni siri ila sikujui.”<br />
“Huwezi kuwajua wote mdogo wangu.”<br />
“Mh! Nikusaidie nini?”<br />
“Nimetumwa na Muddy.”<br />
“Muddy! Muddy ndiye nani?”<br />
“Mumeo.”<br />
<br />
“Mimi nina mwanaume anayeitwa Muddy?”<br />
“Sasa unashangaa au unakataa? Ndoa yako na Muddy imevunjika lini wakati mpaka jana usiku majira ya saa sita mmenipita Daraja la Salenda mkiwa pamoja, leo hii unamkana?”<br />
“Basi muda mfupi baada ya kutuona wewe ndipo tulipoachana.”<br />
“Sasa nani kamuacha mwenzake?”<br />
“Maswali gani hayo?”<br />
<br />
“Ndiyo maana nipo hapa,” Balkis alisema kwa kujiamini.<br />
“Wewe ni nani kwa Muddy?” Ashura alihamaki.<br />
“Kabla sijakujibu nataka useme ukweli mbele ya mwanaume wako, upo tayari kurudiana na Muddy?”<br />
“Sipo tayari.”<br />
<br />
“Na ukirudiana naye tena?”<br />
“Nitembee uchi.”<br />
“Rudia.”<br />
“Nitembee uchi.”<br />
“Kaka umesikia?” Balkis alimgeukia mwanaume wa Ashura na kumuuliza.<br />
“Umesikia?”<br />
<br />
“Kuwa?”hi akirudiana na Muddy.”<br />
“Basi ni hayo niliyofuata hapa.”<br />
“Mbona umeniuliza hivyo?” Swali la Balkis lilimtisha Ashura.<br />
“Si umeachana na Muddy?”<br />
<br />
“Ndiyo, nirudiane naye kwa kitu gani alichonacho, tena muda si mrefu ataokota makopo.”<br />
“Usiokote makopo wewe, tena kabla sijaondoka nawapeni onyo mchezo wenu wa kudhulumu mali za watu utawatokea puani,”<br />
Balkis alimweleza Ashura ambaye bado alikuwa akimshangaa kwa maswali yake.<br />
<br />
Nini kiliendelea? Fuatilia katika Gazeti la Risasi Jumamosi.<br />
Vituko<br />
ndani ya daladala<br />
Abiria wawili ambao majina yao hayakujulikana, juzikati walitwangana makonde mazito baada ya mmoja wao kutoa nauli ya shilingi 200 badala ya 300.<br />
<br />
Abiria wa kwanza alipanda daladala hiyo Buguruni akielekea Gongo la Mboto na wa pili Vigunguti.<br />
Kondakta alipoanza kutoza nauli, abiria wa kwanza alitoa shilingi 200. Kitendo hicho kilionekana kumkera abiria wa pili kwa kumwambia kwa nini katoa nauli nusu.<br />
<br />
Abiria hao walianza kuzozana na kondakta akaungana na kauli ya abiria wa pili ya kumtaka wa kwanza kutoa shilingi 300 na si 200.<br />
Hali hiyo ilionekana kumkera abiria wa kwanza na kuamua kumrushia ngumi abiria wa pili. Kitendo cha abiria huyo kurusha konde kilisababisha timbwili kali kwa washkaji hao kuanza kutwangana kavukavu.<br />
<br />
Mbaya zaidi abiria wa kwanza alikuwa amekaa kiti cha mbele na walipoanza kurushiana makonde mazito gari lilianza kuyumba na kusababisha abiri wengine kuanza kupiga kelele ya kumuomba dereva asimamishe gari.<br />
<br />
“Dereva simamisha gari utatuua, tunakuomba sana tumeshinda salama tunataka tufike nyumbani tukiwa wazima, tafadhali,” alisikika abiria mmoja huku wengine wakimuomba Mungu awaepushe na balaa hilo.<br />
<br />
Wakati abiria wakipiga kelele, daladala hilo ilikuwa mwendo mkali. “Jamani mnataka kutuua kwa sababu ya shilingi 100? Acheni kugombana nitampa konda,” jamaa mmoja alisikika akisema.<br />
Gari liliposimama jamaa hao walishuka na kuanza kukunjana vema na abiria wengine wakaingia ndani ya gari na kumwambia dereva aendeshe.<br />
Mabondi hao wasiotambuliwa na shirikisho la ngumi Bongo waliachwa kituoni hapo wakitifuana.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf536ab5f10023524"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf536ab5f10023524"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf536ab5f10023524"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf536ab5f10023524"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf536ab5f10023524"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf536ab5f10023524"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf52d632926005290">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.43.<br />
<br />
<br />
Muddy alishtuliwa katika usingizi mzito na sauti ya Balkis, aliposhtuka alijishangaa kujiona bado yupo hai hakufa kama alivyodhamilia.<br />
“Muddy vipi?”<br />
<span class="text_exposed_show"> Muddy hakumjibu alimshangaa Balkis aliyekuwa ameshikilia barua mkononi.<br />
<br />
“Muddy mbona unanuka sumu ya panya?”<br />
Bado Muddy hakuwa najibu aliendelea kupepesa macho na kuitazama glasi aliyokunywa sumu ilikuwa juu ya sturi.<br />
“Muddy kwa nini unataka kujiua?” Balkis alimuuliza akiwa ameshika glasi iliyokuwa na sumu.<br />
“Umejuaje?”<br />
<br />
“Muddy nikufundishe mara ngapi swali mwenzake jibu na si swali kwa swali.”<br />
“Umeisoma hiyo barua?”<br />
“Niisome ili iwe nini, haya nilikueleza tokea awali kwa nini hutaki kunielewa?”<br />
“Samahani Balkis nimechanganyikiwa.”<br />
<br />
“Nilikueleza toka awali hutakufa bali unaelekea kwenye wendawazimu na usiponisikiliza sasa hivi utaokota makopo.”<br />
Muddy alishangaa jinsi Balkis mwanamke mrembo mara kumi Ashura ameonesha mapenzi ya kweli kwake. Kingine kilikuwa uelewa wa ajabu wa Balkis kuonekana kumfahamu vizuri yeye na Ashura bila kuhadithiwa na mtu.<br />
<br />
Hatua ya kupelekwa mahakamani ili wakagawane vitu pia deni la mkewe lililokuwa likizaa liba kila kukicha lilizidi kumchanganya. Alijikuta akinyanyuka na kuketi kwenye kitanda na kumuuliza Balkis.<br />
“Balkis unaonekana unajua mambo mengi juu yangu ya Ashura?”<br />
“Ndiyo maana nipo hapa kuokoa maisha yako, kwa vile lengo la mkeo wa uongo limetimia.”<br />
“Yote haya umeyajulia wapi?”<br />
<br />
“Utajua ukinipa moyo wako uliojeruhiwa niuponye.”<br />
“Kwa ukweli niliouona nipo tayari kukukabidhi moyo wangu.”<br />
“Je, Ashura akirudi kukubembeleza?”<br />
“Kwa uliyonieleza siwezi kurudiana na mwanamke yule ambaye kwangu ni muuaji.”<br />
<br />
“Nakuhakikishia kama utakuwa mkweli nitayabadili maisha yako, lakini chonde unigeuke baada ya kuwa na maisha mazuri utanisamehe.”<br />
“Nikuhakikishia nitakupenda kwa moyo wangu wote, najiona kiumbe mwenye bahati kupendwa na mwanamke mrembo tena mwenye maisha mazuri. Nakuapia kukupenda mapenzi ya dhati.”<br />
“Asante Muddy.”<br />
***<br />
Balkis baada ya kujua Muddy ataletewa barua ya kuitwa mahakamani aliingia ndani kwa Muddy bila kuonekana na kwenda kukaa sebuleni kusubiri kitakacho tokea. Baada ya barua kuletwa na kukabidhiwa Muddy, alijua nini kitafuata. Baada ya kuisoma na kuonekana amechananyikiwa alitumia muda ule kuficha kila kitu ambacho angetumia kwa ajili ya kujitoa uhai. Hata alipokwenda dukani aliyemuuzia sumu ya panya, Balkis alijigeuza na kumuuzia kitu kingine kisicho na madhara yoyote.<br />
<br />
Kwa vile alikuwa amechanganyikiwa hakuichumza aliiweka kwenye glasi na kuichanganya na kuinywa kisha aliinywa. Lakini Balkis alikuwa amemuwekea dawa za usingizi ambazo zilimlevya baada ya kunywa na kulala usingizi mzito. Baada ya kumuona amelala, ndipo alimpomwacha na kwenda kwa Ashura mke wa Muddy.<br />
******<br />
Siku ya pili Muddy alifika mahakama kama ilivyopangwa, baada ya kesi kusikilizwa iliahilishwa wiki moja. Muddy alishangaa kutomuona Balkis mahakamani, baada ya kutoka mahakamani aliamua kwenda nyumbani kwao Balkis ili akajue nini kimemsibu baada ya kukosekana asubuhi ile kama alivyomuahidi kufika. Aliendesha gari lake ambalo kutokana na maelezo ya Balkis kuwa litapigwa mnada pamoja na nyumba na kugawana fedha zake, ambazo nazo zitachukuliwa na mtalaka wake na kumuacha bila kitu.<br />
<br />
Njia nzima alikuwa na mawazo juu ya hatima ya maisha yake kama atanyang’nywa kila kitu. Alipofika maeneo ya Daraja la Salenda alitembea taratibu kuitafuta nyumba ya kina Balkis ambayo aliamini ilikuwa maeneo yale.<br />
Lakini alijikuta akichanganyikiwa kutoliona jumba la kifahari alilopelekwa na Balkis. Mawazo yake yaliamini huenda amekosea eneo.<br />
<br />
Kutaka kupata uhakika wa sehemu aliyopelekwa usiku na Balkis, aliendesha gari mpaka sehemu waliyotelemka na mkewe usiku. Alipofika pale alirudi taratibu huku akipepesa macho kuangalia labda ataliona jumba la kifahari. Lakini hakuona chochote zaidi ya miti na bahari kwa nyuma.<br />
<br />
Alijikuta akijiuliza lile jumba alilolala mbona halionekani, alipanda ndani ya gari na kuanza kulitafuta kwa kuendesha gari taratibu kuelekea Masaki labda ataliona jumba lile. Aliendesha gari taratibu huku akipepesa macho labda ataliona jumba la kifahari kama lile ambao katika maisha yake hakuwahi kuona.<br />
<br />
Lakini gari lilizidi kwenda bila kuliona, majumba mengi alioyaona yalikuwa mazuri lakini hayakuweza kufikia hata robo ya uzuri wa jumba la kina Balkis Ambalo lilikuwa na eneo kubwa tofauti na majumba yaliyokuwa yamepangana pia maeneo yake yalikuwa madogo.<br />
<br />
Mpaka anafika Sea cliff Hotel hakuona jumba lile alilopelekwa na Balkis, aliamini kabisa atakuwa amekosea tu. Aligeuza gari na kurudi tena hadi sehemu aliyoachwa na mkewe usiku na kuonana na Balkis. Aliamua kutelemka kwenye gari na kutembea kwa miguu kufuata njia aliyopelekwa na Balkis, alikumbuka hakwenda njia ya Masaki bali alirudi kama anakwenda Daraja la Salenda.<br />
<br />
Muddy alitembea taratibu huku akipepesa macho huenda akaliona jumba lile la kifahari, lakini mpaka anavuka Daraja la Salenda bado hakuona jumba lile.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf52d632926005290"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf52d632926005290"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf52d632926005290"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf52d632926005290"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf52d632926005290"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf525f14179548513">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.44.<br />
<br />
<br />
Hakukata tamaa alitembea hadi Agha Khan, pia nyumba zilikuwa zile zile za siku zote alizozizoea. Baada ya kutembea kwa muda mrefu alijikuta akichoka sana na kuamua kurudi taratibu kulifuata gari lake ili arudi nyumbani. Alitembea kwa mwendo wa kivivu huku kiu na njaa ikiwa kali.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Alimwita muuza maji ambaye alimletea maji, alikunywa kidogo na mengine alijimwagia kichwani kupunguza uchovu. Lakini ilikuwa tofauti na alivyofikiria, alihisi usingizi wa ajabu na mwili kuchoka maradufu. Alitafuta mti wa kivuli uliokuwa pembeni ya bahari na kujilaza chini yake.<br />
<br />
Usingizi mzito ulimpitia uliomfanya alale kwa muda mrefu, alishtuka saa moja usiku, giza lilianza kuimeza nuru ya mchana. Alijikuta amelala pembeni ya maji yaliyokuwa yakirudi baada kupwa kuanzia asubuhi. Alishangazwa na sehemu aliyojikuta kuwa eneo la ndani ya bahari wakati yeye alilala nje ya bahari kwenye miti ya pembezoni. Alinyanyuka na kujikung’uta kisha taratibu alielekea sehemu lilipokuwa gari lake. Wasiwasi wake mkubwa gari linaweza kuibwa au kuchukuliwa baadhi ya vitu.<br />
<br />
Alijiuliza kama gari litaibwa ataieleza nini mahakama, lakini ilikuwa ajabu gari lilikuwa lipo katika usalama pia hakuna kitu chochote kilichopotea. Alimshukuru Mungu na kuingia kwenye gari ili arudi nyumbani, lakini kabla hajawasha gari ili aondoke alishtuka kumuona Balkis.<br />
Balkis alitokea mbele yake na kulisogelea gari huku akichanua tabasamu pana, alipomfikia alimsemesha:<br />
“Muddy vipi?”<br />
<br />
“Safi.”<br />
“Za toka jana?”<br />
“Nzuri.”<br />
“Mbona upo huku?”<br />
“Mbona hukuonekana mahakamani kama ulivyoniahidi?”<br />
<br />
“Kwa hilo naomba samahani mpenzi wangu, nilitumwa na baba asubuhi nilijua nitawahi lakini amini usiamini ndiyo narudi. Na hivi nilikuwa nimetumwa tena nashangaa kukuona hapa.”<br />
“Balkis huwezi kuamini toka nizaliwe leo nimesulubika vibaya.”<br />
“Kwa nini tena mpenzi wangu?”<br />
<br />
“Baada ya kutoka mahakamani...”<br />
“Kabla ya kuendelea hebu nielezee imekuwaje huko?”<br />
“Kesi imehahirishwa mpaka wiki ijayo.”<br />
“Hakuna kitakachobadilika, kila kitu wamekwishakamilisha hata hakimu wa kesi yako ameshachukua chake mapema, kinachosubiriwa ni kukumaliza tu. Lakini nakuhakikishia fedha watakazochukua zitawatokea puani.”<br />
“Utawapeleka polisi?”<br />
<br />
“Wakafanye nini, ila utasikia tu nini kitawatokea.”<br />
“Alafu...”<br />
“Nimekuelewa Muddy, kwanza samahani kwa kutotokea mahakamani, umesema umesulubika kivipi?”<br />
“Hivi kwenu wapi?”<br />
“Muddy, si hapo mbele.”<br />
“Wapi?”<br />
<br />
“Unataka kupajua au kufika, twende maana sasa hivi nipo peke yangu.”<br />
“Sehemu gani?”<br />
“Si hapo mbele? Unaona nyumba ile kwa nyuma.”<br />
“Mbona jana tulikwenda huku?”<br />
“Si ndipo tunapopitia, kwani tatizo nini?”<br />
<br />
“Hakuna tatizo twende nikapumzike nimechoka hapa nilipo pia nina kiu na njaa kali.”<br />
Kama kawaida Balkis aliingia kwenye gari na kuliendesha, pamoja na Muddy kukaza macho ili ajue nyumba ile ipo wapi. Gari lilienda kidogo na kukata kidogo, Muddy hakuamini kuona jumba la kifahari lile lile alilolala jana yake. Baada ya kupaki gari sehemu yake aliteremka na kumfungulia mlango Muddy kisha alimshika mkono na kumuongoza mpaka ndani.<br />
<br />
“Karibu mpenzi wangu,” alimwambia kwa sauti ya mahaba huku akimlegezea macho na kumfanya Muddy asahau tabu zote alizokutana nazo.<br />
Kama kawaida alipelekwa kuoga kisha alifungwa vazi refu na kupelekwa kwenye meza iliyokuwa na vyakula tayari. Wakati akiendelea kula chakula kitamu ambacho kwake ilikuwa siku ya kwanza kukila, Balkis alimuaga kwenda kuoga. Aliondoka kwa mwendo wa madaha na kumfanya Muddy aache kula na kumsindikiza kwa macho huku akiusifia utundu wa Rabuka kumuumba binti mrembo kama yule.<br />
<br />
Kwake aliona kama ndoto kumpata msichana mzuri kama Balkis pamoja na uzuri wake lakini umemuonesha mapenzi ya kweli kiasi cha kumsahau mkewe Ashura. Akiwa katikati ya chakula, alimuona Balkis akisogea mezani akiwa amejifunga upande wa khanga.<br />
<br />
Kila dakika Balkis alizidi kujijaza moyoni kwa Muddy ambaye kwake aliona ngekewa kuokota dhahabu katikati ya soko la Kariakoo. Baada ya chakula kama kawaida alipelekwa kwenye chumba alicholala jana yake. Kwa raha za muda mfupi hakutamani kufa na kujilaumu kwa uamuzi wa kijinga aliotaka kuchukua.<br />
<br />
Kama kawaida alfajiri alirudishwa kwake huku akijiuliza kwa nini baba yake arudi alfajiri tu anatoka wapi. Kitu kingine kilichomchanganya kilikuwa jumba zuri analoishi Balkis lipo sehemu gani mbona hajawahi kuliona. Wazo lake lilikuwa mchana arudi tena kulitafuta.<br />
<br />
Lakini aliporudi alipitiwa na usingizi na kuamka jioni ya siku ile na wakati huo Balkis alikuwa amekwishafika na kumfanya siku ile aimalize nyumbani, lakini bado alitaka kutoka usiku ule kama Balkis akiondoka ambaye alikuwa halali pale na kwenda kufanya uchunguzi wake.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf525f14179548513"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf525f14179548513"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf525f14179548513"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf525f14179548513"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf525f14179548513"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf525f14179548513"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.45.<br />
<br />
<br />
Baada ya Balkis kuondoka majira ya saa nne usiku, Muddy aliamua kurudi tena maeneo ya Daraja la Salenda kufanya uchunguzi wa jumba lile la ajabu. Aliingia kwenye gari lake na kwenda hadi sehemu aliyokutwa na Balkis. Alisimamisha gari lake na kufunga kila sehemu kwa usalama wa gari lake kisha aliteremka na kutembea taratibu kuifuata njia aliyopita na Balki<span class="text_exposed_show">s.<br />
<br />
Kila alivyolitafuta lile jumba la kina Balkis hakuliona, alijikuta akitoka sehemu moja kwenda nyingine bila mafanikio. Saa zilimkatikia kwa kuzurula kulitafuta lile jumba ambalo aliamini kwa muono wake akiwa ndani yake kama akiwa kwa mbali angeliona kutokana na kuwa na taa kila kona ya jumba lile zilizokuwa na mwanga mkali.<br />
<br />
Lakini kila alipotupa macho labda ataziona taa angani, kulikuwa na kiza tu kilichotawala angani. Bado hakuamini alirudi sehemu aliyoanzia zaidi ya mara kumi ili aanze upya kulitafuta jumba la kifahari la kina Balkis. Muda ulizidi kukatika, kutokana na kutembea sana kulitafuta jumba hilo alijikuta akichoka sana na kukaa chini ya mti mmoja apumzike kidogo ili arudi kwenye gari lake na kurudi nyumbani kulala kwani usiku ulikuwa mkubwa.<br />
<br />
Alipokaa chini ya mti usingizi haukuchelewa ulimchukua, ulikuwa usingizi mtamu ajabu uliomfanya alale kama yupo kitandani. Kibaridi cha alfajiri kilimshtua kwenye usingizi mzito na kujikuta amelala pembeni ya ufukwe chini ya mnazi, sehemu ambayo ilimchanganya kidogo.<br />
<br />
Alitembeza macho yake na kuwaona watu waliokuwa wakiteremsha samaki kwenye boti. Sehemu ile ilimchanganya sana na kujiuliza pale ni wapi? Pamoja na kuwa amejilaza chini ya mnazi bado hakuna mtu aliyekuwa na habari naye kwani kila mmoja alikuwa na hamsini zake.<br />
<br />
Wengi walipita pembeni yake wakiwahi kununua samaki walioletwa na majahazi asubuhi ile. Akiwa bado amekaa chini akitafakari yupo wapi, kijua nacho kilianza kuchomoza kwa mbali lakini bado baridi iliendelea kumchonyota mwilini.<br />
<br />
Alijinyanyua taratibu alipokuwa amekaa na kuanza kutembea taratibu pembeni ya bahari huku akijitahidi kuyakumbuka maeneo yale ambayo yalikuwa mageni kichwani mwake. Aliona akikaa kimya atazidi kupotea, ilibidi amuulize kijana mmoja aliyekuwa na kapu lililoonekana limejaa samaki wabichi, alionekana ni mchuuzi aliyelangua na kwenda kuwauza mitaani.<br />
<br />
“Samahani ndugu,” Muddy alimuuliza baada ya kumkaribia.<br />
“Bila samahani kaka yangu.”<br />
“Kwanza ni vizuri kutanguliza salamu kuonesha uungwana, habari za asubuhi?”<br />
“Nzuri tu.”<br />
“Eti hapa ni wapi?”<br />
“Kigamboni.”<br />
<br />
“Mungu wangu, kuja huku si lazima utumie pantoni?”<br />
“Kutoka wapi?”<br />
“Mjini.”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Sasa mimi nimefikaje bila kutumia Pantoni?”<br />
“Kutoka wapi?”<br />
“Mjini.”<br />
“Kwani wewe umefikaje huku?”<br />
“Hata najua, hii kali ya mwaka.”<br />
<br />
“Samahani kaka, mbona kama unajishangaa kwani wewe mara ya mwisho ulikuwa wapi?”<br />
“Njia panda ya barabara ya Ali Hasani Mwinyi na Masaki.”<br />
“Ulikuwa ukifanya nini?”<br />
“Mmh! Tuachane na hayo, hebu nioneshe njia ya kuelekea kivuko cha Pantoni?”<br />
“Twende pamoja na mimi naelekea huko huko.”<br />
<br />
Muddy aliongozana na yule kijana kuelekea kwenye kivuko cha Pantoni, njiani alijawa na mawazo jinsi alivyojikuta Kigamboni wakati yeye alikuwa maeneo ya Daraja la Salenda. Alijiuliza kuhusu gari lake atalikuta kwenye hali gani, alipofika kivukoni bahati nzuri alikuta kivuko ndiyo kinapakia abiria na magari.<br />
<br />
Alipanda na kutulia kwenye siti huku kichwa chake kikiwa hakikubaliana na kilichotokea.<br />
Bado alijawa na mawazo juu ya kujikuta Kigamboni bila kujielewa, kivuko kilivyofika mwisho aliteremka na kuelekea kwenye daladala za kuelekea Mwenge iliyomrudisha mpaka njia panda ya kuelekea Masaki. Alipofika alilikuta gari lake lipo katika hali ya usalama.<br />
<br />
Aliingia ndani ya gari lake na kurudi hadi kwake, alishangaa alipofika kwake kumkuta Balkis amekaa mlangoni akilia. Alijikuta akishtuka, akateremka kwenye gari bila kufunga mlango na kumfuata alipokuwa amekaa.<br />
“Mpenzi unalia nini?”<br />
“Muddy hunipendi.”<br />
“Mimi?” Muddy alishtuka kusikia vile.<br />
<br />
“Muddy nazungumza na nani?”<br />
“Na mimi.”<br />
“Ulikuwa wapi?”<br />
“Nilitoka kidogo alfajiri kuna sehemu nilikwenda mara moja.”<br />
“Muddy unanipenda?”<br />
“Tena sana.”<br />
“Niambie ukweli ulikuwa wapi?”<br />
“Kama nilivyo kueleza mpenzi,” Muddy alijua Balkis alikuja asubuhi ile.<br />
“Nikuambie nini mpenzi zaidi ya hayo.”<br />
<br />
“Mbona kichwani una majani na mwili na nguo zimechafuka?”<br />
Kauli ile ilimshtua Muddy na kujikuta akijikagua upya na kujikuta kweli alikuwa amechafuka kwa mchanga wa bahari pia kichwani alikuwa na majani. Alijikuta akipatwa na kigugumizi, alijifikiria amjibu nini Balkis aliyekuwa akimtazama usoni huku machozi yakimtoka.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf507b72a46213945">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.46.<br />
<br />
<br />
<br />
“Muddy nipo hapa toka saa tano usiku baridi lote limeniishia nikijua haupo mbali, kumbe umekwenda kwa wanawake zako,” Balkis alijiliza kiuongo.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Nisamehe Ba..Ba..lkis,” Muddy alijitetea baada ya kujua kuwa ameumbuka.<br />
“Niambie ukweli ulikuwa wapi?”<br />
<br />
“Nilikufuata kwenu.”<br />
“Kufanya nini, wakati niliondoa kwako hukuniambia kitu?”<br />
“Nililipenda jumba lenu nilitaka kuliona kwa macho yangu nikiwa kwa nje.”<br />
“Si ungenieleza unataka kupajua kwetu ili nikupeleke kuliko kunichunguza au huniamini?”<br />
<br />
“Nakuamini lakini basi tu, yaani nimechanganyikiwa, jumba kama lile sikuwahi kuliona hata mchana huwa silioni maeneo yale.”<br />
“Narudia tena, kwa nini usiniulize jumba letu lilipo? unaweza kulitafuta mwaka mzima na usilione.”<br />
<br />
“Naomba unisamehe kwa yote yaliyojitokeza.”<br />
“Muddy nilishakusamehe tangu siku ya kwanza nilipokuona ukipasuliwa moyo wako kwa kisu butu bila ya ganzi na mkeo wa bandia, niliamini mtupo uliotupwa haukujua ungeangukia wapi na muanguko wako ungekuwa mkubwa sana na usingesimama tena.”<br />
<br />
“Nashukuru Balkis kwa kuyaokoa maisha yangu, nisamehe kwa yote, siyo kwamba sikuamini la hasha, bali nilipenda kuuona utukufu wa utajiri wa familia yako. Bado nipo njia panda kujiuliza jumba zuri kama lile limejengwa lini maeneo yale.”<br />
“Maeneo gani?”<br />
<br />
“Si pale pembeni ya njia panda ya kuelekea Masaki.”<br />
“Nataka nikutaadharishe kitu kimoja, yaani usije tena maeneo yale kwani baba yangu akikuona anaweza hata kukutoa uhai.”<br />
“Atanijuaje?”<br />
<br />
“Mbona anakujua, aliponiuliza nilimdanganya, sasa kama atakuona tena maeneo yale lazima atajua namdanganya na atakufanyia kitu kibaya.”<br />
“Je, akinikuta kwenu?”<br />
“Kwa sasa baba yupo, hivyo hutuwezi kwenda tena mpaka tutakapooana.”<br />
“Kwa hiyo utakuwa unakuja kulala hapa?”<br />
<br />
“Ndiyo maana yake.”<br />
“Si umesema nyumba hii itapigwa bei itakuwaje?”<br />
“Usiwe na wasiwasi kila kitu niachie mimi, ukitoka mahakamani nitakupeleka kwenye nyumba yako mpya.”<br />
<br />
“Nitashukuru mpenzi wangu.”<br />
Balkis baada ya kuingia ndani aliisikia nyumba ukinuka sana, aliogopa kusema kwa kuhofia kumuudhi mpenzi wake. Alitafuta mbinu ya kumuondoa Muddy ili afanye usafi ndani mle.<br />
<br />
Alimtuma kitu ambacho alijua hawezi kukipata karibu, alijua nafasi ile ingempa fursa ya kuwaita wajakazi wake kufanya usafi kwa muda mfupi. Alimuomba samahani kabla ya kumtuma:<br />
“Samahani mpenzi wangu.”<br />
“Bila samahani.”<br />
<br />
“Najua umechoka lakini naomba nikutume kitu.”<br />
“Nitume tu mpenzi wangu.”<br />
“Kwa vile nataka kufanya usafi, naomba kaninunulie udi sehal”<br />
“Upo sehemu gani?” ”Kwenye maduka wanayouza manukato utaupata.”<br />
“Hakuna tatizo wacha niwahi.”<br />
<br />
“Nioneshe ufagio.”<br />
Baada ya kumpa ufagio Muddy alitaka kuondoka na gari lakini Balkis alimkataza alijua akitembea kwa miguu atachukua muda mrefu kurudi kuliko akitumia gari.<br />
“Unaweza kuupata karibu wala usitumie gari.”<br />
“Hakuna tatizo.”<br />
<br />
Muddy aliondoka na kumwacha Balkis akijifanya anafagia, baada ya kuondoka tu, aliacha kufagia na kujishika kwenye paji lake la uso. Haikuchukua sekunde wajakazi kumi walikuwa mbele yake wakiwa wamepiga magoti.<br />
“Rabeka mwana wa mfalme una shida gani?” Waliuliza kwa pamoja.<br />
<br />
“Nataka mfanye usafi wa nyumba yote, sitaki kusikia harufu mbaya kama hii.”<br />
Mara moja wajakazi walianza kusafisha nyumba nzima, ilikuwa ajabu waliondoka vitu vyote vya ndani na kuviweka vipya na vyenye thamani kwa muda mfupi, ndani pakabadilika, pakapendeza na kuvutia kila kona ya nyumba ilinukia kwa harufu nzuri.<br />
<br />
Muddy alijikuta akitembea umbali mrefu kutafuta udi sehal, kila alipouliza watu hawakuujua. Alijikuta akikata tamaa na kuamua kurudi kumweleza Balkis kuwa udi wenye jina hilo kila alipouliza watu hawakuujua. Kutokana na kwenda umbali mrefu ilibidi wakati wa kurudi apande gari, jasho likimvuja kwa kutembea.<br />
<br />
Alipofika nyumbani aliingia ndani lakini alishtuka kukuta nyumba yake ikiwa imebadilika na kupendeza sana, aliviona vitu tofauti kiasi cha kuamini kuwa alikuwa amekosea, hakukuwa kwake. Alitoka nje ili akaitafute nyumba yake lakini mlangoni alikutana na Balkis akiwa amebeba siagi na jam.<br />
<br />
“Vipi mpenzi mbona nimekuona umeingia na unatoka?”<br />
“Ha! Hapa ni kwangu?” Alishtuka.<br />
“Eeh! Kwako, kwani vipi?”<br />
“Umefanya usafi mkubwa hivi kwa muda gani?””Usinione nipo hivi mimi ni mwanamke wa shoka.”<br />
<br />
“Na mbona kuna vitu vipya?”<br />
“Sasa kipi cha ajabu, yote haya nimeyapanga kwa muda mrefu, nilipokuwa nakuja kulala hapa. Nilimtuma mtu avilete vitu hivi, wakati unaondoka vilikuwa vinaingia.”<br />
“Sasa nyumba ikiuzwa?”<br />
<br />
“Achana na wazo hilo hebu nenda kaoge ufungue kinywa.”<br />
Muddy hakujibu kitu alichukua taulo na kwenda kuoga, nyumba ilikuwa ikinukia kama ujinini kwa akina Balkis. Muddy alipotoka kuoga alikuta chai imeshatayarishwa juu ya meza, ilikuwa tamu ambayo Muddy aliwahi kuinywa nyumbani kwa akina Balkis tu.<br />
<br />
Pamoja na kuisifia chai lakini Muddy kila alipomuangalia Balkis moyo wake haukuamini kama alikuwa na mwanamke mzuri kama yule tena tajiri mwenye mapenzi ya dhati kwake.</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf51eee3a89595327"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4fe4f0475985797">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.47.<br />
<br />
<br />
“Muddy nihakikishie kuwa huwezi kurudiana na Ashura?”<br />
“Nakuhakikishia kukupenda siku zote na kamwe sitarudiana na yule mwanamke muuaji.” “Muddy unayosema yanatoka moyoni au mdomoni?”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Yanatoka moyoni mwangu?”<br />
“Ukinigeuka?”<br />
“Nifanye lolote.”<br />
<br />
“Muddy kama unayosema ni kweli basi kitu nilichotaka kukifanya naachana nacho.”<br />
“Kipi hicho?”<br />
“Nilitaka kusimamia kesi yako kuhakikisha hawachukui kitu chochote.”<br />
“Kwa nini usifanye hivyo?”<br />
“Naacha ili maisha yako yakiwa mazuri mtu yeyote asikuguse.”<br />
“Kwa hiyo nitakuwa na maisha mazuri zaidi ya haya?” Muddy aliuliza.<br />
“Mara kumi ya haya.”<br />
<br />
“Usiniambie!”<br />
“Kwangu fedha si tatizo, ninachokitaka kutoka kwako ni mapenzi ya kweli, sihitaji kitu kingine.”<br />
“Nakuahidi utayapata hapa.”<br />
“Basi tegemea kuishi maisha ya raha mpaka kufa kwako.”<br />
“Asante mpenzi wangu,” Muddy alisema huku akimkumbatia Balkis.<br />
***<br />
Muda ulipofika Muddy aliitwa mahakamani na hukumu ilikuwa ile ile ya kugawana mali. Kwa vile alishaelezwa na Balkis maisha yake baada ya hukumu, hakuchanganyikiwa baada ya kuelezwa yale. Baada ya hukumu ile, Muddy pia alitakiwa kumlipa fidia ya fedha ambayo ilimfanya asipate kitu katika mali zitakazouzwa, vikiwemo gari na nyumba.<br />
<br />
Ashura alishangaa kumuona Muddy pamoja na pigo zito yupo katika hali ya kawaida. Baada ya hukumu Muddy alitoka nje ya mahakama na kwenda moja kwa moja kwa Balkis aliyekuwa akimsubiri. Muddy alishtuka kumuona Balkis akiwa pembeni ya gari la kifahari.<br />
“Karibu mpenzi.”<br />
“Asante.”<br />
“Pole na masaibu yote.”<br />
“Asante,” walikumbatiana, kitendo kile hakuna aliyekiona zaidi ya Muddy peke yake.<br />
“Nina imani mambo yamekwenda kama nilivyokueleza?”<br />
“Yaani umekuwa kama wewe ndiye uliyeyapanga yote, hakuna hata kimoja kilichokwenda kinyume.”<br />
<br />
“Basi huyo ndiye Ashura ambaye pia hilo si jina lake halisi.”<br />
“Una maana gani kusema hivyo?”<br />
“Nitakueleza, kila mwanaume aliyemchezea mchezo huu anamjua kwa jina hili lakini jina halisi anaitwa Shuuna.”<br />
“Ina maana hata hayo majina aliyotumia kwa hao mabwana wa awali unayajua?”<br />
“Nayajua.”<br />
“Alikuwa anaitwa nani?”<br />
“Twende kwanza nyumbani ukapumzike, mengine tutazungumza tukifika.”<br />
Muddy aliingia kwenye gari na kuondoka, kabla ya kuingia kwenye gari Ashura alishtuka kumuona Muddy na mwanamke mrembo aliyejitambulisha kuwa ndiye mkewe siku aliyokwenda kwake kumuonya.<br />
<br />
Alijikuta akikosa raha na kujiona wamefanya kazi bure sawa na kutwanga maji kwenye kinu. Waliona kama hawakufanya kitu na kujikuta akimuuliza mwanaume wake.<br />
“Yule mwanamke mwenye fedha Muddy kamtoa wapi?” Ashura aliuliza.<br />
<br />
“Hata mimi nashangaa, ni wazi wameanza uhusiano kipindi mkiwa wote.”<br />
“Ndiyo maana hata ilipotolewa hukumu hakushtuka.”<br />
“Hata mimi nilishangaa kuona anakubali kila kitu.”<br />
“Kwa hiyo tutakuwa tumefeli?”<br />
“Hapana, hatujafeli kwani tulivyovitaka tumevipata, ila kuna biashara nyingine nzuri,” mwanaume wa Ashura alisema.<br />
<br />
“Biashara gani?”<br />
“Tukafungue mashitaka ya kudai kuhujumiwa penzi lako lililosababisha muachane na mumeo wakati bado unampenda.”<br />
“Aisee, wazo zuri sana! Kweli wewe bwana mipango, sasa mpango huo tuufanye lini?”<br />
<br />
“Kwanza tupajue wanapoishi ili tufanye mpango wa kufungua mashitaka.”<br />
“Hilo wazo, mbona mwaka huu tutatengeneza fedha mpaka zitukimbie.”<br />
“Hiyo ndiyo kazi yetu.”<br />
“Lakini Mussa kuna jambo nimekumbuka.”<br />
“Jambo gani hilo?”<br />
<br />
“Unakumbuka yule mwanamke alivyotuonya kuhusu tabia yetu kuwa itatutokea puani?”<br />
“Sasa wewe unamuogopa, atatufanya nini mwanamke yule?”<br />
“Mmh! Nashangaa moyo unanienda mbio nilipomkumbuka.”<br />
“Si kwa vile amekuchukulia mumeo.”<br />
<br />
“Yule si mume wangu nilikuwa naye kibiashara zaidi.”<br />
“Basi mpango wa haraka ni kudili na Muddy kuhakikisha anaokota makopo.”</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4fe4f0475985797"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4fe4f0475985797"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4fe4f0475985797"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4fe4f0475985797"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4fe4f0475985797"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4fe4f0475985797"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4f65f4b74413904">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.48.<br />
<br />
<br />
<br />
Wakati wakipanga kuchukua fedha za Balkis, muda huo Muddy alikuwa akikaribishwa kwenye jumba la kifahari.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Karibu mpenzi wangu hapa ndipo kwako ishi kwa furaha na mapenzi ya kweli,” Balkis alimkaribisha kwa sauti tamu.<br />
“Ha! Siamini.”<br />
<br />
“Hata lile gari ni lako.”<br />
“Usiniambie!” Muddy alizidi kupigwa na butwaa.<br />
“Ukweli ni huo, leo usiku kutakuwa na sherehe fupi ya kufunga ndoa yetu ili uweze kunitumia kihalali kama mkeo.”<br />
<br />
“Hakuna tatizo, asante sana mpenzi.”<br />
Muddy alishukuru kwa kupiga magoti huku machozi yakimtoka na kujiuliza bila ya Balkis maisha yake yangekuwaje baada ya kufanyiwa utapeli na Ashura. <br />
<br />
**** <br />
Ashura na mwanaume wake baada ya kutoka mahakamani waliongozana na madalali kwenda kuuza mali za Muddy zikiwemo gari na nyumba siku ile ile, kutokana na mipango iliyopangwa mapema. Baada ya kufanikiwa kuuza gari na nyumba waliendelea kufurahia mafanikio yao kufuatia kazi yao ya utapeli na kujipanga kwa ajili ya kupambana na Balkis kuhakikisha wanapata fedha kupitia kwa Muddy.<br />
<br />
Pamoja na kupata vitu walivyovitaka kutoka kwa Muddy, bado Ashura moyo wake ulikosa raha, alijiuliza atamtazamaje Muddy siku wakikutana kutokana kuonekana ameingia kwenye maisha mazuri tofauti na awali walipokuwa pamoja.<br />
<br />
Baada ya kumuacha Muddy na kuonesha kuchanganyikiwa, alitegemea kusikia amejinyonga. Kufuatia kupona kifo hicho, Ashura alitegemea siku ya hukumu angemuona Muddy akitoka mahakamani na kuanza kuokota makopo, lakini ilikuwa ni kinyume na mategemeo yake.<br />
<br />
Wasiwasi wake Muddy lazima angelipa kisasi, wazo lake lilikuwa kumuwahi kabla hajawahiwa yeye. Akiwa amekaa na mwanaume wake, Ashura alimueleza jambo:<br />
“Mussa nina jambo linaniumiza akilini mwangu.”<br />
“Lipi tena mpenzi?”<br />
<br />
“Nina wasiwasi na Muddy kutulipizia kisasi.”<br />
“Ni kweli hata mimi nilikuwa na wazo hilo.”<br />
“Sasa tufanye nini kabla hajafanya lolote, maana akitulia atajipanga na yule dada anaonekana ana fedha hivyo anaweza kutufanyia kitu kibaya.”<br />
“Ondoa hofu hawawezi kutufanya lolote zaidi ya sisi kuwamaliza wao.”<br />
“Hayo ndiyo maneno.” Ashura alipata faraja.<br />
***<br />
Wakati Ashura na Musa wakipanga mipango yao, usiku wa siku ile ufukweni mwa Bahari ya Hindi maeneo ya Daraja la Salenda kulikuwa na sherehe kubwa ya harusi kati ya Balkis na Muddy. Katika kundi la watu wote waliokuwepo kwenye sherehe ile Muddy peke yake ndiye aliyekuwa mwanadamu, lakini waliobakia walikuwa majini.<br />
<br />
Lakini hakuwajua kwa vile walikuwa katika maumbile ya kibinadamu, Muddy alimuoa rasmi Balkis na kuwa mkewe wa halali. Ilikuwa sherehe kubwa kuwahi kutokea katika maisha ya Muddy. Baada ya harusi walilala kwenye kitanda cha bembea kilichowabembeleza mpaka kunakucha.<br />
<br />
*****<br />
Taarifa ya ndoa ya Balkis ilifika chini ya bahari kwa Mfalme Barami Hudirud, kitendo kile kwake alikiona kama ni dharau kutoka kwa mwanaye kufunga ndoa na mwanadamu. Alimfuata mkewe aliyekuwa amekaa kwenye bustani akibembea kwenye kiti.<br />
<br />
“Mama Balkis,” alimwita kwa sauti ya juu iliyomshtua.<br />
“Mtukufu Mfalme wa chini ya bahari, mbona sauti kali, kuna usalama?”<br />
“Mwanao ananitafuta nini?”<br />
<br />
“Kwani kafanya nini tena mtukufu mfalme?”?”Tunamkataza nini na anafanya nini?”<br />
“Amefanya nini?”<br />
“Anaweza kuvunja amri yangu?” Mfalme Barami alisema huku akipiga ngumi kifuani kwa hasira.<br />
<br />
“Mume wangu, lakini si bado anaendelea kuleta vizazi vya wanawake?”<br />
“Kwa nini ameolewa na mwanadamu?”<br />
“Ha! Ndiyo kafanya hivyo!” Malkia Huleiya alishtuka.<br />
“Eeh! Tena nasikia watwana na vijakazi walikuwepo kwenye harusi hiyo.”<br />
“Usiniambie!”<br />
<br />
“Kwa jinsi alivyovunja amri yangu, wote waliohudhuria harusi ile watakutana na adhabu kali,” alisema kwa hasira mpaka povu likamtoka mdomoni.<br />
“Mume wangu usimguse mtu yeyote ni wewe uliyempa amri mwanao kwa watwana na vijakazi juu ya kuheshimu amri zake.”<br />
<br />
“Basi kama sivyo hivyo nitamtuma mtwana mkuu Muhuru akammalize huyo mwanaume.”<br />
“Bado hujatumia busara, kumbuka kosa lako lolote litatugharimu, kitendo cha kukataa kumuondoa mwanaume wa kwanza huku kilizua patashika na ulipotaka kumuua ulisikia alichosema mwanao. Hivi umuue huyu aliyefunga naye ndoa itakuwaje?”<br />
<br />
“Sasa kuna haja gani kuendelea kuleta vizazi vya wanawake wakati ameishajiamulia kuolewa na mwanadamu?”</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4f65f4b74413904"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4f65f4b74413904"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4f65f4b74413904"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4f65f4b74413904"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4f65f4b74413904"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4f65f4b74413904"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4f65f4b74413904"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4ef0a3722015942">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.48...B<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
“Bado hujatumia busara, kumbuka kosa lako lolote litatugharimu. Kitendo cha kutaka kumuondoa mwanaume wa kwanza huku kukiwa na patashika ulipotaka kumuua ulisikia alichosema mwanao. Hivi umuue huyu aliyefunga naye ndoa itakuwaje?”<br />
“Sasa kuna haja gani kuendelea kuleta vizazi vya wanawake wakati ameshajiamulia kuolewa na binadamu?”<br />
<span class="text_exposed_show"> SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Labda ana sababu zake, ngoja akija tumuulize.”<br />
“Hakuna cha kumsubiri, tumtume Muhuru aende akamwite mara moja.”<br />
“Siamini, kama jana kafunga ndoa leo aje huku, hebu kuwa na subira mume wangu.”<br />
Walikubaliana kumsubiri ili aje awaeleze kwa nini amevunja amri ya mfalme wa bahari, tena akiwa binti wa mfalme.<br />
<br />
BAADA YA MIEZI MIWILI<br />
Maisha ya Muddy yalibadilika ghafla, kila aliyemuona alimshangaa. Mmoja kati ya watu waliomshangaa alikuwa ni Ashura aliyemuona akitoka super market akiwa ameongozana na Balkis katika mwonekano wa mahaba mazito. Roho ilimuuma na kujikuta akipata wivu wa kutaka kuwa na Muddy.<br />
Aliamini kuwa kilio cha Muddy alichokitoa siku alipomuacha, kama angemuomba warudiane angeweza kukubali. Alipanga kumtafuta na kumuomba msamaha.<br />
<br />
Ashura aliamua kumtafuta Muddy kwa udi na uvumba kila kona ya mji. Lakini alishangaa kila alipomuona Muddy na kumfuata alipomkaribia Balkis alitokea bila kujua ametokea wapi, kitu ambacho kilimkosesha amani ya moyo wake. Hata alipojaribu kumfuatilia kwa nyuma alimpotea kimiujiza. Aliamini njia rahisi ya kumrudisha mikononi mwake ni kwenda kwa mtaalam wake aliyekuwa anakaa Mbagala Kimbangulile, Mzee Chujio.<br />
<br />
Aliwasha gari na kuelekea Mbagala kwa mtaalam ili akamvute tena Muddy kama alivyofanya mwanzo na kupelekea kuisahau familia yake. Alipofika Mtoni kwa Azizi Ali dada mmoja aliomba msaada kwenye gari lake. Hakutaka kumnyima lifti, alimsaidia.<br />
<br />
“Unafika wapi dada yangu?” alimuuliza baada ya kuingia kwenye gari na kufunga mlango.<br />
“Mbagala Zakheem,” alijibu yule dada kwa sauti ya chini.<br />
“Ooh! Mimi nafika mbele, nitakushusha kituoni.”<br />
“Nitashukuru.”<br />
<br />
Wakati safari ikiendelea mwanamke aliyeomba msaada alianzisha mazungumzo.<br />
“Dada yangu huku ni mwenyeji?”<br />
“Hapana nakwenda kumuona mtu mmoja Mbagala mwisho.”<br />
“Nani mganga Chujio?”<br />
“Mmh!” Ashura alishtuka.<br />
<br />
“Mbona umeshtuka?”<br />
“Walaa, siendi huko.”<br />
<br />
“Lakini dada shida ya nini kumuendea Muddy kwa mganga wakati mmekwisha achana?” Kauli ile ilimshtua sana Ashura.<br />
“Nani amekwambia mimi nakwenda kwa mganga, pia habari za Muddy nani kakueleza?”<br />
Ashura alishtuka kujiona yupo uchi japo amevaa nguo, alijuta kumpa lifti yule mwanamke ambaye aliharibu safari yake yote.<br />
<br />
“Ashura,” mwanamke aliyepewa lifti kwenye gari alimwita jina lake.<br />
“Ha! Umejuaje jina langu?” Ashura alizidi kumshangaa mtu aliyempa lifti kwa kumjua kwa mapana.<br />
<br />
“Nijue unataka kufanya nini nitashindwa kujua jina lako? kwanza jina lako si Ashura.”<br />
“Kama siitwi Ashura naitwa nani?”<br />
“Shuuna.”<br />
<br />
“Mungu wangu! Umenijuaje?”<br />
Ashura nusura aliingize gari kwenye mtaro kwa mshtuko, ilibidi alisimamishe pembeni maeneo ya Mbagala Misheni.<br />
<br />
“Kwani kuna siri, la muhimu achana na Muddy endelea na maisha yako, pia mpango wenu wa kumfuatilia Muddy na mkewe mtaokota makopo ninyi kabla ya huyo Muddy.”<br />
“Wewe ni nani?” Ashura alimuuliza huku jasho likimtoka.<br />
“Mke wa Muddy,” sauti ilijibu pembeni.<br />
<br />
“Muongo...Ha!” Ashura alijibu huku akigeuka kumtazama aliyejiita mke wa Muddy, wakati huo manukato makali yalinukia ndani ya gari. Hakuamini kumuona mtu aliyempa lifti amebadilika na kuwa mke wa Muddy, Balkis.<br />
<br />
“Punguza hofu, sipo hapa kwa shari bali kukuonya kwa kitu unachotaka kukifanya, kumbuka nilikuuliza mapema kuhusu kurudiana naye nawe ulinihakikishia hutarudiana naye tena.<br />
<br />
“Sasa sikiliza Ashura, huenda utashangaa kuniona hapa. Sitaki kujieleza sana, ila ukitaka vita na mimi ambavyo najua hutaweza kushinda endelea na mambo yako. Nitakufanya kitu kibaya ambacho kitabakia katika kumbukumbu zako mpaka unafukiwa chini.<br />
<br />
“Mwambie na mpumbavu mwenzako mpango unaopanga wa kutaka kuichukua mali yangu mtakufa kifo kibaya. Leo sikuja kwa shari nimekuja kistaarabu. Mara ya pili utashangaa na hutaamini kuwa ni mimi,” Balkis alisema kwa sauti kali kidogo iliyomtisha Ashura.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4ef0a3722015942"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4ef0a3722015942"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4ef0a3722015942"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4ef0a3722015942"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4ef0a3722015942"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4ef0a3722015942"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.49<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
“Sasa sikiliza Ashura huenda utashangaa kuniona hapa, sitaki kujieleza sana ila ukitaka vita na mimi najua huwezi, nitakufanyia kitu kibaya ambacho kitabakia katika kumbukumbu yako mpaka unafukiwa chini.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
“Mwambie na mpumbavu mwenzako kwamba mpango mnaoupanga wa kutaka kuzichukua mali zangu mtakufa kifo kibaya. Leo sikuja kwa shari bali kwa ustaarabu, mara ya pili utanishangaa, hutaamini kuwa ni mimi,” Balkis alisema kwa sauti kali kidogo iliyomtisha Ashura. SASA ENDELEA...<br />
<br />
Baada ya kusema maneno yale, Balkis aliufungua mlango wa gari na kutoka nje huku akifyonya kwa sauti kali, alipolizunguka gari akatoweka.<br />
Baada ya kuondoka eneo lile, Ashura alishtuka kama mtu aliyetoka usingizini na kujiuliza alichokiona na kukisikia kama kilikuwa ni cha kweli au alikuwa akiota.<br />
<br />
Wazo lililomjia haraka aliamini kabisa kuwa ile ilikuwa ni ndoto, aliamua kwenda kwa mganga kupata tiba ya kumrudisha Muddy mikononi mwake.<br />
Alijishangaa mwanaume aliyemgeuza mradi amekuwa kero moyoni mwake kila dakika alijikuta akimpenda na kumtamani kuwa naye tena.<br />
<br />
Aliendesha gari huku akiapa kutompa msaada kiumbe yeyote kwa kuhofia kukutana na matatizo ambayo bado aliamini kuwa ni ndoto.<br />
Hakuamini kama mtu angeweza kugeuka mara mbili katika hali ya kawaida, kwake alijua ile ilikuwa ni ndoto mbaya tu.<br />
<br />
Alipofika Mbagala Rangi Tatu alikata kushoto na kuelekea Kimbangulile, alipofika kwa mganga alishangaa kukuta watu wakiwa wamejaa kuonesha kulikuwa na jambo.<br />
<br />
Alisimamisha gari mbali kidogo na nyumba ya mganga na kuteremka kisha akajisogeza kwenye kundi la watu ambapo kila mmoja alikuwa akisema lake. Alimsikia mmoja akisema;<br />
“Lazima yule atakuwa ni jambazi aliyefanyiwa kitu kibaya na mganga.”<br />
“Hapana mbona hakutoka mle ndani yule lazima atakuwa ni jini tu.”<br />
<br />
Yalikuwa naneno yaliyomchanganya Ashura na kujiuliza mganga amefanya nini, ilibidi amwite pembeni dada mmoja ili apate kumhoji vizuri.<br />
“Samahani dada yangu kuna nini?”<br />
“Mmh! Kuna jambo limetokea linawachanganya watu wengi.”<br />
“Jambo gani?”<br />
<br />
“Mzee Chujio ameuawa.”<br />
“Mzee Chujio gani?”<br />
“Yule mganga.”<br />
“Mganga?” Ashura aliuliza kwa mshtuko.<br />
“Eeh, unamfahamu?”<br />
<br />
“Sasa dada yangu nani asiyemjua mzee Chujio sehemu hii?”<br />
“Basi ndiyo hivyo, ameuawa katika mazingira ya kutatanisha.”<br />
“Una maana gani?”<br />
<br />
“Nasikia kuna dada mmoja mrembo alikuja na kuingia ndani kwa mganga na kuwaacha wateja wachache wakiwa kwenye foleni. Lakini inasemekana hakutoka, baada ya wateja kusubiri kwa muda bila kusikia wakiitwa ndani waliamua kuingia lakini cha ajabu wakamkuta mganga amelala chini akiwa amekufa na kutoka funza mdomoni kama aliyefariki wiki moja iliyopita.”<br />
<br />
“Funza mdomoni?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Sasa jamani mtu wa kutoka funza si mtu aliyekufa zaidi ya wiki?” Ashura alisema kwa mshtuko.<br />
“Hapo ndipo watu walipochanganyikiwa na kuamini kuwa yule mwanamke mzuri alikuwa ni jini.”<br />
<br />
“Jini! mna maana gani?”<br />
“Wanasema alikuwa mzuri sana, tena alikuwa akinukia na alipoingia ndani hakutoka.”<br />
“Alivaa nguo gani?”<br />
“Mmh! Hebu muulize yule dada aliyesimama katikati ya watu,” alimuonesha dada mmoja aliyekuwa akizungumza na watu huku akilia na kuweka mikono kichwani.<br />
“Naomba uniitie.”<br />
<br />
Yule binti alimfuata yule dada aliyekuwa akizungumza huku akitokwa na machozi, baada ya kusogea karibu ya Ashura, ilibidi ajitambulishe kuwa ni mmoja wa wateja wa mzee Chujio mtu aliyemtegemea kwenye mambo yake.<br />
“Samahani mdogo wangu hata mimi nilikuwa nimekuja kwa mzee Chujio lakini kuna habari zimenichanganya sana. Nini kimemsibu mganga wetu?”<br />
<br />
“Dada yangu hata kuzungumza nashindwa, siku tano zilizopita mzee Chujio alinisaidia matatizo yaliyonitesa kwa miaka kumi. Dawa alizonipa zilinionesha yote aliyonieleza, dada yangu walimwengu ni wabaya, niliteswa na mke mwenza na kufikia hatua ya kunuka mwili mzima hata kukaa mbele za watu nilikuwa siwezi.<br />
<br />
“Nilitengwa na watu, wanaume walinipenda kwa kuniona, lakini waliponisogelea walikuwa wakikimbia kutokana na harufu kali kama ya mzoga uliooza. Leo dada yangu nilikuwa nafuata dawa na kupatiwa kinga baada ya awali kuondolewa tatizo langu.<br />
<br />
“Ajabu wakati nasubiri kuingia kwa mganga alipita dada mmoja mrembo na kuingia ndani bila kufuata foleni. Kwa vile ilikuwa ni zamu yangu nilitaka kumfuata ndani kumtoa kwani hakuonesha ustaarabu, lakini wenzangu walinisihi nikamuacha amalize shida yake ndipo nami niingie.<br />
“Baada ya muda kidogo tulisikia watu wakibishana, kauli ya mganga ilikuwa ya juu akionesha kuna kitu hakukubaliana na yule mwanamke mrembo mwenye kunukia manukato.<br />
<br />
“Mganga alisema hawezi kufundishwa kazi na mtu, mara tulisikia sauti ya yule mwanamke mrembo akisema kuwa hana jinsi ile ndiyo zawadi yake.<br />
“Baada ya hapo kilipita kimya kirefu huku muda ukizidi kuyoyoma.<br />
<br />
“Baada ya nusu saa bila kusikia mazungumzo wala yule mwanamke mrembo kutoka, niliamua kuingia ndani kujua kilichokuwa kikiendelea.<br />
“Nilipoingia nikamkuta mganga akiwa amelala chini, kilichonishtua zaidi ni funza waliokuwa wakimtoka mdomoni kama mtu aliyekufa muda mrefu.”</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4dae93542289800">JIINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.50<br />
<br />
<br />
<br />
“Funza?” Ashura aliuliza tena japo taarifa ya kutoka funza alielezwa mapema.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Funza dada, kama mtu aliyekufa muda mrefu.”<br />
<br />
“Unataka kuniambia kabla ya kutokea tukio lile ulionana naye?”<br />
“Tena alitoka nje na mgonjwa aliyekwenda kumfanyia tiba nyuma ya nyumba yake, aliponiona alitaka kujua hali yangu, nilimweleza ninavyoendelea na kuniambia vitu vyote alivyovitafuta kwa ajili ya kazi yangu vimepatikana...Yaani..,” Kufikia pale yule dada aliangua kilio mikono kichwani, Ashura aliingia kwenye kazi ya kumbembeleza.<br />
<br />
“Mdogo wangu hebu nyamaza kwanza.”<br />
“Dada inauma, haiwezekani niwe miye, nimeteseka muda mrefu, napata tiba mganga anauawa katika mazingira ya utata,” aliendelea kulia kilio cha kukata tamaa. Ashura, japo alijitahidi kujikaza na kumbembeleza kwa kumlalia kifuani, lakini moyoni alikuwa na maumivu makali kama angepata sehemu iliyojificha, basi naye angeangua kilio ambacho hakuna mtu ambaye angeweza kumbembeleza.<br />
<br />
Kifo cha mzee Chujio kilikuwa pigo kubwa maishani mwake, ndiye aliyekuwa tegemeo lake katika mambo yote aliyoyafanya ya kuwatapeli wanaume kwa kuwapumbaza kwa dawa. Alijiuliza nani atakayemsaidia katika maisha yake baada ya kifo cha mzee Chujio ambaye alimgeuza kama Mungu wa pili.<br />
<br />
“Unasema ulimuona?” Ashura kwa kuchanganyikiwa alijikuta akiuliza swali alilojibiwa awali.<br />
“Ndiyo.”<br />
“Unasema alipoingia ndani hakutoka?”<br />
“Ndiyo.”<br />
“Au wakati anatoka huyo mwanamke ulikuwa umesinzia?”<br />
“Dada yangu kusinzia tusinzie wote tulio<br />
kuwa tunasuburi huduma?”<br />
“Alivaa nguo gani?”<br />
“Gauni refu jekundu lenye maua shingoni na kifuani, sielewi maua yale ya rangi gani kutokana na kumeremeta.”<br />
“Mmh! Shingoni alikuwa na mkufu wenye herufi M?”<br />
“Eeeh.”<br />
“Mtandio wake wa bluu yenye maua ya kumetameta?”<br />
“Huo huo!”<br />
“Ana kipini cha mkufu?”<br />
<br />
“Eeeh dada, umemjuaje?”<br />
“Mmh! Kazi ipo,” Ashura aliguna na kusema kwa sauti ya chini.<br />
“Kwani unamfahamu?”<br />
“Kuna mtu nilikutana naye njiani uliponielezea alivyovaa nilikisia basi lazima atakuwa yeye.”<br />
“Kwa hiyo si jini kama watu wanavyomdhania?”<br />
<br />
“Mmh! Sijajua, kwani hakuna mlango wa kutokea nyuma?”<br />
“Dada kama wewe ni mteja wa mzee Chujio, chumba chake unakijua, mlango utoke wapi?”<br />
“Mna uhakika hakutoka?”<br />
“Angetoka tungemuona kama si mimi basi wenzangu wangemuona.”<br />
“Mmh! Nina wasiwasi alitoka hamkumuona.”<br />
<br />
<br />
“Sawa alitoka, kile kifo nacho cha muda mfupi mtu aoze na kutoka funza kwa sekunde chache kinatokana na nini?”<br />
“Inawezekana alimnywesha sumu kali iliyomuozesha tumboni na kuzalisha funza.”<br />
“Mmh! Labda.”<br />
<br />
“Basi dada, acha nirudi zangu hata mimi nimechanganyikiwa sana.”<br />
“Sawa dada, lakini mimi ndiye nimechanganyikiwa hata kuliko familia yake.”<br />
Wakati huo polisi walifika kuchukua mwili wa marehemu, alishuhudia mwili wa mzee Chujio ukitolewa huku familia yake na wateja wakiangua vilio.<br />
<br />
Ashura alishindwa kujizuia, alikimbilia kwenye gari lake na kujifungia, alilia hadi macho yakamvimba. Alijiuliza yule mwanamke atakuwa nani, japo ilikuwa vigumu kukubali kuwa Balkis ni jini, lakini mambo yaliyomtokea kwenye gari alipombadilikia kama kinyonga yalimfanya aanze kuamini kabisa mke wa Muddy ni jini.<br />
<br />
“Mungu wangu Muddy atakuwa ameoa jini?” Alijikuta akipayuka kwa sauti.<br />
“Haiwezikani lazima nifanye chini juu nimtoe kwenye balaa lile.”<br />
Ashura alijiingiza kwenye vita nyingine ya kujua hatima ya Muddy kwa Balkis kwa kuamini kuna njia ya kuyafukuza majini. Aliwasha gari lake na kurudi nyumbani.<br />
*duh!!tamuje??<br />
<br />
ITAENDELEA KESHOOOOO...........</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123baf4e2c17f28187542"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b30605850346207">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis).........EP.51.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
Katika kutembeza macho aliwaona wajukuu wa mzee Njiwa wakicheza nje ya uzio, aliona kama atamuua mmoja basi mzee Njiwa Manga ataacha kazi ya kuwatibu ili ashughulikie msiba na kuwafanya Ashura na mwanaume wake kuondoka ili warudi siku nyingine. SASA ENDELEA...<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Aliamini kama watatoka bila kupatiwa kinga yoyote angetumia nafasi ile kuwamaliza wote ili aweze kuishi na Muddy bila tatizo japo alijuwa kwa upande wa baba yake kulikuwa na vita nyingine.<br />
<br />
Kila alivyotaka kuteremka roho ilimkataza kwa kuwaonea huruma viumbe wasio na hatia.<br />
<br />
Kutokana na uwezo wake aliweza kuyasikia yote yaliyokuwa yakizungumzwa ndani na kupanga kama atakubaliana nao kabla ya kuwapa kinga naye, hatakuwa na budi kuua mtoto mmoja.<br />
<br />
Ashura na mwanaume wake waliingia katika chumba cha mzee Njiwa Manga na kukaa kwenye mkeka.<br />
“Karibuni,” mzee Njiwa Manga aliwakaribisha.<br />
“Asante,” walijibu kwa pamoja.<br />
<br />
“Mh! Niwasaidie nini?”<br />
“Mzee tunahitaji msaada wako, tuna vita nzito na mwanamke mmoja jini.”<br />
<br />
”Mmejuaje ni jini wakati majini hayaonekani?”<br />
<br />
“Anatutokea katika umbile la kibinadamu na wakati mwingine katika maumbile tofauti, pia tunatokewa na mambo ya kutisha.”<br />
<br />
“Tena jana kamuua mganga mmoja Mbagala kifo cha kutisha,” Ashura aliongezea.<br />
<br />
“Mmh! Majina yenu?” Aliwauliza huku akichukua kibao cheusi na chaki.<br />
<br />
“Naitwa Shuuna.”<br />
<br />
“Shuuna...” mganga alilirudia jina lile kwa sauti ya chini huku akiliandika kwenye kibao.<br />
<br />
“Mbona unaonekana una majina mengi?” Mganga Njiwa Manga alimuuliza Ashura.<br />
<br />
“Lakini hili ndilo langu la kuzaliwa.”<br />
<br />
“Sasa nikusaidie kwa jina gani kwani yote uliyatumia na watu tofauti wanakujua kwa majina hayo?”<br />
<br />
“Kwa sasa natumia jina hili.”<br />
<br />
“Kama ukifanikiwa kurudi kwa Muddy utatumia jina gani?”<br />
<br />
Swali lile lilimfanya Ashura akae kimya na kukosa la kujibu kwa kuona kama siri yake inatoka nje.<br />
<br />
“Lakini mzee suala la Muddy tulishaachana nalo, kama kutusaidia msaidie kwa jina la Shuuna,” Tonny aliingilia kati mazungumzo.<br />
<br />
“Najua mmekuja pamoja lakini kila mmoja ana mawazo yake ambayo sitaki kuyaingilia kwa vile siyo kazi yangu,” mzee Njiwa Manga alijibu kwa fumbo lililomuacha gizani Tonny bila kujua dhamira ya Ashura kwa Muddy ilikuwa nini.<br />
<br />
“Naomba niachane na mwenzako kwanza, hebu nawe nieleze jina lako?”<br />
“Naitwa Antony.”<br />
“Antoniii,” alilirudia jina lile kwa sauti ya chini huku akiliandika kwenye ubao.<br />
Baada ya kuandika alitulia kwa muda akiandika vitu kwenye ubao na kukohoa kidogo kisha akauliza:<br />
<br />
“Nimeona yote, sasa shida yenu nini hasa?”<br />
<br />
“Mzee kama tulivyokueleza kuwa tuna tishio la mwanamke mmoja ambaye ni jini, anatishia maisha yetu.”<br />
<br />
“Kwa hiyo mnataka nini?”<br />
<br />
“Tunataka utukinge ili tuweze kupambana naye.”<br />
“Mnamjua jina lake?”<br />
<br />
“Balkis,” Ashura alijibu.<br />
Mganga aliliandika jina lile, kama kawaida alilirudia kwa sauti ya chini.<br />
“Balkis...Balkis.”<br />
Baada ya kutulia kwa muda alisema:<br />
“Lakini mbona mimi sioni madhara ya huyu mnayemuogopa?”<br />
<br />
“Mzee huyu ni mtu mbaya sana, amenitokea mara nyingi kwenye gari katika sura tofauti na kutishia maisha yetu,” Ashura alisema huku macho yamemtoka pima kwa kusistiza.<br />
<br />
“Mbona hapa panaonesha jini huyo ni mpole sana kuliko majini wengine?”<br />
<br />
“Si kweli, ana roho mbaya sana, amemuua mzee Chujio kifo kibaya sana,” Ashura alisema.<br />
“Unajua sababu ya kuuawa mzee Chujio?” mganga aliuliza.<br />
<br />
“Kutokana na maelezo ya huyo mwanamke jini anasema aliingilia kazi yake na kuwa mbishi ndio akaamua kumfanya vile.”<br />
<br />
“Sasa hamuoni na mimi nikiingilia kazi si yangu anaweza kunifanya kama mzee Chujio?”<br />
<br />
“Hawezi.”<br />
<br />
“Kwa nini asiweze?”<br />
<br />
“Tunasikia wewe ndio kiboko ya majini.”<br />
<br />
“Ni kweli kazi yangu ni kutibu na si kushindana na majini.”<br />
<br />
“Lakini mzee kazi yako si kutusikiliza wateja shida yetu na kukupa kiasi ukitakacho,” Tonny alimueleza mganga..<br />
<br />
“Sikiliza kijana, mimi si mchawi ni mganga wa kuwasaidia wenye matatizo, ndiyo maana nipo mpaka leo.Waganga wengi wamepoteza sifa zao kutokana na kuingilia kazi ya wachawi.<br />
<br />
“Tumekuwa tukifanya makosa ya kuingia kwenye kazi ya kutesa, kuua au kuingia kwenye vita na viumbe kama majini ambayo wakati mwingine huwa hayana matatizo na watu.”<br />
<br />
“Sasa mzee utatusaidiaje?”<br />
<br />
“Mpaka sasa sijajua shida yenu nini?”<br />
<br />
“Tunataka kinga ili tusiweze kudhuriwa na jini.”<br />
<br />
“Jini gani wa kuwadhuru ninyi?”<br />
<br />
“Balkis,” Ashura alijibu.<br />
<br />
“Balkis atawadhuru vipi bila ninyi kumchokoza?”<br />
<br />
“Yule hana cha kumchokoza bali huamua kuua bila sababu,” Ashura alitengeneza uongo.<br />
<br />
“Sitawapa dawa yoyote zaidi ya kauli ya Balkis mwenyewe.”<br />
<br />
“Mbona hatukuelewi, kauli gani?”<br />
<br />
“Mtaisikia muda si mrefu kutoka kwake Balkis.”<br />
<br />
Mzee Njiwa alitoka nje na kurudi na kitezo chenye moto, akakiweka mbele yake, akatoa mavumba kwenye chupa kisha akasema:<br />
<br />
“Hii dawa kazi yake kuyavuta majini mazuri, kama Balkis ni jini mbaya hatakuja nikimwita.”<br />
<br />
Baada ya kusema vile alianza kuweka mavumba kwenye moto huku akisema:<br />
<br />
“Balkis binti mfalme wa bahari, naamini wewe ni jini mwema nakuomba uje mbele yangu, lakini kama si jini mwema ukiingia himaya yangu ndiyo mauti yako...Balkis njoo mbele ya wanadamu hawa wana mashtaka juu yako.”<br />
<br />
Je, Balkis ni jini mzuri au mbaya?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b30605850346207"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b30605850346207"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b30605850346207"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b30605850346207"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b30605850346207"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b30605850346207"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis).........EP.52.<br />
<br />
<br />
“Nimewaonesha ishara nyingi za vitisho ili wajue mimi si kiumbe wa kawaida ili wachane na mimi, lakini wamekuwa wabishi, kabla ya kuja huku niliwapa onyo zito lakini wamekuwa kama kenge, hawasikii mpaka watoke damu masikioni.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Tena wana bahati kubwa leo ningepata dhambi nyingine, wakati natoka nyumbani niliwaona wamekaribia kwako lakini kasi yangu ilichelewa kidogo na kuwakuta wameshaingia kwenye ngome yako.<br />
<br />
<br />
“La sivyo kama ningefanikiwa kuwatia mikononi ningewaulia mlangoni kwako na kama ungewasikiliza na kuwapatia tiba kabla tiba yao haijatimia ningemuua mjukuu wako mmoja ili uhalalishe kazi hii na wangetoka ningewamalizia mbali,<br />
<br />
” Balkis alisema kwa sauti isiyotaka mzaha, huku kauli yake ikizidi kuwatisha moyoni walioomba msaada wa mzee Njiwa Manga.<br />
<br />
<br />
“Nimekuelewa sana Balkis binti wa mfalme Barami, sasa ulikuwa unataka nini?”<br />
“Kama nilivyowaeleza waachane na mimi, waendelee na maisha yao.”<br />
“Wakifanya hivyo utakuwa na vita nao?”<br />
<br />
<br />
“Niwe nao ili iwe nini ikiwa kila mmoja na maisha yake, ila tofauti ya hapo nitakachokifanya Mungu anajua.”<br />
“Nina imani mmesikia yote aliyosema Balkis, niliwaeleza ni mpole mwenye huruma na upendo kwa viumbe wenzake.<br />
<br />
Napenda kuwaeleza kuwa maelezo yake ndiyo tiba yenu na mkitoka hapa mkienda kinyume na haya aliyosema, nisione mtu hapa, mtamalizana wenyewe, mmenisikia?”<br />
<br />
<br />
Alijibu kwa kunyanyua vichwa kwani hata midomo ilikuwa mizito, baada ya majibu yao ya kibubu mzee Njiwa Manga alimgeukia Balkis.<br />
<br />
<br />
“Nina imani wamekuelewa ila wakienda kinyume mimi simo.”<br />
“Wewe unasema hivyo lakini mioyo yao imejaa tamaa ya mali na uhai wa watu, narudia tena sitawaua ila nitawaadhiri mbele za watu, hilo litakuwa pigo kubwa na mkizidi nitawageuza mbwa.”<br />
<br />
<br />
“Nimekuelewa sana Balkis unaweza kwenda,” mzee Njiwa Manga alisema.<br />
<br />
<br />
Baada ya kuruhusiwa kutoka alinyanyuka na kutoka chumbani katika umbile la kibinadamu, wote walimsindikiza kwa macho hadi nje.<br />
<br />
<br />
<br />
Waliokuwa wamekaa nje kusubiri huduma macho yao yalishuhudia mwanamke mzuri akipita mbele yao huku wakijiuliza amepita saa ngapi kutokana na watu wengine kuwepo kwa muda mrefu. Balkis baada ya kutoka katika uzio wenye nguvu wa mzee Njiwa Manga alitoweka.<br />
<br />
<br />
Baada ya kuondoka Balkis, mzee Njiwa Manga aliwageukia wateja wake na kusema:<br />
“Nina imani tatizo lenu limekwisha?”<br />
“Mzee litakwisha vipi wakati umemsikia mwenyewe amesema nini,” Tonny alihoji.<br />
“Kasema nini?”<br />
“Si amesema tukifuatilia mambo yake atatugeuza mbwa,” Ashura alijibu.<br />
“Sasa mnataka kufuatilia mambo yake?”<br />
“Hapana.”<br />
“Sasa tatizo nini?”<br />
“Tulikuwa tunaomba kinga.” Tonny alisema.<br />
“Ya nini?”<br />
“Ili tujikinge na matatizo ya wanadamu na majini.”<br />
“Ili?”<br />
“Mzee kama hujui kazi yako, kwani wanadamu wanakuja kwako kutafuta nini?”<br />
“Tiba ya matatizo yao.”<br />
“Sasa mbona hutaki kutusaidia?”<br />
“Kwani shida yenu iliyowaleta hapa ni nini?”<br />
“Kuzuia nguvu za jini Balkis.”<br />
“Sasa niwape kinga ya nini?”<br />
“Anaweza kutugeuka na kutufanyia kitu kibaya.”<br />
“Hawezi na sina tiba yoyote labda muwe na tatizo lingine.”<br />
“Hatuna, ni hili hili la huyu mwanamke ndilo linalotutisha, unamuona kwa macho tu lakini ni kiumbe kibaya sana.”<br />
<br />
<br />
“Yule hana ubaya kama nilivyowaeleza, lakini mioyoni mwenu mna dhamira mbaya naye, kwa hilo mimi halinihusu kama mnataka ushindani dawa hiyo sina.”<br />
“Kwa hiyo huna msaada wowote kwetu?” Tonny aliuliza.<br />
<br />
<br />
“Msaada niliowapa ni mkubwa kuliko kukuchanjeni au niwape dawa ya kufukiza.”<br />
“Mzee msaada gani uliotupa zaidi ya kutuacha njia panda?” Tonny alizidi kuhoji.<br />
<br />
<br />
“Msaada niliowapa hamuujui lakini ni mkubwa sana, najua mmezunguka kwa waganga wengi kwa kazi zenu za dhuluma. Hamkuwahi kukutana na tatizo kisha mkatibiwa bila kunywa, kujifusha au kuchanjwa dawa? Mliyekuwa mnamuona adui ameeleza hataki kitu gani, sasa mnataka nifanye nini?”<br />
”Basi inatosha inawezekana na wewe umemuogopa,” Tonny alisema kuonesha alitaka zaidi ya yale aliyoelezwa.<br />
<br />
<br />
“Kweli nimemuogopa nipo kwa ajili ya kutibu si kujiingiza kwenye matatizo ya kujitakia, kutokana na maelezo yake nilikuwa nampoteza mjukuu wangu kwa ajili yetu. Nawaeleza mkikosea kwenda kwa mganga mwingine kitakachowakuta hamtakisahau mpaka mnakufa.”<br />
“Tumeelewa.” Tonny alijibu kwa shingo upande.<br />
“Basi mnaweza kwenda ili niendelee na wenzenu.”<br />
“Sasa mzee tukupe kiasi gani?”<br />
“Nina imani hamkuona nilichokifanya, nendeni msitoe kitu chochote.”<br />
“Hapana mzee hata ya kuangalizia, sijui elfu moja?”<br />
“Hapana nimewasamehe kila kitu.”<br />
Walitoka huku wakiamini mzee Njiwa Manga uwezo wa kutibu umepungua ndiyo sababu ya kushindwa kuwasaidia kupambana na Balkis.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis).........EP.53.<br />
<br />
<br />
“Sauda,” walisema mashoga zake waliokuwa wakilia huku mikono ikiwa kichwani, wengine hata nguo ziliwaanguka bila kujua.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
“Sauda kafanya nini?”<br />
“Ame...”<br />
“Amefanya nini mbona mnanichanganya, mke wangu kafanya nini jamani?” mganga alijikuta kwenye mtihani mzito wa kujua mkewe amefanya nini kwani muda mfupi uliopita alimtuma dukani.<br />
<br />
Mara aliingia mwanamke mwingine aliyekuwa akilia huku akisema:<br />
“Haiwezekani Sauda atutoke kirahisi namna hii.”<br />
“Huu lazima uchawi haiwezekani njiwa amgonge afe,” mwingine alisema huku akijitupa chini kwa uchungu.<br />
“Jamani mke wangu kafanya nini?” pamoja na kuwasikia wakisema lakini hakuwaelewa.<br />
<br />
<br />
Mara watu waliingia na mwili wa mkewe ambaye alikuwa amekwishapoteza uhai.<br />
<br />
<br />
\“Ha! Amefanya nini?” Kakakuona alitaharuki.<br />
<br />
<br />
Alimvamia mkewe ambaye alikuwa amefunikwa kanga, akamfunua na kumwinamia! Hakuamini alichokiona mbele yake.<br />
<br />
<br />
“Sauda mke wangu umepatwa na nini? Kwa nini nilikutuma kwenda kuchukua dawa? Kwa nini nilikuwa na wazo baya? Maskini mke wangu nimekuponza, ulikuwa ukizungumza na wanawake wenzako, ona sasa umebadilika jina na kuitwa marehemu! Nini faida ya kazi yangu?” Mganga alilia kama mtoto mdogo huku akimgeuza mkewe ambaye alikuwa ameanza kupoa.<br />
<br />
<br />
Ashura na mwanaume wake nao walikuwa wametoka na kushuhudia tukio lile. Balkis naye hakuwa mbali, moyo ulimuuma kwa kitendo chake cha kuyachukua maisha ya kiumbe kisicho na hatia.<br />
<br />
Machozi ya damu yalimtoka.<br />
<br />
Kila mganga alipokuwa anamlilia mkewe kwa maneno ya uchungu na yeye ndivyo alivyokuwa akiumia na kulia zaidi.<br />
<br />
<br />
Ashura alipoangalia pembeni alishtuka baada ya kumuona Balkis akiwa katika kundi la watu huku naye machozi yakimtoka. Baada ya kumuona alipatwa na mshtuko mkubwa, akaanguka na kupoteza fahamu. Hali ile iliwatisha watu wote waliokuwa pale.<br />
<br />
<br />
Mganga alimwacha mkewe na kukimbilia ndani kuchukua dawa ya unga kwa ajili ya kuzuia nguvu zozote mbaya.<br />
<br />
Aliimwaga hewani lakini Balkis aliwahi kuondoka eneo lile na kwenda kukaa njiani kuwasubiri Ashura na mwanaume wake. Mganga baada ya kufanya vile bado hakuamini, aliuchukua mwili wa mkewe na kuuingiza ndani kujaribu tiba zote anazozijua akiamini atafanikiwa kumrudisha mkewe.<br />
<br />
Alikuwa amesahau kuwa hakuna mtu wala kiumbe chochote dunia chenye uwezo wa kurudisha roho ya mtu au kiumbe zaidi ya Muumba peke yake.<br />
Licha ya kuhangaika zaidi ya saa nzima kurudisha roho ya mkewe iliyopotea, bado hakufanikiwa.<br />
<br />
Hatimaye alikubaliana na ukweli kwamba mkewe amefariki.<br />
<br />
Ilibidi atoe taarifa za kifo cha mkewe kwa ndugu na jamaa, mipango ya mazishi ikaanza. Kutokana na kuchanganyikiwa na kifo cha mkewe alisahau hata kama kuna wateja aliokuwa akiwashughulikia.<br />
<br />
<br />
Ashura baada ya kupata nafuu alijikuta akichanganyikiwa kwa kuamini kabisa kifo cha mke wa mganga kimefanywa na Balkis. Wasiwasi ulizidi kumpanda na kujiuliza kama ni yeye basi hata maisha yao yalikuwa hatarini.<br />
<br />
<br />
“Tonny nimemuona Balkis?”<br />
“Wapi?”<br />
“Alikuwa kwenye kundi la watu.”<br />
“Mwongo!”<br />
“Kweli! Tena alikuwa analia machozi ya damu.”<br />
“Mungu wangu! Unataka kuniambia aliyefanya haya ni yeye?”<br />
“Inawezekana kabisa, si unakumbuka kauli aliyotoa kwa mzee Njiwa Manga kuwa kama angetusaidia angemuua mjukuu wake.”<br />
“Sasa unafikiria anaweza kutufanyia kitu kibaya?”<br />
“Hata mimi nimechanganyikiwa.”<br />
“Sasa mganga atatusaidia nini?” Tonny aliuliza huku mapigo ya moyo yakimwenda kwa kasi.<br />
“Wee! Tena nyamaza, inavyonekana sisi ndiyo chanzo cha kifo cha mkewe.”<br />
“Kwa hiyo unaniambia nini?”<br />
“Tuondoke, ikiwezekana tusirudi tena na Balkis tuachane naye,” Ashura alisema huku akitetemeka.<br />
<br />
Wakati huo watu walizidi kusogea eneo la tukio, kila mtu alikuwa akisema lake juu ya kifo cha ghafla cha mke wa Kakakuona.<br />
<br />
<br />
Wapo walioelezea jinsi walivyomuona njiwa yule akimpiga kichwani mke wa mganga na kutoweka kisha kuanguka chini na kupoteza uhai.<br />
<br />
<br />
“Kweli kabisa Balkis ndiye aliyemuua mke wa Kakakuona,” Tonny alipata uhakika.<br />
<br />
<br />
“Sasa unaona tumechokoza nyuki wakati hatuna mbio.”<br />
“Sijui tufanye nini ili Balkis atuelewe?”<br />
“Nimekueleza tuachane naye.” <br />
“Atatuelewa?”<br />
“Mmh! Kazi ipo, kama amejua tunataka kumuua unafikiri atatufanya nini?” Ashura alisema kwa sauti ya kukata tamaa.<br />
<br />
<br />
“Hapo ndipo ninapochanganyikiwa, kwa nini tusiendelee kuwa hapa ili mganga atupe hata kinga ili asitudhuru?”<br />
“Tonny hebu kuwa na akili, umesikia aliyefanya vile ni Balkis mganga atatufanya nini, hiyo milioni mbili yako itarudisha roho ya mkewe?”<br />
“Mmh! Na kweli, kwa hiyo unasemaje?”</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis).........EP.55.<br />
<br />
LIPOISHIA Jumamosi<br />
“Nilikuwa na mambo yangu binafsi wala hayahusiani kabisa na majini,” Ashura alipindisha kwa kuamini mwanaume wake akijua kuwa alifuata dawa ya kurudiana na Muddy angekasirika.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Ashura alikuwa na siri nzito moyoni mwake kama angefanikiwa kurudiana na Muddy, mwanaume aliyeamini kuwa bila ya mipango yao ya utapeli alikuwa ndiye sahihi kwake. Mpango wake ulikuwa kumuua mwanaume wake kwa kumuwekea sumu kwenye chakula ili aishi na Muddy katika maisha ya ndoa.<br />
<br />
“Kama nilivyokueleza kabla ya kujua kuwa yule mwanamke ni jini, nilikwenda kwa ajili ya kuangalia jinsi ya kumuingia na kuweza kuchukua mali yake.<br />
Lakini ilionesha si kiumbe wa kawaida na kama ulivyosikia, mzee Chujio alizidiwa nguvu na yule mwanamke. Lakini kwa mzee Njiwa Manga kutokana na historia ya watu hajawahi kushindwa suala la majini.”<br />
<br />
“Tonny mbona hatuelewani nani ana majini mpaka twende kwa mzee Njiwa Manga?”<br />
“Kumbuka tunataka mali ya Muddy na mkewe ambaye ni jini, huoni tunahitaji msaada wa mtu mwenye uwezo wa kupambana na majini.”<br />
<br />
“Mmh! Kama ana uwezo huo kuna umuhimu wa kwenda kwake.”<br />
<br />
“Hakuna njia nyingine kwa mambo niliyoyaona yamenitisha bila hivyo tunaweza kupotea.”<br />
<br />
Walikubaliana kwenda siku iliyofuta kwa mganga Njiwa Manga ili kutafuta uwezo wa kupambana na Balkis.<br />
<br />
**** <br />
Siku ya pili Ashura na mwanaume wake walikwenda Bagamoyo kwa mganga Njiwa Manga, kwa vile Tonny alikuwa hajakwenda kipindi kirefu, ilibidi aulizie sehemu anayoishi. Alielekezwa na kwenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa mganga huyo, walipofika walikuta magari aina tofauti zaidi ya kumi kuonesha kuwa siku ile kulikuwa na wateja wengi.<br />
<br />
Ilibidi wakae kwenye benchi kusubiri kwa muda mbele yao kulikuwa na wagonjwa zaidi ya ishirini, walijumuika pamoja na kusubiri tiba. Wingi wa watu ulitaka kuwakatisha tamaa na kutaka kuondoka.<br />
<br />
“Tonny kwa nini tusiondoke turudi kesho mapema, huoni tutachelewa kutoka?” Ashura alimwambia mwanaume wake.<br />
<br />
“Kwani tunawahi nini? Kwa vile tumeishafika hata usiku tutarudi, nataka nikueleze ukweli pamoja na kujionesha siogopi kitu, lakini siri niliyokuwa nayo moyoni ni Mungu tu anajua.<br />
<br />
Kama yale maajabu yangerudia basi ningekufa kwa hofu.<br />
<br />
“Nilikuona ulikuwa mwenye hofu kubwa na niliyasikia mapigo yako ya moyo yakikimbia kama gari lililokatika breki na kunifanya nisimame kidete,” alisema Tonny.<br />
<br />
“Mmh! Wee acha tu, kama angezidisha ningekufa, yaani maneno yako yalinitia nguvu ya ajabu. Kwa kweli nimeanza kuwa muoga wa kila kitu hata upepo sasa hivi ukivuma naogopa najua amekuja,” alijibu Ashura.<br />
<br />
“Wee acha, baada ya kugundua yule mwanamke ni jini niliishiwa nguvu na kuamini simuwezi kwa lolote zaidi ya kutumia nguvu za ziada kuja hapa kwa mzee Njiwa Manga ndipo penye ufumbuzi bila hivyo tutaumia,” alisisitiza Tonny.<br />
“Kwa hilo hata tukikaa siku mbili sioni tatizo, sasa hivi namuogopa yule mwanamke kama kifo,” alimalizia Ashura.<br />
<br />
Wakati wakibadilishana maneno hayo, Balkis hakuwa mbali na nyumba ya mzee Njiwa Manga, wakati alipokuwa akitoka kwa wazazi wake chini ya bahari aliwaona Ashura na mwanaume wake wakikaribia kuingia kwa mganga Njiwa Manga. Alijitahidi kuwawahi wasiingie, kasi yake iliishia nje ya uzio wa nyumba ya mganga huyo.<br />
<br />
Alijipiga chini kwa hasira na kusababisha patokee mtikisiko mdogo uliowashtua watu, hakutaka kukubali kushindwa, alijigeuza njiwa na kwenda kwenye mti mrefu uliokuwa pembeni ya nyumba ya mganga Njiwa Manga.<br />
<br />
Aliweza kuwaona wateja wa mganga huyo akiwemo Ashura na mwanaume wake, lakini nguvu za dawa za mzee Njiwa Manga zilimzuia asiweze kufanya lolote.<br />
<br />
Akiwa na hasira alipanga kuwasubiri na kuwatia adabu baada ya kuonesha kiburi. Wasiwasi wake ulikuwa kwenye nguvu za yule mzee zingeweza kummaliza na kudhurumiwa mpenzi wake.<br />
Kwa upande wa mali yake aliamini hakuwepo wa kuichukua kwa vile ilikuwa ndani ya uwezo wake.<br />
<br />
Katika vitu alivyovipanga maishani mwake vilikuwa ni kubeba mimba ya Muddy kuwafanya wazazi wake hasa baba yake asiwe na nguvu ya kumlazimisha kuolewa na jini mwenzake.<br />
Alijua kama Ashura akifanikiwa kupata kinga ya kumdhibiti, lazima atamnyang’anya mume wake na kumlazimisha kuendelea kufanya kazi asiyoipenda ya kuchukua vizazi vya wanawake.<br />
<br />
Akiwa juu ya tawi la mti akichanganyika na ndege wengine, moyo ulimuuma na kujiuliza amfanye nini mganga ili asiwape uwezo wa kudhulumu haki yake. Alijikuta akiwachukia baadhi ya binadamu ambao aliamini kabisa hawakutakiwa kuhurumiwa zaidi ya kuuawa japo siku zote roho yake haikupenda kufanya vile.<br />
<br />
Akiwa anawatazama wateja waliokuwa wakienda kupata tiba kwa mzee Njiwa Manga, aliwaona Ashura na mwanaume wake wakinyanyuka na kwenda kuonana na mganga huyo. Alijikuta akipandwa na hasira lakini eneo lile lilikuwa lina nguvu za ajabu zisizowezesha nguvu za kichawi na kijini kuingia katika himaya yake.<br />
<br />
Alipotazama huku na kule, aliwaona wajukuu wa mganga wa Njiwa Manga wakicheza, akaamua kumuua mmoja.<br />
<br />
Kwanini Balkis alitaka kumuua mjukuu mmoja wa mganga Njiwa Manga?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis).........EP.57.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
Mzee Njiwa alitoka nje na kurudi na kitezo chenye moto na kukiweka mbele yake, alitoa mavumba kwenye chupa na kusema:<br />
<span class="text_exposed_show"> “Hii dawa kazi yake kuyavuta majini mazuri, kama Balkis ni jini mbaya hatakuja nikimwita.”<br />
Baada ya kusema vile alianza kuweka mavumba kwenye moto huku akisema:<br />
“Balkis binti mfalme wa bahari, naamini wewe ni jini mwema nakuomba uje mbele yangu, lakini kama si jini mwema ukiingia himaya yangu ndiyo mauti yako...Balkis njoo mbele ya wanadamu hawa wana mashtaka juu yako.”<br />
SASA ENDELEA ...<br />
<br />
Moshi ulikuwa mwingi kiasi cha kujaa chumbani, baada ya muda upepo mkali ulianza kuvuma na kusababisha baadhi ya vitu kutaka kupeperuka lakini mzee Njiwa Manga aliutuliza kwa kusema:<br />
“Najua una hasira lakini naomba uwe mpole kama ulivyo, wewe ni mpole tena mwenye upendo kwa wanadamu.”<br />
Upepo ulitulia taratibu wakati huo Balkis akiwa katika umbile la njiwa alijikuta akizidiwa na nguvu na kudondoka toka juu ya mnazi na kujikuta akijitahidi asianguke na kuingia kwenye dirisha la chumba cha uganga cha mzee Njiwa Manga.<br />
Alitua pembeni ya mzee Njiwa Manga, Ashura na mwanaume wake walishtuka kumuona njiwa mzuri sana mwenye rangi nyeupe aliyepakwa wanja mwekundu uliozunguka katika macho yake.<br />
Manyoya yake yalikuwa kama ya plasitiki iliyokuwa ikimelemeta.<br />
“Karibu Balkis kwa mzee Njiwa Manga.”<br />
Balkis katika umbile la njiwa hakujibu kitu alitulia akiwatizama Ashura na mwanaume wake. Mzee Njiwa Manga alisema:”Najua hukupenda muda huu kuwa hapa, lakini nimekuita kwa nia njema kwa vile wewe ni jini mwema mwenye upendo kwa wanadamu. Nakuomba uwe kwenye umbile tunaloweza kuzungumza kibinaadamu.”<br />
Baada ya kusema vile kilipita kiza cha ajabu na baada ya muda ilirudi hali ya kawaida. Sehemu aliyokuwa njiwa alikuwepo Balkis katika umbile la kibinaadamu.<br />
Ashura na mwanaume wake kidogo wakimbie kwa hofu.”Msihofu, kama nilivyowaeleza kwa dawa niliyoichoma ni jini mwema tu anayeweza kuingia katika himaya yangu. Balkis asalam aleykumu.”<br />
“Waaleiykum msalaam,” alijibu kwa sauti tamu.<br />
“Karibu.”<br />
“Asante.”<br />
Balkis aligeuza uso wake na macho yake yaligeuka rangi na kutoa machozi ya damu, kitu kilichozidi kuwatisha Ashura na mwanaume wake.<br />
“Hapana Balkis huna sifa hiyo wewe ni mpole nimekuita hapa kwa makusudi ya kuwaeleza hawa wanadamu ubaya wao mbele yako.” Mganga Njiwa Manga alisema huku akimshika kichwani na kumpigapiga taratibu kumpunguza hasira. Balkis alitikisa kichwa kuonesha amekubali.<br />
“Balkis.””Abee.”<br />
“Nataka uniambie unataka nini wafanye hawa wanadamu wajue wewe si adui yao?””Wanajua wenyewe, nilizungumza nao nini,” Balkis alijibu kwa sauti tamu kama kinanda.<br />
“Naomba unieleze mbele yao.”<br />
“Nikisema mimi nitaonekana muongo, napenda waseme kwa vinywa vyao.”<br />
“Eti mlizungumza nini na Balkis?” mzee Njiwa Manga aliwageukia na kuwauliza.<br />
“A...ali...nikataza nisimfuate mume wake ambaye ni mtalaka wangu,” Ashura alijibu katika hofu kubwa.<br />
“Na kingine?”<br />
“Tusimfuatilie maisha yake.”<br />
“Mmefanya yote aliyowaeleza?”<br />
Wote walibakia kimya wakitazama chini, mganga alimgeukia Balkis na kumuuliza.<br />
“Wewe umeona nini?”<br />
“Hawa walio mbele yako ni viumbe wabaya kuliko hata nyoka, wamepoteza maisha ya wanaume zaidi ya wanne na Muddy kama nisingemuwahi alikuwa wa tano. Wamekuwa na tabia za kuwatafuta wanaume na huyu mwanamke kujifanya anawapenda sana, kisha anajitambulisha kwa majina tofauti.<br />
“Kila mwanaume anamfahamu kwa jina tofauti kama waliokufa kwa ajili yao wakisimamishwa mbele yake watamtaja kwa majina tofauti, Muddy anamtambua kwa jina la Ashura lakini wengine walimtambua kwa majini ya Fatuma, Hilki, Masha.<br />
“Lakini jina lake halisi ni Shuuna, kwa utaalamu wako nina imani majina hayo yote umeyaona alipojitambulisha kwako na kujua sababu ya majina hayo?”<br />
“Ndiyo,” Mzee Njiwa Manga alijibu kwa sauti ya chini.<br />
“Hawa si viumbe wa kuonewa huruma hata mara moja, hebu angalia kila kukicha wamekuwa wakipanga mipango ya kudhulumu mali za watu na kuwatoa roho zao bila hatia kwa kigezo cha uzuri wa Shuuna. Hivi mimi na yeye nani mzuri?”<br />
Balkis alinyanyuka na kujigeuza pande zote kuonesha ufundi wa Maulana kumuumba katika umbile la uzani.<br />
“Ni wewe Balkis mwana wa mfalme wa chini ya bahari.”<br />
“Mbona siui watu kama ninyi? Mtauliza kwa nini nilimuua mganga Chujio, kiburi chake kilimponza. Nilijua mtakwenda kule na kutaka kinga ya kupambana na mimi kama alivyowasaidia kudhulumu na kutoa roho za watu wasio na hatia. Lakini kwa busara zangu nilimuonya na kuonesha kiburi kwake ndicho kilichomponza.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis).........EP.59.<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
Walitoka huku wakiamini mzee Njiwa Manga uwezo wake wa kutibu umepungua ndiyo sababu ya kushindwa kuwasaidia kupambana na Balkis.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
BAADA ya kutoka kwa mganga wakiwa ndani ya gari lao walianza kujadiliana kuhusiana na maneno ya mzee Njiwa Manga.<br />
“Sasa tutafanya nini?”<br />
“Kwa nini tusiachane naye?”<br />
<br />
“Mmh! Lazima atatufanyia kitu kibaya, si umemuona ametokwa na machozi ya damu kwa hasira, anaweza kutufanya kitu kibaya.”<br />
“Sasa tufanyeje?”<br />
<br />
“Lazima tutafute njia nyingine, unajua mzee yule nimemtoa akili, shida yake ni fedha na si kutaka kujua tutafanya nini.”<br />
“Tena namshangaa anajifanya hataki fedha wakati anafanya kazi ile ili kusukuma maisha yake,” Ashura aliongezea.<br />
“Ooh! Nimekumbuka kuna sehemu moja kuna mtaalam mmoja nina imani anaweza kutusaidia. ” Tonny alisema.<br />
<br />
“Kama ni hivyo tusirudi nyumbani tupitie huko huko maana bado simuamini yule mwanamke amenitisha sana, lakini Tonny asiwe kama mzee Chujio tukaumbuka?”<br />
“Namuamini ameshawahi kunifanyia mambo mengi ambayo sikuwahi kukushirikisha, y ule mzee huwa haulizi ukimueleza chochote hata kuua anafanya,tena anapenda kuua kama nini.”<br />
<br />
“Tena huyo ndiye mzuri sana, lakini tutafika salama?” Ashura alikuwa na wasiwasi.<br />
“Sifa ya yule mganga ukiwa na wazo la kwenda kwake kuanzia hapo unakuwa salama hakuna kitu cha kukuzuia.”<br />
“Tena huyo anafaa, kwa nini hukusema mapema?”<br />
“Nilimuamini babu yule baada ya kujua ana sifa ya kutatua matatizo ya majini.”<br />
<br />
“Basi tuelekee, leo hatuna kazi nyingine zaidi ya kuujua mwisho wa Balkis.”<br />
Safari ilielekea kwa mganga mwingine, njia nzima ilikuwa ni mitihani mingi kutokana na gari kuteleza bila utelezi na kuona mambo ya kutisha lakini safari iliendelea. Matukio hayo yalimtisha sana Ashura kufikia hatua ya kumuomba mwanaume wake wasitishe safari yao.<br />
“Tonny kwa nini tusirudi huoni safari yetu imejaa matukio ya kutisha tunaweza kupata ajali mbaya na kufa?”<br />
<br />
“Shuuna hivi ni vitisho vya Balkis baada ya kugundua tunakwenda kwa mganga mwenye uwezo wa kumuangamiza. Hawezi kutufanya lolote ni kuhangaika kwake kwa mfa maji tu.”<br />
“Mmh! Yaani naogopa kuna kipindi niliona mti wa ajabu umetokea ghafla barabarani, nilijua tunakufa na kufumba macho, nilipofumbua nilishangaa kuona tumevuka salama.”<br />
<br />
“Shuuna hizo ni hila za majini, ule si mti ni kiini macho tu ukiukwepa tu umeumia lazima gari litapinduka.”<br />
“Jamani! Ningekuwa mimi ningeukwepa.”<br />
“Lazima ungepinduka, barabara hii umepita mara ngapi?”<br />
“Mara nyingi tu.”<br />
<br />
“Huo mti uliwahi kuuona?”<br />
“Sijawahi kuuona.”<br />
“Basi mimi nimepasua katikati ya mti ule hakuna kitu kilichoizuia gari kupita.”<br />
“Mmh! Kweli yule mwanamke ni jini.”<br />
<br />
“Awe jini mara ngapi?”<br />
“Tukipata dawa itatusaidia sana.”<br />
“Hesabu tumemkomesha, yule bwana alisema katika dunia hii hawezi kurudisha roho ya mwanadamu tu, kwa vile ni kazi ya Mungu peke yake. Lakini chochote kinachowezekana kwa mwanadamu kwa uwezo wa Mungu anakifanya kwa ukamilifu.”<br />
<br />
Baada ya kufanikiwa kuvuka vizingiti vya Balkis walifika Vingunguti walikata kushoto njia ya kuingia Jeti Rumo, waliifuata njia ile mpaka maeneo ya Kijiwe Samli. Tonny alisimamisha gari mbele ya duka moja ambapo pembeni yake kulikuwepo na vijana wakicheza drafti.<br />
“Tumefika,” Tonny alisema huku akizima injini ya gari.<br />
“Mbona yupo kwenye makazi ya watu?” Ashura aliuliza.<br />
<br />
“Siku hizi huduma zimewafuata watu, hakuna waganga wa kizamani kuwa kijijini nyumba za majani. Waganga wa siku hizi wanakwenda na wakati hata mavazi yao si kaniki na ngozi na shanga kibao.”<br />
Baada ya kufunga gari na kuliacha katika hali ya usalama aliifuata njia ya uchochoro kati ya nyumba ya duka na ya kawaida na kutokea mtaa wa pili walikata kulia kuelekea kwa mganga.<br />
<br />
“Tonny huku umepajuaje?”<br />
“Kuhangaika, unafikiri kama tungekuwa tunamtegemea mzee Chujio peke yake ingekuwaje?”<br />
“Mmh! Na kweli, ona kama alivyotutoa nishai yule mzee sijui kunguru, baada ya kifo cha mzee Chujio tungekwenda wapi?”<br />
“Atajijua mwenyewe kama anaitwa Njiwa au bundi, mzee yule kanichefua hana lolote kumbe sifa za uongo.” Tonny alimkandia mzee Njiwa Manga.<br />
<br />
Nini kitaendelea? Kweli mganga huyu ana uwezo wa kumdhibiti Balkis?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123d463fd033937624417">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) EP.61.<br />
<br />
<br />
Ilipoishia:<br />
ILE ilimfanya akose raha na kutokwa na machozi, alipata wazo la kuwahi chini ya bahari kabla uchawi wa kumuua haujafanywa. Lakini alikumbuka ana deni na baba yake la kuachana na Muddy mwanaume aliyepanga kuachana naye baada ya kumpa ujauzito ambao wazazi wake hawatakuwa na nguvu na kumruhusu aishi naye.<br />
<span class="text_exposed_show"> Sasa endelea...<br />
<br />
ALIJIKUTA akiuapia moyo wake kuwa atapigana mpaka tone la mwisho la damu yake lakini hatarudi chini ya bahari. Akiwa amesimama pembeni ya nyumba kwenye mti wa jirani katika umbile la njiwa, alijiuliza atafanya nini ili aweze kujiokoa na hatari ile.<br />
<br />
Alishuhudia Ashura akitoa laki tano kwenye mkoba na kumpatia mganga ambaye alinyanyuka ili akachukue vifaa vya kutengengeneza dawa ya kummaliza. Balkis juu ya mtu alijikuta akipoteza uwezo wake wa kawaida baada ya kuamini wakati wowote anaweza kufanyiwa kitu kibaya.<br />
<br />
Alijua waganga wengi huwavuta majini kwa dawa na kuwamaliza, akiwa ametota kwa jasho kwenye manyoya yake kwa hofu ya kifo. Alimuona mganga akitoka uani kwake na kumwita mkewe aliyekuwa akizungumza na wanawake wenzake. <br />
“Mke wangu,” alimsikia akimwita mkewe kwa sauti ya juu kidogo.<br />
<br />
“Abee mume wangu,” alimuona mkewe aliyekuwa amevalia nguo na vito vya dhahabu kila kona kuonesha kwamba wanaishi maisha ya kifahari.<br />
“Hebu nenda dukani kaniletee ile kiboko ya majini.”<br />
<br />
“Kuna mtu ana jini nini?” Alimuuliza huku akipokea fedha.<br />
“Kuna jini mmoja anawakosesha raha wateja wangu.”<br />
“Sasa unataka kumfanya nini, unataka kumtia kwenye chupa nini?”<br />
<br />
“Namuulia mbali, unajua jini ukilifungia kwenye chupa likitoka linaweza kukumaliza. Dawa yake sasa hivi ni kulimalizia mbali, itakuwa wakijua wanakuja Kakakuona watakuwa wanakimbia wenyewe.”<br />
“Ngapi nichukue?”<br />
<br />
“Kwa vile nammaliza kazi kabisa nichukulie tano na ndimu kumi na nne na sindano kumi na nne.”<br />
“Mmh! Mbona nyingi sana leo umepania.”<br />
“Nimemuona ana kiburi, pia ana mchezo wa kutaka ushindani, nikimfunga anaweza kutoka, si unajua siku hizi watu wakikuta kitu lazima wakifungue.”<br />
<br />
Kauli ile ilimshtua Balkis ambaye aliamini siku ile ndiyo ilikuwa ni mwisho wa maisha yake, wazo la haraka lilikuwa ni kurudi kwao na kuwa tayari kukubaliana na matakwa ya baba yake ya kuachana na Muddy ili awe salama.<br />
“Mmh! Haya kazi kwenu,” mkewe mganga alisema huku akitokea mlango wa nyuma kwenda duka la dawa za asili.<br />
<br />
Balkis alimuangalia mke wa mganga na kumuona ni mweupe asiye na kinga imara ya kuzuia nguvu za majini, kutokana na kukataa kuchanjwa na mumewe. Kwa vile mumewe alimpata baada ya kuja kutibiwa kutafuta dawa ya kuolewa na kigogo mmoja na mganga akamgeuzia kibao cha kutengeneza dawa ambayo ilimfanya yule mwanamke ampende mganga badala ya mtu aliyemkusudia.<br />
<br />
Baada ya kufanikiwa kumpata, ilibidi akubaliane na mkewe ambaye hakutaka kuishi kiganga zaidi ya maisha ya kifahari ya kujirusha kwa kutembelea gari. Kutokana na uwezo wa mganga wateja wake wengi walikuwa watu wenye uwezo hivyo kumfanya asiwe na shida ya fedha ndogo ndogo.<br />
<br />
Pamoja na mkewe kutoishi kama mke wa mganga na muda wote kuvaa nguo na vito vya thamani, bado alikuwa akijua baadhi ya dawa ambazo zilikuwa zikitumiwa na mumewe.<br />
Hata pale mumewe alipokuwa safarini alielekezwa jinsi ya kuzitengeneza na kuwapa wateja lakini mumewe alipokuwa nyumbani yeye aliendelea na maisha yake ya kujiachia.<br />
<br />
Balkis aliona ile ndiyo nafasi yake ya kufanya kitu kitakachomfanya mganga asifanye lolote juu yake. Alikurupuka kutoka juu ya mti kama njiwa na kumgonga kichwani mke wa mganga ambaye alikwenda juu na aliporudi chini hakuomba hata maji.<br />
<br />
Waliokuwepo pembeni walimuona njiwa mweupe akimgonga kichwani na kupotea katika mazingira ya kutatanisha. Kelele na kilio cha mtu aliyeingia kwa mganga zilimshtua mganga aliyekuwa ameanza kuandaa vifaa vya kummaliza Balkis. Aliacha na kutoka na kukutana na mfanyakazi wake wa mapokezi.<br />
<br />
“Vipi?” alimuuliza baada ya kumuona amechanganyikiwa.<br />
“Mama.”<br />
“Amefanya nini?”<br />
“Ame....”<br />
<br />
“Yupo wapi?” aliuliza huku presha imempanda.<br />
“Yupo nje ya nyumba.”<br />
“Kafanya nini?”<br />
“Si...sijui.”<br />
<br />
Mara alisikia sauti za vilio vya mashoga wa mkewe ambao walikuwa wakizungumza naye muda mfupi uliopita, vilio vile vilizidi kumtisha na kumchanganya.<br />
“Jamani kuna nini?” Aliuliza tena macho yakiwa yamemtoka pima.</span></div></span></div><span class="fcg"></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123d65608a45964151448">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) EP.63.<br />
<br />
ILIPOISHIA<br />
“Hatuna jinsi<br />
“Huu si wakati wa kulaumiana tutafute njia ya kujiokoa kwa Balkis.”<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
“Mmh! Huoni tukitafuta mganga mwingine ni sawa na kuongeza mafuta kwenye moto?”<br />
“Sasa tutafanya nini?” Tonny alionesha kuchanganyikiwa na kusahau kama wanatakiwa kuondoka eneo lile na badala ya kujilaza kwenye usukani.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Tonny hebu ondoa gari kama huwezi nipishe miye niendeshe.”<br />
“Ashura njoo uendeshe nina imani Balkis anajua mimi ndiye mbaya wake namba moja, hata sijui itakuwaje?”<br />
“Tonny we twende nyumbani lolote litakalotokea tuwe tayari kukabiliana nalo.”<br />
<br />
“Mmh! Haya sina jinsi yaani najuta kumfahamu Balkis.”<br />
“Lakini si tumeambiwa ni kiumbe mwenye huruma?”<br />
“Si umesema umeona akitokwa na machozi ya damu kuonesha hasira unafikiri mtu tuliyetaka kumuua atakuwa na huruma na sisi?”<br />
<br />
“Bwana wee hebu tuondoke mengine tutayajua huko huko.”<br />
Tonny alijikaza na kuwasha gari kisha waliondoka eneo la Kiwalani, Balkis aliwaona kwa mbali wakija, akiwa amejawa na hasira kutokana na kiburi walichokionesha alikosa adhabu inayowafaa kutokana na roho zao mbaya ili wasirudie tena kumfuatafuata. Adhabu aliyoipanga ilikuwa kuhakikisha kwanza anamtia aibu Ashura na mumewe kwa kumgeuza kiumbe wa ajabu asiyependwa na wanadamu au wanyama.<br />
<br />
Hakutaka kuwasumbua aliwaacha warudi mpaka nyumbani kwao ili aweze kufanya alichokikusudia. Ashura na mwanaume wake walishangaa kwenda mpaka nyumbani kwao bila kukutana na tatizo lolote, walipofika walishukuru Mungu.<br />
Baada ya kuingia ndani hata kabla hawajakaa vizuri mlango uligongwa, Tonny alikwenda kuufungua na Ashura alikwenda chumbani. Alipofungua alipatwa na mshtuko uliomfanya aanguke chini na kupoteza fahamu.<br />
<br />
Ashura aliyekuwa chumbani alishitushwa na kishindo cha mtu kuanguka chini, alimwita mwanaume wake huku akitetemeka ili ajue kimetokea nini.<br />
“Toooni,” aliita kwa sauti ya juu bila kupata jibu, woga ulimwingia.<br />
<br />
Alirudia tena kumwita Tonny bila jibu lolote, alitoka chumbani huku akiwa na wasiwasi, kabla ya kufika sebuleni alisikia harufu ya manukato aliyoyazoea kuyasikia wakati Balkis akiwa karibu yake. Harufu ile ilimjulisha tayari walikuwa wamevamiwa ndani ya nyumba yao.<br />
<br />
Mlangoni alikuwepo Tonny aliyekuwa amelala chini, alianza kutetemeka. Akiwa bado katika hali hiyo, mlango uligongwa tena, alitamani kurudi chumbani kwake lakini alijikaza na kusogea hadi mlangoni na kuufungua. Alipofungua alikutana uso kwa uso na Balkis, kwa woga alioupata haja ndogo ilimtoka bila kutarajia.<br />
“Samahani Balkis,” aliomba msamaha huku akipiga magoti kwa kujua kiama kimefika.<br />
<br />
“Ya nini?”<br />
“Najua nimekukosea.”<br />
“Kosa gani?”<br />
“Unajua, naomba usituue.”<br />
<br />
“Kuua ni kazi ya Mungu peke yake si ya kiumbe chochote.”<br />
“Mbona ume..,” Ashura alisita kusema Balkis kamuua mke wa mganga Kakakuona kwa kuhofia kumzulia jambo ambalo huenda hakulitenda na kumuongezea hasira.<br />
“Nimefanya nini?”<br />
<br />
“Hujafanya kitu.”<br />
“Najua ulitaka kusema nini.”<br />
“Ha...ha...pana,” Ashura alitetemeka kwa hofu.<br />
“Kwanza mmwagie maji mwenzako azinduke, nashangaa anakuwa mwoga wakati yeye ni bingwa wa kutoa roho za watu.”<br />
“Naomba unisamehe Balkis najua kiasi gani tumekuudhi.”<br />
<br />
“Hebu fanya kwanza niliyokuagiza,” Balkis alisema kwa sauti kali kidogo.<br />
Ashura alikwenda jikoni na kurudi na maji kwenye bakuli.<br />
“Mmwagie kidogo kichwani.”<br />
<br />
Ashura alifanya kama alivyoelekezwa, baada ya kumwagia maji mwanaume wake alirudiwa na fahamu. Tonny alipozinduka alishtuka kujikuta yupo mbele ya Balkis. Alinyanyuka na kupiga magoti mbele ya Balkis kuomba msamaha.<br />
“Samahani Balkis najua umekuja kutudhuru, lakini tunakuhakikishia hatutarudia tena kukufuata,” Tonny alisema huku akitokwa na machozi.<br />
<br />
“Kabla ya kuzungumza lolote naomba Ashura aende akajisafishe, siwezi kuzungumza na mtu aliyejipaka najisi.”<br />
Ashura alikwenda bafuni kujisafisha kisha kubadili nguo na kurudi mbele ya Balkis bila kujua nini hatima yao baada ya kumchokonoa kwa muda mrefu. Baada ya kurudi alisogea kwa mwanaume wake na kuungana naye kupiga magoti.<br />
<br />
“Naomba mkae chini, magoti yenu yataniongeza hasira niwageuze kuwa manyani”<br />
Baada ya kukaa alimuuliza Ashura swali lake la awali.”<br />
“Ashura, uliuliza mbona nimemuua mke wa mganga?”<br />
<br />
“Ha...ha...pana sikumaanisha hivyo.”<br />
“Naona unataka kunichefua nikugeuze kuwa nyoka sasa hivi muuaji mkubwa, hivi mimi nikifa ninyi mtafaidika nini?”<br />
Hakuna aliyejibu kitu, wote walibakia kimya nyuso zao wamezielekezea chini kwa aibu.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123d65600ee6559356557">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) EP.64.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
“Naomba ukae chini, magoti yenu yataniongeza hasira niwageuze nyani.”<br />
<span class="text_exposed_show"> Baada ya kukaa alimuuliza Ashura swali lake la awali.”<br />
“Ashura ulisema mbona nimemuua mke wa mganga?”<br />
“Ha..ha..pana sikumaanisha hivyo.”<br />
<br />
“Naona anataka kunichefua nikugeuze nyoka sasa hivi muuaji mkubwa wewe, hivi mimi nikifa ninyi mtafaidika nini?”<br />
Hakuna aliyejibu kitu, wote walibakia kimya wakiwa wameangalia chini kwa aibu. SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Kwa kweli wanadamu ni viumbe wenye kiburi kuliko kiumbe chochote kilichoumbwa na Mungu. Matendo yenu mabaya kuliko hata ya shetani. Shetani siku zote humvuta mtu kwenye dhambi lakini si kuua. Ninyi kila kukicha mnatoa roho za watu kwa ajili ya mali.<br />
<br />
Mmesababisha nimuue mke wa mganga bila sababu kutokana na nia yenu ya kuhakikisha nakufa. Jamani kosa langu nini, kama Hemed mliachana baada ya kumfilisi, sasa hivi umemuona mzuri?”<br />
Ashura hakujibu kitu, aliendelea kuinama na kumfanya Balkis aendelee kuzungumza kwa hasira huku machozi ya damu yakizidi kuichafua nguo aliyokuwa amevaa.<br />
<br />
“Kwa vile mmekuwa kenge msiosikia mpaka mtoke damu masikioni, sasa chagueni adhabu yoyote ila iwe mbaya kuliko zote zilizowahi kutolewa chini ya jua.”<br />
“Tunaomba utusamehe,” walisema kwa pamoja huku wakitamani kunyanyuka kwenda kumlamba miguu.<br />
“Sitawasamehe, lazima niwape adhabu kubwa sana ambayo hata mimi mtekelezaji itaniuma moyoni mwangu kwa jinsi mtakavyoteseka,” Balkis alisema kwa hasira.<br />
<br />
Wote walibakia kimya wakishindwa kujua wachague adhabu ipi, kila adhabu waliyoifikiria ilikuwa nzito kwao. Baada ya kukaa kimya, Balkis alisema huku akitembea taratibu ndani ya nyumba na kuifanya nyumba inukie vizuri:<br />
“Ashura, adhabu yako ya kwanza ni kutembea uchi mbele za watu kama tulivyokubaliana, baada hiyo itafuata nyingine ambayo nitaijua mwenyewe.”<br />
“Na wewe,” alimgeukia Tonny aliyekuwa amejikunyata kwa hofu ya maisha yake.<br />
<br />
“Tena wewe ndiye nitakayekufanya kitu kibaya, kwanza nitakugeuza nzi wa kijani maisha yako yawe chooni na jalalani, adhabu nyingine nitajua hapo baadaye.”<br />
“Ni semehe Ba..ba..lki....”<br />
“Shatap mashetani nyie,” alimkata kauli kwa sauti kali.<br />
“Nina imani mzee Njiwa Manga aliwaeleza vizuri japo mwanzo hata mimi niliwaeleza lakini mlijitia viburi, sasa kiburi chenu kitawatokea puani.”<br />
“Tusamehe hatutarudia tena.”<br />
“Hebu niambieni kosa langu nini?” aliwauliza huku akiwa amewakazia macho.<br />
“Hu..hu..na kosa.”<br />
“Sasa kwa nini mnataka kuniua?”<br />
“Tu..tu..sa..sa..mehe.”<br />
“Nina imani uwezo wangu mlikuwa hamuufahamu lakini leo ndiyo mtaujua.”<br />
“Balkis haki ya nani tunakuahidi hatutarudia tena,” walirudia kupiga magoti mbele yake.<br />
<br />
“Hivi mngefanikiwa kuniua haya magoti mngempigia nani? Kumbukeni nimepata dhambi kwa ajili ya mtu mwingine hivyo lazima nitimize nilichopanga kuwafanyia.”<br />
Wakati wakizungumza yale, Balkis alihisi mabadiliko mwilini mwake yaliyomfanya ahisi kizunguzungu kikali.<br />
<br />
Kwa haraka alishika kwenye paji la uso na kutoweka mle ndani. Ile hali ilimtisha na kuamua kwenda moja kwa moja chini ya bahari kuwahi kujisalimisha kwa wazazi wake. Wasiwasi wake ulikuwa huenda mganga ameamua kulipa kisasi baada ya mkewe kuuliwa.<br />
<br />
Akiwa amechoka alijivuta huku kizunguzungu kikizidi, akatembea kwa kujivuta huku akipepesuka lakini alipofika lango kuu la kuingilia kwenye jumba la mfalme alianguka chini na kupoteza fahamu. Vijakazi na watwana walifika na kumuokota hadi ndani ya jumba kuu akiwa hajitambui kabisa.<br />
<br />
Malkia Huleiya alishtuka kupata taarifa za kuletwa Balkis akiwa hajitambui, akiwa na kanga mkononi alikimbilia sebuleni na kumkuta Balkis akiwa amelazwa chini akiwa hajitambui.<br />
<br />
“Amefanya nini?” aliuliza kwa mshtuko.<br />
“Hatujui Malkia Mtukufu,” walijibu kwa pamoja.<br />
“Mmemkuta wapi?”<br />
“Lango kuu Malkia Mtukufu.”<br />
“Mpelekeni chumbani mara moja.”<br />
Walimbeba na kumpeleka chumbani na kumlaza kitandani, baada ya kumlaza walitoka.<br />
<br />
Malkia Huleiya alichanganyikiwa na kujiuliza mwanaye kafanywa nini na wanadamu. Alijua ile itakuwa vita na wanadamu ambao ni viumbe hatari aliokuwa akiwaogopa usiku na mchana.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4af8db2145587819"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123d655f9827137535223">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) EP.65.<br />
<br />
<br />
“Mpelekeni chumbani mara moja.”<br />
Walimbeba na kumpeleka chumbani na kumlaza kitandani, baadaye walitoka. Malkia Huleiya alichanganyikiwa na kujiuliza mwanaye kafanywa nini na wanadamu. Alijua ile itakuwa vita na wanadamu ambao ni viumbe hatari aliokuwa akiwaogopa usiku kucha. SASA ENDELEA...<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
ALITAKA kwenda kumwita mumewe Mfalme Barami aliyekuwa kwenye kikao na baraza lake la mawaziri lakini alipata wazo la kumfuata mganga mkuu Bunusa ili akaangalie hali ya Balkis. Alimtuma mtwana kumfuata mganga mkuu Bunusa.<br />
Bunusa alifika mara moja na kupelekwa chumba alichokuwa amelazwa Balkis ambaye muda wote alikuwa amepoteza fahamu.<br />
“Bunusa naomba msaada wako hali ya mwanangu ni mbaya sana.”<br />
<br />
“Hakuna tatizo,” Bunusa alisema huku akifungua mkoba wenye vitendea kazi.<br />
Alimshika Balkis kichwani, kifuani, tumboni na miguuni kisha alimshika kwenye paji la uso na kutulia kwa muda akipata ripoti za uchunguzi wa mwili wake. Baada ya muda alipumua pumzi nyingi kuonesha kuna jambo. Malkia Huleiya akimfuatilia kutaka kujua vipimo vile vina majibu gani.<br />
<br />
Baada ya kuvuta pumzi ndefu alimgeukia Malkia Huleiya na kumwambia:<br />
“Balkis haumwi ugonjwa wa kutisha ni hali ya kawaida.”<br />
“Bunusa, Balkis hajatokewa na hali hii toka nilipomzaa, leo atokewe na tukio la kutisha useme hana ugonjwa wa kutisha?”<br />
<br />
“Nimesema hali aliyonayo si ugonjwa, ila tatizo kubwa ni uchovu, inaoneka kafanya kazi kwa mwezi mzima bila kupumzika. Kutokana na hali aliyokuwa nayo lazima hali hii imtokee.”<br />
“Hali! Hali gani hiyo?”<br />
“Ya ujauzito.”<br />
<br />
“Unasema ana nini?”<br />
“Ana ujauzito ambao hakujua kama anao na ndiyo uliomfanya kuchoka baada ya kufanya kazi nzito.”<br />
“Mungu wangu ujauzito wa nani, wa jini au mwanadamu?” Malkia Huleiya aliuliza huku akiweka mkono wake kifuani kuzuia mshtuko.<br />
“Wa mwanadamu.”<br />
<br />
“Ooh! Mbona mwana huyu amenitafutia matatizo, baba yake nitamweleza nini anielewe.”<br />
“Ni kweli hili ni tatizo inaonesha taarifa hizi za kupata ujauzito wa mwanadamu zitakuwa na mpasuko mkubwa ndani ya familia.”<br />
“Sasa nitafanya nini? Tuutoe kabla baba yake hajajua?”<br />
<br />
“Mmh! Katika kosa lingine kubwa mtakalofanya ni kuutoa ujauzito huu, nia kubwa ya mwanao ni kubeba ujauzito na kuzaa na mwanadamu kisha arudi kwa baba yake kwa kuamini hatakuwa na jinsi tena ya kuzuia matakwa yake.”<br />
“Ooh! Sasa Bunusa utanisaidia kitu gani ili kutoleta mtafaruku mkubwa.”<br />
“Dawa ni kumrudisha duniani ili aendelee na maisha yake na mumeo asijue chochote.”<br />
“Tutafanyaje?”<br />
<br />
“Nitampa dawa ya kumrudisha katika hali yake kisha arudi duniani kuendelea na maisha yake.”<br />
“Lakini watwana na vijakazi wanajua alikuja, si watamwambia?”<br />
“Hao ni wa kuwaita na kuwaeleza wasizungumze chochote kuhusiana na Balkis na kutoa vitisho vikali.”<br />
“Sawa nitafanya hivyo.”<br />
Mganga mkuu Bunusa alianza kumshughulikia Balkis kwa kumnusisha dawa iliyomfanya apige chafya na kuzinduka. Balkis alijishangaa kuwa mbele ya mama yake na mganga mkuu Bunusa.<br />
<br />
“Mama,” alimwita kwa sauti ya chini.<br />
“Abee mwanangu, unaendeleaje?”<br />
“Sijambo kidogo, baba yupo wapi?”<br />
“Yupo kwenye baraza na mawaziri wake.”<br />
<br />
“Mmh! Siamini kama nipo salama, asante Bunusa nilijua ndiyo basi.”<br />
“Ndiyo basi kwa vipi?” Malkia Huleiya alimuuliza mwanaye.<br />
“Nilijua mganga niliyemuulia mke wake kaamua kunimaliza.”<br />
“Ni kweli alikuwa na wazo la kukumaliza lakini kiburi chako ndicho kilichokusaidia,” mganga Bunusa alisema.<br />
“Ni kweli alinitumia kombora?”<br />
<br />
“Walaa.”<br />
“Sasa nini kile?”<br />
“Ni kizunguzungu kikali, inaonesha umefanya kazi ngumu bila kupumzika na kusababisha uchoke sana.”<br />
“Mmh! Mbona kazi hiyo ni ndogo, nimekwishafanya nyingi zaidi ya hizo bila matatizo.”<br />
“Ni kweli, lakini sasa hali yako haikuruhusu kuusumbua mwili kwa muda mrefu.”<br />
“Hali! Hali gani?”<br />
<br />
“Ya ujauzito.”<br />
“Ujauzito?” Balkis alishtuka huku akishika mikono kifuani kwake.<br />
“Eeh, vipi hukuutegemea?” Bunusa alimuuliza.<br />
Swali lile ambalo lilikuwa zito kulijibu mbele ya mama yake, Malkia Huleiya alimgeukia mwanaye aliyekuwa bado amekaa kitandani.</span></div></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123d655f0df8085772767">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) EP.67.<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
Balkis baada kurudi kutoka chini ya maji alikuwa na furaha isiyo na kifani alipogundua dhamira yake ya kubeba ujauzito wa mwanadamu imetimia. Alimkuta Muddy akiwa amejilaza kitandani, alipofika alimkumbatia na kumbusu, japo jambo lile lilikuwa ni la kawaida kila alipoondoka na kurudi baada ya kukaa siku moja bila kuonana na mpenzi wake. SASA<span class="text_exposed_show"> ENDELEA...<br />
<br />
LAKINI siku ile furaha iliongezeka mara mbili kitu kilichomshtua Muddy.<br />
“Vipi mpenzi kulikoni mbona una furaha sana?”<br />
“Muddy niambie zawadi yoyote unayoitaka kwangu nikupe.”<br />
“Ya upendo.”<br />
<br />
“Muddy ya kitu kingine kwani hakuna kiumbe nitakayempenda chini ya jua kama wewe.”<br />
“Sihitaji zawadi zaidi ya hiyo.”<br />
“Basi mimi nakuchagulia zawadi ya kuyafanya maisha yako yawe kama ya peponi hata kama sipo.”<br />
“Ina maana unataka kuniacha?’<br />
<br />
“Hapana mpenzi ni tahadhari tu, mimi ni kiumbe siwezi kuishi milele.”<br />
“Nashukuru kwa hilo.”<br />
“Nikwambie kitu?”<br />
“Niambie.”<br />
<br />
“Nina ujauzito wako.”<br />
“Utani huo!” Muddy alishtuka kusikia vile.<br />
“Ndiyo maana nimejawa na furaha isiyo na kifani na nikifanikiwa kujifungua salama nitakupa zawadi kubwa sana isiyo na mfano.”<br />
<br />
Balkis alimkumbatia Muddy kwa furaha huku akiomba ajifungue haraka kabla baba yake mfalme Barami hajatimiza dhamira yake ya kuvunja mpango wa uhusiano wake na Muddy ili aolewe na jini mwenzake.<br />
****<br />
Balkis baada ya kupata habari njema za kupata ujauzito wa Muddy, alikuwa mwenye furaha kupita kiasi. Lakini aliamini furaha yake ingekamilika baada kuwakomesha wabaya wake. Adhabu aliyoipanga ingemfanya aishi kwa furaha mpaka muda wa kujifungua lakini hakutaka kuwaua.<br />
<br />
Wakati akipanga adhabu ya kuwapa Ashura na mwanaume wake, upande wa pili ulishangaa kuona siku zikikatika bila kusikia chochote kutoka kwa Balkis. Waliamua kufanya kazi zao kama kawaida huku wakiachana kabisa na Balkis.<br />
Ashura akiwa katikati ya mji akiendelea na mambo yake ya ununuzi wa vitu muhimu kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Balkis naye alikuwa karibu yake bila mtu yeyote kumuona. Alipomkaribia aliokota udongo kidogo kisha alimpulizia mwilini.<br />
<br />
Ashura akiwa amebeba mfuko mkubwa akielekea kwenye gari alihisi kama kuna vitu vinamuwasha mwilini. Ilibidi aweke mzigo chini ili ajikune kwanza, kila muda ulivyozidi kwenda ndivyo alivyohisi nguo zake zikimuwasha kama vile zimemwagiwa upupu.<br />
<br />
Alianza kuvua nguo huku akipiga kelele za kuwashwa, kila mtu alishtuka na kumshangaa kumuona mwanamke akivua nguo zote na kubakia mtupu. Wasamaria wema walimsogelea na kumvisha lakini alizikataa nguo zake na kusema zinamuwasha.<br />
<br />
Ilikuwa ni kihoja Ashura aliadhirika mbele ya watu, kila alipopewa nguo na kinamama waliokuwa wameshikwa na mshangao kumuona mrembo kama yule akionekana amepandwa na mapepo. Ashura aliondoka pale na kuanza kutembea bila ya kuwa na kitu mwilini, alielekea baharini.<br />
<br />
Ilikuwa ni adhabu aliyokubaliana na Balkis kama atamfuata Muddy aliyekuwa mumewe wa zamani. Baada ya kuridhika na adhabu yake alimtokea kwa mbele akiwa na upande wa kanga. Ashura alipomuona alipiga magoti kumuomba msamaha.<br />
“Balkis najua jinsi gani tulivyokukosea lakini sasa hivi tumeachana na wewe, naomba utusamehe.”<br />
“Adhabu ya kutembea uchi nani aliichagua?”<br />
<br />
“Mimi.”<br />
“Sasa mbona hukutaka kutembea uchi baada ya kujua kabisa dhamira yako ilikuwa nini juu ya Muddy?”<br />
“Nisamehe Balkis.”<br />
“Balkis unayemuomba akusamehe angefariki ungemuomba nani msamaha?”<br />
<br />
“Najua tulikuwa na dhamira mbaya kwako lakini tumegundua makosa yetu tunakuahidi hatutakufuata tena.”<br />
“Nilikuonyeni mara ngapi, kama ningekuwa na roho mbaya hata mali ya Muddy usingechukua. Lakini nilifanya vile ili muachane na mpenzi wangu, bado hamkusikia mliendelea kunichokonoa, kuonesha sitaki kuwafanya lolote nilimuua mganga wenu lakini bado mliendelea kunitafuta.<br />
<br />
“Mzee Njiwa Manga alitukutanisha mbele yake na kukuonyeni lakini bado mliona labda utani na kufikia hatua ya kumdharau kuwa hana uwezo wa kukabiliana na mimi. Mkaamua kwenda kwa mganga mwingine kwa lengo la kuchukua mali yangu na kunimalizia. Hebu nieleze ni kiumbe gani mwenye moyo wa uvumilivu wa kiasi hicho?”<br />
“Hakuna.”<br />
<br />
“Basi adhabu yangu ya awali ya kukutembeza uchi baada ya wewe mwenyewe kutamka kwa mdomo wako imetimia kama utamfuata Muddy. Ya pili nitakugeuza mbwa atakayeishi kwa mateso mpaka hapo nitakapojifungua salama. Kama mwanangu akifariki na wewe na mumeo mtakufa.”<br />
<br />
<span> “Ni...ni...ni..sa...sa...,</span><wbr></wbr><span class="word_break"></span>” hakumaliza kusema alitemewa mate usoni na Balkis huku akisema:<br />
“Kuwa mbwa mweusi.”<br />
Ashura aligeuka mbwa mweusi, Balkis aliendelea kusema:<br />
Kazi imeanza Ashura ameshageuzwa mbwa.</span></div><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123d655e94a1a96891584">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) EP.68.<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
Ya pili nitakugeuza mbwa atakayeishi kwa mateso mpaka hapo nitakapojifungua salama.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Kama mwanangu akifariki na wewe na mumeo mtakufa.”<br />
<br />
<br />
“Ni..ni..ni..sa..sa..,” hakumaliza kusema alitemewa mate usoni na Balkis huku akisema:<br />
“Kuwa mbwa mweusi.”<br />
<br />
<br />
Ashura aligeuka mbwa mweusi, Balkis aliendelea kusema:<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Hii ni adhabu itakayokufanya uhangaike, hutapendwa na wanadamu mpaka hapo utakapotoka kifungoni na sasa namfuata mwanaume wako, naye ana adhabu kubwa kuliko hii.”<br />
<br />
Balkis baada ya kusema vile aliondoka na kumuacha Ashura kwenye umbile la mbwa asijue aende wapi. Wazo lilikuwa kuendelea kuwa pale ufukweni mpaka jioni ndiyo aende kwake. <br />
<br />
Nyumbani, Tonny alikuwa akijiandaa kwenda kwenye mihangaiko yake akiamini kabisa Balkis aliamua kuwasamehe.<br />
<br />
Alikuwa anakwenda kwenye kabati kuchukua glasi ili anywe juisi kabla ya kuondoka.<br />
<br />
Hakujua kama Balkis tayari yumo mle ndani na alikuwa na hasira za ajabu baada ya kujua Tonny ndiye aliyekuwa na kimbelembele wa kumuua.<br />
<br />
<br />
Wakati anakwenda kwenye kabati alimpulizia vitu kama matone ya maji, Tonny alishtuka lakini hakujali sana. Alipokaribia kwenye kabati alishtuka kujiona amegeuka kiumbe wa ajabu.<br />
<br />
Kilichomshangaza ilikuwa ni kujiona kwenye kioo mwili wake ukiwa umeota mizizi na kutoka damu.<br />
<br />
Tonny alishtuka na kujiangalia, akawa anashangaa kuuona mwili wake ukiota mizizi iliyoingia ardhini huku ukitoa damu.<br />
<br />
Alianza kusikia maumivu makali zaidi ya mtu aliyeng’olewa jino bila ganzi.<br />
<br />
Alijiuliza yale mateso makali yanatokana na nini na kwa nini aote mizizi mwilini kama mti lakini hakupata jibu.<br />
<br />
<br />
Balkis alimwacha apate mateso makali kwa kuongeza kumpulizia maji maji mwilini na kuufanya mwili wa Tonny utoe ufa, kila sehemu ya mwili ilipasuka, damu zilimtoka na maumivu yake yalikuwa makali sana.<br />
<br />
Kila alipopiga kelele kuomba msaada sauti yake haikutoka.<br />
<br />
<br />
Alitamani ardhi ipasuke ili immeze lakini haikuwezekana.<br />
<br />
Alishangaa kuona damu yake iliyokuwa ikitoka mwilini, kila ilipondondoka chini ilipotea, akajiuliza inakwenda wapi lakini hakupata majibu.<br />
<br />
Maumivu aliyoyasikia hakukuwa na mfano wake. Alilia mpaka machozi yalimkauka kutokana na maumivu kuongezeka ukali kila dakika kutokana na mwili wake kupasuka kila kona.<br />
<br />
<br />
Balkis alitoa adhabu ile kwa zaidi ya saa mbili kisha alijitokeza mbele yake, Tonny alipomuona alishtuka na kutamani kumlamba miguu lakini hakuweza kutembea baada ya sehemu ya mwili wake kuzama chini ya ardhi.<br />
<br />
Kila alipofumbua mdomo kuomba msamaha sauti haikutoka akawa anarusha mikono kama anaimbisha kwaya bila ujumbe wake kumfikia mlengwa.<br />
<br />
<br />
Balkis alisimama na kumtazama kwa hasira, mara machozi ya damu yalimtoka akifikiria ampe adhabu gani kubwa kuliko zote alizowahi kumpatia kiumbe aliyemchukiza.<br />
<br />
Alitamani kumchuna ngozi na kumwacha atembee na maumivu bila kufa lakini alikumbuka adhabu ya kupasua pasua mwili ilikuwa inatosha kwani maumivu yake yalitofautiana kidogo na mtu aliyechunwa ngozi bila ganzi.<br />
<br />
Tonny aliendelea kurusha mikono kuomba msaada kama mtu aliyekuwa anataka kukata roho.<br />
<br />
<br />
Aliusikia mwili wake ukiwa umekauka kama kipande cha kuni kilichopigwa na jua kwa muda mrefu.<br />
<br />
Ulimi nao ulikauka kama mti na kushindwa hata kuunyanyua.<br />
<br />
Yalikuwa mateso makali kuliko hata shetani motoni, moyoni Tonny alijiapia kama atatoka salama kwenye mateso yale mazito asingerudia tena kufanya makosa.<br />
<br />
Aliona kuokoka kwake ni sawa na ngamia kupita katika tundu la sindano.<br />
<br />
<br />
Balkis alijikuta akiingiwa na huruma, alisogea karibu na kumshika kichwani.<br />
<br />
Dakika ileile Tonny alirudi katika hali ya kawaida lakini bado mwili wake ulimuuma kama kidonda.<br />
<br />
Tonny alipiga magoti mbele ya Balkis kuomba msamaha.<br />
<br />
<br />
“Najua tumekukosea, lakini nakuahidi hatutafanya upumbavu mwingine, tupo chini ya miguu yako, tunaomba utusamehe.”<br />
<br />
<br />
“Sawa mmekosa, hebu nielezeni kosa langu kwenu ni nini?”<br />
“Huna kosa lolote.”<br />
<br />
<br />
“Kwa nini mlidhamiria kuniua?”<br />
<br />
<br />
“Tusamehe Balkis ni shetani mbaya tu alitupitia.”<br />
<br />
<br />
“Leo unaniomba msamaha, ningekufa ungemuomba nani?”<br />
<br />
<br />
“Najua tumekukosea kwa kiasi kikubwa.”<br />
<br />
<br />
“Labda mlikuwa mnaona natania, mwenzako nimempa adhabu ya kutembea uchi mbele za watu muda si mrefu.”<br />
“Ha!” Tonny alishtuka kusikia vile.<br />
“Unashtuka nini, si alisema mbele yako akimrudia Muddy atafanya nini?”<br />
“Atatembea uchi.”<br />
“Mbona kamfuata mume wangu kupitia waganga.”<br />
“Nilikuwa sijui.”</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b001a2826291603"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123d655db768708393161">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) EP.69.<br />
<br />
<br />
“Najua tumekukosea kwa kiasi kikubwa.”<br />
“Labda mlikuwa mnaona natania, mwenzako nimempa adhabu ya kutembea uchi mbele za watu muda si mrefu.”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Ha!” Tonny alishtuka kusikia vile.<br />
“Unashtuka nini, si alisema mbele yako akimrudia Muddy atafanya nini?”<br />
“Atatembea uchi.”<br />
“Mbona kamfuata mume wangu kupitia waganga hakutembea uchi?”<br />
“Nilikuwa sijui.”<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Utajuaje na roho yako imejaa tamaa na harufu ya damu za viumbe wasio na hatia?”<br />
“Ni kweli nilikuwa na roho mbaya lakini nimeujua ubaya wangu, nitajirekebisha.”<br />
“Kama nilivyokueleza Ashura amevua nguo mbele za watu na kupata aibu ya mwaka.”<br />
“Mungu wangu yupo wapi?”<br />
“Atakuja usiku kwa njia ya kujifichaficha.”<br />
“Kwa hiyo nguo kavua kwa hiyari yake?”<br />
“Kwani wewe adhabu uliyoipata umeipenda?”<br />
“Hata.”<br />
“Au nikuongeze?”<br />
“U...u...usifanye hivyo ni...ni...”<br />
“Baada ya tapeli mwenzako kuvua nguo mbele za watu, na kumpa adhabu ndogo aliyoichagua mwenyewe pia nimempa adhabu yangu atakayotesekanayo kwa muda mrefu.”<br />
<br />
“Ungemsamehe nina imani hawezi kurudia tena,” Tonny alimuonea huruma Ashura na kujisahau yeye.<br />
“Kwa sasa sitawasamehe lazima nitimize kile nilichokipanga kuwafanyia.”<br />
“Usituue Balkis.”<br />
“Niliapa kamwe sitawaua ili kizazi chenu kijue madhara ya ubaya ni nini?”<br />
“Sasa utatufanya nini?”<br />
“Mpenzio tayari nimeshamgeuza kuwa mbwa.”<br />
“Mungu wangu!”<br />
“Na wewe kama nilivyokueleza nitakugeuza kuwa nzi wa kijana, maisha yako yatakuwa jalalani na chooni hakuna mwanadamu atakayekupenda.”<br />
“Jamani si nitakufa?”<br />
“Hutakufa, hayo ndiyo maisha niliyowachagulia baada ya kuwabembeleza kwa muda mrefu, Lakini mmekuwa na viburi pamoja na kuwatisheni bado mkawa na masikio magumu kama kenge, nina imani adhabu ya leo itakuonesha mimi ni kiumbe wa aina gani.<br />
<br />
<br />
Kwa vile sitaki dhambi ya kuua na kisasi ni haki ya kila kiumbe, nilichokuchagulia ndicho saizi yako.”<br />
“Balkis naomba uni...sa...sa... “<br />
Bwana wa Ashura hakumalizia kuomba msamaha alipuliziwa kitu kama unga huku Balkis akisema:<br />
“Kuanzia leo utakuwa nzi wa chooni.”<br />
<br />
<br />
Muda uleule Tonny aligeuka kuwa nzi wa kijani, ghafla mazingira ya pale nayo yakabadilika na kumfanya Tonny kuruka na kwenda moja kwa moja jalalani.<br />
<br />
Alijikuta akiishi maisha mapya ambayo yalimlazimisha kuishi chooni na kwenye majalala.<br />
<br />
<br />
Tonny pamoja na kuishi kwenye harufu kali ya mizoga na kinyesi hakuwa na jinsi kwa kuamini kuwa maeneo yale ndiyo yaliyokuwa salama kwake kwa kuogopa kuuawa na mwanadamu pale atakapokwenda ndani mwake kwa kuamini kuwa yeye ni binaadamu.<br />
<br />
<br />
Balkis baada ya kutoa adhabu ile alirudi kuilea mimba yake kwa kuamini kuwa hakukuwa tena na mwanadamu atakayemfuatilia maisha yake.<br />
<br />
Balkis alikuwa akiyafurahia maisha yake na Muddy kwa kuamini muda si mrefu wataitwa baba na mama.<br />
<br />
<br />
Baada ya kiza kuingia, Ashura aliondoka ufukweni na kurudi nyumbani akiwa katika umbile lake la mbwa.<br />
<br />
<br />
Alitembea huku akiomba Mungu afike salama nyumbani kwake, moyoni akijiuliza Tonny atamuelewa kutokana na umbile lake jipya alilokuwa nalo, alifikiria hivyo bila ya kujua kwamba mpenzi wake naye maisha yake yalikwishabadilika na kuwa kiumbe cha jalalani na chooni baada ya kugeuzwa kuwa nzi.<br />
<br />
<br />
Hakutembea umbali mrefu mvua kubwa ilianza kunyesha, alikimbilia kwenye nyumba moja iliyokuwa njiani na kujibanza upenuni.<br />
<br />
<br />
Mwenye nyumba alitoka na kumfukuza akiamini ni mbwa.<br />
<br />
Kutokana na mvua kuwa kubwa na barabara kujaa maji, Ashura alijitahidi kumwambia yule mwanadamu kuwa yeye si mbwa bali ni mwanadamu.<br />
<br />
<br />
Sauti yake ilikuwa ni ya mbwa kwa kuwa aliitoa kwa kubweka, tu hicho kilizidi kumuuzi mwenye nyumba ambaye aliingia ndani na kutoka na bakora na kumtoa mbio.<br />
<br />
Ashura hakuwa na jinsi ilibidi aingie kwenye mvua iliyokuwa ikiendelea kunyesha huku akiogelea kwenye maji machafu yaliyokuwa yakitoka kwenye mitaro.<br />
<br />
<br />
Aliendelea kunyeshewa na mvua kubwa iliyoambatana na radi, kuna kipindi alizama ndani ya maji na kujitahidi kuogelea ili kuendelea na safari yake.<br />
<br />
<br />
Hata alipopata sehemu ya kujibanza bado hakuona umuhimu wa kufanya hivyo kutokana na kusikia baridi kali mwilini mwake iliyotokana na kulowana kwa mvua.<br />
<br />
<br />
Aliendelea na safari yake yenye mateso huku akitaka amkute Tonny nyumbani na kuomba amtambue na kukubali kuishi naye kwenye umbile lile la mbwa.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123d655d3549622797272">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) EP.70.<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
Alitembea ndani ya maji katika mvua kubwa ya radi, kuna kipindi alizama ndani ya maji na kujitahidi kuogelea na kuendelea na safari yake.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
<br />
Hata alipopata sehemu ya kujibanza bado hakuona umuhimu wa kujibanza kutokana na kusikia baridi kali kutokana na kulowa mwili wote na maji.<br />
<br />
<br />
Aliendelea na safari yake yenye mateso ya shetani motoni huku akiomba Mungu amkute Tonny nyumbani pia amtambue na kukubali kuishi naye kwenye umbile la mbwa. SASA ENDELEA...<br />
<br />
Alishangaa kutembea umbali mrefu bila kufika, alijikuta akichoka huku njaa kali na kiu ikiwa imemshika na kushindwa kujua atakula wapi.<br />
<br />
<br />
Alipofika eneo ambalo alijua ndipo kwao alishangaa kuona hakuna nyumba yao, alizunguka mpaka kuna kucha huku akiteseka na baridi kali bila mafanikio.<br />
<br />
<br />
<br />
Ashura alitamani kifo lakini kilikuwa mbali naye, alijiuliza mateso yale mpaka lini au ndiyo ya kudumu lakini hakupata jibu.<br />
<br />
<br />
Alitamani amuone Balkis mbele yake ili amueleze ya moyoni kuwa amekoma na hatarudia tena katika maisha yake.<br />
<br />
Katika hali ya kawaida aliamini kabisa Balkis hakuwa na kosa lolote, japo walitaka kumuua mateso yale yalikuwa makubwa heri angemuua akajua moja lakini si mateso ya kutengwa na jamii kwa kumchukia kila atakapokwenda kwa kujulikana mbwa kumbe mwanadamu yalikuwa makubwa sana.<br />
<br />
<br />
Wakati akiteseka vile, Tonny naye alikuwa kwenye mateso mazito pembeni ya jalala kwenye tawi la mti uliokuwa na afadhali kutokana na mvua kuwa kubwa sana.<br />
<br />
<br />
<br />
Baada ya mvua kukatika aliendelea kukaa kwenye tawi lile ambalo mvua haikufika sehemu ile kama ingefika aliamini angekufa.<br />
<br />
<br />
Lakini chini yake kulikuwa na mzoga wa mbwa aliyekufa siku mbili zilizopita na kutoa harufu kali ambayo iliongezeka baada ya kunyeshewa na mvua.<br />
<br />
<br />
<br />
Harufu ilikuwa mbaya sana lakini hakuwa na jinsi, aliendelea kuvumilia kwa kuhofia kupoteza maisha yake kutokana na eneo lote kuwa na maji ya mvua iliyokuwa inanyesha kwa nguvu.<br />
<br />
<br />
Yalikuwa mateso makubwa kutokana na adhabu ya kuvuta harufu kali ya uchafu na mizoga.<br />
<br />
<br />
<br />
Njaa na kiu ilikuwa kali pamoja, licha ya umbile la kugeuzwa nzi bado alikuwa na akili za binadamu asingeweza kula mizoga wala kinyesi.<br />
<br />
<br />
<br />
Aliamini asingefikisha siku nyingi lazima angekufa kwa njaa.<br />
<br />
<br />
Aliwaza kama Balkis angetokea mbele yake angemuomba amuue kuliko kumtesa vile,<br />
<br />
kama siku moja hali ilikuwa vile kwa mwezi mzima ingekuwaje.<br />
<br />
Majira ya saa tisa za usiku akiwa amejikunyata kwa baridi kali la usiku kucha aliamshwa usingizini.<br />
<br />
<br />
Alipofumbua macho hakuamini kumuona Balkis mbele yake, alitaka kufunua mdomo wake kumuomba msamaha, lakini angewezaje kuzungumza katika umbile kama lile la nzi.<br />
<br />
<br />
<br />
Balkis alimchukua na kwenda naye sehemu na kumtemea mate, palepale Tonny alirudi katika umbile lake la kawaida.<br />
<br />
<br />
Alikuwa amemletea chakula kitamu, alimkaribisha.<br />
“Karibu chakula, najua huwezi kula chakula cha nzi ambacho ni kinyesi na uchafu kwa vile wewe bado mwanadamu.”<br />
<br />
<br />
“Ba..ba..ba..lkis naomba u..uni..samehe,” Tonny alipiga magoti huku akitetemeka.<br />
<br />
<br />
“Tonny sikuja kusikiliza msamaha wako, ulishaomba sana siku za nyuma, nimekuletea chakula kula niondoke.”<br />
“Basi niue kabisa chakula hiki sili,” Tonny alionesha jeuri kwa Balkis.<br />
<br />
<br />
“Tonny hunijui hata kuwaletea chakula kizuri ni huruma yangu, lakini mlitakiwa mle kinyesi na uchafu.”<br />
“Nimesema sili niue kabisa,” Tonny alionesha jeuri kwa Balkis kuonesha yupo tayari kwa lolote.<br />
<br />
<br />
“Tonny usinione nakuchekea ukaniona ni bwege mwenzio, sasa hivi nitakugeuza funza maisha yako yawe ndani ya kinyesi usiniletee upumbavu unijue eeh! Alaa,” Balkis alibadilika na kusema kwa hasira huku macho yake yakiwaka kama taa na usiku ule yalikuwa kama tochi yenye mwanga mkali.<br />
“Ba..ba..si ni..ni..<br />
<br />
”<br />
“Nyamaza mpumbavu mkubwa wewe, ni kiumbe gani anayeweza kuwaletea chakula na maji baada ya kutaka kumuua zaidi ya mara mbili?” Balkis alimuuliza huku amemshikia kiuno na kitumbo chake kilionekana kwa mbali.<br />
“Na..na..te..seka Balkis harufu ni mbaya sana naomba unitafutie adhabu nyingine.”<br />
<br />
<br />
“Huwezi kunichagulia adhabu kwa vile muda wa kubembelezana ulikwisha, hebu maliza kula nataka nimpelekee na mwenzako, muda unakwenda kukipambazuka ujue hali mpaka kesho kama saa hizi.”<br />
<br />
<br />
Tonny hakuwa na jinsi, alikula chakula kile kilichokuwa kitamu ajabu, hakuwahi kula chakula kitamu kama kile, alikuwa akijiuliza Balkis ni kiumbe gani pamoja na ubaya waliomfanyia bado kawaletea chakula kitamu na maji. Moyoni aliamini huenda atamsamehe.<br />
<br />
<br />
Lakini ilikuwa tofauti na alivyodhania baada ya chakula ambacho alishiba vizuri na kunywa maji matamu, alimpulizia vitu kama unga, vilipomgusa usoni palepale aligeuka hali yake ya mwanzo ya nzi........JE NINI KITAENDELEA?</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b098d4693816428"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123e0b5a1f78d24702996">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) .....EP.71.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
Lakini ilikuwa ni tofauti na alivyodhania baada ya kula chakula ambacho alishiba vizuri na kunywa maji matamu, Balkis alimpulizia vitu kama unga vilipomgusa usoni, palepale aligeuka hali yake ya mwanzo ya nzi.<br />
<span class="text_exposed_show"> SASA ENDELEA ...<br />
<br />
Alitamani kuomba msamaha lakini alichelewa, alichukuliwa na kurudishwa kwenye tawi la mti na kukumbana tena na harufu kali ya uchafu wa mzoga wa mbwa aliyekuwa akinuka.<br />
<br />
Kwa harufu ile kama angekuwa katika umbile la kibinaadamu basi angetapika mpaka utumbo. Lakini bahati nzuri alikuwa kwenye umbile la nzi, aliendelea kuteseka na harufu na baridi kali.<br />
<br />
Balkis baada ya kutoka kwa Tonny alikwenda moja kwa moja kwa Ashura aliyekuwa amelala pembeni ya nyumba mbovu.<br />
Karibu yake kulikuwa na mtaro wa maji machafu lakini yeye aliichagua sehemu iliyokuwa kavu. Lakini ukali wa ubaridi ulikuwa ukimpata kisawasawa.<br />
<br />
Alijuta kwa mambo yote aliyoyafanya kwa kuwatepeli wanaume kwa ajili ya Tonny ambaye ndiye aliyemuingiza kwenye kazi ile ya kuolewa na wanaume na mwishowe kuwadhulumu kwa kuvunja uhusiano.<br />
<br />
Kitu kilichowafanya wanaume zaidi ya wawili kujiua baada ya kufilisika na wengine kupatwa na ukichaa.<br />
Aliamini hali ile ingemtokea na Muddy lakini kwa bahati ya ajabu Balkis aliyaokoa maisha yake. Alitamani Balkis atokee mbele yake amuombe msamaha lakini hakuonekana.<br />
Usingizi ulimpitia pale alipokuwa amejilaza huku akichonyotwa na njaa pamoja na kiu.<br />
<br />
Alishtuliwa kutoka usingizini na kujiona akiwa mbele ya Balkis, kama Tonny alivyotaka kuomba msamaha, naye alikuwa kama anataka kumuuma Balkis aliyemchukua na kumpeleka sehemu iliyokuwa nzuri, alimtemea mate na muda uleule alibadilika kurudia katika umbile lake la kibinadamu.<br />
<br />
Ashura baada ya kurudi katika hali yake ya kawaida alipiga magoti mbele ya Balkis na kuanza kuomba msamaha.<br />
“Balkis nisamehe sana nimekosa, adhabu ya leo inatosha hali yangu ni mbaya,” alisema huku akibubujikwa na machozi.<br />
<br />
“Hii si adhabu ya siku moja ni ya muda mrefu kama nilivyokueleza muombeni Mungu nijifungue salama, kama mwanangu akifa au mimba ikitoka mjue na nyinyi maisha haya yatakuwa ya milele kwenu.”<br />
“Naomba unisamehe, sitarudia tena, niliyokutananayo leo yanatosha, ukiongeza zaidi nitakufa.”<br />
<br />
“Ashura sikufuata kuombwa msamaha, nimekuletea chakula, kula haraka kabla hapajakucha, ukichelewa utalala na njaa, kuonana na mimi tena ni mpaka kesho muda kama huu, tapeli mwenzako kanichelewesha na wewe unataka kufanya hivyo.”<br />
<br />
“Nani, Tonny?”<br />
“Eeh.”<br />
“Yupo wapi?”<br />
“Yupo jalalani.”<br />
<br />
“Anafanya nini?”<br />
“Kwani nzi makazi yake wapi?”<br />
“Mungu wangu umemgeuza kuwa nzi?”<br />
<br />
“Tena ana bahati angeendelea kuniletea ujeuri ningemgeuza kuwa funza na makazi yake yangekuwa kwenye kinyesi milele.”<br />
“Sa...sa...”<br />
“Ee...eeh! Hebu kula niondoke.”<br />
<br />
Ashura hakuwa na jinsi alikula chakula kitamu na kuamini kama Balkis ameamua kumletea chakula ambacho hakuwahi kula katika maisha yake ya kibinaadamu, lazima atakuwa amerudiwa na roho ya huruma na kumsamehe.<br />
<br />
Lakini dhana yake ilikuwa ni tofauti, baada ya kumaliza kula alirudishwa katika umbile lake la mbwa na kurudishwa alipotolewa na Balkis akatoweka.<br />
****<br />
Siku zilikatika huku adhabu ya Ashura na mwanaume wake zikiendelea, walikuwa wakiteseka kwenye maumbile yao ya mbwa na nzi. Maisha ya Tonny yalikuwa ya jalalani na chooni japo hakuweza kula uchafu.<br />
Ashura maisha yake yote yalikuwa ni kuzurura jiji zima kutafuta sehemu iliyokuwa salama kutokana na kukimbizwa kila kukicha na watoto watukutu.<br />
<br />
Mimba ya Balkis iliendelea vizuri na baadaye alijifungua salama salmini watoto mapacha wa kike na kiume, kila mmoja alifanana na mzazi wake mmoja.<br />
Wa kike alifanana sana na mama yake na wa kiume alifanana na baba yake. Balkis alifurahi sana na kuamini dhamira yake ilitimia.<br />
<br />
Aliamua kwenda chini ya bahari na wanawe kuwatambulisha kwa wazazi wake, wakati akiwa njiani kuelekea chini ya bahari.<br />
Baba yake Mfalme Barami alikuwa na mazungumzo mazito na mkewe juu ya kukosa taarifa za Balkis.<br />
<br />
“Mke wangu hivi huyu mtoto anataka kupimana nguvu na mimi?”<br />
“Kwani tatizo ni nini?”<br />
<br />
“Hulioni? Tangu nilipomueleza aachane na yule mwanaume amepotea, haleti tena vizazi vya wanawake mwaka unakatika.”<br />
“Mume wangu jambo hili linatakiwa busara siyo kutumia nguvu.”<br />
<br />
“Kama anaona ni utani, nitamtuma Pweku mtwana mkuu akamuulie mbali huyo mwanaume wake.”<br />
“Mume wangu unatafuta vita mpya.”<br />
“Na nani?”<br />
<br />
“Siamini kama Balkis atakubali kirahisi mwanaume wake auliwe, atawamaliza watwana wako wote kwa kuwaua.”<br />
<br />
“Inamaana sasa hivi mwanao anataka kunipanda kichwani?”<br />
<br />
Walinyamaza kuzungumza baada ya kusikia kelele za chereko chereko nje, zilikuwa ni shamrashamra zilizowashangaza wote.<br />
<br />
Msafara ulikuwa ukiingia ndani, ukiongozwa na vijakazi na watwana akiwemo mtwana mkuu Pweku, sherehe kama ile hutumika kukaribisha mgeni aliyezaliwa.<br />
<br />
Balkis alionekana akiwa juu kwenye farasi mwenye matandiko ya dhahabu.<br />
Mama yake Balkis Malkia Huleiya alipowaona watoto wa Balkis, alikimbia kwenda kumpokea mwanaye na wajukuu zake kwa furaha ya ajabu.<br />
<br />
Mfalme Barami alikuwa amebaki njia panda, asielewe kilichokuwa kikiendelea mpaka wageni wale walipokuwa wakiingia ndani, hakujua watoto wale aliokuwanao Balkis walikuwa ni wa nani.</span></div></span></div><span class="fcg"></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123e24517714e24734431">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) .....EP.72.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
Mama Balkis, Malkia Huleiya alipowaona watoto wa Balkis alikimbia mbio kwenda kumpokea mwanaye na wajukuu zake kwa furaha kubwa. Mfalme Barami alikuwa bado yupo njia panda, mpaka wanaingia ndani hakujua watoto aliokuwa nao Balkis ni wa nani.<br />
<span class="text_exposed_show"> SASA ENDELEA...<br />
<br />
BAADA ya kuingia ndani, Balkis alijua amefanya makosa. Alipiga magoti mbele ya baba yake na kusema:<br />
“Mtukufu mfalme wa bahari, najua nitakuwa nimefanya kosa kubwa la kuzaa na binadamu, lakini sikuwa na jinsi. Nimefanya hivi kutokana na moyo wangu kuwa na hofu kuu kwa Muumba wetu.<br />
<br />
Niliamua kukaidi amri yako na kufunga ndoa na binadamu ambaye niliamini atanisaidia kupata watoto ambao ndiyo ilikuwa kiu yangu kubwa.<br />
<br />
Pia nilijua nitaepukana na dhambi ya kuvunja ndoa za watu pia kuwanyima watu haki zao za kupata watoto. Najua nimekukosea lakini uamuzi huu niliona unafaa kwa kuamini siku ya mwisho mbele ya Muumba nitahukumiwa mwenyewe kwa vile tayari najua zuri na baya.<br />
<br />
Hawa mbele yako ni wanangu wapendwa Zaaanuna na Labeiiki, kwa vile nimefanya kosa una haki ya kunifanya lolote, nipo radhi kwa adhabu yoyote ila nakuomba usiwaue wanangu.”<br />
Kauli ile ilikuwa kama mshale mkali moyoni kwa Mfalme Barami.<br />
<br />
Aligeuka bubu ghafla na kushindwa amfanye nini Balkis, mwanaye kipenzi aliyefanya kosa kubwa la kuzaa na binadamu. Lakini mke wake naye aliwahi mbele ya mume wake na kupiga magoti kumuombea msamaha mwanaye.<br />
<br />
“Mume wangu, Balkis ndiye mtoto wetu wa pekee, kama kosa amekwishafanya. Najua amekuudhi sana lakini nakuomba umsamehe mwanao. Kama adhabu naomba unipe mimi mama yake, nipo radhi kwa adhabu yoyote lakini wajukuu zangu usiwaguse.”<br />
“Kwa kweli hata sijui nifanye nini, basi tu kwa vile ni mwanangu lakini bila hivyo ningekuchemsha supu na kukunywa kwa jinsi nilivyochukia.”<br />
<br />
“Najua nimekuudhi sana baba yangu lakini niliamini kuna aliye zaidi yako ambaye si mwingine bali Muumba wetu ambaye ana uwezo wa kufanya lolote bila kuingiliwa na mtu. Ni yeye ndiye mwenye adhabu kali yenye kuumiza.”<br />
“Nimekuelewa mwanangu sina jinsi, karibu nyumbani wewe na wajukuu zangu ambao siwezi kuwafanya lolote kwa vile hawana hatia.”<br />
<br />
“Baada ya kunisamehe naomba nimlete na mkweo mbele yenu mumtambue.”<br />
“Kwa vile tayari una watoto wake hatuna la kufanya zaidi ya kukubali kumtambua.”<br />
“Na hawa watoto watakuwa wa nani?” Malkia Huleiya alimuuliza Balkis.<br />
<br />
“Ni wa kwetu wote.”<br />
“Wataishi wapi?”<br />
“Huku, duniani watakuja siku moja moja.”<br />
“Kwa hiyo hata mimi nitafurahi kucheza na wajukuu zangu,” Malkia Huleiya alionesha furaha kubwa.<br />
Ilikuwa ni furaha kubwa kusamehewa na kutambuliwa rasmi watoto wa Balkis kwa mfalme Barami.<br />
***<br />
Balkis baada ya kupata ruhusa ya kumpeleka mume wake kwao, alijikuta akijawa na mawazo juu ya kumweleza Muddy kuwa yeye ni jini, tena anayeishi chini ya bahari. Siku zote Muddy alijua Balkis ni binadamu wa kawaida. <br />
<br />
Alirudi hadi duniani na kumkuta Muddy amejipumzisha sebuleni akisikiliza nyimbo laini kutokana na kuambukizwa na Balkis kupenda kusikiliza nyimbo za Bara Asia.<br />
“Vipi mbona umerudi peke yako, watoto wapo wapi?” Muddy alimuuliza Balkis baada ya kumuona yupo peke yake.<br />
“Nimewaacha nyumbani.”<br />
<br />
“Mke wangu, watoto wadogo kama wale umewaacha nyumbani?”<br />
“Nimekufuata wewe twende kwa wazazi wangu.”<br />
“Mmh! Itakuwaje si ulisema baba yako mkali sana?”<br />
“Ni kweli lakini kwa sasa hakuna tatizo, watoto wamemaliza kila kitu.”<br />
“Sawa tunaweza kwenda.”<br />
<br />
Siku zote Muddy alijua Balkis hakai nje ya Dar es Salaam, kabla ya kuondoka Balkis alijikuta akipata wakati mgumu kumueleza Muddy kuwa yeye ni jini, lakini mwenzake aliitambua hali ile mapema. Alimsogelea na kuzungumza naye kwa sauti iliyomtoa machozi Balkis.<br />
“Nini tena malkia na kipenzi changu?”<br />
<br />
“Muddy nina wakati mgumu wa kujieleza kwako.”<br />
“Kujieleza nini tena mpenzi wangu?”<br />
“Najua hunifahamu vizuri, nina imani ukinielewa unaweza kuniacha.”<br />
“Siwezi kukuacha, hata ungekuwa jini siwezi kukuacha nakupenda sana Balkis.”<br />
<br />
Kauli ya kusema hata kama angekuwa jini ilimshtua sana Balkis na kujiuliza anayosema ni kweli au ni kusherehesha maneno. Lakini kwa njia nyingine yalimpa nguvu ya kusema bila wasi.<br />
“Muddy unanipenda?” alimuuliza huku akimtazama kwa jicho la mahaba.<br />
“Zaidi ya kukupenda.”<br />
<br />
“Nikikueleza kitu huwezi kuniacha?”<br />
“Hata ukisema unahitaji uhai wangu, kwa mapenzi yangu mazito kwako nipo tayari na nitakufa nakupenda.”<br />
“Kweli Muddy?”<br />
“Kweli kabisa kwani bila wewe sasa hivi mimi ningekuwa nani?”<br />
“Muddy mimi si binadamu.”<br />
<br />
“Kama si mwanadamu wewe ni nani?”<br />
“Mimi ni jini.”<br />
“Nani?” Muddy alishtuka na kusogea nyuma toka alipokuwa amekaa, kitendo kile kilimfanya Balkis apige magoti mbele ya Muddy kuomba asimuache.</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123cb4b241e3235489085"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_50123e24501907231357759">JINI LA DARAJA LA SALENDA (Balkis) .....EP.73.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA<br />
“Muddy unanipenda?” Alimuuliza huku akimtazama kwa jicho la mahaba.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Zaidi ya kukupenda.”<br />
“Nikikueleza kitu huwezi kuniacha?”<br />
<br />
“Hata ukisema unahitaji uhai wangu, kwa mapenzi yangu mazito kwako nipo tayari na nitakufa nikikupenda.”<br />
“Kweli Muddy?”<br />
“Kweli kabisa, kwani bila ya wewe sasa hivi mimi ningekuwa nani?”<br />
“Muddy mimi si mwanadamu.”<br />
<br />
“Kama si mwanadamu ni nani?”<br />
“Mimi ni jini.”<br />
“Nani?” Muddy alishtuka na kusogea nyuma kutoka alipokuwa amekaa, kitendo kile kilimfanya Balkis apige magoti mbele ya Muddy na kumuomba asimuache. SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Muddy usiniache<br />
nakupenda sana.”<br />
“Balkis unayosema ni kweli?”<br />
<br />
“Kweli mpenzi wangu mimi ni jini la chini ya bahari na baba yangu ni mfalme wa majini katika bahari hiyo. Kukubali kuwa na mimi umeokoa vizazi vya wanawake mia ambavyo nilitakiwa nivitoe ili nipate dawa ya uzazi na kuniwezesha kuolewa na jini mwenzangu.”<br />
“Balkis unayosema ni kweli?”<br />
<br />
“Ni kweli kabisa.”<br />
“Kwa nini hukunieleza mapema?”<br />
“Ujini wangu ndiyo uliokoa maisha yako na hata kuendelea kukulinda na akina Ashura waliokuwa wakiendelea kuyafuatilia maisha yetu.”<br />
<br />
“Balkis japo moyo wangu umeshtuka kusikia wewe ni jini lakini bado nitaendelea kukupenda maisha yangu yote. Sikuwahi kuamini kama jini ana roho nzuri kuliko mwanadamu, niliamini majini ni wabaya na kama ungenieleza mwanzo ningeachana na wewe.<br />
Nakuahidi kwenda mbele ya wazazi wako kujitambulisha na kuwa tayari kuishi na wewe.”<br />
Kauli hiyo ilimfanya Balkis alie machozi ya furaha na kumkumbatia Muddy.<br />
<br />
“Asante Muddy kwa kuonesha mapenzi ya kweli, nitakupenda milele.”<br />
“Nikushukuru wewe kuonesha mapenzi ya kweli kwangu pia, kulinda maisha yangu kwa nguvu zote.”<br />
“Muddy niwafanye nini akina Ashura waliopanga kukuua na kuniua mimi?”<br />
“Kwani bado wanatufuatilia?”<br />
<br />
“Walikuwa wanataka kuniua nikawawahi na kuwageuza mbwa na nzi ili niweze kujifungua salama.”<br />
“Kwa hiyo mpaka sasa bado wapo katika hali hiyo?” Muddy alishtuka.<br />
“Ndiyo.”<br />
“Wewe ulitaka kuwafanya nini?”<br />
<br />
“Lolote utakaloliamua wewe nipo tayari kulifanya kwa vile umeusikia ubaya wao.”<br />
“Naomba uwasamehe.”<br />
“Kwa kuwa umesema wewe nitawasamehe.”<br />
Naomba kabla ya kwenda kuwaona wazazi wako wawe wamerudi katika hali yao ya zamani.”<br />
<br />
Baada ya makubaliano, Balkis alitoka na kurudi na mbwa na nzi aliyekuwa juu ya mgongo wa mbwa na kusema:<br />
“Hawa ndiyo maadui zetu.”<br />
Muddy hakuamini kuwaona mbwa na nzi na kuelezwa kuwa ni Ashura na mwanaume wake. Balkis aliwatemea mate wote wakarudi katika hali yao ya kawaida ya kibinaadamu.<br />
<br />
“Mna bahati kubwa kwa kuwa mpenzi wangu amewasamehe, japo hata mimi nilikuwa na wazo la kuwasamehe, nashukuru Mungu nimejifungua salama. Kuanzia leo nina imani kwa adhabu ndogo ambayo hailingani na dhamira yenu ya kuniua kwa kipindi cha mateso imetosha kuwafanyeni viumbe wapya. Naomba mkaendelee na maisha yenu.”<br />
<br />
“Asante Balkis, asante Muddy, tunaapa kwa mbigu na ardhi kuwa hatutathubutu hata kuua nzi, mateso tuliyoyapata yametosha. hatukufa lakini cha moto tumekiona.”<br />
“Nakutakieni maisha mapya nina imani mtakuwa viongozi wema na kuwaeleza watu kuwa ubaya haulipi na jini si mbaya ila roho mbaya ya kiumbe chochote ndiyo mbaya.”<br />
<br />
Ashura na mwanaume wake walirudi kwao na kukuta kila kitu chao kikiwa katika hali ya usalama. Balkis naye alikwenda mpaka chini ya bahari kumtambulisha mumewe Muddy. Ilikuwa sherehe kubwa ambayo haikuwahi kutokea chini ya bahari iliyobadilisha amri ya jini kuolewa na mwanadamu.<br />
<br />
Pia, Balkis alichukua nafasi ile kuwarudishia vizazi vyao wanawake wote ambao baada ya kusumbuka sana kutafuta watoto, wote walifanikiwa kupata watoto bila kujua kuwa kitendo cha Muddy kumkubali Balkis ndiyo ilikuwa tiba yao.<br />
Baada ya hapo maisha ya Muddy na Balkis yaliendelea bila watu kujua kama Balkis ni jini zaidi ya Ashura na mwanaume wake. Muddy na Balkis kila mmoja alimpenda mwenzake mapenzi ya dhati.<br />
<span> *******MWISHOOOOOO********</span><wbr></wbr><span class="word_break"></span>**********8</span></div></span></div></div></div></div></div></div></div></div></div></div></div></div></div></div></div></div></div></div></span></div><span class="fcg"> </span>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com5tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-73625961877052066192012-07-23T11:16:00.001-07:002012-07-23T11:16:05.198-07:00STORY BOMBA YA MALOVEEEE.....<a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/my-wifeep1.html?spref=bl"></a><span class="hasCaption"></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c01c1fdc0f76208524"> <img alt="" class="spotlight" src="https://fbcdn-sphotos-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash4/427916_353507498042165_1653511438_n.jpg" style="height: 338px; width: 480px;" /></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c01c1fdc0f76208524"> </div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c01c1fdc0f76208524">USIFE HARAKA MPENZI WANGU<br />
<br />
HANA haraka anapotembea, ukimtazama anaonekana kujiamini sana. Tabasamu mwanana linaupamba uso wake, lakini mavazi yake yanaonesha asivyo mtu wa dhiki! Hata kama siyo sana, lakini uwezo wa kubadilisha mboga ulikuwa mikononi mwake!<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Anatoka kwenye duka hili maalum kwa kuuza kadi na zawadi mbalimbali lililopo ghorofa ya saba, katika jengo moja la KPC Towers, katikati ya Jiji la Dar es Salaam. Anatembea taratibu kuifuata lifti iliyokuwa mita chache sana mbele yake.<br />
Anatabasamu!<br />
Ni kweli anatabasamu!<br />
<br />
Tena basi alikuwa na kila sababu ya kutabasamu, maana zilibaki wiki tatu tu, kabla ya ndoa yake na mpenzi wake wa siku nyingi Cleopatra ifungwe. Mkononi mwake ana bahasha ya khaki ambayo ndani yake kuna zawadi kwa ajili ya Cleopatra wake. Alijua anachotakiwa kumfanyia Cleopatra!<br />
<br />
Siku zote alikuwa akinunua apple tu, mambo yanakuwa sawa! Huo ulikuwa ugonjwa mkubwa zaidi kwa Cleopatra. Alipoifikia, akabonyeza kitufe fulani mlangoni, mlango ukafunguka. Akaingia na kusimama, punde mlango ukajifunga, akabonyeza kwenye herufi G akimaanisha kwamba anataka kushuka chini!<br />
<br />
Ni kijana mtanashati sana, anayevutia kwa kila mwanamke aliyekamilika. Anaitwa Deogratius Mgana. Mfanyakazi wa shirika moja lisilo la kiserikali jijini Dar es Salaam. Ana furaha moyoni mwake, maana anakwenda kufunga ndoa na chaguo lake.<br />
<br />
Kwanini asitabasamu!<br />
Hakika ana haki ya kutabasamu!<br />
“Ni kweli lazima nitabasamu, kwanza nusu ya ndoto zangu tayari zipo kwenye mstari. Lazima nijisikie vizuri,” akawaza mwenyewe akiwa kwenye lifti.<br />
<br />
Akabaki ametulia kimya akiwa amesimama kwenye lifti ile, ikaanza kushuka taratibu kwenda chini. Ghorofa ya sita, ghorofa ya tano, ghorofa ya nne...alipofika ghorofa ya tatu, lifti ikasimama. Hapo akajua kuna mtu aliyekuwa akitaka kushuka chini. Mlango ulipofunguka, wakaingia wanaume watatu, wote wamevaa miwani za jua.<br />
“Mambo bro?” Mmoja akasalimia.<br />
<br />
“Poa,” akaitikia Deo.<br />
Lifti ikaanza kushuka taratibu, walipofika ghorofa ya tatu, ikasimama. Mlango ulipofunguka tu, ghafla wale vijana watatu wakamsukuma hadi nje. Mara mlango ukafunga.<br />
<br />
“Paaaaaa!” Mlio wa risasi ukasikika.<br />
Deo akaanguka chini, akianza kuvuja damu!<br />
<br />
* * *<br />
Alisikia vizuri sana mlio wa simu yake, lakini aliamua kupuuzia! Si kwamba hakutaka kwenda kupokea, lakini alikuwa na kazi muhimu sana aliyokuwa akiifanya, zaidi ya kwenda kupokea simu!<br />
Cleopatra alikuwa anapika!<br />
<br />
Chakula kizuri ambacho mpenzi wake alikuwa anakipenda sana. Alikuwa anapika viazi vya kukausha, maarufu kama maparage, ambavyo Deo alikuwa akipenda sana. Siku hiyo Deo alipanga kwenda nyumbani kwa akina Cleopatra, Mikocheni.<br />
<br />
Ilikuwa zimebaki wiki tatu tu ndoa yake na Deo ifungwe. Siku ambayo alikuwa akiitamani sana na kuomba ifike haraka. Mlio wa simu yake ukaisha ghafla. Akaendelea na mapishi yake jikoni, lakini baada ya muda mfupi sana, simu ikaita tena kwa mara nyingine...<br />
<br />
“Nani huyo aaah!” Cleopatra akasema kwa hasira kidogo.<br />
“Mi’ nampikia Deo wangu bwana alaaah!” Akasema tena, akifunika kile chakula jikoni na kufunga kanga vizuri.<br />
Yap! Kama ungekuwepo, ungeamini kweli Cleopatra alikuwa mwanamke mrembo. Pamoja na kwamba alikuwa amevaa kanga, lakini umbo lake lenye namba nane liliweza kuonekana vyema kabisa. Cleopatra alijaaliwa umbo zuri sana la kuvutia.<br />
<br />
Ona anavyotembea...<br />
Kama anaionea huruma ardhi. Ana hips pana zinazozidisha uzuri wake, ana macho mazuri yenye uwezo wa kumchanganya mwananaume yeyote yule. Labda niseme kwamba, Cleopatra alikuwa mwanamke mrembo sana.<br />
<br />
Alivyofika sebuleni, simu ikaacha kuita. Akachukia sana, lakini akiwa anainua ili aweze kujua aliyekuwa akimpigia ili aweze kumpigia tena, akashangaa simu yake ikianza kuita tena. Kwenye kioo cha simu yake likaonekana jina ‘My Deo’!<br />
“Jamani, kumbe ni sweetie!” Akasema akibonyeza kifufe cha kijani ili kumsikiliza.<br />
<br />
Ilikuwa ni namba ya Deo ikionekana kwenye kioo cha simu yake...<br />
“Yes baby, najua hujasahau kuninunulia apple na napenda kukujulisha kwamba, maparage yako yanakaribia kuiva, ila sijui ungependa nikuandalie juice ya nini? Machungwa, maparachichi, maembe au mananasi? Maana kila kitu kipo kwenye friji!” Cleopatra akasema kwa sauti iliyojaa mahaba mazito sana.<br />
<br />
“Samahani dada, mimi siyo mwenye simu!” Sauti hii ya kiume, tulivu yenye mikwaruzo kwa mbali ilisikika kwenye simu ya Cleopatra.<br />
“Sasa kama wewe si mwenye simu, kwanini umepiga? Kwanini unakosa ustaarabu?” Cleopatra akamwuliza yule mtu akiwa na hasira sana.<br />
<br />
“Samahani sana dada’ngu, lakini nadhani ni vyema ukawa mtulivu na kuuliza kilichotokea. Si kawaida mtu kupiga simu isiyo yake kwa watu ambao wamehifadhiwa kwenye simu hiyo. Hiyo ingetosha kabisa kukufanya ugundue kwamba kuna tatizo!” Mtu huyo akasema akizidi kuonesha kwamba anahitaji utulivu wa Cleopatra.<br />
<br />
“Ndiyo...enhee kuna nini? Hebu niambie, maana tayari nahisi nimeanza kuchanganyikiwa!”<br />
“Sina shaka wewe ndiye Cleopatra!”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Ni nani wako?”<br />
<br />
“Ni mchumba’ngu, kwani vipi?”<br />
“Usijali, tuliza moyo dada yangu. Mimi ni Dk. Palangyo wa Hospitali ya Taifa Muhimbili. Huyu ndugu mwenye simu, ameletwa hapa na wasamaria wema, baada ya kupitishwa katika Kituo cha Polisi Oysterbay!”<br />
“Anaumwa na nini dokta?” Cleopatra akauliza akianza kulia kwa huzuni.<br />
<br />
“Amepigwa risasi na watu wasiojulikana katika Jengo la KPC Towers. Hata hivyo, hana hali mbaya sana, matibabu yanaendelea, lakini nimeona ni vyema kukujulisha ili uwafahamishe na ndugu wengine!”<br />
“Asante dokta kwa taarifa, baada ya nusu saa nitakuwa hapo,” Cleopatra akajibu akizidisha kilio chake.<br />
<br />
Akatoka mbio, hadi chumbani kwake. Hakukumbuka kwenda kuipua chakula jikoni. Akavaa haraka na kutoka hadi getini! Ghafla kumbukumbu zake zikarudi!<br />
“Mama yangu, nimeacha chakula jikoni na jiko linawaka,” akawaza akirudi ndani mbio.<br />
<br />
Ilikuwa ni hatari sana, maana alikuwa anapikia jiko la umeme. Mara moja akarudi ndani na kuzima jiko, akaipua kile chakula na kutoka kwa kasi sana.<br />
“Wewe vipi mwenzetu, mbona hivyo?” Mama yake Cleopatra akamwuliza baada ya kumuona mwanaye anaonekana kuwa na haraka ambayo hakujua ni ya nini.<br />
<br />
“Nitakupigia simu mama!”<br />
“Unakwenda wapi?”<br />
“Mama nitakupigia!”<br />
“Patra, mwenzako si anakuja au haji tena?”<br />
<br />
“Mama Deo amepigwa risasi, yupo hospitalini,” akasema Cleopatra akiwa tayari ameshaingia kwenye gari.<br />
Akapiga honi kwa nguvu, mlinzi akafungua haraka. Cleopatra akaondoa gari kwa kasi sana. Alikuwa anakwenda Muhimbili, huku nyuma akiwa amemuacha mama yake akiwa mwenye mawazo.</span></div><br />
<div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"> </span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"> </span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5eb365e03683586">USIFE KWANZA MPENZI WANGU......EPISODE 2.<br />
<br />
Akiwa jikoni anaandaa chakula kwa ajili ya mpenzi wake, Cleopatra anapokea simu kutoka Muhimbili, akipewa taarifa kwamba Deo, mpenzi wake amepigwa risasi na amelazwa. Taarifa hizo zinamshtua sana. Anatoka na gari haraka kwenda hospitalini. Nini kitatokea? Endelea...<br />
<br />
CLEOPATRA aliendesha gari kwa kasi sana, hakujali ajali barabarani, alikuwa tayari kwa lo<span class="text_exposed_show">lote litakalotokea! Aliendesha kwa kasi ya ajabu sana. Kutokea nyumbani kwao Mikocheni hadi Muhimbili, alitumia dakika ishirini!<br />
<br />
Hakukubali kukaa foleni, aliendesha kama daladala, kwani alipenyeza pembeni, sehemu zilizokuwa na foleni kubwa. Alipofika hospitalini, akaegesha gari lake kisha akapiga zile namba na kuzungumza na yule daktari.<br />
<br />
“Nimeshafika dokta!”<br />
“Ok! Uko wapi?”<br />
“Kwenye maegesho!”<br />
“Tukutane MOI!”<br />
<br />
“Sawa dokta.”<br />
Bila kupoteza muda, Cleopatra akachanganya miguu hadi ilipo wodi ya Taasisi ya Mifupa (MOI). Akiwa kwenye lango kuu la kuingilia, akamwona mwanaume mmoja mrefu aliyevaa koti jeupe na miwani, akahisi angekuwa ndiye daktari aliyekuwa akimfuata.<br />
<br />
“Sorry, ni dk. Pallangyo?” Cleopatra akauliza akimkazia macho.<br />
“Yes, karibu!”<br />
“Ahsante!”<br />
“Nifuate!”<br />
<br />
Dk. Pallangyo akatangulia na Cleopatra akimfuata nyuma. Safari yao ikaishia ofisini kwa daktari yule.<br />
“Karibu sana dada yangu!”<br />
“Ahsante!” Cleopatra akajibu na kuketi kwenye kiti, kwa mtindo wa kutazamana na daktari.<br />
<br />
“Ulisema mgonjwa ni nani wako?”<br />
“Mchumba wangu!”<br />
<br />
“Oh! pole sana...kilichotokea ni kwamba, mwenzio amepigwa risasi ya begani, lakini inaonekana kutokana na mshtuko alioupata, umesababisha apoteze fahamu. Tunashukuru kwamba risasi haijatokeza upande wa pili, kwahiyo tumefanikiwa kuitoa, lakini bado hajazinduka!”<br />
<br />
“Mungu wangu, atapona kweli?”<br />
“Uwezekano huo ni mkubwa sana, lakini tuombe Mungu, naamini atakuwa sawa.”<br />
<br />
“Naweza kwenda kumuona tafadhali?”<br />
“Bila shaka!” Dokta akamjibu na kusimama.<br />
<br />
Akaonesha ishara kwamba Cleopatra amfuate. Akasimama na kumfuata nyuma yake.<br />
<br />
* * *<br />
Deogratias alikuwa amelala kimya kitandani, Cleopatra akiwangalia kwa jicho la huruma, simanzi tele ikiwa imemjaa moyoni mwake. Moyo wake unashindwa kuvumilia, macho yake yanazingirwa na unyevunyevu. Chozi linadondoka!<br />
<br />
Chozi la huzuni!<br />
Deo ametulia kitandani, mwili wake ukiwa umefunikwa kwa shuka jeupe, isipokuwa kuanizia kifuani, bandeji inaonekana mkononi mwake. Mapigo ya moyo wake yanakwenda taratibu kabisa!<br />
<br />
“Deo wangu...Deo...Deo jamani...amka mpenzi wangu. Naomba usife kwanza mpenzi wangu jamani. Hebu amka baby, tufunge ndoa...bado nakupenda...” akasema Cleopatra akilia kwa uchungu.<br />
<br />
Deo hakusikia kitu, alikuwa katika usingizi mzito akiwa hajui chochote kinachoendelea. Alikuwa amepoteza fahamu na hakuwa na uwezo wa kusikia chochote.<br />
<br />
Wasiwasi wa Cleopatra ulikuwa mmoja tu; Kwamba Deo akifa asingeweza tena kufunga naye ndoa, tendo ambalo alikuwa akilisubiria kwa muda mrefu sana. Cleopatra akazidi kulia. Alitamani sana kuliona tabasamu la Deo.<br />
<br />
Alitaka kuona akiongea, akimbusu, akimkumbatia na kumwambia maneno matamu ambayo amekuwa akimwambia mara nyingi sana.<br />
Hilo tu!<br />
<br />
Lakini Deo hakuweza kufanya chochote kati ya hivyo. Alikuwa amelala kitandani kama mzigo, hana taarifa kama mpenzi wake Cleopatra alikuwa kitandani kwake akilia.<br />
<br />
“Basi dada yangu, mwache apumzike, usijali, huna sababu ya kulia. Atapona tu!”<br />
<br />
“Lakini inaniuma dokta, bado wiki tatu tufung ndoa. Tayari ndoa imeshatangazwa mara ya kwanza kanisani, bado mara tatu ili nifunge ndoa na Deo wangu, sasa itawezekanaje tena? Si ndiyo nimeshamnpoteza? Si tayari nimeshapoteza ndoa?” Cleopatra akasema akionekana kuwa na uchungu sana.<br />
<br />
“Hapana, hana hali mbaya, wiki tatu ni nyingi sana, kabla ya muda huo atakuwa amesharejea katika hali yake ya kawaida, bila shaka atapanda madhabahuni kufunga ndoa na wewe!”<br />
<br />
Maneno ya Dk. Pallangyo kidogo yalimpa moyo Cleoptara, lakini ndani ya moyo wake, aliendelea kuwa na uchungu mwingi sana, kwani Deo alikuwa kila kitu katika maisha yake.<br />
<br />
Yeye ndiye aliyekuwa wa kutimiza ndoto zake za kuingia kwenye ndoa, lakini sasa zinakaribia kuzimika!<br />
Lazima aumie!<br />
<span> Lazima ateseke!...</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5eb365e03683586"><span class="text_exposed_show"><span> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5eb365e03683586"><span class="text_exposed_show"><span> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5eb365e03683586"><span class="text_exposed_show"><span> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5eb365e03683586"><span class="text_exposed_show"><span> </span></span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5d3389321717316">USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE.3.<br />
<br />
leopatra analia mbele ya kitanda cha Deogratius, ambaye alikuwa amelazwa baada ya kupigwa risasi. Zilibaki wiki tatu tu, kabla ya ndoa yao. Machozi machoni mwa Cleopatra yaligoma kabisa kufutika!<br />
Dokta akamtoa nje, akimbembeleza na kumpa moyo kwamba asijali, mgonjwa wake angepona. Cleopatra haamini hilo, anazidi kulia kwa uchungu, mawazo tele kichwani mwak<span class="text_exposed_show">e yakizidi kumzonga.<br />
Alichowaza yeye ni ndoa tu! Atafungaje wakati mpenzi wake alikuwa amelazwa wodini? Endelea kufuatilia...<br />
<br />
AKIWA katika mawazo ya kumuumiza moyo, simu yake ikaita. Akaangalia jina la mpigaji akakutana na jina lililoandikwa ‘My Mumy’. Alikuwa ni mama yake mzazi akimpigia. Kwa muda akaiangalia ile simu akijishauri kupokea, lakini alisita.<br />
<br />
Alijua sababu ya simu ya mama yake, kwa vyovyote vile, angetaka kujua kuhusu Deo, jambo ambalo aliamini lingeweza kuamsha machozi upya, kitu ambacho hakutaka kabisa kitokee. Lakini baadaye akaamua kupokea...<br />
<br />
“Patra uko wapi?” Ndiyo neno alilokutana nalo baada ya kupokea simu ya mama yake.<br />
“Hospitalini!”<br />
<br />
“Upo sehemu gani, maana na mimi tayari nimeshafika hapa Muhimbili!”<br />
“Nipo huku MOI mama!”<br />
<br />
“Nakuja!”<br />
Muda mfupi baadaye, mama yake akatokea. Cleopatra alipokutanisha uso na mama yake, machozi kama maji yakaanza kumwagika machoni mwake. Akamkimbilia na kumkumbatia.<br />
<br />
“Mama Deo wangu anakufa mama...” akasema kwa hisia za uchungu sana.<br />
“Hapana mwanangu, hutakiwi kuwaza hayo mama...yupo wapi?”<br />
“Wodini!”<br />
“Twende...”<br />
<br />
“Hawaruhusu kwenda sasa hivi, muda wa kuwaona wagonjwa umepita!”<br />
“Tatizo ni nini hasa lakini?”<br />
“Amepigwa risasi!”<br />
“Na nani?”<br />
<br />
“Hawajulikani mama.”<br />
“Wapi?”<br />
“Mjini. Daktari anasema aliletwa na wasamaria wema baada ya kumuokoa!”<br />
<br />
“Maskini, ana hali mbaya sana?”<br />
“Haongei mama, amepigwa risasi ya bega, lakini dokta anasema imekuwa vizuri maana haijatokeza upande wa pili.”<br />
“Mungu ni mwema mwanangu.”<br />
<br />
“Namuomba sana amponye ili tufunge ndoa yetu kwanza.”<br />
“Sote ndiyo dua yetu!”<br />
Kwakuwa muda ulikuwa umeshapita wakaondoka kwa ahadi ya kurudi jioni kumuona.<br />
<br />
****<br />
Saa 11:00 jioni, Cleopatra na mama yake walikuwa wanaingia katika wodi aliyolazwa Deo. Hawakuamini walipofika kitandani mwake na kumuona akiwa amefumbua macho yake. Cleopatra akalia kwa furaha.<br />
“Pole sana sweetie!”<br />
<br />
“Ahsante!” Deo akajibu kwa sauti ya taratibu sana.<br />
“Shikamoo mama...” Deo akasalimia.<br />
<br />
“Marahaba mwanangu, pole sana!”<br />
“Ahsante mama!”<br />
“Ilikuwaje?” Cleopatra akauliza akiketi kitandani kwa Deo.<br />
<br />
“Hata sielewi, nakumbuka nilikuwa kwenye lifti, nilipofika ghorofa ya tatu lifti ikasimama, wakaingia wanaume watatu, tukaanza tena kushuka hadi ghorofa ya pili, ikasimama tena. Ghafla nikasukumwa nje, kilichofuata ilikuwa ni mlio wa risasi.<br />
<br />
“Nikashtuka sana na kupoteza fahamu. Nilipozinduka, nikajikuta nipo hapa hospitalini.”<br />
“Unaweza kumkumbuka kwa sura hata mmoja wao?”<br />
“Hapana.”<br />
“Pole sana, lakini unajisikiaje sasa?”<br />
<br />
“Siwezi kujielezea, nahisi maumivu ya mkono na bega, lakini sielewi hali yangu hasa!”<br />
“Pole sana, utapona usijali,” mama yake Cleopatra akasema.<br />
“Nashukuru sana mama.”<br />
<br />
Cleopatra akamlisha chakula huku akimwambia maneno matamu ya kumtia moyo! Kidogo Deo akaanza kujisikia vizuri baada ya kupata faraja kutoka kwa mpenzi wake. Muda wa kuwaona wagonjwa ulipopita wakaondoka zao.<br />
<br />
“Ugua pole dear, kesho asubuhi nitakuja kukuona.”<br />
“Ahsante sana mpenzi wangu, nakupenda sana. Ahsante kwa kujali kwako!”<br />
“Ni wajibu wangu...utapenda kula chakula gani asubuhi?”<br />
“Chochote tu baby!”<br />
<br />
“Chagua mwenyewe mpenzi wangu!”<br />
“Nadhani mtori utanifaa zaidi.”<br />
“Ok! lala salama, ugua pole, you will be okay!”<br />
“Thank you baby!”<br />
<br />
Cleopatra na mama yake wakaondoka, wakamuacha Deo akiwa ametulia kimya kitandani, akisikilizia maumivu yake ya bega. Mpaka wakati huo, hakuelewa ni kwanini watu wale walimpiga risasi, maana hakuwa na fedha na wala hawakumwibia! Hilo liliendelea kuzunguka kichwani mwake bila kupata majibu.<br />
<br />
***<br />
Anahisi kama ameguswa na mkono wa mtu, anajaribu kuyafumbua macho yake kwa shida kidogo kutokana na mzigo wa usingizi aliokuwa nao! Alilala sana siku hiyo. Uchovu na usingizi ulisababishwa na mambo mawili; Deo alikuwa hajalala usiku mzima kwa maumivu ya bega, ndiyo kwanza asubuhi hiyo alianza kuhisi usingizi.<br />
<br />
Dawa alizokunywa, zilikuwa kali na zilimchosha sana mwili wake. Hayo yalitosha kabisa kumfanya, saa moja hii ya asubuhi, macho yake yaendelee kuwa mazito. Anajaribu kuyafumbua kwa shida na kumtazama mtu huyo!<br />
Akashtuka sana!<br />
<br />
Hakutegemea kukutana na sura hii hospitalini. Nani amemwambia kwamba amelazwa? Ni jana tu, alipata matatizo, leo hii amejuaje? Nani amempa taarifa za yeye kuumwa? Yalikuwa maswali yaliyofumuka mfululizo kichwani mwake, bila kupata majibu stahiki!<br />
Anazidi kumwangalia mwanamke huyu ambaye naye amesimama kama ameganda...<br />
<br />
“Pole Deogratius...pole sana kwa matatizo!” Mwanamke huyo akatamka kwa sauti ya taratibu sana.<br />
Deo hakuitika!<br />
<br />
“Maskini Deo, najua ni kiasi gani unaumia, najua kwamba ni jinsi gani ndoa yako itakavyokuwa na ugumu wa kufungwa. Bila shaka mmebakiza wiki tatu tu, sidhani kama utaweza kupanda madhabahuni ukiwa katika hali hii...pole sana...ni majaribu tu ya shetani,” akatamka kwa yakini, akiongea kwa mpangilio mzuri sana.<br />
Deo hakujibu neno!<br />
<br />
“Huyu vipi? Amejuaje nipo hapa? Amejuaje natarajia kufunga ndoa? Amejuaje mambo yangu?...amejuaje?” Akazidi kujiuliza Deo, lakini majibu hakuwa nayo.<br />
<br />
“Nakupa pole huitiki, kwanini? Au hujapenda mimi kuja hapa?” Mwanamke yule akasema, akionekana kusononeka na mapokeo ya Deo.<br />
<br />
Kwa ghafla sana, macho ya Deo yakaanza kupatwa na unyevunyevu, baadaye machozi yakaanza kuchuruzika machoni mwake. Ubongo wake ukasafiri miaka kumi nyuma. Akayatupa macho yake juu ya dari, kisha kumbukumbu zote za maisha yake yaliyopita zikaanza kumjia kama anatazama sinema ya kusisimua...<br />
<br />
Sinema ya maisha yenye kila aina ya machafuko na mataabiko. Mateso, dhiki na kuonewa. Masimango, kutukanwa na kudhalilishwa. Ilikuwa sinema mbaya, lakini yenye mwisho mzuri wa kupendeza, mwisho ambao baadaye uliingia shubiri.<br />
Ikawa chungu!<br />
Sinema ikaanza...</span></div></span></div><span class="fcg"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5eb365e03683586"><span class="text_exposed_show"><span> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5eb365e03683586"><span class="text_exposed_show"><span> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5eb365e03683586"><span class="text_exposed_show"><span> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5be976846404119">USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE.4.<br />
<br />
<br />
Cleopatra analia mbele ya kitanda cha Deo aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, hali yake ni mbaya na anatamani sana kuona Deo wake akiamka ili waende wakafunge ndoa yao kanisani.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Baada ya saa kadhaa, Deo anazinduka, Cleopatra na mama yake walipoenda baadaye, walimkuta Deo akiwa ameshazinduka, hawezi kuzungumzia vizuri jinsi alivyopata ajali ile. Wanaondoka kwa ahadi ya kurudi tena asubuhi inayofuata.<br />
<br />
Muda mfupi baada ya wao kuondoka, anaingia mwanamke mmoja na kumpa pole kwa matatizo aliyoyapata. Deo hajibu kitu muda wote mwanamke yule alipokuwa akizungumza. Lakini baadaye, Deo akaonekana kuwa na mawazo ya ghafla!<br />
<br />
Akili yake ikasafiri miaka kumi iliyopita, akaanza kukumbuka matukio yote yaliyotokea katika maisha yake. Kila kitu kikaanza kuonekana kama sinema ya kusisimua.<br />
Je, anakumbuka nini? Endelea....<br />
<br />
Oktoba 22, 1999 – Dar es Salaam<br />
Ni siku nyingine ya pilikapilika, kama ilivyokuwa kwa siku zilizotangulia, leo pia Deo ameamka saa 11:00 alfajiri kama kawaida yake. Alipoamka kitu cha kwanza kufanya ni kumwagilia maji maua, kufanya usafi wa mazingira na kuwapeleka watoto shule.<br />
<br />
Aliporudi, alitoka nyumbani kwa bosi wake Mburahati, akaenda sokoni Tandale, kilometa zaidi ya kumi na tano kwa miguu. Hapo ndipo anapofanya kazi ya kuuza mchele hadi saa 11:00 jioni, anapoanza safari nyingine ya kurudi nyumbani kwa miguu.<br />
<br />
Siku yake humalizika kwa kufunga mifuko ya barafu hadi saa sita za usiku anapopata muda wa kupumzika, kabla ya kukurupushwa tena alfajiri inayofuata.<br />
Hayo ndiyo maisha yake!<br />
<br />
Deogratius Mgana, kijana mchapakazi, hajawahi kupumzika hata siku moja tangu alipoanza kazi katika nyumba ya mzee Maneno, miaka mitatu iliyopita. Alikuja Dar es Salaam, akitokea nyumbani kwao Kiomboi Singida kwa lengo moja tu, kutafuta maisha. Mshahara wake ukiwa ni shingili elfu arobaini na tano tu, kwa kazi zote anazofanya.<br />
<br />
Akiwa ametulia kwenye ubao wake sokoni, anatokea dada mmoja mrembo sana. Si mgeni machoni mwake, ni mteja wake wa kila siku, ambaye amekuwa akimhudumia mchele karibu mara mbili au tatu kwa wiki!<br />
“Mambo kaka?” Dada yule akamsalimia.<br />
<br />
“Poa, karibu!”<br />
“Ahsante, nipimie kilo tano!”<br />
“Usijali!”<br />
<br />
Deo akampimia mchele aliohitaji na kumuwekea kwenye mfuko, kisha akampa. Yule msichana akalipa na kuondoka...baada ya hatua nne, akarudi tena.<br />
<br />
“Samahani kaka, nimeshakuwa mteja wako wa kudumu sasa, nadhani ni vizuri kujua jina lako. Mimi naitwa Levina, wewe je?”<br />
“Deogratius, lakini wengi wanapenda kuniita Deo!”<br />
“Nashukuru kukufahamu, sasa nimeridhika, kwaheri!”<br />
“Poa!”<br />
<br />
Deo alimwangalia Levina hadi alivyoishilia, namna alivyokuwa akitembea, namna alivyokuwa akiongea vilimpa picha ya tofauti sana. Alianza kuhisi eti huenda Levina anampenda, lakini alijishangaa, maana lilikuwa jambo gumu kidogo!<br />
<br />
Levina ampende yeye?<br />
Muuza mchele?<br />
Mbona alikuwa anawaza mambo makubwa sana? Lakini bado hakutaka kuuhakikishia ubongo wake moja kwa moja juu ya hilo. Aliamini kwamba lazima kulikuwa na kitukinaendelea. Kwanini atake kujua jina lake? Ana umuhimu gani hasa?<br />
<br />
“Au zali la mentali nini? Si kawaida mteja kutaka kujua jina langu bila sababu za msingi. Lazima kuna kitu kinaendelea, lazima....” akawaza Deo akiwa anamwangalia mpaka anavyoishilia mbali.<br />
<br />
Akabaki akiwa na mawazo mengi kichwani mwake, tayari hisia za mapenzi dhidi ya Levina zilianza kumuingia, lakini aliwaza sana namna ya kumuingia, hakuwa na hadhi ya kutoka na Levina.<br />
<br />
****<br />
“Mambo Deo?”<br />
“Poa Levina, mzima?”<br />
“Nipo poa!”<br />
“Za nyumbani?”<br />
“Salama kabisa.”<br />
<br />
“Ngapi leo?”<br />
“Pima kilo kumi!”<br />
“Wewe kwani mna sherehe?”<br />
“Hapana ni bajeti tu!”<br />
<br />
Deo akapima mchele alioagizwa, akamimina kwenye mfuko na kumkabidhi Levina, aliyeupokea huku akiachia tabasamu mwanana kabisa.<br />
“Ahsante sana Deo!”<br />
“Nashukuru pia!”<br />
“Samahani Deo, naweza kupata namba zako za simu?” Levina akamwuliza.<br />
<br />
“Simu?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Mimi sina, labda nikupe namba za nyumbani!”<br />
“Hapana, nataka namba zako mwenyewe!”<br />
“Sina.”<br />
<br />
“Kwanini?”<br />
“Maisha Levina!”<br />
“Ok! basi chukua zangu...ukimaliza kazi zako nipigie kwenye kibanda cha simu, nahitaji kuzungumza na wewe!” Levina akasema akiandika namba na kumkabidhi Deo akiambatanisha na noti ya elfu tano.<br />
“Ahsante sana Levina, nitakupigia!”<br />
“Usiache tafadhali, ni muhimu sana!”<br />
“Sawa.”<br />
<br />
Levina ni nani hasa? Anataka kumwambia nini Deo? Fuatilia..</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5be976846404119"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5be976846404119"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5be976846404119"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5be976846404119"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE.5.<br />
<br />
“Samahani Deo, naweza kupata namba zako za simu?” Levina akamwuliza.<br />
“Simu?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<span class="text_exposed_show"> “Mimi sina, labda nikupe namba za nyumbani!”<br />
<br />
“Hapana, nataka namba zako mwenyewe!”<br />
“Sina.”<br />
“Kwanini?”<br />
“Maisha Levina!”<br />
<br />
“Ok! basi chukua zangu...ukimaliza kazi zako nipigie kwenye kibanda cha simu, nahitaji kuzungumza na wewe!” Levina akasema akiandika namba na kumkabidhi Deo akiambatanisha na noti ya elfu tano.<br />
“Ahsante sana Levina, nitakupigia!”<br />
“Usiache tafadhali, ni muhimu sana!”<br />
“Sawa.”<br />
ANZA SASA KUISOMA....<br />
<br />
DEO alibaki na maswali mengi sana kichwani mwake bila kuwa na majibu, bado kitu kikubwa kilichokuwa kinamsumbua ni kwamba, ni kweli hisia zake zilikuwa sawa kwamba Levina alikuwa anampenda au zilikuwa hisia zake mwenyewe?<br />
<br />
Hakujua hakika!<br />
Lilikuwa suala gumu sana kichwani mwake kupitishwa moja kwa moja kuwa Levina alikuwa anampenda, hata hivyo ndani ya moyo wake alijua wazi kuwa kabisa yeye alimpenda sana Levina.<br />
“Nitampataje jamani huyu msichana? Nahisi kabisa moyo wangu unaniambia kuna kitu fulani, ni kweli nampenda sana Levina,” akawaza Deo.<br />
<br />
Siku nzima alishinda akiwa na mawazo, alitamani sana kumpigia simu Levina ili amsikilize alichokuwa akitaka kumwambia, lakini kwa sababu alikuwa na wateja wengi alishindwa kufanya hivyo, lakini kubwa zaidi kelele za pale sokoni zilimfanya ashindwe kumpigia kwakuwa alifahamu kwamba hawataweza kuelewana vyema!<br />
<br />
Jioni alifunga biashara yake na kuanza kurudi zake nyumbani, kwakuwa alipewa pesa na Levina na pia alikuwa na haraka ya kuwahi kumpigia simu, akaona bora apande daladala.<br />
<br />
Akachepuka kutoka sokoni Tandale hadi Manzese ya Agerntina, pale akapanda daladala iliyompeleka mpaka Magomeni ya Mwembechai, akashuka na kutafuta kibanda cha simu.<br />
“Habari yako dada?” Deo akamsalimia mhudumu wa kibanda cha simu.<br />
“Salama, karibu kaka’ngu!”<br />
<br />
“Nahitaji kupiga simu.”<br />
“Sawa, naomba namba.”<br />
Deo akamtajia.<br />
<br />
Yule dada akabonyeza zile namba kwenye simu, kisha akaweka saa yake ya kuhesabu muda tayari na kumpatia Deo simu.<br />
“Hallow,” sauti laini ya kike ilisikika upande wa pili, baada ya kupokelewa.<br />
<br />
“Hallow, habari yako?”<br />
“Nzuri, bila shaka ni Deo?”<br />
“Umejuaje?”<br />
“Kwanza sauti yako, lakini pia wengi wanaonipigia simu namba zao nimezi-save!”<br />
“Niambie Levina.”<br />
<br />
“Poa!”<br />
“Nimekupigia kama ulivyoniambia.”<br />
“Hujakosea kitu Deo, tena umefanya vizuri sana, maana nilikuwa nawaza namna ya kukupata kama usingenipigia.”<br />
“Sawa...sawa...nini kipya?” Deo akauliza.<br />
<br />
Kimsingi hakuonekana kuwa na jambo lolote la kuzungumza zaidi ya kusubiri kumsikiliza Levina.<br />
“Sikia Deo, kuna kitu cha muhimu sana nilitaka kuzungumza na wewe, lakini naona kama mazingira hayafanani kabisa.”<br />
“Kivipi?”<br />
<br />
“Nahisi upo kwenye kelele sana, kiasi kwamba hata hutakuwa na usikilizaji na uelewa mzuri wa nitakayokuambia.”<br />
“Kwani unataka kuniambia nini?”<br />
<br />
“Subiri Deo, usiwe na haraka kiasi hicho, huwezi kupata muda nikazungumza na wewe nje ya kazini kwako?”<br />
“Kama lini?”<br />
“Wewe off yako ni lini?”<br />
<br />
“Jumapili, ingawa si mapumziko ya moja kwa moja!”<br />
“Kivipi?”<br />
“Huwa siendi sokoni, lakini kazi nyingine za nyumbani zinaendelea kama kawaida.”<br />
“Sasa?”<br />
<br />
“Naweza kujaribu kutoka mara moja, lini unataka tuonane?”<br />
“Itakuwa Jumapili, lakini kesho nitakuja tena kuzungumza na wewe zaidi!”<br />
“Sawa.”<br />
“Haya usiku mwema mwaya Deo!”<br />
<br />
“Ahsante,nawe pia ulale salama.”<br />
Wakakata simu zao.<br />
Deo akalipa na kuanza kutembea kwa miguu akienda Mburahati, nyumbani kwa bosi wake. Ndani ya moyo wake alijihakikishia kumpenda Levina, lakini ufukara wake ulimfanya ashindwe kuelewa namna ambavyo angeweza kumfanya Levina awe wake.<br />
<br />
Alifika nyumbani nusu baadaye, kwanza alikabidhi mahesabu, akaingia bafuni kuoga. Aliporudi alifikia mezani kupata chakula cha usiku, kabla ya kwenda jikoni kuanza kazi ya kufunga mifuko ya barafu kama ilivyo kawaida yake.<br />
<br />
***<br />
Kama ni mateka, alikuwa mateka asiye na hali, ambaye pamoja na kutekwa kwenyewe, alikuwa tayari kufanywa mateka. Levina alijishangaa sana jinsi alivyotokea kumpenda Deo.<br />
<br />
Hakika hakuwa hadhi ya mwanaume wa kuwa naye, uwezo wao kifamilia, heshima waliyonayo wazazi wake ni kati ya mambo ambayo yalimchanganya sana na kumfanya ashindwe kuwa na maamuzi ya moja kwa moja ya nini cha kufanya kwa ajili ya Deo.<br />
<br />
Pamoja na yote hayo, moyo wake ulikuwa na kitu kimoja tu...<br />
Mapenzi!<br />
Alimpenda sana Deo, lakini alikuwa na changamoto nyingi sana kichwani mwake. Kwanza aliwaza juu ya wazazi wake...hakujua kama wangekubaliana na wazo lake la kuolewa na Deo, kijana fukara ambaye hana mbele wala nyuma.<br />
<br />
Hilo lilimchanganya sana kichwa chake, lakini alijipa moyo kwamba siku moja lazima Deo angekuwa mikononi mwake, yeye akiwa mama na Deo akiwa baba.<br />
<br />
“Hilo nitahakikisha nalitimiza, maadamu nimempenda, hayo mengine nitajua baadaye!” Akawaza Levina.<br />
<br />
***<br />
“Mambo Deo,” alikuwa ni Levina akimsalimia Deo, asubuhi ya siku iliyofuata alipokwenda sokoni.<br />
“Poa, za nyumbani?”<br />
“Salama.”<br />
“Kilo ngapi?”<br />
<br />
“Hapana, leo sihitaji mchele, nimekuletea zawadi yako,” akasema Levina akimkabidhi bahasha ya khaki.<br />
Deo akapokea...<br />
“Hiyo ni simu Deo, imebidi nikununulie ili kurahisha mawasiliano yetu.”<br />
<br />
“Mh! Ahsante sana jamani, lakini kwanini umeamua kufanya hivi?”<br />
“Kwa sababu sisi ni marafiki, unajua tunatakiwa kudumisha urafiki wetu kwa kuwasiliana mara kwa mara, au wewe hupendi tukiwa marafiki?”<br />
“Napenda sana, nashukuru sana!”<br />
<br />
“Usijali, line imo humo humo ndani, tayari nimeshakuwekea vocha za elfu ishirini, zikiisha nijulishe nikuongeze nyingine.”<br />
“Ahsante sana,” Deo akashukuru tena.<br />
<br />
Haikuwa rahisi kuamini jambo hilo, zawadi ile kwa Deo ilikuwa zaidi ya zawadi,ule ulikuwa uthibitisho tosha kwamba Levina alikuwa anampenda.<br />
Levina hakukaa muda mrefu sana, akaaga na kuondoka.<br />
<br />
***<br />
Siku zilivyozidi kwenda na kuwasiliana, mapenzi kati ya wawili hawa yalizidi kuchipuka kwa kasi, lakini si Deo wala Levina aliyekuwa tayari kueleza hisia zilizokuwa ndani ya moyo wake.<br />
<br />
Wote waliishi na siri nzito za mapenzi ndani ya nafsi zao, lakini leo Levina amepata wazo la kufanya ili aweze kumnasa Deo. Alitumia kila njia kumuonesha kwamba anampenda na alichokuwa akikisubiri siku zote ni Deo kumtamkia kwamba anampenda, lakini hilo halikutokea.<br />
<br />
Deo naye alishangazwa na jinsi Levina alivyopenda kuwa naye karibu na kumsaidia mambo mbalimbali, lakini aliogopa kumwambia kwamba anampenda, akihofia kupoteza urafiki wao ambao kwake ulikuwa na manufaa makubwa sana.<br />
<br />
Levina ameshapata njia za kumsogeza karibu Deo ili iwe rahisi kwake kutamka kwamba anampenda. Alipanga mpango hatari, haukuwa mwingine zaidi ya kufanya jitihada mfanyakazi wao wa kiume wa nyumbani atimuliwe ili amfanyie Deo mipango ya kupata kazi nyumbani kwao.<br />
<br />
Hapo ndipo angempata Deo kwa urahisi zaidi, maana angekuwa anammiliki. Hilo alijihakikishia kulifanya.<br />
<br />
Je, nini kitatokea? Levina atafanikiwa kumpata Deo? Usikose kufuatilia ..........</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE.6.<br />
<br />
Levina ametekwa kimapenzi na Deo. Kilichopo akilini mwake ni kumfukuzisha kazi kijana wao wa nyumbani ili nafasi hiyo ichukuliwe na Deo, hapo angempata kirahisi zaidi.<br />
Je, itawezekana? Endelea...<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> LEVINA alikuwa mateka wa mapenzi, alimpenda sana Deo na alitaka kuhakikikisha anakuwa wake wa maisha yake yote. Kitu pekee kilichokuwa kichwani mwake ilikuwa ni namna gani angeweza kumwondoa Rashid nyumbani kwao na kufanya jitihada za kumwingiza haraka sana Deo nyumbani, hapo lengo lake lingeweza kutimia bila mushkeli kabisa.<br />
<br />
“Mimi ndiye ninayejua thamani ya penzi langu kwa Deo, najua kama nikimwambia ghafla anaweza kunichukia na kuniona malaya, lakini nikimsogeza kwanza nyumbani, naamini itakuwa vyema zaidi maana hataweza kupindua,” akawaza kichwani mwake Levina.<br />
<br />
“Lazima atakuwa wangu, lazima...” akazidi kujihakikishia ushindi.<br />
Tayari alishakuwa na mbinu zake, mipango ilikuwa tayari kabisa, kilichobaki ilikuwa ni utekelezeji tu.<br />
<br />
“Rashid hana ujanja wowote kwangu, mimi ndiye Levina na nitahakikisha namtoa nyumbani,” akazidi kupanga mipango ya kummaliza.<br />
<br />
****<br />
Ilikuwa Jumapili asubuhi, nyumba ikiwa kimya kabisa, wazazi wa Levina, mdogo wao mdogo pamoja na house girl wote walikuwa wamekwenda kanisani, nyumbani wakiwa wamebaki Levina na Rashid, kijana wa kazi.<br />
<br />
“Rashidiiiiiii....” Levina akaita akiwa amekaa sebuleni akiangalia runinga.<br />
“Naam dada...”<br />
“Njoo!”<br />
“Nakuja.”<br />
<br />
Rashid akakimbia haraka hadi sebuleni alipokuwa akiitwa na Levina. Akamkuta akiwa ametulia kwenye sofa.<br />
“Mambo kaka?” Rashid akasalimia.<br />
“Poa,mzima?”<br />
“Nipo poa, nina shida moja muhimu nataka unisaidie.”<br />
“Nini?”<br />
<br />
“Naomba uniazime simu yako mara moja, maana yangu imekufa display!”<br />
“Haina pesa lakini.”<br />
“Usijali, ninayo nitaongeza, kuna mtu nataka kuchat naye kidogo!”<br />
“Hii hapa.”<br />
<br />
“Poa basi, nikimaliza nitakushtua, unafanya nini nje?”<br />
“Nakatia fensi, si unajua tena dingi akija akikuta sijakamilisha anaweza kuniletea muziki?”<br />
“Poa bwana endelea.”<br />
<br />
Levina akachukua ile simu na kuiangalia kwa dharau...<br />
“Nakumaliza na simu yako hii hii,” akawaza kichwani mwake Levina.<br />
<br />
Zoezi kubwa lililokuwa likiendelea ni kutuma meseji kutoka kwenye simu ya Rashid kwenda kwenye simu yake, huku akijibizana naye. Alipomaliza, akafuta meseji zote zilizoingia na kutoka kwenye simu ya Rashid, ili kuondoa ushahidi.<br />
<br />
Baadaye akamrudishia Rashid simu yake.<br />
“Umefanikiwa kuwasiliana naye?” Rashid akamwuliza Levina.<br />
“Siyo kuwasiliana naye, ni kuwasiliana nao?”<br />
“Kwani walikuwa wangapi?”<br />
“Nilikuwa nachat na marafiki zangu kibao, si mmoja kama unavyodhani.”<br />
<br />
“Poa, mi nipo nje.”<br />
“Sawa kaka Rashid.”<br />
Kwa alivyokuwa akizungumza, ni kama muungwana mwenye roho nzuri na upendo, lakini kikubwa alikuwa amepanga kumfukuzisha kazi Rashid.<br />
<br />
Ni kijana aliyefanya kazi kwao kwa muda mrefu sana, akiaminiwa sana na wazazi wake, isingekuwa rahisi kumtoa nyumbani kwao kienyeji kutokana na utendaji wake kuwa bora kwa miaka mitatu aliyoishi kwa uaminifu mkubwa katika nyumba ile.<br />
<br />
****<br />
“Samahani kwa kukusumbua Deo, naamini wewe ni rafiki yangu, ni kweli?” Levina alimwambia Deo, jioni moja alipomsubiri Magomeni Mwembechai, ambapo Deo alikuwa anarudi nyumbani Mburahati.<br />
“Naamini hivyo, sisi ni marafiki.”<br />
<br />
“Kweli?”<br />
“Naamini hivyo au?”<br />
“Hata mimi pia, lakini nilitaka kupata uhakika kutoka kwako.”<br />
“Sisi ni marafiki Levina.”<br />
“Bila shaka huwezi kunificha chochote katika maisha yako.”<br />
“Hilo halina ubishi.”<br />
<br />
“Ulisema unaitwa Deo, ukoo wako ni nani na wewe ni kabila gani?”<br />
“Mh! Jamani, kwanini?”<br />
“Nataka tu, kujua.”<br />
“Niite Deogratius Mgana, ni mwenyeji wa Kiomboi, Singida, nikimaanisha kwamba mimi ni Mnyiramba.”<br />
<br />
“Ok! nimefurahi sana kukufahamu kwa uzuri Deo, mimi ni Levina Masamu, ni Mchaga wa Old Moshi.”<br />
“Oh! Ahsante sana kukufahamu zaidi, lakini kwanini umeniuliza yote hayo?”<br />
<br />
“Nina maana yangu, utaijua baadaye kidogo. Samahani, mshahara wako ni shilingi ngapi kwa mwezi?”<br />
“Nalipwa elfu arobaini na tano.”<br />
“Jamani zinakutosha kweli?”<br />
“Nitafanyaje Levina, maisha...”<br />
“Elimu yako ikoje?”<br />
<br />
“Mimi?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Darasa la saba tu, nilifaulu lakini wazazi wangu wakakosa fedha za kuniendeleza.”<br />
<br />
“Usijali, vipi utakuwa tayari nikikutafutia mahali pengine utakapolipwa fedha nyingi zaidi?”<br />
“Ndiyo, hata sasa hivi.”<br />
<br />
“Kweli?”<br />
“Ndiyo!”<br />
Levina akafurahi sana, mpango wake ulikuwa unanukia kukamilika.</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250">USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE.8.<br />
<br />
Mpango wa kumtoa Rashid nyumbani kwao unaendelea, nia hasa ya Levina ni kumwingiza Deo nyumbani kwao.<br />
Lakini moyoni aliumia sana, maana machozi ya Rashid yalikuwa yanamuuma sana!<br />
Ni kweli alimsingizia. Nini kitatokea? Endelea kuisoma...<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
LEVINA aliumia ndani kwa ndani, alikiri kabisa kwamba Rashid hakuwa anahusika na chochote katika mchezo ule. Kitu pekee kilichomsukuma kufanya vile ni mapenzi yake ya dhati pekee, hakuwa na kitu kingine ndani yake zaidi ya hivyo.<br />
<br />
Tangu Rashid alipoondoka kwenda chumbani kwake kukusanya mizigo yake, alijisikia mkosaji sana.<br />
Mwenye roho mbaya sana!<br />
Alijihisi kama si binadamu kabisa!<br />
Sifa zote mbaya akajipa yeye!<br />
<br />
Mama yake aliweza kugundua tofauti aliyokuwa nayo mwanaye, akaona njia pekee ya kugundua kilichokuwa kikimtatiza mwanaye ni kumuuliza tu!<br />
“Nini tatizo tena mwanangu?”<br />
Levina akabaki kimya!<br />
“Levina...” mama yake akaita.<br />
<br />
“Abee...” Levina akaitikia kwa kushtuka kidogo.<br />
Ni kama alikuwa amegutuka kutoka katika usingizi mzito, lakini ukweli haukuwa huo. Levina alikuwa na mawazo ya usaliti. Kusema uongo na kumnyanyasa Rashid kwa sababu ya mapenzi.<br />
“Una nini mama?!!”<br />
<br />
“Inaniuma sana mama...” Levina akasema machozi yakidondoka machoni mwake, ni kama alikuwa akiumizwa na meseji za Rashid, lakini ukweli halisi haukuwa huo.<br />
Ndani ya nafsi yake alikuwa akiumizwa na kitendo cha kumsingizia na si kufanyiwa kama ambavyo alitaka kutengeneza.<br />
<br />
“Lakini ndiyo nimemtimua hivyo.”<br />
“Amekosa adabu kabisa, yaani siku zote hizo naishi naye kama kaka yangu halafu anakuja kuniambia maneno machafu kiasi hicho? Hana adabu kabisa...” akasema Levina lakini kichwani mwake kukiwa na kitu kingine.<br />
<br />
Moyoni mwake alihifadhi kitu tofauti kabisa, alikuwa na siri nzito sana, ambayo hakutakiwa kumwambia mtu yeyote, ilikuwa ni siri ambayo alitakiwa kuijua yeye na moyo wake pekee.<br />
<br />
“Potelea mbali, kama ni kazi anaweza kupata mahali pengine, lakini nitapata wapi mwanaume kama Deo, lazima nifanye hivi, sina namna!” Akazidi kuwaza kichani mwake.<br />
<br />
“Usijali mwanangu, nimeshamtimua huyu mwanaharamu. Hutakiwi kuwa na mawazo mwanangu na mimi mama yako nipo. Tena subiri...wewe Rashid, unasubiri nini? Kwani una mizigo gani mingi ya kuchukua muda mrefu kiasi hicho?” Akasema mama Levina akisimama kumfuata chumbani kwake.<br />
<br />
Mama Levina alikuwa amevimba kwa hasira, akafika chumbani kwa Rashid na kumwita kwa sauti kubwa...<br />
“Si naongea na wewe, hebu toka haraka nyumbani kwangu.”<br />
<br />
“Natoka mama,lakini siku moja utakuja kugundua ukweli, siwezi kufanya mambo ya ujinga kiasi hicho mama, lakini kwakuwa wewe umeamua kumuamini Levina sawa!”<br />
<br />
“Tena funga domo lako kabisa wewe mwanaharamu, inaonekana unataka kunigombanisha na mwanangu, unataka kuniambia mwanangu anaongopa?”<br />
“Ndiyo mama!”<br />
“Kwa lipi hasa?”<br />
<br />
“Sijui mama, lakini ukichunguza utagundua ukweli.”<br />
“Tena ishia hapo hapo kuniita mama, anayeruhusiwa kuniita mama ni yule anayeheshimu wanangu na kuwachukulia kama dada zake, si wewe mpumbavu!”<br />
“Hapana mama!”<br />
<br />
“We’ mwendawazimu, sina muda wa kubishana zaidi na wewe. Paki vitu vyako, nakwenda kukuchukulia pesa zako uondoke!”<br />
Rashid akabaki kimya.<br />
Mama Levina akaenda ndani haraka na kuchukua fedha alizokuwa akidaiwa na Rashid kisha akarudi na kumkuta tayari ameshajiandaa.<br />
<br />
“Chukua pesa zako, tena nimekuongezea na elfu thelathini zikusaidie, ondoka kwangu!”<br />
“Ahsante mama, lakini Mungu mwenyewe ndiye anayejua ukweli wa haya yote!”<br />
<br />
“Hayo mahubiri yako huwa nakutana nayo kanisani, sasa sioni kama hata hapa nyumbani kwangu panafaa kuhubiriwa!”<br />
“Siyo mahubiri mama, ni ukweli kabisa kutoka ndani ya moyo wangu!”<br />
“Ukweli wa nini?”<br />
<br />
“Sijamtumia zile meseji mimi mama.”<br />
“Hivi wewe una akili? Zile namba ni zako au za nani?”<br />
“Zangu.”<br />
<br />
“Sasa kama ni zako, kwanini unaruka?”<br />
“Unajua mama...juzi...” mama Levina hakumpa nafasi ya kumalizia utetezi wake.<br />
<br />
“Hebu toka kwangu haraka tafadhali, sidhani kama bado nina nafasi ya kuendelea kuusikiliza utumbo wako, ondoka tafadhali!”<br />
Rashid alikuwa anataka kumweleza mama Levina kwamba kuna siku alimuazima simu yake, lakini hakupewa nafasi hiyo.<br />
<br />
Rashid akaondoka analia, mama Levina akiendelea kufoka huku akirusha mikono. Alikuwa amekasirika sana. Pamoja na utendaji kazi wake kuwa mzuri kwa muda mrefu aliokuwa akikaa naye, lakini siku aliyasahau yote hayo kwa meseji iliyoonekana kutumiwa mwanaye.<br />
<br />
****<br />
Mto wote ulikuwa umelowana kwa machozi, Levina alikuwa na uchungu sana ndani ya moyo wake. Usiku huo ulikuwa mgumu sana kwake, aliteswa na watu mawili; DEO NA RASHID!<br />
<br />
Alifanya dhambi ya kumsingizia Rashid kwamba amemtongoza na akafukuzwa kazi. Hilo lilimuuma, lakini lingepoa kama kweli Deo angekubali kuwa naye. Lakini aliteseka sana, akiwa hana uhakika kama kweli Deo atamkubalia.<br />
<br />
Tabu yote ya nini? Usiku ule ule, akachukua simu na kumpigia Deo.<br />
Je, nini kitatokea?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d576db1481614595">USIFE KWANZA MPENZI WANGU.......EPISODE.9.<br />
<br />
Zoezi la kwanza la Rashid kuondoka nyumbani kwao, linakamilika. Zoezi lililokuwa linafuata kwa Levina ilikuwa ni kuhakikisha Deo anaingia nyumbani kwao. Pamoja na mafanikio yale makubwa, moyo wake haukuwa na amani kabisa kutokana na fitna alizomfanyia Rashid.<br />
<br />
Hata hivyo, kikubwa zaidi kwake ilikuwa ni Deo kukubali kwenda nyumbani kwao na baadaye alitama<span class="text_exposed_show">ni sana Deo mpenzi wake wa maisha yake yote. Hiyo ndiyo ilikuwa ndoto yake kubwa. Akiwa katika lindi la mawazo, akaamua kumpigia simu Deo.<br />
Je, nini kitaendelea? Endelea kuisoma...<br />
<br />
LEVINA aliumia sana ndani ya moyo wake, akaona ni vyema kama angenyanyua simu yake na kumpigia Deo. Alitaka kujua hisia zake zina nini juu yake. Hakutaka kufanya mambo kwa hasara!<br />
<br />
Akachukua simu na kwenda moja kwa moja kwenye Menu, akabonyeza Contacts kisha akaanza kutafuta jina la Deo, alipolipata akabonyeza kwenye kitufe cha kijani ili kuruhusu upigwaji simu.<br />
<br />
Punde tu, sauti ya Deo ikasikika...<br />
“Vipi Levina mbona usiku sana?”<br />
“Nina matatizo Deo!”<br />
“Matatizo gani?”<br />
“Naomba nikuulize kwanza maswali yangu!”<br />
<br />
“Uliza.”<br />
“Mimi ni rafiki yako?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Unaniamini?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Unanipenda?” Levina akauliza kwa sauti ya taratibu, lakini iliyochanganyikana na kilio cha kwikwi kwa mbali.<br />
Deo hakupata shida sana kugundua kwamba Levina alikuwa analia. Pengine hilo si neno sana, lakini kwanini amemuuliza kama anampenda? Hata kama anampenda, ndiyo alie?<br />
Kwanini analia?<br />
<br />
Hakujua!<br />
Kimya cha muda mfupi kikapita, Deo akiwa ametulia kwenye simu na Levina akiendeleza kilio chake cha chini chini huku kwikwi zikisikika kwa mbali.<br />
“Levina,” baadaye Deo akaita.<br />
“Bee!”<br />
“Nini tatizo?”<br />
<br />
“Si tatizo, napenda kusikia ukinijibu!”<br />
“Uliuliza nini?”<br />
“Nilikuuliza kama unanipenda?”<br />
“Ni kweli nakupenda Levina, wewe ni rafiki yangu na umekuwa msaada kwangu kwa kila kitu, lazima nieleze ukweli, nakupenda, kwani wewe hunipendi?”<br />
“Swali gani hilo Deo?”<br />
<br />
“Samahani kama nimekuudhi, lakini ndani ya moyo wangu natambua kwamba tunapendana, mimi nafahamu hilo, naamini hata wewe ni kama mimi.”<br />
“Kweli.”<br />
“Lakini ni kwanini unalia?”<br />
“Silii ila sauti yangu leo haipo vizuri sana.”<br />
“Unakohoa?”<br />
<br />
“Ndiyo!”<br />
“Pole sana.”<br />
“Ahsante.”<br />
“Nina swali lingine kwako Deo!”<br />
“Uliza.”<br />
<br />
“Lakini kabla sijauliza, nataka unihakikishie kwamba utajibu ukweli wako wote na hutanidanganya jambo lolote.”<br />
“Hilo kabla hujauliza, naamini unatambua kabisa jinsi nilivyo mkweli.”<br />
“Umewahi kuona mtu akilia?”<br />
<br />
“Mara nyingi sana, hata leo kuna mtoto nimemuona akilia.”<br />
“Siyo mtoto, nazungumzia mtu mzima.”<br />
“Ndiyo, kwenye misiba huwa wanalia sana, nimeshaona mara nyingi, kwani kuna nini, mbona unaniacha na maswali?”<br />
“Lakini vipi kama ukiona mtu mzima analia?”<br />
“Nitajisikia vibaya sana.”<br />
<br />
“Umeshawahi kumuona mtu akilia kwa ajili yako?”<br />
“Hapana.”<br />
“Utapenda siku moja hilo likitokea?”<br />
“Hapana.”<br />
“Basi usiku mwema.”<br />
<br />
“Kwanini?”<br />
“Nimekutakia usiku mwema Deo.”<br />
“Lakini sijakuelewa kabisa. Mbona leo maneno yako yamekuwa magumu sana kuingia kichwani mwangu? Kwani kuna nini kimetokea?”<br />
“Hakuna...nilitaka kujua tu unachowaza kichwani mwako!”<br />
“Nikuambie kitu Levina?”<br />
<br />
“Nakusikiliza.”<br />
“Nitalala nikiwa na mawazo sana leo. Maneno yako yananiacha na maswali mengi yasiyo na majibu kabisa. Mpaka sasa sijajua maana ya kauli yako.”<br />
“Siku moja utajua....”<br />
“Usiku mwema.”<br />
<br />
“Na wewe pia!”<br />
Wakakata simu zao.<br />
Deo akapata wakati mgumu sana wa kuwaza mambo kichwani mwake bila kupata majibu. Alikuwa katika wakati mgumu sana wa kujaribu kuwaza kilicho kichwani mwa Levina kitu ambacho kwa hakika kisingekuwa rahisi kuelewa.<br />
<br />
“Sijajua anamaanisha nini? Anyway itajulikana baadaye!” Akawaza na kujifunika shuka kisha akaishilia usingizini.<br />
<br />
****<br />
Siku nzima ilikuwa kama wiki kwa Levina, kichwa kilikuwa kinamuuma mawazo mengi yakimsumbua. Hakuwa na kitu kingine kilichomtesa zaidi ya Deo, aliendelea kuwaza namna ya kumsogeza karibu yake.<br />
<br />
“Nampenda sana Deo, ni kweli kwamba nampenda sana, lazima nitumie kila njia, nihakikishe anakuwa wangu. Hilo lazima nitalifanya,” akawaza Levina akiwa kazini kwake Posta.<br />
<br />
Levina baada ya kumaliza kidato cha sita, wazazi wake walimkabidhi moja ya maduka yao yaliyopo mjini, Levina alipewa duka la simu lililopo Posta Mpya jijini Dar es Salaam.<br />
Alichojua yeye ni kwamba alikuwa msimamizi wa duka lile kubwa, lakini wazazi wake walipanga kumwachia moja kwa moja kama lake. Walimfanya msimamizi mkuu, akishughulikia kila kitu, mpaka mishahara ya wafanyakazi, walichokifanya wao ni kukagua mahesabu ya fedha zinazoingia na kutoka benki.<br />
<br />
Mali ikipungua dukani, ilikuwa ni kazi ya Levina kuagiza au kwenda nje ya nchi kununua mzigo mwingine wa dukani.<br />
Akionekana mwenye mawazo tele kichwani mwake, simu yake ikatoa mlio wa ujumbe mfupi wa maneno, mara moja akaufungua na kusoma.<br />
<br />
Ilikuwa meseji kutoka kwa mama yake, alijikuta anarudia kusoma zaidi ya mara mbili ile meseji akiwa haamini kabisa alichokiona.<br />
Ujumbe ule ulisomeka; “Levina ni wiki moja sasa tangu Rashid ameondoka, hatuna house boy, sasa kama unaweza ni vizuri ukashughulikia hilo, tukapata mtu mwingine haraka.”<br />
Levina akatabasamu.<br />
<br />
Ilikuwa nafasi nzuri kwake ya kumwingiza Deo nyumbani kwao.<br />
“Yes, mambo yanakwenda kama nilivyopanga, afadhali,” akasema kwa sauti ya taratibu akiachia tabasamu.<br />
<br />
***<br />
Jioni Levina aliwahi sana kurudi nyumbani, akamkuta mama yake sebuleni, baada ya kumsalimia akamwambia...<br />
“Mama nilipata sms yako ya mchana, nimeanza kuifanyia kazi, ndani ya siku tatu tutapata mtu mwingine.”<br />
<br />
“Oh! Usijali binti yangu, ameshapatikana kijana mwingine kutoka Bagamoyo, atakuja kuanza kazi kesho.”<br />
Uso wa Levina ukasawagika kwa huzuni.<br />
<br />
Itaendelea,..........</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d568101837371095">USIFE KWANZA MPENZI WANGU,.....EPISODE.10.<br />
<br />
Jioni Levina aliwahi sana kurudi nyumbani, akamkuta mama yake sebuleni, baada ya kumsalimia akamwambia...<br />
“Mama nilipata sms yako ya mchana, nimeanza kuifanyia kazi, ndani ya siku tatu tutapata mtu mwingine.”<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Oh! Usijali binti yangu, ameshapatikana kijana mwingine kutoka Bagamoyo, atakuja kuanza kazi kesho.”<br />
Uso wa Levina ukasawagika kwa huzuni.<br />
Sasa endelea...<br />
<br />
KWA sekunde kumi na tano, Levina alikuwa ameganda akimwangalia mama yake, ni kama hakusikia vyema maneno yale, hata kama aliyasikia vizuri lakini yalionekana kuwa magumu sana kupenyeza kwenye ngoma za masikio yake.<br />
<br />
Anamwangalia mama yake kwa macho yanayozungumza jambo fulani, ingawa haijulikani moja kwa moja kuwa anazungumza nini. Mama yake aliweza kugundua tofauti aliyonayo mwanaye haraka sana.<br />
<br />
“Vipi Levina mwanangu, mbona kama hujafurahia?”<br />
“Siyo hivyo mama?”<br />
“Bali nini tena?”<br />
“Nimeshangaa, maana tayari nilishaanza taratibu za kumpata huyo mtu.”<br />
<br />
“Kwani umeshampata?”<br />
“Kuna dada mmoja ameniambia kwamba jioni ya leo atakwenda kuzungumza naye. Yupo kaka mmoja amesema anaishi Mburahati, kwahiyo akionana naye atajaribu kumweleza.”<br />
“Ni mfanyakazi au yupo tu, nyumbani?”<br />
<br />
“Anafanya kazi!”<br />
“Sasa atawezaje kutoka?”<br />
“Kasema atamshawishi, maana hata pale halipwi mshahara mkubwa, lakini pia atamwambia mazingira ya kazi ni mazuri.”<br />
“Sawa, ngoja tuone.”<br />
<br />
“Na huyo mwingine uliyesema?”<br />
“Huyo kila kitu kipo tayari, nimeshafanya naye mawasiliano na tumekubaliana aje kesho!”<br />
“Sasa itakuwaje? Maana sitaki kuonekana mwongo kwa rafiki yangu.”<br />
<br />
“Kesho tutapata majibu kamili, kama akija huyo wa Bagamoyo sawa, asipokuja basi utanijulisha makubaliano ya huyo kijana mwingine atakayezungumza na rafiki yako leo usiku.”<br />
“Sawa mama, mimi nipo ndani,” akasema Levina.<br />
“Sawa mama.”<br />
<br />
Levina akajikongoja mpaka ndani akionekana kuwa na uchangamfu kidogo, bado alikuwa akiomba sana huyo kijana wa Bagamoyo asitokee ili Deo apate nafasi ya kuingia kwao.<br />
“Itawezekana tu, maadamu moyo wangu umempenda, naamini itakuwa hivyo,” akawaza Levina.<br />
<br />
Baada ya kubadili nguo, aliingia bafuni kuoga, alipotoka alionekana kuwa na nguvu kidogo, akachukua simu na kumpigia Deo.<br />
“Uko wapi?”<br />
“Nipo njiani naelekea nyumbani.”<br />
<br />
“Umefika wapi sasa hivi?”<br />
“Ndiyo nakaribia kushuka Mwembechai!”<br />
“Ok! ukishuka naomba unisubiri!”<br />
“Kwani wewe uko wapi?”<br />
“Nipo home, lakini natoka sasa hivi nachukua taxi nakuja.”<br />
<br />
“Basi jitahidi ufanye haraka!”<br />
“Usijali, sina muda mrefu sana nitakuwa hapo.”<br />
“Poa.”<br />
Levina akabadili nguo haraka na kutoka. Alipopita sebuleni alimkuta mama yake akiwa amekaa pale pale!<br />
<br />
“Haya wapi tena?”<br />
“Natoka kidogo mama!”<br />
“Ila saa hizi ni usiku na baba yako hapendi kabisa utoke usiku.”<br />
“Mama siendi mbali, nakwenda hapo Mwembechai mara moja.”<br />
“Unatoka na gari?”<br />
<br />
“Hapana, sitaki baba ajue nimeenda mbali kama akirudi mapema, ni bora alione gari atajua nipo jirani!”<br />
“Kumbe hutakuwa jirani siyo?”<br />
“Mama...!!! Mwembechai si mbali, lakini ni mbali pia mama. Kwa baba kule ni mbali!”<br />
<br />
Mama Levina akacheka.<br />
“Uwahi kurudi,” akasema mama Levina akiendelea kutabasamu.<br />
“Nakuahidi mama.”<br />
Levina akaondoka zake.<br />
<br />
***<br />
Levina alifurahi sana kukutana na Deo, moyo wake ulikuwa ukisisimka sana kila alipokutanisha macho yake na Deogratius.<br />
Alikuwa mwanaume pekee ambaye aliweza kuutetemesha moyo wake.<br />
“Nina habari njema Deo!”<br />
“Juu ya nini?”<br />
<br />
“Unakumbuka mara ya mwisho nilizungumza nini na wewe?”<br />
“Ndiyo, nakumbuka vizuri sana.”<br />
“Ilikuwa ni nini?”<br />
“Kuhusu kazi nyingine!”<br />
“Halafu?”<br />
“Kusoma.”<br />
<br />
“Safi sana, kumbe unakumbuka vizuri sana, sasa tunaanza na kimoja baada ya kingine. Kama nilivyokuambia sisi ni marafiki na nitakuwa tayari kutumia kila njia nihakikishe nakufurahisha!”<br />
”Nimefurahi kusikia hivyo.”<br />
“Nimekupatia kazi, tena nyumbani kwetu kabisa.”<br />
<br />
“Unasema kweli?” Deo akauliza akiwa haamini kabisa alichoambiwa na Levina.<br />
“Kwanini isiwe kweli?” Levina akauliza akitabasamu.<br />
<br />
Tabasamu lililomchoma Deo moyoni, kwa mara ya kwanza alikiri kumuona Levina akiwa ameachia tabasamu zuri zaidi kuliko siku zote!<br />
Uzuri wa Levina ukawa hadharani!<br />
Je, nini kitaendelea......</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d568101837371095"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d568101837371095"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d568101837371095"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d568101837371095"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d905194fcd5e08171837">USIFE KWANZA MPENZI WANGU .....EPISODE..11<br />
<br />
Pamoja na taarifa kutoka kwa mama yake kwamba alishapata kijana mwingine wa kazi, bado Levina hakukata tamaa kuhusu Deo. Usiku ule ule akatoka na kwenda kukutana naye Mwembechai.<br />
<br />
Levina akamweleza kwamba amempatia kazi nyumbani kwao, Deo akafurahi sana. Furaha iliyosababisha Levina aachie tabasamu mwanana! Uzuri wake ukawa hadharani!<br />
<span class="text_exposed_show"> Nini kitatokea? Endelea kuisoma...<br />
<br />
DEOGRATIUS akagundua kitu kipya kabisa kutoka kwa Levina, aligundua kwamba alikuwa msichana mzuri kupindukia! Tabasamu lake lililoacha sehemu kubwa ya meno yake nje, lilisababisha aone vijishimo vidogo mashavuni mwake na hivyo kuzidisha urembo wake.<br />
<br />
Alihisi moyo wake kama umepigwa na shoti ya umeme, alikuwa amesimama mbele ya mwanamke mrembo sana tofauti na matarajio yake. Levina alikuwa mzuri zaidi ya alivyofikiria.<br />
Kwanini anamsaidia sana?<br />
<br />
Kwanini anakuwa naye karibu sana? Hayo yaliendelea kuwa maswali ambayo hayakuwa na majibu ya moja kwa moja kichwani mwake. Alibaki ameganda akimwangalia Levina ambaye sasa aliamua kucheka kabisa. Furaha ya Levina ilikuwa ni kuona jinsi Deo anavyomkubali yeye.<br />
<br />
Hakujali umasikini wake, alichojua yeye ni mapenzi tu. Moyo wake ulianguka kwake, alitamani sana awe mpenzi wake wa dhati ndani ya moyo wake.<br />
<br />
“Deo!” Levina akaita kwa sauti tamu sana.<br />
“Naam!”<br />
“Vipi?”<br />
“Poa.”<br />
<br />
Levina akacheka.<br />
“Mbona unanicheka?”<br />
“Sijakucheka Deo!”<br />
“Bali!”<br />
<br />
“Nimecheka. Unajua kuna tofauti kubwa sana kati ya kucheka na kumcheka mtu. Mimi nimecheka, sijakucheka. Umeona tofauti hiyo?”<br />
“Haya mama wa Kiswahili, siwezi kushindana na wewe, hapo umenishinda.”<br />
“Enhee stori nyingine?”<br />
<br />
“Sina!”<br />
“Basi poa, acha mimi nirudi zangu home, si unajua tena dingi hajaingia, sasa akija na kunikuta sijafika nyumbani mpaka saa hizi haitakuwa sawa!”<br />
<br />
“Sawa basi. Enhee niambie, naanza lini kazi?”<br />
“Una hamu eeh!”<br />
<br />
“Sasa kumbe ningefanyaje?”<br />
“Subiri kidogo, mpaka kesho nitakupa jibu kamili la lini utaanza kazi rasmi.”<br />
<br />
“Sawa.”<br />
“Usiku mwema.”<br />
“Nawe pia!”<br />
<br />
Deo akaondoka, Levina akaendelea kumkazia macho mpaka alipoondoka. Baada ya hapo akavuka upande wa pili, akachukua taxi nyingine na kurudi zake nyumbani. Kwa bahati nzuri, baba yake alikuwa bado hajafika nyumbani.<br />
“Una bahati, baba yako hajafika!”<br />
<br />
“Acha tu mama!”<br />
“Enhee vipi, mambo yanaendaje?”<br />
“Huyo kijana yupo mama, hata kesho anaweza kuja!”<br />
<br />
“Sawa basi, lakini naomba tusubiri hadi kesho, kama yule wa Bagamoyo hatakuja basi atakuja huyo, unajua tayari nilishamuahidi na huyo mtu alimuhangaikia sana!”<br />
“Sawa mama,” Levina akasema kwa sauti ya chini lakini ndani ya moyo wake akiumia sana.<br />
<br />
Alitamani sana huyo kijana asitokee ili Deo wake aweze kwenda nyumbani kwao. Hiyo ilikuwa dua yake kubwa.<br />
“Mimi naingia chumbani mama.”<br />
<br />
“Sawa, bado nipo hapa naendelea kuangalia taarifa ya habari.”<br />
Muda mfupi baada ya Levina kuingia chumbani kwake, simu ya Mama yake ikaita. Namba hakuzijua, lakini mara moja akapokea!<br />
“Nani mwenzangu?” Ndiyo neno la kwanza mama Levina kutamka mara baada ya kupokea simu.<br />
<br />
“Mama Happy wa Bagamoyo...samahani mama Levina, nimekupigia na namba ya kibandani, simu yangu haina chaji!”<br />
“Usijali, vipi za huko?”<br />
“Bwana wangu, si salama.”<br />
<br />
“Kuna nini tena?”<br />
“Yule kijana amefiwa na mama yake, kwahiyo anatakiwa kwenda kwao Morogoro kesho, kurudi ni baada ya wiki mbili!”<br />
“Duh!”<br />
<br />
“Ndiyo mwenzangu, matatizo yamemfika kijana wa watu, kwa jinsi alivyokuwa na hamu na hiyo kazi, yaani amechanganyikiwa kabisa!”<br />
“Poleni mwaya, umpe pole na yeye, hakuna jinsi, maana nilikuwa na shida ya haraka sana na kijana wa kazi, sasa nalazimika kutafuta mwingine.”<br />
<br />
“Hakuna shida, haikuwa riziki yake!”<br />
Wakakata simu zao. Muda ule ule mama Levina akamwita binti yake, ambaye alifika baada ya muda mfupi sana.<br />
<br />
“Levina nimepigiwa simu na Happy sasa hivi, yule kijana amepatwa na matatizo. Amefiwa na mama yake, kwahiyo hataweza tena kuja labda mpaka baada ya wiki mbili, nimemwambia mama Happy kwakuwa nina haraka, nalazimika kutafuta mwingine kwahiyo basi zungumza na huyo rafiki yako, yule kijana aje kesho aanze kazi mara moja!”<br />
<br />
“Sawa,” Levina akajibu kwa sauti ya chini sana, akionekana kuwa na huzuni lakini ndani ya moyo wake alikuwa akishangilia kwamba Deo wake alikuwa anakwenda kuwa karibu naye.<br />
<br />
****<br />
Levina alivyoingia tu chumbani kwake, kitu cha kwanza ilikuwa kuchukua simu yake na kumpigia Deo haraka sana.<br />
“Vipi?”<br />
<br />
“Habari njema zaidi ya zile za saa ile!”<br />
“Zipi tena Levina?”<br />
“Unatakiwa kuanza kazi kesho, vipi utaweza?”<br />
“Nitaweza!”<br />
“Kweli?”<br />
<br />
“Kweli kabisa.”<br />
“Basi fanya juu chini, kesho tukutane saa 3:00 asubuhi!”<br />
“Sawa.”<br />
Wakaagana.<br />
<br />
****<br />
Kama walivyokubaliana, siku iliyofuata walikutana Mwembechai, Deo akiwa na begi lake, tayari alikuwa ameshaacha kazi alipokuwa akifanya mwanzoni na akawa tayari kwenda kuanza kazi kwa akina Levina.<br />
<br />
Wakaingia sebuleni na kukutana na mama yake Levina akiwa anamsubiria kwa hamu...<br />
<br />
“Karibu mwanangu!” Mama Levina akamwambia Deo.<br />
“Ahsante mama!”<br />
“Jisikie uko nyumbani!”<br />
<br />
“Ahsante mama.”<br />
“Nina imani maelekezo yote umeshapewa na Levina, kama bado atakupa. Acha mimi niwahi kazini, nawatakieni siku njema,” akasema mama Levina akisimama na kupiga hatua za kuondoka.<br />
<br />
“Ahsante!” Deo akajibu akiona haya.<br />
Mama Levina akaondoka zake, akawaacha Deo na Levina tu nyumbani. Levina aliposikia muungurumo wa gari la mama yake nje, akajua tayari ameshaondoka. Akamkazia macho Deo, aliyekuwa amesimama kama mlingoti!<br />
<br />
Mara ghafla akamsogelea na kumkumbatia kwa nguvu! Kilikuwa kitendo cha haraka na ghafla sana, kilichomshtua sana Deo. Akabaki ameduwaa akimwangalia bila majibu!<br />
Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d905194fcd5e08171837"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d905194fcd5e08171837"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d905194fcd5e08171837"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d905194fcd5e08171837"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018">USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE.12<br />
<br />
Levina anafanikiwa kumsogeza Deo karibu yake, baada ya kumtafutia kazi ndani mwao. Nini kitaendelea? Songa nayo...<br />
<br />
Levina alimshangaa Deo kwa kutoonesha furaha kwa kupata kazi.<br />
<span class="text_exposed_show"> “Jamani Deo mbona huoneshi furaha?”<br />
“Levina mbona nipo happy.”<br />
“Muongo, au hukupenda kuja kufanya kazi hizi?”<br />
“Kwa nini nisipende.”<br />
<br />
“Basi Deo nakwambia achana na mshahara utakao lipwa nitahakikisha nakuongezea pesa zaidi ya mshahara wako.”<br />
“Nitashukuru Levina.”<br />
“Basi twende nikakuoneshe chumba chako.”<br />
<br />
Levina alichukua begi la Deo na kumpeleka kwenye banda la uani kulikokuwa na chumba kimoja. Baada ya kuingia chumbani alitoka na kurudi na ufagio na shuka za kumtandikia. Deo alishangaa mtoto wa tajiri yake kumuhangaikia vile, baada ya usafi wa chumba alimtandikia kisha alimkaribisha.<br />
<br />
“Deo karibu hiki ndicho chumba chako.”<br />
“Asante.”<br />
“Vipi umekipenda?’<br />
”Nimekipenda.”<br />
<br />
Baada ya kumuonesha kile chumba alimuelekeza kazi zote alizotakiwa kuzifanya kisha alimuacha aendelee na majuku ya siku ile. Levina alirudi hadi sebuleni kutaka kujiandaa kwenda mjini kwenye duka.<br />
<br />
Lakini roho haikumpa alisogea hadi dirishani kumtazama Deo aliyekuwa katika vazi la bukta na singland, alijikuta akitabasamu mwenyewe jinsi moyo wake ulivyofurahi kuwa na Deo mwanaume aliyeutesa moyo wake.<br />
<br />
Kuwa mbali na Deo aliona kama kuinyima uhuru nafsi yake, aliamini muda ule ambao wazazi wake hawapo ni muda mzuri wa kujisogeza karibu na Deo. Alitoka hadi uani ambako Deo alikuwa ameanza kazi ya kupunguza majani, alisogea karibu yake huku kidole kikiwa mdomoni kujipa ujasiri.<br />
<br />
“Deo,” alimwita huku akiachia tabasamu pana.<br />
“Levina si umesema unawahi kazini?”<br />
“Ndiyo Deo lakini bado nina muda, Deo,” Levina alimwita Deo huku akimtoa majani kichwani.<br />
“Unasemaje Levina?”<br />
“Kazi unaionaje?”<br />
<br />
”Ndiyo naianza lakini siyo mbaya.”<br />
“Leo kuna kitu nataka kukueleza.”<br />
“Kipi hicho?” Deo aliuliza bila kumuangalia.<br />
“Deo acha kwanza kukata majani nisikilize.”<br />
<br />
“Levina hii ndiyo kazi iliyonileta acha niifanye, we wahi kazini jioni tutazungumza nitakuwa nimepunguza kazi si unajua leo ndiyo siku ya kwanza nitaonesha picha mbaya.”<br />
“Deo ufanye kazi usifanye kazi mimi ndiye mwenye mamlaka, na kukuleta hapa si kufanya kazi hii.”<br />
<br />
“Si kazi hii, kwa kazi gani?”<br />
“Ili uwe karibu na mimi”.<br />
“Kivipi?”<br />
“Deo lazima usome alama za nyakati kila ninachokifanya lazima ujiulize kina maana gani.”<br />
<br />
“Levina mimi na wewe tumefahamiana kitambo umekuwa msichana ambaye umeonesha kunijali, nimekuwa nikivunia upendo wako na kujikuta nikikosa cha kukulipa.”<br />
“Deo cha kunipa unacho hakihitaji pesa wala nguvu.”<br />
“Kipi hicho?”<br />
<br />
“Deo lazima leo nikueleze ukweli...na..na..ku...,” Levina hakumalizia aliweka kidole mdomoni huku mkono ukitetemeka baada ya kupoteza ujasiri wa kulitamka neno toka moyoni mwake.<br />
“Levina unasemaa!”<br />
<br />
Levina aliona aibu na kukimbilia ndani huku akimwacha Deo akijiuliza maswali yasiyo na majibu, alijiuliza Levina alimaanisha anampenda. Kama ni kweli ulikuwa mtihani ambao aliamini kabisa mapenzi ni kikohozi kamwe wasingeyaficha. Kwa muonekano wa haraka ilionekana familia yake ilikuwa ikimpenda sana na kumjali.<br />
<br />
Aliamini kama wazazi wake wakigundua lazima wangemfukuza kazi, alijua lazima atataabika kutokana na kuacha kazi iliyokuwa ikimuingizia riziki. Pia alikuwa na mtihani mwingine kama atamkatalia Levina lazima atamfukuzisha kazi, lakini hakutaka kuingilia sana mawazo ya Levina.<br />
<br />
Levina alikimbia hadi chumbani kwake na kuanza kulia kutokana na kukosa ujasiri kuwasilisha uju mbe wake. Alichukua kitambaa cha mkononi na kufuta machozi. Mara simu ya mama yake iliingia, aliipokea na kuzungumza.<br />
“Haloo Mamy.”<br />
<br />
“Levina upo wapi?” Alimuuliza kwa ukali kidogo.<br />
“Mbona hivyo mama?”<br />
“Hujanijibu upo wapi?”<br />
“Mamy nipo njiani nakwenda mjini.”<br />
<br />
“Jitahidi uwahi kuna mteja wa jana mlikubaliana afuate simu dukani amefika muda, bado duka halijafunguliwa.”<br />
“Namjulisha sasa hivi.”<br />
<br />
Alikata simu na kukimbia bafuni kuoga kisha alibadili nguo haraka haraka kuwahi dukani, alitoka hadi uani alipokuwa Deo akikata majani alitembea kwa mwendo wa kunyata alipomkaribia alimgusa begani, Deo alipogeuka alikutana na busu la mdomoni.<br />
“Deo bai, nawahi kazini kazi njema.”<br />
“Na wewe pia.”<br />
<br />
Levina alitembea kwa haraka kuelekea kwenye gari lake ili awahi kwenye mihangaiko yake. Nyuma alimuacha Deo na maswali mengi juu ya vitendo vya kimahaba vya Levina, Levina alibadilika kwa muda mfupi hakuwa yule mpole na mnyenyekevu muda wote, alikuwa ni mtu aliyeonekana kuchizika kimahaba.<br />
<br />
Kauli ya Levina ilimfumbulia fumbo zito moyoni mwake la muda mrefu la huduma zote zilizoelekezwa kwake na Levina haikuwa bure na ukweli wake ulikuwa umedhihirika muda mfupi uliopita. Deo alicheka na kuendelea kupunguza majani huku umbile la Levina msichana mrembo tena anayetoka katika familia tajiri lilitawala katika ubongo wake.<br />
<br />
Nini Kitaendelea?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">USIFE KWANZA MPENZI WANGU ......EPISODE .13.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
Kauli ya Levina ilimfumbulia fumbo zito moyoni mwake la muda mrefu la huduma zote zilizoelekezwa kwake na Levina haikuwa bure na ukweli wake ulikuwa umedhihirika muda mfupi uliopita. Deo alicheka na kuendelea kupunguza majani huku umbile la Levina msichana mrembo tena anayetoka katika familia tajiri likiwa limetawala katika ubongo wake.<br />
<span class="text_exposed_show"> SASA ENDELEA...<br />
<br />
Mbinu za Levina kumuingiza ndani ya jumba lao lilimfanya Deo acheke peke yake kwa kicheko cha chini chini huku akitikisa kichwa, kama alikuwa akizungumza na mtu alisema kwa sauti ya chini.<br />
<br />
“Kweli Levina kiboko, mbinu zake mwenyewe sina hamu.”<br />
Baada ya kumaliza kukata majani aliyakusanya na kuyapeleka kwenye shimo la takataka lililokuwa nyuma ya banda la ng’ombe.<br />
***<br />
Levina akiwa ndani ya gari lake akielekea kwenye duka lao la simu, macho yake yalikuwa yametazama mbele huku akikanyaga mafuta taratibu kutokana na foleni ya jijini. Pembeni ya barabara alimuona mvulana mmoja na msichana wakitaniana katika hali ya mapenzi.<br />
<br />
Aliwakazia macho mpaka alipowapita, alitabasamu na kuchukua simu yake iliyokuwa kwenye dash boad na kuifungua upande wa picha. Aliifungua na kuijaza picha ya Deo kwenye kioo cha simu, picha ambayo alipiga kwa siri bila yeye kujijua.<br />
<br />
Aliibusu simu na kusema kwa sauti ya chini.<br />
“Lazima Deo atanielewa si mtoto mdogo.”<br />
Kutokana na foleni ya barabarani kila gari liliposimama aliiangalia picha ya Deo na kutabasamu. Aliikumbatia simu kifuani katika mahaba mazito na kufumba macho huku akisindikizwa na muziki mtamu wa kizazi kipya wa Suma Usemao Mapenzi ni sumu.<br />
<br />
Alirudia maneno ya kiitikio kimoyomoyo, kumbe wakati huo foleni ilikuwa imeshasogea lakini Levina alikuwa amejisahau na mahaba mazito ya picha ya Deo kwenye simu yake. Hata kelele za honi hakuzisikia kutokana na kujifungia ndani ya gari huku akipulizwa na kiyoyozi. Sauti ya kugongwa dirisha ndiyo iliyomshtua alipofumbua macho aligundua foleni imefika mbele ambapo alibadili gia na kukanyaga mafuta akiwaacha watu wakimsindikiza na matusi mazito ya nguoni lakini hakuyasikia.<br />
<br />
Hata alipofika dukani muda wateja walipopungua alitumia muda huo kuzungumza na Deo huku akimpigia simu mfanyakazi wa ndani ampatie Deo chakula kizuri na kila kitu ambacho baba yake alikitumia wakati wa chakula. Kingine alimuonya mfanyakazi wa ndani kuwa mbali na Deo bila kufanya utani wowote.<br />
<br />
“Haloo Deo.”<br />
“Ooh, Levina za kazi?”<br />
“Zimezidi kuwa nzuri baada ya kusikia sauti yako.”<br />
“Nashukuru kusikia hivyo.”<br />
<br />
“Vipi unafanya nini sasa hivi?”<br />
“Mmh, nimepumzika ndiyo nimemaliza kula.”<br />
“Umekula nini Deo?”<br />
“Chakula.”<br />
<br />
“Chakula gani?”<br />
“Ndizi na nyama.”<br />
“Matunda je?”<br />
“Nimepata.”<br />
<br />
“Juisi?”<br />
“Nimepata.”<br />
“Umeshiba?”<br />
“Nimeshiba.”<br />
<br />
“Muongo, usione aibu wewe kwa sasa ni zaidi ya baba yangu mzazi.”<br />
“Kivipi?”<br />
“Umekuwa mtu muhimu sana maishani mwangu, kuwa nawe karibu nimefarijika. Nilijihisi ufahari siku uliyonikubalia kuja kufanya kazi kwetu.”<br />
<br />
“Mh!”<br />
“Usigune Deo, lazima niseme ukweli, Deo nakupenda sana.”<br />
Maneno yale yalimfanya Deo anyamaze kwa muda kitu kilichomnyima raha Levina na kuona mbegu yake huenda hakuipanda muda muafaka. Lakini kwa upande mwingine alijiona yupo sawa kutokana na moyo wa kupenda ulivyo.<br />
<br />
Siku zote macho yakiona moyo unapenda na moyo ukipenda subira hakuna tena na subira ikitoweka aibu hukimbia. Aliamini mchuzi wa mbwa ulitakiwa kunywewa ungali moto.<br />
<br />
Hakujutia kauli yake kumueleza ukweli Deo kuwa anampenda, ulikuwa ujumbe sahihi toka moyoni mwake ambao aliamini kupitia njia ya simu kidogo ujasiri ulikuwepo. Lakini kimya cha Deo kilimfanya akose raha moyoni kwake aliamini kama Deo hataafiki ombi lake lilikuwa sawa na kutwanga maji kwenye kinu.<br />
<br />
“Deo,” Levina alimwita baada ya kupita ukimya mfupi.<br />
“Levina.”<br />
“Mbona hunijibu, kujivua nguo mbele yako si umalaya Deo, usinihukumu kwa jinsia yangu bali kwa upendo wangu mzito moyoni mwangu. Deo sikuwa na njia yoyote ya kukueleza kuwa nakupenda, naomba uheshimu hisia zangu.”<br />
“Levina,” Deo alimwita Levina kisha alishusha pumzi nzito.<br />
<br />
“Deo,” Levina aliitikia upande wa pili na sauti yenye dalili za kilio.<br />
“Levina naogopa sana mimi kuwa sehemu ya matatizo yako katika furaha zako za kila siku.”<br />
“Deo kunikubalia ni kuniingiza kwenye matatizo?”<br />
<br />
“Sina maana hiyo!”<br />
“Muongo Deo, unataka kuongopa nini?”<br />
“Levina wewe ni mtu muhimu sana kwangu, nilikuwa na maana kutokana na kujitoa kwangu na mimi kuniona ni sehemu ya furaha yako. Nami najitoa kwako kwa nguvu zote ili kukuhakikishia zile raha ulizokuwa ukizitafuta kwangu unazipata.”<br />
“Kweli Deo?”<br />
<br />
“Siwezi kukudanganya.”<br />
“Waooo, I can’t beleave my dear, Thanks God thanks Deo I love you soooo much.”<br />
Levina alishangilia kukubaliwa ombi lake na kujisahau kama yupo dukani na kuwashangaza wateja waliokuwa dukani wakisubiri amalize kuzungumza kwa simu.<br />
Nini kitaendelea?</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><span class="hasCaption">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE .14.<br />
<br />
ILIPOISHIA<br />
“Waooo, I can’t beleave my dear, Thanks God thanks Deo I love you soooo much.”<br />
Levina alishangilia kukubaliwa ombi lake na kujisahau kama yupo dukani na kuwashangaza wateja waliokuwa dukani wakisubiri amalize kuzungumza kwa simu.<br />
<span class="text_exposed_show"> SASA ENDELEA...<br />
<br />
Hata baada ya kumaliza kuzungumza na simu, uso wa Levina ulionesha dhahiri kuwa amezama ndani ya dimbwi la huba. Aliendelea kuchekacheka mwenyewe kama mwendawazimu bila kujali idadi kubwa ya wateja ambao walikuwa wakisubiri kuhudumiwa. Akili yake ilijawa na taswira ya Deo kiasi cha kusahau kazi.<br />
<br />
“Oya sista vipi? Tumesimama muda mwingi kusubiri huduma we uko bize na simu tu! Tuhudumie tafadhali!”<br />
Kauli ya mmoja wa wateja waliokuwa wamesimama kusubiri huduma kwenye duka la simu la kina Levina ilimzindua kutoka kwenye mawazo yaliyoiteka akili yake.<br />
<br />
Oops! Im sorry, samahani wateja, hii simu imetoka kwa mtu muhimu sana, enhe, ulisema unataka Nokia toleo gani?”<br />
“Nokia 5130c-2!”<br />
“Mimi nakudai chenji yangu, naona simu imekupagawisha kabisa, shemeji nini?”<br />
<br />
Levina aliendelea kuwahudumia wateja waliokuwa wakiingia na kutoka kwenye duka lao la simu. Wakati akiendelea na kazi, majibu ya Deo yalikuwa yakiendelea kuzunguka kichwani mwake kama filamu nzuri ya kusisimua.<br />
<br />
Wateja walipopungua, alichukua simu yake na kuendelea kuitazama picha ya Deo aliyompiga bila mwenyewe kujijua, akawa anaitazama huku usoni akiwa na bonge la tabasamu! Moto wa penzi la Deo ulikuwa umewaka kikweli ndani ya moyo wake, akawa anasubiri kwa hamu muda wa kufunga duka ufike haraka ili akaonane na Deo, kipenzi cha moyo wake.<br />
<br />
***<br />
Kuchanganya mapenzi na kazi ni suala ambalo Deo alikuwa akiliogopa sana. Mara kwa mara alikuwa akijiambia mwenyewe kuwa safari ya kutoka nyumbani kwao Shinyanga hadi Dar es Salaam ilikuwa ni kutafuta maisha, hivyo hakuwa tayari kuona anashindwa kutimiza ndoto zake kwa sababu ya kuchanganya mapenzi na kazi.<br />
<br />
Alipofikiria kitakachotokea endapo uhusiano wake na Levina ungegunduliwa na wazazi wa Levina, alijikuta akibatilisha majibu aliyompa Levina siku ile. Alichokiamua ni kutojihusisha kwenye uhusiano wa kimapenzi na Levina, aliamua kuelekeza nguvu na akili zake kwenye kazi.<br />
<br />
Saa zilizidi kuyoyoma na hatimaye muda wa Levina kurudi nyumbani ukawa umewadia. Akilini mwake, Levina alikuwa akiwaza namna atakavyomkumbatia na kumkiss Deo mara atakapowasili nyumbani kwao. Alipanga kufanya kila linalowezekana ili kumfanya Deo ampende kama yeye anavyompenda.<br />
<br />
Baada ya kufunguliwa geti na kwenda kuegesha gari lake, Levina alishuka akiwa na hamu kubwa ya kuoanana na Deo. Nyumbani kwao hakukuwa na mtu mwingine yeyote zaidi ya mfanyakazi wao na Deo kwani wazazi wake walikuwa bado hawajarejea kutoka kwenye mihangaiko yao.<br />
<br />
‘Jamani Deo! Nilikukumbuka sana sweetie, yaani nilikuwa naona saa haziendi,’ aliongea Levina kwa sauti ya kudeka na kumkumbatia Deo kimahaba. Katika hali ambayo hakuitegemea, Levina alishangaa kumuona Deo akikunja sura na kumsukuma pembeni, kisha akaondoka na kuelekea chumbani kwake na kumuacha Levina akiwa bado haamini kile kilichotokea.<br />
<br />
“Kwa nini unanitesa Deo, nifanye nini ili uamini kuwa ni kweli nakupenda?” Aliongea Levina huku akimfuata Deo.<br />
“Tafadhali sana Levina, sina maana ya kukutesa lakini naona kama najihatarisha sana pamoja na kukuweka wewe kwenye matatizo.”<br />
<br />
“Kivipi Deo, mi sikuelewi mwenzio?”<br />
“Namaanisha hivi, nakupenda sana Levina lakini sitaki kuwaudhi wazazi wako! Naamini wakigundua watakasirika sana na watanitimua hapa kwenu, nimetoka mbali sana Levina kuja mjini kutafuta maisha, sitaki mapenzi yaniharibie maisha yangu ya baadaye…”<br />
<br />
Wakati Deo akiendelea kujitetea mbele ya Levina, walisikia geti la nje likifunguliwa na gari la wazazi wa Levina likaingia ndani. Kwa haraka Deo alitoka nje na Levina naye akaelekea chumbani kwake huku wakiahidiana kuzungumza vizuri baadaye wakiwa peke yao.<br />
<br />
***<br />
Deo alijitahidi kuficha hisia zake mbele ya wazazi wa Levina. Bado hofu ilikuwa imeupamba mtima wake. Muda wa chakula cha jioni ulipowadia, kama kawaida familia nzima ilijumuika Dinning room kwa ajili ya maakuli. Kwa makusudi kabisa, Levina alijisogeza na kukaa jirani na Deo, akamsaidia kumpakulia chakula na kumkaribisha kwa heshima.<br />
<br />
Wakati wakiendelea kula huku wakibadilishana mawazo hapa na pale, Levina alikuwa akimtazama Deo usoni kwa kuibia na kuishia kutabasamu mwenyewe. Mchezo ule ulishtukiwa na mama yake Levina, ambaye hata hivyo alijikausha ili awanase vizuri.<br />
<br />
Kwa aibu alizokuwa nazo Deo, alijikuta akishindwa hata kula kwa uhuru kwani mamcho ya Levina yalikuwa hayabanduki kwake. Kaamua kujikaza kiume na kumtaza na yeye usoni bila kujali kuwa wamekaa na baba na mama. Macho yao yalipogongana, wote walitabasamu kimahaba, hali iliyomfanyampaka baba Levina kushtuka.</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90966419b6498515018"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE.16<br />
<br />
<br />
Penzi linachipuka kutoka ndani mwa Levina kwenda kwa Deo, kijana anayefanya kazi nyumbani kwao kwa kasi ya ajabu sana. Anashindwa kufanya kazi vyema kutoka na hisia hizo kali za mapenzi. Anajaribu kumweleza Deo, ambaye alimkubalia kwa shangwe!<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Hili lilimfanya afunge duka lake haraka na kurejea nyumbani ili aweze kupata wasaa wa kuzungumza na Deo, lakini jambo la ajabu, alipofika akakuta Deo akiwa na maamuzi mengine mapya! Hakuwa tayari kuwa naye kimapenzi, kiasi cha kumsukuma mbali!<br />
<br />
Baadaye wakiwa kwenye meza ya chakula, Levina alionesha alama zote kuwa anampenda Deo au walikuwa katika uhusiano, jambo ambalo baba yake, aliligundua! Akahisi kuwepo kwa jambo linaloendelea kimya kimya! Je, nini kitatokea? Endelea kufuatilia...<br />
<br />
MZEE Masamu aligundua kitu kupitia macho ya mwanaye aliyekuwa akimwangalia Deo kwa macho yaliyojaa ubembe wa mahaba. Ni kitu ambacho hakukipenda hakika, hakutaka kabisa mwanaye awe na uhusiano na kijana yule. Hakuwa na hadhi ya familia yao.<br />
<br />
Mara ghafla, akasogeza pembeni sahani yake ya chakula na kunawa mikono yake, jambo hilo lilimshangaza sana mke wake.<br />
“Vipi baba Levina?!”<br />
“I’m okay!”<br />
<br />
“No dady, you are not okay, vipi chakula hujakipenda?” Mama Levina akasema kwa sauti ya taratibu sana.<br />
“Nimeshiba mama Levina,” akasema mzee Masamu akimwangalia Levina kwa macho yenye kiashiria kibaya.<br />
<br />
Mama Levina aliweza kugundua kwamba kuna jambo ambalo si la kawaida lilikuwa likiendelea. Anamfahamu vizuri sana mume wake, hakuwa na kawaida ya kushiba haraka kiasi kile, lazima kulikuwa na kitu. Naye akasogeza sahani yake pembeni na kunawa mikono.<br />
“Mom, kwanini mnasusa chakula?” Levina akauliza kwa mashaka kidogo.<br />
<br />
“Shiiiiii...” mama Levina akamnyamazisha mwanaye.<br />
Deo akagundua kwamba mchezo wa Levina ulikuwa umegundulika, mara moja akanawa mikono na kukimbilia chumbani kwake. Bwana na Bibi Masamu wote kwa pamoja wakaongozana kwenda chumbani kwako kulala.<br />
<br />
“Mume wangu mpenzi, nini tatizo? Nini kimetokea mpenzi wangu, maana naona haupo sawa kabisa!” Mama Deo akamwuliza mumewe walipoingia chumbani kwao.<br />
“Unataka kusema hujaona chochote?” Mzee Masamu akasema kwa hasira.<br />
“Nini tena dear?”<br />
<br />
“Hivi unakumbuka kwanini tulimwondoa Rashid hapa nyumbani?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Unaona anayofanya mwanao?”<br />
“Nani Levina?”<br />
<br />
“Kwani nani mwingine?”<br />
“Kivipi basi mume wangu?”<br />
“Hujaona anavyomwangalia yule kijana?”<br />
“Kwakweli sijawa makini kuwaangalia mume wangu!”<br />
<br />
“Sasa wewe kuwa makini au usiwe makini, lakini nataka kukuambia kwamba, sitaki matatizo katika familia yangu! Deo hana hadhi ya kuwa na mwanangu!”<br />
“Kwani amesema anataka hivyo?”<br />
“Hapana, lakini dalili zipo wazi.”<br />
“Nitazungumza na Levina!”<br />
<br />
“Siyo utazungumza naye, nenda ukaongee naye sasa hivi, sihitaji matatizo katika familia yangu. Narudia tena sihitaji matatizo katika familia yangu, nenda kazungumze naye tafadhali.”<br />
<br />
“Nimekuelewa mume wangu, ngoja niende nikaongee naye.”<br />
Mama Levina akatoka haraka na kumuacha mumewe chumbani akiwa amefura kwa hasira. Alipofika sebuleni, alimkuta Levina akiwa anamalizia kuondoa vyombo mezani.<br />
“Levina nahitaji kuongea na wewe!”<br />
<br />
“Natoa vyombo mama!”<br />
“Achana navyo isitoshe si kazi yako, kwani Helena yupo wapi? Hiyo ni kazi yake, haikuhusu wewe hata kidogo.”<br />
“Najua mama, lakini...” Levina akaendelea kujitetea.<br />
“Wewe tusikilizane!”<br />
<br />
“I’m coming mom!”<br />
“Hurry up!”<br />
“Ok mom!”<br />
Levina akaacha kila kitu na kujisogeza kwa mama yake, aliyekuwa amekaa kwenye sofa kubwa pale sebuleni.<br />
<br />
“Hebu niambie, nini kinaendelea kati yako na Deo?!” Mama yake akamwuliza mara baada ya kukaa sofani.<br />
“Unamaanisha nini mama?”<br />
“Macho yako yanaonesha jinsi unavyofahamu ninachomaanisha!”<br />
“Sijui kitu mama, kwani vipi?”<br />
<br />
“Sasa mimi sina kitu cha kuzungumza zaidi au kubembelezana na wewe, lakini nataka kukuambia kwa kifupi sana, kama una wazo la kuanzisha uhusiano na Deo, futa kabisa wazo hilo!”<br />
“Uhusiano?”<br />
“Ndiyo nimekuambia sasa, ondoa wazo hilo kichwani mwako na kama mmeshaanza tafadhali acha mara moja!”<br />
<br />
“Maamaaa...mimi na Deo wapi na wapi mama?”<br />
“Hili agizo limetoka kwa baba yako!” Mama Deo akaongeza kusema.<br />
“Mungu wangu, kweli mama?” Levina akashtuka sana.<br />
“Nadhani unamfahamu vizuri sana mzee Masamu, unajua hasira zake, sasa endelea na upuuzi wako ndiyo utajua kitakachotokea!” Mama yake akasema na kusimama kisha akaondoka zake.<br />
<br />
Levina akabaki pale subuleni akiwa mwenye mawazo mengi sana kichwani mwake. Alimfahamu vizuri sana baba yake, kama ni kweli yeye ndiye alikuwa ameagiza aachane na Deo, basi hali ilikuwa mbaya kuliko alivyofikiria.<br />
<br />
Jambo hilo lilimtisha sana, lakini halikusababisha penzi lake dhidi ya Deo lishuke, bado alihisi penzi zito sana moyoni mwake, alimpenda sana Deo na hakuwa tayari kumpoteza.<br />
Je, Levina atatii kauli ya mama yake?</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d9096611206660650774">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE.18<br />
<br />
Tayari mambo yamekuwa mabaya kwa upande wa Deo, ambaye Levina anaonekana kumpenda sana, lakini kitu cha ajabu ni kwamba, Levina anashindwa kuficha hisia zake na hivyo kusababisha baba mzazi wa Levina mzee Massamu kuhisi kitu!<br />
<br />
Jambo hilo lilimtisha sana Deo, ambaye aliingia chumbani kwake akiwa na mawazo tele akianza kuhofia kupoteza ajira yake. Akiwa bado <span class="text_exposed_show">ana mawazo, usingizi ukiwa umekataa kabisa kumchukua, akasikia mtu akigonga mlango. Akashtuka sana.<br />
<br />
Alipouliza aliyekuwa akigonga ni nani, hakujibu! Je, nini kitatokea? Endelea kuisoma...<br />
<br />
DEO alishtuka kuliko kawaida, mawazo tele kichwani mwake yakamuandama, kitu kilichoingia kwa kasi sana akilini mwake ni kwamba aliyekuwa akigonga mlango ule alikuwa ni mzee Massamu.<br />
<br />
Hapo hakika ungekuwa mwisho wa ajira yake. Jambo ambalo hakutaka kabisa litokee. Akasogea mpaka kwenye kitasa cha mlango wa chumbani kwake, akasogeza mdomo wake kwenye tundu la funguo, akauliza kwa sauti ya chini kabisa...<br />
“Nani?”<br />
<br />
“Fungua!” Sasa akajibiwa na sauti ya kike, ambayo haikuwa ngeni sana masikioni mwake.<br />
Alikuwa ni Levina.<br />
“We’ Levina, acha ujinga bwana, rudi chumbani kwako.”<br />
“Fungua kwanza, kuna kitu nataka kukuambia.”<br />
“Nini?”<br />
<br />
“Fungua.”<br />
Deo akatumia muda wa dakika mbili tatu kuwaza, kisha akaamua kwenda kufungua ili kuepuka kelele za levina ambazo zingeweza kusababisha matatizo zaidi.<br />
“Haya unasemaje?” Akamwuliza baada ya kufungua mlango.<br />
“Kabla hata sijakaa?” Akauliza Levina kwa sauti ya chini, ambayo Deo alishtuka sana kuisikia, akihisi kama ni kubwa.<br />
<br />
“Ongea taratibu bwana...” Deo akasema kwa woga.<br />
“Niongee taratibu nini? Unamuogopa nani?”<br />
“Wazazi wako.”<br />
“Wameshalala bwana.”<br />
<br />
“Kwani unasemaje?”<br />
“Acha utoto, inamaana hujui kwamba mimi nakupenda?”<br />
“Najua.”<br />
“Sasa?”<br />
“Sitaki tena.”<br />
<br />
“Unasemaje?”<br />
“Sitaki tena.”<br />
“Utataka Deo, lazima utake, hujui ni kwa kiasi gani nimehangaika kukupata. Hujui nimefanya mambo mangapi na wakati mwingine kuwakosea watu kwa sababu yako.”<br />
“Lakini Levina ukumbuke kwamba ulisema unanileta kazini.”<br />
<br />
“Ndiyo nakumbuka.”<br />
“Sasa?”<br />
“Lakini si nilikuambia kwamba nakupenda? Unadhani ningeweza kufanya mambo yote hayo hivi hivi tu!”<br />
<br />
“Hivi unajua kwamba haya mambo ni ya hatari sana? Kwanza baba yako anaonekana ameshaanza kuhisi kwamba kuna kitu kinaendelea, huoni kwamba ni tatizo kwangu? Hivi nikipoteza kazi, unadhani nitakuwa mgeni wa nani mimi?”<br />
<br />
“Acha kuwaza mambo ya kijinga...” akasema Levina akivua gauni lake jepesi la kulalia.<br />
“Acha kufanya hivyo Levina.”<br />
<br />
Levina hakusikia kitu, akalitupa mbali baada ya kumaliza kulivua na kumsogelea Deo, kisha akamsukuma kitandani. Kama mzigo Deo akaanguka kitandani na mara Levina akamzidi ujanja, dakika chache baadaye wakajikuta wakiwa kwenye kiota cha huba ya mapenzi, wakiwa wamesahau shida zote za ulimwengu.<br />
<br />
***<br />
“Umeongea naye?” Mzee Massamu akamwuliza mkewe.<br />
“Ndiyo.”<br />
“Anasemaje?”<br />
“Aseme nini?”<br />
“Kwahiyo hajasema chochote?”<br />
<br />
“Simaanishi hivyo...kifupi amekataa.”<br />
“Amekataa?”<br />
“Ndiyo amekataa.”<br />
“Sasa kuanzia leo anza kuwafuatilia utapata majibu, tena nahisi huenda huwa wanalala pamoja usiku. Ngoja muda uende kidogo, nataka kwenda kuhakikisha mwenyewe leo.”<br />
<br />
“Sawa mume wangu, unajua kama itakuwa ni kweli, utakuwa mchezo mbaya sana.”<br />
“Siyo mchezo mbaya tu, sitaki mwanangu ajiingize kwenye matatizo. Unajua kuolewa na lofa, ni sawa na kukaribisha ulofa katika familia. Hilo siwezi kuliruhusu likatokea katika familia yangu. Siwezi kabisa.”<br />
“Ni kweli kabisa baba Levina...itakuwa aibu kwa familia,” akasema mama Levina akiunga mkono kauli ya mumewe.<br />
<br />
***<br />
Saa nane na dakika zake za usiku, Mzee Massamu aliamka kitandani na kutoka nje taratibu kabisa. Akaenda moja kwa moja hadi kwenye mlango wa chumba cha Levina. Akatega sikio kusikia kama Levina alikuwa akihema ndani, lakini hakusikia kitu. Kwakuwa taa ilikuwa haijazimwa, akaamua kuchungulia kupitia kwenye tundu la ufunguo kuangalia kama alikuwemo mle ndani.<br />
<br />
Hakuwepo!<br />
Akashtuka sana.<br />
Akashika kitasa cha mlango na kukizungusha taratibu, mlango ukafunguka wenyewe. Mzee Massamu akaingia mpaka ndani na kuangalia kila kona, hakuona mtu! Ni kweli Levina hakuwemo ndani.<br />
“Shiiiti, huyu mtoto amekwenda wapi?” Akawaza.<br />
<br />
Papo hapo likaja wazo lingine, akahisi huenda alikuwa ameingia msalani, kwa bahati nzuri choo kilikuwa mle mle ndani. Kwahiyo akaamua kuita kwa sauti ya chini...<br />
“Levina...Levina...we Levina...” lakini Levina hakuitika.<br />
Hapo akaamua kuusogelea mlango wa chooni, akajaribu kuusukuma kwa nguvu! Ukafunguka!<br />
Levina hakuwepo!<br />
<br />
“Lazima atakuwa chumbani kwa Deo,” akawaza na kutoka chumbani kwa Levina haraka.<br />
Akapiga hatua za taratibu hadi kufikia mlango wa Deo. Korido nzima ilikuwa kimya kabisa. Alipoufikia mlango wa Deo alitarajia kusikia kelele za mahaba chumbani, lakini hakusikia.<br />
<br />
Chumba kilikuwa kimya kabisa. Hakujiuliza mara mbili, akajaribu kuusukuma ule mlango ambapo ulifunguka mara moja kwakuwa haukufungwa!<br />
Alihisi kuchangikiwa!<br />
Akahisi kuzimia!<br />
<br />
Alichokiona mle chumbani, ilikuwa vigumu sana kuamini. Macho yake yaliona gauni la kulalia la mwanaye likiwa chini, huku nguo yake ya ndani ikiwa juu ya kiti! Deo alikuwa amelala na mwanaye wakiwa kama walivyozaliwa!<br />
Alihisia harufu ya damu!<br />
Akatamani kuua!<br />
<br />
Lakini akajipa moyo!<br />
“Deo unamfanya mwanangu hivi?” akajisemea moyoni mwake.<br />
Haikuwa na maana kwao maana wote walikuwa wameishilia kwenye usingizi mzito, wakiwa kama walivyozaliwa. Busara ya Mzee Massamu ikatumika, akaamua kutoka mle chumbani taratibu na kurudi chumbani kwake. Akamkuta mkewe akiwa macho. Kwa hali aliyoingia nayo, mkewe akajua lazima kulikuwa na kitu kibaya kimetokea.<br />
<br />
“Vipi mume wangu?”<br />
“Nenda mwenyewe chumbani kwa Deo ukajionee.”<br />
“Kuna nini?”<br />
“Nenda mke wangu,” akasema Mzee Massamu akitoka jasho mwili mzima.<br />
Je, nini kitatokea?</span></div></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span><div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d9096600a52655686595">USIFE KWANZA MPENZI WANGU ....EPISODE.21.<br />
<br />
Mzee Massamu ametoka chumbani kwa Deo na kushuhudia akiwa amelala na mwanaye Levina, akamwamsha mkewe na kumwambia aende akajionee mwenyewe chumbani kwa Deo. Nini kitatokea? Endelea...<br />
<br />
MAMA Levina ni kama alikuwa haelewi kabisa anachoambiwa na mumewe. Alimwangalia bila kupata majibu ya moja kwa moja. Kwanini anamwambia aende akajionee mwenyewe chumbani k<span class="text_exposed_show">wa Deo.<br />
<br />
“Mume wangu, niambie tafadhali, kuna nini?”<br />
“Nenda mama, nenda ukaoane mwenyewe!”<br />
Mama Levina hakutaka kuuliza swali lingine zaidi, akatoka na kunyata hadi kwenye mlango wa Deo, kwa haraka za mzee Massamu, hakuufunga ule mlango, kwa hiyo mama Levina alivyotokeza tu akaona kila kitu!<br />
Nusu azimie!<br />
<br />
Akajikaza sana, lakini akashindwa, macho yake yakaanza kumwaga machozi. Hakutaka haraka, akaufunga ule mlango na kuwaacha waendelee na usingizi wao. akatoka haraka hadi chumbani kwao.<br />
<br />
Huko akamkuta mumewe akiwa amejiinamia kwa mawazo tele. Mama Levina naye akaungana naye, yeye akaenda kujitupa kwenye sofa kubwa na kuyatupa macho yake juu ya dari.<br />
Akawaza alichowaza!<br />
<br />
Majibu hayakupatikana!<br />
Lakini akiwa katikati ya mawazo hayo, kumbukumbu za zamani zikaanza kurejea kama sinema ya kusisimua! Akakumbuka jinsi Levina alivyomweleza kuhusu kijana wao wa kazi aliyepita, ambaye alifukuzwa baada ya kumuonesha meseji za mapenzi akimtongoza!<br />
<br />
Ni Levina yule yule!<br />
Iweje leo alale na kijana wa aina ile ile? Mama wa watu akawaza lakini hakupata majibu.<br />
“Hii ni laana, huu ni upuuzi mtupu,” akajisemea moyoni mwake.<br />
<br />
Lakini ghafla kuna kitu kilianza kuingia kichwani mwake kwa kasi ya ajabu, kwamba kuna uwezekano mkubwa Levina alimsingizia yule kijana wa mwanzoni ili aweze kupata nafasi ya kumuingiza yule kijana nyumbani kwao.<br />
<br />
Hilo lilikuja kichwani mwake hasa kutokana na kukumbuka tukio la kumweleza Levina kwamba alikuwa amepata kijana mwingine kutoka Bagamoyo, akalipokea bila furaha. Lakini baadaye aliposikia kwamba kijana huyo amefiwa na alitakiwa kusafiri kwenda kwenye msiba, zikawa taarifa njema kwake na kumleta Deo!<br />
<br />
Kila kitu kikafunguka kama sinema ya kusisimua. Akagundua uchafu wote alioufanya Levina.<br />
“Shiiit! Kumbe ndiyo maana alikuwa anafanya yote yale ili aweze kuja kufanya uchafu wake na huyu mpuuzi siyo?” akawaza kichwani mwake mama Levina.<br />
<br />
Baba Levina alikuwa kimya kabisa, hakuelewa kilichokuwa kikiendelea. Alimpenda sana mwanaye, siku zote aliamini bado alikuwa kigori, lakini kitendo cha kushuhudia uchafu wake, tena mbele ya macho yake kabisa kilimchoma sana moyo wake.<br />
“Mama Levina...” baba Levina akaita.<br />
<br />
“Abee mume wangu!”<br />
“Umeona?”<br />
“Acha tu!”<br />
“Sasa?”<br />
“Sasa nini tena, zaidi ya kumtimua huyo mpumbavu hapa nyumbani?”<br />
<br />
“Sawa, tulale, hili nitalimaliza mwenyewe asubuhi!”<br />
“Sawa mume wangu, lakini ukweli ni kwamba sijaamini kabisa kama Levina angeweza kutuabisha kiasi hiki!”<br />
<br />
“Hata mimi pia, sina amani kabisa. Nahisi kama dunia nzima inaniangalia mimi. Huyu mtoto ametuvua nguo kabisa!”<br />
Wakaamua kulala, lakini wakiwa na majonzi tele mioyoni mwao.<br />
<br />
***<br />
Mzee Massamu aliamka mapema sana siku hiyo, lakini kila alipokuwa akitaka kutoka nje, alijikuta miguu yake ikikataa kabisa. Alihisi alikuwa na hasira kali ambayo ingeweza kusababisha madhara makubwa.<br />
Baada ya kujishauri kwa muda mrefu, akatoka hadi sebuleni huku akiendelea kufunga tai yake shingoni.<br />
<br />
Akiwa sebuleni, akafungua pazia kuangalia nje, akamuona Deo akikatia majani ya fensi, akahisi moyo wake kwenda mbio sana.<br />
Akaketi kwenye kiti, akachukua viatu vyake, akafunga kamba na kutoka nje. Alipofika mlangoni, akajikuta anasita kuinua mguu wake kupiga hatua nyingine.<br />
<br />
“Deo,” akajikuta ameita.<br />
“Naam baba,” Deo akaitika haraka na kukimbia alipokuwa amesimama mzee Massamu.<br />
“Shikamoo baba!” akasalimia Deo.<br />
“Mar-haba bwana, mzima?”<br />
“Sijambo!”<br />
<br />
“Hata mimi naona hujambo!” Mzee Massamu akamjibu.<br />
Kwa mara ya kwanza alimuona mzee huyo akiongea naye kwa muda mrefu, tena maneno ambayo yalionekana kuwa na mafumbo ndani yake. Moyo wake ukapiga kambi!...Puuu!<br />
“Mchezo umeshtukiwa nini?” akawaza.<br />
<br />
“Hivi hapa ndani una mke?” swali hili likazidisha utata kichwani mwake.<br />
“Mke?”<br />
“Kwani umekuja kuoa au kufanya kazi?” Lilikuwa swali gumu kidogo kujibu. Akabaki anababaika akikosa cha kuongea.<br />
<br />
“Hivi, unajua huyu Levina nimeteseka naye kwa kiasi gani?” akamwuliza tena.<br />
Deo akanyamaza kimya.<br />
“I’m talking to you!” akasema kwa Kiingereza, hapo ndipo Deo hakuelewa chochote kabisa.<br />
Deo bado aliendelea kubaki kimya.<br />
<br />
“Sikia kijana...huwa nina roho nzuri sana, lakini pia nina roho mbaya sana. Naweza kukutwanga risasi kufumba na kufumbua...naomba ndani ya dakika tano, uwe umeshaondoka hapa kwangu...haraka sana naomba ufutike!”<br />
“Sawa mzee.”<br />
<br />
“Ingia ndani uchukue kila kilicho chako, uondoe nuksi nyumbani kwangu!” akasema Mzee Massamu akionekana kuzidiwa na hasira.<br />
Deo akabaki anatetemeka, hakuwa na neno lolote la kuongea, kwa hali aliyoonekana kuwa nayo Mzee Massamu, kama angeongea neno lolote, angeweza kuishia kupigwa risasi na kufa pale pale. Mzee Massamu akaondoka na kuingia kwenye gari lake, hapo Deo akaingia ndani na kuchukua nguo zake, akaondoka.<br />
<br />
Hakumuaga Levina wala mama yake. Alijua ni kiasi gani angepata matatizo kama angefanya hivyo! Akatokomea mitaani akiwa anajuta. Usiku mmoja tu, ndiyo chanzo cha matatizo yale. Alikuwa anarudi kwenye dhiki ambayo tayari alishaisahau. Anarudi kwenye maisha yake ya mitaani!<br />
Akaikumbuka Singida!<br />
Alitakiwa kurudi kwao Singida!<br />
<br />
***<br />
Alikuwa amezama kwenye kumbukumbu ambazo zilibaki kuwa historia, Deo anaumwa, risasi zimepenyeza kwenye bega lake. Hana matumaini tena ya kufunga ndoa na mpenzi wake Cleopatra. Akiwa ameyatoa macho yake pale kitandani, sasa ameweza kumkumbuka vizuri mwanamke yule mrembo aliyekuwa amesimama.<br />
<br />
Yes, alikuwa ni Levina!<br />
Levina Massamu!<br />
“Pole na kuumwa!” Levina akatamka akimkazia macho.<br />
Deo hakujibu!<br />
“Pole sana mwaya, kwahiyo ndoa itaahirishwa?” akauliza tena Levina.<br />
<br />
Uso wa mwanamke huyu, ulikuwa wa upole, lakini aliachia tabasamu mwanana wakati wote alipokuwa akizungumza. Tabasamu ni kitu cha ajabu sana kwa wakati huu ambao Deo anaugulia maumivu kitandani.<br />
<br />
Anatabasamu na wakati yeye yupo kitandani? Tena na tundu la risasi begani! Moyo wa Deo ukaingiwa ubaridi, mara akajihisi kuumia sana, machozi kama maji yakaanza kumiminika machoni mwake. Punde, akamuona mpenzi wake akija uelekeo ule. Mpenzi wake mpya ambaye alikuwa bibi harusi mtarajiwa!<br />
Cleopatra!!!<br />
<br />
Msomaji wangu mpenzi, kama kuna mahali nimekuacha kidogo, piga simu namba 0656 819552 nikuelekeze. Hii ni simulizi tamu ambayo itakuacha na mafunzo makubwa. Usikose kuendelea nayo</span></div></span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965f3a22226012909">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE.22.<br />
<br />
Deo amefukuzwa nyumbani kwa mzee Massamu alipokuwa anafanya kazi, haijulikani alipoelekea, lakini upande wa pili anaonekana akiwa amelezwa hospitalini Muhimbili. Mbele yake amesimama mwanamke ambaye sasa amemkumbuka vizuri, ni Levina aliyekutana naye sokoni Tandale akiwa anauza mchele.<br />
<br />
Je, baada ya Deo kufukuzwa nyumbani kwa mzee Massamu alikwenda wapi? I<span class="text_exposed_show">likuwaje akakutana na Cleopatra na kuamua kuachana na Levina? Kwanini waliachana na nani aliyempiga Deo risasi? Endelea kufuatilia...<br />
<br />
DEOGRATIUS aliyakodoa macho yake akiwa hajui la kufanya, akamwangalia Levina kwa umakani, lakini akiwa na maswali mengi sana kichwani mwake. Mosi, Levina alijuaje kwamba yeye anaumwa? Nani alimpa taarifa hizo?<br />
<br />
Hata hivyo, hayo hayakuwa maswali magumu sana, swali gumu zaidi ambalo lilimchanganya kichwa chake ni akina nani wale waliompiga risasi na kwanini walifanya hivyo?<br />
Akiwa katika maswali hayo, anamuona mwanamke mwingine akija uelekeo wa kitanda chake akitokea mlango mkubwa wa kuingilia pale wodini. Alimfahamu vizuri sana.<br />
<br />
Ni Cleopatra!<br />
Macho ya Cleopatra yalikuwa na wasiwasi mwingi, lakini alipokaribia yakaonesha ukali kidogo. Ukali uliosababishwa na kiumbe kilichokuwa mbele ya kitanda cha Deo.<br />
<br />
Levina!!!<br />
“We’ malaya unafanya nini hapa?” Cleopatra akauliza kwa sauti ya chini lakini iliyojaa ukali.<br />
“Umeniita nani?”<br />
“Malaya!”<br />
“Nani?”<br />
<br />
“Malaya!!! Kwani hujasikia au hutaki? Au hufahamu kwamba wewe ni malaya?”<br />
“Cleopatra mimi ni malaya?”<br />
“Tena mchafu!”<br />
<br />
“Ok! Ahsante sana, ahsante sana mama, sikuja kwa ugomvi, nilikuja kwa ajili ya kumsalimia mgonjwa!”<br />
“Mgonjwa?”<br />
“Ndiyo Deo!”<br />
“Anakuhusu nini Deo?”<br />
<br />
“Ni boyfriend wangu wa zamani, kwahiyo sina tatizo kuja kumsalimia akipata matatizo!”<br />
“Kwanza aliyekupa taarifa za Deo kuumwa ni nani? Tena haraka kiasi hicho?”<br />
“Unataka kumjua?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Ipo siku utamjua, lakini kwa leo hupaswi kumjua...kwaheri...kwa mara nyingine tena Deo pole sana mwaya, najua unaumia na una maumivu mawili! Ya kuugua, lakini pia una maumivu ya kusogeza ndoa yako mbele, pole sana...” akasema Levina na kuanza kupiga hatua kuondoka pale kwenye kitanda cha Deo.<br />
<br />
Deo hakuzungumza chochote, Cleopatra naye hakuwa na la kuzungumza zaidi ya kumsindikiza kwa macho mpaka alipopotea mbele ya macho yake. Akamgeukia Deo aliyekuwa ameyatoa macho yake kwa kukata tamaa kabisa. Akapiga magoti pale na kumbusu usoni mwake.<br />
<br />
“Pole mwaya Deo wangu!”<br />
“Ahsante...” akaitikia Deo kwa taabu kidogo.<br />
“Unajisikiaje sasa?”<br />
“Nina nafuu!”<br />
<br />
“Utapona mpenzi wangu, naamini hadi siku ya ndoa yetu utakuwa umeshapona kabisa na utaweza kwenda kanisani kutimiza ahadi yetu ya muda mrefu!”<br />
“Siamini Cleopatra!”<br />
“Kwanini?”<br />
“Nakufa Patra, nakufa mpenzi wangu!”<br />
<br />
“Hapana baby, usife kwanza mpenzi wangu kabla hatujafunga ndoa yetu...subiri kidogo mpenzi wangu, unioe kwanza...” akasema Cleopatra akilengwa na machozi machoni mwake.<br />
<br />
“Siamini kama nitapona mpenzi, moyo wangu una maumivu makali sana, lakini hata mwili wangu naona unauma, sioni tumaini kabisa, nakufa mpenzi wangu!”<br />
“Hufi baba!”<br />
“Nakufa!”<br />
<br />
“Usife kwanza mpenzi wangu, nakupenda Deo!”<br />
Deo hakujibu kitu, alikuwa na mambo mengi sana kichwani mwake. Alikuwa na maumivu ya kupigwa risasi, lakini pia alikuwa na maumivu na ndoa yake na Cleopatra!<br />
<br />
Alimkumbuka sana Levina, kila alipojaribu kukumbuka sababu ya kuachana kwao, hakuona kama alistahili!<br />
Akazidi kulia.<br />
“Unalia nini mpenzi wangu?” Cleopatra akauliza.<br />
“Maumivu mpenzi!”<br />
<br />
“Pole sana!”<br />
“Ahsante!”<br />
“Hivi dokta ameshakuja kukuona?”<br />
“Sijajua!”<br />
“Namaanisha baada ya kuzinduka!”<br />
“Hapana.”<br />
<br />
“Ngoja niende kumwita mara moja,” Cleopatra akasema na kusimama mara moja kisha kwenda ofisini kwa daktari.<br />
Muda mfupi baadaye daktari alikuwa ameshafika kitandani kwa Deo na kuanza kumpima na kumjulia hali yake.<br />
“Pole sana Deo, unajisikiaje sasa?” Dokta akamwuliza.<br />
“Kidogo nina nafuu.”<br />
<br />
“Usijali, kilichotokea ni mshtuko tu, hujaumia sana, utakuwa sawa wala usiwe na hofu!”<br />
“Lakini dokta kama nilivyokuambia, wiki tatu zijazo tunafunga ndoa, anaweza kuwa ameshapona kabisa?”<br />
<br />
“Bila shaka, tutajitahidi kadri ya uwezo wetu, maadamu yupo chini yetu, kila kitu kitakuwa sawa, kikubwa ni kumuomba Mungu tu!”<br />
“Ahsante sana, naweza kumpa chakula kwa sasa?”<br />
“Umemletea nini?”<br />
“Ndizi nyama!”<br />
<br />
“Sawa, lakini hakikisha anakula chakula laini na chenye kumpa hamu ya kula. Unaweza kumpa.”<br />
“Ahsante Dokta.”<br />
Dokta Pallangyo akaondoka zake na kumuacha Cleopatra akiwa na mgonjwa wake. Akatayarisha chakula na kuanza kumlisha kwa upendo.<br />
<br />
“Nakupenda sana Deo wangu, sipo tayari kukupoteza katika maisha yangu, usijali utapona!”<br />
“Ahsante mpenzi wangu kwa kunipa moyo!”<br />
<br />
Muda wa kuwaona wagonjwa ulipoisha, Cleopatra alitakiwa kuondoka na kumuacha Deo peke yake, jambo ambalo lilimuhuzunisha sana. Moyo wake uliumizwa sana na jambo hilo, lakini hakuwa na jinsi, alitakiwa kuondoka!<br />
“Nitakuja kukuona mpenzi wangu, ugua pole na ulale salama.”<br />
<br />
“Ahsante, msalimie mama!”<br />
“Sawa, nitamsalimia.”<br />
Akaondoka.<br />
<br />
***<br />
Macho yake yalikuwa yanagoma kufumbuka kabisa, alihisi kama yanauma kwa mbali, hata hivyo hakuwa na tatizo la macho, alikuwa na tatizo la bega, lakini macho yake yalikuwa yakipambana na nuru ya asubuhi baada ya kuzoea giza kwa usiku mzima.<br />
<br />
Akajilazimisha kuyafumbua, akayafumbua kwa tabu kidogo. Alipofumbua tu, akakutanisha macho yake na sura ambayo haikuwa ngeni kwake hata kidogo. Alimfahamu vizuri sana msichana aliyekuwa amesimama mbele yake.<br />
Alikuwa ni Levina!<br />
<br />
“Habari za asubuhi Deo? Samahani nimekuja kukusalimia, nimefika mapema sana hapa, lakini sikuona sababu ya kukusumbua katika usingizi, ndipo nikaamua kukusubiri uamke mwenyewe...pole sana,” akasema Levina akiweka uaridi jekundu mezani kwa Deo.<br />
<br />
“Ahsante Levina!”<br />
“Unajua kwanini nimekuja mapema yote hii?”<br />
Deo hakujibu kitu, alitingisha kichwa kuashiria kwamba hakujua sababu.<br />
<br />
“Nilitaka kuwa wa kwanza kuijua hali yako baada ya kuamka leo, lakini pia nilitaka kukuthibitishia kwamba huyo Cleopatra wako hakupendi kama anavyokudanganya, kama angekuwa anakupenda asingeweza kulala usingizi ukiwa wewe unaumwa, alipaswa awahi kukuona...upo hapo?” Akasema Levina akimwangalia Deo usoni.<br />
<br />
Deo hakujibu kitu!<br />
Akabaki anashangaa, akiwa katika hali ya mshangao huo, akamuona Cleopatra akiwa anaingia wodini. Sekunde chache baadaye alikuwa amesimama mbele yake.<br />
<br />
Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia</span></div></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d909661aed1a34366772"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....... EPISODE..23.<br />
<br />
Levina amekuwa wa kwanza kufika hospitalini kumwona Deo akiwa na uaridi mkononi mwake. Anaeleza hisia zake jinsi alivyokuwa akimpenda. Akiwa amesimama pale Cleopatra akaingia wodini akitembea kwa kunyata, baadaye anafika na kusimama mbele ya kitanda chake! Sasa endelea...<br />
<br />
ALIONEKANA kabisa kuchukizwa na kitendo cha Levina kufika hospitalini kumuona D<span class="text_exposed_show">eo, tena kabla yake. Akamwangalia Levina kwa macho yaliyojaa hasira sana, akabenua midomo na kurudisha macho yake kwa Deo aliyekuwa pale kitandani. Akamwonea imani.<br />
<br />
“Lakini Levina unatafuta nini kwangu?” Cleopatra akamwuliza.<br />
“Kivipi?’<br />
“Hujui?”<br />
<br />
“Nimekuuliza kivipi? Mtu anayeuliza maana yake ni kwamba hajui; mimi sijui ndiyo maana nakuuliza. Haya niambie kivipi?”<br />
“Kwanini unakuja kumwangalia mpenzi wangu?”<br />
“Kuna ubaya gani?”<br />
“Ubaya upo?”<br />
<br />
“Upi?”<br />
Cleopatra akakaa kimya!<br />
Ni wazi kwamba hakuwa na jibu la haraka na la moja kwa moja. Maana ni kweli hakukuwa na ubaya katika kumjulia hali mgonjwa.<br />
<br />
“…najua unaogopa kusalitiwa? Ni kweli?” Levina akamwuliza akimwangalia usoni.<br />
Cleopatra akaendelea kubaki kimya.<br />
“Mbona kimya? Unaogopa nitakuibia Deo wako siyo?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Lazima uwe na woga huo….lazima…tena ni kawaida kabisa. Maana siku zote mwizi huwa na hofu sana ya kuibiwa…kwasababu wewe ni mwizi wa waume za watu, ndiyo maana unahofia nitakuibia, mwanamke huna haya kabisa…hivi unajua nilimtoa wapi Deo? Alikuwaje na nilifanya nini hadi ukamkuta akiwa katika hali hii?<br />
<br />
“Unajua? Leo unajifanya unampenda, unajua alikuwaje kabla hajaanza kukuvutia? Unajua hali aliyokuwanayo kabla ya kuwa handsome na kupata kazi nzuri? Wewe ni mpumbavu sana mtoto wa kike.<br />
<br />
Kwa taarifa yako sina haja na Deo tena, ninachokifanya hapa ni ustaarabu tu wa kuja kumjulia hali kama binadamu mwingine, si zaidi ya hapo. Mwone alivyo na sura ya huruma? Utadhani ni mkarimu kumbe muuaji mkubwa!” Akasema Levina kisha akashika njia ya kutokea nje.<br />
<br />
Cleopatra akabakia akimwangalia Levina anavyoishia.<br />
“Amekuambia nini?” Cleopatra akamwuliza Deo aliyekuwa amelala kimya kitandani.<br />
“Amenipa pole!”<br />
“Kingine?”<br />
<br />
“Kaniletea ua!”<br />
“Amesema kuwa anakupenda?”<br />
“Hapana.”<br />
“Wewe unahisi nini?”<br />
<br />
“Kwakweli siwezi kujua, lakini naona kikubwa hapa ni mimi na moyo wangu. Sidhani kama nitabadilisha uamuzi wangu. Bado wewe ni wangu, nitafunga ndoa na wewe. Nakupenda sana Cleopatra, usiwe na wasiwasi na hilo mama, nakupenda sana.”<br />
“Kweli?”<br />
<br />
“Niamini.”<br />
Cleopatra akainama pale kitandani kisha akamwangushia busu mwanana shavuni mwake, machozi yakaanza kumiminika kama maji.<br />
<br />
“Naomba asikudanganye kwa lolote, nakupenda mpenzi, lazima tutimize dhamira yetu.”<br />
“Usijali mpenzi wangu.”<br />
Akamnywesha uji na kumpa matunda akala. Muda wa kuwaona wagonjwa ulivyoisha, akaaga na kuondoka zake.<br />
<br />
***<br />
Ilikuwa asubuhi mbaya zaidi kwa Deo, zaidi ya jana yake. Alikuwa akimuwaza sana Levina. Tena safari hii alikuwa akimuwaza kama mwanamke asiye na hatia. Ni kweli hakuwa na sababu za kumuacha na kutaka kuoana na Cleopatra. Kulikuwa hakuna njia yoyote ya kubadilisha kilichokuwa mbele yake, ni kweli alikuwa anakwenda kufunga ndoa na Cleopatra.<br />
<br />
Tena wiki mbili na siku chache baadaye. Tayari ndoa ilikuwa imeshatangazwa kanisani, kwahiyo isingekuwa rahisi hata kidogo kughairi. Akayatupa macho yake juu ya dari, mawazo tele yakamjaa. Kwa hakika alimkumbuka sana Levina. Mawazo yake yakarudi asubuhi ile ya fumanizi.<br />
<br />
Siku ambayo alifukuzwa na mzee Massamu nyumbani kwao na Levina. Akaikumbuka siku hiyo na mtiririko wa matukio mengine mengi yaliyoonesha mapenzi ya dhati kutoka kwa Levina. Matukio yale yakashuka kama sinema ya kusisimua…<br />
Akakumbuka vizuri…<br />
<br />
***<br />
Kitu cha kwanza Deo kufanya alipofika Magomeni kwenye mataa, ilikuwa ni kumpigia simu Levina, lakini simu yake ilikuwa haipatikani. Akarudia tena na tena, lakini jibu liliendelea kuwa lile lile, haipatikani! Akachanganyikiwa.<br />
<br />
Hapo akajua alitakiwa kuanza maisha yake mapya, ambayo kwa vyovyote yangekuwa ya tabu na shida nyingi! Hakuwa na jinsi ndivyo hali halisi ilivyokuwa…na alitakiwa kukabiliana nayo!<br />
<br />
Hakuwa na kitu kingine chochote zaidi ya begi lake dogo mgongoni lililokuwa limehifadhi nguo zake. Ndani ya begi hilo, pia alikuwa na kiasi cha shilingi laki mbili na arobaini elfu, alizokuwa amezihifadhi wakati akifanya kazi ya kuuza mchele sokoni Tandale! Alikuwa na mawazo tele kichwani, huku akikosa uamuzi wa muelekeo.<br />
<br />
Alisimama pembeni mwa sheli, karibu kabisa na geti la kuingia katika Hoteli ya Travertine. Akaangalia barabara nne, moja ya Kawawa ikitokea Ilala kwenda Kinondoni, nyingine ya Morogoro ikitokea Ubungo kuelekea Posta.<br />
<br />
Akaanza kuwaza atumie ipi? Aende wapi? Kwa nani?<br />
Hakuwa na majibu ya haraka ya wapi aelekee, lakini kikubwa zaidi ni kwamba, aliumizwa sana na kitendo cha kuingia kwenye mateso kwa sababu ya starehe ya usiku mmoja. Hilo lilimchoma sana moyo wake.<br />
<br />
“Lakini nilimwambia Levina hakusikia…sasa ona sasa sina kazi, nabaki nahangaika,” akawaza Deo, lakini hilo haikuwa dawa.<br />
<br />
Alitakiwa kujua anaelekea wapi baada ya tukio hilo. Wazo lililoingia haraka kichwani mwake ni kwenda kutafuta kwanza gesti kwa ajili ya kujibanza kwa siku kadhaa wakati akitafuta kazi. Sehemu pekee ambayo aliamini angepata chumba cha bei nafuu ni Manzese.<br />
<br />
Akaingia kwenye gari la Ubungo, akashukia Manzese – Tip Top na kukata mitaa, akakodisha gesti ya elfu mbili kwa siku!<br />
“Utakaa siku ngapi?” Mhudumu akamwuliza.<br />
<br />
“Kwasasa nitakulipa elfu kumi kwa ajili ya siku tano, kama nitaendelea nitakuongeza pesa nyingine.”<br />
“Sawa, nenda namba sita.”<br />
“Ahsante sana.”<br />
<br />
Deo akaondoka na kwenda kufungua mlango wa chumba namba sita kama alivyoelekezwa, akaingia na kujitupa kitandani. Mawazo tele kichwani mwake. Akiwa bado hajatulia vizuri, simu yake ikaanza kuita, akaichukua haraka, jina lilioonekana kwenye kioo, lilikuwa la Levina.<br />
Akapokea.<br />
<br />
“Umeridhika sasa siyo? Naamini roho yako ipo kwatu sasa…” akasema Deo kwa sauti iliyojaa hasira kwenye simu.<br />
“Niridhike na nini Deo?”<br />
“Kunisababisha nifukuzwe kazi? Sasa maisha yangu yameharibika kama ulivyokuwa unataka siyo?”<br />
<br />
“Sina maana hiyo Deo, kumbuka kwamba mimi nakupenda na sipo tayari kuona maisha yako yanaharibika. Ndiyo maana nimekupigia simu, kwanza uko wapi? Nataka kukutana na wewe!”<br />
<br />
“Kukutana na mimi?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Unataka nini kwangu?”<br />
“Ni juu ya maisha yako. Nia yangu ilikuwa kukusaidia, bado nahitaji kukusaidia.”<br />
Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE .24.<br />
<br />
Licha ya Levina kumsababishia afukuzwe kazi, bado Deo hakati tamaa ya maisha na anaendelea kujipa moyo kuwa ipo siku mambo yake yatatulia.<br />
<br />
Levina analazimika kufanya kazi ya ziada ili kubadili fikra za Deo anayemchukulia kama mtu aliyepania kumharibia maisha yake. Baada ya kumshawishi kwa muda mrefu, Deo anakubali kukutana tena na Levina na wanajikuta w<span class="text_exposed_show">akifungua ukurasa mpya katika maisha yao. Endelea mwenyewe…<br />
<br />
Kitendo cha kupoteza kazi kwa sababu ya mapenzi kilikuwa ni pigo lililomgharimu Deo kwa kiasi kikubwa. Kumbukumbu za yote aliyofanya na Levina ilikuwa ikipita kichwani mwake mithili ya mkanda wa sinema ya kusisimua, hakuamini kuwa kila kitu kimeharibika na kufikia mwisho kwa sababu ya mapenzi.<br />
<br />
Wakati hayo yakiendelea kupita kichwani mwake, alikuwa akifikiria juu ya ombi la Levina kutaka kukutana naye tena.<br />
“Unataka nini kwangu? Deo alirudia kuuliza swali lile, na majibu ya Levina yakawa ni yaleyale, kwamba alikuwa akimpenda na alikuwa tayari kumsaidia.<br />
<br />
“Siwezi kukuruhusu unione tena, najua lengo lako ni kuniharibia maisha yangu, niache nife peke yangu ili ufurahi.”<br />
<br />
“Usiseme hivyo Deo, lengo langu ni kukusaidia na sitokata tamaa mpaka hapo nitakapofanikiwa,” alijibu Levina kwa sauti iliyoonesha kuwa alikuwa akilia kwa uchungu. Mazungumzo kwa njia ya simu yaliendelea lakini msimamo wa Deo ukawa ule ule, hakutaka kuonana tena na Levina.<br />
<br />
Deo akiwa amejilaza pale kitandani, aliendelea kusanifu mandhari ya chumba kile cha kulala wageni alichofikia. Kwa hakika hakuwa na hadhi ya kukaa kwenye chumba kama kile, ila kutokana na yaliyomsibu aliamua kuvumilia na kuyaacha yote yapite.<br />
<br />
Usiku wa siku ile aliuona kama mwaka mzima kwani mpaka kunapambazuka alikuwa hajapata hata tone la usingizi. Kulipopambazuka tu, Deo aliinuka pale kitandani na kwenda kupiga mswaki, lakini kabla hajatoka, simu yake iliita tena na alipoitazama aligundua kuwa ni Levina ndiye aliyekuwa akipiga. Aliitazama simu ile bila kuipokea kwa dakika kadhaa hadi ilipokatika.<br />
<br />
“Anataka nini kwangu? Sihitaji tena kuwa na mpenzi, bora peke yangu,” alijisemea Deo kimoyomoyo. Akiwa bado anatafakari, simu ya Levina iliingia tena, akaipokea kwa jazba…<br />
<br />
“Si nilishakwambia uniache Levina? Sitaki uendelee kunifuatilia tafadhali,” kabla Deo hajamaliza Levina alimkata kauli…<br />
<br />
“Najua unanichukia sana Deo kwa yaliyotokea, lakini amini nakuambia ipo siku utaelewa kuwa nina lengo zuri sana na wewe. Naomba unielekeze mahali ulipo, nina jambo muhimu sana la kukuambia ambalo ni lazima nikuambie leo,” aliongea Levina kwa hisia, jambo lililomfanya Deo arudishe moyo nyuma.<br />
<br />
“Njoo mpaka Manzese, mwambie konda akushushe Tiptop.”<br />
“Nakuja na usafiri binafsi, wala usihofu na nitakuwa hapo baada ya muda mfupi,” alijibu Levina kwa furaha na akaanza kujiandaa.<br />
<br />
“Jamani Deo, nisamehe kwa yote yaliyotokea, nakupenda na niko tayari kukufanyia lolote, amini kuwa sina lengo la kukuharibia maisha yako,” alianza kujitetea Levina mara baada ya kufika Manzese alikoelekezwa na Deo.<br />
<br />
Kitendo cha kumkuta akiwa amepanga chumba katika gesti chafu, yenye mashuka machafu na kitanda kibovu huku dari na kuta zikiwa katika hali mbaya kilimuumiza sana Levina, akashindwa kuificha huzuni yake.<br />
<br />
“Siridhishwi na wewe kuishi mahali hapa, kuonesha kuwa kweli nimepania kukusaidia nataka nikutafutie nyumba nzuri ili tupange vizuri malengo ya maisha yetu ya baadaye,” aliongea Levina huku akiwa amemkumbatia Deo.<br />
<br />
Baada ya mazungumzo ya kina yaliyochukua muda mrefu, Deo alikubali msaada wa Levina na wakatoka kwa ajili ya kwenda kutafuta nyumba ya kupanga.<br />
<br />
Kwa msaada wa madalali aliokuwa akifahamiana nao, walifanikiwa kupata nyumba nzuri ya kuishi maeneo ya Sinza Bwawani, wakakamilisha malipo ya kodi ya mwaka mzima iliyotolewa na Levina ‘cash’, kisha mipango ya kuhamia makazi mapya ikaanza kufanywa mara moja.<br />
<br />
“Mimi nafikiri tukitoka hapa tukanunue kitanda na godoro zuri, kisha vitu vingine vidogo vidogo vitafuata,” alisema Levina.<br />
<br />
“Sawa mama, mimi nakusikiliza wewe.”<br />
Mpaka jioni ya siku ile inafika, tayari Deo alishanunuliwa vitu vyote muhimu vya kuanzia maisha vikiwemo kitanda kizuri na godoro, meza, zulia na viti. Deo akaanza maisha mapya. Angalau sasa alianza kuamini kuwa Levina alikuwa na mapenzi ya dhati kwake.<br />
<br />
Maisha yakawa yanasonga mbele huku mapenzi kati ya Deo na Levina yakizidi kuchanua siku baada ya siku. Ikafika mahali Deo akayasahau machungu yote aliyopitia maishani mwake, akawa anazifukuzia ndoto zake zilizoonekana kupotea kwa kipindi kirefu.<br />
<br />
“Uliwahi kuniambia kuwa una malengo ya kujiendeleza kimasomo, huoni kuwa huu ni muda muafaka,” Levina alimuuliza Deo wakiwa faragha.<br />
<br />
“Ni kweli baby, lakini naona kama nitakuwa nakupa mzigo mkubwa sana, natamani kuja kuwa mhasibu lakini kila nikitazama naona kama kuna kazi nzito mbele yangu.”<br />
<br />
“Wala usihofu Deo, nilishakwambia kuwa nataka kuyabadili maisha yako, amini nakwambia kuwa nitashughulikia masuala yote ya wewe kuanza masomo, cha msingi jiweke tayari.<br />
“Hamna shida sweet, sitakuangusha.”<br />
<br />
Siku chache baadaye Deo akaandikishwa kuanza rasmi masomo ya muda mfupi (Qualifying Test) ili kujiweka tayari kabla ya kujiunga na chuo cha Uhasibu kwani ndoto zake zilikuwa ni kuja kuwa mhasibu.<br />
<br />
Deo akayaanza maisha mapya ya uanafunzi. Licha ya kwamba umri wake ulikuwa mkubwa, hakuona aibu kujichanganya na vijana wadogo katika masomo ya elimu ya sekondari kwa muda mfupi (QT).<br />
<br />
Hiyo ilimpa nguvu kubwa kwani hatimaye alikuwa akielekea kutimiza ndoto zake za siku nyingi kwa msaada mkubwa wa Levina. Aliahidi kumpenda na kumfanyia mema Levina kwani aliyoyafanya kwa ajili yake hayakuwa na kifani.</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965d17a5828788606">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE..25.<br />
<br />
Deo na Levina wameanza ukurasa mpya wa maisha yao ya kimapenzi kiasi cha kusahau yote yaliyowahi kuwasibu. Kwa msaada mkubwa wa Levina, Deo anaanza maisha mapya akiwa katika makazi mapya na anajitahidi kuzifukuzia ndoto zake, hasa ya kusoma na kupata kazi, lakini ghafla mambo yanaanza kubadilika. Shuka nayo…<br />
<br />
Deo aliendelea na masomo ya kujiendeleza na ak<span class="text_exposed_show">awa anaonesha juhudi kubwa katika kila anachokifanya. Alijiapiza kuwa ataendelea kumpenda na kumheshimu Levina kwa maisha yake yote kwani alimbadilisha kabisa.<br />
<br />
Kutokana na juhudi alizozionesha kwenye masomo, haikumchukua muda Deo akawa na uwezo wa kufanya vizuri mitihani na kujibu maswali kwa ufasaha mkubwa, hali iliyomfanya awe kivutio kikubwa kwa wanafunzi wenzake.<br />
<br />
Wasichana wengi walianza kumshobokea na kujifanya wanataka awafundishe. Kwa kuwa alishajiwekea nadhiri ya kutomsaliti Levina, alikaa nao mbali.<br />
<br />
Maisha yalizidi kusonga na hatimaye Deo akamaliza masomo yake kwa mafanikio makubwa. Alifaulu vizuri mtihani wake na kupata vyeti vilivyomuwezesha kujiunga na Chuo cha Uhasibu cha Planet Link Accountancy ambako alisomea stashahada ya uhasibu.<br />
<br />
Kwa kipindi chote hiki maisha ya kimapenzi kati yake na Levina yalikuwa yakizidi kupamba moto siku baada ya siku.<br />
<br />
“Deo malengo yako si yanakaribia kutimia? Bila shaka haitakuwa vibaya tukianza kufikiria kujenga familia yetu, au unasemaje?”<br />
“Ni kweli sweet, lakini kwanini tusisubiri nimalize kabisa halafu nikishapata kazi ndiyo tuanze kufikiria hayo?”<br />
<br />
“Unajua mimi ni mwanamke niliyekamilika, siwezi kuendelea kukaa hivihivi, wenzangu wataanza kunicheka kwamba sizai, mi nataka nikuzalie mtoto wakati wewe unaendelea na masomo yako,” alisema Levina kwa sauti ya mahaba akiwa amejilaza kifuani kwa Deo.<br />
<br />
Licha ya Deo kukwepakwepa, lakini hatimaye aliukubali ushauri wa Levina, wa kutafuta mtoto wa kuupamba uhusiano wao.<br />
“Lakini huoni kwamba litakuwa tatizo kuzaa kabla hatujafunga pingu za maisha,” alihoji Deo huku akizichezea nywele za Levina wakiwa kitandani.<br />
<br />
“Sidhani kama hili litakuwa tatizo, nimehiyari mwenyewe na hakuna wa kunizuia. Nakupenda sana Deo.”<br />
<br />
***<br />
<br />
MIAKA MITATU BAADAYE<br />
Deo alifanikiwa kumaliza salama masomo yake na kupata kazi kama mhasibu wa Kampuni ya Usafirishaji Mizigo ya Snox Carries LTD ya jijini Dar es Salaam. Kwa upande wa Levina tayari alishajifungua mtoto wa kike aliyekuwa na umri wa mwaka mmoja na miezi kadhaa, waliyempa jina la Precious wakiwa na maana ya kitu cha thamani.<br />
<br />
Baada ya kupata mtoto, maisha yalibadilika sana na sasa wakawa wanatumia muda mwingi kumuhudumia na kumfikiria mtoto wao kuliko wanavyojijali wao.<br />
<br />
Deo alikuwa akirudi nyumbani kutoka kazini anamsaidia mkewe malezi ya mtoto wao Precious. Pesa walizopata walizitumia pamoja kufanya mambo mbalimbali ya kimaendeleo. Maisha yao kwa ujumla yalibadilika na usingeweza kudhani kuwa huyu ndiye Deo wa miaka ile.<br />
<br />
“Levina! Nadhani sasa wewe ni mke wangu na nina mamlaka yote juu yako na wewe una mamlaka juu yangu,” aliongea Deo jioni moja wakiwa wanapunga upepo kwenye bustani ya maua nje ya nyumba wanayoishi.<br />
<br />
“Ni kweli mume wangu!”<br />
“Lakini mbona siku hizi hutaki mimi niguse simu yako kama zamani, unapigiwa simu usiku halafu unaenda kupokelea nje na wakati mwingine unaikata mbele ya macho yangu, tatizo nini?”<br />
<br />
“Wewe nawe kwa wivuu! Hakuna anayekuzidi mume wangu kwa kila kitu, siwezi kutoka nje na kukusaliti, amini nakwambia Deo, mimi ni wako peke yako…” alisema Levina huku akimsugua sugua mumewe mgongoni kimahaba.<br />
<br />
Licha ya kujibiwa hivyo, Deo alibaki na dukuduku moyoni kwani mabadiliko ya mkewe yalishaanza kumtia hofu. Tangu mkewe aache kunyonyesha miezi michache iliyopita, alianza tabia za ajabu ambazo zilimfanya ahisi anaibiwa mali zake. Mkewe alikuwa akichelewa kurudi nyumbani bila sababu za kueleweka, na alipokuwa akimuuliza kisingizio kikubwa kilikuwa ni ubize wa kazi.<br />
<br />
Siku nyingine alikuwa akirudi nyumbani ananukia pombe, hali iliyotoa ishara kuwa tayari mwenzake anamsaliti. Shughuli zote za kumlea mtoto zikabaki kwa Deo na msichana wa kazi aliyetafutwa kwa lazima baada ya kuona Levina ameanza kubadilika. Ilifika mahali hata suala la kufurahishana faragha likaanza kupungua taratibu.<br />
<br />
“Najua umenisaidia sana maishani Levina, Bila wewe nisingekuwa hapa nilipo leo, lakini kaa ukitambua kuwa mabadiliko yako ya tabia unayonionesha kwa sasa yanauumiza sana mtima wangu.<br />
<br />
“Kama kuna kosa nililokuudhi niambie na naahidi nitajirekebisha kwani bado nakuhitaji Levina wangu.” Uzalendo ulishaanza kumshinda Deo, ikafika mahali akawa anamwaga machozi mbele ya mkewe akimsihi ajirudi kama alivyokuwa hapo mwanzo.<br />
<br />
Jibu la Levina siku zote lilikuwa ni kwamba anampenda Deo na kamwe hawezi kumsaliti, lakini kumbe nyuma ya pazia alikuwa akimfanyia mambo ya kusikitisha sana.<br />
<br />
Usiku mmoja, Deo akiwa na mwanae mdogo Precious sebuleni, mkewe alichelewa kurudi, na hata aliporudi saa tano usiku alikuwa akipepesuka na kunuka pombe. Alipoingia ndani, aliweka simu yake mezani na kupitiliza bafuni kwenda kuoga.<br />
<br />
Akiwa bafuni, ujumbe mfupi wa simu uliingia kwenye simu yake, Deo akaiwahi na kuichukua kutaka kujua ni nani aliyemtumia meseji mkewe usiku wote ule.<br />
<br />
Alipoifungua na kuisoma, hakuamini macho yake…akarudia kuisoma tena… akajikuta mwili wote ukiishiwa nguvu. Wakati anaisoma kwa mara ya tatu, mkewe akawa anatoka bafuni. Macho yao yakagongana.</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965d17a5828788606"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965d17a5828788606"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965d17a5828788606"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965d17a5828788606"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965d17a5828788606"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965d17a5828788606"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965d17a5828788606"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965c98d7e45827485">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE.26.<br />
<br />
Baada ya Deo kufukuzwa nyumbani kwa akina mzee Massamu Magomeni, ameamua kwenda kuanza maisha mapya katika gesti moja iliyopo Manzese Tip Top. Levina amewasiliana naye na amefika hadi kwenye gesti hiyo ambapo ameonesha nia yake ya kumsaidia.<br />
<br />
Tayari ameshampangia nyumba yenye vyumba viwili, Sinza. Deo amesoma elimu ya sekondari kwa miaka miwili na baada ya<span class="text_exposed_show"> hapo akasomea masomo ya Uhasibu katika chuo kimoja jijini Dar.<br />
<br />
Akiwa anaendelea na masomo, Levina anamweleza Deo nia yake ya kuzaa mtoto, lakini jambo hilo Deo anapingana nalo. Je, nini kitatokea? Endelea...<br />
<br />
SUALA la kuzaa na Levina lilikataa kabisa kupenya kwenye ubongo wa Deo, alijaribu kuvuta picha ya miaka mitatu ijayo akaona hatari kubwa kuzaa na Levina. Hakujua ilikuwaje, lakini akahisi kwamba Levina angeweza kubadilika na kumsababishia jakamoyo la mapenzi moyoni mwake.<br />
<br />
Aliona kuzaa naye, ingekuwa tiketi ya kuingia kwenye matatizo, lakini pia aliona wazi vita iliyokuwa mbele yake ikimuhusisha yeye na wazazi wa Levina. Hilo hakutaka kabisa litokee.<br />
<br />
“Levina haiwezekani, kama nilivyokuambia siwezi kuzaa na wewe!”<br />
“Kwanini unanifikiria vibaya lakini?”<br />
“Vipi?”<br />
<br />
“Kwamba nitakusaliti?”<br />
“Ni kweli, lazima baadaye utanigeuka na kuninyanyasa.”<br />
“Kwanini unahisi hivyo?”<br />
<br />
“Lakini kwani ni vibaya kukueleza hisia zangu? Nilichokifanya ni kukueleza nilichokuwa nahisi kichwani mwangu. Sijui kwanini sina amani na wewe, nahisi matatizo tupu kuendelea na wewe katika uhusiano huu tena na kuzaa.”<br />
<br />
“Mh! Siamini kama huniamini kwa kiwango hicho?”<br />
“Siyo hivyo Levina, nawajua wanawake mimi, tena wale wanaotoka kwenye familia za kitajiri.”<br />
“Unajua nini sasa?”<br />
<br />
“Sikiliza nikuambie Levina, wewe mpaka sasa hivi unaishi kwenu na unatambua kabisa kwamba nilifukuzwa kwenu baada ya kugundulika nina uhusiano na wewe, unadhani baba yako akigundua kwamba una mimba yangu itakuwaje?”<br />
<br />
“Lakini atakayekuwa amebeba mimba ni mimi au yeye?”<br />
“Ni wewe ndiyo, lakini atakayepata matatizo ni mimi!”<br />
“Basi tuachane na hayo mpenzi wangu, tatizo si kuhusu mtoto tu siyo?”<br />
“Ndivyo!”<br />
<br />
“Basi huo mjadala tuukatishe kwasasa tusiharibu penzi letu kwa jambo dogo, mambo mengine tutajua baadaye!”<br />
“Sawa.”<br />
“Enhee lini sasa utakuja kulala kwangu?”<br />
“Kwahiyo ndiyo unanifukuza au?”<br />
<br />
“Sina maana hiyo, muda utakaoondoka, si vibaya lakini hata nikikuambia muda huu. Hapa ni kwako mama.”<br />
“Ahsante sana mpenzi kwa maneno yako matamu!”<br />
“Nakupenda sana Levina wangu!”<br />
<br />
“Nakupenda pia Deo!”<br />
“Lakini bado hujaniambia ni lini utakuja kulala kabisa hapa?”<br />
“Mh! Mpaka nipange safari ya uongo...acha nifikirie kwanza nitakujulisha mpenzi wangu!”<br />
<br />
“Sawa mama!”<br />
Waliendelea na mazungumzo hadi saa mbili za usiku, ndipo Levina alipoondoka Sinza kuelekea nyumbani kwao Magomeni.<br />
<br />
***<br />
Usiku mzima Deo aliendelea kufikiria kuhusu Levina, alishindwa kuelewa ni kwanini mawazo yake yalienda mbali kiasi kile. Hakujua ni kwanini aliwaza kusalitiwa na mwanamke ambaye amekuwa chachu ya mafanikio yake.<br />
Hata hivyo, alijitahidi kuubembeleza usingizi hadi alipofanikiwa kulala.<br />
<br />
***<br />
Levina aliendelea kuwa msada mkubwa sana katika maisha ya Deo. Alimsaidia kwa kila kitu kwa siri, alifanya uhusiano wao kuwa siri kubwa, kwani wazazi wake wasingekubali awe katika uhusiano naye wakati hali ya maisha yake ikiwa chini sana.<br />
<br />
Alihakikisha anaendelea kufanya kazi kwa bidii, mtaji wake haushuki na badala yake faida inazidi kuongezeka. Jambo hilo lilizidi kuwafurahisha wazazi wake, kwani alionekana msichana mwenye bidii kubwa katika kazi zake.<br />
<br />
Siku moja aliamua kuvunja ukimya kwa kuamua kumshirikisha mama yake kuhusu uhusiano wake na Deo. Ilikuwa kazi ngumu sana lakini ilikuwa lazima amweleza ukweli ili kujua kama mama yake angemuunga mkono. Ilikuwa Jumamosi, ambapo mzee Massamu alikuwa kazini.<br />
<br />
“Mama kuna kitu nataka kukuambia muda mrefu sana lakini nashindwa, ila naona leo ni muda muafaka wa kukuambia.”<br />
“Ni nini mwanangu?”<br />
“Mama nina mpenzi ambaye nataka kumtambulisha hapa nyumbani.”<br />
“Umeanza lini tena hayo mambo mwanangu?”<br />
<br />
“Lakini muda umefika mama, umri wangu unaniruhusu!”<br />
“Sawa, ni nani huyo mwanaume mwenyewe!”<br />
“Unamaanisha nini?”<br />
“Ni wa hapa mtaani kwetu?”<br />
“Hapana!”<br />
<br />
“Ni wa wapi?”<br />
“Kwasasa anaishi Sinza.”<br />
“Sawa, kama ni kijana mwenye heshima zake na mmependana, mwambie atume ujumbe wa wazee tutawasikiliza, lakini chunga asije kuwa ni mzururaji asiye na mpango mzuri na maisha yako ya baadaye!”<br />
<br />
“Hapana si mzururaji, lakini sidhani kama mtamkubali!”<br />
“Kwanini?”<br />
“Ni Deo mama!”<br />
“Deo?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Deo gani?”<br />
“Yule aliyekuwa akifanya kazi hapa nyumbani?”<br />
“Wewe una kichaa kabisa, baba yako hawezi kukubaliana na hilo jambo, yaani unataka kuolewa na houseboy?”<br />
“Hapana si houseboy tena, sasa anamalizia masomo yake ya Uhasibu!”<br />
“Lini alianza kusoma?”<br />
<br />
“Tangu kipindi kile, nilikutana naye akasema kwamba kuna mfadhili amejitolea kumsaidia, ndiyo huyo anayemlipia mpaka sasa hivi!”<br />
“Kwa ninavyomjua baba yako, sijui kama atakubaliana na wewe.”<br />
“Ndiyo maana nimeoomba msaada wako mama, nampenda sana Deo!”<br />
<br />
“Nitajaribu kuongea naye, ingawa sina uhakika kabisa kama atakubaliana na jambo hili!”<br />
“Nisaidie mama!”<br />
“Nitajaribu!”<br />
<br />
Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia simulizi hii ya kusisimua</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965c98d7e45827485"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965c98d7e45827485"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965c98d7e45827485"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965c98d7e45827485"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965c98d7e45827485"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965c98d7e45827485"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965c98d7e45827485"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE.27<br />
<br />
Penzi la Levina na Deo linazidi kunoga kiasi cha Levina kuamua kumweleza mama yake na kumwomba amuweke sawa baba yake mzee Massamu. Inakuwa vigumu mama yake kumwelewa, lakini anaahidi kujitahidi kuzungumza naye, mtihani ambao ni mgumu zaidi. Je, atakubaliwa? Endelea...<br />
<br />
JIONI baada ya chakula cha usiku Levina aliingia chumbani kwake kulala na kuwaacha waza<span class="text_exposed_show">zi wake sebuleni wakiendelea kuangalia runinga. Mama Levina alionekana kuwa na jambo alilotaka kumwambia mumewe lakini alikuwa anasita.<br />
<br />
Mzee Massamu aliweza kugundua hilo kupitia macho yake. Kila kitu kilionekana wazi kwamba ana jambo alilotaka kusema, lakini alikuwa akisita sana.<br />
“Mama Levina mke wangu, uko sawa?”<br />
<br />
“Kwanini?”<br />
“Nahisi kama kuna kitu unataka kuniambia!”<br />
“Ni kweli!”<br />
“Sema basi, kwanini unakaa na jambo wakati wa kuniambia nipo hapa?”<br />
<br />
“Ni kuhusu binti yetu Levina.”<br />
“Amefanyaje tena?”<br />
“Mh! Eti amepata mchumba!”<br />
“Amepata mchumba?”<br />
<br />
“Ndiyo!”<br />
“Sasa si amlete hapa nyumbani tuzungumze naye?”<br />
“Tatizo siyo hilo!”<br />
“Bali?”<br />
<br />
“Tatizo ni huyo mtu mwenyewe.”<br />
“Kwani ana nini? Unafahamu?”<br />
“Ndiyo namfahamu... hata wewe unamfahamu!”<br />
<br />
“Kwa hiyo unataka kuniambia anaishi hapa hapa mtaani kwetu?”<br />
“Sina maana hiyo... namaanisha Deo!”<br />
“Deo?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Yule kijana aliyekuwa akifanya kazi hapa nikamtimua?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Bado wanaendelea na upumbavu wao? Hivi kwanini mwanao anataka kuniletea balaa katika familia yangu? Yaani yeye ni wa kuolewa na ‘Shamba Boy’, mpuuzi asiye na mbele wala nyuma?”<br />
<br />
“Lakini mwenyewe anasema eti alivyoondoka hapa alipata mfadhili, akamsomesha na sasa anamalizia Stashahada yake ya Uhasibu na Biashara!”<br />
<br />
“Hata kama, mimi sitaki kumsikia kabisa yule kijana. Kwanza hana adabu, hawezi kufanya upumbavu ndani ya nyumba yangu.<br />
Kwanza nenda kamwite Levina haraka sana!”<br />
<br />
Mama Levina akasimama na kwenda chumbani kwa Levina, akamgongea na muda mfupi baadaye Levina alitoka.<br />
“Baba yako anakuita!”<br />
“Nakuja mama!”<br />
<br />
Levina akatoka na kwenda sebuleni, alipokutana na uso wenye hasira kali wa baba yake akaanza kutetemeka. Kabla hata hajafungua kinywa chake kuongea chochote, tayari alikuwa na majibu kwamba ombi lake la kuolewa na Deo lilikuwa limekataliwa.<br />
<br />
“Levina binti yangu, kwanini unataka kuniletea nuksi katika familia yangu? Kwanini unataka kuniabisha? Kwanini lakini?!” Mzee Massamu akauliza mfululizo.<br />
“Kivipi baba?”<br />
<br />
“Sitaki kuvuta maneno mengi, lakini ninachotaka kukuambia ni kwamba sitaki kusikia unaendelea na yule mpuuzi wako. Kama kweli mimi ni baba yako basi fahamu kwamba sitaki uwe na uhusiano na yule Deo, nimemaliza!”<br />
<br />
“Lakini baba...” akasema Levina.<br />
“Hakuna cha lakini... nenda kalale ‘please’!”<br />
Levina hakuweza kubishana na baba yake, mara moja akainuka na kuelekea chumbani kwake. Baba yake alikuwa amekasirika sana na hakutaka kuendelea kumuudhi.<br />
<br />
Alikuwa na maumivu makali sana moyoni mwake, kwani Deo alikuwa mwanaume ambaye alimpenda sana kwa moyo wake wote na hakutegemea kuolewa na mwanaume mwingine yeyote zaidi yake.<br />
<br />
Aliingia ndani kwake kwa unyonge huku mawazo tele kichwani mwake yakimuandama. Muda mfupi baada ya yeye kuingia chumbani kwake, wazazi wake nao wakainuka na kuingia chumbani kwao.<br />
<br />
***<br />
Mzee Massamu hakufurahishwa kabisa na ujumbe wa mwanaye, hakutarajia kama bado angekuwa anaendelea na uhusiano na Deo, kijana ambaye kwake hakuwa na thamani kabisa.<br />
<br />
“Mke wangu, zungumza na mwanao. Wewe ni mwanamke mwenzake kwa hiyo ni rahisi kukuelewa. Kifupi sitaki kusikia habari za huyo Deo!”<br />
<br />
“Nimekuelewa mume wangu, nitajitahidi kuhakikisha anaelewa.”<br />
“Najua lipo ndani ya uwezo wako, naomba ufanye hivyo.”<br />
“Sawa.”<br />
<br />
***<br />
Levina alipuuza maamuzi ya wazazi wake, pamoja na kwamba mama yake aliendelea kumsisitiza akatishe uhusiano wake na Deo, lakini alikaidi. Aliwahakikishia kwamba ameachana naye, lakini ukweli ni kwamba bado alikuwa na Deo.<br />
<br />
Alikuwa akienda nyumbani kwake mara kwa mara na mwisho wa wiki alikuwa akitoka naye kwenda sehemu mbalimbali za burudani. Hata hivyo siri ya kwamba wazazi wake hawakutaka aendelee na uhusiano naye, iliendelea kuwa yake peke yake. Hakutaka kabisa kumshirikisha Deo.<br />
<br />
Deo hakujua chochote kinachoendelea, lakini pia hakujua kama Levina alizungumza na wazazi wake kuhusu yeye. Aliendelea na masomo vizuri mpaka alipohitimu na kupata Stashahada yake. Hapo sasa ndipo alipotakiwa kutafuta kazi.<br />
<br />
“Usihangaike mpenzi wangu, nitakutafutia. Kuna rafiki yangu mmoja anakaa Mbezi, hebu twende jioni tukazungumze naye, tuone uwezekano wa kupata kazi kwenye kampuni ya baba yake ambayo naye pia anafanya kazi hapo, tena ana cheo!”<br />
“Sawa mpenzi.”<br />
<br />
Kama walivyokubaliana, jioni wakaenda Mbezi Beach nyumbani kwa huyo rafiki yake. Walipofika walipokelewa vizuri sana. Wakaamua kukaa nje kwenye bustani nzuri ya maua.<br />
“Karibuni!”<br />
<br />
“Ahsante sana!”<br />
“Deo, kutana na rafiki yangu anaitwa Cleopatra. Nimesoma naye kunzia ‘O- Level’ hadi ‘Advance’, tumeshibana sana!” alisema Levina huku akimwangalia Cleopatra aliyekuwa akicheka.<br />
<br />
“Cleopatra huyu hapa ni boyfriend wangu, anaitwa Deogratius lakini waweza kumuita Deo. Ndiyo huyu niliyekuwa nakuambia kuhusu ile ishu, amemaliza juzi tu, lakini kichwa chake ni mashine, kama akipata kazi kwenye kampuni yenu ataonyesha maajabu!”<br />
<br />
“Nice to meet you Deo!” (Nimefurahi kukutana na wewe Deo) Akasema Clepatra wakipeana mikono.<br />
“Me too!” (Hata mimi pia) Akajibu Deo akimwangalia kwa aibu.<br />
<br />
Cleopatra akahisi kitu cha ajabu sana mwilini mwake, alihisi kama anaungua na moto mkali wa mahaba. Ghafla alijikuta akiwa mnyonge, Deo alimvutia sana.<br />
<br />
Thamani ya urafiki wao haikuwa na maana sana, mawazo mapya yakauvamia ubongo wake.<br />
“No! Lazima nimpate huyu kijana...tena ataanza kazi wiki hii, nitampanga kwenye kitengo changu, hapindui huyu...” akawaza akiendelea kuung’ang’ania mkono wake.<br />
<br />
“Vipi shosti, mbona salamu imekuwa ya muda mrefu hivyo? Shemeji yako huyu ujue...” akasema Levina kwa utani, lakini moyoni alikuwa anamaanisha.<br />
“Mwanamke kwa wivu wewe!!!” Akasema Cleopatra akimwachia mkono Deo.<br />
<br />
Je, nini kitatokea katika ligi hii ya mapenzi? Usikose kufuatilia</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216">USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE.28.<br />
<br />
Baada ya kufanikiwa kusoma na kumaliza masomo yake ya Stashahada ya Uhasibu na Biashara, Deo anasaidiwa na mpenzi wake, Levina kutafuta kazi. Harakati hizo zinawakutanisha na Cleopatra, rafiki wa siku nyingi wa Levina ambaye ni bosi kwenye kampuni ya baba yake.<br />
<br />
Katika hali isiyo ya kawaida, Cleopatra anajikuta akivutiwa mno kimapenzi na Deo, na anajiweke<span class="text_exposed_show">a nadhiri ya kumpata. Je, nini kitaendelea?<br />
<br />
Vipi shosti, mbona salamu imekuwa ya muda mrefu hivyo? Shemeji yako huyu ujue…” akasema Levina kwa utani, lakini moyoni alikuwa akimaanisha. Mwanamke kwa wivu wewe!” Akasema Cleopatra akimwachia mkono Deo.<br />
<br />
Ukweli ambao Cleopatra alishindwa kuuficha mbele ya shoga yake wa siku nyingi Levina, ni kwamba alitokea kumzimikia ghafla Deo, na sasa alitamani kumpindua na kulionja penzi la Deo. Moyoni alijiwekea nadhiri kuwa lazima atafanya chochote kinachowezekana ilimradi ampate Deo.<br />
<br />
Mazungumzo yaliendelea wakiwa kwenye bustani ya maua, nyumbani kwa akina Cleopatra, Mbezi Beach na kwa moyo mkunjufu akakubali kumpatia Deo kazi katika kampuni ya baba yake ambayo yeye ndiyo alikuwa bosi.<br />
<br />
“Shaka ondoa, kazi umepata Deo, Levina ni mtu wangu tangu kitambo, siwezi kumuangusha,”<br />
“Ahsante sana!” Alijibu Deo kwa furaha akiamini sasa maisha yake yatabadilika.<br />
<br />
Mazungumzo ya kawaida yakawa yanaendelea kati ya Levina na Cleopatra. Baada ya kukaa pamoja na kuzungumza mengi, hatimaye muda wa Deo na Levina kuondoka ulifika.<br />
<br />
Kama ilivyokuwa wakati wa kusalimiana mara ya kwanza, Cleopatra alijikuta akiganda kwa Deo, hali iliyozidi kumtia hofu Levina.<br />
“Hii ni ‘business card’ yangu, chukua tafadhali,” aliongea Cleopatra wakati akimkabidhi Deo kadi yake ya mawasiliano.<br />
<br />
“Namba yako nitachukua kwa Levina kwa ajili ya kukutaarifu siku ya kuja kuripoti kazini.”<br />
“Sawa! Nashukuru sana,” alijibu Deo huku akionesha wazi jinsi alivyofurahi kupata kazi.<br />
<br />
“Hee shosti, utanikwaza sasa hivi! Kuagana tu ndiyo mpaka umgande shemejiyo kama ruba! hebu mwachie huko, na wewe ndiyo utakuwa mlinzi wake kazini, ole wako nisikie unamtaka,” alisema kwa utani Levina lakini akionekana kumaanisha kile alichokisema.<br />
<br />
Cleopatra alimuachia mkono Deo na wakaanza kuondoka. Akilini mwake, Deo alishahisi kuwa amezimikiwa na bosi wake mtarajiwa, lakini kwa jinsi alivyokuwa anampenda Levina, alijiapiza kuwa kamwe hawezi kumsaliti.<br />
<br />
“Deo mpenzi, unaenda kuanza kazi, na sasa kila mtu anakusifia kuwa wewe ni ‘handsome’, tafadhali usije ukanisaliti mpenzi wangu,” alilalama Levina huku akimkumbatia Deo kimahaba.<br />
“Siwezi honey, amini nakwambia.” <br />
<br />
*** <br />
Siku chache baadaye Deo aliitwa kwa ajili ya kufanyiwa usaili (Interview) ambapo alikidhi vigezo vyote. Kesho yake akaanza kazi akiwa kama mhasibu kwenye kampuni ya baba yake Cleopatra ya Planet-link Enterprises, ambayo Cleopatra ndiyo alikuwa msimamizi wa shughuli zote (bosi).<br />
<br />
Kama alivyokuwa amejiapiza tangu siku ya kwanza anakutana na Deo, alimuweka kwenye kitengo cha uhasibu, hali iliyowafanya wawili hao kuwa karibu muda mwingi wawapo kazini.<br />
<br />
“Nitakufundisha kazi mpaka utakapozoea vizuri, usisite kuniuliza chochote kinachokusumbua na nitakupa msaada unaouhitaji,” alisema Cleopatra wakati akimkaribisha Deo ofisini.<br />
<br />
Tofauti na alivyokuwa mwanzo, Deo wa sasa hakuwa tena yule ‘shamba boy’. Alikuwa akionekana ‘smart’ muda wote, huku ‘u-handsome’ aliojaaliwa na Mungu ukichanua na kuwachanganya wanawake wengi, Cleopatra akiwa mmoja wapo. <br />
<br />
Kwa kadri siku zilivyokuwa zinazidi kusonga, Cleopatra alizidisha vituko kwa Deo, akimtega kwa kila namna ili anase kwenye himaya yake.<br />
“Leo naomba tutoke wote nikakupe ‘lunch’!” Cleopatra alimwambia Deo.<br />
<br />
“Sawa, hakuna shida! Ngoja nimalizie kazi kidogo ‘then’ tutatoka.” <br />
Wakiwa kupata ‘lunch’, Cleopatra alikuwa akimchombeza Deo kwa maneno ya uchokozi huku akimsisitiza kuwa asije kumwambia Levina kuwa wametoka pamoja.<br />
<br />
“Namjua shoga yangu, Levina. Ana wivu sana akimpenda mtu, kwa hiyo tafadhali usije kumwambia kitu.”<br />
“Lakini mi naona hakuna tatizo lolote akijua, si tumetoka ‘lunch’ ya kawaida, hata mwenyewe angekuwepo tungejumuika pamoja.”<br />
<br />
“Ni kweli Deo, lakini sitaki kukorofishana na Levina.”<br />
“Poa nimekuelewa!”<br />
“Nikwambie kitu Deo, ‘You are soo handsome!’ (Wewe ni mzuri sana).<br />
Deo hakujibu kitu zaidi ya kutabasamu kwa haya, hakuzoea kusifiwa maishani mwake.<br />
<br />
Baada ya kumaliza kupata chakula cha mchana, walirudi kazini na kuendelea na shughuli za kawaida, kila mtu akiwajibika sehemu yake.<br />
Siku zilizidi kusonga ambapo Deo na Cleopatra wakazidi kuwa jirani.<br />
Ilifika mahali ikawa bila kumuona Deo, Cleopatra hawezi kwenda kupata chakula cha mchana peke yake. Akaanza mazoea ya kumpelekea zawadi ndogondogo. Urafiki wao ukazidi kushamiri.<br />
“Deo!”<br />
<br />
“Naam Bosi!”<br />
Aah! Si nilishakukataza kuniita bosi? Niite jina langu bwana.”<br />
“Im sorry, naam Cleopatra”<br />
“Leo ukimaliza kazi jioni una ratiba gani?” <br />
“Nitamsindikiza Levina kwa shangazi yake Mabibo.”<br />
<br />
“Basi kama leo utakuwa taiti, naomba wikiendi hii nikutoe ‘out’.”<br />
“Labda nikamuombe kwanza ruhusa Levina, akikubali sawa.”<br />
“Acha mambo ya kitoto Deo, we unafikiri Levina atakuruhusu kutoka na mimi? Halafu si nilishakwambia mambo yangu na wewe usimwambie? Usiniangushe bwana.”<br />
<br />
“Ok basi poa, si Jumamosi eti eeh!”<br />
“Eeh! Nataka nikakupe zawadi nzuri niliyokutunzia kwa siku nyingi,” alijibu Cleopatra kwa kudeka huku akimtazama Deo kwa jicho la huba.”<br />
<br />
Hatimaye Jumamosi ikafika, siku ya miadi ambayo Cleopatra na Deo walikubaliana kutoka ‘out’ pamoja.<br />
“Huwa unatumia kinywaji gani? Namaanisha bia gani?”<br />
“Pombe huwa sinywi, labda soda tu.”<br />
<br />
“Leo kwa kuwa uko na mimi , naomba unywe japo kidogo uchangamshe akili,” alisema Cleopatra huku akiendesha gari lake kuelekea Kunduchi Wet and Wild Hotel. Mawazoni mwake, alikuwa akipanga mengine, na aliamini ile ndiyo siku yake ya kumfaidi Deo.<br />
<br />
Je, nini kitaendelea</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE.29<br />
<br />
Siku chache baada ya Levina kumtambulisha mpenzi wake Deo kwa Cleopatra na kufanikisha kumpatia kazi kwenye ofisi ya baba yake, dhambi ya usaliti inachukua nafasi yake.<br />
<br />
Cleopatra anatumia ushawishi wa pesa na madaraka yake kumpata Deo kirahisi na kufanikiwa kujivinjari naye. Levina anahisi kitu ingawa anakosa ushahidi. Wazazi wake bado wanamuandama wakimta<span class="text_exposed_show">ka aachane kabisa na Deo kwa kuwa hana hadhi ya kumuoa.<br />
Je, nini kitandelea? Shuka nayo…<br />
<br />
“Huwa unatumia kinywaji gani? Namaanisha bia gani?”<br />
“Pombe huwa sinywi, labda soda tu.”<br />
<br />
“Leo kwa kuwa uko na mimi , naomba unywe japo kidogo uchangamshe akili,” alisema Cleopatra huku akiendesha gari lake kuelekea Kunduchi Wet and Wild Hotel. Mawazoni mwake, alikuwa akipanga mengine, na aliamini ile ndiyo siku yake ya kumfaidi Deo.<br />
<br />
“Twende tukakae kule pembeni,” alisema Cleopatra kwa sauti iliyojaa mbwembwe za kimalavidavi. Akamshika mkono Deo na kumuelekeza mahali pa kukaa.<br />
<br />
Walienda kukaa kwenye kona moja iliyokuwa imejificha, wakaanza kupiga stori huku Cleopatra akitumia uwezo wake wote kumtega Deo.<br />
“Tuongeze raundi nyingine,” alisema Cleopatra huku akimalizia chupa ya kwanza ya kilevi alichozoea kukitumia.<br />
<br />
Japokuwa Deo hakuwa na kawaida ya kunywa pombe, kutokana na ushawishi wa Cleopatra alijikuta akipiga ‘moja moja’ kukwepa kuonekana dhaifu mbele ya mrembo yule. Kadri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele, ndivyo pombe zilivyokuwa zinawakolea vichwani mwao. Wakaacha kuoneana aibu kama ilivyokuwa wakati wanaingia eneo hilo.<br />
<br />
“Deo! Naomba nikwambie kitu.”<br />
“Niambie Cleopatra, nakusikiliza.”<br />
“Naomba usinifikirie vibaya kwa hili nitakalokueleza, nimevumilia nimeshindwa mwenzio.”<br />
<br />
“Wala usijali. Jisikie huru kuzungumza chochote.”<br />
“Deo, nakupenda Deo. Naomba uwe wangu mahabuba.”<br />
“Lakini Cleopatra, si unajua kuwa mi niko na rafiki yako Levina na ndiye aliyenikutanisha na wewe?”<br />
<br />
“Najua sana Deo, lakini Levina ana nafasi yake, na mimi naomba unipe nafasi yangu.”<br />
“Hapana Cleopatra, sipendi kumkosea Levina, amenisaidia vingi sana.”<br />
“Nikubali Deo, itakuwa siri yetu, hakuna atakayejua.”<br />
<br />
Licha ya Deo kujivunga sana, Cleopatra aliendelea kumganda kama ruba akimtaka akubali ombi lake la kuwa wapenzi. Kwa kuwa tayari kilevi kilikuwa kimeanza kukolea ndani ya vichwa vyao, Cleopatra hakuona aibu tena na hakutaka kulaza damu, akajisogeza mwilini mwa Deo na kujilaza kifuani.<br />
<br />
Uvumilivu ulianza kumshinda Deo, akawa haeleweki anachokiongea kama amemkubali Cleopatra au la.<br />
“Tuondoke dear, mi nimechoka nataka kwenda kulala.”<br />
“Si utanifikisha nyumbani kwanza ndiyo wewe uelekee kwako.”<br />
“Hapana Deo, mwenzio naogopa peke yangu. Nifikishe kwanza nyumbani kwangu.”<br />
<br />
Cleopatra na Deo waliondoka eneo lile wakiwa wamekumbatiana, wakaongozana hadi kwenye gari walilokuja nalo. Deo akakaa pembeni huku Cleopatra akiwa nyuma ya usukani.<br />
<br />
Breki ya kwanza ilikuwa nyumbani kwa Cleopatra. Walipofika tu, Cleopatra alishuka haraka haraka na kumshika Deo mkono, akawa anamvutia ndani kama kondoo anayepelekwa machinjioni.<br />
<br />
Deo hakuwa na ujanja tena, yeye mwenyewe alishadatishwa na yote yaliyokuwa yanafanywa na Cleopatra.<br />
Akaamua kujiachia. Dakika chache baadaye, walikuwa juu ya uwanja mkubwa wa fundi seremala, chumbani kwa Cleopatra, wakiwa na suti za kulalia.<br />
<br />
***<br />
Levina alikuwa chumbani kwake, akifanya usafi wa kawaida. Pingamizi la wazazi wake juu ya kumpenda Deo, lilimfanya muda mwingi awe anajifungia chumbani peke yake.<br />
<br />
Mawazo na fikra zake zote zilikuwa juu ya Deo, alimpenda kiukweli na moyoni alijiwekea nadhiri kuwa lazima aolewe naye.<br />
“Nimemkumbuka Deo wangu, ngoja nimcheki hewani,” alijisemea Levina huku akijilaza kitandani na kuchukua simu yake ya mkononi.<br />
<br />
Simu ya Deo ilikuwa ikiita bila kupokelewa, hali iliyomtia hofu Levina. Alirudia mara ya pili lakini hali ikawa ni ile ile. Aliendelea kujaribu mara kadhaa lakini haikupokelewa.<br />
<br />
“Amepatwa na nini Deo wangu? Siyo kawaida yake.”<br />
Aliongea Levina huku akitafuta viatu vyake kutoka chini ya kitanda. Alishindwa kuvumilia, akahisi labda Deo amepatwa na tatizo hivyo akaamua kumfuata nyumbani kwake. Alitoka nyumbani kwao bila kuaga, akanyata hadi mlango wa nje na kuwaacha baba na mama yake wamekaa sebuleni.<br />
<br />
Alipofika kwa Deo, alikutana na ukimya wa ajabu ambao uliashiria kuwa Deo hakuwemo ndani, hali iliyozidi kumtia hofu.<br />
“Atakuwa wapi muda huu?” Alijiuliza Levina bila kupata majibu.<br />
<br />
Alijaribu tena kupiga namba yake, lakini safari hii simu ya Deo ikawa haipatikani kabisa. Akahisi labda huenda amezidiwa na kazi ofisini kwao ndiyo maana amechelewa kurudi. Akaamua kumpigia simu shoga yake Cleopatra ili kujua kulikoni.<br />
<br />
“Namba ya mteja unayempigia, haipatikani kwa sasa, jaribu tena baadaye,” majibu yale kutoka kwenye simu yake ya mkononi yalimmaliza nguvu kabisa.<br />
Akilini mwake kengele ya hatari ilishaanza kulia, akahisi huenda shoga yake anamzunguka kwa kutoka na Deo kwani tangu siku ya kwanza wakati anamtambulisha kwake, Cleopatra alionekana kumzimikia.<br />
<br />
Hakutaka kuamini kuwa muda huo inawezekana wakawa pamoja kutokana na jinsi alivyokuwa anamuamini Deo. Kitu pekee alichoona kinafaa ilikuwa ni kurudi nyumbani kwao kupumzika kwani hakuaga wakati anaondoka, jambo ambalo alijua litawaudhi wazazi wake.<br />
<br />
Moyoni alikuwa anaumia sana kumkosa Deo, kipenzi cha nafsi yake usiku ule, akawa hapati majibu ni wapi aliko, yuko na nani na anafanya nini. Wivu wa mapenzi uliwaka mtimani mwake.<br />
<br />
“Ulikuwa wapi usiku wote huu?” Baba yake Levina, Mzee Msammu alimpokea kwa maswali makali.<br />
<br />
“Na wewe Levina, mpaka nashindwa kukutetea kwa baba yako. Ulikuwa wapi saa hizi? Au ndiyo huyo ‘shamba boy’ wako anakuzuzua?” Alidakia mama yake. Levina hakuwa na jibu, akainamisha kichwa chake chini.<br />
<br />
Akilini hakuwa anajali alivyowaudhi wazazi wake kwa kuondoka bila kuaga, ila alikuwa akifikiria kwa nini Deo hayuko nyumbani kwake usiku kama ule, huku simu yake ikiwa inaita bila kupokelewa na baadaye ikawa haipatikani.<br />
”Si tunaongea na wewe? Mbona hujibu? Kiburi siyo?”<br />
<br />
***<br />
Deo alishtuka kutoka kwenye usingizi mzito na kujikuta yuko mikononi mwa mwanamke tofauti na yule aliyemzoea. <br />
“Hee! Imekuwaje tena?” Alijiuliza Deo huku akiitazama saa ndogo iliyokuwa pembeni ya kitanda. Ilikuwa ni tayari saa sita za usiku.”<br />
<br />
“Oooh! Shit.” Alijisemea baada ya kugundua kuwa kumbe alikuwa amelala na Cleopatra kitanda kimoja, tena wote wakiwa kama walivyozaliwa. Hakutaka kuamini kama amemsaliti kirahisi namna ile mpenzi wake aliyemtoa mbali, Levina.</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><span class="hasCaption">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE.30.<br />
<br />
Bila kutarajia Deo amejikuta akitoka na bosi wake Cleopatra. Haikuwa dhamira yake, ni baada ya kuleweshwa na mwanamke huyo.<br />
<br />
Siku nyingine, Deo akiwa ametoka na Levina, simu yake inaita, alipoangalia jina la mpigaji akaona ni Cleopatra, akaogopa kupokea.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Kitendo hicho kikasababisha Levina amnyang’anye ile simu. Je, nini kitaendelea?<br />
Sasa endelea...<br />
<br />
LEVINA alikuwa amevimba kwa hasira, alianza kuhisi mchezo mbaya ukiendelea kati ya Cleopatra na Deo wake. Aliiangalia ile simu mpaka ikakatika yenyewe.<br />
<br />
“Hebu niambie ukweli, anataka nini kwako huyu mwanamke?” Levina akamwuliza Deo.<br />
<br />
“Hapo utakuwa unanionea mpenzi wangu, unadhani ni rahisi kugundua kitu kilichopo ndani ya kichwa cha mtu mwingine? Sijui ana shida gani, lakini itakuwa ni mambo ya ofisini!”<br />
“Ofisini mpaka Jumapili?”<br />
<br />
“Sijajua mpenzi wangu. We’ achana naye bwana...”<br />
“Niachane naye kirahisi-rahisi tu!” Levina akasema kwa hasira na muda huo huo tena simu ikaanza kuita.<br />
<br />
Safari hii Levina akaipokea haraka...<br />
“Cleopatra habari yako?” Sauti yake ilionesha kabisa ilikuwa ya shari.<br />
<br />
“Poa shoga, enheee vipi mzima wewe?”<br />
“Mzima. Vipi tena simu na shemeji yako saa hizi?”<br />
“Kwani vipi Levina? Inamaana hatuaminiani? Nataka kumpa maagizo muhimu ya kesho, maana kuna mahali nitapitia asubuhi, naomba kuzungumza naye!” Cleopatra akasema kwa kujiamini sana.<br />
<br />
“Ok! Ongea naye huyu hapa...” akasema akimpatia simu Deo.<br />
Cleopatra hakuwa na lolote, zaidi ya habari za mapenzi, lakini kwa sababu tayari alishasikia sauti ya Levina, hakutaka matatizo, akajifanya kumuagiza Deo kazi fulani za ofisini.<br />
<br />
Ilikuwa kama kipande kwenye sinema ambacho kilipata wasanii walioweza kuuvaa vyema uhusika.<br />
<br />
Deo aliweza kuzungumza na Cleopatra na kujifanya kweli walikuwa na mazungumzo ya kikazi. Kwa kiasi kikubwa walifanikiwa kumfumba macho Levina, ingawa naye hakuwa na uhakika wa asimilia mia moja.<br />
<br />
Baada ya mazungumzo kukamilika, Levina alionekana hana furaha kabisa, lakini akajitahidi kuilazimisha.<br />
“Kwani mpenzi wangu, bado unamuwaza vibaya Cleopatra?”<br />
<br />
“Hata kama ungekuwa ni wewe ungeweza kama ninavyowaza mimi.”<br />
“Lakini si ulisema Cleopatra ni rafiki yako na mnaaminiana?”<br />
“Ndiyo.”<br />
<br />
“Sasa kwa nini unamfikiria mabaya? Wakati mwingine ukimfikiria mwenzako mabaya, hata kama alikuwa hana mpango wa kufanya kitu kibaya anaweza akafanya.”<br />
<br />
“Lakini mimi ndiyo namjua Cleopatra, naufahamu udhaifu wake na aina ya wanaume anaowapenda!”<br />
<br />
“Ndiyo kusema mimi nachukuliwa tu kama mzigo, yaani sina hisia wala uamuzi wangu peke yangu kama mwanaume? Unadhani anaweza kunikokota tu bila uamuzi wangu mwenyewe?<br />
<br />
“Kwani unanichukuliaje Levina? Au kwa sababu ulinipata kirahisi ndiyo maana unahisi mwanamke yeyote pia anaweza kunipata? Kumbuka mimi nilikupenda kwa mapenzi ya dhati ndiyo maana nipo na wewe muda huu.<br />
<br />
“Sijafurahishwa kabisa na maneno yako, siamini kama kweli hatuamini kwa kiwango cha juu kiasi hicho. Tafadhali sana Levina usinivunjie heshima yangu! Naumia sana moyoni mwangu kwa jinsi unavyonihisi, usivyoniamini!” Deo aliongea maneno hayo kwa uchungu sana.<br />
<br />
Yalikuwa yanatokea kinywani tu, ndani ya moyo wake kulikuwa na kitu kingine kabisa. Deo alikuwa ameshatekwa na Cleopatra.<br />
“Samahani sana mpenzi wangu, sikuwa na nia ya kukuudhi, lakini Cleopatra ndiyo amenipa wasiwasi.”<br />
<br />
“Hata kama...huyo ni Cleopatra. Inamaana mimi huniamini kwa sababu tu Cleopatra anaonekana labda kuwa na nia ya kuninasa?”<br />
“Sijasema hivyo dear...naomba unisamehe mpenzi wangu!”<br />
“Ok! Yaishe!”<br />
<br />
Mahali pale hapakuwa na amani tena kwao, wakaamua kuondoka zao. Safari yao iliishia nyumbani kwa Deo, Sinza, ambapo walikaa hadi usiku wa saa 3, ndipo Levina aliondoka.<br />
<br />
***<br />
“Vipi yule fala alishtuka?” Cleopatra alimwuliza Deo, asubuhi wakiwa ofisini.<br />
“Kama ni sanaa, hapa ndiyo nyumbani. Nimemuweka sawa, hajashtuka kabisa.”<br />
<br />
“Safi sana...sasa Deo mpenzi wangu nimekupandisha mshahara mara mbili ya ule uliokuwa unapata awali. Katika barua yako nimeandika kwamba umepandishwa kutokana na kutimiza vyema majukumu yako ya kazi.<br />
<br />
“Nimeandika hivyo lakini ukweli ni kwamba, nimekuongeza mshahara kwa sababu umeweza kutimiza majukumu yako vyema ya kimapenzi kwangu. Hongera sana...” akasema Cleopatra akimkabidhi Deo barua yake.<br />
<br />
Deo hakuamini!<br />
Akabaki anaikodolea macho ile barua akitamani kuifungua. Akiwa anataka kuifungua, Cleopatra akamzuia.<br />
<br />
“Utafungua ofisini kwako, haraka ya nini mwanaume?”<br />
“Poa mpenzi wangu!”<br />
“Kazi njema.”<br />
“Ok!”<br />
<br />
***<br />
Penzi la siri kati ya Cleopatra na Deo lilizidi kukolea siku hadi siku. Miezi sita imekatika tangu walipofungua ukurasa huo wa mapenzi. Deo amekuwa muda mwingi zaidi na Cleopatra kuliko Levina.<br />
<br />
Mapenzi yake kwa Levina yamefifia kabisa, hachagui majibu ya kumpa na hamjali kabisa. Jambo hilo linamuumiza sana Levina moyo wake lakini Deo hajali.<br />
<br />
Ndani ya moyo wake, anashangaa akimpenda zaidi Cleopatra ambaye alikuwa mkali zaidi faragha kuliko Levina. Alishindwa kuelewa jambo moja; Deo hakumpenda Cleopatra kwa mapenzi ya dhati, fedha na mapenzi ndivyo vilivyomchanganya.<br />
<br />
Usiku huu akiwa amelala, anagutuswa na simu yake ya mkononi iliyokuwa ikiita. Akajivuta taratibu na kuuruhusu mkono wake kuchukua simu iliyokuwa pembeni ya mto na kuangalia jina la mpigaji!<br />
<br />
Ni Cleopatra!<br />
Usiku huu?<br />
Akapokea...<br />
<br />
“Nina jambo moja muhimu sana nataka kukuambia Deo...nimechagua muda huu, maana naamini akili yako itakuwa imetulia na majibu utakayonipa yatakuwa yanatoka moyoni mwako...” Cleopatra alianza kusema mara baada ya Deo kupokea simu.<br />
<br />
“Ni nini mpenzi wangu?” Deo akauliza.<br />
“Naomba UACHANE na LEVINA ili UNIOE mimi, tafadhali sana nakuomba.<br />
<br />
Kumbuka mimi na wewe tunapendana na sioni sababu ya kuendelea kuibana. Nina mali nyingi za wazazi wangu ambazo kwa kutumia akili yako, tutaziendeleza na kuishi maisha mazuri.<br />
<br />
Tafadhali mpenzi usiseme hapana...naomba unikubalie!” Sauti laini ya Cleopatra ilisikika kwenye spika ya simu ya Deo.<br />
<br />
Deo hakuwa na jibu la haraka. Haikuwa rahisi kiasi kile kumjibu Cleopatra! Kila alipokumbuka alipotoka na Levina, alichanganyikiwa na kinywa chake kuwa kizito kufunguka.<br />
<br />
Je, nini kitatokea?</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d93a0454ab5a16698649"><span>USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE.32.v</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d93a0454ab5a16698649"><span> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d93a0454ab5a16698649"><span>Fedh</span><wbr></wbr><span class="word_break"></span>a ndiyo chanzo cha usaliti wa Deo kwa Cleopatra. Hakuwa na mpango wa kumsaliti mpenzi wake Levina, lakini fedha zilizungumza na kununua penzi.<br />
<br />
Cleopatra amekolea kabisa katika penzi la Deo, kiasi cha kuamua kumpigia simu usiku na kumwambia kwamba aachane na Levina ili amuoe yeye!<br />
<br />
Unakuwa mtihani mkubwa sana kwa Deo ambaye anakosa kitu cha kufanya.Je,<span class="text_exposed_show"> nini kitatokea?<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
KWA kiasi kikubwa Deo alijitahidi sana kubana pumzi zake, lakini alishindwa kabisa! Alijikuta akishusha pumzi ndefu sana alizokuwa amezibana kwa muda mrefu.<br />
<br />
Pumzi hizo zilizotoka bila hiyari, ziliweza kumfikia Cleoptara na kuzisikia vyema kupitia simu.<br />
“Deo!” Cleopatra akaita simuni.<br />
“Ndiyo mpenzi wangu.”<br />
<br />
“Mbona hivyo?”<br />
“Vipi?”<br />
“Umehema kwa kasi sana, kwani kuna nini?”<br />
<br />
“Cleopatra jambo ulilonieleza ni zito sana, linahitaji muda wa kutosha kuweza kulifikiria kabla ya kutoa maamuzi. Si jambo jepesi hakika.”<br />
“Kwa nini?”<br />
<br />
“Kumbuka nilipotoka na Levina, amenisaidia mangapi, leo hii kweli nimsaliti? No...roho yangu inakataa kabisa, moyo wangu hautaki!”<br />
“Kwani hunipendi?”<br />
<br />
“Najua nakupenda, lakini tulikubaliana tangu mapema kwamba penzi letu ni la siri na Levina hatakiwi kujua, sasa leo itawezekanaje mimi niwe mumeo?”<br />
<br />
“Acha ujinga Deo, bado unapenda maisha ya shida? Nataka kubadilisha maisha yako. Kwa kuishi na mimi utakuwa mpya. Kama nilivyokuambia, wazazi wangu wana mali nyingi sana, hakuna mrithi pekee zaidi yangu. Kubali kunioa tafadhali!”<br />
<br />
“Natakiwa kufikiria zaidi Cleopatra!”<br />
“Mpaka lini?”<br />
“Asubuhi nikija ofisini nitakuwa na jibu!”<br />
“Kweli?”<br />
<br />
“Niamini.”<br />
“Ok! Usiku mwema, jua nakupenda sana Deo!”<br />
“Nakupenda pia Cleopatra!”<br />
<br />
Deo alibaki na maswali mengi sana baada ya Cleopatra kukata simu. Kichwani alikuwa na mawazo yasiyo na majibu sahihi.<br />
<br />
Alikiri kumpenda, lakini si kwa kumuoa na kuachana moja kwa moja na Levina. Alikumbuka vizuri sana wema aliofanyiwa na mwanamke huyo, kumuacha ilikuwa ni sawa na kumtakia kifo.<br />
<br />
“Nitafanyaje mimi jamani? Lakini mpaka kesho lazima nitakuwa na majibu sahihi juu ya jambo hili...” akajisemea moyoni mwake na kulazimisha usingizi ambao ulikuwa mgumu sana kupatikana.<br />
<br />
***<br />
Simu ya mezani kwake ndiyo iliyomnasua Deo mawazoni, bado alikuwa akiwaza kuhusu ombi la Cleopatra. Akanyanyua mkonga wa simu na kupeleka sikioni. Akakutana na sauti ya mwanamke.<br />
“Vipi Deo?”<br />
<br />
“Poa Cleopatra, habari za asubuhi?”<br />
“Zitakuwa nzuri iwapo utanipa jibu zuri juu ya yale tuliyoongea jana usiku!”<br />
Deo akanyamaza!<br />
<br />
Hakuwa na jibu!<br />
“Deo...” Cleopatra akaita simuni.<br />
“Nakusikia Cleopatra.”<br />
“Labda kama vipi uje ofisini kwangu!”<br />
<br />
“Hapana naweza kukujibu hata hapa.”<br />
“Haya niambie!”<br />
“NIMEKUBALI!”<br />
“Unasemaje?”<br />
“Nimekubali Cleopatra!”<br />
<br />
“Kwa hiyo upo tayari kufunga ndoa na mimi?”<br />
“Bila shaka.”<br />
“Umenifurahisha sana, sasa utakapokuwa tayari kuja kwetu utaniambia sawa mpenzi?”<br />
“Nimekuelewa.”<br />
<br />
“Nitakuwa na zawadi yako nzuri sana kwa kukubaliana na ombi langu, umenifurahisha sana kwakweli!”<br />
“Nitashukuru sana dear.”<br />
<br />
“Unaweza kuchagua au nikuchagulie mwenyewe?”<br />
“Yoyote utakayopenda wewe naamini itakuwa nzuri na bora kwangu. Nakupa uhuru mpenzi wangu!”<br />
“Sawa.”<br />
<br />
Ukurasa mpya wa mapenzi kati ya Cleopatra na Deo ukafunguka. Sasa hawakuwa kama wapenzi wa kuibana tena, walikubaliana kuoana!<br />
<br />
***<br />
Ni kumbukumbu zinazomtesa sana Deo, ambaye yupo kitandani amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili siku chache kabla ya ndoa yake baada ya kupigwa risasi ya bega!<br />
Cleopatra yupo mbele yake akimwangalia..<br />
<br />
“Mbona kama una mawazo sana?” Cleopatra akamwuliza.<br />
“Hapana nipo sawa, ni maumivu tu!”<br />
“Lakini unajisikiaje sasa?”<br />
<br />
“Kwakweli bado naumwa, ingawa nafuu yangu ni kubwa sana.”<br />
“Sawa, acha mimi niende, nitakuja kukuona tena kesho mpenzi wangu!” Akasema Cleopatra na kuondoka zake.<br />
<br />
Usiku mzima Deo alikuwa akifikiria kuhusu Levina, mwanamke ambaye alikuwa msaada mkubwa katika maisha yake halafu akamuacha na kutaka kumuoa Cleopatra.<br />
<br />
Hakujua ni kwa nini mawazo haya yamemjia wakati huu anaoumwa. Muda huu ambao yupo kitandani akiugulia maumivu ya kupigwa risasi! Wakati huu wa kuelekea kwenye ndoa yake na Cleopatra!<br />
Alijaribu kuwaza kichwani mwake lakini majibu yalikuwa magumu kupatikana.<br />
<br />
***<br />
Ni kama alikuwa kwenye ndoto, akihisi mikono laini yenye joto ikipapasa kifua chake, lakini alipojaribu kutuliza kichwa chake na kuhisi vizuri mikono ile laini ikipapasa kifuani mwake, akagundua kwamba, hakuwa ndotoni!<br />
<br />
Hapo Deo akafumbua macho yake haraka. Hakutegemea kumuona mtu aliyekuwa amesimama mbele yake. Alikuwa ni Levina.<br />
Levina Massamu.<br />
“Habari za asubuhi Deo?” Levina alimsalimia Deo kwa sauti ya taratibu sana.<br />
<br />
“Salama, vipi? Ni saa ngapi saa hizi?” Deo aliitikia na kuuliza maswali hayo mfululizo.<br />
“Ni saa 12:15 za asubuhi Deo!”<br />
“Mapema sana!”<br />
<br />
“Ndiyo...mtu mwenye mgonjwa ambaye kwake ni muhimu, hupenda kuwa wa kwanza kwenda kumuona hospitalini. Hufika mapema kwa ajili ya kumuamsha na kuhakikisha anakuwa msafi.<br />
<br />
“...hata hivyo usijali najua hiyo ni kazi ya Cleopatra, lakini nimekuja na ujumbe mmoja tu kwako...baada ya leo sitakuja tena kukuona hospitalini...” akasema Levina kwa sauti ya taratibu sana.<br />
<br />
Deo hakuweza kufungua kinywa chake kusema chochote, aligeuza macho na kutingisha kichwa chake kuashiria kukukubaliana na maneno yake.<br />
<br />
“fikiria upya kuhusu suala la kumuoa cleopatra. najua zimebaki siku chache sana kabla ya kufunga naye ndoa, lakini fikiria zaidi kama kuna uhalali wa kumuoa na kuniacha nikidondosha machozi. nikisononeka na kunyanyasika! nakutakia siku njema!”<br />
<br />
Levina alitamka maneno hayo kwa simanzi nzito kisha akaondoka na kumuacha Deo akimuita, lakini Levina hakugeuka nyuma.<br />
Akiwa anakaribia mlango mkubwa wa kutokea wodini, macho yakagongana na ya Cleopatra aliyekuwa akiingia.<br />
<br />
Hakuna aliyemsemesha mwenzake, zaidi Cleopatra alisimama na kumsindikiza Levina kwa macho mpaka alipopotea machoni mwake.<br />
“Huyu mwanamke hajui kuachwa? Mbona anajipendekeza hivyo?” Akawaza Cleopatra akielekea kilipo kitanda cha Deo.<br />
<br />
Kumbuka matukio yote haya Deo anayakumbuka akiwa amelazwa baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana. Je, nini kitaendelea? Levina atafanikiwa kumpata Deo? Usikose</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><span class="hasCaption">USIFE KWANZA MPENZI WANGU......EPISODE 33.<br />
Fedha ndiyo chanzo cha usaliti wa Deo kwa Cleopatra. Hakuwa na mpango wa kumsaliti mpenzi wake Levina, lakini fedha zilizungumza na kununua penzi.<br />
<br />
Cleopatra amekolea kabisa katika penzi la Deo, kiasi cha kuamua kumpigia simu usiku na kumwambia kwamba aachane na Levina ili amuoe yeye!<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Unakuwa mtihani mkubwa sana kwa Deo ambaye anakosa kitu cha kufanya.Je, nini kitatokea?<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
KWA kiasi kikubwa Deo alijitahidi sana kubana pumzi zake, lakini alishindwa kabisa! Alijikuta akishusha pumzi ndefu sana alizokuwa amezibana kwa muda mrefu.<br />
<br />
Pumzi hizo zilizotoka bila hiyari, ziliweza kumfikia Cleoptara na kuzisikia vyema kupitia simu.<br />
“Deo!” Cleopatra akaita simuni.<br />
“Ndiyo mpenzi wangu.”<br />
<br />
“Mbona hivyo?”<br />
“Vipi?”<br />
“Umehema kwa kasi sana, kwani kuna nini?”<br />
<br />
“Cleopatra jambo ulilonieleza ni zito sana, linahitaji muda wa kutosha kuweza kulifikiria kabla ya kutoa maamuzi. Si jambo jepesi hakika.”<br />
“Kwa nini?”<br />
<br />
“Kumbuka nilipotoka na Levina, amenisaidia mangapi, leo hii kweli nimsaliti? No...roho yangu inakataa kabisa, moyo wangu hautaki!”<br />
“Kwani hunipendi?”<br />
<br />
“Najua nakupenda, lakini tulikubaliana tangu mapema kwamba penzi letu ni la siri na Levina hatakiwi kujua, sasa leo itawezekanaje mimi niwe mumeo?”<br />
<br />
“Acha ujinga Deo, bado unapenda maisha ya shida? Nataka kubadilisha maisha yako. Kwa kuishi na mimi utakuwa mpya. Kama nilivyokuambia, wazazi wangu wana mali nyingi sana, hakuna mrithi pekee zaidi yangu. Kubali kunioa tafadhali!”<br />
<br />
“Natakiwa kufikiria zaidi Cleopatra!”<br />
“Mpaka lini?”<br />
“Asubuhi nikija ofisini nitakuwa na jibu!”<br />
“Kweli?”<br />
<br />
“Niamini.”<br />
“Ok! Usiku mwema, jua nakupenda sana Deo!”<br />
“Nakupenda pia Cleopatra!”<br />
<br />
Deo alibaki na maswali mengi sana baada ya Cleopatra kukata simu. Kichwani alikuwa na mawazo yasiyo na majibu sahihi.<br />
<br />
Alikiri kumpenda, lakini si kwa kumuoa na kuachana moja kwa moja na Levina. Alikumbuka vizuri sana wema aliofanyiwa na mwanamke huyo, kumuacha ilikuwa ni sawa na kumtakia kifo.<br />
<br />
“Nitafanyaje mimi jamani? Lakini mpaka kesho lazima nitakuwa na majibu sahihi juu ya jambo hili...” akajisemea moyoni mwake na kulazimisha usingizi ambao ulikuwa mgumu sana kupatikana.<br />
<br />
***<br />
Simu ya mezani kwake ndiyo iliyomnasua Deo mawazoni, bado alikuwa akiwaza kuhusu ombi la Cleopatra. Akanyanyua mkonga wa simu na kupeleka sikioni. Akakutana na sauti ya mwanamke.<br />
“Vipi Deo?”<br />
<br />
“Poa Cleopatra, habari za asubuhi?”<br />
“Zitakuwa nzuri iwapo utanipa jibu zuri juu ya yale tuliyoongea jana usiku!”<br />
Deo akanyamaza!<br />
<br />
Hakuwa na jibu!<br />
“Deo...” Cleopatra akaita simuni.<br />
“Nakusikia Cleopatra.”<br />
“Labda kama vipi uje ofisini kwangu!”<br />
<br />
“Hapana naweza kukujibu hata hapa.”<br />
“Haya niambie!”<br />
“NIMEKUBALI!”<br />
“Unasemaje?”<br />
“Nimekubali Cleopatra!”<br />
<br />
“Kwa hiyo upo tayari kufunga ndoa na mimi?”<br />
“Bila shaka.”<br />
“Umenifurahisha sana, sasa utakapokuwa tayari kuja kwetu utaniambia sawa mpenzi?”<br />
“Nimekuelewa.”<br />
<br />
“Nitakuwa na zawadi yako nzuri sana kwa kukubaliana na ombi langu, umenifurahisha sana kwakweli!”<br />
“Nitashukuru sana dear.”<br />
<br />
“Unaweza kuchagua au nikuchagulie mwenyewe?”<br />
“Yoyote utakayopenda wewe naamini itakuwa nzuri na bora kwangu. Nakupa uhuru mpenzi wangu!”<br />
“Sawa.”<br />
<br />
Ukurasa mpya wa mapenzi kati ya Cleopatra na Deo ukafunguka. Sasa hawakuwa kama wapenzi wa kuibana tena, walikubaliana kuoana!<br />
<br />
***<br />
Ni kumbukumbu zinazomtesa sana Deo, ambaye yupo kitandani amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili siku chache kabla ya ndoa yake baada ya kupigwa risasi ya bega!<br />
Cleopatra yupo mbele yake akimwangalia..<br />
<br />
“Mbona kama una mawazo sana?” Cleopatra akamwuliza.<br />
“Hapana nipo sawa, ni maumivu tu!”<br />
“Lakini unajisikiaje sasa?”<br />
<br />
“Kwakweli bado naumwa, ingawa nafuu yangu ni kubwa sana.”<br />
“Sawa, acha mimi niende, nitakuja kukuona tena kesho mpenzi wangu!” Akasema Cleopatra na kuondoka zake.<br />
<br />
Usiku mzima Deo alikuwa akifikiria kuhusu Levina, mwanamke ambaye alikuwa msaada mkubwa katika maisha yake halafu akamuacha na kutaka kumuoa Cleopatra.<br />
<br />
Hakujua ni kwa nini mawazo haya yamemjia wakati huu anaoumwa. Muda huu ambao yupo kitandani akiugulia maumivu ya kupigwa risasi! Wakati huu wa kuelekea kwenye ndoa yake na Cleopatra!<br />
Alijaribu kuwaza kichwani mwake lakini majibu yalikuwa magumu kupatikana.<br />
<br />
***<br />
Ni kama alikuwa kwenye ndoto, akihisi mikono laini yenye joto ikipapasa kifua chake, lakini alipojaribu kutuliza kichwa chake na kuhisi vizuri mikono ile laini ikipapasa kifuani mwake, akagundua kwamba, hakuwa ndotoni!<br />
<br />
Hapo Deo akafumbua macho yake haraka. Hakutegemea kumuona mtu aliyekuwa amesimama mbele yake. Alikuwa ni Levina.<br />
Levina Massamu.<br />
“Habari za asubuhi Deo?” Levina alimsalimia Deo kwa sauti ya taratibu sana.<br />
<br />
“Salama, vipi? Ni saa ngapi saa hizi?” Deo aliitikia na kuuliza maswali hayo mfululizo.<br />
“Ni saa 12:15 za asubuhi Deo!”<br />
“Mapema sana!”<br />
<br />
“Ndiyo...mtu mwenye mgonjwa ambaye kwake ni muhimu, hupenda kuwa wa kwanza kwenda kumuona hospitalini. Hufika mapema kwa ajili ya kumuamsha na kuhakikisha anakuwa msafi.<br />
<br />
“...hata hivyo usijali najua hiyo ni kazi ya Cleopatra, lakini nimekuja na ujumbe mmoja tu kwako...baada ya leo sitakuja tena kukuona hospitalini...” akasema Levina kwa sauti ya taratibu sana.<br />
<br />
Deo hakuweza kufungua kinywa chake kusema chochote, aligeuza macho na kutingisha kichwa chake kuashiria kukukubaliana na maneno yake.<br />
<br />
“fikiria upya kuhusu suala la kumuoa cleopatra. najua zimebaki siku chache sana kabla ya kufunga naye ndoa, lakini fikiria zaidi kama kuna uhalali wa kumuoa na kuniacha nikidondosha machozi. nikisononeka na kunyanyasika! nakutakia siku njema!”<br />
<br />
Levina alitamka maneno hayo kwa simanzi nzito kisha akaondoka na kumuacha Deo akimuita, lakini Levina hakugeuka nyuma.<br />
Akiwa anakaribia mlango mkubwa wa kutokea wodini, macho yakagongana na ya Cleopatra aliyekuwa akiingia.<br />
<br />
Hakuna aliyemsemesha mwenzake, zaidi Cleopatra alisimama na kumsindikiza Levina kwa macho mpaka alipopotea machoni mwake.<br />
“Huyu mwanamke hajui kuachwa? Mbona anajipendekeza hivyo?” Akawaza Cleopatra akielekea kilipo kitanda cha Deo.<br />
<br />
Kumbuka matukio yote haya Deo anayakumbuka akiwa amelazwa baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana. Je, nini kitaendelea? Levina atafanikiwa kumpata Deo? Usikose</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d92b23a8098a19114216"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965bda68453706550"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965c98d7e45827485"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965c98d7e45827485"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption"><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031ecb92286230028">USIFE KWANZA MPENZI WANGU....EPISODE.35<br />
<br />
<br />
Deo yupo kitandani Muhimbili, matukio yote katika maisha yake ya kimapenzi na Levina yanaonekana kama sinema. Anakumbuka siku Levina alipogundua rasmi kwamba anatoka kimapenzi na Cleopatra.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Levina akiwa mezani na mama yake wakipata chakula cha usiku, mama yake anagundua tofauti ambayo mtoto wake anayo. Anajaribu kumuuliza lakini hasemi kitu.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
MAMA Levina akaacha chakula na kumwangalia mwanaye vizuri machoni, ambaye alionekana wazi kuwa na jambo zito linalomsumbua. Alitaka kujua namna ambavyo angeweza kumsaidia.<br />
<br />
“Levina, lazima uniambie ukweli!”<br />
“Unataka ukweli gani mama?”<br />
<br />
“Nataka kujua nini kinakusumbua, maana naona haupo sawa. Kuna jambo linakutatiza. Lazima.”<br />
“Hapana mama.”<br />
<br />
“Wewe ni mwanangu, nimekuzaa na kukulea mwenyewe, sijasaidiwa na mtu, hivyo nakujua ulivyo. Hapo una tatizo lakini hutaki kusema. Hebu kuwa wazi, mama una nini?”<br />
<br />
“Nothing mom, niamini.”<br />
“Wewe utakuwa na mimba!”<br />
“Mama!”<br />
<br />
“Mama what? You must have a pregnant!”<br />
“Hapana mama, sina mimba. Kwa nini unanifikiria hivyo?”<br />
“Sasa nifikirie nini?”<br />
<br />
“Mama ni kweli nina tatizo, lakini si mimba.”<br />
“Ok! Niambie, ni nini kinakusumbua?”<br />
“Ni Deo mama.”<br />
“Deo? Tena?!”<br />
<br />
“Mama nampenda, lazima niwe mkweli bado niliendelea kuwa na uhusiano naye na nilimsaidia sana lakini sasa hivi amenisaliti mama, anatoka na bosi wake ambaye ni rafiki yangu!” Levina akasema kwa uchungu sana akikaribia kudondosha machozi.<br />
<br />
Mama yake akaumia sana, moyo wake ukaingiwa na ganzi, pamoja na kwamba mwanaye alimuudhi kwa kukaidi maagizo yao lakini bado aliona ana kila sababu kama mama kumsaidia mwanaye katika hali aliyokuwa nayo.<br />
“Lakini mwanangu, kumbuka kwamba hapa tunatakiwa kujadili kuhusu wewe na siyo huyo Deo tena.”<br />
“Kivipi mama?”<br />
<br />
“Wewe unazungumzia juu ya mwanaume unayempenda lakini yeye hakupendi, unajua kama ingekuwa ni kesi ya wewe kumpenda na yeye kukupenda, yaani mkapendana, halafu kukawa na tatizo fulani, basi ingekuwa rahisi lakini hapa ni kinyume chake.<br />
<br />
“Kifupi Levina binti yangu unatakiwa kufahamu kwamba huyo mwanaume hana mapenzi na wewe, huna haja ya kuendelea kumuweka moyoni mtu ambaye hakupendi. Najua ni kiasi gani unateseka na kuumia. Najua kwa sababu hata mimi nimepita huko lakini huyo Deo si mwanaume sahihi kwako!” Mama yake aliongea kwa sauti ya chini sana akihitaji usikivu wa mwanaye.<br />
“Kweli mama?”<br />
<br />
“Ndiyo hivyo mwanangu, si mwanaume atakayeweza kuyashika maisha yako sawasawa, bado una muda wa kusubiri mwanangu!”<br />
“Mama!” Levina akaita.<br />
<br />
“Mwanangu!”<br />
“Nitajua mwenyewe cha kufanya!”<br />
“Angalia isiwe kuwa na madhara kwako lakini!”<br />
<br />
“Nipo makini kwa kila ninachokifanya mama. Naamini unanifahamu nilivyo, nakupenda na sitakwenda kinyume!”<br />
“Nenda kapumzike mwanangu, kabla hujalala hakikisha unasali. Tuliza kichwa chako mwanangu, usiwe na mawazo sana!”<br />
<br />
“Nimekuelewa mama, nakupenda sana.”<br />
“Nakupenda pia binti yangu.”<br />
Levina akaondoka na kwenda chumbani kwake kulala, kichwa chake kilikuwa kizito kuliko kawaida.<br />
<br />
***<br />
Deo alikuwa mezani kwake, akiendelea na kazi kama kawaida, simu yake ikaanza kuita, alipoangalia kwenye kioo cha simu, akagundua ni Levina ndiye alikuwa akimpigia. Deo akashtuka sana!<br />
<br />
Ilikuwa ni wiki mbili baada ya Levina kumfuma akiwa na Cleopatra nyumbani kwake, ni siku hiyo ndiyo aliyoamua kuweka ukweli hadharani kwamba yupo na Cleopatra kimapenzi. Pamoja na ujeuri na maneno makali, dhamira iliendelea kumsuta Deo kwa kitendo alichomfanyia Levina.<br />
<br />
Hakumtendea sawa, hilo hata moyo wake ulimdhibitishia. Aliiangalia ile simu ikiendelea kuita kwa muda mrefu bila kupokea.<br />
<br />
“Nitamwambia nini?” Akawaza akiangalia simu iliyoanza kuita tena kwa mara ya pili.<br />
<br />
Levina alikuwa msaada mkubwa katika maisha yake, ni yeye ndiye aliyemtoa kwenye dhiki na shida. Aliyemsomesha na kumtafutia kazi. Kwa hakika hakupaswa kumtenda. Alijishauri sana lakini mwisho wake akaamua kupoikea...<br />
<br />
“Haloo!” Sauti ya Deo ilisikika ikionekana dhahiri kuwa na woga ndani yake.<br />
“Deo!”<br />
“Yes!”<br />
<br />
“Kwa nini umenitenda hivyo? Kwa nini lakini Deo? Ni kweli nastahili kufanyiwa yote hayo? Wema wangu wote kwako, malipo yake ndiyo haya?”<br />
<br />
“Najua nimekukosea Levina, tena nimekosea sana lakini unatakiwa kufahamu kwamba, sikufanya hayo kwa makusudi Levina.”<br />
<br />
“Unamaanisha nini unaposema hukukusudia?”<br />
“Namaanisha kwamba hayakuwa makusudi yangu mpenzi.”<br />
“Kumbe ni nani amefanya hayo.”<br />
“Ni mimi lakini kwa shinikizo.”<br />
<br />
“Shinikizo la nani?”<br />
“Cleopatra.”<br />
“Kwa hiyo huyo Cleopatra ndiyo amebeba moyo wako, yeye ndiye anakuamulia mambo yako?”<br />
<br />
“Sina maana hiyo lakini nilihofia kupoteza kazi.”<br />
“Lakini hiyo kazi si mimi ndiye niliyekutafutia? Kwani ningeshindwa vipi kukutafutia nyingine ili uendelee kuwa wangu?”<br />
<br />
“Lakini nilijua kabisa hizo fedha zako za mawazo, mwisho wake ungekuwa mbaya. Levina hata kama umenisaidia unanisimanga sana, bila shaka ungeendelea kunisimanga haya ningekuoa. Kifupi nimeamua kuwa na Cleopatra, haya ni maamuzi yangu na moyo wangu, hayawezi kubadilishwa na mtu yeyote. Nimemaliza!” Akasema Deo kwa hasira na kukata simu.<br />
<br />
Levina alijaribu kumpigia kwa mara nyingine, akawa anaiangalia simu bila kupokea. Baadaye akaamua kuzima kabisa.<br />
<br />
<br />
<br />
***<br />
Macho ya Deo yalikuwa yananyemelewa na machozi, moyo wake ulikuwa unapingana kabisa na kitu kilichokuwa mbele yake. Ulikuwa unapingana kabisa na ndoa. Alihisi kumkosea sana Levina ambaye hakuwa na hatia kwa aliyofanyiwa.<br />
<br />
Akiwa kwenye kumbukumbu za mawazo hayo, Cleopatra anatokea, tabasamu lake linayeyuka baada ya kuona wekundu katika macho ya Deo. Anakimbia haraka hadi kitandani.<br />
<br />
“Kuna nini?” Akauliza.<br />
“Hakuna kitu.”<br />
<br />
“Hapana mpenzi, kwa nini unajiumiza? Dokta ameshakuruhusu, tafadhali naomba utulize moyo wako, turudi nyumbani.”<br />
“Sawa.”<br />
<br />
“Lakini kuna jambo moja muhimu, nimezungumza na mama kuhusu hali yako, amesema ni vizuri ukapumzike nyumbani kwanza hadi utapopata nafuu, hali yako haikuruhusu kukaa peke yako. Lazima uwe chini ya uangalizi wa karibu.”<br />
“Sawa.”<br />
<br />
Taratibu zote muhimu zikafanyika, Deo akaruhusiwa. Cleopatra akamshika mkono hadi kwenye gari, akamwingiza taratibu na kufunga mlango. Akaendesha gari mpaka nyumbani kwao Mikocheni.<br />
<br />
Deo alipokelewa kwa upendo mkubwa, akafikia kwenye moja ya vyumba vya wageni. Cleopatra alikuwa na wasiwasi sana, alitamani mpenzi wake apone haraka ili waweze kupanda madhabahuni kufunga ndoa yao.<br />
<br />
***<br />
Mipango yote ilikuwa tayari, Deo alikuwa na hali nzuri zilibaki siku tano tu, kabla ya ndoa. Deo akiwa mwenye mawazo sana, asubuhi ya Jumatatu aliamka akiwa mchovu zaidi kuliko siku zote. Cleopatra alipokwenda kumsalimia chumbani kwake, akashangaa kumkuta Deo katika hali ile.<br />
<br />
Hakuwa na furaha, uso wake ulionekana wazi kuwa na jambo zito sana. Cleopatra akakaa kitako kitandani na kumtulizia macho yake usoni.<br />
“Vipi mpenzi wangu? Nahisi kama kuna tatizo.”<br />
“Ni kweli kuna tatizo.”<br />
“Ni nini?”<br />
<br />
“NAJUA HUKUTARAJIA KUSIKIA MANENO HAYA, LAKINI SINA JINSI, LAZIMA NIKUAMBIE. NIMEFIKIRIA KWA MUDA MREFU SANA JUU YA NDOA YETU, NIMEAMUA TUSITISHE. SITAKI KUFUNGA NDOA TENA NA WEWE! SITAKI...” Deo akasema kwa kumaanisha.<br />
<br />
Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia simulizi hii ya kusisimua</span></div></span><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"> </span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"> </span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"> </span></div><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"> </span></div></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965d17a5828788606"><span class="text_exposed_show"><br />
</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d90965e5107474861263"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><span class="text_exposed_show"></span>usife kwanza mpenzi wangu....episode.36<br />
<div class="fbPhotosPhotoCaption" id="fbPhotoSnowliftCaption" tabindex="0"><span class="hasCaption"><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"> <br />
<br />
Deo ameamua kutua mzigo mzito moyoni mwake, amemwambia Cleopatra kwa uwazi kabisa kwamba hawezi kumuoa tena kwa kuhofia kumuudhi Levina ambaye alimsaidia sana hadi kupata elimu na baadaye kazi, jambo hilo linaungwa mkono na mama yake Cleopatra. Deo anaondoka zake.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> Akiwa ndiyo kwanza anaingia nyumbani kwake, Deo anapokea ujumbe mfupi kutoka kwa Levina ambaye anamshukuru kwa kusikia sauti yake. Kwa Deo inakuwa maajabu, maana hakumweleza chochote kuhusu uamuzi wake. Jambo hilo linamchanganya sana Deo.<br />
SASA ENDELEA…<br />
<br />
ALIRUDIA kusoma ule ujumbe mara mbili zaidi, lakini maneno yaliendelea kuwa yale yale, kutoka kwa mtu yule yule, yakiwa ndani ya simu yake yeye mwenyewe! Deo akapigwa na butwaa.<br />
<br />
“Amejuaje haya?” Akajiuliza, lakini hakupata majibu.<br />
Akajivuta hadi mlangoni, akafungua mlango na kuingia ndani, akaenda kujitupa kwenye sofa kubwa akihema kwa kasi. Hapo akaanza kumkumbuka kwa upya kabisa Levina. Kuna kitu kilianza kumwingia akilini mwake.<br />
<br />
Hakuwaza tena juu ya meseji ile iliyoingia kwenye simu yake kimaajabu, alimuwaza Levina, mwanamke ambaye alimpenda kwa mapenzi yake yote, pasipo shinikizo kutoka kwa mtu yeyote. Pasipo matarajio ya kupata kitu chochote! Alimpenda yeye tu!<br />
Mapenzi tu!<br />
<br />
Penzi la dhati!<br />
“Kuna kitu natakiwa kufanya,” akawaza akiangalia simu yake.<br />
Wazo la kumpigia Levina likamwingia akilini mwake.<br />
<br />
Ilikuwa lazima azungumze naye. Wakati huo hakuwaza tena kuhusu kazi, suala la kazi halikuwa na maana sana kwake. Kwa kutumia vyeti vyake alikuwa na uhakika mkubwa sana wa kupata kazi sehemu nyingine, kuliko kuendelea kukaa na mateso moyoni kwa kuishi na mwanamke ambaye mapenzi yake yalikuwa ya wasiwasi.<br />
Akabonyeza namba za Levina na kumpigia, kiasi cha sekunde nane tu, Levina alikuwa hewani akizungumza na Deo…<br />
<br />
“Haloo Levina!”<br />
“Yes Deo, mambo vipi?”<br />
“Poa, lakini sipo sawa sana!”<br />
“Nini tatizo?”<br />
“Kuna kitu nahisi kinaniumiza sana moyoni mwangu, Levina naomba unisamehe kwa yote yaliyotokea, tafadhali sana, nakuomba kwa moyo wangu wote. Mimi ni binadamu na nilipitiwa, siku zote kwenye maisha ni vyema kukosea ili kupata nafasi pia ya kujifunza.<br />
<br />
“Waswahili wanasema, watu wanajifunza kutokana na kukosea. Nakuomba unisamahe ili niweze kuishi kwa amani moyoni mwangu!” Deo akasema kwa sauti ya chini sana akionekana kujutia sana yaliyotokea.<br />
“Deo!” Levina akaita.<br />
<br />
“Nakusikia mama…”<br />
“Ni kweli unaomba msamaha kwa moyo wako wote?”<br />
“Kweli kabisa, naweza kuapa kwa namna yoyote unayotaka!”<br />
“Hakuna sababu ya kuapa, ni wewe mwenyewe na nafsi yako, kama ni kweli unajua umekosea ni vizuri na ni rahisi kusamehewa.”<br />
<br />
“Kweli Levina najuta kukukosea, nimetambua kosa langu, nisamehe tafadhali!”<br />
“Nilishakusamehe Deo, lakini ukweli ni kwamba sijakusamehe kikamilifu!”<br />
“Unamaanisha nini?”<br />
<br />
“Namaanisha kwamba nilishakusamehe tangu siku nyingi, lakini si kwa moyo wangu!”<br />
“Sawa, naomba basi kuanzia leo uwe umenisamehe kwa moyo wako Levina!”<br />
“Inawezekana Deo, lakini kuna masharti mawili!”<br />
“Masharti?” Deo akauliza kwa mshangao mkubwa.<br />
“Ndiyo kuna masharti mawili, kama ukiweza kuyatimiza, basi nitakusamehe moja kwa moja na nyongo iliyokuwa ndani ya moyo wangu itaondoka.”<br />
<br />
“Ni masharti gani hayo? Niambie tafadhali!”<br />
“Si kwa haraka kiasi hicho, lakini nitakuambia.”<br />
“Lini?”<br />
“Nipe muda, lazima nikutane na wewe, nahitaji kuzungumza na wewe, tena uso kwa uso.”<br />
“Itakuwa lini?”<br />
“Nitakujulisha, kwa sasa pumzika kwanza.”<br />
“Sawa Levina, lakini nina ombi moja kwako!”<br />
“Nakusikia!”<br />
<br />
“Isiwe muda mrefu sana, siwezi kukaa na hili jambo muda mrefu, nahisi moyo wangu unaungua!”<br />
“Usijali najua ni kiasi unateseka, najua pia ni kiasi gani unataka kuishi huru. Yote hayo nayajua na nitayachukulia kwa uzito mkubwa, muda ukifika nitambia!”<br />
<br />
“Nimekuelewa vizuri, lakini nilikuwa na lingine!”<br />
“Nini tena?”<br />
“Nimepata meseji yako muda si mrefu!”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Umejuaje hayo?”<br />
<br />
“Siku zote kama kitu unakipenda, ni rahisi kujua kinavyoendea hata kama hutapewa taarifa. Nimejua kwa sababu nakupenda Deo!”<br />
“Lakini haraka sana!”<br />
“Ni kwa sababu nakupenda sana!”<br />
“Haya bwana.”<br />
“Siku njema Deo!”<br />
“Kwako pia.”<br />
<br />
Deo hakutoa simu haraka sikioni pamoja na kwamba alikuwa ameshaagana na Levina ambaye alishakata simu. Ni kama alikuwa amepigwa bumbuwazi au hajui kinachoendelea. Moyo uliendelea kuteswa na mapenzi, alimtaka sana Levina kwa wakati huu.<br />
<br />
Aligundua kwamba penzi lake kwa Levina lilikuwa zito na lenye thamani zaidi ya Cleopatra ambaye alijilazimisha kutokana na mali zake.<br />
“Nitampata Levina wangu, lazima arudi tena kwangu, lazima...” akawaza akisimama na kujivuta chumbani mwake.<br />
***<br />
Mama Cleopatra baada ya kutoka chumbani na kuwaacha Deo na Cleopatra aliifuata simu yake chumbani kwake na kumpigia Levina ili kutafuta ukweli.<br />
<br />
“Hujambo mwanangu?”<br />
“Sijambo mama shikamoo...” Levina akasalimia.<br />
“Marhaba...haya mbona mwenzio anafanya mambo ya ajabu unashindwa kuniambia binti yangu?”<br />
“Nani mama? Patra?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Amefanya nini tena?”<br />
“Unamjua Deo?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Unamjuaje?”<br />
<br />
“Mama Deo alikuwa mpenzi wangu, lakini Patra kwa sababu ya pesa zake ak....” Levina alishindwa kumalizia sentesi yake na kuanza kulia</span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="text_exposed_show"> </span><span class="hasCaption">USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE.37<br />
<br />
Mama Cleopatra baada ya kutoka chumbani na kuwaacha Deo na Cleopatra aliifuata simu yake chumbani kwake na kumpigia Levina ili kutafuta ukweli.<br />
“Hujambo mwanangu?”<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Sijambo mama shikamoo...” Levina akasalimia.<br />
“Marhaba...haya mbona mwenzio anafanya mambo ya ajabu unashindwa kuniambia binti yangu?”<br />
“Nani mama? Patra?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Amefanya nini tena?”<br />
“Unamjua Deo?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Unamjuaje?”<br />
<br />
“Mama Deo alikuwa mpenzi wangu, lakini Patra kwa sababu ya fedha zake ak....” Levina alishindwa kumalizia sentesi yake na kuanza kulia.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
YALIKUWA maumivu makali sana kwa Levina ambaye alianza kukumbuka tangu siku ya kwanza alipokutana na Deo sokoni na kuvutiwa naye. Akakumbuka jinsi alivyofanya mbinu na kuhakikisha anaingia nyumbani kwao kama mfanyakazi wa ndani lakini ndani ya moyo wake akiwa na kitu tofauti kabisa na hicho.<br />
<br />
Ni Levina huyo huyo ndiye aliyejitolea kumsomesha Deo hadi kufikia mafanikio na kupata kazi. Kunyang’anywa na rafiki yake mpenzi, waliokua na kusoma pamoja kulimuuma sana ndani ya nafsi yake. Alishindwa kuzuia hisia zake na kujikuta akianza kulia kwenye simu.<br />
<br />
Alianza kwa sauti ndogo, lakini jinsi kumbukumbu zile mbaya zilivyozidi kumsumbua, ndivyo alivyozidisha kilio chake.<br />
Mama Cleopatra akapata kazi ya kumbembeleza Levina.<br />
<br />
“Pole sana mwanangu, naomba usilie, nimeshajua kila kitu na huyu kijana mwenyewe ameamua kuachana na Patra na kwa jinsi anavyoonekana, anajutia sana kitendo alichokifanya. Nahisi bado anakupenda na ni mapenzi hayo ndiyo yanayomsukuma kusema ukweli leo hii na kuamua kuachana naye.<br />
<br />
“Kuna uwezekano mkubwa sana akarudi kwako na kukuomba msamaha, tafadhali naomba umsamehe na nitakuwa tayari kuwasaidia kwa namna yoyote. Najua thamani ya mapenzi mwanangu, najua maumivu ya kunyang’anywa mpenzi. Tafadhali mwanangu rudisha moyo wako, naomba umkubalie huyo kijana!” Mama Levina akasema kwa sauti ya utulivu sana.<br />
<br />
“Kweli mama?”<br />
“Ndiyo mwanangu!”<br />
“Lakini unadhani Deo ana mapenzi ya kweli mama? Si ni aina ya wanaume ambao wanaweza kuyumbishwa ovyo?”<br />
“Ni tamaa tu, halafu ukumbuke kwamba alikuwa na hofu ya kufukuzwa kazi.”<br />
<br />
“Mama, sasa ni kwanini asiwe na hofu na mimi ambaye ndiye niliyemtafutia hiyo kazi, akawa na wasiwasi wa kupoteza tu hiyo kazi bila kumkumbuka aliyemfanya akaipata?”<br />
<br />
“Umeongea jambo la msingi sana mama, lakini ujue kwamba, shetani naye ana mambo yake. Naweza kusema kwamba alipitiwa, lakini kiukweli mwanangu mpatie nafasi nyingine, utaona mabadiliko yake. Atakuwa amejifunza.”<br />
“Sawa mama, nitajitahidi!”<br />
<br />
“Siyo kujitahidi, naomba iwe hivyo!”<br />
“Sawa mama.”<br />
“Niahidi Levina!”<br />
“I promise you mom!” (Nakuahidi mama)<br />
“Thank you my daughter!” (Nashukuru binti yangu)<br />
<br />
Kila mmoja alikuwa na lake kichwani mwake, mama Cleopatra alikuwa na nia ya dhati ya kumsaidia Levina ambaye alikuwa sawa na mwanaye kwa namna walivyokuwa marafiki wakubwa. Bado aliona thamani yake kama mwanaye.<br />
<br />
Hakufikiria juu ya aibu ya watu wengi walioalikwa kwa ajili ya sherehe hiyo, kwake yeye sherehe hiyo isingekuwa na maana kama ingefungwa ndoa huku Levina akilalamika.<br />
<br />
Levina alifurahishwa sana na maelezo ya mama yake Cleopatra, alimuona mzazi bora ambaye anaangalia usawa na kuonesha mapenzi yake kwa watoto wake wote. Bado alikuwa akifikiri vizuri suala la kurudiana na Deo.<br />
Moyoni mwake Deo alikuwepo!<br />
Amejaa tele!<br />
<br />
***<br />
Mawimbi yalikuwa yanapiga kwa kasi sana ufukweni mwa Bahari ya Hindi eneo la Coco. Watu walikuwa wengi sana Jumamosi hiyo walipunga upepo baharini. Ilikuwa jioni, mishale ya saa 11:30, jua likianza kung’ang’ania kupotea na giza kusita kuchukua anga!<br />
<br />
Ni kama vitu hivi viwili vilikuwa vikishindana, mashindano hayo yalifanya ufukwe kuwa na rangi kama ya dhahabu, mwanga kuwa hafifu kiasi na kupendezesha mandhari ya Ufukwe wa Coco.<br />
<br />
Pembeni kabisa, juu ya jiwe kubwa, walikuwa wamekaa Deo na Levina, mikononi mwao kila mmoja alikuwa ameshika box lenye maji ya matunda wakinya taratibu kwa mrija. Levina ndiye aliyemwalika Deo kwa mtoko huo akitaka kuzungumza naye na kumpa masharti yake aliyosema anataka kumpa.<br />
<br />
Deo alikuwa kimya akisubiri kusikia masharti ya Levina ambaye alikuwa amependeza sana jioni hiyo. Tayari Deo alikuwa ameshapona kabisa, afya yake ikianza kunawiri na makunyanzi usoni yakianza kupotea.<br />
<br />
“Kwanza kabisa, naomba unisamehe kwa kukukosesha kazi. Najua kama siyo mimi, ungekuwa unaendelea na kazi yako. Kwa hilo naomba sana unisamehe Deo!” Levina alianza kwa kutamka maneno hayo.<br />
<br />
“Hapana Levina usiseme hivyo, mimi ndiye mkosaji. Halafu hiyo kazi haina maana yoyote kwangu kama wewe hutakuwa na amani na mimi. Hutakuwa na furaha na mimi. Haitakuwa na maana yoyote kabisa. Napenda kuona unafurahi!”<br />
<br />
“Deo lazima utambue kwamba nakupenda sana, nilikupenda kwa moyo wangu wote na nimeshindwa kukutoa moyoni mwangu!”<br />
“Najua!”<br />
<br />
“Nitakupa masharti mawili, najua ni magumu sana, lakini ukiyaweza nitakusamehe milele.”<br />
“Nipo tayari Levina niambie tu mama!”<br />
“Labda nisisitize tena kwamba, nakupenda sana, siwezi kuacha kukupenda katika maisha yangu yote, sharti la kwanza ili nikusamehe Deo, unatakiwa ukubali kufunga ndoa na mimi!” Levina akasema akimwangalia Deo usoni.<br />
<br />
“Kwa hilo nipo tayari, sijui kuhusu wazazi wako!”<br />
“Mambo ya wazazi niachie mimi, kama umekubali basi vizuri, sharti la pili ni gumu kidogo, lakini nalo ukikubaliana nalo nitakusamehe!”<br />
“Sema mpenzi, nipo tayari kwa chochote!”<br />
<br />
“Deo naomba unisamehe kwa nitakalokuambia, najua litakuumiza na hutanielewa kirahisi, lakini ndiyo ukweli wenyewe. Naomba unielewe kwamba sikuwa na nia mbaya, nia yangu ilikuwa nzuri kabisa, lakini lazima unisamehe Deo!”<br />
“Ni nini? Hebu niambie basi Levina...” akasema Deo akimkazia macho Levina.<br />
<br />
“MIMI NDIYE NILIYEKODI WATU WAKUPIGE RISASI KWENYE LIFTI!” Levina akasema akilia.<br />
“Unasemaje?” Deo akauliza kwa sauti ya ukali sana.</span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span><br />
<div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031c6ba9a26603982">USIFE KWANZA MPENZI WANGU......EPISODE.38<br />
<br />
<br />
“Deo naomba unisamehe kwa nitakalokuambia, najua litakuumiza na hutanielewa kirahisi, lakini ndiyo ukweli wenyewe. Naomba unielewe kwamba sikuwa na nia mbaya, nia yangu ilikuwa nzuri kabisa, lakini lazima unisamehe Deo!”<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> “Ni nini? Hebu niambie basi Levina...” akasema Deo akimkazia macho Levina.<br />
“MIMI NDIYE NILIYEKODI WATU WAKUPIGE RISASI KWENYE LIFTI!” Levina akasema akilia.<br />
“Unasemaje?” Deo akauliza kwa sauti ya ukali sana.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
HAIKUWA rahisi kwa Deo kuamini kwamba Levina ndiye aliyefanya jaribio la kutaka kumuua, moyo wake ulibadilisha mapigo na hasira yake kuwa kubwa. Aliyatoa macho yake akimwangalia Levina, akiwa haamini kabisa kwamba angeweza kufanya kitendo kile.<br />
<br />
“Levina ulitaka kuniua?” Deo akauliza kwa hasira.<br />
“Siyo hivyo mpenzi wangu!”<br />
“Siyo hivyo vipi na umekiri kwamba ulituma watu wanipige risasi.<br />
“Deo kabla sijakuambia lazima nikupe masharti ili nikusamehe. Ni kweli nilifanya kosa, lakini kosa lenyewe ni katika kulinda penzi langu!”<br />
“Ulitaka kuniua au kunilinda?”<br />
<br />
“Kwani uliuawa?”<br />
“Hapana.”<br />
“Kuna kitu uliibiwa?”<br />
“Hapana!”<br />
<br />
“Basi ndiyo unatakiwa kufahamu kwamba nilifanya hivyo kwa ajili ya kukupata. Deo sikuwa na njia nyingine, vinginevyo wewe ungefunga ndoa na Cleopatra. Sikiliza nikuambie Deo, mimi nakupenda sana, moyo wangu una mzigo mzito wa mapenzi ambayo siwezi kufananisha na kitu chochote.”<br />
“Sijui kama ni rahisi kukuelewa!”<br />
<br />
“Lakini unataka kuelewa?”<br />
“Ndiyo!”<br />
“Ngoja nikusimulie...” Levina akasema akikaa sawa sawa kwa ajili ya kumweleza kisa kizima kilivyokuwa.<br />
<br />
***<br />
Alikuwa amekaa mwenyewe kwenye meza ya peke yake, macho yake yakiangaza kila upande, ni kama alikuwa anawasubiri watu wafike katika baa ile. Ilikuwa ni usiku wa saa mbili na dakika zake, Levina ametulia kwenye kona akinywa soda yake taratibu kabisa.<br />
<br />
Akiwa anaendelea kuangaza macho yake, simu yake ikaita. Haraka akapokea akiangalia kwenye mlango mkubwa wa kuingilia pale baa.<br />
“Yes...” akatamka Levina akisubiri sauti ya upande wa pili.<br />
“Ni wewe uliyekaa hapo kwenye kona peke yako?”<br />
“Ndiyo!”<br />
<br />
“Ok! Tunakuja, nimeshakuona!” Sauti nzito ya kiume ilisikika kwenye spika za simu ya Levina.<br />
Dakika moja baadaye, wanaume watatu walikuwa wamekaa kwenye viti kuizunguka meza aliyokuwa amekaa yeye. Walisalimiana kisha wote wakakaa kimya.<br />
<br />
“Karibuni sana, mimi ndiye Levina niliyemuagiza Asnath awatafute, nimefurahi kukutana nanyi!” Akasema Levina.<br />
“Hata sisi pia.”<br />
“Kama Asnath alivyowaambia, sina haja ya kumuua huyo jamaa, hakikisheni mnampiga risasi ya bega, nataka alazwe, mambo mengine nitamaliza mwenyewe!”<br />
<br />
“Unataka hiyo kazi ikamilike baada ya muda gani?” Mmoja wao akauliza.<br />
“Ndani ya wiki moja kutoka sasa, unajua amebakiza siku chache sana kabla ya kufunga ndoa, ni hiyo ndiyo ambayo sitaki ifungwe!”<br />
“Sawa, chetu?”<br />
<br />
“Ninazo...naona niwalipe nusu kwanza, kazi ikikamilika nitawamalizia. Chukua hii...” akasema Levina akimkabidhi bahasha iliyovimba!<br />
“Ahsante sana, hatuna muda wa kusubiri zaidi, kila kitu umeshatuelekeza kwenye simu, namba yake ya simu tunayo, anapofanyia kazi tunapajua, kazi iliyobaki ni ndogo sana, ni kumfuatilia baasi!”<br />
<br />
“Sawa, nawatakieni kazi njema yenye mafanikio!”<br />
“Itakuwa hivyo, usijali!”<br />
“Ok! Poa.”<br />
Wale vijana wakasimama na kumuacha Levina akiwa amekaa kimya sehemu ile. Moyoni mwake alitamani sana zoezi lile likamilike, hakutaka kabisa Cleopatra afunge ndoa na Deo, mwanaume wa maisha yake.<br />
<br />
“Tutaona sasa, mimi si katili, lakini wakati mwingine inabidi ili niweze kutetea penzi langu, naamini sasa nitafanikiwa,” akawaza Levina akisimama na kutoka katika baa hiyo.<br />
<br />
***<br />
Deo aligandisha macho yake usoni mwa Levina akiwa haamini kabisa anachosimuliwa, hakutegemea kama Levina angefanya tukio kubwa kiasi kile.<br />
“Lakini levina hukuwa na njia nyingine zaidi ya hiyo?” Deo akamwuliza akiwa ameyatoa macho yake.<br />
<br />
“Unadhani ningetumia njia gani hapo? Hata kama ni wewe ungetumia njia gani?”<br />
“Kwanini usingenitafuta tukaongea?”<br />
“Deo ulikuwa unatafutika wewe? Hata simu yangu ulikuwa unaiona kama kinyaa, sikuwa na njia nyingine Deo, naomba unisamehe lakini nitakusamehe kama na wewe utanisamehe na kutimiza ahadi zako zote!”<br />
<br />
Deo akatulia kwa muda akatafakari, aliyaona makosa yake lakini pia aligundua kwamba Levina hakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya tukio alilolifanya ambalo liliweza kuwarudisha tena pamoja.<br />
<br />
Alipata maumivu makali sana, aliteseka sana hospitalini, lakini mwisho wa siku aligundua wakulaumiwa ni yeye mwenyewe. “Nimekusamehe Levina!”<br />
“Nimekusamehe pia Deo!”<br />
“Sasa?” Deo akauliza akiwa anamwangalia Levina machoni.<br />
“Nini tena mpenzi wangu?”<br />
<br />
“Kuhusu ndoa, itawezekana kweli kuoana?”<br />
“Nini kinachoshindikana chini ya jua?”<br />
“Wazazi wako baby, hawanitaki kabisa hilo ndiyo tatizo.”<br />
“Kuna kitu nilikuwa sijakuambia sweetie!”<br />
“Kitu gani?”<br />
<br />
“Nilishaongea na mama kila kitu...hakuna tatizo tena, mzee Massamu huwa haongei kwa mkewe Diana. Lazima kieleweke, kwa hiyo ondoa shaka mpenzi wangu. Tutapanda madhabahuni na kufunga ndoa yetu!”<br />
“Kweli dear?” Deo akauliza akiwa ametoa macho.<br />
“Niamini mimi mpenzi wangu!”<br />
<br />
Deo na Levina wakasimama, kisha wakakumbatiana. Hawakuogopa macho ya watu. Walichojua wao ni kitu kimoja tu, kuwa wanapendana!<br />
Kama Levina alivyosema, haikuwa kazi ngumu mama yake kumshawishi baba yake mzee Massamu kuhusu Deo kumuoa Levina hasa kwa kuwa tayari alikuwa na sifa walizokuwa wanazihitaji.<br />
<br />
Deo akasafiri hadi nyumbani kwao Singida, akawaeleza wazazi wake juu ya kupata mchumba, hakuna aliyepingana naye. Taratibu zote zikafanyika, ndoa ya kifahari ikafungwa jijini Dar es Salaam.<br />
<br />
Watu wengi sana walihudhuria, akiwemo Cleopatra ambaye tayari walishaweka mambo sawa. Mama yake Cleopatra ndiye aliyewakutanisha na kuwapatanisha. Jambo la kushangaza zaidi, Cleopatra ndiye alikuwa Mweka Hazina wa kamati ya sherehe ya Deo na Levina.<br />
<br />
Ukawa mwisho wa machozi kwa Levina na mwanzo wa maisha ya furaha, akiwa na mwanaume aliyeota kuwa naye, mwanaume aliyemuhangaikia kwa muda; aliyekuwa tayari kufanya chochote kwa ajili yake.<br />
Mwanaume wa maisha yake!<br />
<br />
UNLIMITED SWAGGAZZ:<br />
Nawashukuru sana wasomaji wangu wapenzi kwa kufuatilia simulizi hii kuanzia mwanzo hadi mwisho, naamini haijakuacha kama ulivyokuwa, kuna kitu umejifunza.<br />
<br />
<span> *********MWISHO***********</span><wbr></wbr><span class="word_break"></span>*</span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="hasCaption"><span class="text_exposed_show"> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d94031db3b9274548796"><span class="text_exposed_show"> </span></div></span></div><div class="fbPhotosSnowliftFeedback" id="fbPhotoSnowliftFeedback"><div class="fbPhotoSnowliftActionLinks "><span><span class="UIActionLinks UIActionLinks_bottom" data-ft="{"tn":"=","type":20}"><button class="like_link stat_elem as_link" data-ft="{"tn":">","type":22}" name="like" title="Tilkendegiv, at du synes godt om dette" type="submit"><span class="default_message"></span></button> </span></span></div></div><div class="highlighter"><div class="innerWrap"><span class="highlighterContent"></span><textarea autocomplete="off" class="enter_submit DOMControl_placeholder uiTextareaNoResize uiTextareaAutogrow textBox mentionsTextarea textInput" id="uvhw9i_269" name="add_comment_text" placeholder="Skriv en kommentar..." role="textbox" title="Skriv en kommentar..."></textarea></div></div></div></div></div></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d568101837371095"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d568101837371095"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d568101837371095"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d568101837371095"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d582334d54939250"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5aed50f56750478"><span class="text_exposed_show"> </span></div></span><div class="fbPhotoTagList" id="fbPhotoSnowliftTagList"><span class="fcg"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5be976846404119"><span class="text_exposed_show"> </span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5be976846404119"><span class="text_exposed_show"> </span></div></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5eb365e03683586"><span class="text_exposed_show"><span> </span></span></div><div class="text_exposed_root text_exposed" id="id_500d8c6d5eb365e03683586"><span class="text_exposed_show"><span> </span> </span></div></div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com1tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-65831141898894207162012-07-23T10:34:00.001-07:002012-07-23T10:34:00.239-07:00MAMBO YA KUFANYA UNAPOBOREKA....<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEimQG3PRL6auH7baPSIhl0HZ5okgt17YwytKyDwXwbgsbAW_DWUp8xSUfbLleUN9HAnh7yr0iXxTQA6VbB5e2Dm9Z4jLEEIsir_uM5tNf5IpF6-czqotobqiTB-8R5mECJbyu9WcZ_j6i_W/s1600/482124_395647403828174_1577490870_n.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEimQG3PRL6auH7baPSIhl0HZ5okgt17YwytKyDwXwbgsbAW_DWUp8xSUfbLleUN9HAnh7yr0iXxTQA6VbB5e2Dm9Z4jLEEIsir_uM5tNf5IpF6-czqotobqiTB-8R5mECJbyu9WcZ_j6i_W/s320/482124_395647403828174_1577490870_n.jpg" width="273" /></a></div><a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/my-wifeep1.html?spref=bl"></a><span class="hasCaption"><br />
Maisha tunayoishi yamejaa kasi zinazosababisha watu wengi kuboreka. Tangu asubuhi tunapoamka, tunakutana na mambo mengi yanayozichosha akili zetu na kutuletea msongo. Zifuatazo ni dondoo nyepesi zinazoweza kukutoa kwenye hali ya kuboreka na kukurudisha kwenye furaha na uchangamfu.<br />
<br />
1. Fanya mambo unayoyapenda<br />
<span class="text_exposed_show"> Kila mtu ana jambo ambalo akilifanya hujisikia furaha. Kama ni kuangalia au kucheza soka, kusikiliza muziki laini, kuangalia filamu, kutembea kwenye bustani za maua au vinginevyo, fanya kwa lengo la kutuliza mawazo na hisia zako, utaona mabadiliko.<br />
<br />
2. Jenga picha nzuri akilini<br />
Yawezekana umeboreka kwa sababu umejaza fikra nyingi chungu mawazoni mwako. Futa yote uliyokuwa unayafikiria na vuta taswira ya mandhari tulivu.<br />
<br />
3. Imba kwa sauti<br />
Bila shaka kuna wimbo unaoweza kuuimba vizuri. Bila kujali kama umesahau baadhi ya mashairi au la, imba kwa sauti huku ukijisikiliza kwa makini, jilazimishe kufurahia jinsi unavyoimba. Wataalam wa ubongo na akili wanaeleza kuwa kusikiliza ‘tune’ yako mwenyewe husaidia sana kutuliza mawazo.<br />
<br />
4. Jichanganye na marafiki<br />
Yawezekana huna mazoea ya kujichanganya sana na marafiki au watu wanaokuzunguka. Unapohisi umeboreka, jilazimishe kuchangamana na wenzako, shiriki kwenye mazungumzo au shughuli wanayoifanya na utahisi ahueni kubwa.<br />
<br />
5. Tafakari kuhusu kilichokukwaza<br />
Kama umeboreka kutokana na kazi nyingi, mazingira uliyopo au kwa sababu ya watu waliokuzunguka, jiulize kwa makini na ukishabaini sababu iliyokufanya uwe hivyo, tafuta njia ya kujitoa. Unaweza kuondoka mahali ulipo na kwenda sehemu nyingine tulivu kwa muda, akili ikitulia rudi na endelea na utaratibu wako.<br />
<br />
6. Zitawale pumzi zako<br />
Miongoni mwa mbinu inayoaminika kutuliza akili pale unapoboreka ni kuzitawala pumzi zako. Unapohisi kuna jambo haliko sawa, unashauriwa kuanza kuvuta hewa taratibu kwa kutumia pua na kuitoa kupitia mdomo. Vuta pumzi ndefu na ibane kwa sekunde kadhaa, kisha anza kuiachia taratibu.<br />
<br />
7. Washirikishe wenzako<br />
Kama jambo lililokufanya uboreke unahisi liko nje ya uwezo wako, washirikishe watu unaowaamini na usione aibu kuomba msaada. Wataalam wa saikolojia wanaeleza kuwa, jambo unaloliona ni zito na halitatuliki, ukianza kulijadili na wenzako utagundua kuwa kumbe linawezekana.<br />
<br />
8. Kunywa maji mengi<br />
Maji yanaelezwa kuwa na uwezo mkubwa wa kutuliza mifumo mbalimbali ya mwili, ukiwemo mfumo wa kufikiri. Unapoona umeelemewa na hisia chungu, kunywa maji mengi taratibu na yaache yasambae kwenye mishipa yako ya damu. Unashauriwa kuwa na mazoea ya kunywa angalau glasi nane kwa siku.<br />
<br />
9. Jipe muda wa kupumzika<br />
Kupata muda wa kutosha wa kupumzika ni miongoni mwa vitu vinavyopunguza kwa kiwango kikubwa kuboreka. Mapumziko ya kitandani (siyo kulala usingizi) husaidia kutuliza mwili na akili. Jijengee ratiba ya kupumzika kitandani kabla ya kulala. Pata muda wa kutosha wa kulala angalau saa 8 kila siku. Lala muda muafaka na amka mapema.</span></span>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-72363730836455405982012-07-23T10:30:00.001-07:002012-07-23T10:30:11.821-07:00SOMA STORY TAMU YA MAPENZI.......<a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/my-wifeep1.html?spref=bl"></a><img alt="" class="spotlight" src="https://fbcdn-sphotos-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash3/576498_346126962113552_731042338_n.jpg" style="height: 276px; width: 460px;" /><br />
<span class="hasCaption"> UMESHINDWA KUWA MWAMINIFU KWA MPENZI WAKO???<br />
<br />
NAKUPONGEZA wewe msomaji mpya wa safu hii. Kama ndiyo unaanza kusoma hapa leo, umechagua sehemu sahihi ya kukuza fikra zako kwenye suala zima la uhusiano, maisha na saikolojia kwa ujumla wake.<br />
<span class="text_exposed_show"> Wadau wa kona hii na wale wanaofuatilia kwenye gazeti damu moja na hili, Risasi Mchanganyiko kila Jumatano kwenye safu ya All About Love wanakubaliana na mimi kuwa siku hadi siku maisha yao ya kimapenzi yanakwenda vizuri.<br />
<br />
Leo tunajadili eneo muhimu sana katika uhusiano; Uaminifu. Wengi wanaweza kunishangaa kidogo, wakiamini kwamba suala la kuwa mwaminifu linamuhusu mhusika moja kwa moja.<br />
Kwamba kama mtu akitaka kuwa mwaminifu au kinyume chake ni uamuzi wake mwenyewe! Hoja hiyo ni ya kweli, lakini si kwa asilimia zote. Kuna vitu vingine ambavyo vinasaidia kumfanya mtu awe mwaminifu.<br />
Ndugu zangu, wakati mwingine suala la uaminifu si la hiyari! Kuna vitu inabidi vifanyike ili angalau uwe katika wingu la uaminifu, halafu unaongeza na nia yako ya kutaka kuwa mwaminifu, ndipo unafanikiwa.<br />
SAUTI ZA WADAU<br />
Nilipata kuwasiliana na watu wanne wa jinsi tofauti wenye tatizo moja; Wameshindwa kuwa waaminifu. Kutokana na ufinyu wa nafasi, utawasikia wawili kati yao.<br />
Wa kwanza: “Kaka Shaluwa, mimi nina mpenzi wangu ambaye nipo naye kwenye uhusiano, huu mwaka wa tatu. Tunapendana sana. Mimi kama msichana kuna wakati natongozwa na wanaume.<br />
“Kwa sababu ninajua nina mwanaume wangu, huwa nawatosa, lakini wakati mwingine najikuta nakosa nguvu. Nakiri kumsaliti mpenzi wangu mara tatu, ila roho inaniuma sana. Tatizo ni nini kaka yangu? Naomba unisaidie, maana sipendi kumsaliti mpenzi wangu.”<br />
Wa pili: “Mimi ni mwanaume mwenye miaka 37, nimeoa na nina watoto wawili na mke wangu mpenzi. Nimemfuatilia sana, kiukweli ni mwaminifu kupindukia. Hata mimi napenda sana kuwa kama yeye, lakini ndiyo hivyo, nashindwa. Nimeshatoka na wasichana wawili, sipendi kabisa hali hii.”<br />
FUNZO<br />
Kwa maelezo yao, tunaona namna ambavyo watu hao ambao wapo kwenye uhusiano (mwingine kwenye ndoa) lakini wanawasaliti wenzi wao. Hata hivyo, si kwa kupenda – wanafanya hivyo na moyoni wanaumia.<br />
Jiangalie na wewe rafiki yangu mpenzi. Unamheshimu mpenzi/mwanandoa mwenzako kwa kuwa naye peke yake au unamsaliti? Hebu angalia ndani ya nafsi yako, ni jambo unalopenda kulifanya au linakuumiza?<br />
Sikia rafiki yangu, usaliti ni sumu ya mapenzi. Ni mwanzo wa kumkosoa mpenzi wako na kuziona kasoro zake. Habari zaidi ni kwamba, mtu anayechanganya sana wapenzi ni rahisi kupoteza uwezo wa kupenda.<br />
Hujikuta akiwachukia watu wa jinsi ya pili, huongozwa zaidi na tamaa na msisimko wa mapenzi hupungua. Zipo athari nyingine nyingi zinazotajwa kisaikolojia kwa mtu asiye mwaminifu. Wanasaikolojia wanakwenda mbali zaidi – wanasema si ajabu mhusika kuanza kupoteza imani na hata yeye mwenyewe. Hajiamini tena.<br />
UNATAKA KUWA MWAMINIFU?<br />
Huu ndiyo mwongozo wako katika somo hili. Kwa maneno mengine, kama wewe ni msaliti na unapenda tabia yako, ishia hapa. Usiendelee kusoma hii mada maana haikufai. Inawezekana ni mwaminifu na unatamani kuendelea kudumu katika uaminifu wako, ni jambo zuri na mada hii ni kwa ajili yako. Twende tukaone sasa.<br />
<br />
WEKA NIA<br />
Si uchawi, ni imani ya ndani ya moyo wako. Kila kitu kinaanza na nia. Kama ni kweli unatamani kuwa mwaminifu kwa mwenzi wako, anza kujenga hili kuanzia moyoni mwako. Jiambie kuwa unapenda kuwa mwaminifu siku zote na unatamani kuendelea hivyo.<br />
ANZA NA KINYWA<br />
Hili ni jambo la kwanza kabisa kwako wewe ambaye unahitaji kuwa mwaminifu. Nimesema tangu mwanzo kuwa unaweza kuwa na nia ya kutaka kuwa mwaminifu, lakini ukaangushwa na mambo madogo ambayo yatakufanya baadaye ujute.<br />
Kinywa chako ni kitu muhimu sana kuzingatia. Pima maneno yako. Usipende kuzungumza lugha chafu, maneno yasiyofaa au stori za mapenzi (hasa na watu wasio wa jinsia yako).<br />
Inawezekana usione umuhimu wa hili, lakini rafiki yangu, nikuambie kitu kimoja? Unapoweka mazoea ya kuzungumza na marafiki zako mambo ya mapenzi, ni rahisi sana kujiingiza kwenye usaliti.<br />
Utaanza kama burudani, mipaka ikishavukwa utajiona sehemu ya stori zenu. Namaanisha unaweza ukatamani au kuvaa uhusika wa stori yenyewe, hapo sasa inakuwa rahisi kuingilika hata kama nia yako haikuwa hiyo.<br />
Zungumza kwa busara, achana na utani usio na maana. Kinywa chako kioneshe namna unavyojiheshimu. Kama una mazoea ya kujenga utani sana, ni rahisi mtu kukujaribu kimapenzi, akiwa na ngao ya utani!<br />
Ukikubali amekubeba, ukikataa anakuambia: “Nilikuwa nakutani bwana...hutaniwi wewe?”<br />
Umeona eeh?!<br />
Basi sawa...ngoja nipumzike hapa kwa leo. Endelea kuyatafakari haya, wakati ukisubiri wiki ijayo kwa mwendelezo wake.</span></span>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-55554942185514948902012-07-23T10:26:00.001-07:002012-07-23T10:26:26.308-07:00UKITAKA SALAMA KTK MAPENZI....USIFANYE HAYA.....(TIPS ZA MALOVEE)......<a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/my-wifeep1.html?spref=bl"></a><img alt="" class="spotlight" src="https://fbcdn-sphotos-a.akamaihd.net/hphotos-ak-prn1/540209_347391618653753_693272882_n.jpg" style="height: 557px; width: 400px;" /><br />
<span class="hasCaption"> Ni Jumatatu nyingine ambayo tunakutuna tena kwenye UNLIMITED SWAGGAZ PAGE km kawa tunaendelea kupeana elimu ya masuala yahusuyo mapenzi. Leo tunaendelea pale tulipoishia wiki iliyopita kuhusu makosa ambayo hupaswi kuyafanya kwenye uhusiano wa kimapenzi.<br />
<br />
<span class="text_exposed_show"> KUSHINDWA KUSOMA ALAMA<br />
Zipo alama muhimu ambazo ni vema kuzijua na uzibaini kwa mwenzi wako kabla hujazama kwenye dimbwi la mapenzi. Bahati mbaya wengi hutawaliwa na papara, matokeo yake hushindwa kubaini vitu ambavyo vinaweza kumfanya apate uelekeo wa uhusiano wake.<br />
Katika pointi hii, nashauri watu kwenda kwa mwendo wa kinyonga badala ya kupiga mbizi bila kujua kina cha maji. Kusoma alama muhimu kwa mwenzi wako mapema ni sawa na kutegua kitendawili. Itakusaidia kujua kama kweli uliyenaye ana mapenzi ya kweli au anaweza kuwa laghai.<br />
Wengi wanapoingia kwenye uhusiano wa kimapenzi hueleza kuwa wanapenda, tena huweka wazi kuwa hisia zimeanguka kwa wale wanaowapenda. Hata hivyo, huacha mambo mengi ndani ya uvungu wa nyoyo zao. Wewe utakuwa mshindi, endapo utaweza kumsoma mwenzi wako na kumuelewa kinagaubaga.<br />
Pointi hapa ni kuwa mwanzo kabisa wa uhusiano, yapo mambo mengi ambayo kila mmoja hujitahidi kuyazungumza. Hiyo huita kujiweka wazi lakini imethibitika kitaalam kwamba maelezo ambayo hutolewa ni asilimia 40 tu, zilizobaki hufichwa. Asilimia 60 zilizobaki utazifichua kwa kusoma alama muhimu.<br />
Nyongeza ni kwamba mara nyingi wengi hujitahidi kusema uongo mwanzoni mwa uhusiano. Hata kama mtu anapenda lakini hudanganya hili na lile pengine kwa hofu, tahadhari au kama pointi ya kushinda penzi. Mantiki hapa ni kukutaka uwe makini na umsome mwenzako kwa undani kabisa.<br />
Katika kipengele cha kusoma alama muhimu, kuna vitu vya msingi vya kuzingatia ambavyo ni hivi vifuatavyo;<br />
<br />
1) Jamii: Mwenzi wako anasimama vipi na jamii yake? Usiingie kichwakichwa kwenye mapenzi na mtu ambaye hata jamii yake inamuona ni tatizo. Vilevile, yule ambaye ni muoga inabidi uanze kumtia wasiwasi mapema. Ni kwa ajili ya maisha yako, hivyo ni vema kuchangamka.<br />
Hutakiwi kugundua muda umeshapita kuwa mwenzi ana tabia usizopenda. Mapema msome na umuelewe. Chunguza msimamo wake kwenye jamii, anavyojiamini, je, anaonesha kuwa na dira ya maisha. Kama hana uelekeo, unatakiwa kuachana naye haraka.<br />
<br />
2) Hisia: Zisome hisia zake, je ni mtu anayejali? Unatakiwa kujua kama hisia zake zipo karibu kwa kiasi gani. Atakapotakiwa kukutimizia haki yako ya faragha, atakuwa tayari kwa wakati? Ni aibu mmeshakuwa na uhusiano kwa muda mrefu ndiyo unaanza kulalamika kwamba mwenzi wako hakutimizii huduma ya uwanja wa wawili.<br />
Lingine kwenye hisia, unatakiwa ujifunze kujua kama mwenzi wako ni mtu wa kulipuka au kinyume chake. Inawezekana ni kweli mwenzi wako anakupenda lakini akawa ni mtu wa jazba, tatizo dogo ‘anapaniki’ utadhani nyoka aina swila, kakanyagwa mkia. Mjue halafu umpime, je, unaweza kumvumilia? Jiridhishe mara mbili, vinginevyo bwaga manyanga.<br />
<br />
3) Muonekano: Ni kipengele kidogo muhimu ndani ya kifungu cha kushindwa kusoma alama kama sehemu mojawapo inayowafanya wengi kufanya makosa kwenye uhusiano. Muonekano si suala la baadaye, inatakiwa mapema sana umtathmini halafu ujiridhishe kama anakufaa au kinyume chake.<br />
Ni aibu umeshaingia kwenye uhusiano, halafu baadaye unamsaliti mwenzi wako na kuanza kuwatolea macho wale ambao unaona ni wazuri zaidi. Hakikisha kwamba mwanzo kabisa kwenye uhusiano wako, unajiridhisha kuwa anao mvuto unaokutosha......</span></span>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-65334894925265546122012-07-23T10:12:00.001-07:002012-07-23T10:12:37.681-07:00STORY TRAAAAM YA MALOVEEE....<a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/my-wifeep1.html?spref=bl"></a><span class="hasCaption"> </span><img alt="" class="spotlight" src="https://fbcdn-sphotos-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash3/541229_347415618651353_1125809140_n.jpg" style="height: 568px; width: 380px;" /><br />
<br />
<span class="hasCaption">SIMU SIO KIPIMO CHA MOYO WA MTU......<br />
<br />
Baada ya salamu, tuwe pamoja kwenye mada yetu ya leo ambayo naomba uelewe undani wake usije kusema hujanielewa. Sasa hivi kati ya watu kumi, watano wanamiliki simu ya mkononi. Hii imekuwa ikirahisisha mawasiliano, lakini baadhi ya watu wamebadili maana ya simu na kuibebesha kazi nyingine ambayo si yake.<br />
<span class="text_exposed_show"> <br />
Nimekuwa nikipokea malalamiko ya matatizo mengi katika mapenzi sababu kubwa ikiwa ni simu ya mkononi. Wengi wamewaona wapenzi wao kama si waaminifu na wengine kuamini kabisa hawapendwi, sababu ikiwa ni hii simu ya mkononi.<br />
<br />
Kumekuwa na utaratibu wa kutumiana ujumbe wa mapenzi kwa wapenzi ambao huwa kama ndiyo tafsiri hasa ya yaliyo moyoni.<br />
<br />
Si ujumbe mzuri tu wa simu bali hata kuzungumza maneno matamu yatokayo midomoni yanayoonyesha ninyi kama wapenzi mnapendana kwa dhati.<br />
<br />
Kutokana na hali hiyo, wengi huamini kwa asilimia 100 kuwa wanapendwa, lakini mawasiliano yanapopungua au kukatika mhusika mmoja au wote lazima wataanza kuamini kuwa mapenzi yamepungua.<br />
<br />
Nataka kuwafumbua masikio wote wanaoamini simu ndiyo tafsiri sahihi ya mapenzi, niwaambie tu kuwa mapenzi ya kweli hayakai ndani ya simu, bali moyoni mwa mtu, si wote wanaopenda kutumia simu wakati wote.<br />
<br />
Wapo ambao hupenda kutumia usiku tu na wapenzi wao hasa wanapokuwa wamepumzika, kwa kuwa mchana huwa na mambo mengi. Hapa wenza wengine hasa wale wasiojua muda sahihi wa kuchati au kuzungumza na wapenzi wao, huamini kuwa mapenzi yamepungua.<br />
<br />
Kipindi cha kazi ni muda wa kujuliana hali na siyo wakati sahihi wa kuchati au kuzungumza kwa muda mrefu, wengine wapo kazini lakini muda mrefu wanazungumza mambo ya mapenzi na kujisahau, wanatakiwa kutambua kuwa simu ina wakati wake.<br />
<br />
Kwa hali kama hiyo, wengi hushindwa kuelewa maana ya simu kwamba si kipimo cha mapenzi bali upendo wa mtu upo moyoni.<br />
<br />
Wengi wamekuwa wakiamini yote yanayoandikwa katika ujumbe wa mapenzi ni mapenzi kamili, unaweza kuwa na mpenzi ambaye kawaida yake ni kuchukua ujumbe wa mapenzi kwenye gazeti na kukutumia lakini si kilichomo moyoni mwake.<br />
<br />
Kuujua upendo wa kweli si kwa maneno au ujumbe mtamu bali vitendo vya kuonyeshana kweli mnapendana.<br />
<br />
Asilimia kubwa ya walioanzisha uhusiano kwa njia ya simu, wameumizwa na hizohizo simu, hadi kufikia hatua ya kusafiri umbali mrefu na mwisho wake kukuta tofauti kubwa na yaliyoandikwa kwenye ujumbe au maneno matamu kwa njia ya simu.<br />
<br />
Napenda kuchukua nafasi hii kuwaeleza wote ambao huamini ujumbe au maneno matamu katika simu ndiyo mapenzi kamili, usiukabidhi moyo wako kwa mtu kwa ajili ya simu.<br />
<br />
Siku zote ili kupata mpenzi wa kweli, unatakiwa kutumia muda mrefu kuchunguza tabia yake, ukiridhika ndipo uutoe moyo wako ukiamini unayempa ni mtu sahihi.</span></span>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-47466616487535603682012-07-22T16:26:00.001-07:002012-07-22T16:26:09.457-07:00MY WIFE....EP.1.<!--[if gte mso 9]><xml> <w:WordDocument> <w:View>Normal</w:View> <w:Zoom>0</w:Zoom> <w:TrackMoves/> <w:TrackFormatting/> <w:HyphenationZone>21</w:HyphenationZone> <w:PunctuationKerning/> <w:ValidateAgainstSchemas/> <w:SaveIfXMLInvalid>false</w:SaveIfXMLInvalid> <w:IgnoreMixedContent>false</w:IgnoreMixedContent> <w:AlwaysShowPlaceholderText>false</w:AlwaysShowPlaceholderText> <w:DoNotPromoteQF/> <w:LidThemeOther>DA</w:LidThemeOther> <w:LidThemeAsian>X-NONE</w:LidThemeAsian> <w:LidThemeComplexScript>X-NONE</w:LidThemeComplexScript> <w:Compatibility> <w:BreakWrappedTables/> <w:SnapToGridInCell/> <w:WrapTextWithPunct/> <w:UseAsianBreakRules/> <w:DontGrowAutofit/> <w:SplitPgBreakAndParaMark/> <w:DontVertAlignCellWithSp/> <w:DontBreakConstrainedForcedTables/> <w:DontVertAlignInTxbx/> <w:Word11KerningPairs/> <w:CachedColBalance/> </w:Compatibility> <m:mathPr> <m:mathFont m:val="Cambria Math"/> <m:brkBin m:val="before"/> <m:brkBinSub m:val="--"/> <m:smallFrac m:val="off"/> <m:dispDef/> <m:lMargin m:val="0"/> <m:rMargin m:val="0"/> <m:defJc m:val="centerGroup"/> <m:wrapIndent m:val="1440"/> <m:intLim m:val="subSup"/> <m:naryLim m:val="undOvr"/> </m:mathPr></w:WordDocument> </xml><![endif]--><!--[if gte mso 9]><xml> <w:LatentStyles DefLockedState="false" DefUnhideWhenUsed="true"
DefSemiHidden="true" DefQFormat="false" DefPriority="99"
LatentStyleCount="267"> <w:LsdException Locked="false" Priority="0" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Normal"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="9" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="heading 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 7"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 8"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 9"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 7"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 8"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 9"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="35" QFormat="true" Name="caption"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="10" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Title"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="1" Name="Default Paragraph Font"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="11" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtitle"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="22" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Strong"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="20" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Emphasis"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="59" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Table Grid"/> <w:LsdException Locked="false" UnhideWhenUsed="false" Name="Placeholder Text"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="1" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="No Spacing"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" UnhideWhenUsed="false" Name="Revision"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="34" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="List Paragraph"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="29" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Quote"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="30" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Quote"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 1"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 2"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 3"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 4"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 5"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 6"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="19" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtle Emphasis"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="21" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Emphasis"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="31" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtle Reference"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="32" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Reference"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="33" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Book Title"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="37" Name="Bibliography"/> <w:LsdException Locked="false" Priority="39" QFormat="true" Name="TOC Heading"/> </w:LatentStyles> </xml><![endif]--><!--[if gte mso 10]> <style>
/* Style Definitions */
table.MsoNormalTable
{mso-style-name:"Tabel - Normal";
mso-tstyle-rowband-size:0;
mso-tstyle-colband-size:0;
mso-style-noshow:yes;
mso-style-priority:99;
mso-style-qformat:yes;
mso-style-parent:"";
mso-padding-alt:0cm 5.4pt 0cm 5.4pt;
mso-para-margin-top:0cm;
mso-para-margin-right:0cm;
mso-para-margin-bottom:10.0pt;
mso-para-margin-left:0cm;
line-height:115%;
mso-pagination:widow-orphan;
font-size:11.0pt;
font-family:"Calibri","sans-serif";
mso-ascii-font-family:Calibri;
mso-ascii-theme-font:minor-latin;
mso-fareast-font-family:"Times New Roman";
mso-fareast-theme-font:minor-fareast;
mso-hansi-font-family:Calibri;
mso-hansi-theme-font:minor-latin;
mso-bidi-font-family:"Times New Roman";
mso-bidi-theme-font:minor-bidi;}
</style> <![endif]--> <div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgXtjUI-2UEoVteclLE4jhnIKP73VizZbL35y550ocz7DtG0salClqBWCz_wyC5zAsrFnt-aaK8L2I9Fsoj0oCDivaJ6wvXkRCGBSrRC0IRnsFEBzLRpU2Yk_cpftKy9OxYlGZFVlxUjOq3/s1600/482124_395647403828174_1577490870_n.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="320" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgXtjUI-2UEoVteclLE4jhnIKP73VizZbL35y550ocz7DtG0salClqBWCz_wyC5zAsrFnt-aaK8L2I9Fsoj0oCDivaJ6wvXkRCGBSrRC0IRnsFEBzLRpU2Yk_cpftKy9OxYlGZFVlxUjOq3/s320/482124_395647403828174_1577490870_n.jpg" width="273" /></a></div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><span style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 12.0pt; mso-fareast-font-family: "Times New Roman"; mso-fareast-language: DA;"> MY WIFE....EP.1.<br />
<br />
Katika maisha yangu sikuwahi kuwaza kuua hata nzi kutokana na huruma niliyokuwa nayo.<br />
Watu wengi walipenda kuniita mlokole japo historia yangu yote niliishi maisha ya kutokuwa na dini nikiamini Mungu wa Wakristo ndiye Mungu wa Waislamu kutokana na mafundisho ya dini zote niliyoyafuatilia.<br />
Utashangaa kwa nini niliishi bila kuwa na dini ikiwa wazazi wangu wana dini, tena dini tofauti, baba Muislamu na mama Mkristo. Katika maisha yao hakuna aliyekubali kumfuata mwenzake na kukubaliana, kila mmoja aishi katika imani yake. Hivyo basi, nikawa mtoto wa wazazi wa dini mbili, pamoja na wazazi wangu kuishi kila mmoja na dini yake, waliishi katika upendo wa hali ya juu kwa kila mmoja kuheshimu imani ya mwenzake.<br />
<br />
Nilipopata ufahamu nilijikuta nipo njia panda kwa vile sikutaka kumuudhi mmoja wa wazazi wangu kwa kumpendelea mmoja. Halafu kitu cha ajabu nilikuwa mtoto mmoja kama roho, hivyo niliamua kusimama katikati ya wazazi wangu kwa kutochagua dini yoyote. Lakini nilikuwa nafahamu kipi mwanadamu anatakiwa kukifanya ili usimuudhi Mungu.<br />
<br />
Katika maisha yangu yote niliamini tofauti ya dini mbili ni ndogo sana lakini anayetakiwa kuabudiwa ni Mungu mmoja. Tokea hapo niliishi nikiwa sina dini na kuishi kama mpagani, tofauti yangu nilikuwa najua Mungu ni mmoja na ndiye anayetakiwa kuabudiwa, lakini sikwenda msikitini wala kanisani na malumbano ya dini hizi mbili mimi yalikuwa hayanihusu.<br />
<br />
Wazazi wangu nao walikubaliana na mimi baada ya ushawishi wa kila mmoja kugonga mwamba. Huu ulikuwa muktasari wa maisha yangu ya awali ya kunifanya nisiwe na dini kwa ajili ya mapenzi ya wazazi wangu.<br />
Kutokana na malezi mazuri ya wazazi wangu, niliweza kuishi sehemu yoyote na mtu wa aina yeyote, siku zote heshima na ucheshi ndivyo vilinifanya watu wanipende.<br />
<br />
Kama nilivyosema awali, nilikuwa mtu wa huruma na heshima kwa wakubwa na wadogo, lakini mateso ya mapenzi yalinifanya nigeuke niwe na roho mbaya kukiko shetani.<br />
<br />
Kuna maelezo niliwahi kusikia wakati nakua kwamba kuna matendo mengine shetani anakimbia akimuona mwanadamu anatenda. Baada ya kuteswa sana na mapenzi ilifikia hatua kutoa roho ya mtu kwangu ilikuwa kitu cha kawaida hata kwa kosa dogo la kuombana msamaha kwa kuamini hakuna kiumbe kibaya duniani kama mwanadamu ambaye hatakiwi kupewa nafasi kwa vile kama ukimchekea basi atakuumiza wewe.<br />
<br />
Mkasa wangu unaanzia pale nilipotimiza miaka 21, nilitoka kwa wazazi wangu na kusafiri nje ya mkoa kwenda kufanya kazi baada ya rafiki yangu kupata kazi ya ujenzi.<br />
<br />
<br />
Hivyo, hakutaka kuondoka peke yake, alinichukua na mimi huku wazazi wangu wakiniasa niishi na watu kwa heshima na taadhima. Nami niliwaahidi wazazi wangu kuwa nitaishi kama walivyonielekeza.<br />
Nilitengana na wazazi wangu kwa mara ya kwanza toka nitoke tumboni kwa mama wangu. Nilifika mkoani na kufikia kwa ndugu wa rafiki yangu. Kwa vile tulifika Jumamosi jioni sana, tulilala na kesho yake tulipumzika na kupata nafasi ya kupelekwa sehemu ya kazi.<br />
<br />
Ulikuwa mradi mkubwa sana ambao tuliambiwa utachukua miaka mitano kwisha, siku ile tulipumzika na kesho yake tulikwenda kuanza kazi. Siku ya pili tuliamka asubuhi na mapema na kwenda eneo la ofisi ambapo ndipo mnapangiwa kazi. Ilikuwa kuna tofauti kubwa na vijana wengi tuliowakuta nje ya geti wakisubiri kuitwa, lakini sisi tulikuwa na mwenyeji, mjomba wa rafiki yangu ambaye alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa mradi ule ambao ulikuwa chini ya Wataliano, tuliingia bila kuitwa.<br />
Basi huo ndiyo ukawa mwanzo wa kuanza maisha ya kujitegemea, tulianza kwa kulipwa kwa kutwa kama wenzetu kwa wiki mbili, baada ya hapo tulichaguliwa vijana kama ishirini tuliopewa mkataba na kulipwa kwa mwezi na posho yetu kuongezeka tofauti na wenzetu waliokuwa wakilipatwa kwa kutwa.<br />
Maisha yalikwenda vizuri huku mimi na mwenzangu tukihama kwa ndugu zake na kupanga chumba kimoja na kukaa wawili. Wazazi wangu nao walikula jasho langu kila mwezi kwani niliwatumia robo ya mshahara wangu nao walizidi kuniombea kwa Mungu ili niendelee kupata zaidi.<br />
<br />
Siku zilikatika huku nami nikipevuka kiakili na mawazo kufikia hatua ya kuhitaji mwenza. Nyumba tuliyokuwa tumepanga kulikuwa na binti mmoja ambaye Mwenyezi Mungu alimjalia umbile dogo lakini nzuri na sura jamili (nzuri). Binti yule alitokea kunipenda sana kiasi cha kumueleza mama yake angependa aolewe na mimi.<br />
Moja ya njia ya kuonesha ananipenda aliniomba mambo yote ya kike ayafanye yeye kama vile kunipikia chakula cha jioni baada ya kazi, kufua nguo na kusafisha chumba lakini sikumpa nafasi ile kwa kuhofia wazazi wake.<br />
Pamoja na mimi kumpenda sana bado sikumkubalia kutokana na kuwaheshimu sana wazazi wake ambao siku zote walinilea kama mtoto wao.<br />
<br />
Siku moja usiku baada ya kutoka kazini, mama mwenye nyumba ambaye ni mama mzazi wa yule binti aliniita kwa kumtumia yule binti. Nami niliitikia wito ule, baada ya kuingia sebuleni kwao, nilikaribisha kwenye kochi lililokuwa karibu na alipokaa mama mwenye nyumba.</span></div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><span style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 12.0pt; mso-fareast-font-family: "Times New Roman"; mso-fareast-language: DA;">MY WIFE....EP.2.<br />
<br />
Siku moja majira ya usiku baada ya kutoka kazini mama mwenye nyumba ambaye ni mama mzazi wa yule binti aliniita kwa kunmtumia yule binti. Nami niliitikia wito ule, baada ya kuingia sebuleni nilikaribisha kwenye kochi lililokuwa karibu na alipokaa mama mwenye nyumba.<br />
SASA ENDELEA...<br />
“Kazala,” mama aliita kwa sauti ya chini.<br />
“Naam mama,” niliitikia kwa unyenyekevu mkubwa.<br />
“Nimekuita mwanangu nikueleze jambo moja la muhimu sana.”<br />
“Sawa mama.”<br />
“Kwanza wewe dini gani?”<br />
“Sina dini,” nilimjibu kwa mkato.<br />
“Muongo, hebu niambie ukweli wewe ni dini gani?”<br />
“Kweli mama sina dini.”<br />
“Sasa kama ukipata mwanamke mwenye dini utafanya nini?”<br />
“Sitafanya chochote nitaiheshimu dini yake, lakini mi nitabakia sina dini?”<br />
“Kwa nini?”<br />
Sikumficha nilimuelezea maisha ya wazazi wangu na kitu gani kilichonifanya nisiwe na dini.<br />
“Lakini hata kiserikali mtu anapotimiza miaka kumi na nane ana haki ya kuamua chochote bila kuingiliwa, hivyo ulikuwa na nafasi ya kuchagua dini yoyote ya baba au ya mama.”<br />
“Ni kweli, lakini bado kwa mimi sikutakiwa kufanya hivyo.”<br />
“Kwa nini?”<br />
“Nimesimama kati ya baba na mama yangu wote nawapenda na sitaki kumuudhi mmoja kati yao.”<br />
“Sasa mwanangu kuna kitu nimekuitia, mdogo wako Suzana anakupenda sana tena sana kapitiliza kukupenda. Siku zote amekuwa akikuonesha kwa vitendo imeonekana kama umuelewi. Mpaka kuja kunieleza mimi mama yake basi ujue yamemfika shingoni. Kutokana na tabia yako ambayo imekuwa tofauti na wavulana wengi nimeamini unafaa kuwa mkwe wangu.<br />
“Nakuomba uwe mkwe wangu muoe Suzy kwa kweli ni mwanamke mzuri ambaye atajivunia katika maisha yako. Najua utashtuka mama kumpigia debe mwanaye lakini kwa hili sikuwa na jinsi.”<br />
“Nimekusikia mzazi wangu naomba unipe muda ili nami niwasiliane na wazazi wangu.”<br />
“Kuwasiliana na wazazi wako si vibaya, lakini kwanza ni wewe kukubaliana na mwenzako.”<br />
“Mimi nimekubali.”<br />
“Nashukuru kwa majibu yako mazuri, basi nakuruhusu, uwasiliane na wazazi wako, usihofu gharama nitakusimamiane mpaka mwisho wa harusi yenu.”<br />
“Nashukuru mzazi wangu.”<br />
Baada ya kutoka kwa mama mwenye nyumba nilirudi chumbani kujipumzisha, haikupita muda mlango iligongwa alikuwa Suzy.<br />
“Karibu,” nilikabiribisha bila kunyanyuka kitandani.<br />
Alisukuma mlango na kuingia ndani akiwa na sinia lililofunikwa kawa.<br />
“Karibu chakula Kazala.”<br />
Sikutaka kubisha lakini nilitaka tule pamoja Suzy hakukataa tulikuwa pamoja. Tokea siku ule Suzy akawa na uhuru wa kuja kwangu lakini sikuwa na tamaa ya mwili kwa kujiapia mpaka nimuoe kabisa. Mipango ilienda vizuri na Suzy akawa mke wangu ndoa ilifungwa kwa mkuu wa wilaya kila mtu akiwa na imani yake.<br />
Namshukuru Mungu maisha yalikuwa mazuri kwa mke wangu kuonesha mapenzi ya kweli nami pia nilimpenda mapenzi ya dhati. Miezi sita baada ya kuoana tulihama nyumba ya wazazi wa mke wangu na kwenda kukaa kwenye nyumba nyingine ya familia yao iliyokuwepo umbali kidogo toka kwetu, wakati huo mke wangu alikuwa na ujauzito wa miezi minne.<br />
Nyumba tuliyohamia ilikuwa na wapangaji wawili na sisi tulikuwa sehemu ya nyumba mbele iliyokuwa ya kifamilia. Kazi nayo iliendelea vizuri kila siku kuondoka asubuhi na kurudi usiku. Maisha yalisoga muda ulipofika mke wangu alijifungua mtoto wa kike.<br />
Mwenetu alikuwa vizuri mpaka alipofikisha mwaka mmoja na miezi saba nilipatwa na mshtuko kushindwa kutembeza zaidi ya kukaa na kujibuta kwa matako. Katika maisha yangu pamoja ya kutokuwa na dini bado sikuuamini uchawi hata kidogo japo niliusikia kuwa upo. Hali ya mwanangu ya kutotembea ilinishtua sana. Katika kuulizia kwa watu waliomuona mtoto wangu walisema mtoto wangu inawezekana amebemendwa.<br />
Kauli ile ilinishtua sana baada ya kuelezwa maana ya kubemenda ni mtu kutoka nje ya ndoa, kwa upande wangu sikuwa na shaka kwa vile sikuwa na mpenzi mwingine zaidi ya mke wangu mama Zawadi. Pia kwa upande wa mke wangu hata kwa mtutu nisingekubali kutoka nje ya ndoa kwani nilimuamini sana.</span></div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><span style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 12.0pt; mso-fareast-font-family: "Times New Roman"; mso-fareast-language: DA;">MY WIFE....EP.3.<br />
<br />
<br />
LIPOISHIA:Kauli ile ilinishtua sana baada ya kuelezwa maana ya kubemenda ni mtu kutoka nje ya ndoa, kwa upande wangu sikuwa na shaka kwa vile sikuwa na mpenzi mwingine zaidi ya mke wangu mama Zawadi. Pia kwa upande wa mke wangu hata kwa mtutu nisingekubali kutoka nje ya ndoa kwani nilimuamini sana.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
Nikawa njia panda kuelewa hali iliyomkuta mwanangu kama inatokana na mtu kutoka nje ya ndoa basi walikuwa wamekosea nikiamini huenda tatizo alilonalo mwanangu huenda linafanana na hilo.<br />
<br />
Jumapili moja niliyokuwa nyumbani, nilitoka na mwanangu ambaye nilimpenda sana pamoja na kuchelewa kutembea. Nikiwa natoka dukani nilikutana na mama mmoja wa makamo na kusalimiana naye. Nilipishana naye lakini sikupiga hatua mbili aliniita.<br />
“Baba Zawadi.”<br />
“Naam mama,” niliitika huku nikigeuka kumsikiliza.<br />
“Samahani mwanangu.”<br />
“Bila samahani mama.”<br />
“Basi naomba tusogee pembeni tuzungumze.”<br />
“Hakuna tatizo mama yangu.”<br />
Nilisogea pembeni kidogo ya barabara na kusimama kwenye uchochoro wa kutokea mtaa wa pili.<br />
“Naam mama,” nilianzisha mazungumzo.<br />
“Mwanangu nimekuita ili tuzungumze kitu kimoja, nina imani hukijui kinachofanyika nyuma kwa vile unatoka asubuhi na kurudi usiku kinachotendeka mchana hukijui.”<br />
“Ni kweli mama.”<br />
“Unamuonaje mjukuu wangu Zawadi?”<br />
“Kwa kweli mama hata mimi nashindwa kuelewa.”<br />
“Unashindwa kuelewa nini ikiwa mwanao mnamtesa bila kosa.”<br />
“Mama tunamtesa kivipi?”<br />
“Unaona hii miguu ya mwanao ipo sawa?” aliniuliza huku akiishika miguu ya mwanangu iliyokuwa haina nguvu.<br />
“Haipo sawa, kwa kweli nachanganyikiwa hata sijui sababu ni nini japo watu wananiambia kitu ambacho naamini si kweli.”<br />
“Kitu gani hicho?”<br />
“Achana nacho hakina umuhimu,” sikutaka kumuambia habari ambazo mimi niliona ni za kizushi.<br />
“Kitu gani?”<br />
“Utayaweza maneno ya watu mama, kila kukicha hawakosi ya kusema.”<br />
“Maneno gani?” yule mama alikazania swali lake.<br />
“Achana nayo hayana umuhimu.”<br />
“Inawezekana uliyoambiwa ndiyo nitakayokueleza leo.”<br />
“Nina imani si hayo.”<br />
“Haya, tuachane na hayo, unajua matatizo ya mtoto kuchelewa kutembea yanatokana na nini?”<br />
“Kwa kweli sijui.”<br />
“Yapo mambo mengi, moja kuchezewa na walimwengu na lingine ni kubemendwa.”<br />
“Kwa hiyo tatizo la mwanangu linatokana na nini?”<br />
“Mkeo atamuua mtoto huyu, kwa nini unakuwa na moyo wa kikatili kiasi hiki, kama hawezi kumlea basi mumpeleke kwa bibi yake kuliko kumtesa bila sababu.”<br />
“Mama sijakuelewa, mke wangu amemfanya nini mtoto?”<br />
“Anambemenda.”<br />
“Eti?”<br />
“Anambembenda na mwisho wake atamuua.”<br />
“Mmh! Una maana gani?”<br />
“Mkeo si muaminifu, wote mtaani wanajua, ukitoka na yeye nyuma anatoka anarudi muda umekaribia kurudi.”<br />
“Sasa mama kutoka kwa mke wangu inaingiliana vipi na mwanangu kuchelewa kutembea?”<br />
“Baba jasho la janaba ni baya kwa mtoto hasa ikiwa mliyekutana si wazazi wa mtoto, mmoja wenu akikosa uaminifu na akamshika na uchafu wake lazima mtoto atadhurika.”<br />
“Sasa mama mke wangu mbona muaminifu?” kauli ile ilinishtua.<br />
“Baba acha kusema hivyo, sisi ndiyo tunayejua, isingekuwa huyu mtoto wala nisingenyanyua mdomo wangu, ningekuacha ili siku moja ujionee mwenyewe uchafu wa mkeo.”<br />
“Kwa hiyo chanzo cha matatizo ya mtoto ni mke wangu?” nilijikuta nikikosa amani moyoni.<br />
“Baba usiandikie mate, kwa vile mkeo hata aibu hana, siku moja rudi nyumbani mchana utajionea mwenyewe. Kabla ya kufanya lolote fanyia kazi haya niliyokueleza. Ukipata majibu ndiyo utajua mkeo muaminifu au siyo, utapata kiini cha matatizo ya mkeo.<br />
“Ila nakuomba kabla ya yote mtoto wako mpeleke kwa bibi yake kisha fanya uchunguzi wako.”<br />
“Asante mama kwa maelezo yako.”<br />
“Ila nakuomba ukienda kwako usioneshe mabadiliko yoyote, kuanzia Jumatatu siku yoyote rudi nyumbani ghafla mchana utaniambia niliyokueleza ni kweli na maendeleo ya mwanao utayaona kwa muda mfupi akiwa mbali na mama yake.”<br />
“Asante mama.”<br />
Niliagana na yule mama ambaye alikuwa mtu wa heshima na nilimuheshimu sana pale mtaani. Nikiwa narudi, njia nzima nilikuwa na mawazo mazito juu ya maneno niliyoelezwa na sababu ya matatizo yanayomfanya mwanangu ashindwe kutembea.<br />
Kingine ambacho sikutaka kukikubali mara moja ni kuhusu kutoka kwa mke wangu nje ya ndoa. Kwa kweli sikuamini mke wangu kama angeweza kutoka nje ya ndoa hasa kutokana na ukimya pia kuonesha mapenzi mazito kwangu.</span></div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><span style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 12.0pt; mso-fareast-font-family: "Times New Roman"; mso-fareast-language: DA;">MY WIFE....EP.4.<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
<br />
Kingine ambacho sikutaka kukikubali mara moja ni kuambiwa kuwa mke wangu huwa anatoka nje ya ndoa.<br />
Kwa kweli sikuamini kama mke wangu angeweza kufanya hivyo, kutokana na ukimya wake na jinsi anavyoonesha mapenzi mazito kwangu.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
Nilifikiria kama ni kweli mke wangu ndiye chanzo cha matatizo ya mtoto, ina maana hajui au anafanya makusudi. Nilipofika nyumbani nilijitahidi kuficha mabadiliko mke wangu alinichangamkia huku akimchukua mtoto ambaye siku zote alimuonesha mapenzi makubwa.<br />
Siku hiyo nilikuwa nyumbani kimwili lakini kiakili nilikuwa mbali sana, kwa kuwa nilikuwa nikiwaza yote niliyoelezwa na wote walioguswa na hali ya mwanangu kuchelewa kutembea kiasi cha watu kumtania kwa kumwita fundi majiko.<br />
Japokuwa mwanangu alikuwa hatembei lakini alikuwa akiongea maneno yote akiwa amekaa kama fundi anayetengeneza majiko.<br />
Kila nilipomuangalia mke wangu sikummaliza, nilivyomuamini na maneno yale nilichanganyikiwa huku upande mwingine nikiona kama maneno yale yalikuwa ni njama za kutaka kuivunja ndoa yangu.<br />
Mke wangu alikuwa mpole na wala hakuwa muongeaji kabisa, muda wote alikuwa kimya mpaka miye nianze kumsemesha.<br />
Niliificha siri ile moyoni mwangu japokuwa kuna wakati moyo ulikubali na wakati mwingine ulikataa kuamini kile kilichokuwa kikisemwa.<br />
Siku ya pili ilikuwani ni Jumatatu nilitakiwa kwenda kazini nilipanga kurudi mchana ili nishuhudie kile kinachosemwa kama ni kweli au la.<br />
Siku ya siku nilipofika kazini, nilisingizia kuumwa kwa vile sikuwahi kuomba ruhusa kutokana matatizo yoyote nilikubaliwa na kurudi nyumbani saa sita kasorobo mchana.<br />
Nilipofika nilikuta mlango ukiwa umefungwa, nilipiga simu ya mke wangu lakini haikuwa hewani. Nilizunguka upande wa pili nilimkuta mtoto wangu Zawadi akichezea matope bila kuwa na mtu yeyote wa kumwangalia.<br />
Nilibisha hodi chumba cha jirani, alitoka jirani yangu ilhali akiwa amepatwa na mshtuko mkubwa sana kwa kuniona muda ule.<br />
“Ha! Shemeji leo umerudi mchana?” alisema huku akimtoa Zawadi kwenye matope na dalili zote zikionesha kwamba kwa kipindi cha mchana, mtoto yule huwa anaachwa peke yake na tayari alikwisha kula kiasi kikubwa cha matope kutokana na mdomo ulivyoonesha.<br />
“Sijisikii vizuri,” nilimjibu kwa sauti ya chini huku roho ikiniuma kwa malezi mabaya aliyokuwa akipewa mwanangu.<br />
Hali ile ilianza kunipa picha ya maneno niliyoelezwa, jirani yangu mama Sonono alianza kumsafisha matope kisha aliingia ndani kwake na kutoka na ufunguo na kunipa huku akisema:<br />
“Shem naomba unitolee na nguo za Zawadi.”<br />
“Hakuna tatizo.”<br />
Niliingia ndani huku nikijiuliza mke wangu atakuwa amekwenda wapi, pia kama nisingekuja mwanangu angekula matope na kuwa mchafu mpaka saa ngapi. Baada ya kumtolea nguo nilimuuliza:<br />
“Mama Zawadi ameenda wapi?”<br />
“Amesema ameitwa na mama yake.”<br />
“Kila siku huwa anaitwa na mama yake?” Nilimshtukiza kwa swali ambalo nilijua hakulitegemea.<br />
“Siku nyingine huwa sijui anaenda wapi.”<br />
“Kwa hiyo akiondoka wewe ndiye unakuwa mlezi wake au siyo?”<br />
“Kwani vipi shem?”<br />
“Nakuuliza wewe ndiye mlezi wake, hebu angalia nimemkuta mtoto anakula matope, kwa siku zote anazoondoka kazi yako ni kumlisha mwanangu matope?” Nilimuuliza kwa hasira.<br />
“Ha...ha...pana shem.”<br />
“Niambie ukweli mke wangu amekwenda wapi maana nimetoka kwao?”<br />
“Si...si...jui akiondoka huniachia mtoto.”<br />
“Huwa anarudi saa ngapi?”<br />
“Jioni kabla hujarudi.”<br />
“Asante.”<br />
Nilimchukua mwanangu na kumpeleka kwa mama mzazi wa mke wangu na kumuuliza kama mke wangu alifika pale nyumbani kwake.<br />
Majibu yalikuwa ni tofauti na nilivyoelezwa, nilimuomba nimuachie mtoto. Alikubali kitu cha ajabu hakuniuliza swali lolote zaidi ya kumchukua mtoto.<br />
Nilirudi nyumbani kumsubiri mke wangu aniambie alikokuwa amekwenda.</span></div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><span style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 12.0pt; mso-fareast-font-family: "Times New Roman"; mso-fareast-language: DA;">MY WIFE....EP.5.<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
NILIMCHUKUA mwanangu na kumpeleka kwa mama mzazi wa mke wangu na kumuuliza kama mke wangu alifika kwake.<br />
Alijibu kuwa hajamuona, nilimuomba nimuachie mtoto. Alikubali kitu cha ajabu hakuniuliza swali lolote zaidi ya kumchukua mtoto. Nilirudi nyumbani kumsubiri mke wangu aniambie alikwenda wapi.<br />
SASA ENDELEA...<br />
Majira ya saa kumi na mbili na nusu mke wangu alirudishwa na gari, kwa vile nilishaelezwa muda wake wa kurudi, nilitoka na kukaa nje, ufunguo nilimpatia mama Sonono na kumwambia akija amwambie kuwa mtoto amechukuliwa na mama yake mzazi.<br />
Alipofika aliteremka na kukimbilia kwa mama Sonono kuulizia ufunguo.<br />
Baada ya muda nilimuona akitoka barabarani akiwa kama anayetafuta kitu, huku akiwa anapiga simu, baada ya muda gari lililomleta lilirudi.<br />
Kabla hajapanda kwenye gari nilijitokeza na kumwita.<br />
“Mke wangu.”<br />
Alishtuka kuniona mpaka simu ikamponyoka chini huku akisema kwa sauti kubwa:<br />
“Ha! Mume wangu!”<br />
“Vipi mpenzi ingia twende nina safari nyingine,” sauti kutoka ndani ya gari ilimhimiza aingie kwenye gari.<br />
“John nenda tu, mume wangu.”<br />
“Mumeo kafanya nini tena mpenzi?”<br />
“John ondoka mume wangu huyu hapa.”<br />
“He!” Sauti ilitoka kwenye gari na gari kuondoka kwa kasi bila kufunga mlango mmoja. Sikutaka kutaharuki nilimuuliza:<br />
“Unatoka wapi?”<br />
“Kwa mama.”<br />
“Yule nani?”<br />
“Bwana wa shoga yangu alinipa lifti.”<br />
“Mmh! Sawa.”<br />
“Vipi mbona mapema?”<br />
“Kawaida tu kwani kuna ubaya?”<br />
“Hakuna, Samahani mume wangu, nilikwenda kwa mama na kupishana naye huku nyuma alikuja na kumchukua Zawadi, nilikuwa naomba nimfuate.”<br />
“Sawa, hakuna tatizo, utanikuta.”<br />
Alisogea mbele na kukodi teksi iliyompeleka kwao, niliingia ndani nikiwa nimefura kwa hasira nikiwa siamini nilichokiona na kuanza kuamini yote niliyoelezwa juu ya uchafu wa mke wangu.<br />
Nilimsubiri kwa hamu kubwa arudi anieleze sababu ya kujifanya kondoo mwenye ngozi ya chui.<br />
Kitu cha ajabu mezani kulikuwa kumeandaliwa kila kitu kuonesha kwamba mke wangu kabla ya kuondoka hufanya kila kitu kwa ajili ya chakula cha jioni ili akirudi hata kama amechelewa chakula kionekane kuwa ni tayari.<br />
Miye nilipokuwa narudi niliamini kuwa mke wangu hakutoka kwa vile chakula kilikuwa kimeshatayarishwa.<br />
Nilikwenda hadi chumbani na kujilaza kitandani miguu ikiwa chini bila ya kuvua viatu, niliweka mikono kichwani huku macho yangu yakitazama juu nisiamini nilichokisikia, hata nilichokiona kwa macho yangu.<br />
Nilipatwa na mtikisiko wa moyo kwa mara ya kwanza tangu niwe na akili timamu japokuwa niliishawahi kuona na kusikia usaliti ndani ya ndoa za watu.<br />
Nikiwa katikati ya mawazo mke wangu alirudi akiwa na mtoto na moja kwa moja alikuja kukaa pembeni yangu huku akijichekesha.<br />
Nilijiuliza mama yake amemwambia nini kutokana na kuwa katika hali ya kawaida tu.<br />
“Vipi mume wangu?”<br />
“Poa.”<br />
“Mbona kama haupo sawa?”<br />
“Nipo sawa,” nilimjibu kwa sauti ya chini.<br />
“Hapana mume wangu lazima utakuwa na tatizo.”<br />
“Nipo sawa.”<br />
“Nakuja,” mke wangu alisema huku akinyanyuka na kwenda nje akimuacha mtoto pembeni.<br />
“Baba,” mwanangu Zawadi aliniita.<br />
“Mama,” nilipenda kumwita hivyo kwa kuwa alikuwa akitumia jina la mama yangu mzazi.<br />
“Pipi api?”<br />
“Nitakwenda kukununulia.”<br />
“Tende dukani baba kanunue pipi,” mwanangu alisema huku akijivuta kwangu na kunishika mkono, niliamua kumpelekea dukani.<br />
Nilimuangalia mwanangu na kujikuta nikitokwa na machozi ya uchungu, alizidi kunilazimisha ninyanyuke. Nilinyanyuka kitandani na kumbeba mpaka dukani ambako nilimnunulia pipi na biskuti.<br />
Wakati napita kurudi ndani nilimsikia mke wangu akizungumza na mama Sonono. Kwa jinsi walivyokuwa wakizunguza niliamini kabisa alijua bado nilikuwa chumbani.<br />
“Dada umeniangushia jumba bovu,” nilisikia sauti ya mama Sonono ikilalamika.<br />
“Jumba bovu vipi, kwani anajua nilikwenda wapi?”<br />
“Kurudi kwa mumeo kuna sababu, hata maswali yake yalionesha anajua mengi juu yako, hata mtoto kwa mama yako alimpeleka yeye.”<br />
“Wewee usiniambie!” sauti ya mke wangu ilionesha kushtuka.<br />
“Kweli, kabisa ila alinikataza nisikuambie.”<br />
“Jamani kwa nini umenigeuka?”<br />
“Sikuwa na jinsi nilihofia kupigwa na mumeo kwa jinsi alivyokuwa angeweza kumtafuna hata mtu.”<br />
“Akupige kwani wewe ndiye uliyetoka nje ya ndoa, wa kupigwa ni miye, kwanza jeuri hiyo ataitoa wapi?” mke wangu alizungumza kwa sauti ya kujiamini.<br />
Maneno yale yalionesha dhahiri kwamba mke wangu alifanya yote yale kwa vile alikuwa na kitu alichokuwa akikitegemea.<br />
“Dada ukitoka tena uondoke na mwanao sitaki ugomvi na mumeo, kwani ataona labda mimi ndiye ninayekufanyia mipango.”</span></div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><span style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 12.0pt; mso-fareast-font-family: "Times New Roman"; mso-fareast-language: DA;">MY WIFE....EP.6.<br />
<br />
<br />
LIPOISHIA;<br />
<br />
“Akupige kwani wewe ndiye uliyetoka nje ya ndoa, wa kunipiga ni mimi, kwanza jeuri hiyo aitoe wapi?” Mke wangu alizungumza kwa sauti ya kujiamini.<br />
Maneno yake yalionesha kabisa kuwa mke wangu alikuwa akifanya mambo yake huku akijua kuwa kulikuwa na kitu anachokitegemea.<br />
“Dada ukitoka tena uondoke na mwanao sitaki ugomvi na mumeo na ambaye anaweza kuona labda miye ndiye ninayekufanyia mipango.”<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Mi mtoto mdogo? Nitaondoka naye kwani kazi anafanya yeye? nitamuweka kwenye kochi kisha namaliza haja zangu, hilo shoga lisikupe shaka, basi baadaye.”<br />
Kwa vile ilikuwa giza mke wangu alitupita mimi na mwanangu bila ya kutuona na kuingia ndani.<br />
Nami niliingia ndani na kukutana naye mlangoni, aliponiona aliniuliza:<br />
“Vipi umetoka wapi?”<br />
“Dukani.”<br />
“Eti, kwani mume wangu leo umerudi saa ngapi?”<br />
“Kwani vipi?”<br />
“Nasikia umerudi mapema?”<br />
“Tatizo ni nini?”<br />
“Sasa umerudi mapema ili iweje?”<br />
“Sina ruhusa ya kurudi nyumbani kwangu mapema?”<br />
“Siyo hivyo.”<br />
“Sasa tatizo nini?”<br />
“Ujaji wako umeonekana umekuja kwa sababu.”<br />
“Ndiyo umekuja kwa sababu maalum.”<br />
“Sababu gani?”<br />
Nilijikuta nikipata nafasi ya kufungua yaliyo moyoni mwangu.<br />
“Niambie ulikwenda wapi?”<br />
“Kutembea.”<br />
“Kwa ruhusa ya nani?”<br />
“Nilisahau kukuaga naomba unisamehe kwa hilo.”<br />
“Aliyekurudisha ni nani?”<br />
“Ni rafiki wa shoga yangu.”<br />
“Naomba uniambie ukweli la sivyo leo nitakufanyia kitu kibaya sana,” nilimtisha.<br />
“Unataka kunifanyia kitu gani?” alishtuka.<br />
“Usiponieleza ukweli nitakufanyia kitu kibaya ambacho hutakisahau maisha mwako.”<br />
“Unataka ukweli gani mume wangu?” mke wangu aliingia woga.<br />
“Ninajua kila siku nitokapo nawe huku nyuma unatoka, huwa unakwenda wapi?”<br />
“Nani kakuambia?”<br />
“Si kujua aliyeniambia, bali ni wewe kunieleza ninapotoka nawe unatoka, unakwenda wapi?”<br />
“Waongo hao mi sijawahi kutoka, ni leo tu.”<br />
“Mama Zawadi naomba uniambie ukweli,” nilipandisha sauti.<br />
“Nilikwenda kwa shoga yangu na wakati wa kurudi mpenzi wake alinipa lifti kwenye gari lake.”<br />
“Huyu mtoto kakukosea nini?”<br />
“Kwa vipi?”<br />
“Mbona unamfanya kama yatima, kama unafanya uchafu wako basi mhurumie mtoto, unaridhika na hali ya mtoto ya kuteseka hivi?”<br />
“Nimemtesa kivipi?” majibu ya mke wangu hayakuonesha kushtushwa na hali ya mtoto wetu.<br />
“Kila ukiondoka unamwacha kwa mama Sonono mtoto hana matunzo, leo tu nimemkuta akila matope, kwani nini umekuwa mkatili kiasi hiki mke wangu?”<br />
“Mume wangu mtoto kuchezea matope ni kitu cha kawaida tu.”<br />
“Uchafu unaoufanya umesababisha mtoto aendelee kuteseka chini kama fundi majiko, au unataka azeeke akiwa amekaa?”<br />
“Mwanao mvivu tu wala si mimi.”<br />
“Taarifa zako za kumharibu mtoto kila mtu mtaani anazijua, wanamuonea huruma mtoto, ona miguu ilivyolegea kwa umalaya wako.”<br />
“Sawa mimi malaya, basi nipe talaka yangu.”<br />
“Tatizo si talaka bali kumuonea huruma mtoto.”<br />
“Mi si malaya naomba talaka yangu.”<br />
“Hapa talaka haitoki kuanzia leo mtoto atakaa kwa mama na siku nirudi halafu nisikukute utanitambua.”<br />
Kwa kweli mke wangu nilikuwa nampenda sana, sikumfanya lolote tulilimaliza kwa kuniomba msamaha kwa kuondoka bila kuaga lakini suala ya kutoka nje ya ndoa alilipinga kwa nguvu zote huku akiniuliza:<br />
“Lini tulipokutana kimwili ulikuta nimetumika? Mara nyingi mimi ndiye ninayekulazimisha kufanya mapenzi kama ningekuwa si mwaminifu kulikuwa na haja gani ya kulazimisha mapenzi kwako?”<br />
Kwa kweli sikuwa na jibu, kwa upande mwingine nilimuona kama mke wangu yupo sawa kutokana na tangu nimuoe hakuwahi kutoa udhuru kitandani. Tena kwa upande mwingine nilikuwa namuonea huruma kutokana na kazi zangu ambazo hunilazimu kurudi nikiwa nimechoka. Suala la mtoto kumpeleka kwa bibi yake alikubaliana nalo.<br />
***<br />
Maisha yaliendelea huku nikiamini kabisa kuwa mke wangu amejirekebisha, alipokuwa akitaka kutoka nyumbani alikuwa lazima aage ndipo atoke.</span></div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><span style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 12.0pt; mso-fareast-font-family: "Times New Roman"; mso-fareast-language: DA;">MY WIFE....EP.7<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA:<br />
<br />
Nilipotoka kazini nilikwenda sehemu aliyonielekeza na kushtuka kukuta amepanga kwenye nyumba ya gharama iliyokuwa ndani ya fensi, kitu kilichonipa wasiwasi na kujiuliza kama kodi aliyolipa mke wangu ikiisha nitaweza kuilipa. Mke wangu alinipokea kwa furaha.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
“Karibu mume wangu kwenye makazi mapya.”<br />
“Asante.”<br />
“Mbona kama unashangaa?”<br />
“Nashangaa kwa mambo mawili, kwanza nyumba nzuri sana na pili na wasiwasi kodi yake ni kubwa.”<br />
“Ni kweli kodi ni kubwa lakini ni sehemu nzuri tutakayoishi bila bughuza za watu.”<br />
“Nyumba yote kwa mwezi shilingi ngapi?”<br />
“Laki moja na nusu.”<br />
“Mke wangu laki moja na nusu kwa mwezi umelipa kwa muda gani?”<br />
“Mwaka mzima.”<br />
“Ndiyo shilingi ngapi?”<br />
“Hesabu unajua, zidisha laki na nusu mara kumi na mbili.”<br />
“Sasa mimi nitaweza kulipa fedha zote hizo?”<br />
“Nitakusaidia, kuwa na amani moyoni mwako.”<br />
Sikutaka kuhoji sana fedha zote hizo kazipata wapi, kwani Waswahili wana msemo wao kuwa ukimchunguza sana bata huwezi kumla na ukimchunguza sana mkeo hutaweza kuishi naye. Tuliyaanza maisha ya Uzunguni, sehemu waliyokuwa wakiishi watu wenye uwezo. Kwa kweli maisha ya makazi mapya yalikuwa mazuri sana yenye furaha na amani.<br />
Kwa muda mfupi, afya yangu ilirudi katika hali ya kawaida baada ya kuteseka kwa muda mrefu kutokana na vituko vya mke wangu. Kutokana na kuonesha mke wangu amejirekebisha tulimchukua mtoto wetu na kuishi naye. Heshima aliyoonesha ilimshtua hata mama yake mzazi.<br />
Maisha yalisonga mbele, mke wangu akashika ujauzito wa pili, kitu kilichozidi kunipa faraja moyoni mwangu. Lakini ilikuwa tofauti kwa upande wa pili, mke wangu hakupenda kubeba ujauzito kwa vile mtoto wetu alikuwa bado mdogo.<br />
“Mke wangu tatizo nini?”<br />
“Huoni Zawadi bado mdogo.”<br />
“Miaka mitatu si michache na mpaka unajifungua atakuwa amesogea sana.”<br />
“Kwa upande wangu nilipanga kuzaa baada ya Zawadi kufikisha miaka mitano.”<br />
“Basi bahati mbaya, itabidi uzae hivyohivyo.”<br />
“Siwezi, lazima niitoe hii mimba.”<br />
“Usiitoe mke wangu, Zawadi tutampeleka kwa bibi yake ili asipate shida.”<br />
“Bado nina hamu ya kumlea mwanangu, kama mtoto utapata tu muda ukifika,” mke wangu bado alishikilia msimamo wake.<br />
“Nakuomba usiitoe hiyo mimba, nipo chini ya miguu yako mke wangu,” nilimbembeleza mke wangu mpaka nikampigia magoti.<br />
“Kwa hilo siwezi kukusikiliza, sihitaji senti tano yako, nitatoa kwa fedha zangu.”<br />
Kwa mara nyingine mke wangu alinizidi nguvu, nikamkubalia kwa shingo upande. Siku ya pili nikiwa kazini, majira ya saa tisa alasiri, mke wangu alinipigia simu kunijulisha kuwa amefanikiwa kuitoa mimba salama. Nilimkubalia lakini upande wa pili moyo uliniuma sana, hata kazi ilinishinda na kwenda sehemu ya peke yangu ambapo nililia sana kumpoteza mwanangu mtarajiwa.<br />
Jioni niliporudi, nilimkuta mke wangu nyumbani, hali yangu ya unyonge ilimshtua mke wangu na kunifuata nilipokuwa nimekaa, akawa ananibembeleza.<br />
“Mume wangu, najua kiasi gani nilivyokuumiza lakini sikuwa na jinsi, nilifanya vile kwa maana kubwa. Kwa sasa ni vigumu kunielewa lakini amini nilichokifanya si kukukomoa bali kumpa nafasi Zawadi. Kumbuka makosa yangu ya awali yalimtesa mwanangu hivyo sasa hivi nina deni la kumlea.”<br />
Kutokana na kumpenda sana mke wangu, nilikubaliana naye. Maisha yalisonga huku akionesha mapenzi mazito kwangu, kitu kilichofuta mawazo ya kutoa ujauzito.<br />
Siku zote kimya kingi kina mshindo mkuu. Mwezi mmoja baada ya kutoa ujauzito, asubuhi moja nilidamka kwenda kazini huku hali yangu kiafya ikiwa si nzuri.<br />
Nilijitahidi kwa kuamini mwanaume si mtu wa kujilegeza. Nilipofika kazini, nilijitahidi kufanya kazi lakini kutokana na kufanya kazi juani, hali yangu ilibadilika na kuwa mbaya hivyo niliruhusiwa kwenda hospitali kupata matibabu.<br />
Nilikwenda hadi hospitali ya wilaya na kupata huduma japo dawa nilikwenda kununua duka la kuuza dawa. Nilibeba dawa zangu na kurudi nyumbani kupumzika. Nilipofika nyumbani, ndani ya geti nilikuta kuna gari ambalo kwangu halikuwa geni sana japo sikukumbuka nililiona wapi.<br />
Baada ya kutafakari, niligundua lile gari ndilo lililomshusha mke wangu, nikashtuka kulikuta nyumbani kwangu na kujiuliza limefuata nini pale. Niliingia ndani na kukuta sebuleni kuna pombe kali juu ya meza na glasi mbili.<br />
Sikujishughulisha navyo, nilielekea chumbani, nilipofika kwenye mlango wa chumbani, nilikuta umefungwa kwa ndani, nikasikia sauti mbili ya mwanamke na mwanaume. Sauti ya mwanamke ilikuwa ya mke wangu ya kiume sikujua ni ya nani. Kwa haraka nilitoka mpaka nje na kuzunguka dirishani na kuchungulia ndani.</span></div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><br />
</div><div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0cm;"><span style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 12.0pt; mso-fareast-font-family: "Times New Roman"; mso-fareast-language: DA;">MY WIFE....EP.8.<br />
<br />
<br />
ILIPOISHIA;<br />
<br />
MLANGO nilirudisha na kuzima taa ya sebuleni na kukaa kwenye kochi ili kumsubiri mke wangu ambaye sikujua atarudi muda gani.<br />
Mpaka muda ule ilikuwa ni saa saba na nusu za usiku.<br />
SASA ENDELEA...<br />
<br />
Nilijitahidi kukaa macho ili mke wangu akirudi na kugonga, niweze kumuona. Kuna kipindi nilipitiwa na usingizi niliposhtuka nilitoka mpaka nje kuangalia kama labda nitamuona mke wangu akiwa amerudi na kuniita na kushindwa kumsikia.<br />
Nilizunguka nyumba nzima bila kumuona mke wangu na kurudi tena sebuleni kumsubiri.<br />
Siku ya pili ilinikuta nikiwa bado nipo sebuleni nikimsubiri mke wangu, nikiwa najiandaa kwenda chumbani, mke wangu aliingia akionesha amekunywa pombe kitu ambacho hakuwahi kukifanya katika maisha yake yote niliyomjua na nywele zake zilikuwa timtim.<br />
“Ooh! Mume wangu, habari za asubuhi?”<br />
“Nzuri, habari za wapi?”<br />
“Nilikwenda kwa mama wakati narudi shoga yangu alinipigia simu kuwa kuna harusi ya ndugu yake. Nilijua nitawahi kurudi kumbe sherehe ni sherehe kuja kushtuka muda umekwenda na usafiri ulikuwa wa tabu nikaamua kulala huko huko.”<br />
“Kwa nini hukunipigia simu?”<br />
“Wakati unanipigia simu ilizimika hata kabla sijakujulisha.”<br />
“Na mbona umekunywa pombe, umeanza lini?”<br />
“Mume wangu sherehe ina vishawishi vingi, lakini sikunywa sana.”<br />
Nilijikuta kwa mara nyingine nikishindwa kumhukumu mke wangu, niliamua kumsamehe kwa vile nilikuwa nampenda sana. Ila nilimuomba asiondoke nyumbani bila kuaga pia asiwe anakunywa pombe.<br />
Mke wangu kama kawaida yake aliniomba msamaha na kuniahidi kuwa hataweza kuondoka bila ya kuaga, pia hatarudia tena kunywa pombe.<br />
Nilimsamehe mke wangu kwa vile nilikuwa nampenda sana na sikutaka kumpoteza maishani mwangu kwa kuamini kuwa yeye ni kila kitu kwangu.<br />
Baada ya tukio lile mke wangu alitulia na heshima ya ndoa ikarudi ndani kama kawaida.<br />
Wakati huo mtoto wetu alikuwa amekazana kutembea, kwa kitendo cha mwanangu kutembea niliwashukuru sana majirani. Wiki moja baada ya tukio la mke wangu kulala nje aliniomba tuhame mtaa ule.<br />
“Mume wangu naomba tuhame hapa.”<br />
“Tuhame hapa twende wapi?”<br />
“Sehemu yoyote lakini mbali na hapa.”<br />
“Kodi si itatusumbua?” Nilimwambia kwa kuwa hali yangu ya kiuchumi aliijua.<br />
“Mume wangu unafanya kazi, acha kujilegeza, inatakiwa sasa hivi tuishi maisha ya kwetu wenyewe bila kuwategemea watu,” yalikuwa maneno ya kweli lakini yalitakiwa maandalizi ya muda mrefu hasa nikizingatia kulipa kodi ya miezi sita kwa haraka ulikuwa mtihani mkubwa kwangu.<br />
“Lakini mbona mama alisema hii ni nyumba yako amekupa baada ya kuoana?” Ilibidi nihoji baada ya mke wangu kulazimisha kuhama.<br />
“Kazala, husikii tunavyosimangwa kuhusu hii nyumba, hasa wewe mume wangu maneno yao kwa kweli huwa yananiumiza sana pale wanapokusema vibaya eti nimekuoa badala ya kunioa, hayo ni maneno gani mume wangu?”<br />
“Mmh! Sina jinsi kwa vile ni haraka sana, nipe wiki nijaribu kukopa kazini ili tutafute nyumba.”<br />
“Kuhusu kodi ya kuanzia nitalipa mimi itakayofuata utalipa wewe.”<br />
“Hakuna tatizo,” nilikubaliana naye bila kuhoji fedha ataitoa wapi kwa kuhofia kubadili uamuzi wake.<br />
Siku ya pili nilipokwenda kazini mke wangu alinipigia simu na kunijulisha kuwa amekwisha hamisha kila kitu na kunielekeza nikitoka kazini niende sehemu alipo na siyo pale tena.<br />
Nilipotoka kazini nilikwenda sehemu aliyonielekeza na kushtuka kukuta amepanga kwenye nyumba ya gharama iliyokuwa imo kwenye uzio, kitu kilichonipa wasiwasi na kujiuliza kama kodi aliyolipa mke wangu ikiisha nitaweza kulipa. <br />
<br />
ITAENDELEA JUMAMOSI IJAYO....</span></div><div class="MsoNormal"><br />
</div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-65716233232193905042012-07-21T09:00:00.001-07:002012-07-21T09:00:34.279-07:00Usithubutu ‘kufeki’, penzi bora hujitengeneza lenyewe Part -2.<a href="http://alongoa-alongo.blogspot.com/2012/07/wema-wolper-waanza-upya.html?spref=bl"></a><br />
<h1> <span style="font-size: large;">Usithubutu ‘kufeki’, penzi bora hujitengeneza lenyewe Part -2.</span></h1><span style="font-family: arial,helvetica,sans-serif;"><a href="http://us.123rf.com/400wm/400/400/keeweeboy/keeweeboy1002/keeweeboy100200133/6419286-loving-black-couple.jpg" rel="nofollow" target="_blank"><img class="align-center" src="http://us.123rf.com/400wm/400/400/keeweeboy/keeweeboy1002/keeweeboy100200133/6419286-loving-black-couple.jpg?width=650" width="650" /></a></span><br />
<div style="text-align: justify;"> <b><span style="font-size: medium;"><b>Bila shaka wasomaji wangu wote ni wazima wa afya na mnaendelea na majukumu yenu. Tunaendelea na mada yetu kuanzia pale tulipoishia.</b></span></b></div><div style="text-align: justify;"> <b><span style="font-size: medium;"><b>Twende pamoja...</b></span></b></div><div style="text-align: justify;"> <b><span style="font-size: medium;">MZEE Nelson Mandela ‘Madiba’, alitoa talaka kwa bibi yetu, Winnie. Waliishi miaka mingi, wakazaa watoto ambao wengine kwa sasa ni wakubwa kabisa. Baadaye akagundua Winnie si bahati yake, leo yupo kwenye ndoa na Graca Machel, maisha yanaendelea.<br />
Kumbe Graca ndiye bahati ya Mzee Mandela. Ilivyo ni kwamba Winnie alitangulia kwa lengo la kukamilisha safari ya maisha ya babu yetu huyo anayeheshimiwa mno duniani. Chukua mfano huo, halafu jipe matumaini. Maisha ni matamu mno bila ya huyo wako ambaye si bahati yako.<br />
Napenda tena nitie mkazo kwamba mapenzi ni magumu. Kama Mandela yalimuumiza, inashindikana vipi kwako? Ukimpata wa bahati yako, hata uwe maskini unaweza kung’ara na maisha yako yakatawaliwa na faraja, ila ukitumbukia sehemu ambayo si yako, ni mateso ya moyo na sononeko lisilokwisha.<br />
Hapa nifafanue kuwa yule ambaye anajiona yupo kwenye uhusiano salama, basi aendelee hapohapo kwa sababu ndipo kwenye bahati yake. Kwa wale wenye maumivu pale walipo, basi wajiangalie mara mbilimbili. Maisha yanaendelea. Maisha bora yanajengwa na mtu mwenye akili iliyotulia.<br />
Huwezi kuwa na matatizo, akili haitulii kwa sababu ya misukosuko ya kimapenzi, ukadhani kwamba utajenga maisha imara. Hapo utakuwa unajidanganya. Tibu kwanza janga lako la mapenzi ili maisha yako yanyooke. Ikiwezekana, jipe muda wa kukaa ‘singo’. Inawezekana.<br />
Beba zingatio kuwa lipo kundi la watu wanaowachezea wenzi wao lakini maisha yao ya kimapenzi bado ni imara. Japo anayetendwa ni maumivu kwake, ila mtendaji ni sawa tu. Haumii, anamnyanyapaa mwenzi wake na anaendelea kupendwa. Ni bahati tu.<br />
Wewe unasaga miguu na kuumiza kichwa. Kila siku unajitahidi kumtafuta mwenzi bora wa maisha yako lakini hujampata. Badala ya furaha, unavuna machungu mtindo mmoja. Usijione una bahati mbaya, badala yake endelea kuitazama mbele kwa matumaini.<br />
Huyo huelewani naye kwa sababu siyo wa bahati yako. Wako yupo na bahati mbaya hujamfikia. Jambo la kufanya si papara, kuwa mtulivu, utampata kwa urahisi. Ukijifanya bingwa wa kuwapanga na kuwapangua, hutafanikiwa, matokeo yake utampita na mwenzi bora wa maisha yako bila kujua.<br />
Penda kutazama mifano kwa walio karibu yako. Je, wanaishi vipi na wenzi wao? Kama nao picha haziendi, tambua kwamba wanalazimishana. Watu wanaopendana, haiwezekani kila siku wakawa wanasumbuliwa na migogoro. Kuna mawili, moja litakuwa sahihi.<br />
Mosi; wote hawapendani ila walijikuta wapo pamoja kwa mvuto wa tamaa za mwili, nao wakajidanganya ni mapenzi, hivyo wakawa pamoja. Pili; kama mosi haikuwa sahihi, basi itakuwa mmoja anapenda, mwingine analeta utani, hivyo kufanya misuguano isiyoisha.<br />
Mapenzi yana nguvu yenye mvutano mithili ya sumaku. Hoja hapa ni kuwa endapo kutakuwa na mapenzi ya kweli, mara nyingi mtajikuta mpo kwenye mstari mmoja, kwani kuna nguvu ya asili ambayo hamuioni, inayowaweka pamoja muda wote. Ni nadra kutofautiana.<b>,,itaendelea........</b></span></b></div><div class="tb"> </div><div class="tb"> <b style="color: red;"><span style="font-size: medium;">Usithubutu ‘kufeki’, penzi bora hujitengeneza lenyewe..t...PART.1</span></b><br />
<div class="tb"> </div><a href="http://yvonnesliteratureblog.files.wordpress.com/2010/04/sexy.jpg" rel="nofollow" target="_blank"><img class="align-center" src="http://yvonnesliteratureblog.files.wordpress.com/2010/04/sexy.jpg?width=450" width="450" /></a><br />
<div style="text-align: justify;"> <b><span style="font-size: medium;">YALIANZA kuumbwa maisha halafu mapenzi ndiyo yakafuata. Aliumbwa Adam, baadaye akaletewa Hawa kisha mapenzi ndiyo yakaanza. Hii ina maana kuwa maisha yalianza kwa upande wa Adam kabla ya mapenzi. Hili zingatia katika kutafsiri sura ya kule uendako maishani.<br />
Hata wewe jiulize, ulipozaliwa ulikuwa hujui mapenzi ni nini? Hapa sizungumzii mapenzi ya kawaida, yale ambayo mtu anaweza kuyapata kutoka kwa wazazi wake au ndugu zake wengine. Yanayotajwa hapa ni mapenzi katika maana yake halisi. Mapenzi ya ndani kabisa.<br />
Yale ambayo huwafanya watu waziache familia zao za asili na kwenda kutengeneza nyingine. Nayazungumzia yale ambayo yanawafanya watu wanauana, wengine wanakunywa sumu. Yanayowatesa watu mpaka wanashindwa kula na kadhalika. <br />
Swali ni moja; Kama iliwezekana kuishi bila mapenzi mpaka ulipofikisha umri wa utu uzima, iweje leo yakutawale mpaka ushindwe kujiendesha mwenyewe? Haipingiki kwamba mapenzi ni muhimu lakini hayapaswi kutawala ubongo wako. Utafeli haraka.<br />
Mapenzi ni mazuri kwako endapo utaweza kuyamudu. Yakikushinda wewe ni mtumwa. Kaa, tuliza akili halafu tafakari. Baada ya hapo chukua hatua. Haijalishi umeshaathirika kiasi gani, muhimu kwako ni kuzingatia kwamba inawezekana kubadilika.<br />
Japo unapenda mno, unajitahidi kuonesha unajali katika mazingira yoyote. Umemfanya mwenzako sawa na mboni yako kwa namna unavyomtunza. Kama yeye harudishi mapenzi unayompa, hajali na kukupa heshima kulingana na ile unayompa, angalia maisha yako kwanza.<br />
Angalizo; Ukimng’ang’ania sana, atakugeuza punda. Atajipa kiburi kwamba anaweza kufanya lolote nawe utatii kwa sababu unampenda. Usidanganywe na imani zisizokuwepo, binadamu hawekwi kiganjani wala kwenye chupa. Una akili hai, tazama mbele pengine hapo si kwenye bahati yako.<br />
Kama anashindwa kukuthamini kwa namna unavyompenda, hawezi kuyapenda maisha yako. Atakutumia atakavyo, akishatimiza malengo yake, atakuacha ukihangaika na dunia. Wakati huo yeye yupo na mtu wake anayempenda, atakuwa anakucheka.<br />
Akikaa na marafiki zake, atawaambia kwamba yeye ndiye alikuwa nyota yako, kwamba ulipokuwa naye maisha yako yalikuwa rahisi na hivi sasa umechoka baada ya kuachana naye. Hatazungumza jinsi alivyokutesa, akakuweka roho juu, akakusababishia maumivu ya moyo mpaka ukashindwa kutekeleza majukumu yako.<br />
Usikubali muda wako upotee bure. Maisha yako ni ya thamani, yupo nawe leo lakini kesho inawezekana si wa kwako. Lakini maisha yatabaki kuwa yako kwa mazingira yoyote yale. Hoja yangu hapa ni kwamba mapenzi yasikutawale mpaka ukasahau maisha.<br />
Wengi waliishia njiani, walijiaminisha wanapendana kutoka ndani ya kuta za nyoyo zao. Wakaahidiana kuwa hakuna kitakachowatenganisha. Siku yalipotimia, ahadi zote zikayeyuka. Hupaswi kung’ang’ania ulipo, bali yafaa ujiulize, je, hapo ndipo kwenye bahati yako?<br />
Watu kwenye ndoa wameachana, si kwamba walipenda la hasha! Wachumba wanaishia njiani, vilevile marafiki walioamini wanachanua, wakapeana mkono wa kwa heri. Ni vizuri kukubali kwamba jitihada hazishindi kudura. Pamoja na mapenzi yako makubwa, unavyojali, unavyomheshimu kama si bahati yako hamuwezi kudumu.<br />
Haijalishi utu wako ni wa thamani kiasi gani.</span></b></div></div><div class="tb" style="text-align: justify;"> </div><div class="tb"> </div><div class="tb"> <b style="color: red;"><span style="font-size: medium;">NI KOSA KUMWAMBIA MPENZI WAKO MUWAPO FARAGHA KUWA ''UMECHOKA''</span></b><b><span style="color: red; font-size: medium;">........PART .1</span></b>.</div><a href="http://cdn.sheknows.com/articles/couple-smiling-in-bed.jpg" rel="nofollow" target="_blank"><img class="align-center" src="http://cdn.sheknows.com/articles/couple-smiling-in-bed.jpg" /></a><br />
<b><span style="font-size: medium;">TUNAENDELEA kuyajadili mapenzi. Kuna vitu vingi ambavyo vinasababisha uhusiano wa wengi kudumu. Maelewano, kusikilizana, kuheshimiana na mengineyo, lakini unyumba ni chachandu yenye nguvu. Nimekuwa nikiwashauri wasomaji wangu vitu vingi lakini hili nimeteua nilichambue kwa ufafanuzi leo.<br />
Kuna watu ambao wamekuwa hodari kujisifu kuwa wao hutoa unyumba kwa ‘kibaba’. Yaani huwapimia wenzi wao. Kwa mitazamo yao, hujiona wapo sahihi. Tabia hii ipo kwa wanawake zaidi, japo kuna wanaume ambao nao ni wagumu kutekeleza mahitaji ya wapenzi wao.<br />
Hata hivyo, kuna kitu cha kuweka sawa hapa; Wakati mwanamke anapobana ‘staftahi’ kwa mwenzake, huhesabika ni mchoyo! Kwa mwanaume yeye huonekana ni goigoi. Kwamba mambo hayawezi ndiyo maana hatekelezi shughuli. Ataambiwa ana tatizo la zile nguvu zetu!<br />
Mwanamke anaweza kujisifu hata kwa wenzake. Akiwa kwenye vikao vya kusukana au katika soga nyingine, atajimwagia sifa tele kwamba yeye inaweza kupita miezi bila kuingia uwanjani na mwenzi wake. Hili, linawafanya wanaume wengi wateseke na matokeo yake hutafuta tiba mbadala.<br />
Mwanaume hawezi kujisifu kwa marafiki zake kuwa yeye huwa akisumbuliwa na mwenzi wake, humpa mgongo! Ni wazi akisema hivyo atachekwa. Yaani mwanamke kugomea kutoa unyumba ni ushujaa wakati mwanaume akikataa, atachukuliwa kwamba ana tatizo la kiafya! Dhana hii sikubaliani nayo, kwahiyo nahitaji kutoa shule!<br />
Kwangu mimi, kila aliye mvivu wa kuingia shughulini ana tatizo! Kwa mwanaume na mwanamke, wote wana kasoro ya nguvu, kwa maana hiyo wanahitaji tiba mbadala ili waweze kusherehekea tendo. Wanatakiwa kuboresha mvuto wao katika ndoa au uhusiano, na nafasi ya kutekeleza hilo ipo!<br />
Ni lazima watu waheshimu uhusiano wao wa kimapenzi. Pia waelewe kwamba moja kati ya vitu vinavyoshikilia penzi lao ni unyumba. Ni wakati muafaka kwako sasa, kuachana na mawazo ya kale. Punguza uvivu na ujue kuwajibika inavyotakiwa, kwa maana ni njia ya kutibu amani yako mwenyewe na mwenzio.<br />
Utafiti unaonesha kwamba asilimia kubwa ya ndoa zinazovurugika kila siku, nyuma yake huwa na shambulio la wanandoa kutopeana huduma ya tendo. Kwamba, wanavumiliana lakini mwisho sauti itasikika kwa majirani. Watakapokuwa wanagombezana usiku, siri hugeuka sirini.<br />
Tendo la ndoa, hukamilisha furaha ya wawili walioamua kupendana. Tunapoamua kuacha siasa na kuzingatia ukweli kwa vipimo vyake, watu wengi (hasa wanaume), wanapoingia kwenye uhusiano wa kimapenzi, lengo lao la kwanza ni kutimiza haja zao kimwili kwa mtu husika. Nazungumza kwa utafiti!<br />
Walikutana barabarani, akavutiwa ndiyo maana akaanza misele. Anapofanikiwa, vikwazo vya baadaye, inakuwa siyo matarajio yake. Alichotarajia ni kwamba baada ya kukubaliana kuingia kwenye sehemu yenu ‘spesho’, atakuwa hapimiwi! Kwa kiwango chochote atakachohitaji, mwenzi wake atamridhia.<br />
Aghalabu, wapenzi ambao wanajikuta wapo kwenye mgogoro wa tendo, mara nyingi hukabiliwa na tatizo la usaliti. Ni theluthi moja ya wanawake wanaoweza kumvumilia mwanaume ambaye hamtoshelezi kimwili, wakati kwa wanaume ni moja ya kumi tu ndiyo wenye kuvuta subira mpaka siku watakapokumbukwa.<br />
“Huyu mbona yupo hivi, kila siku anasema kachoka, atakuwa na mtu huko nje,” ni kauli ambayo ni rahisi kupita kichwani kwa mwanamke, pale ambapo anakabiliana na mwenzi ambaye haguswi chochote na tamaa za mwili, ingawa inaelezwa kwamba ni moja ya kumi ya wanawake ndiyo hukosa usingizi kwa kunyimwa tendo.itaendelea......</span></b>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-2904902086023626002012-07-16T03:14:00.001-07:002012-07-16T03:14:16.442-07:00GETSUGA THE GREAT´S STATISTIK "VIDEO"<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><br />
<iframe allowfullscreen='allowfullscreen' webkitallowfullscreen='webkitallowfullscreen' mozallowfullscreen='mozallowfullscreen' width='320' height='266' src='https://www.blogger.com/video.g?token=AD6v5dyGcOIQrWYUTwg4v63BX-CypugfNOPggM52z7igkk9cfIKpUzoaFUedbTQawIHnNjcmJkvK6pNzSSDFSopZSA' class='b-hbp-video b-uploaded' frameborder='0'></iframe></div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-16562240250686113952012-07-16T02:27:00.001-07:002012-07-16T02:27:40.808-07:00Watu wenye tabia hii husababisha mapenzi kuwa magumu-3<strong><a href="http://www.psychologies.co.uk/wp-content/uploads/2011/01/test-sexuality.jpg" rel="nofollow" target="_blank"><img class="align-center" src="http://www.psychologies.co.uk/wp-content/uploads/2011/01/test-sexuality.jpg?width=650" width="650" /></a></strong><br />
<strong>Na:Luqman Maloto</strong><br />
Bila shaka msomaji upo safi na unaendelea na majukumu ya ujenzi wa taifa. Tunaendelea na mada yetu kuanzia pale tulipoishia wiki iliyopita. Twende pamoja...<br />
Kundi hilo ndilo linatajwa kwamba wahusika wake hawajatulia.<br />
Hata hivyo, upo ukweli uliotimia kuwa mitaani kwa jamii ya watu wa kawaida, wapo wachafu kuliko. Mwanamke mmoja anaweza kuwapanga wanaume watano kwa siku. Akitoka huyu anakwenda kwa mwingine. Anabadili nyumba za kulala wageni.<br />
Huyu, hajitambulishi kama changudoa. Atasimama pembeni na kwamba yeye ni mtu mwenye heshima zake. Akiwaona machangudoa usiku wa manane wakiwa wamejipanga mawindoni na mavazi yao ya nusu uchi, atawalaani. Ni msemo wa nyani haoni makalioni kwake!<br />
Huko nyuma nilishawahi kueleza mfano wa wanandoa kusalitiana. Nikabainisha kwamba baadhi ya wanaume hufanya makosa pale wanapowakataza wanawake wao kufanya kazi. Eti wanataka wakae tu nyumbani. Hapa ndiyo kuna jambo, kwani mtu anapokaa bila kazi, hukaribisha hisia za karibu.<br />
Hii ikanifanya nijenge hoja kutokana na muongozo wa kisaikolojia kwamba akina mama wa nyumbani, ni kundi hatari mno kusaliti ndoa. Mara nyingi wanakuwa hawapo bize, kwa hiyo hisia za kimapenzi zinakuwa karibu na matokeo yake hujikuta wakifanya zinaa na watu wa kushangaza.<br />
Hujawahi kusikia mke wa mtu katembea na ‘houseboy’ wake? Vipi mwanamke kufanya zinaa na mdogo wa mume wake? Je, muuza bucha kujilia vyake nyakati za mchana kwa ofa za robo ya nyama anayomuongezea mke wa mtu aliyekwenda kununua kilo mbili? Hayo yapo kwenye mazingira yetu ya kila siku.<br />
Kila siku wauza magenge na maduka, wanaingilia ndoa za watu. Nafasi hizo wanazipata kwa sababu ya kutokuwepo ubize kwa wanawake hao. Asili yetu tunapenda utani, hivyo wakitaniana mara mbili, mwanamke anahama kihisia. Keshokutwa asubuhi mume akiondoka, huyo anakimbilia gengeni.<br />
Huu ni mfano katikati ya mada yetu. Mtu wa aina hii akiwaona machangudoa barabarani, atawalaani kupita kiasi. Hata hivyo, mtindo wa maisha yake hauna tofauti na changudoa kutokana na ukweli kwamba mtu mwenye staha na heshima, hawezi kujilimbikizia vidumu. Mume usiku, mchana muuza bucha au houseboy, haijakaa vizuri.<br />
Inabidi kutoa mfano wa aina hii kutokana na ukweli kwamba masistaduu wanaweza kukaa vibarazani na kusogoa kuwa mbona wake za watu wanaojionesha ni watu makini, nao wanacheza sana mechi za nje?Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-84242846153062038262012-07-16T02:23:00.001-07:002012-07-16T02:23:50.153-07:00Usithubutu ‘kufeki’, penzi bora hujitengeneza lenyewe -2<span style="font-family: arial, helvetica, sans-serif;"><a href="http://us.123rf.com/400wm/400/400/keeweeboy/keeweeboy1002/keeweeboy100200133/6419286-loving-black-couple.jpg" rel="nofollow" target="_blank"><img class="align-center" src="http://us.123rf.com/400wm/400/400/keeweeboy/keeweeboy1002/keeweeboy100200133/6419286-loving-black-couple.jpg?width=650" width="650" /></a></span><br />
<strong>Bila shaka wasomaji wangu wote ni wazima wa afya na mnaendelea na majukumu yenu. Tunaendelea na mada yetu kuanzia pale tulipoishia.</strong><br />
<strong>Twende pamoja...</strong><br />
MZEE Nelson Mandela ‘Madiba’, alitoa talaka kwa bibi yetu, Winnie. Waliishi miaka mingi, wakazaa watoto ambao wengine kwa sasa ni wakubwa kabisa. Baadaye akagundua Winnie si bahati yake, leo yupo kwenye ndoa na Graca Machel, maisha yanaendelea.<br />
Kumbe Graca ndiye bahati ya Mzee Mandela. Ilivyo ni kwamba Winnie alitangulia kwa lengo la kukamilisha safari ya maisha ya babu yetu huyo anayeheshimiwa mno duniani. Chukua mfano huo, halafu jipe matumaini. Maisha ni matamu mno bila ya huyo wako ambaye si bahati yako.<br />
Napenda tena nitie mkazo kwamba mapenzi ni magumu. Kama Mandela yalimuumiza, inashindikana vipi kwako? Ukimpata wa bahati yako, hata uwe maskini unaweza kung’ara na maisha yako yakatawaliwa na faraja, ila ukitumbukia sehemu ambayo si yako, ni mateso ya moyo na sononeko lisilokwisha.<br />
Hapa nifafanue kuwa yule ambaye anajiona yupo kwenye uhusiano salama, basi aendelee hapohapo kwa sababu ndipo kwenye bahati yake. Kwa wale wenye maumivu pale walipo, basi wajiangalie mara mbilimbili. Maisha yanaendelea. Maisha bora yanajengwa na mtu mwenye akili iliyotulia.<br />
Huwezi kuwa na matatizo, akili haitulii kwa sababu ya misukosuko ya kimapenzi, ukadhani kwamba utajenga maisha imara. Hapo utakuwa unajidanganya. Tibu kwanza janga lako la mapenzi ili maisha yako yanyooke. Ikiwezekana, jipe muda wa kukaa ‘singo’. Inawezekana.<br />
Beba zingatio kuwa lipo kundi la watu wanaowachezea wenzi wao lakini maisha yao ya kimapenzi bado ni imara. Japo anayetendwa ni maumivu kwake, ila mtendaji ni sawa tu. Haumii, anamnyanyapaa mwenzi wake na anaendelea kupendwa. Ni bahati tu.<br />
Wewe unasaga miguu na kuumiza kichwa. Kila siku unajitahidi kumtafuta mwenzi bora wa maisha yako lakini hujampata. Badala ya furaha, unavuna machungu mtindo mmoja. Usijione una bahati mbaya, badala yake endelea kuitazama mbele kwa matumaini.<br />
Huyo huelewani naye kwa sababu siyo wa bahati yako. Wako yupo na bahati mbaya hujamfikia. Jambo la kufanya si papara, kuwa mtulivu, utampata kwa urahisi. Ukijifanya bingwa wa kuwapanga na kuwapangua, hutafanikiwa, matokeo yake utampita na mwenzi bora wa maisha yako bila kujua.<br />
Penda kutazama mifano kwa walio karibu yako. Je, wanaishi vipi na wenzi wao? Kama nao picha haziendi, tambua kwamba wanalazimishana. Watu wanaopendana, haiwezekani kila siku wakawa wanasumbuliwa na migogoro. Kuna mawili, moja litakuwa sahihi.<br />
Mosi; wote hawapendani ila walijikuta wapo pamoja kwa mvuto wa tamaa za mwili, nao wakajidanganya ni mapenzi, hivyo wakawa pamoja. Pili; kama mosi haikuwa sahihi, basi itakuwa mmoja anapenda, mwingine analeta utani, hivyo kufanya misuguano isiyoisha.<br />
Mapenzi yana nguvu yenye mvutano mithili ya sumaku. Hoja hapa ni kuwa endapo kutakuwa na mapenzi ya kweli, mara nyingi mtajikuta mpo kwenye mstari mmoja, kwani kuna nguvu ya asili ambayo hamuioni, inayowaweka pamoja muda wote. Ni nadra kutofautiana.Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-90228536335325972562012-07-15T11:43:00.001-07:002012-07-15T11:43:26.522-07:00HISIA NZURI AFYA YA MOYO<span class="hasCaption">Hisia nzuri ni afya ya moyo<br />
<br />
Utafiti uliofanywa na wataalamu wa Marekani umebaini kuwa wanawake wanaoishi kwa matumaini hupunguza uwezekano wa maradhi ya moyo.<br />
<br />
Utafiti wa hivi karibuni wa watafiti wa Marekani unakariri utafiti wa awali uliofanywa na kundi la wataalamu wa Uholanzi ukionyesha kupungua kwa uwezekano wa hatari ya magonjwa ya moyo kwa wanaume.<br />
<span class="text_exposed_show"> Taarifa zinazohusiana<br />
<br />
<br />
Utafiti uliofanywa kwa kutumia wanawake laki moja,ulichapishwa katika jarida la kisayansi, uligundua kuwa watu wanaoishi kwa hofu walipatikana kua na shinikizo la damu pamoja na kolestroli au kupungua kwa njia za damu katika mishipa.<br />
<br />
Pamoja na hayo hisia za mtu kama tabia ya chuki kwa wengine pia yanabadili hali ya afya.<br />
<br />
Wanawake wenye matarajio mema wana asili mia 9% ya kupatwa na magonjwa ya moyo na asili mia 14% ya kuuawa kwa magonjwa yenye uhusiano wa maradhi ya moyo.<br />
<br />
Wanawake wa aina hiyo walilinganishwa na wengine ambao huishi kwa kinyongo, chuki na kijicho kwa wenzao kimawazo au kwa ujumla kuwashuku wenzao. Hawa wana asili mia 16% kufariki katika kipindi kifupi kuliko wanaoishi kwa matumaini makubwa ya kufanikiwa.<br />
<br />
Uwezekano mkubwa uliopo ni kwamba mtu anayeishi kwa matumaini huwa na uwezo wa kukabiliana na mitihani ya kimaisha, mfano wa kukidhi mahitaji yao wanapoumwa.<br />
<br />
Utafiti huu ulionelea kuwa wanawake wanaofanya mazowezi mara nyingi walikuwa wembamba kuliko wenzao wanaoishi na kinyongo.<br />
<br />
Mchunguzi mkuu Dr Hilary Tindle, naibu profesa wa dawa katika Chuo kikuu cha Pittsburgh, alisema kua ushahidi mwingi tulioupata unaonyesha kua muendelezo kwa kiwango kikubwa cha fikra za kutojiamini ni hatari kwa afya."<br />
<br />
Msemaji wa shirika la Uingereza ''British Heart Foundation alisema kua: "tunafahamu kuwa chuki na unyonge husababisha kemikali fulani mwilini ambazo zinaweza kuzidisha uwezekano wa maradhi ya moyo, ingawa hatuelewi kikamilifu ni kwanini.<br />
<br />
Matumaini au hata chuki ni hisia zinazoweza kuambatanishwa na tabia zinazokubaliana na afya njema, uvutaji sigara au chakula kibovu ambavyo vyote vinaweza kuchangia katika afya ya moyo.<br />
<br />
"habari njema kwa wanawake ni kua mbali na sura yako, chaguo lako katika maisha mfano wa chakula au kutovuta sigara kuna athari kwa moyo usiokua na matatizo kuliko kua na uso mrembo.<br />
<br />
Bado kuna hitajika uchunguzi zaidi kujifunza sababu hisia za aina hii huathiri afya.<br />
TAKE OR DUMP IT, ITS UP TO YOU!</span></span>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-33599121720495889172012-07-13T13:51:00.001-07:002012-07-13T13:51:45.040-07:00WEMA AVAMIWA NA MAJAMBAZI<div class="postbody"> <div class="xg_user_generated"> <a href="http://api.ning.com/files/hxEThKxbygT1OASEWRXtvXOg709jt6GKo2CRQdVIp7LVUTf1Ef7iw**eKD4t4AzQJ62*B8P-LQrzgT9UpUPuDOEf666uj6CJ/wema.jpg" target="_self"><img class="align-center" src="http://api.ning.com:80/files/hxEThKxbygT1OASEWRXtvXOg709jt6GKo2CRQdVIp7LVUTf1Ef7iw**eKD4t4AzQJ62*B8P-LQrzgT9UpUPuDOEf666uj6CJ/wema.jpg?width=650" width="650" /></a><a href="http://api.ning.com/files/YJJKArGjbe*A*WZ7985U214UQaCY1zFbvo8IBbIZ1*wtnX-mIQKb*AlNcnAOpMr*-QDGdXHap8JVJ*BiAWmO*LmRns-jVAbo/wemampyakabisa.jpg" target="_self"><img class="align-center" src="http://api.ning.com:80/files/YJJKArGjbe*A*WZ7985U214UQaCY1zFbvo8IBbIZ1*wtnX-mIQKb*AlNcnAOpMr*-QDGdXHap8JVJ*BiAWmO*LmRns-jVAbo/wemampyakabisa.jpg?width=650" width="650" /></a><strong>Na Musa Mateja</strong><br />
SIKU chache baada ya kuanika utajiri wake, staa wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu (pichani), amevamiwa na majambazi na kukombewa vitu kadhaa huku gari lake aina ya Toyota Lexus lenye namba za ujsali T 211 BXR likinusurika kuibwa, Ijumaa lina kila sababu ya kukujuza.<br />
Tukio hilo lilijiri usiku wa kuamkia Julai 9, mwaka huu, nyumbani kwake Kijitonyama, jijini Dar es Salaam ambapo majambazi hayo yaliingia ndani kwake kwa kuruka ukuta licha ya kwamba kuna walinzi wawili.<br />
KIKWAZO CHA NGUVU<br />
Hata hivyo, baada ya kuzamia ndani ya geti, majambazi hayo yalishindwa kuingia ndani kabisa kutokana na milango madhubuti iliyopo kwenye nyumba hiyo ya kisasa.<br />
WAJIPOZA KIDOGO<br />
Kule ndani ya geti, walivunja mlango wa gari hilo na kuiba vitu mbalimbali kama kifaa cha kudhibiti mwenendo wa umeme ndani ya gari (control box), vifaa vya kufungulia vioo, milango na madirisha (power window) na vioo vinavyomuongoza dereva kuona nyuma (side miller).<br />
Vitu vingine ambavyo viliambatana na wizi huo ni ‘makapeti’ ya ndani na vitu vingine vidogovidogo ambavyo vilikuwa ndani ya geti hilo.<br />
WEMA AWASHANGAA WALINZI WAKE<br />
Akielezea mazingira ya tukio hilo, Wema alisema kuwa hata yeye ameshangazwa na uvamizi huo ambao umemfanya kuibua maswali mengi kuliko majibu hasa akizingatia kuwa tukio hilo limetokea wakati nyumba yake ina walinzi wawili.<br />
“Ni kweli nimeibiwa hivyo vitu kwenye gari na vingine vilikuwa nje, ila mazingira ya kuvamiwa na yale majambazi yananitia shaka sana maana walinzi wangu wawili walikuwepo muda wote, sasa sijui nini kilitokea?” alisema Wema kwa sauti ya kupooza.<br />
Akaendelea: “Sikuwa na namna kwao, nilikwenda kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Oysterbay ili angalau nisaidiwe utatuzi wa jambo hili sambamba na kuwabananisha walinzi wangu ambao walikuwepo usiku wa tukio.<br />
“Naamini kama geti la kutokea nje lingekuwa legelege, wangeiba na gari lenyewe. Lakini hili geti ni gumu, mpaka kulifanya lifunguke wangeweza kuchukua masaa matano ambapo kungekuwa kumekucha.”<br />
INAWEZEKANA SABABU IKAWA HII?<br />
Katikati ya <a href="http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/wema-avamiwa-na-majambazi#" id="_GPLITA_0" style="text-decoration: underline;" title="Powered by Text-Enhance">Juni</a> mwaka huu, staa huyo ambaye pia ni Miss Tanzania 2006, alitangaza kupitia runinga kwamba anamiliki nyumba hiyo huku akisema ina kila kitu ndani.<br />
Kwa mujibu wa picha zilizoenea kwenye mitandao mbalimbali Bongo, sebule ya nyumba hiyo inaweza kushawishi ‘wazee wa kazi’ kunyatia kwani Meneja wa Wema, Martin Kadinda alisema manunuzi ya nyumba hiyo pamoja na samani zake shilingi Milioni 4OO ‘ziliteketea’.<br />
HABARI ZA KIPOLISI ZATHIBITISHA<br />
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, Charles Kenyera hakupatikana siku ya Jumanne kuzungumzia tukio hilo licha ya kwamba, habari za kipolisi zilithibitisha Wema kukumbwa na uvamizi wa watu wanaodhaniwa ni majambazi.<br />
</div></div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-15926595703253033372012-07-12T23:20:00.001-07:002012-07-12T23:20:08.587-07:00WEMA, WOLPER WAANZA UPYA<div class="postbody"> <div class="xg_user_generated"> <a href="http://api.ning.com/files/gNwEwSyAg74LNyTCiTkntIYOZ9x4qbjHjwwsH4XWB8DcWL14wFqIuXU82XgWU-4W3hyoR*0KPUzdk-yeV9kgQHNEKIHf89js/wemaa.jpg" target="_self"><img class="align-center" src="http://api.ning.com:80/files/gNwEwSyAg74LNyTCiTkntIYOZ9x4qbjHjwwsH4XWB8DcWL14wFqIuXU82XgWU-4W3hyoR*0KPUzdk-yeV9kgQHNEKIHf89js/wemaa.jpg?width=650" width="650" /></a><br />
<strong><a href="http://api.ning.com/files/sYeHMTEA60LJva*937mK0FvV6Ptf3ND9aThMlGw15GHLajtzDY2XVBu*5rOEJzcOEvinywBVxfKbQNf-NlOJx3kayEWV8Ike/wemanawolperkitandani1.jpg" target="_self"><img class="align-center" src="http://api.ning.com:80/files/sYeHMTEA60LJva*937mK0FvV6Ptf3ND9aThMlGw15GHLajtzDY2XVBu*5rOEJzcOEvinywBVxfKbQNf-NlOJx3kayEWV8Ike/wemanawolperkitandani1.jpg?width=650" width="650" /></a></strong><br />
<strong><a href="http://api.ning.com/files/pcx1r2j7v4*tJGQvgctTs4Et0FJ-N1HL5znaVxxPJShyCOkkoSutn5hynE5myuRdHKuIlvyiyTZ0A4u6PtIFhstIo1DEzEYb/wemanawolperkitandani3.jpg" target="_self"><img class="align-center" src="http://api.ning.com:80/files/pcx1r2j7v4*tJGQvgctTs4Et0FJ-N1HL5znaVxxPJShyCOkkoSutn5hynE5myuRdHKuIlvyiyTZ0A4u6PtIFhstIo1DEzEYb/wemanawolperkitandani3.jpg?width=650" width="650" /></a></strong><br />
<strong><a href="http://api.ning.com/files/XKXymOiqBUuybmrgTwKDScC*BcCa1CdInPBfF1La-7c2p-SgxtwpYRhw36RA6nRn0SngeEnptc7uc9VQ5s7Hi9N7SOgLVkim/wemanawolperkitandani.jpg" target="_self"><img class="align-center" src="http://api.ning.com:80/files/XKXymOiqBUuybmrgTwKDScC*BcCa1CdInPBfF1La-7c2p-SgxtwpYRhw36RA6nRn0SngeEnptc7uc9VQ5s7Hi9N7SOgLVkim/wemanawolperkitandani.jpg?width=650" width="650" /></a></strong><br />
<strong>Musa Mateja na Shakoor Jongo</strong><br />
MASTAA wanaotesa katika filamu za Kibongo, Wema Sepetu na Jacqueline Wolper wameonekana kudhamiria kuachana na yaliyopita na kuanza maisha mapya baada ya kunaswa wakiwa chumbani katika hoteli moja maarufu jijini Dar es Salaam, Risasi Mchanganyiko lina data.<br />
Tukio hilo limenaswa hivi karibuni na kamera ya gazeti hili ikiwa ni siku chache baada ya kuthibitisha kumaliza tofauti zao, Jumamosi, Julai 7, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Temeke, Dar muda mfupi baada ya kumaliza pambano lao la kirafiki la mchezo wa masumbwi.<br />
<strong>CHANZO KINATIRIRIKA</strong><br />
“Watu walisema eti Wema na Wolper wamepatana kinafiki, sasa ngoja niwape mchongo...wapo hotelini (akiitaja hoteli yenyewe lakini tunaificha jina kwa sababu maalum) tena katika chumba kimoja.<br />
“Hawana uadui wale tena, sasa aibu itabaki kwa wale wanaowagombanisha na kupeleka umbeya kila upande,” kilidadavua chanzo hicho kwa sharti la kutochorwa jina lake gazetini.<br />
<strong>TIMU YA RISASI MZIGONI</strong><br />
Bila kupoteza muda, ‘wazee wa kazi’ walichukua vitendea kazi vyao na kukimbilia katika hoteli waliyoelekezwa ambapo kweli walifanikiwa kuwakuta Wema na Wolper wakijiachia kwa raha zao.<br />
Hawakuonesha mshtuko, wala kuzuia waandishi wetu wasiwafotoe picha, badala yake ndiyo kwanza waliweka na pozi.<br />
<strong>SHUKA MOJA, KITANDA KIMOJA</strong> <br />
Wakiwa na nyuso zenye matabasamu ya nguvu, Wema na Wolper walikuwa wamelala katika kitanda kimoja na kujifunika shuka moja huku wakiendelea na stori za hapa na pale.<br />
Kwa namna ilivyokuwa ni kama hapakuwahi kutokea bifu lolote kati yao.<br />
Waandishi wetu walifanikiwa kuzungumza nao juu ya tofauti zao na hali ilivyo hivi sasa baada ya kuweka mambo sawa.<br />
<strong>WEMA ANATOA YA MOYONI</strong><br />
“Nina furaha sana kiukweli, tangu tumemaliza pambano letu pale Taifa (Uwanja wa Taifa) tumekuwa kwenye upendo na amani kama zamani.<br />
“Unajua hakuna maana ya kuwa na bifu...sisi bado ni vijana na tunahangaika kusaka maisha, kwa nini tudumu kwenye bifu? Wolper ni rafiki yangu na yote yaliyopita tumeshayasahau.”<br />
Wema alipopewa nafasi aeleze chanzo cha bifu lao, alisema: “Hayo yameshapita, siwezi kuyazungumzia tena, ninachojua ni kwamba tumepatana na tumefungua ukurasa mpya.”<br />
<strong>KUTOKA KINYWANI MWA WOLPER</strong><br />
“Siwezi kusema nilikuwa na ugomvi na Wema, zile ni changamoto tu na kwa sasa zimeisha, sina la kuongeza. Nadhani sasa mtupishe tuendelee na mapumziko yetu.”<br />
<strong>RAFIKI WA WOLPER ADUWAA</strong><br />
Shostito wa karibu na Wolper ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini, alisema hakutegemea kama tofauti kati ya shogaye na Wema zingeisha.<br />
“Nimeamini hakuna rafiki wa kudumu na pia hakuna adui wa kudumu duniani, maana nilikuwa nina shida na Wolper akanimbia nimfuate hotelini, nilipokwenda nikashangaa kumkuta na Wema,” alisema.<br />
<strong>KALAMU YA MHARIRI</strong><br />
Kukosea ni sehemu ya ukamilifu wa binadamu, kama Wema na Wolper mmegundua makosa yenu kila mmoja kwa wakati wake anapaswa kujua thamani ya urafiki wake kwa mwenzake na kuanza ukurasa mpya wa kweli.<br />
Bifu halina maana kwa wasanii, mkiendelea kuwa katika umoja, bila shaka mtapiga hatua katika sanaa yenu.<br />
</div></div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-11912924995645604922012-07-12T23:15:00.001-07:002012-07-12T23:15:17.935-07:00Usijipe presha, kama unampenda muamini kisha aziba masikio!<div class="postbody"> <div class="xg_user_generated"> <br />
<a href="http://style.popcrunch.com/wp-content/uploads/2008/05/jessica_alba.jpg" rel="nofollow" target="_blank"><img class="align-center" src="http://style.popcrunch.com/wp-content/uploads/2008/05/jessica_alba.jpg?width=650" width="650" /></a><br />
Assalam alaikum mpenzi msomaji wangu wa safu hii. Mambo vipi? Natumani kwamba muwazima kabisa na mnaendelea vyema na majukumu yenu ya kila siku. Mimi namshukuru Mungu kwani amekuwa akinipa nguvu ya kuandika haya ninayoamini yana manufaa kwenu.<br />
Ndugu zangu, ili uweze kudumu katika uhusiano wako unatakiwa kujenga mazingira ya kumuamini sana mpenzi wako. Nasema hivyo kwa kuwa, mapenzi ni imani. Ni sawa na kuamini Mungu yupo licha ya kwamba hujawahi kumuona.<br />
Vivyo hivyo, amini tu kwamba mpenzi wako anakupenda kwa dhati licha ya kwamba hujaufungua moyo wake na kathibitisha kwamba ndani yake uko wewe peke yako.<br />
Mpende, muamini na weka akilini mwako kwamba, kamwe hawezi kukusaliti licha ya kwamba kinyume chake pia ni sawa. Hiyo itakusaidia wewe kuendelea kuishi maisha ya furaha na amani bila kuwa na presha.<br />
Jiulize, ni wanaume wangapi ambao wake zao wanagawa penzi nje ya ndoa lakini wao wanawaamini kupita maelezo? Ni wanawake wangapi ambao waume zao ni viwembe kwelikweli lakini wanawaamini kupindukia? Unadhani ni kwa nini? Ni kwa sababu wamejijengea mazingira ya kuwaamini wenzao wao wa kiwango kikubwa na kuziba masikio yao kukwepa wambeya.<br />
Tutambue tu kwamba, katika maisha kuna kitu kuridhika. Unapokuwa na mtu ambaye anakupa kila aina ya furaha maishani mwako bila kuonesha tabia zozote zinazokutia mashaka juu ya penzi lake, huyo mpende, mheshimu na muamini.<br />
Hata kama kuna uwezekano wa yeye kuwa anaficha makucha yake na kuyachomoa pale anapokuwa mbali na wewe, kwa sababu huna uhakika na hujawahi kumuona, chukulia kwamba yeye ni msafi kisha yaache maisha yenu yaendelee kuwepo.<br />
Nasema hivyo kwa sababu, tukianza kuchunguzana hakuna ambaye ni msafi kwa asilimia mia moja. Kila mtu anajiamini mwenyewe lakini huwezi kuiamini nafsi ya mwenzako kwa asilimia zote.<br />
Ndiyo maana nikasema, unapoingia katika uhusiano na mtu ambaye umetokea kumpenda sana, ongea na moyo wako. Moyo wako ndiyo utakueleza kama mpenzi wako ni muaminifu ama siyo na pindi utakapoona dalili za kwamba ni tapeli wa mapenzi mwenye lengo la kutaka kukuchezea kisha kukuacha solemba, usimng’ang’anie eti tu kwa sababu umeoza kwake, muache!<br />
Tatizo tulilonalo wengi ni kutokuwa tayari kuwakosa wale ambao tumetokea kuwapenda sana bila kujua kwamba unaweza kutokea kumpenda mtu lakini yeye akawa hana mapenzi ya dhati moyoni mwake dhidi yako. Ifike wakati tukubaliane na uhalisia kwamba, unapoona uliyenaye anakuzingua, yupo mwingine mwenye penzi la dhati kwako ambaye anasubiri umuache huyo uliyenaye ili awekeze penzi lake kwako.<br />
Kwa kumalizia naomba niseme kwamba, mapenzi ya siku hizi usipoangalia yanaweza kukufanya ukawa chizi. Hii ndiyo inayosababisha baadhi ya watu kufikia hatua ya kusema kwamba, hawahitaji kuwa na wapenzi katika maisha yao. Kwa nini? Kwa sababu kila uhusiano wanaoingia wanakutana na usanii.<br />
Elewa kwamba, una haki ya kupenda na kupendwa, ukishampata yule unayedhani atayafanya maisha yako kuwa ya furaha, mpende kwa dhati na muamini kwamba hawezi kukusaliti lakini, wakati huo hutakiwi kubweteka, chunguza nyendo zake na kama utabaini kwamba anajiheshimu, ongeza mapenzi kwake lakini kama utabaini kuwa hajatulia, muache.<br />
</div></div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-53048598678604305432012-07-12T23:10:00.001-07:002012-07-12T23:10:21.857-07:00<a href="http://allswaggazz.blogspot.com/2012/07/barnaba-anaswa-na-demu-gesti.html?spref=bl"></a><br />
<br />
<table align="center" cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="margin-left: auto; margin-right: auto; text-align: center;"><tbody>
<tr><td style="text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiT9A4oYv3XNhyLwrZdTEtncTfjZKMAFm5wpCcRHCuNIi-XEMxdaIlrSjPhyphenhypheno48rb5ClLoSjOurQjTHuxHkjQxVZInOnXhGZorAdsfVKQtdQQ4m-rG9d-zppsgRgn8zX8NP6rCiZuj6Qxlu/s1600/wedding-beach-sunset.jpg" style="margin-left: auto; margin-right: auto;"><img border="0" height="150" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiT9A4oYv3XNhyLwrZdTEtncTfjZKMAFm5wpCcRHCuNIi-XEMxdaIlrSjPhyphenhypheno48rb5ClLoSjOurQjTHuxHkjQxVZInOnXhGZorAdsfVKQtdQQ4m-rG9d-zppsgRgn8zX8NP6rCiZuj6Qxlu/s200/wedding-beach-sunset.jpg" width="200" /></a></td></tr>
<tr><td class="tr-caption" style="text-align: center;"><br />
</td></tr>
</tbody></table><span class="Apple-style-span" style="font-family: Arial,Tahoma,Helvetica,FreeSans,sans-serif; font-size: 13px; font-weight: bold; line-height: 18px;">mimi ni msichana wa makamu sijaolewa ila nimepata mkaka ninaye mpenda ambaye ni mzungu, japo mimi nampenda sana lakini wazazi wangu hawataki kabisa kusikia nikiolewa naye(wakidai ni bora nitafute mume muafrica na mtanzania mwenzangu kama nataka kuolewa)....</span><span class="Apple-style-span" style="font-family: Arial,Tahoma,Helvetica,FreeSans,sans-serif; font-size: 13px; font-weight: bold; line-height: 18px;"><br />
</span><span class="Apple-style-span" style="font-family: Arial,Tahoma,Helvetica,FreeSans,sans-serif; font-size: 13px; font-weight: bold; line-height: 18px;"><br />
</span><span class="Apple-style-span" style="font-family: Arial,Tahoma,Helvetica,FreeSans,sans-serif; font-size: 13px; font-weight: bold; line-height: 18px;">kwasasa mimi ni mjamzito na bado sijawaambia wazazi wangu kwani najuwa hawatafurahia, lakini mimi na mpenzi wangu huyu tumefurahi sana kujuwa tunaleta mtoto duniani, na yeye anataka kunioa ili tuwe pamoja katika kumtunza mtoto kasheshe inabaki nyumbani wazazi nitawaelezaje wanielewe???????</span><span class="Apple-style-span" style="font-family: Arial,Tahoma,Helvetica,FreeSans,sans-serif; font-size: 13px; font-weight: bold; line-height: 18px;"><br />
</span><span class="Apple-style-span" style="font-family: Arial,Tahoma,Helvetica,FreeSans,sans-serif; font-size: 13px; font-weight: bold; line-height: 18px;"><br />
</span><span class="Apple-style-span" style="font-family: Arial,Tahoma,Helvetica,FreeSans,sans-serif; font-size: 13px; font-weight: bold; line-height: 18px;">saa ingine nafikiria kutoroka tu na yeye tukaishi bila ndoa lakini sisi ni binadamu kuna leo na kesho itakuwaje tukigombana na nyumbani nimetoroka? jamani nitafanyaje?</span><br />
<br />
<br />
<br />
<h1> Maisha ya ndoa siyo maigizo, tafakari kwanza!</h1><br />
<a href="http://www.pinkdivacafe.com/okc/wp-content/uploads/2012/03/happy-couples.jpg" rel="nofollow" target="_blank"><img class="align-center" src="http://www.pinkdivacafe.com/okc/wp-content/uploads/2012/03/happy-couples.jpg" /></a><br />
BADO tunaendelea kujifunza mbinu za kuwa wanandoa bora. Mada hii imelenga zaidi kuzungumza na vijana ambao wana mitazamo mikubwa kabla hawajaingia ndani ya ndoa.<br />
Pamoja na changamoto nyingine, wapo ambao wanaishi kwa kuigiza tabia ambazo si za asili yao. Hapo sasa ndipo kwenye tatizo na umuhimu wa mada hii unapopatikana.<br />
Kuna mambo mengi ya msingi ya kuzingatia kabla ya kuingia kwenye ndoa ili mwenzako awe sahihi na ndoa yako isiwe mateso.<br />
Wiki iliyopita tulianza kuona baadhi ya mambo muhimu ya kuzingatia, leo tunaendelea. Jambo kubwa kwako ni kusoma kwa umakini na kuweka ubongo wako tayari kupokea kitu kipya. Karibu darasani.<br />
MVUTO NI ZAIDI YA UPENDO?<br />
Kuna baadhi ya watu utawasikia wakisema: “Mpenzi wangu ananivutia sana, yaani ni mzuri sana. Najua hata nikitoka naye, marafiki zangu watanisifia kwa kuchagua vizuri.”<br />
Hizi ni fikra potofu ndugu zangu. Mapenzi ya kweli hayapo kwenye sura wala umbile la mtu. Vipo vigezo vya muhimu kabisa vya kuzingatia tofauti na uzuri wa sura.<br />
Sura hubadilika ndugu zangu, binadamu wanazeeka, kuna kuugua na matatizo mengine ambayo yanaweza kubadilisha mwonekano ambao ulikuvutia awali. Je, yakitokea hayo ndiyo utakuwa mwisho wa kumpenda?<br />
Kama leo hii unamuoa kwa sababu umevutiwa na matiti yake madogo, akishazaa na kunyonyesha kisha yakaanguka, ndiyo mwisho wa kumpenda? Umempendea ngozi yake nyororo, akipata ‘aleji’ ya mafuta, ngozi ikaharibika na kuwa na mabakamabaka utakuwa mwisho wenu?<br />
Wewe mwenye mpango wa kuolewa na mwanaume mwenye kigezo cha kifua cha kimapenzi, kesho akifutuka na kuwa na kitambi utamuacha? Ndugu zangu, kiukweli ni kwamba kigezo cha uzuri wa sura na umbile si sahihi kabisa katika kuchagua mwenzi wa maisha. <br />
Vipo vitu vingine muhimu zaidi vya kuangalia. Uzuri ni sifa ya ziada. Kwangu mimi naweza kusema ni sifa tangulizi kabla ya mambo mengine ya msingi ambayo nitayafafanua katika mada hii.<br />
Kama ulikuwa unaishi katika dunia ya fikra hizo, hama ndugu yangu. Uko gizani, njoo kwenye nuru.<br />
ANAJUA MAPENZI?<br />
Ndugu zangu, msinielewe vibaya katika kipengele hiki, msije mkadhani nahamasisha ngono kabla ya ndoa. Hapa namaanisha mapenzi kwa maana ya upendo. <br />
Je, mwenzi wako mtarajiwa ni faraja kwako? Anakusaidia unapokuwa na matatizo makubwa ya kiafya? Yupo nawe bega kwa bega katika maswaibu yanayokukuta? Lazima awe na mapenzi ya dhati na wewe.<br />
Lazima mwezi wa maisha yako awe anakupenda kweli kweli. Ambaye anaweza kuifanya siku yako kuwa bora. Ndugu zangu, unaweza usione umuhimu wa jambo hili, lakini nataka kuwaambia kwamba, mwenzi ambaye hata kutumia neno baby, sweetie, mumy, dear, d na mengineyo ni shida, ni tatizo.<br />
Unatakiwa kuwa na mtu ambaye ukiwa na matatizo kazini, anakuambia: “Usijali baby, yataisha. Nipo kwa ajili yako. Mimi ndiyo faraja yako.”<br />
Dalili za mwenzi wa aina hii utaziona mapema sana. Anza kumfuatilia kuanzia sasa hivi utagundua. Lazima awe na maneno matamu ambayo yatakutuliza jazba zako wakati ukiwa na mambo binafsi yanayokukwaza.<br />
Nawe ambaye unatarajia kuingia kwenye ndoa na mwenzako, jifunze kuwa na maneno matamu. Kuwa mtu wa karibu na mwenzako muda wote, sikiliza shida zake, kuwa mshauri wake mkuu. Hapa nasisitiza, sizungumzi na jinsi moja. Wote wanahusika.<br />
Wapo baadhi ya watu wanalalamika: “Mwanaume gani nikimuomba fedha za matumizi hanipi. Mbona wenzangu wanatunzwa na wanaume zao?” Hiyo siyo sahihi marafiki. <br />
Maisha ya siku hizi ni kusaidiana. Kuwa mpenzi wake haimaanishi atamaliza shida zako zote, wakati mwingine hata wewe unapaswa kumsaidia. Hayo ndiyo mapenzi ya kweli. Marafiki, natamani kuendelea lakini nafasi yangu ni ndogo sana. Wiki ijayo tutamalizia.Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-6930011716100651392012-07-12T15:45:00.001-07:002012-07-12T15:45:14.758-07:00Somewhere Blog: BARNABA ANASWA NA DEMU GESTI<h3 class="post-title entry-title" itemprop="name" style="background-color: #9bc3e9; color: #2808aa; font-family: Impact, sans-serif; font-size: 42px; margin: 0px; position: relative;">BARNABA ANASWA NA DEMU GESTI</h3><div class="post-header" style="background-color: #9bc3e9; color: #2808aa; font-family: Arial, Tahoma, Helvetica, FreeSans, sans-serif; font-size: 16px; font-weight: bold; line-height: 1.6; margin: 0px 0px 1em;"><div class="post-header-line-1"></div></div><div class="post-body entry-content" id="post-body-3240680057602433195" itemprop="articleBody" style="background-color: #9bc3e9; color: #2808aa; font-family: Arial, Tahoma, Helvetica, FreeSans, sans-serif; font-size: 16px; font-weight: bold; line-height: 22px; position: relative; width: 646px;"><div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on"><div class="postbody"><div class="xg_user_generated"><strong><a href="http://api.ning.com/files/tq2LL6dteoJjskIM4*dXPmqc9NFgYyAC8BoJSCdC0ml5cMETAwYtciWiYrffZ0JUDtquixLV9-IIT8Zz2Y4lmvWmIMgrK900/1.jpg" style="color: black; text-decoration: none;" target="_self"><img class="align-center" src="http://api.ning.com/files/tq2LL6dteoJjskIM4*dXPmqc9NFgYyAC8BoJSCdC0ml5cMETAwYtciWiYrffZ0JUDtquixLV9-IIT8Zz2Y4lmvWmIMgrK900/1.jpg?width=650" style="-webkit-box-shadow: rgba(0, 0, 0, 0.199219) 0px 0px 0px; background-color: #df0cdf; background-position: initial initial; background-repeat: initial initial; border-bottom-left-radius: 0px; border-bottom-right-radius: 0px; border-top-left-radius: 0px; border-top-right-radius: 0px; border: 1px solid rgb(223, 12, 223); box-shadow: rgba(0, 0, 0, 0.199219) 0px 0px 0px; padding: 8px; position: relative;" width="650" /></a></strong><br />
<strong><a href="http://api.ning.com/files/JxeguhR*jUWP0DdP94g20ft59GdSiZzFsIhYgE4StSWMlit*CHKrfUZC0i4nNoOwAIPiqaGBhX9-bSE0jKOGm8vFvo2b5XLO/barnabanadem3.jpg" style="color: black; text-decoration: none;" target="_self"><img class="align-center" src="http://api.ning.com/files/JxeguhR*jUWP0DdP94g20ft59GdSiZzFsIhYgE4StSWMlit*CHKrfUZC0i4nNoOwAIPiqaGBhX9-bSE0jKOGm8vFvo2b5XLO/barnabanadem3.jpg?width=650" style="-webkit-box-shadow: rgba(0, 0, 0, 0.199219) 0px 0px 0px; background-color: #df0cdf; background-position: initial initial; background-repeat: initial initial; border-bottom-left-radius: 0px; border-bottom-right-radius: 0px; border-top-left-radius: 0px; border-top-right-radius: 0px; border: 1px solid rgb(223, 12, 223); box-shadow: rgba(0, 0, 0, 0.199219) 0px 0px 0px; padding: 8px; position: relative;" width="650" /></a></strong><br />
<div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Siku chache baada ya mwanamuziki Barnaba Elias kutangaza kujaaliwa mtoto wa kiume aliyezaa na mwanamke anayeishi naye, msanii huyo hivi karibuni alinaswa akiwa na demu mwingine kwenye nyumba ya kulala wageni mjini hapa.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Barnaba alifika Zanzibar kwa ajili ya kufanya shoo kwenye Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar (ZIFF) linaloendelea Kisiwani Unguja ambapo paparazi wetu akiwa kwenye gesti ya Malindi alimuona binti mmoja akiingia na kumtaka mhudumu ampe funguo za chumba alicholala msanii huyo.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">“Mimi naomba unipe funguo za chumba atakacholala Barnaba kwani ndicho nitakacholala,” alisema binti huyo ambaye inadaiwa alitokea Dar.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Kauli hiyo ilimshangaza mhudumu wa mapokezi ambaye alimtaka demu huyo kurudia alichokisema na jibu likawa:</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">“Nimekwambia hivii, chumba anacholala Barnaba ndo’ changu, wewe nipe funguo mwenyewe atakuja muda si mrefu.”<br />
Kufuatia maelezo hayo, mhudumu huyo aliamua kutoa funguo ambapo demu huyo alikwenda kuingia kwenye chumba namba 5.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Mwandishi wetu aliendelea kufuatilia mkanda mzima ambapo baada ya Barnaba kumaliza shoo yake kwenye Ukumbi wa Ngome Kongwe, alirudi kwenye gesti hiyo akiwa ameongozana na demu huyo kisha kuingia ndani.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Kesho yake mishale ya saa 4:30 asubuhi, mhudumu wa gesti hiyo alimtaka Barnaba kuachia chumba ili waweze kufanya usafi ambapo kauli hiyo ilimtibua msanii huyo ambaye alitaka aruhusiwe kuendelea kuwepo pale hadi saa 10 jioni.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Kutokana na mazingira hayo, ulitokea msuguano kati ya wahudumu na Barnaba lakini baadaye msanii huyo alilazimika kuondoka katika gesti hiyo akiwa ameongozana na demu huyo.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Jitihada za kumpata Barnaba kuzungumzia uhusiano uliopo kati yake na demu huyo hazikuweza kuzaa matunda mpaka tunakwenda mtamboni.</span></b></i></div></div></div></div></div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-8049987705945352502012-07-12T15:39:00.001-07:002012-07-12T15:39:44.820-07:00Somewhere Blog: AUNT EZEKIEL ANA MIMBA MIEZI SITA<h3 class="post-title entry-title" itemprop="name" style="background-color: #9bc3e9; color: #2808aa; font-family: Impact, sans-serif; font-size: 42px; margin: 0px; position: relative;">AUNT EZEKIEL ANA MIMBA MIEZI SITA</h3><div class="post-header" style="background-color: #9bc3e9; color: #2808aa; font-family: Arial, Tahoma, Helvetica, FreeSans, sans-serif; font-size: 16px; font-weight: bold; line-height: 1.6; margin: 0px 0px 1em;"><div class="post-header-line-1"></div></div><div class="post-body entry-content" id="post-body-1400841912228707243" itemprop="articleBody" style="background-color: #9bc3e9; color: #2808aa; font-family: Arial, Tahoma, Helvetica, FreeSans, sans-serif; font-size: 16px; font-weight: bold; line-height: 22px; position: relative; width: 646px;"><div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on"><div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="http://1.bp.blogspot.com/-yJSjUuf_LLo/T_7eVlffRSI/AAAAAAAAAhE/8nnorIVI6lo/s1600/2ddd.jpg" imageanchor="1" style="color: black; margin-left: 1em; margin-right: 1em; text-decoration: none;"><img border="0" src="http://1.bp.blogspot.com/-yJSjUuf_LLo/T_7eVlffRSI/AAAAAAAAAhE/8nnorIVI6lo/s1600/2ddd.jpg" style="-webkit-box-shadow: rgba(0, 0, 0, 0.199219) 0px 0px 0px; background-color: #df0cdf; background-position: initial initial; background-repeat: initial initial; border-bottom-left-radius: 0px; border-bottom-right-radius: 0px; border-top-left-radius: 0px; border-top-right-radius: 0px; border: 1px solid rgb(223, 12, 223); box-shadow: rgba(0, 0, 0, 0.199219) 0px 0px 0px; padding: 8px; position: relative;" /></a></div><div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="http://4.bp.blogspot.com/_1dH5vairjeU/S_KkOxfs3NI/AAAAAAAABRM/vynYy-emSlE/s1600/IMG_1668.jpg" rel="nofollow" style="color: black; margin-left: 1em; margin-right: 1em; text-decoration: none;" target="_blank"><img class="align-center" src="http://4.bp.blogspot.com/_1dH5vairjeU/S_KkOxfs3NI/AAAAAAAABRM/vynYy-emSlE/s1600/IMG_1668.jpg?width=650" style="-webkit-box-shadow: rgba(0, 0, 0, 0.199219) 0px 0px 0px; background-color: #df0cdf; background-position: initial initial; background-repeat: initial initial; border-bottom-left-radius: 0px; border-bottom-right-radius: 0px; border-top-left-radius: 0px; border-top-right-radius: 0px; border: 1px solid rgb(223, 12, 223); box-shadow: rgba(0, 0, 0, 0.199219) 0px 0px 0px; padding: 8px; position: relative;" width="650" /></a></div><div class="postbody"><div class="xg_user_generated"><strong></strong><br />
<strong></strong><br />
<strong></strong><br />
<strong></strong><br />
<strong></strong><br />
<div style="text-align: justify;"><strong></strong><i><b><span style="font-size: medium;">SIKU chache baada ya staa wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel kuripotiwa kufunga ndoa mjini Dubai, mchumba wa staa huyo aliyetambulika kwa jina moja tu la Jeff amesema kuwa, anashangazwa na Aunt kuolewa huku akiwa na ujauzito wake, Amani linashuka na mistari ya habari hii.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Akizungumza na Amani jijini Dar hivi karibuni, Jeff amesema kuwa taarifa za kuolewa kwa Aunt alizipata akiwa nchini China na kushtuka sana.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">“Kinachonishangza ni huyo jamaa anafungaje ndoa na mwanamke ambaye ana ujauzito wangu wa miezi sita ambao aliondoka nao kwenda Dubai?” alihoji Jeff.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Jeff aliendelea kutiririka kama mtu alikuwa akiimba mashairi ya Muziki wa Injili kuwa, kingine kinachomuumiza ni tabia ya Aunt kumuomba fedha za matumizi akiwa Dubai huku akijua kwamba amefunga ndoa na mtu mwingine.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">“Wanawake ni mama zetu lakini ni wauaji wakubwa, inakuwaje anagawa mimba ya mtu kwa mwanaume mwingine halafu mbaya zaidi nilipokuwa China kila wiki alikuwa akiniomba fedha za matumizi nami nikawa namuagiza aende sehemu kuchukua kumbe ni mke wa mtu!” alishangaa Jeff.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Juhudi za kumpata Aunt ili kuthibitisha madai hayo ya ujauzito hazikuweza kufua dafu baada ya simu yake anayoitumia huko Umangani kutokuwa hewani.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">Jambo lingine lililomshtua Jeff ni kusikia kuwa aliyemuoa Aunt huko Dubai anaitwa Sunday Dimonte kwani msanii huyo ‘alisevu’ namba yake kwa kutumia jina hilo.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"><i><b><span style="font-size: medium;">“Nilipomuuliza kwa nini ananisevu kwa jina la Dimonte, Aunt aliniambia kuwa jina hilo lilimaanisha mpenzi kwa Lugha ya Kifaransa,” alisema kwa masikitiko Jeff.</span></b></i></div></div></div></div></div>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-28312665567615806182012-07-11T14:04:00.001-07:002012-07-11T14:04:09.760-07:00LOVE STORIES<a href="http://allswaggazz.blogspot.com/p/love-stories.html?spref=bl">LOVE STORIES</a>:<br />
<br />
<br />
<br />
<div class="tb"> <h1> Watu wenye tabia hii husababisha mapenzi kuwa magumu</h1></div><strong><a href="http://api.ning.com/files/yH8ht7WGh5T8me*pa5gYs6cBTR4ViVuPPVazqv6MNefJZ3L2QsSUnVuNIZUKbWocBqqpT40sGP6kuppJS6sYK4Z5Lk4xa9ld/loveee.jpg" target="_self"><img class="align-center" src="http://api.ning.com:80/files/yH8ht7WGh5T8me*pa5gYs6cBTR4ViVuPPVazqv6MNefJZ3L2QsSUnVuNIZUKbWocBqqpT40sGP6kuppJS6sYK4Z5Lk4xa9ld/loveee.jpg?width=650" width="650" /></a></strong><br />
<strong><br />
</strong><br />
<div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Mapenzi yamekuwa magumu. Ni mzigo mzito kuubeba. Yanaendelea kujeruhi wengi, bado ni mateso kwa wengine. Sasa hivi, asilimia kubwa ya watu inaamini kwamba kupata mwenzi sahihi wa maisha ni ndoto za alinacha. Ni kamari, ni bahati nasibu.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Maendeleo yamekuja na mambo leo. Kile kinachoonekana ni Uzungu, kimeathiri kwa kiasi kikubwa ustaarabu wetu. Mila na desturi zetu vimepokwa na utandawazi uliotujia. Hii inamaanisha kwamba uhusiano wa kimapenzi wa sasa, hauendani na sura ya utamaduni wetu.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Vijijini kuna unafuu japo na kwenyewe fujo zimeshaingia na mambo yameshabadilika. Mijini ndiyo matatizo yenyewe. Ulimwengu wa digitali na fursa za mitandao zinatutia wazimu. Tunataka kuiga mitindo ya maisha ya wenzetu, matokeo yake tunageuka watumwa wa mapenzi.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Hayakuletwa mapenzi ili yawaumize watu, yapo kwa ajili ya kutoa faraja ndani ya jamii. Yalivyo ni kwamba baada ya misukosuko ya kimaisha, vurugu mechi za kusaka riziki na mihangaiko mingine ya kimaisha, angalau unaweza kusahau yote unaporejea kwa mwenzi wako.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Hata hivyo, mapenzi hugeuka matatizo pale ambapo kazini umeondoka pakiwa moto, unarudi nyumbani nako pia unakuta moto. Unakosa sehemu ya kwenda kujishikiza. Faraja inaota mbawa. Hapa ndipo tafsiri ya mapenzi inapokosa mashiko. Jitazame, muangalie na mwenzako!</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Japo ni ukweli usiopingika kuwa mapenzi siku zote hayapo tambarare hata kwa wenza waliostaarabika, ila katika kundi la mabrazameni na masistaduu ni mtihani. Kuna usemi kwamba glasi hugongana kabatini, nakubaliana nao lakini kwa makundi hayo ni pasua kichwa.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Mabrazameni na masistaduu ni zao la mapenzi ya Kichina, yaani uhusiano bandia. Inawezekana akiwa kwako akajilegeza kama amefika, kumbe anao wengine wengi. Hili ni janga zito kwa maisha ya sasa. Uaminifu haupo, uzinzi na usaliti vimekuwa fasheni ya kutukuzwa.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Wengine siyo masistaduu wala mabrazameni, wapo kawaida au pengine wana muonekano wa heshima mno. Hata hivyo, ukichimbua hulka zao ndiyo utachoka. Ni wakali wa kuwapanga foleni, akitoka kwa huyu anakwenda kwa yule. Mapenzi yametawaliwa na rangi ya Shetani.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Wapo wanaobadili wapenzi kwa sababu za tamaa, lipo kundi linaloamini miili yao ni mtaji wa kupata fedha, wengine shida za maisha zikasababisha uamuzi huo wa kujidhalilisha, wapo ambao ni tabia. Bila kugusa huku na huko hatosheki. Makundi yote hayo yamezingirwa na Ibilisi.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Mume wa mtu, anapewa sifa ya ‘uchapaji’ wa vidosho. Kwamba anajua kuwapanga kila kona. Nyumba za kulala wageni, anaingia kama nyumbani kwake. Yaani wanamjua, ni mteja wao hodari. Akifika, wanampeleka kwenye chumba anachokipenda.</span></b></i></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Wapo wanaopiga simu, yaani namba za nyumba za kulala wageni zimejaa kwenye simu yake. Akijibiwa kwamba Sinza Kumekucha hakuna vyumba, anapiga Vatican, nako akikosa anajaribu Mori. Inahitaji sala na dua kuishi na mtu wa aina hiyo. Kuna mawili, kama hatakupa maradhi, omba usijue tabia yake, atakuua kwa presha.</span></b></i></div><h3 class="post-title entry-title" style="color: red;"> <span style="font-size: large;"> </span></h3><h1> Siri nzito za kumpagawisha mpenzi wako!</h1><div class="xg_module_body"> <div class="postbody"> <div class="xg_user_generated"> <div style="text-align: center;"> <a class="noborder" href="http://api.ning.com/files/xAAmx6Na99TiMmge8ek9-A8g0taq0th1MiknHEgVa-3Z030TaF1BkOu5eNqJWrDSkYaZfDRuyMQdMYKbf7ByhxPuInb0NMJn/lovers.jpg" target="_blank"><img height="640" src="http://api.ning.com/files/xAAmx6Na99TiMmge8ek9-A8g0taq0th1MiknHEgVa-3Z030TaF1BkOu5eNqJWrDSkYaZfDRuyMQdMYKbf7ByhxPuInb0NMJn/lovers.jpg?width=221" width="473" /></a></div><div style="text-align: justify;"> <i><b><span style="font-size: medium;">Ili uweze kuwa na furaha maishani, lazima uwe katika uhusiano imara usiotetereka. Kama unaishi na mke au mume ambaye moyo wako umemchagua lazima furaha itatawala katika nyumba yenu. Lakini rafiki zangu, huwezi kuwa katika ndoa yenye furaha kama hukuwa na mchumba bora. Kwa maneno mengine, lazima uanze kuboresha uchumba wako kwanza, uwe na uhakika kwamba mwenzi uliyenaye ni sahihi ili ukiingia kwenye ndoa usijute.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Mapenzi ni sawa na bustani nzuri ya maua rafiki zangu, wakati mwingine inahitaji mbolea, kumwagiliwa maji na hata kupaliliwa. </span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Kwa kufanya hivyo utazidisha ladha ya mapenzi na kuyafanya yazidi kuwa na nguvu zaidi ya awali. Lakini kama hutamwagilia, hutaweka mbolea, hutapalilia, hesabu kwamba mapenzi yako yanaweza kuanza kupoteza nguvu taratibu na hatimaye kufa kabisa.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Kikubwa ambacho nimepanga kuzungumza nanyi leo ni jinsi ya kumpagawisha mwenzi wako ili awe wako peke yako. Umeshawahi kufikiria kwamba, kama ukishindwa kutimiza mambo fulani katika penzi au ndoa yako, mwenzi wako anaweza kuwa wa kushea?</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Kama bado, inakubidi ufahamu hilo kuanzia leo. Mpenzi anahitaji mambo mengi ili aendelee kuwa mwaminifu kwenye penzi lenu. Ni kweli kwamba uaminifu upo kwa mtu mwenyewe, kama mtu ni mwaminifu basi atadumisha uaminifu uliopo ndani yake, lakini kama kuna mambo unakosea, lazima utasalitiwa!</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Tena basi, kama mwenzi wako anakupenda, atakusaliti huku analia! Kwanini? Kwasababu analizwa ba kitendo ambacho hajapenda kukifanya ila wewe mwenyewe ndiyo umemlazimisha afanye hivyo.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Kuna nini zaidi katika dhana ya usaliti?</span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Tukiachana na tamaa, hulka na ushawishi, wakati mwingine mpenzi anaweza kusaliti kwa kukosa yale ya muhimu zaidi katika penzi au ndoa yake.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Kwa bahati mbaya sana, watu wa aina hii huwa hawasemi moja kwa moja kuwa wanakosa vitu fulani au wanapenda vitu fulani, badala yake hutumia lugha za ishara zaidi na kama hutaelewa basi huona suluhisho ni kutafuta pumziko lingine.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Hapa sasa mwenzi wako anakuwa si wako peke yako tena! Lakini lazima uhakikishe mpenzi wako anaendelea kuwa wako bila kushea na mtu yeyote na jambo hili linawezekana kabisa ikiwa wewe mwenyewe utataka iwe hivyo.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Zipo hatua au mambo mengi ya kumfanyia mpenzi wako ili awe wako peke yako, lakini hapa nitakupa yale ya msingi zaidi yatakayokusaidia katika penzi lako.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Njia hizi za siri nimezifananisha na shamba au bustani, ambayo ina mahitaji yake. Sasa katika uchambuzi huu, nitaainisha jinsi ya kuitunza bustani hii ya mapenzi ili kuifanya bora zaidi kila siku.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Kitu cha kwanza kabisa ni mbelea. Hapa nazungumzia penzi ambalo tayari limeshakuwa penzi! Kama ni bustani basi tayari mboga zako zimemea vizuri.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Lakini ukumbuke kwamba, bustani yako haitaweza kuendelea kuwa bora kama haitakuwa na matunzo. Hapa penzi linahitaji mbolea.</span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Mbolea ninayoizungumzia hapa ni maneno matamu yaliyojaa huba. Fikisha hisia zako kwa mwenzi wako kwa namna ya kipekee iliyojaa penzi la dhati.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Mweleze jinsi unavyompenda na jinsi maisha yako ambavyo hayawezi kukamilika bila yeye. Huu ni wakati wako wa kumsumbua kwa meseji zilizojaa tungo za mahaba, kadi, maua na zawadi ndogo ndogo.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Baadhi ya wanandoa wakishaoana, huacha utaratibu huu. Kuna wanaosema: “Ah! Hayo mambo ya kizamani bwana, kipindi akiwa demu wangu, sasa hivi yupo ndani, kwanini nihangaike?”</span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Haya ni makosa makubwa ndugu yangu. Shamba bila mbolea kuna mavuno kweli? Huwezi kuvuna.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Kitu kingine muhimu katika bustani, kama ujuavyo mpenzi msomaji wangu ni maji. Bustani yako itahitaji maji kwa ajili ya kuzidisha ustawi wa mazao yako. Hapa unatakiwa kuwa mbunifu zaidi katika mambo yanayohusu mapenzi moja kwa moja.</span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Unatakiwa kubadilisha aina ya ufanywaji wa mapenzi, mahali pa kukutana na hata sehemu za mitoko. Inashauriwa ili kuboresha penzi ni vizuri kutoka sehemu mbalimbali na mwenzi wako. Inapendeza zaidi angalau mara tatu kwa miezi sita, kulala na mwenzako hotelini. </span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Hapa utakuwa unanakshi zaidi penzi lako. Outing yako ni vyema ikawa ya kimahaba zaidi, kuanzia mavazi, sehemu mnazotembelea n.k</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Mfanyie mwenzi wako mambo ya kimahaba sana mnapokuwa wawili. Mbusu, mkumbatie, mwambie jinsi unavyojisikia wa pekee kuwa wake. Utundu wako wote umalizie hapa, ukifanya hivyo utakuwa umemwagilia bustani yako vyema.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Baada ya muda bustani huota majani mengine ambayo si mboga! Yawezekana kabisa, kwa bahati mbaya uchafu ukaingia bustanini. Wakati wa palizi ni muda sahihi wa kuondoa vyote hivyo.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Hata katika mapenzi pia hutakiwa kufanya jambo hili. Kugombana au kupishana kiswahili kwa wapenzi ni jambo la kawaida sana, hivyo ni vyema kuweka sawa tofauti hizo mapema, kabla tatizo halijawa kubwa zaidi. Hii ndiyo palizi ninayoizungumzia.</span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;">Usikae na kinyongo moyoni mwako, kuwa mjanja, hata kama ni yeye ndiye aliyekosea, zungumza naye ukimweleza jinsi ambavyo hupendi mgombane, mkimweleza hisia zako kwamba unatamani sana muelewane katika siku zote za maisha yenu. Weka mambo sawa.</span></b></i></div></div></div></div><h3 class="post-title entry-title" style="color: red;"> <span style="font-size: large;"> </span></h3><h3 class="post-title entry-title" style="color: red;"> <span style="font-size: large;"> </span></h3><h3 class="post-title entry-title" style="color: red;"> <span style="font-size: large;"><a href="http://sethought.blogspot.com/2012/07/ukitaka-kuua-penzi-lako-fanya-haya.html">UKITAKA KUUA PENZI LAKO FANYA HAYA HAPA,FASTA TU</a></span> </h3><div class="post-info"> <div class="post-footer-line post-footer-line-1"> <span class="post-author vcard"> </span> </div><div class="post-footer-line post-footer-line-2"> <span class="post-labels"> </span> <span class="post-comment-link"> </span> </div></div><div style="background-color: white; color: blue; text-align: justify;"> <i><span style="font-size: medium;"><strong>Ukitaka kufa mwakani unatakiwa kufanya mambo flani ya hovyo hovyo mwaka huu,utakufa tu..</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Ukimeza dawa ya sumu usitegemee itageuka kuwa ARV,itakuua tu</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Kuna aina flani ya watu wanapenda sana kujitafutia matatizo,wakiwa In love huwa wanajaribu kuwa too much,kwa vitu ambavyo sio vya msingi hata na havimuongezei lolote zaidi ya matatizo.</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Kuna vitu ukifanya unajua kabisa kwamba vitakusaidia kupalilia penzi lako,kuliwekea mbolea ili likue zaidi...Concentrate kufanya hivyo</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Ila kuna watu huwa wana-opt kufanya mambo ambayo yanawaua wao wenyewe na mwisho wa siku huishia kujuta tu.</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Baadhi ya Mambo ambayo yameua mahusiano mengi sana na yanaendela kuua hata leo,na hata kesho yataua ni haya yafuatayo,Chonde chonde usifanye haya maana huwezi jua Damage ambayo yanafanya kwenye uhusiano wako:</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>1.MISTRUST</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Sifa moja ya Penzi imara ni lile ambalo mnaaminiana...Mtu anaweza kuaga kwenda home na ukajua anaenda home kweli bila kuwa na chembe ya shaka kwamba atachepuka na kufanya Call Diversion.Ukiona penzi ambalo halina Trust,hilo penzi liko ICU na litakata Roho muda wowote.Hamtafika popote. Mistrust huwa haiji hivihivi,huwa ni zao la mambo mengi yaliyotokea ambayo yamemfanya mmoja kati ya wapenzi kupunguza imani na mwingine.Dawa ni kuhakikisha mnamaintain highest level of Trust at all time.Na moja ya njia rahisi sana ya kurudisha trust iliyopotea ni kuwa wawazi...Wawazi kwenye ratiba zenu za kila siku..Thats through Communication..Hakikisheni mna communication muda wote,ifanyeni kuwa ratiba na sio utumwa,itawasaidia kuwa in touch na kila mmoja atajua ratiba ya mwenzie na kuwa at peace</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>2.EPUKA U-SPY</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Kwenye Mapenzi hakutakiwi kuwa na mtu yeyote aliyesomea CCP Moshi...Hiki ni chuo cha mapolisi na maspy wa usalama wa taifa....Mapenzi ni eneo huru ambalo kila mmoja anapaswa kuwa huru....Sio mpenzi kaacha simu tayari umekwapua...Kuna vitu haviko kwenye Katiba ya Muungano...Simu ya Mtu ni personal property yake..Dont sneek,dont Spy...Ukimuomba simu kuitumia kupiga au kutext usijifanye spy na kuchungulia Inbox..Akigundua atakumind na itakuwa big issue...uhuru wa mtu binafsi uheshimiwe,haikusaidii lolote sanasana utakumbana na vitu ambavyo hutapenda utaishia kununa na kumbe hujavielewa..We are so different,mahusiano yangu na watu wangu niliozoeana nao ni tofauti na wewe...U can see messages na ukadhani ni za cheating kumbe ni kawaida...Stay safe...Dont be a police...Dont Spy,hata uwe tempted namna gani..hii imewacost wengi sana,BEWARE</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>3.EPUKA UBIZE</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Ubize ni msala.Ukikubali kuwa mpenzi wa mtu jua kuna uhuru unapoteza...Japo uhuru kidogo...Mpenzi wako anakuwa priority na ni jukumu lako kuhakikisha anapata Attention....</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Ndio unasoma lakini una mpenzi,dont replace him/her with books</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Ndio unafanya kazi,una vikao,na assignments,na presentations,na warsha,na kila kitu ILA,una Mpenzi...Dont replace him/her with ur job...Kama huwezi kumanage Shule na Mpenzi....Kazi na Mpenzi....Chonde nakusihi,BE SINGLE,lasivyo utazingua tu mtu wa watu,atafeel hapendwi...hajaliwi..Atacheat,...na wala usimlaumu maana wakati ukiwa bize na mshule wako na mkazi wako,kuna mtu alikuwa na kazi na alimjali...Swali kwake ni Je,kwann huyu ameweza and my Boy ameshindwa???USIMLAUMU LIKITOKEA HILO,kosa ni lako 100%</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>4.EPUKA EXPECTATIONS</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Kuna watu hawana simile...Dakika 2 tu nyingi wamewaza Mbinguni...</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Mapenzi yanataka Patience....Anzeni mapenzi vizuri...Know him/her.....Jadili mustakabali wenu pamoja,akupe views zake....Then kama kuna kitu cha kuwasongesha mbele kila mmoja aseme/....Kama kuna vikwazo vya kusonga mbele kwenye hatua kubwa zaidi kama Ndoa mathalani,viwekwe wazi</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Ni jambo liko wazi,kuna watu ni wazuri kuwa wapenzi tu lakini sio waume....Kuna watu wanafit kuwa Girlfriends tu lakini sio Wife material....Thats the naked truth</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Mtu huyu ukimforce awe mume au mke inakula kwako....</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Ndoa ni Institution maalum kwa watu maalum kwa sababu maalum</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Kama wewe sio Mtu Maalum usiingie kwenye hiyo Institution Maalum maana hutakuwa na sababu maalum</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>The point is,usiexpect makubwa katika muda mfupi...give yourselves time to see ile sababu maalum ya kuwaingiza kwenye jukumu maalum..mkiona maono yenu hayaoani kufika kule usiforce...</strong></span><br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Hakuna sababu ya kuwa fancy wa Ndoa halafu mkae Mwaka 1 muachane,utakuwa umejichafulia CV bure wakati ungeweza kutulia ukapata the right guy or right woman</strong></span><br />
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Dont be over-ambitious....Stay in ur lane and choose the best out of the rest</strong></span></i></div><div style="background-color: white; color: blue; text-align: justify;"> <i><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></i></div><div style="background-color: white; color: blue; text-align: justify;"> <i><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></i></div><span class="widget-item-control"> </span> <div id="uds-searchControl"> <a href="http://allswaggazz.blogspot.dk/p/love-stories.html" name="uds-search-results"></a></div><a href="http://allswaggazz.blogspot.dk/p/love-stories.html" name="7206439458840762341"></a> <h3 class="post-title entry-title"> <span style="font-size: large;"><a href="http://sethought.blogspot.com/2012/06/aina-za-wanawake-ambao-wanaume.html">AINA ZA WANAWAKE AMBAO WANAUME WANAPENDA</a></span> </h3><div class="post-info"> <div class="post-footer-line post-footer-line-1"> <span class="post-author vcard"> </span> </div><div class="post-footer-line post-footer-line-2"> <span class="post-labels"> </span> <span class="post-comment-link"> </span> </div></div><i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Sometimes Wanawake huwa wanajiuliza Maswali mengi,wafanyeje ili wapendwe,wanahisi wana bahati mbaya,kila wanapojitoa mioyo yao inaumizwa.Jamaa hawakai,wanatupia kitu,wanakula mzigo wanatembea na Bwana..Mioyo yao imejaa matundu na hawaamini kabisa kama Wanaume huwa wanapenda,imefikia point wanadhani Wanaume hutamani tu kumbe SI KWELI!</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;"></span></strong></span> </b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Wanaume nao wana taste zao,hawaendi tu kama Mbwa koko,jalala moja baada ya jingine,HAPANA...Know their taste and you will enjoy theirs.</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Sifa za Mwanamke ambae Mwanaume atavutiwa na kukaa ni hizi zifuatazo,JITAZAME,kama huna any of these,you better try to learn to have them,its not too late:</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: lime;">1.MWANAMKE MWENYE MSIMAMO</span></strong></span> </b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Jambo moja muhimu,the number 1 thing ambacho Mwanaume anaangalia kwa Mwanamke ni Msimamo wako...Sio Mwanamke uko kama Feni,kila sehemu unapulizia upepo,Mashariki,Magharibi kote wewe...Hapo sahau,tena sahau sana.Mwanaume anahitaji kuwa na uhakika,Mwanamke aliyemkabidhi moyo hana mishemishe na hayumbishwi na lolote,na chochote na penzi lake liko safe</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Unaweza kuwa na kila kitu,Mzuri wa Sura na kila kituuuu,na bado usimpate Mwanaume wa Maana kama huna sifa hii,hakuna muujiza kwenye hili,ndo wanaume walivyoumbwa,if you lack this hamna Mwanaume wa Maana utapata,utapata vimeo kama ulivyo!</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: lime;">2.MWANAMKE MUELEWA</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Men are simple creatures,they love to live simple,and take them simple as they are...</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Ukiwa aina ya Mwanamke unamind vitu...kitu kidogo ugomvi...Unaongea na nani...Uko wapi..Na nani,Kwanini,hee,jamani kama Mahaakama kuu??Hapa unapoteza Credits</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Kuwa aina ya Mwanamke muelewa ambae utamfanya Mwanaume ajisikie vibaya kufanya kitu flani ambacho ulishamwambia asifanye before...Lakini sio kukaripia na kununa kwa sababu amerudia..let him realize that amefanya kitu cha kukuudhi na hujareact,and if hes a man enough,he will know and apologize</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Ila kama ni gumegume basi tena,litakausha na ndo inakuwa issue hapo...Are u patient enough to handle it??kazi kwako,ila kuna wanawake wana uwezo huu,learn from them wamewezaje..No matter how complicated the man is,they know how to handle him</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Jua Lugha ya kutumia ambayo utafikisha ujumbe and yet you dont show him kwamba umemind na unamkaripia...kumkaripia Mwanaume ni msala mpya,hata kama ana kosa atakumind na itakula kwako...Una ulimi mzuri kufikisha ujumbe??</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: lime;">3.MWANAMKE DIRECTOR</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Baba ni kichwa cha nyumba....mimi huamini Mama ni macho yaliyo kwenye kichwa hicho</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Women play a very vital role in DIRECTING THE HEAD TO THE RIGHT WAY</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Kichwa bila macho si utajigonga tu????Mwanamke ni jicho...</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">Ukikalia kujiremba tu na kuwaza mambo mengine bila kujua kuna kichwa kinasubiri maelekezo yako,utaonekana bogus..kutwa uko kwenye Umbea,huna muda wa kujua ur man anafanya nini,ana plan gani mwaka huo,unamsaidiaje kuzifikia,sasa we faida yako nini kwenye maisha yake??</span></strong></span> </b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: #e06666;">be the kind of a woman ambae Mwanaume aki-achieve jambo anasema I have a woman beside of me who engineered this...Kama hujawahi kufikia hatua ya kuwa appreciated na ur man kwa jambo hili jua kuna mahali umefeli...Na hili haliji hivihivi,linakuja pale kunapokuwa na proper communication between you and ur man...Bila good communication:</span></strong></span> </b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"> <strong><span style="color: #e06666;"> 1.Hutajua what ur man is up to </span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"> <strong><span style="color: #e06666;"> 2.Kwa sababu hujui what he is up to hutakuwa na msaada.</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"> <strong><span style="color: #e06666;"> 3.Akifaulu,jua haupo kwenye picha ya mafanikio yake na ur simply useless</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"> <strong><span style="color: #e06666;"> 4.Akifeli,ur part of his failure kwamba humsaidii lolote..ur simply useless and actually absent in his life kwa sababu uwepo wako haumsaidii its better he becomes alone!YOU HEARD???</span></strong></span></b></i><br />
<br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: magenta;">Women have planning and control ability,USE IT...Usikae tu kama muuza genge unasubiri wateja,Do your job and Win him!</span></strong></span> </b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong><span style="color: lime;">4.MWANAMKE MSAFI NA MZURI</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> <span style="color: #e06666;">Usafi huu sio wa nguo tu na kunukia,ni zaidi ya hilo...</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> <span style="color: #e06666;">Usafi unaanzia ndani..Msaidie Mwanaume awe msafi pia,rohoni hadi mwilini...Rohoni how???Jitu halisali,halikumbuki kuna Mungu,lipo tu,unadhani mtajenga Familia gani baadae???</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> <span style="color: #e06666;">Msaidie kum-remind kukumbuka hilo,Mafanikio ya nje huanzia ndani..Dirty inside,Dirty Outside...Mambo mengine anafanya nje na yanaku-affect kwa sababu umefeli ku-inspire change ya ndani...Ngumu hii lakini ndo hivyo..You can save a lot of energy kama atakuwa msafi wa ndani,everything outside will be set automatically...Whatever u see in physical started in Spiritual...Yeah right! Hata ulimwengu uliumbwa,na vyote unavyoviona baada ya Plan ya Spirit kumalizaika.Soma Kitabu cha Mwanzo kwenye Biblia,uone Uumbaji ulifanyikaje...Same applies na hapa,Uumbaji wa vitu vya nje,Mahusiano imara,Familia bora,inajengwa ndani..</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> <span style="color: #e06666;">Sio kazi yako ni kuuliza Baby hatuendi Club,Baby this...Unamkumbusha kusali???Utatengeneza mme freemason bila kujua...Mtu hasali we upo tu unaona sawa...CHANGE!</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> <span style="color: #e06666;">Huu usafi mwingine wanawake mmejaliwa,biashara za kunuka kikwapa no,Kusafisha nyumba vema saafiii...mengine si kama kawa??Mpango mzima uko hapo.</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> <span style="color: #e06666;">Uzuri huwa ni subjective...Unaweza kuwa mzuri kwangu lakini ni wa kawaida kabisa kwa mwingine....Ukiwa msafi unaweza ukamfanya Man wako aone potential,hata kama wewe sio mzuri sana lakini anaona Kiongozi wa Familia inside you and he will definitely opt you.</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> <span style="color: #e06666;">Hamna limbwata wala nini,tupa kule mbali...</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> <span style="color: #e06666;">Kama huna hizi sifa 4,aisee waza upya...Unaweza bahatisha ndulute ukaolewa,lakini jusitegemee muujiza,goma litapata Pancha tu...Jamaa hataweza kukaa na nunda...Atajutia Mahari aliyolipa ila atasepa kimyakimya..</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> <span style="color: #e06666;">To avoid that,please make sure you do your Homework well ili Mtihani ukija unafaulu tu bila shida...</span></strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> </strong></span></b></i><br />
<i><b><span style="font-size: medium;"><strong> <span style="color: #e06666;">Jitathmini halafu KAA HUMO!</span></strong></span> </b></i>.Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-2746939146160617435.post-65399473674769210362012-07-10T23:33:00.001-07:002012-07-10T23:33:19.949-07:00BABY POWDER ( Full Length)<iframe allowfullscreen="" frameborder="0" height="270" src="http://www.youtube.com/embed/1swLPfBMlSI?fs=1" width="480"></iframe>Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/06203748277314080730noreply@blogger.com0