MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.46.


































MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.46.

BASI la shule lililobeba watoto kumi na nane linalipuliwa kwa bomu, watoto wote wanakufa palepale lakini baadaye yanapatikana mabaki ya watoto kumi na sita tu! Hiki kinakuwa ni kitendawili kwani kila mtu alikuwa na uhakika watoto waliopanda ni kumi na nane.

Ukweli wa tukio hili ni kwamba, watoto wawili (Dorice na Dorica) waliondolewa kwenye gari na watekaji kabla ya bomu kulipuliwa. Watekaji hao walitumwa na Victor Federov, Mrusi bilionea asiye na mtoto ambaye wakati wa umasikini wake aliwahi kuwauzia Phillip na Genevieve mbegu zake za kiume.

Phillip na mke wake Genevieve hawaelewi juu ya jambo hili, wanalia kwa kupoteza watoto wao wawili katika ajali hiyo mbaya iliyomfanya Genevieve aanguke chini na kupoteza fahamu, mshipa wa damu ukapasuka kwenye ubongo kwa sababu ya kupanda kwa shinikizo.

Maisha ya Phillip baada ya hapo yanabadilika, akawa na kazi moja tu ya kumuuguza mke wake mpaka alipofariki na kufanya jumla ya watu waliofariki kwenye familia yake kufikia watatu. Amechanganyikiwa na kuwa kama mwendawazimu, akitambea na kuongea peke yake njiani.

Kwa msaada wa ushauri wa kisaikolojia aliopewa hatimaye alirejea katika hali ya kawaida, ndipo akakutana na mwanamke nje ya duka kubwa la Imalaseko katikati ya jiji, wakapanda kwenye gari kwa ajili ya maongezi, mwanamke huyo alipovua wigi na kujifunua uso wake, Phillip alishtuka na kuanza kulia.
Je, nini kitaendelea? Mwanamke huyo ni nani? SONGA NAYO…

“NINI kilikupata dada yangu?”
“Hunikumbuki?”
“Kabisa.”
“Mbona umelia?”
“Nakuonea huruma.”

“Nikikusimulia historia ya maisha yangu utanikumbuka, umewahi kuwa na rafiki msichana aliyeungua vibaya ndani ya gari?”
“Wewe ni Lina?!” Phillip aliuliza tena mshangao macho yakiwa yamemtoka, hakuwa tayari kuamini kama kweli msichana aliyekuwa mbele yake ndiye Lina aliyewahi kuwa msichana mrembo ambaye sasa uso wake ulikuwa umejaa makovu.

“Ni mimi, habari za siku nyingi Phillip?”
Phillip hakujibu, akaendelea kububujikwa na machozi, kichwani mwake taswira ya Lina wa zamani ilikuwa ikionekana, hakika alikuwa ameharibika, uso wake ukiwa umejaa makovu makubwa, ilivyoonekana upasuaji wote wa kumrekebisha sura haukuwa na mafanikio makubwa kwani sura yake ya awali haikurejea. Hasira nyingi sana akazielekeza kwa Zamaradi.

“Nisamehe!” Phillip alisema neno hilo pekee kwikwi ya kulia ilipomwachia.
“Kwa kipi Phillip?”
“Nahusika sana na ajali yako.”
“Unamaanisha nini? Ulijua itatokea? Ilikuwa ya kupangwa?”
“Hapana, ni historia ndefu naomba tu unisamehe.”

“Hakuna shida, naweza kukusamehe lakini ni vizuri ukanieleza pia ni kwa nini unaniomba msamaha?”
Phillip akajifuta machozi kisha kuanza kumsimulia Lina kila kitu kuhusu maisha yake, namna alivyoishi katika dunia mbili tofauti, inayoonekana na isiyoonekana akiwa mume wa Zamaradi, jini mwenye hasira ambaye alimshambulia kila mwanamke aliyemtaka kimapenzi. Lina alikuwa kimya akisikiliza.

“Ndiyo maana nilikuwa sikubali uhusiano wa kimapenzi na msichana yeyote, lakini mabinti walinilazimisha na Zamaradi akawadhuru, ajali yako ilisababishwa na Zamaradi, yeye ndiye aliyemuua Monalisa pia katika ajali! Nisamehe sana kwa yaliyotokea, haikuwa nia yangu.”

“Mh! Hii ni habari mpya, sikuwahi kufahamu jambo hili.”
“Huo ndiyo ukweli.”
“Huyo Zamaradi yuko wapi sasa?”

“Nilipokutana na marehemu mke wangu na kuamua kuwa na uhusiano naye kimapenzi, Zamaradi alijaribu kutushambulia lakini kwa sababu tulikuwa tumekabidhi maisha yetu kwa Mungu na tulilindwa saa ishirini na nne alishindwa kutudhuru, tangu siku hizo sikuwasiliana tena na ulimwengu usioonekana, nikamuoa mke wangu na kuzaa watoto wawili mapacha ambao sasa wote wameniacha!”

“Pole sana, nimesikia kila kitu kilichotokea, tuyasahau ya zamani tuangalie ulimwengu unaofuata mbele yetu.”
“Umeolewa?”
“Hapana, bila shaka hakuna mwanaume ambaye anavutiwa na mimi kwa jinsi nilivyo.”

“Usiseme hivyo, mshukuru Mungu.”
“Ahsante kwa kunitia moyo lakini mimi pia nataka nikuambie hata kama umepoteza mke na watoto wako, simama imara, endelea na maisha, usivunjike moyo, unakumbuka sura yangu mimi?”
“Ndiyo”

“Ilikuwa ya kuvutia, nikaipoteza katika ajali ya moto lakini bado nilisonga mbele, baada ya upasuaji wa kurekebishwa kufanyika, angalau kuwa hivi nilivyo niliendelea na masomo kwa msaada wa Umoja wa Mataifa mpaka nikapata shahada mbili za Uchumi na kuajiriwa nchini Marekani, nimehamishiwa hapa mwezi uliopita kuwa Mwakilishi wa Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa, WFP!”

“Kweli?”
“Ndiyo”
“Umenitia moyo.”
“Hivyo ndivyo maisha yalivyo Phillip, Wazungu wanasema life is a series of events, yaani maisha ni mfululizo wa matukio, linaondoka hili linaingia lile, hivyo unatakiwa kusimama imara.”

“Ahsante sana.”
“Unaelekea wapi hivi sasa Phillip?”
“Nazungukazunguka tu!”
“Karibu nyumbani basi.”
“Hakuna shida twende nikapafahamu.”

Lina akashuka na kuzunguka upande wa pili ambako alikaa kwenye usukani, akawasha gari na kuondoka moja kwa moja kupitia Barabara za Ohio, Ali Hassan Mwinyi na baadaye Haile Selasie kuelekea Masaki ambako Lina alipiga honi kwenye jumba lenye lango kubwa na likafunguliwa.
“Mh!” Mlinzi akaguna.

“Vipi?”
“Gari ni lenyewe, sauti ni ile ile akini bosi siye.”
“Mungu wangu…” Lina aliongea akijigusa kichwani na usoni, alikuwa amesahau kuvaa wigi na sura yake ya bandia ndiyo maana mlinzi wake akashtuka, kwa muda wote walioishi pamoja hakuwahi kumwonesha jinsi alivyokuwa.

“Wewe fungua lango, mambo mengine hayakuhusu.”
“Bosi haruhusu wageni kuingia bila miadi.”
“Nakuambia fungua, unataka kazi au?”
“Eebwana ee, usinizingue, rudi kinyumenyume egesha pale nje umsubiri mpaka aje.”

“Sawa, ngoja nikamlete.” alijibu Lina na kuanza kurudi kinyumenyume bila ubishi, akaligeuza gari kwa kasi na kuondoka hadi barabarani ambako alizunguka upande wa pili na kuvaa wigi pamoja na sura yake ya bandia, akarejea tena kwenye usukani na kuendesha kwenda nyumbani kwake ambako baada ya honi lango lilifunguliwa.

“Karibu bosi!”
“Ahsante sana.”
“Walikuwa wamekuacha barabarani?”
“Ndiyo, kazi nzuri sana, nilitaka kukujaribu ili nione kama watu wanaweza kuingia hapa kwangu kwa urahisi tu. Safi sana, chukua hii elfu kumi utakunywa soda”

“Teh! Teh! Teh! Ahsante bosi nitaendelea kufanya kazi kwa uaminifu mkubwa.”
Gari likaingizwa ndani ya kuegeshwa sehemu yake, Lina akashuka na kumfungulia Phillip mlango kisha kumwita mlinzi na kumtambulisha kwamba huyo alikuwa rafiki pekee aliyeruhusiwa kumtembelea wakati wowote usiku na mchana bila kizuizi, Phillip na mlinzi wakashikana mikono.

“Naitwa Phillip.”
“Mimi ni Marwa, kutoka Taa-rime!”
“Nafurahi kukufahamu.”
“Na mimi hibyo, hibyo!”

Phillip na Lina wakaanza kupandisha ngazi kuingia ndani ambako tofauti na watu wenye uhusiano wa kawaida, Lina akaanza kumtembeza Phillip kwenye nyumba yake kuanzia jikoni kisha kupandisha ngazi hadi kwenye chumba chake cha kulala ambako aliketi kitandani na kumwomba Phillip afanye hivyo hivyo.
“Kaa tu usiogope, hakuna tatizo, jisikie uko nyumbani.”

“Ahsante.”
Kwa mara ya kwanza tangu apoteze familia yake, Phillip alijisikia faraja ya kweli moyoni mwake, akaketi kitandani kando ya Lina na wakaanza kuongea mambo mbalimbali kuhusu maisha tangu walipoachana, Lina hakuficha ukweli wake kwamba tangu aungue kwa moto hakuwahi kukutana na mwanaume hata akamwambia neno “Nakupenda” ingawa alikuwa na mafanikio makubwa mno maishani mwake.

“Pole!”
“Ahsante Phillip.”
“Nakupenda.”
“Kha!”
“Mbona unashangaa?”
“Una uhakika?”

“Ndiyo.”
“Hausemi tu kwa sababu una mfadhaiko baada ya kupoteza mke na watoto?”
“Hapana, nakupenda Lina, nilivutiwa na wewe wakati ule ukiwa na sura ile, sidhani kama nahitaji kubadilika leo ukiwa na sura hii, upendo wangu ni wa kweli, naomba uniamini.”

“Ghafla mno…”
“Mapenzi ya kweli hayana maandalizi, isitoshe mimi ndiyo chanzo cha yote yaliyokukuta, naomba uamini nakupenda. Wewe ndiyo utakuwa faraja ya mtima wangu, utanipunguzia maumivu niliyonayo ndani, nikiwa na wewe nitakuwa mtu tena”

Lina akainamisha kichwa chake chini, machozi yakaanza kudondoka na kulowanisha sakafu. Phillip akamsogelea na kumnyanyua, kisha kumkumbatia, akamvua wigi na sura ya bandia, halafu akamlaza chali kitandani na kuanza kumpiga mabusu mfululizo. Hisia za Lina zikawa kama mtu aliyekuwa akipigwa na shoti ya umeme.
“Usinishangae Phillip, ni miaka mingi sijakutana na jambo hili.”
“Basi leo ndiyo leo.”
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.47.


KILIKUWA chumba chenye ukubwa usiopungua mita za mraba hamsini, kilijazwa samani nyingi zenye thamani kubwa, ukutani kukiwa na picha kubwa ya mwanaume akiwa na watoto wawili mapacha. Mwanaume kwenye picha hiyo ndiye aliyekuwa ndani ya chumba hicho akiwa ameketi nyuma ya meza kubwa, akiiangalia picha kubwa iliyokuwa mbele yake kwa umakini, ghafla akatabasamu.
“Siwezi kuamini kama hawa watoto wako mikononi mwangu!” aliwaza Victor Federov.

Moyo wake ulikuwa umejaa furaha kubwa kupindukia, ujio wa Dorice na Dorica ambao hivi sasa waliitwa Mariya na Marina ulifanyika kwa wakati muafaka. Kitu pekee kilichomsumbua akilini mwake ni kwa namna gani angeweza kuificha siri hiyo isivuje, kwani aliwahusisha watu wengi katika zoezi la utekaji na alielewa duniani hapakuwa na siri ya watu wawili, lazima siku moja kama si Ditrov basi watu aliokuwa nao, mmoja lazima angefungua mdomo na kuueleza ulimwengu namna watoto wake walivyopatikana. Mawazo hayo yalimfanya auchukue mkono wa simu uliokuwa kando yake na kuanza kupiga namba ya Ditrov.

“Ndio mkuu.”
“Uko wapi?”
“Ofisini kwangu.”
“Naomba uje haraka.”
“Sawa.”
Simu ikakatika.

Dakika tano baadaye mlango wa ofisi yake ukagongwa na Ditrov akaingia na kuketi mbele ya meza ya Victor. Mwili wake ulikuwa umeongezeka zaidi sababu ya mazoezi, fedha nyingi aliyolipwa katika zoezi la kuwateka Dorice na Dorica ilikuwa imebadilisha kabisa maisha yake, sasa hakuhangaikia mambo madogo madogo tena, mara nyingi baada ya kazi alitumia muda mwingi kwenye jengo la mazoezi.

“Ndio bosi nimeitika wito.”
“Ahsante, suala langu sio kubwa, nataka kukuuliza kama watu wote ulioshirikiana nao kwenye operesheni hii unawafahamu!”
“Sana, ni rafiki zangu.”
“Wakati wowote unaweza kuwapata?”
“Bila shida.”

“Sasa sikiliza.”
“Ndiyo.”
“Duniani hakuna siri ya watu …?”
“Wawili.”
“Ningependa kuona watu hawa wote wanakufa.”
“Mh!”

“Mbona umeguna? Nitalipa dola laki tano.”
“Kweli?”
“Bila shaka.”
“Kama dola laki tano zipo, mimi naweza kufanya hivyo kazi bila matatizo. Ni kiasi cha kutafuta Blood Pressure Uplifter, ambayo wakishainywea kwenye chai au kinywaji chochote, shinikizo la damu litapanda na watakufa mmoja baada ya mwingine.”

“Unaweza kufanya hivyo?”
“Bila matatizo, ndiyo kazi yangu.”
“Hiyo dawa utaipata wapi?”
“Ninayo.”
“Kabisa?”

“Tangu enzi za KGB,” Ditrov aliongea akimaanisha Shirika la Ujasusi la Urusi ambalo aliwahi kulifanyia kazi miaka mingi kabla.
“Basi kama ni hivyo, tekeleza.”
“Fedha yangu?”
“Ukimaliza kazi njoo unione.”

“Ahsante.”
Ditrov akaondoka kichwani mwake akifikiria dola laki tano ambazo angelipwa akimaliza kazi ya kuwaua watu wote alioshirikiana nao kwenye zoezi la utekaji, alielewa ingekuwa kazi rahisi sababu wote walimwamini. Alichokifanya kuanzia siku hiyo ni kuwa anawaita mmoja baada ya mwingine na kumpakia ndani ya gari lake hadi ufukweni mwa bahari kwa ahadi kwamba walikuwa wanakwenda kupunga upepo, huko aliitoa dawa hiyo na kumchanganyia mlengwa kwenye kinywaji, dakika chache baada ya kunywa hali ilibadilika, Ditrov akambeba ndani ya gari, njiani alikufa.

Alichokifanya ni kutumia boti maalum aliyopewa na Victor Federov kuubeba mwili huo mpaka katikati ya bahari ambako aliufunga jiwe na kuuzamisha hadi kwenye kina cha maji, akiamini huko usingeonekana milele. Alifanya hivyo mpaka akawamaliza wote, akimpa taarifa Victor Federov juu ya maendeleo.
“Hongera sana, njoo ofisini leo usiku kama saa saba hivi uchukue hundi yako.”

“Nakuja bosi.”
Katika muda huo huo aliopangiwa, ofisi ikiwa haina mtu, Ditrov alipandisha ngazi mpaka ofisini kwa Victor Federov ambako alipokelewa kama shujaa, akaketi kusubiri hundi yake, Victor alipofungua droo, badala ya kutoka na kitabu cha hundi, mkono ulitoka ukiwa na bastola yenye kiwambo cha kuzuia sauti.

“Nilikuambia duniani hakuna siri ya watu wangapi?”
“Wawili.”
“Inabidi Ditrov ufe ili nibaki peke yangu.”
“Hapana mzee nisamehe.”
“Paa! Paa! Paa!”

***
Kitanda kilikuwa kinacheza kama vile ni cha spiringi, ingawa kilitengenezwa kwa mbao imara za mninga, Phillip alikuwa kazini akijituma impasavyo mwanaume aliyekuwa akitafuta sifa. Alitaka kumwonyesha Lina kwamba uzuri wake haukuwa umbile la sura tu, bali hata kwenye ukanda wa sita kwa sita alikuwa ni mtaalam haswa.

Lina alikuwa akilia, si kwa maumivu bali kwa raha aliyokuwa akiipata. Ilikuwa imepita miaka mingi tangu akutane mara ya mwisho na mwanaume kimwili, moto uliomteketeza uliondoka na uzuri wake wote, hivyo hakuna mwanaume aliyevutiwa naye labda kwa wale walioangalia maumbile, maana mtaji peke yake aliokuwa nao ulikuwa ni hips zilizochomoza kama vilele vya mlima Meru!

Miili yao ilikuwa imelowa kwa jasho ingawa kulikuwa na kiyoyozi chumbani kilichoonyesha joto lilikuwa sentigredi kumi na nane. Mashuka yote yalikuwa yamelowa, kijana Phillip akiwajibika, kwake kitendo cha ngono kilikuwa ni njia ya kumsahaulisha yaliyokuwa yakimsumbua akilini mwake, aliichukulia ni kama faraja.

“Ahsante!” Lina alitamka maneno hayo Phillip alipojitupa kando yake.
“Karibu.”
“Sijawahi.”
“Hujawahi nini?”
“Kukutana na mtu wa aina yako, umezidi kunitia uchizi.”
“Nakupenda Lina.”

“Nakupenda pia Phillip, miaka yote, kama uliyoyasema ni kweli, basi mapenzi yangu kwako ndiyo yalinisababishia hata huu ulemavu.”
“Ndio maana niko na wewe, ndio njia pekee ya kukulipa kwa kile ulichopoteza kwa ajili yangu.”

Wakakumbatiana, Lina akiwa tayari kuanza tena lakini Phillip alimshauri wapumzike. Nusu saa baadaye ndipo walipoendelea mpaka usiku wa manane, kiasi kwamba Phillip hakuweza kuondoka tena, huo ndio ukawa mwanzo wa kuishi ndani ya nyumba hiyo akifarijiana na Lina ambaye kwake Phillip alikuwa kila kitu. Miezi sita ikapita na taarifa za uhusiano wao zikaenea kila mahali, wazazi wa Genevieve wakafurahishwa na jambo hilo wakiamini Phillip angesahau maumivu aliyokuwa nayo.

“Kuna jambo nataka kukueleza.”
“Jambo gani?” Lina aliuliza.
“Nimefikia uamuzi wa kukuoa, wewe peke yako ndiye unaweza kunisahaulisha vifo vya mke na watoto wangu,” alisema Phillip.

Hakuwa na habari kabisa juu ya kilichotokea, kwamba watoto wake hawakuwa marehemu bali walitekwa na vijana wa Victor Federov.
“Unasema kweli Phillip?”
“Kweli kabisa.”
“Nipo tayari.”
 
 
 
 
 MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.48.

“Lakini kuna kitu kimoja tu nataka kukueleza, kama utakubaliana nacho basi tutafunga ndoa yetu ili tuishi kwa furaha, kikikushinda basi tena maana mimi sina la kufanya, ni maumbile na sitaki kurudia tena kufanya kitendo nilichokifanya huko nyuma.”

“Kitu gani hicho unachotaka kunieleza, usizunguke, niambie tu.”
“Bila shaka nimewahi kukueleza kwamba nina uwezo wa kutoa mbegu za kiume lakini hazina uwezo wa kurutubisha yai la mwanamke, hii ina maana kama tukioana hatutakuwa na uwezo wa kuwa na motto. Je, hilo ni kikwazo kwako?”
“Hapana hata kidogo, cha muhimu kwangu ni kuwa na mtu anayenipenda, watoto ni majaliwa ya Mungu.”

“Ahsante Lina,” Phillip aliongea akimvuta na kumkumbatia, kilichofuata baada ya hapo ni sauti zao kuendelea kushuka huku wakinong’ona, neno I love you, likisikika mara nyingi, ghafla ukimya ukasikika na milio ya “Jwig!Jwig!Jwig!” ikasikika! Kilikuwa ni kitanda kikipiga kelele. Phillip alikuwa kazini akifanya kila alichoamini alikuwa na utaalam nacho ingawa hakuwa na uwezo wa kupata mtoto.

Siku iliyofuata kazini Lina alikuwa na jambo moja tu, kuwataarifu rafiki na wafanyakazi wenzake juu ya kilichokuwa kikifuata maishani mwake. Kila mtu akawa na hamu ya kumwona Phillip, aliyejitolea kumuoa Lina. Siku ya siku ikafika, Phillip akatambulishwa kwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam kwenye tafrija ndogo iliyofanyika katika Hoteli ya

Johannesburg, ambayo pia Phillip aliitumia kumvisha Lina pete ya uchumba.
Kamati ikaundwa na utaratibu wa michango kama ilivyozoeleka nchini Tanzania ukafuata. Kiasi kikubwa cha fedha kikakusanywa na hatimaye harusi kubwa tena ya kifahari iliyosimamiwa na familia ya Lina pamoja na familia ya Genevieve na ndugu wa Phillip ikafanyika, ndoto ya Lina kuolewa na Phillip ikatimia.

Wakaanza kuishi pamoja kama mke na mume, katika maisha yaliyojaa furaha, huzuni zote zilizokuwa zimewafunika zikaondoka ingawa Phillip hakuisahau familia yake. Kila Jumapili ilikuwa ni lazima asindikizwe na mke wake wakiwa njiani kuelekea kanisani hadi makaburini ambako alisali akimkumbuka mke wake Genevieve na watoto wao Dorice na Dorica.

Hakuwa hata na hisia kidogo kwamba watoto wake walikuwa upande wa pili wa dunia, nchini Urusi wakiishi na baba yao wa kuwazaa, pia wakiwa hawana kumbukumbu ya mahali walikotokea baada ya kumbukumbu zote kufutwa kichwani kwa sindano za dawa iitwayo Memory Eraser.
***
Ditrov alikuwa amelala sakafuni, risasi mbili zikiwa zimepenya mwilini. Kulikuwa na dalili zote kwamba alikuwa amekufa na Victor akiamini siri yake ya kuwatorosha Dorice na Dorica kutoka Tanzania isingevuja, alisogeza mfuko mkubwa wa nailoni aliokuwa ameuandaa kwa ajili ya kazi hiyo na kuanza kumwingiza ndani yake huku mwili wake wote ukitetemeka.

Alikuwa na uhakika asilimia mia moja hakuna mtu angegundua kilichokuwa kikiendelea, taratibu akausogeza mfuko kando na kuanza kuisafisha sakafu mpaka alipohakikisha imetakata bila doa lolote la damu, akaunyanyua tena mfuko na kuupeleka mpaka kwenye lifti. Alipoingia ndani akabonyeza alama iliyoandikwa G, ili kuiamuru lifti ishuke moja kwa moja mpaka chini kulikokuwa na maegesho ya magari.

“Afande! Afande! Afande!” aliita alipotoka kwenye lifti bila kuuchukua mwili wa Ditrov, alitaka kuhakikisha hakuna mtu eneo hilo, ukimya ulimthibitishia kwamba aidha askari alikuwa amelala au alikuwa amepandisha juu kwa walinzi wenzake.

Akarejea kwenye lifti na kufungua, akaubeba mwili mpaka kwenye gari na kufungua buti kisha kuuingiza ndani na kufunika. Kwa kasi akazunguka upande wa dereva na kufungua mlango, akawasha na kuondoka kwa kasi, sehemu ya kutokea askari walimsimamisha lakini walipogundua ni bosi wao hawakuwa na swali.

“Nahitaji jiwe, kamba ninayo,” aliwaza akiendesha gari kuelekea nyumbani kwake.

Nyumba yake ilijengwa ufukweni kabisa na alimiliki boti iendayo kasi, hiyo ndiyo alipanga kuitumia kwa ajili ya kazi iliyokuwa mbele yake. Bahati nzuri hakuwa na mlinzi, alitumia mbwa na nyaya za umeme, hivyo alichofanya baada ya kuingia ndani ya ngome yake kabla hajafungua buti na kuutoa mwili wa Ditrov ni kutafuta jiwe kubwa na kushuka nalo hadi ufukweni, akalifunga vizuri na kamba.

Bila kupoteza wakati akaja kwenye gari, akafungua buti na kuutoa mwili wa Ditrov ukiwa kwenye mfuko wa nailoni usiovujisha damu na kuubeba begani huku akikimbia nao ufukweni.

Akaangaza macho yake huku na kule bila kuona mtu yeyote zaidi ya mbwa wake waliokuwa wakibweka, kilichosikika dakika chache baadaye ni muungurumo wa boti ikikata maji kuelekea katikati ya bahari.

Dakika ishirini hivi baadaye, alizima injini na boti kusimama. Giza lilikuwa nene kila upande, hivyo hakumhofia mtu yeyote, haraka akalikamata jiwe na kulitupa majini kisha kuusukuma mfuko, taratibu ukaingia majini na kuanza kuzama.

Huo ukawa mwisho wa Ditrov. Badala ya kusikitika, Victor Federov alitabasamu na kuwasha boti yake kisha kuondoka kwa kasi kurejea nyumbani ambako aliegesha na kuingia ndani bila mtu yeyote kugundua.

Hakupata usingizi hata kidogo mpaka kulipopambazuka asubuhi,akajiandaa kwa ajili ya kwenda kazini ambako alifanya kazi kama kawaida, saa nne na nusu alimpigia simu katibu muhtasi wake na kumwomba amwitie Ditrov.
“Hajaonekana tangu asubuhi bosi.”

“Haiwezekani, mtafuteni haraka sana nina kazi ya kufanya naye.”
“Sawa bosi.”
***
“Jina lako unaitwa nani?”
“Marina!”
“Na mwenzako?”

“Mariya.”
“Ninyi ni mapacha?”
“Ndiyo.”
“Baba yenu ni nani?”
“Victor Federov.”

“Ahaaa! Kumbe ni ninyi?”
“Ndiyo.”
“Karibuni sana Moscow International School.”
“Ahsante.”

Victor Federov aliwapenda sana watoto wake, kuthibitisha jambo hilo alihakikisha wanapata elimu bora. Alikuwa na fedha nyingi, utajiri wake ulitisha hata kama angetumia fedha zake kwa fujo kiasi gani, haikuwa rahisi kuzimaliza hivyo aliona ni bora kusomesha watoto wake kwenye shule nzuri ili wapate elimu bora itakayowasaidia kuendesha miradi yake vizuri baada ya yeye kuondoka duniani.

Shule aliyoona inawafaa ni Moscow International School, ambayo kwa mwaka kila mtoto alilipiwa milioni ishirini na tano. Watoto walimfurahia baba yao, hawakuwa na kumbukumbu yoyote tena juu ya Tanzania wala Phillip na Genevieve.
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.49.

VICTOR Fedorov alipohakikisha kwamba sasa alikuwa amemaliza zoezi zima la mauaji, alirejea nyumbani kwake na kuingia moja kwa moja chumbani kwake ambako alijitupa kitandani, hakika alijiona mshindi kwa kazi aliyokuwa ameifanya na sasa siri juu ya watoto ilikuwa imebaki kuwa yake peke yake.
Hakupata usingizi hata kidogo mpaka kulipopambazuka asubuhi, akajiandaa kwa ajili ya kwenda kazini ambako alifanya kazi kama kawaida, saa nne na nusu alimpigia katibu muhtasi wake na kumwomba amwitie Ditrov.

“Hajaonekana tangu asubuhi bosi.”
“Haiwezekani, mtafuteni haraka sana nina kazi ya kufanya naye.”
“Sawa bosi,” katibu muhtasi alijibu.
Kwa muda wa nusu saa katibu muhtasi aliendelea kumtafuta Ditrov kwa namba zote alizozifahamu lakini hakupatikana, yeye pia akaingiwa na hofu, kwani haikuwa kawaida ya Ditrov kutofika kazini bila sababu yoyote na hakuwahi hata mara moja kuzima simu zake za mkononi.

“Lazima atakuwa na matatizo huyu,” aliwaza katibu muhtasi akinyanyua simu ili amtaarifu bosi wake.
“Ngrii! Ngrii! Ngrii!” simu ilisikika upande wa pili ikiita.
“Ndiyo.”
“Bosi mpaka sasa sijafanikiwa kumpata Ditrov.”
“Umepiga simu yake ya mkononi?”

“Ndiyo, bosi, tena zote mbili.”
“Sasa atakuwa wapi huyu?”
“Kwa kweli hata mimi inanishangaza.”
“Jaribu kwa mara ya mwisho kumtafuta nitahitaji majibu kama bado atakuwa hapatikani basi taarifa itolewe polisi, sawa?”
“Nitafanya hivyo,” alijibu katibu muhtasi na kukata simu.

***
Wakaanza kuishi pamoja kama mke na mume, katika maisha yaliyojaa furaha, huzuni zote zilizokuwa zimewafunika zikaondoka ingawa Phillip hakuisahau familia yake, kila siku ya Jumapili ilikuwa ni lazima asindikizwe na mke wake wakiwa njiani kuelekea kanisani hadi makaburini ambako alisali akimkumbuka mke wake Genevieve na watoto wao Dorice na Dorica.

Wiki moja baada ya kufunga ndoa maisha yakiwa ya furaha Lina alitakiwa kurejea kazini, hivyo alilazimika kumpa Phillip taarifa juu ya habari hiyo.
“Mpenzi!”
“Ndiyo,” Phillip aliitika
“Kesho nitaanza kazi.”

“Vyema mke wangu mimi nitakuwepo tu hapa nyumbani.”
“Nyumbani?”
“Ndiyo.”
“Ok! Nahitaji kufahamu ulisomea nini?”
“Nilisomea mambo ya sheria.”
“Unao uzoefu wa kutosha?”

“Kabisa.”
“Basi nitakutafutia kazi nahitaji utoke nyumbani ili usiwe mpweke.”
“Mwaa! Mwaa!” Phillip alimbusu Lina mfululizo.
“Ahsante nakupenda Phillip, hakika nitakufanya kuwa mwanaume mwenye furaha siku zote.”

“Nitafurahi sana Lina, nakuwa mpweke zaidi pale ninapokumbuka familia yangu, hakika niliipenda lakini naona yalikuwa mapenzi ya Mungu wote wakaniacha, naamini ujio wako kwangu utanirejeshea furaha iliyopotea miaka mingi kabla.”

“Hakika nakupenda amini,” Lina aliongea huku akimkumbatia Phillip wote kwa pamoja wakajifunika shuka na kulala. Kwao usiku ulionekana kuwa mfupi, hakuna aliyekuwa akitamani kumwacha mwenzake kitandani lakini kwa Lina ilikuwa ni lazima afanye hivyo kutokana na kazi yake. Hivyo alijilazimisha na kuamka kitandani kisha kuingia bafuni kuoga na kujiandaa tayari kwa kwenda kazini.
“Nitarejea muda si mrefu, nikuletee nini mpenzi?”
“Mh! Mh!” Phillip aliguna.

“Sema basi nikuletee kitu gani?”
“Nakuhitaji wewe,” alisema Phillip akimvuta Lina na kumpiga busu huku akimtakia siku njema.
Taratibu akatoka chumbani na kufunga mlango nyuma yake huku akimwacha Phillip kitandani.

****
Kwa muda wa saa tatu katibu muhtasi aliendelea kujaribu simu ya Ditrov bila majibu yoyote na hata alipojaribu kutuma mtu nyumba kwake na sehemu mbalimbali ambazo alifahamu angeweza kuwepo, bado hakupatikana.
“Ni vyema nikamtaarifu bosi juu ya Ditrov kwamba hapatikani,” aliwaza akinyanyua simu na sekunde mbili tu baadaye sauti nzito ikasikika upande wa pili.

“Ndiyo.”
“Bosi sijafanikiwa kumpata.”
“Unasema?”
“Ditrov hapatikani tumejaribu kufuatilia sehemu mbalimbali ambazo mara nyingi hupenda kutembelea, majibu yanayotolewa ni yaleyale kwamba hajaonekana.”

“Mh! Piga simu polisi kisha utoe taarifa, inawezekana ametekwa au kuuawa na watu fulani, unanisikia?”
“Ndiyo.”
“Nahitaji kufahamu majibu ya polisi mara moja na kama inawezekana msako mkali ufanyike, nataka Ditrov apatikane haraka iwezekanavyo,” alisema Victor Fedorov kwa hasira kali na kukata simu.

“Haa! Haaa! Haaa!” Victor Fedorov alicheka huku akinyanyuka kitini taratibu akasogelea picha kubwa iliyokuwa ukutani kisha kuibusu.
“Merina! Mariya! Nitawapenda mpaka kufa siko tayari kuwapoteza kwa gharama yoyote ile, ndiyo maana nimeamua kumuua Ditrov ili kuficha siri hii. Mwaa! Mwaa!” Victor Fedorov aliongea akiikodolea macho picha hiyo.

Je, nini kitaendelea? Ditrov ndiyo huyo amezamishwa baharini.
 
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.51.

ILI asigundulike kwa mauaji ya Ditrov anampigia simu katibu muhtasi wake akimtaka amtaarifu Ditrov kwamba alikuwa akimhitaji ofisini kwake kwa kazi maalum. Ditrov anatafutwa kwa muda bila mafanikio.

Katibu muhtasi anamrejeshea majibu kwamba mpaka wakati huo bado Ditrov alikuwa hajapatikana sehemu yoyote ile.
Uamuzi pekee wa Victor Fedorov aliyekuwa akifahamu wazi mauaji aliyoyafanya, anaamuru taarifa hizo zitolewe kwa jeshi la polisi ili msako maalum ufanyike haraka na Ditrov apatikane.

Ili kuficha siri ya mauaji ya Ditrov, Victor Fedorov anaudanganya umma wa Urusi kwamba naye pia yuko tayari kufanya kila kinachowezekana ili mradi tu Ditrov apatikane, hivyo ameamua kwenda makao makuu ya polisi na kuzungumza na mkuu wao ili kama jeshi hilo lingehitaji msaada wowote kutoka kwake basi wasisite kumweleza.

Baada ya maongezi hayo wote wawili waliagana na Victor Fedorov akatoka nje ya ofisi moja kwa moja akaliendea gari lake na kupanda kisha kuwasha na kuondoka kwa kasi ya ajabu, kwa kumwangalia alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa kwa upotevu wa Ditrov lakini ukweli ni kwamba aliidanganya dunia, aliufahamu ukweli wote na mpaka wakati huo alishaamini kwamba Ditrov alikuwa marehemu hivyo isingekuwa rahisi kupatikana tena.
Je, nini kinaendelea? SONGA NAYO…

Jeshi la polisi nchini Urusi lilidhamiria kufanya kila kilichowezekana ambapo Ditrov alitafutwa kila pembe, Urusi ikabinuliwa nje ndani, vyombo vya habari, zikiwemo televisheni, vikirusha matangazo na kuonyesha picha ya Ditrov kwamba alikuwa amepotea katika njia ya kutatanisha na alikuwa akitafutwa kwa udi na uvumba na yeyote ambaye angefanikisha kupatikana kwake awe mzima au marehemu basi angelipwa kiasi kikubwa cha fedha.

Watu nchini humo wakanyanyuka, wakaingia katika msako, Ditrov alikuwa akisakwa, kiasi kikubwa cha fedha alichokitangaza Victor Fedorov kiliwachanganya watu wengi.Wakati msako huo ukiendelea, Victor Fedorov alikuwa akifuatilia kila kitu kwa karibu, aliwaona watu wote kuwa wajinga kwake, kwani ukweli ni kwamba mpaka wakati huo Ditrov hakuwa tena hai, hicho ndicho alichoamini, hivyo hata zawadi aliyokuwa ameitangaza kwa umma alifahamu wazi kwamba isingekwenda kwa mtu yeyote yule.

“Hata kitokee nini hawawezi kumpata niko tayari kufanya kila kitu watakachohitaji ili mradi tu kuuficha ukweli huu, sipo tayari, duniani hakuna siri ya watu wawili, hivyo kifo cha Ditrov kimefanya siri kubaki kwangu peke yangu, Mungu atanisamehe,” aliwaza akiangalia tangazo lililomwonyesha Ditrov likipita kwenye televisheni kubwa iliyokuwa ofisini kwake.

Mpaka wakati huo jeshi la polisi lilishafanikiwa kukagua hospitali zote nchini Urusi na kupata kibali cha kuingia katika vyumba vya kuhifadhia maiti kumsaka mtu huyo lakini bado hakupatikana sehemu yoyote, nao pia wakaanza kupoteza matumaini kwani upotevu wa mtu huyo ulisababisha kusimamisha kazi zao nyingi sana kutokana na Victor Fedorov kuwa na nguvu na ushawishi mkubwa sana ndani ya nchi hiyo.

Wiki ya kwanza ikapita msako ukiendelea kwa nguvu zote, wiki ya pili nayo ikapita hatimaye mwezi bila Ditrov kupatikana sehemu yoyote. Jeshi likashindwa kuelewa ni wapi alikokuwa mtu huyo.
“Ngrii!Ngrii!Ngrii!” mlio simu ukasikika ndani ya ofisi ya Mkuu wa Polisi.
“Ndiyo.”

“Sawa mkuu, hakuna shida hata sisi wenyewe tumeona ni vyema tukapumzika ili tujipange tena upya kutafuta njia nyingine, zoezi hili limekuwa gumu sana kwetu,” aliongea Mkuu wa Polisi ofisini kwake.

Victor Fedorov aliyekuwa upande wa pili wa simu ndiye aliyekuwa akiongea na mkuu huyo wa polisi akimpa ushauri wa juu ya zoezi hilo kwamba sasa lilikuwa limeshindikana hivyo watafute mbinu nyingine zitakazowezesha kupatikana kwa Ditrov.

Mkuu wa polisi alikubaliana na Victor na kusitisha zoezi hilo akiwa haelewi kabisa upande wa pili wa myu huyo, akaunga mkono hoja na kukata simu.

“Sasa nina hakika Ditrov atakuwa amekufa, laiti kama angepona angeshajitokeza ninavyomfahamu mimi ni mtu hatari sana huyu, hawezi kuwa hai akaendelea kujificha ni lazima angetoka na kuuelezea umma kila kitu,” aliwaza Victor Fedorov akiwa ndani ya ofisi yake.

***
Kitendo cha Lina kuongea na bosi wake na kumweleza kwamba katika ofisi yao alihitajika mwanasheria anayefahamu vyema sheria, kilikuwa ni kama bahati ya mtende, akatembea taratibu na kurejea ndani ya ofisi yake, huku machozi ya furaha yakimtoka, alishindwa kuelewa ni bahati gani iliyokuwa ikimtokea, machozi ya furaha yakaendelea kumtoka.

“Ahsante baba, Mungu kweli unatenda, hatimaye Phillip naye amepata kazi?” alijiuliza.
Kwa siku nzima, muda kwa Lina ulikwenda taratibu, saa zilikuwa hazisogei hamu yake kubwa ikiwa ni kurejea nyumbani na kumweleza Phillip juu ya habari aliyokuwa ameipata.
“Phillip atafurahi sana kusikia habari hii,” aliwaza.

Akiwa ofisini kwake akakivuta kiti na kuketi, sauti nyingi zikimwijia kichwani mwake, tangu siku aliyokutana na Phillip jinsi alivyomweleza kwamba bado alikuwa akimpenda na hatimaye kufunga ndoa na sasa alikuwa mke wa mwanaume aliyempenda kwa moyo wake wote.

“Ni kweli Phillip amefiwa na mke na watoto wake, lakini ilikuwepo sababu jambo hilo litokee ili mimi niweze kumpata, masikini Genevieve watoto wake Dorice na Dorica nauahidi moyo wangu kumpa Phillip furaha yote mpaka mwisho wa maisha yetu, hakika ninampenda kwa dhati,” alijisemea Lina kwa sauti ya chini chini.

Muda wa kurejea nyumbani ulipofika, hakuwa na sababu ya kuendelea kukaa ofisini, haja ya moyo wake ilikuwa ni kufika nyumbani na kumkuta mume wake mpendwa Phillip ili amweleze habari njema aliyokuwa nayo.
Huku akitembea kwa madaha, mkononi akiwa amening’iniza funguo akalisogelea gari lake akaingia ndani na kisha kuondoka kwa mwendo wa kasi, mawazo yake yote yakiwa kwa Phillip.

“Ninampenda, nafahamu wazi hata yeye ananipenda hanidanganyi hata kidogo, nitafanya kila kitu kuhakikisha simpotezi, mwanaume niliyempenda akanifanya nikapata matatizo mengi maishani mwangu ndiye aliyeko ndani ya nyumba yangu sasa tena akiwa mume wangu!” aliongea Lina huku akizidi kukanyaga mafuta.

Kwa mwendo wa saa moja na dakika kadhaa tayari alikuwa nje ya lango la nyumba yake, bila kuchelewa akapiga honi na lango likafunguliwa, akapita moja kwa moja ndani bila kusema kitu chochote na mlinzi wake.

“Mh!” mlinzi aliguna akishuhudia gari likizidi kutokomea. Kilikuwa ni kitendo cha ajabu sana kwani mazoea aliyokwishajijengea ilikuwa ni lazima asimamishe gari na kumtania kidogo lakini siku hiyo haikuwa hivyo kwa Lina ilionekana kuwa tofauti.
“Pengine anaumwa au kuna nini kimempata? Si kawaida ya bosi wangu kuwa hivyo lazima takuwa na walakini. Ngoja nisogee karibu nione,” aliongea mlinzi akisogea kwa mwendo wa pole.

“Bosi!” aliita.
“Bee!” Lina akaitika akitembea kwa kasi kuelekea lango la kuingilia ndani ya nyumba yake.
“Nini tatizo si kawaida yako kuwa hivyo unaumwa?”
“Mh!” alijibu akiingia ndani.
Mlinzi huyo alibaki hapo akiwa haelewi ni kitu gani kilikuwa kimempata bosi wake huyo, haraka akapata wazo kichwani mwake akaamua kuzunguka upande wa pili wa nyumba ambako dirisha la chumba cha bosi lilikuwepo huko.

“Ngoja nisimame hapa kama kuna tatizo nitajua kupitia hapa,” aliongea mlinzi akisogea kwa kunyata dirishani.
“Darling! Darling! Uko wapi? Tafadhali njoo, nakuhitaji haraka sana!” sauti ya Lina ilisikika.
“Yes baby!” (Ndio mpenzi) sauti ya Phillip ikasikika kwa chini kutoka chumbani.
“Bado umelala?” Lina aliuliza.

“Ndiyo!” Phillip akajibu.
Kwa mwendo wa haraka h Lina akatembea kuelekea chumbani akafungua mlango na kuingia, Phillip bado alikuwa kitandani akiwa amelala na shuka likiwa limemfunika mpaka kichwani.
“No! Unaumwa?” Lina aliuliza.
“Mh!” Phillip alijibu akitingisha kichwa.

Bila kuchelewa Lina akalivuta shuka na kulitupa pembeni, Phillip akaonekana na alipomwangalia vyema usoni aligundua alikuwa akilia kwani macho yake yalivimba kupita kiasi.
“What happened?” (Nini tatizo?)
“Familia yangu, mke na watoto wangu wapendwa!” alijibu Phillip kwikwi ya kulia ikizidi kumkaba.

“Sikiliza mume wangu hebu niambie unachohitaji tufanye nini ili upate furaha iliyopotea, niambie niko tayari kutoka moyoni mimi siipendi hali hii!”
“Watoto! Nahitaji kupata mtoto angalau mmoja,” aliongea Phillip akilia kwa uchungu.

Maneno hayo pekee yalimfanya Lina aelewe ni kiasi gani Phillip alikuwa katika upweke bila kuchelewa akaanza kuvua nguo moja baada ya nyingine na kuzitupa pembeni kisha kukisogelea kitanda na kupanda juu yake akamvuta Phillip na kumkumbatia, mabusu mfululizo yakishuka juu ya mwili wa Phillip na neno I love you, likisikika.

Mlinzi akiwa amesimama nje ya dirisha bila kuelewa ni kitu gani kilikuwa kikitokea alisikia sauti nyingine.
“Jwig!Jwig!Jwig!” kitanda kikipiga kelele.
“Mh!” mlinzi aliguna akiondoka eneo hilo.

Je, nini kitaendelea? Nini kitatokea baada ya Lina kumweleza Phillip juu ya kazi iliyopatikana ofisini kwao? Je, watafanya nini kupata watoto? Fuatilia kesho kama kawa USIKU MWEMA NAWAPENDA NYOOOTE.....
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.52.

KITENDO cha Lina kuongea na bosi wake na kumweleza kwamba katika ofisi yao alihitajika mwanasheria anayefahamu vyema sheria, kilikuwa ni kama bahati ya mtende, baada ya kumaliza maongezi Lina anatembea na kurejea ndani ya ofisi yake, huku machozi ya furaha yakimtoka, anashindwa kuelewa ni bahati gani iliyokuwa ikimtokea.

Muda wa kurejea nyumbani unapofika, ni wakati huo ndiyo haswa aliokuwa akiusubiri kwa hamu kubwa, ili akamweleza Phillip habari njema aliyokuwa ameipata.Moja kwa moja anatembea kutoka nje ya ofisi yake kisha kulielekea gari lake aina ya Land Cruiser, anafungua mlango na kuingia ndani yake kisha kuliwasha na kuliondoka kwa mwendo wa kasi mawazo yake yote yakiwa kwa Phillip.

Kwa mwendo wa saa moja na dakika kadhaa tayari alikuwa nje ya lango la nyumba yake bila kuchelewa akapiga honi na lango likafunguliwa, akapita moja kwa moja ndani bila kusema kitu chochote na mlinzi wake, hali ambayo ilimshtua sana mlinzi huyo, kwani haikuwa kawaida ya Lina kufanya hivyo ilikuwa ni lazima amtanie kidogo kisha kuelekea kwenye maegesho.

Hofu inamwingia mlinzi, hivyo kumlazimu kumfuata kujua ni kitu gani kilikuwa kimempata bosi wake, ananyata mpaka karibu na dirisha la chumba na kusikiliza, anasikia maongezi kidogo na baada ya muda sauti ya kitanda inasikika, anaguna na kuondoka eneo hilo.

Upande wa pili wa hadithi hii tunamwona tajiri Victor Fedorov akiwa kifua mbele katika msako wa Ditrov, anaitumia nafasi hiyo kuficha uovu kwani ukweli wote anaufahamu. Zoezi hilo linaendelea kwa muda mrefu bila mafanikio, hatimaye jeshi la polisi linasimamisha msako ili kutafuta njia mbadala ya kumpata Ditrov. Taarifa hizo ndizo zinamfanya Victor Fedorov ajione mshindi.

Je,nini kitaendelea? Ditrov amekufa kweli? Nini hatima ya Phillip na Lina? SONGA NAYO…

Kwa muda wa saa mbili mfululizo, Phillip na Lina walikuwa kitandani kila mmoja akimwonyesha mwenzake ufundi wake wote kuhakikisha anapata furaha aliyoitarajia. Si Phillip wala Lina wote wawili walikuwa katika ulimwengu mwingine wakisahau shida na matatizo yote yaliyokuwa yamepita katika maisha yao.

“Phillip” Lina aliita.
“Naam mke wangu”
“Leo nahitaji uniambie ni kitu gani nitakufanyia ili uwe na furaha, sihitaji kuona machozi yako kila wakati, yananisikitisha mno!”
“Unajua nini?”

“Mh!” Lina aliguna.
“Lina.” Phillip aliita huku macho yake yakimuangalia Lina.
“Bee.”
“Nahitaji mtoto hata mmoja tu”
“Hicho tu?”
“Hakika ndicho.”

“Phillip ni jambo la kuzungumza tu na si kuliweka kichwani mwako.”
“Nitazungumza nini Lina ili hali unafahamu wazi kwamba sina uwezo wa kuzaa!”
“Najua lakini kwangu hilo si tatizo.”
“Kwangu ni tatizo mpenzi, nahitaji mtoto hata mmoja tu ambaye ataniita baba nami nitamwita mwanangu.”

“Mh!” Lina akaguna tena huku akionyesha kusikitishwa na maneno ya Phillip.
Kwa muda wote wapenzi hao walikaa kimya kila mmoja akifikiri ni jinsi gani wangeweza kupata watoto, kwa Lina halikuwa swali gumu kwani yeye alikuwa ni mzima kwa kila kitu tatizo pekee lilikuwa kwa Phillip ambaye mbegu zake hazikuwa na uwezo wa kurutubisha yai la mwanamke hivyo hata kama wangefanya tendo la ndoa kwa muda wa zaidi ya miaka kumi bado uwezekano wa kupata mtoto usingekuwepo.

“Phillip!” Lina aliita akimgusa mumewe begani.
“Nakusikia.”
“Twende tukaoge kisha tujadiliane kuhusu jambo hili.”
“Sawa.” Alijibu Phillip wakinyanyuka kutoka kitandani wakajikongoja hadi bafuni na kuanza kuoga.

Kwa muda wa dakika kumi nzima waliutumia kuoga bafuni huko Lina akiongea mambo mengi kuhusu mapenzi, nia yake kubwa ikiwa ni kumfanya Phillip aondokane na msongo wa mawazo uliokuwepo kichwani mwake. Hatimaye wakamaliza na kurejea tena chumbani ambako Lina alimkaribisha Phillip kwenye kiti maalum kisha yeye akaelekea sebuleni ambako alifungua jokofu akatoa boksi la juisi, akachukuwa glasi mbili na kurejea chumbani.

Kwa mwendo wa madaha huku akiwa ndani ya taulo dogo la rangi nyeupe, Lina alitembea mpaka karibu kabisa na Phillip, akaweka vitu alivyokuwa navyo mezani kisha kumsogelea Phillip na kumbusu mfululizo.
“Mwaa!Mwaaa!Mwaaa!”
“Ahsante,” alijibu Phillip kwa sauti ya chini.

Akiwa hapo, Lina alifungua boksi na kuanza kumimina juisi kwenye glasi moja baada ya nyingine na kumkaribisha Phillip huku akinyanyua glasi na kuipeleka mdomoni mwake kisha kuirejesha tena kwa Phillip kama ishara ya kuonyesha pendo zito alilokuwa nalo juu yake.
“Nakupenda.”
“Mimi pia nakupenda Lina.”

“Ahsante, lakini pia nina habari njema sana kwako.”
“Kuhusu mtoto?” Phillip aliuliza.
“Mh! Hapana lakini ni njema.”
“Tafadhali nieleze usikawie.”
“Mh! Mh!” Lina aliguna mfululizo.

“Hebu shika mapigo ya moyo wangu yanasubiri habari hiyo kwa hamu kubwa, tafadhali nieleze kabla sija…” Phillip aliongea lakini kabla hajafika mwisho wa sentensi yake Lina akanyoosha mkono wake na kuziba mdomo wa Phillip.
“Kunywa juisi kwanza nitakueleza si habari mbaya ni njema sana wewe mwenyewe hakika utafurahi.”
“Kweli?”

“Kabisa.”
Taratibu wakaendelea kunywa juisi huku mikono ya Lina ikipita huku na kule mwilini mwa Phillip huku maongezi matamu kati yao yakiendelea.
Hakika wawili hao walipendana kwa dhati, hawakuwa tayari kukumbuka historia zao za nyuma na hata ilipotokea jambo hilo likajirudia vichwani mwao basi waliona ilikuwepo haja ya kupuuza mawazo hayo na kuendelea na starehe.

Muda ukazidi kusonga bila Lina kufungua mdomo wake kumweleza Phillip kitu chochote, moyoni akitafakari ni jinsi gani habari hiyo ingepokelewa kwani alifahamu wazi kwa Phillip kupata kazi ingekuwa njia moja wapo ya kumwondoa katika msongo wa mawazo aliokuwa nao na hilo lingekuwa limekwisha na jambo ambalo lingebaki kuwa kitendawili katika maisha yao, watoto ambao kwa Lina japo alikuwa mwanamke kamili hakuona umuhimu wowote alichohitaji yeye kwa wakati huo ni kuwa na mwanaume aliyempenda kwa dhati na si kingine.

“Tafadhali Lina hebu nitoe katika mateso haya, nahitaji kufahamu ni kitu gani unataka kunieleza.”
“Hakuna jambo baya mpenzi wangu ni habari juu ya kazi”
“Kazi?”
“Ndiyo.”
“Imefanya nini?”

“Amini tayari umepata kazi”
“Mungu wangu! Unasema kweli Lina?”
“Ni kweli na si ndoto, Phillip tayari umeishika kazi mikononi mwako.”
“Wapi na lini?”
“Hivi sasa ninavyozungumza na wewe kesho asubuhi na mapema tutaongozana, kitu cha muhimu ni vyeti vyako vyote.”

“Sehemu gani?”
“Ofisini kwetu, Phillip ni bahati iliyoje, leo nilipoingia tu ofisini bosi wangu akaniita na kunieleza kwamba shirika letu lilihitaji mtu anayefahamu vyema sheria, akili yangu ikakumbuka kwamba hata wewe ulisoma sheria na uliimudu vyema kazi hiyo.”

“Lina ahsante kwa mara nyingine, nimeamini unanipenda nami ninakupenda pia, moyoni mwangu naanza kuamini kabisa kwamba Mungu alikuwa nayo sababu ya mambo yaliyotokea nyuma ya kupoteza mke na watoto wangu wote akifahamu wazi kwamba nitakutana na mwanamke mwingine atakayenipenda kama Genevieve, Mungu azilaze roho za wapendwa wangu hawa mahali pema peponi amina,” alisema Phillip machozi yakimtiririka, wakati hayo yakiendelea Phillip alihisi ni ndoto lakini alipofungua macho vizuri na kumwona Lina mbele yake akiwa katika sura ya kutabasamu, akanyoosha mikono na kumwelekea ambapo bila kuchelewa Lina akajichomeka katikati ya mikono hiyo wakakumbatiana na kuanza kulia.

***
Wiki moja baadaye Victor Fedorov akiwa ofisini kwake akiamini kabisa kwamba kila kitu kilikuwa kimekwenda kama alivyotaka, anashtushwa na taarifa ya habari kwenye televisheni.
“Mh ni kitu gani hiki?” anajiuliza akisogea karibu kabisa ili kusikiliza kwa ukaribu.

Mamia ya watu nchini Urusi walikuwa wakiandamana kupiga hoja ya jeshi la polisi kuhusu msako wa Ditrov, kwa ilivyoonekana wengi walikuwa wameumizwa na jambo hilo na walichokihitaji kwa wakati huo ni kufahamu ukweli juu ya mauaji hayo, wakisisitiza na kulaani kwa nguvu zote uamuzi huo, wananchi wengi wakidai kwamba nyuma ya pazia kulikuwa na siri nzito kwani kabla Ditrov hajapotea tayari washirika wake wote alioshirikiana nao katika kazi waliaminika kufa tena vifo vya kutatanisha.

“Mh! Ni lazima niwafunge midomo, wataniletea matatizo hawa, sihitaji dunia ifahamu kwamba ninahusika na vifo hivi, nataka iendelee kubaki siri tena siri kubwa, sasa ni wakati wa kuonyesha jeuri ya fedha zaidi ili kulifanya jeshi la polisi likae kimya milele,” aliongea Victor akinyanyua mkono wa simu.
 
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.53.

“Hello!” akaita Victor Fedorov kwa sauti nzito.

“Ndiyo,” sauti upande wa pili ikajibu.

“Ah! Naweza kuongea na mkuu wenu, tafadhali?” aliuliza na ukimya wa ajabu ukatokea kwake akiwa bado ameshikilia mkono wa simu.

Akili yake yote ilisharuka, hakuelewa ni nini kingefuata baada ya hapo kwani kwa jinsi wananchi walivyokuwa wamekasirishwa na mauaji yaliyotokea, waliapa kufanya chochote ili mradi tu wapate ukweli juu ya vifo vya ndugu zao.

Walikuwa tayari kufa lakini jeshi la polisi litoe tamko ambalo lingewaridhisha wote.

Pamoja na kiyoyozi kikali kilichokuwa ndani ya ofisi yake asubuhi hiyo Victor Fedorov alikuwa akitiririkwa na jasho mwili mzima akifahamu wazi kwamba kama ingetokea siri yake ikagundulika basi angepoteza kila kitu alichokuwa nacho, si utajiri tu hata watoto wake na heshima aliyokuwa amejijengea kwa muda mrefu.

Akiwa hapo taswira za watoto wake pacha, Mariya na Marina zikamwijia kichwani mwake, ni watoto hao ndiyo walisababisha afanye mauaji yaliyotokea ili kuficha siri.

“Naitwa Victor Fedorov, nahitaji kuonana na wewe tena ikiwezekana leo hii, ni muhimu sana, kuna taarifa nimeiona ofisi kwangu sasa hivi juu ya wananchi wanavyoandamana imeniumiza sana napenda nami niungane nao kufanya msako huo kwani nimepoteza mtu muhimu sana katika kazi zangu,” alisema akipigapiga meza kuonyesha msisitizo.

“Karibu!” mkuu wa jeshi alijibu upande wa pili wa simu.

“Ok! Nitafika hapo ofisini kwako muda si mrefu, ni vyema tukapata muda wa faragha kwa mazungumzo yetu na ningeomba asiwepo mtu mwingine yeyote wakati wa maongezi hayo.”

“Sawa hilo litafanyika,” sauti upande wa pili ikajibu na hapohapo simu ikakatwa.

Mkuu wa jeshi la polisi hakuelewa siri iliyokuwa ikimsumbua Victor Fedorov, alimwamini kwa asilimia mia moja kwamba naye alikuwa ameumizwa na mauaji hayo ndiyo maana alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha msako unafanyika kwa namna yoyote ile.

Victor Fedorov akasimama kutoka kitini mwake na kutembea mpaka mbele ya kioo kikubwa kilichokuwa ndani ya ofisi yake, hapo akaweka tai yake vyema na kuangalia uso wake na kwa kutumia kitambaa kidogo alichokuwa nacho akajifuta uso wake kisha kuchukua miwani ya rangi nyeusi akaivaa.

Kwa alivyoonekana, alidhamiria kuficha siri ya mauaji lakini msaada mkubwa ungetoka kwa jeshi hilo la polisi na kitu pekee ambacho angefanya ni kutumia fedha tu ili mambo yaende kimya na hatimaye kupotea kabisa.

Akatoka nje ya ofisi yake na kumuaga katibu muhtasi wake kisha kutembea mpaka sehemu alipoegesha gari lake na kupanda, mwendo alioondoka nao eneo hilo ulimshangaza kila mmoja aliyemwona kwani haikuwa kawaida yake.

“Mh!” mmoja wa wafanyakazi wake akaguna.

“Leo kuna tatizo hapa si kawaida ya bosi, hata miwani ulishawahi kumwona ameivaa?” mwingine alidakia.

“Mimi naona kupotea kwa Ditrov kumesababisha matatizo makubwa sana, alikuwa ni mtu wake wa karibu sana.”

“Nakuunga mkono, hali hiyo imemchanganya kabisa bosi wetu,” yalikuwa ni maongezi ya wafanyakazi wawili waliokuwa nje ya ofisi wakimshuhudia Victor Fedorov akitokomea.

Dakika kumi baadaye alishafika makao makuu ya jeshi la polisi Urusi, akaegesha gari na kushuka na kuanza kutembea kuelekea ndani ya ofisi, huku akiwa mwenye wasiwasi mwingi.

Aliangaza huku na kule na kuingia ndani ambako alipokelewa na kukaribishwa moja kwa moja kwenye ofisi ya mkuu wa jeshi.
“Habari za muda?”

“Njema tu, pole na kazi.”

“Ah, tumeshazoea sisi, ndiyo kazi zetu.”

“Kuna jambo moja tu kwa sasa,” alisema Victor kwa kujiamini.

“Sawa kabisa.”
Mkuu wa jeshi akakaa vyema ili kumsikiliza Victor Fedorov.
“Kuna kitu gani kinaendelea mpaka sasa juu ya msako wa Ditrov?” Victor Fedorov aliuliza akivua miwani yake.

“Mh! Kama tulivyokubaliana, kwamba tusitishe zoezi mpaka tujipange upya halafu tuendelee lakini cha kushangaza wananchi wameanza kuingia mitaani kupinga uamuzi huo huku wakisisitiza msako uendelee tena kwa nguvu zote, wengi wakidai kwamba kabla ya kupotea kwa Ditrov washirika wake wote waliuawa tena vifo vya kutatanisha.

“Kwa hiyo ninyi kama jeshi mmeamua nini?”
“Tuendelee na msako…” alisema mkuu wa jeshi lakini kabla hajamaliza sentensi yake kelele za ajabu zikasika kutoka nje ya jengo.

“Ndiyo, tunataka uchunguzi uendelee, tunataka kufahamu ndugu zetu wako wapi, tunajua kuna mtu mkubwa anayefanya mauaji hayo, pengine kwa sababu zake binafsi au kuficha siri fulani…Tunamtaka huyo atafutwe na ahukumiwe!” sauti zilisikika zikizidi kusogelea karibu kabisa.

“Choma hiyo! Choma jengo bila kuogopa, hakuna kurudi nyuma tunahitaji kufahamu ukweli tumechoshwa na jeshi kila wakati kutudanganya tu, chomaaaaa!” sauti zilisikika zikisogea kuelekea makao makuu ya Jeshi la Polisi la Urusi.

“Mungu wangu!” mkuu wa jeshi alisema.

“Nini tena?”
“Wananchi hatimaye wameamua kuja mpaka huku, hili jambo siyo dogo hata kidogo ni lazima msako uendelee haraka sana,” alisema Mkuu wa Jeshi la Polisi la Urusi huku akinyanyua simu. Lakini kabla hajabonyeza namba mlango wa chumba chake ukafunguliwa kwa nguvu na askari mmoja akaonekana.
“Mkuu kuna matatizo.”

“Kimetokea nini?”

“Wananchi!”

“Wanafanya nini?”

“Wameamua kujitokeza kupambana na polisi eti wanadai kwamba kuna siri kubwa tunayoifahamu kuhusu mauaji yanayotokea.”

“Kwahiyo?”

“Wanaonekana wana hasira sana, tena wameshachoma vituo vya polisi karibu mji mzima na sasa wameingia hapa makao makuu.”

“Hebu nitoke kuongea nao.”

“Mkuu hapana, hutaweza! Wanaonekana kuwa na hasira nyingi sana.”

“Ni lazima kifanyike kitu hapa kunusuru usalama wetu na mali za nchi.”

“Kipi?”


“Mabomu ya machozi kuwatanya kwa nguvu sehemu zote ambazo wameandamana, umesikia?”

“Ndiyo mkuu,” alijibu askari huyo akitoka mbio kuelekea nje ambako alishuhudia maelfu ya watu wakizidi kusonga mbele kulielekea lango kuu ili waingie ndani na kufanya walichokitarajia.

Askari huyo alipotupa macho mbele ili kuangalia vizuri, alishuhudia maaskari wengi wakiwa chini.

Lilionekana kuwa jambo la kutisha wananchi walikuwa wamedhamiria kwa nguvu zote kuingia mitaani si kufanya fujo bali kulitia hekaheka jeshi la polisi ili liweze kuendelea na msako wake badala ya kukaa kimya.

“Hatimaye mwisho wangu umekuwa mbaya!” Victor Fedorov aliongea kwa sauti huku akinyanyuka kitini.

“Unasema?” mkuu wa jeshi aliuliza.

“Mh!” Victor Fedorov aliguna, na tayari alishaukamata mlango wa chumba akaufungua na kutoka nje huku akikimbia.

Je, nini kitaendelea? Siri yake imegundulika? Nini hatima yake?
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.54.


Walikuwa ni watoto wazuri, hakuna mtu aliyewaona watoto hao na kusita kutoa sifa midomoni mwao, japo walikuwa wadogo lakini uzuri wao ulionekana waziwazi na watu wengi kusema kwamba wakikuwa wangekuwa tishio kwa wanaume wengi nchini Urusi.

Ni watoto hao Pacha Mariya na Merina ndiyo walikuwa wakileta machafuko nchini Urusi bila wao wenyewe kufahamu siri nzito ilikuwa imefichwa, wakilelewa vyema na kusoma katika shule ya gharama huku wakihudumiwa kwa kila kitu walichohitaji wakiandaliwa kuja kuwa warithi wa mali za baba yao.

Kila aliyewaona watoto hao hakusita kujiuliza maswali juu yao, kwani walimfahamu vyema Victor Fedorov na historia ya maisha yake alishawahi kuoa wanawake kadhaa na kuachana nao bila kuzaa nao watoto lakini ghafla watoto wawili wakaibuka na watu kuelezwa kwamba walikuwa ni watoto wake.
“Mh! watoto wazuri sana!”
“Ni kweli”
“Ni wa nani?”
“Victor Fedorov”
“Huyu tajiri hapa Urusi?”
“Haswa ndiye.”
“Amezaa lini na wapi?”
”Kwa kweli hilo swali hata mimi sifahamu ila wenyewe watoto ukiwauliza wanasema Victor Fedorov ndiye baba yao.”

“Mh! Haya ukiwaangalia wamefanana naye lakini walikuwa wapi na mama yao ni nani?”

“Mambo ya Ngoswe mwachie Ngoswe mwenyewe,” walikuwa ni walimu wawili wakiongea wakati watoto hao wakipita mbele yao.
***
Taarifa aliyokuwa ameipata Phillip kutoka kwa Lina ilimpa furaha ya ajabu mno, hakika hakuwaza wala kutegemea tena kwamba baada ya kifo cha mke na watoto wake wapendwa angerejea katika hali ya kawaida kwani alishapoteza matumaini na hakuwa na furaha tena lakini kukutana na Lina kulirejesha furaha iliyopotea miaka mingi huko nyuma.

“Ahsante mke wangu ninakupenda.”
“Nakupenda pia Phillip.” Lina alijibu macho yake yote yakimwangalia Phillip.

“Hakika sina cha kukuzawadia laiti kama ningeweza…”aliongea Phillip lakini sentensi yake ikakatishwa na busu la Lina ambalo lilitua moja kwa moja mdomoni mwake.

“Najua unachotaka kusema.”
“Mh! Nini?”
“Unataka kuzungumza juu ya mtoto.”
“Ni kweli kabisa mke wangu sina uwezo wa kuzaa.”
“Tutapata mtoto.”
“Kwa njia gani?”
“Hata kama tutalazimika kutumia fedha zote tulizonazo lakini tupate mtoto!”
“Kivipi Lina?”
“Nitakueleza siku nyingine leo tupumzike kwa ajili ya kesho nitahitaji utafute vyeti vyako vyote na kuviweka pamoja tayari kwa kazi kesho.”
“Kesho?”
“Ndiyo!”
“Mh!” Phillip aliguna.
“Kwa nini unaguna?”
“Kesho sijajiandaa kabisa mke wangu.”

“Nasema kesho ni lazima tuondoke wote hapa nyumbani kwenda ofisini.”

“Sawa tuombe uzima,” alijibu Phillip na wote wakajitupa kitandani taratibu wakiwa hapo waliongea hiki na kile hatimaye wakapitiwa na usingizi.

***
Baaada tu ya kutoka ofisini kwa mkuu wa jeshi la polisi, Victor Fedorov huku akipishana na watu wengi njiani alifanikiwa kulifikia gari lake na kuingia ndani, akaliwasha na kuondoka hapo kwa kasi ya ajabu kichwani mwake akiwaza kitu kimoja tu watoto wake.

Ni kweli alifahamu wazi kwamba wakati huo walikuwa shuleni lakini hakuelewa walikuwa katika hali gani kwani kwa jinsi hali ilivyoonekana mambo yalikuwa yameharibika kabisa.
“Watoto wangu,”alitamka Victor Fedorov.

Shule waliyosoma Mariya na Merina haikuwa umbali mrefu sana kutoka mahali Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Urusi yalipokuwa hivyo wasiwasi wake ukazidi kuongezeka maradufu.

“Kwa jinsi hali ilivyo lazima niwafuate watoto wangu,” aliwaza Victor Fedorov akiendesha gari kwa kasi kuelekea huko, kichwani akamkumbuka Ditrov na unyama aliomfanyia, akaziona pia taswira za watoto wake Mariya na Merina wakimfurahia machozi ya uchungu yakamtoka lakini akajipa moyo na kusonga mbele kuelekea shuleni kwa watoto wake.

Kwa mwendo wa dakika kumi nzima aliendesha gari hatimaye akafanikiwa kufika eneo la shule akiwa hapo akashangazwa na ukimya wa ajabu uliokuwepo, hapakuonekana dalili ya walimu wala wanafunzi.

Haraka bila kuchelewa Victor Fedorov akaegesha gari lake na kushuka huku akiangaza macho huku na kule.

“Kimetokea nini hapa?” akajiuliza mwenyewe akitembea kwa kasi kuelekea majengo ya ofisi za walimu huko nako hakukuta mtu.
“Mungu wangu watoto wangu, haiwezekani,” aliongea Victor Fedorov akiingia mlango mmoja baada ya mwingine kukagua.

Shule ilikuwa kimya kabisa, hapakuonekana mtu yeyote eneo hilo zaidi ya karatasi zilizokuwa zikipepea juu kutoka ndani ya majengo kwenda nje. Moyo wake ukamwenda mbio, jasho jingi likamtoka na alipojaribu kupaza sauti yake na kuita majina ya watoto wake halikupatikana jibu lolote.

“Nimekwisha!”alisema Victor Fedorov akiporomoka chini kama mzigo.

Je, nini kitaendelea?
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.55.

Oleg Malenko alikuwa ni mwanaume wa Kirusi, alizaliwa na kukulia nchi Urusi miaka mingi iliyopita, alikuwa ni baba wa watoto wawili na mke mmoja, jina lake lilifahamika kwa wengi kutokana na kazi zake za uvuvi kwani aliendesha maisha yake kwa kazi hiyo.
Alikuwa ameifanya kazi hiyo kwa muda wa miaka isiyopungua kumi na tano na bado, pamoja na umri wake mkubwa. aliendelea kuifanya kwani ndiyo kazi pekee iliyoendesha maisha yake na familia yake.
Alfajiri ya siku hiyo kama ilivyokuwa kawaida yake, alitoka nyumbani kwake mapema kuliko kawaida akimuaga mke na watoto wake kwamba alikuwa akielekea kazini kwake jambo ambalo liliishangaza sana familia yake lakini hawakutilia mashaka hali hiyo kwani walimfahamu vyema.
Hakuishi maeneo ya mbali sana kutoka ufukweni ambako ndiko aliegesha mtumbwi wake mdogo, hivyo kwa muda wa dakika kumi tu tayari alishafika eneo la ufukweni, huku akiwa na taa ndogo mkononi mwake aliangaza macho yake huku na kule akijaribu kuangalia kama kulikuwa na mtu mwingine eneo hilo lakini hakuona kitu.
Kwa ujasiri alitembea na kuusogelea mtumbwi wake kwa kutumia taa ndogo aliyokuwa nayo mkononi ambapo aliangaza ndani ya mtumbwi huo kuangalia kama kulikuwa salama. Bila kuchelewa akaiweka taa ndogo aliyokuwa nayo mikononi mwake na kuanza kuusukuma mtumbwi huo kuelekea majini, tayari kwa kuanza kazi.
Alfajiri ya siku hiyo bahari ilionekana kuwa kimya kabisa, hapakuwa na purukushani kama ilivyokuwa kila siku, hivyo kuwa na uhakika kabisa kwamba angevua samaki wengi kwa sababu hakukuwa na watu wengine.
Kwa mwendo wa dakika kumi nzima aliendelea kupiga kasia akisonga mbele zaidi, lengo lake likiwa ni kufika mahali ambako aliamini samaki wengi zaidi walipatikana lakini ghafla mbele yake aliona kitu cha ajabu ambacho hakukitarajia, moyo wake ukamwenda mbio pamoja na kwamba kwa wakati huo nchini Urusi kulikuwa na hali nzuri ya hewa, lakini Oleg alitiririkwa na jasho jingi si kwa sababu ya kazi aliyokuwa ameifanya bali kwa kitu kilichokuwa mbele yake.
“Mungu wangu ni papa!”alijiuliza akinyanyua taa yake ndogo na kumulika eneo hilo.
Akayatoa macho yake yote kuangalia mbele lakini kwa sababu ya mwanga mdogo uliokuwepo hakuweza kuona vyema, woga ukazidi kumwingia na wazo pekee lililomwijia kichwani mwake ni kugeuza mtumbwi wake haraka na kurejea alikotoka, jambo ambalo hakuwa na uhakika nalo kama angefanikiwa.
Akiwa hapo alishuhudia mtumbwi wake ukiyumbishwa huku na kule, tayari alijua alikuwa katika hatari.
“Leo ninakufa, sidhani kama nitasalimika, ” alijisemea Oleg huku machozi yakimbubujika.

***
Usiku ulionekana kuwa mrefu mno kwa Phillip, mawazo na akili zake zote zikiwa kwenye kazi ambayo Lina alikuwa amemuahidi. Moyoni akamshukuru Mungu kwa mara nyingi kwa kumwona na kumchagua yeye, ni kweli alikuwa katika majonzi mazito lakini alikuwa amepewa njia nyingine tena.
“Jambo moja tu sasa litakalonisumbua ni jinsi gani nitapata tena watoto? Nahitaji watoto ambao watakuwa warithi wa mali zangu hapo baadaye,”aliwaza kichwani mwake akivuta shuka na kujifunika.
Asubuhi ya siku hiyo yeye ndiye alikuwa mtu wa kwanza kuamka kitandani, taratibu bila kumwamsha Lina alitoka ndani ya chumba na kuelekea jikoni ambako aliandaa kila kitu kwa ajili ya kifungua kinywa na kurejea chumbani ambako alifungua kabati akatoa nguo na kunyoosha tayari kwa maandalizi ya kwenda kazini.
“Darling?” (Mpenzi)
“Yes baby.” (Ndiyo mpenzi)
“Amka! Amka ukaoge sasa,” akasema Phillip kwa sauti ya kunong’ona.
“Mh!” Lina aliguna akijinyosha kitandani.
“Muda umefika?”
“Zamani sana mke wangu.”
Taratibu akafunua shuka na kunyosha mkono kuchukua simu yake ambayo haikuwa mbali, akatupa macho yake hapo na kugundua kwamba muda ulikuwa umewadia na alitakiwa kufanya haraka ili wasichelewe.
Taratibu akashusha miguu yake kitandani huku akiwa katika hali ya usingizi, Phillip akamshika mkono na kumuongoza moja kwa moja mpaka bafuni ambako walioga na kutoka.
“Utavaa nini leo?”
“Mimi?”
“Ndiyo.”
“Nguo tayari nimeshanyoosha.”
“Unasema kweli?”
“Hakika, nimeamka kitambo kidogo.”
Lina akasogea na kumbusu Phillip usoni ikiwa ni ishara ya kumshukuru, hakika watu hawa walikuwa katika penzi motomoto, kila mmoja akifanya mambo mazuri kwa mwenzake kadiri alivyoweza.
Kwa pamoja wakavaa na kutoka chumbani kuelekea sebuleni ambako nako mambo yalizidi kumshangaza Lina kwani tayari chai ilishatengwa mezani, kazi yake ilikuwa ni kusogea na kunywa.
“Leo umenifanyia mchezo wa ajabu sana mume wangu.”
“Kwa sababu nakupenda kupita kawaida.”
“Najua, nami pia ninakupenda sana Phillip.”
Kwa pamoja wakasogea mezani na kuketi hapo, wakanywa chai na walipomaliza Lina akachukua ufunguo wa gari lake aina ya Land Cruiser na kumkabidhi Phillip.
“Wewe leo ndiye dereva.”
“Mh! Una uhakika?”
“Kabisa gari hilo ni lako sasa.”
“Na wewe je?”
“Nitapata lingine muda si mrefu.”
“Ahsante kwa kunipenda mke wangu.”
“Usijali.”
Huku mkono wa Phillip ukiwa kiunoni mwa Lina, taratibu wakitembea kuelekea eneo gari lilipoegeshwa, Phillip akabonyeza kitufe fulani kwenye ufunguo na milango ikafunguka kisha kushika mlango mmoja wa mbele akaufungua na taratibu akamkaribisha Lina ambaye aliingia na kuketi huku akitabasamu.
Phillip naye akaelekea upande wa pili kwa dereva na kuingia ndani yake, akawasha gari kisha kutoka nje ya lango huku akipunga mkono kwa mlinzi ambaye naye aliachia tabasamu.

***
Baada ya kutangaziwa hali ya machafuko nchini Urusi uamuzi pekee uliofikiwa na uongozi wa shule ni kufunga shule kwa muda, mkutano ukaitishiwa na wanafunzi kupewa taarifa kwamba uongozi wa shule ulikuwa umeamua kusitisha masomo kwa muda kutokana na hali ilivyokuwa na kuwataka wanafunzi warejee majumbani mwao mpaka hali itakapotulia.
Uamuzi huo pekee uliwafanya Mariya na Merina kutoa machozi, hawakuwa na uhakika kama wangeweza kufika nyumbani kwao salama bila matatizo yoyote, isitoshe walizoea kuletwa shuleni na kufuatwa na sasa walikuwa wakirejea nyumbani wenyewe bila dereva.
“Mariya!” Merina aliita.
“Bee!”
“Twende huku.”
“Mimi sitaki nitakaa hapahapa kungojea gari la nyumbani.”
“Haliji sasa hivi na hali inazidi kuwa mbaya twende!”alisema Merina akimvuta Mariya ambaye muda wote alikuwa akilia.
Kwa pamoja huku kukiwa na purukushani nyingi, wakafanikiwa kutoka nje ya lango la shule wakiwa hawaelewi ni wapi waelekee.
“Merina! Mariya!” wakasikia majina yao yakitajwa.
Wakatupa macho yao kugeuka ili waangalie ni wapi sauti hiyo ilitoka na alikuwa ni nani aliyewatamka kwa majina.
“Mh! Unamjua?” Merina aliuliza.
“Hapana!”
“Lakini anatufahamu mbona ametuita kwa majina?”
“Hebu twende tukamsikilize pengine ametumwa na baba aje kutuchukua!”
“Mimi naogopa!” Mariya alijibu huku akisita.
Mbele yao alionekana mwanaume mrefu, mwili wake ulikuwa umejazia, na kwa kumwangalia harakaharaka alionekana kuwa ni mtu wa mazoezi. Kichwani alivaa kofia kubwa, machoni alikuwa na miwani ya rangi nyeusi. Huku wakitetemeka kwa hofu, wakasogea karibu kabisa na mwanaume huyo.
“Mariya! Merina!” akaita tena.
“Bee!” wakaitika huku wakitetemeka kwa hofu.
“Safi dili limekamilika,”alijibu mwanaume huyo na kwa haraka akawakamata kwa nguvu na kuanza kuwavuta kuelekea sehemu ambayo hawakuifahamu.
Je, nini kitaendelea? Watoto hawa wamepelekwa wapi? Je, watapatikana au ndiyo mwisho wao? Ni nani huyu aliyewachukua?
 
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.56.

Wakionekana wenye furaha mara kadhaa wakipigana mabusu bila kujali kwamba walikuwa barabarani, Phillip aliendesha gari na hatimaye kwa muda wa nusu saa wakafika ofisini.
Ni Phillip aliyekuwa wa kwanza kushuka garini na kuzunguka tena upande wa Lina kisha kufungua mlango na kumshika mkono akimkaribisha.

“Ahsante”
“Mwaaa!”Phillip aliachia busu.
Kitendo hicho kilishuhudiwa na watu wengi waliokuwa wamefika ofisini muda huo. Hakika mapenzi yao yalipendeza.
“Si Lina yule?”
“Ndiye.”

“Na yule?”
“Mume wake.”
“Mh! Makubwa haya.”
“Kwa nini?”
“Si umeona mwenyewe,” yalikuwa ni maongezi ya wasichana wawili waliofanya kazi ofisi moja na Lina.
Kwa pamoja wakatembea njiani wakipishana na watu kadhaa na kuwasalimia na Lina alifanya utambulisho kidogo na kuendelea mbele.

“Ngo!Ngo!Ngo!” Sauti ya mlango ukigongwa ilisikika.
“Ndiyo.” Sauti kutoka ndani ikajibu.
Taratibu Lina akashika kitasa na kusukuma mlango kuingia ndani. Macho yake yakagongana moja kwa moja na bosi wake aliyekuwa ameketi nyuma ya meza kubwa ofisini kwake asubuhi hiyo.
“Karibu sana Lina.”

“Ahsante,” alijibu Lina na alipofungua mlango vizuri alionekana kuongozana na mtu mwingine.
“Karibuni sana,” aliongea bosi huyo akijiweka vyema kitini huku macho yake yakimwangalia Phillip.
***
“Watoto hawa watanipa kile ninachokitafuta,” aliwaza mwanaume huyo akizidi kuwavuta watoto Mariya na Merina kuelekea sehemu ambayo hawakuifahamu.

Badru Divostroc alikuwa ni mwanaume katili aliyeogopwa na watu wengi nchini Urusi kwa vitendo vyake vya kimafia, kutokana na ukatili wake huo watu wengi nchini humo wakambandika jina la Kuntakinte.
Kwake yeye kupata alichokihitaji halikuwa tatizo, hakuogopa kumwaga damu za watu ili mradi tu atimize alichokikusudia.

Kwa muda mrefu alifuatilia kwa ukaribu habari za tajiri Fedorov alitaka kumfahamu lakini hakupata mwanya huo, hivyo taarifa za Mariya na Merina ambao walikuwa ni watoto wa Victor Fedorov kuingia nchini Urusi kulimpa furaha ya ajabu.
Baada ya kufuatilia kwa kina na kugundua kwamba Victor Fedorov aliwapenda watoto wake kuliko kitu kingine, aliamua kuwafuatilia kwa ukaribu akichunguza shule waliyosoma na ni gari lililowapeleka na kuwafuata kuwarudisha nyumbani.
Kwa muda wa mwezi mzima alifanya kazi hiyo hatimaye akafanikiwa kugundua njia zote na namna watoto hao walivyopelekwa shuleni na kufuatwa wakionekana kuwa katika ulinzi madhubuti.

Ni machafuko yaliyokuwa yakitokea nchini Urusi kwa wakati huo kwake yeye aliona ni kama bahati kwani nia yake ya kufanya utekaji nyara wa watoto wa tajiri kama Victor Fedorov kungempa alichokikusudia.
“Leo nitajaribu kufanya utekaji nitatumia akili zangu zote kuwapata watoto wa Fedorov halafu…,”aliwaza huku akinyanyuka kitandani.

Akiwa chumbani kwake akaisogelea televisheni yake na kuiwasha macho yake yakakutana moja kwa moja na habari za maandamano makubwa ya wananchi nchini Urusi waliokuwa wakipinga matokeo ya jeshi la polisi baada ya kusitisha msako wa kumsaka Ditrov, wananchi walikuwa wakiandamana mitaani wengi wakishinikiza msako uendelee.
“Hureee! Hureee utajiri huo mikononi mwangu,”alipiga kelele akirukaruka chumbani mwake.

Taarifa hiyo iliamsha vyema hisia zake, kwani kwa muda mrefu alikuwa amefanya kila alichoweza kupata utajiri aliokuwa nao Victor Fedorov lakini hakufanikiwa, sasa ulikuwa umekaribia kuingia mikononi mwake.
Haraka bila kuchelewa akavuta suruali yake aina ya jeans, fulana pamoja na koti kubwa akavaa, akageuka tena upande mwingine akavuta soksi za mikononi na kuzivaa kisha kofia kubwa pamoja na miwani ya rangi nyeusi akakisogelea kioo kilichokuwa chumbani kwake na kujiangalia na kutikisa kichwa kwa jinsi alivyobadilika.

Taratibu akanyanyua gorodo na kuchukua bastola yake ndogo na kuipachika kiunoni.
“Hakuna mtu atakayeweza kunitambua kwamba mimi ndiye Badru…,’aliongea akifungua mlango ili atoke nje.
Akitembea kwa kujiamini moja kwa moja akaliendea gari lake aina ya Noah akaingia na kuliwasha, mawazo yake yote yakiwa juu ya watoto wa Victor Fedorov, aliamini kama angefanikiwa kuwapata watoto hao na kuwateka hakika angepata malipo makubwa kutoka kwa tajiri huyo.

Kwa mwendo wa dakika kumi nzima aliendesha gari hatimaye akafanikiwa kufika shule waliyosoma watoto hao. Akaliegesha gari lake mbali kidogo na shule kisha kushuka na kutembea njiani akipishana na watu wengi wakikimbia huku na kule.

“Wale pale,”aliongea akisogea karibu kisha kuanza kuwaita kwa majina.
“Wewe ni nani?”

“Hakuna haja ya kunifahamu, twendeni huku.” Sauti ya mwanaume huyo ikajibu akiwavuta watoto hao.
“Mariya” Merina aliita huku akilia.
“Bee.”
“Huyu ni nani na tunakwenda wapi?” Merina aliuliza swali jingine tayari wote wawili walikuwa wakilia huku wakijaribu kujitoa mikononi mwa mwanaume huyo.

Kwa nguvu zake zote aliwavuta watoto hao mpaka wakalifikia gari ambalo lilikuwa limeegeshwa nje kidogo ya eneo la shule akafungua mlango na kuwatupia ndani yake, akaangaza macho huku na kule kuangalia kama kulikuwa na mtu yeyote karibu eneo hilo, wengi walionekana wakikimbia kunusuru maisha yao.

“Ninachohitaji hivi sasa ni fedha, Victor Fedorov ni lazima atoe fedha kuwaokoa watoto wake vinginevyo nitawaua,” Badru aliwaza kisha aliwasha gari na kuliondoa kwa kasi.
 
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.57.

Mshtuko aliokuwa ameupata hakika ulikuwa hauelezeki, kupotea kwa watoto wake wawili? Lilikuwa ni swali ambalo halikuwa na jibu kichwani mwake, kwa dakika tano nzima aliendelea kubaki chini akiwa haelewi ni kitu gani angefanya ili kuwapata watoto wake Mariya na Merina.

Machozi yakamtiririka, alipojaribu tena kupaza sauti yake akiwaita kwa majina bado hakusikia sauti yoyote zaidi ya mwangwi uliopenya moja kwa moja masikioni mwake. Victor Fedorov akajiona ni mwanaume mwenye mkosi maishani mwake.

Akiwa haelewi ni kitu gani afanye, alijikongoja na kunyanyuka chini bado akiendelea kuangaza macho yake huku na kule pengine kuona kama walikuwa wamejificha mahali na baada ya kumwona wangejitokeza awachukue na kwenda nao nyumbani. Haikuwa kama alivyowaza, bado Merina na Mariya hawakuonekana sehemu yoyote ile ndani ya shule. Jasho jingi likimtiririka, alijikongoja na kulifikia gari lake akafungua mlango na kuingia ndani kisha akaliwasha na kutoka eneo hilo la shule.

“Watakuwa wapi hawa? Nini kimewapata watoto wangu,” alijiuliza maswali mfululizo bila kupata majibu.
Nje ya lango la shule bado vurugu iliendelea kuongezeka, watu wengi wakionekana kukimbia huku na kule kuokoa maisha yao, akakodoa macho yake yote kuangaza kila upande akiwatafuta watoto wake lakini bado hakuwaona, lakini akiwa hapo akajipa moyo na kuamini kwamba huenda walimu waliamua kuwarudisha nyumbani kwa sababu ya machafuko yaliyokuwa yametokea siku hiyo.

“Nakwenda nyumbani watakuwa huko nina uhakika,” aliwaza akikanyaga mafuta kusonga mbele.
Victor Fedorov aliishi nje kidogo ya jiji, hivyo ilimchukua muda wa dakika arobaini kufika kwenye makazi yake, kichwani mwake akiwa na mawazo mengi juu ya usalama wa watoto wake ambao mpaka wakati huo hakufahamu kabisa ni wapi walipokuwa na kama walikuwa hai au wamekufa.

“Piii!Piiii!” ilikuwa ni honi nje ya lango la kuingilia nyumbani kwake.
Mara moja bila kuchelewa mlinzi alilifungua lango, akaingia ndani ya ngome ambapo aliliegesha gari lake kisha akashuka haraka.

Akazungusha macho yake huku na kule ndani ya ngome yake lakini hakuona kitu, hata alipojaribu kuangalia gari ambalo mara kadhaa liliwapeleka shule watoto wake na kuwafuata, nalo pia halikuonekana sehemu yake.
“Watoto wamerudi?” aliuliza kwa sauti ya ukali.
“Hapana bosi.”

“Unasema kweli?”
“Nina hakika.”
“Zhukov naye yuko wapi?”
“Sijamwona.”

“Mungu wangu watoto wangu!” alisema Victor Fedorov akichomoa simu yake ya mkononi mfukoni, akaonekana akibonyeza namba kadhaa kisha kuiweka sikioni na kusikiliza. Akiwa hapo mlinzi akamshuhudia bosi wake akitoka mbio kuelekea ndani bila kusema chochote, alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa kabisa.

Aliingia ndani na dakika mbili baadaye alitoka nje mkononi akiwa na bastola, na bila kusema chochote akaamuru lango kuu lifunguliwe, akaingia ndani ya gari kisha kuliwasha na kutoka mbio kama vile alikuwa katika mashindano.
“Nitaua! Nasema nitaua sina mchezo mbele ya watoto wangu,” alisema peke yake ndani ya gari.

Huku akiwa katika mwendo wa kasi, Victor Fedorov aliendelea kuangaza macho yake huku na kule pembezoni mwa barabara lakini bado hakuwaona watoto wake. Alikuwa ameamua kuingia mwenyewe barabarani akiwasaka kwa udi na uvumba watoto wake Mariya na Merina ambao mpaka wakati huo hakujua walikuwa wapi na kitu gani kilikuwa kimewapata. Kwa saa saba mfululizo aliendelea kuwasaka huku akijaribu kuwasiliana na watu mbalimbali kwa msaada, lakini bado hawakupatikana sehemu yoyote.

Hatimaye akaamua kuingia katika hospitali moja baada ya nyingine akiuliza kama kulikuwa na majeruhi yeyote au watu waliofariki, lakini bado jibu liliendelea kubaki palepale; hakukuwa na kitu cha aina hiyo.

“Fyuuu!”akashusha pumzi kwa nguvu. Victor Fedorov hakuwa tayari kuwapoteza watoto wake alikuwa tayari kutumia kila kitu alichokuwa nacho lakini si kuwakosa maishani mwake, hakika aliwapenda kupita kawaida katika maisha yake yote yaliyobaki duniani, aliamini hakuwa na ndugu mwingine zaidi ya watoto hao.

Siku hiyo ikapita kukiwa hakuna dalili zozote za kuwapata watoto wake na hata alipojaribu kurejea nyumbani na kuangalia bado walikuwa hawajaonekana, akiwa hapo akamkumbuka Ditrov na kuamini kwamba pengine asingemuua angekuwa msaada mkubwa katika kupatikana kwa watoto wake.

“Ditrov angekua hai hakika ninaamini watoto wangu wangepatikana,” aliwaza akijifuta machozi.
Kwa siku tatu mfululizo bado watoto waliendelea kusakwa huku na kule nchini Urusi pamoja na machafuko yaliyokuwepo, nchi hiyo ilibinuliwa nje ndani, msaada mkubwa ukifanywa na polisi lakini bado hawakupatikana.

Hatimaye siku ya nne asubuhi Victor Fedorov akiwa ameshakata tamaa juu ya kuwapata watoto wake, wazo likamjia kichwani mwake kwamba ajaribu kutangaza katika vyombo vya habari juu ya kupotea kwa watoto.

Huku akiwa mwenye mawazo mengi akakubaliana na wazo hilo.
“Nitakwenda kwenye televisheni ya taifa na kutangaza pengine kuna mtu amewaona sehemu fulani,” aliwaza akilini mwake.

Ndani ya nyumba yake hakukulika wala kukakalika, mawazo na akili yote ilielekea kwa watoto wake. Hivyo asubuhi hiyo alitoka nyumbani kwake na jambo moja tu; tangazo.

Akaingia ndani ya gari lake na kuliwasha bila kusema chochote akamwonyesha mlinzi ishara na lango likafunguliwa, taratibu akaanza kutoka nje, lakini kabla hajafika mbali mbele yake aliona kitu ambacho hakikuwa cha kawaida.

“Mh ni kitu gani kile?” alijiuliza akizima gari lake na kushuka kukielekea kitu hicho moyoni mwake akiwa na wasiwasi mwingi.

Je, ni kitu gani hicho? Nini hatima ya Mariya na Merina? Watakufa au wataokolewa?
 
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.58.

JASHO jingi lilikuwa kitiririka mwilini mwake, akatembea taratibu kukielekea kitu kilichokuwa mbele yake hatua chache tu tayari akawa amekifikia, alipotupa macho yake vyema kuangalia aligundua ilikuwa ni bahasha kubwa nyeupe na juu yake iliandikwa kwa maandishi ya rangi nyekundu akasimama kwa muda akijaribu kusoma ni kitu gani kiliandikwa juu yake.

“Victor Fedorov!” Moyo wake ukazidi kumwenda mbio, kitendo cha kukuta bahasha hiyo nje ya lango lake hakikuwa cha kawaida tena na jina lake kwa maandishi ya rangi nyekundu? Likawa ni swali jingine kichwani mwake akazidi kuchanganyikiwa.

Bila kupoteza wakati akiwa haelewi ni kitu gani kingetokea akapiga moyo konde na kuinama kuikota bahasha hiyo na kwa ujasiri wa hali ya juu haraka akaifungua ndani na kutoa kipande kidogo cha karatasi nacho pia kiliandikwa kwa rangi nyekundu.
“Anayeua kwa upanga naye hufa kwa upanga” Kilisomeka kipande hicho cha karatasi.

Victor Fedorov akiwa haamini maneno aliyokutana nayo ndani ya karatasi hiyo akapikicha macho yake tena na kurudia bado yaliendelea kusomeka hivyo hivyo kama mwanzo.
“Mungu wangu!” Akasema kimoyomoyo akiketi chini na kuendelea kusoma zaidi.

“Ninachohitaji kwako ni fedha, ili uweze kuwapata watoto wako Merina na Mariya kama unawahitaji wakiwa hai. Ninatoa muda wa saa ishirini na nne tu kuanzia sasa vinginevyo watakuwa marehemu, nakuhakikishia watakufa kifo kibaya kwa kuwakata kiungo kimoja baada ya kingine hadi umauti uwafike.
Kumbuka kama unawapenda watoto wako ni vyema ukafanya kila unachoweza ili uweze kuwapata na usijaribu kutumia jeshi la polisi kwa usalama zaidi.

Mara tu utakapokuwa tayari nitapenda unitaarifu kwa namba hizo hapo chini ili tukubaliane, sawa?
Tahadhari mimi ni mtu hatari sana, ukigeuka nyuma utaniona , kushoto, kulia na mbele pia nipo hivyo kabla hujafanya maamuzi yoyote tumia busara zako zote vinginevyo utajuta…
Kwa heri.” Ilisema sehemu ya barua hiyo.

“Ni Ditrov.”Alinong’ona.
Victor Fedorov akahisi vitu kama maji maji vikitiririka ndani ya suruali yake, hakika hakuamini alichokisoma kichwani mwake taswira ya Ditrov ikamjia akahisi pengine mtu huyo hakufa kama alivyofahamu.
“Noooo!” Akapaza sauti.

Akatupa macho yake pande zote nne bila kuona kitu akayerejesha tena kwenye saa yake ya mkononi akasoma akagundua amebakiza saa kumi na tisa tu muda aliokuwa amepewa na mtu aliyedai kuwa na watoto wake uwadie vinginevyo wangekufa.
“Mariya! Merina!” Akaita akikimbia kuelekea ndani ya nyumba yake, bila kukumbuka gari alilokuwa ameliegesha pembeni kidogo.

Moja kwa moja akagonga lango na mlinzi kulifungua bila kusema chochote akazama ndani akikimbia huku akilia.
“Kuna nini tena?” Mlinzi aliuliza lakini hakujibiwa kitu chochote.
Tayari Victor Fedorov alishazama ndani, kitu cha kwanza bila kupoteza wakati akaisogelea simu akainyanyua ili apige namba aliyokuwa ameisoma kwenye kipande cha barua kilichokuwa mkononi mwake.

Huku machozi yakimbubujika akakikunjua kipande hicho na kuanza kuzisoma namba na kubonyeza moja baada ya nyingine kisha kuweka mkono wa simu sikioni akisikiliza upande wa pili.

Takribani dakika tatu nzima simu hiyo iliita bila kupokelewa akili yake ikazidi kuvurugika akiwa haelewi ni kitu gani angefanya upande mmoja wa akili yake ukimwambia atoe taarifa hiyo kwa Jeshi la Polisi na mwingine ukimwambia kufanya hivyo ni kuwapoteza watoto wake wapendwa Mariya na Merina kwani alishapewa onyo juu ya jambo hilo.

“Hapana ngoja niwe mvumilivu nitawapata tu, isije kuwa ni Ditrov hana huruma mtu huyu anachokisema kinakuwa kweli, atawaua watoto wangu!” Alijiuliza maswali mengi mfululizo bila kupata majibu.
Dakika tano nzima baadaye alikuwa tena katika simu akibonyeza namba zile zile na kusikiliza ghafla akasikia sauti nzito upande wa pili ikapokea.

“Ah!Ah!” Kigugumizi kikamshika pamoja na ukatili wake wote Victor Fedorov hapo alikuwa hana ujanja tena, alikuwa tayari kupoteza kila kitu alichokuwa nacho lakini si watoto wake, aliwapenda kupita maelezo.

“Niko tayari...sawa…ndiyo…hapana…usiwaue…nitakupa hata kama ni utajiri wangu wote….Mungu wangu…niambie unapatikana wapi…nimekuelewa sitafanya hivyo… niambie unataka kiasi gani?” Yalikuwa ni maongezi katika simu na mtu mwingine upande wa pili ambaye hakuonekana na baada ya maongezi hayo simu ikakatwa.

Akiwa amepigwa na butwaa, taswira za watoto wake Mariya na Merina zikamjia, masikioni mwake akasikia sauti zao wakimwita na kumwomba asiwaache wafe, Victor Fedorov akalia kama mtoto mdogo.
 
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.59.

SURA yake ilikuwa imebadilika kabisa, macho yakabadilika na kuwa ya rangi nyekundu, mwili wake ukaanza kutetemeka kama mtu aliyekuwa na homa kali, Victor Fedorov akauona utajiri wote aliokuwa nao haukuwa na maana kwake kama tu angewakosa watoto wake ambao kwa hakika alikuwa ametumia kiasi kikubwa cha fedha ili kuwapata na sasa walikuwa katika hatari nyingine ya kifo kama tu asingetimiza jambo alilotakiwa kulifanya ndani ya saa chache alizopewa.

Kwa muda wa dakika tano aliendelea kutafakari na hakuelewa ni kwa nini mtekaji huyo alifanya tendo hilo, akavuta kumbukumbu zake nyuma akijaribu kufikiria watu wote aliowahi kuwakosea na kuwadhulumu lakini hakuna alichokumbuka.
Mara kadhaa taswira ya Ditrov ilimjia lakini akatupilia mbali mawazo juu ya mtu huyo na kuamini kwamba tayari alishakufa.

“Nilimuua ili kuficha siri sikuwa na tatizo jingine kabla!” alisema akitembea kukielekea kiti kilichokuwa mbele yake. Huku jasho jingi likimtiririka, akakisogelea kiti na kuketi, moyoni mwake akiwa na hofu juu ya watoto wake.

“Nitatoa kiasi chochote cha fedha atakachohitaji mtu huyo ili mradi tu niwapate watoto wangu!” aliwaza akijifuta machozi.
Alipotupa macho yake kwenye saa yake ya mkononi hofu ikazidi kumwingia, mbele yake kulikuwa na saa kumi tu zilizobaki katika saa ishirini na nne alizopewa na muuaji.

Haraka akanyanyuka kitini na kusogelea tena simu akapiga namba zilezile alizobonyeza mwanzo kisha kuiweka simu sikioni, alikuwa hapo kuzungumza na mtu huyo ataje kiasi hicho cha fedha na sehemu ambapo angezikuta na yeye kupata watoto wake wakiwa salama.
***
Ilikuwa ni familia yenye furaha kupita kawaida, kila mtu aliyewaona aliona wivu, hakika walivutia, walikuwa na kila sababu ya kuitwa mke na mume. Lakini pamoja na mambo yote hayo kutawala maishani mwao, jambo moja tu lilikuwa likiwasumbua ni wapi wangepata mtoto.

Kwa mwanamke halikuwa tatizo sana, kazi kubwa ilikuwa kwa mwanaume ambaye alitumia muda mwingi kufikiria namna gani angeitwa baba kama ilivyowahi kutokea miaka mingi kabla.
“Darling” (mpenzi), Phillip aliita siku moja asubuhi.
“Yes baby!” (Ndiyo mpenzi)

“Ni miaka minne sasa tupo kwenye ndoa lakini mimi sina uwezo wa kuzaa nataka tuliongelee jambo hili ili tufikie muafaka juu ya nini cha kufanya, napenda niitwe baba hata kama mtoto huyo atakuwa si wa kwangu,” alisema Phillip.
“Unamaanisha nini Phillip?”
“Sina nia mbaya, ila nataka nikupe nafasi ya wewe kuzaa kwa sababu huna tatizo lolote.”
“Mh!” Lina akaguna.

“Ni ukweli mke wangu nakupenda sana lakini nitakupenda zaidi utakapofanikiwa kuniletea mtoto.”
“Phillip mbona sikuelewi, mtoto atoke wapi? Ni kweli mimi sina tatizo lakini nitampata wapi mtoto ili hali wewe ndiye mume wangu na tayari una tatizo?”

“Tafuta mwanaume yeyote ambaye atakuwa tayari kuzaa na wewe Lina halafu mimi nitalea mtoto huyo!” alisema Phillip akilengwalengwa na machozi.
Ilikuwa ni kauli ngumu sana kuitamka mdomoni hasa kwa mwanaume aliyempenda mke wake kupita maelezo, lakini haikukwepeka kwa sababu walihitaji mtoto ndani ya nyumba ambaye angekuwa mrithi wa mali zote walizokuwa nazo.

Lina akamwangalia Phillip kwa muda, hakuwa tayari kuamini kauli aliyoisikia mdomoni mwa Phillip, kwani katika muda wote walioishi pamoja ndani ya nyumba Phillip alionyesha kumpenda na mara kadhaa akimwomba kuwa mwaminifu katika mapenzi yao.
“Phillip!” Lina aliita.

“Yes honey” (ndiyo mpenzi) aliitikia Phillip huku macho yake yakimwangalia Lina kwa huruma.
“Unamaanisha unachosema?”
“Hakika, wala sina utani juu ya hilo.”

“Ni kwa nini umefikia hapo, hivi kweli unanipenda?”
“Nakupenda kupita maelezo wewe mwenyewe unafahamu.”
“Sasa?”
“Nataka kuitwa baba.”

“Phillip hutaumia kugundua kwamba mkeo unayempenda kwa dhati amekutana na mwanaume mwingine kisha kupata ujauzito?”
“Nimekaa na kufikiria kwa muda mrefu si kwamba sitaumia, ninachohitaji ni wewe kufanya kila unachoweza upate ujauzito halafu mimi nitautunza mpaka utakapojifungua mke wangu.”
“Phillip kumbe hunipendi,” alisema Lina akibubujikwa na machozi.

Phillip akanyanyuka kitini na kusogea karibu kabisa na kiti alichoketi Lina kisha kumkumbatia wote kwa pamoja wakaanza kulia.
“Uamuzi wangu si mbaya, ninachohitaji wewe uwe na furaha mke wangu matatizo yangu mimi yasikufanye ukakosa kuitwa mama maishani mwako,” aliongea huku akimpigapiga Lina mgongoni.

“Phillip hivi utajisikiaje kuona mimi ni mjamzito halafu si wa kwako?”
“Kwa sababu nimetoa idhini mimi mwenyewe sitaumia, ninachotaka ni wewe uitwe mama na mimi baba basi.”
“Ni ngumu Phillip, mimi siwezi kulisaliti penzi letu acha tubaki hivihivi bila mtoto naamini Mungu alikuwa na makusudi juu ya hilo.”

“Unasema?” aliuliza Phillip akinyanyuka kitini, alikuwa hatanii bali alimaanisha alichokuwa akikisema. Haja ya moyo wake ilikuwa ni kuitwa baba bila kujali ni wapi mtoto huyo angepatikana.
“Phillip.” Lina akaita huku akijaribu kumfuata.
“Lina nataka mtoto!”

“Phillip haiwezekani mimi siko tayari kusaliti penzi letu.”
“Unanipenda?” Phillip aliuliza kwa kujiamini.
“Nakupenda sana mume wangu.”
“Basi nataka mtoto!” aliongea Phillip huku akitembea kuondoka eneo hilo.
 
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.60

“Mungu wangu! Ni papa?”alijiuliza huku akinyanyua taa yake ndogo na kumulika eneo hilo huku akitetemeka kwa hofu.
Akayatoa macho yake yote kuangalia mbele lakini kwa sababu ya mwanga mdogo uliokuwepo hakuweza kuona vyema. Woga ukazidi kumwingia na wazo pekee lililomjia kichwani kwa wakati ule lilikuwa ni kugeuza mtumbwi wake haraka na kurejea alikotoka, jambo ambalo hakuwa na uhakika nalo kama lingesaidia kuokoa maisha yake.

Akiwa hapo alishuhudia mtumbwi wake ukiyumbishwa huku na kule, akajua tayari amejiingiza kwenye hatari.
“Leo ninakufa huku nikijiona,” alisema Oleg Malenko huku machozi yakimbubujika kwa wingi mashavuni. Hofu kuu ilikuwa imemkumba na hakuna alichokuwa anakisubiri zaidi ya kifo, tena cha kuliwa na papa.

Aliifanya kazi ya uvuvi kwa kipindi kirefu lakini hata siku moja hakuwahi kukutana na dhahama kama ile. Zaidi alifanya kusimuliwa na wavuvi wenzake kwamba watu wengi hufa baharini, hasa wavuvi baada ya mitubwi yao kuvamiwa na kupinduliwa na samaki wakubwa.

Kwa Oleg Malenko siku hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kushuhudia tukio hilo, akaamini kabisa kwamba kifo kilikuwa kimemkaribia. Taswira za mke na watoto wake zikawa zinapita kwa kasi kichwani mwake kama filamu ya kusisimua, machozi ya uchungu yakawa yanamtoka.

Akiwa katika mawazo hayo, haraka alipata wazo la kupiga kasia kwa nguvu na kugeuza mtubwi wake kwa kasi kurejea upande aliokuwa mara ya kwanza lakini tayari alishachelewa, akahisi mtumbwi ukivutwa kurudi nyuma kwa kasi ya ajabu.
“Nakufaa! Nakufaa!” alisema kwa lugha ya Kirusi akiomba msaada.

***
Muda mfupi baada ya kuzamishwa baharini akiwa amefungwa jiwe kubwa mwilini mwake ili asipate nafasi ya kujiokoa kwa lengo la kupoteza ushahidi, Ditrov alirejewa na fahamu baada ya kupigwa na baridi kali. Alijaribu kufurukuta kwa kupiga mbizi ili kujiokoa lakini hakufanikiwa.

Alipotumia nguvu za ziada alizokuwa nazo mwilini mwake, bado aliendelea kutapatapa na sasa akawa anavutwa kuelekea chini ya bahari na lile jiwe kubwa alilokuwa amefunganishwa mwilini. Akiwa katikati ya hali ya kupoteza fahamu na uzima, alikumbuka picha ya tukio zima lililotokea ofisini kwa bosi wake, Victor Fedorov hadi wakati ule. Alikumbuka jinsi alivyofyatuliwa risasi bila huruma ambazo zilipenya kwenye mwili wake na kumsababishia maumivu makali.

Akiwa katika hali hiyo kwa takribani dakika kumi nzima, aliendelea kujivuta huku na kule ndani ya maji ili kujiokoa lakini zoezi hilo lilionekana kuwa gumu kwake. Akawa anazidi kuzama! Ditrov alizidiwa nguvu na maji, akaanza kukata tamaa lakini upande mwingine wa akili yake alikuwa na matumaini makubwa ya kusalimika na kifo.
“Ma…ji!” alitamka kwa tabu akiwa bado anatapatapa, moyoni akasikia sauti ikimwambia kuwa hapaswi kukata tama kwani kufanya hivyo kungemaanisha kifo chake.

“Sitaki ku…fa!” akatamka tena kwa tabu.
Hali yake ilizidi kuwa mbaya, uwezekano wa kutoka baharini akiwa salama ukazidi kupungua kutokana na maumivu aliyokuwa anayahisi baada ya risasi kuupenya mwili wake na kusababisha atokwe na damu nyingi. Pamoja na kuwa jabali, Ditrov hakuwa na uhakika kama angesalimika lakini bado hakukata tamaa.

Ghafla akiwa katika hali ya kukata tama, alikumbuka kitu. Wakati anaingia ofisini kwa Victor Fedorov, ndani ya mfuko mmoja katika suruali yake alikuwa na kisu kidogo cha kukunja, akaamini huenda kingemsaidia kuokoa uhai wake.
Kwa nguvu zake zote alijitahidi kuingiza mkono mfukoni lakini hakufanikiwa, akajaribu tena upande mwingine wa suruali yake na kukumbana na maumivu makali.

Licha ya maumivu hayo alijaribu tena kuusogeza mkono wake zaidi mpaka akaufikia mfuko wa suruali, kwa taabu kubwa akafanikiwa kugusa kitu kigumu na kuamini kwamba kilikuwa chenyewe.
Akiwa katika hali ya kutapatapa akafanikiwa kuupenyeza mkono mfukoni na kuchomoa kisu, kwa taabu kubwa akakishika vyema na kujaribu kuikata kamba ili ajinusuru na umauti uliokuwa ukiinyemelea roho yake.

Hakuwa tayari kukutana na kifo. Ni kweli alifahamu wazi kwamba kila binadamu angeonja mauti lakini hakuwa tayari kufa kikatili kiasi hicho.
“Nitajaribu mpaka mwisho, ikishindikana basi,”aliwaza akilini mwake.
Kwa nguvu kidogo alizokuwa nazo alikishika vyema kisu kidogo alichokuwa nacho mkononi, licha ya maumivu makali aliyokuwa nayo upande wake wa kulia, aliikamata vyema kamba aliyokuwa amefungwa shingoni na kuanza kuikata.

“Krii!Krii!Krii!” aliendelea kusugua kisu katika kamba ili ikatike na kumwacha huru. Kwa takribani dakika tano nzima aliendelea kung’ang’ana na kisu lakini zoezi hilo lilionekana kumshinda. Akaanza kuhisi fahamu zikipotea na nguvu kidogo alizobakiwa nazo zikamwishia. Licha ya hayo yote, bado hakuchoka, alitaka kuendelea kujaribu.

***
“Ngrii!Ngrii!Ngri” Ulikuwa ni mlio wa simu ndani ya nyumba ya Victor Fedorov. Aliinuka taratibu huku akitetemeka na kuisogelea simu hiyo ili aipokee akiwa haelewi ni nani alikuwa akipiga.
“Ndiyo,” akajibu huku akitetemeka.
“Muda unazidi kuyoyoma! Ninachohitaji kutoka kwako ni kiasi cha dola milioni 290 ili niweze kuwaachia watoto wako. Ningependa fedha hizo nizipate ndani ya Msitu wa Beloomut, kusini mwa Jiji la Moscow kwa usalama zaidi.

“Msitu wa Beloomut?” aliuliza lakini kabla hajapata jibu kutoka upande wa pili wa simu, alisikia sauti za watoto wake wakimwita.
“Daaaady!” (Babaaaa!) kilio kikali kilifuatia nyuma yake, Fedorov akazidi kuchanganyikiwa akili.

Je, nini kitaendelea? Victor Fedorov atakuwa tayari kutoa kiasi hicho cha fedha ili kuwakomboa watoto wake? Ni kwa nini muuaji ametaka fedha hizo zipelekwe kwenye Msitu wa Beloomut?
ITAENDELEA, HOPE SINA TENA KESI NA NYINYI........SIKU NJEMAA....LOVE U ALL.
 
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.61.

HALI yake ilikuwa mbaya hakuwa na uwezo wa kutoka baharini akiwa salama, risasi zilizoupenya mwili wake zilifanya amwage damu nyingi. Pamoja na kuwa jabali, Ditrov hakuwa na uhakika kama angesalimika.
Ghafla akiwa katika hali ya kukata tamaa akakumbuka kitu wakati anaingia ofisini kwa Victor Fedorov, mfuko mmoja katika suruali yake alikuwa na kisu kidogo cha kukunja akaamini huenda kisu hicho kingemsaidia kwa asilimia zote.

Kwa nguvu zake zote akajitahidi kuingiza mkono mfukoni lakini hakufanikiwa akajaribu tena upande mwingine wa suruali yake na kukumbana na maumivu makali lakini pamoja na maumivu hayo akajaribu kuusogeza mkono wake zaidi mpaka kuufikia mfuko wa suruali. Kwa taabu kubwa akafanikiwa kukuta kitu kigumu na kuamini kwamba kilikuwa chenyewe.

Akiwa katika hali ya kutapatapa akafanikiwa kuupenyeza mkono mfukoni na kukichomoa kisu kwa taabu kubwa, akakishika vyema na kujaribu kuikata kamba ili ajinusuru na umauti uliokuwa ukiinyemelea roho yake.
Hakuwa tayari kukutana na kifo, ni kweli alifahamu wazi kwamba kila binadamu angeonja mauti lakini hakuwa tayari kufa kwa ukatili kiasi hicho, hivyo alitaka kujiokoa.

Upande mwingine wa hadithi hii tunamwona Victor Fedorov na sharti alilopewa la kuzipeleka fedha hizo kwenye msitu wa Beloomut. Je, atafanikiwa kuzifikisha na kuwapata watoto wake? SONGA NAYO…

“Tafuta mwanaume yeyote ambaye atakuwa tayari kuzaa na wewe Lina halafu mimi nitalea mtoto huyo,” maneno hayo yalijirudia kichwani mwa Lina.
Hali ya hewa ikabadilika ghafla furaha yote iliyokuwepo ndani ya nyumba ikapotea, Phillip akiwaza jambo moja tu mtoto, hata Lina alipojaribu kumpa ushauri bado hakusikiliza.

“Phillip mimi siko tayari,” alisema Lina.
“Unamaanisha nini?”
“Siko tayari kusaliti penzi letu sababu kubwa ikiwa ni mtoto.”
“Mimi ndiyo mumeo nimeshasema tafadhali fanyia kazi maneno yangu.”

“Hapana, kwa hilo nimekataa.”
“Lina unanipenda kweli?”
“Asilimia mia moja.”
“Basi fanya ninachotaka.”

Lina hakujibu kitu akainamisha kichwa chake chini huku kwikwi ya kulia ikimkaba, hakuwa tayari kukubaliana na maneno ya mumewe, kwake yeye mapenzi yangekuwepo tu hata bila kupata mtoto. Ni kweli yeye binafsi alikuwa mzima, tatizo lilikuwa kwa mume wake lakini tangu mwanzo alishakubaliana nalo.
Akiwa katika mawazo hayo akamshuhudia Phillip akitoka sebuleni na kuelekea chumbani huko hakuchukua muda mrefu sana akamwona tena akitoka mkononi akiwa na funguo za gari.

“Phillip!” Lina aliita lakini hakuitikiwa badala yake akashuhudia macho makali ya Phillip yakimwangalia, yalionyesha dalili zote kwamba alikuwa na hasira kali. Akamshuhudia akifungua mlango na kutoka nje bila kusema neno lolote.
Uchungu wa ajabu ukaugubika moyo wa Lina, hakuwahi kushuhudia katika kipindi chote cha miaka minne alichoishi na Phillip kama mke na mume kwamba siku moja ingegeuka na kuwa shubiri.

Machozi ya uchungu yakamtiririka mashavuni mwake.
“Mtoto! Mtoto analeta matatizo katika penzi letu,” alisema Lina akinyanyuka kitini kuelekea nje huko nako akamshuhudia Phillip akiwasha gari na kutokomea kwenda sehemu ambayo haikujulikana.

***
Msitu wa Beloomut ulikuwa ni wa hatari sana, kila mtu nchini Urusi aliuogopa, wengi wakaupachika jina la msitu wa ajabu kwa matukio mbalimbali ya kutisha yaliyowahi kutokea ndani yake.
Iliaminika kwamba mpaka wakati huo zaidi ya Warusi elfu moja walishakufa baada ya kuingia ndani ya msitu huo na wengi wao miili yao haikuonekana kabisa. Ni matukio hayo ya kutisha ndiyo yaliyosababisha serikali ya nchi hiyo kuingilia kati na kuutangaza msitu huo kwamba ulikuwa tishio na watu kupewa onyo kwamba asitokee mtu yeyote kwenda eneo hilo.

“Msitu wa Beloomut?” lilikuwa ni swali likipita kichwani mwa Victor Fedorov, pamoja na kuwa mwanaume wa shoka, jina hilo lilimtia wasiwasi, akavuta kumbukumbu zake mara kadhaa juu ya matukio mabaya yaliyowahi kutokea katika msitu huo, akaangua kilio.

Kwa Victor Fedorov kiasi cha fedha alichotakiwa kukipeleka kwenye msitu huo hakikuwa tatizo, utajiri wake ulitisha lakini kitu kimoja tu kilimsumbua akilini mwake, ni majanga mengi juu ya msitu huo, hakuwa tayari kwenda kufa lakini aliwahitaji sana watoto wake na ili awapate ni lazima apeleke fedha hizo sehemu aliyoelekezwa.

“Niko tayari kutoa kiasi hicho cha fedha lakini je, nitanusurika? Watoto wangu watakuwa hai?” bado aliendelea kujiuliza kichwani mwake. Pamoja na maswali yote hayo bado taswira za Merina na Mariya ziliendelea kuzunguka ndani ya akili yake, hakuwa tayari kuwapoteza, hao ndiyo ndugu pekee aliokuwa nao.

“Nitafanya kila ninachoweza kuwakomboa watoto wangu hata ikitokea mimi mwenyewe nikafa lakini wao wapone,” aliwaza.
Akili yake ikaonekana kusimama, kwa mara ya kwanza akamkumbuka Ditrov, kwa wakati huo alionekana kuwa ni mtu muhimu sana kwake, aliamini kabisa kwamba mtu huyo angekuwepo maishani mwake kila kitu kingekwenda kama alivyotaka kwani fedha zilikuwa kila kitu katika maisha yake.

“Sitaki kujutia kifo cha Ditrov, nitapambana kiume,” alisema kwa sauti ya kunong’ona.
Akiwa na hofu, taratibu alianza kutembea kuelekea chumbani ambako alifungua mlango na kuingia ndani akanyoosha moja kwa moja mpaka kwenye moja ya makabati makubwa na kufungua. Pamoja na utajiri wote aliokuwa nao, Victor Fedorov aliweka kiasi kikubwa cha fedha ndani ya nyumba ili kukwepa usumbufu wa kwenda benki mara kwa mara.

Huku machozi yakimbubujika, akanyoosha mkono na kuvuta moja ya mifuko iliyoonekana ndani ya kabati hilo na kuutoa nje, fedha nyingi zikaonekana na bila kupoteza muda akaanza kuchukua bunda moja moja na kuyahesabu.
“Nitafanya kila kinachowezekana kuwapata watoto wangu hata akitaka nusu ya utajiri wangu nitampa lakini …” hakumalizia sentensi hiyo mara mlio wa simu ndani ya nyumba yake ukasikika.

***
Kwa muda wa saa nne mfululizo Lina aliendelea kumsubiri Phillip lakini hakuonekana, hata alipopiga simu yake ya mkononi haikupatikana. Lina akachanganyikiwa, hakuelewa ni wapi alikuwa na kitu gani kilimpata kwani hali aliyoondoka nayo nyumbani siku hiyo haikuwa ya kawaida.
“Mungu nisaidie arejee nyumbani akiwa mzima, nitaendelea kusubiri kama saa moja mbele asipotokea nitakwenda kutoa taarifa polisi, pengine amejinyo…” alisema Lina na sentensi yake kukatizwa na honi ya gari nje ya lango la nyumba yao iliposikika.

Haraka akasimama kitini ili achungulie nje, akamshuhudia mlinzi akilisogelea lango lakini badala ya kufungua akachungulia, hofu ikazidi kumwingia.
“Ngoja niende mwenyewe,” alijisemea Lina akitembea kutoka nje kuelekea langoni na bila kusema chochote akauliza swali moja tu kwa mlinzi huyo.

“Ni Phillip?”
“Hapana ni mgeni tu.””Mgeni? Hebu nimwone,” alisema naye pia akachungulia.
Ilikuwa ni sura ngeni kabisa kati yao, alipoliangalia gari pia hakulifahamu, taratibu akasogea na kumsabahi kijana aliyesimama nje ya gari.

“Ndiyo kaka nikusaidie?”
“Samahani sijui hapa ndiyo kwa Phillip?”
“Ndiyo!”alijibu Lina akionekana mwenye wasiwasi mwingi.
“Amenituma barua hii hapa,” alisema kijana huyo akinyoosha mkono kumwelekea Lina ili amkabidhi bahasha ndogo iliyokuwa mikononi mwake.
 
 
 
 
 
 

MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.62

HUKU akitetemeka aliunyoosha mkono na kupokea barua hiyo macho yake yote yakimwangalia kijana aliyemkabidhi, alitaka kumsoma vyema na kumwelewa alitoka wapi na alitumwa na nani.
“Ahsante kaka sijui naweza kukuuliza jambo?”
“Uliza tu dada yangu.”

“Naweza kufahamu barua hii imetoka wapi na kwa nani?”
“Mh, kwa kweli sifahamu mimi nimetumwa tu kuileta hapa.”
“Uliambiwa umpe nani?”
“Mke wake Phillip?”

Tayari mashavu ya Lina yalishajaa machozi, kichwani mwake alielewa kabisa kwamba barua hiyo ilitoka kwa Phillip hivyo alitaka kuthibitisha jambo hilo.
Baada ya maongezi hayo kijana huyo aliingia ndani ya gari lake na kuliwasha kisha kuondoka.
Taratibu huku mapigo ya moyo yakimwenda mbio, Lina alijikaza na kutembea kuingia ndani lakini hakufika mbali sana akaketi chini. Haraka akaanza kuchana bahasha ili asome barua iliyokuwa ndani.

Mke wangu mpendwa,Kwanza kabisa amini kwamba ninakupenda kwa dhati Mungu ni shahidi juu ya hili, nimeamua kuondoka hapo nyumbani kutokana na hasira iliyokuwa ndani yangu. Lengo langu kwako si baya ni zuri, sihitaji kitu kingine kutoka kwako zaidi ya mtoto, napenda unizalie mtoto mmoja tu nami niitwe baba. Jambo nililokueleza mwanzo sikukosea, nilitamka nikiwa na akili zangu timamu. Lina naamini unanipenda ndiyo maana ukaamua kunipokea mimi na matatizo yangu yote. Tafadhali fanya kila unachoweza ili lengo letu litimie.

Najua itakuwia vigumu kuamini maneno yangu lakini kipande hiki cha barua ni ushahidi tosha kwamba siwezi kukuruka hata kitokee nini, nakupenda mke wangu.
Ni kweli inauma sana lakini hakuna jinsi fanya unavyoweza tafuta mwanaume ambaye wewe mwenyewe utamridhia na uhakikishe unapata ujauzito wake, mimi binafsi sihitaji kumfahamu hata kidogo ninachohitaji ni wewe kupata ujauzito basi.

Najua kichwani mwako utakuwa na maswali mengi ambayo hayatapata majibu lakini huo ndiyo uamuzi wangu, Lina uvumilivu umefikia mwisho. Tafadhali mke wangu niamini niko tayari tena kwa moyo mkunjufu, nahitaji mtoto.
Kama utakuwa tayari kukubaliana na jambo hili na mimi mumeo, basi nipigie simu na kunijulisha nami nitakuwa tayari kurejea nyumbani tuendelee kuishi kama awali.

Sisi wewe tu unayelia machozi hata mimi mwenyewe nakiri kutoka ndani ya moyo wangu huku nilipo sina raha hata kidogo akili yangu yote ikiwa kwako mke wangu mpenzi.
Tafadhali chukua hatua fanya maamuzi sahihi kisha utanijulisha.
Nakupenda.
Ilimaliza barua hiyo.

Kwikwi ya kulia ikamkaba Lina, hakuwa tayari kuamini maneno yaliyokuwa ndani ya barua hiyo, taswira ya Phillip ikamjia kichwani mwake mfululizo, siku zote aliamini kwamba Phillip alikuwa ni mwanaume wa maisha yake lakini sasa kulikuwa na dalili zote kwamba penzi lao lilikuwa likielekea mwisho.
“Nampenda sana Phillip lakini kwa hili sipo tayari,” alisema Lina huku akijifuta machozi, haraka akanyanyuka na kukimbilia ndani.

Ulikuwa ni mtihani mwingine tena katika maisha yake. Hakuwahi kusikia wala kuona mwanaume aliyeweza kumtoa mkewe kwa mwanaume mwingine ili wafanye tendo la ndoa lengo hasa likiwa ni kupata ujauzito.
“Mh! Phillip hivi amepatwa na nini? Kwangu mimi mtoto si kitu, ninachojali ni mapenzi ya dhati, kwa nini asikubaliane na mimi? Mungu wangu tafadhali okoa jahazi hili lisizame, mimi siko tayari kufanya hivi anavyotaka.” Aliongea Lina machozi yakimbubujika.

Hatimaye usiku ukaingia bila kumwona Phillip akirejea nyumbani hapo ndipo akaamini kwamba mwanaume huyo alikuwa akimaanisha alichokisema.
“Nitamsubiri mpaka asubuhi niangalie kama kweli hatarudi basi nitajua cha kufanya.”
Usiku mzima hakupata hata lepe la usingizi, muda wote akimfikiria Phillip na mtihani aliokuwa amempa. Upande mwingine wa akili yake ulimwambia kwamba huenda mtu huyo alikuwa akimpima imani lakini upande mwingine ulimweleza wazi kwamba Phillip hakutania. Hatimaye mapambazuko yakawadia, Phillip akiwa bado hajarejea nyumbani, akayaamini maneno yake.

Siku nzima Lina alishinda ndani, aliamua kupiga simu kazini kwake na kuwaeleza kwamba siku hiyo asingeweza kudhuhuria kwani alikuwa mgonjwa hivyo alihitaji kupumzika ili kuangalia afya yake. Aliamua kuuficha ukweli kwa kudanganya hivyo ili tu asipate bughudha, huku akiwa na mawazo mengi kichwani mwake Lina bila kula kitu chohote alirejea kitandani kwake na kulala usingizi.

Saa zikazidi kusonga, hatimaye mchana ukaingia, akiwa hapo akapata wazo la kuamua kumpigia mmoja wa marafiki zake ofisini ili aongee naye na kumuuliza kama alishamuona Phillip ofisini siku hiyo. Akaisogelea simu kisha kubonyeza namba kadhaa na kuiweka sikioni.

“Habari?” alisikika akisalimia mtu upande wa pili wa simu ambaye hakuonekana akatulia kidogo na kisha kujibu.
“Oh! Leo naumwa rafiki siko sawa, nauliza jambo moja tu vipi leo umemwona shemejio?” akatulia tena.
“Yupo, basi nilitaka tu kujua kama amekuja maana anaweza kusema amekwenda kazini kumbe kapita kona,” alidanganya kisha wakaagana na simu kukatwa.

“Yaani Phillip! Phillip ananitenda hivi? Ameshindwa kurejea nyumbani lakini ameweza kwenda kazini? Lazima atakuwa na mwanamke sehemu fulani.
Amepata wapi nguo za kuvaa? Kwa inavyoonekana Phillip hatanii anamaanisha anachokisema…lakini mimi siwezi kufanya anavyotaka…mh! Naona penzi letu limefikia mwisho,” aliwaza Lina. Lakini ghafla akarejesha akili yake nyuma na kukumbuka mmoja wa marafiki zake katika ofisi yake alivyokuwa akimsifia Phillip, alionekana kumpenda kama si kumtamani.

“Inawezekana Magreth amenigeuka? Mara kadhaa amekuwa akimsifia sana Phillip, pengine ndiko huko alikokwenda? Hapana nitafanya uchunguzi kwanza.”
Wiki nzima ikakatika bila Phillip kurejea nyumbani, hali hiyo ikazidi kumtia Lina kizungumkuti, ni hapo ndipo alipoamua kumpigia simu Phillip na kumweleza kwamba anamwomba arejee nyumbani ili wafanye mazumgumzo.
“Tafadhali mume wangu naomba urudi nyumbani tuzungumze,” alisema Lina huku akilia.
“Je, umekubaliana na mimi?” aliuliza Phillip.

Kwa muda alikaa kimya akijaribu kutafakari ni jibu gani angempa mume wake ili akubali na kurejea nyumbani, hakuwa na jinsi alimhitaji mno. Huyo ndiye alikuwa mwanaume wa maisha yake, hakika alimpenda Phillip kwa dhati.
“Ni…ko…taya…ri,” alitamka Lina huku akilia.
 
 
 
 
 

MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.63.
BAADA tu ya kufanikiwa kuikata kamba na kutumia nguvu kidogo alizokuwa nazo huku damu nyingi zikimwagika sehemu ya bega la kushoto, alijaribu kupiga mbizi, lengo lake likiwa ni kujiokoa, kichwani mwake hakuwa na matumaini yoyote pamoja na kwamba alishapitia mambo mengi ya Kimafia lakini hilo kwake lilionekana kuwa gumu.

Kadiri alivyoendelea kupiga mbizi ndivyo fahamu nazo zilivyozidi kupotea taratibu, nguvu zikaonekana kumwishia, akazama mara ya kwanza na kuibuka juu akijaribu kupunga mikono hewani kuona kama angepata msaada wowote lakini haikuwa hivyo, akazama mara ya pili na kuibuka huku akimeza maji mengi akaanza kukata tamaa ya kuiona dunia akiwa hai.

Ni wimbi hilo ndilo lililotingisha mtumbwi wa Oleg Malenko na kumfanya kuamini kwamba sasa kifo chake kilikuwa kimekaribia kwa kuliwa na samaki mkubwa, kichwani mwake hakuelewa kabisa kwamba alikuwa ni mtu aliyekuwa akitapatapa baharini ili kujiokoa.

“Hapana nitahakikisha najiokoa, sipo tayari kuliwa na samaki hapa baharini,” alisema akiweka vizuri mtumbwi wake lakini ghafla alipotupa macho yake vizuri eneo hilo huku mapigo yake ya moyo yakimwenda mbio, alishuhudia mikono ya mtu ikichomoza kutoka ndani ya maji.

“Mh! Mbona naona mikono?” alijiuliza akimulika eneo hilo kwa taa yake ndogo aliyokuwa akiitumia katika shughuli zake za uvuvi. Macho yake hayakukosea ni kweli alikuwa ni mtu ambaye hakuelewa alikuwa mzima au mfu, kwa macho alionekana tayari alishakufa.
“Inawezekana amekufa lakini nitajuaje? Ni lazima nimguse kwa kasia ili nione pengine anaweza kuwa amezimia tu,” aliwaza.

Ghafla akiwa katika mawazo hayo alishuhudia mtu huyo akizama na kuibuka juu akitapatapa kama mtu aliyekuwa akikata roho kisha kutulia kimya, mwili wake ukaelea juu ya maji. Haraka bila kuchelewa, Oleg, kwa kutumia kasia alilokuwa nalo mkononi mwake, akalikamata vyema na kusogea karibu kabisa na mwili wa mtu huyo ambaye kwa kumwangalia mara moja alionekana kuwa amekufa.

Akiwa na hofu, akamgusa mtu huyo kwa kutumia kasia.
“Uko hai kweli wewe? Masikini wamekuua?” alijiuliza Oleg kwa Kirusi akizidi kumgeuza mtu huyo ambaye bado alionekana kutulia.

***
“Tafadhali mume wangu naomba urudi nyumbani njoo tuzungumze,” alisema Lina huku akilia.
“Je, umekubaliana na mimi?” aliuliza Phillip.
Kwa muda alikaa kimya akijaribu kutafakari ni jibu gani angempa mume wake ili akubali na kurejea nyumbani, hakuwa na jinsi alimhitaji mno, huyo ndiye alikuwa mwanaume wa maisha yake hakika alimpenda Phillip kwa dhati.
“Ni…ko…taya…ri,” alitamka Lina huku akilia.

Akiwa hapo ghafla akasikia simu upande wa pili ikikatwa bila kupewa jibu lolote.
“Amekata simu?” alijiuliza huku akijifuta machozi.
Ulikuwa ni mtihani mgumu kweli kwa Lina lakini alitakiwa kuufanya na kufaulu kama tu alimhitaji Phillip maishani mwake, huku akilia akarejea moja kwa moja na kuketi kwenye kiti, tayari ilishatimu saa kumi na mbili za jioni na mawazo yake yote yakiwa kwa Phillip ambaye mpaka wakati huo hakuelewa kama angerejea nyumbani au la kwani hakuwa ametoa jibu lolote.

“Piii! Piii! Piii!” ilikuwa ni honi nje ya lango la nyumba yao.
“Naomba Mungu awe yeye, niongee naye na kumbembeleza ili anielewe mimi siko tayari kufanya tendo la ndoa nje ya ndoa yetu,” alijisemea Lina.
Mawazo yake hayakukosea ni kweli alikuwa ni Phillip, Lina akanyanyuka kitini na kuusogelea mlango kisha kuufungua akimkaribisha ndani.

“Karibu mume wangu.”
“Mwaa!” lilikuwa ni busu lililotua moja kwa moja usoni mwa Lina kutoka kwa Phillip. Akiwa haamini alichokishuhudia kwa macho yake machozi ya uchungu yakamtoka Lina.
“Tafadhali usilie mke wangu yote haya yanatokea kwa sababu moja tu, mtoto!”
“Phillip, maisha bila mtoto hayaendi?”

“Yatakwenda lakini mtoto ni lazima Lina, sikia nimekuja kwa suala moja tu,” alisema Phillip safari hii akionekana mpole.
“Ndiyo.”
“Lina ninakupa mwezi mmoja tu nipate matokeo ya mjadala wetu vinginevyo utanikosa kabisa katika maisha yako,” alisema Phillip akionyesha umakini wa hali ya juu.
“Phillip hapana, bado nakupenda, nakuhitaji mume wangu.”

“Basi kama hivyo ndivyo fanya ninachotaka.”
“Nitafanya unachokitaka mume wangu lakini na nani?”
“Hilo suala nakuachia wewe mimi nimetoa ruhusa fanya unachoweza Lina wewe ni mwanamke tumia akili zako.”

“Mh!” Lina aliguna tayari Phillip alishanyanyuka kwenye kiti na kumwacha hapo peke yake akatembea kuuelekea mlango wa chumba chao, akaufungua na kuingia ndani. Lina akamwaga machozi, ni kweli alikuwa amefanikiwa kumrejesha Phillip nyumbani lakini hakuwa tayari kukabiliana na mtihani uliokuwa mbele yake kwani alishatumia akili zake zote kumshawishi kuondokana na mawazo hayo lakini ilionekana kushindikana, haja ya Phillip ilikuwa ni mtoto basi.

***
“Nitamuokoa hata kama atakuwa amekufa nitamzika kwa heshima zote, hastahili kuachwa kama mzoga!” alisema Oleg.
Moyo wake uliingia huruma na aliumia zaidi alipomwangalia mtu huyo akielea majini mwili wake ukiwa mtupu bila nguo.
“Ni kwa nini watu wanafanya ukatili wa aina hii? Alikosa nini huyu mpaka kustahili adhabu hii? Mungu nisaidie!” alisema mfululizo, muda wote huo akiendelea kumtingisha mtu huyo kwa kutumia kasia.

Dakika tano nzima aliendelea kumtingisha bila mtu huyo kujigeuza wala kujitingisha hapo ndipo akaamini kwamba tayari alishakufa hivyo kufikia uamuzi wa kumtoa ndani ya maji ili ampeleke ufukweni na huko angetafuta sehemu na kumzika kwa heshima zote.
 
 
 
 
 

MSICHANA NDOTONI MWANGU.....EP.64

Huku akitetemeka na jasho jingi kumtoka, Oleg Malenko alijitahidi kwa nguvu zake zote kumtoa mtu huyo ndani ya maji na kumpandisha juu ya mtumbwi wake tayari kwa kurejea nchi kavu. Aliamini akifika huko ndiyo angefahamu ukweli wote kama alikuwa hai au amekufa.

“Kama atakuwa amekufa basi itakuwa ni bahati mbaya, nitamzika,” aliwaza huku akimgusa mtu huyo shingoni mwake. Baada tu ya kumpandisha ndani ya mtumbwi, bila kuchelewa akaugeuza haraka na kuanza kupiga kasia kurejea nchi kavu. Haikumchukua muda, akawa tayari amewasili ufukweni, akaegesha vizuri mtumbwi wake na kushuka, mikononi mwake akiwa amembeba mtu huyo.

Alipohakikisha kwamba tayari ameshayaacha maji kwa umbali mrefu, kwa haraka alimshusha chini na kumlaza, akainama na kuanza kusikiliza mapigo ya moyo. Kwa takribani dakika tatu nzima alikuwa akisikiliza lakini hakusikia kitu, kichwani mwake akaamini kabisa kwamba mtu huyo hakuwa hai.

“Nitachimba shimo pale haraka haraka na kumfukia hapo,” aliongea kwa kunong’ona. Akaangaza macho yake huku na kule kuangalia kama kulikuwa na mtu yeyote eneo lile lakini hakufanikiwa kuona kitu.
“Huu ndiyo muda, nikichelewa tu watu wakaniona watajua mimi ndiye nimemuua kumbe nasaidia tu,” akiwa katika mawazo hayo ghafla alisikia mtu akikohoa mfululizo.
“Khoo!Khoo!Khoooo!” Oleg Malenko alishtuka na kugeuka kuangalia, lakini hakuona mtu, alipogeuka tena upande mwingine sauti ya kikohozi ikasikika, safari hii kwa nguvu.

Haraka akatupa macho yake kumwangalia mwanaume aliyekuwa amelala chini, huyo ndiye aliyekuwa akikohoa mfululizo. Bila kuchelewa akasogea karibu ili asikie vizuri, hakukosea alikuwa ni yeye.
“Mh! Amekohoa? Hajafa huyu, ngoja nimpe huduma ya kwanza niangalie itakuwajea,” alisema huku akimgeuza mtu huyo na kumlaza kifudifudi. Akapiga magoti juu ya mgongo wake na kumkandamiza ili kumsaidia kutoa maji yaliyokuwa tumboni mwake.

Hakukosea, alichokuwa akikifanya kilikuwa ni sawa kabisa. Kwa takribani dakika tatu nzima aliendelea kumkandamiza mgongoni, maji mengi yakawa yanamtoka hadi alipohakikisha maji aliyoyameza mtu huyo yamekwisha. Akamgeuza na kumlaza kiubavu huku akijaribu kuongea naye.
“Wewe ni nani? Umetoka wapi? Imekuwaje ukawa hapa?” aliuliza mfululizo lakini hakupata jibu kutoka kwa mtu huyo ambaye alilala kimya ardhini akitetemeka.

“Tafadhali niambie nini kimekupata?” aliendelea kuuliza huku akimchunguza vyema mtu huyo.
“Di…t…ro…” aliongea kwa shida lakini kabla hajamaliza sentensi yake, Oleg Malenko akashuhudia mtu huyo akirusha mikono na miguu kisha kutulia kimya.
“Mh! Hizi damu zinatoka wapi?” alijiuliza huku akimfunua upande huo. Macho yake yakakutana na jeraha kubwa.
“Hili ni jeraha la risasi ambalo limesababisha kuvuja kwa damu nyingi kiasi hiki, lazima nifanye kitu kuokoa maisha ya mtu huyu,” alisema huku akijaribu kumnyanyua sehemu aliyokuwa amelala.
Wazo pekee likamjia kichwani mwake kwamba ni lazima mtu huyo apate matibabu haraka hospitalini lakini hakujua atampeleka hospitali gani.

Hiyo ilikuwa ni kwa sababu ya machafuko makubwa yaliyoikumba nchi ya Urusi. Aliendelea kujiuliza ni hospitali gani angempeleka mtu huyo na kupokelewa bila maelezo ya kutosha! Akahisi hiyo ingekuwa hatari nyingine kwake. Alihisi anaweza kuingia kwenye kesi ambayo asingeweza kujinasua kama mtu huyo angekuwa amekufa.

“Hapana, sitampeleka hospitali. Nitampeleka nyumbani kwangu, naamini hajafa. Huko nitampa matibabu mpaka apone kabisa, hapo atakuwa tayari kunieleza ukweli wa nini kilichompata,” alisema Oleg Malenko. Tayari mapambazuko yalishaanza kuchomoza.
***
Mapenzi yote yaliyokuwa katikati yao yalionekana kupotea, furaha ndani ya nyumba ikageuka na kuwa shubiri. Phillip akisisitiza jambo moja tu, mtoto! Kwa muda wa wiki nzima, Lina aliendelea kumbembeleza na kumsihi Phillip aachane na jambo lililokuwepo kichwani mwake na badala yake wale na kufurahia maisha.
“Lina, hakika hujaweza kunishauri juu ya hili. Fanya ninachotaka halafu tutaelewana,” alisema Phillip huku akigeuka upande mwingine wa kitanda, akavuta shuka na kujifunika gubigubi. Hata Lina alipojaribu kumuita, bado hakujibu wala kugeuka. Kwa mara nyingine tena moyo wa Lina ukauma kupita kawaida, akanyanyuka kitandani, akafungua mlango wa chumba na kutoka nje huku akilia.


Wakati akitembea kuelekea sebuleni ghafla wazo likamjia kichwani mwake. Akalikumbuka jina Daniel, kijana mtanashati kweli kweli ambaye kwa muda mrefu alikuwa akimfuatilia Lina akimtaka kimapenzi. Mara zote aliambulia majibu ya karaha na pengine yaliyouchoma moyo wake kama mkuki wa moto.


“Daniel! Sijui atakuwa wapi kwa sasa? Na sijui kama bado atakuwa hajaoa! Je, nitaanzia wapi kumweleza kwamba nampenda ilhali nilishamuumiza moyo? Lakini nitajaribu, sipendi kumpoteza Phillip. Naamini huyu ndiye mwanaume wa maisha yangu yote,” alisema Lina, akakisogelea kiti na kuketi juu yake kwa muda. Aliendelea kutafakari juu ya tatizo lililokuwa ndani ya nyumba yake, alitakiwa afanye kitu fulani ili kuinusuru ndoa yake. Tayari mashavu yake yalishalowa kwa machozi.


“Kesho asubuhi nitamtafuta Daniel, najua atashangaa lakini sina jinsi, huyu pekee ndiye atakayewe…” alisema lakini kabla hajamaliza sentensi yake, kwikwi ya kulia ikamkaba tena.
 
 
 
 
 

MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.65

“Daniel! Sijui atakuwa wapi kwa sasa? Na sijui kama bado atakuwa hajaoa? Je, nitaanzia wapi kumweleza kwamba nampenda ili hali nilishamuumiza moyo? Lakini nitajaribu, sipendi kumpoteza Phillip, naamini huyu ndiye mwanaume wa maisha yangu yote,” alisema Lina akakisogelea kiti na kuketi juu yake, kwa muda aliendelea kutafakari juu ya tatizo lililokuwa ndani ya nyumba yake, alitakiwa afanye kitu fulani ili kuinusuru ndoa yake. Tayari mashavu yake yalishalowa kwa machozi.


“Kesho asubuhi nitamtafuta Daniel najua atashangaa lakini sina jinsi, huyu pekee ndiye atawe…” aliwaza lakini kabla hajamaliza sentensi yake kwikwi ya kulia ikamkaba tena.


Hakika hakuelewa maisha yake yangekuwa vipi kama tu asingeweza kukubaliana na Phillip, mumewe, ambaye mpaka wakati huo hawakuwa na maelewano mazuri ndani ya nyumba. Aliendelea kubaki eneo hilo bila kurejea chumbani hapo, kazi ikawa moja tu kulia mpaka usingizi ulipomchukua ambapo alizinduliwa na sauti ya mlango ukifunguliwa na aliponyanyua uso kuangalia alimwona Phillip akitembea kumsogelea.

Bila kusema kitu alimshuhudia akimwinamia na kumbusu kisha kumpigapiga mgongoni.
“Lina!”
“Yes darling!” alijibu huku machozi yakimbubujika, akili yake ikarejea kwenye mazungumzo yote yaliyofanyika jana yake.


“Naamini umeshapata jibu la tatizo linalotusumbua.”
Bila kujibu chochote akiwa hapo akanyanyua uso wake na kumwangalia Phillip machoni.
“Unalia nini?” lilikuwa ni swali kutoka kwa Phillip baada ya kumwangalia vyema Lina usoni aligundua macho yake yalikuwa yamevimba kupita kawaida.


“Hakika huo ndio msimamo wangu mke wangu, ni kweli inauma lakini sina jinsi.”
“Yupo mtu ambaye nimemfikiria jana usiku, huyu nadhani anaweza kunisaidia.”
“Ni vyema ukafanya hivyo mara moja lakini tu awe ni mtu unayemwamini sana na nisingependa afahamu siri iliyoko kati yetu, cha muhimu ni wewe kujiweka sawa ili kupata ujauzito basi mambo mengine tutajua mbele ya safari. Sawa mke wangu?”


“Sa…wa,” alijibu lina huku akilia.
Bila kusema kitu Phillip akanyanyuka kitini kisha kumnyanyua Lina wote wawili wakaingia chumbani ili kujiandaa kwa ajili ya kwenda kazini, lakini mambo hayakuwa hivyo.

Baada tu ya kuingia ndani huku wote wawili wakiwa kimya Phillip alimnyanyua Lina na kumrushia kitandani naye akifuata kwa nyuma bila kuchelewa, akaanza kumvua nguo moja baada ya nyingine kisha akabaki mtupu kama alivyozaliwa.


“Lina nakupenda,” ilikuwa ni sauti ya Phillip ikipita masikioni mwa Lina.
“Una..se…ma..kwe..li?” aliuliza lina kwa sauti ya kutetemeka.

“Asilimia mia moja mke wangu mambo yote haya yanatokea si kwa sababu mimi nakuchukia hapana…” alisema Phillip akilivuta shuka na wote wawili wakajifunika gubigubi.


Kilichofuata baada ya hapo hakiandikiki kwani ilikuwa ni kama vile watu wakiimba mapambio na wengine kuitikia, mara chache sana sauti ya Lina ilisikika lakini ilimezwa na mabusu mfululizo yaliyotoka kinywani mwa Phillip. Saa mbili baadaye wote wawili walikuwa hoi bin taaban jasho jingi likiwatiririka.
“Nimeamua kufanya hivi kwa sababu nataka uamini kwamba ninakupenda kwa dhati na si kitu kingine, sawa?” Phillip alisema.

“Ahsante!” alijibu Lina akimwangalia Phillip kwa jicho la huruma.
“Hebu nieleze ni nani huyo unayemfikiria?” Phillip aliuliza kwa upole.
“Yupo kijana mmoja anaitwa Daniel huyu tulisoma naye huko nyuma na alinipenda sana.”
“Je, unamwamini?”

“Asilimia zote labda itokee tu kwamba ameoa kwa sasa?”
“Hata kama ameoa tunachohitaji sisi ni yeye kukupa mamba, basi, mambo mengine yote atuachie sisi wenyewe.”

“Nipe muda nimtafute kisha nitakujulisha.”
“Ahsante mke wangu sasa naamini kweli unanipenda.”
“Nakupenda pia Phillip, yote haya nafanya ili kulinda penzi letu, sipendi kukupoteza, wewe ni wangu mpaka mwisho.”
“Najua jambo hilo ila kitu kimoja tu nikuombe.”
“Ni nini hicho?”
“Nihakikishie kwamba baada tu ya kufahamu kwamba umepata mimba hutarejea tena kwa Daniel.”
“Siwezi kufanya hivyo Phillip unanifahamu vyema, jambo hili linatokea kwa sababu wewe ndiye umetaka.”
“Basi nakuamini fanya kila unachoweza umpate kisha utanijulisha kila hatua, sawa?”
“Nitafanya hivyo,” alisema Lina na wote wawili wakanyanyuka na kuingia bafuni kuoga ili wajiandae tayari kuelekea kazini.

Dakika tano baadaye tayari wote wawili walishakuwa tayari wakatoka mpaka nje ambako walisalimiana na mlinzi kisha wakaingia ndani ya gari, Phillip akiketi kwenye usukani, safari kuelekea ofisini ikaanza, njiani wakiongea mambo mengi kuhusu maisha na mapenzi yao na furaha ilionekana kurejea tena katika mapenzi yao.

Kutokana na msongamano wa magari siku hiyo walilazimika kutumia saa moja mpaka kufika ofisini kwao, wakafika na kuegesha gari lao kisha kushuka. Phillip akazunguka mpaka sehemu alipokuwa amesimama Lina na kumshika mkono, kwa pamoja wakatembea kuingia ndani ya ofisi. Yalikuwa ni mazoea ya Phillip kumsindikiza Lina mpaka anahakikisha ameingia ndani ya ofisi yake ndipo yeye atoke na kuelekea ofisini kwake.

Taratibu huku wakionyesha nyuso za tabasamu walitembea mpaka kuufikia mlango wa ofisi ya Lina, akafungua ili aingie ndani lakini kabla hajafanya hivyo akavutwa kwa nyuma.
“Darling!” ilikuwa ni sauti ya Phillip.
“Yes.” (Ndiyo.)
“Nimesahau kitu.”
“Kitu gani?”
Bila kusema kitu chochote akamsogelea Lina na kuanza kumbusu mfululizo bila kujali watu waliokuwa wakipita eneo hilo.
“Ahsante…” alisema Lina akitabasamu.
“Tafadhali kumbuka kumtafuta Daniel” alisema Phillip kwa sauti ya kunong’ona.
***
“Vrooom!Vrooom!” ilikuwa ni sauti ya kitu kikiburuzwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Kwa sababu hakutaka jambo hilo ligundulike na mtu mwingine, aliamua kuuficha ukweli huo kwa kumburuza mtu huyo na kwenda kumweka pembezoni mwa mitumbwi mibovu amwache hapo na yeye atembee kurejea mpaka sehemu ambako aliamini angepata usafiri na amchukue tayari kwa kumpelekea nyumbani kwake ambako angefanya kila kilichowezekana kuokoa uhai wa mtu huyo.

“Nikipata tu usafiri na kuongea na dereva anisaidie kumfikisha mtu huyu nyumbani itakuwa safi, nitamlipa kiasi atakachotaka lakini afiche siri hii,” aliwaza Oleg Malenko.

Haraka bila kupoteza muda alipohakikisha kwamba amemweka mtu huyo sehemu salama, alitoka haraka na kuangaza macho yake huku na kule na alipohakikisha kwamba hapakuwa na mtu, akaanza kutembea kuondoka eneo hilo.

“Nitamsaidia mpaka mwisho bila kuchoka kwa kumwangalia, anaonekana ni mtu mwema, naomba Mungu asije kuwa mtu mbaya,” alijisemea akizidi kusonga mbele.

Dakika tano tu tayari alishatokeza barabarani, akaongoza moja kwa moja mpaka mahali ambako teksi zilisimama hapo kungoja wateja, akaisogelea moja na kuanza kuongea na dereva, kwa dakika tatu nzima walifanya mazungumzo na kuonekana kukubaliana, haraka akazunguka upande wa pili na kupanda kisha gari hilo kuondoka eneo hilo.

“Nitakuonyesha sehemu ya kusimama kisha kuomba msaada wako ili tumchukue haraka kumpandisha ndani ya gari.”
“Hakuna shida,” alijibu dereva huyo kwa lugha ya Kirusi.
Haikuchukua muda tayari wakawasili eneo la tukio, Oleg Malenko akawa mtu wa kwanza kushuka ndani ya gari na kuanza kumwongoza mwenzake lakini kabla hawajamfikia, macho yake yalishuhudia jambo ambalo halikuwa la kawaida.
“Mh!” aliguna.

Je, nini kitaendelea? Lina anakabiliwa na mtihani mzito. Je, atafanikiwa kuufaulu? Oleg Malenko ameona kitu gani? Fuatilia kesho kama kawa!!!goodnite NAWAPENDA NYOOOTEEE!!!
 
 
 
 
 
 

MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.66

HARAKA bila kupoteza muda anaangalia huku na kule na kuhakikisha kwamba alimweka mtu huyo sehemu salama. Oleg Malenko anatoka mbio eneo hilo kuelekea barabarani kichwani mwake akiwa na wazo moja tu, kutafuta gari ambalo lingemsaidia kumfikisha mtu huyo nyumbani kwake na huko angepata matibabu na kupona.

“Nitamsaidia mpaka mwisho bila kuchoka, kwa kumwangalia anaonekana ni mtu mwema naomba Mungu asije kuwa mtu mbaya.” Aliongea akizidi kusonga mbele.

Dakika tano tu tayari alishatokeza barabarani, akaongoza moja kwa moja mpaka mahali ambako teksi zilisimama kwa ajili ya kungoja wateja, akaisogelea moja na kuanza kuongea na dereva, kwa dakika tatu nzima walifanya mazungumzo na kuonekana kukubaliana, haraka akazunguka upande wa pili na kupanda kisha gari kuondoka eneo hilo.

Haikuchukua muda wakawasili eneo la tukio, Oleg Malenko akawa mtu wa kwanza kushuka ndani ya gari na kuanza kumwongoza mwenzake lakini kabla hawajamfikia macho yake yalishuhudia jambo ambalo halikuwa la kawaida.Je, nini kinaendelea?

Upande wa pili wa hadithi hii tunamwona Lina akifikiria jinsi ya kumpata kijana Daniel ambaye angeongea naye na kumshawishi wafanye tendo la ndoa na kupata ujauzito, ni mtihani mgumu lakini alitakiwa kuufanya ili kumlinda mwanaume aliyempenda kwa dhati.

Je, nini kitaendelea hapa? Atafanikiwa kumpata Daniel? Na nini kitatokea? SONGA NAYO…

“Tafadhali kumbuka kumtafuta Daniel,” aliongea Phillip kwa sauti ya kunong’ona.
Ni maneno hayo yaliyofanya kumbukumbu za Lina kurejea upya kichwani mwake, moyo wake ukaenda mapigo ya haraka haraka kama vile mtu aliyekuwa akikimbia mbio ndefu.

“Mungu nisaidie kufanya jambo hili.” Alinong’ona akizama ndani ya ofisi yake. Taratibu akakisogelea kiti kikubwa kilichokuwa nyuma ya meza kubwa na kuketi huku jasho likimtiririka.
“Sina namna ni lazima nimtafute Daniel tu ili kulinda penzi langu kwa Phillip.” Aliwaza.
Kwa muda wa dakika tano nzima alikaa kimya akijaribu kutafakari nini cha kufanya lakini bado hakupata jibu na upande mmoja wa akili yake ulimwambia kwamba kama asingethubutu kufanya jambo hilo hakika angemkosa Phillip maisha yake yote.

Akiwa hapo huku machozi yakimbubujika, Lina akavuta moja ya droo iliyokuwa karibu na meza aliyoketi, akaanza kuchambua karatasi moja baada ya nyingine akitafuta mahali ambako aliamini angeweza kupata maelezo ya namna ya kumpata Daniel.
Alipitia karatasi moja baada ya nyingine na kwa bahati nzuri akafanikiwa kupata moja ya barua ambazo Daniel aliwahi kumwandikia miaka mingi.

“Nimeipata.” Aliongea akiichomoa karatasi hiyo na kuishika vyema mikononi mwake ili asome.
Taswira ya Daniel ikamjia kichwani mwake, akamwona jinsi alivyokuwa ni kweli alistahili kuitwa mwanaume wa shoka kwani alikuwa na kila sababu ya kupewa tunu hiyo, alikuwa ni kijana mrefu, rangi yake ya ngozi pia ilivutia na midomo yake ilikuwa minene na zaidi ya yote, Daniel alikuwa na kifua kipana kilichofanya kila mwanamke aliyemwona amtamani kimapenzi. Hakika alisisimua.
“Anazo sifa zote lakini mimi …” Lina aliongea, hata kabla hajamalizia sentensi yake mlango wa ofisi yake ukagongwa.

***
“Mh!” Oleg Malengo aliguna akijaribu kuangaza macho yake huku na kule kama vile alikuwa akiangalia kitu fulani.
“Kuna nini?” Dereva wa teksi naye akauliza akionesha wasiwasi mwingi.
Bila kujibu swali alilokuwa ameulizwa alitembea haraka kusonga mbele hakika alionekana kama mtu aliyekuwa akisaka kitu ambacho hakikuonekana.

“Kimetokea nini? Mbona alikuwa hapa?” Alijiuliza.
Kwa ujasiri mkubwa akasogea mpaka mahali alipokuwa amemwacha mwanaume aliyemwokoa ndani ya maji lakini hakumwona, alichokuwa amekishuhudia kwa macho yake yote mawili ni alama za mburuzo ulioonekana ardhini.
“Ameondoka.” Aliongea.
“Nani?”

“Yule niliyekueleza kwamba nahitaji unisaidie?”
“Lakini si ulisema ana hali mbaya?”
“Ni kweli nashangaa pengine amepata nguvu.”
“Sidhani hebu kumbuka vizuri ni hapa kweli ulipomwacha?”
“Hakika ni hapa alama zake zi hizi hapa.”

“Mh.” Dereva teksi naye akaguna hakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea.
Kabla ya Oleg Malenko kwenda kutafuta usafiri alipokuwa akimweka mwanaume huyo vyema eneo aliloamini kuwa ni salama na kuondoka kuelekea barabarani kwa ajili ya kutafuta usafiri jambo la ajabu lilitokea, upepo mkali ukiambatana na ubaridi mkali ulipiga eneo la ufukweni na upepo huo ndiyo uliosababisha mwanaume aliyekuwa katika hali ya kutojitambua aanze kutapatapa kutafuta msaada, hatimaye kujikuta amejiburuza na kuelekea nyuma ya mitubwi mibovu iliyokuwa karibu yake.

“Kama kweli una uhakika basi atakuwepo hapa hapa hebu tufuatilie alama za miburuzo kuangalia ilipoishia.” Aliongea dereva teksi huyo na moja kwa moja wakaanza kuufuatilia miburuzo hiyo.
“Umepita hapa.” Aliongea Oleg Malenko.
Akili ya dereva teksi ilikuwa imefanya kazi sawasawa, ni kweli kabisa alikuwa hawajakosea wazo lake la kufuata miburuzo iliyokuwa ikionekana ardhini lilisaidia na hatua chache tu kutoka mahali waliposimama waliona miguu ya mtu.
“Hii ni miguu ya mtu.”

“Ni kweli, hebu tuone,” Oleg Malenko aliongea.
Haraka haraka bila kuchelewa wakazunguka na kuanza kumwangalia mtu huyo usoni, alikuwa ni yule yule aliyekuwa amemwacha muda mfupi uliopita, akamgeuza na kumlaza chali mdomoni alionekana kutokwa na mapovu mengi.
“Mh! Yuko hai kweli huyo?” Dereva teksi aliuliza.
“Sijui hata mimi nashangaa, nilipomwacha muda mfupi hakuwa hivi alikuwa amepoteza tu fahamu.”

“Sasa amefikaje hapa na ni kitu gani kimempata mpaka kufikia hatua hii?”
“Sina jibu ila nisaidie tu tumwondoe hapa.”
“Kwenda wapi, anaonekana tayari ameshakufa huyu.”
Oleg Malenko akainamna na kumshika mwanaume huyo sehemu ya shingo yake kuangalia kama moyo yake yalikuwa yakipiga au la!
“Bado hajafa nasikia mapigo yake yakipiga lakini kwa mbali.”

“Ushauri wangu ni bora umwache afe tu hapa kwani hakuna mtu atakayegundua.”
“Tafadhali nisaidie hata kama atakufa, basi afie ndani ya nyumba yangu wakati nikijaribu kumsaidia.” Aliongea Oleg Malenko kwa sauti ya upole.
“Sawa nitakusaidia wewe tenga tu fedha yangu.” Aliongea dereva huyo kwa lugha ya Kirusi.

Wote kwa pamoja wakainamna na kumnyanyua mwanaume aliyekuwa amelala chini na kuanza kutembea kuelekea sehemu walipokuwa wameegesha gari hapo wakamlaza tena chini na dereva kufungua mlango kisha wakamwinua na kumweka kwenye kiti cha nyuma, wote wakaingia ndani ya gari na safari kuelekea nyumbani kwa Oleg Malenko ikaanza, njia nzima alikuwa akimfikiria mgonjwa aliyekuwa naye, alitaka apone ili amsimulie ni kitu gani kilichompata.

“Naomba Mungu amsaidie asife, apone.” Aliwaza kichwani mwake gari likizidi kuchanja mbuga.
Baada ya mwendo wa nusu saa walishawasili nyumbani kwa Oleg Malenko, yeye akawa mtu wa kwanza kufungua mlango na kushuka bila kusema kitu akamwomba tena dereva wa gari aliyekuja naye amsaidie kumshusha mgonjwa, haraka wakafanya hivyo na kumwingiza mgonjwa ndani ya nyumba.
“Ahsante sana rafiki.” Aliongea Oleg Malenko akimkabidhi dereva huyo kiasi cha fedha kama malipo yake na kumshukuru.

***
“Ngo!Ngo!Ngo!” Sauti ya mlango ikasikika na kumshtua Lina kutoka katika mawazo aliyokuwa nayo. Haraka bila kuchelewa hata kabla hajaitika akaifungua droo na kuitumbukiza barua hiyo haraka alipohakikisha kwamba alikuwa sawa akamkaribisha mtu aliyekuwa mlangoni.
“Ndiyo karibu.” Aliongea kwa sauti ya upole.

Mlango ukafunguliwa na mwanaume mmoja akaonekana akiingia.
“Oh! Karibu sana bosi.” Aliongea Lina akionyesha tabasamu usoni mwake.
“Natumaini hujambo, nimekuja kwa jambo moja tu hapa.”
“Ndiyo bosi.”
“Ah! Mwezi ujao kutakuwa na safari ya kwenda Ujerumani na itatuhusisha mimi na wewe ni vyema ukawa na ufahamu na jambo hilo.”

Badala ya kujibu Lina akainamisha kichwa chake chini, si kwamba hakuifurahia safari hiyo, la hasha! Kichwa chake kilijaa mawazo mengi juu ya ndoa yake na kitu pekee alichokuwa akikihitaji ni kulinda penzi lake kwa Phillip basi.
“Lina!” Sauti ikasikika.
“Bee”

“Kuna nini kinaendelea kichwani mwako? Hauko sawa kabisa.”
“Hapana bosi niko sawa niko tayari kwa safari hakuna shida.” Alijibu Lina kwa sauti ya chini.
Wakaagana, kisha bosi akafungua mlango na kutoka nje akimwacha Lina ndani ya ofisi peke yake.

Huku akitetemeka taratibu akanyoosha tena mkono wake na kufungua droo ambayo ndani yake ilikuwepo barua iliyokuwa na maelezo yote jinsi ya kumpata Danniel akaichukua na kuanza kubonyeza.
“Ngrii! Ngrii! Ngriii,”Simu ilikuwa ikiita upande wa pili.
 
 
 
 
 
 

MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.68

Tafa…dhali okoa mai…sha yangu si..taki kufa…,” alisema mwanaume huyo akijaribu kunyanyuka kitandani ili aketi lakini zoezi hilo lilionekana kuwa gumu kwake kutokana na jinsi hali yake ilivyokuwa.
Oleg Malenko, huku akitia huruma alimsogelea mwanaume huyo na kuanza kumsaidia ili anyanyuke na kuketi. Zoezi hilo lilipokamilika naye pia akaungana naye kitandani lakini kabla hajaanza kusema kitu chochote, mwanaume huyo huku akitetemeka aliomba maji ya kunywa.

“Nisai…die ma…ji ya ku…nywa…,” alisema kwa tabu.
Haraka bila kuchelewa akanyanyuka na kuisogea meza ndogo iliyokuwepo ndani ya chumba kile, akachukua kikombe kikubwa kilichokuwa juu yake ambacho ndani yake kulionekana kuwa na maji.
“Haya hapa.”

Huku akitetemeka mwanaume huyo akajitahidi kukipeleka kikombe hicho mdomoni na kuanza kunywa maji yaliyokuwemo ndani, haikuchukua hata sekunde tatu, yakawa yamekwisha.
‘Inawezekana ana njaa huyu,’ aliwaza moyoni mwake huku akipokea kikombe na kukiweka mahali pake.
Bila kusema kitu chochote, Oleg Malenko akausogelea mlango na kufungua. Akachungulia na kuita jina la mkewe, bila kuchelewa mkewe alifika, ikasikika sauti ya Oleg Malenko ikimwomba asaidie kupiga uji haraka kisha aulete chumbani mle kwa ajili ya mgonjwa.

“Kwani ameamka?”
“Ameamka lakini sijaweza kuongea naye, kwa anavyoonekana anahitaji kupata kitu kidogo cha kula.”
“Afadhali! Mungu ni mwema jamani, nilishakata tamaa.”
“Tafadhali nisaidie sasa hivi.”

“Sawa,” alisema mwanamke huyo na hatua za mtu aliyekuwa akitembea kuondoka eneo hilo zikasikika. Oleg Malenko akarejea ndani ya chumba na kufunga mlango nyuma yake.
“Naweza kukuuliza maswali machache?” alisema huku akisogea karibu kabisa na kitanda alicholala mgonjwa.
Kwa ishara ya kichwa mwanaume huyo akaonesha kukubaliana na jambo alilolisikia kutoka kwa mwenyeji wake.

“Wewe ni nani vile?” aliuliza tena lengo likiwa ni kupata uhakika wa jina alilolisikia mwanzo.
“Ditrov!” alijibu kwa sauti ya kunong’ona.
”Ah! Kumbe ni sawa kabisa na jina ulilolitamka mwanzo kabla hujapoteza fahamu, pole.”
“Ahsante.”

“Nini kilitokea mpaka ukawa kwenye hali hii?”
Ditrov bila kujibu kitu chochote aliinamisha kichwa chake chini na kuanza kulia, aliishuhudia picha nzima ya tukio lote alilotendwa na Federov.
“Mbona unalia?”

“Nisaidie nipone, nitakueleza kila kitu. Ni habari ndefu kidogo lakini yenye machungu mengi,” alisema Ditrov huku akibubujikwa na machozi.
“Nitakusaidia na nina uhakika uta...” alisema Oleg Malenko lakini kabla hajamalizia sentensi yake, mlango wa chumba walichokuwemo ndani yake ukasikika ukigongwa.
“Ngo!Ngo!Ngo.”

***
Muda mfupi baada ya kukata simu ya Daniel, Lina alinyoosha mkono wake tena na kunyanyua mkono wa simu akaonekana akibonyeza namba kadhaa na kuiweka simu sikioni.
“Hallow,” aliita na bila kuchelewa sauti nzito ikijibu upande wa pili wa simu ikasikika.
“Phillip?” aliuliza.

“Yes darling.” (Ndio mpenzi) Ilikuwa ni sauti kutoka upande mwingine wa simu.
“Nimempata! Nimefanikiwa kuongea naye na tumekubaliana kukutana leo jioni Lamada Hoteli kwa mazungumzo zaidi,” alisema Lina na muda wote huo tayari machozi yalishalowanisha mashavu yake.
“Lina?” Phillip akiwa upande wa pili wa simu aliita.

“Be…e” aliitikia kwa sauti ya kutetemeka. Ni sauti hiyo ndiyo iliyomfanya
Phillip ashtuke na kugundua kwamba Lina alikuwa akilia.
“Nakuja hapo sasa hivi,” alisema Phillip na kuikata simu. Bila kuchelewa haraka akanyanyuka kitini na kuufungua mlango wa ofisi yake. Akatoka bila kusema kitu chochote, safari ya kuelekea ofisini kwa Lina ikaanza. Haikumchukua muda, baada ya dakika tatu tu akawa amewasili eneo hilo na kugonga mlango. Aligonga kwa muda lakini hakupata jibu, hatimaye akaamua kuusukuma na kuzama ndani.

“Lina!” aliita baada ya kutupa macho yake mbele na kumwona Lina akiwa amejiinamia tena akionekana kulia.
“Nini kimetokea tena? Kwa nini unalia?” aliuliza mfululizo.
Akiwa hapo akamshuhudia Lina akinyanyuka na kumsogelea kisha kumkumbatia.

“Phillip ninakwenda kufanya jambo ulilohitaji ili kulinda ndoa yetu, siko tayari kukupoteza mume wangu, naamini wewe ni wangu mpaka kifo… lakini ukweli kutoka ndani ya moyo wangu nasikia moto ukiwaka na kunipa maumivu makali. Nashindwa kuelewa ni kwa nini…” alisema Lina na kabla hajafika mwisho wa sentensi yake wakasikia hatua za mtu akisogea karibu kabisa na mlango wa ofisi ya Lina.

Haraka Lina akamwachia Phillip na kujifuta machozi kisha kuzunguka upande wa pili ambako alikivuta kiti chake na kuketi. Hawakukosea, hatua walizozisikia zilikielekea eneo hilo zilikuwa ni za bosi wake Lina ambaye aliondoka hapo muda mfupi uliopita.
Akabisha mlango na kukaribishwa kuingia ndani. Naye alishangazwa na hali aliyomwona nayo Lina.
“Lina nini kimetokea? Unaumwa?” aliuliza kwa sauti ya upole.

“Hajisikii vizuri ndiyo maana na mimi niko hapa, nataka kumpeleka hospitali,” Phillip alidakia.
“Basi ni vyema ukafanya hivyo, nitaongea naye kesho kwani nilikuwa na habari njema za kumpa,” alisema bosi huyo na kutoka huku akifunga mlango nyuma yake.

Alipotoka, kwa haraka Phillip akanyanyuka kitini na kumsaidia Lina kuweka ofisi katika hali ya usafi. Mambo yalipokamilika akamwomba amsaidie kubeba mkoba wake, wakatoka ofisini na kuelekea sehemu ambako waliegesha gari lao, wakapanda na kuondoka eneo lile.
Njia nzima Lina alikuwa akilia. Hakuweza kuvumilia, mara kadhaa alimuuliza Phillip maswali na kujibiwa lakini hakuwa tayari kukubaliana na majibu hayo.

“Sikia mke wangu, nakupenda sana na ili kukuhakikishia nitakupeleka mwenyewe mpaka hotelini na mimi nitakusubiri mpaka mwisho, umenielewa?” aliuliza Phillip akimpigapiga Lina mgongoni.
“Fyuuu!” badala ya kujibu Lina akashusha pumzi.

Phillip akazidi kukanyaga mafuta na nusu saa baadaye tayari walishafika nyumbani hapo wakashuka na kuingia ndani. Kwa muda wote huo, Lina alikuwa kimya kabisa, hakusema kitu chochote. Phillip akamshika mkono na wote kwa pamoja wakaingia chumbani, hawakutoka tena mpaka saa tano baadaye, wote wawili wakiwa wamevalia vizuri.

Walitoka nje ya nyumba yao na kuingia tena ndani ya gari, safari kuelekea hotelini Lamada ikaanza. Njia nzima Phillip alijaribu kuongea na Lina akimsihi na kumbembeleza kuondokana na wasiwasi aliokuwa nao.
“Lina tunaingia hotelini sasa, tafadhali hebu jifute machozi, nisingependa jambo hili ligundulike na watu wengi.”
“Siwezi mume wangu, moyo unaniuma sana. Phillip unanifanya nianze kujilaumu ni kwa nini nilikubali kuolewa na wewe, hivi kweli umedhamiria?” aliuliza Lina.

“Fanya kwa ajili yangu Lina nakuahidi kukupenda mpaka mwisho. Nitakaa hapa hapa nilipokushusha, ukitoka utanikuta nakusubiri, sawa mke wangu?” alisema Phillip huku akimbusu mfululizo.
Taratibu Lina akashuka kwenye gari na kujiweka sawa kisha kumwangalia Phillip kwa macho ya huruma. Bila kusema kitu chochote akaanza kutembea kuondoka eneo hilo.

Je, nini kitaendelea? Lina ndiye huyo ameingia hotelini Lamada kwenda kukutana na Daniel. Nini kitatokea huko? Ditrov naye fahamu zake zimemrejea lakini bado yu katika hali mbaya. Nini hatima yake?
 
 
 
 
 
 

MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.70

JAMANI EPISODE ZIMEJICHANGANYA SANA, POLENI

NDANI ya chumba wanaongea mengi juu ya maisha na jinsi walivyokuwa wamepotezana kwa muda mrefu. Daniel anasisitiza kwamba bado anampenda Lina pamoja na mambo yote yaliyotokea maishani mwao. Muda wote huo Lina alikuwa akibubujikwa na machozi, mara kadhaa taswira ya mume wake Phillip ilimjia kichwani mwake na sauti ikamsisitiza juu ya kuhakikisha anafanya tendo la ndoa ili hatimaye apate ujauzito.

Ni mambo hayo ndiyo yaliyomfanya Lina azidi kulia, kitu ambacho kilimshangaza sana Daniel. Alitumia muda mwingi kumbembeleza Lina ili anyamaze lakini ilionekana kuwa ngumu.

Kwa muda wa saa zima walikuwa chumbani, kazi ikiwa moja tu ya kumbembeleza Lina ili anyamaze ndiyo waendelee na mambo mengine. Hata alipopewa chakula alikataa bila kusema sababu, hatimaye Daniel uvumilivu nao unamshinda. Uchu wa kufanya tendo la ndoa na Lina unamkamata, anaona huo ndiyo muda muafaka kwake.

Taratibu bila kusema kitu chochote baada ya kuwa ameshambembeleza kwa muda mrefu, anasogea karibu na Lina kisha anamnyanyua na kumlaza kitandani huku akimpiga mabusu mfululizo.
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…

HALI ya Ditrov ilikuwa ikiendelea vyema, akipata kila aina ya msaada kutoka kwa Oleg Malenko. Jeraha lake lilishapata nafuu kubwa na mwili wake ulionekana kurejea katika hali yake ya kawaida. Pamoja na yote hayo bado hakuwa tayari kueleza ukweli kwamba alitokea wapi na ni kitu gani kilisababisha akatoswa baharini.

“Nashukuru Mungu unaendelea vizuri, nadhani sasa tunaweza kuongea kidogo kuhusu wewe,” Oleg Malenko alisema.
“Sipo tayari kueleza chochote, kikubwa ninachokuomba ndugu yangu unitunzie siri ya mimi kuwepo hapa katika nyumba yako. Muda si mrefu nitaondoka ili kukuepushia matatizo.”

“Matatizo yapi?”
“Ni historia ndefu sana kuhusu mkasa ulionipata. Ninachokushukuru sana ni kuokoa maisha yangu.”
“Hakuna shida,” alisema Oleg lakini tayari kichwani mwake alishaweka viulizo ni kwa nini mtu aliyekuwa ndani ya nyumba yake hakutaka kueleza ukweli wa nini kilichompata na zaidi ya yote alitaka jambo hilo lifanywe siri.

Hivyo ndivyo maisha yalivyokwenda, Ditrov akawa ni mtu wa ndani muda wote akihitaji kubaki peke yake, jambo ambalo lilizidi kuitia shaka familia ya Oleg Malenko. Wiki ya kwanza ikakatika, hali yake ikazidi kuwa imara na wiki ya pili ilipofika katikati akaamua kuvunja ukimya. Alimwita Oleg Malenko ili waongee.

“Hivi sasa wewe ni kama ndugu yangu kwani umeokoa maisha yangu. Nakushukuru sana lakini naomba msaada mmoja tu kutoka kwako.”
“Sema tu ndugu yangu nitakusaidia.”
“Nahitaji fedha kidogo kwa ajili ya nauli.”

“Kwenda wapi?”
“Nataka kurejea nyumbani,” alidanganya.
“Hakuna shida, nipo tayari kukusaidia. Sijui unahitaji lini?”
“Ikiwezekana kesho asubuhi ili niondoke hapa,” alisema Ditrov akionesha shaka machoni mwake.

***
“Nakupenda mpenzi wangu, ni muda mrefu nimengoja jambo hili litokee hatimaye leo hii limewadia. Nieleze ni kitu gani kimesababisha unitafute Lina, huu kwangu ni muujiza,” alisema Daniel akizidi kumwagia Lina mabusu mfululizo.
“Mh!” Aliguna huku kwikwi ya kulia ikizidi kumkaba.
“Lina,” Daniel aliita.

“Tafadhali toa ushirikiano, kwa nini unalia?”
“Hakuna kitu, nipo sawa.”
“Si kweli! Kama upo sawa hayo machozi ni ya nini sasa?”
“Una…ju…a nini?”

Daniel akatulia kidogo ili asikilize ni kitu gani Lina alitaka kumweleza.
“Nimefurahi kukutana na wewe Daniel, ni muda mrefu umepita eeh?” Aliuliza Lina akimpigapiga Daniel mgongoni. Mawazo na akili zake zote hazikuwa ndani ya chumba hicho, mara kadhaa taswira ya mumewe Phillip ilimjia kichwani mwake na hiyo ndiyo iliyomfanya abubujikwe na machozi muda wote.

***
Nje ya hoteli, Phillip bado aliendelea kubaki hapo akimsubiri mkewe Lina, mapigo yake ya moyo yalikwenda mbio hakuelewa ni kitu gani kingekuwa kimetokea ndani ya chumba kwani tangu mwanzo Lina alishaonesha dalili kwamba hakupenda kufanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine isipokuwa yeye tu.

“Atakuwa amefanikiwa, ni muda mrefu tangu aingie huko,” aliwaza Phillip.
Akaendelea kujiambia mwenyewe kwamba kusingekuwa na tatizo lolote, akatupa macho yake kwenye saa yake ya mkononi na kugundua kuwa tayari ilishatimu saa tatu na nusu za usiku. Mpaka wakati huo hakuwa na taarifa yoyote ya Lina.

“Akichelewa zaidi nitampigia simu,” aliwaza Phillip akitoka ndani ya gari na kutembeatembea kulizunguka gari lake. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda kasi kwani hakufikiria kwamba Lina angechukua muda mrefu kiasi kile.

***
Ndani ya chumba, Daniel aliendelea kuongea mambo mengi juu ya maisha yake baada ya kuachana na Lina. Aliweka wazi zaidi na kumweleza kwamba tayari alishaoa na alikuwa na mtoto mmoja lakini akajiapiza kutoka ndani ya moyo wake kwamba alilazimika kuoa kwani umri ulikuwa ukienda. Akamwambia hakuwahi kumpenda mwanamke mwingine kama ilivyotokea kwa Lina.
“Daniel unasema kweli?”

“Huo ndiyo ukweli wangu, hutaniamini lakini…”
“Usiseme hivyo bwana.”
“Lina ukweli nilikupenda na nitaendelea kukupenda maisha yangu yote, hapa nilipo nahisi nipo ndotoni pengine nitaaamka muda si mrefu.”

“Daniel uko na mimi wala si ndoto.”
“Umefikiria nini mpaka kuamua kunitafuta Lina?”
“Maisha yamesababisha hivyo, wahenga walisema milima haikutani lakini binadamu tunakutana, ndiyo kama hivi.”
“Ahsante kwa kunikumbuka na kuniingiza tena ndani ya moyo wako.”

Ukimya wa ajabu ukatokea kati yao, ghafla Daniel akaanza kumpapasa Lina sehemu mbalimbali za mwili wake huku akimpa maneno matamu yaliyoambatana na mabusu.
“Leo sitarudi nyumbani, nitalala hapa na wewe. Nataka nikuoneshe ni jinsi gani ninavyokupenda Lina. Nataka ujue kwamba mimi ndiye Daniel wa ukweli, niambie unataka nifanye nini?” alisema Daniel huku akizidi kumpapasa mwilini.

Tayari hamu ya mapenzi ilishawaingia, kila mmoja alikuwa akihemka, si Daniel wala Lina wote walikuwa taabani.
“I lov..e yo…u ba…by...”(Nakupenda mpenzi) ilikuwa ni sauti nzito ya Daniel ambayo ilipenya na kwenda moja kwa moja kwenye sikio la Lina aliyekuwa amelala kimya bila kusema kitu chochote. Bila kupata kibali chochote kutoka kwa Lina, Daniel akaanza kumvua viatu na kuvitupa chini, taratibu akapanda juu na kuanza kumfungua vishikizo vya blauzi aliyokuwa amevaa.

“Leo ndiyo leo nataka kuweka historia ya mapenzi kwako,” alisema Daniel. Tayari macho yake yalishabadilika rangi na kuwa mekundu.
“Daniel!” Lina aliita.
“Yes baby.”
“Twende taratibu, usiwe na haraka.”

“Nashindwa kuvumilia, nilikusubiri kwa muda mrefu.”
“Hapana,” alisema Lina akijaribu kuitoa mikono ya Daniel kifuani kwake.
“Basi naomba nitoe tu hii halafu...” alisema Daniel tayari alishamaliza vishikizo vyote vya blauzi.

“Oh! My God!”(Oh! Mungu wangu!) alisema kimoyomoyo, hakuwa tayari kuamini alichokishuhudia juu ya kifua cha Lina. Chuchu ndogo zilizosimama vizuri zilizidi kumpagawisha Daniel, akawa anapumua kwa kasi kubwa.
Je, nini kitaendelea?
 
 
 
 
 
 

MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.72

DITROV amepata nafuu na sasa ameomba msaada kutoka kwa Oleg Malenko ili aondoke sehemu hiyo mara moja na bila kujiuliza kwa kina Oleg anaahidi kumpa msaada huo ingawa hajui anataka kuelekea wapi.

Upande wa pili, Lina na Daniel tayari wapo juu ya kitanda. Daniel anaonekana kuwa na hali mbaya zaidi kwani ana hamu kubwa ya kufanya tendo la ndoa na Lina, mwanamke aliyempenda kwa moyo wake wote lakini akashindwa kulifaidi penzi lake baada ya kumkataa. Nafasi ile ya kuwa wawili tu na Lina chumbani aliiona kama bahati ya mtende kuota jangwani, akazidi kuchanganyikiwa kwani alikuwa akilihitaji mno penzi lake.

Baada ya mazungumzo marefu, akitumia muda mwingi kumbembeleza Lina aliyekuwa akilia, hatimaye Daniel anafanikiwa kufungua vishikizo vya blauzi ya Lina na kuziona chuchu ndogo zikiwa zimesimama kifuani. Kitendo kile kilifanya hamu yake ya kufanya mapenzi izidi kupamba moto, bila kusema kitu akaruka kutoka kitandani na kuanza kuchojoa nguo moja baada ya nyingine huku mhemko ndani yake ukizidi kuongezeka kadiri saa zilivyokuwa zinazidi kusonga mbele.

Bila kusema kitu chochote, anarejea tena kitandani na kulala huku mikono yake ikizunguka juu ya mwili wa Lina ambaye alitulia kimya kitandani, wakiwa hapo mabusu ya mahaba yanamiminika mfululizo juu ya mwili wa Lina.

Nje ya hoteli, uvumilivu umeanza kumshinda Phillip kwani ameshasubiri kwa muda mrefu bila kumwona mkewe akitoka, akaanza kuhisi huenda kuna kitu kibaya kimempata. Anajiambia moyoni kuwa aendelee kusubiri kidogo na kama hatatokea basi ataingia ndani ya hoteli kumtafuta.
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…

“Mbona anazidi kuchelewa? Au kapatwa na tatizo kubwa? Nahisi hayupo sawa, kwa nini harejei?” Phillip alijiuliza maswali mengi ambayo hayakuwa na majibu. Alikuwa akizungukazunguka pale nje kama mtu aliyepoteza kitu. Mara kwa mara alikuwa akiingia ndani ya gari na kushuka, akiwa haelewi nini anachokitafuta. Akili yake ilikuwa haitulii kabisa.

Wivu na hofu vilikuwa vikimshambulia kwa wakati mmoja. Kuna wakati alihisi huenda Lina amenogewa na penzi alilopewa na mwanaume aliyeenda kukutana naye kiasi cha kujisahau. Akili nyingine ilimtuma kuwa huenda ameamua kuondoka na huyo mwanaume ingawa alishindwa kuelewa wamepitia wapi kwani muda wote yeye alikuwa pale nje.
Hofu nayo haikumuacha, alihisi huenda amekumbana na kitu kibaya ambacho kimemdhuru na ndiyo maana hatoki mapema kama walivyokubaliana.

Mambo yote yalikuwa yakipita akilini mwake kama mkanda wa sinema. Japokuwa ni yeye ndiye aliyetoa wazo lile, kwa upande mwingine alijikuta akijutia uamuzi wake lakini kwa kuwa alikuwa na shida ya mtoto, ilibidi avumilie.

Phillip aliendelea kujizungusha huku na kule huku akiangalia saa yake karibu kila baada ya dakika moja. Aliona muda unaenda taratibu sana, akatamani angekuwa na nguvu za ziada za kuweza kuona kilichokuwa kinaendelea kwa Lina.
“Zikipita dakika kumi kama bado hajatoka, itabidi niende mapokezi kuuliza, ikishindikana nitaenda mpaka kwenye chumba alichoingia,” alisema Phillip huku kichwa chake kikichemka kwa mawazo.

Muda ulizidi kuyoyoma bila Lina kutoka, hali iliyozidi kumuweka Phillip kwenye wakati mgumu. Aliendelea kuhesabu sekunde, dakika na saa hatimaye uvumilivu ukamshinda. Kijasho chembamba kilikuwa kikimtiririka, akafunga mlango wa gari na kuanza kupiga hatua za taratibu kuelekea mapokezi huku akiendelea kujiuliza maswali mengi ambayo yote yalikosa majibu.
***
Baada ya kupata nafuu kwa msaada mkubwa wa Oleg Malenko, Ditrov alijiandaa kuondoka huku mawazo mengi yakipita ndani ya kichwa chake. Mazingira yaliyomfanya akaokolewa na Oleg Malenko yalimfanya atambue kuwa Mungu yupo kwani alishakata tamaa ya kuendelea kuishi. Alikuwa akijiuliza mara kwa mara kwamba alimkosea nini bosi wake, Victor Federov mpaka kufikia hatua ya kumpiga risasi na kwenda kumtosa baharini, tena akiwa amefungwa na jiwe kubwa shingoni.

Kila alipokuwa anakumbuka jinsi alivyonusurika kufa, mwili wote ulikuwa ukimsisimka. Baada ya kuagana na mwenyeji wake pamoja na familia yake, Ditrov alianza safari ya kuondoka ndani ya nyumba ya Oleg Malenko, akiwa haelewi anaelekea wapi. Alitembea taratibu mpaka alipotoka nje, akageuka nyuma na kuwapungia mkono Oleg Malenko na familia yake kwa ishara ya kuwaaga.

Wakamsindikiza kwa macho mpaka alipopotea kwenye upeo wa macho yao. Alikuwa anatembea huku kichwa chake amekiinamisha chini akiwa hataki mtu yeyote amtambue. Alikuwa akikwepa macho ya watu kwani aliamini wengi wao walikuwa wanamfahamu.
“Mimi ni mwanaume bwana! Kama Mungu amenisimamia nimenusurika na mauti, hawezi kushindwa kuniongoza mahali pa kwenda wakati najiandaa kulipa kisasi.

Nitatafuta sehemu yoyote ambapo nitajihifadhi wakati nafikiria jinsi ya kurudi kulipa kisasi, lazima nimfunze adabu Victor Federov. Tena kazi itakuwa rahisi kwani anaamini nimeshakufa, hajui kuwa Mungu ambaye nilishaacha hata kumuabudu miaka mingi iliyopita amenipigania na naendelea kupumua,” alisema Ditrov wakati akizidi kuchanja mbuga kuelekea mahali asikokujua.

Kumbukumbu za kuhuzunisha ziliendelea kuzunguka ndani ya kichwa chake, akajikuta akishindwa kuyazuia machozi kumtoka, hasa alipokumbuka maisha aliyokuwa anaishi kabla ya kutokewa na balaa lile na kuponea chupuchupu kufa.
Taswira ya maisha aliyokuwa anaishi, japokuwa yalikuwa yanategemea kufanya shughuli haramu mara chache, ilikuwa ikipita akilini mwake na kumfanya ashindwe kukubaliana na hali halisi.

Maisha mazuri aliyoishi, tena ya kifahari yalimfanya asiamini kuwa wakati ule alikuwa akitangatanga mahali asipopajua na kuishi kama mkimbizi. Maisha ya kujificha kama digidigi hakuyazoea lakini sasa ndiyo alitakiwa ayaishi wakati anajiandaa kulipa kisasi akikwepa kugundulika kabla hajatimiza alichokipanga.

Alitembea kwa muda mrefu mpaka akaanza kuhisi uchovu. Ukizingatia kuwa afya yake ilikuwa bado haijatengamaa, nguvu zilimwisha kirahisi. Akaamua kutafuta mahali pa kupumzika huku akiendelea kujiuliza kichwani mwake ni wapi angekwenda na kupata fedha za kumsaidia kukimu shida zake mbele ya safari. Alipiga moyo konde na kuamini kuwa hakuna linaloshindikana chini ya jua.

“Najua nitapata shida sana lakini haya yote yatapita. Nitaanzia chini kabisa lakini naamini ipo siku nitapata fedha ambazo zitanifanya nirudi tena kwenye daraja la maisha ya kifahari kama ilivyokuwa mwanzo, nikila na kunywa hadi kusaza,” alijisemea Ditrov wakati akiinuka na kuendelea na safari yake baada ya kupumzika kwa muda.
Kichwani mwake hakuwa na ramani ya mahali anapokwenda lakini aliamini atafika tu mahali palipotulia ambapo ndipo yatakapokuwa makazi yake ya muda wakati akijiandaa kulipa kisasi.

***
“Lina,” Daniel aliita.
“Abee,” aliitikia kwa sauti ya chini.
“Kweli unanipenda?”
“Ndiyo!”

“Kama kweli unanipenda tafadhali niache niwe huru juu ya mwili wako. Naomba unipe nafasi ya mimi kufanya ninachotaka, usinishike mikono na kunizuia, niache nifurahie mapenzi yako,” alisema Daniel kwa sauti ya kubembeleza kuonesha kuwa hamu yake ilikuwa imefika juu kabisa.
Lina hakuwa mwepesi wa kukubali Daniel afanye kila alichokitaka kwenye mwili wake. Mara kwa mara alikuwa akiushika mkono wake na kumzuia kumpapasa maungoni mwake, jambo ambalo lilizidi kumpa Daniel wakati mgumu.

“Yaani shida ya mtoto ndiyo inifanye nifanye jambo nisilolitaka, roho inaniuma sana,” alijisemea kimoyomoyo Lina huku dhamira yake ikigoma kabisa kumruhusu Daniel afaidi penzi lake. Daniel hakukata tamaa, aliendelea kumbembeleza Lina kwa maneno matamu huku akitumia ujanja kuupapasa mwili wake.

Cha ajabu, kwa muda wote huo Lina alikuwa akibubujikwa na machozi kama yupo msibani, jambo lililomfanaya Daniel abaki njia panda. Alijiuliza kwa nini Lina analia kiasi kile wakati ni yeye ndiye aliyempigia simu na wakakubaliana kukutana pale.
“Lina mpenzi wangu, naomba nipe haki yangu tafadhali, nionee huruma mwenzio nateseka,” Daniel alisema kwa sauti iliyokuwa inatetemeka baada ya kuzidiwa na haja ya mwili wake kulifurahia penzi la Lina.

Alipoona hamjibu kitu bali anaendelea kulia, aliinuka kidogo na kujaribu kuivua sketi fupi aliyokuwa ameivaa Lina. Lina alishtuka na kuanza kumzuia, wakawa wanavutana pale kitandani.
“Usitumie nguvu Daniel, niache nitavua mwenyewe,” alijitetea Lina lakini Daniel hakutaka kumuelewa. Akaikamata vizuri na kuivua kwa nguvu, Lina akabakia na nguo ya ndani pekee.

“Duu! Leo sijui itakuwaje, si mchezo,” Daniel alijisemea kimoyomoyo wakati akimuangalia Lina aliyekuwa amebakiwa na ‘kufuli’ nyeupe iliyozidi kupandisha mashetani ya Daniel.
“Nipe nafasi mpenzi wangu, mwenyewe utafurahi,” alisema Daniel huku akipeleka mikono yake kujaribu kulitoa kufuli la Lina.
“Subiri Daniel, nitakupa nafasi lakini usiwe na papara, subiri kidogo,” alijitetea Lina huku akibana miguu yake na kumzuia Daniel.

“Hakuna shida, nitasubiri hata ukisema mpaka usiku wa manane. Nakuhakikishia kuwa shughuli nitakayokupa leo, mwenyewe utanitafuta tena.”

Lina alifumba macho na kumruhusu Daniel apitishe mikono yake kiunoni, akawa anampapasa kimahaba huku akimpiga mabusu mwili mzima. Alipoona Lina amejisahau, alishika pindo za kufuli lake na kuanza kuliteremsha kwa kushtukiza. Lina aliwahi kumzuia, lakini likiwa tayari limeshashuka mpaka karibu na magoti. Daniel aliendelea kusumbuana naye, hatimaye akafanikiwa na wote wakabaki kama walivyoletwa duniani.
Je, nini kitaendelea?
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.73

Uwiii!” Daniel alisema kimoyomoyo, macho yake hayakuwa tayari kuamini kile alichokuwa akikishuhudia mbele ya macho yake, uzuri wa Lina haukuwa na maelezo, akili ya Daniel ikazidi kuchanganyika zaidi aliposhusha macho yake na kuangalia mapaja ya Lina.
“Mungu wangu! Ninaota au?” alijiuliza.

“Huoti Daniel unachokiona ndicho.”
“Lina!”
“Yes.”
“Hakika wewe ni mwanamke mrembo,” aliongea Daniel na tayari mikono yake ilikuwa ikipita huku na kule juu ya mapaja ya Lina huku akihemuka, akimeza mate mfululizo.
Akamnyanyua Lina na kumlaza kifudifudi mikono yake yote miwili ikiendelea kucheza juu ya mwili wake laini.

“Hakika wewe ni mwanamke mtamu.”
“Whaaat?” (Nini?)
“Naaminisha wewe ni mzuri sana.”
“Kama wewe Danny.”

“Sidhani,” alisema akishusha mdomo wake na kuanza kumng’ata ng’ata Lina jambo hilo likazidi kuwasha moto zaidi kwa Lina.
“Mh! Mh! Baby, taratibu usiwe na shaka leo ni siku yako.”
“Nahisi kuchelewa Lina tafadhali nipe.”
“Ah! tucheze kwanza kidogo muda ukifika nitakupa.”
“Shiiii! Mh! Uwiii! Yalaaa!” alilalama Daniel.

Kwa muda wa saa mbili mfululizo waliendelea kucheza juu ya kitanda huku kila mmoja akionekana kukolezwa na mwenzake, mara kadhaa Daniel alimgeuza Lina akijaribu kumlaza chali lakini Lina alikataa akimweleza wazi kwamba muda muafaka ulikuwa bado haujafika.
Kwa kuwaangalia wote wawili walikuwa hoi kwa mapenzi kila mmoja akiguna na kuongea maneno yake huku wakiendelea kushikana hapa na pale.

“Lina inatosha tafadhali ni…pe,” aliongea Daniel lakini hakumaliza sentensi yake tayari mdomo wake ukafunikwa na kiganja cha Lina.
“Shiii! Hebu jikaze bwa....” aliongea Lina lakini naye alionekana kuwa hoi kupita kawaida.
Kwa sauti ya upole huku akionyesha tabasamu akamwomba Daniel naye alale ili aweze kumfanyia alichotaka kufanya, bila hiyana taratibu mwanaume akashuka kitandani na kulala akimpa Lina nafasi ya kufanya alichokusudia
“Mh!Mh!Mhhhhh” ilikuwa ni miguno kutoka kwa Daniel.

“Vipi?” Lina aliuliza.
“Imetosha, naomba unipe ki…do..go,” aliongea.
“Niachie nafasi kidogo nikupe raha Daniel ambayo nina hakika hutaisahau maishani mwako.”
Ulimi wa Lina ulikuwa ukipita ndani ya sikio la Daniel.

Ni tukio hilo ndilo lililofamfanya Daniel akajikunja kitandani kama jogoo, raha aliyokuwa ameisikia ilikuwa haielezeki hata kidogo, ni kweli alishakutana na wanawake wengi maishani mwake lakini kwa Lina ilionekana kuwa kiboko.
“Lina niko tayari kuachana na mke wangu nikuoe wewe, unasemaje?”
“Danny! Hebu acha utani unamaanisha unachokisema?”

“Niko tayari hakika sitanii.”
“Unaweza kumwacha sasa hivi tena kwa kumpigia simu?”
“Haijalishi.”
Daniel alikuwa amechanganyikiwa kabisa, akili zake ziligeuka na alikuwa tayari kufanya kila kitu ambacho Lina angemwambia ili mradi tu aendelee kupata raha aliyokuwa anaipata siku hiyo, kichwani mwake akisahau kabisa kwamba alikuwa ni baba wa watoto wawili waliomtegemea kwa kila kitu duniani.

***
Akiwa ndani ya gari lake usingizini, ubaridi mkali wa kiyoyozi ndiyo uliomshitua na kumfanya afungue macho na kuangaza huku na kule ndani ya gari na kugundua kwamba alikuwa peke yake bado, haraka akanyoosha mkono wake na kuwasha redio ndani ya gari na sauti ikasikika ikitangaza kwamba muda huo ndiyo ilikuwa ikitimu saa sita kamili usiku.

“Mungu wangu mpaka saa hizi? Amepatwa na kitu gani huyu mwanamke?”
aliongea Phillip akishuka ndani ya gari.
Akiwa hapo akaangaza huku na kule bila kuona kitu chochote, taratibu akazima gari na kuchomoa funguo kisha kufunga mlango.

“Lina amenisaliti hawezi kukaa ndani ya hoteli kwa muda mrefu kiasi hicho mkataba wangu mimi na yeye ni kuhakikisha anakutana na mwanaume huyo na kufanya naye tendo la ndoa baada ya hapo basi atoke na tuondoke, kwa nini amechukua muda mrefu kiasi hiki? Inawezekana amepewa mambo mazuri mpaka amenisahau?” aliongea Phillip akionyesha hasira nyingi.

Hofu ilishaugubika moyo wake, akiwa haelewi ni kitu gani angekwenda kushuhudia huko, Phillip alianza kutembea kichwani mwake akijiuliza maswali mengi na mara kadhaa akianza kujilaumu kwa kitendo chake cha kumshawishi mkewe kwenda kukutana na mwanaume mwingine ili tu wafanye tendo la ndoa na kupata ujauzito ambao angeulea na kuutunza mpaka mtoto atakapozaliwa. Moyo wake ukauma.
“Hivi kweli anaweza kuwa ameondoka na kuniacha mimi nikiwa hapa? Lina, sidhani lakini akili za mwanamke anazijua mwenyewe pengine ameamua kufanya kweli ili kunikomoa kwani hakuwa tayari kufanya jambo hilo, mimi ndiye nimemlazimisha.”

Lawama nyingi akazielekeza kwake na kujiona ni mwanaume mjinga kiasi gani kwa kitendo cha kuruhusu mkewe kwenda kufanya ngono na mwanaume mwingine, hakika alifahamu wazi kwamba kama dunia ingefahamu jambo hilo basi ingekuwa ni aibu mpaka siku anaingia kaburini.

Huku akiwa na wasiwasi mwingi moyoni mwake taratibu akaanza kutembea, lengo lake likiwa kuelekea eneo la mapokezi ambako angeingia na kuuliza.
“Najua nitakutana na maswali mengi sana hasa ukizingatia kwamba ni usiku
mkubwa lakini nitajibu moja baada ya jingine nikijifanya mimi ni dereva wake niliyekuwa nikimsubiri hapo nje,” aliendelea kuwaza akitembea taratibu.

 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU....EP.74

Kwa fedha kidogo alizokuwa nazo, akiwa haelewi kabisa nini ingekuwa hatima ya safari yake hiyo, Ditrov alijipa moyo na kujiapiza kwamba ni lazima angefanya kila kinachowezekana kusukuma maisha yake kwenda mbele lakini zaidi ya yote akili yake ilifikiria juu ya kulipa kisasi kwa Victor Fedorov. Alijiapiza kuwa hata kama ingechukua miaka mingapi ni lazima jambo hilo litokee, hakufahamu lingetokea vipi lakini aliamini hivyo.

Hasira ya maisha mapya ilikuwa imemkaa Ditrov kupita maelezo, alitaka kurejea kwenye hali yake ya awali na kuwa Ditrov yuleyule wa zamani, bila mtu yeyote kufahamu kwamba hakufa. Alipanga kujichimbia mahali na kuishi kwa siri kubwa akitafuta mbinu za kulipa kisasi kwa mtu aliyeamini kwamba alikuwa ni adui yake.

“Yupo mtu mmoja tu nchini Urusi anayeweza kufanya kazi ninayotaka afanye. Nikitulia kidogo nitamfuta,” aliwaza siku moja akiwa ndani ya chumba chake kidogo kilichokuwa nje kabisa ya mji.

Kwa muda wa wiki mbili mfululizo aliendelea kutafakari juu ya nani angeweza kufanya zoezi ambalo alilihitaji, hatimaye kumbukumbu zake zikamrejesha moja kwa moja kwa kijana mmoja aliyeishi nchini Urusi ambaye aliamini kabisa kwamba angeweza kufanya kile alichokitaka.

Baada ya kuchunguza kwa muda mrefu, alimkumbuka kijana mmoja katili ambaye aliamini kabisa angeweza kufanya kazi ngumu iliyokuwa mbele yake. Mara kadhaa alikumbuka matukio ya kutisha ambayo aliwahi kufanya kipindi cha nyuma.
“Nitampa kazi hii lakini sitaki afanye mauaji yoyote, kama ni kisasi nitalipa mimi mwenyewe,” aliwaza Ditrov.

Kazi yake ikabaki kuwa moja tu, kutafuta simu ambayo angeitumia kuwasiliana na kijana huyo ili ampe kazi hiyo mara moja.
“Kesho nitahakikisha napata simu kwa ajili ya mawasiliano,” alisema Ditrov akijaribu kuzungusha akili yake huku na kule. Akiwa hapo akaingiza mkono katika moja ya mfuko wake wa suruali akijaribu kukagua kama angepata akiba yoyote ambayo ingeweza kumsaidia kupiga simu.

“Yes, hii itatosha kwa kazi hiyo,” alisema huku akitoka ndani. Nyumba aliyokuwa anaishi ilikuwa ndogo na iliyochakaa kupita kawaida. Hapakuwa na jirani yeyote maeneo hayo na ilivyoonekana, nyumba ile ilikuwa imetelekezwa kwa muda mrefu. Hapo ndipo Ditrov alipoweka makazi yake, akiishi peke yake.

Licha ya mvua kubwa iliyokuwa inanyesha, Ditrov aliamua kutoka ili kwenda kutafuta mahali ambapo angepata simu na kupiga nchini Urusi ili aweze kuongea na mtu ambaye aliamini angemsaidia shida yake. Taratibu akatoka na kuanza kutembea, kichwani mwake akiwaza mambo mengi huku akitupa lawama nyingi kwa Victor Fedorov kwamba bila yeye maisha yake yasingekuwa kama yalivyo. Alipofikiria hivyo, moyo wake ukazidi kumuuma.

“Mimi ni mwanaume, naamini nitashinda hata kama gharama yake itakuwa kubwa kiasi gani, lazima nishinde tu,” alisema huku akitokomea kwenda mbele.
Kwa muda wa saa nzima Ditrov alitembea bila kukutana na mtu yeyote zaidi ya magari machache yaliyoonekana kupita eneo hilo kwa kasi huku baadhi ya watu waliokuwa ndani yake wakimshangaa.

“Mh! Kwa nini watu wananishangaa kiasi hiki, inawezekana eneo hili ni hatari?” alijiuliza huku akisonga mbele. Hatimaye nusu saa baadaye alifanikiwa kufika katika mji mdogo ambao hata hakuufahamu jina lake. Akaona maduka kadhaa, huku akiwa na wasiwasi mkubwa akatembea na kusogea katika moja ya maduka yaliyokuwepo eneo hilo. Bado watu walionekana kumshangaa kwani alionekana kuwa mgeni kwa kila kitu.

“Habari yako?” alimsabahi muuza duka.
“Salama nikusaidie nini?”
“Naweza kupata wapi huduma ya simu hapa?”
“Hata hapa unaweza kuipata,” alijibu mzee aliyekuwepo dukani hapo na bila kusema kitu chochote Ditrov akainamisha kichwa chini kama mtu aliyekuwa anakumbuka kitu fulani, alipoinuka aliomba kalamu na karatasi kisha akaanza kuandika namba kwenye kipande cha karatasi.

”Hii hapa.”
Mzee mwenye duka akanyoosha mkono na kuipokea karatasi hiyo kisha bila kuchelewa akabonyeza namba alizopewa. Haikupita hata sekunde mbili, simu ikasikika ikiita upande wa pili.
“Ngrii!Ngrii!Ngrii!” Haraka akakabidhi mkono wa simu kwa mteja wake.
“Mimi ni Ditrov, sikufa kama watu wengi nchini Urusi wanavyofahamu, nilinusurika na nina kazi moja nzito ambayo nitataka uifanye kwa uaminifu mkubwa. Nakupa muda wa siku tatu tu iwe imekamilika, umenielewa?” Aliongea Ditrov kwa ukali, kitendo kilichofanya watu wote waliokuwepo eneo hilo kupigwa na butwaa.

“Mungu wangu kumbe hukufa? Nini kilitokea mpaka ukawa hai? Dunia nzima inafahamu kwamba wewe na washirika wako wote mlishakufa?” Sauti ya upande wa pili ilisikika ikiuliza.
“Ni historia ndefu kidogo lakini kwa ufupi nipo hai.”
“Nisikilize vizuri, tena kwa makini usije ukafanya kosa kabisa.”
“Nipo tayari.”

“Nahitaji kupata fedha ndani ya siku tatu, hakikisha unafanikiwa vinginevyo hata wewe maisha yako yatakuwa hatarini,” alisema Ditrov kwa msisitizo.
“Bosi nitazipata wapi? Tafadhali nipe maelekezo ya kufanikisha zoezi hilo.”
“Wewe ni Mafia nz umeshafanya michezo mingi hatari, hilo kwako halitakushinda. Kumbuka nimekuwa bosi wako kwa muda mrefu hivyo nafahamu wazi siri zote na naamini unajua nini cha kufanya.”

“Mh!”
“Kumbuka nahitaji fedha hizo ndani ya siku tatu, nitakupigia simu baada ya siku mbili kujua umefikia wapi, sawa?” alisema Ditrov na alipomaliza alimkabidhi mkono wa simu muuza duka, akatajiwa gharama ya huduma ile na kulipa.

Je, ni nani huyo? Ataweza kufanya kazi aliyoagizwa na bosi wake na kupata fedha zinazohitajika?
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.75

“Nitahakikisha napata ninachokitaka,” aliongea Ditrov akitokomea kuingia mashambani.
Ditrov alikuwa amedhamiria na alitaka kutimiza alichokitamka kutoka mdomoni mwake pamoja na kwamba alifahamu wazi kwamba pengine zoezi hilo lingeweza kutoa hata uhai wa mtu lakini kwake jambo hilo lilionekana kuwa dogo.

Taratibu huku akionekana mwenye wasiwasi mwingi alianza kutembea na kutokomea kuingia zaidi mashambani ambako ndiko hasa kulikuwa na makazi yake, kichwani mwake akimfikiria Victor Fedorov na unyama aliomfanyia, hakika aliapa kumchukia mtu huyo maisha yake yote na aliuahidi moyo wake kufanya kila kilichowezekana mpaka afanikiwe kulipa kisasi hata kama ingechukua miaka mingapi lakini aliamini jambo hilo lingetokea.

Kichwani mwake alidhamiria kabisa kulipa kisasi, lakini bila fedha? Jambo hilo lisingewezakana, alitaka kuwa na fedha hata kama kidogo tu ambazo zingempatia gari, simu na hata wafuasi wachache ambao angewatumia kumwinda mbaya wake huyo kila sehemu mpaka mwisho na hatimaye kumpata.

“Nikifanikiwa nitatoka huku mashambani na kutafuta makazi mazuri kisha kuanza mchakato wa nini cha kufanya,” aliwaza.
Siku ya kwanza ikapita akiwa bado yuko mashambani na chakula chake kikubwa kikawa ni matunda tu na maji kidogo yaliyopatikana eneo hilo.

Hali yake iliendelea kutengemaa kadiri siku zilivyokwenda mbele, mara kadhaa akiikumbuka familia ya Oleg Malenko na kuishukuru kwa msaada wote iliyompatia.
Akauahidi moyo wake siku moja kurudi kulipa fadhila kwa mema aliyotendewa na familia hiyo.

“Ipo siku nitarudi naomba niwakute hai, najua watanidadisi sana lakini nitarudi na kuwapa shukrani zangu, wameokoa maisha yangu wale, sijui isingekuwa Oleg ingekuwaje kwani nilishakata tamaa nikiamini kwamba sasa ninakufa maji na maiti yangu kuliwa na samaki wakubwa baharini, hivyo hakuna mtu ambaye angefahamu nini kilitokea katika maisha yangu,” aliwaza.

Siku ya pili asubuhi Ditrov alitoka tena kuelekea mji mdogo kwa lengo moja tu la kupiga simu kwa mtu aliyekuwa amempa kazi, alitaka kufahamu aliendeleaje na kumkumbusha kwamba ilikuwa imebaki siku moja tu mbele ili kukamilisha mpango mzima na kumtaka asifanye mchezo na suala hilo vinginevyo angekiona cha moto.

Muda wote akitembea hakudiriki hata mara moja kuinua uso wake na kama alifanya hivyo ni mara moja tu na kuendelea na safari yake, hatimaye akafika kwenye mji mdogo sehemu ileile aliyowahi kupiga simu kwa mara ya kwanza na kutoa namba kisha kuomba msaada wa kupigiwa simu.

Sekunde tatu tu baadaye alikuwa katika simu akiongea na mtu upande wa pili huku akionyesha msisitizo na kwa sababu aliongea kwa lugha ya Kirusi hakuwepo mtu eneo hilo aliyeweza kuelewa ni kitu gani aliongea, wengi walimtazama kwa macho na kugundua kwamba alikuwa na tatizo fulani kwani macho yake yalionekana mekundu muda wote alipokuwa akiongea na simu.
“Sikia kwa makini nitakuwepo tena hapa muda kama huu kukupigia ili nikupe maelezo jinsi ya kunipata mara utakapofanikiwa kuchukua huo mzigo, sawa?” aliongea na kuuliza.

“Sitaki uue lakini kama itatokea nitakupa ruhusa ya kujeruhi tu na si vinginevyo, nadhani unanielewa vyema sina mchezo na kazi yangu hasa pale ninapotaka kitu ni lazima nikipate…”aliongea Ditrov huku akitetemeka, alionekana kama mtu aliyekuwa na homa kali.

Haraka akarudisha mkono wa simu huku akiuliza kiasi cha fedha anachodaiwa, bila kuchelewa akaingiza mkono mfukoni na kutoa kiasi hicho akalipa na taratibu akaanza kuondoka eneo hilo.
“Mh!” Mtu aliyempa huduma ya simu dukani aliguna, alionekana kumshangaa Ditrov kupita kawaida, kwanza kwa jinsi alivyokuwa na sura yake ilitisha.

Mwili wake mkubwa uliojazia vyema ni jambo lililosababisha kuingiwa na wasiwasi na kuamini kabisa kwamba mtu huyo hakuwa wa kawaida alikuwa na kitu alichokuwa akikitafuta.

“Inawezekana akawa ni jambazi huyu,” aliongea macho yake yakimwangalia Ditrov kwa makini.
“Nimesikia akisema kesho atarejea tena hapa dukani kwa ajili ya kupiga simu nitamwangalia tena na kama nitakuwa sijamwelewa vyema nitatoa taarifa polisi haraka ili waje kumkamata na kwenda kumhoji zaidi.”

***
Ndani ya chumba kila mtu alikuwa hoi kupita maelezo, kila mmoja akionekana kumhitaji mwenzake kwa hali na mali.
Mara kadhaa Daniel alipojaribu kupeleka mkono wake kwa lengo la kushika chuchu za Lina ili azitumbukize mdomoni mwake, jambo hilo lilionekana kuwa gumu kwani Lina alimsukuma pembeni akimtaka kusubiri kwanza.

“Lakini kuna tatizo gani mpenzi wangu mimi nakuhitaji sana.”
“Najua lakini mimi siko tayari bado kidogo.””Unataka nikufanyie nini ili unipe nafasi Lina?”
“Mh! Haya inatosha njoo basi.”

Daniel akasogea karibu zaidi na Lina alipotupa macho yake kumwangalia usoni aligundua jambo fulani, macho yake yalikuwa mekundu kupita maelezo na mwili wake ulionekana kutetemeka.”
“Daniel,” aliita.
“Yes, Lina.”

“Nipe kidogo halafu tupumzike, hali yangu kwa jinsi ilivyo hainiruhusu kuendelea zaidi ya hapa naweza kufa kama si kuzimia.”
“Na wewe una haraka kama nini sijui!”
“Nakuambia ukweli usiponipa naweza kufa muda si mrefu, nipe kidogo,” alibembeleza Daniel akionyesha umakini wa hali ya juu.
Maneno hayo yakapenya moja kwa moja masikioni mwa Lina na kumfanya amwonee huruma Daniel kupita kawaida, kwa sauti ya upole akamnong’oneza Daniel sikioni mwake na kumweleza kwamba sasa alikuwa amekubali kufanya kitu alichokitaka.

“Ahsante Lina, nataka uamini kitu kimoja tu.”
“Kipi hicho?” aliuliza Lina kwa sauti ya mahaba.
“Nakupenda sana mpaka sasa siamini kama umenikubali lakini nitaamini zaidi pale tu utakaporuhusu tukafanya tendo la ndoa.”
Lina alikuwa kimya kitandani bila kujibu chochote huku machozi yakimbubujika, taswira ya mumewe Phillip ilionekana mbele yake ikimhimiza juu ya kukubali kufanya tendo hilo na Daniel.

Ni hali hiyo ndiyo ilimfanya Daniel aamini kwamba sasa Lina alikuwa tayari kwa kila kitu bila kujiuliza mara mbili akamsogeza Lina karibu yake kisha kumlaza vizuri kitandani tayari kwa kazi moja tu kutimiza shughuli moja ya kumpa Lina raha ambayo kamwe hataisahau maishani mwake.
“Lala vizuri basi mpenzi wangu tuanze...” aliongea Daniel kwa sauti ya kukatikakatika.

Je, nini kitaendelea?kesho kama kawa ila mjitahidi kuingia blog kwani huko ndo kuna mwanews ya kufa mtu! usipimie as u know me well na blog iko bomba sana inavutia kuna cha ya live hapo hapo yaani kila kitu,USIKU MWEMA NAWAPENDA NYOOOOTEEEE!!!!mwaaaas
 
 
 
 
 
 

MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.76


SIKU ya pili asubuhi, Ditrov alitoka tena kuelekea kwenye ule mji mdogo kwa lengo moja tu la kupiga simu kwa mtu aliyekuwa amempa kazi. Alitaka kufahamu amefikia wapi na kumkumbusha kwamba ilikuwa imebaki siku moja tu mbele ili kukamilisha mpango mzima. Alipanga kurudia kumsisitiza na kumtaka asifanye mchezo na suala hilo vinginevyo angekiona cha moto.

Muda wote wakati akitembea, hakudiriki hata mara moja kuinua uso wake na kama alifanya hivyo, aliangalia sehemu ambayo haina watu na kuendelea na safari yake. Hatimaye akafika kwenye ule mji mdogo, sehemu ileile aliyopigia simu kwa mara ya kwanza, akatoa namba kisha kuomba msaada wa kupigiwa simu.

Sekunde tatu tu baadaye, tayari alikuwa katika simu akiongea na mtu upande wa pili huku akionesha msisitizo. Kwa sababu aliongea kwa lugha ya Kirusi, hakuwepo mtu eneo hilo aliyeweza kuelewa ni kitu gani alichokuwa anaongea. Wengi walimtazama kwa macho yaliyojaa viulizo na kuhisi kwamba alikuwa na matatizo makubwa kwani macho yake yalikuwa mekundu muda wote wakati akiongea na simu.

Upande wa pili, Lina na Daniel wapo ndani ya chumba, kila mmoja akiwa hoi kupita maelezo. Daniel ndiyo alikuwa na wakati mgumu zaidi kwani alionekana kumhitaji mwenzake kwa hali na mali. Mara kadhaa Daniel alipojaribu kupeleka mkono wake kwa lengo la kushika chuchu za Lina ili azitumbukize mdomoni mwake, Lina alikuwa akimsukumia pembeni na kumtaka asubiri kwanza.

Ghafla, Daniel anashuhudia machozi yakitiririka mashavuni mwa Lina, jambo ambalo analiona kama nafasi pekeee ya kutimiza alichokitaka, akamlaza vyema Lina kitandani tayari kwa kazi huku akijifanya kumbembeleza.
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…

KWAKE fedha hazikuwa na maana kuliko maisha ya watoto wake, Mariya na Merina ambao walikuwa kwenye hatari kubwa. Akiwa na hofu nyingi baada ya kumaliza kuweka kiasi cha fedha alichotakiwa kwenye begi, Victor Federov alilikamata sawasawa na kuanza kutembea kutoka nje ya chumba kuelekea sebuleni. Alipofika alipitiliza mpaka nje na kuingia ndani ya gari kisha kuliwasha, akiwa tayari kwa safari ya kuelekea Msitu wa Beloomut ambako alitakiwa kupeleka fedha hizo kama masharti ya kukabidhiwa watoto wake wakiwa hai.

“No way out, I have to do this for my daughters,” (Hakuna jinsi, ni lazima nifanye hivi kwa ajili ya wanangu) Aliongea Victor Fedorov akiwa ndani ya gari lake.

Lakini kabla hajaingia ndani yake alikumbuka kitu kimoja muhimu sana kwa wakati huo, bastola ambayo aliamini kabisa ingeweza kumsaidia kama tu angekutana na hatari yoyote katika safari yake, akalitupa begi la fedha ndani ya gari na yeye kutoka mbio kuelekea ndani ambako haikumchukua hata dakika tatu tayari akawa amesharejea na kuingia ndani ya gari tayari kwa safari ndefu.

Moyoni mwake alikuwa na machungu makubwa, muda mwingi machozi yalikuwa yakimbumbujika. Hakuona tena thamani ya tajiri wake.
“This is the worst day in my entire life” (Hii ni siku mbaya zaidi katika maisha yangu yote) alizidi kuwaza Fedorov.

“Piiii! Piiii! Piii!” Ilikuwa ni honi ya gari akipiga kuomba msaada wa kufunguliwa lango na mlinzi ili atoke. Kwa kasi ya ajabu akaliendesha gari mpaka langoni na kabla hajatoka alisimama na kuongea jambo fulani na mlinzi wake kisha akapandisha kioo na kuondoka.

Njia nzima aliliendesha gari akiwa ni mwingi wa mawazo kwanza maisha ya watoto wake na pili uhai wake yeye mwenyewe hakufahamu kabisa mtu aliyekwenda kukutana naye alikuwa vipi na ni kwanini alisisitiza fedha hizo zipelekwe katika msitu wa Beloomut ambao kwa hakika historia yake haikuwa njema.

“Acha niende cha muhimu ni kupata watoto wangu kama ni hizi fedha nitapata tu nyingine…”Aliwaza akizidi kukanyaga mafuta na gari kusonga mbele.

Mbele yake yalikuwa zilikuwa zimebaki saa saba tu ambazo zingefanya kutimia kwa saa ishirini na nne ambazo alikuwa amepewa na mtekaji wa watoto wake hivyo kuchelewa kwake kungesababisha maradha makubwa na hata kusababisha kupoteza maisha ya Merina na Mariya.

Akiwa katika mwendo wa kasi akatupa macho yake kwenye saa yake ya mkono na kugundua kwamba alitakiwa kufanya kila alichoweza kuhakikisha saa hizo zinamkuta akiwa tayari ndani ya msitu wa Beloomut ili kunusuru maisha ya watoto wake. Akaongeza mwendo wa kasi zaidi na kufanya kila aliyekutana naye barabarani kushangaa na pengine kudhani kwamba alikuwa ni mwizi wa gari aliyekuwa ameiba sehemu fulani.

Kwa Victor Federov mwendo ulionekana kuwa mrefu kila alipotupa macho yake kwenye saa yake aligundua muda ulikuwa ukizidi kusonga kama vile kulikuwa na mtu akihimiza kikimbiza saa mawazo mengi yakazidi kuufunika moyo wake akajikuta ameanza kukata tamaa juu ya kuwapata watoto wake wakiwa hai.

“Oh my God, do something for my daughters, they are the only kids I have” (Oh..Mungu wangu, tenda jambo flani kwa wanangu, ni watoto pekee nilionao) alijikuta akitamka maneno hayo kwa nguvu japo hajawahi kukanyaga kanisani wala msikitini katika historia ya maisha yake.

“Kama sitawakuta wakiwa hai hata mimi sitaona sababu ya kuendelea kuishi nitajipiga risasi ili nife.” Aliwaza machozi yakzidui kuuchakaza uso wake.

***
Hasira kali zilikuwa zimempanda kupita maelezo akisahau kabisa kwamba chanzo cha mambo yote hayo ilikuwa ni yeye kumruhusu mkewe kwenda kufanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine ili tu ashike ujauzito ambao angeulea na kuutunza mpaka mtoto atakapozaliwa.

Phillip alitoka ndani ya gari lake na kufunga mlango nyuma yake bila kujiuliza mara mbili kwamba kitendo alichotaka kwenda kufanya ndani ya hoteli hiyo kilikuwa cha aibu kuwa alitembea moja kwa moja na kuingia mapokezi.
“Habari yako dada?” Aliuliza kwa sauti ya juu.
“Salama tu nikusaidie?”

“Ah! Mh! Ah!”
“Kaka nakusikiliza nimekuuliza nikusaidie?”
“Ndio.”
“Sijui naweza kufahamu jambo fulani hapa?”

“Unaweza na hiyo ndiyo kazi yangu sema tu.”
“Nauliza…nauliza…”Aliongea akirudiarudia.
“Mh!” Msichana wa mapokezi aliguna yeye pia hakumwelewa Phillip alihitaji nini na kibaya zaidi tayari usiku ulikuwa umeshaingia.

“Taratibu bila kusema kitu chochote huku macho yake yote yakimwangalia kwa makini alinyanyua simu na kupiga namba kadhaa hapo kisha kusikiliza.
“Hallow…ndio…tafadhali naomba ulinzi hapa mapokezi… kuna mtu ameingia hapa hata simuelewi…sijui anataka nini…nimeongea naye simuelewi kabisa…inavyoonena kama vile amechanganyikiwa kidogo…tafadhali njoo mara moja… nina hofu kubwa sana…” Aliongea kwa sauti ya chini lakini bado Phillip aliendelea kusimama eneo hilo bila kusema kitu chochote alionekana kama mtu aliyepigwa na butwaa.

Hazikupita hata sekunde tatu tayari watu wawili walioonekana kuwa walinzi waliingia mikononi mwao wakiwa wameshika bunduki. Kwa haraka wakatembea mpaka sehemu ambako alisimama Phillip na kumsabahi.
“Sijui unahitaji nini ndugu yetu hapa?”
“Mh!”
“Tafadhali ongea vinginevyo tutavunja miguu yako sasa hivi.”

“Kwa kosa gani sasa?”
“Hii si sehemu ya kusimama tu kibaya zaidi ni usiku sasa, unahitaji nini tukusaidie?” Mlinzi mmoja aliongea huku akifoka tayari alishaiweka vyema bunduki kulenga miguu ya Phillip.
“Tafadhali msinidhuru niko hapa kuhitaji msaada mmoja tu.”
“Ndio tunaotaka kukusaidia.”

“Nauliza….nauliza dada mmoja anaitwa…Lina.”
“Lina?”
“Ndio.”
“Hebu niangalie kwenye kitabu cha wageni wangu leo.” Haraka dada wa mapokezi akavuta daftari kubwa na kuanza kufunua ukurasa mmoja baada ya mwingine akiangalia jina hilo.”

“Hatuna jina la mtu huyo leo labda kama ana jina jingine.”
“Hapana anaitwa Lina ndilo jina lake.”
Phillip akabaki mdomo wazi hakuwa na namna nyingine ya kueleza kwani jambo lililokuwa likifanyika ndani ya hoteli hiyo chumbani lilikuwa ni siri kubwa bila kutarajia machozi yakaanza kumbubujika.
“Mungu baba, niondolee kikombe hiki kinazidi kuwa cha moto zaidi” aliwaza Phillip akiwa amejiinamia.

Je, nini kitaendelea? Phillip atakuwa tayari kueleza ukweli ili apate msaada wa kumpata Lina? Nini hatima ya Victor Fedorov na watoto wake kwenye msitu wa Beloomut?
 
 
 
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.77

Huku akionekana mwenye wasiwasi mwingi machoni mwake, aliendesha gari mara kadhaa akigeuza shingo yake huku na kule kuangalia usalama kwani alifahamu wazi kwamba sifa za msitu huo nchini Urusi zilitisha kupita maelezo, njia nzima aliendesha gari bila kukutana na mtu yeyote na kwa ilivyoonekana hapakuwepo kiumbe hai kilichoishi ndani ya msitu huo.

Moyoni mwake hakuwa na uhakika kama angeweza kutoka ndani ya msitu huo akiwa salama lakini zaidi ya yote ni watoto wake Mariya na Merina hao ndiyo walikuwa kila kitu na alitaka afanye kila alichoweza kuhakikisha anawapata wakiwa hai.
“Ikitokea nikifa halitakuwa tatizo sana lakini watoto wangu wapone, najua wataweza kuendesha maisha kwa utajiri nilionao, ninashukuru kwamba nimeandika kila kitu kwa wakili wangu…”aliongea.

Victor Fedorov alifanikiwa kuingia ndani ya msitu na kuegesha gari lake sehemu moja iliyoonekana kuwa wazi, hapo akajiweka sawa akiangalia usalama wake, taratibu bila kujiuliza mara mbili akalikamata vyema begi lililokuwa na fedha ndani yake kisha akaichomeka bastola yake kiunoni na kushuka garini.
Akatupa macho yake huku na kule bila kuona kitu chochote, akiwa katika hali hiyo milio ya risasi ikasikika.

“Puuu! Puuu! Puuu!”
“Mungu wangu… hiyo ni milio ya risasi…isijekuwa…” aliongea akijaribu kuzungusha macho yake huku na kule na katika kuangalia vyema macho yake yakakutana na kitu cha ajabu mbele yake, mtu aliyevalia nguo nyeusi na uso wake ukiwa umefunikwa na kuacha sehemu ya macho tu.

Mtu huyo alisimama pembeni kidogo mahali Victor Fedorov alipokuwa ameegesha gari.
“Haaa! Haaa! Haaa” mtu huyo alicheka kwa sauti ya kebehi.
Akitetemeka, akatembea akisogea kuelekea mahali aliposimama mwanaume huyo lakini kabla hajamfikia karibu sauti nyingine ikasikika.
“Victor Fedorov?” mwanaume huyo aliuliza.

“Ndiyo.”
“Vyema umefika muda muafaka kabisa.”
“Watoto wangu wako wapi?”
“Usiwe na haraka watoto wapo lakini nataka kufahamu jambo moja; je umefika hapa na nani?”
“Peke yangu kabisa hakuna mtu…”

“Una uhakika?”
“Asilimia mia moja.”
“Kumbuka kama unaye mtu mwingine kwenye gari lako jambo hilo litamaanisha hatari kubwa pengine kupoteza watoto wote.”
“Ninachokizungumza ni ukweli mtupu, tafadhali chukua fedha hizi hapa kisha unipatie watoto wangu,” aliongea Victor Fedorov machozi yakimbubujika.

Pamoja na ukatili wake wote hapo alikuwa amefunga breki, hakuwa na namna nyingine yoyote ya kufanya zaidi ya kukubali kila alichokuwa ameelezwa ili mradi tu awapate watoto wake Mariya na Merina.
“Daddyyyyy.” (baba.) Sauti hiyo ilipenya moja kwa moja masikioni mwa Victor Fedorov.
Haraka akageuza shingo yake huku na kule kuangalia ni wapi sauti hiyo ilitokea lakini hakufanikiwa kuona kitu chochote, alirudisha macho yake kumwangalia mwanaume aliyekuwa mbele yake.

“Najua wazi huwezi kukosa silaha ni vyema ukaiweka chini haraka.”
Bila kusema kitu chochote akaichomoa bastola yake na kuitupa chini huku akiendelea kumsihi mwanaume huyo kumweleza ni wapi walipokuwa watoto wake.
“Weka pia begi hilo hapo chini na urudi nyuma mita tano!” aliamuru mwanaume huyo.

Taratibu, Victor Fedorov alitii kila alichoelezwa, akaliweka begi chini na kuanza kurudi kinyumenyume, macho yake yote yakimwangalia mwanaume huyo ambaye hakuonekana sura kwani kichwa chake kilifunikwa na kitu kama soksi iliyoacha nafasi ndogo sehemu ya macho tu.

Wasiwasi mwingi ukamfunika na kumfanya ashindwe kuelewa ni kitu gani kingetokea mbele yake baada ya muda mfupi kwani kama ni silaha tayari alishaikabidhi kwa adui aliyekuwa mbele yake.
“Mh!”aliguna huku akiendelea kurudi nyuma akahisi vitu vyepesi vikipenya kutoka ndani ya suruali yake kuelekea chini.

***
Baada ya mhudumu wa mapokezi kusoma kitabu cha wageni kwa muda akitafuta jina la Lina bila mafanikio, aliinua macho yake na kumwangalia Phillip ambaye naye alionekana kulengwalengwa na machozi akimweleza wazi kwamba jina hilo halikuwepo ndani ya kitabu chake labda kama mgeni wake huyo alikuwa na jina jingine alilolitumia.
“Hapana jina lake ni hilo hilo la Lina.”

“Kaka halipo tafadhali niamini na uondoke,” aliongea dada wa mapokezi akitoa ishara kwa walinzi waliokuwepo eneo hilo.
Akiwa katika hali ya kupigwa na butwaa upande mmoja wa akili yake ulimwambia aondoke na kurejea nyumbani huko angeendelea kumsubiri mkewe mpaka atakaporejea lakini upande mwingine wa akili yake ulimwambia atoke nje ya hoteli hiyo na kuingia ndani ya gari lake akae hapo kusubiri mpaka mwisho.

“Mzee nadhani umepata maelezo yanayotosha kabisa kukufanya uelewe, tafadhali tunaomba nafasi hapa.”
Bila kujibu chochote Phillip akainua macho yake na kuwaangalia watu hao, moyo wake ulijaa siri nzito kupindukia lakini hakuwa na uwezo wa kumshirikisha mtu mwingine kwani jambo lililokuwa likifanyika ndani ya hoteli hiyo usiku huo lilikuwa ni siri kubwa.

Machozi yakambubujika, taratibu akaanza kutembea kuelekea nje, moyoni mwake akijilaumu kwa kumtoa mkewe sadaka kwa mwanaume mwingine, akilini mwake akiamini kabisa kwamba Lina alikuwa ameamua kumkimbia.
“Najutia maamuzi yangu haya isingekuwa mimi yote haya yasingetokea, Lina atakuwa ameamua kunitenda kama kisasi,” aliongea Phillip akiukaribia mlango ili atoke nje
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.79

“Hapana! Hapana Mariya usife mwanangu bado nakuhitaji amka uungane na mwenzako Merina yule palee,” aliongea mfululizo akizidi kumtingisha Mariya aliyekuwa amelala chini kimya bila kufungua macho wala kujitingisha.
Hali ilionekana kuwa mbaya, Victor Fedorov alizidi kumtingisha mwanaye ili aamke lakini haikuwa hivyo, Mariya alikuwa amelala ardhini kimya kabisa, akatupa macho yake huku na kule kama vile mtu aliyekuwa akitafuta kitu fulani vile, giza nalo lilianza kutanda katika msitu huo.
“Ni lazima niondoke hapa haraka sana kabla giza halijaingia zaidi,” aliwaza akimnyanyua mtoto wake Mariya na kuanza kukimbia kuelekea kwenye gari lake.
Haraka akamketisha na alipohakikisha kila kitu kilikuwa sawa akaingia ndani ya gari na kukaa kwenye usukani huku akiwa na hofu, akawasha na kukanyaga mafuta, lengo likiwa kuondoka eneo hilo.
Akiwa ndani ya gari baada ya kutoka nje ya msitu huo alisimamisha gari na kuanza kumwita tena Mariya ambaye bado alikuwa ametulia kimya.
“Mariya! Mariya! Nini kimekupata mwanangu?” aliuliza.
“Daddy!” Merina aliita huku akitetemeka, yeye pia afya yake haikuwa nzuri, walidhoofika sana, miili yao ilikuwa michafu kupindukia hata nywele zao zilionekana kujisokota.
“Yes, tafadhali nieleze ni kitu gani kimempata nduguyo?” aliuliza hamu yake kubwa ikiwa ni kufahamu tatizo lililotokea huko nyuma kabla hawajafika eneo hilo.
Merina hakujibu kitu chochote, zaidi aliishia kuangua kilio kilichozidi kumtia wasiwasi baba yao akashindwa kuendelea na safari na kuliegesha gari pembeni kwanza ili azungumze na Merina ambaye alionyesha nafuu kidogo kuliko mwenzake Mariya.
“Baba tafadhali endesha gari ukichelewa kidogo tu hata mimi nitakuwa kama Mari…”aliongea Merina na kabla hajamalizia sentensi yake naye pia akatulia kimya kitini.
Victor Fedorov akazidi kuchanganyikiwa zaidi akashindwa afanye kitu gani kwani kila kitu kilichokuwa kikimtokea katika maisha yake kwa wakati huo kilionekana kuwa kama ndoto, alishatoa fedha nyingi ili kuokoa maisha ya watoto wake lakini ni hao sasa waliokuwa katika hali ya kufa kwani wote walionekana kupoteza fahamu, moyo ukamuuma sana akajutia uamuzi wake wa kuwateka watoto hao kutoka nchini Tanzania na kuwaleta nchini Urusi na sasa walikuwa wakifa bila hatia yoyote.
“Ubinafsi umeniponza pengine Mungu ananipa pigo hili ili nitubu kwa dhambi niliyoifanya ya kuwateka watoto hawa, lakini si ni uzao wangu huu? Hapana, nasema hapana siko tayari nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu wote kuhakikisha maisha yao yanarejea tena naamini watakuwa hawajafa bali wamezimia tu…” aliwaza huku akizidi kukanyaga mafuta.
Akili yake yote ilishahama na kwenda moja kwa moja kuokoa maisha ya watoto wake, alitaka afike nyumbani haraka na kutafuta daktari ambaye angeweza kufanya kila atakachoweza kuokoa maisha ya watoto hao pacha, hata kama safari hii ingegharimu utajiri wake wote aliokuwa nao, Victor Fedorov alikuwa tayari.
Kwa muda wa saa tatu bado alikuwa barabarani, mara kadhaa akisimama na kuwaangalia watoto wake ili kujua hali zao, bado zilikuwa zilezile hawakuzungumza chochote zaidi ya kutulia kimya vitini.
Saa sita baadaye huku akimwagika jasho mwili mzima tayari alishawasili nje ya lango la nyumba yake, akapiga honi na mara moja lango likaonekana likifunguliwa na gari kuzama ndani, bila kusema kitu chochote na mlinzi wake akaliendesha gari mpaka sehemu ya maegesho, akasimama na kushuka haraka garini kisha akafungua milango ya nyuma.
“Mlinzi!”aliita kwa sauti ya juu na mara moja akakimbia na kusimama mbele ya gari lake.
“Tafadhali nisaidie kubeba mtoto mmoja haraka kwenda ndani,” aliamuru tayari mikononi mwake alishambeba Mariya.
Mlinzi hakuchelewa, alimbeba Merina wakaanza kukimbia kuelekea ndani.
***
Huku machozi yakimbubujika, moyoni mwake akiumia, Phillip alianza kutembea kuuelekea mlango wa mapokezi ili atoke nje na kuondoka eneo hilo kama alivyoamriwa.
Walinzi wawili wenye silaha walikuwepo nyuma yake kumsindikiza, wao pia walionyesha kuchukizwa sana na kitendo alichokuwa amekifanya Phillip eneo lao la kazi hivyo hawakuwa na utani walitaka kulinda vyema kibarua chao.
“Tembea haraka bwana tena tunakusihi uondoke eneo hili haraka sana kabla hatujakuchakaza…umesikia bwana mdogo…tembea…” aliongea askari mmoja akimsukuma kwenda mbele. Machozi yakambubujika kwa mara nyingine tena hakuwa tayari kuondoka hotelini hapo na kumwacha mkewe Lina ambaye aliamini kabisa kwamba bado alikuwepo ndani.
Wakati mlinzi wa mwisho anatoka na kufunga mlango nyuma yake sauti kali ikasikika ndani ya hoteli hiyo mwanamke akilia kuomba msaada na kishindo cha mtu akikimbia kuelekea eneo la mapokezi kikasikika.
“Uwiii! Nisaidieni! Tafadhali niokoeni jamani! Anani…”
“Mh!” wote wakaguna.
“Sauti kama ya Lina! Ni sauti ya mk…” aliongea Phillip mfululizo na kushindwa kumalizia sentensi yake, wote wakaonekana wakikimbia mbio kurejea ndani ya hoteli.

Je, nini kitatokea? Sauti iliyosikika ndani ya hoteli Phillip ameitambua kwamba ni ya mkewe Lina, ni kitu gani kimempata huko?
 
 
 
 
 
MSICHANA NDOTONI MWANGU...EP.80

Hapana! Hapana Mariya usife mwanangu bado nakuhitaji amka uungane na mwenzako Merina yule palee,” aliongea mfululizo akizidi kumtingisha Mariya aliyekuwa amelala chini kimya bila kufungua macho wala kujitingisha.
Hali ilionekana kuwa mbaya, Victor Fedorov alizidi kumtingisha mwanaye ili aamke lakini haikuwa hivyo, Mariya alikuwa amelala ardhini kimya kabisa, akatupa macho yake huku na kule kama vile mtu aliyekuwa akitafuta kitu fulani vile, giza nalo lilianza kutanda katika msitu huo.
“Ni lazima niondoke hapa haraka sana kabla giza halijaingia zaidi,” aliwaza akimnyanyua mtoto wake Mariya na kuanza kukimbia kuelekea kwenye gari lake.
Haraka akamketisha na alipohakikisha kila kitu kilikuwa sawa akaingia ndani ya gari na kukaa kwenye usukani huku akiwa na hofu, akawasha na kukanyaga mafuta, lengo likiwa kuondoka eneo hilo.
Akiwa ndani ya gari baada ya kutoka nje ya msitu huo alisimamisha gari na kuanza kumwita tena Mariya ambaye bado alikuwa ametulia kimya.
“Mariya! Mariya! Nini kimekupata mwanangu?” aliuliza.
“Daddy!” Merina aliita huku akitetemeka, yeye pia afya yake haikuwa nzuri, walidhoofika sana, miili yao ilikuwa michafu kupindukia hata nywele zao zilionekana kujisokota.
“Yes, tafadhali nieleze ni kitu gani kimempata nduguyo?” aliuliza hamu yake kubwa ikiwa ni kufahamu tatizo lililotokea huko nyuma kabla hawajafika eneo hilo.
Merina hakujibu kitu chochote, zaidi aliishia kuangua kilio kilichozidi kumtia wasiwasi baba yao akashindwa kuendelea na safari na kuliegesha gari pembeni kwanza ili azungumze na Merina ambaye alionyesha nafuu kidogo kuliko mwenzake Mariya.
“Baba tafadhali endesha gari ukichelewa kidogo tu hata mimi nitakuwa kama Mari…”aliongea Merina na kabla hajamalizia sentensi yake naye pia akatulia kimya kitini.
Victor Fedorov akazidi kuchanganyikiwa zaidi akashindwa afanye kitu gani kwani kila kitu kilichokuwa kikimtokea katika maisha yake kwa wakati huo kilionekana kuwa kama ndoto, alishatoa fedha nyingi ili kuokoa maisha ya watoto wake lakini ni hao sasa waliokuwa katika hali ya kufa kwani wote walionekana kupoteza fahamu, moyo ukamuuma sana akajutia uamuzi wake wa kuwateka watoto hao kutoka nchini Tanzania na kuwaleta nchini Urusi na sasa walikuwa wakifa bila hatia yoyote.
“Ubinafsi umeniponza pengine Mungu ananipa pigo hili ili nitubu kwa dhambi niliyoifanya ya kuwateka watoto hawa, lakini si ni uzao wangu huu? Hapana, nasema hapana siko tayari nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu wote kuhakikisha maisha yao yanarejea tena naamini watakuwa hawajafa bali wamezimia tu…” aliwaza huku akizidi kukanyaga mafuta.
Akili yake yote ilishahama na kwenda moja kwa moja kuokoa maisha ya watoto wake, alitaka afike nyumbani haraka na kutafuta daktari ambaye angeweza kufanya kila atakachoweza kuokoa maisha ya watoto hao pacha, hata kama safari hii ingegharimu utajiri wake wote aliokuwa nao, Victor Fedorov alikuwa tayari.
Kwa muda wa saa tatu bado alikuwa barabarani, mara kadhaa akisimama na kuwaangalia watoto wake ili kujua hali zao, bado zilikuwa zilezile hawakuzungumza chochote zaidi ya kutulia kimya vitini.
Saa sita baadaye huku akimwagika jasho mwili mzima tayari alishawasili nje ya lango la nyumba yake, akapiga honi na mara moja lango likaonekana likifunguliwa na gari kuzama ndani, bila kusema kitu chochote na mlinzi wake akaliendesha gari mpaka sehemu ya maegesho, akasimama na kushuka haraka garini kisha akafungua milango ya nyuma.
“Mlinzi!”aliita kwa sauti ya juu na mara moja akakimbia na kusimama mbele ya gari lake.
“Tafadhali nisaidie kubeba mtoto mmoja haraka kwenda ndani,” aliamuru tayari mikononi mwake alishambeba Mariya.
Mlinzi hakuchelewa, alimbeba Merina wakaanza kukimbia kuelekea ndani.
***
Huku machozi yakimbubujika, moyoni mwake akiumia, Phillip alianza kutembea kuuelekea mlango wa mapokezi ili atoke nje na kuondoka eneo hilo kama alivyoamriwa.
Walinzi wawili wenye silaha walikuwepo nyuma yake kumsindikiza, wao pia walionyesha kuchukizwa sana na kitendo alichokuwa amekifanya Phillip eneo lao la kazi hivyo hawakuwa na utani walitaka kulinda vyema kibarua chao.
“Tembea haraka bwana tena tunakusihi uondoke eneo hili haraka sana kabla hatujakuchakaza…umesikia bwana mdogo…tembea…” aliongea askari mmoja akimsukuma kwenda mbele. Machozi yakambubujika kwa mara nyingine tena hakuwa tayari kuondoka hotelini hapo na kumwacha mkewe Lina ambaye aliamini kabisa kwamba bado alikuwepo ndani.
Wakati mlinzi wa mwisho anatoka na kufunga mlango nyuma yake sauti kali ikasikika ndani ya hoteli hiyo mwanamke akilia kuomba msaada na kishindo cha mtu akikimbia kuelekea eneo la mapokezi kikasikika.
“Uwiii! Nisaidieni! Tafadhali niokoeni jamani! Anani…”
“Mh!” wote wakaguna.
“Sauti kama ya Lina! Ni sauti ya mk…” aliongea Phillip mfululizo na kushindwa kumalizia sentensi yake, wote wakaonekana wakikimbia mbio kurejea ndani ya hoteli.

Je, nini kitatokea? Sauti iliyosikika ndani ya hoteli Phillip ameitambua kwamba ni ya mkewe Lina, ni kitu gani kimempata huko? TUTAENDELEA BAADAE WAPENDWA
 

No comments:

Post a Comment